Search This Blog

Thursday 19 May 2022

PENZI LA SHEMEJI - 5

 





    Chombezo : Penzi La Shemeji

    Sehemu Ya Tano (5)



    Alex akiwa kituo cha polisi akiwa anapewa maelekezo yasiyoeleweka kwenye akili yake simu yake iliita.

    "Haloooo!!!..."

    "Baby nakufaaaaaaaa!!"sauti laini na ya kulalamika ilipenya kwenye ngoma za masikio yake.

    "Aaaaaah!!! Kisa nini? Na wewe nan?"akauliza kwa hamaki kidogo.

    "Jaman baby!..aaaaaaa! Mimi Lily! Nakufa mme wangu nisaidie tafadhali...."sauti ile ikaendelea kulalama.

    "Acha kulia basi unielezee kuna nini? Na kwa nini unasema unakufa?"akauliza

    Askari aliyekuwa naye pale kituoni akageuka kumwangalia kwa sababu ya kushtushwa na taarifa ile.

    "Baby wamenitapeli...aaaaaaa!!! Nakufa mie jaman"sauti ikendelea kulalama.

    "Okey tufanye hivi!...uko wap sasa hivi?"akauliza Alex.

    "Niko hapa uwanja wa ndege najiaandaa kurudi nyumbani"akajibiwa.

    "Kuna kazi nafanya hapa ila itabidi niiahirishe hivyo naomba dakika chache nitakuja huko! Si ulisema Masaki?"akasema Alex.

    "Ndiyo baby naomba uwahi tafadhali"akajibiwa

    "Sawa baby usijal! Ntakusaidia wala usiwe na wasiwasi"akajibu na ile simu ikakatwa.

    "Vip kijana kuna usalama?"akauliza yule askari.

    "Aaaaaah!!! Sijui niseme! Ila kuna msichana wangu mmoja hivi ni mfanyabiashara ndo anadai ametapeliwa"akajibu Alex.

    "Haapa Dar au yuko mkoani?"akauliza tena yule askari.

    "Yupo hapa Dar ila anafanya biashara na watu wa nje hasahasa huko Dubai"akajibu Alex.

    "Oooooh! Pole sana me nashauri tuongozane kwenda kumuona"akasema askari yule mwenye vyeo vyake.

    Wakati wanajadiliana pale simu ya mezani ya yule askari ikaita.

    "Eeee!! Ndiyo....mwambie aingie"akasema kisha akakata.

    Muda mfupi ofisi ikafunguliwa na wakaingia vijana wawili.

    Askari yule akanyenyuka na kupeana nao mkono kisha wakakumbatiana kwa furaha.

    "Poleni sana vijana wangu kwa maswaibu! Ila kalibu! Niwatambulishe kuwa huyu ndiye aliyetupa ile kazi ya jana na leo yuko hapa anaitwa Alex"akasema.

    Alex alisimama na kupeana mikono na wale vijaana.

    "Poleni sana vijana! Ila ndiyo kazi hiyo na mliyekuwa mnapambana naye si mtu wa mchezo kabisa"akasema Alex

    "Kabisa kaka hasa yule mwanamke!! Duuuuu!! Aisee ni noma sana kaka! Anatisha kama simba"akajibu mmoja wa wale askari.

    "Msijali vijana wangu ila vip mkikutana mnaweza kumfahamu?"akauliza Alex.

    "Lazima nitamfahamu kwa sababu mimi ndiye aliyenipiga kabari na kunitumia kama chambo"aakasema mmoja.

    "Swa kuna picha zake tunazo kwenye stoo yetu kule Dubai nitaziomba zije tuzitumie kumtafuta huku Dar"akasema Alex.

    "Wazo zuri sana sasa si tungeondoka tena niko na vijana wangu twende nao tumuone huyo mpenzi wako na hilo swala lako na kisha mimi nitawatoa vijana wangu kidogo waburudike! Unajua wamekaa sero akili yao imevurugwa"akasema askari mkubwa yule.

    "Sawa sawa mimi nina hao vijana wangu niliotoka nao ng'ambo ntakuwa nao kwenye gari yangu na wewe njoo kwa nyuma na hao wako"akasema Alex

    wakakubaliana na kutoka nje na Alex akapanda kwenye gari yake na wale vijana aliokuja nao huku yule askari akipanda na wale askari wake na safari ikaanza.

    Njiani Alex aliwaelewesha vijana wake wale kilichotokea mwanzo mpaka mwisho na wao pia wakabaki kushangaa uwezo wa Shamim.

    "Huyu mdada anapaswa atafutiwe gaidi kama yeye na mwenye uwezo mkubwa sana ndiyo itakuwa rahisi kumdhibiti"akasema mmoja wa wale vijana.

    "Kabisa! Kwa kweli huyo mdada hafai kabisa"akachangia mwenzie.

    Alex alinyenyua simu na kumpigia Lily akaelekezwa mpaka eneo husika.

    Lily au Shamim alikuwa akienda na wale vijana wake kama mpango wao ulivyotaka.

    Aliamua kumhadaa Alex kuwa kabiwa na kutapeliwa mzigo wake ili apata nafasi ya kutimiza kile alichokipanga.

    Ndipo alipoamua kumpigia simu na kumlilia kisanii na kumuomba aende kwake ili yeye atimize lengo lake kuu.

    Akiwa na vijana wake wle sita ndani wakisubiria ujio wa Alex ili watimize lengo lao walishangaa kuona gari mbili zikija uelekeo wa ile nyumba yao.

    Gari moja ilikuwa ya Alex na ile ya pili ya askari.

    Gari zile zilipopaki walishuka na wale askari na Shamim akapata nafasi ya kuwaona vizuri.

    "Tumekwisha! Tumekwisha! Hawa askari ni wale wa jana! Na jana sikubadili sura hivyo wananijua kabisa jaman!"akalalamika Shamim



    Lily alishtuka sana kuwaona wale askari ambao walikuwa wakimfahamu yeye na wale vijana wake pale nje wakiwa na Alex.

    "John utabaki hapa nyie wengine nendeni chumba cha wageni na kaeni tayali na silaha zenu kwa lolote litakalotokea"akatoa maagizo.

    Alisimama dirishani akachungulia nje kumwona Alex akishuka kutoka garini na wale askari.

    "Rama nahitaji utengeneze namna ya kutoweza kujulikana kwa yeyote yulekama itawabidi kuingia ndani kuonana na mimi kataa kuwa hali yangu si nzuri"akasema.

    Aliondoka na kwenda chumbani kwake na kupanda kitandani kisha akajikamuliza rimao za kutosha usoni mpaka macho yake yakawa mekundu kwa machozi kisha akachukua pilipili akatafuna nzima nzima.

    Ule ukali wa pilipili ukamuumiza sana na yeye akajikaza na kile kitendo cha kujikaza kikamfanya azidi kuwa mwekundu usoni na machoni pale.

    Rama aliingia chumbani na kuvaa nguo zilizochakaa sana kisha akavaa kapelo na kujiziba usoni kisha akatoka na kufungua mlango.

    "Kalibuni"akawaambia.

    Yeyote aliyemwona katika hali ile asingeweza kuamini kuwa yule ni yule kijana waliyekumbana naye usiku wa jana kwani alionekana kama mtunza bustani au mifugo tu wa nyumba ile.

    "Bosi wako yupo?"akauliza Alex.

    "Yupo chumbani"akajibu Rama.

    "Naomba uniitie"akasema Alex.

    Rama aliondoka huku akiendelea kukwepa kugongana na wale askari uso kwa uso mpaka alipoingia chumbani kwa Shamim

    Alikaa huko kwa dakika mbili kisha akatoka.

    "Amesema Alex kati yenu aingie ndani kwani hawezi kutoka"akasema Rama.

    Alex alinyenyuka na kuelekea chumbani kwa Lily huku Rama akitoka nje na mkasi kama anaenda kufanya kazi zake za bustani.

    Alex alipoingia chumbani alimkuta Lily kalala kihasarahasara pale kitandani ila akiwa kachakaa sana hasahasa usoni.

    Macho yalikuwa mekundu sana na machozi yalilowanisha usoni na zile shuka alizokuwa kalalia Lily.

    Shami alipomuona Alex alijidekeza na kunyenyuka akamkumbatia na wote wakaangukia kitandani.

    Lily alijiliza pale kimadeko na Alex akawa anampiga piga mgongoni akimbembeleza.

    "Nakufa baby wangu mimi! Sijui nitakuwa mgeni wa nani?"akasema Lily

    Alex alimuonea huruma bila kujua kuwa ule ni mchezo.

    "usilie mama nambie nini kimetokea tafadhali"akauliza Alex.

    "Kipindi kile tumeonana Dubai ndiyo nilikuwa nimeanza kushilikiana na wale jamaa! Hatukufahamiana sana ila tulifanya biashara vizuri! Walifikia hatua ya kuwa wananikopesha mzigo nakuja nauza kisha nawalipa"akaweka kituo na kuendelea kulia.

    "Tulia basi mama usilie nielezee nione namna ya kukusaidia"akasema Alex

    Na hapo ndipo alipopataka Shamim.

    "Juzi juzi kwa sababu nimewaamini wakanambia nichukue mzigo mkubwa sana kwa mara moja ili nijiepushe na gharama kwa sababu gharama zinakalibia kupanda sana na mimi nitakuwa nimepata faida nzuri! Nikakopa benki pesa nyingi sana na kuwatumia waniletee mzigo! Mama yangu weeeeee!! Aaaaaa!!"alielezea na kuanza kulia tena.

    "Nimetapeliwa Alex mpenzi wangu! Wamechukua pesa yangu yote na zile ofisi zao hazipo tena! Nilimtuma rafiki yangu huko alichokutana nacho ni utapeli mkubwa! Simu zao hazipatikani! Ofisi zao zimeshafungwa na hazifanyi kazi! Nimetapeliwa Alex na hapa nina mkopo wa benki na sina biashara nyingine! Najua benki watauza nyumba yangu baba nitabaki maskini mimi"aliendelea kulia mara baada ya kumaliza kusimulia.

    "Naomba nikuulize kitu Lily"akasema Alex

    "Niulize babaa"akasema kinyonge Lily.

    "Unanipenda sana mama?"akauliza Alex.

    "Ndiyo baba tena sana"akasema Lily

    "Kama unanipenda naomba uhamie kwangu na tuoane na kisha haya matatizo ni madogo nitayamaliza"akasema Alex.

    Shamim alimkumbatia Alex kwa nguvu na kumshukuru sana ingawa akiwa kwa nyuma wakati Alex hamuoni alikuwa akishangilia kumuingiza kwenye mtego kiulaini hivyo Alex.

    "Nashukuru sana baba! Nakupenda sana baba! Na niko tayali kwa lolote baba! Nakupenda sana"akasema Lily.

    Na akamvuta Alex kuja mdomoni kwake na kumbusu kwenye lipsi na mashavuni akikwepa kutoa denda ili ile pilipili aliyolamba isije kuhalibu kitu.

    "Haya mama jiandae twende hapo sebuleni kwako kuna rafiki zangu nikakutambulishe tafadhali mke"akasema Alex

    Shamim akashtuka!!

    Akawa kashikwa na hakuwa na ujanja!!!





     Lily alishtushwa na lile ombi la Alex la kwenda kuonana na wale wageni wake ambao yeye aliwatambua vizuri na wao wakimtambua.

    "Kwani lazima nionane nao sasa hivi?"akauliza Lily.

    "Yah! Ni vizuri kwa sababu huyo jamaa ni Askari na angependa akusaidie katika hili jambo lako"akasema Alex.

    "Hapana baby kwa hali niliyonayo sitaweza kwenda naomba tu uwaache waende kisha nikiwa sawa utanikutanisha naye! Siwezi kwenda kwao kwa hali niliyonayo"akasema Lily.

    " Huwezi jitahidi mama?"akauliza.

    "Hapana babaa itakuwa ngumu kwenda hivi nilivyo naomba kesho uwape appointment tutaonana"akasema Lily.

    "Haya mama nimekwelewa"akasema Alex.

    Alex aliondoka pale ndani na kurudi sebuleni alipowaacha wale askari na vijana wake.

    "Samahani kwa usumbufu bosi"akasema Alex.

    "Usijal vip shem mbona hajaja?"akauliza yule askari.

    "Kalia sana kaka na hali yake si nzuri,ameniomba niweke appointment na wewe kesho anaweza kuwa sawa"akajibu Laex.

    "I think atakuwa kachanganyikiwa! Naona tumpe muda akiwa sawa tutawasiliana ndgu yangu" akasema yule askari.

    "Haina shida kaka nasubiri akae sawa nitakupa feedback! Wish you the best"akasema Alex.

    Wale askari waliamka na kuagana na Alex kisha wakatoka.

    Shamim aliyekuwa kajibanza mlangoni akisikiliza kila kilichokuwa kikiendelea alishusha pumzi kwa furaha kuona shida imeondoka mbele yake.

    Mara baada ya Alex kuwaaga wale askari aliwaita vijana wake kutoka kwenye gari na kisha akaongea nao kidogo na kuwaaga waondoke eneo lile.

    Mara baada ya kuondoka Alex alirudi ndani na kumkuta Shamim kalala pale alipomuacha.

    "Vip mama unajisikiaje?"akauliza Alex.

    "Bado siko poa ila naomba unichukulie hapo nje dawa zozote za kupunguza maumivu"akasema Shamim

    "Poa mama"akajibu Alex.

    Alex akaondoka na kutoka akapanda gari na kuondoka.

    Mara baada ya Alex kuondoka Shamim alitoka chumbani na kwenda kwenye chumba alichowaweka vijana wake wale wengine.

    "Faster kuna kazi inahitajika ifanyike"akasema.

    "Kazi gan bosi?"wakauliza.

    "Nyie wawili naomba haraka sana muondoke John ameweka sign kwenye zile gari za askari hivyo mtaitrack na kuwafatilia kisha nipeni majibu ya kila nyendo zao! Yule kiongozi wao hatufahamu ila wale vijana wanatufaham wote! Na kesho napaswa nionane naye kesho sasa tunapaswa kuondoa wale vizuizi mapema ili kazi ibaki rahisi! Kumbuka napaswa kuwa mke wa Alex as soon as possible ili tufanikishe kuzipata mali za bosi"akasema Shamim.

    "Umesomeka bosi"akajibu.



    **********



    Askari Julius Mwita aliyekuwa kamanda wa polisi na mkuu wa kituo cha polisi Oysterbay akiwa na vijana wake walipotoka kwa Alex walielekea mpaka bar moja maarufu Kinondoni na kukaa kupata kinywaji.

    "Sherekeeni vijana wangu! Mngepatwa na matatizo kwa sababu yangu bana! Ila mshukuru yameisha"akasema Afande Mwita.

    "Ila bosi hii kesi ilikuwa mbaya sana na ingekukalia vibaya! Shukuru Mungu tulielewana tusifungue mdomo kabisa"akajibu mmoja.

    Wakaendelea kunywa bia kwa muda mrefu sana kwa pamoja wakipiga stori mbal+mbalia huku wakipeana matumaini ya kuwakamata wale magaidi!

    Walikaa eneo lile mpaka jioni ila yule Mkuu wao akaondoka na kuwaacha wakiendelea kupombeka.

    Saa nne za usiku walikuwa njiani kuelekea nyumbani kwao na kwa bahati nzuri wote walikuwa wakikaa kwenye kota za pamoja hivyo waliongozana kutoka eneo lile.

    Nyuma yao kuna mtu alikuwa akiwafatilia akiwa na lengo moja peke yake kuwamaliza na kupoteza ushahidi muhimu ambao alihisi ungeweza kumzuia kuifanya kazi yake kwa uhuru.

    Walikodi gari ndogo na moja kwa moja ikawapeleka kwenye makazi yao.

    Yule aliyekuwa akiwafatilia alikuwa na pikipiki ya kumsaidia hiyo na yeye alipanda ile pikipiki akiwa nyuma yao.

    Dakika chache baadae walikuwa wakishuka kutoka kwenye ile gari ya kukodi.

    Walipomalizana na yule dereva waligeuka na kuanza kuelekea makwao.

    Ghafla mbele yao alitokeza mwanamke akiwa kavaa nguo nyeusi!

    Kila mmoja alimwangalia kwa makini na ghalfa wakamtambua!!

    Walipomtambua kuwa alikuwa Shamim pombe yote ikawaisha!





     Hakuna aliyeamini alichokiona mbele ya macho yake kati ya wale askari wote wanne waliokuwa pale.

    Pombe yote iliwaisha na wakajikuta wakishikwa na wahka mkubwa juu ya kile kilichokuwa kinatokea mbele yao.

    Shamim hakuwapa nafasi ya kufikilia mara mbili kabla shingo ya mmoja wao haijadondoka chini na kuuacha mwili umesimama wenyewe bila balance na baaada ya muda ukadondoka.

    "Uwiiiiiiiiiiiiiiiiii!!!!" kelele ilimtoka mmoja wao na kuwashtua askari waliokuwa kalibu na makazi hayo yao ambao hawakuwa na shfti ua usiku kwa siku hiyo.

    Shamim aliruka na kumdaka mwingine na kumnyonga huku wale wengine wakipata nafasi ya kukimbia.

    Kukimbia kwa wale kabla hajatimiza lengo kilikuwa kikwazo kwake kwa sababu walienda njia tofauti tofauti.

    Akaamua kumfata yule ambaye jana yake alipiga kabali na kumtumia kutoloka wakati wakiwa na wenzie.

    Akamkimbiza kwa speed kubwa na ya ajabu na kwa sababu yule alikuwa anakimbia huku akigeuka nyuma Shamim akawahi kumshika na kumpa vitasa vya uhakika na yeye akatulia kimya.

    Teke kali la mbavu ndilo lililomshtua Shamim kuwa kuna hali nyingine isiyoya kawaida inayojitokeza eneo lile.

    Aliponyenyua uso wake alikutana na njemba nyingi sana zikiwa zimemzunguka pale chini alipofanyia mauaji ya yule askari.

    Akageuka ili afikilie cha kufanya kupambana nao ila akakutana na ngumi moja ya shavu yenye ukubwa wa jiwe.

    Akahisi kuona nyota nyota!!

    "We unajiamini nini kuweza kumuua askari? Pole sana! Umeingia choo cha kike binti"hayo yalikuwa maneno ya mwisho Shamim kuyasikia kabla hajapoteza fahamu zake.



    ******



    Alex alipotoka kununua dawa ile alirudi kule nyumbani kwa Shamim na kupaki gari kisha akaingia ndani.

    "Samahani kaka dada ametoka muda si mrefu"akasema yule kijana wa Shamim aliyejitengeneza kuwa msaidizi wa kazi za nje.

    "Haaaaaa!!!! Ameondoka? Si alikuwa na hali mbaya? Na kwanini ameondoka?"akauliza maswali mfululizo.

    "Kuna simu ya ghafla alipokea kuhusu hilo swala lake la mzigo uliopotea nahisi kwa sababu amechanganyikiwa ndo maana akatoka hata bila kukuaga"akajibu yule kijana.

    " Dah!!! Atachanginyikiwa sasa!! Nimemwambia atulie hiyo pesa kwangu sio shida!! Dah!! Haya acha mimi niende! Akirudi mwambia tuwasiliane"akasema Alex.

    "Poa haina shida bosi nitamfikishia taarifa"akajibu yule kijana.

    Alex alirudi kwenye gari yake akapanda na kuondoka.

    Alipoondoka tu vijana wale waliobaki pale ndaani wakachukua pikipiki na kuanza kumfatilia taratibu ili kujua nyendo zake zote kama walivyoagizwa na Shamim alipoondoka kuwafatilia wale vijana askari waliokuwa na uwezo wa kuwatambua.

    Alex alipotoka pale aliamua kwenda moja kwa moja nyumbani kwake kwa sababu tangu ametua nchini alikuwa hajafika pale kwake.

    "Tukutane Mikocheni! Tafuteni mwenyejiawalete"aliwataarifu wale vijana wake aliotoka nao Dubai.

    Aliendesha gari mpaka kule kwake na wale vijana akawaelekeza mpaka wakafanikiwa kuja pale nyumbani.

    Walipofika uchunguzi walianza kufanywa kwenye camera zote pale ndani na kwa bahati mbaya picha zote ziligandishwa na hivyo hawakupata chochote cha kuwasaidia.

