Search This Blog

Thursday, 19 May 2022

JAMANI BABA - 1

 





    IMEANDIKWA NA : BEKA

    *********************************************************************************



    Chombezo : Jamani Baba

    Sehemu Ya Kwanza (1)



    “Mume wangu leo nataka kukiri jambo moja

    kwako, naamini litakukera sana lakini naanza

    kuomba radhi nikiwa chini ya miguu yako, ”

    alisema Zainabu akimwambia mume wake ,

    Masalanda. ..

    “Ipi hiyo? Mbona unanitisha mke wangu, mwaka

    wa tatu sasa tangu tumeoana hujawahi

    kuniambia hivyo .”

    “Oooh ! Siku zote nilikuwa nafikiria namna ya

    kukwambia mume wangu .”

    “Sasa niambie basi .”

    Zainabu alianza kuporomosha machozi na

    kumfanya mume wake huyo kushangaa na

    kukifikiria zaidi hicho kitu ambacho kimemfanya

    mkewe aamue kukisema...

    “Labda ameamua kuachana na mimi sasa

    anashindwa kuniambia ?” aliwaza Masalanda .

    “Utanisamehe kweli mume wangu ?”

    “Nitakusamehe mke wangu, we niambie tu.”

    “Unajua ... unajua wakati unanioa nilipokwambia

    nilizaa mtoto akafa na nikawa sipati mimba

    nilikudanganya mume wangu ... ”

    “Ooo! Kumbe hukuwahi kuzaa kabisa?”

    “Hapana, ila... ”

    “Ila nini mke wangu hebu kuwa muwazi jamani!”

    “Nina mtoto... ”

    “Hee! Una nini ?”

    “Nina mtoto mume wangu, nisamehe sana

    sikukwambia nilikuficha kwa sababu nilijua

    utaniacha wakati nakupenda sana mume

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wangu,” alisema Zainabu huku akiendelea kulia.

    Kwa mbali , Masalanda alianza kumuonea

    huruma mkewe . Ni kweli walioana ukubwani

    sana kwani Masalanda alikuwa na mke akafariki

    dunia na mpaka kifo mwanamke huyo hakuwahi

    kumzalia mtoto.

    Wakati anakutana na Zainabu, aliamini atadumu

    naye kwa sababu wote ni watu wazima tayari.

    Aliamini kwamba kwa sababu alishazaa mtoto

    akafa , basi watamtafuta mtoto wao kwa kudura

    za Mungu mwenyewe.

    “Zainabu, ” aliita Masalanda akitumia sauti ya

    unyonge.

    “Abee .”

    “Hebu nijibu maswali yangu kadhaa

    nitakayokuuliza.”

    “Sawa .”

    “Huyo mtoto ana umri gani ?”

    “Miaka ishirini na moja .”

    “Anaishi wapi ?”

    “Yupo kwa shangazi yake, Tanga.”

    “Anaitwa nani?”

    “Mwaija .”

    “Baba yake yuko wapi?”

    “Alishafariki dunia , si nilikwambia. ”

    “Hebu fanya mpango aje hapa, tumlee sisi . Mimi

    nitakuwa baba yake.”

    Zainabu alishtuka kusikia agizo hilo la mumewe

    kwani siku zote , shangazi wa mtoto huyo

    amekuwa akimwambia afanye juu chini

    amchukue binti yake kwani ameanza

    umachepele, anahofia asije akapata ujauzito

    akiwa nyumbani kwake ikaonekana amemtuma .

    “Kweli mume wangu?”

    “Kweli , imetoka moyoni mwangu , sina kinyongo

    na wewe. ”

    Zainabu aliachia tabasamu kavu huku akijifuta

    machozi kwa kanga. Mumewe alimkumbatia,

    akampiga busu wakakaa sawasawa .

    ***

    Ilikuwa siku ya tatu, Mwaija alikuwa ndani ya

    basi la Raha Leo lenye maandishi nyuma

    yanayosomeka; Tanga wadeka. Kila mara

    alimtumia meseji mama yake akimjulisha

    alipofikia. ..

    “Mama sasa tunapita Segera .”

    Mama yake alimjibu sawa , akamtakia safari

    njema.

