Search This Blog

Tuesday, 17 May 2022

MZOEFU - 5

 







    Chombezo : Mzoefu

    Sehemu Ya Tano (5)





    Akili ya kuambiwa jumlisha na ya kwako unafanya maamuzi kamili. Ingawa nilitegemea ushauri wa namna hiyo toka kwa dada angu lakini sikutegemea kama angeuleta kwa namna hiyo.Aliyosema ni kweli ndio sababu hata mimi awali nilihisi hivyo na ndio sababu ya kuomba ushauri lakini mwanaume rijali kama mimi nawezaje kumuacha kirahisi rahisi namna hiyo mlimbwende kama Sun hasa ukizingatia nimeshamgeuzia kibra?. Usiku huo hadi usingizi kunipitia niliwaza mengi na mwisho nilikubaliana na kamati yangu ya ubongo kuwa sitamtongoza Sun lakini pia sitamuacha hivi hivi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    * * * *



    Baada ya siku chungu tele kukatiza huku nikiwa sina mawasiliano yeyote na Malha.Ni siku nyingine tena majira ya usiku nikiwa sebuleni naangalia luninga, simu yangu iliita. Zilikuwa ni namba tu tena nisizozifahamu, mara nyingi huwa sipokei namba ngeni kwa kuhofia kuwa ni wrong number na tunaweza kusumbuana ama kuulizana wee nani!.Sababu hiyo ilinifanya kuipuuzia simu hiyo lakini niliipokea mara moja baada ya kukumbuka kuwa tangu nimeanza kazi Numerator's Entertainment mara nyingi nimekuwa nikipata deal za kwenda kufanya u mc kwenye shughuli mbalimbali.

    " Hello!?" Niliita baada ya kupokea simu kwa ki besi ( sauti ya nne)

    " Hello Tom mamboo!" Ilikuwa ni sauti maridhawa ya kike.

    " Poa tu!...sijui naongea na nani!" Niliongea huku nikinyanyuka kwenda nnje maana mzee ambaye nilikuwa naye alishanigeuza luninga.

    " unaongea na shem wako!" Sauti hiyo ilijibu kwa uzuri ule ule.

    " Sijui shem nani maana nna kaka wengi kweli yani!" Nilijibu kisiasa kumkwepa yeye kuwa shemeji yangu ila kumfanya mimi ndo niwe shemeji yake.

    " Ok unaongea na Salha!"

    " wow Salha! Mambo vipi!?" Nilifurahi baada ya kumjua

    " Mabayaa..Umetususa!" Alilaumu Salha.

    " Sijawasusa jamani mambo tu ndo mengi!" Tayari sauti yangu ilishalegea toka ile ya nne niliyopokelea simu hadi ya kwanza. Kweli wasichana nouma saana.

    "Shem!?" Salha aliita kuonyesha kuwa ana jambo anataka kusema.

    "Yap!" Niliitika kifupi

    " Sijui hapo ulipo uko free ( huru ) kuongea coz ( sababu) nna mazungumzo marefu kidogo!" Kauli yake ilinitisha kiasi cha kutaka kukata simu lakini nikajikaza kiume.

    " Yeah we sema tu niko poa!" Nilijibu huku nikimeza funda la mate lililopita kooni kwa tabu kwani bado nilikuwa na hofu juu ya mazungumzo yake marefu anayotaka kusema.

    " But am sorry kama ntakukwaza shem!" Salha alizidi kunipa hofu.

    " Usijali Salha wee niambie tu!" Nilijibu kishupavu.

    " Hivi kwanini uliachana na dadaangu shem!?" Hatimaye Salha alifungua mazungumzo na swali ambalo kwangu ilikuwa ni kama ngumi ya kushtukiza, lazima inipepese!

    "Kwani Malha yuko wapi!" Badala ya kujibu swali na mimi niliuliza swali ili kujiweka sawa.

    " Yupo Tanga saivi!"

    " Kwanini umeniuliza hilo swali Salha!?" Niliendea na maswali huku nikijipanga kujibu yake.

    " Tom wee nijibu tu alafu utajua kwanini!" Salha alikwepa swali langu lakini tayari nilishajipanga kumlipua.

    "Salha nikikwambia sababu ya kuachana na dadaako hutaniamini milele!" Taratibu nilianza kutega mabomu yangu.

    " kwanini nisiamini!?" Salha aliuliza akiwa na walakini ndani yake.

    " Sababu chanzo ni wewe Salha!" Hatimaye nilimpasulia jipu.

    "Khaa!.. kivipi!" Salha alishikwa na butwaa na kuhoji kwa hamaki.

    "Ndomana nilikwambia huwezi kuamini Salha ila ukweli ni kwamba tangu nilipokuona mara ya kwanza siku ile usiku ulitokea kuuteka sana moyo wangu, kiasi cha kunifanya hata nijute kwanini nilikutana dada yako kwanza.Hata dada yako alipokuwa anakupa simu usiku nikiongea naye unisalimie, hakika nililala usingizi mororo, nimekuwa nikijaribu kuzificha hisia zangu kwako ili nisije kukugombanisha na dadaako lakini kiukwei nilikuwa nashindwa hivyo njia pekee niliyoona inafaa ni kuachana na dada yako ili niwe mbali na wewe kwani isingeleta picha nzuri kukutongoza wewe akati nimeshakuwa na dada yako na wewe usingenielewa hata kidogo!" Nilitoa maelezo marefu bila kupumzika, niliongea taratibu lakini kwa uhakika na sumu niliyokuwa nikimtemea Salha ilionekana imeshaanza kumuathiri kisaikolojia kwani alibaki akijiuma uma asipate la kusema.

    "Salha!?" Nilimuita baada ya kuona yupo kimya.

    " bee!" Aliitika kwa sauti ya uvunguni akionyesha yupo kwenye fikara nzito.

    "Nimejikuta nashindwa kubishana na moyo, Nakupenda sana Salha na wewe kama unanipenda kama nnavyokupenda mimi, tafadhali niambie lakini isiwe leo, nakupa muda wa kufikiri juu ya hilo pia kama hunipendi uwe huru kwani mapenzi ni hisia, mwisho kabisa napenda kukwambia kuwa haya yote niliyokwambia leo ni siri niliyoitunza kifuani kwangu muda mrefu sana, nakuomba uitunze pia!..usimwambie mtu yeyote yule sawaa enh!?"

    " Sawa Tom nimekuelewa!" Alijibu kwa upole Salha huku akionyesha nguvu zimemuisha kabisa hata kubonyeza kitufe cha kukatia simu inaweza ikawa ni tabu.

    " Aya uwe na usiku mwema!"

    " Na wewe pia!"



    Hivyo ndivyo nilivyomalizana na shemeji yangu Salha aliyenitafuta mwenyewe.



    Kiukweli sikuwahi kumpenda Salha hata kumtamani, Na sikuwahi kufikiria kama itatokea siku moja hapa duniani nikaja kumtongoza ila siku hiyo nilithubutu kufanya hivyo kwa sababu kuu mbili.

    Kwanza kabisa sikutaka kuamini hata kidogo kuwa Salha alitaka kunisuluhisha mie na dada yake kwa akili zake mwenyewe kile niliamini lilikuwa ni shinikizo toka kwa dada yake kwa asilimia mia, Kitu kingine sikuamini hata kwa mbali kuwa Malha kweli alienda Tanga ila kile akili yangu ilinituma ni kuwa wapo pamoja muda huo na si ajabu waliniweka loud speaker.Na mara nyingine Salha alipokuwa akikaa kimya nilipokuwa naongea naye sikutaka kuamini ni kwajili ya maneno yangu matamu hata kidogo ila nilichowaza ni kuwa alikuwa akitazamana na dada yake na huenda walijadiliana ajibu nini.

    Kitendo cha mimi kumtongoza Salha ilikuwa ni sawa na kukata mzizi wa fitina kati yangu na dada yake Malha.Sikutaka Malha aendelee kuwa na hisia zozote za mapenzi juu yangu hivyo kitendo hicho cha kumtongozea mdogo wake kama kweli alikuwa naye muda huo kilitosha kabisa kulisambaratisha tumaini lake lililobakia.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Kwa upande mwingine nilichowaza kama Salha hakuwa na dada yake muda huo ni wazi kwamba asingenipigia simu tena maana kama kweli anampenda dada yake asingekubali kutumwa tena sehemu ambayo inaweza kumsababishia matatizo na kama angerogwa na kulikubali ombi langu la kutaka niwe mpenzi wake basi nilikuwa nimemuandalizia zawadi nzuriii ambayo kama ningemkabidhi angenichukia hadi kufa kwake, naam! Hivyo ndivyo ilivyokuwa. Salha hakurudi tena na mimi sikushughulika na yeye wala dada yake abadani.



    * * * *



    Baada ya juhudi zangu za majuma kadhaa, kuumwagilia mti wangu, kuutia mbolea na kuupalilia hatimaye ulizaa tunda murua, Tunda lilinawiri, kupendeza na kuvutia mno lakini ni jinsi gani ya kulichuma hapo ndipo palipohitaji hesabu za hali ya juu sana zaidi ya zile za Magazijuto. Lakini me ni mzoefu bhana ntashindwaje kulila tunda ambalo nimeshalichuma tayari japo ni hatari sana lakini ntakapofanikiwa itakuwa ni raha iliyotukuka.

    Yote hayo nilijiwazia nikiwa njiani kuelekea maeneo ya Kinyerezi.Sehemu ambapo niliweka miadi ya kukutana na Sunshine siku hiyo, ingawa mimi nilikuwa najua nini kinakuja kutokea, Sunshine kwa upande wake sizani kama alifikiria japo kwa bahati mbaya tu nimepanga kitu kama hicho.Kabla ya mualiko huo wa tukutane Kinyerezi kwajili ya kula bata, nilishamualika Sunshine sehemu nyingi tu hivyo halikuwa jambo la kustaajabisha hata kidogo kumualika tena siku hiyo na yeye hakusita kuukubali mwaliko wangu.

    " Uko wapi my sista jamani!" Nilimtext ( nilimtumua ujumbe mfupi) Sunshine mara baada ya kufika ndani ya Lodge matata iliyokuwa ndani ya mtaa huo huku kimoyo moyo nikimshukuru rafiki yangu Amani aliyenielekeza mahali hapo.

    " Am sorry mdogo wangu ndo napanda gari saivi ila hakuna foleni ntafika sasa hivi!" Alijibu Sun ambaye mara zote amekuwa mwaminifu kwangu.

    " Nambie basi utakula nini nikuwekee oda kabisa!" Nilimuhoji Sunshine ili akifika ratiba yangu isichelewe.

    " yaani hadi leo hujajua dadaako anapenda nini!?" Alitania Sun hali iliyonifanya Nione haya kiasi.

    " Samahani boss!" Namimi nilijibu kiutani huku nikimuwekea oda ya chips mayai, mishkaki ya samaki pamoja na soseji kwani ndio vitu anavyopenda huku upande wangu nisiweke oda ya kitu chochote kwani nilikuwa na hamu naye siku hiyo kiasi cha kunifanya hata nikose hamu ya kula.

    " Nimeshafika tayari!" Alinitext Sun nilipokuwa nakikagua chumba kizuri cha suit ( chumba na sebule) nilichokikodi siku hiyo maalumu kabisa kwajili ya mimi na yeye.

    " am coming!"(nakuja) nilimjibu huku nikimfwata aliposhukia chap chap.

    "Wow your looking so mmwah!" Nilimsifia Sun huku nikimpa ki hug ( kumbatio) cha kizushi.

    " thank you!" Alijibu kwa furaha Sun.

    Taratibu mimi na yeye tukaanza kuelekea ilipo Lodge nilimokodi chumba na sikuwa na wasi hata kidogo kuwa angeshtukia kuwa ni Lodge, kwa hatua za awali kutokana na manthari yake kuwa kama hoteli yenye hadhi ya kula vigogo.

    "Leo ndio tutakuwa hapa my dia!" Nilimwambia Sun nilipokuwa nachukua fungua mapokezi.

    "Vyakula vyetu tuleteeni juu saivi enh!" Pia nilimuamuru muhudumu huyo na muda huo Sun hakuwa ameelewa bado nini kinaendelea.

    " Letz go up!" ( twende juu) nilimwambia Sun huku nikimshika mkono kuelekea ghorofa ya pili kilipo chumba chetu.

    "Whaaat!?........Tom??.....unanipeleka wapi!?" Aling'aka kwa hasira Sunshine huku akiuchomoa mkono wake niliokuwa nimeushika.Yote hayo yalitokea baada ya kuona nafungua mlango wa chumba nilichokodi



    Nilitegemea kitu kama hicho kutokea hivyo hali ya Sunshine haikunipa hofu hata kidogo japo ilinitisha.

    " Listen Sun.....!" (Sikiliza) nikiwa nimejipanga kuanza kumwaga sera zangu za kumshawishi Sun ghafla nilisita kutokana na watu wawili waliokuwa wanapita hapo kordoni tulipo, kwa kiasi kikubwa niliwashukuru sana watu hao kwani walimfanya Sun aingie ndani mwenyewe kwani hakutaka kutizamana nao.

    " Tom hii ni nini umefanya lakini?" Sun aliendelea kubwata tulipoingia ndani.Nikiwa nataka tena kujitetea mlango uligongwa hivyo nikaelekea mlangoni.Alikuwa ni muhudumu kaleta vyakula, nikamruhusu aingie ndani kuviweka mezani.

    "Karibu eenh!" Muhudumu huyo alimkarimu Sun alipokuwa anatenga vyakula hivyo mezani pia Sun aliitikia kwa kutikisa kichwa tu.

    Baada ya muhudumu kutoka nilirudi Sun alipo huku nikiwa mpole sana.

    "Karibu ule mamii!" Nilimwambia Sun huku nikimuwekea chakula sawa.

    "Tom?....nimeingia humu kwaajili ya heshima yako tu, wahudumu wasije kukucheka lakini kiukweli sijapenda ulivyonileta hapa hata kidogo....kwani Tom unanionaje mimi!?" Duku duku la Sun lilikuwa bado halijaisha bado alikuwa na hamu na mimi.

    " Basi mama naomba unisamehe tunakuwa kama tumeonana leo bhana!?" Niliongea nikiwa nimekereka na muda huo tayari kichwa kilishaanza kupata moto.

    " Hamna sio hivyo ila ungeniambia mapema!"

    " Aya basi naomba ulee alafu ndio tutaongea!" Nilimbembeleza Sun huku nikiweka chakula sawa.

    "Wee mbona huli!?" Aliuliza Sun ambaye muda wote nilikuwa nikimuhangaikia yeye tu.

    " Nna kazi ya kukulisha wewe tu ukishiba na mimi ntakula!" Nilimwambia Sun huku nikimpa soseji ang'ate.

    "Me ntakula tu na wewe kula!" Mazungumzo ya hapa na pale yalianza kumrejesha Sun katika hali yake ya kawaida na jinsi yeye alivyoanza kuwa kawaida ndivyo na mimi nikaanza kubadilika japo sikujiona lakini niliamini hivyo.

    "Tom vipi wewe!?" Sun aliuliza baada ya kuona sipo katika hali ya kawaida.

    " kwani vipi!?" Badala ya kujibu na mimi niliuliza.

    "Umenyong'onyea alafu macho yako yamekuwa mekundu!"

    " sijisikii poa sana Sun ngoja niagize maji!" Niliongea huku nikiifwata simu ya mezani iliyokuwa chumbani hapo.Baada ya kuagiza maji sikurejea Sun alipo na badala yake nilijitupa kitandani na kulala kifudifudi huku nikipiga mahesabu jinsi ntakavyokula hasara siku hiyo.Chumba vyakula pamoja na zawadi niliyomletea Sun viligonga kwenye laki moja na ushee ukiachilia mbali gharama hizo siku hiyo ni ya Jumapili, siku ya kazi, na niliomba ruhusa kwajili ya shughuli hiyo maalumu ya siku hiyo.Hivyo ukijumlisha na hela ambayo ningepata kazini siku hiyo basi hasara ingefika kwenye laki mbili.Sababu hizo ndizo zilizinifanya kichwa kiniume kwa wakati huo niliwaza sana jinsi Sun akininyima tunda itakavyokuwa tafarani akilini mwangu.



    " Tom!...Tom!?" Ama kweli nilikuwa kwenye fikara nzito hata Sun alipokuja kitandani hapo sikumuona kabisa.

    " amka unywe maji yameshaletwa!" Aliniambia Sun baada ya kufungua macho huku akinifungulia maji hayo.

    " thanx Sun!" Nilishukuru baada ya kuamka na kupiga funda moja kisha nikajilaza tena kama awali, Sun ambaye muda huo alikaa pembeni ya kitanda, alikipakata kichwa chake kw a viganja vya mikono yake, bila shaka kuna jambo zito alikuwa akilifikiria.Taratibu nilipeleka mkono wangu na kuanza kukishika kiuno chake.

    " potelea mbali!...akizingua naita goma (msichana) lingine sasa hivi!" Nilijiwazia nilipokuwa nikiendelea kukitomasa kiuno cha Sun kujaribu bahati yangu.

    "Tom!?" Sun aliita huku akiushika mkono wangu nisimtomase zaidi.Nilihisi anataka kusema nini hivyo sikuitika aliponiita na kwa kuwa nilishaona dalili zote za kunyimwa utamu siku hiyo ikanibidi nimtongoze Sunshine rasmi sasa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Ni kama vile ndicho alichokuwa anakisubiria siku zote kwani licha ya mimi kumtongoza na yeye alinitongoza pia huku akinielezea jjnsi hisia zake zilivyokuwa deep kwangu toka awali.Maneno yake matamu yalisababisha kichwa changu kilichokuwa kikiwaka moto kwa wakati huo kupoa kama vile kimezamishwa kwenye unga wa barafu. Miongoni mwa mambo tuliyojadili wakati tunatongozana ni pamoja na fofauti yetu ya umri pia Sun hakusita kuonyesha hofu yake juu ya wifi yake lakini yote hayo niliyaweka sawa na kumtoa hofu.

    Taratibu nilimvuta Sunshine kitandani na tulianza kutomasana taratibu huku tukinyonyana ndimi zetu na kutengeneza ladha ya ajabu.Baada ya kuhakikisha kuwa ameorojeka vilivyo nilianza kumsaula nguo yake moja baada ya nyingine kwa upande wa juu nilimtoa kiblauzi alichokuwa amevaa hivyo kuzifaidi chuchu saa sita zake zilizosimama na kujaa vilivyo huku ziking'arishwa na rangi nyeupe na kupambwa na chuchu za brown zilizosimama vizuri hakika nilijihisi niko Peponi nilipokuwa nikinyonya maziwa hayo.Nilipojaribu kushuka chini na kutaka kufungua kifungo cha suruali yake alinikamata mkono kwa nguvu kama si yule aliyekuwa amelegea ndembe ndembe.

    "Unataka kufanyaje!?" Sun aliniuliza swali ambalo lilinikata nyege zote.



    Nilihisi Sun ananiletea utani inamana hadi hatua hiyo niliyofikia hakujua nataka kufanya nini ama yalikuwa masihara hayo.Nikaondoka juu ya mwili wake na kujilaza chali pembeni.

    "Tom!?" Sun aliita huku akionyesha shaka na hali yangu iliyobadilika tena ghafla.

    "Yes my dia!" Niliitika bila kufumbua macho.

    " Tumeshakuwa wapenzi sasa naomba tufanye siku nyingine...sawa baby wangu!" Sun alijaribu kunishawishi huku akionyesha kujua nilitaka kufanya nini.

    "Sikiliza Sun...wasichana wengi huona haya kufanya mapenzi siku ya kwanza wanapokutana na mpenzi mpya lakini Sun sisi hatujajuana jana wala juzi, pia nilikupenda kitambo sana ila leo ndio nimeeleza hisia zangu kwako so mi sioni kama kuna tatizo lolote tukifanya leo....Sun nakupenda sana pia naomba ujiamini!" Katika vita vya maneno tu daima huibuka kidedea hasa ukizingatia mimi ni mzoefu wa viumbe hawa, najua nionge nini, niongee vipi na kwa wakati gani. Baada ya blaa blaa za hapa na pale nilifanikiwa kumshawishi Sun anivulie suruali iliyombana.

    Baada ya kuvua suruali yake nakuona mapaja yake myeupe pee yaliyonakshiwa kwa vinyweleo mwanana vilivyolala juu yake hakika shetani wa tamaa alitaka kunitoa roho!. Taratibu nikaanza kuyatomasa huku sehemu zangu nyeti zikidinda na kukomaa maradufu, hakika Sunshine alikuwa mrembo wa haja na nyege zake zilikuwa ni hatari mara mia ya zangu kwani zilipompanda alinikamata kwa nguvu huku akininyonya sehemu mbalimbali za mwili wangu bila kubagua na alipofanikiwa kuupata ulimi aliunyonya kama vile anataka kuung'oa, kusema kweli sikuwahi kunyonywa hivyo kabla ya kukutana naye.Kadrii muda ulivyokwenda ndivyo hali yake ilivyozidi kuwa mbaya na kama nisingempatia huduma ya kwanza mapema huenda angepata ugonjwa wa uchizi.Sikuweza kubaini mara moja kuwa nguo zangu nilizivua mwenyewe ama nilivuliwa hata chupi ya Sun iliyokuwa imesalia mwilini mwake sikujua ilitoka vipi ila muda huo viungo vyetu vya siri vilikuwa vikisagana na kutupatia utamu wa ajabu uliotuhamisha sayari hii inayoitwa dunia na kutupeleka ulimwengu mpya wa burudani.Baada ya purukushani hizo za vuta nikuvute zilizodumu kwa takribani dakika kumi hatimaye nilifanikiwa kufungua champigne ( kufikia mshindo).

    "Woooh oooh oooh!!" Nilidiha huku nikihema kwa kasi nilipokuwa naichomoa mashine yangu toka kwenye utamu wa Sun.

    "Pole baby!" Nilimwambia Sun nakumbusu kwenye paji lake la uso.Shughuli haikuwa ndogo.



    Baada ya kupumzika kidogo hatimaye nilikumbuka kama kuna kiyoyozi maana japo tuliweka nyuzi 16 za baridi lakini haikufurukuta kulizima joto lililozalishwa na miili yetu.Nazani joto hilo lingetumika Kuzalisha umeme basi zingetoka megawati nyingi sana.

    " Twende tukaoge!" Baada ya kukaa kimya kwa muda hatimaye Sun aliongea huku akinyanyuka kitandani sikuwa na la kufanya zadi ya kumfwata nyuma huyu malkia wangu.Kitaulo alichojifunga kifuani mwake na kuacha eneo lake kubwa la mwili likiwa wazi kilinifanya niuone uzuri wake wa ndani ambao sikuwahi kuuona kwa mtu mwingine.Tulipokuwa bafuni hakuna kilichofanyika zaidi ya kumwagiana maji na michezo ya hapa na pale.

    Baada ya kuoga tulirudi tena chumbani na hapo ndipo nilishuhudia maajabu ambayo yalinifanya nipikiche macho kwa kutoamini kile nilichokiona.Ilikuwa ni ajabu lakini ni dhahiri.



    Nakumbuka vizuri kabisa nilipoingia chumbani hapo kitanda kilitandikwa kwa mashuka mazuri meupe.Lakini kilichonishangaza muda huo ni baada ya kuona mashuka hayo meupe pee! Yakiwa yamenakshiwa kwa madoa doa mekundu.Je ni nani aliyoifanya kazi hiyo mie na mpenzi wangu tukiwa bafuni.

    " Baby ulikuwa bikra!?" Nilimuuliza Sun kwa furaha nikiwa siamini macho yangu lakini Sun alinitumbulia macho ya haya pasina kujibu kitu.Wahenga walisema kimya nacho ni jibu.Maumivu ya mashine yangu iliyopata tabu kupenya kwenye utamu wa Sun jumlisha maumivu ya mikwaruzo ya kucha iliyotapakaa mgongoni mwangu ilitosha kuthibisha kuwa nimemtoa Sun bikra.Sikuwahi kukutana na mechi tamu kama ya siku na niliona ufahari mkubwa sana kumtoa mlimbwende huyo bikra hasa ukizingatia kimekuwa kitu adimu kukipata kama nyoka mwenye miguu.Siku hizi binti wa miaka tisa tu ashaiuza siku nyingi.

    " Sun nashindwa kueleza ni jinsi gani nakupenda!" Nilimwambia Sun nilipokuwa natoa shuka hilo lililochafuka na kutandika lingine lililokuwa limekunjwa vizuri nazani lilikuwa maalum kwaajili ya kujifunika.

    " Nakupenda zaidi Tom wangu!" Alijibu Sun huku akinisaidia kutandika shuka.

    Kadrii muda ulivyozidi kwenda ndivyo nilivyojikuta naanza kufall inlove (kuzama kwenye pendo) kwa Sun.Tukiwa tunacheza cheza kitandani nilimuangalia bila kummaliza, hakika niligundua uzuri wa ajabu kila nilipomtazama mrembo huyu. Na kwa kuwa nilishajua ni mgeni wa ngono sikutaka kuviapply (kuvitumia) vitu nilivyocopy toka kwa mtoto wa kitanga kigamboni.Nilitaka nimpeleke taraatibu aenjoy huba langu.Tukiwa bado tunacheza kitandani Sun alipenyeza mkono wake na kushika mmea wa asili ulioota katikati ya mwili wangu.kadrii alivyozidi kuichezea kwa vidole vyake ndivyo ilivyozidi kujaa na kuwa kubwa.waungwana tunasema mmea umestawi.

    " hiiii! mbona inakuwa kubwa sasa!" Sun aliishangaa wazi wazi, hakika alionekana ni mgeni wa kitu hiyo.

    " Utakoma nani kakwambia uichokoze!" Nilimtania.

    "Unajua hata yako nikiichezea inakuwa kubwa!?" Nilimuuliza Sun kwa kumtega!

    "Uwongoo!" Alijibu kama mtoto huku akiwa amebetua mdomo wake kimikogo.

    " Can i prove it!?" ( nithibitishe) niliuliza kimombo kwa pozi naye akajibu ndiyo kwa kutikisa kichwa.

    Taratibu kama vile nazamia chumvini nilishuka kati kati ya mapaja yake na kuanza kuyachezea mashavu ya utamu wake hali iliyomfanya ajimwaye mwaye na kujinyonga nyonga kitandani.Kama hiyo haitoshi niliukamata vizuri mpini wangu na kuanza kuupalaza kati kati ya utamu wake hali iliyofanya kisimi chake kusimama kama kidole cha mtoto mdogo.

    " Unaona!?" Nilimwambia Sun ili akiangalie kisimi chake vile kimetuna lakini kwa bahati mbaya hakuweza hata kunyanyuka na akabaki akiguna tu.Urojo tayari ulishakilowesha kitumbua cha Sun na nilipojaribu kuupalaza tena mpini wangu juu juu uliteleza na kuzama ndani.

    " mmmh mmmh mh!" Sun aligugumia kimya baada ya kumzamishia mpini huo, kama vile nachonga njia taratibu nilianza kusugua upande wa kulia kidogo, kushoto kidogo, juu na chini pia sikupasahau.Njia ilikuwa ni nyembamba na ilikuwa imenibana sana hivyo kitendo cha kufanya hivyo hakikunichukua dakika saba nikawa nimefungua champigne nyingine ( nimepiga bao)

    " Oooh thanx my Sunshine and my moon light!" Nilimshukuru Sun nikiwa nimelala pembeni.Hakujua kwanini namshukuru lakini vitu alivyonipa siku hiyo ni kabambe.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Baada ya ungwe hiyo ya pili kumalizika tulikumbatiana na kulala pamoja.Toka saa kumi za jioni usingizi ulipotupitia tulikuja kushtuka saa mbili za usiku.

    "Sun!?...Sun?" Niliimuita Sun huku nikijikwamua toka kwa mikono yake aliyokuwa amenikumbatia.

    " niiiini!?" Aliniuliza akiwa amekunja sura kuonyesha nimemkatili usingizi wake mnono.

    " Amka usiku umeingia!!" Nilimuhamasisha naye akajizoa zoa kuamka kisha tukaelekea tena bafuni kuoga kwa mara nyingine.

    Baada ya kurudi kila mtu akaanza kuokota nguo zake zilipokuwa.

    " Tafadhali naomba uvue mamii!' Nilimuamuru Sun huku nikimsaidia kuvua chupi yake nyeupe iliyopambwa kwa makopa ya njano sanjari na neno I love you.Sun hakujua nataka kufanya nini ila hakunizuia kufanya nilichotaka.

    " Wee vaa hii!" Nilimwambia huku nikimpa boxer yangu na mimi nikivaa chupi yake.Kitendo hicho hakikumshangaza sana Sun kwani tangu nimejuana naye sikuwahi kuacha vituko.Hatimaye tuliondoka kwenye Lodge hiyo huku nikivuta picha muhudumu atakavyotukana baada ya kukutana na shuka liliongezewa mapambo.



    Siku hiyo niliporudi nyumbani nilikuwa na furaha isiyo kifani pia sikutaka kukaa karibu na mtu yeyote asije akahisi kitu.Nikaelekea chumbani kwangu moja kwa moja, niliivua ile chupi ya Sun na kuiandika tarehe na mwezi wa siku hiyo kisha pale kwenye maandishi ya 'i love you' chini yake nikachora jua linaloangaza nikiwa na maana ya Sunshine, Kisha nikaikunja vizuri nakuiweka kwenye droo langu la vitu nyeti kuifanya kuwa kumbu kumbu muhimu, nikavuta pumzi ndefu nakuiachia baada ya kuwaza kuwa nilipanga nimuonje Sunshine kisha nisepe.



    Ivi inawezekana vipi mtu azindue nyumba kisha aishi ndani yake siku moja tu na atake kuhama?.Kama ningeishikia bango ahadi niliyoupa moyo wangu kuwa ntatembea na Sun mara moja tu kisha niachane naye basi ningekuwa mchoyo wa fadhila na kukosa ubinadamu hivyo kiapo kingine nilichoupa moyo wangu kwa wakati huo ni kwamba nitaachana na Sun mara baada ya kulala naye mara zingine tatu.Baada ya hapo hata nikiachana naye itakuwa sijamtendea vibaya. Kinyume na matarajio yangu na vile nilivyokuwa nimepanga mara ya mwisho kama nakumbuka vizuri nilichoka kuhesabu nnapokutana kimwili na Sun nikiwa nineshalala naye mara kumi na saba, kutupilia mbali zile tatu zangu nilizokuwa nimepatana na moyo wangu.Ama kweli mapenzi hayajaribiwi.Kadrii nilivyokuwa namtafutia Sun sababu nimbwage ndivyo alivyozidi kunipa sababu za kuwa naye.Wakati mwingine kosa nilifanya mimi na msamaha akaomba yeye ali mradi tu penzi letu lisifike kikomo, Tupilia mbali utamu wake tuwapo kitandani, Sun alikuwa ni msichana anayejitambua na kuelewa ni jinsi gani ya kuishi na mume, hata sijui alijifunzia wapi mambo hayo.Lakini nafikiri hii huja yenyewe( automatical) mtu anapokuwa na mapenzi ya dhati.Me nikiwa najitahidi kumfanyia visa na vimbwanga.Yeye alijitahidi kunijali na kunipenda mfano siku moja niliamka sijisikiii kuwasiliana naye kabisa, alituma meseji bila kujibiwa badala ya kutuma meseji ya malalamiko ama kutishia kuachana kama wafanyavyo wasichana wengine alichofanya yeye ni kuziunga line (sim card) zangu zote mbili na vifurushi vya mwezi.Haya sasa hapo nitasingizia nini tena! Sina vocha(credit) ama muda wa kumjibu meseji zake.Kiukweli penzi la Sun lilikuwa ni zito hata shetani asingemudu kulibeba.Jaribio pekee alilowahi kunifanyia Sun ili kujua kama kweli namjali, aliniomba kiasi cha pesa mchana na nilipompatia jioni aliniita na kunirudishia mara tatu ya kiasi nilichompa.Je ni mwanaume gani mwenye akili timamu anaweza kuachana na Sun?.Bila shaka hakuna na hicho ndicho kilichonifanya na mimi pia kubwaga manyanga yangu na kuamua kutulizana kwa kimwana huyu.Kutoka ile mara moja ya kulala naye kisha tuachane sasa tulikuwa tukihesabu miezi kwenye penzi letu lililokuwa likizidi kunawiri na kushamiri kila uchwao.Nani angeweza kulivunja pendo hili imara?. Pendo nililotaka kulikimbia mara chungu mzima lakini juhudi zangu zote zikagonga mwamba na kuangukia pua,Hivyo nikaamua kutulia ndani ya pendo hilo baada ya kung'amua kuna minyororo mizito ya upendo niliyofungwa.Minyororo ambayo isingekatika kirahisi hata kwa moto wa gesi.



    "Sunshine umenishika nikakamatika mpenzi wangu!" Siku moja nilijikuta nikimnong'oneza hivyo Sun wangu tulipokwenda kwenye mkahawa mmoja kwajili ya chakula cha jioni.Sikumwambia hivyo ili kumfurahisha ila ni hali halisi niliyokuwa najisikia toka moyoni mwangu.Mapenzi ya dhati ndiyo yakawa maisha yangu na Sun toka nilipoamua kunyosha mikono juu na kutulia na yeye tu mpaka Siku moja Changamoto kubwa ilipokuja kulitikisa penzi letu.



    Ni takribani wiki moja imepita toka simu yangu ipokee ujumbe mfupi toka kwa Lisa.Ujumbe uliokuwa umeandikwa kwa maneno mengi ya kiingereza, Lisa akiwa anaomba radhi kwa yale yaliyotutenganisha na kuomba nafasi nyingine ya kulijenga penzi letu.Ingawa nilisoma mengi katika ujumbe huo, machache yaligoma kutoka kichwani na yalikuwa yakijirudia rudia kila mara.Japo maneno hayo yaliandikwa kwa kiingereza kilichofupishwa mno lakini yalikuwa na maana hii kwa kiswahili ' usinihukumu kwa jinsi nilivyokuwa jana kwasababu nimebadilika na siishi tena kama jana ila nihukumu kwa jinsi nilivyo saivi!'. Mengi yaliandikwa lakini kauli hiyo ilionekana kubeba maudhui mazima ya ujumbe huo.Sasa nimuhukumu sasa hivi Lisa kwa kosa gani haswaa wakati makosa yake yote yalikuwa ni ya nyuma na hataki yajirudie.Ujio wake Lisa kwa mara nyingine tena kwangu ilikuwa ni changamoto kubwa kwani nakiri sikuwahi kumpenda msichana mwingine yeyote kwa kiasi ambacho nimewahi kumpenda yeye, Mara zote nimekuwa kama mfupa kwa fisi mbele ya pendo la Lisa.Ningekuwa naamini uchawi hakika binti huyu angekuwa amenilisha limbwata. Tofauti na mara nyingine nilipoachana na Lisa kurudiana ilikuwa rahisi sana lakini kwa safari hii mambo yalikuwa tofauti kidogo.Palikuwa na kizingiti kikubwa na kigumu kung'oka kilichoitwa Sunshine.Sunshine ananipenda hadi naogopa! Nilishafanya visa chungu mzima lakini kuachana ilishindikana.Japo avumaye baharini ni papa lakini wengine nao wamo vivyo hivyo avumaye moyoni mwangu ni Lisa lakini Sunshine naye hakuwa wa kubeza hata kidogo.

    Kiukweli walimbwende hawa wawili waliniweka njia panda nisijue pa kuelekea.

    Meseji alizokuwa anatuma Lisa kila siku usiku na mchana tayari zilishaanza kuulemea moyo wangu, nikajihisi simtendei haki mpenzi wangu huyo wazamani kwa kuendelea kumzungusha nisimwambie nimemsamehe au la!

    Kwa kawaida nnapokuwa njia panda katika kufanya maamuzi huwa napenda sana kujumuika na wenzangu katika ibada.Hata siku ya mapumziko ilipofika niliwahi kanisani nipate kutuliza yangu nafsi na siku hiyo ikawa kama vile nimeenda kujichoma mwenyewe kwani hubiri la siku hiyo lilihusu upendo.Wengi wanapenda lakini hawazijui kanuni za upendo.Siku hiyo nilipata kuzijua kanuni za upendo zilizoandikwa na Wakorintho.

    Kwanza kabisa Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Baada ya kuzijua kanuni hizi za upendo nilijiona kama mwenye hatia.

    Nakumbuka siku kadhaa zilizopita Lisa alihoji kama bado nampenda na mie nikajibu bila shaka.

    Sasa iweje bado nafikiria mambo mabaya aliyonitenda ili hali upendo hauhesabu mabaya?

    Iweje nione Lisa aliniumiza hali yakuwa upendo hauoni uchungu??

    Kama nikisema simpendi Lisa mdomo utakuwa umeudanganya moyo na si ajabu mdomo ukapewa ububu na mkono ukalithibitisha hilo kwa maandishi.

    Maneno yote muhubiri aliyokuwa anasema siku hiyo ni kama vile alikuwa ananisema mimi, Muda mwingine nilitamani hata kutoka nnje nisisikie maana kile neno lililonenwa lilitangaza hatia juu yangu. Hadi mwisho wa somo ulipofika moyo wangu ulikuwa umepondeka vya kutosha na siku hiyo nikapanga kufanya maamuzi.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Sikutaka tena kusita sita kwenye njia mbili.Jioni ya siku hiyo nilimuomba Sunshine tuonane ili nimueleze vile nimeamua.



    Kama kawaida jioni ya siku hiyo nilienda mtaani kwao Sunshine na tukakutana katika eneo ambalo tumekuwa tukifanyia vikao vyetu vya jioni toka tumejuana, isipokuwa tu siku hiyo ilifanywa tofauti na maongezi yake, siku zote tumekuwa tukijadili mipango na malengo ya maisha yetu huku tukifurahi na kucheka lakini kwa siku hiyo vinatawala vilio, masikitiko, majuto, hasira, simanzi pamoja na dukuduku, hiyo yote ni baada ya kumuweka bayana Sunshine juu ya kinachoendelea kati yangu na Lisa.Sunshine alionekana kutoamini chochote nnachomwambia hiyo ni kutokana na kuzoea baby wake ni mtu wa utani kila mara, lakini mara baada ya kumthibitishia kuwa nnachomwambia sitanii ndipo kilio kilipoibuka na maneno ya kunialaumu sana, nilimuonea huruma Sun lakini sikuwa na la kufanya, hakuna lugha yeyote nzuri unayoweza kumueleza mpenzi wako anayekupenda sana kuwa muachane naye akakuelewa. Kitendo bila kuchelewa nilimuona Sun chini akiwa kapiga magoti huku akiniomba aongee na Lisa amuachie mpenzi wake, bila Tom yeye hana maana ya kuishi tena kwenye hii Dunia.Kitendo hicho alichokifanya Sun kiliushambulia moyo wangu mithili ya kuku wa kuenyeji waliomwagiwa mchele.Sun hakuwa na kosa lolote hivyo ilikuwa ni haki ausulubu moyo wangu.Hakuna kazi ngumu kama kuachana na mpenzi ambaye hajawahi kukukosea kitu ila mithali niliyoitumia mahali hapo ni hii, ukitaka kumuua Nyani usimuangalie usoni.

    " Tom naomba unisindikize kwetu, sina nguvu!" Hiyo ni kauli ya mwisho aliyoitoa Sun baada ya kushindwa kunisihi nisimuache.Taratibu nikamuinua Sun toka chini alipokuwa nikauweka mkono wake begani mwangu na kunza kumsindikiza kwao. Mapenzi yanaweza yakaua niliamini siku hiyo.

    Baada ya kumfikisha Sun mahali ambapo aliniruhusu nimuache taratibu nilianza kurudi nyumbani huku njia nzima nikifiria maisha mazuri tuliyoishi na Sun na hatimaye historia hiyo nzuri inafungwa kwa mwisho mbaya.Sikuwa na la kufanya zaidi ya kufumba macho, moyoni nilimpenda sana Lisa pamoja na mifarakano yetu ya mara kwa mara pia Lisa alinipenda sana mimi.Barabara hata iwe ndefu vipi haikosi kuwa na kona. Japo Sun naye nilimpenda sana kutokana na mapenzi yake ya dhati kwangu lakini maisha tuliyoishi na Lisa toka utotoni yalinichanganya zaidi, ni kifo pekee ambacho kingenitenganisha na huyo mtoto kwani yeye alikuwa ananijua mimi nnje ndani lakini pia mimi nilimjua yeye hata pengine zaidi ya anavyojijua.



    Hatimaye siku hiyo iliyoututenganisha mimi na kipenzi changu Sunshine ilipita salama salimini lakini siku mbili baada ya hiyo kupitai ikawa na walakini.

    Ni majira ya saa kumi na moja za alasiri jua likiwa limechoka kuwachoma walala hoi na kuanza kutafuta machweo ili lipate kupumzika ndipo na mimi ambaye nilikuwa nimejipumzisha nyumbani muda mfupi baada ya kutoka shule kelele za simu yangu zinasitisha mapumziko ya akili na naamua kuipokea simu hiyo ambayo imepigwa na mtu nnayemfahamu sana. Naipokea kichovu lakini mara tu baada ya kusikia kilichozungumzwa nakurupuka na kuanza kujiandaa kuelekea mahali nilipoitwa.





    " Hapa hadi Sinza bei gani!?" Nilimuhoji dereva wa boda boda kuona kama naweza kuelewana naye bei, kwa haraka niliyokuwa nayo nisingeweza kukaa kwenye foleni hata kidogo hasa ukizingatia kuwa muda huo ni jioni na wakazi wengi wa jiji hili wanatumia barabara chache kurudi makwao.

    " Shachukua boda boda dakika sifuri tu ntakuwa hapo mwanangu!" Nilimpa tumaini rafiki yangu Amani mara baada ya kunipigia tena ili kujua nimefikia wapi katika safari hiyo.

    Kiukweli Amani alikuwa ni rafiki yangu kipenzi tuliyeshibana sana.Kwa kiasi kikubwa shida zangu zilikuwa zake hali kadhalika zake zangu.Hata aliponipigia simu niende nyumbani kwake haraka, niliianza safari bila kufikiri mara mbili mbili.

    " sasa atakuwa na nini huyu Amani asichotaka kuniambia kwa simu!?" Nilijiuliza mwenyewe kwa sauti ya chini iliyobebwa na kasi ya upepo uliopambana na boda boda.

    Ki ukweli toka nimeachana na Sunshine, nimekuwa sina raha wala amani kabisa hasa ukizingatia hali niliyomuacha nayo, hata ningesikia amekunywa sumu nisingeshangaa sana kwa maana hali hiyo ilimruhusu kufanya hivyo. Japo aliyeeniita ni rafiki yangu Amani lakini akili yangu yote ilikuwa kwa Sunshine.Na sikujua hata kwanini niliposikia jina lake moyo wangu ulinipasuka.

    Nikiwa katika hali hiyo ya sintofahamu hatimaye tulifika nilipokuwa nikienda, nilimlipa dereva ujira wake kisha kwa mwendo wa kasi nilianza kutembea huku nikiambatana na hofu kuelekea ilipo nyumba anayoishi Amani.Hatua chache kabla ya kufika nilimpigia simu, sikutaka kwenda moja kwa moja kichwa kichwa kuhofia kujilengesha.

    " Oya njoo basi nipo hapa kwa Mangi tukutane!" Niliongea haraka haraka baada ya Amani kupokea simu yangu, kwa akili zangu za haraka haraka nilijua Amani angenilazimisha kufika kwake lakini nilishangaa utayari wake wa bila kusita sita kuja nilipo hivyo na mimi ambaye nilikuwa nikipima maji kwa wakati huo kujua kina chake nikafanya bidii ya kufika kwa Mangi ili tuonane!.

    Punde si punde Amani naye akawasili,kwa Muonekano wake wa haraka hakuwa mtu mwenye utulivu kabisa na nywele zake zilikuwa zimevurugika sana. Rafiki yangu huyu anapokuwa na jambo linalomchanganya akili hupendelea kukuna kichwa nilifikiri hiyo ndo sababu ya nywele zake kuvurugika.

    " oyaah! Vipi kaka!?" Nilimuhoji kwa shauku Amani aliyeketi na kushika tama kanakwamba anafikiria aanzie wapi.

    " Dah! Mwanangu yaliyonikuta we acha tu!"Amani alianza kufunguka taratibu huku akiweka kiti chake vyema kunipasha habari.

    "Mwanangu shem wako ndio ananiumiza kichwa………sijui kazinguliwa nini kwao kabeba kilicho chake nimemkuta gheto……sasa sijui inakuwaje hapo mwanangu!" Amani aliongea kwa kifupi huku akionyesha ana mengi ya kusema. Kesi yake nayo ilikuwa ni ile ile iliyonikuta mimi siku chache zilizopita'mapenzi' isipokuwa tu kesi hizi zipo tofauti kidogo.

    " Hahaha! Amani bhana…mimi hapo sioni tatizo kwani si mnapendana?……sasa tatizo liko wapi hapo,shem wangu amehamia kwako muishi pamoja!" Niliongea kiutani huku nikijifanya namaanisha nilichokisema hiyo yote ni katika kumchota akili Amani nijue yupo mlengo gani kabla sijampa ushauri kamili.

    " Aaah! Tom mwanangu yaani unaongea kama vile huijui familia yao vile walivyo mabandidu! wee unafikiri kama watakuja kuniletea zogo maskani pale itakuwaje, hata hivyo pamoja na kumpenda sana shem wako hatukupanga kuishi pamoja kwa wakati huu!" Amani aliongea kama vile ananilalamikia.

    " Kwaiyo ndugu yangu wee unataka nifanye nini!?" Nilimuhoji Amani ili nimpe ushauri anaoutaka.

    "Tom nimeshakueleza kila kitu wee si mtu wa kuniuliza swali hilo!" Amani aling'aka.

    " Je utaridhia nnachotaka kukifanya!?" Nilimuhoji tena naye akanijibu ndio kwa kutikisa kichwa baada ya kufikiri kwa muda.

    " Si yupo nyumbani saivi?" Tena niliuliza naye Amani akanajibu ndio.Tukasimama pamoja na kuelekea kwake.Kuna usemi usemao ukitaka kuonekana mjinga basi ingilia mapenzi ya watu siku hii sikuujali usemi huo nnaouzingatia kila mara ili kumuokoa rafiki yangu Amani.

    " Mambo vipi shem!?" Nilimsalimu mpenzi wake Amani aliyekuwa kajilaza kwenye sofa naye akaitikia poa bila kunitizama.

    "Unaweza kutupisha dakika sifuri tafadhali!" Nilimuomba Amani kwa kumnong'oneza naye akatuacha sebuleni peke yetu.

    "Japo umenijibu poa lakini naamini si poa unaeza kuniambia nini kimetokea mpenzi wangu!?" Nilianzisha mazungumzo na shem wangu ambaye tumezoeana kuitana majina yote ya kimapenzi na huenda yupo huru kwangu zaidi kunieleza mambo yake kuliko afanyavyo kwa Amani.

    Baada ya kumuuliza swali hilo alikaa kitako na kunieleza yote yaliyotokea hadi yeye kuchukua maamuzi hayo ya kukimbia kwao na kuhamia hapo.Kesi yake haikuwa kubwa sana ila nadhani aliondoka kwa kuwa alikuwa na pakwenda.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Hivi unampenda Amani kweli!?" Nilimuuliza shem naye akajibu ndio.

    "Me nadhani humpendi! Na kama unampenda kweli basi usingemsababishia matatizo yasiyo na lazima.……hivi unadhani wazazi wako wakisikia umekuja kwake na umezinguana nao watampenda kweli? Si ndio wataona yeye anakupa kiburi na kukufanya uwadharau wao.Ukiachana na hilo ili mfanikiwe kimaisha na kuwa na maisha bora ni lazima muwe na baraka za wazazi hebu nambie maisha yenu yatakuwaje iwapo kila siku wazazi wako wanawalaani juu ya mlichokifanya……unadhani maisha yenu yatakuwa vipi zaidi ya mifarakano isiyoisha kila kukicha na kuandamwa na mabalaa.Kitu pekee nnachokushauri mpenzi wangu rudi nyumbani, mtoto akinyea mkono haukatwi wazazi watakusamehe na watafurahi pia.Kinyume na hapo neno langu sio sheria lakini hamtakuwa na kesho nzuri."

    Tuliongea mengi na shemeji yangu huyo na mwisho wa siku alinielewa na akakubali kurudi nyumbani kwa roho moja.Hivyo nikawa hakimu mzuri kwenye kesi hiyo hakuna nilichokuwa nimebakiza zaidi ya kurudi nyumbani huku nikimuacha Amani amsindikize mpenzi wake kwao.



    * * * *



    Baada ya miezi kadhaa kupita kimya kizito kilitawala kati yangu na Sunshine.Kwa upande mwingine nilifurahishwa na kimya hicho kwani kilimaanisha Sunshine amekubaliana na matokeo.Nilifurahi kwa kuwa wakati mwingine mtu akikupenda sana ukimgeuka anaweza kufanya jambo baya, nashukuru kwa kuwa hali hiyo haikutokea.Kimya cha Sunshine kilimaanisha penzi langu na Lisa kupamba moto.Tulikuwa tukipendana sana kama vile hatukuwahi kuchukiana.

    Siku moja tukiwa tumechati mno kwa njia ya meseji roho yangu ilinituma kumuuliza Lisa swali ambalo sikujua kwanini roho imenisukuma hivyo.

    ' Babe bado unanitunzia mali yangu?' Niliuliza swali hilo kwa ujumbe mfupi huku nikiamini Lisa bado atakuwa na bikra yake niliyokuwa niki ilea lea kuitoa.

    "Mali gani hny?" Lisa alijibu na kuonyesha kuwa hajanielewa.

    " Bikra swtheart!" Nikaweka mambo hadharani.

    "Bby m sorry bt tulivyoachana nilikuwa na hasira hivyo nikapata boy mwingine akaitoa then akanisaliti.Tom i luv u so much baby cz ur alwayz there 4 me!" Lisa alijibu maneno mengi lakini jibu likiwa ni moja tu! Ile bikra niliyomuacha nayo hakuwa nayo tena.Ghafla nakajikuta nakosa hata nguvu ya kushika simu na kuandika neno lingine la ziada.Meseji ya Lisa iliupa moyo wangu tabu zaidi ya mawimbi makali kwa mashua iliyopo katikati ya bahari.Nikashindwa kuamini na kufikiri Lisa ananitania kwa maana kwa kiasi kikubwa nilikuwa nimemrithisha tabia ya masihara.

    ' Come on baby stop joking!' Baada ya kufikiri inaweza kuwa utani nilipata nguvu ya kumtumia Lisa ujumbe mwingine ili kuthibitisha kama ni kweli.

    " Sure bby m nat lie!" Lisa akathibitisha kuwa ni kweli.

    Maskini hali yangu ikawa mbaya ghafla nikavuta picha na kumuona kidume alivyokuwa akishughulika kuitoa bikra ya mpenzi wangu, hakika niliumia sana.Mapigo ya moyo yalienda kasi sana kwa wakati huo sikuweza kufahamu mara moja ni nini kimenisibu ila baada ya muda mchache kupita ndipo nilibaini kuwa toka ile asilimia mia niliyokuwa nikimpenda Lisa sasa ilisalia asilimia hamsini peke yake hiyo ilimaanisha kuwa penzi limegawanyika kati kwa kati.Bora usikutane na bikra kuliko ukutane naye akiwa bikra afu itolewe na mtu mwingine sidhani kama ningeweza kuvumilia tena aina yeyote ya maudhi toka kwa kimwana huyo niliyewahi kumpenda kwa moyo wote.Kama ningekuwa na uwezo basi ningelirudisha penzi langu kwa Lisa lau lifike japo asilimia tisini lakini shida moja ya moyo huwa haupangiwi. Japo Lisa alijiamini kunieleza ukweli kwa kuwa aliamini ningeendelea kumpenda sana lakini alijidanganya, kwa wakati huo ni bora hata angenidanganya ilitoka akiwa anaendesha baiskeli kama wadanganyavyo wasichana wengine lakini ndio hivyo tena maji yalishamwagika,Majira na nyakati vikaendelea kusogea huku bendera ya penzi letu ikipepea nusu mlingoti, tayari Nilishamshusha Lisa thamani na sasa sikuwa mwepesi tena kwake kama ilivyokuwa mwanzo hata kumuita sweetheart nilihisi naidhulumu nafsi yangu."Lakini na mimi mbona nilimtoa bikra Sun!" Wakati mwingine nijikuta najiuliza hivyo ili kuushawishi moyo wangu uendelee kumpenda Lisa kama awali lakini moyo ulionekana kutodanganyika





    Sikuwahi kufikiri hata siku moja kuwa hata mapenzi ya dhati huwa yanafikia tamati lakini jambo hilo sasa lilikuwa dhahiri.Lisa ambaye alikuwa akiuchafya moyo wangu kiasi cha kuninyima hata usingizi leo hii alikuwa hanitishi kwa lolote, Ni ajabu lakini ni kweli kuwa sasa Lisa hakuwa na tofauti yeyote na wasichana wengine mbele ya mboni za moyo wangu.Kama ilivyo ada hakuna anayesalia ukumbini mara baada ya karamu kuisha vivyo ndivyo ingekuwa ngumu kwa mimi kubaki na Lisa hali yakuwa daraja la mapenzi lililokuwa likiziunganisha nyoyo zetu lilishavunjika. Ni rahisi sana kuvumilia kifungo cha miaka mia jela kwa kesi ya kusingiziwa lakini si rahisi hata kidogo kubaki na mtu moyo uliomtema.Hali hiyo ndiyo iliyonipelekea siku moja majira ya jioni kuandika waraka mfupi niliomtumia Lisa kumjuza kuwa nimejiuzulu katika penzi lake.Sikuweza kutambua mara moja ni kwajili ya mshtuko, kutoamini ama maumivu lakini Lisa alikaa kimya siku mbili kabla ya kuujibu waraka wangu.Hadi mara ya mwisho kabla ya kumtumia waraka huo tulikuwa bado tukiishi vizuri na sikuonyesha dalili yeyote ya kumpiga chini, kanuni moja iliyokuwa ndani yangu ni hii, naweza kuchukia jambo baya leo lakini nikalichukulia hatua baada ya wiki mbili hata Lisa niliachana naye wiki kadhaa nyuma lakini nilimjuza baadaye sana.

    Katika kimya chake Lisa hakukaa hivi hivi ukiona kobe kainama jua anatunga sheria, alitumia muda huo vizuri kutengeneza meseji ndefu iliyokuwa na maana ya kutoridhika na maamuzi yangu ya kuachia ngazi lakini aliiandika kwa namna ya kukubali niondoke, mfumo huo mie nauita ' staki natataka'.Tofauti na meseji nyingine Lisa alizokuwa akiniomba turudiane tulipoachana mara kadhaa hapo nyuma, ujumbe huo wa siku hiyo haukuwa na uzito wowote mbele ya macho yangu na nilipokuwa nikiusoma ulinichekesha mithili ya katuni za Madenge.Baada ya moyo wangu kuridhia kuwa huo ni mwisho ambao hautakuwa na mwendelezo mwingine na Lisa niliamua kumjulisha Antie yangu kipenzi kuwa Lisa si mkwewe tena.Mara moja nilitafuta namba zake na kumpigia.

    "Hello!" Baada ya simu kupasua anga na kukanyaga mawingu ya Tabora niliisikia sauti nzuri ya Shangazi yangu.

    "Hello Antie za huko!?"

    "Mtoto mbaya wewe au Dar umepata Antie mwingine!?" Shangazi badala ya kupokea salaam yangu alikimbilia kwenye lawama na ilikuwa haki yake kunilaumu kwani tangu nimeondoka Tabora tumekuwa tukiwasiliana kwa mbinde.

    " Lakini hata wewe umenisusa sana Antie yangu vipi lakini Uncle yuko poa!?"

    " Yupo poa vipi mkwe wangu yupo!?" Kwenye salaam tu Antie akawa amepagusa nilipopataka.

    "Me mbona single boy kitambo tu hadi nimesahau yaani!"Nilimjibu kimzaha shangazi.

    "Hahaha we Tom haukui tu!?" Shangazi alijua nafanya masihara yangu.

    " Kweli Auntie! Lisa tushaachana!"

    "Weeh! Usiniambie……tatizo nini lakini!"

    "Lisa bado ana akili za kitoto Antie!…nasubiri akue kue kidogo tunaweza tukafanya maisha!" Nilimueleza shangazi katika sentensi moja iliyobeba mambo mia huku nikimpa tumaini ambalo halikuwepo kwani sikuwa na mpango tena wa kurudiana na Kimwana yule.

    "Jamani nyie!… mmenisikitisha kweli yani jinsi mlivyokuwa mnapendana vile mmeaachana au Lisa kakuacha Tom niambie nikusaidie!" Shangazi alionyesha wazi masikitiko yake huku akizani huenda Lisa ndio kaniacha lakini nilipomueleza kuwa mimi ndo nimembwaga aliishiwa nguvu kabisa.Nadhani shangazi alikuwa akiufikiria uzuri wa sura,umbo na rangi nzuri ya Lisa lakini hakujua noti hata ipambwe vizuri vipi kama haina thamani hakuna atakayeijali.



    * * * *



    Tangu nimeyajua mpapenzi sikuwahi kuwa mpweke ( single) kwa muda mrefu.Baada ya kuachana na Lisa nilihisi bado nahitaji mapenzi.Ulimwengu huu umejaa walimbwende wa kila namna vipi kidume aliyekamilika kama mimi niishi peke yangu? Wakati Duniani penyewe naishi mara moja tu. Bila shaka haikuwa na haja ya kufanya hivyo.Ni muda mfupi baada ya kujiunga na chuo cha ardhi ili kupata stashahada katika uchoraji wa ramani na hii ni baada ya kuhitimu A level.Katika chuo hichi napata fursa ya kukutana na vimwana wenye uzuri na sifa za kila namna lakini nabaki kuwatizama kwa macho tu, hii ni baada ya moyo kushindwa kuchagua mmojawapo atakayenifaa.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    " Khaah! Hata huyu jamani?" Nilijikuta naushangaa moyo wangu baada ya kujenga mazoea na kipusa mmoja ambaye moyo uligoma kumfungulia mlango aingie ndani.Ukigongwa na nyoka nyasi zikikugusa lazima ushtuke niligundua Lisa hakuondoka hivi hivi ila aliniacha nikiwa nimejifunza mengi.Naam! Sasa nilikuwa muoga wa kupenda hovyo, nilikuwa nikihitaji mtu ambaye atanifaa haswaa si kwajili ya sura yake nzuri wala umbo lake maridadi ila mtu huyo ni yule ambaye atanipenda kwa dhati, Je ni nani huyo!? Kila niliyekuwa nikifikiria huyu ndiye moyo uligoma,sasa ni nani basi! Hapo ndipo nafsi iliposhtuka baada kumkumbuka Sunshine.Naam! Huyu ni binti pekee aliyekubalika kumoyo,Katika kipindi chote nilichoishi na Sunshine alinifanya nijisikie mwanaume haswaa, lakini kukubalika pekee moyoni ilikuwa haitoshi kizungumkuti kilikuja jinsi ya kumpata tena mrembo huyo. " Nilivyoondoka kwa mbwembwe namna ile naanzaje kurudi tena kwa Sun!?" Nilijikuta najiuliza swali ambalo majibu yake yalinifanya nione haya kwa kiasi flani. Nikiwa bado nawaza jinsi ya kumpata tena Sun nilihisi kiu, ila nilipojaribu tu kunyanyuka ili kufwata maji nikapata kizunguzungu cha ghafula, nuru ikapotea nikahisi kama vile nabebwa juu juu na kubwagwa chini baada ya hapo sikujua nini kiliendelea, nilikuja kushtuka dakika chache baadae, Kitu gani kimeniangusha? Swali hilo halikupata jibu la msingi zaidi ya labda hisia nzito nilizokuwa nazo kabla ya kuamka, nikajizoa zoa pale chini nilipokuwa na kukaa vyema kwenye sofa. Ni bahati nzuri tu hapakuwa na mtu karibu aliyeshuhudia kitendo hicho, sikutaka kupoteza hata dakika moja, nikaokota simu yangu mezani nakuanza kuandika namba za Lisa nilizozicopy kichwani na kuzipaste kwenye simu lakini baada ya kupiga ikawa holaaa! Namba hazipatikani masikinii nimepoteza dhahabu nikifuata kipande cha chupa kilichong'aa.Kutopatikana kwa namba ya Sun ilikuwa ni pigo kubwa kwangu.Akili ikachoka, nikaamua kwenda kulala ambapo napo sikupata usingizi bado nilikuwa nikiwaza namna ya kumpata Sun.Ni muda mrefu sasa toka tumeachana na kuifuta namba yake kwa simu, japo niliikariri vizuri kichwani lakini nikahisi huenda nimeisahau, nikainuka toka kitandani na kuelekea katika meza yangu ya kujisomea, Naam! Katika kipindi kile najaribu kuikariri namba ya Sun nakumbuka nilikuwa kwenye meza hiyo hiyo pia nilikuwa nikiichora chora kwenye daftari.Kitendo bila kuchelewa nikaanza kushakura huku na kule hadi nilipolipata daftari ambalo nilihisi litakuwa na namba hizo."Asta la vista!" Nilifurahi mwenyewe baada ya kuziona namba hizo.Kosa lililosababisha namba hizo kutopatikana ni kuwa namba mbili za mwisho niliziweka mwanzo na zile za mwanzo nikaziweka mwisho.Nikaziandika tena kwenye simu kwa ufasaha kisha nikaziangalia mara mbili kuzihakiki kabla ya kupiga tena.

    "Kaa mbali na mie nimeshapenda,kaa mbali na mie nimeshaozaa……" hiyo ni caller tone ya moto band iliyokuwa ikiitumbuiza baada ya kumpiga Sun.

    "Hallo!" Nikiwa najaribu kuifikiria mistari ya wimbo huo simu ikapokelewa.

    "Mambo vipi Sun!?" Nilimsalimu baada ya kuhakiki sauti yake.

    "Poa mzima wewe!?" Alijibu Sun kuonyesha kuwa ameshajua anaongea na nani.

    Baada ya kumaliza salaam moja kwa moja nilimpeleka Sun kwenye dhumuni langu la kumpigia simu, Sun alionekana kushangazwa sana na mimi ambaye hakutarajia kuwa siku moja ningerudi na alikuwa akijitahidi kuniuliza habari za Lisa ambaye kwa muda huo sikutaka hata kulisikia jina lake, baada ya kuongea kwa muda mrefu kidogo na maongezi kufikia mahali pazuri tuliagana kwa miadi ya kumpigia tena baadaye.

