Search This Blog

Thursday 19 May 2022

MUWASHO - 5





    Chombezo : Muwasho

    Sehemu Ya Tano (5)



    Monica alijitahidi ili kuona kama ataweza kufanikisha zoezi lake la kumjeruhi Mernah aliyekuwa ana amini kuwa ndiye aliyetaka kumuuwa,

    "Seif naomba tuachane kwa amani wala sihitaji matatizo mengine tena kwani matatizo niliyoyapata kwa sababu nahisi yanatosha."

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dokta Ivete aliingilia kati na kuanza kuongea maneno yaliyokuwa siyo ya kumtia moyo Mernah japo aliyaongea kwa upole na mafumbo.

    "Siku zote ngazi ina mwisho na siyo kama tunavyosikia kuwa Dunia haina mwisho, kingine nataka nikwambie kuwa kukata tamaa saa nyongine ni vizuri kuliko kutaka ushindi utakaokuweka katika shimo la Giza milele."

    "Asante kwa maneno yako mazuri na yaliyo ujenga moyo wangu kwa zege,"

    Baada ya kuongea maneno hayo Mernah aligeuka na kuangalia mlango kisha akajiweka tayari kuondoka ila kabla bata hajapiga hatua alisikia kitu chenye ncha Kali kimemchoma ile kugeuka aliona ni Monica ameshikilia bomba la sindano akajua kuwa kilichomchomo ni sindano,

    "Monica siwezi kukuchukia wala kuona vibaya kwani mzigo wa mawazo ulioubeba Juu yangu huna ukweli nao,"

    Baada ya kuongea hivyo Mernah aliondoka zake na maumivu yake huku akiwa na mawazo tele Juu ya ya kuvunjika penzi lake na seif.

    ************

    Mambo yalikuwa mambo mkorogano ulikuwa mkubwa japo Mernah aliamuwa kujitenga Seif ila misuguano bado ilikuwa mikubwa kwani Dokta Ivete aliona bado ana kazi ngumu ya kujihakikishia kuwa Seif ni wake peke yake,

    "Seif mbona kama una mawazo ya mbali sana."

    "Nitaachaje kuwa na mawazo wakati siku tatu zimekatika bila kujua alipo Mernah,"

    "Sasa unataka ujue alipo ili iweje?"

    "Ili nijue kama yuko salama,"

    "Na ukiisha jua kama Yuko salama inakuwaje?"

    "Nitafurahi kama takuwa mzima kwani sipendi apate shida."

    "Atazipata tu shida mwaka Juu kwani kakutana na mkono wa Upanga,"

    "Hivi kakufanyaje mtoto wa watu mbona unamuombea mabaya,"

    "Alichonikosea nakijuwa mwenyewe,

    Maisha yaliendelea na hali ya Monica ilizidi kutengamaa na kurudi katika hali yake ya zamani, katika siku alizokaa pale kwa Dokta Ivete alikuwa akimuuliza ni nani aliyemleta hapo,

    " Dokta hivi ni nani aliyenisaidia mpaka nikafika hapa ukaanza kunitibu?"

    "Tulikuogota Mimi na Seif,"

    "Mlipajuaje pale nilipokuwa?"

    "Ni hadithi ndefu sana tuyaache tumshukuru mungu kuona unaendelea vizuri,"

    ************

    Upande wa uongozi ulikuwa ukihojiwa Juu ya taarifa za kapotea kwa mabinti wawili pale chuoni,

    "Sema ukweli hatujapata habari yoyote iliyo ya kweli kuhusu walipo Monica na Mernah,"

    "Hata funu funu hamna?"

    "Fununu zilizopo ni kuwa Monica aliuawa ila hatuna taarifa hizo kiundani zaitukn

    "Aliyeongea taarifa hizo ni nani huenda tukimuona tukafanya naye maongezi tutapata muongozo wa kupata ukweli,"

    "Tunashindwa kumsema kwa kuwa polisi tunawajua mnavyomchukulia mtu hatua hata kama hana kosa,"

    "Basi kama ni hivyo hamtaki kutuambia mhusika tutaondoka na wewe mkuu wa shule mpaka pale upelelezi utakapo kamilika,"

    "Mkitaka kufanya hivyo sawa si mko Juu ya sheria,"

    "Basi bila kutumia nguvu nyanyuka tuongozane,"

    Mkuu wa chuo hakubisha alitii kile alicho ambiwa akaongozana na maofisa wale wa jeshi,

    Wakati polisi wakitoka katika ofisi ya mkuu wa chuo tayari huko nje wanafunzi walikuwa na taarifa zote kuhusu mazungumzo yaliyofanyika huko ndani wakajipanga kuzuiya Mkuu wa Chuo asipelekwe polisi,

    "Hatukubaliiii..........."