    Moyoni Mwaija alikuwa na furaha iliyopitiliza ,

    alitaka sana kuishi na mama yake, hasa

    akizingatia kuwa anaishi katika Jiji la Dar es

    Salaam ambalo aliambiwa lina kila aina ya raha

    na karaha !

    Alipofika Chalinze , mama yake alianza safari ya

    kutoka Kigogo kwenda Ubungo kumpokea binti

    yake huyo ambaye ilikuwa inamuuma sana kuwa

    naye mbali .

    Basi lilifika, Mwaija akashuka, mama akashtuka

    moyoni maana mara ya mwisho alimuacha akiwa

    na miaka kumi na nane . Alimshangaa kumuona

    amenenepa, amenawiri , ametakata ile mbaya.

    Kikubwa zaidi alimshangaza nguo alizovaa.

    Mwaija alivaa suruali ya kubana, wenyewe

    wanaita skintaiti na t- shirt juu. Kwa umbo

    alilokuwa nalo Mwaija , kila mwanaume

    alimuangalia kwa uchu wa mapenzi. ..

    “Ha mama jamani ,” alichangamka Mwaija na

    kumkumbatia mama yake kwa furaha. ..

    “Shikamoo mama.”

    “Marahaba mwanangu, lakini Mwaija hizo nguo

    kweli ni za kuvaa mbele ya watu , si za kulalia

    hizo?”

    “Hamna mama, ndiyo fasheni yenyewe ya siku

    hizi. Mama upo Dar es Salaam lakini hujui

    mitindo?”

    “Mimi sidhani kama nitapenda mwanangu , hata

    baba yako niliye naye siamini kama atakukubali

    kwa mavazi haya . Hapa natamani nikupeleke

    wapi sijui ukabadili nguo ndiyo twende

    nyumbani.”

    “Jamani mama , basi nimekuelewa , twende tu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nyumbani nitavaa kanga nikifika. ”

    Walianza safari ya kwenda nyumbani Kigogo .

    Moyoni mama Mwaija alikuwa anaomba

    mumewe achelewe kurudi nyumbani ili wao

    watangulie kufika na Mwaija abadili nguo haraka

    sana.. .

    “Hivi na huyo shangazi yako ina maana alikuwa

    hakuoni unavyovaa ?”

    “Alikuwa ananiona . ”

    “Sawa ? Akawa anakuacha tu unaharibika

    hivihivi?”

    Mwaija hakujibu swali hilo alihisi halimuhusu

    yeye zaidi ya shangazi yake .

    Kufika nyumbani, mlango ulikuwa wazi ...

    “Mswalie mtume, keshafika huyu , sijui itakuaje?”

    alisema moyoni mama Mwaija , wakaingia ndani .

    Sebuleni alikaa Masalanda , alipomuona Mwaija

    akashtuka.. .

    “Karibuni. ..karibuni sana. ”

    “Asante , shikamoo, ” alisalimia Mwaija huku

    akikaa kwenye kochi kwa adabu .

    “Marahaba, za safari?”

    “Nzuri .”

    “Karibu sana, karibu mwanangu, ” alisema

    Masalanda huku akimkazia macho Mwaija na

    kumshangaza mkewe kwani uchangamfu

    ulikuwa mkubwa tofauti na alivyofikiria.





    “Asante sana . Naamini wewe ndiyo baba

    mdogo?” aliuliza Mwaija .

    “Hapana! Huyo ni baba yako , mambo ya baba

    mdogo yanatoka wapi saa hizi hapa ?” alikuja juu

    mama Mwaija .

    “Sawa , baba!”

    “Ni mimi mwanangu .”

    Mwaija alifurahia mapokezi hayo kiasi kwamba

    alijikuta akifurahi sana tofauti na alivyotaka

    kuamini hasa baada ya kushuka stendi Ubungo.

    Mwaija alioneshwa chumba chake cha kulala.

    Akaingiza mizigo yake ndani , akakiangalia

    chumba hicho kisha akakipenda sana.

    ***

    Ilikuwa usiku wa manane, Masalanda aliamka na

    kuanza kumuwaza Mwaija . Aliwaza tangu

    alipomwona jioni ile akitoka Tanga ...

    “Asante , shikamoo. ”

    “Marahaba , za safari?”

    “Nzuri .”