    Walianza kurekebisha kila sehemu iliyokutana na dhahama ya Shamim wakati wa shughuli ile ya uhakika.

    "Mambo yameenda tofauti na tulivyotarajia inabidi tuwataarifu bosi huko na tuandae utaratibu wa nyie kurudi mapema"akasema Alex

    "Mimi nafikiri swala la sisi kuondoka lisiwepo mpaka pale tutakapompata huyu malaya! Na uhakika yupo hapahapa nchini bado"akajibu mmoja wa wale vijana.

    Waliendelea kujadiliana mpaka walipofika mwafaka Alex akawaaga na kwenda kulala ili apumzike uchovu wa mizunguko ya safari na ya siku ile.

    Alilala mpaka usiku ndipo alipopata naafasi ya kamka.

    Cha kwanza alichokumbuka ni kuwasiliana na Lily au Shamim lakini alipopiga ile namba yake ya simu haikupatikana kabisa.

    Akahisi labda kuna mambo yanaendelea upande wake hivyo anapaswa kumwacha atulie kisha atamtafuta.

    Alipofika sebuleni simu yake ya mkononi ilianza kuita.

    Alipoangalia mpigaji alikuwa yule Afande Mwita.

    "Vip kamanda!? Nilikuwa nimelala ndo naamka hapa?"akasema Alex.

    "Naomba uwahi kituoni haaraka yule mwanamke amekamatwa.alikuwa akiwaua wale askari waliomteka jana! Na amefanikiwa kuwaua watatu ila mmoja kakimbia! Kwa sasa yupo njiani akipelekwa kituoni chini ya ulinzi mkali na uhakika this time hawezi kuleta mchezo!!"aliongea kwa kujiamin askari yule.



    "Una uhakika kuwa mmemkamata ndugu yangu?"akauliza Alex.

    "Ninavyoongea hapa gari iliyombeba iko hapa mbele yangu na tunaelekea kituoni"akasema afande Mwita.

    "Mmewatarifu viongozi wenu juuu ya kukamatwa kwake?"akauliza Alex.

    "Hatujawataarifu ila najua wanaweza kuwa wamezipata taarifa kwani mawasiliano yetu yanatumia redio calls hivyo ripoti ya kukamatwa kwake imesambaa kwa sababu alikamatwa na askari ambao hawakuwa doria kwa sababu mauaji aliyafanyia kwenye kota za polisi"akasema afande Mwita.

    "Kwa hiyo uwezekano wa kuzuia ripoti isifike kwa wakubwa ni ngumu"akauliza Alex.

    "Itakuwa ngumu kaka yangu kwani wewe ulimtaka bila asifikishwe kwa wakubwa? Au ulimtaka mwenyewe?"akauliza afande Mwita.

    "Huyu mwanamke anatakiwa na wakubwa zangu huko Dubai kwa sababu kuna mambo makubwa sana kayafanya huko mabaya!"akasema Alex.

    "Alifanya nini? Au alifanya mauaji?"akauliza afande Mwita.

    "Ndiyo alifanya mauaji kwa bosi mkubwa wa kampuni yetu"akasema Alex.

    "Nikushauri iweke wazi hiyo kesi ili hata wakubwa waifahamu na aweze kusafirishwa kwenda huko kujibu hayo mashtaka"akasema afande Mwita.

    "Itakuwa ngumu kwa sababu huko kesi ni za drug kaka! Tunafanyaje?"akasema Alex.

    "Basi fanya kitu kimoja! Njoo mpaka kituoni tutajua cha kufanya"akasema afande Mwita.

    "Nimekwelewa ila nakuomba muwe makini sana kwani huyo mwanamke ni zaidi ya hatari kaka"akasema Alex.

    "Usijal kaka,tuna gari mbili na askari zaidi ya kumi hivyo hana uwezo wa kututoka kirahisi "akasema afande Mwita.

    "Sawa kaka nakuja muda si mrefu"akasema Alex.

    Mara baada ya kuongea na yule askari Alex aliwaita wale 7ijana wake na kuwapa taarifa ya kila kilichotokea.

    "Una uhakika wamemkamata?"akauliza mmoja wao.

    "Amenihakikishia kabisa"akajibu Alex.

    "Mimi nina ushauri bosi"akasema mmoja wao

    "Ushauri gan? Tuna dakika chache saana kabla hatujaondoka"akasema Alex.

    "Mimi kama kuna mtu simwamini basi ni huyu mdada! Wakati mwingine huwa nadhani ni shetani! Au mzimu flani"akasema yule kijana.

    " Nenda kwenye point yako"akasema Alex.

    "Shamim can do anything at any time bosi! Naomba kumbuka kuwa huyu mdada alikamatwa na hao hao askari jana usiku na akawaacha bila harama hata moja! Sasa anaweza shindwa kuwaumiza na kuondoka? "akasema yule kijana.

    " Sawa nimekwelewa ila sijajua point yako ni nini hasa?"akasema Alex.

    "Namaanisha badala ya kwenda kituoni kufatilia hili swala mara baada ya wao kufika! Basi tuwafatilie hawa watu njiani ili yule shetani akileta shida yeyote tuwe kalibu kumdhibiti"akasema ule kijana.

    "Lakini bosi mimi nina wazo tofauti"akasema kijana mwingine.

    " Lingine tena? Mimi wazo lako nimelipenda kuliko kawaida Shamim haaminiki kabisa! Tunapaswa tufatilie kuwapa ulinzi"akasema Alex.

    "Bosi mimi wazo langu ni tofauti kabisa"akasema.

    "Wazo gan?"akauliza Alex.

    "Sisi shida yetu sio yeye afike polisi salama! Shida yetu ni kumpata na kumpeleka kwa mabosi! Sasa kwanini tusivamie msafara kabla hawajafika polisi tumchukue na kutafuta namna ya kuondoka naye kwenda nje"akasema

    Wazo lile likwa jema kuliko lile la kwanza kwa sababu shida yetu sio afike polisi bali kumpata! Sasa vip mnaweza kuwamiliki askari kumi?"akauliza

    "Hiyo ni kazi ya sekunde chache sana na ndo maana nkakwambia Shamim anaweza kuifanya bosi naomba tuwahi"akasema

    Pale pale wakajiandaa na kubeba vifaa vyao vya kazi ambavyo waliamini vinaweza kuwasaidia kumaliza kazi ya kuwasimamisha wale askari na kumchukua.

    Walichukua kompyuta zao na mtaalam wa kompyuta akaitrack simu ya yule askari na wakapata kufahamu walipofika na njia waliyotegemea kupita.

    Walipanda gari zao na safari ikaanza kwa speed ya ajabu kuelekea eneo husika wakati huo huo wakawa wanaendelea kuifatilia ule msafara kwa kutumia kompyuta.

    Baada ya dakika kumi walifika Mikocheni na kushika njia ya kupandisha ili waiwahi ile gari ya askari.

    "Cha ajabu naona msafara umesimama mita mia mbili hapo mbele"akasema

    Wakaongeza kasi ya gari ile na kwa mbele wakafanikiwa kuziona zile gari za wale askari zikiwa zimesimama.

    Wakatoa silaha zao na kwenda kichwa kichwa huku wakipanga kufyeka yeyote watakayemuona pale.

    Maajabu yakatokea mbele yao!!

    Walikuta gari zikiwa zimesimama huku pakiwa kimya.

    Waliposhuka kukagua walikutana na miili ya wale askari ikiwa imezagaa sana huku wengine wakiwa wamekufa na wengine wakiwa hoi.







     Afande Mwita akiwa kwenye gari ya nyuma ya ile iliyombeba Shamim alifanikiwa kuona yale mapambano ya Shamim na wale askari wake ambayo yalifanyika kwa sekunde chache sana na kwa kasi ya ajabu.

    Kabla hajanyenyua mdomo wake kusema chochote kwa wale askari aliokuwa nao kwenyeile gari Shamim alikuwa keshawazimisha askari wote aliokuwa nao kwenye ile gari.

    Afande Mwita alikiri moyoni kuwa yule hakuwa binadamu wa kawaida kutokana na kasi aliyoitumia kupambana na vijana wake.

    "Afande anawamaliza wenzetu"alishtuliwa na sauti ya dereva wake aliyeshuhudia pia yale mapambano wakati huo yeye alikuwa kwenye lindi la mawazo akiwaza na kujalibu kumtafsiri yule kiumbe aliyekuwa akipambana pale.

    "Ni jini kweli? Shetani au mtu? Mbona sijawahi kuona binadam mwenye kasi ya ajabu kama ile Mungu wangu!"aliwaza mwenyewe akilini.

    Breki za gari yake ndizo zilizomzindua kutoka kwenye yale mawazo ila kabla yeye na vijana wake hawajashtuka na kuamua nini cha kufanya kukabiliana na ile hali.

    Mabomu ya machozi kutoka kwa vijana wa Shamim yalidondoka pale walipopaki gari.

    Hali hiyo ikazidi kuwachanganya zaidi kwa sababu walibaki kupambana na ile gesi huku wakiwa hawaoni chochote kile kwa wakati huo.

    "Bosi tukimbie atatua"akasema askari mmoja.

    "Ukimbie wewe unaona? Mimi sioni kabisa na huko unakoelekea je akiwa yuko huko?"akasema afande Mwita.

    Shamim alipowamaliza wale askari waliokuwa naye kwenye gari alichupa na kutua mbele ya ile gari na kuonana uso kwa uso na dereva na askari wawili waliokaa naye pale mbele.

    Wakati akijiandaa kuwakabili vijana wake wakatokea na kurusha bomu la machozi mpaka kwenye hiyo gari na mmoja wao akamrushia Shamim mask ya kuficha sura isidhulike na ile gesi.

    "Tumemaliza kazi bosi tuondoke"wakamwambia Shamim.

    "Kwenda wap? Nyie zinawatosha?"akauliza Shamim

    walibaki wamepigwa na butwaa bila kumuelewa.

    "Hawa askari wote ni kama wananifahamu kwa sababu wameniona! Sasa wanapaswa kutokuishi"akasema Shamim.

    Wakati vijana wake wakiitafakari ile kauli ya bosi wao Shamim alimpokonya mmoja wao silaha na kisha akaifunga kiwambo cha kuzuia sauti naaa kisha akazunguka mpaka kwenye ile gari.

    Alianza kuwamiminia risasi bila mpangilio na hata aliyejalibu kukimbia hakufika mbali kabla risasi hazijauchakaza mwili wake.

    Alihakikisha askari wale wote amewamaliza wote ndipo akaanza kuwakagua na aliporidhika akaondoka na vijana wake eneo lile.

    Wakiwa njiani kwenye gari yao walipishana na Alex akiwa na vijana wake wakielekea kwenye eneo la tukio.

    "achana nao wewe endesha gari twende"akasema Shamim



    *****



    Alex alibaki amechanganyikiwa haamini kile alichokuwa anakiona.

    Aliwasha tochi ya simu yake na kuanza kuwakagua vizuri wale askari waliokuwa wamezagaa pale chini.

    Akiwa katika kuwakagua alimpata Afande Mwita akiwa anagaagaa akitaka kukata roho.

    Alijalibu kumshtua aone kama anaweza kusema chochote kile ila hakuwa na cha kuongea.

    "Huyu mwanamke ni zaidi ya shetani kwa anayoyafanya"alijisemea Alex.

    "Ila kama unakumbuka walikwambia kuwa kuna sehemu alishikiwa na askari wasiokuwa wa doria labda twende kule tutawapata waliomuona vizuri na wao wanaweza kuwa msaada katika kumpata yeye"akashauri kijana mmoja.

    Alex akatafakari kwa muda kisha akakubaliana na lile wazo.

    "Wazo zuri walisema ni katikati ya Mwenge na Sinza hapo naomba twende haraka hata tusije kukutwa hapa na askari tukawa washukiwa"akasema Alex.

    Wakageuza gari na kisha safari ya kuelekea eneo hilo ikaanza.

    Dakika chache kutokana na umbali wa kutoka eneo lile mpaka Mwenge kutokuwa mkubwa wakawa wamefika.

    "Samahani kuna askari wa hapa walimkamata mwanamke muuaji naweza kuwaona?"alimuuliza mmama mmoja aliyemuona nje

    Cha ajabu eneo lile walikuta watu wamejaa sana huku vilio vikisikika.

    "Kakangu hapa kuna matatizo"akasema huyo mmama.

    "Sawa ila shida yangu ni mmoja katiya hao askari mama"akasema Alex.

    "Yaani kijana wangu hao unaowaulizia wameuawa muda si mrefu hapa ndo maana unaona vilio na kelele"akajibu yule mama.

    Alex akachoka akili!!!





    Range nyeusi iliyotengenezwa katika muundo wa ajabu kwa ndani ikiwa na uwezo wa kubadilishwa kwa ndani na kuwa kama ofisi ya IT ikiwa na kompyuta nne kubwa na na vifaa vingine vyenye uwezo mkubwa katika teknolojia ya ksasa zaidi vikiwa vimeunganishwa na satelite ya kisasa zaidi ikiwa na mifumo mikubwa ya GPS na datalearner za kutosha zilizowawezesha vijana wa Shamim waliobobea katika utaalamu wa kuchezea mitambo ya kisasa zaidi ya kitekenolojia ya kompyuta lakini gari hiyo hiyo kwa nje gari ile ilikuwa gari ya kawaida sana katika macho ya watu.

    Ilikuwa na uwezo wa kubadilishwa na kurudi katika hali ya kawaida kabisa ikiwa na siti zake za kawaida za kuweza kutumika kawaida na watumiaji ila kwa upande mwingine ikiwa na uwezo wa kubadilishwa na kuwa ofisi hiyo ya IT.

    Vijana wa Shamim kwa zaidi ya masaa ishilini walikuwa wakishinda katika ofisi au gari yao hii kuangalia kila kitu kinachoweza kuwa msaada mkubwa sana kwao.

    Gari ilizidi kuchanja mbuga kutoka maeneo yale waliyofanya mauaji ya askari wale waliokuwa wamemteka Shamim.

    "Tuelekee Mwenge nilipokuwa nimekatamitwa"akasema Shamim.

    "Bosi haitakuwa hatari kwako? Na kwanini unaelekea kule?"akauliza kijana mmoja.

    "Nahitaji kuishi na Alex na kukamilisha kazi ya bosi hivyo sipaswi kuacha mtu yeyote yyle aliyepata nafasi ya kuiona sura yangu"akasema Shamim

    "How many ?"akauliza yule kijana.

    "Twenty three"akasema Shamim.

    "Utawapata vip? Na kila mmoja anaishi kwake? Na pia kuna ambao hawakutoka? Huoni kuna hatari?"akasema Kijana yule tena.

    "Saa yangu ilifanya kazi yake kama kawaida kwa kutumia GPS nitawapata ndani ya sekunde chache sana kisha tutaondoka kumtafuta yule aliyetoloka"akasema Shamim

    "Poa bosi"akajibiwa.

    Gari ikageuzwa na kuelekea Mwenge kwenye zile kota.

    Dakika chache baadae walikuwa wameshafika eneo lile.

    Shamim alivishwa tayali kwa aili ya kazi mwili mzima ukiwa na nguo nyepesi nyeusi yenye uwezo wa kuzuia risasi kupenya.

    Alitoa saa yake na kuanza kusoma maeneo waliyokuwa wakipatikana adui zake.

    Akaanza kazi ya kuua mmoja mmoja kimya kimya bila kushtukiwa na akawa ameanza na wale waiokuwa na ndoa kwa kuishi wenyewe.

    Hao hawakumpa wakati mgumu wowote ule ila tabu ikawa kwa wale waliokuwa wakilala na wake zao.

    Ilimbidi kupuliza hewa kutoka kwenye kakopo kake kadogo ndani ya chumba mpaka wale walale ndipo alipoingia na kumgeuza mwanaume kichwa nyuma.

    Wote aliowaua aliwaua kwa style ya aina moja ya kuwageuza shingo zao na kuzivunja kwa kuzigeuza kuangalia nyuma.

    Nyumba ya mwisho ndiyo iliyomletea kizaa zaa kwani mke wa jamaa alikuwa katoka kwenda uani na yeye akajua ni bacherol hivyo akaingia kichwa kichwa na kumvunja shingo.

    Kwa bahati mbaya wakati anamvunja shingo mke wa huyo askari ndiyo akawa anarudi ndani na kumkuta akimalzia.

    "Mamaaaaaaaaaaaaaa!!!"alipiga kelele yule mwanamke kwa woga sana.

    Shamim alishtuka kuona mtu mwingine ndani ya kile chumba wakati mitambo yake ilimwonesha kuwa hakuna mtu tofauti na yule askari.

    Alitulia kwa sekunde chache akitafakari hatua ya kuichukua.

    Wakati yeye akitafakari tayali askari wengine jasiri na shapu wakawa wameshaamka kutokana na zile kele za yule mdada.

    Shamim akataka kumkabili yule mdada ammalize ila kwa sababu ya giza akaamini hatakuwa amemuona sura hivyo akatafuta nhia ya kutosha.

    Alimfata yule mmama na kumbinya kwenye mshipa wa fahamu shingoni akatulia kkwa kupoteza fahamu.

    Shamim aliona dari ikiwa na nafasi ya kupanda na yeye akapanda juu ya celling board na kujificha.

    Alipoangalia kwenda kwa mbele akaona mwanga kwa mbali kwnye ile dari.

    Akaanza kujikunjua na kutembea kwenye ile dari akielekea kule mwanga ulipokuwa.

    Alinyata huku akisikia kelele za watu wa eneo lile mara baada ya kuanza kugundua kuwa askari aliyeuawa kuwa si mmoja bali ni wengi.

    Alijitahidi kutoshtukiwa kabisa mpaka akaufikia ule mwanga.

    Alipochungulia eneo lile akaona kwa nje.

    Kuna gari aliiona ikiwa imepaki eneo lile ikabidi awashe saa yake na kuivuta kwa kalibu.

    "Mmmmmmmh!!! Alex???? Baalaa hili sasa!!"akawaza.



    "Hayaaaaa!!! Alex huyooo!! Nitatokaje?"alijiuliza Shamim akiwa pale juu ya daro.

    Aliangalia upande aliosimama Alex na upande waliosimama wale askari zilikuwa pande mbili tofauti kabisa.

    Kwa sababu hiyo alipaswa achague ni sehemu gani nyepesi ya kshukia!!?? Ni ule upande walipo askari wakiwa wamezagaa sana?? Au ni kule alipo Alex.

    Wakati yupo kwenye lindi la mawazo ya uamuzi alishangaa kuona vijana wanne walioonekana kuwa na asili ya Kiarabu wakitoka kwenye gari na kusimama pembeni ya Alex wakijadiliana naye kitu.

    "Mmmmmmmh!! Bora askari wa Kibongo uwezo wao ni wa kawaida sana! Waarabu tena??? Hapana sitaki shida"akawaza.

    "Bosi tunaachia mabomu ya machozi ili kuwatawanya hawa utoke"earphone ndogo alizovaa zilimpa ripoti kutoka kwa vijana wake.

    "Hapana!! Msifanye hivyo! Toeni gari eneo hilo na muelekeeo wa kaskazini nitawakuta huko"akasema Shamim.

    "Hapana bosi hawa askari ni wengi sana hatuwezi kukuacha peke yako bosi"akasema kijana wake.

    "Nyie ndiyo mnaopambana au ni mimi?"akauliza kwa hasira.

    "Ni wewe bosi lakini ni wengi sana bosi!!"akajibiwa.

    "Upo hapa kwa amri ya nani?"akauliza tena kwa hasira.

    "Yako bosi"akajibiwa.

    "Fanya kama nilivyoagiza"akasema shamim.

    "Sawa bosi na samahani"akajibu kijana.

    Shamim aliwaondoa wale vijana pale kwa sababu yeye alishawaona akina Alex ila wale vijana wake walikuwa hawajawaona na aliogopa wanaweza kuonekana na ikamletea shida.

    Mara baada ya kumaliza kuwasiliana na vijana wake Shamim alichana sehemu ndogo yenye celling board na kushukia ndani ya chumba kimoja.

    Aliposhuka alijalibu kufungua mlango wa kutokea nje ya kile chumba na kufanikiwa kukuta mlango umeegeshwa!

