Search This Blog

Tuesday, 17 May 2022

TANGA RAHA - 3

 







    Chombezo : Tanga Raha

    Sehemu Ya Tatu (3)



    Mama Fety alizungumza huku akijifuta jasho kwa kutumia tenge lake huku kwa mbali machozi yakimlenga lenga.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Jamani wapendwa zangu kupatwa na Dengue sio mwisho wa maisha unaweza ukanywa Parasetam na ukapona”

    “Sasa Eddy zungumza basi ni nani mwenye dengue”

    Mama Fety akazidi kunihimmiza huku machozi yakianza kumwagika na kumfanya nesi anaye fanana na Olvia kuanza kulia

    “Sasa nyinyi kiancho waliza ni nini?”

    “Eddy sema basii nani mwenye dengue?”

    “Hembu totokeni huku nje”

    Tukatoka kwenye chumba cha maabara na wakakaa kwenye moja ya benchi lililopo njee ya chumba hicho na huku wakinisubiria nizungumze.Nitakazama mlango wa kutokea nje na kuukuta upo wazi.

    “Sasa nisikilizeni kwa umakini…….Poleni sana kwa kulia kwani nimoja ya maisha ila ukweli ni kwamba HAKUNA MWENYE DENGUE”

    Nikachomoka kwa kasi kuelekea nje huku nikiwaacha Mama Fety na wezake wakinipormoshea matusi ya nguoni.Nikaendelea kukimbia hadi kwenye moja ya kituo cha taksi na kukuta gari mbili za za kukodi,nikaingia kwenye moja huku nikihema kwa kuchoka hadi dereva taksi akaanza kunishangaa

    “Kaka nipeleke Raskazoni”

    “Sawa elfu thelathini na tano”

    “Powa hata ukitaka hamsini nitakupa”

    “Ila ni Raskazoni sehemu gani kwa maana huu ni usiku mwingi kaka”

    “Kule karibu na kwenye nyumba ya mkuuwa wilaya”

    “Basi utafanya hiyo elfu hamsini”

    “Powa kaka”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Safari ikaanza huku miguuni nikiwa peku na kila safari ikiendelea nikamuona dereva taksi akinitazama kwa macho ya kunichunguza kuanzi chini hadi juu

    “Kaka mbona unaniangalia sana?”

    “Hapana kaka”

    “Au unashangaa mimi kuwa peku?”

    “Ndio sijui umekumbwa na majanga gani?”

    “Wee acha tu ndugu yangu”

    Tukafika getini kwangu nikashuka na kumuomba dereva taksi anisubirie kwa dakika kadhaa nikamchukulie pesa ndani.Nikagonga geti kwa muda kisha Hilda akafungua huku akionekana kutoka usingizini

    “Eddy saa hizi unatoka wapi?”

    “Hembu niache na wewe”

    Nikapimga Hilda kikumbo getini alipo simama na kuingia ndani nikapitiliza moja kwa moja hadi chumbani kwangu nikafungua kabati la nguo na kutoa kiasi cha pesa anacho kihitaji dereva na kutoka nje nikapishana na Hilda kwenye mlango wa kuingilia ndani ikamlazimu kunishika mkono

    “Eddy mbona sikuelewi?”

    “Hunielewi nini?”

    “Umerudi upo shakala baghala viatu huna,nguo zimejikunja kunja?”

    “Hembu niachie kwanza nimlipe jamaa wa watu kisha ndio tuzungumze”

    Nikatoka nje ya geti na kumlipa dereva taksi kisha nikarudi ndani na kumkuta Halda akiwa amesimama sebeleni akionekana kuwa na hasira

    “Haya niambie kilicho kupata huko utokapo ni nini na kurudi saa hizi usiku?”

    “Hembu niandalie chakula kwanza nile nipate nguvu ya kuzungumza “

    “Sawa chakula kipo pale mezani ila nahitaji kujua ni kwanini unarudi saa hizi?”

    “Uaniuliza hivyo wewe kama nani kwa maana sikuelewi?”

    “Sio unielewi nina haki ya kukuuliza mimi kama mpenzi wako na shemeji yako”

    Halda alizungumza kwa hasira huku akinijishika kiuno na kama wanavyofanaya wanawake wengine wanapokuwa na hasira akaazna kunipandisha na kunishuka

    “Wewe mwanamke wewee usitake nifanye kitu amabacho sijatarajia kukifanya kwa wakati huu”

    “Nipige uone”

    “Halda nitakuvuruga”

    “Utanivuriga……..Jaribuuu.Umetoka kulala kwa Malaya zako huko unanirudia usiku kumbe wewe ni Malaya kiasi hicho”

    “HILDA HEMBU NIACHE SITAKI MATATIZO NA WEWE”

    “Utanieleza umetoka kulala kwa nani?”

    “Kulala na mbu wa dengue”

    “Eddy usiniletee dharau wewe mwanaume unajua nitamwambia kila kitu Rahma unacho ki-fanya”

    “Ole waku siku ufungue domo lako utanijua kuwa mimi ni nani”

    “NITASEMA”

    “SEMA UONE NITAKACHO KIFANYA”

    “Nyoo umetoka kufumaniwa huko hata viatu umeviacha utakuja kufa wewe mwanaume maradhi mengi”

    “Nikifa si mimi wewe inakuhusu nini?”

    “Liangalie lile bichwa lake kama bomu la nyuklia”

    Sikutaka kuendelea kumsikilaza Halda maneno yake kwani nikiendelea kuyasikiliaza yatazidi kunichefua roho yangu na siku nzima imekuwa mbaya kwangu tangu asubuhi.Nikavuta kiti cha meza ya kukaa nikakaa na kuanza kula chakula alicho nipikia Hilda ambacho kusema kweli ni kitamu tofauti na vyakula nilivyo wahi kula kwenye maisha yangu

    “Chalula chako kitamu”

    “Nyooo kamwambie huyo Malaya wako uliyetoka kufumaniwa naye ndio akupikie chakula kitamu”

    “Hilda mbona umekuwa jeuri siku hizi jua kuwa penzi lako kwangu ni lamkataba muda wowote linaweza kusitishwa kama mkataba wa David Moyes”

    “WEWE NILETEE USENG* WAKO”

    “Unasemaje wewe mwanamke?”

    “Habari ndio hiyo wewe mseng* kama waseng* wengine”

    Nikanyanyuka kwenye kiti kwa hasira na nikapiga hatua za haraka kumfwata Hilda sehemu aliyo simama na akaanza kukimbia kuelekea ndani kwangu huku na mimi nikimkimbiza kwa nyuma na kabla hajashika kitasa cha mlango wa kuingilia chumbani kwangu akakanyaga maji yaliyopo juu tarzi na gafla akateleza na kuanguka kwa kwa nyuma na kichwa chake kikapiga chini kwa nyuma na damu zikaanza kusambambaa taratibu kutoka sehemu kilipo angukia kich-wa cha Hilda na kuufanya mwili wangu kuanza kutetemeka kwa woga



    Nikamsogelea Hilda na kukuta akirusha rusha miguu yake kama mtu anaye kata roho na kuzidi kunichanganya huku jasho jingi likianza kunitoka mwilini mwangu.Nikasimama kwa muda nisijue nini cha kufanya nikapiga hatua za haraka na kuingia jikoni na kuanza kutafuta kitu nisicho jua,Kwa kuchanganyikiwa nikajikuta nikizunguka jikoni zaidi ya dakika kumi huku kila ninacho kishika kwangu ninakiona ni kibaya.Nikachukua kitambaa cha kukaushia vyombo baada ya kuoshwa kisha nikatoka nacho hadi sebleni.Mapigo ya moyo yakazidi kunidunda kiasi kwamba hadi sauti ya mapigo ya moyo nikaanza kuyasikia yakidunda kwenye kifua changu hii ni baada ya kuto na kutokuuta mwili wa Hilda zaidi ya kuona michuruziko ya damu inayo elekea mlango wa kutokea nje

    Nikajishauri kwa muda kisha taratibu nikaanza kupiga hatua za taratibu kuelekea mlango wa kutokea nje na kabla sijaufungua mlango wa mbele ambao umefugwa na funguo kama Halda alivyo ufunga nikaamua kurudi jikoni huku akilini nikiwaza kwenda kuchukua kisu kwa ajili ya kujilinda kwa chochote kitakacho jitokeza mbele yangu.Nikanza kusogeza kitu kimoja baada ya kingine nikitafuta kisu na sikukiona kwa haraka nikachukua uma wa kulia chipsi na kutoka huku mkono mmoja nikiwa nimeshika kitambaa ambacho sikujua nitakitumia kwenye ni-ni.Nikafungua kwa tahadhari mlango wa nje na kuchungulia na sikuona kitu chochote zaidi ya gari la Hilda

    Nikaanza kujiuliza ni wapi mwili wa Hilda emekwenda na mbaya michuruziko ya damu imei-shia katika mlango wa kutokea nje .Nikageuka na kuufungua mlango na kuingia ndani huku akili ikiwa imevurugika nikapiga hatua za taratibu na kukaa kwenye mguu wa sofa kabla makalio yangu hayajafika kwenye mguu wa sofa taa zote za nyumbani kwangu zikazimika na nikajikuta nikisimama wima kama askari anaye subiria wimbo wa taifa lake.Gafla nikasikia watu wawili sauti ya kiume na yakike zikibishana chumbani kwangu na kujikuta nikizidi kutetemeka kwa woga huku mwili wangu ikinisisimka na vinyweleo vyote vikanisimama.

    Mabishano ya watu hao yakazidi kupamba moto huku mwanamke mwenye sauti kama Hilda akimuomba mwanaume huyo asitoke nje ila mwanaume anang’ang’ania kutoka.Akili yangu kwa haraka ikarudisha kumbukumbu ya mazungumzo ya bibi kuwa Hilda ni mke aliye olewa na jini lililopo kifungoni na sikujua kama ndio lenyewe linalo bishana au kuna jingine.Mwili mzima ukazidi kusisimka huku ukitetemeka na gafla nikastukia nikishikwa begani na kitu chenye mkono wa baridi kiasi kwamba hata kama umevaa jaketi baridi yake ni lazima ipeye kwenye mwili wakoCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Nikajua tayari nimekwisha na taratibu nikageuka huku nikiwa nimeyafumba macho yangu ili nisione ninacho kwenda kuonana nacho,Nikastukia kikinigusa shavuni kwa mkono wake wa baridi na kujikuta nikizidi kutetemeka kwa woga na kwa mbali nikaanza kuyafumbua macho yangu na nikajikuta nikizidi kuyafumbua kwa mshangao kiasi kwamba ninajikuta nikimeza fumba kubwa la mate kulisuuza koo langu ambalo limekauka

    “Rahma”

    Niliita kwa sauti ya chini huku nikitazamana na Rahma ambaye amesimama mbele yangu huku akiwa amevalia gauni jeusi kama anakwenda msibani

    “Shiiiiii”

    Rahma alikiweka kidole chake mdomoni akiniashiria nisizungunze kitu cha aina yoyote na kunifanya nikae kimya huku nikijiuliza maswali imekuwaje kuwaje hadi Rahma ametokea se-hemu hiyo.Akanishika mkono na taratibu tukaanza kupiga hatua za kutoka nje huku macho yangu nikiwa nimeyaelekeza mbele na sikutaka kutazama nyuma na laiti kama nitasikia mlio wowote miguu yangu imejiandaa kwa kazi ya moja tuu ambayo ni kukimbia kuyaokoa maisha yangu

    Tukatoka hadi nje huku Rahma akionekana kuwa na furaha ila kwangu sikuwa na furaha ya aina yoyote na isitoshe bado Rahma ananipa wasi wasi kwani mara ya mwisho kuzungumza naye jana mchana alidai kwamba anakwenda Dubai sasa siji imekuwaje Dubai imekuwa ni kwangu nilipo hamia.Rahma akanishika kiuno na kaniomba nifumbe macho kuna zawadi nzuri anahitaji kunipa,nikafunga jicho moja huku jengine nikiwa nimeacha kajiuwazi kadogo cha kuweza kuona ni nini anacho taka kukifanya Rahma

    ‘Hujafunga baby?”

    “Nimefunga jamani”

    “Mbona hilo jicho lako la kushoto linaona?”

    “Haya ng…….”

    “EDDY KMBIAAAAAAAAAAAAA………..!!!”

    Nikaisikia sauti ya Hilda ikiniomba nifanye ninacho takiwa kukifanya kwa wakati huo,Nikayafumbua macho yangu na kutazama ni wapi alipo Hilda nikastuskia macho yangu yakitua kwenye sura isiyo eleweka ni kipi ni kichwa na yapi ni macho kwani kwa haraka haraka mtu ambaye nilimdhania ni Rahma macho yake yameongezeka na kuwa matatu huku jicho moja likiwa kubwa katikati ya uso wake huku mengine madogo mawili yakiwa pembeni kwenye usawa wa mashavu yake.Kichwa chake kina mapembe marefu pamoja na ulimi mrefu na ndevu nyingi huku mwili wake ukiwa na umbo la Rahma

    Nikachomoka kwa kasi ya ajabu hadi getini na kukuta limefungwa na funguo ambayo sikujua ni wapi Hilda ameiweka cha kushangaza mtu huyo ambaye kwa haraka haraka nikajua atakuwa ni jini akapiga hatua za taratibu huku akicheka na kupiga makofi huku ulimi wake amabao ni mrefu kama ulimi wa kinyonga akiutoa nje na kuuingiza ndani huku vidole vyake virefu vikiwa na kicha ndefu kiasi kwamba nikazidi kuchanganyikiwa

    “KWA JINA LA YESU PEPO MCHAFU TOKAA MBELE YANGU”

    Nilizungumza huku nikiwa nimeunyoosha mkono wangu wa kulia kama wanavyofanya wachungaji wangi wanao ombea watu katika huduma zao mbali mbali za kidini na wala sikujua ni wapi maneno haya yalipo tokea.Mtu huyo akazidi kupiga hatua za taratibu huku akiendelea kucheka kwa kicheko cha kejeli

    “Eddy wewe una dhambi kama sisi Halllllooooooo…kwahiyo huwezi kunidhuru kwa lolote”

    Alizungumza huku ulimi wake akiutoa na kunilamba lamba nao kwenye mashavu yangu huku taratibu kucha zake akizipitisha kwenye kifua changu kusababisha shati nililo livaa kuchanika na kujikuta nikizidi kutetemeka na kuchanganyikiwa

    “Kuomba kwenyewe huwezi sembuse leo uje kunikemea……UMESHINDWA BWANA MDOGO”

    Nikaanza kusali kimoyo moyo huku nikizidi kuongeza juhudi za kuliita jina la Mungu wangu amweze kuniokoa.Jamaa akaninusa nusa kisha akapiga hatua mbili nyuma

    “UNA BAHATI LEO DAMU YAKO NA NYAMA YAKO HAIJAIVA IKIIVA JIANDAE KUWA CHAKULA CHANGU KAMA ULICHOKILA MEZANI LEO”

    Jamaa alizungumza huku akipiga hatua za kurudi nyuma na kuufanya mwili wangu uzudi kutetemeka hapo ndipo nikamuona Hilda akiwa ameegemea kwenye mlango wa kuingilia ndani huku akiwa analia,Jamaa akamsogela Hilda na kumsika kichwani na kumuachia kisha akapotea na kujikuta nikiburuzika taratibu kwenda chini huku mgongo wangu ukiwa unaburuzika kwenye geti nililo liegemea na kunifanya nizidi kuchoka kwani kwa siku mbili nilizo hamia kwenye hii nyumba zimekuwa ni sawa na miaka 200 ya mateso na shinda nynigi

    Nikazidki kuchanganyikiwa baada ya kumuona Halda akinifwata getini kwa haraka nikanyanyuka na kuanza kujaribu kulifungua geti

    “Eddy usinikimbie mimi sio jini”

    Halda alazungumza huku akiongeza kupiga hatua za kunifwata getini na nikajikuta nikisitisha zoezi la kwenda nje na kumtazama kwa umakini

    “Edy nakuomba unielewe mimi sio jini kama unavyo fikiria wewe.Kuna kitu ambacho sikuhitaji nikuambie mapema ila nitalazimika kufanya hivyo”

    “Hilda sikiliza kama ulinileta kunipangisha kwenye hii nyumba ili muje kunila nyama mume-shindindwa nipo tayari nipoteze pesa nilizo lipa kodi niondoke zangu kwenye hii nyumba”

    “Eddy kukimbia nyumba sio suluhisho lamatatizo”

    “Ila”

    “Kuwa na mimi ili haya matatizo yaishe”

    “Wee wee weee usinichanganye kabisa kwanza sijui yule aliyekuja kunilamba lamba sijui ni mumeo alafu bado unaniambia mimi nibaki na wewe.Ndio maana tangu jana nilikuwa niki-kuambia uondoke ila hukutaka kunisikia”

    “Eddy hembu tulia nikusimulie ninacho hitaji kukuambia ukweli kuhusu mimi”

    “Hiyo ndio gia yako ya kunitongozea mimi si ndio?”