    " hatukubaliiii..........."

    "Hatukubaliiii..........."

    Zilikuwa ni sauti za wanafunzi wakipinga mkuu wao wa chuo kupelekwa polisi,

    Polisi baada ya kuona wingi ule wa wanafunzi na kelele zao walitumia hakili ndogo wakafyatua risasi hewani kilichotokea ni kuwa wanafunzi walivaa polisi bila uoga na kuanza kuwapinga huku bunduki zao wakizitupa pembeni na kuziharibu haribu.

    Taarifa zilifika kituo kikuu cha polisi FFU wapatao mia moja wakatumwa chuoni ili kutuliza fujo na kuokoa Askari wenzao waliokuwa wakipokea kipigo cha umbwa mwizi.

    FFU walitumia nguvu kubwa sana kutuliza gasia katika eneo la chuo ila jitihada ziligonga ukuta kwani wanafunzi walikuwa moto zaidi ya FFU



    Hali ilikuja kutulia jioni kabisa majira ya saa saa kumi na mbili pale mheshimiwa Rais alipofika eneo la eneo la chuo na kuongea na wanafunzi wakamshitakia na kumwambia kile wanachokitaka,

    "Mnachokitaka tutakifanya kwani inaonesha kuwa polisi ndio wenye makosa cha kwanza polisi walikuja hapa bila kibari, cha pili waliwafyatulia risasi bila kukaa pamoja mkashauriana, kwa tunaomba radhi kama serikali pili tuko hapa kusikiliza kile mlichosema kuwa mnakihitaji,"

    Tuna taka wenzetu waliokamatwa,"

    "Sawa msihofu dk tano ni nyingi watakuwa hapa,"

    Wana chuoni na Raisi walielewana na kweli hali ilitulia na baada ya mda flani wale wanafunzi waliokamatwa waliachiwa,

    Askari wawili waliuawa na wengine walipelekwa hospital wakiwa mahututi sana,

    **************

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Siku zilikatika habari za fujo zilizotokea pale chuoni ikaanza kupotea vichwani mwa wanafunzi na RAIA wanaoizunguuka shule.

    Habari za fujo seif alikuwa anazijua vizuri sana na baada ya fujo kumalizika seif alikutana kantini na Skola na walikaa meza moja Skola akamuanza Seif kwa kumsabahi, toka kipindi kile Skola amfumanie Seif akiwa na mernah walikuwa hawakuwahi kusaliama wala kuwa karibu.

    "Seif habari yako,"

    "Nzuri za kwako?"

    "Namshukuru mungu,"

    Baada ya salamu kimya kingi kilifuatia kwani kila mmja alikuwa akiwaza aanzie wapi kumsemesha mwenzie, ila siku zote kidume ni kidume tu Seif alianza kutoa maneno machache kwenda kwa Skola.

    "Mbona umehadimika sana wangu? Nilijua uliisha maliza mwaka wako hapa chuoni,"

    "Nipo nimalize usijue?"

    "Nitaambiwa na nani?"

    "Mhhh na wengi mnaojuana,"

    "Kama nani?"

    "Mernah angekuambia,"

    "Mhhh... alafu kweli hebu nikuulize swali Skola na unipe ushirikiano,"

    "Swali gani?"

    "Mala ya mwisho kumuona Mernah wewe ilikuwa link?"

    "Ni siku zimepita,"

    "Huna fununu fununu labda,"

    "Sina Ila nilisikia kuwa aliuawa akiwa na Monica,"

    "Si kweli Monica hajauwa wala mernah kwakuwa juzi juzi nilikuwa nao wote na Mernah tukakwazana kidogo akaondoka kwa hasira hata siku tano hazijakwisha toka aondoke kwa hasira,"

    "Mhhh ulikuwa umewaficha au ilikuwaje ukawa nao bila watu kujua walipo?"

    "Ni story ndefu sana tuyaache hayo,"

    "Kwa nini tuyaachie njiani tuyazungumze yamalizike,"

    "Kuna yupo Monica anapata matibabu kwani alikuwa amejeruhiwa na muuaji,"

    "Muuaji ni nani?"

