Search This Blog

Monday 16 May 2022

SECONDARY SCHOOL - 1

 











    IMEANDIKWA NA : MOONBOY



    *********************************************************************************



    Chombezo : Secondary School

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    Inapoanzia Rasmiiii

    STORY HII INAITWA SECONDARY SCHOOL AU KWA KISWAHILI NI

    ( SHULE YA UPILI ).....

    KWAHIO PIA WAWEZA KUIITA HIVYO TU BASI

    Story hiii mimi ni mtoto wa kitajiri ile mbaya... na wakiume nipo mimi mwenyewe na nina dada zangu wawili wenye asili ya kiarabu. kwani mama yangu yeye pia ana asili ya kiarabu.....

    Ninae dada yangu ambae ana umri wa miaka 25 huyo ni wa kwanza na keshamaliza shule muda tu... kisha ninae dada yangu mwingine ambae tumefuatana.. yeye ana umri wa miaka 22 na yeye bado yupo kidato cha 4... afu anafatiwa na mimi kidume sharbiny rashidy mwenye umri wa miaka 20 na yupo kidato cha 3.... familia yetu ilikua ni familia ya kitajiri sana yaani tulikua ni matajiri waliopindukia....

    Ila katika watoto wote wa mzee rashidy mimi peke yangu ndio nilikua nina rangi tofauti na dada zangu wote. Ila nyumba yetu imezungukwa na wafanyakazi wengi mno. kama kwa raisi vile kumbe ni kwa mtu tu wa kawaida...

    "mwanangu utaenda kesho tu"

    "mamaa mi sijawahi kukosa kwenda shule hivyo nisipoenda naisi kama nitaumwa yani"

    "mmhh haya ila njoo unywe chai basi"

    "nitakula huko huko mamaa"

    "mwajabu? we mwajabu?"

    "abee dada?"

    "umeona mtoto wangu anaenda shule na njaa?"

    ndani kwetu tulikua tuna mfanyakazi ambae ni mtu mzima kabisa na ndio alionilea mimi toka nikiwa mtoto.... hivyo roho inaniuma sana pindi ninapoona anafokewa kwa ajili yangu,

    "kakaa njoo unywe chai"

    Aliniita yule mdada wa makamo kabisa tena hata sio mdada ni mmama kabisa. kwani alitulea mimi na dada zangu wote, lakini dada zangu asa huyu mdogo hua hamueshimu huyu mama na sijui ni kwanini....

    "mamii nimeshiba usijali"

    Nilimuambia kwa kwa utaratibu na heshma zote alizonilea yeye mwenyewe.

    "sheby mwanangu?"

    "sema ukirudi unataka ule chakula gani?"

    Alioniuliza ni mama yangu mzazi

    "aaaa chochote tu mamaa"

    "yaani we mwajabu humuulizi mtoto atakula nini umeuchubua tu"

    "mamaa mbona ivyo lakini?"

    "amna mwanangu ni huyu mtu naona hakujali kabisa yani"

    "ok nitakula ugali na mrenda"

    "haaaaaaa sheby mwanga chakula gani hicho cha kishenzi hivyo?"

    "mamaa kwani hicho mbona pia ni chakula"

    Mara mami kazi akaingilia kati

    "lakini dada kama kapenda mwenyewe kula labda tumuache tu"

    "hapana mwanangu hawezi kula matapu tapu hayo... afu wewe mwajabu umenilelea mtoto wangu vibaya sana wewe"

    "nisamee dada"

    Nilichukua BMX yagu ambayo hua naendaga nayo shule pindi ninapopitwa na school bus, Hua shule ninayosoma ni shule ya serikali iitwayoCHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ASHRAF SEMINARY SCHOOL ni shule ya kiislamu ambayo ina maadili mema kila idara....

    Shuleni mimi ni mtu ambae sina kosa hata moja kutokana na heshma na upole nilionao... mimi nasoma katika shule hio ya kiislamu ambayo ambayo ina maadili mema kede kede....

    Na dada yangu ZAITUNI yeye anasoma katika shule nyingine tofauti na hiii.... hio anayosoma dada yangu zaituni ni shule ya private na ya kitajiri tuuu yaani kama una utajiri wa mawazo huezi kusoma katika shule hio iitwayo ST PETER SUNEKA SECONDARY

    **********************************

    HIII SHULE NILISOMEA KENYA KIUKWELI UKWELI ILA KWENYE HII STORY NITAIFANYA KAMA IPO ARUSHA VILE...... SASA MSIJE MKANIKOSOA NA KUNIAMBIA oohh mbona hio shule ipo kenya...SASA MJUE KUA HIO SHULE NILIISOMEA KWELI KWELI NAIROBI KENYA ILA KWA HII STORI NITAIFANYA KAMA IPO ARUSHA VILE.... YAANI KISTORY STORY IWE ARUSHA LAKINI KIUKWELI IPO KENYA SEHEMU IITWAYO ~KISII~ NA NILISOMEA HIO SHULE KIUKWELI ILA SIO YA UTAJIRI KIHIVYO

    **********************************

    Sasa dada yangu ndio anasomea shule hio ya kitajiri ambayo wanafuzi wao huenda na simu na magari kabisaaa.... tena hio shule kila mwanafunzi ana gari. Ila mimi nimelelewa kimaadili sana na mama mwajabu.... kiasi kwamba hua mimi sinaga makuu kama dada yangu zaituni.... kwani dada yangu nae ana gari la kuendea shule ila mimi nimekataaa kutembelea gari.. na pia hata simu pia sina maana naona haina faida kwangu

    Basi nilifika shjleni kwetu kisha moja kwa moja nikaripoti ofisini ili nijulikane kua nimechelewa shule

    JE? WEWE ULISHAWAHI KUCHELEWA SHULE NA UKAENDA KUJISHTAKI OFISINI???? HEEEEE KAMA HUJARUKA UKUTA NA KUINGIA CLASS,

    "asalam aleykhum?"

    "waalekh msalam vp sheby mbona leo umechelewa shule?"

    "nisamee mwalimu"

    "najua kua sio kosa lako na hunaga tabia hii ya kuchelewa hivyo nenda tu darasani"

    Shuleni kwetu sisi hua tunavaa sale au uniform za kiislam ( panjabi ) na kwa wanawake wanavaa sale za ( hijabu na ushungi juu ) Kiukweli niliingia darasani. afu shuleni kwetu mimi sijawahigi kua mtu wa 3 toka nianze shule. yaani ni nashikaga nafasi ya pili au ya kwanza. Hua walimu wananipena sana hapo shuleni maana mimi hua sina makuu juu ya utajiri wetu. na nina heshma na upole wa hali ya juu kuliko mtu yeyote yule.....

    Basi kama kawaida yangu hua mwalimu akichelewa kuingia darasani hua mimi napitaga ubaoni pale na kuanza kukumbushiana tulioyasoma jana.... shuleni kwetu kuna wanafunzi wa kike ambao hawajafunzwa wakafunzika hivyo hua saa zingine wananisumbua sana kua na mahusiano nao...... ila kwakua mimi mwenyewe nimelelewa kimaadili zaidi hivyo watu kama hao kwangu ni bure tu.

    Ilifika mida ya saa 10 hivi jioni ambao ni muda wa kukwea school bus.. lakini leo sitopanda bus kwani nilikua na kibaskeli changu nilichokuja nacho...

    Sasa nikiwa nipo njiani kuelekea nyumbani mara nikaskia honi kwa nyuma... nikasogea pembeni ili apite sasa nasikia bado tu anapiga honi.. ikabidi nigeuke nimuangalie ni nani anaepiga makele huyo?.....

    Aaaagggyyyyy aseee kumbe alikua ni dada yangu zaituni. Aisee ana masifa hayo, Eti kanipitia tuende wote nyumbani yaani katoka koote huko hadi huku kisa tu aje anichukue....

    "we sheby twende basi"

    Aliniambia hivyo huku akifungua kioo. Sasa alipofungua kioo niliona kajaza marafiki zake wengi hao duuuu. afu ni wazuri ile mbaya Na hao pia wana magari yao ila hua wanapenda kupanga siku watembelee gari ya nani kati yao...

    Sasa wale wanafunzi wenzake wakaanza kumuuliza zaituni

    "mmmh zai yule ndio nani tena?? au ndio shemu wetu?"

    Dada angu aliwageukia kwa hasira

    "nyie tueshimianeni bwana"

    "mmhh sasa tusikuulize je? tukipita nae je? utatulaumu?"

    "bwana nyie yule ni mdogo wangu"

    "mmhh zai muongo sema kweli ni mdogo wako?"

    "ndio"

    "khaaa una mkaka hensamu hadi raha"

    "jesca? tafadhali sana punguza mdomo wako"

    "mmhh sasa tusimsifie kaka yako?"

    "aaahh twendeni bhana kwanza mwenyewe hataki"

    "ah ah bwana zai kua mpole... hebu toa loku basi hata nikampe mkono wangu"



    Kiukweli ndani ya gari kulikua na watoto wazuri mno. yaani mfano kama ningelikua ndio wale wazee wa michepuko sijui ingekuaje, Ila mi nakaza tu kiume kutokana na malezi niliopewa na yule mama..

    "jesca? tafadhali sana punguza mdomo wako"

    "mmhh sasa tusimsifie kaka yako?"

    "aaahh twendeni bhana kwanza mwenyewe hataki"

    "ah ah bwana zai kua mpole... hebu toa loku basi hata nikampe mkono wangu"

    Niliposkia tu hivyo nilipanda baiskeli yangu na kusepa.. maana niliona kama atanitengua uzu wangu, Niliwahi zangu nyumbani kama jinsi alivyo mtoto mwema... kumbuka neno hili kua MCHEZA KWAO HUTUNZWA hivyo nami sikua mtu wa kuruka ruka hovyo...

    Nilifika nyumbani huku nikiwa zangu na swaga za kawaida tu. niliingia ndani na kuweka begi la shule pamoja na kubadili nguo, Baada ya hapo nilikaa mezani na kupata chochote cha kuweka tumboni.... ila mimi peke yangu ndio ninaependwa na wafanyakazi wote mpaka wa kiume.. ni kwasababu hua sinaga maringo na dharau kwa wafanyakazi wetu

    Wakati huo mama angu alikua hayupo kaenda dukani kwake na baba nae kasafiri toka juzi, hivyo nilikua nipo na wafanya kazi tu. kwani dada yangu mkubwa aitwae NUSURA kwa sasa yupo kwenye saluni yake... yaani baada ya kumaliza form 4, alipenda awe msusi Yaani awe na saluni yake binafsi... Na licha ya saluni kuwa nayo pia keshapewa haki yake ya maisha.... Yaani namaanisha kua sisi kama watoto wa familia za kitajiri hua mtoto akitaka kuanza maisha yake binafsi basi anapewa moja ya mali pamoja na kufunguliwa biashara anayoitaka, Hivyo dada yangu nusura alipomaliza tu kidato cha nne, alikaa kama mwaka hivi kisha akaongea na wazazi kua anataka kuanzisha maisha yake binafsi hivyo... alikatiwa upande wa mali yake akapewa... kisha akajenga nyumba yake na kufungua saluni kubwa kabisa jijini arusha.... yaani katika saluni zote jijini humo, hio ndio saluni maarufu kuliko zoteeeeeee

    Lakini pamoja na kujenga nyumba ila bado hajatuhama, yani bado tupo nae nyumbani. kwani kasema hajisikii vizuri kutuacha kwakua ametuzoea. hivyo hakuhama kwa maana ya kutuzoea yani atatumisi sana. kwahio hajahama....

    Na mimi saa mingine naendaga saluni kwake, ila sipapendi kwasababu kuna wamama wenye akili za kitoto hua wananisumbua sana kama nikienda huko, Ila namkubali sana dada yangu nusura kwani huaga hanaga shida na mtu Tena tunaheshimiana vizuri mno na kufurahi, Ila hili lidada lingine hili li zaituni hili, nalichukia kwakua linapenda kunikuadia kwa wenzake tu,

    Basi nilimaliza kunywa chai kisha nikatoka nje ya nyumba ( ndani ya geti ) nikaanza kuzunguka zunguka na kuwasalimia walinzi na magadena boy... ( watunzaji wa bustani )

    Nyumba yetu ni kubwa sana na ina rosheni moja ( gholofa moja ) na ni ya kisasa ile mbaya... basi niliendelea kuwasalimia kama kawaida yangu, heshima kwa kila mtu aliopo ndani ya nyumba yetu...

    Humu ndani ya mjengo wetu kuna watunza bustani wawili wa kiume.. na mfanya usafi wa nje wa kike mmoja... na walinzi wawili ambao hua wanapeana shift za kulinda mlango na kufungua kama kawaida... hivyo hapa yupo mmoja wa mchana hivyo atakuja mwingine ali alinde usiku,

    Wafanyazi wetu ndio hao kwa nje tu ni walinzi wawili na magadena wawili na mfagiaji wa kike mmoja... jumla wapo wafanyakazi watano...CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Afu huku kwa ndani kabisa kuna ma house girl watano, pamoja na yule mama wa muda mrefu.... Yule mama ambae ndio mfanyakazi wa kwanza katka nyumba yetu, na ndio aliotulea sisi wote Japo alimkuta dada nusura akiwa na umri wa miaka 5 hivi... kwahio sisi wawili mimi na zaituni tumelelewa na huyu mama mfanya kazi wa kwanza kuishi ndani kwetu.....

    kwahio huyu mama kwa sasa hafanyi kazi kutokana na muda mrefu alioanzia kazi, hivyo huyu mama kazi yake ni kuwaelekeza hawa ma house girl wadogo jinsi ya kufanya kazi humu ndani na kutunza watoto wa mabosi ambao ni sisi watoto watatu... kwahio ukiona huyu mama anafokewa na mama yangu. basi ujue kua anafokewa kwa kosa la ma hausi geli wadogo.. kwani hakutimiza wajibu wake wa kuwaambia kua familia itakula saa ngapi au nyumba inafanyajwe usafi, ni vitu kama hivyo kwa sisi tunaweza kumuita spervisor ( msimamizi ) hivyo wadogo wakikosea basi ni lazima afokewe huyu mama kwa kujisahau kuwaelekeza wafanyakazi wadogo...

    Ma hausi geli wetu hua hakuna wa darasa la saba hata mmoja. hua ni form 4 tu... na huyo form 4 wenyewe awe hata na DVN 3 au 4 ya 5 kushuka. na awe anaweza kusoma na kuandika kingereza....

    Na wafanyakazi wote wanalipwa laki moja na nusu ( 150, 000 ) mpaka wale wa nje .... ila yule mama yeye analipwa laki tatu ( 300, 000 ) hii ni kutokana na heshma yake ya utu uzima na kuishi na familia hii kwa muda mrefu kama ndugu... na ndio maana mpaka leo bado yupo ndani ya familia hiii.....

    Mama huyu kwa jina lake kamili wanamuita MWAJABU na alianza kazi humu ndani kabla mimi sijazaliwa bado... kwani alikuja hapa akiwa na umri wa miaka 17 na ilikua ni mwaka 1992 ambapo ndio mwaka aliozaliwa dada yangu zaituni.. kwani dada nusura yeye alizaliwa mwaka 1990 na mimi nilizaliwa mwaka 1994 hua tumepishana miaka miwili miwili ila dada nusura kanipita miaka minne au mitano hivi. na zaituni kanipita miaka miwili tu....

    NDUGU MSOMAJI KUA MAKINI NA HUO UTAMBULISHO HAPO JUU... ISIJE BAADAE UKAJIULIZA AU UKANIULIZA KUA MIMI NA ZAITUNI NANI MKUBWA? AU MIMI NA NUSURA NANI MKUBWA???? SITAKI MASWALI YENU NA WAKATI KILA KITU KINAJIELEZA HAPO....... NIMEAMUA KUTANGULIZA INFOMESHENI KWANZA ILI MJUE KUA STORY INAKWENDAJE.... MKUBWA NI NANI NA MDOGO NI NANI. HIVYO KAA UKIJUA KUA MIMI NDIO MTOTO WA MWISHO KWA MZEE RASHIDI NA MAMA YANGU AITWAE LEILA MWENYE ASILI YA KIARABU KABISAAAAAA

    Kwahio mimi na zaituni ni watoto tuliofatana. akitoka yeye ndio natoka mimi. hivyo mimi ndio nilimpokonya ziwa kwa mama yangu.....

    SASA TUENDELEENI NA FULL STORY

    Wafanya kaxi wetu walikua wakishangaa kuona mimi napenda kuwasalimia na kufurahi nao.

    KWA KAWAIDA YA WATOTO WA KITAJIRI HUA WANA ASILI YA KUJISIKIA SANA. YAANI HAWEZI KUMUESHIMU MFANYA KAZI WAO HATA SIKU MOJA, NA PIA ANAKUA NA MARINGO SANA NA ANAPENDA KUNYENYEKEWA SANA, ILA MIMI NILIKUA NIPO TOFAUTI SANA NA WATOTO WENGINE WA KITAJIRI

    Sasa nilipocheki saa yangu niligundua ni muda wa kwenda msikitini kusali magharibi ( swala ya daa 12 jioni ) Nilichukua uzu wangu vizuriii kisha nikavaa kanzu yangu kisha na kibarakashee ( kofia ya kiislam ) Nilichukua BMX yangu na kuelekea msikitini, Bila shaka wala nini.

    Sasa nilipofika njiani nilikutana na marafiki zangu ambao hua sisomi nao shule moja... wao wanasoma kule kwenye sule ya kitajiri ambayo ndio anayosoma dada yangu zaituni..

    "Aaahh sheby vp?"

    "safi tu mambo yanakwendaje?"

    "daahh tupo ila wewe ndio huonekaniki bhana"

    "aa mi nipo tu"

    "vo mbona siku hizi hatukuoni gym? ( sehemu ya mazoezi )?"

    "Aisee chalii yangu side? leo nimechelewa shule ile mbaya kwani leo sikupanda school bus leo"

    "aaahhh sisi kila siku tunakuambia njoo shuleni kwetu fulu bata, yaani tunaingia class na iphone afu mandinga yamejaa school tu... njoo tule bata wewe"

    "aaaa hayo mambo ya kula bata ndio siyataki kabisaa"

    "tatizo malezi uliolelewa ni ya analojia"

    "waaaapi bana sema ni hulka ya mtu tu"

    "ok kwaio waenda wapi sasa?"

    "naenda msikitini mara moja"

    "Eheee afu sharbiny ee?"

    "sema?"

    "unamkumbuka aisha?"

    "aisha??? aisha yupi uyo?"

    "si yule demu flani ninaesoma nae class moja? anaishi pale kwenye geti la kijani pale mbele"

    "Aaaaaa yule mweupe mweupe sio?"

    "Eheee huyo huyo"

    "vp kwani kafanyaje?"

    "mtoto anakuulizia kishenzi yani"

    "ananiulizia? ananiulizia nini sasa?"

    "anaonekana keshakufa kakaaa"

    "heeeeee kafa lini tena? na jana nilimuona pale dukani? aaastakafiru laah"

    "Aaaaahhh sasa dua za nini tena sheby?"

    "si tunamuombea kwa mungu?"

    "ah ah hajafa kama kufa bhanaa"

    "mmhhh kafaje kafaje sasa?"

    "yaani nimemaanisha mtoto keshakupenda yuleeeee"

    "aaaahh hayo mambo ndio nisio yataka bwana... ebu niache niwahi swala kwanza then tumiti baadae kwa story zingine ila sio hizo"

    "mi ndio maana nakuita analojia wewe... ila poa mida basi"

    "poa poa"

    Basi nikaendelea na safari ya kwenda msikitini, Kuswali swala ya saa 12 jioni pamoja na ya saa mbili usiku

    Sasa nikiwa naendelea kwenda mara niliskia nikiitwa na sauti ya kike kabisa... ikabidi nigeuke nimuangalie huyo anaeniita....

    Aaaahhhhh shit kalikua ni hako ka Aisha tulichokua tukikaongelea muda sio mrefu....

    "mambo sheby?"

    Alinisalimia huku akinipa mkono. na mimi nilikua nina uzu.

    "samahani dada nina uzu hivyo sitoupokea mkono wako"

    "itikia tu basi hata kwa mdomo tu"

    "ok poa"

    "unaenda wapi kwani?"

    "naenda kuswali"

    "na mimi pia naenda"

    "heeeeeeee toka lini ukaenda msikitini wewe?"

    "si ndio naanza leo"

    "eeee mungu wangu weee"

    "afu utanipakiza kwenye baskeli yako"

    "heeeeeeee sasa utapanda wapi hapa na unaona hakuna kiti cha nyuma?"

    "mi staki bwana nitakaa hata hapo mbele tu"

    "jamani aisha mwenzio nina udhu wa kuswalia bwana"

    "jamani sheby kwani ntakugusa???"

    "hapana bwana we kama una nia ya kumuomba mungu utakuja ila kama huna basi"

    "ila sheby?? ngoja basi nikuambie mwenzioo"

    "uniambie nini?"

    "kwani sheby.......



    Nilikua namsikiliza huku nikiwa nimekaa mbali kweli

    "ila sheby?? ngoja basi nikuambie mwenzioo"

    "uniambie nini?"

    "kwani sheby utarudi saa ngapi?"

    "mmmhhh nitarudi kama muda wa saa 3 hivi kwani lazima nipitie msaafu kidogo"

    "msaafu?? msaafu ndio nini?"

    "umeona sasa ee? kumbe hata vitabu vya mungu tu huvijui"

    "mmhh poa basi nitakusubiria muda huo au vp?"

    "sawa pia"

    Basi Nikaendelea zangu na safari ya kwenda masjidi kumuomba mungu wangu.... Niliingia zangu msikitini na kua kulipia swala zangu ambazo zilinipita toka mchana....

    Ilinichukua kama dakika 15 hivi hadi kumaliza. hivyo nikatafuta mahali nikae kwa kusoma vitabu vya mungu, kwa kuisubiria swala ya isha, Kwani saa hio ilikua ni mida ya saa 1:35 jioni, Baada ya muda huo kuisha niliswali swala ya isha mida ya saa mbili... baada ya kumaliza kuswali tulianza kusoma dua mbili tatu za kumuomba mungu kwa kila jambo. Nilikua ni mtoto wa kitajiri wa kwanza kwenda msikitini kumuomba mungu.... maana asilimia nyingi ya watoto wa kitajiri hua hawanaga muda wa kwenda katika nyumba za ibada. kwani wanaona tabu kuinama inama au kufumba macho na kupiga makofi kule kanisani. Ila mimi niliushangaza mtaa pamoja hata na msikiti kwa kuwa mtoto wa kitajiri ninaependa kumuomba mungu.. Hata mashehe walikua wakinipenda sana kutokana na heshma na malezi mazuri ambayo nililelewa na MWAJU

    Basi tulimaliza kupiga dua pale msikitini tena mimi ndio nilikua naisoma hio du. Nilikua napenda sana kua ostadhi mzuri na mpaka nifikie kuwa shekhe.

    Kama kawaida yetu waislamu tukitoka lazima tupeane mikono ili kuombeana kheri na kuagana kwa amani... zoezi hilo lilipoisha nilitoka zangu na kuchukua BMX yangu ( baiskeli ndogo za kisharo ) Niliondoka zangu na kuelekea nyumbani huku nikiimba zangu nyimbo za kaswida..... sasa nilipofika chocho moja hivi nilikutana na wahuni ambao ni vibaka wa mtaani. Duuuuuu nikajua leo naoshewa hapa heeeee..... ila uzuri na mimi pia sio haba katika swala la kujitetea....

    "oyaaa vunga kwanza basiii"

    Mmija wao alinisimamisha kwa ubabe kisha wakaja wote afu mmoja akawasha tochi na kunimulika usoni. huku wakiandaa visu na marungu

    "aaaaa kumbe ni huyu chaliii? Asee tumteme ariif uyu si chalii yetu wa kitaa pale mjengoni"

    "yupi uyo?"

    "si sheby uyu asee"

    "aaaaa Ah sheby? sole bhana chalii yetu hatujakujua bhana... tulijua ni ngararu flani kumbe wewe?"

    "afu hainaga kwere kama utatuchomesha mafegi arifu ama nini chalii yangu?"

    Nilijisachi fresh nikawatoa na buku 5. kisha wakaniachia nisepe zangu.

    Hawa wahuni hata sikua nawajua kabisa ila wao wanasema wananijua kabisa ila mimi simfahamu hata ntu mmoja kati yao, Basi niliondoka zangu huku nikiwa naendelea kuimba nyimbo zangu za kaswida.

    Sasa nilipofika mahali nilikumbuka kua aisha atakua ananisubiri, hivyo nilibadili njia nyingine ili nisikutane nae. maana hana jipya la kuongea

    Nilifika nyumbani salama kisha nikaweka bmx yangu vizuri kabisa maana ndio usafiri wangu wa shule kama school bus litaniacha, Nilimkuta mama angu akiwa anacheki tv pamoja na mwaju

    ukiona hili neno MWAJU basi ujue ni huyu mama alienilea mimi na zaituni yaani mfanyakazi wetu wa kwanza. Kwani anaitwa MWAJABU hivyo namkatishia na kumuita MWAJU.... ila mimi hua namuitaga ANTI kwani sihitaji kumuita jina lake hivyo ukisikia neno MWAJU basi ujue ni yeye... na ukisikia neno ANTI pia ni yeye huyo mwajabu ambae ni mfanyakazi wetu wa kwanza na ana umri mkubwa tu. kwani ametulea sisi watoto wote wa humu ndani.

    Niliingia ndani na wafanya kazi kama kawaida yao ya kuongea sana si unajua tena utajiri nao safi afu saa zingine ni kero.

    "mambo?"

    "poa. ila siku zingine nisalimie salamu ya kiislamu sawa dadaa ee?"

    "sawa"

    Nilinyooka zangu mpaka juu, kwani gheto yangu ipo rosheni ya juu. Nilienda mpaka huko kisha nikaenda kuoga zangu.... si unajua vyumba vya kitajiri ni kila kitu humo humo.. bafu huko huko choo huko huko yaani kila taka taka huko ipo... TV ninayo tena ni ya ukutani yenye ukubwa wa inchi 40 kitu cha flati..CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Swaga za mavazi ninayovaa ni swaga hizi hizi za kisasa. ila sivai mlegezo Nilitoka zangu kuoga kisha nikapaka mifuta yangu Afu nikashuka ili nikajumuike na wenzangu kule sebuleni. Nilipofika nilimkuta dada nusura anaangalia kipindi flani hivi cha BBA ( Big Brother Africa ) hua anakipenda sana

    "shkamoo dada"

    "marahaba mambo vp?"

    "poa tu"

    Dada yangu nusura hua sio mkubwa kiviile kwani ana umri wa miaka 24 na mimi nina 20 hivyo nilimuamkia kwakua ni dada yangu na kanipita kiumri. Hivyo hata yeye hua hapendagi nimuamkie. kifupi hapendi kusalimiwa. ila mimi ananiacha tu nimsalimie kwakua tunaheshimiana sana. Mara mama alikuja

    "sheby ulienda wapi?"

    "nilienda msikitini mam"

    "ok na zaituni yuko wapi?"

    "mmhh atakua yupo chumbani kwake labda"

    "hebu kamuite"

    Zaituni yeye pia yupo chumba cha juu, Yaani gholofani huko nilipo mimi na pia dada nusura pia yupo rosheni ya juuu.. kifupi ni familia yote tupo gholofani, na huku chini ni vyumba vya wafanyakazi wote kasoro mlinzi ndio hua haingiagi ndani kulala. kwani yeye ana kigeto chake pale pembeni ya geti...

    Basi niliingia ndani kwa dada yangu huku nikiwa na furaha yangu binafsi.

    "we?"

    "we ndio nani?"

    "unaitwa bwana maswali mengi ya nini?"

    Nilikua naongea na zaituni. kwani hua haziivi kabisa mi na yeye kwani leo tupo sawa kesho tumekwaruzana. si unajya watoto wa kitajiri wanavyokua na masifa...

    "unaitwa na mamaa"

    "sasa si ninakuja"

    "mama anakuita kwa haraka zai"

    "mmhhh nipishe uko"

    Alitoka na kuelekea huko chini kwa mama,

    Nami nikawa nafata nyuma kwa kurudi sebuleni

    "tayari ushamsikiliza?"

    "ndio"

    "sasa mbona umenuna?"

    "nani kanuna?"

    "mmhh haya"

    "afu sheby njoo huku chumbani nikuambie"

    "uniambie nini?"