    Alipotokeza kwenye korido ndefu ya jengo lile kwa bahati nzuri aliiona Main switch ya jengo lile.

    Akaenda na kuizima kisha akakata waya kadhaa ili wasifanikiwe kuiwasha tena.

    Alitulia eneo lile na kusubiri kwa muda

    Kama alivyotazamia askari kiherehere alijileta eneo lile ili awashe umeme ule.

    Askari yule alikutana na ngumi moja ya shingo kwenye mishipa ya fahamu !! Akatulia chini!!!

    Shamim akamvuta taratibu mpaka kwenye kile chumba na kumvua mavazi ya kiuaskari na kisha akayavaa juu ya yale ya kwake.

    Kwa bahati nzuri kwake pia yule askari alikuwa na kofia ya kawaida aliyokuwa kavaa! Hivyo akaichukua na kujifunika.

    "Hii ni silaha yako ya mwisho! Katika mafunzo haya ambayo nimekuwa nikikupa wewe na wenzio Abdul na Majid,nimetokea kukupenda wewe! Ndiyo sababu ya kukupa hii zawadi! Huu ni unga unga ambao ukikutana na hewa tu unaanza kusambaa taratibu! Kadri unavyosambaa ndivyo unavyochanganyikana na oksjeni! Mtu yeyote atakayekuwa kalibu akifanikiwa kuuvuta atapoteza fahamu pale pale na asipowahi kupewa matibabu mishipa yake inaweza kupasuka na damu kuvuja na mwishowe anaweza kufariki!"aliyakumbuka maneno ya mkufunzi wao wa kung fu.

    "Endapo na wewe utakuwa mmoja wa wale waliokalibu na hewa ya huu unga basi moja kwa moja utadhulika! Sasa ili ujikinge ni lazima uwe na hiki kichupa! Hiki ni kama dawa ya mafua,utakachotakiwa kufanya ni kupaka kwenye pua zako kabla ya kuiachia huu unga ufanye kazi!

    Na ukifanikiwa kupaka hii puani hii sumu haitakuathiri kabisa"alikuwa akiyakumbuka bado maelekezo ya yule mkufunzi aliyewasaidia kule Somalia.

    Aliingiza mkono kwenye mfuko wake wa ndani ya taiti na kuutoa ule unga.

    Alitoa na kile kichupa kisha akajipaka kidogo kisha akatokeza mbele ya askari wale waliokuwa pale nje.

    Akiwa kavaa mavazi ya kiuaskari alianza kupita kalibu yao huku akiachia ule unga upigwe na upepo wakati akiendelea na safari.

    Askari walianza kuanguka mmoja baada ya mwingine wakati Shamim akiendelea kuwazunguka taratibu bila wao kutambua.

    Alex alishtukia kitendo cha askari wale kuanguka.

    "Andaeni silaha huyu malaya yuko hapa"aliwaambia wale vijana.

    Wakati wakijiandaa Shamim alikuwa anamalizia askari wachache waliobaki wakikimbia ovyo ovyo kwa woga mara baada ya kugundua kuna hatari inawakabili bila kujua inatokea upande gani?

    Shamim aliondoka eneo lile na kuelekea kule vijana wake walipokuwa nao wakamfungulia mlango wa gari akaingia na ikawashwa na kuondoka eneo lile kwa kasi sana.

    Alex aliona kile kitendo vizuri sana.

    "Ingieni kwenye gari tuwawahi wale paleee!!"aliwaambia vijana wake.

    "Una..........





    Gari iliondolewa kwa kasi ya ajabu kutoka eneo lile na kuacha vumbi likitimka.

    Alex hakuwa nyuma bali na yeye akiwa na vijana wake waliondoa gari lao kasi kumfatilia Shamim na watu wake.

    Uwezo wa gari waliyokuwa wakiitumia akina Shamim na ile Noah waliyokuwa nayo akina Alex vilikuwa vitu tofauti.

    Hivyo walipotoka kwenye barabara za vumbi na kuingia kwenye lami Shamim waliwaacha akina Alex mbali sana.

    Na walipowaacha Shamim akacheza mchezo.

    Akachukua simu yake na kupiga namba ya Alex.

    "Uko wap mme wangu?"alianza na swali mara baada ya simu kupokelewa.

    "Niko njiani kuna sehemu naenda mamaa"akajibu Alex bila kufahamu kuwa anayemfukuzia ndiye anayeongea naye.

    "Naomba nije kwako babaa"akasema Shamim.

    Lile swali lilikuwa gumu kwa Alex kujibu!

    "Baba niko njiani nakuja kwako basi nijibu"akasema Shamim.

    "Niko mbali kidogo mke"akajibu Alex.

    "Mimi sitaki hayo maelezo bali nataka uje sasa hivi! Kwani mimi na hayo unayofanya kipi cha muhimu?"akauliza kimtego Shamim.

    "Basi mama nakuja sasa hivi"akajibu Alex.

    Hakuwa na namna ya kujitetea mbele ya wale vijana wa kiarabu ila kwa sababu alikuwa akiongea kiswahili na wale hawakusikia aliwalaghai na kuahilisha swala la kuwafukuzia akina Shamim na kuwapeleka kwenye ile nyumba waliyofikia na yeye akageuza kurudi kwake.

    Alipofika getini alikuta gari ndogo ikiwa imepaki kwa nje.

    Moja kwa moja akajua ni Lily akamruhusu dereva wake afungue geti na magari yote yakaingia ndani.

    "Mwaaaaa!! Mwaaaaaaa!!"Lily au Shamim alimbusu Alex kimahaba.

    "Vip mama umepoa? Pole kwa matatizo"akasema Alex.

    "Nimeshapoa baba samahani kwa kukuacha kipindi kile kuna mtu alinipa maelekezo ya kufatilia ile mizigo niliyotapeliwa ndo nikaenda kumsikiliza"akajibu Shamim.

    "Pole mke! Vip umefanikiwa?"akauliza.

    "Sijafanikiwa baba bado nafatilia! Twende ndani basi japo ukaniliwaze"akasema Shamim.

    "Oooh!! Nilisahau! Twende mama nikakupe japo faraja kwa sababu nimekumis sana"akasema Alex.

    Walishikana mikono na kisha kuzungusha katika viuno mpaka wakaingia ndani.

    "Vip mama umekula?"akauliza Alex.

    "Nimekulala! Nibebe basi baba twende chumbani"akaongea kimadeko Lily.

    Alex alitii na kumbeba mpaka alipomfikisha kitandani akamlaza.

    Shamim alimvuta Alex shati akasogeza kalibu midomo yao ikakutana na wakabadilishana denda kwa zaidi ya dakika tano.

    Lily alijitahid kucheza na ulimi wa Alex kwa muda wote huo.

    Kisha akamwachia na kumgeuza Alex akawa chini na yeye juu akaanza kumvua shati lake kisha akafatia suruali na viatu vyake.

    Alimalizia na nguo ya ndani.

    Akavua za kwake pia na kumgeukia Alex na kumpa mgongo.

    "Panda baba ukaoge leo nataka nikupe kitotatota niliyokuahidi kipindi kile"akasema Shamim.

    "Kweli nimekumbuka kipindi kile hukunipa kitotatota kabisa! Leo unipe mumy"akajibu kimadeko Alex.

    Alex alikuwa amechoka sana kutokana na mizunguko ya siku hiyo na Shamim pia alikuwa amechoka ila alijiamini yeye ni komandoo na hivyo hapaswi kuchoka.

    Na pia alitaka kutumia udhaifu wa uchovu huo wa Alex kumpagawisha kimapenzi ili afanikishe malengo yake.

    Alimbeba Alex mpaka bafuni na kumlaza kwenye sink.

    "Unaisubiria kitotatota baby si et?"akasema kimahaba Shamim.

    "Ndiyo baby"akajibu Alex.

    Akafungulia maji na kuweka sabuni kisha akavua nguo yake ya ndani nyeupe na safi akaipaka sabuni na kuanza kumsugua Alex sehemu mbali mbali za mwili wake.

    Wakati anamsugua alikuwa akichezea weak point za mwili wa Alex.

    Alex alikuwa akihisi raha ya ajabu wakati akisuguliwa na Shamim na pia akiwa anachezewa hizo sehemu.

    Aliogeshwa kama mtoto mdogo huku wakicheza michezo ya kimapenzi pale kama watoto wadogo.

    Alex alijihisi faraja ya ajabu kutokana na kile kilichokuwa kikitokea.alpohakikisha mwili wa Alex uko safi kabisa alitoa maji ya povu na kuleta maji masafi ya uvuguvugu

    "Sasa ni muda wa kitotatota......



     Alex alikaa mkao wa kula akisubiria kupewa kitotatota kama alivyoahidiwa na Lily.

    Lily alimfata Alex pale kwenye sink na kushika mhogo wa jang'ombe akaumeza wote na kuanza kuumung'unya kwa utalaam wa hali ya juu saana.

    Alex alipata utam wa ajabu ambao hakutarajia kukutana nao.

    Aliendelea na hilo zoezi kwa muda kisha akafungulia maji na kumgeuzia Alex mwili wake kwa style ya kitotatota.

    "Heeee kumbe hii ndo kitotatota??!"mama yangu.

    Alijikuta Alex akiongea bila kutarajia.

    Shamim alicheka mwenyewe kimya kimya alishajjua kwa style ile Alex hakuwa na pa kupumulia.

    Alex akakaa mkao wa kula na kuanza kushughulika kwa uwezo wake wote.

    Kwa style aliyokuwa amekaa Shamim ilikuwa rahisi kwake kutawala ile mechi kwa mauno yake balaa.

    Alex alipewa mzigo hadi kufikia kuongea lugha ambazo hazijulikani kabisa katika ulimwengu huu.

    Cha ajabu Alex alitegemea kwa style au mkao ule wa kitotatota Shamim angechoka mapema na kubadili ili yeye apate nafasi ya kutawala mechi ila tofauti na matarajio yake Shamim alicheza dakika zote tisini akitawala mchezo ule.

    Round ya kwanza iliisha Alex akiwa hoi kiwango kikubwa huku saluti nyingi zikimwendea Shamim.

    Shamim hakutaka kumpa nafasi ya kupumzika,alimbeba moja kwa mja mpaka chumbani kisha akamfuta maji mwili mzima na kumpaka mafuta taratibu mwili mzima.

    Kwa siku hiyo Alex alifanyiwa vitu ambavyo hakutarajia kukutana navyo popote pale.

    "Mama nina ombi moja kwako naomba usinikatalie tafadhali"alisema Alex.

    "Ongea tu mme wangu wala siwezi kukukatalia"akajibu Shamim.

    "Naomba uhamie hapa moja kwa moja na nikamalize taratibu za ndoa kwenu?"akasema Alex.

    Shamim alitabasamu kwa sababu manjonjo yote yale aliyokuwa akifanya lengo lake kuu



    "Junior lengo langu mimi na mabosi wangu lilikuwa kupata uwepo wa zile mali zetu na hivyo nilikubali kuolewa na Alex huku tukitengeneza ndugu wa bandia huko Tanga na tukafanikisha kuishi pamoja ila kuna michezo tulicheza ndoa isifungwe kwa kulipa baadhi ya watu na yeye alivyokuwa zoba akakubali tukaishi huku nyie akiwadanganya kuwa amenioa kwa ndoa halali!

    Nilikaa na Alex kwa zaid ya miaka miwili nikiwa nimeweka vitu vya kuzuia kushika mimba na lengo langu kwake likiwa nisizae nae kwa sababu hakuwa kwenye akili yangu na pia kwake nilikuwepo kikazi pekee.

    Wewe ulipokuja kuishi na sisi kwa mara ya kwanza nilianza kujihisi kupenda kitu ambacho katika maisha yangu yote hakijawahi kutokea kabisa.

    Mara baada ya kukupenda wewe mabosi wangu walishtukia hilo ndipo walipokomaa niharakishe kujua kuhususwala la zile mali zao kutoka kwa Alex.

    Nilitumia mbinu zangu zote na hatimaye nikafanikiwa kujua mali zilipo na kama unakumbuka kuna kipindi niliwahi kusema naenda kupumzisha akili nyumbani.

    Muda huo ndiyo nilipoenda na vijana wangu kuzichukua ile mali.

    Ilikuwa ngumu sana kwa sababu ilitubidi kupigana mpaka kuua lakini nilizipata.

    Tatizo likawa moja! Nilikuwa nimeshakupenda sana na nilihitaji kuishi na wewe kama mke na mme na tayali nilikuwa na kiumbe chako ndipo nikaona hatua ya kwanza nisiwakabidhi mali wale matajiri zangu na pia nimuue kakao kisha nitafute namna ya kuuza ule mzigo nikimbie na wewe tukaishi sehemu ambayo hatutapatikana.

    Matajili wakashtukia hilo ila lile la kumuua kakako niliona nikutumie ili usiweze kunikwepa na ukafanikiwa kumuua kakako.

    Hali ikatokea kama nilivyopanga! Nilivyoenda na nyie Mombasa nilijua yatatokea makubwa na ndo kama ulivyoona!

    Kwa sasa nina maadui wawili kuna serikali ya Tanzania ambayo nilifanya ule uhalifu wa kuua askari wengi na haijanitambua mpaka sasa na pia Abdul!

    Kama unakumbuka mara baada ya Abdul kumuua Majid amesema niwasiliane naye na kumpa ule mzigo kama mabadilishano ya nyie na uhai wangu na nimekubali kumpa.

    Ila kichwani nimepanga sitompa na nitauuza na kutoloka na wewe kwenda kuishi mbali tumlee mwanetu!

    Na huo ndo ukweli wa maisha yangu baba" alimaliza Shamim kusimulia story ndefu ya maisha yake.

    Junior alichoka sana na kumbe Joan pia alikuwa ameshaamka anasikiliza kimya kimya wakati huo gari ikizidi kuchanja mbuga kuelekea mpaka wa Tanzania na Kenya

    "Hapa ili nimuepuke huyu napaswa nimchomee kwa askari wa Tanzania! Najua akishikwa hukumu yake ni kunyongwa na mimi nitabaki huru na Joan wangu"aliwaza Junior



    *SHAMIM kamaliza kusimulia ila Junior anataka kumgeuka! Ataweza??





    "Sikupenda kuwa gaidi Junior na ndiyo sababu ya mimi kukusimulia kila kitu juu ya maisha yangu ili usinichukie na pia unifahamu nje ndani na ikibidi tutimize lengo letu la kuishi pamoja kama mke na mme na kumlea huyu mwanetu aliyeko tumboni kwa amani na furaha"akasema Shamim.

    "Nisikuogope? Mmmmmh!! Huyu hajielewi nini? Naweza ishi na mwanamke roho mkononi wa hivi? Siku nikifanya kosa si ataniua? Hapana lazima nimkabidhi mkononi mwa serikali tu"aliendelea kuwaza Junior kimya kimya.

    Joan alipiga chafya na kila mmoja akafahamu kuwa kaamka.

    "Vip unajisikiaje kwa sasa mdogo wangu?"akauliza Shamim.

    "Angalau kidogo dada"akajibu Joan.

    "Pole sana mdogo wangu"akasema Shamim.

    "Pole Joan"nikasema na mimi.

    "Ahsante ila dada kuna kitu naomba kukwambia"akajibu Joan.

    "Nambie tu mdogo wangu"akasema Shamim

    Nilishtuka kusikia Joan kuna kitu anataka kumwambia Shamim nikataka kumzuia japo kwa ishara ila bahati mbaya akawa haniangalii.

    "Nilikuwa nawasikiliza mwanzo mpaka mwisho wa simulizi yako! Dada nakiri nimekukosea sana kwa kutembea na Junior! Najua unampenda kwa dhati na imefikia hatua una ujauzito wake!

    Nisamehe dadangu na nakuahid na Junior yupo hapa ananisikia haitatokea tena niwe naye na hata akiniambia tena ujinga nitakushtakia! Nisamehe sana dadangu!

    Ulikuwa na uwezo wa kunidhuru ila hujanidhuru na umenisamehe! Nisamehe dada"aliongea mfululizo Joan.

    Niliudhika sana kwa yale maneno yake tena kiwango kikubwa sana kwa sababu moyo wangu ulikuwa unampenda Joan pekee na si Shamim.

    " usijal mdogo wangu! Nakupenda sana tena sana na nimekwelewa! Usijal"akajibu Shamim.

    Safari iliendelea kwa kasi mpaka tulipokalibia mpaka wa Tanzania na Kenya ndipo Shamim akatuamuru tutoke kwenye gari.

    "Nimeongea na Abdul na watu wake kuwa ule mzigo nitawaambia ulipo na kuwakabidhi nikifika hapa mpakani mara baada ya kuvuka salama ila mimi sijawaza kabisa kumkabidhi ule mzigo kwa sababu nafikiia kuuza kwa Wamexico kisha tuondoke na kwenda kujificha Chile au Colombia au Peru huko Amerika ya kusini na kuishi kwa aman! Sasa kuna mawili! Tupitie porini kuingia Tanzania? Au nipite mpakani ila nipambane nao?"akaongea Shamim.

    "Kupigana risasi tena sasa hivi? Hapana dada! Tupite porini kisha tutokee huko"akasema Joan.

    Wazo lile sikulipinga hivyo Shamim akaanza saafari na sisi tukiwa nyuma yake moja kwa moja tukielekea mpakani kwa njia za panya.

    Tulipofika kalibu na mpaka tulitafuta sehemu na kujificha na Shamim akatoa biskuti tukala na kushiba.

    "Itabidi tuingie Dar usiku wa leo hii hii na kukata tiketi keso tuondoke kwenda Mexico nikafanye biashara ile na baada ya hapo tutaenda huko nilikosema kuishi"akasema.

    "Kwani mzigo uko wap dada?"akauliza Joan.

    "Unajua pamoja na kufanya kazi na hao Wasomali nilikuwa na vijana wangu wa siri na ndo wamekuwa wakinisaidia kazi zangu hapa Dar za mauaji hao ndo wanao mzigo na wametangulia nao Mexico"akasema Shamim

    Wakati wote huo akili yangu ilikuwa ikiwaza namna ya kumkamatisha Shamim kwa askari wa Tanzania kwa sababu walikuwa wakimtafuta kwa udi na uvumba huku wakiwa hawajui ni nani na yup? Ili nibaki na Joan! Najua ningemchezesha akili mpaka akanielewa kwa sababu nilishampanda.

    Baada ya kushiba tulivuka salama na kuingia Tanzania! Huko tukapanda gari ndogo kuelekea Tanga mjini mpaka tukafika salama.

    Hatukupumzika tuliunga safari kutoka Tanga kuja Dar.

    Njiani mara baada ya kwenda zaidi ya kilometa mia moja tulikuta kizuizi cha polisi.

    Shamim alijitanda mitandio yake asijulikane na mimi nikatumia nafasi hiyo kama nataka kuchimba dawa nikashuka.

    Mara baada ya kushuka niliwaona askari kadhaa wakiwa wamezagaa pale chini.

    Nikazunguka upande wa pili wa gari ambako Shamim asingeweza kuniona na kisha nikamuita askari mmoja kwa ishara.

    Askari yule alinisogelea pale nilipokuwa.

    "Una shida gan kijana?"aliuliza.

    "Kaka......





    "Mbona unaogopa ogopa kijana? Au una makosa? Ongea nakusikiliza"alisema yule askari.

    Nilishikwa na kigugumizi na kujiuliza hivi Shamim akiwashinda wale askari maisha yangu yatakuwa hatarini kiasi gan?

    Niliwahesabu haraka haraka wale askari na kugundua idadi yao ni kama zaidi ya ishilini nikajipa moyo kuwa hataweza kuwazidi uwezo.

    "Afande mimi kuna jambo nataka kukwambia ambalo litakuwa msaada kwako na kwangu pia"nikasema.

    "Jambo gani hilo kijana? Sema basi muda unaenda na gari litaondoka"akajibu yule askari.

    "Unakumbuka miaka miwli iliyopita huko Dar es salaama kuna askari waliuawa na gaidi mwanamke na serikali ikamtafuta bila kumpata kwa muda wote mpaka sasa?" nikamuuliza.

    "Ndiyo nakumbuka na pia serikali iliweka kiwango cha pesa kwa atakayefanikisha kufichua alipoa" akajibu yule askari.

