Search This Blog

Thursday, 19 May 2022

JAMANI BABA - 5

 





    Chombezo : Jamani Baba

    Sehemu Ya Tano (5)



    ILIPOISHIA

    Asante ila mimi nataka talaka yangu tu kama

    amekwambia kuhusu kumfumania na

    mwanangu. ”

    “Ameniambia lakini unakumbuka mwaka huu ,

    mwezi wa pili na wewe ulifumaniwa kule kwa

    mzee Bakari na yule mzee wa genge la

    Mwembeni, ulimwambia mumeo ?”

    TEMBEA NAYO MDOGOMDOGO. ...

    Kitendo cha kusema maneno hayo tu, Masilinde

    akaona afadhali kwamba naye alipata pa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kujitetea kwani hata mke wake aliwahi

    kufumaniwa.

    “Kumbe alishawahi kufumaniwa?”

    “Ndiyo.”

    “Na nani?”

    “Kwa mzee Bakari, yule mzee muuza genge

    mtaa wa pili ” alisema mzee Kimanama .

    “Mama Mwaija umesikia hayo? Unanishia bango

    wakati hata wewe umewahi kufumaniwa ?”

    Masilinde alimwambia mkewe .

    “Wala sijawahi kufumaniwa, halafu we mzee

    acha uchuro wako hapa. Nataka talaka yangu ... ”

    “Talaka sikupi, kama umenifumania, na wewe

    ushawahi kufumaniwa, kwa hiyo ngoma droo,

    kama umefunga na mimi nimefunga. ..”“ Nasema

    hivi nataka talaka yangu. ”

    “Mimi si ndiye muandikaji wa talaka , siwezi

    kutoa ...halafu niliweka nadhiri kwamba katika

    maisha yangu sitakuja kutoa talaka mpaka

    naingia kaburini... ”

    Kwa hasira, mama Mwaija akamgeukia Mwaija .

    “Halafu na wewe ni lazima uondoke hapa

    nyumbani, nikipewa talaka na wewe safari kwani

    siwezi kuendelea kuishi na mtoto mwenye tabia

    chafu kama yako ... ”

    “Nisamehe mama, sitorudia tena ... ”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hakuna cha msamaha, ungekuwa umefanya

    kosa lingine ningekusamehe lakini siyo kufanya

    mapenzi na baba yako, kwa mwanamke yeyote

    ni aibu kubwa sana .”

    Hapohapo akamgeukia mzee Kimanama .“ Na

    wewe mzee mbeya , umesema kwamba

    nimefumaniwa, lini nimefumaniwa?”

    “Unajifanya hukumbuki ?”

    “Na nani?”

    “Si yule mzee muuza genge, alijifanya

    kukuongezea vimbogamboga kumbe alikutaka na

    ukaingia mkenge, tena mzee nuksi sana kwa

    wake za watu yule. ..” Mama Mwaija akakasirika,

    alijua kwamba hakuwahi kufumaniwa ila mzee

    huyo alikuwa akidanganya, alichokisema ni

    kwamba waende kwa mzee huyo, kweli

    wakaenda na kumkuta akiwa amesimama nje .

    “Karibuni. ..”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Asante , wewe mzee , hujawahi kufumaniwa na

    huyu mwanamke ?” aliuliza mzee Kimanama .

    “Mwanamke gani ?”“Usijifanye hujui, kwani hapa

    wanawake wapo wangapi?”

    “Namuona mmoja tu. .”

    “Sasa kama unamuona mmoja kwa nini unauliza

    jibu? Aya tujibu .”

    “Sijawahi kufumaniwa naye , kwanza hata mapaja

    yake tu sijawahi kuyaona .”

    “Wewe mzee muogope Mungu , leo unaruka na

    wakati siku ile ulipigwa mpaka picha !’

    “Nimekumbuka sasa , kweli nilishawahi

    kufumaniwa, ila si na huyu mwanamke, yule

    alikuwa mama Mwajabu , yule wa mtaa wa tatu,

    mwanamke mweupe wa Kitanga aliyefanana na

    mkeo ,” alisema mzee huyo , alionekana

    kukasirika na hivyo kumzingua mzee Kimanama.

    “Huo sasa utani .. .”

    “Kama ni utani basi jua wewe ndiye umeanza

    kunitania, kwanza naomba muondoke nyumbani

    kwangu kabla sijawaitia polisi . ”Hawakuendelea

    kusubiri, tayari Masilinde akaonekana

    kushindwa, alichokifanya mara baada ya kufika

    nyumbani ni kuanza kuomba msamaha kwa

    mkewe kwa kilichotokea .

