Chombezo : Jamani Baba
Sehemu Ya Nne (4)
ILIPOISHIA
Mwaija alitoka, akarudi nyumbani huku miguu
ikimtetemeka. Alijua mama yake atamla nyama
siku hiyo. Alipofika, alisukuma mlango akaingia
ndani. ..
“Ukitaka salama yako Mwaija uniambie ukweli ni
mwanaume gani uliyekuwa naye pale gesti ? .
Usinidanganye maana mimi nilimwona kwa
macho yangu ,” alisema mama Mwaija .
ENDELEA ...
Mwaija alianza kutetemeka kwa mbali akiamini
mama yake atamtoa sikio kama si kiganja cha
mkono.. .
“Mama nisamehe sana .”
“Nikusamehe kwa sababu gani?”
“Nisamehe tu mama, najua nimekukera sana.”
“Nimekuuliza ulikuwa na nani?”
“Na mwanaume mmoja hivi .. .”
“Anaitwa nani?”
“Abdallah .”
“Anaishi wapi ?”
“Kule chini.”
“Mlikutana wapi mpaka mkakubaliana kuingia
gesti?”
“Siku ile ulinituma mayai dukani ndiyo nikakutana
naye akaomba namba yangu.”
“Ahaa ! Sasa kumbe wewe umekuja Dar kwa ajili
ya kufanya uhuni siyo?”
“Hapana mama ... ”
“Huyo Abdallah kijana mzee ?”
“Yuko kama baba wa hapa ndani .”
“Kwa hiyo kumbe wewe siku moja utaweza hata
kunisaliti mimi mama yako ?”
“Hapana mama , siwezi kufanya hivyo . ”
“Unaweza ,” alisema mama Mwaija huku
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
akimsogelea mwanaye amchape makofi mawili
matatu kabla hajampa ushauri wa kimapenzi,
mara alisikika mtu akiingia akajua ni mumewe na
yeye hakutaka mume wake ajue kuhusu habari
ya yeye kumkuta Mwaija gesti ...
“Vipi mbona kama hamna amani humu ndani ?”
aliuliza Masilinde akijifanya hajui chochote na
sura za wote wawili zilikuwa zikionekana kuwa
na tafrani ...
“Si huyu Mwaija .”
“Amefanya nini ?”
“Nimekwenda msibani, nimerudi hajafanya kazi
yoyote ile .”
“Kwa nini , ye anasemaje ?”
“Hala na kusema ndiyo maana nikawa namsema
hapa.”
“Ah! We Mwaija , umeanza uvivu wako siyo?”
“Hapana baba , nilikuwa nahisi kama kichwa
kinaniuma ndiyo maana .”
“Umekunywa dawa ?”
“Sijanywa .”
“Sasa mama Mwaija kumbe mtoto anaumwa
kichwa angefanyaje kazi ?” aliuliza Masilinde...
“Mimi siamini ndiyo maana nimemgombeza .”
Kurudi kwa Masilinde kidogo kulituliza hali ya
hewa kiasi kwamba mama Mwaija alikwenda
kufanya kazi zake za ndani huku akimtaka binti
yake akanunue dawa anywe , apumzike. ..
“Nenda kanunue dawa sawa , unywe halafu
upumzike,” alisema...
“Sawa mama .”
***
Usiku, muda wa kulala ulifika, Mwaija alitangulia
kwenda chumbani lakini alivizia baba yake
amekaa sebuleni akapita hapo akiwa na kanga
moja tu. Safari hii alimtingishia makusudi
wowowo lake ili kumpa ujumbe kwamba wako
pamoja. ..
“Daaa ! Huyu mtoto ni wa kupangishiwa nyumba,
kweli tena. Haiwezekani akawa ananifanyia hivi
wakati anajua sina uwezo kwa usiku huu .”
Moyoni Masilinde aliamua kwamba , mkewe
atakapoingia kulala amzukie chumbani Mwaija .