    "Basi mimi yule mwanamke najua alipo afande"nikamwambia.

    Alishtuka sana mpaka nikashangaa!!

    " Unajua alipo? Sasa kwanini usiseme ili hata hiyo zawadi uipate? Yuko wap sasa?"akauliza kwa hamaki na mshangao.

    "Bwana afande hapa nilipo nipo naye huyo mwanamke na hapa nilipo maisha yangu yapo hatarini sana kutokana na yeye na nahisi muda wowote ule anaweza kuondoka na roho yangu kwa sababu ni gadi hatari sana"nikamwambia.

    Yule askari alishtuka sana!! Nafikiri alikuwa akikumbuka mambo aliyowahi kuyasikia juu ya Shami.

    "Hebu subiri kidogo kijana! Usiondoke"akasema huku akiondoka.

    Alielekea kule walipokuwa wenzake na kuwaita wakajadiliana kwa muda mfupi kisha wakaja uelekeo niliokuwa.

    "Mungu nisaidie hawa watu waweze kumdhibiti Shamim na mimi nipate nafasi ya kuondoka na Joan tukaishi kwa aman"niliwaza mwenyewe.

    Wale askari waliponifikia mwenzao akawaambia kuwa ni mimi ndiye niiyemweleza.

    "Kijana una uhakika na habari ulizotueleza?"akauliza askari mmoja.

    "Ndiyo nina uhakika asilimia zote"nikajibu.

    "Huyo mwanamke kavaaje?"akauliza tena.

    "Amejifunga hijabu nyekundu kichwani mpaka kuachia uso wenyewe na usoni amevaa miwani ya jua na pembeni yake kuna binti amekaa amevaa kibody che rangi ya blue"nikajibu.

    "Sawa tunaomba utusubiri hapahapa na huyu mwenzetu ila kumbuka taarifa zikiwa za uongo utachukuliwa hatua za kisheria!"akasema.

    "Niko tayali afande wala usiwe na wasi wasi"nilijibu kwa kujiamini kiasi kwamba hata yeye akabaki kunishangaa.

    Waliwaita wenzao wote na kulizunguka lile basi na kisha nane kati yao wakaingia ndani.

    Shamim akiwa kakaa kwenye kile kiti alichungulia nje na kushangaa askari wakianza kulizunguka lile gari walilopanda.

    Alishtuka sana na ikabidi apeleke mkono wake taratibu mpaka kiunoni na kukuta silaha yake iko sawa akatulia.

    Ghafla alishangaa askari wakipanda kwenye lile gari kwa speed.

    Akiwa hajajiandaa kwa lolote alishangaa wakija na kuzunguka kile kiti alichokaa.

    "Ukijitikisa tu kwa namna yeyote ile umekwisha! Tunajua ni kiasi gani ulivyo hatari ila hatutaruhusu kosa hata moja! Tunahitaji kuvaa medali kwa hili tukio"aliongea askari mmoja akimwangalia Shamim kwa macho makali na mekundu utafikiri kavuta bangi.

    Shamim alitulia kama alivyoelekezwa ila muda wote akifikilia cha kufanya ili kuondoka eneo lile kama upepo.

    "Binadamu hafadhiliki! Nimeshasalitiwa na huyu dogo! Aki ya nani atajuta kuzaliwa! Nitamuua kifo kibaya sana labda niuawe sijamtia mikononi"aliwaza Shamim.

    "Nyenyua mikono yako juu na kisha usimame"aliamrisha askari mmoja.

    Shamim akatii na kunyenyuka taratibu mikono yak ikiwa juu alishawapigia hesabu kuwa eneo lile la katikati ya siti za abiria lilikuwa dogo ambalo kama kuna hata mmoja angejipendekeza kuja kumkagua basi angemsaidia kuwamaliza wenzie.

    "Piga hatua taratibu sana tukitoka nje"akaamrishwa.

    Lengo lake likashindwa kutimia tayali!! Kwani alitaka amalize kwenye kaeneo kale kafinyu.

    Abiria walibaki vinywa wazi na macho yakiwa yamewatoka kwa mshangao!! Kwani walichokuwa wakikiona pale ni kitu walichozoea kuangalia kwenye filamu za watu wa nje pelee.

    "Songa mama taratibu"aliambiwa.

    Askari wanne walikuwa mbele yake na wanne nyuma huku silaha zote zikimwangalia yeye.

    Alipotupa jicho lake nje kupitia dirishani alimuona Junior akiwa na askari mmoja wakiongea!

    Aliuma meno yake kwa hasira!!!



     Shamim alikuwa mpole lakini kichwani akiwa na hasira kali sana huku pia akipanga namna ya kuwatoka wale askari.

    Alipelekwa mpaka chini kutoka ndani ya gari ile.

    "Piga magoti chini binti"aliamrishwa.

    Shamim hakuwa na cha kubisha bali alinyenyekea.

    Askari mmoja alikabidhi silaha kwa wenzie na kumfata Shamim pale chini akamkunja mikono kwa nyuma kisha akamfunga pingu.

    Shamim alishindwa kumtumia yule askari kutoloka kutokana na kutokuja na silaha ambayo ingemsaidia Shamim katika kutoloka na pili wingi wa wale askari ulimtisha.

    Junior aliitwa eneo lile na wale askari.

    "Kijana umesema huyu binti ni nani?"akauliza aliyeonekana kuwa kamanda wa kile kikosi.

    "Huyu ni yule mwanamke gaidi aliyewahi kufanya tukio la kuwaua askari Mwenge miaka miwili iliyopita na akapotea"akajibu huku akiwa anaogopa sana.

    "Kijana una uhakika? Kumbuka yule ni gaidi ambaye askari kibao walishindwa kumdhibiti sasa mbona kawa mpole sana hapa? Au umemfananisha?"akauliza tena yule askari.

    "Sijakosea afande! Ninamfahamu mwanzo mpaka mwisho na nimeishi naye akiwa mke wa kakangu! Kama huamin muulize yule mdada aliyebaki ndani ya gari"akasema Junior.

    Ikabidi wapande na kumfata Joan ndani.

    Joan alikuwa muoga sana hivyo alipotishiwa kidogo tu akaropoka kila kitu kuhusu Shamim.

    Simu za upepo zilipigwa haraka sana na ndani ya muda mfupi tu Jeshi la ulinzi na askari waliokuwa maeneo kalibu na Tanga walielekea eneo la tukio.

    Shamim alianza kujuta kwa kutochukua hatua za haraka za kuwatoloka wale askari mpaka lile swala limekuwa kubwa hivyo.

    Ndege ya jeshi la polisi ilitumwa kutoka makao makuu Dar es salaam kuja eneo lile kalibu na Segera kumchukua Shamim.

    Kwenye akili yake alipanga kuwatoloka askari wale akiwa kwenye helikopita angani.

    Walipofika alishangaa wakishuka wanajeshi wenye nyota begani kisha minyororo ya uhakika ikaletwa na yeye kufungwa mikononi na miguunni kisha akabebwa na kuingizwa kwenye ile ndege.

    Askari wale wa jeshi waloonekana kuwa na vyeo vikubwa walipanda naye kwenye ndege na kuondoka kuelekea Dar es salaam.

    Junior na Joan nao walipandishwa kwenye gari ya polisi na moja kwa moja na wao wakasafirishwa kupelekwa makao makuu ya polisi.

    Taarifa ya kukamatwa Shamim ilipenya haraka sana na kuvifikia vyombo vya habari na Taarifa zikaanza kutangazwa.

    "Habari zilizotufikia hivi punde ni kuwa yule gaidi wa Kikenya aliyewahi kuitikisa nchi kwa kuwaua baadhi ya askari wetu maeneo ya Mwenge hapahapa Dar es salaam miaka miwili iliyopita hatimaye kakamatwa muda sio mrefu maeneo ya Segera mkoani Tanga! Tujiunge na repota wetu aliyeko eneo la tukio......."ITV ilisoma habari na vyombo mbalimbali nazo zilirusha taarifa hiyo.

    Waandishi wa habari walijaa jengo la habari huku wengine wakkielekea Wizara ya mambo ya nchi na Usalama kupata uhakika wa hilo.

    Taarifa zikawafikia viongozi wa nchi na Waziri wa mambo ya ndani akaanza kupata usumbufu pia juu ya swala lile.

    Shamim alipelekwa mpaka makao makuu ya Jeshi na huko alipokelewa msobemsobe mpaka kwenye chumba maalumu kwa ajili ya kazi ya kushughulikia wahalifu.

    Kabla chochote hakijaendelea kikosi cha watu tisa kutoka wizara ya mambo ya ndani na usalama wa Taifa ambao walikuwa wakifanya kazi idara ya usalama wa Taifa walifika na kudai kutumwa kuja kumchukua Shamim.

    Kwa sababu ya mambo ya ajabu ambayo walishaelezwa anayoyafanya Shamim hawakuta kumwachia kirahisi mpaka pale walipopata simu ya Waziri mwenye wizara ndipo walipokubali kumwachia Shamim.



    Taarifa ya kukamatwa kwa Shamim iliwafikia vijana wake kwa njia ya mtandao wakiwa Mexico wakimsubiri aende wafanye biashara na wale jamaa zao.

    Mara baada ya kupata taarifa hiyo mjadala mrefu uliibuka kati yao kuhusiana na swala la Shamim.

    Vijana wale sita walijikuta wakigawanyika katika maamuzi.

    Wawili walitaka waahirishe kila kitu na kurudi Tanzania kuangalia uwezekano wa kumkomboa Shamim ila wale wanne waliobaki walitaka ule mzigo uuzwe na kugawana kiwango kile kikubwa cha pesa kisha kila mmoja atafute sehemu na kujibadilisha kisha aishi maisha yake.

    "Hivi mmemsahau bosi Shamim au? Hivi mnaona nyie mna ubavu wa kumsaliti Shamim kweli?? Acheni utani kwenye swala linalomhusu Shamim jaman! Huko Bongo atatoka tu hata kwa kuua jeshi zima! Acheni mawazo duni! Twendeni tukamkomboe jaman!"alisema mmoja wao.

    "Acha uoga wewe! Alisalitiwa Yesu aje kuwa Shamim?? Wewe ni mwanaume jiamin! Yule tunaweza kummaliza akiwa huko huko tukiwa na pesa!"akajibu aliyelazimisha kuhusu ule usaliti

    "Lakin....





     Vijana wale waliendelea kubishana juu ya lile swala la ule mzigo wa Shamim kama wanapaswa kuuza kisha wagawane pesa au waende kumkomboa kisha wauze naye na yeye ndiye awape mgao wao.

    "Mimi nashangaa mnachobishana hapa! Kwani huu mzigo ni wa kwake? Si kawazurumu Wasomali wake? Sasa sisi tukimdhulumu inakuwaje shida? Acheni ushamba huu ni wakati wa kupiga pesa"akasema mmoja wa wale waliokuwa wakitaka wauchukue.

    "Nawaambia ukweli kuuchukua huu mzigo ni kujiweka kwenye wakati mgumu sana kwa sababu hata Abdul na yeye anautaka kwa sababu yeye ndiye kiongozi wa kikosi kwa sasa! Jaman acheni roho ya hivyo"akajibu mmoja.

    Waliendelea kulumbana kwa muda na wale waliotaka wauchukue na kuuza wakamshawishi mmoja wa wale waliokuwa wanapinga mpaka na yeye akakubali.

    Akabaki mmoja aliyefahamika kwa jina la Hussein, yeye alikataa katakata kumsaliti Shamim hata kwa upinde kwa sababu aliufahamu uwezo wake.

    Wakati anaendelea kuwalazimisha wenzie wamwelewe walipeana ishara kisha wakanyenyuka na kuanza kupambana naye.

    Kijana yule alikuwa ameiva kwenyem apambano ingawa kwenye kitengo chao alikuwa akisiamia Teknolojia hivyo kwa sababu ya wingi wao alijikuta anazidiwa na kujikuta akipokea kipigo cha uhakika mpaka akapoteza fahamu na wenzie wakajua wameshammaliza hivyo wakamtelekeza kwenye bonde moja na kutokomea kwenye dili zao za biashara.



    Upande wa Mombasa Abdul na kikosi chake walisubiri sana pale mpakani walipoelewana na Shamim kuwa akifika atawapatia ramani ya namna ya kuupata ule mzigo.

    Walisubiri kwa muda mrefu sana bila kupata mafanikio yeyote yale.

    Wakati wamesimama eneo lile wakijadiliana nini cha kufanya simu ya kiongozi wao Abdul ilianza kuita kwa fujo.

    "Bosi kuna tatizo kidogo"sauti iliongea kutoka kwenye simu.

    "Tatizo gan?"aliuliza ki amri kuonesha ukubwa wake.

    "Shamim amekamatwa bosi"akajibiwa.

    Alishtuka sana kusikia Shamim kakamatwa!!!

    "Kakamatwa? Kakamatwa vip? Na akina nani? Na kakamatiwa wap?"aliuliza maswali mfululizo.

    "Kuna habari tunaiangalia hapa kakamatiwa huko Tanzania eneo la Segera Tanga"akajibiwa.

    "Tanzania??? Tanga?? Kakamatwa vip? Na akina nani? Na amefikaje huko? Si tulielewana kukutana mpakani?"akaendelea kuuliza Abdul.

    "Inaonekana katusaliti bosi ila habari iliyopo ndiyo hiyo! Kakamatwa huko Tanzania na askari na habari imeenea sana sijui tufanyeje?"akajibiwa.

    "Shamim ni wa kunisaliti mimi? Pamoja na kumwokoa kutoka kwenye kifo mpaka nimemuua Abdul kwa sababu yake? Hapana"aliongea akiwa haamin Abdul.

    Alichukua simu yake na kuwasha kisha akaingia kwenye mitandao ya kijamii maarufu kwa habari.

    Alishangaa kukuta picha kadhaa za Shamim akiwa kakamatwa na habari kubwa kwenye mitandao ilimuhusu gaidi aliyekamatwa.

    "Twende Dar es salaam sasa hivi"aliwaagiza vijana wake.

    Walipanda kwenye gari zao na safari kuelekea Dar ikaanza rasmi.

    Abdul alionekana kuwa na hasira kubwa sana juu ya Shamim kutokana na wema aliomtendea siku zote alipopatwa na matatizo.

    Alikumbuka mateso makubwa aliyoyapata pamoja na Shamim wakati wakitumwa huko Uarabuni halafu Shamim anakuja kumgeuka baada ya wema wote huo.

    Waliendesha gari kwa kasi kubwa sana kuliko kawaida na kwa bahati nzuri kutokana na Shamim kukamatwa askari wa barabarani hawakuwa na habari na magari yaliyokuwa yanapita bali walikuwa wamekaa vikundi vikundi wakijadiliana juu ya lile swala.

    "Bosi tunaenda kufanya nini?"aliuliza swali mmoja wa vijana wa Abdul.

    Kwa hasira Abdul alitoa bastora na kumpiga risasi yule kijana kisha akaamuru gari ikasimamishwa na ule mwili ukatupwa nje.

    "Sihitaji maswali ya kipuuzi na pia sitaki makosa katika kazi yangu! Uzembe wowote ule adhabu yake ni kifo! Tunaenda kumchukua Shamim nahitaji ule mzigo utusaidie kujiimalisha! Nimeeleweka?"akasema.

    "Ndiyo bosi"wakajibu.

    "Tunahitaji vijana sita kutoka Mombasa leo hii hii waje na ndege tukutane Dar! Kwa namna yeyote ile lazima tumpate Shamim"akasema



     Vijana wale waliendelea kubishana juu ya lile swala la ule mzigo wa Shamim kama wanapaswa kuuza kisha wagawane pesa au waende kumkomboa kisha wauze naye na yeye ndiye awape mgao wao.

    "Mimi nashangaa mnachobishana hapa! Kwani huu mzigo ni wa kwake? Si kawazurumu Wasomali wake? Sasa sisi tukimdhulumu inakuwaje shida? Acheni ushamba huu ni wakati wa kupiga pesa"akasema mmoja wa wale waliokuwa wakitaka wauchukue.

    "Nawaambia ukweli kuuchukua huu mzigo ni kujiweka kwenye wakati mgumu sana kwa sababu hata Abdul na yeye anautaka kwa sababu yeye ndiye kiongozi wa kikosi kwa sasa! Jaman acheni roho ya hivyo"akajibu mmoja.

    Waliendelea kulumbana kwa muda na wale waliotaka wauchukue na kuuza wakamshawishi mmoja wa wale waliokuwa wanapinga mpaka na yeye akakubali.

    Akabaki mmoja aliyefahamika kwa jina la Hussein, yeye alikataa katakata kumsaliti Shamim hata kwa upinde kwa sababu aliufahamu uwezo wake.

    Wakati anaendelea kuwalazimisha wenzie wamwelewe walipeana ishara kisha wakanyenyuka na kuanza kupambana naye.

    Kijana yule alikuwa ameiva kwenyem apambano ingawa kwenye kitengo chao alikuwa akisiamia Teknolojia hivyo kwa sababu ya wingi wao alijikuta anazidiwa na kujikuta akipokea kipigo cha uhakika mpaka akapoteza fahamu na wenzie wakajua wameshammaliza hivyo wakamtelekeza kwenye bonde moja na kutokomea kwenye dili zao za biashara.



    Upande wa Mombasa Abdul na kikosi chake walisubiri sana pale mpakani walipoelewana na Shamim kuwa akifika atawapatia ramani ya namna ya kuupata ule mzigo.

    Walisubiri kwa muda mrefu sana bila kupata mafanikio yeyote yale.

    Wakati wamesimama eneo lile wakijadiliana nini cha kufanya simu ya kiongozi wao Abdul ilianza kuita kwa fujo.

    "Bosi kuna tatizo kidogo"sauti iliongea kutoka kwenye simu.

    "Tatizo gan?"aliuliza ki amri kuonesha ukubwa wake.

    "Shamim amekamatwa bosi"akajibiwa.

    Alishtuka sana kusikia Shamim kakamatwa!!!

    "Kakamatwa? Kakamatwa vip? Na akina nani? Na kakamatiwa wap?"aliuliza maswali mfululizo.

    "Kuna habari tunaiangalia hapa kakamatiwa huko Tanzania eneo la Segera Tanga"akajibiwa.

    "Tanzania??? Tanga?? Kakamatwa vip? Na akina nani? Na amefikaje huko? Si tulielewana kukutana mpakani?"akaendelea kuuliza Abdul.

    "Inaonekana katusaliti bosi ila habari iliyopo ndiyo hiyo! Kakamatwa huko Tanzania na askari na habari imeenea sana sijui tufanyeje?"akajibiwa.

    "Shamim ni wa kunisaliti mimi? Pamoja na kumwokoa kutoka kwenye kifo mpaka nimemuua Abdul kwa sababu yake? Hapana"aliongea akiwa haamin Abdul.

    Alichukua simu yake na kuwasha kisha akaingia kwenye mitandao ya kijamii maarufu kwa habari.

    Alishangaa kukuta picha kadhaa za Shamim akiwa kakamatwa na habari kubwa kwenye mitandao ilimuhusu gaidi aliyekamatwa.

    "Twende Dar es salaam sasa hivi"aliwaagiza vijana wake.

    Walipanda kwenye gari zao na safari kuelekea Dar ikaanza rasmi.

    Abdul alionekana kuwa na hasira kubwa sana juu ya Shamim kutokana na wema aliomtendea siku zote alipopatwa na matatizo.

    Alikumbuka mateso makubwa aliyoyapata pamoja na Shamim wakati wakitumwa huko Uarabuni halafu Shamim anakuja kumgeuka baada ya wema wote huo.

    Waliendesha gari kwa kasi kubwa sana kuliko kawaida na kwa bahati nzuri kutokana na Shamim kukamatwa askari wa barabarani hawakuwa na habari na magari yaliyokuwa yanapita bali walikuwa wamekaa vikundi vikundi wakijadiliana juu ya lile swala.

    "Bosi tunaenda kufanya nini?"aliuliza swali mmoja wa vijana wa Abdul.

    Kwa hasira Abdul alitoa bastora na kumpiga risasi yule kijana kisha akaamuru gari ikasimamishwa na ule mwili ukatupwa nje.