    “Karibu sana, karibu mwanangu. ”

    “Asante sana . Naamini wewe ndiyo baba

    mdogo?”

    Masalanda akazinduka kutoka kwenye mawazo

    ya jioni, akasema mwenyewe moyoni . ..

    “Anaonekana binti mchangamfu halafu ana akili

    kichwani. Ana heshima zake f’ lani. Yale mavazi

    ndiyo ya watoto wetu wa siku hizi. ”

    Wakati Masalanda akiwaza hayo , mkewe

    alishtuka na kugundua kuwa mumewe hakuwa

    amelala. Akajua ana mawazo kwani anamjua

    vizuri ...

    “Baba Mwaija ,” aliita mama Mwaija kwa kutumia

    jina la binti yake.

    “Naam.”

    “Nahisi kama una mawazo sana ?”

    “Hapana. Sina mawazo .”

    “Kama unayo niambie tu. Unajua binti yetu kaja

    kama ulivyomuona mavazi yake , nilimwambia

    yale si mavazi ya kuvaa humu ndani , akasema

    atajirekebisha kwa hiyo tumvumilie kidogo mume

    wangu.”

    “Sijayashangaa mavazi mimi , mabinti wetu mjini

    siku hizi ndivyo wanavyovaa , sidhani kama kuna

    namna.”

    “Sasa mawazo ni ya nini ?”

    “Nawaza biashara zangu naona kama haziendi

    sawasawa kama zamani .”

    “Mungu atakusaidia mume wangu, biashara

    ndivyo zilivyo , leo nzuri kesho ni mbaya sana .”

    “Sawa , nashukuru pia kwa dua zako .”

    ***

    Kule chumbani, Mwaija alikuwa akichati na jamaa

    yake wa Tanga mjini anaitwa Seif Mabanda ya

    Papa. Licha ya kwamba ilikuwa usiku lakini yeye

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    hakuona tabu ...

    “Mwenzio nimekuja kwa mama Dar , sipo Tanga ,

    hajakwambia Mwanakombo?”

    “Sijasikia. Unarudi lini ?”

    “Mh ! Sijui kama nitarudi tena huko . Mama

    hataki.”

    “Kwa hiyo ina maana umenimwaga?”

    “Jamani sijakumwaga , siku mojamoja we njoo

    huku Dar . ”

    “Mi sijawahi kufika Dar itakuaje?”

    “Mi nitakuelekeza.”

    ***

    Asubuhi Masalanda aliomba kupikiwa chai ili

    anywe kabla ya kwenda kwenye biashara zake. ..

    “We Mwaija ,” aliita mama.

    “Abee mama. ”

    “Hebu mpikie chai baba yako sasa hivi .”

    Chai ilipikwa ingawa mama Mwaija alishangaa

    sana kwani haikuwa kawaida kwa mumewe

    kunywa chai asubuhi pale nyumbani.

    Baada ya dakika kumi na tano tu, chai ilipelekwa

    mezani. Mwaija alibeba kwenye sinia akiwa

    ndani ya kanga moja. ..

    “Loo !” alihamaki moyoni Masalanda lakini

    Mwaija hakusikia.

    “Shikamoo baba.”

    “Marhaba Mwaija , hujambo mwanangu ?”

    “Sijambo baba sijui wewe umeamkaje?”

    “Mimi mzima wa afya, nakuhofia wewe na

    uchovu wa safari.”

    “Nimeamka sawa baba .”

    “Haya tumshukuru Mungu wetu. ”

    “Ni kweli baba.”

    Wakati Mwaija anaondoka, ‘mzigo’ nyuma

    ulionekana unavyosumbuliwa na kutembea hasa

    ikizingatiwa ile kanga moja tu na umbo la Mwaija

    sasa!

    “Hivi huyu binti ndiyo nini hivi ?” alijiuliza

    Masalanda huku macho yake yakimtoka pima

    wakati Mwaija anafuata maji ya kunawa .

    “Chai tayari wewe?” mama mtu aliuliza kutokea

    uani ambako alikuwa akifagia.. .

    “Tayari mama.”

    “Weka na maji kama nilivyokuelekeza kila kitu

    jana usiku .”

    “Sawa mama .”