    "we si uje tu"

    Niliingia chumbani kwake na kukaa kitandani. kwani kawaida ya watoto wa kitajiri huwa hawanaga masharti ya kuingilia katika vyumba vya webzie. tofauti na watoto wa kimasikini Kwani hua watoto wa kitajiri wanapokua wadogo walikua wakilala pamoja na ni jinsia tofaut kabisa ila wanalala kitanda kimoja... ila tusiende mbali sana kwani hata sisi wenyewe ndio jinsi ilivyo yaani mfano dada yangu zaituni anaweza akaja chumbani kwangu na kuanza kuangalia tv mpaka akasinzia kwenye kochi. kisha mimi nambeba na kumlaza hapo hapo kitandani kwangu. na sio kua ni kipindi hicho lahasha bali hata sasa hivi pia na ukubwa wake likija chumbani kwangu linasinzia na kulala kabisa.. na hata wazazi wakituona hawana la kusema kwani si ndugu?? na pia wazazi mfano mama anaweza akaja chumbani kwangu na akamkuta zai kalala chumbani kwangu. lakini kikubwa atakachoongea ni hivi

    "mfunike dada yako brangeti"

    Hivyo hata sasa hivi nikiingia katika chumba cha dada yangu hakuna mtu atakaesema lolote. tofauti na masikini

    Maana najua familia ya kimasikini mtoto wa kiume akishafikisha umri wa miaka 15 haruhusiwi kuingia chumbani kwa mama yake au dada yake. na hio siku akiingia heeeeeeee atakula kibano kutoka kwa dingi duuu...

    Na humu ndani aliokua akiizuia hii tabia ni Anti mwaju yeye hakua akiipenda hii tabia ya kulala wote chumba kimoja pindi mmoja wetu anaposinzia chumbani kwa mwenzake.... kwani hata mimi siku moja nilienda chumbani kwa zaituni ili anielekeze baadhi ya maswali niliopewa shuleni, kwani yeye yupo kidato cha 4 na mimi nipo kidato cha 3 hivyo nilienda chumbani kwake ili anikokotolee swali moja hivi la math ( hesabu ) sasa katika hali ya kuelekezana mimi nilijikuta nimesinzia na kulala hapo hapo chumbani kwake... na nilipozinduka usiku nilijikuta nimefunikwa vizuri tu tena nimelazwa vizuri sana, kuliko nilivyolala mwanzo... na nikiangalia pembeni naona zaituni anakoroma tu. Nilipomuuliza kesho yake kua nani alinilaza vizuri na kunifunika shuka? akanijibu kua ni yeye... hivyo tukawa tumeshazoana kila mmoja kulala kwa mwenzie. na hii tabia ipo mpaka leo na familia yetu pia imezoea kwani licha ya kulala kwa zaituni pia nilishawahi kulala kwa dada nusura. tena na ukubwa huu huu na ilikua hivyo hivyo kulazana vizuri na kufunikana mashuka... ila dada nusura hajawahi kuja kulala kwangu.. kwani yeye ndio dada yetu mkubwa hivyo mimi na zaituni ni watoto tunaefatana hivyo mazoea bado yapo kati yetu....... siku moja zaituni alilala chumbani kwangu na anti mwaju alikemea lile jambo lakini mama angu alikuja juu na kumuambia kua

    "waache watoto wangu bwana kwani wakilala pamoja ni ishara ya upondo kwao kua wanakumbukia utoto. waache watoto walale"

    Afu baada ya kusema hivyo mimi nilikua zangu naangalia kipindi cha kiislamu kwenye tv hivyo mama akaniambia kua

    "sheby?"

    "naam mama?"

    "usimsumbue dada yako mwache alale tu"

    Hivyo mpaka leo hii mmoja wetu akilala kwa mwenzie hali ni hio hio ya kufunikana na kulazana vizuri....

    HIO ?? ILIKUA NI HISTORIA FUPI YA MAISHA TULIOLELEWA NA WAZAZI WETU.... SASA TUENDELEE NA PALE ALIPONIITA CHUMBANI KWAKE

    "fanya fasta mi nataka nikaangalie kaswida"

    "mmhhh we nawe unapenda hizo nyimbo zako mbayaaaa"

    "afu zai kejeli hua spendi"

    "ok yaishe Sasa kuna kitu nataka nikuambie"

    "kitu gani hicho?"

    "ah ah we kubali kwanza"

    "kwani ni kizuri?"

    "ndio.. tena ni kizuri saanaaa"

    "haya nimekubali"

    "sogea sasa nikunong'oneze"

    "mbona una masharti hivyo?"

    "bwanaaaa sheby we si uje tu"

    "haya niambie"

    Nikamtegea sikio ili aseme hicho kitu anachotaka kusema

    "mwenzio mimi nime.........



    Nilikua natega sikio kwa makini sana ili kumsikiliza hicho alichotaka kukiongea. huku akiwa anatabasam zitoooo

    "sogea sasa nikunong'oneze"

    "mbona una masharti hivyo?"

    "bwanaaaa sheby we si uje tu"

    "haya niambie"

    Nikamtegea sikio ili aseme hicho kitu anachotaka kusema

    "mwenzio mimi nimetumwa na jack"

    "ushaanza ujinga wako sio?"

    "heeee? kwani umeshajua hicho alichonituma?"

    "haya kakutuma nini?"

    "anaomba kitabu chako"

    "heeeee? sasa mimi form 3 na yeye form 4 wapi na wapi?"

    "amesema anataka kujikumbushia"

    "mmhh poa nikumbushe asubuhi"

    Nilitoka zangu kwa hasira maana nilijua kuna cha maana anachotaka kuniambia kumbe ni kuombana vitabu, Mimi na zaituni kiumbo tumelingana ila kiumri kanipita miaka miwili, hivyo tukiwa pamoja unaweza sema ni mapacha wasiofanana. maana tumelingana kiumbo ila yeye ndio mkubwa kiumri, Nilishuka zangu hadi siting rum. nikawa nimekaa na dada yangu nusura, tena nilikua nimemlalia mapajani kwake Yaa kichwa changu kime egemea mapaja yake, hio ni ishara ya upendo kwa ndugu. Tulikua tukipiga stori za hapa na pale

    "ivi dada? unaonekana unapenda sana BBA ( Big Brother Africa )"

    "ndio tena hii ninayoangalia ni CD tu ila ya mwaka huu lazima niende nikaiwakilishe tz"

    "aaaaaaaa mi staki uende buana"

    "kwanini nisiende?"

    "mmhhh kule wanakaa ovyo sana"

    "kivipi?"

    "si wakaa bila nguo"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "wai mi siogopi hilo kikubwa nishinde ti"

    "haaaaaa kwahio upo tayari mi mdogo wako nikuone?"

    "kwani we ni kipi usichokijua?"

    "sawaaa navijua vingi ila sio cha dada yangu"

    "hehehehehe kumbe unanieshim dada yako eeehh? basi siendi"

    "itakua vizuri usipoenda"

    Basi nikiwa bado nagala gala katika mapaja ya dada yangu. mara beki tatu ( hausi geli ) kaja pale

    "dada chakula tayari"

    "sawa tunakuja"

    Kwa kawaida nyumba za kitajiri hua zinakua na sebule mbili.. yaani daining room ni sehemu spesho kwa kulia msosi tu. na varandani ni sehemu ya kuangalia tv na kunywa kunywa juice huku stori kwa wingi... Sasa hapo tuliitwa twende tukale msosi,

    Nilifika mezani ambako hua sisi watoto wa maboss tunapakuliwa na wafanyakazi. Ila mimi hio tabia sinaga kwani nikifika tu mezani nachukua msaani wangu na mkijiko kisha najipa msosi mwenyewe, Tuliokaa kwenye meza tulikua ni sisi wana familia tu pamoja na anti mwaju. Tulikula pale na madada zangu wakawa wanang'ang'ania kunilisha Eti kisa ni mdogo wao Yani wamemisi kunilisha toka nikiwa mdogo, Nami si unajua nimeshakua ila swaga za kitoto kitoto bado ninazo zile za kitajiri..... kwa maskini saa hizi ningeshaenda kubeba zege uko kwenye masaiti. na utoto ungekua hamna tena... Mara dada nusura akaanza kuongea

    "ila mdogo wangu na wewe nunua simu"

    Mara zai nae kadakia juu kwa juu

    "Eeee mwaya hebu muambie maana nikimuambia mimi anajifanya hasikii"

    Nikaona ngoja niwajibu moja la titifotati

    "sikia nyie mimi bado nasoma na sihitaji simu aina yeyote Afu we zai fata mambo yako sawa?"

    "umeona sheby anavyonijibu eeh?"

    Mara mama yangu akaingilia kati

    "nyie hebu muacheni kiziwanda wangu, kwani uamuzi wa kuwa na simu ni wake"

    "mmhhh mama ila mdogo wetu kazidi yaani utafikiri ni masikini bwana"

    Alikua ni dada nusura ndio aliongea hivyo

    "afu dada nusura na wewe ushaanza kuniingilia eee?"

    "Mmhhh baasi mwaya mdogo wangu nisamee basi"

    Zai nae akaongea lake liliozua mjadala kamili

    "tatizo ni lile lishule lake analosoma yaani ile shule ina maadili mpaka inakera"

    "Ati nini? Mamaa unamsikia mwanao zai anaizarau shule yangu?"

    "kwanza hio shule nitakuhamisha muda sio mrefu"

    "aaaaaa mamaa sasa ndio mambo gani ayo? mi sihami ile shule"

    "ngoja baba ako aje"

    "oohooo kwani si nitaongea nae"

    "uongee nae nini sasa?"

    "si asikubali nihame"

    "wakati yeye ndio alilitoa hilo wazo"

    "haaaaa jamani mamaa kwani hio shule imewakosea nini?"

    "tatizo unatueibisha kwa kusoma shule ya kimasikini kama ile"

    "Aaaa Eti anti mwaju kweli unaridhika na jambo hilo kweli?"

    "sasa mimi nitafanyaje mwanangu? maana mama yako ndio kasema na mimi sina la kusema"

    "duuuu mbona sina mtetezi?. sasa nasema hivi mtafanya mfanyavyo ila shule mi sihami"

    Nikatoka pale mezani kwa hasira na kukimbilia chumbani kwangu, Nikachukua vitabu vyangu na kuanza kujisomea... hua mi sinunagi kama watoto wengine wa kitajiri walivyo.. kitu kidogo tu kanuna nuuu... mimi nilikasirika tu kidogo..

    Mara ghafla nusura alikuja chumbani kwangu, Na kuwasha tv kisha akakaa kwenye sofa.

    "sheby? umechukia kwani?"

    "aaahhh mnaanzisha mada zenu za ajabu"

    "lakini sio mimi ni dada yako zai ndio kaanzisha"

    "aaaahh zima basi hio tv si unaona najisomea?"

    "mmhh haya nimeizima"

    Sasa alipozima akaja pale kitandani kwangu na kulala kama nilivyolala mimi huku akiangalia ninachokisoma katika kitabu.

    "heee ivi haya masomo mshayafikia kwani?"

    "Eee tena muda tu"

    "mmhh hiki kitabu si cha form 4 hiki?"

    "mmhhh"

    "ni cha nani?"

    "si cha zai"

    "kwaio umeshiba?"

    "aah sili tena kwani mshaniuzi"

    "mmhh na wewe kwani utahamishwa kweli?"

    "ahhh mama saa zingine haeleweki huyu"

    "mmhh huhami bwana"

    "kweli sihami?"

    "walikudanganya tu"

    Duuuu nilifurahi sana kusikia sihami maana shule yetu ni nzuri na ina maadili mema sasa nikihama na kwenda huko kwenye shule ya kihuni ambayo mwanafunzi anaenda na gari kaliii na simu za bei ghali...

    Basi dada yangu alitoka na mimi nikalala zangu, mpaka asubuhi kumekucha ni muda wa kwenda shule.

    Nikajiandaa vizuri kisha nikaenda mesani kwa kunywa chai. nilikuta mkate mlaiini uliopakwa kila aina kipakio cha mkate. Duuuuu nilianza kupiga chai huku nikimsifu kimoyo moyo mtu alienitengea chai hii.

    Mara Anti mwaju katokea Yule mfanyakazi wetu wa kwanza kabisa ambae hua ndio namuita ANTI MWAJU

    "naona unacheka tu peke yako?"

    "hehehehehe ndio anti shkamoo?"

    "marahaba hujambo?"

    "sijambo anti"

    "ok ukimaliza utaweka vyombo pale sawa?"

    "sawa anti"

    Unajua mimi nampenda sana anti mwaju kwasababu hua alinilea katika maadili mema na bado anaendele kunilea hivyo hivyo.... maana hapa kaniambia nitoe vyombo na wakati wafanyakazi wapo tele.,... kwahio hii ni ishara ya malezi mazuri. ila kwa litoto lingine lingeambiwa litoe vyombo... hooooooo angeandamana nyumba nzima.

    Basi nilimaliza kula kisha nikawa natoa vyombo huku nikifuta meza. mara beki tatu mmoja kaja

    "kaka lete nikuseidie"

    "ah ah natoa mwenyewe usijali"

    "ah ah bwana ukionekana unatoa wewe nitafokewa"

    "usijali nitakutetea tu"

    Mara anti mwaju katokea

    "we fatu hebu muache atoe mwenyewe. mimi ndio niliomwambia atoe vyombo. kwani akiwa na kwake ataish ishije?"

    Basi nilitoa vyombo na kufuta meza kisha nikaingia chumbani kwangu ili nichukue begi kisha nitoke zangu nje nisubiri school bus....

    Sasa ile nataka kutoka mara nikakutana uso kwa uso na batuli ambae ni mmoja kati ya mahausi geli wetu.... na hua mahausi geli wetu wote ni wakali na wana maumbo ya mitego ile mbaya...

    "nini shida?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nilimuuliza kwa kawaida tu

    "nimekuja kuchukua nguo nikafue"

    "ooohh Ok subiri nikutolee"

    Nikaanza kumtolea nguo ambazo nilizivaa ili akafue.

    Nilimpa nguo chache tu maana mimi hua sibadiligi kila saa kama mitoto mingine ilivyo na sifa za kutupia mitupio yao....

    "kaka mbona ni chache?"

    "heeeee sasa nikupe hadi nguo safi nini?"

    "boxer huna?"

    "heeeeeeee boxer za nini sasa"

    "buana kaka mi nataka nikazifue tu"



    Nilishindwa kumuelewa huyu mfanya kazi wetu kwa kuzitaka boxer zangu.

    "aaaa asante sana dada ila boxer hua nazifuaga mwenyewe"

    "mmhhh poa"

    Alitoka zake huku akinitingishia mkalio wake mkubwa afu mlainiii. Ila namshukuru mungu kwa kua sina swaga hizo za kutamani tamani hovyo. Nilitoka zangu nje na kuenda kusubiri school bus nje..

    Nilipanda zangu bus kisha nikawa naelekea zangu shule.....

    Humo ndani ya basi wanafunzi wote ni swaga za dua tu.. yaani kila mtu kashika junzuu yake.... nami nikatoa yangu na kuanza kusoma huku gari likiendelea kwenda

    Tulikua tumevaa sare za kiislamu tu. yaani wasichana wamevaa mabaibui na sisi tumevaa panjabi. hizo ndio sare zetu za shule, yaani hakuna cha sketi wala mikaptula hapa,

    Gari iliendelea kusonga mbele huku wanafunzi tukijisomea vitabu vya dini,

    Mara Ghafla mwanafunzi mmoja wa kike akaniita

    "we sheby?"

    "sema?"

    "mambo?"

    "poa"

    "ivi mbona we ni mpole mpole sana wewe?"

    "kwanini useme hivyo?"

    "nimeshangaa jana ulivyojipeleka ofisini eti kisa umechelewa namba"

    "ni hilo tu au kuna jingine?"

    Nilianza kuonekana kukasirika kimtindo mpaka mtoto wa kike akaanza kuogopa ogopa

    "basi yaishe.... ila sheby? vp nipe namba yako basi"

    "namba ya nini?"

    "si ya simu"

    "mi sinaga simu na sitaki simu"

    "mmhhh na wewe unajiendekeza uanalojia"

    "shakira? naomba tueshimiane sawa?"

    "samaani ila kama vp leo tutoroke afu kuna kitu nikakupe nyumbani"

    "heeeeeee ivi una akili wewe? yaani nitoloke shule?"

    Toka mwanzo tulikua tunaongea taratibu kabisa kwasababu si tulikua tumekaa siti moja.. sasa alivyoongea hivyo Nami nikaanza kupayuka kwa sauti kubwa.

    Akaniwahi kwa kuniziba mdomo huku akisema

    "sheby plz nimeponyokwa tu"

    Nilishindwa kuongea kwasababu aliniziba mdomo

    Aliponiachia mdomo wangu sasa sikua tena swaga za kuongea tena... Afu nikimcheki mtoto wa kiislamu mzuriii afu umbo analo la kutosha. ila hakufunzwa vizuri na wazazi wake coz yupo na tabia kama za dada yangu zaituni. Yaani hajatulia kabisa japokua shule tunayosoma ni yenye kufundisha maadili mazuri na elimu ya duniani pamoja na ya Akhera,

    Tulifika shule huku mtoto shakira ananiangalia tu kwa jicho la kuniibia ibia.

    Sikujali kwani nilijua kakasirika kwasababu nilikua nataka kumkosoa mule ndani ya gari, Basi kama kawaida tukifika shuleni hua tunafanya usafi tu kidogo kisha tunaingia darasani.

    Shule yetu sisi pia ni ya kitajiri na sio kua imechoka kama shule zingine. ila sema ni maadili ya kiislamu kua ni lazima mtoto afanye kazi kwa kuwaseidia wakuuu

    Mfano mzuri ni kule shuleni kwa dada yangu, kule hua mwanafunzi hajuagi swala la usafi, tena kama atakuta kiti na kimeza ni kichafu anagoma kuingia Class siku hio. mpaka kikafutwe ndio aingie... yaani kwa kifupi shule yao ina wafanya kazi, hivyo hawanaga muda wa usafi wala hawasimamagi paredi ( mstalini ) eti miguu itaingia tumboni

    Sasa huku shuleni kwetu sio kua wameshindwa kuweka wafanyakazi kama hao, bali ni kwamba sisi wenyewe wanafunzi ndio tunapaswa kua na maadili ya kujisafishia wenyewe shule yetu.. yaani tusikae kilege lege kama watoto wengine wa mabosi.

    Sasa nikiwa zangu mahari nikiwa nimeshika mpira wenye maji. kwa kunyweshea maua. Nilimuona shakira akija karibu yangu huku akiwa kashika skwiza.

    "mmhh nakuona baby"

    "baby? baby ndio nani"

    "oohhh sorry nilikua nataka niseme sheby?"

    Mtoto alikua ananiangalia huku akitabasamu kwa mbaali afu mtoto ana vidimpoz fulani afu mweupeee mzuriii mrefu kiasi flani..

    "ok fanya kazi basi coz cheki kule bado kuna maji maji hebu nenda"

    "ivi sheby? mbona upo kama sio kidume vile"

    "ok poa mimi ni mwanamke si ndio? sawa ila we nenda sitaki kukuona karibu yangu"

    Aliondoka lakini kama hakupenda kabisa kuondoka maeneo yale,

    Ilipofika mida ya saa 1:45 asubuhi tulisimama mstalini ili kama kuna tangazo lolote tuweze kulisikia kwa pamoja......

    Punde sii punde tukaingia darasani Huku nikiwa na shauku ya kutoa somo fulani la sayansi ya mwili wa binaadamu jinsi unavyopata hisia pindi ashikwapo mkono na mmoja wao....

    Ila ilipofika saa 4 tukiwa darasani tumetoka break ( mapumziko ) kwa bahati mbaya kuna taarifa tuliletewa darasani

    Alikuja head master ( mwalimu mkuu ) na kututangazia kua.

    "Assalaamu Aleykhu mwaalimu"

    "Waaleykhu Mssalam walahmatu Lah Wabarakhatu.... mnaweza kukaa"

    Hua tunasalimia kiislamu maana si ASHIRAF SEMINARY SEC SHOOL

    Seminary ni shule zenye maadili ya kiislamu kwa sana, but shule yetu hio inafundisha mpaka masomo ya dunia... yaani sio Quran tu. bali hata masomo ya shule za kawaida

    "aaaa kuna taarifa zimenifikia hivi punde kua mwalimu shufaa hatupo nae tena"

    Wanafunzi wote tulianza kulia kwa uchungu wa hali ya juu. coz alikua ni mwalimu tunaempenda sana na alikua ni ticha wangu wa sayansi. daahhh mwalimu shufaa keshafariki dunia...

    "kwahi tunatoa likizo ya siku tatu... leo ni alhamisi si ndio?"

    "ndio"

    "basi tuondokeni kwa kwenda kumuona mwalimu wetu kamwisho mwisho kwani hat aaaaa ahahahaha aaa twendeni tu nyumbani kwake"

    Mwalimu mkuu alikua akiongea huku akilia kama mtoto. maana mwalimu aliokufa alikua ni mwalimu wa watu wengi sana hivyo kila mtu alilia darasani hapo...

    Haikuchukua muda tulitoka na kwenda kumuona mwalimu shufaa..

    Kisha tukapanda school bus kwa kurudishwa nyumbani, na muda huo ilikua ni mida ya saa 6 mchana.. Tulirudi nyumbani na kuendelea na shuhuli zingine za nyumbani, Huku nikisubiria siku ya kesho ambapo ndio maziko yake

    Kesho yake ilifika na muda wa kuelekea kuzika ulifika, Hivyo mimi siku hio nilienda na gari ya dada yangu zaituni. Ambayo ni gari yake ya kwenda shule.. gari yenyewe ni gari mpya aina BUGHAT gari flan yenye ukubwa mzuri.

    Nilifika kwenye mazishi na nilikutana na wanafunzi karibia wote wa form 3 na 4 kasoro form 2 na 1 ndio hawapo. ni kwasababu ni wadogo wadogo, si unajua vitoto vya siku hizi ni vidogo afu viko secondary. Tulielekea kuzika wanaume tupu ila wanawake hawakuruhusiwa kwenda makaburini,

    Basi baada ya muda tulirudi nyumbani kwa mwalimu ambako kulikua kuna watu wengi sana hivyo hata mimi nilikuepo kati yao na michango ilipita, kama kawaida yangu kutoa vitita

    Ilipofika muda wa saa mbili usiku wanafunzi tulibakia wachache sana kwani wengi wao walikua ni wanawake, sasa kwa kawaida ya msiba hua watu wenye uwezo wa kulala nje basi wanapaswa kulala, Yaani baada ya mazishi hua kuna watu wanalalaga pale nje ya nyumba ya msiba, hivyo kwakua sisi wengi wao ni waisilamu, hivyo tulilazimika kulala usiku ule...

    Nilienda kupaki gari pembeni kisha nikachukua na shuka kisha tukalala hapo nje ya nyumba yenye msiba, Na tulikua wanafunzi wengi wengi kasoro wanafunzi wa kike ndio hawakua wengi

    Tulikua tunapiga story za manabii ambao walishawahi kuja duniani. maana hapo hatukutaka kupiga story zozote tofauti na dini yetu ya kiislamu,

    Ilipofika saa nane nilikua naona nabanwa banwa sana. yaani kama vile mtu anaetafuta joto fulani hivi

    "we nani wewe?"

    Niliuliza kwa utaratiiibu mzuri maana si ilikua ni usiku mkubwa hivyo hatupadwi kupaza sauti zetu

    "sheby naskia baridi"

    "haaaaa sasa we umefata nini huku?"

    "sheby plz nisaidie koti lako"

    Alikua ni shakira ndio niliokua naongea nae

    Yaani katoka huko kwa wanawake wenzake mpaka huku kwa wanaume aaayygggg aseeeee

    Ilibidi nivue koti langu ili ajifunike

    "haya shika afu uende kule kwa wanawake wenzio"

    "kule hakuna nafasi na ndio maana nimekuja huku"

    "mmhhh aisee sasa umekuja wa nini lakini?"

    "nisamee bwana au kama ni koti lako chukua"

    "basiii"

    Basi nilimuacha mtoto shakira alale pale pembeni yangu. kwani sisi watoto wa kiislamu hua hatujafundishwa uchoyo.....

    "sheby?"

    "nini tena jamani uuuwiiii unanikatishia usingizi bwana"

    "bado nasikia baridi"

    "aaaaggyyyyy sasa nifanyaje jamaniii?"

    "tujifunike wote na hilo shuka lako"

    "uuuwwwiii ani shakira una tabu wewe duu haya chukua lote"

    "na wewe je?"

    "mi sitaki tena"

    Basi mtoto alijifunika na lile shuka langu huku akijifanya kama hapati usingizi vile

    Ilipita kama nusu saa hivi nikasikia

    "sheby?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "nini wewe aiseeeee aaaaaa"

    "bado nasikia baridi"

    "afu we nisikilize kwa makini sana.. usinizoee hata mara moja kwanza lete shuka langu"

    Nilimpokonya shuka langu na kuendelea kulala zangu huku nikiwaza mambo yangu ya shule...

    "shebiiiiiiii iiiiiii uuuuiiii"

    "nini jamani mi staki kelele aisee si unaona ni usiku huu?"

    Heeeee sasa kumuangalia vizuri namuona akiwa anatetemeka kweli Nikaona mungu wangu kasije kakafa katoto cha watu,

    "we shakira ndio nini hivyo?"

    "sheby mwenzio naumwa"

    "eee mungu wangu eeee ona sasa ushaanza kuleta homa sasa duu... hebu ngoja niwaamshe wenzangu kwanza"

    "we sheby usimuamshe mtu"

    "kwanini sasa?"

    "nishike shavu uone nilivyo na joto ksli"

    Kweli nilipomshika kwenye shavu alikua ana joto hilo duuu.

    "bwana we nipeleke kwenye gari yako huenda nitapona"

    "mmhhh aisee shakira ni msumbufu wewe"

    "plz sheby kumbuka mwenyezi mungu subuhana hu wataalah hapendi ukaidi sheby"

    "ok basi twende nikupeleke"

    Nilimnyanyua na kumpeleka kwenye gari ambayo nimekuja nayo. na ni gari ya dada yangu zaituni.

    Nilimuingiza katika siti za nyumba na kumuachia shuka

    "sikia hii gari ina tv hivyo ukijisikia utawasha uangalie sawa?"

    "sawa... sasa unaenda wapi sheby?"

    "wacha nikalale na wanaume wenzangu kule"

    Nikamueka vizuri kisha nikamfunika shuka,

    Sasa ile natoka tu kutoka ndani ya gari... nilishangaa kushikwa mkono na shakira huku akisema.

    "sheby plz naomba tulale wote mi naogopa buanaa"

    "aisee shakira kumbuka khadith za mtume muhammadi zinasema hivi?"

    "ah ah nazijua hizo khdith ila hakukataza kukaa na mwanamke karibu"

    "asta khafiru lah. mi sitaki bwana"

    "ok basi na mimi natoka ndani ya gari yako na sitaki tena wacha nife hapa hapa nje?"

    "haya ok ok ok poa tulale tulale"

    Nilikubali kulala nae lakini nia yangu ni nimpe kajoto ili alale na akipitiwa tu namtoroka,

    Nilisogea karibu yake na kuanza kumbembeleza kama mtoto vile huku kichwa chake kikiwa kifuani kwangu

    Lakini tukiwa bado tunaendelea kubembelezana Nilishangaa shakira akianza kunipapasa kifua changu. jambo ambalo kwangu lilikua ni haramu kubwa sanaa

    "we shakira? unafanya nini?"

    "buana sheby natafuta joto ili nilale"

    "sasa ndio unalitafutaje hivyo?"

    "sheby buana we tulia tu nilitafute"

    Sasa mtoto alikua anavuka mipaka ya kunishika, Huku mdomo wake ukiwa shingoni kwangu. Alianza kunilamba shingo yangu huku akichezea chuchu za kifua changu

    "shakira unafanya nini?"

    "buana wewe niache ukooo"

    "shakira ujue tutagombana?"

    "sheby tulia basi usingizi unakuja"

    Alirudia tena kunilamba shingoni huku mkono wake mwingine kuna kitu kashika.

    "umeshika nini huko mkononi?"

    "si anjifu tu"

    Sasa mara shakira aliyatoa matt yake nje kwa juu....

    "heeeeee we shakira huu ni ujinga gani unaufanya mbele yangu Ee? Kumbuka mtume swala"

    Aliniziba mdomo na kuniambia

    "sheby hua mi siwezi kulala bila kutoa matt nje.... na hivi ndivyo ninavyoutafutaga usingizi hivi hata nyumbani"



    Nilishindwa kumuelewa shakira kwa kile anachokiongea. Eti hata kwao hua ndivyo anavyoutafuta usingizi kwa staili hii ya kushikana shikana. Kiukweli Sikuipenda ile tabia hivyo nilimtoa mikono yake katika kifua changu kisha nikamtoa kabisaa mwilini mwangu na kumuekea ngumu ya ukweli ukweli.

    "mazoea na wewe sitaki, kafiri mkubwa wewe"

    "sheby? yani unanitukana mimi?"