    Tofauti kabisa na nilivyofikiria kuwa baadae itakuwa ni kumalizia tu kile nilichokianza mchana lakini sikuamini kile kilichotokea baada ya kumpigia simu majira ya saa nne za usiku.Sun aliniwia mkali mithili ya mzazi wa watoto watukutu na kila mara alikuwa akiyarejea maneno yangu makali niliyomwambia siku ile tunaachana, nikiwa bado najaribu kujitetea kwa sauti ya upole Sun alinitakia usiku mwema haraka haraka na kunikatia simu, ni wazi kwamba hakutaka kuzisikiliza porojo zangu zinazopendeza masikioni pekee, jinsi nilivyo jisikia ni Mola pekee anayejua ama msomaji wangu aliyewahi kufanyiwa mchezo huo.Sikufa moyo kila uchwao niliendelea kumuimbia Sun wimbo ule ule wa kutaka kuwa naye hadi alipoanza kunielewa.

    "Kama nilivyokwambia Tom wangu kweli bado nakupenda lakini nimeshapata mwingine na ananipenda sana yaani mie ndio namsumbua na kilichonifanya nimpende anafanana na wewe!" Ni sauti laini ya Sun ikijaribu kunieleza jambo gumu nilipomtembelea mtaani kwao.

    "Kama kweli bado unanipenda tatizo ni nini Sun, kwanini usimpige chini huyo jamaa.Niamini Sun kweli nimeshindwa kuishi bila wewe mpenzi wangu!"

    " weeh!…weh huo unyama unaweza kuufanya wewe tu! Maumivu niliyoyapata kipindi kile siwezi kumfanyia mtoto wa watu ivyo!"

    "Kwaiyo itakuwaje sasa Sipo tayari kukupoteza Sun…nakupenda!"

    "Kitu pekee nnachoweza kukwambia Tom nakupa miezi mitano ya kusubiri kama utaweza, huyu jamaa akinizingua tu ntakuwa wako tena lakini akinitendea vizuri basi itakuwa imekula kwako!"

    "Ok! Sun haya yote niliyataka mwenyewe na upo sahihi kunipa adhabu yeyote ile uipendayo ila kitu kimoja nnachokusihi naomba unihurumie sababu nateseka juu yako kwaheri naamini tutaonana tena!" Nilimuaga Sun nakuondoka roho yangu ikiwa nyeupe, siku zote nimekuwa mshindi wa michezo ya maneno lakini hakuna marefu yasiyokuwa na nncha leo hii nilizidiwa kete na mtoto wa kike. Niliondoka huku nikijipa moyo kuwa Sunshine atakuwa wangu tena miezi mitano aliyonipa sio mingi.



    Baada ya miezi mitano kwisha nilirudi tena kwa Sun kumkumbusha kuwa muda umefika, japo mimi nilikuwa naziona siku hizo kuwa ni nyingi sana nilipomwambia Sun kuwa miezi hiyo imekatika alionekana kushangaa sana imeishaje upesi namna hiyo kwa maana nyingine kwa upande wake mambo yalikuwa ni mazuri bado hivyo hiyo ilimaanisha hakuna tumaini lingine kati yetu na hata kama lingekuwepo nisingeweza kusubiri tena.Nilichofanya nikumuaga Sun na kumuahidi sitomtafuta kamwe pia moyoni mwangu nilimfuta rasmi na kwa upande mwingine nilimuonea wivu bwana aliyempata kwani alipata mwanamke aliyekamilika haswa.



    Sasa Tom mimi niliishi nusu mtu nusu mfu, raha ya maisha haikuwako tena nilipo mimi.Wakati mwingine nilifikiri ni bora kufa tu.Mapenzi hayakunitendea haki, Kweli mapenzi upofu anayependa hayamuoni.

    Siku moja majira ya usiku nikiwa nimepumzika chumbani kwangu simu yangu iliita na nilipoangalia ni binamu yangu Dora ndiye aliyekuwa akipiga.Maisha yangu mapya yamenifanya kuwa mpweke kiasi cha kupiga stori na mtu yeyote hata aliye wrong namba.

    Baada ya kupokea simu hiyo ya Dora tulipiga porojo nyingi sana hadi ikafikia mahali tukaishiwa vya kuongea na ndipo mada hii ilipozuka sasa.

    "Ivi unajua kwanini nilikuwa namchukia sana Lisa?" Dora alianza kwa kuniuliza na nilipomuuliza kwanini alianza kufunguka.

    " Nilikuwa simpendi kwasababu alikuwa anamnyima rafiki yangu haki yake ya msingi!'

    "Rafiki gani tena!?"

    "Tom usitake kujifanya haumjui rafiki yangu Zabibu wakati nilikuwa nakuja naye kwenu mara nyingi tu pindi bado mnakaa tabora"

    "Sasa Lisa alikuwa anamkatili vipi!?"

    "Tom sidhani kama Dunia hii kuna msichana aliyewahi kukupenda kama alivyokuwa akikupenda Zabibu,Alikuwa anakupenda hadi akikuona anatetemeka na huwezi amini mara zote tulivyokuwa tukija naye kwenu alikuwa anataka kukwambia lakini tukifika anaishia kukutazama tu.Basi tulikuwa hatupendi kweli tukikuona na Lisa!"



    "Sasa kwanini ukamsaliti rafiki yako!?"

    "Huwezi amini Zabibu alikuwa anakusifia hadi mie mwenyewe nikawa naona wivu na nilipopata fursa ikabidi niuonje huo utamu rafiki yangu aliokuwa anauona kwako!……kwani nilifanya vibaya!" Dora aliniuliza kwa kunitega hali nikijua tulifanya vibaya nilimjibu hatukufanya vibaya.

    "Nikuulize kitu!?" Nilimwambia Dora naye alipojibu ndio nikaendea.

    "Saivi Zabibu yupo wapi!?"

    "Yupo huko huko Dar!"

    "Naomba namba yake basi!"CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    "Sikupi!"Dora alijibu kikorofi.

    "Kwanini sasa!?"

    "Unafikiri mie sijui unataka kufanya nini, me mwenyewe nakupenda!"

    "Lakini Dora sie si ndugu!"

    "Aya bhana ulale salaama!" Kabla sijajibu neno akakata simu bila shaka nilimkera japo yeye alinifurahisha sana siku hiyo.

    Uongo dhambi kuacha Lisa msichana mwingine aliyekuwa akiutesa moyo wangu alikuwa ni Zabibu na kama nisingekuwa na Lisa basi ningekuwa na mtoto huyo.Uzuri wake wa asili ulioundwa kwa ngozi yake rangi ya chocolate, nywele zake za singa singa, macho yake ya mviringo, umbo lake namba nane, tabia yake ya upole,akili yake iliyotulia vilimfanya mwanaume yeyote apende kuwa naye.Sikuwahi kufikiria kuwa Zabibu alikuwa akinipenda kiasi hicho na jinsi alivyokuwa akionekana kwa nadra kutokana na kusoma bording toka mdogo kulinifanya nimuone kama malkia pindi anaporudi likizo.

    "Wooooh! Nakupenda Zabibu!" Nilijisemea kimoyo moyo Nilipokuwa nainuka toka kitandani ingawa nilikuwa nimechoka habari za Zabibu toka kwa Dora zilisababisha usingizi wote kunipaa.Ingawa Dora alininyima namba zake moyoni niliapa kumtafuta kwa udi na uvumba hadi nitakapompata. Usiku huo huo nikaanza kutype jina Zabibu kwenye mitandao yote ya kijamii,Twitter,Instagram,Facebook,Skype,Badoo na kwingine koote!,

    Baada ya kuhangaika kila kona kwa siku kadhaa bila mafanikio ndipo wazo jipya liliponijia, ama kweli penye nia pana njia! Nilijisemea mwenyewe baada ya kumpata Zabibu kwa jina tofauti kabisa nilipokuwa nakagua majina ya rafiki wa Dora Facebook.Japo alikuwa katumia jina lingine tofauti kabisa lakini sura yake ya kitoto ( baby face) iliniwezesha kumtambua kirahisi.Baada ya kumpata binti huyo kigoli na kumuelezea jinsi nnavyomzimia kisha nayeye kunipokea kwa mikono miwili hatimaye maisha yangu ya kimapenzi yalirejea kwenye ramani tena.



    "Baby kwanini unasema tutaishi pamoja hadi kufa!?" Zabibu aliniuliza swali hilo siku moja tulipokuwa tukipata chakula cha jioni kwenye mkahawa mmoja.

    "Malkia Wangu nilikupa story ya Lisa na Sunshine nimepitia mengi na sasa nimekuwa MZOEFU!"

    "MZOEFU!?" Zabibu aliuliza kwa herufi kubwa!.

    "Yes baby mimi ni MZOEFU!"

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ********* MWISHO**********



    Nawashukuru wote mliofwatilia Chombezo hii ya kusisimua mwanzo mwisho!!



    One 

0 comments:

Post a Comment

Blog