    Baada ya mumewe kuondoka ndipo mama

    Mwaija alibaini kuwa , mumewe alikuwa

    akihudumiwa huku binti yake akiwa ndani ya

    kanga moko , ilimuuma sana!

    “We Mwaija .”

    “Abee .”

    “Wakati unamhudumia baba yako chai ulivaa

    hivyo?”

    “Ndiyo mama .”

    “Ha ! Ha ! Haaa ! Yaani kweli unavaa hivyo mbele

    ya baba yako Mwaija ? Hebu jiangalie kwanza.

    Ona! Hii mikalio yako ulitaka aione siyo?”

    “Hapana mama , ila ... ”

    “Ila nini ? Au unataka baba yako aingiwe na ibilisi

    juu yako siyo ?”





    “Hapana mama , mimi sikujua kama kwa kuvaa

    hivi baba anaweza kuingiwa na ibilisi .”

    “We hivyo ulivyovaa unaona ni sawa siyo?”

    “Ulivyoniambia ndiyo nimegundua si sawa sasa .”

    Mama alimwangalia bintiye kwa macho makali

    kwa karibu dakika moja nzima huku Mwaija naye

    akishindwa kuondoka na kusimama palepale.. .

    “Nisamehe mama.”

    “Usirudie tena, sawa ?”

    “Sawa mama .”

    “Haya , kaendelee na kazi zako .”

    ***

    Shughuli zilikuwa haziendi sawa kwa Masilinde.

    Kila baada ta muda alivuta picha ya Mwaija. ..

    “Yule binti, daa ! Ni shida kwelikweli. Au kuishi

    mbali na mama ndiyo kawa vile ? Sasa ni kuvaa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    gani vile mbele ya baba ’ake ?”

    ***

    Jioni Masilinde aliporudi nyumbani alimkuta

    Mwaija, mama yake alikwenda kudai pesa zake

    kwa watu aliowakopesha vitenge .. .

    “Shikamoo baba.”

    “Marhaba Mwaija , mzima ?”

    “Mi mzima baba, pole sana kwa kazi.”

    “Nimepoa . Mama yuko wapi?” aliuliza baba mtu

    huyo huku akikaa kwenye sofa...

    “Alisema anakwenda kudai madeni ya vitenge

    sijui.”

    “Ooo! Ni ile biashara yake.”

    “Nikupikie chakula baba?”

    “Hapana, kama kuna juisi naombeni. ”

    “Ipo ,” alisema Mwaija huku akienda kuifuata hiyo

    juisi...

    “Mh !” aliguna Masilinde akimwangalia Mwaija

    alivyovaa jioni hiyo. Alivaa gauni fupi , magoti yote

    yalikuwa nje huku miguu yenye umbile la chupa

    za bia ikionekana vizuri sana na kumfanya

    baba’ake azidi kung’ata ulimi .

    “Karibu juisi baba .”

    “Asante sana mama. ”

    Wakati Mwaija anaondoka kwenda kuendelea na

    shughuli zake , Masilinde alimtolea macho pima

    huku akitingisha kichwa . ..

    “We Mwaija .”

    “Abee baba .”

    “Njoo hapa. ”

    Mwaija alirudi haraka ...

    “Hebu kaa hapo .”

    Mwaija alikaa...

    “Hivi hizo nguo zako za ajabuajabu unazovaa

    hapa kwangu una maanisha nini? Nani

    kakwambia hapa ni hosteli ?”

    “Samahani baba, sikujua kama nitakukwaza .”

    Mara mama yake aliingia ...

    “Afadhali umekuja mama Mwaija ... ”

    “Nini tena ? Halafu wee Mwaija ...”

    Kabla mama’ake hajamaliza kusema, Masilinde

    aliendelea...

    “Nilikuwa namuonya mwanao na hivi viguo

    vyake... ”

    “Na ndiyo nilichotaka kumwambia na mimi .

    Asubuhi nimemsema sana, akabadili . Nashangaa

    saa hizi namkuta hivi tena. ”

    “Nisameheni sana.”

    “Tukusamehe kwani we mwenyewe huoni ?

    Kama utaendelea hivyo hapa nyumbani kwangu

    utahama haraka sana ,” alikuja juu Masilinde.