    Nilitoka kwenye gari na kumfungia huko huko ndani ya gari, kisha mimi nikaelekea kulala na wenzangu pale kwenye mkeka, Wakati huo kweli kulikua kuna baridi ya haswa. ila mimi nilikua ni mtoto wa kiume na mwenye nguvu, Afu isitoshe pia ni mwana mzoezi mzuri hivyo mwili wangu haukukaa hovyo hovyo kama mitoto mingine ya kitajiri ambayo ina miili mikubwa utafikiri ni mtu mzima kumbe ni mtoto wa miaka 15 tu,

    Ilipofika mida ya saa 11 asubuhi Niliamka na kwenda kuoga hapo hapo nyumbani kwa mwalimu. Kisha nikatembea kwa mguu hadi msikitini kuswali swala ya asubuhi,

    KUSWALI HUA NASWALI KILA SIKU NA KILA MUDA WAKE. HIVYO USIJE UKAONA KUA MBONA SAA ZINGINE SIENDI. NI KWAMBA SIO KILA MUDA NITAELEZEA NAENDA MSIKITINI, MAANA STORY NZIMA SI ITAJAA MANENO YA MSIKITINI SASA???? KWAHIO UKAE UKIJUA KUA MSIKITINI NAENDAGA KILA SIKU.... ILA SAA UKIONA SIJAENDA BASI UJUE MUDA FLANI NIKIENDA NITAZILIPIA ZOTE.... HIVYO KUMUOMBA MUNGU KWANGU NI KILA SIKU

    Niliingia masjidi na kuswali vizuuri sana kisha nikatoka na kuelekea msibani huku nikitroti ( kukimbia kimbia ) Nilipofika msibani nilifungua gari na kumuamsha shakira, maana jana nilimfungia ndani ya gari kutokana na ile staili yake ya kupata usingizi mpaka amshike shike mtu ndio alale

    "assalam alekh?"

    Nilianza kumsalimia lakini alionekana kua na jazba za hapa na pale kwa kutomfanya alale jana, Sasa mtoto shakira alitoka kwa hasira na kuelekea kule kwa wanawake wenzie, Nilifunga mlango wa gari fasta fasta na kumfata kule anapoelekea

    "shakira? we shakira? kira?"

    "niache bwana"

    "nini shida kira?"

    "nishakwambia niache ntakueibisha hapa msibani wewe oohoo we haya"

    Mmmhhh niliposikia hivyo tu nikanywea kimyaaaa. Maana hakuna kitu nakiogopa kama kueibishwa mbele za watu kama hivi

    Nilirudi pale kwenye mkeka na kuaga aga wenzangu kisha nikaingia kwenye gari na kuelekea nyumbani huku nikiwaza cha kufanya leo juma mosi. maana siku hii ya leo ilikua ni siku ya juma mosi..... nilifika nyumbani huku nikiwa na haraka ya kwenda mazoezini, maana hua kila asubuhi naendaga GYM ( jim ) kupiga mazoezi. na ndio maana mwili wangu hua ni mwembamba utafikiri naugua ukimwi kumbe ni mazoezi tu. Nilipofika nyumbani niliingia mpaka geto na kuvaa track za mazoezi kisha nikatoka huku nikiwa na taulo langu shungoni. Hua siendagi na gari kabisa

    Nilikua nakimbia kimbia tu taratibu. Mpaka nilifika gym na kuanza kufanya mazoezi ya kukimbia na kubeba beba uzani kidogo ili kuuweka mwili safi na wenye afya nzuri.

    Nilipotoka gym nilirudi zangu nyumbani na kuingia bafuni kisha nikaoga vizuuri kabisa. Nilimaliza na kuanza zangu kujiremba remba kiaina, Hua swaga zangu ni zile zile za kisasa. zile za ujana kuvaa minyonyo iliobana kiaina. nikatupia pamba zangu kisha nikatafuta SNAP BACK nikicheki snap zipo kama 12 hivi Nikachagua moja kisha nikavuta na hedi foni yangu aina BEAT BY DR DREE ( b ) Kisha nikaitupia shingoni afu nikavuta i pad yangu ya music, hua sinaga simu afu ni mpenda music vibaya mno na talent yangu hua ni kudance ( real talent ) napenda kudance sana ila si unajua wazazi ndio vikwazo hivyo talent yangu haijajulikana rasmi kwa wazazi... na hakuna mzazi anaependa mwanae awe muimbaji au mchezaji wa music.... Bali hua tunaibia tu

    Nilishang'aa zangu chini nikatupia DC ya maana Ani ukinicheki tu mwenyewe unaridhika..... je unajua naenda wapi?

    Baada ya kuvaa nilikaa sofani kwanza na kuangalia moja ya quran tukufu iliokua ikionyeshwa....

    Nikicheki saa inaniambia sasa hivi ni saa 5 asubuhi, Nilikurupuka na kuelekea chumbani kwa dada nusura Na kumkuta anavaa nguo. Nilimkuta yupo na khanga moja tu afu ndio katoka kuoga Heeeee na vile dada zangu wote walivyojaaliwa sura na maumbo heee ni mshike mshike hio.

    Lakini licha ya kumkuta hivyo wala hakuna mtu aliekua na wasi wasi... yaani licha ya nusura kua na khanga moja lakini hakushtuka wala hakupepesuka tena ndio kwanza ananiambia karibu..

    "aaahhhh yani bado tu?"

    "namalizia jamani sheby"

    "aah ntaairisha ujue?"

    "ah ah bwana sheby nakutegemea ujue?"

    "fanya fasta basi asee.. kwani zai haendi?"

    "mmhhh anaenda ila haeleweki na hata sasa hivi sijui kaenda wapi"

    "hebu ngoja nikamuangalie chumbani kwake"

    Nilienda hadi chumbani kwa zai lakini hakuepo kwa wakati huo

    "hayupo bhana"

    "Achana nae"

    "aseee yaani bado tu hujavaa?"

    "sheby mdogo wangu? subiri nivae au wataka nikaeibike nini?"

    Nilitoka zangu na kuenda kutulia zangu sebuleni kwa ajili ya kumsubiria nusura atoke, Nilikaa hapo mpaka nilichoka huku nikiwa nasinzia sinzia.

    "asee nusuraa?"

    "tayari jamani heee"

    "twende sasa"

    Dada nusura aliniomba nimsindikize kwenye harusi ya rafiki yake ambae alisoma nae shule moja. sasa ndio maana nimelipuka na yeye pia alilipuka ile mbaya

    "twende sasa"

    "ila dada? huko hakutokua na fujo?"

    "fujo? fujo zitoke wapi na wakati kutakua na ulinzi wa hali ya juu"

    "aahh poa twende ila dua dua si zitakuepo?"

    "dua za nini bwana? huyo mtu ni mkristo"

    "haaa yaani niende kusherekea harusi ya waikristo?"

    "bwana sheby acha izo bwanaaa nisindikizee"

    "aisee je tukiambiwa tufumbe macho afu tupige makofi kwa kumsifu yesu kristo?"

    "kwani ni lazima hufanya hivyo? hio ni maamuzi yako tu"

    "haya ok twende"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sasa ile tunatoka tu mlangoni Niliskia kelele nyingi za honi zikitokea nje. na alikua ni zai ndio alikua akipiga honi ili afunguliwe geti, Nilishangaa akiingia na spidi kali kisha akashuka huku akicheka na kufurahi ile mbaya

    "uuuuuwiiiiii mamaaa mamaaaa mamaaaa?!

    Alianza kumuita mamaa kwa sauti kubwa hadi wafanyakazi wakashangaaa

    "nini wewe unaniitia nini?"

    "kweli siku zote namuonaga braza angu sio rijali kumbe ni shida eee?"

    "unaongelea nini we zai?"

    Aliulizwa na mama na mimi nilikua pembeni

    "yaani mama usijali na wala usihangaike sijui kwa waganga huko kisa sheby... ona hiii"

    Heeeee nilishangaa kuona kitu anachokionyesha mbele ya mama na dada nusura

    "we zai hio chupi ni ya nani na umeitoa wapi?"

    Aliulizwa na mama kusiana na hio chupi aliokua akimuonyesha mama.. na ilikua ni chupi ya kike

    "mama hii chupi niliikuta kwenye gari yangu. na sheby jana ndio alikua nalo hili gari kule kwenye msiba wa mwalimu wao"

    Nilitoa macho hayo huku nikiwa na hasira hizo duuu

    "we sheby mwanangu hii chupi uliitoa wapi?"



    "mamaa mi sijui kuusu hio chupi kwani ndio kwanza naiona hapa"

    Nilianza kua na kigugumizi cha hapa na pale kwasababu sijui hio chupi ilifikaje huko kwenye gari, kiukweli sikua na jibu la kutoa kuusiana na hio chupi, maana sikumbuki kitu chocho kusu hilo. Kiukweli nilijisikia vibaya sana ila Basi kutokana na kutokua na jibu sahihi basi na kesi iliishia pale pale na chupi ikatupwa...

    "we zai huendi harusini?"

    Aliulizwa na dada nusura kua haendi

    "nitaenda ngojeni nioge kwanza"

    "sheby msubiri dada ako mi wacha nitangulie coz mimi ndio mpambe wa bibu harusi"

    "aaahh hili litachelewa bwana"

    "wala tu hachelewi sawa mdogo wangu?"

    "aaa nitamsubiri tu kwa heshima yako"

    Basi dada nusura alipanda gari yake na kuondoka, sasa mimi tena nikawa namsubiri zai ili twende wote huko harusini. na kadi ya kuingilia tunayo maana harusi za kitajiri bila kadi ya mwaliko huingiii ng'oo

    Ilimchukua kama robo saa hivi hadi kumaliza kuoga Kisha akaenda kujibararua na mavipodozi yake, Kama unavyojua wadada zangu wote ni wazuri na wana maumbo ya maana, afu pia ni mashombe shombe kasoro mimi tu ndio sina asili hio.

    Mama yangu ana asiri ya kiarabu kwani baba yake ambae ni babu yangu ni mtanzania na mama yake ambae ni bibi yangu ni muarabu na yupo afrika kusini. Kwahio mama yangu sio muarabu kabisa na wala sio muafrika bali yupo mixer yaani rangi yange haikubezi upande mmoja bali zimechanganyikana kwahio ukitaka kumjua ni mtanzania utaona mixer ya rangi ya ngozi. na ukitaka kujua ni shombe la kiarabu utaona unywele tu. sasa imagen mixer kama hio je? itatotoa watoto wa dizaini gani?.... we acha tu dada zangu ni shida yaani kama ningelikua ni muhuni muhuni duuuu ningesha watamani kitambo sana. ila nashukuru kwa malezi niliopewa ya kumueshimu kila mtu, kuto kumdharau mtu Eti kisa tuna pesa kutamani mapenzi ingali bado ni mdogo na pia dini yetu ya kiislam hairuhusu vitu kama hivyo,

    Baada ya muda dada zai alitoka akiwa kavaa kiajabu mmhhh

    "sasa ni nguo gani hio umevaa?"

    "kwani we unajua nini wewe?"

    "aahaaa kwaio mi sijui kitu ee? sawa"

    "sasa unaenda wapi?"

    "sipandi na wewe gari moja"

    "sasa sheby ndio nini hivyo jamani?"

    "nimekwambia hivi naenda kupanda dala dala"

    Sasa nikiwa ndio naelekea zangu kupanda gari la abiria wengine tofauti na la zai. niliitwa na anti mwaju

    "we pumbavu? rudi hapa haraka"

    "lakini anti si unamuona zai hio nguo alioivaa jamani"

    "nimesema rudi haraka"

    "sawa tuuu ila basi akatishie hata kanga tu"

    Anti mwaju alivua kanga yake na kumpatia zai

    "shika na wewe hebu jizungushie ili ufiche hicho kinguo chako"

    Zai alikubali lakini ni kishingo upande

    "Eeee bora hivyo sasa Kuliko utembee na shekhe mzima na kimini sketi"

    Basi niliingia kwenye gari na dereva ni yeye mwenyewe,

    Dada yangu zai ana umbo la kipekee sana kwasababu hata akivaa gunia lakini bado ataonekana tu. sasa hapa alikua kavaa kamini sketi tena kenyewe ni kepesiii afu alikua na chupi tu afu na hio mipaja yake sasa yote ipo nje.. sasa imagen kitu kama hicho je humo ndani ya gari mi si ningeteseka.

    Tukiwa safarini zai alionekana kukasirika sana kwa kutopewa uhuru wa kuvaa kiguo chake hicho.

    "sasa zai? unanunishwa na nini?"

    "niache"

    "asa usiambiwe ukweli?"

    Wakati huo bado tupo safarini tukielekea kwenye harusi huko kijenge.

    "ila sheby hebu ngoja nikuulize swali"

    "swali gani hilo?"

    "afu mbona anti mwaju anakufokea vile mara akutukane, ivi anajua thamani yako kweli? na aaangesikiwa na mama vile alivyokutukana heeee angefukuzwa kazi siku hio hio hata kama ni wa muda mrefu"

    "unajua wewe hukulelewa katika maadili mema na ndio maana hata lile neno pumbavu kwako limekua kama kifo yani?"

    "ila anti kazidi kukufokea"

    "we muache tu bwana mbona una gubu we zai? ntashuka kwenye mgari wako huuu wewe ooohoo we haya"

    "mmhhh basi yaishe"

    Basi tulikua kama tunakaribia katika hio harusi husika.

    "ila kaka sheby we ni noma kweli yani"

    "noma wa nini tena?"

    "hehehehehe yaani umenipigia mtu mpaka kaacha chupi duuu kweli kaka yangu we ni noma"

    "sikia zai usitake tugombane kabisaa.... kwasababu huezi ukaleta jichupi lako afu ukanisingizia mimi nilikua na mwanamke ndani ya gari"

    "we sheby ivi unajua ile chupi sijaitupa bado, sasa hebu ione hii hapa je? mi naweza kuvaa kichupi kidogo hivi?"

    "asa mi ntajuaje na mwili wako? kwani mi ni mumeo? afu tueshimiane zai"

    "najua ukweli unauma bali mimi sina chupi kama hii afu isitoshe hii chupi ni ndogo kwangu"

    "je? kama uliichukua kwa wafanya kazi ili uje unisingizie je?"

    "kwanza sinaga mazoea na hao wajinga wajinga"

    "ebu lete hio chupi apa"

    Niliishika ile chupi kisha nikaitupa huko nje, na wakati huo gari ilikua ikitembea kwa kasi, hivyo kuipata tena ni ngumu

    "sasa umeitupia nini jamani?"

    "hahahahaha ndio maana nakuambia hio chupi ni yako afu unanibishia"

    "lione vile na ule mkichwa wake"

    "afu zai unanizoea ee?"

    "yaishe Eee?"

    Basi tulifika kwenye harusi ambapo kulikua na shangwe nyingi za kusisimua na kila aina ya burudani kasoro kaswida tu ndio sioni.

    "aaahh sasa hapa pana maana gani kama hata kaswida sioni?"

    "kaswida za nini na wewe?"

    "aahh kaswida muimu bwana"

    "ebu twende uko.. maana wewe ni wa kushikwa mkono"

    "niachie bana zai"

    "weeee twende je? ukipotea huku nitamuambiaje mama?"

    "si unamuambia tu nimepotea"

    "hebu twende"

    "subiri sasa mbona unanivuta tuu?"

    Basi tulikua tunaelekea kwenye viti maalumu kama V.I.P kisha tukaketi na kuletewa vinywaji aina ya pombe pombe fulani hivi..... Ila mimi nilichagua redbull isio na kilevi chochote,

    "nisubiri hapo hapo nakuja"

    "unaenda wapi we zai?"

    "nakuja bwana na wewe"

    Dada zai aliondoka kwenye kiti na sijui alikua anaenda wapi, Haikupita muda mara kuna msichana mrembo na ana umbo hilo afu alikua kavaa mini sketi kama ile ya zai... Alipofika alikaa kwenye siti ya zai

    "samaani kuna mtu apa"

    "usijali sikai sana"

    "ok"

    Niliendelea kupata redbull yangu taratibu huku nikiangalia shoo za watu wanao waburudisha waalikwa waliokua hapo

    "samaani mkaka sjui umekuja na nani?"

    "utaniulizaje swali kama hilo wewe?"

    "samaani basi kama nimekuuzi"

    "kwanza hujanisalimia afu una miswali ya ajabu ajabu tuu"

    "ok mambo vp?"

    "waaaiii staki"

    "kwanini sasa?"

    "nisalimie kidini ndio nitakuitikia"

    "haya tumsifu yesu kristo"

    "Ati nini? wee mwehu nini yani mi nimtumikie yesu? mwehu kweli wewe"

    "sasa matusi yote hayo ni ya nini?"

    "sasa utanisalimiaje kiikristo?"

    "kwani uliniambia dini yako ni ipi?"

    "muislamu"

    "ok Asalama Alekhu"

    "waalaykha"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mbona humalizii?"

    "kwani we si mkristo?"

    "ndio"

    "basi ndio sheria yetu kuitikia nusu"

    "kwasababu ni mkristo?"

    "ndio"

    "mmmhhh we muongo wewe"

    "basi yaishe afu naomba utoke mwenye hicho kiti atakuja sasa hivi"

    "usijali best nitatoka, afu kwani ni nani huyo?"

    "unamtakia nini?"

    "mbona unaringa we boy"

    "kwani nilikuita hapa?"

    "basi nisamee"

    Nikawa naendelea kucheki tamasha pale jukwaani kabla ya mwali kuletwa.

    "ila mkaka we hensamu"

    "najijua hivyo sihitaji sifa nyingi"

    Nilikua najibu hovyo kwakua tayari nimeshamchoka na maswali yake ya ajabu afu kama vile nimemshtukia vile

    Yule dada aliondoka zake baada ya kuona hajibiwi sahihi.

    "poa basi bai"

    "nenda"

    Haikuchukua muda mara zai karudi sasa hapo ndipo nilipojua kua yeye ndie aliemtuma yule dada aje hapa

    "vp nimechelewa ee?"

    "heeeee ile khanga ya anti mwaju umeeka wapi?"

    "ipo huku kwenye kibegi"

    "aaahhh kwahio unaona sahihi kutembea na hio mini sket si ndio?"

    "afu sheby we unajua ni mdogo kwangu hivyo chunga domo lako ilo"

    "haya bwana"

    "Eeehee nimeona ulikua na mschana hapa au ndio wifi nini yule?"

    "Eeee afu nimemtongoza kanikubalia afu mtoto mzuri ana mwili mzuri kinoma... vp ningependa uanze urafiki nae ili awe anakuja homu"

    "haaaaaa unasema kweli sheby?"

    "aaaahh chezea mimi wewe"

    "mbona yule yule ni rafiki yangu afu hata hivyo mimi ndio nimemwambia hapa aje kwahio nishukuru mimi"

    "nyokoooooo lione sasa na hilo lisura lako nininininini nyoooooo heee sijamtongoza wala nini na nilijua tu utakua ulimtuma"

    "nani nyoko? sheby nakuuliza nani nyoko?"

    Mara kuna mama alitokea pale ila mimi nilikua simjui

    "haaaaaa shangazi mamu shkamoo"

    Zai anaonekana kumjua mama huyo tena kamuita shangazi mamu.. basi nami nikaita hivyo hivyo kama dada yangu alivyoita

    "shkamo shangazi"

    "marahaba hujambo?"

    "sijambo"

    Mara huyo shangazi akaanza kuniangalia usoni huku akimuuliza zai

    "zai? mama yako ananiambiaga kua ana kiziwanda wake wa kiume sasa ndio huyu nini?"

    "ndio shangazi. huyu ndio last born wetu"

    "mmhhh ni hensamu kweli"

    Mara shangazi akatoa hela na kumpa zai huku akimwambia kua

    "kaninunulie vocha pale"

    Sasa kwakua mimi ni mtoto wa kiume na napenda kutumwa hivyo nilitaka kutumwa mimi

    "shangazi ngoja niende mimi"

    "ah ah muache aende dada yako tu"

    Mmhhh nilitulia huku nikiendelea kunya redbull yangu... zai alikua keshaondoka na nikawa nimebaki na shangazi

    "ivi shangazi unaitwa nani?"

    Yeye ndio aliniuliza.. kwani mtoto wa kiume kuitwa shangazi na shangazi yake sio kesi na pia haina shida... mbaya ni mtu mwingine tofauti na shangazi kumuita mtoto wa kiume shangazi. ila kwa shangazi hua haina shida, Sasa shangazi aliniuliza jina langu nami nilimjibu

    "naitwa sharbiny"

    "waaoo una jina zuri afu ni hensamu"

    "mmhh asante shangazi"

    "bwana we sheby usiniite shangazi"

    Mmhhh nilishangaa kumsikia shangazi eti nisimuite shangazi

    "sasa nikuite nani shangazi"

    "naitwa mariamu niite mamu"

    "apana shangazi mi sijafunzwa hivyo"

    "ok nipe namba yako basi"

    "mmh mi sina simu"

    "kwanini sheby?"

    "nimeamua tu"

    "ok sema nikununulie tablet au Iphone 6 au samsung galaxy s4 au unataka gari gani??? niambie basi jamani kabla dada yako hajaja"





    Nilishangaa sana kuskia maneno ya ajabu ajabu kutoka kwa huyu mama ambae tunamuita shangazi,

    Nilishindwa jinsi ya kumjibu ila kwakua mimi ni wa kuume na pia sipendi kua na vitu vya anasa anasa kama hivyo ambavyo amenitajia huyu mama,

    Maana kama ni utajiri sisi tunao kuliko yeye

    "samaani shangazi, mimi hua si mtumiaji wa hivyo vitu kwaio sihitaji litu chochote kile kutoka kwako na pia nikivihitaji vitu kama hivyo mama yangu anaweza kuninunulia"

    "ok nimekuelewa mwanangu ila usinifikirie vibaya"

    "wala tu shangazi mbona sina wazo lolote lile"

    "ok naaa vp leo si upitie nyumbani kwangu ukapaone?"

    "hapana shangazi leo naitaji kuwahi nyumbani coz kuna homework za kufanya hivyo sihitaji kuchelewa shangazi"

    Mara dada zai karudi kununua vocha kisha akampa shangazi vocha zake,

    Hakuchukua muda alituaga na kuondoka kwenda kuketi sehemu nyingine, maana ukumbi ni mkubwa kweli

    "vp shangazi kakuambiaje?"

    "mmhhh wala tu tulikua tukipiga stori za hapa na pale tu"

    "Aaahhh nilijua tayari keshakudanganya"

    "kunidanganya nini sasa?"

    "mmhh namjua huyu shangazi anapenda dogo dogo huyu"

    "aaaaa????? kuumbeee?"

    "kumbe nini?"

    "ah ah Amna kitu"

    Basi tulikaa pale kwa muda mrefu kuliko kawaida yangu. Ilifikia mahari mpaka harusi iliisha na watu wameshaenda katika moja ya hanimun zao huko. Tulitoka pale huku nikiwa na dada zangu wote tena ilikua nimemshika dada nusura kiuno na yeye pia kanishika kiuno huku tukiwa tunatembea kuelekea kwenye paking za magari, tumeshikana viuno lakini hakuna mtu anaemuwazia mwenzie uchafu coz tunajuana ni nugu. yaani mimi nilimshika kiuno kiutani utani na yeye pia hivyo hivyo. yani ukituona jinsi tulivyo unaweza sema ni kitu na mpenzi wake. kumbe walaaaaa hatuna hata hilo wazo bali tupo kindugu zaidi, Dada nusura alipanda gari yake na sisi mimi na zai tulipanda gari yetu ambayo ndio tulikuja nayo. na ni gari ya zai ya kuendea shule

    "sheby naomba nipitie marafiki zangu basi"

    "kwaio nishuke nipande daladala si ndio?"

    "hapana simaanishi hivyo"

    "bali unamaanisha nini?"

    "namaanisha niwapitie na wewe ukiwemo?"

    "sitaki wacha niende kwa dada nusura"

    Nilitoka zangu na kuelekea kwenye gari ya dada nusura na kupanda

    "vp mbona umekuja huku?"

    "ah si zai uyo keshaanza safari zake eti apitie marafiki zake"

    "mmhhh yani dada yako nae ana mambo duuu"

    Basi tuliwasha gari na kuondoka zetu,

    Tulipofika njiani tulikutana na wadada fulani wawili ambao ni marafiki wa dada nusura, Aliwapigia honi kwani walikua wanatembea kwa miguu..

    "we fatu? fatuuuu?"

    Dada alimuita mmoja kati ya hao huku akifungua kioo

    "abeeee Ooohhh nusura??? ivi na wewe ulikua kwenye harusi?"

    "ndio nilikuepo kwani hujaniona?"

    "waala sijakuona shost"

    "ok si munaenda nyumbani?"

    "ndio tunaenda ila tuliona tujivute vute kwa miguu tu"

    "ok twendeni basi"

    Wale wadada waliingia ndani ya gari ila mimi nilikua mbele kushoto kwa dereva na nilikua sitikisiki ng'oo wala hata hao wadada wenyewe sikuwaona na wala wao hawakuniona. waliingia wote kwa siti za nyuma, coz mbele nilikuepo mimi na dada yangu ambae ndio dereva mwenyewe.

    Safari ilianza na wale wadada wakaanza kunisalimia

    "mambo mkaka?"

    Niliwaitikia lakini sikugeuka wala nini

    "poa tu"

    Wakamuuliza dada nusura

    "nusura?"

    "abeee?"

    "fanya utambulisho basi au ndio shem nini huyo?"

    "weeeeeee hapana"

    "mmhhh useme mwenzetu maana wewe kwa kunyakua nyakua totoz hujambo"

    "No his my brother"

    "waaaooooo is your brother?"

    "yes"

    "young or big?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "kwani we unamuonaje?"

    "i think his young brother"

    "that is true for thing u think"

    "i need to see him"

    "ehehehehehe fatuuuuu what do u want to my brother?"

    "Nothing but for see him"

    "ok u can tallk with him"

    Nilikua nawasikiliza na hicho kingereza chao kibovu kibovu sijui walikiokota wapi huko, Sasa mdada kaambiwa aongee na mimi anaanza kujishaua shaua kimtindo huku akijifanya kusogea sogea

    "mkaka?"

    "sema?"

    Yaani nilikua nina dharau hizo yani sikua nageuka wala nini nilikua nimeangalia mbele tu huko tunapoelekea

    "geuka basi best"

    "nigeuke ili iweje?"

    "plz naomba tufaamiane ata kwa sura basi"

    "si umeshaniona we vp?"

    "samaani basi kama nimekuuzi"

    Mara dada nusura akaingilia kati huku akiwa kakasirika kwa majibu niliokua nikiwajibu marafiki zake,

    "sheby?"

    "naam"

    "una ugomvi na hao wadada?"

    "hapana"

    "sasa mbona unawajibu hivyo?"

    "lakini dada?"

    "sitaki cha lakini, kinachotakiwa ni kumueshim kila mtu sio kila anaekuita ataongea mbofu, sasa sikia naomba uwaheshim rafiki zangu sawa?"

    "sawa"

    Nilishikwa na hasira nyinginooo mpaka natamano kulia yani duuu. Sasa kwa hasira nilizo nazo niliruka mpaka kule nyuma kabisa na kukaa nao wale wadada

    "haya nimekuja kabisa huku huku sasa mlikua unasemaje?"

    Niliporuka kule wote walianza kucheka afu mi saa hio nipo kati kati yao.

    "mimi naitwa fatu mmhh nasoma chuo cha biashara dares lam na pia nimefurahi sana kukufahamu"

    "ok nashukuru sana Na wewe best sjui unaitwa nani?"

    Nilimuuliza huku nikiwa na tabasam zitooo

    "naitwa jasmini nami pia nasoma chuo dares lam IFM nami pia nashukuru kukufahamu"

    "nami pia nashukuru sana kwa kuwafahamu wote kwa ujumla nami nasema asanteni"

    Nilikua najiandaa kurudi kwenye siti yangu ya mbele maana si walitaka kunijua tu. sasa narudi kwenye siti yangu.. Mara mmoja akasema

    "sasa unaenda wapi si ubaki hapa tupige stori"

    "kwani si mlitaka kunijua tu?"

    "No pia tunataka tujue uchangamfu wako upo wapi?"

    Basi niliendelea kukaa katikati yao huku jasmini namuona keshaanza kung'ata lipsi kimahaba. duuu kumbe tayari keshaanza kunizimia mtoto wa kike. Ila mimi kama mimi sikua na mpango nae

    Sasa dada nusura alishaliona lile kwa rafiki yake jasmini kuonekana kunirembulia huku aking'ata lipsi zake,

    "jasu? jasu? we jasmini we?"

    "abeee nusura? mbona umenishtua jamani?"

    "sikia jasmini wewe ni rafiki yangu tuliosoma shule moja na darasa moja kwahio nakujua na wewe pia unanijua hivyo nakuomba sana stop that u think to my brother"

    "kwani umenionaje?"

    "jasmini? wewe sio mgeni kwangu hivyo nakuelewa sana coz i know u every thing u think about my broda"

    "No nusura umenifikiria vibaya tu kwani mi mbona sina mawazo hayo"

    "i know u like a handsome boy like my broda"

    "ok tufanye yaishe basi ila umenifikiria vibaya"

    "No jasu mdogo wangu bado ni mwanafunzi mdogo sana hivyo sihitaji kuona elimu yake inapotea"

    "ok am so sorry my friends"

    Basi kesi iliishia hapo na dada yangu akaniambia nirudi nilipokua nimekaa mwanza. Hivyo nilirudi kwenye siti yangu ya mbele na kuendelea na safari ya kurudi homu. Tulifika mahari ambapo wale wadada ndio wanahitaji kushuka yaani ndio wamefika maeneo ya kwao. walishuka kisha wakaagana

    Ila dada nusura alimuuliza kitu jasu

    "jasu?"

