Search This Blog

Wednesday 15 March 2023

MKE CHANGUDOA - 2

  


Chombezo : Mke Changudoa

Sehemu Ya : Pili (2)



Ana akaanza kwa kusema, "kule kwetu, mke hana thamani, mfano mama yangu akikuwa anapigwa kila siku na baba, pia alikuwa baba anamfanya mama kama mfanyakazi wake, hakuna siku mama alipumzika, yeye ndio aende shamba yeye ndio afanye kila kitu, mpaka nilikuwa namuonea huruma, ila nimekuja kwenu nimeona utofauti mkubwa sana, tena sana"..... "pole sana ana, ila kuna baadhi ya mila na desturi zinatukandamiza sisi wanawake, pia kuna kitu kinaitwa mfumo dume hii ndio mbaya zaidi. Kikubwa ni kujitambua na kumuomba mungu mwenyewe, wanaume wa hivyo wapotee"..... "yaani mimi baba simpendi hata kidogo"...... "hapana hiyo haibadilishi maana, bado ni baba, kikubwa unapaswa kumuombea aache ulevi, na awe mtu mwema"...... "sawa dada"...... "sawa nenda kaangalie kama shemeji yako amemaliza kula utoe vyombo pale mezani sawa" anna aliamka na kwenda kutoa, vyombo alipofika, alikuta wameshamaliza naye akaondoa vyombo na kusafisha meza, "anna muite dada yako" hasan alimwambia ana, ana akasema "sawa shemeji" ana kaondoka.


"Huyu ni nani hasani?"....... "ni binti anamsaidia saidia kazi mke wangu hapa"....... "mmmmh inamaana mke wako hawezi kufanya kazi zake mwenyewe hapa ndani au ndio wanawake wa dar"...... "hapana, ila nimemfungulia mke wangu ofisi yake, sasa huwa anaendaga ofisi kwake, hivyo huyu dada anabaki na mtoto"...... "ooooh hapo sasa nimekuelewa" wakiwa wanaongea alikuja mke wa hassan, "naam, nimeambiwa unaniita" mke wa hassan aliongea hayo, juma akasema, "shem asante sana kwa chakula, unatokea tanga nini?" mke wa hasan akacheka kisha akauliza "kwanini shemeji?"..... "wali wenyewe kabisa huu, samaki anaviungo vyote vya pwani" hasan akasema, "alisoma course ya mapishi"..... "hahaha, itakuwa kweli, ahsante sana nashukuru mungu akubariki"...... "ahsante kushuru, ahsante kwa kula pia" hassan akasema "mke wangu jiandaeni nimewahidi kuwatoa leo?"...... "sawa ndio namsuka mtoto?"..... "unataka twende wapi"....... "nimepamis the great" juma akadandia, "shem unapajua the great?"


"mbona umeshanga hivyo? Hasan akauliza, akaendelea kusema,"kuna tatizo kujua sehemu kama hizo?" juma akasema "hapana sio ajabu lakini nilijua shem hawez kuwa anaenda sehemu kama hizo, kwa muonekano wake anaonekana amekuwa kwenye familia ya dini sana ndio maana nimestuka kusikia anataja sehemu hiyo." hasan akasema "usilo lijua ni usiku ww giza, ila hata kila mtu anahaki ya kuenjoy maisha kikubwa ni tusimkufuru mungu na kutenda yale akiyoyakataza. Mke wangu sasa the great tutaendaje na mtoto?" mke wa hasan akajibu, "nilipanga twende tukale pale precious food point, halafu tunawarudisha hawa watoto wanalala sisi tunaenda zetu kushanga kidogo"...... "sawa nimekuelewa"...... "ahsante mume wangu" mke wa hasan aliondoka na kwenda kuendelea kumsuka mtoto.


Hassan na juma walikuwa wanaendela na story zao. "hivi unamkumbuka Eva?"...... "hapana simkumbuki"...... "yule demu tuliwahi kwenda wote kwake, anaishi tunduma boda pale?"....... "aaaah nimemkumbuka"....... "hasan unasahau sana"...... "majukumu kaka"...... "sawa, sasa yule manzi bhana, juzi kati alinipigia simu video call nikiwa zangu south, anasema heti amemisi penzi langu"........ "eeeh ukamwambiaje?"...... "nikamwambia mimi nipo south, ila next week narudi home, akaniuliza umeenda lini? Nikamwambia mbona mwaka wa tano huu nipo huku, hakuamini nikamwambia ningekuwa bongo ungeniona hapo, akanambia upo na yule rafiki yako mpole, nikamwambia hapana yule yupo dar, akakusifia sana, anasema, yaani yule mwenzio mstaarabu sana sio kama wewe, halafu anasura nzuri yani hata ukitembea naye unajisikia unatembea na mwanaume haswa, nilicheka sana nikasema inamaana mimi sio mwanaume "......."yule si malaya, malaya anamsifu kila mwanaume ili apate pesa tu maisha yaende mbele, sema anakuelewa sana yuoe manzi"...... "ni kweli mimi amenambia yupo tayari kuolewa na mimi, sema mwanangu yule ukiweka ndani si utakuwa umewawekea masela msosi tu"....... "hapana kila lenye mwanzo huwa na mwisho itategemea huo mwisho upoje? Waswahili wanamisemo mingi sana, ila kuna mmoja husema mbio za sakafuni huishia ukingoni, hivyo zile ni mbio za ujana tu mwisho wake ni uzeeni ijapo kuwa wengine ni wazee na wanaendelea, ndio pale tunasema, mazoe yamejenga tabia na tabia ni sawa na ngozi ya mwili huwezi ibadili? Hivyo basi niseme tu kuwa kama ataamua kukuacha shetani na kuwa mtu wa mungu, basi malaika wema watamlinda. "...... "bro unamoyo sana, kwahiyo unataka kusema yule mwanamke anaweza kutulia kweli?"........ "ndio. Hakuna kinachoshindikana pindi ukiamua."....... "sasa sijui kama ameamua au laah!"....... "twende tukaoge tutoke, maana stor zako wewe haziishi" jua lilikuwa limisha zama na giza lilikuwa limianza kutanda.