    "Simjui,"

    "Hukumuona"

    "Monica anadai aliyetaka kumuuwa ni Mermah ila siyo kweli kwani Mtu aliyempa msaada ni Mernah asingekuwa Mernah angekufa kwani mernah ndiye aliyeniita Mimi na kunielelekeza katika hako kapoli,"

    "Mhhh hapana inawezeka Monica anachoongea ni kweli kwakuwa walikuwa wao wawili tu."

    "Hapana sikubaliani na hilo kama ni hivyo kwanini aliniita ili tumpe msaada,"

    "Ni danganya Toto tu ila yeye ndiye muuaji na inabidi umtolee ripoti polisi."

    "Mimi mwenyewe namtafta alafu ni mtolee ripoti polisi,"

    "Una mtafta wa nini?"

    "Namtafta kwa kuwa ni mtu wangu,"

    "Ahhhh ila ripoti ni mhimu?"

    "Siwezi kumtolewa ripoti kwa kuwa najua hana hatia,"

    "Hana hatia wakatia wakati Monica anadai kuwa Mernah ndiye muuaji,"

    "Alisemalo halijui,"

    "Hali jui wakati yeye ndiye katendewa,"

    "Unayo ongea na wewe huyajui?"

    "Nayo ongea naongea kutokana na maelezo yako,"

    "Tuyaache hayo maongezi maana naona tutafika mbali,"

    "Kama atashindwa kutoa ripoti Mimi nitamsaidia kuitoa,"

    "Skola ukitaka kutibuana na mimi mguse Mernah utakuwa unatafta mengine,"

    "Acha niyatafte alivyonipola wewe anafikili nilifurahi?

    "Acha nikupe ukweli ni kuwa hakukupola bali wewe ulitaka kumpola,"

    "Seif nilikupenda na nitaendelea kukupenda,"

    Seif alinyanyuka akaondoka bila kusema chochote kile ila alikuwa akiwaza cha kufanya Juu ya Skola kwani aliona hana nia nzuri kwa kwa Mernah,

    *Naapa kutoa damu ya mtu yoyote atakae taka kumtemda vibaya Mernah*

    Akiwa katika hali ya mawazo alisikia simu yake inaita akaitoa mfukoni kujua nani anamtafta ila alipoangalia alibaini ni simu Monica kwenda Skola kutoka na setting alizokuwa amefanya.

    "Halloh Skola ni mimi Monica,"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Jamani like zenu ndogo ndio zinachelewesha hadithi hii. Like na koment yako ndio inaleta hadithi hii.

    Endeleaaa....

    "Hallow Skola ni Mimi Monica,"

    "Mke wangu vipi? Uko mzima?"

    "Kiasi chake swty,"

    "Kwanza niambie uko wapi jaman nije?"

    "Nilipo kufika ni rahisi si unapangumbuka kwa Dado?"

    "Ndio,"

    "Njoo moja kwa moja nyumba ya tano kutoka hapo kwa Dado, ila Dado hayupo nilienda kumuulizia wakaniambia kuwa alienda uswizi,"

    "Nakuja mke wangu,"

    Maneno waliyoongea yote Seif aliyasikia akajiuliza afanye nini kumzuiya skola asionane na Monica ila akakosa namna ikambidi atumie mpango wa kuwahi kwenda kuonana na Monica ili ajaribu kumsisitiza asijaribu kumfungulia kesi Mernah,

    Akiwa katika mawazo mengi sana akiwaza afanye nini simu yake iliita akayiangalia kisha akaipotezea kwani hakupenda kuingiza mambo mengi kwenye akili yake alitaka awaze afanye nini ili Mernah asishitakiwe,

    Simu iliita tena kwa awamu tatu bila Seif kuipokea ila baada ya kukatika alisikia SMS inangia kwenye simu, *afadhali kusoma SMS kulikoni kupokea simu*

    Seif aliishika simu kisha akaifungua SMS ile ila alipoisoma alioneka kupagawa akainuka haraka alipokuwalipofikaakatoka nje huku anakipimbia kama mwehu, SMS hiyo ilikuwa ikisema kuwa, *Nakupigia simu hupokei wakati unajua kazi uliyonipa? Mernah nimemuona nikajaribu kumzubaza ili nikupigie simu, nakupigia simu hupokei sasa hiyo itakuwa kazi kweli Mimi Niko hapa kichangani na nimemuona mazingira haya haya?*

    Seif aliongeza spidi ya miguu yake ili aone kama anaweza kuwahi kuonana na Mernah, alipofika barabarani alichukua Piki Piki ili awahi,

    "Dereva wahi vuta moto vuta moto baba,"

    Dereva Piki Piki wanavyopenda kukimbia na yeye kweli alivuta moto Piki Piki ikawa inatereza Juu rami utafikili inataka kupaa,

    Upande wa pili.

    Uoande wa pili Monika alikuwa akipiga story na Dokta Ivete ila baada ya mda wakasikia kengere ikiita kumanisha kuna mtu nje anabisha hodi,

    "Kuna mgeni sikia kengere hiyo,"

    "Ngoja nikafungue,"

    Aliyekuwa anagonga mlango hakuwa mwingine alikiwa ni Monica,

    "Karibu mgeni bila shaka wewe ndie Skola"?

    " ndio,

    "Karibu Monica yuko ndani,"

    "Asante,"

    Skola aliingia ndani ila akaonana uso kwa uso na Monica hakuamini kumuona akiwa mzima alimuangalia mala mbili mbili kisha akamkumbatia huku akisema,

    "Mke wangu pole sana....."

    "Asante vipi wewe umzima?"

    "Mimi mzima kabisa ila nilikumisi nikamisi zaidi penzi lako mpenzi wangu,"

    "Ndio hivyo na Mimi yalinikuta ya kunikuta nikachomwa chupa sehemu za siri ila mungu akanisimamia,"

    "Pole sana mamyto, ila nani alifanya haya yote?"

    "Mernah kwa ninavyoelewa na kwa nilivyosikia,"

    "Huyu Mernah tumfanye nini?"

    "Aaahh.... Ni kumuachia mungu tu,"

    "Khaaaa kumuachia mungu?"

    "Ndio,"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sikia Skola Mimi nikimuona nitamuulia mbali,"

    "Khaaa usifanye hivyo Skola,"

    Wakiwa wanaongea Dk Ivette alikuwa akiwasikiliza tu ila walipofika kwenye suala la kuuwa aliingilia kati na kusema,

    "Mbona mliisha muuwa mnappresha gani?"

    "Tumeisha muuwa?"

    "Ndio,"

    "Kivipi?"

    "Siku ya kesho hataimaliza duniani atakuwa amekwisha tayari kwani sumu aliyonayo mwilini mwake ni kali sana,"

    "Sumu,"

    ................ .......... ...............

    Upande wa pili self alijaribu kuwahi eneo aliloambiwa kuwa Mernah alionekana mda siyo mrefu,

    Alipofika aliangaza huku na kule bila matumaini yoyote yale akaamuwa ampigie simu yule jamaa aliyekuwa amempa kazi,

    Hallow niko maeneo haya uliyoniambia"

    "Njoo kwa mangi mchoma mbuzi,"

    "Sawa,"

    Alijisogeza kwa mangi na kweli akamuona wakakaa wakaanza kuongea,

    "Niambie vipi umemuona wapi mernah"

    "Brother kabla ya yote nikwambie kitu kimoja,"

    "Kipi?"

    "Yule binti ni wa kufa leo au kesho kwa hali aliyonayo,"

    "Unasemaje?"

    "Kama ulivyosikia..."

    "Kwani yukoje kiafya,"

    "Kachoka sana arafu yuko kama ka data kiaina,"

    "Hapana...."

    "Kingine nikuwa masera wamekuwa wakijipigia tu kwani hana akiri vizuri,"

    "Kujipigia nini?"

    "Wanafanya naye mapenzi,"

    "Etiiii?....

    " isitoshe mpaka masera wenye ngoma wamepita naye bila kings,"

    "Kheeeee......,"





    Seif alitaka kuchanganyikiwa baada kusikia kuwa kwa sasa Masera wanajipigia Mernah kilichomuuma zaidi ni pale aliposikia kuwa mpaka masera wenye ukimwi wamepita bila kinga,

    "Acha niendelee kumtafta si umesema kaelekea huku?"

    "Ndio,"

    Seif alianza kuyipiga mitaa kumtafta Mpenzi wake msichana aliyempenda sana ila tamaa na ngono vikawatengamisha ili hali bado anampenda.

    *kweli nilikukosea Mernah ila nahitaji msamaha wako kwani sijielewi mpaka sasa, matatizo yako yote yanayokukabili naamini mimi ndie chanzo umekuwa mwenda wazimu kwa sababu yangu, sura yangu niifiche wapi? Mbona naona Dunia imenikasirikia?*

    Seif na yeye taratibu alianza kudata na akajikuta anaanza kuongea peke yake barabarani bila kujitambua,

    Akiwa katika tembea tembea alimuona msichana aliyefanana na Mernah akamkumbatia kwa nguvu huku akisema,"

    "Mernah wangu kwanini ulinikimbia? Kwanini uliniacha peke yangu?"

    "Eehh mwehu nini? Hebu niachie,"

    Kazi haikuwa rahisi kumzuiya Seif asimnganganie binti huyo aliye mfananisha na Mernah wake, zilipita dakika kumi kasheshe ikiwa inaendelea mpaka alipofika yule kijana aliyekuwa amepewa kazi ya kumtafta mernah,

    "Oyi brother umekuwaje wewe mbona unafakamia watu usio wajua,?

    " aaahhh kumbe ni wewe, hebu sema ukweli huyu siyo Mernah wangu?"

    "Siyo yeye"

    "Ahhh kumbe siyo yeye?"

    "Ndio siyo yeye huyu,"

    "Oky acha niendelee kumtafta,"

    "Pouwa,"

    Seif alitia huruma alikuwa kama kadata vile kwani mambo yote aliyofanya yalikuwa ya kichizi chizi tu,

    Baada ya seif kuondoka yule Dada aliyefananishwa na Mernah alimuuliza yule kijana,

    "Kwani huyu kijana kawaje?"

    "Alikuwa na Mpenzi wake ila Mpenzi wake kwa Sasa ni chizi yaani mwenda wazimu na afya yake haiko vizuri wakati wowote ule anaweza kufa,"

    "Unaweza kuwa unaijua historia yawo?"

    "Hapana ila kuna anaijua aliniambia kuwa anasoma na seif chuo kimoja,"

    "Naomba unikutanishe Naye,"

    "Sasa twende kijiweni maana jamaa anakujaga kijiweni kuchukua ngada,"

    "Sawa,"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Upande wa seif aliendelea kuhangaika kumtafta Mernah wake kwani aliamini bila Mernah hawezi kufanya chochote kile,

    *Mernah umekwenda wapi mbona mboni zangu zinahitaji kukuona ili macho yangu yapate nuru ya kuona?*

    ********"******

    "Sumu?"

    Wote walisitaajabu kusikia sindano ya sumu,

    "Ndio sindano ya sumu, namaanisha kuwa ile sindano uliyomchoma siku ile wakati nakutibu ilikuwa ina sumu kali ndani,"

    "Khaaa Mimi Monica nimeuwa?"

    "Ndio, kwa hiyo dhamira yenu imekamilika,"

    "Ila sikutaka iwe hivyo,"

    Skola aliingilia kati akanena maneno yake kwa furaha sana,

    "Raha iliyoje jamani kusikia habari nzuri kama hii,"

    "Skola usifurahie kifo cha Mernah kwani kumbuka na yeye anahitaji kuishi,"

    "Ndio hivyo kuishi imeshindikana Sasa unata tufanyeje tuongee na mungu?"

    "Imeniuma sana kuona mkono wangu umefanya hivyo,"

    "Isikuume potezea tu Mpenzi wangu."

    Upande wa pili Mernah alionekana akiwa amelala katika ya barabara magari yakashindwa kwenda watu wakamzunguuka kujua kulikoni,





    Watu walikusanyika kujua kipi kimemkuta binti huyo ambaye ni Mernah,

    "Jamani kawaje huyu binti?"

    "Na sisi hatujui,"

    "Huyu binti ni kichaa,"

    "Mhhh jamani hata kama ni kichaa ndio hivyo barabarani?"

    "Jamani anaweza kuwa kichaa ndio ila inaonesha amefariki,"

    Kila mmoja alikuwa akiongea la kwake kama ujuavyo kwenye mkusanyiko wa watu wengi kukiwa na tukio kila mmoja anaongea la kwake,

    Wakati yote yakiendelea hayo alitokea kijana mmoja mtanashati mwenye muonekano mzuri mbele ya macho ya wengi akamuangalia sana Mernah na kwa umakini kisha akamsigelea akambeba kwa mikono yake miwili kisha akaanza kuzipiga hatua kuelekea kwenye gari yake watu wakabaki midomo wazi huku wengine wakijinongoneza,

    "Huyo ndugu yake au msamalia mwema?"