    "Sihitaji maswali ya kipuuzi na pia sitaki makosa katika kazi yangu! Uzembe wowote ule adhabu yake ni kifo! Tunaenda kumchukua Shamim nahitaji ule mzigo utusaidie kujiimalisha! Nimeeleweka?"akasema.

    "Ndiyo bosi"wakajibu.

    "Tunahitaji vijana sita kutoka Mombasa leo hii hii waje na ndege tukutane Dar! Kwa namna yeyote ile lazima tumpate Shamim"akasema







    Hussein kijana aliyekamilika katika mafunzo ya kutumia Kompyuta kwa namna yeyote ile akiwa na uwezo wa kufanya chochote anachojisikia kwa kutumia mtandao huo popote pale aliokotwa na vijana wanaoishi kwenye mazingira magumu katika mji wa Illias nchini Mexico mara baada ya kupigwa na wale vijana wenzake waliokuwa wakifanya naye kazi chini ya uongozi wa Shamim.

    Alikuja kupata fahamu jioni ya siku hiyo hiyo na kujikuta katika kijumba kisicho na hadhi yeyote ile na mzee aliyekamilika kimisuli alikuwa akiendelea kumpatia huduma ya kwanza.

    Alipoona Hussein ameamka alifurahi sana.

    "Hapa nipo wap?"aliuliza Hussein.

    "Upo kwenye mji wa Illias hapa na vijana wangu wamkuokota huko ukiwa hoi na majeraha kadhaa"akasema mzee yule.

    Hussein alijalibu kujinyenyua na akagundua bado ana nguvu za kutosha kumsaidia kutoka eneo hilo.

    Alijalibu kumbembeleza mzee yule aondoke lakini hakupewa ruhusa hivyo ikambdi awe mpole na kuvumilia akipewa matibabu mpaka asubuh ndipo akapewa ruhusa ya kutoka eneo lile.

    Alielekea mjini na kujalibu kurudi kwenye Hotel waliyofikia na wenzake ili kuona kama vitu vyake viko salama.

    Kwa bahati nzuri alikuta kila kitu kikiwa sawa.

    Alivichukua na kubadilisha Hotel kisha akafungua kompyuta zake na kuanza kufatilia habari zilizokuwa kwenye mitandao ya Tanzania.

    Alifanikiwa kuona kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko Tanzania kuhusiana na sakata la kukamatwa kwa Shamim.

    "Lazima nifanye kitu kwa ajili ya bosi! Kanitoa mbali sana Shamim na sasa ni wakati wangu kumwonesha kuwa yeye ni wa muhimu kwangu kuliko kitu chochote kile"aliwaza Hussein.

    Aliondoka kwenye chumba na mizigo yake yote na kuelekea uwanja wa ndege na kutafuta tiketi ya kuja Afrika ila akakosa lakini akapata ya kuelekea London kisha kutoka huko akapata na kuelekea Johansberg.

    Alilala huko na kesho yake akapata tiketi ya kuja Dar es salaam kwenye ndege za Kenya Airways.

    Alipofika Dar alitafuta Hotel na kupumzika mpaka giza lilipoingia akaondoka kuelekea kule walipokuwa wakiishi na Shamim kwa Dar es salaam hii.

    Cha ajabu alishangaa kuwakuta Abdul na vijana wake wakiwa eneo lile wakikagua kila sehemu na akajua kuwa iwe isiwe watakuwa wanatafuta mzigo wao.

    Alitafuta kichochoro na kutulia kisha akatoa Ipod yake ndogo na kuseti mitambo yake ikanasa satelite na kuanza kumwonesha kila kinachoendelea pale ndani ikiwepo na maongezi yao.

    "Lazima tumuue kabla polisi hawajampeleka mahakaman! Haiwezekani mzigo wetu upotelee hewani na huyu malaya atugeuke kirahisi hivyo"alimsikia Abdul akifoka kwa hasira.

    "Mimi nashauri aiuawe kwanza bosi mpaka atuambie mzigo ulipoa"akashauri kijana mmoja.

    "Sisi tuingie pale kijeshi na kisha tumkomboe kama tunamsaidia kisha tumwombe atweleze mzigo ulpo na baada ya hapo tunammaliza! Shamim nimekua naye namfaham nje ndani hawez kunisumbua kwa namna yeyote ile cha msingi twondoken kueleka huko polisi na kumaliza mchezo mzima"akasema Abdul.

    "Sawa bosi! Haya Juma hakikisha vikosi vyote vitatu viko sawa kwa ajili ya mapambano! Kumbukeni hii mali ni haki yetu hivyo tutapambana Jihad kufa au kupona lakini lazima tumpate Shamim"akasema kijana aliyekuwa akiongoza mapambano.

    Waliondoka eneo lile kwa kasi na fujo mpaka kwenye jengo walilofikia na kuwachukua vijana waliobaki eneo lile na kujiandaa vizuri kwa silaha na kimwili kisha msafara ukaaanza kuelekea makao makuu ya Usalama wa Taifa.

    "Shamim ni mtu hatari sana! Ninamjua vizuri ingawa najua hawez kuleta shida mbele yangu! Ila nawaomba muwe makini naye! Najua askari wa Kitanzania hawawezi kutupa shida ila tukishampta Shamim tuwe makini sana"alisema Abdul.

    Walielekea eneo lile na walipokalibia waliacha magari yao kwa mbali sana na kuanza kuingia eneo lile lenye uzio thabiti kabisa kwa tahadhali kubwa sana.

    Walipokalibia uzio na wakijiandaa kuruka walishangaa eneo lile likiwa na mishemishe nyingi sana.

    Askari walikuwa wakizaaa kila kona huku ving'ora vya maagari ya Askari vikiongeza kelele eneo lile.

    Waliambaa ambaa mpaka kalibu kabisa na geti na kukuta mishemishe zikizidi.

    "Katoloka? Katolokaje?? Hapana siamin kwa ulinzi huu wa eneo hili mtu anaweza kutoloka"askari waliokuwa wakizunguka eneo lile walikuwa wakijadiliana.

    Abdul alishtuka sana!!

    "Nani katoloka???...



    Mara baada ya kumkamatisha Shamim kwa askari Junior na Joan walipelekwa makao makuu ya Usalama wa Taifa pia ili kutoa maelezo ya uhakika juu ya Shamim.

    Walipomaliza kutoa maelekezo ya kutosha waliombwa wawe wanakuja mara kwa mara kujua maendeleo ya kesi ile na pia kuwa mmoja wa mashahidi mahakamani.

    "Tunapaswa kuondoka nchi hii mara moja"alisema Junior akimwambia Joan.

    "Tuondoke nchi hii kwenda wap? Na kwanini tuondoke wakati dada tayali ameshakamtwa?"akauliza Joan.

    "Kuna mambo mawili yanaweza kutokea kama tutabaki hapa"akasema Junior.

    "Mambo gani hayo?"akauliza Joan.

    "La kwanza ni kuhusu Shamim! Simwamini kabia mdada yule! Yule ni zaidi ya Shetani! Anaweza kutoloka muda wowote ule mikononi mwa polisi na ikitokea akatoloka basi watu wa kwanza kuuawa ni mimi na wewe"akaelezea Junior.

    "La pili?"akauliza tena Joan huku akionekana kupatwa na wasiwasi kusikia vile.

    "Asipoweza kutoloka anaweza kulipa kisasi kwangu kwa kueleza kuhusika kwangu katika mauaji ya kaka na kwa bahati mbaya sana kwangu Shamim ana video zote za matukio yaliyotokea kipindi cha mauaji ya kaka hivyo anaweza kuyatumia kama ushahidi wa kunikabidhisha mikononi mwa polisi"akasema Junior.

    Joan alishusha pumzi kwa nguvu! Aghuuuuuuuuuuu!!!!!

    "Sio hivyo tu! Yule anaweza kukuweka pabaya Polisi hata kabla ya kutoloka na kisha akatoloka na kukuacha kule! Lakini kwa nini uliamua kumsaliti na kumkabidhisha mikononi mwa polisi wakati katuokoa kwa mengi?"akauliza Joan.

    "Huu sio muda wa kulaumiana au kushikana ubaya! Nilifanya vile kwa sababu nakupenda na sitaki kukupoteza! Cha msingi tuangalie namna ya kutoloka"akasema Junior.

    Waliendelea kujadiliana namna ya kufanya mpaka wanafika nyumbani.

    Walipoingia ndani Junior alianza mikakati kabla ya polisi hawajazuia safari yake.

    Aliongea na rafiki zake kadhaa na pia rafiki zake na kaka yake aliokuwa akiwafahamu kuhusiana na kuziuza baadhi ya mali za kaka yake.

    Kwa bahati nzuri alipata wateja watatu waliogombania mali zile bila kufahamu kama Junior naShamim wana kesi kubwa polisi.

    Alipoamka asubuh cha kwanza alichofanya ni kuwasiliana na hao watu wakaja pale nyumbani na kumalizana juu ya malipo ya nyumba na mali kadhaa za kaka yake pamoja na lile duka lililokuwa Kariakoo akapewa chake na yeye akawakabidhi hati zilizokuwa ndani.

    Kwa bahati nzuri pia kipindi akiwa kwenye penzi zito na Shamim alipewa namba za siri za account ya Shamim hivyo alienda na kukomba pesa za kutosha.

    "Nataka tuwahi kuondoka kwa sababu hata Abdul yule wa Mombasa anaweza kuja nututafuta"alisema Shamim.

    Walipohakikisha kila kitu chao kipo sawa walikata tiketi ya basi na kwenda mpaka Iringa kutokana na muda kuwa umeenda hivyo wasingeweza kupata magari ya moja kwa moja kuelekea Mbeya.

    Asubuhi walipoamka walitafuta sehemu na kupata kifungua kinywa na hapo Junior akanunua gazeti "GAIDI ALIYEKAMATWA JUZI ATOLOKA USIKU WA LEO" hicho kilikuwa kichwa cha habari kwenye gazeti la mwananchi alilonunua Junior.

    Mkojo ulipita bila kupiga hodi na kulowanisha sehemu kadhaa za suruali aliyokuwa kavaa Junior kwa bahati nzuri alikuwa kavaa Jeans hivyo kuwa vigumu kwa mtu kumshtukia.

    Alitetemeka vibaya sana kiasi cha Joan kumshtukia.

    "Wewe vip? Kuna nini? Mbona hivyo?"aliuliza Joan.

    Junior hakutaka kusema chochote kwanza ilibidi asome kwanza ile habari kwa makini ndipo aseme chochote.

    Kwanza hakuamini kabisa kuwa kile anachokiona kilikuwa cha kweli.

    Alianza kusoma taratibu huku mwili mzima mpaka lipsi za mdomo zikitetemeka hali iliyozidi kumchanganya Joan.

    "Jaman Junior! Kuna nini? Si unambie?"aliendelea kuuliza Joan.

    Alipoona Junior hajibu chochote alinyenyuka na kwenda alipokuwa na kuinamia lile gazeti ili aone kilichomshtua Junior ni kipi?

    Aliposoma kile kichwa cha habari tu!!!

    "Mama yangu!!!!!"alijikuta akiropoka.

    Taratibu nguvu zikamwishia na akaanza kwenda chini taratibu.

    Junior alishtuka na kufanikiwa kumdaka kabla hajaanguka vibaya!!





    Hussein alipomaliza kusikiliza yale maongezi kati ya Abdul na vijana wake alijua kuwa Shamim lazima atauawa hata kama sio wale Polisi wa Kitanzania basi Abdul na vijana wake walikuwa na uwezo wa kumpoteza Duniani kwa sekunde chache.

    Aliendelea kucheza na ile computer yake alioiunganisha na Satelite ikaendelea ku search mpaka ikanasa kwenye Rada ya Setikali ya Tanzania na kuanza kutafuta Usalama wa Taifa ilipo.

    Alitumia sekunde chache na akawa amepapata.

    Alipopata ile sehemu ilipojificha aliingiza code namba za Shamim kwenye GPS na kuanza kufatilia alipo kwenye jengo lile.

    Alipopata mahali alipo Shamim alipanda pikipiki yake na moja kwa moja akaelekea eneo husika.

    Alipofika alitafuta jengo la jilani na pale kisha akawasha tena Computer yake na kuangalie eneo lile vizuri.

    Alipohakikisha ramani ya jengo lile yote inaonekana kwenye ile mashine yake aliielekeza pale Shamim alipokuwa.

    Ilipomuonesha Shamim alipo aliandika neno " ENTRACE" kisha akabonyeza kibatani cha ingiza.

    Mashine yake ika search kwa dakika chache ikamuonesha hakuna sehemu ya kutokea zaidi ya mlango ule wa kawaida unaolindwa.

    Akaandika tena" SECTERY AND SAFETY WAY OF HIDDING AND ESCAPING USED BY NDO"akabonyeza itafute.

    Ilitafuta kwa muda mfupi kisha ikaonesha kuelekea Kushoto.

    Ile Computer ikaanza kuonesha alama Nyekundu na ikawa inaelekea kushoto peke yakee kwa muda kisha ikabadilisha welekeo baaada ya kufika kwenye kona moja ikakata kulia na kuendelea mbele kisha ikatulia eneo moja lisilo na kitu au mlango.

    "Mm0mmmh!! Sasa mbona imetulia hapa? Na hakuna mlango!!"alijiuliza Hussein.

    Ikabidi ajiongoze na kuandika " SECTERY ENTRACE" na kuingiza na ile maisheni ika search kwa muda kisha ikamwandikia "ENTER CODE"

    hapo kazi ikawa kama ndo imeanza moja! Akaanza kuhangaika kuingiza code za kubuni.

    Akafikiri na kuona wakati anahangaika kuingiza code bora angemtoa Shamim.

    Alichokifanya alirudi kwenye mwili wa Shamim na kutafuta nini kilisahaulika ambaco askari hawajamvua ambacho kinaweza kuwa msaada kwenye mawasiliano.

    Haraka jibu likarudi kuwa kuna pete aliyovaa ina GPS.

    Shamim akiwa kakaa hana hili wala lile alishangaa pete yake ikiwaka mara mbili.

    Moja kwa moja akajua vijana wake wamefika.

    Aliichukua ilepete na kuiingiza mdomoni kisha akatoboa kwenye sehemu flani ya ulimi sehemu ambayo alishaitengeneza kwa ajili ya mawasiliano ya kitekenolojia.

    "Mmefika?"aliongea na vile vifaa vikapeleka sauti moja kwa moja mpaka kwenye Computer ya Hussein.

    "Ndiyo....naomba uondoke haraka sana kwa sababu sekunde chache zijazo Abdul atakuja kukumalizia hapo hapo"akasema Hussein.

    "Natoka vip? Na unaona ulinzi ulivyo mgumu"akajibu.

    "Wewe ni kamanda na haushindwi kitu! Tafuta namna ya kutoka kwenye hicho chmba na mimi nitakutoa ndani ya jengo hilo"akasema Hussein.

    Shamim aliamka na kwenda mpaka getini,aliangalia kwa makini wale askari wawili waliokuwa pale

    Akabuni mbinu ya kuanza kupiga geti kwa nguvu huku akipiga kelele kuwa anataka kujisaidia.

    Wale askari walienda pale kiboya boya kutaka kumpa kipigo ili arudi ndani na kutulia.

    "Huo mlango unafunguliwa kwa code wamalize hao nimeshaufungua"Hussein alisema.

    Shamim alitumia nafasi finyu ya wale askari kujipendekeza pale na kuwavunja shingo zao kwa haraka kisha akafungua mlango kama alivyoelekezwa na Hussein.

    "Nenda left bos kwa haraka sana"alisema Hussein.

    Shamim alifata maagizo ya kijana wake na kwa speed akaondoka kuelekea kushoto na baada ya mwendo mfupi akatokeza kwenye ile kona na hapo kabla hajapewa maeelekezo ya wapi aelekee likatokea kundi la askari wapatao kama sita hivi.

    Wale askari nao walishtuka kumuona Shamim pale wakati alipaswa kuwa kwenye chumba alichofungiwa.

    Wakati wakishangaa Shamim alijizungusha haraka na kupambana na wawili na kuwamaliza haraka.

    Wale wanne waliobaki wakati wakishangaa kilichotokea mmoja alikutana na ngumi ya mbavu huku mkono wa Shamim ukiwa na pini yenye sumu kijana akalegea na kuanguka.

    "Bosi....bosi.....





    Mara baada ya Shamim kuwamaliza wale askari waliobakia aliendelea na safari kupitia kulia kama alivyoelekezwa na Hussein.

    "Simama hapo ulipo"akasema Hussein.

    Shamim alitulia eneo aliloelekezwa ingawa hauona eneo lolote linaloweza kuwa kama njia ya yeye kutoka ndani ya jengo hilo.

    "XD48DX" Hussein aliingiza hizo code ambazo mara nyingi alizitumia kama code malaya kama ambavyo kuna Funguo malaya na mara kwa mara hizo code hazijawahi shindwa kufungua mlango wa siri wa aina yeyote ile.

    "CODE DENIED"alirudishiwa jibu.

    "Agggggh!!"Hussein aligonga kichwa chake kwa hasira.

    Shamim alisubiri ila akaona kama inaweza kumgharimu hivyo akadandia ukuta na kujibanza kwenye paa lenye kona la ile nyumba.

    Hussein alifikiria sana mwishowe akaamua kujalibu kuibadilisha ile code kinyume nyume

    "DX48XD" then akabonyeza SEND na ile mashine ikaanza kuloaad taratibu.

    Loading.................error........

    Akapiga kete kwa hasira ila hakukata tamaa akaituma tena.

    "CODE ACCEPTED" ilirudisha majibu.

    Alijikuta akishangilia mwenyewe pale alipokuwa.

    Shamim akiwa pale juu alishangaa chini ya ardhi eneo alilotumia kupambana na wale askari likifunguka na kuacha shim lenye ngazi za kushuka ndani likiwa wazi.

    Haraka haraka alishuka na kuingia ndani yake kwa kushuka na zile ngazi.

    Alipomaliza kushuka lile eneo likajifunga taratibu bila mtu yeyote yule kujua.

    "Huo ni mlango wa siri nahisi huwa wanautumia viongozi wa kitengo hicho kutoloka au kwa shughuli zao binafsi"Hussein alimwambia Shamim.

    "Ahsante sana Hussein! Ila nimekukubali wewe ni jembe"akasema Shamim.

    "Una mema mengi umenifanyia bosi lazima nilipe fadhila"akasema Hussein.

    Shamim aliendelea kuambaa ambaa na lile shimo kwa kwenda mbele.

    Hussein alibonyeza kitufe chake na kuandika " SEARCH FOR NEW ENTRACE NEAR THE TARGET" akabonyeza kitufe cha kutuma.

    Computer ikaendelea kutafuta kwa muda mfupi ikawaka alama nyekundu nyuma ya eneo alilokuwa Shamim.

    "Bosi rudi nyuma kwa hatua tatu"akasema Hussein

    Shamim akarudi na kuangalia kwa juu akafanikiwa kuona button yenye namba.

    "Bosi bonyeza XD48DX itafunguka na utokee hapo"akasema Huseein

    Shamim alifanya kama alivyoagizwa kisha eneo lile likafunguka taratibu na yeye akachungulia kwa nje.

    Alijikuta ametokea eneo lenye mihangaiko mingi ya watu na magari.

    Akatoka kwa nje.

    "Aisee hapa ni Kariakoo au? Mbona watu wengi hivi??"akauliza Shamim.

    "Acha mbwembwe bosi dakika moja nitakuwa hapo"

    Shamim alitafuta eneo lilotulia akajificha na kwa sababu giza lilikuwepo hakukosa eneo lenye giza.

    Ndani ya dakika chache Hussein alifika na gari kisha akawasiliana na Shamim akaja na kupanda kwenye gari na wakaondoka.

    "Wengine wako wapi Hussein?"akauliza Shamim.

    " Umesalitiwa bosi!"akasema Husein.

    "Unasema??? Nimesalitiwa?? Una maana akina Aboud wamenisaliti mimi? Ooooo My God! What's going on???"akajikuta maneno yakimtoka haraka.

    "Calm down bosi!! Hali imeshatokea lazima tutafute namna ya ku deal na hili swala coz maadui wamekuwa wengi na Akina Abdul wapo mjini wanakusaka"akasema Hussein.

    "Na mzigo wangu ??"akauliza kwa hamaki Shamim.