    “Hapana Eddy tulia basi nikuambie kitu…….nakuomba twende ndani tukazungumze hilo swala”

    “Wewe na giza lote humo ndani unataka mimi niingie”

    “Wewe twende”

    Hilda akanishika mkono na kuanza kunikokota japo nafsi yangu inasita ila sikuwa na ujanja zaidi ya kumfwata Hilda anapo elekea.Kitendo cha kufungua mlango taa za nyumba nzima zikawaka pasipo kuwashwa na sisi,Michirizi ya damu yote nikakuta haipo kwenye sakafu na nikabaki nimeduwaa hadi Hilda ananikalisha kwenye Sofa ndio nina stuka

    “Eddy”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Naam”

    “Upo tayari kusikliza nitakacho kuambia?”

    “Nipo tayari endapo na wewe utakuwa tayari kuondoka ndani ya nyumba yangu”

    “Sawa nitafanya hivyo…….Eddy ninakuomba unisamehe kwa kukuficha ukweli wa maisha yan-gu,Mimi nimezaliwa katika mchananyiko wa binadamu na Jini”

    “TOBAAAAA….KWA HIYO WEWE NI JINI?”

    “Usiwe na papara…….Siwezi kusema moja kwa moja kuwa mimi ni jini japo ninazitambua sheria na misingi yao…..Baba yanguni ni jini ila mama yangu ambaye sasa ni marehemu yeye alikuwa ni binadamu wa kawaida….Wtu wengi husema watoto wa aina hii wengi wao hawaonekani ila si kweli kuna mambo ukiyafanya kipindi mtoto wa aina hii akiwa mdogo basi maisha yake ataishi kama bidanamu wengine…..Mimi nimeolewa na jini na yule aliye kuja pale ni mdogo wa mume wangu aliyopo gerezani”

    “Haaa shemeji gani ana sura mbaya kiasi kile?”

    “Hahaaaa pale alijaribu kukutisha ila kama mwanzoni ulimuona alivyo kuja katika muonekano kama Rahma”

    “Sasa kwanini siku zote hukuniambia hili swala?”

    “Usinge weza kustahimili na ungepata wasi wasi ambao ungeyagharimu maisha yako”

    “Kivipi?”

    “Ungeweza kuwa hata kichaa au ungekufa kabisa”

    “Mmmmmmm…….”

    “Usigune kila ninacho kuambia kipo kwenye ukweli wa maisha yako na kinacho kutokea si ndo-to japo kwa wakati huu mimi sina nguvu za kijini na nibinadamu kama ilivyo wewe”

    “Acha zako wewe haupo sawa na mimi…..Sasa lipo wapi jeraha la kichwani mwako mbona silio-ni?”

    “Niliponywa na shemeji yangu”

    “Sasa ilikuwaje nilisikia unazungumza naye chumbani na huku yeye akiwepo hapa sebleni”

    “EADDY SIKU ZOTE MAJINNI YANAWEZA KUJIGAWA KATIKA MAUOMBO TOFAUTI TOFAUTI KWA WAKATI MMOJA”

    “Basi ninakuomba mimi leo nisilale hapa”

    “Unataka kwenda wapi?”

    “Popote bora iwe nje ya hapa”

    “Sawa nenda kajiandae”

    “Wewe huondoki?”

    “Wewe nenda kajindae”

    Nikanyanyuka na kuingia ndani kwagu nikafungua droo na kutoa nguo nyingine safi na kuzivaa nikachukua kiasi chote cha pesa kilichopo kwenye kabati langu na kurudi sebleni na kumkuta Hilda akiwa amesimama akinisubiri huku akiwa amevali kanga moja

    “Unakwenda hivyo na kanga?”

    “Ndio”

    “Kwa nini sasa?”

    “Nimeamua”

    Sikutaka kubishana naye zaidi ya kutoka nje na sote tukaingia ndani ya gari na tukafika kwenye hotelo moja iitwayo NAIVERA nikaingia ndani na kumuacha Hilda kwenye gari.Nikalipia chumba na kutoka nje kuzungumza na Hilda ila sikumkuta yeye wala gari lake,nikaingia kwenye chumba nilicho kodi kwa siku tatu ili niipumzishe akili yangu kwa majanga yaliyo nikuta kidogo nikapata usingizi ambao sikuota kitu ca aina yoyote.Nikaja kustuka baada ya simu ya mezani kuita.Nikaitazama kwa muda kisha nikaipokea na kusikia sauti nzuri ya kike

    “Za asubuhi ndugu mteja”

    “SALAMA”

    “Unakaribishwa katia kupata kifungua kinywa je uletewe chumbani kwako au utakuja kunywa katika kumbi zetu”

    “Nileteeni huu huku”

    “Asante na asubuhi njema”

    Simu ikakatwa na nikajirudisha kitandani na kuanza kufikiria hii hatua ngumu ninayo ipitia kwenye maisha ya ngu,Mlango ukagongwa na nikaufungua akaingia msichana mwenye uzuri wa pekee huku akiwa ameshika sinia lenye vikombe vya chai na sahani iliyo funikwa.Kiuno chake chembaba kimebeba mzigo wa makalio makubwa kiasi yaliyo jifichwa kwenye kijisketi cheusi kifupi kinacho yaacha mapaja yake wazi kwa sehemu kubwa na nikajikuta mwili wangu ukianza kusisimka.Kifua chake kikabeba chuchu kubwa kiasi na kunifanya nibaki ninameza mate ya uchu huku koki yangu ikisimama taratibu.Kwenye sura ndio amenimaliza kabisaa kwa jinsi alivyo jipara huku nywele zake akiwa ameziweka kama Rihana nikabaki nimeduwaa huku nikikiangalia kidoti chake cheusi kilichopo karibu na pua yake

    “Karibu kifungua kinywaa”

    Nikaendelea kumtazama kwa mshangao na wala sikuweza kusikia anacho niambia ni nini

    “Kaka karibu chai”

    “UMEOLEWA”

    “Ndio na nini mtoto mmoja”

    “Ni muda gani unaweza ukapata muda tukazungumza?”

    “Sasa hivi tunaweza tukazungumza tuu kwani ndio muda wa mimi kutoka kazini”

    “Una itwa nani?”

    “Habiba”

    “Ohoo unajina zuri kama wewe mwenyewe”

    “Asante zungumza haraka haraka kwa maana ninahitaji nika singout niende nyumbani”

    “Ok unakalia wapi?”

    “Karibu na Makorora Hospitali”

    Nikajikuta hata ninacho hitaji kumuambia kikiyayuka akilini mwangu kama barafu ukiliweka juani na kubaki nikimtazama kama ninajiandaa kupiga picha ya mnato

    “Halooo kaka”

    “Eheeee”

    “Mbona kimya?”

    “Mmmm haya mwaya shemeji ana faidi”

    “Asante wangu basi ninaomba niende”

    “Haya mwaya ila jioni si utakuja?”

    “Wapi?”

    “Kazini”

    “Ndio ninaingia saa nne usiku”

    “Haya mwaya”

    Habiba akafungua mlango na kutoka nikabaki nikijirusha kitandani na kuurudia tena usingizi na wala sikuwa na wazo la kwenda shule kufundisha.Nikastuka mida ya saa saba mchana nikaingia bafuni nikaoga na kunywa chai kisha nikawasha tv na kuanza kutafuta kipindi kizuri kitakacho ifurahisha nafsi yangu.Nikapata kipindi kizuri na kuanza kufwatilia kwa umakini mchezo wa mereka hadi inatimu saa tisa na nusu nikatoka nje ya hoteli nikapata chakula cha mchana na kurudi chumbani kwangu na kujitupa kitandani na kuanza kuutafuta usingizi ambao haukuja kabisa.Mida ya usiku nikatoka na kwenda kula chakula cha usiku.Nikiwa ninarudi chumbani kwangu nikamuona Habiba akiwa anaingia Hotelini akiwa amevalia nguo za kawaida kiasi kwamba uzuri wake umezidi kuongezeka.

    Akanipungia mkono kwa ishara ya kunisalimia na mimi nikamjibu kwa kumpungia mkono kisha nikapiga hatua za kumfwata ila akanikonyeza na kunionyesha mzee wa pembeni aliye kaa kwenye kiti na nikajikuta nimesimama huku nikizuga kwa kuitoa simu yangu mfukononi na kuanza kuiminya minya.Kwa ishara akanimbia aliye kaa kwenye kiti ni bosi wake sikuwa na jinsi zaidi ya kuelekea chumbani kwangu,Hazikupita dakika nyingi mlango ukagongwa na nikaufungua mlango na kumkuta Habiba akiwa amevalia nguo zake nilizo muona nazo,nikamkaribisha ndani na moja kwa moja akakaa kitandani

    “Za muda Habiba?”

    “Sio salama”

    “Kwa nini?”

    “Ninamatatizo makubwa kaka yangu wee acha tuu”

    “Matatizo gani hayo ndugu”

    “Ni historia ndefu kidogo ila ngoja tu nikuambie”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Ehee”

    “Nilikuabia nina mume na mtoto mmoja?”

    “Ndio”

    “Basi mume wangu mimi anafanya kazi Saruji…..na siku zote huwa nilikuwa ninasikia kuwa anamwanamke wa nje tofauti na mimi”

    “Ehee”

    “Watu ambao walikuwa wananimbia siku zote nikawa ninawabishia nikijua ni wafitinishaji wa ndoa yangu…..Sasa leo mchana muwe wangu amefumaniwa na mke wa mtu,amepigwa kiasi kwamba amelazwa hapo Bombo hospital”

    “Duuu pole sana”

    “Weee acha tu kaka ninaumia sana mwanaume ninaye mpenda na kumuamini kunifanyia kitu kama hiki sijui ni nini alikosa kwangu”

    Habiba alizunumza huku machozi yakianza kumwagika na taratibu akaanza kujifuta kwa kutu-mia kitambaa alicho kishika

    “Sasa hali yake inaendeleaje?”

    “Hali yake sio nzuri…..na mbaya zaidi huyo mwanamke aliyekuwa akimchukua mumewe ni bondia maarufu hapa mjini”

    “Duuu pole sana kwa hilo sasa itakuwaje?”

    “Yaani hapa nilipo sielewi…..kurudi kwangu ni aibu watu wananicheka mimi?”

    “Mtoto wako yuko wapi?’

    “Yupo Kange kwa bibi yake mzaa baba”

    “Mmmm pole sana”

    “Yaani kaka yangu hapa sijui nifanyaje nimeomba ruhusa ya kumuuguza mume wangu ila hata hamu ya kwenda huko hospitalini sina”

    Habibi alizungumza huku taratibu akijisogeza nilipo huku akiendelea kulia na taratibu kichwa-chake akakilaza kwenye mapaja yangu na mkono wangu mmoja nikauweka kwenye ziwa lake na kuliminya kumfanya astuke na kunitazama kwa jicho kali la hasira



    “Ohh samahani dada yangu”

    Nilizungumza huku nikiutoa mkono wangu kwenye ziwa lake na taratibu Habiba akajinyanyua kutoka alipo jilaza kwenye mapaja yangu na kukaa kitako

    “Samahani tena dada yangu kwa kukushika......”

    “Usijali kaka yangu ila kwa sasa ninaomba mimi niondoke”

    “Sawa hakuna shaka”

    “Naomba unipe namba yako ya simu”

    Nikamtajia Habiba namba zangu kisha na yeye akataja zake nikajaribisha kuzipiga kabla hajato-ka na simu yake ikaita

    “Kaka hivi nisave nani?”

    “Save Eddy”

    “Mmmmm”

    “Mbona unaguna”

    “Yaani majina ya Eddy sina imani nayo kabisa tangu mume wangu aniafanyie hili tukio nimeto-kea kuyachukia kupita maelezo”

    “Kwani anaitwa nani?”

    “Ana mjina mbaya kama huo wako wa EDDY”

    Nikabaki nikicheka Habiba akajiweka sawa nguo zake na kutoka chumbani na kuniacha nikiji-liaza chali kitandani huku nikiikariri namba yake kwa kwichwa ili isiwe rahisi kuisa-hau.Nikanyanyuka na kufunga mlango kwa funguo kisha nikarudi kitandani huku nikijitahidi kuutafuta usingizi kwa juhudi zote.Nikachukua mto mmoja nikaukumbatia huku nikiuwekea mguu kwa juu ndani ya dakika tano nikaanza kuhisi nilicho kikumbatia sio mto ila kinaendana na umbo la mtu.Nikakurupuka na kujitoa mikononi mwa msichana mzuri aliye kaka kitandani huku akiwa na night dreas tu na katika kumbu kumbu zangu nilimuona huyu msichana siku yangu ya kwanza alipo nitokea Olvia Hitler na alikuwa ni miongoni mwa wasichana aliye kuwa akimpepea na kitu kinacho fanana na mkia wa Simba

    “Usiniogope kwani sikuja kwako kwa mabaya”

    “Wewe ni nani?’

    “Unanfahamu ila itanibidi nijitambulishe jina langu”

    “Sasa jamani mutanniua mimi”

    “Huwezi kufa.....kwanza mimi ninaitwa Vicky ni jina ninalo litumia nikiwa ulimwenguni ila niki-wa nyumbani nina jina langu”

    Sikuweza kuogopa sana kutokana nimesha wazoea hawa viumbe ambao wananiandama tangu nilipo hamia katika nyumba yangu mpya

    “Mtakatifu Olvia Hitler amenituma nije kukupa ujumbe huu”

    “Ujumbe gani?”

    “Yeye kwa sasa hayupo katika maeneo unayo ishi amekwenda nchini kwetu kwa ajili ya mazungumzo na baba yake mzazi”

    “Haya nashukuru.....Jibadilieshe na uniachie mto wangu”

    “Hapana kuna kitu nahitaji kutoka kwako”

    Vicky akanifwata kwa kasi na ndani ya dakika moja nikajikuta nipo kama nilivyo zaliwa kisha taratibu akaanza kuninyonya mdomo wangu hapo ndipo nikagundua ladha iliyopo kwenye mate ya mwanadamu na jini.Vicky akaivua nightdreas yake na kuimalizia nguo ya ndani kisha akanipandisha kitandani

    “Unataka unione kama nani?”

    “Kivipi?”

    “Unataka unione katika muonekano kama wa msichana gani unaye mpenda duniani?”

    “Mmmmmm Angelina Jolie”

    Ndani ya sekunde kadhaa Vicky akageuka na kuwa kama Angelin Jolie mwan mke mwenye mvuto wa kudumu duniani ambaye ni mcheza filamu maarufu nchini Marekani na duniani kwa ujumla na nikabaki nimeduwaa

    “Ume fanyaje fanyaje......!!?”

    “Unataka na wewe ujue?”

    “Ndio”

    “Tumalize kwanza alafu nitakufundisha”

    Vick akiwa katika muonekano wa Angelin Jolie akaishika koki yangu na kuikalia na shuhuli ikaanza huku moyoni nikijikuta ninasahau kama huyo ni jini na anacho kifanya ni kitu cha kuiba utamu wa Rahma na Olvia mbaye hadi sasa hivi hakuwa wazi kwangu

    “Potelea pote tutajua mbele ya safari”

    Nilizungumza kimoyo moyo huku nikiendelea kuminya kiono cha Vicky na kwajinsi ya wem-bamba alio nao Angelin Jolie ikazidi kunipa hamasa ya kuzidisha kasi kwani kila ninavyo muweka anakwenda.Nikazidi kugundua kuwa katika hali ya kawaida wanawake ambao ni binadamu wanautamu wao na hawa majini nao wana utamu wao ambao umewazidi kwa kiasi kidogo japo sio sana.Mechi ikaendelea huku Vicky akitoa miguno kama ya raha na kadri nilivyo zidi kuongeza kasi ya kumburudisha Vicky ndipo akaanza mchezo ulio anaza kunikosesha imani na yeye

    Sura zake zikaanza kubadilika taratibu kutoka sura moja hadi nyingine na nyingi ni zawaa-wake maarufu duniani akiwemo Beyonce na Nick Minaj nikazidisha kasi na akabadilisha sura yake na kuwa Rihana na nikazidi kuongeza kasi ili nifurahie kuziona sura za watu wanao fwa-ta.Mapigo yakaanza kudunda kwa kasi na kujikuta nimeduwaa kama nimegandiswa na rimoti kwenye Tv hii ni baada ya kuiona sura yangu ikiwa inanitazama huku ikiwa na macho ya kike yanayo nirembulia kiasi kwamba nikabaki nimetulia

    “Vipi mbona uendelei?”