    “Na kweli utahama hapa. Nilishakwambia tangu

    unakuja kwamba hayo mavazi yako mimi

    sikubaliani nayo lakini nahisi kama hunielewi

    vile. ”

    “Nimewaelewa. ”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haya kabadili haraka sana ,” alisema Masilinde.

    Mwaija alisimama kwenda kubadili nguo . Wakati

    anatembea macho ya Masilinde yalikuwa kwake

    huku akisema .. .

    “Unavaa viguo vya ajabuajabu kama hosteli !”

    Mwaija alianza kukata tamaa ya kuendelea

    kuishi kwenye nyumba ile kwani mavazi ya ajabu

    yanayopigwa vita ndiyo zake . Hakuwa na nguo

    ye heshima hata moja.

    “Sasa itabidi kila gauni nivae na kanga juu ,”

    alisema moyoni huku akilitungua gauni jingine na

    kulivaa, akatupia na kanga moja juu yake,

    akatoka...

    “Si hivyo sasa, ulikuwa unashindiwa nini tangu

    mwanzo?” alihoji Masilinde huku akiachia

    tabasamu pana !

    Mwaija alipoona baba huyo anatabasamu na

    yeye akaachia la kwake, wakatabasamu wote ...

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hapo sasa unaonekana binti mzuri, uliyelelewa

    kwa maadili ya wazazi wako , si kama saa zile .

    “Asante baba .”

    Mwaija aliondoka kwenda nje . Wakati anakwenda

    macho ya Masilinde yakamsindikiza , akashtuka ...

    “Mamaaaa. ..kumbe ishu si viguo vifupi , ishu ni

    kwamba amejaaliwa makalio. Ona. ..eee . ..laaa!”

    alisema moyoni huku akisimama kumwangalia

    vizuri binti huyo .

    Japokuwa alivaa kanga juu ya gauni lakini

    wowowo lake lilionekana wazi na kutingisha kwa

    kadiri mguu mmoja ulipokuwa unakwenda mbele

    na kuacha mwingine nyuma. ..

    “Haiwezekani ! Hivi kweli mama yake ni huyu

    mke wangu au alipewa mwingine siku

    anajifungua?”

    Hapo mama Mwaija alikuwa chumbani kwake ...

    “We Mwaija ,” aliita Masilinde lakini kwa sauti

    ambayo kama hakutaka mkewe asikie kule

    chumbani.

    “Abee baba .”





    “Unaweza kuniletea maji ya kunywa?”

    “Sawa baba .”

    Mwaija alitoka kwa kasi kwenda kuchukua maji,

    nyuma wakati anaondoka , Masilinde

    alimtumbulia macho mpaka akataka kusimama

    kabisa.. .

    “Mama wee! Huyu si mtoto, ni mkubwa

    mwenzangu,” alisema moyoni baba huyo.

    “Karibu maji baba ,” Mwaija kwa heshima zote

    alimpa maji baba yake huyo tena akionesha

    ishara ya kupiga magoti.

    “Asante .”

    Wakati Mwaija anaondoka, Masilinde akaita

    tena...

    “Mwaijaaaa .”

    “Abee baba .”

    Mwaija alirudi mbiombio. ..

    “Abee baba .”

    “Hivi, naweza kupataa. ..aaa .. .kupata aaa ! Dah!

    Sijui kupata nini ? Naweza kupata kipande cha

    mkate?”

    “Ndiyo baba , ngoja nikaangalie kule. ”

    Mwaija aliondoka. Kwa jinsi alivyolitingisha safari

    hii, Masilinde alijikuta akisimama na kusema kwa

    sauti ya juu ...

    “Noo.. .oooo !”

    Mama Mwaija alishtuka kumsikia mumewe

    akisema noo kwa sauti kubwa sana, akatoka

    chumbani mbio ...

    “Nini mume wangu?”

    Masilinde alishindwa kusema ni nini? Jasho

    jembamba lilikuwa likimchuruzika mfano wa mtu

    aliyetoka kunywa chai ya moto bila kupumzika .. .

    “Eti Mwaija, kuna nini ? Mbona baba yako

    amepiga kelele?”

    “Hata mimi sielewi mama, nimemsikia tu

    akisema noo !”

    “Mh ! Mume wangu, unadhani ni nini ?”

    “Nahisi kama nipo hovyo kimoyo !”

    “Kwa nini ?”

