Search This Blog

Wednesday 15 March 2023

HURUMA YA DUDU - 1

 

IMEANDIKWA NA: UNKNOWN

**************************************

Chombezo : Huruma Ya Dudu

Sehemu Ya : Kwanza (1)


Nakumbuka ilikuwa mwaka jana tarehe 8 mwezi wa 8, siku ambayo niliamua kutoka kijijini kwetu tukuyu kisha nilihamia mbeya mjini. Ni baada ya kuuza mpunga wangu, nilipata pesa za kutosha, niliamua kwenda mjini ili nikaanze maisha yangu. 

Nilifika mjini, kwakuwa nilikuwa nina pesa; sikupata tabu ya kutafuta chumba. Nilibahatika kupata chumba cha bei powa katika mtaa uitwao Sai. Nililipa kodi ya miezi sita, nilinunua  vifaa vyote kuanzia kitanda, godoro, vyombo na mazaga zaga mengine. 

Baada ya kukamilisha chumba changu, nilitulia geto nikiwaza kuhusu biashara ya kufanya. Kichwa changu kiliwaza biashara nyingi. Niliwaza kuuza vyombo vya nyumbani au kuuza nguo. Niliwaza sana sikupata jibu!!

"Ila wauzaji wa nguo ni wengi sana, bora niuze vyombo, niwe napitisha nyumba hadi nyumba..biashara ikiwa kubwa nitafungua duka la vyombo" Niliwaza nikiwa juu ya godoro. Hapo njaa ilinibamiza ila sikuhisi njaa, si unajua maisha ya getho. 

Niliamua niuze vyombo. Niwe navipitisha mtaa kwa mtaa, nyumba hadi nyumba nikisaka wateja. Nilipanga kuanza biashara hiyo siku iliyofuata. Nilikoleza jiko, nilipika mboga, nilipika wali, nilipiga msosi kisha nililala. 

Kutokana na ugeni nililala sana chumbani kwangu. Nililala hadi mida ya jioni ndipo niliamka. Hadi muda huo sikujua nyumba ina wapangaji wangapi, hao wapangaji ni akina nani, sikujua chochote na wala sikutaka kujua. 

Nilipanga kutojihusisha na wanawake. Kwanza sikuwahi kufanya mapenzi, siujui utamu wa mapenzi wala simjui mwanamke. Hata kitumbua cha mwanamke sijawahi kukiona, sijui kina umbo gani, ila huwa nasikia watu wakisema kitumbua ni kitamu sana!!

"Nimekuja mjini kutafuta maisha, nimekuja kufanya kazi. Kama nimeamua kuuza vyombo basi natakiwa kukomaa na vyombo...sitaki mwanamke hata mmoja. Sitaki kujihusisha na mapenzi wala upumbavu wa kijinga. Labda kama nikioa..la sivyo sitaki mwanamke." Niliwaza nikiwa juu ya godoro. 

Nilitoka chumbani, niliamua kwenda kukaa nje nikashangae mataa. Nilifunga mlango wa chumba changu, nilipiga hatua kuelekea nje. Kabla sijafika mbali, niliitwa na mama mwenye nyumba. 

"We kijana..wewe mgeni..."

"Mimi au?" Nilijibu baada ya kugeuka

"Ndiyo wewe...hivi unaitwa nani?"

""Mwakitombile"

"Unaitwa nani? Sijasikia vizuri"

"Naitwa Mwakitombile"

"Eh! Mwakitombile? Ndo jina gani hilo?"

"Kama ni ndefu sana unaweza kuniita MWAKI" Nilijibu nikijichekesha. 

"Haya njoo hapa nikupe miongozo ya hii nyumba"

Nilimfuata mama mwenye nyumba. Alikuwa ni mama mtu mzima, hata hivyo alijaaliwa kila kitu. Kama ujuavyo wamama wa zamani ambao walijaliwa makalio ya asili, sio ya mchina. Mapaja ya nguvu, mguu wa shoka na kifua chenye maembe makubwa. Kichwani alivaa mzura. Nilifika kwake kisha nilitaka kukaa chini;

"Usikae chini, njoo ndani tuongee" aliniambia akiwa anaelekea ndani. 

Nami nilimfuata huko huko ndani, hadi kwenye sofa. Nilizungusha macho nikishangaa uzuri wa sebule yake, jamani kuna watu wana maisha mazuri. Mama alikuwa ana flat screen nchi 100, Sabufa 10, Sofa zilizunguka kila sehemu, kapeti la manyoya, meza za vioo, kabati la chuma, feni 6 na madude mengine. Nilishindwa kuvumilia,nilimuuliza;

"Mama mjengo hii nyumba ni yako au ya kukodi?"

"Ni yangu..mbona unaniuliza hivyo?" aliongea akicheka

"Aisee nabisha...nyumba imejaa vioo na vyuma tu!!...ile flat screen kama ya Rais wa marekani ni yako?"