    "abeee?"

    "ila najua hatujagombana kabisa? maana usije ukasema oohoo nimegombana na nusura kisa ni mdogo wake, hivyo naomba urafiki we tu uendelee vile vile sawa mama?"

    "usijali mbona sijapaniki kitu? nipo fresh tu wala sina kinyongo na wewe"

    "ok poa sasa si mtakuja kesho salun?"

    "mmhhh kesho si juma pili?"

    "ndio"

    "hapana kwa upande wangu mimi kesho nina bonge la usafi hapo ndani we acha tu"

    "na wewe fatu utakuja?"

    "mmhhh nami pia nina nguo za kufua ile mbaya"

    "mmhhh hayeni bwana kama mumenichusa"

    "wala hatujakususa best ila juma tatu tutakuja usijali"

    "poa"

    Basi waliachana kihivyo kisha na sisi tukaingia njia ya kwetu.

    Tulifika nyumbani kama mida ya saa 11 jioni hivi, Ilibidi niingie bafuni kwanza nioge ili nitoe jasho la kubanana kwenye harusi kule. baada ya kumaliza kuoga nilikuja zangu sebuleni na kuangalia tv katka kipindi cha mawaiza ya kiislam ila usingizi ulikua ukininyemelea kidogo, kiasi kwamba sina muda naweza kulala hapa hapa sofani... Muda huo dada zai yeye alikua bado hajarudi nyumbani.

    ****

    Nikicheki muda ulikua umefika muda wa kwenda kuswali hivyo nikazunguka nyuma ya nyumba na kuanza kutawadha au kujiweka udhu wa kuswali msikitini... Nilipofika nyuma ya nyumba nilikutana na mmoja kati ya wafanyakazi wa nje... yaani yule mfanyakazi ambae anafanya usafi wa nje tu, Nilimkuta akifua vichupi vyake.

    "za saa izi boss?"

    Alinishobokea kihivyo ila mimi sikupenda kuitwa boss, maana humu ndani karibia wote wananiitaga boss au boss mdogo. Sasa hua sipendi kuitwa hilo jina

    "nani boss?"

    "si wewe"

    "silitaki hilo jina"

    Mtoto ni mzuri na umbo lake saafii afu kavaa kitu cha kanga tu. kwani hata chupi tu yenyewe hana coz ndio hio anayoifua sasa hivi.

    "basi nisamee ila sasa nikuiteje?"

    "mi si naitwa sharbiny hivyo niite sheby tu"

    "mmh hapana bwana nitakua nimekuzarau mtoto wa boss wangu"

    "wala tu tena utakua umenieshim sana kuliko kuniita boss"

    "sawa nitajaribu ila mi nitakuita kaka sheby?"

    "sawa ila wewe ni mkubwa kwangu"

    "sio sana ni kama mwaka mmoja hivi ndio nimekupita"

    "ok ila hizi nguo sio za kufulia huku hizi nguo ni siri yako mwenyewe coz huezi kuoga bafuni afu ukaja kufulia huku nyuma ya nyumba"

    "sawa kaka nimekuelewa ila kule bafuni umeme ulikatika hivyo kulikua na giza"

    "oohooo basi hakuna shida"

    Sasa nikaanza kumchokoza mtoto wa kike huyu,

    "kwahio utaniambia hapo hujavaa kitu kabisa?"

    "buana kaka mi staki utani wako uoo"

    "mmhh sasa si nimekuuliza tu"

    "Tehetehetehetehtehtehte basi ngoja nikavae"

    "ah ah malizia tu kufua"

    Alijishtukia kua aende akavae chupi ili nisije nikamsemea kua ana tabia mbaya ya kukaa bila chupi... Sasa mtoto alivyoinama na kuendelea kufua nguo... siiiiiiiii aiseee alinikosha na huko nyuma jinsi kulivyo tikisika kwa kukosa chupi iliobana, mpaka mwenye akaanza kujistukia hivyo kila saa akawa anaamka na kujifunga kanga vizuri

    "kaka?"

    "sema dija?"

    Huwa anaitwa hadija hivyo tunamkatishia na kumuita dija

    "mbona unaniangali hivyo?"

    "mmhh nimependa tu kukuangalia"

    Akawa anatabasamu huku akiendelea kufua chupi yake

    "hizo chupi zipo ngapi? maana naona humalizi kufua"

    "ni moja tu si hii"

    "aaaa usinionyeshe bwana"

    "kwanini?"

    "mmhhh si unajua mi wakiume hivyo nikiiona naweza zua majanga bure"

    Sasa mtoto akiwa anafua? makalio yake yalikua yakitikisika. Nikaangalia huku na kule sioni wale magadena boy. afu nikicheki muda ndio ule wa kagiza giza flani hivi...

    Nilimsogelea hadi karibu yake kisha nikamuuliza

    "vp nikushike ata mkono tu?"

    "jamani kaka sasa unishike ili iweje?"

    "ili nifurai tu"

    "tehethtehtehtehtehte mi siwezi kukukatalia kwani wewe si ndio mtoto wa boss wangu"

    "vp ulishawahi kuwa na mpenzi wewe?"

    "bwana kaka sheby kwani unataka nini?"

    Mtoto alianza kujua kile ninachokihitaji hivyo maswali kwake yalikua ni mengi mno, huku sauti yake ilishaanza kulegea legea. Na muda huo nilikua nimeshika kata ya kunawia au kutawazia au kujiweka safi kwa ajili ya kwenda kuswali...

    Nilijishtukia kua nataka kufanya ushenzi ambao sikuutarajia. sasa nikaachana na dija sasa nikaanza kupiga hatua ya kumuacha dija

    "kaka?"

    "nini dija?"

    "mbona hunishiki sasa?"

    "mh mh nimeairisha"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "bwana kaka nishike mkono tu kama ulivyotaka mwanzo"

    Unajua mahouse girl wakipendwa na watoto wa mabosi hua wanajiona kama masupa staa vile... na sio vibosi kama hivi vya mtaani No bali utajiri wetu sisi ni sawa na utufananishe na BAKHRESA au MANJI ndio sawa na utajiri wetu sisi hivyo ukimpenda house girl wenu... yaani kukukatalia ni asilimia 2 tu lakini hizo asilimia 98 zote ni lazima akukubali hata kama sio hensamu. Sasa mtoto nae akaendelea kufua chupi yake huku namuangalia kwa kumuibia.. sasa mbaya zaidi ni ile kanga ilikua imeloana hivyo ilikua imenata katika mwili wake...

    Aisee sikutaka kuivungia Nilitupa ile kata yenye maji kisha nikamsogelea karibu na kumtekenya kidogo, maana si alikua kainama

    "buaana kaka sheby umenishtuaaa"

    "unashtuka na nini?"

    "ona sasa umeshaniamsha mashetani yangu"

    "mashetani gani?"

    "mwenzio nina ha... ha.ha....ha"

    "nini sasa dija si useme?"

    Nilianza kumshika mbavu huku nikimpumulia shingoni na kumpa joto liliomfanya afumbe macho kwa raha alioipata

    "kaka sheeeeebyyyy?"

    "nini?"

    "utaweza?"

    "nishindwe kwanini?"

    "mmhhh nakuonaga wewe ni laini laini sana"

    Sikutaka kumjibu kitu nilimvuta kwa nguvu na kumuegemeza ukutani kisha mi nikawa kwa juuu... kumbe mtoto nae alikua ana nguvu sio mchezo kwani nilishangaa nimegeuzwa na kuwekwa ukutani afu yeye ndio akawa kwa mbele kisha akaanza kuniomba denda...

    Mimi nilishika tu makalio yake ambayo aliyasitili na kanga tuuuuu kwani chupi ndio ile aliokua akiifua... hivyo hata kanga yenyewe ilikua ni upande wa kanga... Niliyaminya makalio yake na kuivuta ile kanga

    "sssssssssiiiiiiii uuuuwiiiii kaka sheby buaaanaaaa"

    "nini dija?"

    "umeniminya maka.. ... maka ...yangu"

    "nini?"

    "rudia tena buana kaka sheny"

    Nimshika shika paja zake... Aisee mtoto alijaaliwa mapaja sii mchezo.. "kaka sheby?"

    "sema?"

    "videole vyako vina nini?"

    "havina kitu dija"

    "sasa mbona huvitumiii?"

    Niliishika ile kanga yake na kuivuta kabisa na kubaki uchi wa mnyama

    "kaka sheby"

    "dijaaaa mbona unaita sanaa?"

    "wala siiti sana ila angalia usije ukawa unamenya dafu Alafu kulila huezi"

    "aaaaaah dija hayo ni matusi sasa"

    "wala sio matusi kaka sheby coz mimi hapa nilipo nahitaji maandalizi mazuri toka kwako"

    "kwahio we unaona mi siwezi sio?"

    "kitu kama hicho coz mbona hata sio likivimba na wakati ushanivua nguo"

    "livimbe nini sasa?"

    "si huo muhogo wako"



    Dija aliniuliza maswali mengi ambayo sikuweza kujua majibu yake coz kitu alichokua anakiongea kilikua ni kama kweli ila sio kweli hivyo niliendelea kumshika shika na kumnyonya matiti yake...

    "kaka sheby?"

    "nini dija?"

    "nataka niinyonyonye nanii yako"

    sasa nikiwa najibalaguza kuitoa nanii yangu ili inyonywe niliona kuna watu wanatuchungulia huku nikimsikia zaituni akisema

    "mama? mama? njoo umuone kaka sheby kitu anachofanya huku nyuma"

    "anafanya nini?"

    "yupo na hadija afu sheby amemkumbatia hadija akiwa uchi"

    "weeee zai unasema kweli?"

    "ndio njoo umuone mwanao unaemsemea kua sio rijali"

    "jamani mwanangu kumbe anaweza"

    "umeona sasa kua umezaa kidume?"

    "kweli mwananfu nilijua sio rizki kumbe anaweza jamani?"

    Sasa nikiendelea kutafakari maneno yao kati ya mama na dada yangu zaituni, nilishangaa naitwa na anti mwaju

    ****

    "we sheby? sheby?"

    "naam anti?"

    "huend msikitini saa hizi saa 12:30 jioni hii?"

    "haaaaa kumbe kumekucha afu aseee daaahh ngoja nikatawazie msikitini tu"

    Aiseee kumbe nilikua naota vile tulivyokua tukifanya na dija... ilikua ni njozi tu aiseee duuuu...

    Sasa nilipojicheki kwenye bukta duuu nilikua nimesha jichapia bao.. daahhh ile njozi ni mbaya sana kwangu..

    Niliingia bafuni tena na kuoga ili kutoa ule uchafu nilioutoa baada ya ndoto ile chafu..

    Nilipomaliza kuoga nilitoka na kuvaa kanzu kisha nikatoka zangu kuelekea msikitini... kwani hata kuchukua uzu nitachukulia msikitini. kwani naogopa kwenda huko nyuma ya nyumba ili yasije yakanikuta ya ukweli ukweli..

    Hivyo nilichukua baiskeli yangu kama kawaida kisha nikaelekea masjidi

    BAADA YA SIKU HIO KUPITA

    Na leo ni juma pili mida ya saa 4 asubuhi. Nikiwa tayari nimeshafanya yangu ya asubuhi subuhi kama mazoezi vile na vingine vingi tu.

    Leo juma pili sikua na pakwenda na hata mama leo yupo nyumbani, kwani juma pili hua hafungui dox lake lenye nguo za jinsia zote. Tulikua tunakunywa chai mezani na tulikua tupo kafamilia kote kasoro wafanya kazi tu ila Anti mwaju hua tunakulaga nae meza moja...

    Tulikua tukipiga story za kumtania Anti mwaju kua ujana wake wote hana mtoto hata wa dawa. Ilikua ni utani tu ila yale maneno ni kama yalimchoma kiasi flan na kuanza kububujikwa na machozi, Kila mtu aliomba msamaha kwa maneno alio ongea na hata mama angu pia alimuomba msamaha kwa kumkosea. ila mimi sikusema chochote kuusiana na hilo. nilikua kimyaaa

    Na mama na dada nusura wanajua kua mwanae alifariki pale alipojifunguaga. Hivyo ukiongea nae kuusu mambo ya watoto basi hua ni lazima aangue kilio...

    "afu sheby mwanangu?? vp lile swala la uhamisho wa shule?"

    "aaa mmaaa mi sihami bwana"

    "sheby mwanangu unatutia aibu mwanangu"

    "aibu gani?"

    "shule unayosoma ni ya kimaskini sana na haikufai kabisa mwanangu"

    "mi sihami bwana"

    "ngoja baba ako aje"

    "kwani anarudi lini?"

    "we subiri tuu si kesho ndio anakuja"

    "Amna bwana mi sihami na nshasema ivyo sihami"

    Nilikasirika sana kuskia mambo yao ya kunihamisha shule, na ni watu wawili ndio wanapenda nihamie huko kwenye lishule lao ambalo wanafunzi wake huenda na kila anachokitaka.. Nilitoka zangu nje na kukutana na rafiki yangu jakson. alinipitia nimpeleke shoping

    "Aaa jack niaje mtu wangu?"

    "poa nambie?"

    "daahh nashkuru mungu alhamdulilah tumeamka salama"

    "mbona tulipanga saa 4 kamili afu hukuja asee?"

    "aayaaa sory jack kwani nimekuweka sana?"

    "daa sio sana but unazingua chalii"

    "ok poa am so sory my friends"

    "tatizo lako huna simu sheby"

    "lakini si ungekuja kugonga geti jack?"

    "Eeeee hapo kwenu nije nigonge geti kweli?"

    "kwani kuna nini?"

    "eti kuna nini wakati mjengo wenu kama mjengo wa raisi nije nitolewe baru"

    "aaa waapi bhana huo ni woga wako tuu"

    "ok twenzetu"

    Basi tulipanda kwenye gari ya jackson na kusepa zetu shoping.. Jackson pia yeye anasoma kwenye ile shule ya kitajiri kule anaposoma zaituni, Yaani marafiki zangu wote wanasomea shule hio ya kitajiri ambayo ni ya kihuni sana. coz mwanafunzi anaingia class na simu. au ananyoa kiduku kabisa.

    "sasa jack? leo juma pili kuna dox yeyote ipo wazi kweli?"

    "kuna moja ambayo haifungwagi siku za juma pili"

    "aaaa poa"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Haikuchukua muda mrefu tulifika dukani hapo ambapo kulikua kuna nguo za kila aina, ila halikuti duka la mama angu. coz duka la mama angu ndio duka kubwa na la kwanza katika jiji hili la arusha, Tena karibia madox yote ya hapa mjini huwa wanakuja kufungashia pale kwetu. maana mama angu anauzaga kwa jumla na reja reja, Basi tuliingia ndani ya duka hilo na kuanza kuchagua viwalo.

    "jack?"

    "sema"

    "huko si upande wa wanawake huko?"

    "amna nacheki cheki na boxer huku na pia demu wangu kanigongea nimchukulie skin kama mbili"

    "duuuuuu haya bwana"

    Mi nilibaki kuangalia tu mipamba iliopo hapo, Sijakaa vizuri niliona watoto wakali ambao walikua kule ndani ndani ya nguo zao kule nao walikua wakichagua vyao,

    Nilshangaa mtoto mmoja kaniita kule kule ambako kuna nguo za ndani za kike, yaani hio rumu moja ina nguo za ndani za kike tu. Hua siwazi kitu japo spendagi kabisa ila nilimueshimu tu.

    "mambo mkaka?"

    "poa tu"

    Nilianza kumuona akiniangalia kuanzia chini mpaka juu, huku akirembua. nikajua huyu ndio wale wale wanawake wa mjini, Sijakaa vizuri mara akaanza kunishika shati yangu

    "nini we dada?"

    "plz naomba uniseidie kuchagua nguo"

    "tafadhali sana naomba tueshimiane sawa?"

    "jamani plz mkaka"

    Mtoto alikua anatamani kulia kabisa kisa nimsaidie kumchagulia nguo..

    "ok sawa twende sasa nikakuchagulie"

    "wapi? si hizi hapa"

    "mschiuuuu"

    Nilimsunya afu nikamsukuma uko

    "sheby mbona unamsukuma dada wa watu?"

    "jack uyu dada hana akili kabisa, yaani ananiambia mi nimchagulie chupi"

    "lakini sheby? kwani kuna ubaya gani?"

    "eeee huoni ubaya hapo ee?"

    "sioni mimi, tena kitoto cha watu kikali ile mbaya yani"

    "jack tutagombana sasa hivi... coz nazani unanijua vizuri hua kugombana hatukawii"

    "ok poa basi yaishe... nishamaliza kama vp twenzetu"

    Tuliondoka pale lakini jack alirudi nyuma pale alipoitwa na yule mdada niliemsukuma muda si mrefu.. ilionekana kama walikua wanapeana namba za simu,

    Sikutaka kuwafatilia coz kwangu niliona ni ujinga tu

    Basi jack alikuja kisha tukapanda gari.. tayari kwa kurudi nyumbani

    Tuliondoka zetu hapo dukani tukiwa na furaha yetu binafsi

    "sheby?"

    "sema?"

    "kumbe mtoto alishakupenda asee Afu na wewe unakua na ugumu wa ajabu ajabu ambao hauna hata maana coz hata huyo shehe wenu ana mke na kama hana mke basi atakua na mchumba je? wewe ni mtu gani usiotaka urafiki na wanawake?"

    "jack naomba tueshimiane sana tena sana"

    "ok poa basi yaishe"

    Tulifika mahari mimi nikashuka zangu na kuelekea nyumbani. coz na yeye pia alikua keshafika kwao,

    Ilikua ni mida ya saa tisa hivi nikiwa nyumbani napata chakula. Nilikumbuka kua mida ya saa kumi tutaelekea mpirani... kule maeneo za soeto kule kwenye basketball coz hua napendaga sana kuucheza,

    "sheby una safari gani jioni hii?"

    Zaituni ndio aliniuliza hivyo huku akiwa kama anajiandaa

    "sina but naitaji kwenda mazoezini"

    "mmhh basi kama una pakwenda coz nilitaka unipeleke mahali"

    "we nenda tu mwenyewe"

    Basi nilimaliza kula kisha nikavaa nguo za mazoezini, na kutoka zangu

    Huku nikiwa nimeshika mpira wa basketball Kuelekea soweto uzunguni,

    Nilimpitia jackson ambae ni rafiki yangu wa karibu na pia ni jirani angu.

    Nilimkuta dada ake na jack ambae ni pacha wake aitwae jackline, Nilimuuliza mdada huyo ambae alitoka kumwaga maji nje,

    "samaani sista"

    "bila samaan"

    "Aaaa kwanza sijakusalimia, Mambo zako?"

    "poa mzima wewe?"

    "nmhh mi mzima naaa sijui nimemkuta jack?"

    "ndio yupo ndani"

    "sijui utaweza kuniitia?"

    "mmhuu ingia tu ndani"

    "apana bwana niitie tu"

    "ok poa basi ngoja nimuite"

    Dada alikua ana makusudi duuu masna alikua akinitingishia nyuma utafikiri napendaga kumbe walaa sina hata mpango nao, Nilikua nimetulia hapo nje nikiwa namsubiria jackson mchizi wangu japo ananishaurigi ujinga ila haina noma.......

    "we jackiiiii?"

    "nini wewe unanisumbua?"

    "unaitwa na mwenzio huku"

    "nani uyo?"

    "we si utoke tu? kwani ni mzazi humo ndani?"

    "afu we pumbavu ushaanza kunizoea ee?"

    "nikuzoee we pesa?"

    "ipo siku itakunyoosha tu mwehu wewe"

    "lione vile hebu toka uko unaitwa"

    Walikua wakigombana hawa ndugu tena ni mapacha wa kiume na wakike. na wote ni jack jack....

    Mi nilijua ni mimi na zaituni ndio tunagombanaga nyumbani kwetu kumbe hata hawa duuuu

    "aaaa the don sheby nambie babu?"

    "poa sema?"

    "fresh tu vp? naona upo na basketball?"

    "yes ujui torati nini?"

    "aaaaaa nisijue tena?"

    "ok twenzetu basi"

    "poa ngoja nivae gwanda"

    "fanya fasta si unajua tumesha too late babu?"

    Basi jack hakuchukua muda akatoka kisha tukaelekea mpirani kwa miguu na wala sio kwa gari. Kama kawaida yetu story za hapa na pale haziishi..

    "oyaa mbona ulikua unamkoromea sista wako?"

    "aaaa anazingua sana yule"

    "amna bana mueshim sista wako afu istoshe pacha sasa"

    "tatizo hata yeye hana heshma na mimi"

    "mmhhh poa bana ila najua hata mimi nina bifu na dada yangu ile mbaya"

    "hehehehehehehe kumbe hata nyie? afu dada yako anaonekana korofi lile"

    "weeee ni mkorofi yuuuuleee ooohoooo ni shidaaa"

    "mmhhh mi sipo huko"

    Basi tulifika uwanjani ambapo tulianza mazoezi ya kucheza basketball huku mademu wakiendelea kushangilia huku na kule,

    "mmhhh sheby? mbona mademu wanakushangilia wewe tu?"

    "mmhh mi sijui"

    "mmhh sheby we utakua una nyota ya mademu wewe sio bure"

    "kwanini?"

    "yaani sisi tunafunga tena magoli ya point lakini hatuoni kelele ng'oo ila wewe ukimpokonya mtu mpira tu mademu wote wanakushangilia"

    "acha hizo bana mi sijui ni kwanini?"

    Basi tulikua tunaendelea kucheza mpira wa mikono uitwao BASKETBALL...

    Ilifika mida ya mpira kuisha basi mademu walikua wakinipongeza kwa jinsi nilivyokua nacheza ila sijafunga hata bao moja lakini sifa zote nilikua namwagiwa mimi utafikiri ndio nilikua mfungaji bora....

    Sasa kuangalia huku na kule simuoni jack

    Nilianza kumtafuta muda huo wa kwenda nyumbani... ilikua ni muda wa saa moja kasoro.

    Nilimuona mahali akiwa na demu afu akanikonyeza kua nitangulie tu home coz keshajipatia demu.....

    Basi mademu walinipongeza kila mtu na maneno yake. Lakini mimi ni wambuzi ule ule kua sitakagi utani na mwanamke wa aina yeyote ile

    Sasa nikiwa zangu njiani huku nikidundisha dundisha mpira chini.

    kuna jamaa alikua akinifata nyuma nyuma

    "mambo?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alinisalimia lakini niliishangaa sauti yake afu yeye ni wakiume kabisa

    "poa nambie?"

    "saafi tu"

    Niliendelea na safari yangu huku nikiuchezea mpira

    "oya mkaka mbona kauzu ivyo?"

    "yes kauzu ndio staili yangu"

    "waaaooo hua napenda wakaka wakauzu"

    "samaani sana hio ni sauti yako au unaigiza hapa? maana wewe ni wakiume wewe"

    "bwana mi nishajitoa mapemaa"

    "kivipi yani?"

    "mmmhuuu mi nataka tuongee basi na kama ni swala la pesa usijali"

    "tuongee kuusu nini? au una timu ya basketball tushindane?"

    "waaaaalaaa tuu"

    "ok samaani naomba niwai nyumbani"

    "oyaaaaaa"

    "nini we chaliii?"

    "una bodi zuri"

    "skia we chaliii naomba tueshmiane sawa? laa sivyo utachezea kichapo sasa hivi"

    "aaaaa mtoto hensamu hupaswi kua na mkorofiii"

    "afu we..... kama vile nishakushtukia wewe"

    "kivipi?"

    "usikute we ndio dume jike wewe"

    "mmhhuu nashkuru kwa kulifahamu hilo... sasa vp utaweza kuniudumia?"

    "weee faalaaa nini wewe hebu nitokee hapa"

    Sasa nilipokua naondoka kibabe babe nilikutana na wengine tena kama sita hivi afu walikua na mabody ya kimazoezi vizuri tu.... nikajua leo napigwa mpaka raha yaani leo naivishwa hapa duuu

    Sasa nikaanza kurudi nyuma nyuma huku nikikaa tayari.. ila huyu mmoja wa kwanza akaniambia kua

    "usikimbie hao ni wenzangu na walinituma nianze mimi"

    "kwaio hawa nao ni wanaume feki kama wewe?"

    "ndioooo vp utatupa huduma eee?"

    "samaanini sana jamani naombeni njia"

    Mara mmoja kati ya wale sita akajitokeza na kusema

    "mbona mademu walikua wakikushangilia pale na hukua ukisema chochote zaidi ya kutabasamu tu sasa iweje sisi utukunjie ndita?"

    "sikia broo naomba ujieshim sana"

    "na sisi tunasema hivi sikia broo tumekuona una body ya kutuhudumia na kuna muda ulipokua unaruka tuliona umbo la naniii yako hivyo tumeipenda broo"

    Daaahhh mtoto wa kiume nilikua nashangaa kwa jambo ambalo kwangu ni geni kabisaaaaa......

    Nilianza kutafuta njia ya kukimbilia ili niwakwepe wasije wakanikazia hapa hapa... Sasa walinishtukia kama nataka kukimbia. maana hata kugombana nao siwezi coz wapo kama saba hivi.

    "broo vp tusaule zetu?"

    "sikieni mimi sitofanya ushetani wowote na nyie"

    "dogooo afu unajua we bado dogo sana afu ndio tumeitamani nanii yako iyooo si ujivunie kua kidumee wewe?"

    Duuuuu sikukaa vizuri nilishangaa nimedakwa na watu wawili huku mmoja naona keshaanza kusaula nguo zake... yaani hawa wanataka mimi ndio niwafanye wao

    Sasa nikiangalia mtoto wa kiume nilikua nimesha taitika afu huku mwingine ndio kwanza ananisigelea kinyume nyume eti niduu nae na wakati ni wakiume....

    "skieni washkaji"

    "nini dogo kama ni pesa tutakupa kikubwa utufikishe mzigoni"

    "sikieni basiiiii"

    "tusikie nini wewe mkamue mwana uyooo"

    "Oyaaa mimi ni mwenzenu nipo kama nyie rafki zangu"

    "Eti nini??? yani na wewe pia upo kama sisi? sasa kwanini tusijiunge pamoja upige pesa dogo?"





    Nilijikuta nikiwa na kigugumizi cha hapa na pale kuhusiana na hilo la kwenda kupiga kazi kutokana hali niliokua nayo,

    "amna unajua mimi sipendi kila mtu ajue"

    "sikia dogo afu kwanza unaitwa nani?"

    "naitwa sheby"

    "hebu tupe namba ya simu coz tayari umeshakua mwenzetu wewe"

    "aaa kwa bahati mbaya sina simu kwakweli"

    "ila inatakiwa tudai haki zetu sheby. au unaonaje?"

    "ni kweli ila ni kama nilivyokuambia kua mimi hua sipendi mtu anijue"

    "sasa we wanakuridhishaje?"

    "aaaa ninae mtu wangu spesho ambae namlipa"

    "ila fresh pia kwaio sasa inakuaje? sisi ngoja tukuache au sio?"

    "poa basi tutaendelea kuonana"

    "poa bana sheby"

    Niliachana nao pale maeneo walipokuepo

    UNAJUA MASHOGA WA SIKU HIZI PIA WANAJAZIAGA MWILI, HIVYO NI HATARI KWA WEWE MWANAMKE UNAEJIFANYA UNAPENDA WANAUME WENYE MIILI YA MAZOEZI, NA MASHOGA WAPO WA AINA MBILI KUNA WALE WA KAZI KAMA KUIGIZA HIVI HUA NI LAZIMA UTAMKUTA ANA BODI KUBWA LA MAZOEZI UTAFIKIRI NI DUME LA SHOKA KWELI KUMBE NI SHOGA

    NA KUNA HAWA AMBAO WANAJIUZA WENYEWE, HAWA HUA HAWANAGA MABODI MAKUBWA TENA NDIO KWANZA WANAJIWEKA KIDEMU DEMU.... SASA HAWA WALIOKUJA SASA HIVI MMOJA WAO YULE WA KWANZA NI WA KUJIUZA AFU WALE WENGINE WALIOKUA NA MABODI MAZURI YA MAZOEZI WALE NI SPESHO KWA KAZI ZA FILAMU NA NDIO MAANA WAKANIAMBIA KWANINI NISIUNGANE NAO NIKAPIGA PESA.

    Sasa vile naachana na wale mashoga tu nilikutana na zaituni akiwa na gari yake, na alikua amenifata maana nyumbani hua wanatakaga saa mbili tu niwe nyumbani sasa leo nimepitiliza kutokana na hawa mashoga,

    Zaituni alishuka kwenye gari na kuniuliza

    "wale ni akina nani?"

    "wale ni wachezaji wenzangu"

    "muongo sheby hebu niambie ukweli coz wale wakaka mi nawajua vizuri tu"

    "sasa si ndio nakuambia ni maplayer wenzangu?"

    "hapana sheby hapa hunidanganyi kitu ng'oo coz wale wakaka ni mashoga wale"

    "kwaio kama ni mashoga unatakaje?"

    "sheby mdogo wangu ivi umzima kweli?"

    "zaituni naomba sana tueshmiane"

    "maskini sheby mdogo wangu usikute umeshajiunga kwenye kundi hilo wewe"

    "sasa kwani inakuusu?"

    "sheby ni kweli upo huko?"

    "ndio kwani vp?"

    Nilimuona zai akianza kulia huku akipanda kwenye gari kisha akaondoka kwa hasira......

    Niliendelea kutembea zangu kwa mguu huku nikifanya mazoezi na usiku huo,

    Nilifika nyumbani mida ya saa 2:30 nikamkuta zai keshafika nyumbani, sasa ile naingia tu ndani nilianza kupokelewa na zai huku akiniambia

    "niseme kwa mama?"

    "asa useme nini sasa?"

    "si wewe na rafiki zako"

    "acha unafki"

    Niliingia zangu chumbani kwangu na kuelekea bafuni moja kwa moja nikaenda kuoga... Nilikua nafikiria sana kuusiana na dada zai kama atamuambia mama kwa vile alivyonikuta kule njiani na wale jamaaa, Nilimaliza kuoga nikatoka huku nikijipangusa maji na taulo

    "heeeeeee asa nani kakuambia uingie chumbani kwangu bila hodi?"

    "kwani una kipi ambacho sikijui?"

    "zai? naomba tueshmiane sawa?"

    "tuyaache hayo... ivi sheby? ivi ni kweli una hali hio?"

    "kwani hata nikiwa nayo inakuhusu?"

    "sasa si uniambie"

    "sikuambii sasa"

    Mara dada nusura alikuja kwa spidi kali

    "nyie mnatupigia kelele bwana"

    Aliongea hivyo kisha mimi nikamjibu

    "mmmmnhhh dadaa yani kutoka huku juu hadi huko chini unasikia sauti zetu kweli?"

    "amna si nilikua napita kutoka rumu ile kule"

    "aaaaahhh nikajua ni kutoka huko chini"

    "sasa mlikua mnagombana nini?"

    "si hili li zai hapa"

    "kafanyeje?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "muuulize"

    Nilikua naendelea kujifuta maji mwilini huku nikiwa nimevaa boxer, maana hata mimi mwenyewe saa mingine nawakutaga dada zangu wana taiti tu ila hakuna anaemuwaza mwenzie.. yaani malezi ambayo tumezoeshwa ni mabaya sana... coz naweza kwenda hata kwa dada nusura nikamkuta ana taiti lakini haniambiii toka nivae... bali bado wananichukulia kama mtoto mdogo vile. hivyo hata mimi wamenikuta natoka kuoga na boxer. ila siwawazii kua ni wanawake wala nini bali nawachukua kama dada zangu na wala sina wasiwasi.... ila hua kama yupo uchi kabisa ni lazima anifukuze au asiniruusu kuingia... ila chupi na taiti wananiruusu kuingia coz hata nikiingia hua sinaga tabia ya kumkodolea macho... yaani kifupi nakua kama vile nipo na mwanaume mwenzangu...

    Coz kama ukiwa geto na mchizi wako.. afu akiwa anabadili nguo huoni haja ya kumuangalia. coz alichonacho ndio hicho we ulicho nacho hivyo hata hawa dada zangu ninapokua chumbani kwake hua naona kama vile nipo na mwanaume mwenzangu..... yaani sina lile wazo la kusema kua ngoja nimuangalie dada yangu kipapa chake au mapaja yake... au makalio yake.. yaani sina hata wazo la kumtamani kabisaaaaa....

    Sasa hapa wote wamenikuta mdogo wao nina boxer tu. lakini pia wao hawana hilo wazo la kusema labda tumtupie mdogo wetu macho. yaani hata jinsi tunavyo ongea hua tunaongea utafikiri wote tuna nguo.. kumbe mmoja wetu yupo uchi.

    "haya wewe zaituni ulikua mnapiga kelele za nini?"

    "mdogo wa mgonjwa huyo"

    "mgonjwa??? mgonjwa wa nini?"

    "muulize si huyo hapo"

    "Eti we sheby unaumwa nini kwani?"

    "wala tu mbona siumwi kitu"

    "sasa mbona mnanichanganya nyie?"

    Tulikua kimya wote huku dada etu akiwa kakasirika ile mbaya, Maana hakuna anaetaka kusema

    "we zai hebu niambie sheby ana nini?"

    "mdogo wako mgonjwa huyo"

    "sasa ni mgonjwa anaumwa nini?"

    "nilimkuta leo njiani kasimama na wakina bakari shoga"

    "heeeeee sasa kusimama nao tu ndio kosa?"

    "we mteteee tu ila dogo lako sio rizki hilo"

    "heeee we zai maneno gani hayo unaongea mbele yangu na kwa mdogo wako?"

    "si tunamuambia ukweli"

    "afu mbwa toka apa fala wewe"

    Alimpiga kibao cha mgongo na kumtoa nje kisha akanirudia mimi.,..

    "Ehee we sheby anachokisema zai ni kweli?"

    "mmhhhh? hhhmm? hhhmmm? mmmmhh?"

    "mmmnhhhhh nini hebu niambie nijue ili nikamuambie mama tukushuhulikie sheby"

    "lakini dada?"

    "sitaki kusikia lakini. bali niambie ni kweli una hali hio?"

    "mmhhh waaapiii zai muongo tuuu"

    "ila licha ya hivyo hata mimi nilishakutilia mashaka maana hupendi wanawake kabisa wewe"

    "aaaaa sasa dada na wewe wataka uninyase nyase sio? sasa kama wewe na zai hali moja mi ndugu yangu ni nani sasa?"

    "basi mdogo wangu.. mi mbona sikunyasi nyasi?"

    "aaaa mmezidi kuniandama sana"

    "pole basi.. au nisamee mimi basi sawa? haya vaa nguo basi"

    Dada nusura nae alitoka zake huku akiwa na wasiwasi na mimi sana. ila mimi nilikua zangu Cool tu sina swaga na mtu. na huo uchafu wao wanaonibambikia mi siujui hata kidogo.

    BAADA YA SIKU HIO KUPITA

    Sasa leo ni juma tatu nikiwa najiandaa kwenda shule. nilioga kwanza kama kawaida yangu kisha nikavaa Uniform za shule.. huku nikiitwa na mfanya kazi kua chai tayari. Hua chai yangu inakuaga nzito kuliko zote....

    Ghafla zai alikuja na kuanza kunywa chai pale meza moja na mimi..

    "mambo?"

    Alinisalimia kama kawaida

    "poa"

    "mbona kuitikia tu mpaka ujishauuueee?"

    "kwani ni mdomo wako lakini?"

    "lione vile... na nitamuambia mama tu"

    "mwambie kwani inahuuu?"

    "sawaaa"

    Yaani mimi na zai tulikua hatupatanagi na sijui ni kwanini. maana tunaelewana dakika mbili na muda huo huo tunagombana tena... Zai aliondoka na kuelekea chumbani kwa mama.

    Nikapiga zangu chai nzitoooo

    Baada ya hapo nilichukua begi langu huku nikiwa na furaha binafsi kwa moyo wangu....

    Sasa nikiwa napiga hatua ya kutoka nje ya geti nilishtuka kwa kusikia kelele za zaituni huko ndani.. zikiniita mimi

    "shebiiiiiiii? we shebiiiii?"

    "nini bwana mi nitachelewa school bus"

    "mama ukuuuu"

    "sasa kama ananiita kwanini asingeniambia toka saa hio bwana nyie?"

    "bwana shebiiiiii mama kaanguka ukooo"

    "kaanguka??? mungu wangu eee we zai utakua umemfanya nini mama?"

    "mi sijui"

    "muite dada nusura huko kwake"

    Nilikimbizana na ngazi kuelekea chumbani kwa mama na kumkuta yupo chini hajiwezi kabisa

    "mamiii? mamii ni nini kwani?"

    "we sheby mamii kafanya nini?"

    Aliniuliza dada nusura huku akianza kulia

    "sasa unalia nini dada hebu kageuze gari vizuri... afu we zai njoo tumbebe basii"

    "ah ah wewe zai kageuze gari vizuri wacha nimbebe na sheby fanya haraka"

    Tulianza kua vichaa ndani ya muda mfupi huku nikiwa sina akili hata moja... Nilitupa begi la shule kisha tukaanza kumbeba mama etu..

    HOSPITALINI

    Tulikua tupo nje ya mlango wa wodi ambayo anafanyiwa matibabu. Siku hii ya leo wote mimi na zai hatukwenda shule kabisa.... tena zai alikua analia huku akiniangalia

    "we sheby mama kafanyaje?"

    "mi sijui ila alikua na zai ndani kule"

    "we zai mama kafanyeje?"

    "nilinaniiii?"

    "ulinaniii? ulinanii nini sasa?"

    Mara ghafla dokta kaja, tukaamka wote kwenye kiti na kumfata dokta

    "dokta vp huko mamaa yupo sawa kweli?"

    "cha kwanza naombeni niseme kua tumshukuru mungu kwa wema wake"

    "doktaaaa hebu tuambie mamiii wetu anapumua au?"

    "kijana kua mpole... ila kabla sijaeleza hali yake. kuna jambo kaniambia niwafikishie ninyi watoto wawili"

    Tuliposikia tu hivyo nilimuona dada nusura akianza kutokwa na machozi

    "dokta hebu niambie mamii wangu yupo katka hali gani?"

    "kijana kua mpole... afu kaniambia nikupime wewe"

    "afu we dokta falaas ninj wewe? yaani mi nakuuliza mambo ya mama angu afu unaniletea swaga za kupima hapa"

    Nilijikuta nimekua mkorofi ghafla na kuishika lile likoti lake la kidokta na kulikata vifungo vyake...

    "we mtoto mbona mkorofi wewe?"

    "sema mama angu ana hali gani?"

    "si uende ukamuangalie yupo mzima tuuuu.... yaani hii mitoto mingine sijui ipojeee?"

    Niliingia ndani huku nikilengwa na machozi ya mbali

    "mamiii shida ni nini mamiii?"

    "mwanangu sheby"

    Nilienda na kumkumbatia mama angu huku machozi yakimtoka kwa uchungu...

    "mama hizo presha zilianza lini?"

    "wala sio presha mwanangu... ila kuna kitu kaniambia dada yako zai"

    Nilimuangalia zai kwa hasira hizo duu

    "kwani kakuambia nini mamaa?"

    "jamani mwanangu? ujue nakutegemea sana mwanangu"

    "kwani kuna shida gani mama mbona mi nipo sawa tuuuu"

    Mama alikua akilia kwa uchungu huku kama akinionea huruma....

    "eti ni kweli una tatizo hilo mwanangu?"

    "lipi hilo?"

    "dada yako kuna jambo kaniambia kua una urafiki na wakina bakari.. na ndicho kilicho nidondosha na kupoteza fahamu maana mwanangu nakutegemea wewe"

    Nilisubiri mama amalize maongezi yake huku akilia

    "mwanangu? jua nami nahitaji mjukuu kutoka kwako mwanangu, vp eti ni kweli?"

    Kwanza kabla sijamjibu niliamka moja kwa moja na kwenda kumkusanya zai hata kama ni dada yangu.....

    Nilimkusanya na kumgongeza ukutani huku nikimpa mavibao ya maana kwa umbea wake

    "we fala unataka uniulie mama angu kwa umbea wako sio? we fala si nakuuliza wewe?"

    "bwana sheby niachie bwana iiiiiiiiiiiii iiiiiiiiiii uuuuuuiiiiiiiii"

    Zai alianza kulia lakini nilimua wala simuachiii hata kidogo Ani nilikua nampa adabu nzuri kutokana na umbea wake.

    Sasa mama alianza kupiga kelele kwa kuniita

    "sheby muache dada yako sheby?"

    Dada nusura nae alianza kutetea mpaka akashindwa kutuamulia...

    "jamani nusura waamulie wadogo zako"

    "we shebiiiiii? we sheby muache mwenzako jamani"

    Nilikua mtoto wa kiume sisikii la muazini wala la mnadi swala....

    "sheby mdogo wangu muache mwenzako utamuumizaaaa"

    "jamani hawa watotoo"

    "weeeeeee sadikiiiii muache mwenzio?"

    Heeeeee wote tulishtuka kwa kusikia hilo jina la sadiki... Hata kumuadhibu zai niliacha na kumuangalia dada nusura kwa hilo jina alioliita

    Hata mama mwenyewe alishangaa kusikia hilo jina... na hakutaka kulimezea mate kabisa.....

    Mama alimuuluza dada nusura ambae ndio alitaamka hilo jina la sadiki

    "we nusura? huyo sadiki ni nani?"

    CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kila mtu alistuka kwa kusikia hilo jina, kwasababu humo ndani hakukua na dokta yeyote wa kiume yani tulikua ni sisi tu katika hio wodi aliolazwa mama angu

    Dada nusura alianza kujing'ata ng'ata huku akishika kichwa kuashiria sijui ni kwanini aliropoka hilo neno.

    "nusura si nakuuliza huyo sadiki humu ndani ni nani?"

    "oohhhh mama nisamee coz nilikua nafikiri ni sadiki na judi"

    "sadili yupi huyo na judi?"

    "si wale watoto wa shangazi sandra"

    "sasa mbona umewataja hapa?"

    "hapana ila kuna siku pia miliwakuta wakipigana kama hivi na mimi ndio niliowaamulia, hivyo niliita kama hivi nilivyoita sasa hivi"

    "mmhhh ulinishtua wewe haaaa"

    Basi kesi iliishia pale pale na hata mama alipona kwa kusikia lile jina,

    Basi Tulipewa ruksa ya kurudi nyumbani, kwani mama alipata mshtuko tu wa ghafla hivyo hakukua na sababu yeyote ya kukaa hospitalini.

    Lakini nilianza kua na wasiwasi lutokana na lile jina... coz naisi kama vile dada nusura alinilenga mimi. Japo kweli shangazi sandara ana mtoto wa kiume anaeitwa sadiki. Ila huenda kakosea kweli maana kama ni kweli mimi naitwa sadiki basi sitokua mtoto wa hii familia tena...

    UNAJUA NI KWANINI SITOKUA MMOJA KATI YA HII FAMILIA?????

    BASI WE TWENDE SAWA JUU YA STORY HII NZURI ILIOTUNGWA NA MIMI MWENYEWE #Sharbiny_Rashidy_a_k_a_MoonBoy

    UKIIKOSA HII STORY WE KAFE TU... MAANA NAJUA WATUNGAJI NI WENGI ILA STORY NZURY NI CHACHE HIVYO WAACHENI WAIGEEEEEE

    TWENDE KAZIIIIIIII NA STORIIIIIII

    Tulifika nyumbani huku tukiwa wote tuna wasiwasi juu ya mama etu.

    Siku hio ilikua ni siku ya juma tatu ambapo ilikua ni siku ya kwenda shule ila tulisitisha kwenda kwasababu ya mshtuko uliompata mama etu.. na hata hapo tulipo bado tuna yunifomu za shule, Ila wazo langu lilikua ni kuenda shule hata kama ilikua ni saa 6 mchana...

    "sheby mwanangu? leo usiende shule mwanangu, si unaona hali ya mama yako sio nzuri?"

    "mama? lakini zai na nusura si wapo"

    "ok sawa wapo.. je? wewe na wao nani mwanaume?"

    "ok nimekuelewa mamii ila basi ngoja nikatoe ruksa"

    "wahi mara moja basi"

    Nilitoka hapo na kuchukua BHUGAT ( gari ) ya dada zai na kuwahi shule kutoa taarifa kua leo nina tatizo

    Ilinichukua nusu saa tu hadi kufika hapo kisha nikaingia kwa mbwembwe za kawaida tu. Niliingia mpaka ofisini kwa mwalimu mkuu na kuongea nae

    "Assalam aleykhu mwalimu?"

    "waaleykh msalam vp mbona hupo kidarasa darasa leo?"

    "ni kweli mwalimu kwani mama yangu alipata mshtuko wa ghafla asubuhi hii wakati ndio nilikua nakuja shule.. hivyo hicho ndicho kilichonikwamisha mwalim"

    "oooo pole sana kijana naaaa vp mumeshampeleka hospitali?"

    "ndio tumeshampeleka na amepata nafuu kidogo"

    "ok sasa we nenda muangalie mama hali yake na kama atakua salama basi kesho njoo shuleni sawa? na kama hali itaendelea kua mbaya utaendelea kua nae karibu hadi atakapo pata nafuuu"

    "aaaa ni kweli ila sitoweza kukaa zaidi ya siku mbili but kesho tu nakuja shule"

    "sawa ila usimuache mama peke yake"

    "sawa na nashkuru sana mwalimu"

    "usijali rashidy"

    Sasa ile kutoka tu nje nilikutana na shakira uso kwa uso.

    "nina maongezi na wewe"

    Aliniambia huku akiingia ofisini kwa kuomba ruksa ya kuondoka na mimi kwa dakika 5 tu... maana shule yetu huezi kuongea mwanafunzi mwenzio tofauti na mambo shule. hivyo kuomba kwake ruksa ni kwamba ana maongezi tofauti na shule.

    Basi nikawa namsubiri aje tuongee hayo maongezi yake....

    "mmhh vp?"

    "afu salam gan hio tunapeana?"

    "we wataka salam gani?"

    "nisalimie kiislam bana"

    "ok hio mi hainiusu kikubwa tuingie ndani ya gari tuongee"

    "sikia shakira"

    "hakuna cha sikia we ingia kwenye gari"

    Nilipanda kwenye gari huku nikifikiri ni maongezi gani hayo.

    Niliendesha gari kwa spidi na kulisimamisha mahari,

    "sasa unatafuta nini huko?"

    Nilimuuliza shakira. maana alikua anafunua funua siti za gari na sijui alikua anatafuta nini.

    "aaaahhh bwana unavurugha siti we shakira"

    "ivi sheby unakijua ninachokitafuta humu ndani ya gari lako?"

    "sijui"

    "basi we tulia na nisipoiona utailipia kwa kuninyonya denda"

    "ati nini?? we mpuuzi nini wewe?"

    "haaaaa sheby? yani mi ni mpuuzi?"

    "tena zaidi ya sana"

    "kwanini lakini unitukane?"

    "unaropoka tu ujinga bila kufikiria kitu"

    "we subiri niendelee kukitafuta yaani uombe niipate tu ndio utapona"

    "sikia wewe? kama ni simu naomba twende dukani hata sasa hivi kuliko kuchangua hizo siti sio vizuri"

    "sheby jamani? kuna kitu nilikisahau juzi usiku"

    "ulisahau nini?"

    "nilisahau chupi yangu?"

    "Eeeeheeeeee pumbavu sana kumbe ni wewe ndio uliacha mchupi wako kwenye gari?"

    "sasa unafoka nini?"

    "eti sasa unafoka nini?... na wakati mimi niliisiwa vibaya"

    "umeisiwa nini?"

    "si nimeambiwa nimesex humu kwenye gari"

    "kwani ni vibaya kusex humu ndani?"

    "pumbavu sana wewe"

    "Eeeeee baba naomba uache kunitukana.. afu kwa taarifa yako nahamishwa shule babu"

    "mi hainiusu hio ila niambie kwanini uliacha chupi humu ndani?"

    "sheby buana mi hua siwezagi kulala na chupi mwenzio"

    "sasa kwanini usingeiweka kwenye kibegi?"

    "nisameee ila kwani umeiweka wapi?"

    "weeee mwehu nini wewe yaani nikuhifadhie chupi mimi?"

    "kwani ni vibaya?"

    "mschiiuuuuuu"

    Nilisunya huku nikiwa na hasira nyingi mno kwani mtoto wa kike aliniboa sana...

    "pole basi kama nimekuuzi... ila swala langu lipo pale pale"

    "swala gani?"

    "nilisema nikiipata utakua umepona ila nikiikosa utailipia kwa kuninyonya denda"

    "afu we pumbavu staki mazoea shuka kwenye gari chapu"

    Nilishangas mtoto akianza kutoa sauti lainiiii ile dauti ya chumbani kabisaaaa ile lainiiiiiii

    "shebiiii mtoto wa kiume!!! unaonekana mtoto umejaaliwa.. afu unanifukuza kwenye gari yako kweli?? sawa haina shida ila kaa ukijua sheby I LOVE YOU..... nakupenda sana sheby, na nipo tayari kukupa mwili wangu muda wowote uutakao. sheby? njoo basi unilipe chupi yangu"





    Nilianza kutetemeka mtoto wa kiume huku mtoto akianza kunisogerea na kufunua kifua chake.

    "mh mh sikia kama ni hio chupi yako twende dukani ukachukue hata box zima kuliko nifanye dhambi ya ufala kama huu"

    "wala sina shida ya hilo box lako kwani chupi yenyewe ni ya elfu mbili tu hivyo lengo ni kukupata wewe tu"

    "sitaki sasa"

    "sheby mbona kama sio mtoto wa kiume vile?"

    "shakira nakuomba ushuke kwenye gari haraka sana"

    "sheby? ivi upo sirias kweli?"

    "shukaaaaaa tena fasta"

    Nilikua nimekasirika kweli na sikua nataka utani na mwanamke.

    Aliposhuka niliitoa gari mbio hadi nyumbani kwetu

    Nikaingia ndani kwa hasira huku nikiwapita akina zai sebuleni... walishangaaa kuona napita spidi hadi chumbani kwangu..

    Ghafla mama alikuja huku wakina zai wakiwa nyuma kwa kufata mama

    "nini shida mwanangu?"

    "wala tu hakuna shida mamaa"

    "sasa mbona umeingia kwa hasira hivyo?"

    "wala tu sina tatizo"

    Mara zai kadakia juu kwa juuu

    "najua tu ni kwanini?"

    "we nawe tulia.. ushaanza kumchokoza kaka ako"

    "mmhh sasa asiambiwe?"

    "kimyaaa"

    "tatizo unamdekezaaa"

    "zai hunisikii? si nimekuambia kimya?"

    Baada ya hapo waliondoka zao na kuniacha chumbani kwangu....

    baada ya kama nusu saa hivi mama aliniita sebureni

    "sheby?"

    "naam?"

    "njooo"

    Nilifika mara moja coz si unajua mimi ndio kiziwanda afu ndio mtoto pekeee wa kiume katika hii familia hivyo heshma kwangu ilikua ni sehemu ya maisha yangu

    "ndio mama?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "sasa mwanangu? nakuomba uende ofisini mara moja"

    "mamaa lakini huko kwenye duka lako la nguo si ungemuambia zai aende"

    "ndio huko keshaenda zai ila mi nasemea kule head office"

    "mmhhh lakini kule mi nitaweza kusimamia kweli? maana nakumbuka sijawahi kwenda hata siku moja ila nakumbuka ulinionyesha tu"

    "sasa nani ataweza?, na vyote ni uridhi wako mwanangu..... we nenda afu mbona nilishawahi kukupeleka au sio wewe?"

    "mmhh sio mimi ila sawa nitaenda kujaribu maana napajua kidogo"

    "tatizo umezidi ubize mwanangu yani mpaka ofisi zako huzijui??? Afu sio kujaribu nenda kafanye kazi... maana ndio sehemu zako zote utakazo zizuia hivyo wapaswa kujua mapemaaaa"

    "sawa mamiii nitaenda... ila nitaenda na baiskeli"

    "hapana chukua gari yangu hio hapo nje au kachague gari yeyote kule uwani kuliko uende na baskeli"

    "mamiii lakini si nimependa mwenyewe?"

    "mmhhh sawa mwanangu ila nachukia kuigiza kama maskini mwanangu"

    "wala tu mamiii"

    "ok kuna zile karatasi utakwenda nazo ili ukazitie saini maana ilikua nifanye leo lakini ndio kama hivi hali imekua mbaya"

    "sawa niandalie tu ili niondoke sasa hivi"

    "ok sawa mwanangu"

    Basi nilipewa hizo dokoment fulani na kuziweka katika bahasha kisha nikaitoa baiskeli yangu na kuanza kuiosha kwanza.... Mara alitokea dija

    "kaka naomba nikusaidie kuosha"

    "wala tu usijali kwani naiparua parua vumbi tu"

    "sawa"

    Nilimaliza kuiosha BMX yangu kisha nikaianza safari ya kuelekea ofisini kwetu

    Nilikua natembea taratiibu tu huku nikiwa nimeshika dokoment za ofice katika bahasha. Na huko ninapoenda hakuna mfanya kazi yeyote yule anaenijua. labda meneja wetu ndio ananifahamu ila sio sana coz aliniona muda mrefu sana. na ilikua ni nje na kampuni....

    Huko ninapokwenda ni HEAD OFFICE ( ofisi kuu ) Yaani hio ndio ofisi yetu kubwa kwa makampuni yaliopo tanzania. coz tuna makampuni mengi mpaka wazee wenyewe wanayasahau yalipi matawi hayo.... Coz kwa hapa tanzania tuna kampuni zisizopungua 10 za transpot.. na viwanda kama 6 hivi na sheli zisizopungua 4... na vyote hivyo oda zao zinatoka head office hivyo ofisi hio ni kubwa kuliko hivyo unavyofikiria... ni kama ulishawahi kuingia kwenye ofisi za T.R.A jinsi vitengo vilivyokua vingi humo ndani. coz ni ofisi yenye roshen ( gholofa ) 3

    Nilikua ndio nakaribia ofisini hapo kwa kuendesha baiskeli aina ya BMX

    Nilifika ofisini hapo nikakuta wafanyakazi wakiendelea kuchakalika na kazi. Afu kulikua kuna watoto duuuuuuuu kweli dingi aliajili mademu tu ila sio wafanya kazi. maana naona mademu tu ndio wanapishana...... Afu cha kushangaza askari wa geti ni demu kavaa gwanda tu..

    "we mtoto unaenda wapi uko?"

    "shkamoo afande?"

    Niliogopa kwa kusikia hilo lisauti la kike afu linene hilo duuu... Sasa nikaona ngoja nijifanye nimekuja kuaply ( kuomba kazi) kazi

    "sema shida yako kwanza"

    "afande? mimi juzi nilikuja kutafta kazi sasa boss aliniambia leo nije na vyeti na CV zangu"

    "we mtoto muongo sana wewe ulikuja lini hapa?"

    "nilikuja juz ijumaa ila alionifungulia alikua sio wewe"

    "heeee mi mbona mchana nipo kila siku?"

    "mmmh labda siku hio ulienda chooni"

    "pumbavu wewe unanituka mimi?"

    "nisamee afande"

    "nikusamee nini? toka nje?"

    "jamani afande plz nina shida na kazi coz mama yangu anaumwa na baba yangu kasingiziwa kesi na kaka yangu amekufa juzi na dada yangu anajiuza tu na kuvuta bangi hivyo mimi ndio tegemezi la familia afande.. plz niruusu tu mamiii wangu"

    Afande akaangalia huko na huko afu akanyoosha mkono na huku kwangu huku akisema kwa utaratiiibu

    "we dogo una shing ngapi apo?"

    Mmhhh nilishangaa kuona geti lenyewe linalipiwa kwa yule mtu mwenye shida ya private...

    Sasa nikitaka kutoa pesa walet yangu ilikua imevimba pesa tupu hivyo akiiona hio walet ataona kua namuinjoi kutafuta kazi... labda huenda mimi ni mtu fulani ndani ya kampuni hiii...

    "kwani unataka shing ngapi afande?"

    "kaki tu inatosha dogo..fanya fasta"

    "sasa afande? utanidai bac nikitoka coz hapa nina efu kumi tu"

    "dogo unanizoea?"

    "basi afande nakupa mama"

    Nilijisachi sana ilimladi tu nisiitoe walet, maana walet yangu ilikua hata kubana haibani ng'ooo kwa wingi wa pesa.... Nilibahatisha elfu kumi kwenye mfuko wa shati hivyo nikampa ile elfu kumi..

    "nipe basi chenchi afande?"

    "chenchi ya nini?? hebu nenda uko"

    "afande sijala eti mchana"

    "sasa inaniusu mimi? au nikutoe nini?"

    "aaah ah basi chukua tu"

    Nilipita vizuri getini japo ni kwa mbinde...

    Nilipita moja kwa moja hadi kwa secretary wa kampuni hii. aisee ni mzuri huyo duuu

    "za saa iz dada?"

    Yaani kwanza aliniangalia kuanzia chini mpaka juuu. coz nilikua nimevaa kawaida tu wala sijavaa suti wala kulipuka... bali nilivaa mbano wangu na tishet kali afu nikatingishia na kibarakashee kwa juu..

    "salama nikuseidie nini?!

    "naomba nimuone meneja muajiri tafadhali"

    "meneja??? una apointment nae?"

    "mh mh hapana sina"

    "ok kaa pale nimuulize"

    Nikakaa mtoto wa kiume huku nikiona visketi tu vikijipitisha tu mbele yangu

    Mara kuna mtoto mkali katoka kwenye kitengo chake na kunifata mimi

    "mambo?"

    "safi tu shkamoo?"

    "heee unamuamkia nani sasa?"

    "si wewe"

    "weeeeeee mi bado mschana wewe"

    "sasa mbona umejifunga manguo hadi usoni?"

    Nilimzingua but hivyo ndivyo ninavyotaka mimi. watu wavae kiheshima

    "weee ofisini kwetu hua tumeambiwa tukivaa kimini unafkuzwa kazi"

    "kwaio kumbe umevaa kwa ajili ya kazi tu?"

    "ndio"

    "mmhhh haya"

    "vp umeleta oda nini?"

    "kwani vp?"

    "ah ah naona umeshika madocoment apo"

    "wala tu nimekuja kuomba kazi"

    "koho koho ukoho ukoho koho oooohhh duuu umesemaje vile?"

    "nimekuja kuomba kazi humu kwenu"

    Akamgeukua secretary na kumuambia kua

    "sesi? unamsikia uyu mtoto?"

    "kanasemaje ako?"

    "eti kamekuja kuomba kazi?"

    "heeeeeee hako kataweza kazi za humu kweli hako katoto"

    "nashangaaa.... afu we dogo humu kwenye kampuni hii hawaajiri watoto wadogo kama wewe"

    "lakini nina miaka 20 jamani"

    "heeeeee kumbe bado toto"

    Mara secretary akasema kua

    "we dogo? umeishia langapi?"

    "mhhh darasa la saba"

    "puuuuhahahahahahahahaha sasa lasaba nani atakuajiri?"

    "jamini lakini hapa nina CV na cheti cha kumaliza darasa la saba"

    "we unatupotezea tu muda hapa.. we nenda kaendelee kusoma uko"

    Sasa sijakaa vizuri mara wakatoka wafanyakazi wote. maana ilikua ni muda wa kwenda kula lanchi

    "heee we sesi haka katoto ni ka nani?"

    Sasa wale waliokua wakitoka ndioa wakawa wanasemezana

    "afu ni kahensamu"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "we dogo mambo?"

    "poa shkamoo?"

    "heeeeee anamuamkia nani sasa?"

    "mwenzangu hata mi nashangaa"

    "kana heshma eee?"

    "sanaaa"

    Mara meneja katoka huku kakunja sura hio duuu

    "sesiiiiii?"

    "ndio boss?"

    "ulisema kuna mgeni wangu?"

    "ndio ni huyo hapo"

    "huyu mtoto huyu ndio ananiita kwa mkwara wote huo?"

    "ndio afu anataka kazi"

    Nikadakia juu kwa juuu huku nikisimama

    "ndio nataka kazi bosi"

    "tulia wewe funga domo lako ilooo"

    Nilikaaaa kwa unyongeee huku nikiwasikilizia

    Mara kuna wengine wanne wamekuja kuomba kazi wako na mavyeti yao....

    Walianza kumsalimia meneja huku wakiinama ile kiheshima.

    "shkamooo boss?"

    "marahaba hamjambo?"

    "hatujambo boss?"

    "Enhee shida ni nini?"

    "boss tumekuja kuomba kazi"

    "ivi nyie hapo nje kuna bango limeandikwa kua hapa kuna kazi?"

    "hapana boss ila tumekuja tu kwakua tulisikia kua kuna nafasi"

    Nilijikuta nimedakia juu kwa juu

    "eti bosi kumbe kuna nafasi za kazi?? nipe basi bosi"

    "we mtoto acha mdomo mchafu..... afandeeee? afandee? we afande?"

    "abee bosi?"

    "toa hizi taka taka hapa?"

    "sawa afande"

    Daaahh tulianza kushikwa tanganyika jeki na yule afande wa kike

    "afande utatuumiza bwana"

    "tokeniiiii"

    Nikaona hapana hii sio haki kabisa

    "afande niachie haraka"

    "unasemaje we mtoto?"



    Nilianza kua mjeuri maana najua wakisikia tu kua mimi ndio part of this watachanganyikiwa mno. Sasa tulikua tumeshikwa tanganyika jeki huku suruali yangu ikiwa inajikunja jikunja kwa kushikwa na afande huyo.

    "afande utatuumiza"

    "sasa si mtoke?"

    "lakini hii ni haki yetu kuomba kazi kama jinsi nyinyi mlivyokuja kuomba kazi hapa, hivyo ninachokiomba mimi naomba mtuache"

    "tuwaache mkiwa kama nani?"

    "ok sawa tuitieni meneja muajiri"

    "meneja muajiri au boss mkuuu anaumwa kwaio hayupo"

    "basi tunamsubiri hapa hapa"

    "afu we mtoto wewe ndio kiburi si ndio?"

    "hapana ila ni haki yetu kupata kazi"

    Nikaona ngoja nimtoe chemba huyo meneja ili niangalie kwenye upande wa rushwa

    "boss hebu tuongee kiutu uzima basi"

    "utaongea nini wewe mtoto?"

    "we si uje tu"

    Nilitoka nae yule meneja kwa pembeni kisha nikaanza kuongea nae... huju wale vijana wanne wanao omba kazi nikawa kama tegemezi lao, maana wao walionekana kua waoga mno.

    "sasa boss? hebu tuelewane kwanza kiutu uzima sawa?"

    "hebu sema wacha kuzunguka zungukaa"

    "ok sasa boss vp bwana sisi tunataka kazi ndugu yangu. na kama vp tutaangaliana kwenye upande wa maji ya kunywa au unasemaje?"

    "we nani kakuambia mi nataka rushwa?"

    Alikua akiongea huku akiangalia huku na kule kama kuna watu watamuona kisha akaniambia kua

    "hebu njoo huku coz unaonekana una akili sana we dogo mmhhh?"

    "ndio mzee nina shida na kazi"

    "ok hebu sema sasa"

    "sasa boss? mimi naweza kutoa chochote kile ili nipate kazi"

    "ok sawa kijana ila unaweza kutoa chochote kile?"

    "lakini nafasi zipo boss?"

    "aaa tena zipo nafasi 6 za nguvu"

    "sasa mbona ulikua unatubania?"

    "aaaa si unajua maisha haya dogo langu?"

    "ok kwaio sasa utatuchaji shing ngapi?"

    "kwa nyie toeni mia na hamsini kila mmoja tu"

    "aaaa kaka sasa sisi ndio tunatafuta kazi afu unatupiga pesa yote hio?"

    "ok poa kwakua ni madogo zangu toeni ata laki laki kila mmoja basi"

    "ok atilist hio nitajitaidi hata kuwalipia na hawa ndugu zangu"

    "heeee unawalipia na wale wengine?"

    "ndio, ni ndugu zangu niliwaacha hapo nje"

    Niliitoa walet yangu na kuesabu shilingi laki tatu peee... mpaka mwenyewe alishtuka

    "heeeeee we dogo?? umekuja kuomba kaaaaaziiiii au umekuja kutuinjoi tu?"

    "kwanini boss?"

    "haaaaaa yaani walet imevimba kuliko boss?"

    "we shika hiii laki 4 zako afu utandai laki 1 kwa ajili yangu"

    "aaaa dogoooo pesa si hizo umerudisha kwenye walet? tena walet yenyewe haijastuka hata kidogo kama imetolewa pesa"

    "sikia boss unajua mimi ndio nayaanza maisha hivyo hapa nakwenda kununua kitanda na kupangisha chumba kimoja afu sina hata chombo.. yaani kifupi ndio nayaanza maisha"

    "ok kwaio lini utanimaliza hio laki yangu?"

    "aaaaa kaka tufanye mshahara kaka"

    "ila usiponilioa ni nje"

    "haina shida kaka"

    Basi broo alituchukua na kutuingiza ndani kwa wote. kisha akaanza kutuuliza maswali kabla ya intaviu..

    "haya hebu nione vyeti vyenu"

    Sasa hapo mimi sikua na vyeti bali nilikua na docoment za kusaini tu hivyo mimi nikawa nimewekwa pending kwanza kisha akaniita mimi peke yangu

    "sasa wewe vyeti vyako vipi?"

    "bosi nilisahau kuvibeba nikajua ndio vyenyewe kumbe ni mikaratasi mingine tu"

    "sasa itakuaje?"

    "labda kesho boss?"

    "mh mh apana mi nataka tumalize leo leo"

    "basi bosi nifanye kama umeona vyeti vyangu alafu nitakuongezea kidogo"

    "dogo tafadhali sana kwanza pesa yako hujaimalizia cha pili vyeti huna je nitaelewekaje kwa mkuu wangu endapo atadai vyeti vyako afu nikamuambia sina?"

    "lakini boss?"

    "hakuna cha lakini mi nataka vyeti vyako......Ehee nanyie vp si nimewaambia mkalete barua za wazamini na barua za viongozi wenu wa mtaa na paspoti nne"

    Nikaona sasa hii ni mateso yaliokisiri mno Yaani hongo utoe bado uhangaikie mabarua???? aaa yani hii sio haki kabisa inayoendelea ndani ya kampuni hiii...

    Sasa mimi nikamjibu boss badala ya hawa vijana ambao wapo wavulana wawili na wasichana wawili

    "lakini boss? mbona hatuioni faida ya hongo?"

    "kivipi?"

    "sisi tumetoa hongo ili vingine ufanye wewe, sasa iweje uanze kutupa hizo kazi za kuzunguka kwa watendaji mabalozii sasa basi tupe pesa yetu ili tufatilie hivyo vitu"

    "kwahio hivyo vyeti na paspot utaleta huleti?"

    "kwa upande wangu mimi sileti"

    "basi naomba utoke nje ya ule mlango paleee.. na nyie nataka kesho mulete hivyo vigezo kisha niwafanyie intaviu sawa?"

    Wakamjibu boss kua

    "lakini boss? sisi ni wageni ambao hata mabalozi wetu hatuwajui na hata huyo mzamuni tutamtoa wapi?"

    "okeeee na mimi hapo sina cha kuwaseidia kwani hapo ni sheria ichukue mkondo wake"

    "kwaio boss? kazi tunayo au?"

    "kiukweli hata pesa zenu sizitaki"

    "ok kwai ndio umekataa kutupa kazi sio?"

    "ebu tokeni mbele ya macho yangu na pesa yenu siwapi afu hamnipeleki popote tokeniiiiii"

    tulitoka pale kuelekea pale alipo sesi ambae ndio secretary wa kampuni hiiii.

    "dada samaani naomba simu yako mara moja"

    "heeeee ulinipa pesa ya vocha?"

    "tafadhali sana naomba kwa mara moja tu"

    "sitakiiii heee kwani lazima?"

    "ok shika hii elfu kumi"

    "yes ayo ndio mambo sasa"

    Mara meneja akaja mpaka pale tulipo

    "nyie bado hamjaondoka tuuu?"

    "aiseee ndugu tuondoke zetu tusije zua balaa... twendeni tukajaribu kwenye kampuni nyingine"

    "subiri kwanza niongee na mtu fulani"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tulikua tukiongea sisi tuliokua tuna shida ya kazi, kwani wenzangu walikua wanaogopa sana karibia watetemeke... afu nikicheki kuna watoto wazuri nao wanataka kazi...

    "we kijana? unataka kumpigia nani?"

    "hapana boss bali nataka nimjulishe mama angu kua nimekosa kazi"

    "yaani katika mapumbavu we ni namba moja kweli wewe...hebu nipisheni mimi mschiuuu"

    Nilipewa simu na yule sesi huku akiniangalia jnsi ninavyofanya

    "mmhhh simu yako siwezi kuitumia hebu andika hizi namba mwenyewe"

    Nikampa simu yake kisha nikaanza kumtajia namba moja baada ya nyingine, huku meneja akiangalia tukio zima jibsi linavyofanyika

    "Enhe taja hizo namba zako"

    "ok ni 0714"

    "Enhee?"

    "4194"

    "heeee mbona kama namba ya boss wetu hio?"

    "kwani zimeisha dada?"

    "ok endelea"

    "mwisho ni 87 tu"

    "si nilikuambia kua hii ni namba za boss wetu...we umezitoa wapi?"

    "we piga tuuu shida ni nini?"

    Alikua anasita kupiga Nikampokonya ile simu na kuipiga tena niliweka laudi spika.... huku meneja akiwa anazunguka zunguka tu huku na kule.

    "haloo sesi? ivi mwanangu si kafika huko?"

    "hapana hapa huongei na sesi bali unaongea na kijana sharbiny hapa.... sasa boss? huku kuna vijana wanataka kazi je? kuna nafasi au hakuna?"

    "we unaongelea nini? mbona sikuelewi sheby?"

    "nakuuliza boss huku kuna nafasi au hakuna?"

    "zipo nafasi kama sita hivi ila hazijapata watu bado"

    "sasa hapa kuna vijana wanahitaji kazi je? wapewe kazi ama?"

    "okee mwambie kevin awakague vyeti vyao afu awafanyie intaviu then awape kazi"

    "ok na je kuna rushwa yeyote inatakiwa kupokelewa?"

    "hapana lakini ni kwanini unauliza hivyo sheby?"

    "ok boss asante na natumai tutapata kazi... nakutakia mchana mwema baibai"

    Nilikata simu kisha nikamgeukia meneja.... huku sesi akishangaa kujibiwa vizuri na boss wao

    "lakini mbona umeongea vizuri na boss?"

    "hio haikuusu.... sasa kevin naona umesikia kila kitu afu cha kwanza naomba unipe pesa yangu"

    "pesa sikupi na nitampigia simu boss na kumuambia kua hawa watu hawana vigezo kamilia vya kufanya kazi na sisi"

    "kweli?"

    "afu we kijana sijui umeibia wapi namba ya boss wetu pumbavu wewe"

    "sawa we tukana tu"

    "afandeeee?"

    "beeeeee"

    "njooo piga hawa watu"

    Sasa afande ile kuja tu mara simu ikaita kwa sesi

    "haloo boss?"

    "Eti sesi kuna tatizo gani?"

    "mbona hakuna kitu boss"

    "mumemuona mtoto wangu wa pekee? na ndio bosi wenu huyo maana hana tofauti na mimi wala baba yake"

    "lakini nadhani bado hajafika huyo mtoto wako"

    "tayari mbona keshafika, au mumemdharau?"

    "hapana boss hatuwezi mzarau boss"

    "sasa mbona hamjui?"

    "kwa kwa......kwa ...kwa kwani ni yupi boss?"

    "si huyo nilieongea nae kupitia simu yako"

    "yesu wangu"

    Sesi aliiponya hadi simu na kuidondosha chini huku akiwa kabaki mdomo wazi na kutoa macho

    Kevin akamuuliza sesi

    "sesi vp nani ulikua unaongea nae?"

    "boss"

    "kasemaje kwani?"

    "boss wako?"

    "nani boss wangu?"

    Akanyoosha kidole kuashiria ni mimi

    "kivipi sesi?"

    "ndio mtoto wa boss huyo"

    "whaaat?"



    Kevin na afande walikua wakitetemeka ile mbaya coz hata mimi naweza kufukuza mtu tena bila wasi wasi.

    "boss? chukua pesa yako.. afu naomba unisameee coz ilikua ni utani tu"

    Mara na afande kaja na elfu kumi yangu

    "boss naomba unisamee boss na ile pesa yako hii hapa. nisameee baba maana nategemewa baba"

    Mara na sesi kaja yena karibia apige goti jabisa maaba ndio walinicheka pale mwanzo nilipowaambia mimi ni darasa la saba...

    "boss tafadhali sana unisameee mimi coz nilikua nina shida na pesa kidogo ila sio tabia yangu"

    Waliniomba msamaha woote na kunirudishia pesa zangu nilizowahonga kwa ajili ya kazi. na toka muda huo wanijue sikutoa neno lolote lile. Bali nilimuamuru tu kevin kua

    "kevin?"

    "yess boss?"

    "wacheki vyeti vyao then uwapige picha hapa hapa kisha uwape kazi"

    "sawa boss..... asee njoeni huku jamani"

    Basi wale jamaa walipotoka walinishukuru sana kwa kuwaseidia kwa kiasi kikubwa sana

    "ok sasa msiondoke kwanza coz kuna kikao naitisha ambacho kitawausu hata nyinyi ambao ni wageni"

    "sawa boss"

    Ilipofika mida ya saa tisa hivi niliitisha kikao katika rumu maalum kwa ajili ya vikao

    "kevin?"

    "yes boss?"

    "itisha kikao mara moja afu nataka nione wafanyakazi wote mpaka wa nje"

    "sawa boss?"

    Nilielekea zangu kwenye ofisi yangu na kuendelea kupokea baadhi ya oda zilizokua zikija...

    Mpaka walipokusabywa wote kisha nikaja kuitwa

    "boss tayari wanakusubiria"

    "ok nakuja"

    Niliweka vitu sawa kisha nikaelekea kikaoni kwa maelekezo mapya ya kiofisi

    Nilifika katika rum ya kikao ambapo niliwakuta wafanyakazi wasiopungua 60 "Kaaaa mbona wafanyakazi wengi hivi jamani?"

    Nilijiuliza mwenyewe huku nikikaa kwenye kiti kikuu.

    "za mchana jamani?"

    Nilianza kuwasalimia kwa staili hio kisha wakaitikia kwa wote

    "nzuri boss"

    "ok.. kwanza kabisa nahita kuwajua meneja mwajiri na mkurugenzi wa kampuni hii na mtunza hazina na au kiongozi yeyote aliepewa cheo humu ndani asimame"

    Walisimama wote ndio nikaweza kuwajua kwa majina hadi sura,

    "ok mnaweza kukaa but wewe meneja muajiri? hiii kampuni uliambiwa kua inaajiri watu kwa rushwa?"

    "hapana boss"

    "ila?"

    "aaaa nilipitiwa tu coz nina matatizo hivyo nimeona nijaribu hivyo ili nitatue shida zangu boss"

    "ok we unalipwa pesa ngapi?"

    "mmmm mimi?"

    "sasa naongea na nani?"

    "nalipwa laki 5 boss"

    "Astakafiru lah, yaani laki 5 afu bado unakula rushwa kweli?"

    "boss? nilipitiwa tuuu"

    Mara wafanyakazi wote wakasema kua

    "hapana huyo ndio tabia yake"

    "mi najua ni tabia yake.... ok na wewe afande? hii kampuni ipo spesho kwa kuingiza wafanyakaziiiiiii au ipo spesho kwa kuingiza wateja na wenye shida?"

    "boss ni kwa kuingiza wote wote"

    "ok je wewe ulipokuja kuomba kazi ya ulinzi kuna mtu alikuzuia?"

    "hapana boss"

    "kwanini umenizuia mpaka nikakupa pesa?"

    "nisamee boss"

    "secretary? unalipwa pesa ngapi?"

    "nalipwa laki 3 boss"

    "laki tatu ulishindwa kunipa dakika moja ya kuongea na simu yako eti kisa sikukupa hela ya salio kweli"

    "nisamee boss ni tamaa tu"

    "ok kuna yule dada alinicheka sana muda ule niliposema natafuta kazi ivi ni yupi?"

    "ni mimi boss"

    "unaitwa nani vile?"

    "naitwa ashura"

    "ok ulinicheka pale mapokezi ni kwanini umefanya hivyo?"

    "nisamee boss"

    "sasa sikieni kwa wote..... kuanzia leo hiiii sitaki kusikia wala kuona rushwa aina yeyote humu ndani... Afu humu ndani muna dharau wote sasa sikieni... kuanzia leo sitaki luona unamdharau mgeni wa aina yeyote ile. maana mimi najua nimedharauliwa hapo mpaka basi yani....

    Sasa nasema hivi kampuni hiii kama kulikua na onyo na makalipio ndio ufukuzwe kazi, sasa hivi haipo tena yaani ukionyesha dalili kati ya hizo ni kufukuzwa kazi moja kwa moja yani hakuna bodi ya kumfikiria mtu kwa ujinga wake... tumeelewana?"

    "ndio boss"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "wala musiwe na wasiwasi wa kua nitawafukuza kazi leo bali hilo ni onyo la mwisho.... coz najua wapo ambao mnategemewa na familia zenu hivyo kwa kosa hili nilioliona kwa leo hii? mi naomba nilimezeee tu.... ila jueni kua dharau zenu aziwafikishi mahari coz unaweza ukamdhara mtu aliekuja hapa. afu mwisho wa siku umefukuzwa kazi hapa na ukaenda kuomba kazi kwake..... mi sijui kitakachoendelea ila sidhani kama utapata kazi hapo... hivyo acheni kabisa dharau zenu hizo sio nzuri sawa?"

    "sawa boss"

    "afu we afande? pale getini upo spesho kwa ajili ya kufungulia watu na magari yao, ila hukuambiwa uzuie mtu... kama mtu anatafuta kazi mruusu aje akose mwenyewe ila sio umzuie wewe...naomba hio tabia ife kuanzia leo"

    "sawa boss"

    "secretary na wafanyakazi wote acheni dharau zenu hizo....afu kevin naomba mtu akose kazi kwa vigezo ila sio pesa..afu hivyo vitu vyako unavyowatuma sijui barua ya baloz au mtendaji hio haipogo kwenye kampuni hiii bali ni paspot saizi 3 na barua ya maombi ya kazi tuuu. tena paspot zenyewe unaweza kuwapiga hapa hapa coz kamera ipo pale na ipo kwa ajili ya kazi hio.. sawaa?"

    "sawa boss"

    "ok afu swala lingine? mimi naitwa sharbiny rashidy ila naomba mniite sheby inatosha but hilo la boss silitaki sawa?"

    "sawa boss"

    "nini??? mnarudia tena?"

    "tusamee tu boss coz tunashindwa kukuita hilo jina"

    "ok poa vovote vile nyie niiteni tu"

    "asante boss"

    "ok nadhani kikao kimeisha ila kuna mtu ana swali lolote?"

    "hapana boss?"

    "ok je? kuna kazi nyingi za kufanya humu ndani?"

    Aliinuka meneja na kunijibu kua

    "aaahh ni kweli kazi zipo ila zilisitishwa kwakua kuna sehemu zingine ni lazima boss apitie hivyo kazi kubwa ipo kwako boss"

    "ok sasa nikusanyieni kazi zote niwekeeni pale mezani kwangu kisha leo naomba mfurahie kwa kula nyama hapo nje sawa?"

    "ndioooooooooo"

    "ok swala ni hili kwanza nikusanyieni hizo kazi..... afu vijana wawili wakachukue mbuzi watatu wakuchoma Afu vijana wengine wakachukue vinywaji aina yeyote ile kasoro kilevi.... yaani nikiona pombe hapo nje nazipasua na alieleta ajiandae kwa kuacha kazi"

    "sawa boss asante kwa ofaa"

    Basi kikao kiliisha na wafanyakazi wote walitoka nje ambapo ndani ya geti la kampuni hii kuna uwanja mzuri wa paking za magari hivyo hapo hapo ndipo wanapojipongeza..

    Baada ya kama nusu saa hivi sherehe ilianza na watu walikua wakila nyama kwa wingi... wakati huo mimi nipo afisini naendelea kusaini baadhi ya mikataba na oda mbali mbali za nje ya nchi... Nilikua nipo bize sana tena hata zile kelele zao huko nje zilikua zikiniboa sana tu... nilifunga mlango ili nisizisikie hizo sauti zao. Nilishangaa mlango ukigongwa na sikua nahitaji kuona mtu yeyote pia niliwaambia wasinisumbue

    Nilimruusu aingie ila nilishangaa kumuona sesi ndio alikua akija.

    "sesi?"

    "abee boss?"

    "si nilishawatangazia kua sihitaji usumbufu?"

    "samaani boss hii ni private me & u"

    "private???? private gani?"

    "tukae kwanza basi boss"

    "ok sema, kuna shida yeyote huko nje?"

    "hapana"

    "au vinywaji vimepungua? basi shika pesa kaongeze"

    "No No No vinywaji na nyama vyote vipo"

    "sasa tatizo ni nini?"

    "hapana but naomba kuuliza kitu"

    "kitu gani?"

    "mbona simuoni hata boss wa kike"

    "boss wenu wa kike anaumwa"

    "simaanish maadam sonia"

    "bali unamaanisha nini?"

    "namaanisha wifi yetu"

    "wifi yenu kwa nani?"

    "bosiiiiiii kwani we huna mpenz?"

    "sesi? ebu naomba utoke sawa?"

    "bosiii kwani ni vibaya kuuliza?"

    "afu nani kakuambia unywe pombe? si nimesema pombe ni marufuku???"

    "nimenunua mwenyewe na wala hakuna alieleta"

    "basi kama una maswali zaidi naomba uje kesho kwa maadam sonia coz naisi umelewa sesi"

    Unajua mimi ni kijana ambae sipendi kuamsha hasira mapema kutokana na udhaifu wangu binafsi

    "bosii haya maswali yangu yanakuusu wewe"

    "haya uliza chapu chapu niendelee na kazi"

    "boss? unajua mi ni msichana mdogo tu afu nikikuangalia kama vile tunaendana boss plz kama huna mpnz naomba nizibe pengo hilo"

    "afu we ni mkubwa kwangu nikajua utanishauri cha maana kumbe ndio kwanza unajitongozesha kwangu?"

    "boss? unajua wewe ni hensamu na sio mimi hata wakina ashura wana mpango wa kuja ofisini kwako ilimladi tu watembee na wewe"

    "kumbe hii kampuni ni chafu kiasi hiki?"

    "wala tu kampuni sio chafu ila uchafu umeuleta wewe"

    "kwanini?"

    "wasichana wote humu ndani wameshakutamani kimapenzi na sio kwa pesa zenu"

    "basi njoo kesho"

    "sitaki na ukikataa napiga kelele unanibaka"

    "haaaaaa sesi? ivi unaweza kuniambia kitu kama hicho?"

    Mara akajidondsha chini huku akigala gala mpaka kile kisket chake kikapanda juuuu

    Sasa nikawaza nitantoa kwa janja gani? maana inaonekana keshalewa tayari

    Nikaona ngoja nimdanganye atoke ili nifunge mlango

    "sasa sesi?"

    "abee boss?"

    "nimekubali ila mi siwezi kusex na wewe coz unanuka pombe afu kikwapa kinatema hicho...au kama vp kaoge afu uje tena"

    "boss unasema kweli??"

    "ndio tena wahi sasa hivi uje"

    "bosiiii unasema kweli au unatania?"

    "hata mi mwenyewe nimekupenda ghafla tu yani"

    "ngoja basi nikaoge nije sawa?"

    "sawa"

    Alipotoka tu nikafunga mlango na kurudi mezani kisha nikaendelea na kazi huku nikiwa na mawazo kibao juu ya jambo hili....

    Sasa sijakaa vizuri mara meseji imeingia kwenye simu ya sesi

    "Heeee kaacha simu?"

    Nilijisemea kimoyo moyo huku nikijiuliza kua ngoja nikate hii meseji kisha nimpigie mama ili nimuambie tabia ya wafanyakazi wake... sasa ile meseji ilitumwa na BOSS yaani jina liliotuma hio meseji ilikua limeandikwa BOSS... ila sikua na shauku ya kuisoma kwasababu hainiusu.. lakini kwakua ile simu ya sesi siwezi kuitumia. nilijikuta nimeifungua madala ya kukata. Nilitamani nisiisome ila nilishangazwa kwa kusoma herufi za mwazo zilizoniusu mimi.... Heeee ilibidi nianze kufungua inbox upya na kuanza kufatilia mwanzo wao wa kutumiana meseji mpaka wakafikia hio meseji ya mwisho...... Asee sikuamini macho yangu kwa kusoma hizi meseji jinsi zilivyo na sii mwingine bali alikua ni mama yangu SONIA ndio waliokua wakitumiana meseji na sesi... walianza hivi

    BOSS : "sesi upo wapi saa hii?"

    SESI : "nipo kazini boss"

    BOSS : "una kazi gani hapo?"

    SESI : "wala tu nipo nje leo mwanao katupa ofa ya kula nyama"

    BOSS :"ok na yeye yupo wapi?"

    SESI :"yupo ofisini kwake anaendelea kutia saini baadhi ya mikataba na oda mbali mbali"

    KUMBUKA HIZI NI MESEJI NA SIO KUONGEA KWA SIMU

    BOSS :"ok sasa nataka nikupe kazi maalum kwa ajili yako"

    SESI :"kazi gani boss?"

    BOSS :"naomba ukamtongoze mwanangu kule kule ndani"

    SESI :"what?? hapana siwezi boss"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    BOSS :"kwanini sesi? plz usiniangushe na pia nitakulipa donge nono"

    SESI :"hapana boss coz yule anaonekana ni mdogo kwangu boss"

    BOSS :"wala tu mbona mnalingana tu na pia huenda ukawa umempita mwaka mmoja au miwili tu"

    SESI :"boss mi siwezi kujidhalilisha kwakweli"

    BOSS :"sesi nitakupa milioni 2 kwa kufanya kazi hio tu"

    SESI :yesu wangu boss? sasa akikubali je?"

    BOSS :"akikubali we sex nae tu hapo hapo afu unipe taarifa sawa?"

    SESI :"mmmhh boss mtihani wako mbona mgumu?"

    BOSS :"basi nakuongezea milioni moja"

    SESI :"boss? pesa sio tatizo"

    BOSS :"sesi? unajua wewe ndio mrembo na mwenye umbo la kuvutia hivyo hebu nenda na ujifanye umelewa"

    SESI :"boss mi nitafukuzwa kazi boss"

    BOSS :"akikufukuza mimi nitakuja kukurudisha"

    SESI :"boss? nihakikishie usalama wangu"

    BOSS :"sesi? kazi bado utajua nayo na pesa juuu ila ukishindwa nitakupa laki 5 za kujaribu tu"

    SESI :"ok nipe mwongozo mwanao anapendelea nini?"