    “Nadhani basi tu, siku hazilingani mke wangu. ”

    “Pole sana mume wangu .”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Haya asante sana . We nenda kaendelee na kazi

    zako.”

    Mama Mwaija alirudi chumbani, Mwaija naye

    akaendelea kwenda kuchukua kile kipande cha

    mkate.

    “Hiki hapa baba ,” alisema Mwaija baada ya

    kurudi.

    “Nashukuru sana ,” alisema Masilinde huku

    akiangalia ukutani ili asilione lile wowowo la binti

    huyo.

    ***

    Usiku uliingia , mama Mwaija alitangulia kulala

    siku hiyo kwani alichoka sana, mumewe

    Masilinde alikuwa akifuatilia habari kwenye tivii

    huku Mwaija akiosha vyombo.

    Mara zote alipokuwa na vyombo vingi alikatiza

    navyo sebuleni kuvipeleka kabatini kulingana na

    ramani ya nyumba yenyewe.

    Hali hiyo ilisababisha kusindikizwa na macho ya

    baba yake huyo wa kambo mwanzo hadi mwisho

    na kufuatiwa na kutingishwa kwa kichwa .. .

    “La! Mtoto huyu ! Sijui !”

    Mwaija alipomaliza kuosha vyombo aliingia

    chumbani kwake na kuvua nguo, akatungua

    upande wa kanga na kujifunga kukatisha kwenye

    nido, akatoka ili akaoge , kwa hiyo akapita

    sebuleni tena , Masilinde akashtuka

    alivyomwona ...

    “Mwa ... aaija!”

    “Abee baba .”

    “Unakwenda kuoga ee?”

    “Ndiyo baba .”

    “Haya , kaoge vizuri mwanangu , ujisugue ee !”

    “Sawa baba .”

    Mwaija alizama bafuni akiwaza upendo wa baba

    huyo kwamba ni wa hali ya juu kuliko alivyokuwa

    akifikiria kabla !

    “Mama alitaka kunionesha huyu baba ni mkatili

    lakini kumbe wala,” alisema Mwaija huku

    akijimwagia maji.

    Masilinde alishindwa kujizuia, alisimama ,

    akaenda kwanza chumbani kwake . Alimkuta

    mkewe amelala fofofo, akatoka kwa kunyata hadi

    kwenye mlango wa bafuni, akasimama hapo !

    “Sijui nisukume mlango niingie ? Lakini kwa

    mshtuko anaweza kupiga kelele mama’ke

    akaamka. Labda nisimame hapahapa mpaka

    atakapotoka,” aliwaza moyoni Masilinde.

    Akiwa bado kwenye mawazo , ghafla Mwaija

    alitoka bafuni ...

    “Ha !” alishtuka Mwaija akasita kuendelea

    kutoka.. .

    “Babaa!”

    “Mwaijaa. ”

    “Nimeogopa baba .”

    “Umeogopa nini mwanangu jamani ?”

    “Nilidhani nimekutana na mwizi.”

    “Hamna , ni mimi baba yako Mwaija . ”

    “Sawa ,” alisema Mwaija, akampita baba yake ili

    kwenda ndani .

    Masilinde akageuza kichwa kumwangalia . Na

    vile alitoka kuoga, kanga ilimshika mwilini na

    kule kutembea, baba akamtungia mlio, akawa

    anasema. ..

    “Mbende. ..mbende. ..mbende. ..mbende ...Mwaija , ”

    akamalizia na kumwita .

    Mwaija aligeuka haraka sana .. .

    “Umebakiza maji na mimi baba yako nioge ?”

    “Hapana baba , ngoja nikuwekee tu dakika moja. ”

    “Sawa mwanangu , nasubiri hapahapa. ”

    Mwaija aliweka chini kikopo chenye sabuni,

    akageuza kwenda kumuwekea maji baba yake .

    Alimpita mlangoni , akazama bafuni kuchukua

    ndoo! Masilinde kwa vile alikuwa amevaa suruali,

    alijikuta akiingiza mkono mmoja mfukoni.

    Mwaija wakati anatoka na ndoo alimgusa kwa

    bahati mbaya baba yake. ..

    “Ha ! Samahani baba. ”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Samahani ya?”

    “Nimekugusa kwa bahati mbaya .



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog