Chombezo : Jamani Baba
Sehemu Ya Tano (5)
ILIPOISHIA
Asante ila mimi nataka talaka yangu tu kama
amekwambia kuhusu kumfumania na
mwanangu. ”
“Ameniambia lakini unakumbuka mwaka huu ,
mwezi wa pili na wewe ulifumaniwa kule kwa
mzee Bakari na yule mzee wa genge la
Mwembeni, ulimwambia mumeo ?”
TEMBEA NAYO MDOGOMDOGO. ...
Kitendo cha kusema maneno hayo tu, Masilinde
akaona afadhali kwamba naye alipata pa
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kujitetea kwani hata mke wake aliwahi
kufumaniwa.
“Kumbe alishawahi kufumaniwa?”
“Ndiyo.”
“Na nani?”
“Kwa mzee Bakari, yule mzee muuza genge
mtaa wa pili ” alisema mzee Kimanama .
“Mama Mwaija umesikia hayo? Unanishia bango
wakati hata wewe umewahi kufumaniwa ?”
Masilinde alimwambia mkewe .
“Wala sijawahi kufumaniwa, halafu we mzee
acha uchuro wako hapa. Nataka talaka yangu ... ”
“Talaka sikupi, kama umenifumania, na wewe
ushawahi kufumaniwa, kwa hiyo ngoma droo,
kama umefunga na mimi nimefunga. ..”“ Nasema
hivi nataka talaka yangu. ”
“Mimi si ndiye muandikaji wa talaka , siwezi
kutoa ...halafu niliweka nadhiri kwamba katika
maisha yangu sitakuja kutoa talaka mpaka
naingia kaburini... ”
Kwa hasira, mama Mwaija akamgeukia Mwaija .
“Halafu na wewe ni lazima uondoke hapa
nyumbani, nikipewa talaka na wewe safari kwani
siwezi kuendelea kuishi na mtoto mwenye tabia
chafu kama yako ... ”
“Nisamehe mama, sitorudia tena ... ”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Hakuna cha msamaha, ungekuwa umefanya
kosa lingine ningekusamehe lakini siyo kufanya
mapenzi na baba yako, kwa mwanamke yeyote
ni aibu kubwa sana .”
Hapohapo akamgeukia mzee Kimanama .“ Na
wewe mzee mbeya , umesema kwamba
nimefumaniwa, lini nimefumaniwa?”
“Unajifanya hukumbuki ?”
“Na nani?”
“Si yule mzee muuza genge, alijifanya
kukuongezea vimbogamboga kumbe alikutaka na
ukaingia mkenge, tena mzee nuksi sana kwa
wake za watu yule. ..” Mama Mwaija akakasirika,
alijua kwamba hakuwahi kufumaniwa ila mzee
huyo alikuwa akidanganya, alichokisema ni
kwamba waende kwa mzee huyo, kweli
wakaenda na kumkuta akiwa amesimama nje .
“Karibuni. ..”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Asante , wewe mzee , hujawahi kufumaniwa na
huyu mwanamke ?” aliuliza mzee Kimanama .
“Mwanamke gani ?”“Usijifanye hujui, kwani hapa
wanawake wapo wangapi?”
“Namuona mmoja tu. .”
“Sasa kama unamuona mmoja kwa nini unauliza
jibu? Aya tujibu .”
“Sijawahi kufumaniwa naye , kwanza hata mapaja
yake tu sijawahi kuyaona .”
“Wewe mzee muogope Mungu , leo unaruka na
wakati siku ile ulipigwa mpaka picha !’
“Nimekumbuka sasa , kweli nilishawahi
kufumaniwa, ila si na huyu mwanamke, yule
alikuwa mama Mwajabu , yule wa mtaa wa tatu,
mwanamke mweupe wa Kitanga aliyefanana na
mkeo ,” alisema mzee huyo , alionekana
kukasirika na hivyo kumzingua mzee Kimanama.
“Huo sasa utani .. .”
“Kama ni utani basi jua wewe ndiye umeanza
kunitania, kwanza naomba muondoke nyumbani
kwangu kabla sijawaitia polisi . ”Hawakuendelea
kusubiri, tayari Masilinde akaonekana
kushindwa, alichokifanya mara baada ya kufika
nyumbani ni kuanza kuomba msamaha kwa
mkewe kwa kilichotokea .
“Mke wangu naomba unisamehe ni shetani
alinipitia nakuahidi sitarudia tena kosa hilo ,
nisamehe mama na nipo chini ya miguu yako,”
Masilinde alimwangukia mkewe .
“Ukitaka tuelewane kuna sharti moja .”
“Lipi ?”
“Huyu malaya sitaki akae hapa nyumbani. ”
“Eeeh ! Amekuwa malaya tena, huyu si mtoto
wako wa kumzaa!”
“Hata kama , umekubaliana na mimi?”
“Sawa . Kwa hiyo nikampangie chumba ili atoke
hapa?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Umpangie chumba! Nani kasema hivyo , unataka
uwe unajiachia kila siku, haiwezekani, huyu arudi
Tanga.”
“Arudi Tanga?”
“Ndiyo.”
“Mbona unamtupa hivyo ?”
“Mimi si ndiye mama yake ! Arudi Tanga .”
Kwa sababu mke wake aliamua hivyo na
hakutaka kumpoteza kwa kuendelea kudai
talaka, akakubaliana naye.
Alichokifanya mzee huyo ni kumsisitizia Mwaija
kwamba waendelee kuwasiliana hata kama
angekuwa wapi kwani bado moyo wake
ulimpenda sana na hakutaka kumuacha.
“Kwa hiyo ndiyo hivyo baby, tuwe tunawasiliana,
usimuogope mama yako, kutembea nje ya ndoa
ni faulo za kawaida tu, kama kuchezewa rafu
uwanjani, ” alisema mzee huyo .Siku iliyofuata
mama Mwaija aliamua kumrudisha Mwaija
Tanga. Mawasiliano na msichana huyo
yaliendelea kisiri na baada ya wiki moja, mzee
huyo akamtumia binti huyo nauli na kumvuta
tena Dar , kipindi hiki akampangia chumba
kabisa, mtaa wa Tandale karibu na Kwa Mtogole.
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Utakuwa ukiishi hapa mpenzi , hapa sasa kwa
raha zetu , mama akipiga simu, mwambie upo
Tanga, siku nyingine akisumbua sana, kata simu
kisha baadaye utamwambie network inazingua, ”
alisema mzee huyo .
“Sawa kipenzi .”
Wakabusiana na mzee kupata kiburudisho chake
kwa saa moja na kisha kurudi nyumbani huku
akiwa mwepesiii, hakuacha kumtembelea Mwaija
nyumbani hapo , kazi ikawa ni kujilia tunda kila
siku.
Mwezi mmoja ulikatika tangu Mwaija aondoke
nyumbani hapo . Siku hiyo mama kama mama,
uchungu wa mwana ulimwingia , akaamua
kumpigia Mwaija japo amjulie hali . ..
“Ni mtoto wangu wa kumzaa , siwezi kumtupa
hivi. Mwenye makosa ni baba yake, kwani si
anajua yule ni mwanangu ?
“Sidhani kama Mwaija ndiye aliyemtongoza baba
yake wa kambo . Lakini mwanangu yule naye
amezidi uzuri . We mtoto mdogo wowowo vile ,
kiuno kiuno kweli . Mguu wanasema wa bia,
halafu yale macho mwanangu yale ndiyo
yanayomponza kabisa, ” alisema mama Mwaija
simu ikiwa sikioni tayari. ..
“Shikamoo mama,” Mwaija alimsalimia baada ya
kupokea.. .
“Marhaba , hujambo ?”
“Mi sijambo.”
“Hajambo shangazi yako ?”
“Hajambo .”
“Maisha yanaendaje?”
“Kawaida tu mama. ”
Mama Mwaija alishtuka kusikia kelele za wapiga
debe wakisema ...
“Msasani Posta... Msasani Posta.”
“Mwaija ,” aliita. ...
“Uko Dar ?”
“Hapana mama , niko Tanga.. .”
“Unanidanganya mimi wewe?”
“Hapana mama , kwa nini ?”
“Mbona nasikia watu wa daladala wakisema
Msasani Posta?”
“Siyo Msasani mama , unasikia vibaya .
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Wanasema Mkwakwani Posta. Siku hizi Tanga
kuna daladala za Mkwakwani Posta, ” alisema
Mwaija huku akitetemeka.
“Kweli ?”
“Kweli mama , kwani we hujui kuna daladala za
Mkwakwani Posta?”
“Mi nimesikia Msasani Posta.”
“Hapana mama bwana. ”
“Haya , shangazi yako anaendeleaje ?”
“Anaendelea vizuri . Nipe niongee naye .”
“Mimi nipo mtaani , nimemwacha nyumbani.”
“Ukirudi tu, nipe niongee naye. ”
“Sawa mama .”
Mwaija alipomaliza kuzungumza na simu na
mama yake , akampigia Masilinde.. .
“Baby uko wapi ?”
“Kazini, vipi ?”
“Kimenuka. Njoo haraka sana.”
“Nini?”
“Ungekuja baby bwana .”
“Oke, nakuja sasa hivi . ”
Mwaija alizidi kutetemeka, hasa alipoambiwa
akifika nyumbani ampe simu shangazi yake ili
mama yake aongee naye .
Ndani ya nusu saa , Masilinde akawa amefika
nyumbani kwa Mwaija huku akiwa na sura yenye
mshangao.. .
“Vipi Mwaija , kuna nini ?”
“Inabidi niende Tanga haraka sana , hata
nikiondoka leo hii .”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Kuna nini ?”
“Mama. ”
“Mama gani?”
“Mkeo .”
“Kafanyaje?”
“Kanipigia simu .”
“Enhe , kasema anakwenda Tanga kesho? Maana
kama anasafiri kesho tatizo liko wapi, mi si
nitamzuia tu?”
“Siyo hivyo baby. Mama kasema nimpe simu
shangazi aongee naye, nikamwambia nipo
mtaani, shangazi nilimwacha nyumbani. ”
“Sasa ikawaje?”
“Akasema nikirudi atataka aongee naye . Na
mimi najua lazima baadaye jioni mama atapiga
tena. Halafu akaniuliza Mwaija upo Dar ?
Nikamwambia hapana mama, akasema mbona
nimesikia sauti za daladala zikisema Msasani
Posta? Nikamdanganya siyo Msasani Posta ni
Mkwakwani Posta. Ndiyo akatulia.”
“Kha! Kwani we leo ulifika Msasani ?”
“Si ulinikubalia niende kwa yule rafiki yangu .”
“Oo ! Sasa sikia , sidhani kama ni ishu.. .”
Kabla Masilinde hajamaliza , mama yake alipiga
tena...
“Huyo , anapiga ,” alisema Mwaija ...
“Usipokee kwanza. ..nataka kujua , kwani
shangazi kule Tanga ana simu ?”
“Hapana, alikuwa akitumia ya kwangu. ”
“Oke. Sasa itabidi tumkodishe mwanamke,
tumwambie ajifanye shangazi yako , aiige sauti ,
wewe utamwambia sauti ya shangazi ilivyo. ”
“Shangazi ana sauti ndogo sana , utadhani
mtoto.”
“Ah! Kumbe ni hivyo , hata mimi naweza kuigiza
sauti ya kitoto . Hebu pokea mwambie ongea na
shangazi, ” alisema Masilinde.
Mwaija aliogopa lakini mama yake aliendelea
kupiga, ikabidi apokee . ..
“Haloo mama .”
“Umesharudi nyumbani?”
“Ndiyo.”
“Nipe shangazi yako. ”
“Huyu hapa , ongea naye. ”
Masilinde alijibana sawasawa , akavuta pumzi
inavyotakiwa ili atoe sauti ya kitoto .. .
“Halo. ”
“Ee, wifi za leo?”
“Njema, za huko Dar ?”
“Huku kwema wifi , unaendeleaje na huyo binti
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
yako?”
“Tunaendelea vizuri , ila mi mwenyewe kifua
kidogo si kizuri sana .”
“Oo ! Pole, ndiyo maana sauti inatoka kama
inataka kukatika. ”
“Ee. Umeona ee?”
“Ee. Pole sana. haya, nilitaka kukusalimia tu wifi
maana huyo aliniambia alitoka, nikamwambia
akirudi niongee na wewe .”
“Asante sana wifi yangu. Msalimie sana
Masilinde.”
“Haya zimefika wifi .”
Baada ya kumaliza kuongea na mke wake
akijifanya ni shangazi mtu, Mwaija na Masilinde
walicheka kiasi cha kushindwa kuhimili na
kujishika matumbo yao lakini kumbe simu
ilikuwa haijakatwa upande wa pili..
“Hivi nitarudi vipi nyumbani leo ? Hii si aibu
kubwa! Yaani mke wangu amejua kila kitu
kuhusu mtoto wake . Niliomba samahani siku zile
yakaisha, kaenda Tanga nikamleta tena mjini
sasa faida yake ndiyo haya yanayonitokea .
“Mbaya zaidi kuna wakati Mwaija alinishukuru
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kwa kumpangia chumba, sasa pale mama yake
si amesikia kila kitu !” alitafakari Masilinde,
akaishiwa nguvu na kuanguka chini kisha
akapoteza fahamu .
Mwaija alifanya kazi ya ziada kumzindua mpenzi
wake huyo lakini alipozinduka na kutulia kidogo
wote wakawa na swali moja ni kwa nini mama
Mwaija baada ya kukatiwa simu muda huo
hakupiga tena?!
Wakiwa wanafikiria kuhusu hilo , simu ya Mwaija
ikaita ikiwa kwenye meza ndogo...
“Hebu angalia ni yeye?” alisema Masilinde...
“Mimi naogopa, angalia wewe, ” alisema Mwaija .
Simu iliendelea kuita na kila mmoja akiwa hataki
kuangalia nani aliyepiga .. .
“Angalia Mwaija .. .”
“Angalia wewe bwana mimi naogopa .”
Mwishowe, Masilinde alijitoa fahamu , akaenda
kuangalia...
“Mh ! Yeye bwana ,” alisema akiwa ameishika
simu.. .
“Mimi sipokei hata iweje! Mama anaweza kuniua
hata kwenye simu,” alisema Mwaija huku
akitetemeka.
Chumba kilizizima , kila mmoja alikosa amani,
alikosa raha! Ilifika mahali wote walikaa
kitandani wakiwa wamejiinamia kwa mawazo.
Kila mmoja aliwaza la kwake , lakini hakuna
aliyemwambia mwenzake alichokuwa
akikiwaza...
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Mwaija , mimi nadhani kuanzia leo tuamue moja ,
tuwe mke na mume au tujiue , kwa kuwa najua
mimi na mama yako kurudiana hakupo hata
iweje?”
Kabla Mwaija hajajibu, meseji kwenye simu yake
iliingia, ikaingia pia kwenye simu ya Masilinde...
“Mh ! Hizo meseji atakuwa yeye, ” alisema
Mwaija. Sasa alianza kujijua kumbe yeye ni
bogasi kupita wasichana wote duniani . Kuna akili
ilikuwa ikimwambia...
“Hivi kweli wewe na akili zako unaweza kumpa
penzi mume wa mama yako? Ona sasa,
umejiingiza kwenye matatizo maishani mwako .. .
mume wa mama yako hata kama hajakuzaa , ni
baba yako tu. ”
Masilinde ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungua
meseji hiyo na kuisoma tena kwa sauti .. .
“Nimeamua kujiua ili kuepuka aibu na fedheha
hii.”
Mwaija naye akaisoma meseji yake kwa sauti ...
“Mwaija , endelea kufaidi penzi la baba yako
maana uliona mimi nafaidi peke yangu , tukutane
ahera.”
Masilinde alikurupuka, akaondoka mbio kwenda
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kwake. Mwaija naye hakutaka kusubiri, alifuata
nyuma. Walimkuta mama Mwaija ameshakata
roho kwa kujinyonga kwa kamba .
Kilio kilianzia hapo, majirani walipofika , Masilinde
alikiri kusababisha kifo cha mkewe , Mwaija
naye alikiri kuchangia mama yake kujinyonga .
Wakaahidi kutoendelea na uhusiano tena, Mwaija
alirudi Tanga kwa shangazi yake ambako mpaka
sasa anataabika na maisha akiwa kama
mwendawazimu.
MWISHO.
0 comments:
Post a Comment