    "Walinigeuka na kunipiga vibaya sana! Hebu angalia hizi alama...wameuza na kutokomea kusikojulikana"alisema Hussein akimwonesha Shamim alama.

    "We need money to survive Hussein,ngoja nichek balance yangu bank"akasema Shamim.

    Akachukua simu iliyounganishwa na teknolojia ya kisasa zaidi ya Hussein na kucheza nayo akiangalia kwenye account yake ya bank.

    "Your balance is 00.00000"

    Jibu hilo lilisababisha kijasho chembamba kitililike kutoka shingoni na kushuka na mchilizi wa uti wa mgongo mpaka makalioni.

    "Nini bosi mbona umechange ghafla? Kuna tatizo??"akauliza Hussein.

    "Junior......Junior.....fuck u......u'r going to be the 1st to die"akasema Shamim.

    "Kuna nini bosi?? Junior kafanya nini?"akauliza Hussein.

    "Junior amechukua pesa yangu kwenye account yote"akajibu Shamim







     Junior alishtuka sana kutokana na hali iliyomkuta Joan.

    Ikabidi aombe watu wamsaidie kumbeba Joan na kutafuta gari ikamkimbiza hospitali haraka sana.

    Alipokelewa haraka na kuanza kuhudumiwa na daktari aliyekuwa pale.

    "Amepatwa na mshtuko mdogo tu kijana usiwe na wasi wasi atakuwa sawa muda si mrefu"akasema Daktari akimwambia Junior.

    Junior alikaa kwenye dawati dogo lililokuwa pale na kusubiri.

    Baada ya saa nzima Joan alirudiwa na fahamu na Daktari akashauri aachwe apumzike kwa saa nyingine.

    "Hapana Dokta tuko safarini naomba tuondoke "akajibu Junior.

    Walirumbana kwa muda na Daktari yule na mwishowe Junior akashinda na kuruhusiwa kuondoka na Joan.

    Walielekea kwenye Hotel waliyopanga bila kusemeshana chochote.

    Walipofika Junior akaanza kupanga vitu vyao ili waondoke.

    "Vip? Mbona unapanga mizigo?"akauliza Joan.

    "Itabid tuondoke leo hii hii na magari yanayotoka Dar kuelekea Mbeya na huko tutajua cha kufanya ili kutoloka kwenda mbali ambako hataweza kutupata"akajibu Junior.

    "Hivi unaweza kumkimbia Shamim wewe? Umesahau kuna kifaa alikuwekea mwilini na hujui kilipo kinachomsaidia kukuona popote pale? Me sikushauri hivyo bali tungerudi na kumtafuta kisha umuombe msamaha na kwa sababu Shamim anakupenda atakusamehe"akasema Joan.

    "Nini? Nirudi Dar? Kwa Shamim? Nafikiri humjui Shamim vizuri! Nakuhakikishia uwe umeenda mwenyewe! Au amekukamata yeye atakachokufanya ni kukukata kiungo kimoja kimoja kama nyama ya kuku mpaka uishe! Siwezi"akasema Junior.

    "Mmmmmh!"akaguna Joan.

    " Hapa cha msingi totoloke haraka na huko mbele nitaitoa hii GPS kwenye ulimi! Kwa sababu alinambia mwenyewe kuwa aliifunga kwenye ulimi wangu"akasema Junior.

    Walikusanya mizigo yao yote na kisha wakatoka Hotelin na kuelekea stand ya mabasi.

    Junior alinunua kofia kubwa iliyoweza kuziba sehemu kubwa ya uso wake na pia akamnunulia Joan ya kwake kwa sababu alijua mara baada ya Shamim kutoloka askari wangewatafuta na wao na hivyo alilenga kujilinda kabla hajatambulika.



    Shamim alichukia sana kiwango ambacho hata Hussein alijua kuwa kweli Shamim kachukia sana.

    Shamim alichukua tena ile simu na kupiga namba kadhaa

    "Nipe taarifa ya mali zangu zote?"akauliza.

    "Kwa taarifa ya haraka tu ni kuwa yule dogo uliyekuwa unaishi naye kauza mali zote kwa bei ya hasara na ametoloka hajulikani alipo mpaka sasa"akajibiwa.

    "Umeshindwa vip kuzuia hili?"akauliza kwa ghadhabu.

    "Kila kitu alikifanya usiku wa kuamkia leo na sikufaham chochote na pia watu walijua umekamatwa na hauwezi kutoka bosi ndo maana wakakubali na izingatiwe kuwa dogo alikuwa na hati zote"akajibiwa.

    Alikata simu kwa hasira!!.

    "Junior ana GPS jalibu kumtafuta harakaaa!!"alifoka Shamim akimwambia Hussein.

    Hussein aliona hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya hivyo akawasha Laptop yake na kuanza kucheza nayo kwa kasi kubwa sana.

    Ndani ya dakika chache alam nyekundu ikaanza kuwaka.

    Ikabid Hussein aanze kufatilia ile alam inapowakia na kuiiingiza kwenye Google Maps.

    "Yupo Iringa bosi kwa muda huu"akasema Hussein.

    "Huyo anatoloka kuelekea Mbeya na nahisi amelenga safari yake iwe kuelekea Afrika ya Kusini! Very simple ntamdaka kama paka anavyodaka panya! Tunapataje pesa now?"akasema Shamim akimwelekeza Hussein.

    "Hakuna zaidi ya Bank bosi"akaibu Hussein.

    "Kuna vifaa vya kazi hapa ndani?"akauliza Shamim.

    "Kila kitu Bosi"akasema Hussein

    "Washa gari na tafuta Bank iliyopo kalibu"akasema Shamim.

    Walitoka eneo lile speed na Shamim akarudi kwenye siti za nyuma na kuvaa nguo za kazi huku akibeba vifaa vyake vyote kisha akabeba mfuko maalumu wa kazi.

    Gari ilipaki kwenye Bank ya biashara maeneo ya posta umbali wa mita kama mia na hamsini kisha Shamim akashuka na kupotelea gizani.

    Askari wanne walikuwa wamegawana vitengo vya Bank ile kwenye swala la ulinzi huku kila mmoja akiwa eneo lake.

    Askari wa kwanza alijikuta chini kama mzogo maa baada ya kupuliziwa dawa maalumu ya usingizi iliyokuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa haraka zaidi.

    Wa pili aligeuka ili kutafuta sehemu apumzike akakutana na Shamim uso kwa uso na yeye akapuliziwa dawa na Shamim akamuwahi shingoni na kumminya kwenye mshipa wa fahamu akaanguka chini.

    Akakiona kioo cha ofisi ya bank ile.

    Alitoa spray yake ya kukatia vioo akaanza kukata taratibu.

    "Tulia hivyo hivyo ulivyo..."alisikia sauti ikimwambia na kweli akahisi kitu cha baridi kikimgusa kisogoni.





     Abdul hakuamini kama alichokisikia ni kweli kabisa kinaweza kuwa kimetokea.

    "Hapana siamin!! Yaani na ulinzi wote huu ameweza kutoloka?? Lazima nihakikishe"aliwaza Abdul.

    Alitoa ishara kwa vijana wake na wakaondoka na kutambaa kwa tumbo mpaka wakawafikia askari wawili waliokuwa eneo lile na kuwaweka chini ya ulinzi kisha wakawakokota mpaka Abdul alipokuwa kasimama.

    "Sina shida na nyie ila nahitaji mnijibu swali langu pekee!"akasema huku akiwa kawawekea bastora shingoni.

    "Nani aliyetoloka??"aliwauliza na wakati huo huo wale askari walikuwa wakitetemeka kwa uoga uliopitiliza kwani tangu wamalize mafunzo yao na kuwa askari kamili hawakuwahi kuwekewa silaha hata siku moja shingoni mwao hivyo siku hiyo waliiona kama siku mbaya zaidi katika maisha yao.

    "Ametoloka.....ametoloka yule!"akajibu mmoja.

    Abdul aliachia bonge la kofi kwenye shavu la yule askari mpaka akaanguka chini.

    "Ametoloka yule gaidi aliyekuwa amekamatwa! Tafadhali usiniue"yule askari aliyebaki alisema haraka ili aepukane na ile adhabu ya Abdul.

    "Shamim ametoloka? Ametoloka vip? Na huo ulinzi wote mlionao?? Niambie ametoloka vip?"aliongea kwa hasira akimpiga na kitako cha bunduki yule askari.

    "Hakuna anayejua alivyotoloka jaman! Mtatuua bure wakati sisi hatuhusiki na chochote kile jaman"alilalama yule askari.

    Abdul alitoa bastora yake na kuwapiga risasi askari wale mpaka alipohakikisha wote wamekufa.

    Akaanza kuzunguka zunguka huku na kule akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa.

    Kwa hesabu zake za haraka alitegemea kumkuta Shamim kizuizini akiwa kafungw pingu mikono na miguu kiasi cha kutoweza kufurukuta kisha ammalize kirahisi mara baada ya kuwamaliza askari watakaokuwa wakimlinda.

    Kitendo cha Shamim kutoloka mikononi mwa askari wa usalama wa Taifa kilimfanya amuone Shamim kama mzimu ambao kupambana nao ilikuwa kazi kubwa sana.

    "Bosi mimi naona tuahilishe kupambana na Shamim na turudi Mombasa kuendeleza zile mali zilizobaki ni nyingi na zinatosha"alisema askari mmoja.

    "Unasema??"aliuliza kwa hasira Abdul.

    "Unajua gharama ya hiyo mali aliyochukua Shamim?? Unaweza kuropoka ujinga kama huo mbele yangu??"alifoka Abdul.

    Alimmiminia risasi zisizo na idadi huyo askari pale chini mpaka zilipoisha kwenye ile silaha yake ndipo akatulia huku akitweta.

    Pamoja na kumuua yule askari lakini katika hali halisi lile swala la Shamim lilimuumiza kichwa sana.

    "Tunaanza msako wa Shamim usiku huu huu kabla hakujakucha tuwe tumemtia mkononi! Tunatawinyka wengine wataenda kwake a wengine mtaani maeneo aliyopenda kuwa na tuwe tunapena ripot"akasema Abdul.

    "Lakini bosi Shamim alifungwa GPS itakayotusaidia kumpaka kirahisi"akasema mmoja wao.

    "Naomba uongee ukiwa na akili zako zote sawa? Kumbuka unayemuongelea ni zaidi ya mzuka! Kwa akili yako atakuwa bado na hiyo GPS wakati ameasi?? Haya ondoka haraka"akafoka.



    Upande wa Shamim aligeuka taratibu na kuangaliana na yule askari usoni.

    "Unataka nini eneo hili na muda huu?"akauliza yule askari.

    "Nataka roho yako!"akajibu Shamim kwa kujiamin.

    "Heeeee!!"alipigwa na mshangao yule askari.

    Akawahi kubonyeza kitufe cha kutoa risasi ila Shamim akamuwahi na kubana kidole cha kubonyezea na kwa maumivu yale yale yule askari akiwa hajapata nafasi ya kufikiri Shamim akabonyeza kibutton cha kufungia sehemu ya uweka risasi kisha akaziachia na risasi zote za ile silaha zikadondoka chini.

    Kisha akamuachia yule askari silaha yake.

    Askari akabinyeza lakini hakuna risasi iliyotoka.

    Kwa wakati huo Shamim alikuwa na hasira kali sana za kusalitiwa na Junior pamoja na vijana wake.

    Aligeuka kama anampa mgongo yule askari.

    Na kwa kiherehere chake akainama kuokota risasi badala ya kukimbia.

    Shamim aligeuka na vifaa vitatu vya ularuzi na sekunde zilizofata mwili wa askari ulke ulitapakaa damu huku utumbo wake ukichungulia nje.

    Hakutoa japo mlio wowote ule.

    Kwa kujiamin kabisa Shamim akaingia ndani ya benki ile huku akizimiwa kamera na Hussein aliyekuwa na Laptop yake kwenye gari.



     Gari ilikuwa katika mwendo kasi kupita kawaida huku ikiendeshwa na Herman mmoja wa vijana walioasi kutoka katika utawala na uongozi wa Shamim.

    Ilipita mji wa Madison bila kusimama na kuelekea moja kwa moja katika mji wa Crystal Cedar na kusimama ili wapate chakula cha mchana kabla ya kuendelea na safari.

    "Ant samahan!"alisema Aboud.

    "Bila samahan!"akajibu Catherine mhudumu wa muda mrefu wa wa mgahawa ule wa Mc Leakey.

    "Kuna umbali gani hapa mpaka kwenye mji wa Brownsvile kwenye mpaka wa Mexico kupitia kwenye mji wa St Antonia Texas nchini Marekani?"akauliza.

    "Ni kama masaa matano hivi kama gari yenu ina speed nzuri ila kama mnaenda kwa mwendo wa kawaida ni masaa saba"akajibu yule binti.

    Wakaridhika na jibu lake.

    "Tutaingia usiku na kwa mujibu wa maelekezo ya wale jamaa tunapaswa kukutana kabla ya kufika mji wa Brownsville ila kuna mji tutapita wa Laredo na kumaliza bishara eneo lile ndo tutavuka kuingia Texas"akasema Herman.

    Wakakubaliana kuongeza speed ya gari yao ili wawahi kufika Laredo.

    Speed iliongeza mara baada ya kutoka kwenye mgahawa ule kuelekea eneo la biashara.

    Wakiwa kwenye gari Mahmoud Jr akatoa Laptop yake na kuanza kutembelea mitandao mbalimbali ya habari na mwishowe akafika kwenye blog za Watanzania.

    "Haaaaaaaaaaaaaa!!! Mungu wangu"aliropoka kutokana na habari aliyokutana nayo.

    "Vip tena wewe?? Mbona unatushtua?"wakauliza wenzake.

    "Shamim???......balaa limeanza jaman!!"akasema tena.

    Ikabidi wenzie wamnyang'anye ile Laptop yake na kuangalia kilichoonwa na mwenzao.

    Kila aliyeangalia ile habari alibaki akishangaa bila kuongeza neno lolote.

    Ilibidi dereva apaki gari lao pembeni na wakajadiliana cha kufanya.

    "Jaman hali imeanza kuingia mdudu! Na huyu atakuwa Hussein tu na si mwingine! Shamim asingeweza kutoka!"akasema Herman.

    "Jaman tusilaumiane jaman! Cha msingi tuendelee na safari kisha tuuze mzigo huu na mara baada ya kuuza kila mmoja atajua pa kuelekea bila kumwambia mwenzie ili hata Shamim akikupata ushindwe kujua mwenzio alipo na kumtaja"akashauri mmoja wao.

    Waliendelea kushauriana na mwishowe wakaamua kuendelea na safari yao.

    Wakati wakiwa safarini Herman aliendelea kucheza na Laptop yake kwenye mitandao yao kisha akakutana na ujumbe kwenye email yake uliomshtua sana.

    "MMENISALITI SIYO?? POA NIPO NYUMA YENU NA NAWAPA SIKU MBILI PEKEE NTAWATIA MKONONI MWANGU"



    Upande wa Shamim alipommaliza yule askari aliingia ndani ya bank ile na kuiba kiwango kikubwa sana cha pesa na kutoka kurudi kwenye gari.

    Alimkuta Hussein akicheza na mtandao huku akiendelea kulinda lile eneo.

    Wakati Shamim anapanda kwenye gari alijikwaa na kujigonga tumbo.

    Tumbo lilianza kumuuma akasaidiwa na Hussein kupanda.

    "Hussein nahisi nakoelekea sitaweza kupambana kirahisi"akasema

    "Kwanini bosi?"akauliza Hussein.

    "Mimba!!"akasema Shamim.

    Hussein alishtuka sana kusikia vile kwani hakutegemea kuwa pamoja na mihangaiko ya kazi bosi wake angeweza kuwa na ujauzito.

    "Ujauzito? Mmmmmh!! Ya nan tena bosi?"akauliza Hussein.

    "Ya Junior"akaongea taratibu kisha akaweka kituo.

    La mimba lilimshtua sana Hussein ila ile mimba kuwa ya Junior ilimpa mshtuko mkubwa zaidi.

    "Bosi........."akasema Hussein.

    "Nyamaza kwanza! Naomba umtafute Junior alipo kwa sasa!"akasema Shamim.

    "Ana GPS?"akauliza Hussein.

    "Ndiyo anayo"akasema Shamim.

    "Code bos!"akauliza Hussein.

    "GC11 angalia kwa makini namhitaji sasa hivi"akasema Shamim.

    Akaanza kumtafuta kwa kuunganisha mitambo yake kwa satelite huku akiunganisha na Google map.

    Sekunde chache baadae taa ikaanza kuwaka katikati ya Tanzania.

    Akaifailia aki zoom ile ramani yake mpaka ikasoma eneo alilolitaka.

    "Yupo Iringa bosi"akasema Hussein.

    "Are you sure?"akauliza Shamim.

    "Yes bosi hii ni Iringa"akajibu.

    Shamim akatoa ile simu ya Hussein na kuchukua namba flani kutoka kwenye karatasi kwenye mkoba kisha akapiga.

    "Kisu!"akaita Shamim.

    "Naam"sauti ya upande wa pili iliitika.

    "Kuna tenda ya kuua lakini bili yake isizidi millioni sita"akasema Shamim.

    "Ok kwa sababu yako nitafanya"akasema Kisu kwenye simu.

    "Jiandae kesho asubuhi unapaswa kuwa Iringa! Hupaswi kumpoteza na ni lazima kesho afe"akasema kwenye simu.





    Mwanadamu mwenye sura mbaya yawezekana kuliko wote ambao nilishawahi kuwaona maishani mwangu aliingia kwenye mkoa huu wenye baridi sana wa Iringa akiwa na lengo la kutimiza kazi iliyomleta katika mji huu.

    Ungepata nafasi ya kukutana na Kisu kama hujawahi kupitia maisha ya kibabe ubabe basi ungeweza kujikojolea peke yako.

    Alikuwa na sura iliyoharibika zaidi ya mwanajeshi aliyetoka kwenye vita ya Iraq au huko Somalia na ungepata nafasi ya kumwangalia kwa ukalibu ungedhani kuwa amelipuliwa na bomu na kufikia hatua ya kuharibika sura kiasi kile.

    Sura yake ilikuwa na jicho moja bovu na pia kovu kubwa sana lililouzunguka uso wake.

    Alama hiyo hakuzaliwa nayo bali siku aliyoenda kinyume na maagizo ya Shamim alijikuta kwenye ndoo yenye acid huku akidumbukizwa uso wake mzima kwenye ndoo hiyo.

    Kwa bahati mbaya jicho moja liliharibika vibaya sana ikabidi awekewe jicho la kondoo ila lile la pili likapona ingawa nalo liliharibika kiasi.

    Sura hiyo mbaya ujumlishe na umbo kubwa alilojaaliwa Kisu ndivyo vilivyomsaidia katika kuifanya kazi hii kwa uhakika.

    Kazi ya kuua kwa Kisu ilikuwa ajira tosha aliyofundishwa na Shamim kwa siri sana na kufanikiwa kuiweza vizuri bila tatizo na aliifanya kwa kiwango kizuri kama wewe unavyoweza kuifanya kazi yako kwa ustadi.

    Aliingia kwenye Bar aliyeoelekezwa na Hussein aliyekuwa akifatilia nyendo za Junior na Joan kwa kupitia kompyuta yake kwa mitambo aliyoiunganisha na satelite.

    Alipoingia pale ndani ndiyo muda ambao Joan alikuwa kapoteza fahamu kwa kuanguka na baada ya muda mfupi aliamka.

    Kutokana na tukio lile kujaza watu wengi sana eneo lile alishindwa kwenda kulitekeleza kwa uhakika ikabidi atulie akitafuta wakati mwafaka kwa ajili ya kazi ile.

    Muda mfupi baadae aliwaona Junior na Joan wakiondoka eneo lile mpaka magari ya kukodi yalipokuwa na kisha wakachukua Tax na kuondoka.

    "Naomba uifatilie ile gari mpaka mwisho nitakulipa vizuri"Kisu alimwambia dereva wa pikipiki aliyemkuta eneo lile.

    Wakaanza kuwafatilia akina Junior taratibu bila wao kujua wanafatiliwa.