    BOSS :"kwakweli mwanangu hana starehe yeyote ile anayoipenda.... na ni mtu anaejieshim sana hivyo ukiona anakataa fanya kama vile unataka kumdhalilisha kama vile anataka kukubaka.... kwani hua hapendi kuebika kwa watu"

    SESI :"sasa kama hapendi starehe yeyote? je? mimi nitawezaje jamani boss?!

    BOSS :"sasa si ndio utumie usichana wako mpaka usex nae kabisaaa"

    SESI :"ok ngoja nikajaribu basi"

    BOSS :"ok nakutakia mafanikio mema"

    Sasa baada ya hapo ndio sesi akaja kwangu na kuanza kuongea na mimi utumbo utumbo wake huo. Sasa BOSS baada ya kuona SESI anachelewa kurudisha majibu kua kafanikiwa au bado? sasa BOSS ndio akatuma hii meseji ambayo hata mimi mwenyewe sikuamini macho yangu kama mama yangu mzazi anaweza kuandika meseji kama hio... Eti aliandika hivi



    Nilijiuliza sana kuusiana hizi meseji kua huyu mama aliandikiwaaa au aliandika mwenyewe? Nilijiuliza sana swala hilo ila sikulipatia jibu. Ila hii meseji ya mwisho.... Eti aliandika hivi

    BOSS :"sesi? vp mbona kimya? au umefanikiwa? na vp kakupiga bao ngapi? naomba nijibu haraka nijue bac"

    Hivyo ndivyo alivyoandika BOSS huyo, ila nilibaki na maswali kua ni kwanini mama angu ananifatilia kuusiana na jinsia yangu? kweli najua huenda ni upendo wa mama kwa mtoto lakini mbona kwa mama angu imezidi sasa???

    Nilikua nazunguka humo ndani nikiwa nimeshika simu ya sesi ambae ndio secretary wa kampuni yetu. Nilikua sina hata hamu ya kazi tena maana nilishavurugwa kiakili kabisaa. Ghafla mlango uligongwa. Nikaiweka ile simu pale pale nilipoikuta mwanzo... kisha nikaenda kufungua mlango Alikua ni sesi ndio karudi kuoga maana hii kampuni au ofisi kuu hua ina mabafu kabisa yaani ni kampuni ya kisasa mno..

    Nilimfungulia mlango lakini nimeshajua kila kitu kuusiana na hilo

    "boss nimerudi, sasa vp tuendelee"

    Nikashangaa kapambua nguo zote akabakiwa na chupi peke yake coz kama ulivyoona mwenyewe kua kaambiwa ni lazima asex na mimi ili apewe milion 3 na BOSS wake huyo.. Nilimuangalia kwa dharau huku nikihesabu vidole vyangu kama vile tasbiii.... ile ambayo ipo kama rozali. sasa kwa sisi waislam tuna jinsi ya kuhesabu pingili za vidole vyetu vya mkono kwa kuyataja majina ya mungu na mitume wake...Sasa nilikua nawaza cha kufanya kwa wakati huo... maana mtoto tayari keshanisogelea mpaka karibu yangu na kuanza kunikumbatia huku chuchu zake zikinichoma, maana si zipo wazi? hivyo nilikua nawaza cha kumuambia huku nikijisemea kimoyo moyo hivi

    "Astakafiru laah, Astakafiru laah, Astakafiru laah, Astakafiru laah, Astakafiru laah, Astakafiru laah, Astakafiru laah"

    Nilitaamka hivyo mara 7 kisha nikapata wazo la kumuambia sesi

    "sesi?"

    "abee boss?"

    "tucheze dili"

    "dili? dili gani tena?"

    "aliokutuma nenda kamuambie hivi nimesimamisha na nimekupiga bao 5 za nguvu tena msistizie kua mwanao ni rijali mzuri sana tena ndio nimempenda kabisaaaa..... nenda kamuambie maneno hayo sawa?"

    Sasa kusikia hivyo akaikimbilia simu yake na kukuta meseji moja imeshasomwa, hivyo ikampelekea kujua kua mimi ndio nilioisoma hiyo meseji...

    "boss? ni kweli nimetumwa na mama ako lakini sio uamuzi wangu"

    Sasa baada ya kuona nimegundua ukweli sasa ndio anaanza kuona aibu na kuficha matiti yake huku akizisogelea nguo zake. Niliangalia tu pembeni ili avae nguo zake kwa amani, Baada ya kumaliza kuvaa nguo alinifata mpaka pale nilipokua nimesimama huku akiangalia chini kwa aibu. maana nimeshajua kua amejidhalilisha kwa mtu ambae tumepishana miaka miwili au mitatu hivi kisa kaahidiwa pesa....

    "boss? naomba unisamee coz najua mimi ni sawa na dada yako kiumri ila kwa maumbo tupo sawa hivyo naomba unisamee kama dada yako boss"

    "ok mimi mbona sina kinyongo na wewe? na kama ni kukusamehe nilishakusamee baada ya kujua umetumwa na boss wako.. ila nimekudharau sana baada ya kujua kua unapenda pesa kuliko utu wako"

    Mtoto alianza kulia baada ya kusikia kua nimemdharau baada ya kunionyesha nyeti zake....

    "wala usilie dada yangu coz naisi ni maisha tu"

    Nilimkumbatia na kumpa moyo kua asijali kwani yote ni maisha tu, Lakini kiukweli sesi aliumbika vibaya mno kiasi kwamba hata nilipomkumbatia nilianza kujiskia vizuri ila nashukuru kua bado hali ya kidini ipo ndani ya moyo wangu hivyo sikua na wazo hilo tena...... Nilimuuliza sesi kua

    "sasa sesi? utamuambiaje aliikutuma?"

    "nitamuambia hivyo ulivyoniambia"

    "ok fanya hivyo sasa hivi.. na nitakupa pesa zaidi ya aliokuahidi yeye"

    "wala sihitaji pesa yako boss but itasema tu kua unaweza"

    "ok anza sasa"

    Sesi aliichukua simu yake na kuanza kumtafuta boss wake kisha akampandia hewani... ilipokelewa fasta fasta ile mbaya kisha nikamuambia aweke laudi spika

    "haloo boss?"

    "Ee sesi vp imekuaje?"

    Kabla hajamjibu nikamuambia sesi kua

    "kua na furaha sasa afu cheka cheka huku ukinisifia vizuri kabisa"

    Kweli sesi alikua yupo kama muigizaji vile..

    "Tehetehtehtehtehtehte boss? mwanao ni shida yaani alivyonifanya sikuamini macho yangu kwakweli"

    "weeeee sesi unasema kweli?"

    "yaani boss kweli hapa umezaa kidume cha nguvu yani huezi amini kaenda raundi 5 za afya mpaka nilienda bafuni kuoga kwanza"

    "jamani sesi sijui nikupe nini? ivi unasema kweliiii au unanidanganya?"

    Sasa sesi nae akaanza kutetemeka baada ya kusikia kama vile boss wake amejua kwa kusema kua anamdanganya au vp?

    Sasa nikamuwahi sesi Kabla hajaingiza uoga kabisa

    "sikia sesi... we kua jasiri wacha kutetemekaaa"

    Sesi aliendelea kujibalaguza kwa kumdanganya boss wake

    "boss mi nikudanganyie nini boss? na wakati hapa nilipo naskilizia maumivu tu"

    "Aaahahahahahahah we sesi kwani ulikua ni bikra?"

    "hapana boss ila nina muda mrefu sijakutana na mwanaume sasa leo ni kama vile kanitoa bikra yani"

    "ok sasa kuanzia leo nataka uwe mkwe wangu sawa?"

    Sesi hapo alishindwa kujibu hilo swali... Hivyo sesi alifunika maiki kisha akaniuliza mimi kua

    "boss? sasa nimuambiaje?"

    "sikia mwambie kua mi simtaki kwanza ni mdogo kiumri afu ana uume mkubwa kuliko saizi ya nanii yangu... sema hivyo"

    Sesi alirudisha simu sikioni kisha akamuambia boss wake hivyo hivyo nilivyomuambia....

    "boss? unajua mtoto wako bado ni mdogo kwangu"

    "wewe shida yako ni nini sesi?"

    "bwana boss mi wazazi wangu watakataa kuolewa na mwanafunzi"

    "ok ila nakuomba kitu kimoja sesi plz plz plz"

    "kitu gani hicho boss?"

    "ila naomba usimuambie mtu"

    "simuambii mtu boss"

    "naomba kama utapata mimba usiitoe plz plz sesi?"

    "bossiii sasa nikipata mimba nitailea vp na haya maisha boss?"

    "usijali sesi.. mimi nitailea badala yake na yeye pia ana uwezo wa kuilea ila sitaki nimkabidhi majukumu hayo"

    "mmhhh sawa boss nitafanya hivyo?"

    "nitafurahi sana sesi? na katika ile pesa niliokuahidi nakuongezea milioni 2 iwe milioni 5 au vp mkwe?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mmhhh boss mara hiii nishakua mkwe tena?"

    "jamani sesi plz naomba uwe mkwe wangu"

    "mmhhtehtehtehtehtehtehtehte sawa nimekubali"

    Nilikasirika kusikia eti kakubali kua mkwe wake

    "sasa naomba uende nyumbani na uje kazini wiki ijayo sawa mkwe?"

    "ahahahahaha Asante boss"

    "ah ah usiniite boss tena, niite mama au mama mkwe"

    "mmhhh sawa mama"

    "ila nakupa wiki hio ili uwe unahudhulia hospitali ili kujua kama umepata sawa?"

    "sawa mama"

    "alafu siku hio ukiniambia una mimba, ujiandae kupokea TOYOTA VX MAYAI kwa ajili yako sawa?"

    "asante mama"

    "ok nashukuru kwa kuifanya kazi yangu vizuri"

    "nashukuru na mimi pia mama mkwe"

    Walikata simu kisha nikaichukua ile simu ya sesi na kuizima kabisa kisha nikamgeukia

    "unaona ujinga ulioufanya sasa?"

    "kwani nimefanya nini boss?"

    "yaani umekubali ukwe kirahisi rahisi tu?"

    "lakini si nimemdanganya tuuu"

    "ok umemdanganya ee? nakuuliza umemdanganya si ndio?"

    "ndio nimemdanganya ila?"

    "ila nini tena?"

    "boss? unajua mama yako hana nia mbaya lakini"

    "kwaio kama hana nia mbaya ndio iweje?"

    "mama ako inaonekana anataka mjukuu"

    "aaaaa bwaaana ee? atajiju mwenyewe"

    "sasa sikia boss?"

    "nini tena?"

    "mama yako anataka mjukuu kutoka kwangu"

    "kwaio kama anataka mi nifanyeje?"

    "nataka unitie mimba ya ukweli boss"

    "Eti nini? we fala nini hebu nisogelee nisije kutia mikofi bure mimi"

    "bosiiiii? kama hutonitia mimba namuambia ukweli mama ako kua hukunifanya chochote"

    "aaaaaaaa sasa utaaribu we vunga kama wiki mbili hivi afu mwambie mimba imetoka"

    "sitaki kumdanganya tena mwanamke mwenzangu"

    "kwaio sasa na mimi sitaki"

    "basi nampigia simu"

    "simu ipi? simu yako si hii hapa ninayo"

    "namba yake naijua kichwani"

    "ivi sesi mbona una gubu sana we mwanamke Eee? au tayari keshakunogesha na hizo ahadi alizokupa?"

    "nimeshasema boss mi nataka mimba kutoka kwako"



    Nilikua kama sielewi chochote kile coz sesi keshanogeshwa na ahadi alizopewa na kujisahau utu wake, Lakini mtoto wa kiume nilikaza hivyo hivyo na wala sikua wakupaparika. Kwani kutia mimba naweza, tena mimi mwenyewe ndio najijua urijali wangu ila sema malezi niliolelewa ni malezi makali mno. yaani nimelelewa katika malezi ya kidini, Hivyo tendo la kufanya mapenzi kwangu naona kama haramu kubwa sana katika maisha yangu, na nilishasemaga kua sitokaa kuja kusex hata siku moja.

    Sasa sesi alikua anaumiza kichwa kwa kupata mimba coz hawezi kubeba mimba tofaut na mimi kwasababu ikija kugundulika kua haikua mimba yangu... heeee sesi atakiona cha mtema kuni, hivyo sesi anaomba sana kwa mungu ili nikubali kumpa mimba ili hizo ahadi alizo ahidiwa azipate,

    "boss? sasa unanifikiriaje?"

    "kuusu nini?"

    Nilikua zangu bize naendelea kusaini mikataba mbali mbali ya kampuni zinazotaka kuweka tawi katika kampuni yetu....

    "nataka mimba"

    "siwezi"

    "kivipi sasa?"

    "sesi? hebu naomba unieshim sawa? mimi ni tofauti na huyo boss wako unaemtegemea sawa? kwahio nakuomba sana niache nifanye kazi"

    Sesi alikua kama haelewi kinacho endelea Yaani alikua hataki kuelewa hicho ninachokiongea.

    "boss? mimi nitampigia simu kua hukufanya na mimi chochote"

    "lakini sesi? mbona mijidume ipo mngi tu? si uende ikakupe mimba huko"

    "nimesema nakutaka wewe. na niko tayari kuipokea mimba hio"

    "ivi sesi? nifanye nini ili unielewe?"

    "uni..uni...uniiingizie hio nanii yako"

    "sasa skia.. mimi nitakupa mara mbili ya hivyo ulivyoahidiwa na huyo boss wako"

    "kivipi?"

    "vyote alivyokuaidi kua ukipata mimba atakupa vx mayai... sasa mimi nakupa vx mbili na milioni 10 juu"

    "acha utani boss?"

    "kweli nakuambia ila ujue tu jinsi ya kumdanganya huyo boss wako"

    "lini sasa utanipa?"

    "hata kesho ukita nakupa"

    USIYARUKE HAYO MAANDISHI HAPO CHINI???????

    NDUGU MSOMAJI WA STORI HIII... MIMI NILISHASEMA KUA SISI NI MATAJIRI WA HASWA...... YAANI KWA HAPA TANZANIA LABDA UTULINGANISHE NA BAKHRESA. LABDA NDIO UTAWEZA KUJUA UTAJIRI WETU ULIVYO. HIVYO USISHANGAE KUONA MIMI MTOTO NAWEZA KUTOA KIASI CHA SHILINGI MILIONI 50 KWA SIKU,.... COZ HATA MTOTO WA BAKHRESA HAWEZI KOSA HATA MILIONI 100 AU NA ZAIDI KWENYE AKAUNTI YAKE HUKO BENKI..... HIVYO MIMI MWENYEWE KILA WIKI NAWEKEWA MILIONI MOJA KWENYE AKAUNTI YANGU NA WAZAZI WANGU.. KWA AJILI YA KUNUNUA VITU VIDOGO VIDOGO AMBAVYO SIO LAZIMA NIWAELEZE WAZAZI... JAPO HATA KAMA NIKIELEZEA WATANUNUA. ILA WAMENIFUNGULIA AKAUNTI YA BENKI KWA AJILI YA VITU VIDOGO VIDOGO NINAVYOVIPENDA MIMI... SASA IMAGEN TOKA NAANZA SHULE YA MSINGI MPAKA LEO SECONDARY SCHOOL JE? NITAKUA NA PESA NGAPI KWENYE AKAUNTI YANGU? NA JE? NITASHINDWA KUNUNUA HATA GARI MBILI ZA KUMTULIZA HUYU BWEGE??? ACHA UTANI WEWE... WACHA NIHONGE MIEEE

    Sasa mtoto alizima fegi kuskia hata kesho naweza kumpa hizo pesa na gari,

    Basi kwa sababu hio mtoto aliniinamia na kunibusu kwenye paji la uso kwa furaha.... Sasa ndio nikajiuliza kua,

    "kumbe alikua anapenda kubeba mimba kisa ni utajiri weeeetuuu sasa nimeeelewa.. na tena naarisha kumpa hivyo vitu"

    Mara kama kanistukia kuna kitu nilikua nawaza kwa muda huo. Hivyo akaniuliza kwa furaha kubwaaa

    "mbona umebadirika ghafla boss?"

    "wala tu ila nimeairisha kukupa hivyo vitu"

    "Whatt?????"

    "Whati unasoma unaandika?"

    "nakusemea kwa mama ako hukusex na mimi"

    "waaaaiiiii kaseme kwani itadhuru nini?? tena itakudhuru wewe mwenyewe"

    "kivipi?"

    "si umeshaanza kumdanganya boss wako kua umesex na mimi"

    "mungu wangu boss nisamee basi na naomba ushauri basi"

    "Ebu niachie mimi...afu muda wa kwenda nyumbani umefika toka nje?!

    "bossiiii"

    "nimesema toka njeeeeee?"

    Sesi alitoka lakini alikua analia kwa kumtolea nje kwa kila kitu....

    Kweli ulifika muda wa kuondoka na kwenda nyumbani. kwani ilikua ni saa 11:15 jioni... sikua na cha kubeba hivyo nilitoka mikono tupu kisha nikafunga ofisi ya boss vizuri na ufu nikatoka na ufunguo.....

    "sesi? we sesi?"

    Sesi nilikua namuita lakini alikua haitiki kabisa...

    "ok ashura?"

    "abeee boss?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "kevin yuko wapi?"

    "yupo toilet boss"

    "ok akija mwambie....aaaa basi huyo anakuja mwenyewe"

    "aaaa boss?"

    "sema kevin?"

    "saaafi tu...na tunashukuru kwa kutuandalia kasherehe ketu"

    "hahahaha kawaida tu...ok sasa? hebu hakikisha watu wote wametoka then funga ofisi sawa?"

    "ok sawa boss. naaa kule ofisini kwako umefunga?"

    "yes nimefunga na ufunguo ninao"

    "ok haina shida boss we kapumzike tu sisi tutafunga"

    "sawa"

    Basi nilichukua BMX yangu na kutoka zangu.... wafanya kazi wananishangaa kwa kuona naendesha baiskeli badala ya gari

    Nilitoka zangu pale huku nikiwa na mawazo juu ya sesi kutaka ujauzito kutoka kwangu. Nilikua naumiza kichwa sana tu huku nikiendesha baiskeli yangu...

    Hua sinaga pakupitia tofauti na msikitini. Hivyo niliingia zangu masjidi na kuanza kusali swala zilizonipita kuanzia mchana. maana swala ya asubuhi niliiswalia nyumbani, japo haiswiii kwa mwanaume kuswalia nyumbani kama mwanamke. Basi nililipia baadhi ya swala kisha nikachukua mswaafu wa hapo masjidi na kuupitia kidogo. Nikicheki muda inaelekea ni saa 12 kasoro. Niliona ngoja niende nyumbani nikaoge kisha nje kuswali swala ya saa 12 jioni.

    Nilitoka pale masjidi taaratibu kabisa huku nikiimba nyimbo zangu za kiislamu...

    Sasa nilipofika nyumbani kwa nje ya geti Nilishangaa kusikia mziki nyumbani kwetu.... Nikagonga geti kisha mlinzi akafungua. kabla sijaingia nikamuuliza mlinzi

    "asee kuna nini uko tena?"

    "kuna sherehe"

    "heeeeee ya nani tena? coz hakuna mtu aliezaliwa mwezi huu ndani kwetu"

    "kwa mimi naona hiii sherehe inakuusu wewe"

    "kivipi?"

    "sijui ila we ingia tu"

    "mh mh apana mi siingiii"

    Nikafungua kadirisha cha mlinzi kile ambacho kipo kwenye geti kwaajili ya mlinzi kumchungulia anaegonga. Sasa nikawa nachungulia ili nione hio sherehe yenyewe ipoje ipoje....

    Mara anti mwaju kaniona. Akaja mpaka nje huku akiwa na yeye kapendeza ile mvaya

    "we sheby mbona upo nje?"

    "ah mi sielewi kupoje huko ndani"

    "jamani mwanangu hio ni sherehe yako"

    "sherehe yangu ya nini sasa?"

    "mi mwenyewe sijui"

    "kivipi lakini ant?"

    "mimi nilishangaa marafiki wa mama yako wamekuja na marafiki wa dada yako zai"

    "sawa sikatai ila nataka nijue sababu ya hii sherehe"

    "kiukweli sijui.... ila we ingia tu"

    "hapana anti mi siingii"

    "hapana sheby nakuomba ingia.... kwasababu utamueibisha mama ako"

    "bora aeibike tu kuliko kufanya sherehe pasipo watu wengine kujua"

    "hapana mimi sikukubalii kabisa, kwasababu hapo walipo wanakusubiria wewe tu"

    "sitaki kwakweli bora waende hao wageni"

    "sheby?"

    "naam anti?"

    "heshma imeshuka si ndio?"

    "kivipi anti?"

    "naona umeshindwa kueshim wito wangu si ndio?"

    "lakini anti?"

    "lakini nini? sasa mi nasema ingia ndani"

    "antiiiii"

    "iiingiaaa ndaaanii?"

    "sawa basi naingia"

    Daaahhh anti alinilazimisha kuingia ndani huku nikiwa sijapenda kushereheka na hio sherehe yao. Niliingia na kushangaa mama angu kanikimbilia huku akisema

    "sapraaaaaizi my baby boy"

    Tukakumbatiana kwa furaha huku nikijichekesha kinafiki nafiki.

    "mamaa?"

    "nini mwanangu?"

    "sherehe ya nini sasa?"

    "mwanangu mi nimefurahi tu kwa leo sasa kwanini nisifurahi na watoto wangu?"

    "lakini mamaa?"

    "hebu acha maswali yako mwanangu njoo utukatie keki hapa"

    Ilibidi tu nimueshim mama angu, hivyo nilifika pale katikati na kuanza kutambulishwa kwa wageni waliokuja

    "jamani mabibi na mabwana, huyu ndio kijana niliowaambia mwanzi, na huyu ndio last born wangu... nampenda sana"

    Watu waligonga cheazi kwa furaha ya kunifahamu mimi. Sasa mama akaniambia nizunguke nimsalimie kila mtu daahhh. Nikaona nikikataa itakua sio heshma nzuri... Hivyo nikaanza kuwasalimia wote kwa kuwapa mkono. ila cha ajabu wengine walikua wakinitekenya kwwnye mkono afu nikimuangalia ananikonyeza.... Mmhhhh nilishindwa kuelewa kinachoendelea.

    Baada ya masaa kadhaa kupita sherehe ilikua imekwisha. sasa mama alikua kawasindikiza marafiki zake kwa kutumia gari...

    Sasa nilipomuona zai nikamfuata na kumshika mkono huku nikimburuza mpaka geto kwangu huku nikiwa na hasira hio duuu...

    Nilimfikisha hadi geto kisha nikambwaga kitandani kwangu kisha nikaanza kuvua mkanda wangu

    "heee sheby? unataka kunifanya nini sheby?"

    "tuliaaa, nyie si mnaniona mi hanisi si ndio?"

    "sheby una nini wewe? hebu kumbuka mi ni dada yako sheby"



    Nilikua sitaki kuskia kauli yake ya kua ni dada yangu. Niliuvua mkanda kisha nikauweka sawa kwa ajili ya kuchapa mtu,

    "yaani usiponambia, huu mkanda utakuishia mwilini wote"

    "sasa nikuambie nini?"

    "hio sherehe inamuusu nani?"

    "mmhhhh mi sijuiii"

    "aaahaaa hutaki kusema si ndio?"

    "subiri kwanza sasa"

    "sema sasa"

    Nilikua nimekua mkali ghafla ili tu nijue hio sherehe ni ya nani na inahusu nini... coz kila ninaemuuliza pia hawataki kunijibu kwa usahihi ulionyooka. but zai najua yeye ndio kipenzi cha mama hivyo najua tu atakua kaambiwa kuusiana na hii sherehe ya ghafla ghafla hivi...

    "mama aliniambia kua, wewe kuna kitu umefanya ofisini..kwaio ndio maana kakuandalia sherehe kwa hicho ulichokifanya ofisini na secretary wetu"

    Aliposema tu hivyo yaani kila kiyngo kilinilegea huku nikijiuliza kimoyo moyo kua

    "kwanini mama anapenda mi niwe mzinifu?"

    Nilijiuliza lakini sikujipatia jibu hata kidogo

    "sepa zako basi"

    Nilimfukuza zai chumbani kwangu huku nikichukua taulo na kwenda bafuni.. .Nilioga chapu chapu maana nilikua nachelewa msikitini kusali. maana wamenichelewesha na haya masherehe yao..... Nilimaliza kuoga kisha nikatupia kanzu na kibaraka shee. Kisha nikawa natoka zangu huku nikihesabu tasbii yangu.. Nilipotoka nje ya geti nilikutana na wasichana kama 6 hivi.. wakali kinoma

    Kama kawaida yangu nikawasalimia kiislamu warembo hao

    "Assalam Aleykh?"

    "poa tu mambo zako?"

    "kama amuezi si mtulie tu kuliko kuharimu salamu?"

    Nilianza kuwagombeza kwakua hawakuitikia salamu yangu ya kiislamu

    "we mkaka mbona una gubu wewe? kwani ni lazima tuitikie hio salamu yako?"

    Mara zai akatokea huku kajitanda vizuri

    "Eee ushaanza misele saa hizi mtoto wa kike watoka kwenu"

    "heeee sasa nisiwasindikize marafiki zangu"

    "sasa utarudi na nani usiku huo?"

    "si wewe apo"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "mschiuuuuuuu mwehuuu nini wewe? yaani niache kwenda msikitini eti niwasindikize nyie? ivi hilo neno umeongwaa au umeropokwa?"

    "ah ah mimi nawasindikiza hawa halafu mi nakuja kukusubiri pale nje ili ukitoka turudi wote"

    "kama utaweza kusubiri hadi saa 5"

    "heeee sheby saa 5 unafanya nini huko?"

    "aaaa ebu nenda ukooo"

    Waliondoka zao huku mimi nikitembea kwa miguu taratiiibu kabisa, kwani siku hio sikutaka kua na baiskeli, Hivyo nilikua sloo moo.. Nilipofika msikitini nilitawadha vizuri kisha nikaingia masjidi na kuswali swala ya saa 12 ambayo ilinipita

    Baada ya kumaliza kulipia swala hio Nilichukua mswahafu na kuanza kujisomea maana nilikua nimeshaumaliza hivyo nilikua naurudia tu. Nilikua naisubiria swala ya INSHA yaani swala ya saa 2 usiku... Ilifika mida hio kisha nikaswali na baada ya hapo tukasoma dua mbili tatu za kweda kulalia...

    Baada ya dua waislamu wote tukawa tunaagana kwa kutakiana kheri ya siku ijayo..

    Basi nilitoka zangu pale masjidi na kuangaza angaza pembeni kama ningemuona zai. maana si alisema atanisubiria...

    Sasa kutazama maeneo flani kwenye mti niliona wasichana wawili na mmoja wao alikua ni zai ila mwingine sikua namfahamu.

    "we zai?"

    Nilimuita kwa umbali huku kama nikianza safari ya kurudi nyumbani.

    "abeee?"

    "twende sasa"

    akawa anakuja na yule rafiki yake. ila huyo rafiki yake sikua namjua kwani alikua kajitanda na mitandio kibao...

    "mambo sheby?"

    "alinisalimia huku akiwa bado kajifunika kanga usoni...

    "safi tu, kwani we nani?"

    Nilimuliza huku nikimuona zai kama anamsukuma sukuma aongee.....

    Sasa uzuri ni kwamba na mimi pia ni jeuri na ni mtu mwenye zarau kwa yule mwenye zarau na mimi. Niliivuta ile kanga yake na kumuona sura. Alikua ni aisha.. kama unakumbuka kuna siku nilikutana nae nikiwa naelekea masjidi usiku...

    "kwanini umejifunga na wakati sio taipu yako?"

    Nilimuuliza huku nikijichekesha mwenyewe coz nashangaa sana kwa hawa watoto wa kike wanaonifata kwa njia tofaut tofaut

    "nilitaka kujaribu kua unampenda nani kati ya msichana wa kiislamu na yule ambae ni wa kawaida"

    "hahahaha mimi wote siwapendi"

    "kwanini sasa sheby?"

    Sasa maongezi yakiendelea baina yangu na aisha nilishangaa kumuona dada zai katangulia mbele Eti aniachie nimtongoze aisha. Niliona tu zai anajipa tabu tu. maana hizo swaga za kutongoza mimi hua sinaga kabisa..... kwanza hata kutongoza yenyewe sijui

    "mwenye tu hua siwapendi"

    "au walikutenda nini sheby?"

    Sasa mtoto alikua keshaanza kunisogelea karibu huku akinigusa gusa ili nijiskie mwerere...

    Afu sauti yake kaishua kabisa yaani anaongea na pua kama kudeka si kudeka. yani kakaakaa kimahaba mahaba tu.

    "wala tu...sema mi siwapendi kabisa"

    "sasa sheby??"

    "nini?"

    Mtoto wa kiume nilikua nakaribia nyumbani, ila aisha yeye kapitiliza kwao kwa ajili ya mimi

    "mi nakupenda sheby?"

    "Enhe ivi wewe? unaakili kweli?"