Walijianda na kisha wakaita tax na kuelekea sehemu ambayo walipanga kupata dinner, waliagiza chakula wakala waki enjoy kwa pamoja, walipomaliza hassan akasema, "mke wangu nisubiri na shemeji yako hapa, acha mimi niwapeleke watoto nyumbani maana naona sarha ameanza kusinzia narudi muda si mrefu" hassana akaondoka akamuacha juma na mke wake. Hassan akawapeleka watoto akawafikisha nyumbani kisha alihakisha usalama upo wakutosha ndio akaondoka kurudi alipowaacha mke wake na juma. Upande wa juma na mke wa hasan walikuwa na maongezi, juma akimwambia mke wa hasan. "shemeji wewe mrembo sana yaani kama malaika" juma alianza kumsifia shemeji yake, "shemeji ushawahi kuwaona malaika au ni hadithi tu?"....... "wewe msuzu bwana yaani ukigombea umiss dar hapa hukose taji, kwanini hukugombea enzi za ujana sijui utoto maana sasa hivi unaoneka kama under twenty vile?"........ "shemeji unamaneno wewe?"...... "hivi shemeji, uunampenda kweli huyu jamaa?"...... "unamaanisha nini kuniuliza hivyo?"


"sina nia mbaya shemeji nimeuliza tu"...... "nampenda sana mume wangu, yaani moyoni mwangu yeye ndio number one nampenda kushinda chochote kwenye hii dunia"...... "kwa hiyo hata mama yako humpendi kama unavyompenda yeye"...... "kwasasa mume wangu ndio number moja, mama yangu hayupo amefariki kwahiyo sina mwengine zaidi yake"...... "baba yako je"....... "shemeji bhana huelewi?"....... "nakuelewa sana shemeji, ila fresh hongera sana"...... "hongera ya nini?"...... "mnapenda sana"...... "ahsante sana nashukuru"...... "kesho nataka nikatafute nyumba ninunue halafu nitafute na gari nzuri ya kutambia mjini hapa"...... "hongera mungu akubariki"......... "na wewe huna unachotaka nikununulie?"......... "ahsante fanya kwanza vitu vya muhimu" hasana alifika na kisha wakaondoka kuelekea the great, safari ya dakika kumi na tano mpaka kufika tabata, walipofika walitafuta sehemu wakakaa, hasan akamuita mhudumu, wakaagiza vinywaji, juma aliagiza pombe lakini hasan na mke wake walikunywa vinyaji laini, na wakaagiza na nyama, "sasa kama hamnywi pombe mumefwata nini hapa?" juma aliwauliza hasana na mke wake, hasana akajibu kwa kusema, "tumemiss tu haya mazingira sio kwamba tumefwata pombe, kuna wakati unatakiwa ubadilishe mazingira ya kukaa sio kila siku sehemu moja"...... "sawa bhana"


Pembeni ya meza waliyokaa walikuwa wamekaa madada poa, walikuwa aakipiga story, "mnamuona huyo msichana hapo namjua"....... "unamjua umemuona wapi?"...... "yule tumefanya naye sana kazi manzese"...... "acha bwana itakuwa umemfananisha"...... "kweli tena nakuapia"....... "mmmmmh sawa, kwahiyo siku hizi kaolewa au?"....... "malaya haolewi wewe nani yupo tayari kuwekwa ndani hapa?"....... "yaani niwekwe ndani nisile bata nani kasema?" wakacheka kicheko kile kilimstua jumaa akajikuta anawaangalia wale wasichana sana, mke wa hasan akasem "mume wangu naomba tuondoke inatosha kukaa hapa" hassa akasema "malizieni tuondoke zetu" walimalizia vinywaji na nyama kisha wakaondoka zao.


ITAENDELEA


0 comments:

Post a Comment

Blog