    Vicky aliniuliza huku sauti yake ikiwa kama yangu na zinafanana ila tofauti iliyopo kati yetu ni miili tu, Kwani Vicky mwili wake umebaki kama wa Angelin Jolie ila kwenye sura yake ndio ipo sura yangu.Vicky akacheka kwa kicheko cha ajabu na kuishika koki yangu na kuikalia tena vizuri na kuanza kuikatikia huku nikiwa nimelala chali.Taratibu akaanza kukishusha kichwa changu ili nimbusu na gafla sura yake ikabadilika na kuwa mbaya ya babu mzee wa miaka 85 kwenda mbela na galfa nikajikuta nikipoteza faamu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ***

    Kwa mbali nikahisi mlango ukigogwa kwa nguvu nikapapasa papasa kwa kutumia mkono wangu na kugundua nipo juu ya godoro,nikafumbua macho yangu huku kichwa kikiwa kinani-uma sana.Nikakaa kitako na kujikuta nipo kama nilivyo zaliwa.Saa ya ukutani inaonyesha ni saa nane mchana nikanyanyuka na kujifunga taulo na kwenda kufungua mlangoni na kukutana na watu wasio pungua kumi huku kati yao wakiwemo askari watatu,meneja aliye nionyesha jana Habiba na wafanyakazi wengine wa hoteli hiyo na walipo niona wote wakashtuka

    “Yupo hai”

    Mmoja alizungumza huku akininyooshea kodole na kunifanya nizidi kushangaa

    “Vipi kwani?”

    Nilizungumza kwa sauti nzito iliyo jaa mikwaruzo ya makoozi na kuawafanya watu waliopo mlangoni kutazamana tazamana huku wakitupiana swali nililo wauliza

    “Wewe ni bwana Eddy si ndio?”

    Polisi mmoja aliniuliza huku akiwa ananitazama kwa macho makali na mimi nikabaki nikimtazama kwa macho yaliyo jaa usingizi mwingi

    “Ndio”

    “Sisi tulipata taarifa leo asubuhi kwamba kuna mteja wao ambaye ni wewe amefariki ndani ya chumba hichi”

    Nikastuka na wenge lote la usingizi likakata na kuendelea kumsikiliza askari huyu anaye zun-gumza kwa lafudhi ya kikurya

    “Basi sisi tukaja hapa kwa lengo moja ili tuchukue maiti na hapa tulikuwa tunamsubiri huyu meneja ili atupe ruhusa tuvunje hilo limlango”

    “Kwa nini mulinihisi nimekufa?”

    “Kwani nikawaida ya muhudumu wa usafi kufanya usafi pale ifikao saa nne asubuhi kwenye vyumba vya hoteli na kwawakati huo mteja unatakiwa kuwa nje ila ni tofauti na wewe uliye ku-wa ukigongewa mlango na hufungui hadi sasa hivi”

    “Sijafa nashukuru”

    Nikaufunga lango na kuacha minongono ikiendelea mlangoni nikapitiliza moja kwa moja hadi bafuni nikajitazama kwenye kioo huku nikiwa ninauchunguza mwili wangu na sikuona mabadiliko ya aina yoyote.Nikafungua bomba la maji ya mvua na kuoga kisha nikarudi chumbani kwangu na kuvaa nguo zangu na kutoka nje na sikukuta mtu mlangoni ila kilicho nikosesha raha ni baadhi ya watu kunitazama huku wakininyooshea nyoshea vidole huku wengine wakinong’onezana.Nikaondoka eneo la Hoteli na kwenda moja kwa moja sehemu moja inayo itwa Forodhani ambapo ni sehemu ya watu kupumzika na ili kutafakari maisha yao na unaweza kujipatia chakula kutoka katika mgahawa ulipo eneo hili huku ukiitazama bahari kwa mbali kidogo

    Nikakaa kwenye meza ya kwangu peke yangu na kununua gazeti kwa muuza magazeti aliye-pita karibu yangu na kusubiria niletewe supu niliyo iagiza kwa muhudumu wa eneo hi-li,Nikaanza kusoma gazeti ambalo ni la michezo nikafungua kurasa moja baada ya nyingine huku nikitafuta ni sehemu ipi yenye habari nzuri ili nisome.Moyo ukaanza kudunda taratibu baada ya kuiona picha ya Angelin Jolie akiwa na mume wake Brand Pitty na kujikuta nikizikumbuka sura za jana usiku.Nikafungua kurasa ya mbele na kujikuta nikizidi kuliona gazeti ni chungu.Hii ni baada ya kuiona sura ya Beyonce na Nick minaj picha hizi zikiwa zimeandikwa maandishi yaliyo zidi kunipa hofu

    ‘BEYONCE KATIKA SURA MOJA NA NICK MINAJI’

    “Samahani kaka hichi kiti kina mtu?”

    Ikanilazimu kusha gazeti kidogo ili niweze kumuona mtu anaye nisemesha na kukutana na sura ya dada mmnene kiasi aliye valia baibui jeusi huku akiwa amejipara ma kuifanya sura yake izidi kuwa kuwa nzuri

    “Hakina mtu?”

    “Ninaweza kukaa?”

    “Ndio”

    Nikaachana naye na kuendelea kulisoma gazeti langu,muhudumu akaniletea supu yangu nikaanza kuinywa taratibu huku nikiendelea kulisoma gazeti langu katika upande wa hadisi za muandishi mashuhuri Tanzani E.J.Shigongo

    “Samahani kaka unaweza ukanipa ukurasa wan je?”

    Nikamchomolea ukurasa wa nje na mimi nikaendelea kutiririka na story iliyoanza kunipoteza mawazo yangu na kusahau kipindi kigumu cha maisha ninacho pitia.Nikajikuta nikicheka mweyewe baada ya kukuta kisa kilicho niacha nifurahi

    “Ahaaa huyu jamaa nom asana”

    Nilijikuta nikijisemea mwenyewe na kumfanya dada wa watu kuacha kusoma anacho kisoma na kuniuliza

    “Mbona unacheka?”

    “Kuna jamaa kwenye hii story ya Shingongo amenifurahisha sana”

    “Ahhh ila huyo kaka anajua kuandika sana story?”

    “Tena sana huwa ninamkubali sana sijui kama kuna mtu anaweza kumfikia jamaa kwa maana anakuteka kihisia na kujikuta unacho kisoma kinapita kama mkanda wa video kwenye akili ya-ko”

    “Ndio ila kuna jamaa mmoja hivi nilizikuta story zake facebook naye akijitahidi anaweza akam-fikia Shigongo”

    “Kwa Tanzania hakuna anaye muweza huyu jamaa”

    “Kaka huyo kaka ninaye kuambia anaandika stori nzuri kiasi kwamba unajikuta unafurahi?”

    “Anaitwa nani?”

    “Anaitwa Eddazaria G.Msulwa ana page yake inaitwa Story za Eddy humu ndani kunastory nzuri balaa”

    “Mmmmm hao waandishi ubwabwa hawawezi kufika level za huyu jamaa”

    “Una account ya Facebook?’

    “Sina”

    “Ndio maana unabisha ila kwa huyu jamaa ninaye kuambia ana uwezo mkubwa”

    “Ahhh hao waandishi wa Facebook wengi wao mawazo yao finyu kama kidole cha mwisho huwa hawana jipya”

    “Wee kaka unadharau kweli mimi nakuambia huyo jamaa anakipaji cha tofauti na wengine am-bao nimewahi kuzisoma story zao.....Kama huto jali ngoja niingie sasa hivi Facebook nikuo-nyeshe hizo story”

    “Powaa”

    Nikaendelea kusoma story huku nikisubiria dada akiminya minya simu yake kubwa na wengi wetu tumesha zoea kuziita screen touch.

    “Ehee hizi hapa nimezipata”

    Dada akanipa simu yake kabla sijaanza kuzisoma simu yake ikaita na jina lililojitokeza ni My husand(mume wangu) ikanibidi nimrudishie simu yake na akaanza kuzungumza na mtu wake

    “Baby jamani mbona nimefika muda mwingi sijakuona”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mimi nimekaa hapa chini kwenye mti nipo na kaka mmoja hivi amevaa shati jeusi”

    “Jamani wewe mwanaume una wivu....Haya naondoka”

    “Sawa jamani naondoka natafuta pa kukaa”

    Dada akakata simu na kunitazama huku akishusha pumzi nyingi

    “Mume wako anaoenekana na wivu sana ehee?”

    “Wee acha hapa nimemuambia nimekaa na mwanaume basi anataka nihame.....Acha nifanye hivyo kaka yangu kwa maana akinikuta hapa anaweza akanipiga vibao mbele za watu”

    “Sawa mwaya”

    “Asante kwa gazeti na ukarimu wako”

    “ Na wewe pia asante kwa kampan yako”

    “Ila kaka nakushauri wewe jiunge na Facebook usome story za huyu jamaa alafu bado ni bwana mdogo sana”

    “Ahaaa kumbe yeye mwenyewe bado ni mdogo na nyinyi munazisoma story zake?”

    “Udogo sio ishu ila anashangaza kwa jinsi ya story zake zilivyo tamu”

    “Haya mwaya”

    Tukapeana mikono na dada niliye kaa naye kisha akaenda kukaa kwenye meza nyingine na ndani ya dakika mbili kuna jamaa akakaa kwenye kiti kilichopo kwenye meza aliyopo yeye huku akionekana akiwa na hasira na akaanza kufoka foka na kila kitu anacho kizungumza kinahusiana na yeye kukaa na mimi

    “Sasa jamani kukaa tu na mwanaume ndio unanifokea fokea kiasi hicho mbele za watu?”

    “Kwanini ukae naye hukuona meza zote hizi?”

    “Zilikuwa zimejaa watu”

    “Wewe mwanamke Malaya sana na yule bwege pale ndio anakutia jeuri na kujifanya unanipan-dishia sauti?”

    Jamaa alizungumza huku akininyooshea kidole mimi ikanibidi niliweke vizuri gazeti na kuwatazama jinsi wanavyo jibizana

    “Hembu muache kaka wa watu wala yeye hausiani na mimi kukujibu wewe....Ila ukweli ni kwamba mwanaume wewe una gubu.Unadhani nilivyo kaa naye ndio amenivua chupi?”

    “Wewe mwanamke nitakuwasha makofi sasa hivi mbele za watu”

    “Mimi si nimeshakuwa ngoma yako hata ukinipiga unadhani nitashangaa.Wewe nipige tuu”

    Watu wa meza nyingine waliacha kufanya wanayo yafanya na tukaendelea kuutazama ugomvi ila kwangu nikajikuta moyo wangu ikiniuma kwa jinsi jamaa anavyo mgombesha mpenzi wake pasipo kuwa na sababu ya msingi.Jamaa akamzaba mpenzi wake kofi ambalo lilisikika vizuri kwa watu tulio karibu na meza yao.Nikashindwa kuvumilia nikaliweka gazeti mezani na kwenda hadi kwenye meza walipo wao

    “Na wewe Chok* umefwata nini hapa?”

    Jamaa alaizungumza huku akiwa anahema kwa hasira na mbaya zaidi mimi ni mrefu na jamaa ni mfupi kiasi kwamba nikawa ninamtazama kama mtoto mdogo

    “Acha kuwanyanyasa wanawake hujui hawa ndio wazazi wetu”

    “Wewe fala nini...Nani awe na mama Malaya kama huyu mwanamke hapa?”

    “Rama mimi leo unaniita Malaya........”

    “Wewe Malaya na wazazi wako wotee Malaya munakazi ya kukalia umasikini wa kuomba omba”

    “Nashukuru mimi ni masikini bora na wewe kwenu mulio matajari ila ninaona hapo ulipo fikia kunatosha ni bara tuachane”

    Dada wa watu alizungumza huku akimwagikwa na machozi kiasi kwamba nikazidi kumuonea huruma

    “Oya kaka hembu kuwa mstaarabu,usimtukane mwenzoko ni maswala ya kukaa chini na kuya-maliza kumbukeni nyinyi ni wapenzi”

    “Wee niaje kwanza juu wewe ndio muhusika wa hili swala alafu unaniletea michongo yako ya kiseng* seng*”

    “Powa ila tazama jinsi munavyo jizalilisha mbele za watu”

    “Hayakuhusu.......Wewe Malaya si umesema tuachane sasa lete hiyo simu niliyo kununu-lia,cheni,herein na saa vyote nivulie”

    Dada wa watu akaanza kuvua kitu kimoaja baada ya kingine huku akilia ikanibidi nimzuie asiendelee kuvivua

    “Kwani vitu vyote hivi vina gharimu shilingi ngapi?”

    “Wewe vipi......Huna pesa ya kunilipa”

    “Sema ni shilingi ngapi nikulipe?”

    “Laki nne na nusu”

    “Subiri”

    Nikafungua waleti yangu iliyo jaa pesa alizo niachia Rahma kisha nikaanza kumuhesabia kiasi anacho kihitaji kisha nikamuwekea juu ya meza na jamaa akabaki ameshangaa

    “Unashangaa nini chukua pesa zako uondoke”

    Jamaa akazichukua na kuzihesabu na kukuta zipo kamili kisha akamtazama mpenzi wake anaye lia

    “Wewe ingekuwa si huyu jamaa ningekuvua hadi chupi”

    Dada akataka kuzungumza ila nikamziba mdomo na kujua kitakacho endelea hapo kitakuwa nai fujo.Jamaa akaondoka na kuwaacha watu wengine wakimshangaa huku akionekana mshamba.Nikamshika mkono dada na kurudi naye kwenye meza tuliyo kuwa tumekaa naye na nikapata kazi ya kuanza kumbembeleza hadi akanyamaza

    “Hivi yule jamaa yako ana akili vizuri?”

    “Hana hata kidogo”

    “Sasa na wewe imekuwaje ukawa naye mwanume kama yule?”

    “Kaka yangu wee acha tuu ni mambo ya dunia ndio yananifanya nikajikuta nipo naye”

    “Kwanza umekula?”

    “Sijala kaka yangu....hapa ninapo zungumza nina mia tatu ya dala dala tu kwani tulipanga na ja-maa tuje tukatane hapa ili anipe pesa za kuitunza familia yangu”

    “Pole kwa hilo”

    Nikamuita muhudumu na dada akaangiza chakula anacho ana kihitaji na baada ya muda kikale-tewa chakula anacho kihitaji nikamuacha ale kwanza ndio tuzungumze.Akamaliza na akanishu-kuru kwa msaada nilio mpatia

    “Kwa hiyo wewe unaishi na wazazi?”

    “Ndio ila wazazi wangu ni wazee sana ambao hawajimudu kimaisha na mimi ndio mtoto wao wa pekee niliye bakia nikiwashuhulikia wengine wawili wa kiume ambao ni kaka zangu wamekuwa mateja na wala hawana muda wa kujishulisha”

    “Mmm pole sana kwani unaishi wapi?”

    “Ninaishi Magomeni”

    “Mmmmm na wewe una mpango gani wa kimaisha kwa maana jamaa ndio hivyo amesha kua-cha?”

    “Yaani hata mimi sijielewi.....Ila kidogo ninafanya fanya kazi za kutengeneza dawa za miti sham-ba,Kazi ambayo alinifundisha baba ila kwa hapa mjini hailipi kutokana watu wengi wanakimbi-lia kwa wamasai na sisi watu wa kawaida hutuacha tukiwa na ujuzi mwingi kupita hata hao wamasai”

    “Ahaaa sasa wewe unatengezeza dawa gani na dawa gani?”

    “Dawa ya chango kwa wanaweke,dawa ya kuongeza nguvu za kimume,dawa za kufukuza majini na vimizuka daw...........”

    “Ehee hapo hapo kwenye hiyo dawa ya kufukuza majini unaweza ukanisaidia?”

    Ndio ukihitaji ninaweza kwenda kukuchukulia?”

    “Wapi?”

    “Nyumbani”

    “Powa basi kama huto jali nikupe pesa ukodi boda boda ukanichukulie hiyo dawa”

    “Sawa”

    “Unaitwa nani?”