    "Mhh sijui labda nduguye mbona kamchukua kimya kimya?"

    Wengine nao walikuwa wakisema yao,

    "Inawezekana kweli akawa nduguye?"

    "Labda anamchukua kwa ajiri ya kafara huyo maana watu tuko tofauti kifikira na mtazamo,"

    Minongono ilizidi maneno mengi yakasemwa na machache akayasikia ila akapotezea akaendelea na mambo yake.

    ****************

    Upande wa pili Seif alizidi kuranda randa mtaani akimtafta Merinah wake asijue kuwa merinah ameogotwa na mtu asiye julikana na haijulikani mtu huyo amempeleka wapi,

    Akiwa katika hangaika ya kumtafta Mernah alipoteza simu akabaki hana mawasiliano yoyote na mtu,

    Seif alipotupa jicho upande wa pili alimuona msichana aliyefanana na scola akamva na kuanza kumpiga makofi yule binti akapiga ukelele wa kuomba msaada huku akisema,

    "Mwiziiii.......mwiziiiii.....mwiziiii.."

    Kelele zile zilizuwa taflani kubwa na watu wakaja wamejaa jazba wakaanza kumpiga Seif bila kumuhurumia nazani na wewe unajua vizuri jinsi mwizi anavyokabiliwa na raiya.

    ******************

    "Jamani habari za seif kuna mwenye nazo? Maana kakaa kimya sana,"

    Monica alihoji kuhusu seif na wote wakawa kama wametoka usingizini,

    "Mhhhh unajua kweli Seif hatuna habari zake hebu skola mpigie simu,"

    "Ngoja nifanye hivyo,"

    Walipiga ila simu haikuja na majibu yoyote yale.

    "Mbona hapokei simu?"

    "Mhhh... Dokta hebu jaribu wewe kumpiga,?"

    Dokta naye alipiga ila yeye akawa na bahati ikapokelewa japo haikupokelewa na Seif,

    "Hallow... Habari yako?"

    "Nzuri wewe nani unapokea simu ya mume wangu?"

    "Hunijui ila fanya haraka njoo hapa mtaa wa idirisa ka/koo mumeo anapigwa na nzengo anatuhumiwa wizi,

    "Nini wewe unachosema?"

    "Kama ulivyosikia, wahi"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Dokta alikata simu akawambia wenzie,

    "Twendeni nyie Seif anakufa huko?"

    "Kuna nini tena,"

    "Nitawambilia kwenye gari,"

    Safari ilianza ya kwenda huko aliko elezwa Dokta ila Monica na skola walikuwa wakitoa macho sana wakijiuliza kuna nini?"

    "Twambie basi presha zitatuuwa,"

    "Seif anashambuliwa na nzengo,"

    "Kwa kosa gani?"

    "Wizi wa kupora."

    "Wizi wa kupora mbona vioja hivi tena?"

    "Siyo vioja anaweza kuwa amesingiziwa,"

    *******************

    Seif alizidi kushambuliwa na wananchi na pale alipojitetea kuwa siyo mwizi hakuna aliyemuelewa.



    Kipigo kwa seif kiliendelea kuwa kikali sana mpaka ikafikia hatua ya kuonekana anaenda kuyiaga dunia,

    Tairi na mafuta vililetwa ili kumchomelea mbali Seif aliyekuwa anatuhumia kwa wizi, alivikwa tairi na kumwagiwa mafuta ila kabla kiberiti hakijahusika kuwasha moto mlio wa risasi ulisikika watu wote wakashituka kana kwamba walikuwa usingizini,

    Aliyetokea kutoa msaada hakuwa polisi hakuwa mgambo wala mwanajeshi bali alikuwa ni binti mdogo mwenye miaka 19 mwenye asili ya kihindi,

    Risasi ya pili ilisikika na kufanya watu kuanza kusambaratika kwa kuogopa kufa,

    "Wote tokeni hapo atae pinga nitampiga risasi,"

    Baadhi ya vijana wanaojiita wababe wa kitaa walijifanya hawasikii amri ile na kuendelea kubaki pale pale, binti wa kihindi alipoona wanasita kutoka alimpiga mmoja wao risasi ya mguu hapo ndipo wakaona kuwa kweli binti huyo yuko siriasi wakakimbia wote,

    Baada ya kutawanyika binti huyo aliwatishia vijana wawili kwa bastora na kuwambia wamuingize kwenye gari yake,

    Baada ya patashika za hapa na pale yule binti aliondoka eneo hilo akiwa na Seif ndani ya gari,

    *****************

    Scola, Monica na Dokta walifika eneo la tukio ila hawakumkuta Seif eneo hilo,

    "Atakuwa wapi?"

    "Tuulize,"

    "Si unaona watu wako makundi makundi tusogeye tusikilize wanayo zungumza,"

    Waliwasogelea na kuanza kusikiliza watu wanachozungumza, walianza kufuatiria maongezi ili kuona kama watapata muongozo wa kumpata Seif,

    "Kwa kipigo kile haponi mtu kabisa,"

    "Lakini kaperekwa hospital anaweza kupona,"

    "Aaaa.. Wapi si wakupona yule,"

    "Yule hata akipona atakuwa na kirema cha maisha,"

    "Hiyo ni kweli kile kipigo siyo cha mchezo,"

    "Amshukuru yule Demu wa kihindi kumchukua na kumpeleka hospital,"

    "Jamaa ana nyota huyo yule Demu sijui katokea wapi,"

    Monica na wenzie walienda pembeni wakaanza kujadili Yale waliyoyasikia,

    "Inaonesha kuna mtu amemchukua tena binti wa kihindi? wanajuana vipi?"

    "Hatuwezi kujua wanajuana vipi? Ila cha mhimu ni sisi kujiunga na kuwa kitu kimoja tukamtafta,"

    "Sawa,"

    *******************

    Upande wa pili Seif alifikishwa katika hospital ya Aghakan akapokelewa na manesi waliomkimbiza Chumba cha wagonjwa mahututi ila walipomfikisha mlangoni ilikuwa tabu kupokelewa,

    "Kuna mgonjwa wa jinsia tofauti humu,"

    Yule binti akahoji,

    "Inamaana mnachumba kimoja tu cha wagojwa mahututi?"

    "Hapana, kuna tatizo la kiufundi limetokea ndio maana tunatumia chumba hiki kimoja,"

    "Kwa hiyo nifanyeje? Mtu wangu afie hapa?"

    "Hapana ngoja tutoe gari ya wagonjwa wamuwahishe Regency Hospital,"

    Wakiwa katika mabishano ya hapa na pale Dokta Sharihiya kutokea nchini India aliamuru Seif naye aingizwe humo ndani apatiwe matibabu,

    "Muachane aingizwe humo, chukueni kitanda kingine mumuwe mgonjwa,"

    "Sawa,"

    "Arafu mwite Dk. Hamiyah aje amshugurukiye,"

    "Sawa,"

    Madaktari zaid ya kumi walijifungia humo ndani na kuanza kutoa huduma kwa wagojwa wote wawili,

    Binti wa kihindi alikaa nje kusubiri kujua hatima ya Seif itakuwa nini kupona au kufa,

    *Akipoteza maisha nitafanya nini? Mwili nitaupeleka wapi simjui ndugu yake hata mmoja?*

    *ila akiwa Muislam itakuwa rahisi nitatoa taarifa msikiti wowote ule watamzika,*

    *ila kwa baadae ndugu zake wakijua si nitakuwa kwenye wakati mgumu?*

    Akiwa katika mawazo mengi Dokta Hamiya alitoka nje akauliza,

    "Ndugu wa mgonjwa wa Mernah yuko wapi?"

    "Nipo,"

    "Na ndugu wa Seif?

    " nipo,"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sawa tuwe hapo hapo Dokta Sharihiya anakuja kuwajuza hali za wagojwa wenu,"

    "Sawa,". Wote waliitika.

    Baada ya Dakika tano Dokta Sharihiya alitoka akiwa na madokta wote waliokuwemo humo ndani, ila sura zao ziriashilia habari mbaya,

    "Ndugu zangu nasikitika kuwapa taarifa mbaya za wagojwa wenu siyo kosa letu kwani tumejitahidi kwa uwezo wetu ila tumeshindwa,"

    "Tupe majibu acha kuzunguuka,"



    MWISHO

 

0 comments:

Post a Comment

Blog