    "lakini hujaniuliza huo upondo upoje"

    "najua huo upendo wako"

    "lakini sheby??? kwani we hujawai kuwa na mpenzi?"

    "na sitaki kuwahi"

    "basi naomba niwe wa kwanza kwako"

    Aliongea utumbo wake huku nikitembea kwa spidi kuelekea getini kwetu... maana tulikua tumeshafika nyumbani sasa ile nataka kuingia. Nilishangaa nimezuiwa kwa mbele na aisha huku akiwa kanishika tai... sijakaa vizuri mara kanisogezea mdomo.

    "sheby? unajua naumia sana juu yako, so plz naomba unipoze japo na denda tuuu plz nakuomba"

    Sijakaa vizuri mara dada zai katokea huku akisema

    "mpe mtoto wa watu kaka heee mpaka afe?"

    baada ya kuongea hivyo afu akaingia zake ndani,

    Sasa ile namuangalia zai kugeuka huku kwa aisga... Aisee nilikutana na mdomo lainiiii ulionifanya nishindwe kujitoa katika kinywa hicho

    Sasa maskini mtoto wa kiume hata denda tu sijawahi kula... sasa mtoto alikua ananilazimishia

    Sasa ile nakubali tu kula denda Nilishtukia nimepigwa kibao cha mkono. huku nikisikia sauti ikisema kua

    "nani kakufunza huu upuuzi?"

    Nilishangaa kusikia hio sauti na wakati kila siku naambiwa mimi sio riziki



    Alikua sio mwingine bali ni Anti mwaju. hivyo nilifurahi sana kwa kusikia vile ila pia nilishtuka sana kuskia hivyo, kwani kauli alioiongea anti mwaju ni kauli nzuri ila mbaya zaidi kama mama angeisikia ingelikua tabu kuliko.

    "we msichana ivi huna kwenu? Ee? si nakuuliza ivi huna kweeenu?"

    Aisha alibaki kutetemeka maana hamjui huyu anti mwaju ni nani yangu hivyo akimuangalia anamuona kama mama yangu vile, hivyo aisha alianza kuomba msamaha kwa kile kilichotokea kwa wakati huo. Kiukweli hata mimi nimefurahi kwa anti alivyotufumania maana nilikua tayari nimeshaingia mkenge kabisa. yaani aisha alinitaiti mpaka shetani alinipitia na kujikuta nakubali kupokea denda la aisha... ila hakufanikiwa kuninyonya ila ndio nilikua nakubali kunyonywa denda, hivyo kama sio anti mwaju kutokea pale. duuu ningekamulia mate mpaka ningekoma. maana aisha alikua ana uchu na mimi mpaka basi.

    Anti mwaju alimuelewa aisha hivyo akamwambia kwa uzuri tu kua

    "we msichana? naomba iwe mwazo na mwisho kumfatilia mwanangu sawa?"

    "sawa mama nimekuelewa"

    "haya unaweza kwenda tu ..........na wewe ingia ndani haraka"

    Niliingia huku nikimpongeza anti kwa kuwahi kunifumania. maana nisingependa itokeee

    "anti?"

    "mmhhh"

    "nakushukuru sana kwa hili"

    "lipi hilo?"

    "najua utajiuliza kwanini ila sikupenda kitokee"

    "kisitokee kinini sasa?"

    "hiki ulichotukuta nacho hapa"

    "mwanangu? kwani ulifikiri mi napenda uyajue hayo? wewe bado ni mdogo sana ila wazazi wako wanakuharibu mwanangu"

    "mi pia sipendagi anti...coz mpaka nimekubali kuonekana shoga kwa ajili tu wasinibebeshe mazambi yao"

    "mwanangu sheby? mimi ndio niliokulea toka ukiwa mdogo, hivyo nakujua jinsi ulivyo kua wewe ni rijali ila kwa malezi niliokulea mwanangu? nashukuru yamekukaa vyema"

    "nashukuru sana anti, coz malezi yako yananifanya niishi kwa amani sana katika hii dunia... ila tatizo ni wanawake wananisumbua antiii"

    "Eeehehehehehe mwanangu? usijali kabisa, kwasababu najua ni haka kasura kako ndio kanawachanganya ila watakuchoka tu"

    "watanichoka? kivipi?"

    "namaanisha hivi? ukikua vizuri si lazima uwatokeee?"

    "aahahahahaha Anti bwana duuu... mi sitaki pia hivyo coz tumefundishwa madrasa kua tusikimbilie anasa kwani zipo na bado zinaendelea kuwepo... kwaio mimi nataka mke wangu ndio awe wa kwanza kwangu"

    "mmmhhh mtoto muongo wewe"

    "kweli anti, mi sitaki starehe na udogo huu"

    "ndio vizuri ila angalia isije kua kweli?"

    "nini hio?"

    "si hivyo wanavyokuzania"

    "Antiiii mbona huniamini? Au nikuonyeshe ili uamini?"

    "weeeee shenzi yako kua na adabu pumbavu wewe... hebu twende uko"

    Daaahhh Anti alikasirika ghafla huku tukielekea ndani. Nilipoingia ndani nilinyooka moja kwa moja hadi chumbani kwangu. Nilipofika nikaanza kujiandaa kwa kuweka vitu vyangu vya shule.. maana kesho nitakwenda shule,CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sasa nikiwa naendelea kupanga nguo na madaftari huku nikiwa na furaha ya kesho shule, maana napenda shule vizuri mno.. Ghafla nilishangaa mlango umesukumwa na mtu kuingia

    Alikua ni zai kaja huku akiwa na furaha fulani hivi

    "we unacheka cheka nini sasa?"

    "leo ndio nimekuamini we ni noma"

    "noma??????? noma wa nini?"

    "yaani ulivyomfanya aisha mpaka nimependa yani"

    "mschiuuuuuuuu (msunyo) Yaani we unawaza ngono tuu?"

    "jamani sheby?? ivi huoni aibu watu wakikudhania kua wewe ni gay? (shoga)?"

    "zai? naomba uondoke chumbani kwangu, coz ntakubutua sasa iviii"

    "ok tuyaache hayo... hebu niambie ukweli coz aisha kanambia eti ulimzungusha ulimpapasa ulimdenda ulimmmmhhhmm eti ni kweli?"

    "ahahahahaha kakudanganya uyooo hohohohohoho na wakati namshukuru anti kwa kutukuta"

    "Anti? anti ndio kafanyaje?"

    "alinizuia nisifanye, Asee nilishukuru mungu duuu"

    "haaaaaa yaani anti kakuzuia?"

    "heeee kwani vp? si amenilinda kama mtoto ake?"

    "kuuuumbe Anti mwaju ndio anakusababisha uwe mjinga mjinga ee?? ngoja nikamwambie mama"

    "ah ah zai??? zaiiii?"

    "nini? niachie"

    "vungaaa basi... nilikudanganya tuu"

    "sitaki niachie nikamsemee huyo anti wako unajifanya unampeeenda"

    "sikia basi zai... we zaiiii? aaaa sio poa ivooo"

    Daaahh Asee dada zai ni mbea duu ani kitu kidogo tu anafikisha hadi kwa mama???

    Sasa sijakaa vizuri mara niliskia sauti ya mama ikimuita Anti mwaju

    "mwajuuu? we mwaju weee?"

    "abeee dada?"

    "njooo hapa"

    "ndio dada kwani kuna nini?"

    "umemzuia nani hapo nje?"

    "mbona sijamzuia mtu dada"

    "nani kakuambia umzuie mwanangu na mpenzi wake?"

    "nisamee dada ila ndio malezi mazuri kumkataza kwani bado ni mdogo"

    "shatapp... yaani mimi nahangaika kwa waganga kila mahali, ili tu nijue mwanangu ni mzima au laa.. afu kumbe wewe ndio chanzo? kwanini lakini mwajuuu?"

    "dada naomba unisamee sintorudia tena"

    "afu usikute umeniharibia mwanangu wewe???"

    "mama sheby?? sasa mimi nimemharibu na nini?"

    "wewe si ndio umemlea toka akiwa mdogo?"

    "lakini mbona mwanao ni mzima tu dada?"

    "mzima kwani wewe ndio umelala nae?"

    Mungu wangu mieee.. Asee mtoto wa kiume nilikua natokwa na machozi kwa kusikia Anti mwaju anavyodhalilishwa mbele ya wafanyakazi wadogo..

    Sikuweza kuvumilia kabisa kwani maneno anayo yasema mama ni makali mno. utafikiri sio mwanamke mwenzi vile

    "mamaaa? basi inatosha... inatosha"

    "sheby tulia kwanza huyu mwanamke anakuharibu afu we hujijui tu"

    "anaeniharibu ni wewe au yeye?"

    "mwanangu?? yaani mimi nikuharibu wewe?"

    "sasa ana kosa gani huyu? kazi kumuonea tu... au kisa ni mimi kuwepo humu? basi kuanzia leo naondoka zangu"

    "ah ah sheby usifanye hivyo mwanangu"

    Nilikua naelekea chumbani kwangu huku nikiwa na hasira kali. yaani nilikua hadi natetemeka mikono kwa hasira...

    "mwaju? hebu nenda jikoni kaendelee na kazi"

    Mama alimsamee mwaju na kumwambia akaendelee na kazi. huku mama angu na zai wakinifata nyuma nyuma... niliingia chumbani kwangu na kutafuta begi la nguo na kuanza kupangilia nguo zangu...

    "sheby mwanangu una nini lakini?"

    "nimesema niache bwana"

    "jamani sheby sasa mabegi ya nini? hebu punguza hasira mwanangu"

    Mama karibia alie kwa kunizuia kuondoka.

    "niachie bwana mamaa"

    "kwani shida ni nini mwanangu?"

    "tatizo nyie mnapenda kumuone mwanamke wa watu nyie... ivi kawakosea nini? eee? au kisa hana mtoto ndio mana mnamnyanyasa sana?"

    "mwanangu baasi, nishamsamehe"

    "haitoseidia kitu kunizuia kuondoka"

    "lakini sheby? nisamee basi mimi mama yako"

    "kwanini mamiii unashindwa kumuamini mtu? eee?... miaka mingapi ulimuacha na mimi na zai na dada sauda? mpaka ukarudi ukatukuta watoto wako wote ni wazima wa afya... leo unakuja kumjibu mwanamke wa watu hovyo na wakati kakulelea watoto wako wote? kwanini mamiii?... kama ni kuniharibu si angeshaniharibu toka huko zamani? leo hii humuamini na wakati ulimuachia nyumba nzima na watoto wako. afu bado unamtolea maneno machafu vile kwanini mamaaa????"

    Nilikua naongea kwa hasira na kwa sauti kali mpaka koo likanikauka.. na hapo nilipo nilikua nimesimama na vidole kwa gasira na uchungu wa kutukaniwa mlezi wangu...

    "sikia sasa nikuambie mamiii mimi naondoka nyumbani kwako, ila kaa ukijua mimi sina tatizo lolote. mimi ni mzima na sio shoga kama mnavyofikiria na sijawahi kufanywa wala sijawahi kumfanya mtu... hivyo swala lenu la mimi ni shoga sitaki kulisikia. na ili mumueshi iii mumu... mumu... hhhiiii mumu... aaahhh mumu"

    Ghafla nilidondoka chini huku nikiwa naumwa na kichwa. hivyo toka muda huo sikua najitambua tena. ila nilikua nasikia. coz hata mtu akifa sii kua hasikii. anasikia vizuri sana ila kujibu tu ndio anashindwa... hivyo mimi nilikua nasikia yote waliokua wakiongea

    "sheby? sheby? sheby mwanangu? jamani shebiiiiiii?"

    "mama? sheby kafanyaje??"

    Huyo alikua ni zai akimuuliza mama

    "hebu kamuite mlinzi haraka"

    Zai alitumwa akamuite mlinzi. maana mwanamke ni ngumu kujua mtu aliizimia na mtu aliokufa.

    Mlinzi alikuja huku akiwa na wasiwasi... na wakati hua nilikua nimetulia tena nimepoa mwili kabisaaa

    "juma? hebu muangalie mwangu kawaje?"

    Huyo juma sikua najua anafanya nini maana hata nikishikwa sijihisi kama nimeshikwa ispokua ni kusikia tu ndio nasikia... kwahio hata ukinikata panga la mguu siwezi jua wala kuhisi maumivu yeyote. kwani hata hapo mama kanishika lakini sijui na wala sihisi kama nimeshikwa...

    Mara ghafla nikamsikua mama akimuuliza mlinzi kua.

    "juma? umegundua nini kwa mwanangu?"

    Lakini juma hakuongea kitu chochote

    "we juma si useme mwanangu ana nini"

    "mmmnhhh?"

    "mnhhh nini sasa si useme?"

    "bo bo boss boss bo bo boss?"

    "niambie bwana mbona unantolea macho tu?"

    "bosiiiiii uuuwiiiiiiii bosiiiiiii uuuwiiiiiii uuuuuwwiiii aaaaiiii"

    "juma? unataka kusema mwanangu mwanangu a, a, a, a, a, ame amekufa?"





    Nilikua naskia tu mama akimuuliza mlinzi kuhusu mimi. Ila mlinzi pia hakujua kilichonipata, hivyo alibaki tu na yeye akilia

    "bosiiiiii uuuwiiiiiiii bosiiiiiii uuuwiiiiiii uuuuuwwiiii aaaaiiii"

    "juma? unataka kusema mwanangu mwanangu a, a, a, a, a, ame amekufa?"

    "bosi mi sijui"

    Niliskia tu likibao likimuangukia mlinzi huku mama akisema

    "pumbavu mjubwa wewe.. hebu nenda kafungue geti haraka.... Na wewe zai kageuze gari"

    Mama likua ni mkali kupindukia, ila huezi amini mama alinibeba mwenyewe bila hata kuseidiwa. Alipofika nje mara anti mwaju kaja huku analia

    "jamani dada sheby ana nini?"

    "mi sijui kadondoka tu na kukata kauli"

    "jamani naomba nimuone kwanza"

    "hebu sogea bwana mwaju aaaaa?"

    "jamani sheby pole"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Alikua akitoa pole ila siwezi kumjibu hata kidogo...

    "dada ngoja twende wote dada"

    "wewe mwaju kaa na nyumba.. si unaona wote sisi tunaenda hospitali?"

    "sawa dada ila naomba apone mwanangu"

    "atapona tu"

    Anti mwaju ndio alionilea na ananijua vyema hivyo lazima anione kama mwanae vile.. hivyo hata akiita mwanangu msishangae, kwani hilo ni jina tu kama unavomuita mtu braza na wakati humjui....

    Mama mwenyewe ndio alikua dereva Afu dada nusura ndio kanipakata kwenye mapaja yake. na huku upande wa miguu alikuepo zai hivyo mwili wangu ulikua juu ya mapaja yao.. maana ni lazima wanibebe coz ni mdogo wao wa mwisho, kwani zai ni dada yangu kanipita miaka miwili hivi na nusura kama miaka minne au mitano.. hivyo hatujaachana saaana kivile, yaani kidigitali ni sawa na wote tupo sawa kiumri.

    Mama aliikimbiza gari kwa spidi kali mpaka hospitalini, Nilishushwa kwenye gari na kutaka kupakizwa kwenye machela.. ila mama alikataa na kunibeba mwenyewe hadi wodi, nilipofikishwa wodini kwanza chap chap nikaanza kupimwa fasta fasta na usiku huo huo. maana nakumbuka ilikua ni mida ya saa 2 hivi na madakika ila kwa sasa sijui coz sina fahamu kabisa. Dokta alinipima na kugundua kua mado nipo hai bali ni maji ya mwili ndio yalikauka kwa ghafla.

    "dokta mwanangu kapatwa na nini?"

    "aaaaa mwanao ana matatizo ya kutoongea sana. hivyo atakapoongea sana na kwa hasira nyingi mwaweza mpoteza maramoja. hapa ameongea mpaka maji yamekauka mwilini. hivyo ngoja hizi dripu mbili za maji ziishe ndipo tuweze kutoa matibabu mengine. hivyo naomba muende nyumbani ili muje kesho mida ya saa nne mkiwa na breki fasti kwa ajili yake....

    "dokta mi siwezi kwenda nyumbani kabisa"

    mara zai na nusura nao wakagoma kurudi

    "na sisi pia hatuendi"

    Dokta alioneka kama kushangaa japo simuoni. huku akisema

    "sasa jamani mkinigomea hivi je mtalala wapi?"

    Mara simu ya mama angu ikaita ila sijui ni nani anampigia

    "haloo mwaju?"

    "...................."

    Sikuskia anachoongea mwaju coz haikuwekwa laudi spika

    "bado ila inasemekana alipata tu mshtuko"

    ".................."

    "huu sio muda wa kulaumiana mwaju aaalaaa"

    "..............."

    "kaa na nyumba vizuri na wandugu zako hao mi nalala huku huku"

    Alimaliza kuongea hivyo kisha zai akauliza

    "beki 3 anasemaje? maana anavyompenda sheby mmhh utafikiri ni katoto chake vile"

    "zai?"

    "abee mama?"

    "nafumba macho na kufumbua nisikuone hapa ospitalini"

    "kwanini mama?"

    "toka hapa... mshenzi mkubwa wewe, ivi kwanini hupendi kumueshim mwaju wewe? ivi hujui kua yule ndio kakufanya mpaka leo upo duniani? je angekuekea sumu je?"

    Mara dada nusura kaingilia kati

    "mama basi yaishe. kumbuka tupo wodini mama"

    "hapana huyu mtoto ni mshenzi sana huyu anashindwa kumueshim mlezi wake? we ulifikiri ni mfanya kazi tu yule? yule ni sawa na mama yako, kakosa kukuzaa tu.. mshenzi wewe kua na adabu mbwa wewe"

    Daaahh mama angu alikua ana hasira na kua mkali juu ya anti mwaju. Dokta aliingilia kati huku akisema

    "mama? tafadhali sana kuna wagonjwa hawaitaji kelele mama"

    "usijali dokta ila mi hawa watoto wanazidi kunichanganya tuu"

    "ok sasa mama mimi nina ombi moja.... naomba abakie mmoja tu kwa ajili ya kumuangalia"

    "nusura mwanangu? nendeni nyumbani si mnajua kule kuna wafanyakazi tu?"

    "mamaa? kwani mimi sipaswi kumuangalia mdogo wangu?"

    "lakini mimi si nipo"

    "mmhhh sawa..... zai twende"

    "staki mi nalala na mdogo wangu huku huku"

    Mara dokta akaingilia kati juu ya zai kukataa kuondoka

    "we mtoto hebu nakuomba nenda coz huku kuna uwezekano wa kulala muuguzi mmoja tu na sio zaidi...hivyo mkilala hapa mtaniharibia kazi wanangu"

    Baada ya dokta kusema sana sasa zai na dada nusura wakaondoka zao. na mama nae akalala hapo hapo tena maskini alilala kwa kukaa. coz hakukua na vitanda vya wauguzi bali ni vya wagonjwa.

    BAADA YA SIKU HIO KUPITA

    Na sasa ni asubuhi mida ya saa 2 hivi. nilikua nimepata nafuu kidogo ila bado sijaamka

    Nilimsikia mama akiongea na dokta. maana tayari keshajua nimepata nafuu ila bado sijaamka

    Lakini mama alikua anaongea na dokta kuusu hili swala langu la kutopenda wanawake. na nilikua nawasikia vizuri tu....

    "dokta? mwanangu nahisi ana tatizo"

    "ah ah mama shebiiii punguza mawazo, mwanao alipata mshtuko tu na kuishiwa na maji mwilini ila tayari keshaamka hana tatizo, tena mnaweza hata kuondoka"

    "doktaaaaaa? mbona hunielewi? mimi simaanishi hivyo"

    "sasa unamaanisha nini?"

    "mwanangu naona kama hana nguvu za kiume"

    "heeeee umemjuaje wewe kama hukutembea nae?"

    "dokta tueshimiane sawa?? mimi nitawezaje kutembea na mtoto wangu?"

    "inawezekana vizuri tu, ila hebu niambie umemjuaje?"

    "aaaaaa mi nadhani sina kizibitisho sahihi ila mbona hapendi wanawake?"

    "aahahahahahaha sasa mtoto umlee mwenyewe afu ushindwe kumjua? afu pia? mbona mwanao bado ni mdogo sana.. na sidhani kama ana umri wa kushawishiwa na wanawake"

    "kwani mvulana anashawishika kimapenzi na umri gani?"

    "mmmmhhhhh ni kuanzia miaka 15 hivi ndio utamuona anaanza tabia ya kugeuza macho pindi anapokutana na mwanamke"

    "sasa mbona mwanangu ana miaka 20 na mwezi mmoja sasa?"

    "mmhhhhhh sijui kwakweli ila labda malezi pia"

    "kivipi dokta?"

    Mama angu alikua ana shauku ya kujua zaidi kuhusu mimi. ila dokta yeye anamuambia vizuri bila kumkopesha kitu

    "mtoto wako anapenda dini?"

    "yes...tena sana yaani ukitaka mgombane mkataze kwenda msikitini"

    "ooohooooo basi kwishi nehi?"

    "kwishi nehi? kivipi dokta?"

    "sio kua kaisha labda hawezi? bali dini yake hamruusu kufanya hivyo kwaio hapo hakuna mjadala tena labda aamue kuingiwa na shetani ndio aanze hio tabia"

    "lakini pamoja na hayo. kuna tetesi niliziskia kwa muda mrefu"

    "tetesi gani hizo?"CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "niliambiwa kua kuna siku alikutwa kwenye kikundi cha vijana wanao lawitiana"

    "mmhhhh unataka kuniambia mwanao ni shoga?"

    "mmhhh sina hakika sana ila nasikia sikia tuuu"

    "mmmhhhh ila hapana kama ni shoga angeonyesha udhaifu fulani hivi"

    "hebu kampime ili tupate uhakika doktaaa"

    "wala hio haina haja ya kupima bali we kaa nae chini kisha muulize kinaga ubaga kuusu yeye"

    "mhhhh dokta nitawezaje?"

    "utaweza tu, kwani si mwanao?"

    Mama angu alionekana kama hakufurahishwa na majibu ya dokta. Mama alikuja hadi pale nilipolazwa, maana walikua wakiongea kwa upande mwingine ambapo pametenganishwa na bodi fulani hivi ( siring bodi ) Sasa aliponifikia pale kitandani aliniamsha ili niweze kunywa chai.

    "sheby mwanangu? sheby? amka unywe cha baba"

    Daaa nilikua nimelala kwa muda mrefu sana....

    Niliamka kisha nikapiga chai safiii.

    Baada ya kumaliza kunywa chai Tulipewa ruksa ya kurudi nyumbani. Hivyo zai alikuja na gari kisha tukaondoka hospitali hapo.

    Tulifika nyumbani mida ya saa 8 hivi maana tulipitia dukani kwa mama then tulikaakaa kama masaa kadhaa ndipo tuliporudi nyumbani, Nilipofika nyumbani nilioga fresh kisha nikaelekea zangu masjidi mida ya saa 9 hivi alasili. Nilienda kuswali kisha nikaingia madrasa na kujisomea baadhi ya dua ambazo nazipenda sana kuzipitia katika vitabu vya mungu.

    Nilikaa mpaka saa mbili tulipomaliza kusali isha, ndipo nikarudi zangu nyumbani. Sasa leo nilikua nina hamu na mihogo ya kupika. hivyo nilinunua mihogo mibichi nilipotoka msikitini.....

    Sikumsumbua mtu wala nini Niliingia jikoni chapu na kuanza kuipika. maana mimi siii haba kwenye kupika nipo vizuri mno. Mara alikuja Beki 3 mmoja aitwai jesca

    "kaka utaungua.. mbona hukusema nikupikie tu?"

    "aaa hua hata nyie mnachokaga hivyo sikutaka kukusumbua.."

    "hapana kaka sheby.... coz sisi ikifika mwisho wa mwezi tunalipwa. sasa nisipofanya hivi je? nitalipwaje?"

    "mmmhhh baasi, ila napika mwenyewe kwa leo"

    "Tehehehehe kwanza umekosea wenzio hawakorogagi mihogo"

    "wanakorogaje kama sio hivyo?"

    "njoo sasa nikuonyeshe"

    Sasa mimi nikawa mbele afu yeye yupo nyuma yangu akinifundisha kupika futari... Sasa mtoto alikua ananigusa na matiti yake mgongoni kwangu. kwa vile anavyonifundisha. Nilikua navumilia tu ila hali ilikua sii shwari kabisa. Mara ananihemea shingoni duuu... ilikua ni karaha mwanzo mwisho Afu chuchu za jesca zilikua bado mbichiiiiiiiii. Nilikua nabonyea kila saa ili asinigusishe matiti yake. lakini mtoto alikua kama anafanya kusudi vile.

    "kaka nini? mbona hutulii?"

    "mmmhh Ah Ah sina kitu sema tumbo linaniuma"

    "pole"

    "asante"

    Sasa ghafla akanikumbatia kabisa

    "we jesca nini?"

    "yesu wangu nisamee boss"

    "mi spendi hio tabia bwana"

    "lakini kaka? wewe si unaskia baridi?"

    "ndio ila muda sii mrefu naenda kuchukua sweta"

    "weeeee kaakaaaa?"

    "nini?"

    "sweta la nini sasa?"

    "si la baridi?"

    "si uniombe mimi niwe sweta"

    Jesca alikua anaongea huku anaangalia chini. na kung'ata kidole

    "ahahahaha sasa we una sweta gani wewe?"

    "niruusu uone"

    "ahaa..bwana acha utani coz masweta yako hayanienei"

    "bwana kakaaaaaaa sio sweta hilo"

    Sasa aliposema hivyo nikajua alichomaanisha ni nini...

    Sasa nikajifanya kama shetani kanipitia.. nikamsogelea na kumkumbatia kisha nikamuuliza

    "vp sweta lenyewe ni kama hili?"

    Akajibu

    "ndio ila zima taa kwanza"



    Nilishangaa mtoto kajilainisha kwangu bila hata ya kutongozwa, Lakini nikajua kua hii ndio tabia ya mahausgeli kutamani au kupenda watoto wa mabosi wao. Mtoto wa kiume nilikua na akili zangu zote ila nilijikuta kama nakubali vile. Ila wakati huo taa bado hatujazima Jesca alianza kuninyonya shingo huku akitoa miguno ya kimahaba.

    "we jesca? tabia gani hio? mi staki bwana"

    "subiri kaka we si ulitaka joto?"

    Mara sufuria ikaanza kumwagika jikoni, ndipo jesca alipobanduka mwilini mwangu na kwenda kuopoa safuria. Sasa ule mwanya wa kwenda kuopoa nami nikajikataa zangu kimya kimya....

    Nilikimbilia geto kwangu maana sikua nataka bali nilimjaribu tu ili nione ana ugumu gani. Lakini jesca yeye alichukulia ni kweli ila mimi sikua nataka kweli, Ilipofika saa 3 na robo usiku.... Anti mwaju ndio aliniletea kile chakula huku akiwa kakasirika sana, tena alionekana kutokua na raha kabisa

    Alikiweka kile chakula mezani kisha akaondoka

    "Anti? anti? Anti?"

    "nini?"

    "mbona leo huna raha mamiii shida ni nini?"

    Hakutaka kujibu ila nilijua tu sababu ni nini

    Hivyo nilimfuata mpaka pale alipo kisha nikaanza kumuomba msamaa kwa kua nilimuambia mama kua anti mwaju kanizuia kua na demu hapo nje. mpaka akafokewa na mama

    "Antiii? sio mimi niliosema kwa mama anti"

    "najua sio wewe mwanangu ila kwanini umwambie dada ako?"

    "kweli nilimuambia zai lakini ilikua kama hadith tu wala sikumaanisha kama ulikosea"

    "basi mwanangu usilie sasa"

    Anti alianza kunibembeleza huku akinilisha futari ile....

    "kwanini unapenda futari hivyo?"

    "mmmhhh Anti hata mi mwenyewe sijui ila nimemisi mwezi wa ramadhan ( mwezi mtukufu )"

    "nilijua tu unakumbukia mwezi mtukufu"

    "ndio..afu na wewe ulikua unanirostishiaaa"

    Basi tulikua tukifurahi huku anti mwaju bado ananilisha kama katoto vile... tena wala haniwazi kua tayari nimeshakua. Afu alikua kakaa kwenye kitanda na mimi pia nilikua kwenye kitanda sambamba na anti mwaju.

    Mara mama angu katokea na kumkuta anti mwaju. Alituangalia tu maana hawezi kumkataza kunilishaCHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "heeeeeee ni kwamba mumekumbukia miaka hio au mumeamua tu?"

    "mmhhh dada nampenda sana sheby hivyo kila ninapomuona namhisi kama bado ni kachanga sana hata kula hakawezi"

    "mmhhhhhhh haya na kulishana kwenu"

    Ila mama angu alikua anaona wivu kwa kuona anti mwaju ananipenda kuliko yeye... Yaani hii nafasi ya kunilisha ni yake ila kapokonywa na anti mwaju... eti kisa alinilishaga toka nikiwa na miezi mitatu.

    "ilaaaa mwaju??"

    "abeee dada?"

    "usisahau kumpa dawa"

    "sawa"





    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog