Search This Blog

Wednesday 15 March 2023

MDOLI WA DUKANI - 1

 

IMEANDIKWA NA: UNKNOWN

**************************************

Chombezo : Mdoli Wa Dukani

Sehemu Ya : Kwanza (1)


#ONYO USISOME STORY HII KAMA HUNA MWENZA??

“When should I expect it to arrive”.

“Something like next month”.

“Okay thanks i´ve sent the money in advance”.

“Ok Worry not,soon yo´ll have your haul”.

“okay thanks”.

Yalikuwa maongezi kwa lugha ya kingereza kati ya bosi wangu na mhudumu wa kampuni moja kutoka china iliyojihusisha na utengenezaji wa midoli mbalimbali.Bosi alikuwa akiagiza mzigo wa midoli ambayo tuliihitaji sana katika duka letu kubwa la nguo.

Hivyo baada ya kuwasiliana na wale wachina waliokuwa nchini mwao basi aliambiwa asubiri ndani ya mwezi mzigo wake utafika.Midoli tuliyohitaji sana pale dukani ilikuwa ya kiume kwani tulibadilisha mfumo wa uuzaji wa bidhaa zetu.

Mwanzoni tulikuwa tunauza nguo za kike pekee na hivyo midoli tuliyokuwa nayo mingi ilikuwa ya kike na hivyo baada ya uamuzi huo wa kuanza kuuza nguo za kiume tuliamua kuagiza shehena kubwa ya midoli ya kiume kwa ajili ya kuonesha bidhaa zetu.

Hatimaye mwezi ulifika baada ya ile simu kupigwa na ndipo bosi wangu alipokea simu kutoka bandarini iliyokuwa ikimjulisha kuwa mzigo wake umefika.Basi bosi alijiandaa akawasha gari na kuelekea mpaka bandarini akiniacha mimi na wafanyakazi wengine wawili wa kike tukiendelea na kazi ya mauzo.

Jioni ya siku hiyo bosi alirudi na gari kubwa iliyopaki nje ya duka letu na kuanza kushusha ile midoli.Ilikuwa midoli mizuri na mikubwa ya kiume ambayo kwa kuiangalia nilijua ingeweza kufanya display nzuri ya mavazi yetu pale nje na hata ndani ya duka.

Baada ya midoli kutolewa yote tuliipokea na kuanza kazi ya kuiingiza ndani na asubuhi ya shughuli ya kuipanga nje na ndani ya duka ile midoli ilianza.”Jeni wewe chukua kundi hili nenda kaipange kule ndani, hii waachie Hanifa na na Ummy.”

Aliniambia bosi basi nikafuata kundi langu la midoli nikibeba mmoja mmoja na kuipeleka kule ndani ya duka.Nilibeba midoli kama kumi hivi na kuipanga vizuri lakini mdoli wa kumi na moja nilivyoubeba nilishangaa mdoli huo kuwa mzito sana na hata kifungashio ulichokuwa umewekewa kilikuwa cha tofauti kabisa.

Sikutaka kuongea kitu, nilikomaa mwenyewe hivyohivyo mpaka nikauingiza ndani ingawa nilichoka balaa na kulowa jasho mpaka bosi akaniuliza vipi mbona umelowa jasho utazani ulikuwa unanyanyua vyuma.Basi miye nilicheka tu nikaingia zangu ndani .

Baada ya kila mmoja kumaliza kuipanga midoli na bosi baada ya kukagua akajiridhisha basi tulipewa nguo ambazo tulitakiwa kuivalisha ile midoli kwa ajili ya display.Nilichukua boksi la nguo mbalimbali na kuanza kuivalisha ile midoli.

Nilipoufikia ule mdoli mzito baada ya kuutoa kwenye kifungashio chake, kwanza kabisa katika sehemu yake ya ubavuni niliona kukitoa mwanga Fulani wa bluu,nilistuka nikatoa mkono haraka lakini ule mwanga uliendelea kutoka.Nikajikuta nimepeleka mkono na kugusa palena ndipo nilishangaa ule mdoli ukifungua macho na kunigeukia huku ukitabasamu.Macho yake yalifanana kama ya binadamu.

“Hellow miss Jenny´im Mathew specialized sex machine, am at your service”(Habari miss Jeni jina langu ni Mathew ni mtaalamu wa kufanya mapenzi, nipo kwa ajili yako.)

Ilisikika sauti ya ule mdoli,iliyozidi kunishangaza.Nilibaki naushangaa ule mdoli maana kiukweli niliona maajabu sikuwahi kuona mdoli wa aina ile.Basi nilianza kuuvalisha shati harakaharaka, lakini nikashangaa unanizuia kwa kunishika mikono.

“Miss Jenny your not in mood, im sorry then press the button on my chest to switch me off”Uliniambia ule mdoli huku ukitabasamu ukiniomba radhi kwa kuwa sikuwa tayari kufanya mapenzi na kuniambia niuzime.Na kweli nilivyotazama kifuani mwake niliona batani ya bluu ikiwakawaka nikaizima.

Baada ya kuuzima ulitulia kama mdoli na macho yake hayakucheza tena.Basi nikiwa nimejawa hofu kwa maajabu yale nilianza kuuvalisha nguo ule mdoli haraka lakini nilipoufikia maeneo ya kiunoni nilistuka baada ya kukuta kumevimba.Nilipogusa nilikutana na sehemu za kiume kama za binadamu.Ulaini na kila kitu kilifanania na za binadamu.Tofauti ni kuwa zile zilikuwa na  ubaridi Fulani hivi.ghafla nikahisi kitu kikigusa juu ya uchi wangu uliokuwa ndani ya ushungi niliokuwa nimevaa asss!!


ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

Blog