Kwa hiyo aliendelea kuwepo sebuleni huku
mkewe naye akiendelea kuwepo jikoni lengo lake
mumewe akiingia chumbani tu aende chumbani
kwa Mwaija kumpa semina ya mapenzi mapema.
Kila alipotokea sebuleni, alimwona mumewe
amekaa macho pima ...
“Mh ! Huyu naye halali ?” alisema moyoni mama
Mwaija.
Masilinde naye, kila aliposimama na kuchungulia
jikoni, alimwona mkewe bado jikoni .. .
“Mh ! Huyu leo vipi kwani? Wenzie tunataka cha
kulalia yeye anaweka ukuta , ” alisema moyoni
Masilinde.
Saa saba kamili usiku , mama Mwaija na
mumewe walikuwa bado hawajaingia chumbani .
Lakini mwisho wa yote , mama Mwaija alishindwa
yeye, akaenda kulala...
“Mimi nakwenda kulala,” alisema mwanamke
huyo.. .
“Sa. ..aaawa ,” Masilinde naye alisema huku
akisinzia. ..
“Wewe bado kwani ?” aliulizwa Masilinde...
“Naangalia taarifa ya habari ya ITVT ,” alijibu
Masilinde bila kutambua kwamba muda ulikuwa
umekwenda sana .
“Taarifa ya habari saa hizi mume wangu ?”
“Kwani kuna nini ?”
“Ipo ?”
“Si ndiyo nasachisachi hapa, ” alijibu Masilinde
huku akiminyaminya rimoti.
Mama Mwaija alikwenda kulala, Mwaija kule
chumbani alikuwa hoi kwa usingizi, alikuwa
akikoroma lakini mlango wa chumba chake
ulikuwa wazi kwani wakati anakwenda kulala
aliamini Masilinde anaweza kuzama ndani kama
alivyowahi kufanya .
Masilinde alipoona ukimya ndani mwake ni
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
asilimia mia moja , alisimama sebuleni,
akajinyoosha kisha akaanza kutembea polepole
kuelekea chumbani kwa Mwaija. Njiani alikuwa
akijiambia...
“Nitalala mwepesi sana leo . Mtoto haishi kiu ,
ukimwangalia tu kiu inapanda , jamani! Kuna watu
ni wanawake wengine ni wana wa wake .”
Alishika kitasa, akakizungusha , mlango
ukafunguka, akaanza kuzama ndani taratibu .. .
“Nasikia akikoroma , amelala muda mrefu sana, ”
alisema moyoni Masilinde na kuingia chumbani
humo ...
“We baba Mwaija , huko nako kwa mtoto unaingia
kufanya nini mume wangu jamani?
Masilinde alisimama mlangoni na kugeuka
kumwangalia mke wake . ..
“Nimesikia kama Mwaija analia, sasa nimekuja
kumwangalia , hebu ingia wewe,” alijitetea
mwanaume huyo ...“ Kinachomliza ni nini sasa,
asisemwe?” alisema mama Mwaija huku akienda
chumbani kwa Mwaija . ..
“Na mimi nimehisi hivyohivyo , pengine
ulivyomsema.”
Kule chumbani, kumbe Mwaija alikuwa macho .
Hata yeye alijua baba yake huyo wa kambo
angeenda kumpa msosi wa usiku ndipo alale
kwa hiyo alisikia mlango ukifunguliwa na alisikia
swali la mama yake kumuuliza mumewe
anakwenda kufanya nini chumbani kwa mtoto.
Pia, Mwaija alisikia utetezi wa baba yake
kwamba alimsikia akilia . Kwa hiyo aliposikia
mama yake anakwenda akaanza kulia ...
“Ooo.. .uuui! uiiii ... ”
“Wewe nini?” aliuliza mama yake baada ya
kuzama ndani .
“Kichwa mama .”
“Dawa si umekunywa?”
“Nilikunywa .”
“Ulikunywa ngapi ?”
“Vidonge viwili. ”
“Ulibakiza vingine ?”
“Ndiyo.”
“Basi vimalizie, ” alisema mama Mwaija , lakini
mume wake akagoma . ..
“Hapana! Hawezi kunywa dawa nyingine muda
huu . Lazima yapite masaa manne mpaka
matano .”
“Haya , lala mpaka yapite masaa matano ndipo
unywe tena , umesikia ?”
“Sawa mama ,” alisema Mwaija huku moyoni
akisema.. .
“Wewe, umekutana na watu wajanja kuliko
wewe, kalale mama, utazeeka bure kunifuatilia
kila saa .”
“Labda na wewe baba Mwaija ungeingia umpe
moyo kwamba asiwe na wasiwasi maana naona
kama anatetemeka ,” mama Mwaija alimwambia
mumewe aliyekuwa amesimama nje ya mlango ...
“Kweli ,” alisema baba huyo huku akizama .
Kutokana na udogo wa chumba, mama Mwaija
hakuona sababu ya kubaki humo , akatoka na
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kusimama nje .. .
“Au kama anahisi kichwa kimekazana akitie
maji,” alisema mama Mwaija ...
Masilinde alipozama ndani tu alirudisha mlango
huku akisema .. .
“Naona leo kuna mbu wengi sana.”
Alikwenda kusimama jirani na kitanda na
kumwinamia Mwaija, akamsogelea na kutoa
ulimi, Mwaija akaudaka...
“Mmmmm.. ..”
“Mmmm.. .mmmm.”
Waligugumia wote lakini kwa tahadhari kubwa ili
mama Mwaija asisikie kule nje ya mlango. ..
“Lakini huyo tangu utoto kichwa chake si kizuri ,”
mama Mwaija alisema. ..
“Halafu naye ana tabia ya kutopenda kutumia
chandarua,” aliendelea kusema mwanamke
huyo.. .
“Mwaija ,” aliita Masilinde...
“Niambie mpenzi wangu. ..”
“Mbona mama anaongeaongea sana ?”
“Hata mimi namshangaa ...”
“Basi nipe tena denda mpenzi wangu ,” alisema
Masilinde, akapewa .. .
“Mmmm.. .”
“Mmmmm.. .mmm.. .”
“Mwambie asilie , akizidiwa asubuhi nitampeleka
hospitali akapime malaria ,” mama Mwaija
aliendelea kushauri , kukosoa na kuelekeza
wakati wenzake walikuwa wamezama kwenye
dimbwi la mahaba mazito , denda hadi mate
yanachuruzika. ..
“Akikusumbua mchape makofi mume wangu ,
mtoto mdogo kama huyo asitupelekeshe sana ,”
aliendelea mama Mwaija .
Sasa, Masilinde alianza kumshikashika Mwaija
sehemu mbalimbali za mwili kiasi kwamba,
Mwaija akajikuta anashindwa kuvumilia na
kuanza kuweweseka ...
“Jamani baba ... ”
“Haaa ! Atasikia mama yako wewe , kelele za nini
sasa?” alisema Masilinde lakini akaendelea,
safari hii akamshika nido na kuminyaminya. ..
“Baba jamani !”
“Weee . Acha kusema kwa sauti. ..”
“Halafu kama hataki kulala mwache si tukalale,”
kule nje mama Mwaija aliendelea kusema huku
akipiga mwayo wa usingizi...
“Hebu lala basi tumalizie hapahapa chapuchapu ,”
Masilinde alimwagiza Mwaija .. .
“Weee , mama akiingia je ?”
“Si chapuchapu ? Kwani hujui maama ya
chapuchapu?”
Mwaija aliamini kuwa , kwa uchapuchapu
aliousema Masilinde kila kitu kingekwenda
sawasawa. ..
“Lakini iwe chapuchapu kweli mpenzi , ” alisema
akitoa kanga mwilini mwake na kuitupia kando,
akalala.
Kule nje , mama Mwaija alijiuliza swali moja tu,
kwamba tangu mumewe ameingia chumbani kwa
Mwaija hajamsikia akisema chochote wala
Mwaija kuendelea kulia , kuna nini ?
“Halafu huyu mume wangu vipi sasa ? Mbona
nampa maagizo lakini na yeye hasemi chochote
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
kwa mtoto, ina maana gani sasa ya yeye
kuingia?” alijisemea moyoni mama Mwaija .
Chumbani mechi ya chapuchapu ilianza lakini
kumbe Masilinde naye akabaini kuwa , mkewe
anaweza akashtuka kwani tangu ameingia
hajasema chochote . Kwa hiyo ili kumzuga
akaanza.. .
“Halafu kumbe wewe Mwaija hutumii chandarua ?
Hii si malaria ? Ni kwa nini lakini?”
“Nitatumia baba ,” alisema Mwaija huku
akichanganya makiki ya karibukaribu mpaka
Masilinde akajikuta tayari mambo yako njiani . ..
“U .. .u ...uta .. .a ... nza li ...li ?”
Maneno hayo ya Masilinde yakamshtuka mama
Mwaija kule nje , akakimbilia mlangoni na kuzama
ndani.
“Haa! Mume wangu jamani ?!” alisema kwa
mshtuko mama Mwaija na kupiga mwereka .
Hakuamini macho yake kwani alimkuta mumewe
akiwa uwanjani kabisa na akicheza mechi
sawasawa. ..
“Mwaija ,” aliita Masilinde akitoka uwanjani .
“Baba , mama kafa. ..mama kafa,” alisema Mwaija
huku akitoka kitandani na kuanza kulia kwa
sauti.. .
“Nyamaza Mwaija , mama hajafa , amepoteza
fahamu tu na ataamka muda mfupi ujao, ”
alisema Masilinde akiwahi kumziba kinywa ili
asiendelee kulia.
“Kweli baba mama hajafa?” Mwaija alimwuliza
Masilinde baada ya mzee huyo mkware kutoa
mkono kinywani mwake . “Mwaija naomba
yaamini maneno yangu , mama yako hajafa!”
Masilinde alimwambia Mwaija .
“Kama hajafa itakuwa afadhali, ila sijui
nitamwambia kitu gani anielewe baada ya
kutufumania,” Mwaija alimwambia Masilinde
ambaye alimweleza asiwe na wasiwasi kwa hilo .
Kwa mbali , mama Mwaija alichezesha mguu wa
kulia kisha akakohoa, kidogo Mwaija akapata
amani ya moyo ...
“Lakini baba unadhani mama akiinuka atanifanya
nini mimi?”
“Usiwe na wasiwasi Mwaija, nitazungumza naye,
atakuelewa tu.”
“Mh ! Ataniua , mi namjua vizuri mama. ”
“Hawezi kukuua Mwaija, hata mimi namjua
vizuri mke wangu. ”
Wakati wote huo , si Mwaija wala Masilinde
aliyekuwa amevaa nguo. Hakuna aliyekumbuka
kwamba walikuwa kama walivyozaliwa. Mama
Mwaija alifumbua macho , akaangaza kulia ,
kushoto na kujishangaa. Aliinuka na kukaa kwa
muda kisha macho yake yakatua kwa Mwaija ...
“Mwaija mwanangu ,” aliita mwanamke huyo na
kuanza kulia huku akiendelea kusema ...
“Nimekukosea nini mimi mama yako mpaka
kunitenda vile mwanangu jamani ?”
“Mama nisamehe... ”
“Nikusemehe nini Mwaija , hukujua kama huyu ni
baba yako ? Hata kama hajakuzaa lakini ni baba
yako maana ni mume wa mama yako. ”“ Mke
wangu ungesimama kwanza twende chumbani
kwetu,” alisema Masilinde. ..
“Sitaki , kwanza naomba unipe talaka yangu.
Unatembea na mwanao Masilinde?”
“Twende tukaongee sasa mke wangu. ”
“Nimesema sitaki .”
“Mama msikilize baba, ” alisema Mwaija ...
“Mwaija tulia. ..kwanza nataka kukuuliza,
umeshatembea na baba yako hii leo mara ya
ngapi?”
“Ni leo tu mama.”
“Siyo kweli. Naanza kuhisi hata kule gesti
mlikuwa wote . Yule mwanaume wa gesti ni
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
wewe Masilinde.”
“Si mimi mke wangu. ”
“Ni wewe bwana, unabisha nini ? Huyu binti ni
mgeni kabisa mtaani, kusema amepata
mwanaume mara hii, mimi nakataa.”
Masilinde alibaki kimya. Aliona kimenuka. Alianza
kujutia kitendo chake cha kutembea na binti yake
huyo hali akijua ni mtoto wa mke wake .. .
“Masilinde,” aliita mama Mwaija.
“Naam.”
“Nini kimekuvutia kwa mtoto wako ? Hilo umbo au
uzuri wa sura ?”
Masilinde kimya!
“Nijibu Masilinde!”
“Ushetani tu mke wangu. ”
“Kwa hiyo shetani wako wewe ni mpaka kwa
mtoto wako ?”
“Ni bahati mbaya mke wangu .”
“Mh ! Mimi nataka talaka yangu... we unadhani
mimi nitaishi vipi na mwanangu kwenye nyumba
hii wakati umeshalala naye ?”
“Nitafanya kitu mke wangu .”
“Kitu cha ?”
“Kitu cha kukufanya uishi na amani.”
“Kitu gani ?”
“Nitampangia chumba huyu Mwaija nje ya hapa
nyumbani.”
“Ili upate nafasi ya kwenda kila siku kwake, si
ndiyo?”
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
“Sina maana hiyo.”
“Maana yako ni ipi Masilinde?”
Mara, mlango uligongwa, mzee mmoja anaitwa
Kimanama aliingia .. .
“Karibu mzee wangu ,” alikaribisha Masilinde
kutokea chumbani, akatoka na yeye kwenda
sebuleni.. .
“Bwana mi sikai, nina shida kidogo ,” alisema
mzee Kimanama huku akikaa japokuwa alisema
hakai. .!
“Nakusikiliza, ila hata mimi nafurahi umekuja
mzee wangu. Kuna tatizo hapa ... ”
“Lipi tena ?”
“Aaah ! Mke wangu amenifumania,” alisema
Masilinde bila woga , akili haikuwa yake. Moyoni
hakuwa tayari kumpoteza mama Mwaija ...
“Mke wako amekufumania ?”
“Ndiyo.”
“Na nani?”
“Na mtoto wake !”
“Na mtoto wake ?”
“Ndiyo.”
“Ambaye si wa kumzaa wewe?”
“Si wa kumzaa mimi. Nimemkuta naye .”
“Sasa ?”
“Anadai talaka, yuko ndani chumbani.”
“Hebu mwite. ”
Masilinde alikwenda kumwita mkewe , akamwita
na Mwaija , wote wakajaa sebuleni ...
“Mama pole sana ,” mzee Kimanama alimwambia
mama Mwaija .
“Asante , ila mimi nataka talaka yangu tu kama
amekwambia kuhusu kumfumania na
CHANZO: https://deusdeditmahunda.blogspot.com/
mwanangu. ”
“Ameniambia lakini unakumbuka mwaka huu ,
mwezi wa pili na wewe ulifumaniwa kule kwa
mzee Bakari na yule mzee wa genge la
mwembeni, ulimwambia mumeo ?”
ITAENDELEA
0 comments:
Post a Comment