    Walienda mpaka kwenye Hotel waliyofikia na kushuka kisha Junior akamshikilia Joan mkono na kuingia naye ndani.

    Kisu alimkabidhi yule dereva wa bodaboda shilingi elfu kumi na kuondoka bila kuongea chochote kile.

    Yule dereva aliondoka haraka sana ili tajiri wake asijekubadili mawazo kwa sababu pesa ile ilikuwa kubwa kulingana na eneo walilotembea.

    Junior walipoingia chumbani na kuanza kujadiliana juu na kilichotokea na namna ya wao kutoloka Kisu alikuwa kasimama nje ya mlango wa chumba kile akiwasikiliza kwa makini.

    Baada ya muda mfupi majadiliano yalikoma na Junior na Joan wakafungua mlango ili watoke na kutoloka kama walivyopanga.

    Walikutana na mdomo wa bastola iliyofungwa kiwambo cha kuzuia sauti isitoke umbali mrefu ikiwatazama mbele yao.

    "Ingekuwa poa sana kama mngekuwa wapole na tukarudi ndani kujadiliana kwa amani badala ya kuleta fujo kisha nimwage damu hapaha"alisema Kisu.

    Taratibu huku wakitetemeka kuliko kawaida walianza kurudi nyuma mpaka ndani.

    Kisu aliwaeelekeza wakae kitandani na yeye akakaa kwenye sofa iliyokuwa pale ndani.

    Kwa kumwangalia tu Junior alimkumbuka kuwa huyu ndiye yule muuaji ambaye alikuwa akiua watu kule Mosji kwenye msiba wa kaka yake hasa wakati ule alipokuwa kwenye wakati mgumu kalibia kukamatwa kwa mauaji ya kaka yake.

    "Kisu!?!"alijikuta akiropoka.

    "Ndiyo mimi Junior na kazi yangu unaijua vizuri! "akasema Kisu.

    Akatoa vitu flani kutoka kwenye mkoti wake na kuviweka kwenye meza kisha akatoa karatsi na kuiweka pale mezani.

    Akaanza kuchukua vile vitu na kuviweka kwenye ile karatas.

    "Naomba muda kidogo nile kijiti niwe freshi kisha twendelee na kilichonileta"akasema.

    Akaisokota ile karatasi na vile vitu vikiwa ndani yake ikawa kama sigara kisha akaanza kuvuta kwa fujo na kusababisha moshi wa ile bangi ujae pale ndani.

    Kisu akatoa simu na kupiga namba kadhaa.

    "Bosi nimewapata na wako mbele yangu........ndiyo....haina shida kama unataka kusikia jinsi itakavyofanya mauaji haya"akasema

    Akachukua simu yake na kuweka roud speaker kisha akaiweka pembeni ya Junior.

    Akatoa ile silaha yake na kupiga risasi.

    "Paaaaaa!

    "Paaaaaa!!

    Milio miwili ya risasi ilisikika kwenye sehemu ya kusikilizia kwenye simu ya Shamim.







    Shamim aliisikia ile milio miwili ya risasi na kelele zilizopigwa kwa maumivu makali na kisha Kisu akachukua ile simu na kuongea naye.

    "Nimemaliza kazi uliyonituma"akasema Kisu.

    "Nashukuru kwa kumaliza kazi ila bado hujamaliza kama tulivyokubaliana"akasema Shamim.

    "Haina tatizo bosi nipe maelekezo ya sehemu husika"akasema Kisu.

    "Nenda mpaka Bagamoyo kalibu na yale majengo ya makumbusho njiani kabla hujayafikia kuna contena la blue na ingia ndani ya lile kontena kwa ndani kuna sehemu katikati ipo kama imepakwa rangi ya blue.banda ile alama ya blue na mlango utafunguka kuingia chini! Huko ndo kila kitu kitaishia"akasema Shamim.

    "Nimekwelewa bosi"akajibu Kisu.

    "Kila kitu utaacha chini ya uangalizi wa wale utakaowakuta kule na kama kuna maagizo mengine nitakutafuta"akasema Shamim.

    "Nimekusoma mkuu"akajibu kisu.

    "All the best"akasema Shamim na kukata simu.

    Kwenye chumba alichowekwa Shamim wakati akiwa chini ya ulinzi wa usalama wa Taifa kijana mmoja matata sana na aliyekuwa akiaminiwa na serikali katika mambo yanayohusu usalama wa Taifa alikuwa akijalibu kutafuta japo chochote kilichoanchwa na Shamim kiweze kumsaidia katika utendakazi wake.

    Aliona unywele mdogo sana pembeni ya eneo mapambano yalipotokea na akauchukua.

    "Nahitaji DNA test za hii nywele ili niweze kulinganisha na ile sample iliyopatikana kipindi kile"akasema kijana huyu.

    Mkuu wa kitengo cha usalama wa Taifa alichagua kumpa kazi kijana huyu ambaye bado damu yake ilikuwa inachemka aliyepitia mafunzo mbalimbali juu ya ujasusi ili waweze kumtia mikononi Shamim ili kuliondoa jeshi la polisi katika aibu kubwa ya kutoloka mtuhumiwa akiwa mikononi mwao.

    "Kijana mtu unayeenda kumtafuta siyo wa kitoto ujue! Ni mtu aliyeiva tena yawezekana kuliko wewe hivyo inakupasa uwe zaidi ya makini"Martin alikumbuka maneno ya mkuu wake wa kazi.

    Alitoka eneo lile na kufata mkondo wa mapambano wa Shamim ulivyoenda mpaka eneo lile lenye mlango wa siri.

    "CCTV zinasema aliingilia hapa kwenye mlango wa siri! Nahitaji maelezo kuhusiana na huu mlango"akasema.

    "Huu ni mlango wa siri ambao hakuna askari anayeufahamu zaidi ya wakubwa kwa sababu ndiyo unaotumiwa wakati wa matatizo"akasema mmoja wa vijana walioongozana naye.

    "Ina maana kuna mtu kwenye idara aliyempa siri juu ya huu mlago? Na aliwezaje kufungua wakati hauna namba hapa na haufunguliwi bila kompyuta ya ndani?"akauliza.

    Wakati anaongea na wale vijana aliokabidhiwa kufanya nao kazi simu yake ikalia.

    "Ndiyo bosi"akasema.

    "Hali inazidi kuwa mbaya na wananchi hawataweza kutuelewa kama tutaendelea kushindwa kumshika huyu binti"akasema mkuu wake wa kazi.

    "Kuna nini kwani?"akauliza Martin.

    "Kuna matukio matatu yameripotiwa tangu atoloke! Kuna bank imeibiwa na askari wameuawa na pia kuna vijana sita wamekutwa wameuawa huku walizni na majirani wa nyumbani kwake nao wakikutwa wamekufa"akasema mkuu wake.

    Taarifa ile ilimchanganya sana Martini kwani alianza kuona ugumu wa kazi aliyopewa.

    Abdul alipokea simu iliyomuacha njia panda juu ya kuendelea kumsaka Shamim.

    "Bosi Shamim amewaua wenzangu wote hapa na amenambia nikupe taarifa usiendelee kumfatilia atakumaliza mapema sana"hiyo ilikuwa taarifa kutoka kwa kijana wake.

    Dakika chache baadae Abdul alikuwa eneo la tukio na kufanikiwa kushuhudia vijana wake kadhaa miili yao ikiwa imezagaa chini ikiwa imeharibika vibaya.

    "Wewe ndiye umeachwa hai si ndiyo?"akamuuliza yule kijana.

    "Ndiyo bosi"akajibu yule kijana kibwege sana.

    Risasi kadhaa zilikichakaza kifua cha yule jamaa.

    Na hapohapo simu yake ikaanza kuita tena.

    "Ndiyo ongea"akasema.

    "Bosi nimemfatilia yule mpenzi wake na Shamim yule Junior nimemkuta hapa ameuawa hotelini"akasema aliyepiga simu.

    "Ameuawa? Ina maana Shamim yupo Dar au Iringa? Mbona mnanichanganya?"alijibu Abdul.

    Abdul alikuwa na haki ya kuchanganyikiwa kwa sababu alitegemea kumpata Junior kisha amtumie kama chambo ya kumnasa Shamim



    Abdul hakuamini kile kilichotokea pale alipowakuta vijana wake wakiwa chini hawana uhai.

    Wakati akihangaika kuziangalia zile maiti alikututana na ujumbe kwenye karatasi moja ikiwa chini.

    "UKIENDELEA KUNIFATILIA ITAFATA ZAMU YAKO" aliusoma kwa makini ule ujumbe na kujikuta akizidi kutishika juu ya shamim.

    Hakumwambia mtu chochote kati ya wale vijana wake aliokuwa nao bali aligeuka na kupanda gari yake kisha akaondoka eneo lile.

    Alifika kwenye ile nyumba waliyofikia na vijana wake akaingia moja kwa moja ndani.

    Alipitiliza mpaka chumbani kwake ili apate nafasi ya kupumzika na kuwaza cha kufanya juu ya Shamim.

    "Kalibu sana"sauti ya Shamim ilimpokea chumbani.

    Alishtuka sana tena sana!!!! Kumkuta Shamim akiwa ndani kwake ametulia akimwangalia.

    "Aa..umei..."alijikuta kigugumizi kikimshika na kushindwa kuongea chochote.

    Ghafla akili ikamjia na akapeleka mkono wake kiunoni ili achukue silaha kwani alishaona dalili za mapambano zimeshaanza.

    Hakufaikiwa kutoa ile silaha kabla Shamim hajamrukia na kumpa pigo moja takatifu lililompelekea agonge mlango na kutoka nje ya chumba.

    Shamim alitaka amalizane na Abdul ndani bila wale vijana wake kujua ila kitendo cha kutupwa mpaka nje kilisababisha washtuke na kuingia ndani haraka.

    Risasi nyingi zilipigwa kuelekea eneo alilokuwa Shamim na isingekuwa wepesi wake wa kuruka na kutua kwa mbali basi risasi zile zote zingetua mwilini kwake.

    Alitoa visu vyake vya kutosha na kujiandaa kwa mapambano.

    Risasi ziliendelea kurindima kwenye ile sebule na kuichachafya ila hakuna iliiompata Shami kwan alikuwa kajiegesha sehemu nzuri.

    Walipoona ukimya umezidi wakaamini wameshammaliza na hivyo wakaanza kusogelea eneo lile ili kushuhudia kama wamemmaliza kweli.

    Shamim akiwa kajilaza pale chini aliibuka kama mzuka na kuachia visu vinne vikatua kwenye miili ya vijana wale na kuwafanya waende chini kwa maumivu.

    Alijizungusha haraka na kukutana ana kwa ana na watatu miongoni mwao akatoa mapigo ya uhakika kwenye shingo zao na wao bila ridhaa yao wakaenda chini.

    Wakawa wamebaki vijana wanne waliokuwa wakijiandaa kutumia bastora zao kummaliza.

    Shamim alimuwahi mmoja na kumuweka kama ngao hivyo risasi za wale wenzake zikatua kwenye mwili wa huyo.

    Kisha akamsukuma na kuwagonga wale waliokuwa wakishambulia.

    Wakati wakipambana na ile maiti Shamim hakukawia kuwachoma sindano yenye sumu haraka haraka kila mmoja akalegea na kutulia huku mwili wake ukianza kuwa mweusi kama mkaa.

    Kabla hajaamua cha kufanya alipokea teke mbili za mbavu kutoka kwa Abdul aliyekuwa pembeni akiangalia mchezo mzima ulivyokuwa ukienda.

    Shamim alienda chini mzima mzima huku akisikia maumivu makali sana.

    "Mama yangu hivi mimba yangu itakuwa salama kweli? Napaswa kuwa makini sana"aliwaza mwenyewe.

    Abdul alimfata pale pale chini bila kumpa nafasi akamshindilia ngumu za haraka haraka usoni, Shamim akatapakaa damu.

    " siwezi kukupa nafasi ya kufikiri Shamim! Nakujua ulivyo mbaya"aliongea kwa nyodo Abdul.

    Akafatia mateke ya haraka hara kwenye mbavu tena na kuzidi kuhatarisha maisha ya kiumbe kile cha tumboni.

    Shamim alijitutumua na kuamka ili akabiliane na Abdul.

    Abdul alikuja kichwa kichwa akijua ameshampa Shamim maumivu yatakayosababisha ashindwe kumkabili ila alishangaa ngumi zake zikipanguliwa kiustadi bila matata.

    "Haaaaaaaa!!"alijikuta akishangaa mpaka kufikia kuongea.

    "Sema tena Heeeeee!!"alisema Shamim.

    Abdul akataka kurudi nyuma ajipange ila Shamim hakumpa nafasi.

    Alimpa mapigo ya haraka haraka ila yote Abdul aliyaona ikabidi Shamim atumie akili ya ziada.

    Akaambatanisha pini yenye sumu katikati ya vidole vyake na wakati Abdul akipangua akachomwa na ile sindano.

    "Umenichoma nini wewe malaya?"akauliza

    Ila alijikuta nguvu zikimwishia taratibu na mwishowe akaanguka chini mwenyewe.

    Shamim alikaa na kutulia akipumua mara baada ya kazi hiyo nzito.

    Ila wasi wasi wake ukawa juu ya yale mapigo ya kwenye mbavu kama mwanae tumboni atakuwa salama kweli!

    Wakati akiwaza hayo alishangaa simu yake ikawa inaita.

    "Hussein kuna tatizo?"aliuliza.

    "Junior katoloka na inaonekana ameng'oa GPS kwa sababu simpati kabisa"akasema.

    "Unasema!??"akauliza kwa mshangao.



    Wakati Kisu anajiandaa kutoka Dar kuelekea Iringa alipewa maelekezo ya kazi anayoenda kuifanya na Shamim vizuri.

    "Namhitaji yule mwanaume kwa sababu nampenda sana na pia nina kiumbe chake tumboni! Nisingependa kuona mwanangu hamfaham baba yake"alisema Shamim.

    "Kwa hiyo mimi naenda kufanya nini Iringa sasa? Na si ni yeye aliyekusaliti?"akauliza Kisu.

    "Yule mdogo wangu ambaye amekuwa mwiba kwenye uhusiano wangu na yule kijana ndiye natafuta namna ya kumwondoa Duniani"akasema Shamim.

    "Kwa hiyo unataka nimuue yule binti waliyenaye?"akauliza Kisu.

    "yap! Nahitaji yule binti aondoke Duniani ila nataka tucheze michezo miwili kwa wakati mmoja"akasema Shamim.

    "Michezo gan?"akauliza Kisu.

    "Nahitaj kuwapoteza maboya serikali na pia kumpoteza boya Abdul hivyo nahitaj Junior aonekane kafa kwa macho ya wengi ila siri yake nibaki nayo mimi na wewe"Akasema Shamim.

    "Kivip?"akauliza Kisu.

    "Ukifika mpige risasi ya kifuani kwenye moyo yule binti mbele ya Junior! Kisha mpige na Junior risasi ya bega la kulia"akasema Shamim.

    "Baada ya hapo?"akauliza Shamim.

    "Kuna maiti ya askari niliyemuua jana utaondoka nayo na kwenda nayo Iringa nimeshaivisha sura bandia ya Junior na hata kimo ni kile kile! Utakapofika utaiingiza ndani na kumvua Junior nguo kisha mvishe yule na muache! Naamin kila mmoja ataamin kuwa ni Junior na ujue serikali itamtafuta Junior kwa ajili ya kuwasaidia kunishika"akasema Shamim

    waliendelea kupeana maelekezo ya nini kifanyike mpaka wakaelewana.

    Shamim akampa Kisu malipo yake ya awali.

    "Kisu!!"akaita Shamim.

    "Naaam!!"akaitikia Kisu.

    "Huwa siruhusu makosa katika kazi zangu! Pili huwa sisalitiwi! Tatu sitegemei uzembe"akasema Shamim.

    "Usijal bosi"alijibu Kisu lakini moyoni alikuwa bado na hasira na Shamim kutokana na kile kitendo alichowahi kufanyiwa na kuhalibiwa sura.

    Kisu alipoingia Iringa alihakikisha amefaham Hotel waliyofikia akina Junior na kwa siri akafanikiwa kuingiza ule mwili ndani ya chumba chao.

    Ndipo alipoana kuwafatilia mpaka wanarudi na kupaki mizigo ili waondoke akajitokeza.

    Alipomaliza kuvuta bangi alimpiga risasi Joan kama alivyoelekezwa na Shamim na kisha akampiga Junior risasi ya bega.

    "Junior niko kazini lakini napaswa kukusaidia"akasema Kisu.

    "Unanisaidiaje wakati umeshamuua mpenzi wangu?"akauliza Junior huku kashikilia bega lake lililokuwa likivuja damu nyingi sana.

    "Sikulazimishi kukusaidia! Hapa nimetumwa kukuua hivyo kama huhitaji kuishi sema! Mwenzio ni lazima afe na wewe unapaswa kufa kama hutaki msaada"alisema Kisu.

    "Kivip?"akauliza Junior.

    "Nina hasira na Shamim! Yeye ndiye aliyenifanya niwe hivi! Na kisasi changu nitalipa kwa kukusaidia wewe kutoka mikononi mwake na akamatwe na kunyongwa"akasema Kisu.

    Junior hakuelewa kinachoongelewa na Kisu akaona anazidi kupoteza muda hivyo ikabidi ainame uvunguni na kutoa ule mwili aliopewa na Shamim.

    "Vua nguo zako sasa hivi"akasema Kisu.

    Junior bado hakumwelewa ila Kisu ikabidi atumie nguvu na kumvua nguo zote Junior akavalisha ule mwili uliokuwa pale kisha akaupiga risasi mbili za tumboni na kuchukua baadhi ya damu iliyokuwa ikivuja kutoka kwa Junior akampaka yule maiti.

    "Vaa hizi nguo kisha tuondoke kutoka hapa"akasema Kisu.

    Junior alikuwa anaenda kama ng'ombe.

    Alifanya alichosema Kisu ingawa ilimuum sana kumwacha mpenzi wake aliyekuwa anampenda sana Joan ila hakuwa na namna.

    "GPS yako iko kwenye ulimi! Nakupeleka kwenye kambi ya siri ya Shamim kama alivyoniagiza na kazi yangu itakuwa imeisha ila nitarudi na vijana wangu na kukukomboa ili isijulikane kuhusika kwangu na mchezo huu"akasema Kisu.

    Walipanda gari n safari ya kuelekea Bagamoyo ikaanza.

    Walienda kwa muda mrefu sana na mwishowe wakafika na Kisu akawakabidhi vijana wa siri wa Shamim kisha akaondoka mara baada ya kukabidhiwa pesa yake yote.

    Alipotoka pale alienda mpaka Bagamoyo mjini na kuwasiliana na vijana wake waliokuwa Dar es salaam waje Bagamoyo kumkomboa Junior.

    Waliingia kwenye kambi ile usiku sana



    "Nimemaliza kazi ya kwanza ya kumteketeza Abdul napaswa nihakikishe mzigo wangu naupata kisha nipumzike haya mambo ya mapambano kwa ajili ya mwanangu aliyeko tumboni"alisema Shamim.

    "Sawa bosi ila kumbuka Junior katoloka na askari wanakutafuta! Tunakwepa vip hilo?"akauliza Hussein.

    "Junior hajatoloka ila aliyetoloka ni Kisu! Alipomfikisha pale Bagamoyo alirudi kumkomboa na nilishajua hilo tangu mwanzo hivyo niliandaa vijana wangu wakapambana nao na kuwashinda! Ila Kisu aliweza kufanikiwa kumtoa GPS Junior ila hakufanikiwa kuondoka naye"akasema Shamim.

    "Kwa sasa Junior yuko wap? Na Kisu tunamfanyaje?"akauliza Hussein.

    "Hussein leo nilipokuwa napambana nimeshindwa kwa sababu ya hiki kiumbe! Nahitaj kuachana na haya mambo ya mapambano ili nisijempoteza mwanangu! So andaa safari tuondoke kuelekea Mexico"akasema Shamim

    Kwa sababu kikwazo kikubwa kwake kilikuwa ni Abdul hivyo haikumuwia vigumu kuanza mipango ya safari mara baada ya kubadilisha sura yake na kutumia miongoni mwa sura kadhaa bandia alizokuwa nazo.

    Hussein aliandaa taratibu za safari ile mpaka ilipokamilika.