"Ah ah ah! Ila we mpangaji una mambo..inaonekana we ni mshamba sana"

"Sanaa...yani mimi ni mshamba wa mwishoo..duniani hapa hakuna mshamba kama mimi"

"Mh! sasa kama ni hivyo; mkeo anakuweza kweli?"

"Mke gani?"

"Kwani wewe huna mke?"

"Simjui mwanamke mimi"

"Ebu rudia..umesema humjui mwanamke? Una maana gani?"

"Mi sijawahi kufanya mambo hayo..hapa nilipo nimetokea huko mashambani"

Baada ya kauli yangu, Mama mwenye alitabasam kisha alisimama, alinifuata. Sikujua anataka kunifanya nini, ila baada ya kunifikia, alikaa pembeni yangu kisha alinitazama alafu aliniuliza;

"Kwahiyo leo ndo mara yako ya kwanza kuona vyombo vya chuma?"

"Ndiyo mama"

"Je umewahi kuona kitanda cha chuma?"

"Kitanda cha chuma? Hapana...kwanza katika dunia hii hakunaga kitanda kama hicho"

"Mh kwahiyo unabisha?"

"Ndiyo nabisha"

"Unataka kukiona?"

"Ndiyo"

"Sawa simama kisha twende chumbani kwangu ukakione"

Mama mwenye nyumba alisimama, nami nilisimama, alipiga mwendo kuelekea chumbani kwake. Nami nilimfuata..tulienda kuona kitanda cha chuma. 

 UNAJUWA KILICHOTOKEA HUKO CHUMBANI? NI ZAIDI YA UTAMUUU




"Je umewahi kuona kitanda cha chuma?"

"Kitanda cha chuma? Hapana...kwanza katika dunia hii hakunaga kitanda kama hicho"

"Mh kwahiyo unabisha?"

"Ndiyo nabisha"

"Unataka kukiona?"

"Ndiyo"

"Sawa simama kisha twende chumbani kwangu ukakione"

Mama mwenye nyumba alisimama, nami nilisimama, alipiga mwendo kuelekea chumbani kwake. Nami nilimfuata..tulienda kuona kitanda cha chuma. 

Tulifika chumbani kwake, huko sasa nilipagawa. Nilijiuliza hicho ni chumba au duka la mapambo? Jamani kuna watu wanalala sehemu nzuri duuh! Kila kitu kilikuwa cha chuma, kuanzia kabati la nguo, kitanda hadi godoro; vyote vya chuma!!

Nilizubaa nikiwa nashangaa mataa ya chumba na paa la mamaa mwenye nyumbaa!! Chumba kilikuwa kitamu zaidi ya chombezo za mwandishi wa CHOMBEZO TAMU. Nilibaki mdomo wazi, mama mjengo alinicheka tu. 

"Kwahiyo leo ndo mara yako ya kwanza kuona kitanda cha chuma?"

"Ndiyo...kwanza bado siamini, haiwezekani hadi chaga ziwe za chuma."

"Kwani huko kwenu kijijini ulikuwa unalala kwenye vitanda gani? Au vya mbao?"

"Bora hata mbao.. kijijini sikuwahi kulala kwenye kitanda, nilikuwa nalala juu ya majani ya mpunga"

Mama mwenye nyumba alicheka nusura ajikojolee. Aliniona zoobaa la mwisho. Alinitazama usoni kisha alicheka tena..aliniona mbumbumbu, alinidharau kweli kweli..aliniona kopo la mafuta ya kupaka!

"Kwahiyo hujawahi kuonja ladha ya bumunda?"

"Bumunda ndo nini?"

"Kitumbua"

"Vitumbua nakulaga...nakula na uji wa mchele"

"Ah ah ah! Namaanisha hujawahi kuingiza dudu kwenye kitumbua cha mwanamke?"

"Mi sijawahi mimi..kwanza baba na mama walinikataza kujihusisha na mapenzi. Walisema hadi nioe"

"Kwahiyo unasubiri hadi uoe?"

"Ndiyo...bila kuoa sitofanya huo ujinga"

"Oh! safi, unaonekana unajitambua sana"

"Sanaa, mimi hata kijijini kwetu nilikuwa naongoza mitihani yote ya chekechea."

"Unaonekana tu..wewe ni mfano wa kuigwa kwa vijana wenzio ambao wanafanya ngono kabla ya kuoa au kuolewa. Vijana hao hawana thamani tena, wakiingia kwenye ndoa hawana jipya tena..wanajua kusaliti, kucheat, wanaenda mbele na nyuma, wanazijua staili zoote"

"Staili ya kuruka sarakasi au?"

"Eeh hizo hizo..ila wewe ni bogas sijapata kuona"

"Ni kweli, kwetu huwa tunakula maboga"

Mama mjengo alinitazama alinionea huruma, alitikisa kichwa kulia kushoto akinisikitikia. Alinitazama kuanzia chini hadi juu, nilikuwa na mwili mkubwa akili ndogo. Alitamani aniralue makofi ili nikae sawa!

"Wewe ni punguani?"

"Ndiyo mama angu"

"Looh! Alafu nikuulize kitu?"

ITAENDELEA



0 comments:

Post a Comment

Blog