    “Mke wangu naomba unisamehe ni shetani

    alinipitia nakuahidi sitarudia tena kosa hilo ,

    nisamehe mama na nipo chini ya miguu yako,”

    Masilinde alimwangukia mkewe .

    “Ukitaka tuelewane kuna sharti moja .”

    “Lipi ?”

    “Huyu malaya sitaki akae hapa nyumbani. ”

    “Eeeh ! Amekuwa malaya tena, huyu si mtoto

    wako wa kumzaa!”

    “Hata kama , umekubaliana na mimi?”

    “Sawa . Kwa hiyo nikampangie chumba ili atoke

    hapa?”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Umpangie chumba! Nani kasema hivyo , unataka

    uwe unajiachia kila siku, haiwezekani, huyu arudi

    Tanga.”

    “Arudi Tanga?”

    “Ndiyo.”

    “Mbona unamtupa hivyo ?”

    “Mimi si ndiye mama yake ! Arudi Tanga .”

    Kwa sababu mke wake aliamua hivyo na

    hakutaka kumpoteza kwa kuendelea kudai

    talaka, akakubaliana naye.

    Alichokifanya mzee huyo ni kumsisitizia Mwaija

    kwamba waendelee kuwasiliana hata kama

    angekuwa wapi kwani bado moyo wake

    ulimpenda sana na hakutaka kumuacha.

    “Kwa hiyo ndiyo hivyo baby, tuwe tunawasiliana,

    usimuogope mama yako, kutembea nje ya ndoa

    ni faulo za kawaida tu, kama kuchezewa rafu

    uwanjani, ” alisema mzee huyo .Siku iliyofuata

    mama Mwaija aliamua kumrudisha Mwaija

    Tanga. Mawasiliano na msichana huyo

    yaliendelea kisiri na baada ya wiki moja, mzee

    huyo akamtumia binti huyo nauli na kumvuta

    tena Dar , kipindi hiki akampangia chumba

    kabisa, mtaa wa Tandale karibu na Kwa Mtogole.

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Utakuwa ukiishi hapa mpenzi , hapa sasa kwa

    raha zetu , mama akipiga simu, mwambie upo

    Tanga, siku nyingine akisumbua sana, kata simu

    kisha baadaye utamwambie network inazingua, ”

    alisema mzee huyo .

    “Sawa kipenzi .”

    Wakabusiana na mzee kupata kiburudisho chake

    kwa saa moja na kisha kurudi nyumbani huku

    akiwa mwepesiii, hakuacha kumtembelea Mwaija

    nyumbani hapo , kazi ikawa ni kujilia tunda kila

    siku.





    Mwezi mmoja ulikatika tangu Mwaija aondoke

    nyumbani hapo . Siku hiyo mama kama mama,

    uchungu wa mwana ulimwingia , akaamua

    kumpigia Mwaija japo amjulie hali . ..

    “Ni mtoto wangu wa kumzaa , siwezi kumtupa

    hivi. Mwenye makosa ni baba yake, kwani si

    anajua yule ni mwanangu ?

    “Sidhani kama Mwaija ndiye aliyemtongoza baba

    yake wa kambo . Lakini mwanangu yule naye

    amezidi uzuri . We mtoto mdogo wowowo vile ,

    kiuno kiuno kweli . Mguu wanasema wa bia,

    halafu yale macho mwanangu yale ndiyo

    yanayomponza kabisa, ” alisema mama Mwaija

    simu ikiwa sikioni tayari. ..

    “Shikamoo mama,” Mwaija alimsalimia baada ya

    kupokea.. .

    “Marhaba , hujambo ?”

    “Mi sijambo.”

    “Hajambo shangazi yako ?”

    “Hajambo .”

    “Maisha yanaendaje?”

    “Kawaida tu mama. ”

    Mama Mwaija alishtuka kusikia kelele za wapiga

    debe wakisema ...

    “Msasani Posta... Msasani Posta.”

    “Mwaija ,” aliita. ...

    “Uko Dar ?”

    “Hapana mama , niko Tanga.. .”

    “Unanidanganya mimi wewe?”

    “Hapana mama , kwa nini ?”

    “Mbona nasikia watu wa daladala wakisema

    Msasani Posta?”

    “Siyo Msasani mama , unasikia vibaya .

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wanasema Mkwakwani Posta. Siku hizi Tanga

    kuna daladala za Mkwakwani Posta, ” alisema

    Mwaija huku akitetemeka.

    “Kweli ?”

    “Kweli mama , kwani we hujui kuna daladala za

    Mkwakwani Posta?”

    “Mi nimesikia Msasani Posta.”

    “Hapana mama bwana. ”

    “Haya , shangazi yako anaendeleaje ?”

    “Anaendelea vizuri . Nipe niongee naye .”

    “Mimi nipo mtaani , nimemwacha nyumbani.”

    “Ukirudi tu, nipe niongee naye. ”

    “Sawa mama .”

    Mwaija alipomaliza kuzungumza na simu na

    mama yake , akampigia Masilinde.. .

    “Baby uko wapi ?”

    “Kazini, vipi ?”

    “Kimenuka. Njoo haraka sana.”

    “Nini?”

    “Ungekuja baby bwana .”

    “Oke, nakuja sasa hivi . ”

    Mwaija alizidi kutetemeka, hasa alipoambiwa

    akifika nyumbani ampe simu shangazi yake ili

    mama yake aongee naye .

    Ndani ya nusu saa , Masilinde akawa amefika

    nyumbani kwa Mwaija huku akiwa na sura yenye

    mshangao.. .

    “Vipi Mwaija , kuna nini ?”

    “Inabidi niende Tanga haraka sana , hata

    nikiondoka leo hii .”

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kuna nini ?”

    “Mama. ”

    “Mama gani?”

    “Mkeo .”

    “Kafanyaje?”

    “Kanipigia simu .”

    “Enhe , kasema anakwenda Tanga kesho? Maana

    kama anasafiri kesho tatizo liko wapi, mi si

    nitamzuia tu?”

    “Siyo hivyo baby. Mama kasema nimpe simu

    shangazi aongee naye, nikamwambia nipo

    mtaani, shangazi nilimwacha nyumbani. ”

    “Sasa ikawaje?”

    “Akasema nikirudi atataka aongee naye . Na

    mimi najua lazima baadaye jioni mama atapiga

    tena. Halafu akaniuliza Mwaija upo Dar ?

    Nikamwambia hapana mama, akasema mbona

    nimesikia sauti za daladala zikisema Msasani

    Posta? Nikamdanganya siyo Msasani Posta ni

    Mkwakwani Posta. Ndiyo akatulia.”

    “Kha! Kwani we leo ulifika Msasani ?”

    “Si ulinikubalia niende kwa yule rafiki yangu .”

    “Oo ! Sasa sikia , sidhani kama ni ishu.. .”

    Kabla Masilinde hajamaliza , mama yake alipiga

    tena...

    “Huyo , anapiga ,” alisema Mwaija ...

    “Usipokee kwanza. ..nataka kujua , kwani

    shangazi kule Tanga ana simu ?”

    “Hapana, alikuwa akitumia ya kwangu. ”

    “Oke. Sasa itabidi tumkodishe mwanamke,

    tumwambie ajifanye shangazi yako , aiige sauti ,

    wewe utamwambia sauti ya shangazi ilivyo. ”

    “Shangazi ana sauti ndogo sana , utadhani

    mtoto.”

    “Ah! Kumbe ni hivyo , hata mimi naweza kuigiza

    sauti ya kitoto . Hebu pokea mwambie ongea na

    shangazi, ” alisema Masilinde.

    Mwaija aliogopa lakini mama yake aliendelea

    kupiga, ikabidi apokee . ..

    “Haloo mama .”

    “Umesharudi nyumbani?”

    “Ndiyo.”

    “Nipe shangazi yako. ”

    “Huyu hapa , ongea naye. ”

    Masilinde alijibana sawasawa , akavuta pumzi

    inavyotakiwa ili atoe sauti ya kitoto .. .

    “Halo. ”

    “Ee, wifi za leo?”

    “Njema, za huko Dar ?”

    “Huku kwema wifi , unaendeleaje na huyo binti

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yako?”

    “Tunaendelea vizuri , ila mi mwenyewe kifua

    kidogo si kizuri sana .”

    “Oo ! Pole, ndiyo maana sauti inatoka kama

    inataka kukatika. ”

    “Ee. Umeona ee?”

    “Ee. Pole sana. haya, nilitaka kukusalimia tu wifi

    maana huyo aliniambia alitoka, nikamwambia

    akirudi niongee na wewe .”

    “Asante sana wifi yangu. Msalimie sana

    Masilinde.”

    “Haya zimefika wifi .”

    Baada ya kumaliza kuongea na mke wake

    akijifanya ni shangazi mtu, Mwaija na Masilinde

    walicheka kiasi cha kushindwa kuhimili na

    kujishika matumbo yao lakini kumbe simu

    ilikuwa haijakatwa upande wa pili..





    “Hivi nitarudi vipi nyumbani leo ? Hii si aibu

    kubwa! Yaani mke wangu amejua kila kitu

    kuhusu mtoto wake . Niliomba samahani siku zile

    yakaisha, kaenda Tanga nikamleta tena mjini

    sasa faida yake ndiyo haya yanayonitokea .

    “Mbaya zaidi kuna wakati Mwaija alinishukuru

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kwa kumpangia chumba, sasa pale mama yake

    si amesikia kila kitu !” alitafakari Masilinde,

    akaishiwa nguvu na kuanguka chini kisha

    akapoteza fahamu .

    Mwaija alifanya kazi ya ziada kumzindua mpenzi

    wake huyo lakini alipozinduka na kutulia kidogo

    wote wakawa na swali moja ni kwa nini mama

    Mwaija baada ya kukatiwa simu muda huo

    hakupiga tena?!

    Wakiwa wanafikiria kuhusu hilo , simu ya Mwaija

    ikaita ikiwa kwenye meza ndogo...

    “Hebu angalia ni yeye?” alisema Masilinde...

    “Mimi naogopa, angalia wewe, ” alisema Mwaija .

    Simu iliendelea kuita na kila mmoja akiwa hataki

    kuangalia nani aliyepiga .. .

    “Angalia Mwaija .. .”

    “Angalia wewe bwana mimi naogopa .”

    Mwishowe, Masilinde alijitoa fahamu , akaenda

    kuangalia...

    “Mh ! Yeye bwana ,” alisema akiwa ameishika

    simu.. .

    “Mimi sipokei hata iweje! Mama anaweza kuniua

    hata kwenye simu,” alisema Mwaija huku

    akitetemeka.

    Chumba kilizizima , kila mmoja alikosa amani,

    alikosa raha! Ilifika mahali wote walikaa

    kitandani wakiwa wamejiinamia kwa mawazo.

    Kila mmoja aliwaza la kwake , lakini hakuna

    aliyemwambia mwenzake alichokuwa

    akikiwaza...

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mwaija , mimi nadhani kuanzia leo tuamue moja ,

    tuwe mke na mume au tujiue , kwa kuwa najua

    mimi na mama yako kurudiana hakupo hata

    iweje?”

    Kabla Mwaija hajajibu, meseji kwenye simu yake

    iliingia, ikaingia pia kwenye simu ya Masilinde...

    “Mh ! Hizo meseji atakuwa yeye, ” alisema

    Mwaija. Sasa alianza kujijua kumbe yeye ni

    bogasi kupita wasichana wote duniani . Kuna akili

    ilikuwa ikimwambia...



    “Hivi kweli wewe na akili zako unaweza kumpa

    penzi mume wa mama yako? Ona sasa,

    umejiingiza kwenye matatizo maishani mwako .. .

    mume wa mama yako hata kama hajakuzaa , ni

    baba yako tu. ”

    Masilinde ndiye aliyekuwa wa kwanza kuifungua

    meseji hiyo na kuisoma tena kwa sauti .. .

    “Nimeamua kujiua ili kuepuka aibu na fedheha

    hii.”

    Mwaija naye akaisoma meseji yake kwa sauti ...

    “Mwaija , endelea kufaidi penzi la baba yako

    maana uliona mimi nafaidi peke yangu , tukutane

    ahera.”

    Masilinde alikurupuka, akaondoka mbio kwenda

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kwake. Mwaija naye hakutaka kusubiri, alifuata

    nyuma. Walimkuta mama Mwaija ameshakata

    roho kwa kujinyonga kwa kamba .

    Kilio kilianzia hapo, majirani walipofika , Masilinde

    alikiri kusababisha kifo cha mkewe , Mwaija

    naye alikiri kuchangia mama yake kujinyonga .

    Wakaahidi kutoendelea na uhusiano tena, Mwaija

    alirudi Tanga kwa shangazi yake ambako mpaka

    sasa anataabika na maisha akiwa kama

    mwendawazimu.



    MWISHO. 

0 comments:

Post a Comment

Blog