    Wakati huo huo Shamim alijalibu kila njia kumshawishi Junior asahau kuhusu Joan na waanze maisha upya huku wakijiandaa kulea mtoto wao.

    Kwa Junior ilikuwa ngumu ila alikubali ili aondoke kwenye mabalaa ya hapa nchini lakini akipanga huko mbele atawageuka wenzake na kutokomea.

    Safari ilipokamilika walikwea pipa na kuelekea Mexico kwa amani bila bughudha.

    Walipokelewa uwanja wa ndege na matajiri wa kiMexico waliokuwa wakishilikiana na Shamim katika biashara.

    Shamim alipotoka gerezani aliwasiliana na hawa matajiri nao wakawatafuta wale vijana wake waliomsaliti na kuwakamata kabla hawajauza mzigo ule.

    Hivyo siku hiyo Shamim alipelekwa mpaka sehemu waliyofungiwa na kuwaona.

    "Hawa sitawaua ila naomba wasipewe chakula mpaka siku wakifa kwa njaa"alisema Shamim.

    Matajiri wale waliokuwa wakiufaham uwezo wa Shamim na wakimuogopa sana walitii na kutelekeza kila alichoagiza.

    Shamim alipewa pesa kutokana na mauzo ya ule mzigo na kisha yeye akamgawia Hussein asilimia thelathini ya kile kilichopatikana.

    "Nakutakia maisha mema Hussein popote utakapopenda kuishi na ukiwa na shida wasiliana nami kupitia zile njia zetu za mawasiliano"alisema Shamim.

    Walikumbatiana huku kila mmoja akitoa machozi na kisha Hussein akaondoka.

    Shamim aliondoka na Junior na kwenda kuishi Marekani kwenye mji wa Maryland na wakanunua eneo kubwa kwenye ufukwe wa Beach Heaven na kujenga mjengo wa maana kisha wakaishi kwa amani.

    Upendo na amani ilianza kutawala kwenye maisha ya Shamim na Junior na taratibu Junior akaanza kumsahau Joan na kuanza kumpenda Shamim hasa kutokana na Kiumbe alichokuwa nacho.

    Miezi saba mbele Shamim alijifungua mtoto kwenye Hospital ya Asbury Hospital.

    Walifanikiwa kupata mtoto wa kiume waliyempatia jina la Alex kama ukumbusho wa kaka yake Junior.

    Miaka mitatu baadae.

    Mpelelezi maarufu nchini Tanzania aliyefatilia kwa muda mrefu juu ya taarifa za gaidi wa Kisomali kama wao walivyoamini alipata mgeni ofisini kwake.

    "Naitwa Kisu"alijitambulisha.

    "Kisu!? Jitambulishe kwa jina lako halisi kijana hapa ni sehemu ya usalama wa Taifa sio unakuja na majina ya ajabu ajabu hapa"akafoka Martin.

    "Naitwa Jacob Sulleiman maarufu kama Kisu"akajibu.

    "Hilo ndo jina sasa4 enhee!! Unashida gani kijana?"akauliza Martin.

    "Nina taarifa muhimu sana za kuweza kukusaidia wewe"akaongea kwa kituo Kisu.

    Martin alitulia na kumwangalia kwa makini Kisu.

    "Taarifa za kunisaidia mimi! Enheee! Taarifa gani hizo?"akauliza Martin.

    "Ni kuhusu gaidi ambaye amekuwa akiisumbua akili yako kwa zaidi ya miaka mitatu Shamim"akasema kwa kituo Kisu.

    Martin alishtuka na kusimama wima!! Akamtazama vizuri kisu.



    Tangu Alex jr alipokuwa mdogo malengo ya Shamim yalikuwa kumfanya mtoto wa kipekee sana.

    Alianza kumpa mafunzo hatari sana tangu kipindi hicho ili kumfanya aone kama sehemu ya maisha yake.

    Pamoja na kupelekwa shule ila Shamim aligombana sana na Junior juu ya swala la kumpeleka mtoto yule shule ya kulala huko huko kwa sababu alitaka awe tofauti na watoto wengine.

    Miaka mitatu aliyokuwa nayo Alex jr ilitosha kuanza mazoezi makali na ya uhakika ya kumfanya zaidi ya komandoo wa kawaida.

    Wakati mwingine Shamim aliomba ruhusa kwA Junior ya kusafiri akapumzike na mwanaye kwenye fukwe mbali mbali za nchii hii ya Marekani na kwa sababu Junior alikuwa busy sana na kusimamia biashara walizofungua kwenye mji huu aliwaachia wakaenda wenyewe.

    Trip hizo ambazo zilikuwa zikichukua hata wiki mbili Shamim alikuwa akielekea China au Japan na mara chache sana alielekea Korea kwa walimu mabudha waliokuwa na uwezo mkubwa wa kutoa mafunzo kwa ili kumpa mwanaye mafunzo makali sana yatakayomfanya aweze kupambana na mtu yeyote yule Duniani hapa.

    Shamim aliamin mazoezi ndiyo yaliyomsaidia kuweza kuvuka vizuizi kadhaa katika maisha yake mpaka sasa kuwa hapo.

    Alex jr alipofikisha miaka mitano alishakomaa vya kutosha katika maisha ya Karatee na Kung fuu na Kombat.

    "Mama kwani sisi ni wamarekani?"aliuliza Alex.

    "Hapana sisi sio wamarekani mwanangu! Ila sisi ni Watanzania"alijibu Shamim.

    Mara kwa mara Alex alikuwa akijiuliza juu ya asili yake kwani hakuona kama walikuwa wakichangamana saana na wale wamarekani weusi waliokuwa wakiishi nao jilani.

    "Watanzania? Ndo wakina nani hao?"akauliza Alex.

    "Sisi asili yetu ni huko Afrika katika nchi flani hivi ndogo inaitwa Tanzania"akasema Shamim.

    "Sasa kwanini tunaishi huku? Kwanini tusiende kuishi huko? Na ni lini utanipeleka huko nipajue?"akauliza Alex.

    Shamim alifikiria kwa muda na kuona kuwa kuna umuhimu wa kumpeleka mwanae Tanzania apafahamu ili hata siku wao hawapo aweze kujua asili yake ilipo.

    "Haya mwanangu nitakupeleka upafahamu"alisema Shamim.

    Maisha yakaendelea kwa upande wao kuwa mazuri kwa sababu hakuna aliyejua asili ya Shamim na Junior hawakupata shida kabisa.

    Lakini mara kwa mara Alex jr aliendelea kuwasumbua na kuwasisitizia kuhusu kwenda Tanzania ili apafaham kwao.

    Junior alipinga sana lile swala kwa sababu aliona kama kurudi huko ni kujiweka katika mazingira magumu.

    Shamim alisisitiza kuwa miaka imepita mingi hivyo kesi yao itakuwa ilishasahaulika.

    "Hukumbuki kuwa uliishi na kakangu miaka mitatu ukitafutwa na bado askari walikuwa hawajasahau?"akasema Junior.

    "Junior kumbuka ama yako kule kijijini Moshi hajui kama uko hai au umekufa! Twende tafadhali japo apate nafasi ya kumuona mjukuu wake"akaendelea kusisitiza Shamim.

    Kwa sababu ya shinikizo kutoka kwa Shamim na mtoto wao Alex jr ilibidi Junior akubali ingawa kwa shingo upande.

    Taratibu za safari zikaanza kuandaliwa ili kuwafanikishia safari ile.

    Shamim ikabidi aweke tahahali kabla ya tatizo kuwakuta hivyo akawasiliana na Hussein na kumwomba amfanyie mpango wa vijana sita walioiva kimafunzo ili waweze kumsaidia kwa shughuli zake za ulinzi wakati wote atakapokuwa huko Tanzania.

    Wakati Hussein anatafuta vijana kwa ajili ya kazi ya kumlinda Shamim atakapokuwa Tanzania habari zilipenya taratibu na kumfikia Kisu kwa sababu yeye pia alikuwa na kikosi chake.

    Aliposikia kuwa anayetaka ulinzi anatoka Marekani damu ikachemka na kuhisi kuwa anaweza kuwa Shamim.

    Ikabidi atoe kijana wake mmoja kwa siri na kumuunganisha na jamaa aliyepewa tenda ya kutafuta vijana wa kazi.

    "Angalia kwa makini hizi sura saba zilizoko kwenye hizi picha! Huyo gaidi anatumia hizi sura hivyo ukiona kama unayeenda kumlinda ana mojawapo ya sura hizi tafadhali wasiliana na sisi haraka"alisema Kisu akimwonesha picha kadhaa za sura za bandia za Shamim.

    Ikabidi afanye mawasiliano na Inspekta Martin....



    Watu watano walikuwa kwenye chumba kidogo sana na cha siri katika jengo la Usalama wa Taifa wakijadiliana jambo nyeti sana kwa nchi yao ambalo walipaswa kulitekeleza siku hiyo hiyo.

    Mkuu wa Majeshi bwana Kisaba

    Mkuu wa Usalama wa nchi bwana Kajuni

    Waziri wa Ulinzi bwana Herman

    Waziri wa mambo ya ndani bwana Gady

    Na mpelelezi maarufu nchini bwaa Martin Mpao

    "Kijana naomba nikukumbushe kuwa unayemzungumzia ni gaidi mzoefu na ambaye ameshatuacha solemba zaidi ya mara mbili!!!"alisema Herman.

    "Na uhakika kiongozi na ninachowaambia! Mlinipa kazi ya kufatilia hii kesi na hatimaye nimekuja na majibu kwa nini msiniamin? Nawahakikishia ni yeye kabisa"akajib Martini.

    "Jaman tusirumbane! Hapa tupange mikakati juu ya cha kufanya! Na tuwe na tahadhali ya kutosha sana kwa sababu mtu mwenyewe yule ni kama jini"Akasema Kajuni.

    "Kwani kijana wewe umejipanga vip na hili swala?"akauliza Gadi.

    "Nimeshaandaa vijana wangu na askari kama kumi ili wazingire uwanja wa Taifa pale ili akishuka tu tumtie mikononi na kumleta huku"akasema Martini.

    "Kyaaaaaaaaa!!"walijikuta wote wanamsonya.

    " We una akili kweli? Yule ni wa kuleta tena hapa? Af unataka kumshika na vipolisi? Unamjua kweli?"akafoka Herman.

    "Kwani anaingia sa ngap?" akauliza Kisaba.

    "Anaingia sa tisa mchana huu"akajibu.

    Walitazamana kwa muda na kupeana ishara.

    "Kumbe bado muda mfupi! Sasa sikia! Wewe toka nje mara moja tujadiliane"wakamwambia.

    Martin alinyenyuka na kutoka nje ili awaache viongozi hawa wajadiliane kama walivyodai.

    "Sasa jaman sikieni! Kwa mara nyingi huyu gaidi katushushia heshima sana na idara yetu haiaminiki! Kumbuka ilifikia hatua mheshimiwa akataka kutuondoa kwenye hizi nafasi! Sasa nawaambia hii ni nafasi pekee kwetu kujichukulia sia kubwa ya nchi hii"alisema mkuu wa majeshi.

    "Umeongea jambo la msingi sana! Hata mimi nilifikiria hivyo! Tukimkamata sisi tutapandisha chati yetu sana na izingatiwe tuna malengo ya kuja kuiongoza hii nchi bwana" akasema Kajuni.

    "We naye akili yako inawaza kama ya yule mtoto! Unafikiri unaweza kumkamata? Mara ngapi umemkamata na akakuachia aibu? Unataka aibu tena?"akasema waziri wa ulinzi.

    "Kwani wewe una mpango gani?"akaulizwa.

    "Yule tunapaswa tumuulie pale pale uwanja wa ndege bila maswali na tuandae na waandishi wa habari! Sisi ni viongozi hilo litatupandishia chati yetu sana hapa nchini! Picha zitachukuliwa na DNA na ikigundulika kuwa ni yeye ujue tumeshakuwa wakombozi wa nchi hii dhidi ya magaidi"akajibu.

    "Tumuue?? Duuuuuu!! Hiyo sio hatari kweli? Na tutajibu vip kuhusu mauaji hayo?"akauliza waziri wa mambo ya ndani.

    " sikia! Vijana wetu mara kadhaa wameshindwa kumdhibiti mtuhumiwa! Na imefikia hatua wamemkamata na bado akatoloka hivyo na sisi tulipopata taarifa za kiitelijinsia za kuonekana kwake tumeona tusiwatumie vijana wetu! Bali twende wenyewe na alipojalibu kuleta shida ikabidi tummalize pale pale kwa sababu hatari yake tunaijua"akasema

    "Wazo zuri sana! Na ikitokea akawa yeye kweli nchi hii itatuheshimu na yawezekana ikatupandishia chati yetu ya kuingia madarakani mwaka ujao"akajibu Kajuni.

    "Wewe naye!! Unawaza madaraka peke yake!"akataniwa kidogo.

    "Lazima niyawaze kwa sababu ndiyo yatakayonifanya niwaweke nyie rafiki zangu pazuri! Si unaona jamaa anavyotubana"akajibu Kajuni.

    "Sasa sikia mimi nashauri tuwaodnoe polisi na usalama wa Taifa katika hili swala! Naomba nilete kikosi cha makomandoo wa jeshi ishilini walioiva vizuri kabisa! Ili wawe msaada kwetu"akasema

    "Haina shida hilo limepita"akajibiwa.

    Martini akaitwa na kuingia kwenye kikao huku akikuta nyuso za wale viongozi zikiwa za tabasam

    "Sikia kijana! Waondoe vijana wako wote kwenye hilo zoezi na wewe utaambatana na sisi wakati wa kwenda huko! Kuna makomandoo wa Jeshi ambao tumewaandaa watachukua hii Operesheni! Cha msingi tupe sura walizovaa hao watu ili tuwape vijana wetu"akasema waziri wa ulinzi.

    Martin akashtuka na kuhisi dalili mbaya!!!





    Kabla ya safari Shamim aliwasiliana na Hussein na kumuomba waongozane katika safari hiyo kwa sababu ya kuweka uwezekano wa tatizo kutokea basi ingebidi Hussein aingilie kati na kusaidia.

    "Hussein hakuna anayekufahamu hapa Tanzania kwa sababu hiyo nachukua tahadhali mapema! Tusijekujikuta tunapata matatizo na kukamatwa wote na akakosa wa kumsaidia mwenzake! Hivyo wakati tunatoka naomba ubaki nyuma na mwanangu Alex jr"akasema Shamim.

    "Ok bosi nimekwelewa!"akasema Hussein.

    "Mumy! Kuna tatizo?"akauliza mtoto Alex.

    "Nothing my son! Kila kitu kiko sawa kabisa"akajibu Shamim

    Mtoto alivyoongea hivyo kuna kitu kilitokea ghafla kwenye moyo wa Shamim na akahisi kuumia sana moyo.

    Ilibidi ainame chini na kutulia kwa muda akijiuliza kilichotokea ninini? Moja kwa moja akachukulia hiyo kama ishara ya huko mbele lazima kuna tatizo litatokea na mambo hayatakuwa mepesi.

    Ile hali ilidumu kwa dakika kama tano kisha ikaisha.

    Junior yeye hakuwa na wasiwasi wala hakutaka kujishughulisha na chochote juu ya wale.

    Muda huo yeye alikuwa kaweka earphone zake masikioni akisikiliza mziki wa Maria Carey.

    Wakati wao wanakuja na ndege huku Tanzania timu ya wanajeshi waliofuzu katika mafunzo yote ya kikomandoo walishawasili uwanja wa ndege na kuchukua nafasi zao wakisubiria mtu wao awasili.

    Wote walikuwa wamevaa nguo za kawaida sana lakini wakiwa wamejizatiti vya kutosha ili kupambana na Shamim.

    Mawaziri wale wawili,mkuu wa majeshi na kijana Martin wote pia walikuwa pale pale uwanjani sehemu ya kupokelea abiria wakisubiri muda utimie wafanye kazi.

    Shamim ndege waliyopanda ilipitia Cairo kisha ikasimama pia Nairobi.

    Shamim aliwashauri wenzie washukie pale na kutafuta namna ya kuingia Tanzania bila kupitia uwanja wa ndege ila Junior alikuwa king'ang'anizi akidai amechoka sana hivyo hakutaka usumbufu.

    Aliwalazimisha mpaka wakakubaliana naye na uzuri Junior na Shamim walikuwa wamebadilisha sura na kuwekewa sura za bandia hicho kilimpa kujiamini ila hakujua kuwa picha ya sura ya bandia ya Shamim ilishafikia idara zote za polisi.

    Walifika uwanja wa ndege kama muda uliopangwa ikiwa ni saa tisa zajioni.

    Waliposhuka walipita eneo la ukaguzi bila shida huku Shamim akitembeza macho yake kwa kasi kuangalia kama kuna wana usalama pale.

    Mpaka wanaingia eneo la mapokezi hakuona sura ya kuitilia wasiwasi ila alipotokeza tu sura yake eneo la mapokezi aliona sura kadhaa ambazo alihisi moja kwa moja kuwa ni askari kutokana na uzoefu wake kwa hawa viumbe.

    "Hussein rudi nyuma kabisa tuwe mbali kuna tatizo"aliongea kwa kutumia vyombo vyake vya mawasiliano na kumfikia Hussein aliyemchukua mtoto na kujifanya kuzunguka zunguka kwa nyuma zaidi.

    "Tunaomba usimame hivo ulivyo na uko chini ya ulinzi! Ukileta ubishi wowote ule umekwisha"aliambiwa na mmoja wa maafisa aliowaona pale.

    Wale mawaziri na mkuu wa jeshi wakiwa na Martini walinyenyuka na kusogea eneo lile.

    Walipofika walikuta Shamim akiwa anawaangalia wale maafisa wa jeshi akijiuliza cha kufanya pale.

    Junior alipaniki na kuhalibu picha nzima.

    "Nyie mna akili? Mnanifaham?"aliongea kwa kujiamini kwa sababu alijua ana sura badia.

    Kosa lingine likafatia kutoka kwa Junior na ambalo wale viongozi wakubwa walitaka litokee ili wapate cha kujitetea kuwa walikuwa wakipambana.

    Junior akasogea na kumshika Shamim ili waondoke.

    Bastora tano zilitoka kwenye viuno vya wale viongozi watano na kuwalekea akina Shamim.

    Kwa sababu alikuwa mwepesi akashtukia lile tendo na kumshika Junior akamgeuzia upande wa pili ili wakwepe zile risasi.

    Viongozi wale hawakufanya makosa wakaachia risasi kadhaa kuelekea walipokuwa akina Junior.

    Ingawa Shamim alijalibu kukwepa ila wingi wa zile risasi na eneo kuwa dogo vikamponza na risasi kadhaa zikapenya kwenye mwili wake.

    Viongozi wale hawakuacha kupiga risasi.

    Shamim aliendelea kunyeshewa mvua ya risasi sehemu mbali mbali za mwili wake wakati Junior alishaaga Dunia kitambo.

    Walipohakikisha hatikisiki wakaita waandishi waliowaanda na kuongea nao.

    "Mara nyingi sana jeshi la polisi limeshindwa kumdhibiti huyu gaidi wa kike ila leo tumeamua kuingilia kati na tumefanikiwa kummaliza"waliongea kifupi na kuahidi wakutane ukumbi wa habari kwa maelezo zaidi.

    Wakati tendo lile linatokea Alex jr aliona na kushtuka ila Huusein akamziba mdomo na kugeukia kwingine.

    Alex jr aliwaona wale viongozi watano wakati wakimalizia kumuua mama yake pale chini na kuwakalili.

    Kesho yake vyombo vya habari vyote vikatawala swala la kuuawa kwa Shamim huku wale viongozi watano wakijichukulia sifa kubwa na wengine kupandiswha vyeo.

    Shamim alizikwa na serikali kwa siri bila mtu yeyote kufahamu alikozikwa na wala kuhudhulia mazishi.

    Hussein aliondoka na yule mtoto Alex jr kurudi Marekani na kuishi naye.

    Habari ya Shamim serikali ikajua imeizikia hapo!! Haikujua!! Haikujua!! Haikujua Shamim alikuwa na mtoto na kawaida mtoto wa nyoka ni nyoka!!

    ******** END **********

0 comments:

Post a Comment

Blog