    “Mwajuma”

    “Sawa mimi ninaitwa Eddy”

    Nikatoa noti ya elfu kumi na kumkabidhi akaaondoka huku nikibaki na pochi yake kubwa ambayo sikutaka niufungue ndani.Ndani ya dakika 45 akarudi akiwa na kifuko cheusi na ku-niomba twende nyumbani kwangu.Sikuwa na kipingamizi tukakodi bajaji hadi nyumbani kwangu nikafungua geti tukaingia na dereva bajaji akaondoka baada ya kumlipa.Tukafika sebleni na kushangaa kumuona mwenzangu akianza kuvua baibui lake na kubakiwa na skintait iliyo mchora umbo lake lililo jazia huku kifuani maziwa yeke makubwa kiasi yakiwa yamezibwa na sidiria na kuyafanya yajichore vizuri.CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Gafla akaanza kuzichangua nywele zake huku akipiga chafya za mfululizo kiasi kwamba nikaanza kumuogopa.Akasimama kwa muda akitazama mlango wa kuingilia chumabi kwangu na akaanza kunguruma kama Simba huku mwili wake akiutunisha misuli

    “HAPA NDIPO KWENYE MLANGO WA KUINGILIA KUZIMU”

    Alizungumza kwa sauti nzito ya kiume na sikujua ameitolea wapi,akanigeukia huku sura yake ikiwa imejikunja na kuufanya uzuri wake wote kama mwanamke kupotea

    “TUNAHITAJI DAMU YAKO”

    “Ehhhh......!!”

    “DAMU YAKO”

    Akaanza kupiga hatua zenye vishindo vya hali ya juu huku akinifwata taratibu,nikaona sio se-hemu nzuri ya mimi kukaa nikachomoka kwa kasi na kuufungua mlango wa kutokea njee na kwapupa nilizo nazo zilizo chaganyikana na woga nikajikuta nikipiga mwereka mmoja mkali na kuanguka kifudi fudi kama mtoto anayeanza kutembea.Nikastuka zaidi baada ya kuona miguu ya watu wawili wakiwa wamesimama mbele yangu.



    Nikainyanyua sura yangu na kukutana na Hilda akiwa na msichana mwengine ambaye siku-wahi kumuona hata siku moja.Wakabaki wakinishangaa kwani hawakujua ni kitu gani kinacho-nikimbiza.Nikananyayuka na kuanza kujifuta futa vumbi lililo jaa kwenye mwili wangu

    “Eddy unatatizo gani wewe?”

    Nikatazama nyuma na sikumuona Mwajuma na kuukuta mlango ukiwa umefungwa,

    “Eddy mbo haueleweki?”

    “Wee niache tuu sijajua ni kwanini ulinileta kwenye hii nyumba?”

    Nilizungumza huku nikipiga hatua za kwenda nje na kuwafanya Halda na mwanzake kunifwata kwa nyuma huku wakiniongelesha na wala sikuwaelewa ni nini wanacho kizungumza.Nikakaa kwenye msingi wa bustani ya maua iliyopo nje ya ukuta wa nyumba yangu na Hilda akasimama mbele yangu huku akiwa amejishika kiuno

    “Eddy hembu niambie una tatizo gani?”

    “Tatizo ni hii nyumba hembu tazama nina siku kadhaa nimesha anza kuchakaa kiasi hichi je ni-kikaa wiki hapa si nitakuwa tambara la deki”

    “Jamani Eddy kwani humo ndani kuna tabu gani.....?”

    “Hembu nitolee unafki wako hapa inamaana hujui kinacho endelea humo ndani?”

    “Sawa japo na tambua ila sio wewe kukimbia kimbia utakuja uumie kwa vitu vya kitoto”

    “Wewe unaumwa nini kwanza ninaomba umpigie simu baba mwenye nyumba aje hapa ili mka-taba kama ni vipiti tuuvunje na mimi anipe nusu ya malipo na hiyo pesa nyingine mimi ninasa-mehe”

    “Eddy.....”

    “Hakuna cha Eddy wewe unaona Raha hivi mimi ninavyo teseka Si ndio?”

    “Shem kwani tatizo ni nini?”

    Rafiki wa Hilda akaniuliza na kunifanya nibaki nikimtazama pasipo kumjibu kitu cha aina yoyote hadi akajistukia

    “Muulize huyo rafiki yako”

    “Shosti wala hakuna kitu huyu mwanaume ni uwoga wake tuu”

    Sote tukastuka baada ya geti kupigwa kikumbo hadi likafunguka na hapakuwa na mtu aliyetoka na tukajikuta tukikimbia huku kila mtu akishika njia yake.Baada ya kukimbia kwa muda nikaji-kuta nikiporomosha katika kilima cha bichi ya Raskazone.Nikatafuta sehemu na kukaa ili kiji-upepo kinipige vizuri na nikapata wazo la kuingia ndani ya bichi hiyo,Nikalipa kiingilio na kuta-futa sehemu iliyo tulia na kukaa huku nikijishauri jinsi ya kurudi nyumbani kwangu.Nikajikuta nikiyafwatilia mazungumzo ya wanaume wawili walio kaa pembeni yangu

    “Katika ulimwengu huu hakuna kitu kinacho shindikana mbele ya Jina la Yesu kristo”

    “Kweli mchungaji kwa maana nilipo toka ni mbali sana hadi leo ninatazamika kama mtu kweli Mungu ni mwema”

    “Unajua shetani anamambo mabaya sana katika ulimwngu huu,Huwa hapendi kuona watu wa Mungu wakifanikiwa kiasi kwamba anawafunga kwa mambo ya ajabu ajabu kama wewe jinsi alivyo kupeleka kuzimu”

    “Yaani kipindi kile sikujua ilikuwa vipi kwa maana nilikuwa ni muumini mzuri wa dini.Ila kuna siku nilikutana na dada mmoja katika mtandao wa Facebook....Basi tulikuwa marafiki wa kuchati chati hadi ikafikia hatau tukawa ni wapenzi kabisa...”

    “Hambe ngoja kwanza......Inavyoonekana tatizo lilianzi hapo?”

    “Ninavyo hisi kwa maana yule dada aliniambia kuwa yeye anatokea Zanzibar na tukapanga siku tukutane Dar kipindi nilipokuwa ninafanya kazi kwenye bandari ya Dar es Salaam.......Haikuwa ngumu kwa sisi kukutana na kutokana nilikuwa ninajuana na watuw engi ambao ni manahoza wa boti zinazo kwenda Zanzibar niliwatumia wao kufanya upelelezi juu ya binti huyo na wakanihakikishia kwamba yupo na anajiheshimu”

    “Ehee ikawaje”

    Nikakohoa kidogo na kuwafanya mchungaji na mtu wake kunitazama kisha wakaendelea na mazungumzo yao

    “Basi nilimtumia tiketi ya boti nakumbuka ilikuwa ni mwezi wa sita tarehe kama sita mwaka el-fu mbili na tisa(2009).Akaja hadi Dar baada ya ya kuipokea tiketi ambayo nilimkabihi rafiki yangu ambeye alijuwa ni mfanyakazi kweye boti za Baresa.Mchungaji nisiku danganye yule mtoto alikuwa ni mzuri na asili yake ni mwarabu....Ila kitu kilicho kuwa kikinishangaza mimi kila ilipokuwa ikifika saa sita usiku alikuwa anataka kwenda baharini kwa madai ya kwenda kuoga na kutokana tulikuwa tupo karibu na bahari nikawa ninamruhusu kama kawaida.Ile tabia ikaanza kunichosha ikanibidi siku nimfwatile hadi baharini na kukuta akabadilika na kuwa kama hawa NGUVA......Aisee ile siku Mchungaji niliogopa kupita maelezo na mbaya zaidi alikuwa na wezake wawili ambao nao walikuwa kwenye maumbo kama lake wakichezea maji.

    Kilicho niingiza kwenye matatizo ni simu yangu kuita na enzi zile ile misimu yenye makelele ya kichina ndio yalikuwa yameingi.Nikastukia kibao kimoja ambacho zikujua nimepigwa na nani na nikajikuta nimeangukia kwenya maji na wakanichukua hadi katikati ya kina kirefu na kutokana na uzoefu wangu wa bahari nilipajua kuwa pale ni Nungwi”

    Nikajikuta nikishusha punzi kwa nguvu baada ya jamaa kupiga fumba la soda kwani story ya jamaa ilizidi kunisisimua mwili wangu na nikajiweka vizuri kwenye kiti huku nikiendelea kusikiliza stori ya jamaa kwani kwa mbali nilisha anza kusahau yaliyonikuta kwangu

    “Basi baada ya wao kunichukua wakanizamisha kama mara mbili hivi nikanywa mafumba kad-haa ya maji nikajikuta nikiishiwa na nguvu za mwili wangu.......”

    “Wakati wanakuchukua kwenye maji hadi mukafika nungwi mulikuwa munakimbia ua munafanyaje?”

    “Mchungaji nilikuwa wala sielewi tunakimbia au tunakwenda taratibu kwa maana nilijikuta tu tumefika Nungwi na kufumba na kufumbua nikajikuta nipo kwenye mjia ambao sikuuelewa kama ni duniani au kuzimu kwani niliona watu wa ajabu sana kiasi kwamba mara kwa mara nikawa ninapoteza fahamu......Waliniingiza kwenye moja ya shimo ambalo kulikuwa na funza wa moto ambao hutoboa mwili kwa haraka kiasi kwamba nilipata maumivu makali”

    “Pole Joseph....Unajua siku nilikuwa nimelala Mungu akaniletea maono kwamba kuna mwana-damu ambaye ni wewe upo kwenye hali ngumu sana na akanipa maagizo nifanye maombi juu yako na nifunge kwa siku 7 huku nikiomba na kula kipande cha mkate kwa siku na glasi ya ma-ziwa”

    Nikaanza kujifikiria sijui nimshirikishe mchungangaji majanga niliyo nayo ila ikanibidi nikae kimya huku nikiwasikiliza

    “Mchungaji sikuweza kuamini kama nitarudi tena duniani kwa maana walikuwa wakinileta hadi huku duniani kuangalia ndugu zangu wanavyo hangaika katika kunitafuta kiasi kwamba nikawa ninatamani niweze kuwasemesha ila nikawa ninashindwa......Nakumbuka mwaka 2010 wakaanza kunifundisha kazi ya kuua watu kwa kusababisha mambo yanayoweza kusababisha ajali.Hata ile ajali ya Nungwi ya kuzama kwa MV Speace mimi pia nilikuwa ni miongoni mwa vijakazi tuliokuwa tunaichukua miili ya watu waliokuwa wanakaribia kufa na kuwapeleka chini ya bahari kiasi kwamba wale watu tulikuwa tunawatumikisha katika kuwaleta wanadamu wengine amabao huku duniani wanakaa kihasara hasara”

    “Ndio maana watu huwa ninawahubiria kila siku kuwa ndugu tubuni dhambi zenu mwisho wa dunia unakaribia ila bado wameiweka miiyo yao kuwa migumu”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kweli mchungaji unayo yasema.....Kule kuna mateso sana....Na usiombe ukatembea na jini lazi-ma ipo siku atakupeleka kuzimu”

    Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbioa kiasi kwamba nikaanza kupata wasiwasi baada ya kusikia kuna safari ya kwenda kuzimu

    “Na kabla sijapata nafasi ya pekee ya kutoka kule kuna Malkia wao alitumwa kuja Tanga kuian-gamiza kupitia mwanaume mwenye nyota kubwa ambaye herufi yake inaanziwa na ‘E’ ila siku-jua hiyo ‘E’ ni nani?”

    Mwili mzima ukaanza kunitetemeka kiasi kwamba nikaanza kujihisi haja ndogo ikitaka kunitoka kwa woga

    “Huyo Malkia wao anaitwa nani?”

    “Sisi kule tulikuwa tunamuita Mtukufu Malkia ila jina lake nililisikia siku akiitwa na baba yake ambaye anaitwa Hitler na mtoto wake anaitwa sijui Oli.. nini?”

    “OLVIA”

    Nikajikuta nikiropoka na kuwafanya wanitazame kwa mshangao na kumfanya jamaa kutingisha kichwa akiashiria jina nililo litaja ndilo jina halisi la Malkia wao na kunifanya nizidi kuogopa.Mchungaji akanitazama kwa macho makali hadi nikajikuta nikitazama pembeni nikijifanya kama vile sielewi kitu kinacho endelea

    “Kijana”

    Mchungaji aliniita na kujikuta nikigeuka na kumtazama pasipo kuzungumza kitu chochote

    “Unaweza kuja na kujumuika nasi hapa?”

    “Ahhaa....Asanteni”

    “Njoo tuu kijana wangu kwani kuna ujumbe wako nimeupata hapa nataka niseme nawe japo kwa ufupi tuu”

    “Huo ujumbe umetoka kwa nani?”

    “Wewe sogea Mungu atakonyooshea mkono wake na wala usiogope”

    Nikanyanyuka na kukaa kweye kiti cha pembeni na mchungaji akaniomba nimpe mkono ka ishara ya kusalimiana.Nikaanza kujihisi mkono ukinitetemeka kiasi kwamba nikajikuta niki-chomo kwa nguvu kuto kwenye viganja vya mchungaji.

    “Kijana usiogope kijana....Mimi ninaona unamatatizo katika maisha yako ila jina la bwana wetu Yesu kristo litafanya maajabu juu ya maisha yako........”

    “Umejuaje kuwa mimi ninamatatizo?”

    “Nimekuona tuu jinsi unavyo teseka na majanga ya dunii hii na nafsi yako hivi sasa ipo kuzimu na wanaifanyia mpango wa kukufanya wewe kuwa kiongozi wa ambaye utaweza kuiteka hii Tanga na kuwa ndio Makao makuu ya kuzimu kwa Tanzania”

    Nikabaki nikimtazama mchungaji huku mdomo ukiwa wazi na mwili mzima ukazidi kunitete-meka

    “Mchungaji twende kwangu kuna tatizo?”

    “Kwako ni mbali na hapa?”

    “Hapna ni hapo juu tuu”

    “Sawa...Joseph kama huto jali ywende tukaifanye kazi ya bwana”

    Tukanyanyuka na kutoka nje ya bichi na kwauzuri wanagari lao walilo jia katika sehemu hiyo,Tukaingia na nikaanza kuwaelekeza hadi tukafika nyumbani kwangu na sikuwakuta Hilda na mwenzake ila geti tumekuta limejifunga vizuri.Nikafunga geti na kuwakaribisha na kabla mchungaji hajaingia ndani nikaanza kumuona akizungumza zungumza mwenyewe maneno nisiyo yaelewa ila watu husema mtu akizungumza kwa mtindo huo ananena na roho.Mchungaji akafungua mlango na huku akiendelea kuomba na Joseph naye akawa na kazi ya kuomba ila mimi nikawa na kazi ya kuwafwata kwa nyuma hadi sote tukaingia ndani na kwa bahati mbaya tukamkuta Mwajuma akiwa amelala chini huku akitoka damu za pua

    Mchungaji akazidisha sauti ya kuomba na kila anvyozidi kuomba ndivyo jinsi hali ya hewa ikazidi kubadilika ndani ya nyumba hadi ikafikia hatua nikaanza kuogopa.Upepo mkali unaokwenda mithili ya kimbuka kikali ukaanza kuzunguka sebleni na baadhi ya vitu vikaanza kuanguka chini ikiwemo vyomvo vilivyopo ndani ya kabati.Nikastukia nikamuona Joseph akirushwa na kupiga ukutani na akatulia kimya na gafla nikamshugudia mchungaji akichmwa na kisu kilichoruka kutoka kabatini na kikatua kifuan kwake



    Mchungaji akakishika kishu kilicho mchoma na kukichomoa na kuzidi kuomba huku akiiongeza sauti ya juu huku akiliitaja jina la Yesu kristo.Miale ya radi na kurumo ikanza kupiga maeneo ya dari na kusababisa nilale chini kwa woga ila mchungaji hakulala chini na akazidi kuomba na taratibu na mimi nikajikuta nikiisema

    “SHINDWA KATIKA JINA LA YESU KRISTO”

    Nikaendelea kurudia rudia maneno hao mara gafla nikajikuta nikinyamaza baada ya Olvia Hit-ler kusimama kwenye moja ya kona huku akiwa amevalia nguo nyekundu na sura yake ikiwa imejawa na hasira kali sana kiasi cha macho yake kutoa mwanga mkali

    “Wewe pepo unayetaka kuchukua watu wa bwana leo hii ndio mwisho wako nakufunika na kukurudisha kuzimu katika jina la YESU KRISTO wa nadhareti TOOKKKKAAAAAAAAAAAAAAA”

    Olvia Hitler akayumba kidogo akionekana kama ametetemeshwa kwa maneno hayo ila akanita-zama kwa macho makali na kuninyooshea mkono na kujikuta nikikabwa shingo na kitu nisicho kiona na taratibu nikaanza kunyanyuliwa kwenda juu.Mchungaji akaunyoosha mkono wake mmoja kwangu huku akiomba kwa nguvu na kujikuta nikianguka chini na gafla Olvia akapotea na hali ya ndani ikaanza kutulia na baada ya muda ikarudi katika hali ya kawaida ila vitu vingi vimechanguka na kukaa katika sehemu tofauti na nilivyokuwa nimevipanga

    Mchungaji akasogea taratibu na kukaa kwenye sofa huku jasho jingi likimwagika na nikaonda shati lake likilowana na damu

    “Mchungaji umeumia hapo kwenye kifua”

    “Hakuna tabu ni jeraa dogo ila tafuta maji na chumvi unilete hapa”

    Nikatoka kiwoga woga na kwenda jikoni na kuanza kuitafuta chumvi na baada ya muda nikaipata kisha nikaweka maji kwenye kikombe na kurudi sembeni.Mchungaji akavichanganya kwa pamoja maji na chumvi kiasi akaviombea na kujipaka kwenye jeraha lake na kuifanya damu kuacha kutoka.Akasimama na kumshika Joseph kichwani na kuanza kumuombea taratibu hadi Joseph akapia chafya na kunyanyuka.Akamfwata Mwajuma na kumtazama kwa muda kisha akamnyooshea mkono na kuanza kumuombea na gafla Mwajuma akaanza kujikunja kunja mithili ya nyoka anaye tambaa.Mchunagaji akazidi kuomba na baada ya muda Mwajuma akaanza kukoroma huku mapovu yakianza kumwagika mdomoni hadi ikafikia hatua akaanza kutoa vitu vyeusi mdomoni zikiwemo irizi mbili kubwa.Nikabaki nikashangaa kwani kwenye maisha yangu sijawahi kuona kitu kama hicho kikitoka mdomoni mwa wa mtu.Mwajuma akatulia na baada ya muda akakaa kitako huku akihema akionekana amechoka sana

    “Unajisikiaje binti?”

    “Vizuri”

    “Nyanyuka na ukae kwenye kiti”

    Mwajuma akanyanyuka na kukaa kwenye kochi huku akiwa anashangaa shangaa

    “Bnti unaitwa nani?”

    “Anaitwa Mwajuma”

    “Ahaa Mwajuma hali yako inaendeleaje?”

    “Salama tu nipo wapi?”

    “Mimi ni Eddy umenikumbuka?”

    “Ndio nakukumbuka mbona nipo hivi baibui langu lipo wapi?”

    Nikatizama tizama chini na kuliona baibui la Mwajuma nikaliokota na kumpa akalivaa na kisha mchungaji akamuoba aende bafuni akaoge.Nikamuonyesha Mwajuma bafu la kuoga na nikamuonyesha na chumba changu kama atatoka bafuni aweze kuingia kupaka japo mafuna na nikampa na taulo langu kisha nikarudi sebleni na kukaa kwenye sofa moja wapo lililopo sebleni kwangu

    “Kijana kwanza napenda kulijua jina loko?”

    “Mimi ninaitwa Eddy Praygod”

    “Unajina zuri..”

    “Asante mchungaji”

    “Amini Mungu yupo na shetani huwa hana nafasi katikati ya watu wa Mungu,Pale mwanzoni Shetani aliweza kuyateka maisha yako na kuyachukua na kuyafanya ni maisha ya ajabu....Ila kwa sasa ninakuomba umpokee Yesu kuwa bwana na mwokozi wa maisha yako”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Mchungaji mimi nipo tayari yaani nimechoka na haya matatizo humu ndani?”

    “Hii nyumba niya kwako?”

    “Hapna nimepanga tuu”

    “Ahaa inabidi sisi tuondoke na kesho nitakuja na wana maombi kuifanyia maombi na kuvunja ngome ya shetani iliyokuwa imejegwa humu ndani kwako”

    “Ngoja kwanza mchungaji ina maada bado haya madudu yamo humu ndani?”

    “Hapna ila kuna utawala wa Malaika wa bwana ila kunahitajika maombi ya nguvu kiasi kwamba tuweze kuteketeza kila lililo zao la shetani humu ndani”

    “Mmmmm.....”

    “Mbona unawasi wasi sana?”

    “Yaani leo siwezi kulala humu ndani naogopa sana mchungaji”

    “Ndugu ninakuomba ulale ndani ya nyumba yako na hakuna chochote kibaya kitakacho tokea na roho wa bwana atakufunika”

    “Mchungaji ninahisi unipendi mimi ninaona twende nikalele kwako hadi kesho tutakapo rudi na hao wana maombi wako ndio na mimi nirudi humu nani”

    “Basi kwa hilo hakuna shida”

    Nikaingia ndani kwangu na kuanza kuvua nguo na nikabaki kama nilivyo zaliwa na kuanzakutafuta nguo ya kuvaa kabatini na gafla nikastukia mlango ukifunguliwa na Mwajuma akaingia hukua akiwa amejifunga taulo kifuni na baada ya kuniona tukabaki tukiwa tumetazamana na nikalishuhudia taulo alilo jifunga Mwajuma lilianguka chini na akabaki kama alivyo zaliwa na kuanza kupiga hatua za kunifwata sehemu niliyo simama.

    “Mwajuma nini unafanya?”

    “Unajua ni nini nataka”

    “Ila mwajuma hao watumishi wa Mungu wapo hapo sebleni huoni kama watastukia”

    “Ila wao pia si wana wake zao na mimi nataka kuwa mke wako”

    “Mwajuma sio kirahisi kama unavyo dhania”

    Mwajuma akanishika kiuno na kunivutia kwake kisha akaupeleka mkono mmoja kwenye kiko yangu na kuanza kuichezea chezea kiasi kwamba nikajikuta nikianza kulainika na kujikuta na kianza kumshika makalio yake makubwa na kuanza kuyatomasa kwa vidole vyangu vilaini kiasi kwamba Mwajuma akazidisha kasi ya kuichua koki yangu.

    Mwajuma akanigandamiza kwenye kabati nakuendelea kufanya anacho kufanya kisha akaanza kushuka taratibu na kuanza kuinyonya kiko yangu huku mikono yangu ikiwa imemshika nywele zake ndefu kiasi

    “Eeeh mola wee sijui ni lini nitaacha hii dhambi”

    Nilijisemea kimoyo moyo na kumnyanyua Mwajuma na kumuweka kitandani na kuanza kuichezea ikulu yake kwa muda kisha nikakumbuka malango sijaufunga na funguo umerudishiwa tu.Nikataka kunyanyuka ila Mwajuma akanizuia na nikajikuta nikirudi kitandani na kuendelea na shuhuli ya kupeana mambo huku mikono yangu nikimziba mdomo Mwajuma asipige kelele hadi mchungaji na Joseph wasisikie.Kusema ukweli Mwajuma anajua kukitawala kitanda kwani kila aina ya mikao aliweza kuniwekea na kujikuta nikimaliza mechi haraka

    “Eddy tuendelee”

    “Mmmmm tufanye siku nyingine”

    “Kwa nini wakati leo upo kwako?”

    “Wewe elewa ilo sawa”

    “Sawa ila bado ninahamu na wewe”

    “Mmmm wewe vaa nguo zako uende sebleni ukanisubirie”

    “Basi ngoja nikaoge tena”

    “Ahaaa wewe vaa utakwenda kuoga kwenu”

    Tulizungumza kwa sauti ya chini ambayo si rahisi kwa mtu wanje kuweza kusikia,Mwajuma akavaa nguo zake na kujipara vizuri na kutoka ndani ya chumba changu,Nikajifunga taulo na kuingia bafuni nikaoga haraka na kurudi chumbani kwangu nakuvaa nguo zangu na kurudi sebleni na kumkuta mchungaji akimuhoji hoji maswali Mwajuma

    “Mchungaji nipo tayari sasa”

    “Sawa tuondokeni”

    Tukatoka nje ya nyumba na nikaifunga nyumba yangu na sote tukaingia kwenye gari na safari hii Joseph akawa ndio dereva na tukaelekea hadi nyumbani kwa kina Mwajuma na kuwakuta wazazi wake na kama alivyo nieleza mwazoni kwamba wazazi wake ni wazee sana ndivyo kweli tulivyo wakuta.Nikatoa pesa kiasi na kumkabidhi na tukaahidi kurudi siku inayofwata.Tukafika kweye jumba la mchungaji lililopo maeneo ya Sahare na nikakuta baadhi ya watu ambao nahisi ni waumini wa kanisa la mchungaji huyo ambaye hadi sasa hivi sijajua anasalisha kanisa gani

    Watumishi wake tulio wakuta wakaanza kumsalimia huku wakipeana mikono kisha mimi na Joseph tukaingia ndani na kumkuta dada wa makamo na kwaharaka haraka miaka yake inaweza kuwa 31-35 akiwa amealia vitenge vya gharama na cheni za dhahabu huku mkononi mwake akiwa ameshika biblia

    “Mama mchungaji bwana Yesu asifiwe?”

    “Amein za huko mulipo toka”

    “Ni kwema ila sio sana”

    “Kaka bwana Yesu asifiwe”

    Mama mchungaji alizungumza huku akinishika mkono na mimi nikaitikia kama yeye alivyo muitikia Joseph kisha tukakaa kweye sofa za dhamani sana na ukubwa wa jumba hili ninaufananisha na majumba ya matajiri wa Nigeria

    “Haya Jose kuna yapi yaliyo wakuta huko”

    “Mama mchungaji ya huko ni makubwa kwa maana tumetoka kuvunja ngome ya shetani yaani mtu unaweza ukasema ni filamu ya kuigiza ila leo ndio nimezidi kuamini kama shetani yupo duniani na anafanya kazi”

    “Ohhh kila siku huwa vita yetu sisi si ya wili wa damu na nyama ila vita vyetu ni vya roho na shetani siku zote huwa anazunguka zunguka ili atafute mtu ammeze”

    “Kweli mama mchungaji ndugu yetu Eddy hapa tulikutana naye maeneo ya bichi kule Raskazoni basi akatuomba twende naye kwake na kufika kulikuwa na nguvu fulani ya shetani ambayo tulianza kusali na baba mchungaji ila mimi nilijistukia nikirushwa na kutupwa chini na sikujua kilicho endelea ila nimekuja kuzinduka nikajikuta sehemu nzima imechanguka changuka”

    “Ohhh poleni sana ila Jose siku zote huwa ninakuambia uwe unasali hadi mwisho wa ibada ila wewe kabla hatujamaliza muda wa kusali unachomoka na kwenda kulala leo naona umepata changamoto”

    “Kweli ni changamoto....Ndugu yangu Eddy huyu ndio mke wa mchungaji anaitwa mama Yudia”

    “Nashukuru kukufahamu mama mchungaji”

    “Hata mimi nashukuru kukufahamu karibu,Jisikie upo nyumbani na sehemu takatifu yenye ulinzi wa bwana”

    “Nashukuru”

    “Mama mama....Mbona mwalimu mwenyewe haji?”

    Tulisikia sauti ya msichana ikitokea gorofani na sote tukajikuta tukitazama juu na nikamuona binti mmoja mrefu na mwenye umbo la kujazia kiasi kwamba anasifa na vigezo vyote vya kuitwa msichana mrembo akishuka kwenye ngazi huku akiwa amevalia bukta fupi na tisheti kuwa

    “Nimepigia simu yake amesema atakuja”

    “Saa ngapi mama wakati hadi sasa hivi inaenda saa moja hii hajafika kama hataki na yeye aseme”

    Nikahisi msichana huyu ndio atakuwa ni Yudia kwani anafanana sana na mama yake,Akakaa kwenye kochi alilo kaa mama yeka huku akizichomeka earphone zake masikioni akisikiliza mziki kupitia simu yake kubwa screen touch

    “Hembu usinilalie hapa nilipo nimechoka kama nini?”

    “Jamani mama nakulalia kidogo hembu weka paja vizuri”

    “Yudia nitakuchapa hembu niondolee uvivu wako hapa”

    “Mama akikulalia Junio wala haumchapi ila nikikulalia mimi unaongea”

    “Sasa wewe uanjifananisha na Junio mwenzako yeye ni dogo wewe jidada lizima la form four unanilalia lalia”

    Yudia akanyanuyka na kukaa kwenye kochi hukua akiendelea kuminya minya simu yake

    “Yudia mbona hujawasalimia kaka zako”

    “Shikamoo kaka Jose huyo mwengine mimi wala simjui”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Kisa humjui ndio humsalimii?”

    “Sasa mama nitamsalimiaje mtu ambeye mimi simjui”

    Yudia alizungumza huku akinitazama kwa macho ya dharau ikanibidi nikae kimya kwa maana watoto wengi wanaoishi kwenye mazingira mazuri kama haya ya mchungaji huwa mara nyingi hudekezwa na wazazi wao kwa madai wanaishi maisha ya kizungu

    “Junio mwenzako yupo wapi?”

    “Amelala ndani kwake?”

    “Anaumwa?”

    “Wewe si unakijua toto lako la mwisho kila likitoka shule inakwenda kulala”

    “Samahani jamani kwa kuyakatisha mazungumzo yetu”

    ‘Hakuna shida mama mchungaji”

    “Eheee kaka Eddy ilikuwaje?”

    Nikajikoholesha kidogo na kuanza kuzungumza kwa sauti ya upole

    “Kunanavitu vilikuwa vina nisumbua nyumbani kwangu basi leo mchungaji alipo viombea nahisi vitakuwa vimekwisha”

    “Mama mama”

    “Nini wewe?”

    “Kuna watu wanapenda sana kuiga majina ya watu?”

    “Hembu niachie upuuzi wako?”

    “Kweli mama kuna watu wanapenda sana kuchukua chukua majina ya watu”

    “Nani aliye chukua majina ya watu?”

    “Si huyo kaka hapo eti na yeye anajiita EDDY”

    “Kwani mtu akiitwa Eddy kuna dhambi?”

    “Sio dhambi ila ameliiga jina la kaka mmoja hivi Facebook anaandika story naye anaitwa Ed-dy....Yaani nikoboko”

    “Hembu nitolee upuuzi wako na hayo mafacebook yako ndio maana unafeli darasani”

    “Sasa mama kufeli darasani ndio kumechangiwa na facebook?”

    “Ndio kila saa ni simu na wewe sijui ni muda gani utapata muda wa kushika daftari na kusoma”

    “Nitasoma”

    “Samahani mdogo wangu Yudia kwani ni masomo gani yanakusumbua darasani?”

    “Biology,Math na Physics”

    “Ugumu wa hayo masomo upo wapi?”

    “Mmmm waalimu wetu wakifundisha wala siwaelewi wanakazi ya kutufokea fokea na kusema tutafeli”

    “Basi kama huto jali nitakufundisha”

    “Mmmm mtu mwenyewe mbona unaonekana hujui chochote sijui haka kama umefika form four”

    “Wewe Yudia acha dharau.....Kwanza nyanyuka uende chumbani kwako sitaki fujo au umfwate huyo baba yako huko nje”

    “Sawa najua mama siku hizi hunipendi”

    Yudia akasimama kwa hasira na kuondoka na kupandisha nagazi za kuelekea gorofani huku akizungumza maneno ya chini chini

    Tukaendelea na mazungumzo huku na nikaanza kumuadisia Mama mchungaji kila kitu kilicho tokea na akabaki akinipa pole kwa yale yaliyonikuta.Mchungajia ajaingia huku akionekana ku-choka na moja kwa moja akaanza kupandisha ngazi na mke wake akawa anamfwata kwa nyuma nikabaki na Joseph

    “Hivi mchungaji ana watoto wangapi?”

    “Wawili,wa kwanza ni huyu wa kike na wapili ndio huyo mdogo wa kiume amelala”

    “Ahaa anafamilia ndogo na nzuri?”

    “Ndio hawa ndio watu wanaojua kupanga maisha...Sema maisha yake mengi mchungaji ameishi Marekani”

    Tukaendelea kuzungumza zungumza na Joseph hadi muda wa chakula ukawadia na tukaalikwa kwenye meza ya chakula na tukajumuika na familia nzima ya mchungaji pamoja na wafanyakazi wake wa ndani wapatao wanne

    “Jamani huyu ni kaka yenu anaitwa Eddy na atakuwa nasi leo hadi kesho kwahiyo ninaomba mumuheshimu kama munavyo niheshimu mimi.Haswa wewe Yudia nimepata malalamiko yako kutoka kwa mama yako kuwa umeonyesha tabia chafu mbele ya Eddy sasa sitaki hilo swala ljirudie tena”

    “Lakini baba mimi mtu simjui ila mama ananilazimisha niweze kumsalimia”

    “Sawa ila sitaki hiyo tabia mbaya ijitokeze tena la sivyo nitakurudisha shule za bodi au nikupe-leke kijijini kwa bibi yako ukaishi huku”

    Yudia akakaa kimya na kunitazama kwa jicho kali la hasira kisha akaendelea kula huku sura yake akiwa ametazama chini

    “Kaka Eddy unafanya kazi gani?”

    Junio aliniuliza swali na kunifanya nitabasamu kisha nikamjibu kwa sauti ya upole

    “Mimi ni mwalimu wa sekondari”

    “Waoo unafundisha masomo gani?”

    “Physics.Mathe,Biology na Chemestry”

    “Alafu leo nimepewa homework ya Mathematics alafu sijaifanya hadi sasa hivi sielewi elewi na kesho madaftari yanahitajika”

    “Upo kidato cha ngapi?’

    “Form one”

    “Usijali nitakuelekeza”

    Tukaendelea kula na baada ya kumaliza watu waote tukakusanyika sebelini na mama mchungaji akasoma neno kutoka kwenye biblia na kuanza kututufundisha kama anahubiri kanisani kisha baaya ya kumaliza tukaimba nyimbo kadhaa na mchungaji akaongoza sala ya kulalia na baada ya kumaliza akatuaga na kwenda chumbani kwake kulala.Junio akaniomba nimsubiri aniletee vitabu na madaftari yake nimeulekeze

    ”Jose utamuonyesha Eddy chumba cha kulala sasa atachagua alale gporofani au vyumba vya chini”

    “Sawa mama”

    Mama mchungajia akaondoka na kutuacha tukiendelea kutazama Tv na chaneli hito iaonyesha-mahubiri ya mchungaji maarufu kutoka Nigeria TB.Joshu

    “Yaani huyu jamaa anakarama ya Mungu kwa maana kile anacho kitabiri ndicho kinacho kuwa”

    “Kweli”

    “Jose hembu badilisha chaneli na chomeka huo waya wa king’amuzi cha DSTV”

    Yudia alizungumza huku akijirusha kwenye kochi akitokea jikoni huku mkononi kwake akiwa amaeshika tunda akilila na kulitafuna kwa fujo kiasi kwamba anakera

    “Kidogo ngoja tumalizie hichi kipande cha mahubiri”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hutaki au?”

    “Ila Yudia huko ndani kwako pia si una DSTV”

    “Leo nimejisikia kuangalia hapa sebleni”

    Joseph hakutaka kufanya ubishi zaidi ya kunyanyuka na kwenda kubadilisha nyaya za king’amuzi na kumuwekea Yudia kitua anacho kitaka.

    “Kaka njoo nikuonyeshe chumba cha kulala”

    Nikaondoka na Joseph na akaanza kunionyesha vyumba vya chini na nikaipenda kimoja amba-cho kipo mwisho wa kordo na kimekaa vizuri.

    “Nitalala humu”

    “Sawa....bafu na choo vyote vipo humu humu ndani?”

    “Sawa wewe unalala wapi?”

    “Mimi chumba changu kipo juu gorofani”

    Nikakichunguza chumba vizuri na kurudi sebleni na kumkuta Junio akinisubiri akiwa na vitabu vyake.Akanionyesha chumba cha kusome na sote tukaingia ndani na nikakuta vitabu vingi viki-wa ndani ya chumba hicho ambacho kinafanana na maktaba.Tukakaa kwenye viti na Junio aka-weka vitubu vyake kwenye meza na nikaanza kumfundisha kitu kimoja baada ya kingine.Tangu niwahi kufundisha sikuwahi kukutana na mwanafunzi muelewa kwa haraka kama Junio kwa maana kila ninacho mfundisha anakielewa haraka na nikimpa maswali hujibu vizuri kama nilivyo mfundiha

    Yudia akaingia huku na yeye akiwa na madaftari yake ila simu yake ameifungulia mziki kiasi cha kunifanya nisitishe zoezi la kumfundisha Junio na sote tukabaki tukimtazama

    “Lakini dada Yudia mbona unamakusudi sana?”

    “Na wewe koma”

    “Sio nikome,wewe si ulikuwa sebeli ukitazama Tv sasa huku umefwata nini?”

    “Kwani siku zote nikiingia humu huwa ninafwata nini?”

    “Tangu lini wewe umekuja kusoa huku muda kama huu”

    “Ndio leo basi na mimi nimekuja kusoma”

    “Haya basi zima simu yako”

    “Ili iweje?”

    “Wewe si unaona jinsi unavyo tupigia makelele”

    “Kusoma bila mziki mimi siwezi”

    “Muangalie yale manywele yake kama vile pepo linalotoka kaburini sijui kwa nini baba wewe hakuombei”

    “Alafu wewe Junio uaniingilia kwenye anga zangu ngoja nikuonyeshe”

    Yudia akasimama kwa hasira huku akimfwata Junio na nikasimama katikati yao na kumshika Yudia asimfwate Junio.Junio akakusanya vitabu na madaftari yake na kuanza kupiga hatua za kwenda nje huku akimzomea Yudia na kumfanya apandishe hasira zaidi na akaanza kutumia nguvu kujitoa mikononi mwangu na kwabati mbaya nikajikuta mikono yangu ikikutana kifuani mwa Yudia na kuyashika maziwa yake madogo kiasi na kumfanya anaze kulegea.

    Ikanibidi nimuachie na akanza kumkimbiza Junio nikabaki nimesimama na kunza kutazama ta-zama vitabu vilivyomo ndani ya chumba hichi,Yudia akaingia huku akisunya na kuja sehemu nilipo simama

    “Alafu wewe ndio chanzo cha kumpa kiburi Junio”

    “Ila wewe ndio mchokozi”

    “Unataka kuuona uchokozi wangu si ndio?”

    “Hapana”

    Nikastukia Yaudia akainisukuma na kuniegemeza kweye ukuta uliochomekwa vitabu na kuanza kunifungua vifungo vya shati langu

    “Wewe mtoto unataka nini?”

    “Tulia la sivyo ninapiga kelele kuwa unataka kunibaka”

    “Wewe piga ila sipo tayari kufanya unachotaka kufanya”

    “Mamaaa”

    Yudia akapiga kelele na kunifanya nimzibe mdomo huku nikiwa ninamshangaa.Akaifungua zipu ya suruali yangu na kabla hajauingiza mkono kwenye suruali yangu tukasikia sauti ya mama yake ikimuita huku akija sehemu ya chumba hichi tulichopo na kunifanya nianze kutetemeka



    Wazo la haraka likanijia kichwani kwangu na nikalitekeleza kwa haraka ambalo nikaanguka chini na kunza kurusha rusha miguu kama mtu aliyepandwa na mapepo huku nikitoa makelele ya kunguruma na mikono yangu mara kwa mara nikiipeleka kwenye zipu yangu na kuifunga na kumfanya Yudia kusimama mlanoni kwa woga akimsubiria mama yake kuingia ndani ya chumba cha kusomea.Mama Mchungaji akaingi na baada ya kuniona nipo kwenye hali niliyo nayo ambayo kwangu ninaigiza ili kuua soo la kufumaniwa na mtoto wa mchumaji.

    “Kalete biblia yangu ipo sebleni ya juu”

    Yudia akatoka ndani ya chumba huku akinisogelea na kuniwekea mkono kichwa ni na akaanza kuniombea kimya kimya wala sikujua kama anaomba,Nikajikuta nikianza kutulia taratibu huku macho yangu yakiwa yametua kifuani mwa mama mchungaji kwani ukubwa wa maziwa yake yenye rangi nzuri ya kuvutia yakanifanya mawazo yangu kuanza kufikiria vitu vya ajabua ajabu.Yudia akafungua mlango na kuja hadi sehemu tuliyopo

    “Hiyo biblia ipo wapi?”

    “Sijaiona”

    “Nimeiweka kwenye meza ya computer fanta haraka hali ya mwenzanu inakuwa mbaya”

    “Sasa mama si umuamshe baba?”

    “Baba yako yupo kwenye maombi binafsi hembu fanya haraka kailete biblia hembu fanya haraka”

    Yudia akaondoka na kumuacha mama yake akiendelea kukemea mapepo ambayo sikuwa nayo japo nimekubwa na vituko visvyo kuwa na kichwa wala miguu ila ninajielewa mimi mwenyewe,Nikaona nisimpotezee m mama wa watu muda nikasimama na kukaa kitako na kujifanya mapepo yamenitoka

    “Unajisikiaje Eddy?”

    “Salama tuu”

    “Ohhhh thak’s Loard”(Ohhhh asante bwana)

    Mama mchungaji alizungumza huku akijifunga tenge lake vizuri na mimi nikanyanyuka na kukaa kwenye kiti

    “Tukuletee kitu cha kula?”

    “Haoana ninajisikia vizuri tuu”

    “Mama nimeiona”

    Yudia alizungumza huku akiingia ndani ya chumba tulichopo na akajikuta akiwa ameishika biblia huku akitushangaa kwa maana alihisi atanikuta nikiwa ninarusha rusha miguu kama mara ya kwanza

    “Ameshapona?”

    “Ndio amesha pona lete hiyo biblia nimpe mistari ya kusoma ili akajisome chumbani kweke”

    Yudia akampa mama yake biblia na akaanza kunisomea mistaria ambayo nitwakenda kusoma chumbani kwangu.Nikaikariri na nikaagana nao na kuondoka ndani ya chumba na moja kwa moja nikaingia katika chumba ambacho Joseph alinionyesha.Nikapanda kitandani huku nikijichekea kimoyo moyo kwa kitendo nilicho kifanyaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Hii ya leo kali kumbe na mimi ninaweza kuigiza inanibidi niingie bongo movie”

    Nilikisemea kimoyo moyo huku nikilirudia tendo nililokuwa nimelifanya na kujikuta nikicheka kwa sauti ya chini.Nikasimama na kuvua nguo zangu na kuingia bafuni na kufungulia maji ya bomba la mvua na kuanza kuoga huku nikipiga mluzi usio eleweka ni wa nyimbo gani.Nikastuka baada ya kuusikia mlango wa kuingilia chumbani kwangu ukifumguliwa kutonana na mapovu niliyokuwa nayo usoni nikanawa uso wangu haraka haraka kwa kutumia maji masafi na kujifunga taulo na kuchungulia na kuukuta mlango ukiwa umefungwa kama nilivyo ufunga

    “Mmm labda sijausikia vizuri itakuwa ni hii miluzi yangu ya kijinga”

    Niliijifariji na kutudi tena bafuni na safari hii nikaoga haraka haraka na kutoka na kupanda kitandani na nikakumbuka mistari aliyo ambiwa na mama mchungaji na uzuri zaidi biblia ipo sehemu ya wazi ambayo nikaichukua na kuifungua na kujikuta nikistuka baada ya kuto kuikuta na anadihi hata moja.Nikairudisha mezani huku mapigo ya moyo yakianza kuniienda mbio huku nikianza kupata na wasiwasi

    “Isije kuwa Olvia amekuja huku kwa mchungaji?”

    Nilijiuliza maswali ambayo hayana majibu ya uhakika,nikachukua shuka nikajifunika gubigubi kuanzia miguuni hadi kichwani kwa lengo la kutokuona kitu cha aina yoyote kitakacho endelea ndani ya chumba nilichopo.Usingizi ulianza kunichukua taratibu na gafla chumba nilicho lala kikaanza kutwaliwa na makelele ya watu wakilia huku wengine wakicheka,nikanyanyuka huku nikiwa nimeyaziba masikio yangu nisiendelee kuyasikia makelel yanayoendelea.Nikaanza kupiga hatua za kwenda mlangoni ila nikastukia nikamuona mdogo wangu ambeye alifariki tukiwa wadogo akisimama mlangoni huku macho yeke yakiwa yanatokwa na damu huku mikono yeke akiwa ameinyooshea kwangu

    “Kaka Eddy njoo njooo huku nilipo”

    Gafla kwenye kona ya kushoto akatokea Mama yangu huku akiwa ameshika panga mkononi mwake akionekana akiwa ametokea shamba akaanza kunitazama kwa macho ya huruma huku machozi yakimwagika taratibu huku kichwa cheke akikitingisha kwa ishara ya kunisikitikia

    “Eddy mwanangu nakuomba uondoke ndani ya hii nyumba si pazuri tafadhali mwanangu tafadhali mwanangu”

    Sauti nzito ya baba nikaisikia ikitokea nyuma yangu na kujikuta nikigeuka kwa haraka na kumkuta baba mwili wake ukiwa ni mweusi kupita maelezo huku macho yake yakiwa yametoka kwa nje huku yakiwa yamejaa uweupe mkubwa kiasi kwamba nikazidi kuogopa

    “Eddy ondoka ndani ya hii nyumba tafadhali mwangu ONDOKAAA.....”

    Makelele yakazidi kunichanganya na taratibu wakaanza kunisogelea huku wakiniweka katikati na kutaka kunikumbatia na gafla nikajikuta nikiwasukuma na kustuka nikiwa nimekaa kitandani huku jasho jingi likiwa linanimwaika na kumkuta Yudia akiwa anamalizia kuvua nuo zake na kubaki kama alivyo zaliwa na sikuja hata ndani kwangu ameingia muda gani.Akapanda kitandani kwangu na kunifunua shuka nililo jifunga

    “WEE....”

    “Shiiii”

    Yudia akanilaza kitandani na kunikalia kiunoni huku akinitazama kwa macho malegevu huku na mikono yangu akichanua na nikawa kama ninasulubiwa

    “Eddy emenifanya nishindwe kulala kwa ajilia yako”

    “Ila wewe kumbuka kuwa wewe ni mwanafunzi”

    “Kwani mwanafunzi ndio hapewi raha.....Nataka unipe japo kidogo kabla ya baba na mama hawajafanya yao”

    “Hawajafanya yao yapi?”

    “Tupotezee hilo”

    Sikuwa na ujanja kwa jinsi Yudia alivyo niweka nikajikuta nikitulia na kumuacha Yudia kufanya yake taribu akaanza kuichua koki yangu hadi ikawa tayari kwa mapambano nikashangaa kuona koki yangu ikizama yote kwa Yudia ambaye kwa muonekano ni msichana mdogo kwa umri japo umbo lake ni kubwa kiasi kwama linamvuto wakumshawishi mwanaume wa aina yoyote kumtamani.Yudia akaendelea kujipa raha ila kwa upande wangu sikuwa na amani kabisa na akilini mwangu nikaanza kufikiria maneno niliyotokwa kuambiwa muda mcahche uliopita katika ndoto na kwajinsi tunavyo fanya hili tukio nikawa ninahisi kama mchungaji anatushuhudia uchafu wetu.Hadi tunamaliza kupeana raha Yudia akaonekana kuridhika na akajizala kitandani huku akihema na jasho likimwagika

    “Eddy nikuambie kitu?”

    “Niambie tu”

    “Unajua kama baba na mama sio wachungaji kama watu wanavyo wadhania....Ila hii ni siri ninakuomba usimwambie mtu yoyote”

    Nikajikuta mapigo ya moyo yakianza kuniende mbio kiasi kwamba nikajikuta nikinyanyuka kitandani na kukaa huku nikimtazama Yudia kwa macho makali kiasi huku nikiwa siamini manen anayo niambia

    “Ikifika saa nane na nusu usiku nitakuonyesa ibada wanazo zifanya baba na mama na baadhi a watu kwenye kanisa lao”

    “Unajua hadi sasa hivi sijakuelewa vizuri unamaanisha nini?”

    “Ngoja ukajishuhudie na macho yako ndio utaelewa ninamaanisha nini kwani sasa hivi ni saa nane kasoro utaona tu kila kitu”

    Tukakaa hadi mida ya saa nane usiku Yudia akaninong’oneza na kuniambia huu ndio wakati maalamu wa wazazi wake kwenda kwenye sala zao ambazo sikujua ni sala za aina gani wanazo zifanya wao.Tukatoka ndani ya chumba huku tukinyata na Yudia akiwa amevaa gauni lake la kulalia na tukafika sebleni na taa zote tukakuta zimezimwa na Yudia akaniomba tuingie ndani ya chumba cha kusomea nikataka kumuuliza swali ila nikasita na kujikuta nikiingia ndani ya chumba hicho na Yudia akasimama kwenye moja ya ukuta wenye vitabu na kuusukuma na ikafunguka njia ya mlango mwembamba amabao unaruhusu mtu kuingia.

    “Twende”

    Yudia akaniambia na sote tukaingia ndani ya ya chuma hicho ambacho kinagiza totoro ila kwa mbali kuna taa za vibatari zinazo waka kwa kwa mwana makali na Yudia akaniomba nisipige kelele ya aina yoyote kwani watu wapo kwenye ibada na ikitokea nitafanya kitu kama hicho utakuwa ndio mwisho wa maisha yetu.Katika chumba tulicho ingia kuna mabenchi kama ya kanisani ambayo kwa mbele yake kuna madhabahu ambayo wamesimama watu wachache walio valia mavazi meusi na mekundu ambayo yamewafunika vichwa vyao huku moshi mchache ukiwa umetawala kwenye madhabahu hiyo.Tukajifichwa kwenye moja ya benchi na kuendelea kuwashuhudia watu wapatao theladhini wakiimba nyimbo amabazo sikuzielewa ni nyimbo za aina gani kwani hata tune yake si kama nilizo wahi kuzisikia

    “Pale baba na mama yako ndio wapi hao?”

    “Baba ni yule aliyeshika lile jitabu kubwa na mama yule akiyeshika msalaba wenye nyoka mbele”

    Nikaendelea kutazama kwa umakini na kuanza kujiuliza kama dini yenyewe wanayo ifanya huyu mchungaji na baadhi ya waumini wake ipo hivi je nguvu za kuwaombea watu na wakatokwa na mapepo wameziotoa wapi

    “Wanatumia lunga gani kuzungumza pale?”

    “Kile ni kirusi kilicho changanyikana na kireno”

    “Wewe unakifahamu?”

    “Ndio naelewa wanacho kizungumza....Kaka pale baba anasema kwamba hali ya waumini inazidi kuongezeka kanisani na anatoa pongezi kwa kanzi nzuri waliyo ifanya katika kuongeza wafuasi wa kanisa lao ambalo ni jipya kwa hapa Tanga”

    Tukaendelea kutazama mambo wanayo yafanya na baada ya muda nikamuona mchunaji akinyoosha mkono wake kwenye kioo kikubwa na gafla ikatokea picha yangu kipindi nikiwa nipo sebleni kwa mchungaji ninakula na nikaanza kujikuta nikitetemeka kiasi kwamba nikataka kunyanyuka na kuondoka ila Yudia akanizuia nisiondoke

    “Wanasema kuwa wewe ni miongoni mwa watu wenye nyota zenye nguvu duniani na wanahitaji waichukue ili waweze kuongeza kasi kubwa ya ukuaji wa makanisa yao”

    Maneno ya Yudia yakazidi kunichanganya kiasi kwamba nikatamani ardhi ipasuke na niingie na inimeze

    “Na wanasema adhimio hilo watalifanya kesho saa sita kamili mchana watakapo kuja nyumbani kwako kukuombea.....Na wanataka damu yako ndio itakuwa ufunguo mkubwa wa nguvu zao ambazo wanazo hitaji kuzipata kutoka kwako”

    Galfa hali ya hewa ikaanza kubadilika mbela ya madhabahu na upepo mkali ukatawala na radi vikaanza kutawalia kila pande ya madhabahu ila watu walio kuwepo wakabaki wakiwa wamesimama huku mikono yao wameinyoosha mbele kana kwamba wanapokea kitu kutoka juu.Mwanga mkali ukatoka kwenye sehemu ya madhabahu yao na gafla wakatokea watu wawili walio valia nguo nyeupa na mmo akiwa ni mwanaume na mwingine akiwa ni Olvia Hitler na kunifanaya mwili mzima kunyong’onyea na kuishiwa nguvu kabisaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/



    Olvia Hitler akasimama katikati ya mchungaji na muumini mwengine na akawawekea mikono kichwani mwao na kuanza kuzungumza maneno ambayo sikuwa ninayeelewa na kusababisha hali ya hewa kuzidi kutisha ndani ya kanisa lao la siri ambalo kusema kweli linatisha kupita maelezo.Upepo mkali mithili ya kimbunga ukaanza kuzunguka kwa kasi ndani ya kanisa huku kikiwa kama kinachungunza kitu fulani ndani ya chumba

    “Eddy tuondoke ule upepo ni jini linaanalia usalama”

    Tukaanza kutambaa chini mimi na Yudia na kabla hatujaufikia mlango tulio ingilia tukastukia watu wawili walio valia nguo nyeusi zilizo wafunika hadi vichwa vyao wakasimama mbele ye-tu.Yudia akasimama na kuwasukuma huku na yeye akiwa anazungumza manena ya ajabu kawa wafanyavyo watu waliomo ndani ya kanisa lao na kuwafanya watu hao kuangukia pembeni kisha na mimi nikanyanyuka na tukaanza kukimbia kuelekea kwenye mlango mwengine ambao ni tofauti n mlango tulio ingilia.Katika mlango tulio ingili tukakuta vipande vya miti vilivyo fungwa tambaa lenye mafuta ya taa vikiwaka huku vikiwa vimechomekwa kwenye sehemu za ukuta wa sehemu hii na kuufaanya mwanga wake kuwa hafifu tofauti namwanga wa taa,Yudia akachomoa kimoja na kutangulia mbele huku akiniomba nimfwate

    Tukaendelea kutembea kwa mwendo wa haraka huku kila wakati nikiwa nitazama nyuma kuangalia kama kuna watu wanao tufwata ila sikuona,Tukaendelea kwenda mbele urefu kidogo nikaanza kusikia kelele za watu wakilia na wasiwasi wangu ukaanza kunitawala

    “Eddy usiogope hao ni miongoni mwa watu wanao sadikika kuwa duniani wamekufa ila wapo huku wamehifadhiwa na kila ifikapo mwisho wa wiki wawili huwa hutolewa sadaka ya kuteke-teza”

    “Sadaka ya kuteketeza ndio sadaka gani?”

    “Yaani wanapelekwa mbele ya Mungu wao ambeye ni yule mzee aliye kuja na yule mwanamke ndio malkia wao”

    Tukafika sehemu ambayo tukakuta chumba kikubwa chenye giza kilicho fungwa na gati kubwa huku kukiwa na mnyororo ulio fungwa na kufuli kubwa kiasi kwamba si rahisi kwa mtu kutoka ndani ya chumba hichi.Yudia akasogea huku akiwa ameshika kipande cha mti kinacho waka na kumulika kwa ndani ya chumba hicho na kujikuta nikiona watu wenye ngozi nyeusi mithili wamepakwa vumbi la mkaa huku wakiwa na nywele ndefu na chafu kiasi kwamba kinawafanya watishe tu kwamuonekano wao wakaanza kunyoosha mikono wakiomba msaada wa kutoka huku wengi wao wakiwa ni wamama na wanaume

    “Eddy watu hawa wanateswa sana na laiti baba na mama wakikushika nao watakuleta huku”

    “Hawa hawawezi kutoka?”

    “Hawawezi kwani hawa huki duniani walipo kuwa walisha zikwa na watu walisha wasahau”

    Tukazidi kwenda mbele huku nikijiuliza maswali ni jinsi gani Yudia amekuwa jasiri wa kuweza kuyatambua mambo ambyao ni yakuzimu japo kwa muonekano wake ni binti mdogo sana

    “Yudia umeyajuaje haya mambo?”

    “Baba na mama walinichagua mimi kuwa miongoni mwa waridhi wao katika kanisa lao kisheta-ni tangu mimi nikiwa mdogo,Kwa mara ya kwanza tulikuwa Marekani basi mama na baba wa-kawa wananifundisha mbinu zao zote ndio maana utaona siwaheshimu kwa maana wana roho mbaya na pele ulipo kuwa ukiona wanawekewa mikono kichwani walikuwa wanapewa nguvu na za ziada za kuweza kukukabili wewe”

    “Mmmmm kwani mimi nina nguvu gani ya kuwafanya wao wapewe nguvu ya kunikabili mimi?”

    “Eddy wewe kuna watu wanakulinda pasipo wewe mwenyewe kujua kama wanakulinda......Na watu hao ndio wanaokufanya wewe usiletwe huku na ikitokea watu hao wakauwawa basi wewe ndio utakuwa mwisho wa maisha yako kwa duniani na utaletwa huku kwenye shimo la giza na utakuwa ni miongoni mwa wale watu tulio wapiti pele wakiomba msaada”

    “Yudia wale watu ulio wasukuma hawata weza kutufwatilia?”

    “Wale hawawezi kutokana nimeyapoteza mawazo yao na kwanza walikuwa wamechelewa kwenye ibada na pale wamerudi majumbani mwao na afadhali nimekutana nao mimi na kama wangekutana na baba mwenye au kiongozi yoyote mule ndani ya kanisa leo wangesimulia”

    Tuakafika kwenye sehemu yenye vichwa vingi vya watu walio wafiki duniani na mifupa ya miili yao imezagaa kila sehemu ya chumba hichi,Yudia akaokota fuvu moja na kunipa nikishike kipande cha mti kinacho waka moto

    “Hili fuvu lilikuwa la msanii mmoja maarufu Tanzania na yeye nyota yake ilikuwa ni kubwa sana ila akishindwa kuiongoza na mwisho wa siku akajikuta akiletwa huku na kutolewa sadaka”

    Kila kitu anacho nieleza Yudia kikazidi kunichanganya kiasi kwamba nikajikuta nikikaa kimya pasipo kumuuliza kitu cha aina yoyote.Tukaondoka sehemu hii na kuzidi kwenda mbele na kutokea sehemu nyenye ngazi tukapanda na kutoka nje na tukatokea kwenye moja ya bustani zilizopo kwenye jumba la mchungaji.

    “Eddy kuna pete nitakupa ambayo hawa watu hawata weza kukuona hata yule mkuu wao kwani hii pete ninayo mimi mwenyewe tu na nilipewa kipindi nipo mdogo na mzee ambaye alikuwa ni kiongozi wao kipindi cha nyuma na alitokea kunipenda na kunifundisha mambo mengi”

    Tukaingia ndani na moja kwa moja tukapanda gorofani na kabla hatujaingia chumani kwake mlango wa chumba kimoja ukafungulia na akatoka mfanyakazi wa ndani na akaonekana kus-tushwa sana baada ya kutuona,akataka kurudi ndani ila Yudia akamuita na kumgandamiza ukutani kama mtu anayetaka kumpiga msichana wa watu

    “Nisikilize wewe OLE WAKO.....OLE WAKO NISIKIE UMEMUAMBIA MTU YOYOTE KUHUSIANA NA HILI TUKIO LA KUINGIA NA EDDY CHUMBANI KWANGU.....UTANIJUA MIMI NI NANI”

    Msichana wa kazi akatingisha kichwa akionekana kuelewa onyo hili kisha Yudia akamuachia na msichana wa kazi akarudi ndani kwake kwa haraka kisha mimi na yeye tukaingia ndani kwa Yudia.Chumba cha Yudia kimetawaliwa na mapicha makubwa ya makatuni huku kikiwa kimepangwa vizuri kwa umaridadi wa hali ya juu na kukifanya kiwe vizuri.

    Akafungua kwenye droo ya kabati lake na kutoa kisanduku kidogo cha chuma kisha akakifungua kwa namba za siri anazo zijua yeye mwenyewe na kikafunguaka na akatoa pete moja nzuri ya kung’aa sana kisha akanisogelea na kuniomba nimpe mkono wangu wa kushoto kisha akanivisha kwenye kidole cha kati na kwauzuri ikakaa vizuri

    “Eddy ninakuomba usiivue hii pete kwa maana siku ukiivua ndio utakuwa mwisho wa maisha yako....na kama unataka kujikinga na kitu kibaya wewe inyooshe mbele na kitu hicho hakita we-za kukudhuru hata wale wanao kutafuta pia hawata weza kukudhuru ikiwemo kina baba na majini wake”

    Yudia akanibusu mdomoni kisha akanifungulia mlango wa chumbani kwangu na kuniomba ni-toke.Nikaelekea chumbani kwangu na sikupata usingizi hadi kukapambazuka na mlango wangu ukagongwa na nikashuka kitandani na kuufungua mlango nikakutana na mama mchungaji akiwa amejifunga matenge yake akionekana ametoka kulala

    “Eddy Bwana Yesu asifiwe”

    “Amen”

    “Umeamka salama?”

    “Ndio mama sijui nyinyi mumeamkaje?”

    “Salama tu....Chai ipo tayari karibu mezani”

    “Asante mama”

    Mama mwenye nyumba akaondoka na nikabaki nikimtazama kwa macho ya kujiuliza ni kwanini wanakuwa na roho za ajabu.Nikafunga mlango wangu na kuingia bafuni na kusimama mbele yak ii kikubwa kilichopo ndani ya bafu hilo,nikafungua maji kwenye bomba na kuanza kunawa uso wangu gafla nyuma yangu kukasimama mtu mwenye sura ya kutisha na kunifanya nistuske ila nikaona kama anashangaa shangaa huku akinusa nusa kwenye sehemu niliyo simama na nikagundua hanioni ndio maana ana nusa nusa.Nikasogea pembeni taratibu pasipo kumgusa kisha nikamyooshea mkono wa kushoto wenye pete na kustukia mtu huyu akianza kuyumba huku akitokwa na damu iliyo chananyikana na uweusi mdomoni mwake na hapa ndipo nikaamini kuwa pete aliyo nipa Yudia inafanya kazi vizuri.Nikaushusha mkono wangu na kumfanya mtu huyo kupotea mbele ya macha yangu na damu zote zilizo tapakaa chini zikawa zimepotea kwenye sakafu.Sikuogopa sana kutokana vimbwanga kama hivi nimevizoea na kwanu ni kawaida sana kuona vitu kama hivi.Nikatoka bafuni na kujifuta maji na taulo kisha nikajiweka sawa nguo zangu na kutoka ndani kwangu na kuelekea sebleni na kuwakuta watu wote wakiwa wamejumuika mezani kwa ajili ya kunywa chai,nikakaa kwenye kiti kilicho andaliwa na kusalimiana na kila mmoja na mchunajia akatuomba tufumbe macho yetu ili aongoze sala.Tukaanza kunywa chai taratibu huku mara kwa mara macho yangu yakiwatazama mchungaji na mke wake na kujikuta nikijisemea kimoyo moyo

    “Kwa mtindo huu mbinguni kufika ni baadaye sana”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Tukamaliza kunywa chai na kuwaomba mchungaji na mke wake waniruhusu kuna sehemu ni-nahitaji kwenda

    “Sasa Eddy huoni kama tutachelewa kufanya maombia nyumbani kwako?”

    “Hiyo seemu ninayo kwenda sio mbali sana na hapa....Ninakwenda kuchukua pesa yangu mara moja kisha nitarudi”

    “Ahaaa huyo mtu unamdai kiasi gani cha pesa”

    “Laki nane”

    “Mama Yudia nenda kwene koti langu la suti niliyo ivaa juzi kuna pesa naomba utoe laki nane na nusu uje nazo hapa”

    “Lakini baba si mumuache aende zake munamng’ang’ania nini kwani ni ndugu yetu huyu?”

    Yudia alizungumza kwa kisirani kama alivyokuwa akifanya jana usiku na kuwafanya watu kad-haa walio kaa mezani kuguna akiwemo na Junio

    “Dada Yudia kwanini unamchukia sana kaka Eddy?”

    “Na wewe koma sizungumzi na mbwa naongea na mwenye mbwa.....SAWA?”

    “Ehhe Yudia mwanangu mbona unatabia mbaya kiasi hichi hata hupuumziki hujui kama kuna wagani au hakuana”

    “Mama na wewe hizo roho zenu za ajabu ajabu zitawaponza na sitaki mumpe pesa yoyoyte”

    “Mama Yudia hembu achana neye nenda kalete hizo pesa”

    “Mama ukienda kuanzia leo mimi sio mtoto wenu wa kumzaa.....Hamuwezi kumpa mtu baki pesa zite,Yeye amekuwa nani hadi mumpe?”

    “Mchungaji ili musigombane na Yudia ngoja mimi niende mara moja ila nitarudi muda sio mre-fu”

    “Basi ngoja nimuambie Joseph akaupeleke na gari”

    “Hapana mchungaji nitarudi muda sio mrefu”

    “Sawa”

    Yudia akanyanyuka na kutoka nje na mimi nikaagana nao kutoka na sikumuona Yudia sehemu alipo ila sikuwa na shaka sana,Mlinzi wa gatini akanifungulia geti na kumkuta Yudia akiwa amesimama pembeni ya geti huku machozi yakiwa yanamwagika

    “Yudia mbona unalia?”

    “Eddy najua kwamba huto rudi tena huku na nilifanya vile ili wasielewe kitu kinacho endelea japo nimekudhalilisha ninakuomna unisamehe”

    “Usijali asante kwa yale yote uliyo nifanyia kwan sinto weza kukusamehe”

    “Ngoja nikupe namba yangu ya simu”

    Yudia akaiandika namba yake ya simu kwenye simu yangu kisha na nikamtajia na yakwangu na akaiandika na akanikumbatia huku machozi yakimwagika kisha akiivua cheni aliyo ivaa shingoni na kunivisha

    “Ho ni ukumbusho wangu kwako”

    “Asante ila tutawasiliana”

    Nikamuachia Yudia na kuondoka zangu huku nikimuacha Yudia akinipungia mkono na mimi nikampungia na kuongeza mwendo na kuondoka katika eneo la nyumba ya mchungaji na nikafka kwenye kituo cha waendesha pikipiki na kukodi pikipiki ikanipeleka hadi kwenye shule ninayo ifundisha na baadhi ya wanafunzi wakaja kunipokea kwa furaha.Wakanisindikiza hadi ofisini na kuwakuta waalimu wengine nao wakaonekana kufurahi kwa kuniona japo nimewakuta wapo kwenye kikao.Wanafunzi wakarudi zao madarasani na mimi nikasalimia na waalimu wote na kukaa kwenye kiti changu nilicho kizoea na kikao kikaendelea kama kawaida na mada kubwa ilihusiana na utivu wa nidhamu kwa baahi ya waalimu wa kike.Mwalimu aliye kanywa sana ni Madam Recho ambaye amezoeleka kuwa anatabia ya uchonanishi kwa baadhi ya waalimu na hata baadhi ya wazazi wanao taka kuwahamishia watoto wao kwenye shule yetu.Sikuchangia kitu cha aina yoyote hadi kikao kikaisha.Mwalimu mkuu akaniita ofisini kwake na sikuwa na tukaongozana hadi ofisini kwake

    “Sir Eddy unaendeleaje?”

    “Salama tuu mkuu sijui nyinyi hapa?”

    “Sisi tunaendelea salama”

    “Vipi Zena Alisha toka hospitali?”

    “Ndio aliruhusiwa jana yupo nyumbani kwake kama utapata muda tunaweza kwenda kumuona”

    “Sawa”

    Kabla mkuu wa shule hajazungumza chochote mlango wa ofisini kwake ulagongwa na akamruhusu anaye gonga kuingia.Akaingia rafiki wa Rahma na kumuomba mkuu wa shule boksi za chaki ambazo ameagizwa na mwalimu wa taaluma.Akaonyeshwa boksi kubwa lenye chaki analibeba na kuondoka nalo na kumfanya mkuu wa shuke kubaki akimtazama rafiki wa Rahma kwa nyuma jinsi makali yake yanavyo tingishika

    “Mmmm watoto wa siku hizi”

    “Wana nini mkuu?”

    “Wanadatisha sana mtu unaweza ukajikuta unafungwa hivi hivi”

    “Haaa ndio hivyo mkuu”

    “Ila kuna mtoto wa kiarabu ninamfukuzia hadi leo ila bado hajanikubalia”

    “Kwa nini hajakukubalia?”

    “Mtoto kila nikimpa maneno matamu ya kiutu uzima anadia kuwa atanijibu na tayari ameshanilia pesa yangu si chini ya milioni”

    “Ehee”

    “Kweli Eddy ninakuambia hivi kama mwanangu na hapa shule nataka nifanye mapinduzi kidogo ya utawala....”

    “Kwa nini?”

    “Nimeamua tuu nataka nifanye mpango wa kukupandisha wewe na kuwa makamu mkuu wa shule”

    “Huyu wa sasa hivi naye atakuwa wapi?”

    “Huyu anahama zimebaki siku tatu za yeye kuwepo hapa na mimi kama mkuu wa shule ninahi-taji kupendekeza mtu mwenye akili timamu.....Sio kama hawa kina Recho akili zao zipo makalioni hawaheshimu kazi kabisa”

    “Mkuu huoni majukumu unayo nikabidhi nimakubwa tofauti sana na muda wangu nilio kuwepo kazini?”

    “Ahaa muda wako wa kuwepo kazini hauna shida cha msingi ni utendaji wako wa kazi kuna watu wapo kazini sasa ni mwaka wa 30 ila utendaji wao ni mbovu kupindukia”

    “Sasa itakuwaje kwa waalimu wanao nichukia?”

    “Wewe unaogopa kuchukiwa potelea pote ila cha msingi ni kwamba unakuwa msaidizi wangu ila kuna kajikazi nahitaji nikupe kwa maana wewe unapendwa sana hapa shule na wanafunzi wengi hilo halipingiki”

    “Kazi gani mkuu?”

    “Nahitaji unifanyie mpango kwa yule msichana niliye kuambia”

    “Anaitwa nani?”

    “Anaitwa RAHMA anasoma kidato cha nne”

    Nikajikuta nimekaa kimya nikimtazama mkuu wa shule huku nikijiuliza kama akili zake zina-fanya kazi sawa sawa au ndio uzee unamchanganya





    Nikakaa kimya huku nikimtazama mkuu wa shule machoni kwani sikujua ni nini nimuambie

    “Eddy ukihitaji hata pesa mimi nitakupatia ili tu nimpate Rahma”

    “Ila mkuu mbona msichana mwenyewe simuoni hapa shule”

    “Amesafiri ila akirudi tu nataka niweke mambo sawa”

    “Usijali mkuu wangu”

    Nikajikuta nikinyanyuka kwenye kiti nilicho kaa na kumuaga mkuu wa shule na kumuahidi nitalifanyia kazi na nikarudi ofisini kwa waalimu wengine na kuwakuta kila mmoja akiendelea na shuhuli yake kutokana sikuja kikazi nikabaki nikiwa ninajisomea baadhi ya vitabu vinanavyohusiana na masomo yangu ninayo yafundisha.Simu yangu ikaingia ujumbe mfupi wa meseji na nikakuta ni namba ya Rahma

    “BABY UWAHI KURUDI NIPO NYUMBANI KWAKO NA HALDA”

    Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kuona saa ya kwenye simu yangu inaonye-sha zimabaki dakika kumi kutimu saa sita kamili kabla haujafika muda tulio ahidiana na mchungaji juu ya kwenda kufanya mamombi ambayo kwa wakati huu kwangu sikuyaona na umuhimu wa aina yoyote kwani mchungaji mwenyewe anaushirikiano na Olvia Hitler.Nikanyanyuka kwa haraka na kabla sijaufikia mlango wa kutokea ofisini simu yangu ikaita na kuikuta ni namba ya mchungaji,nikabaki nikiitazama pasipo kuipokea na kumfanya madam Recho kuzungumzaCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    “Jamani si mzime misimu yenu inatupigia kelele”

    Niakageuka na kumtazama madam Recho na sikuseme kitu cha aina yoyote zaidi ya kuminya kitufe cha kupokelea simu na kuiweka sikioni na kuisikia sauti ya mchungaji

    “Mpendwa tumefika nyumbani kwako tupo hapa getini tunaomba utufungulie mlango kwa maana tunapiga honi nahisi uisikii kutokana na mziki ulio ufungulia kwa sauti ya juu”

    “Ahh...Sawa mchungaji nakuja”

    Nikakata simu na kubaki nikiwa nimetizama chini huku nikishush pumzi na sikujua nifanye nini kuhusiana na swala la kwenda nyumbani kwa kwangu kwani hali ya hewa imesha haribika.

    “Eddy unapakwenda?”

    Mkuu wa shule aliniuliza na nikamjibu kwa kutingisha kwichwa nikiashiria kuwa sina pa kwenda

    “Basi twende sehemu moja kama huto jali”

    “Sawa mkuu”

    Tukatoka ofisini na kuingia kwenye gari ya mkuu wa shule na sikujua ni wapi tunakwenda na ndani ya gari sikuzungumza kutu cha aina yoyote hadi tukafika kwenye moja ya mtaa ambao sikuujua jina lake na sote tukashuka kweye gari na mkuu wa shule akaminya kengele ya getini kwenye nyumba nzuri na baada ya muda geti likafunguliwa na akatoka msichana mdogo anaye onekana ni mfanyakazi wa ndani na baada ya kumuona mkuu wa shule akaanza kumchangam-kia huku wakitaniaana kwa baadhi ya maneno kisha akatukaribisha ndani na moja kwa moja tukapitiliza hadi sebleni na tukakaa kwenye sofa na msichana wa kazi akasimama na kuiwasha tv iliyopo ukutani na kuaanza kuadilisha badilisha chaneli zilizopo kweye king’amuzi wanacho kitumia

    “Babu siku hizi mambo yako sio mabaya naona dada akakupendezesa ana”

    “Kawaida babu yangu”

    “Mmmm kweli ni kawaida kwani hiyo inye uliyo ifungashia utaweza kusema kuwa wewe ndio mwenye nyumba”

    “Babu jamani hujaacha vituko vyako?”

    “Ndio ukweli na siku hizi unanga’aa sana”

    “Asante”

    “Haya huyu mwenzako yupo wapi?”

    “Dada amekwenda hospitalini mara moja ila muda si mrefu atarejea”

    “Ahaa amakwenda hospitali gani?”

    “Buriani”

    “Eddy hapa ni nyumbani kwa madam Rukia”

    “Ahaaa asante”

    Mfanyakazi wa ndani akaondoka na kwenda jikoni na kutuacha tukia tunatazama Tv baada ya muda kidogo mkuu wa shule akanyanyuka na kuniambia anakwenda mara moja jikoni kuzun-gumza na mfanya kazi wa ndani.Nikabaki nikitazama Tv galfa nikasikia simu yangu ikiita na ni-kaitoamfokoni na kuikuta ni namba ya mchungaji,Sikutaka kuipokea nikaiweka simu pembeni huku nikitafakari ni kitu gani nifanye.Simu ikaita kwa mara tatu mfululizo na sikuipokea na kwabahati nzuri ikaanza kutoa ishara ya kuishiwa na chaji na taratibu nikanyanyuka na kuele-kea jikoni kumuuliza mfanyakazi wa ndani kama anaweza kunipatia chaji ya pini nyembam-ba,Kila ninavyo karibia kufika jikoni nikazidi kuisikia miguno ya watu kulalamika ikanilazimu kunyata taratibu na kwakupitia kajiuwazi ka dirisha nikamuona mkuu wa shule akinyonya ma-ziwa ya mfanyakazi wa ndani anayeonekana kulegewa na kunogewa na penzi la mkuu wa shule.Taratibu nikaanza kuhisi mabadiliko kwenye suruali yangu kwani koki yangu taratibu imeenza kuleta fujo.

    Mkuu wa shule akaimalizia khanga ya mfanyakazi wa ndani katika kuivua na kuitupa china na kumfanya mfanya kazi wa ndani kuzidi kutoa miguno kiasi kwamba nikazidi kupata shinda kwenye suruali yangu,akili yangu moja ikanituma niingie na mimi nijumuike ila akili yangu moja ikasita kulifanya ninalo lifikiria na kubaki nikiendelea kuwatazama kwa jinsi wanavyo fanya yao na kujikuta nikilisogelea dirisha la jikoni vizuri ili nioene kila kitu.Mkuu wa shule mkono wake mmoja akauiniza kwenye ikulu ya mfanyakazi wa ndani iliyo zungukwa na ukuta wa chupi nyembamba na kuanza kuichezea ikulu ya mfanya kazi huyo na kumfanya taratibu kuanza kwenda chini huku akitoa vilio vya raha hadi wote wakajikuta wamelala sakafuni kisha mkuu wa shule akaipanua miguu ya mfanyakazi wa ndani kisha akamvua chupi yake na kuendelea kuichezea ikulu ya mfanyakazi wa ndani kiasi kwamba mfanyakazia akanyanyuka kama mbogo mwenye hasira na kuyashika mashavu ya mkuu wa shule na kuikutanisha midomo yao na kuanza kunyonyana kisha kwa nguvu akamlaza mkuu wa shule chini na kuvifungua vifungo vya shati kisha akaanza kumnyonya kifua kizima cha mkuu wa shule na kujikuta nikibadilisha mapozi ya miguu yangu kwani koki yangu nzima imesimama kiasi kwamba nikahisi ushirikiano wake na boxer unaanza kuwa mgumu

    Mfanyakazi wa ndani akaifungua zipu ya suruali ya mkuu wa shule hapo nikajikuta nikistaajabu kwani mkuu wa shule mashine yake imelala na kushindwa kuelewa wakati wote aliokuwa akifanya mautundu kumbe mtu mzima haendi mtungi.Mfanyakazi wa ndani akaanza kuinyonya koki ya mkuu wa shule zaid ya dakika kumi ila haikusimama kabisa kiasi kwamba nikaanza kumuona mfanyakazi wa ndani akiaanza kuchoka

    “Babu bwana wewe kila siku ni hivi hivi unanipandisha nye*e ila kufanya hatufanyi”

    “Babu uzee mwaya”

    “Ila wewe si umeniambia kuwa hadi ustuliwe na mwanaume mwenzako ndio ina simama”

    “Sasa nitamwambia nani?”

    “Kwani yule uliye kuja naye si unaweza kumwambia?”

    “Mmm hapo napo kuna mtihani?”

    “Sio mtihani kwani wewe kila ukija unanipandisha maruhani alafu kuyashusha unashindwa na leo sinto taka kupiga punyeto nataka unipe haki yangu”

    Nikamshuhudia mkuu wa shule akishusha pumzi nyingi huku akionekana kuwa katika wakati mgumu kiasi kwamba hakujua afanye nini.

    “Babu nenda bwana mimi leo hapa hutoke hadi unipe haki yangu”

    “Sasa unadhani Eddy atakubali kuniingiza mashine yangu kwenye nanilio yangu ili yangu isi-mame?”

    “Hilo utalijua mwenyewe ila mimi nataka sasa hivi umesha nipandisha majini ya kidigo sasa na-taka uyashushe”

    Mkuu wa shule machozi yakaanza kumlenga lenga na kumuona akinyanyuka kiunyonge na kuivaa suruali yake na kwaharaka nikarudi sebleni na kukaa kwenye makochi na kujiweka vizuri na kujifanya sijui ni kitu gani kinacho endelea.

    “Eddy”

    Nikageuka baada ya kuisikia sauti ya mkuu wa shule ikiniiita na kumkuata akiwa anajifunga vi-zuri vifungo vya shati lake na kabla hajazungumza chochote tukastukia mlango ukifunguliwa na akaingia Madam Zena huku mguu wake mmoja ukiwa umefungwa bandeji kwenye sehemu ya chini.Akaonekana kushangaa kuniona nyumbani kwake,Akamsalimia mkuu wa shule na mimi akanipa salamu huku sura yake akiwa ameikunja kidoo na akakaa kwenye sofa jengine na kuiweka pochi yake kwenye meza ya kioo na kumuita mfanya kazi wake wa ndani na baada ya dakika kadhaa mfanyakazi wake akaja huku akiwa amevalia khanga yake

    “Mbona wageni hujawatengea vinywaji?”

    “Ndio nilikuwa ninamalizia kuitengeneza juisi”

    “Sasa hiyo juisi si nilikuambia kuwa uitengeneze tangu asubuhi?”

    “Nilikuwa nafanya usafi dada”

    “Haya kalete hiyo juisi”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Mfanya kazi wa ndani akaondoka na kutuacha tukiwa kimya huku macho yangu nikitazama mechi ya marudio ya kombe la dunia

    “Zena unaendeleaje?”

    “Naendelea vizuri tu baba”

    “Vipi maumivu maumivu?”

    “Kidogo yamepungua ila ikifika mida ya saa kumi na mbili jioni huwa mguu unavuta sana”

    “Pole nimeona leo nije na Eddy ili kuweza kuzitatua tofauti zilizopo kati yenu”

    Mfanyakazi akarudi akiwa amebeba glasi tatu zilizo jaa juisi na kuziweka juu ya meza kisha akatukaribisha

    “Alafu wewe Amina si nimekuambia hiyo tabia ya kushinda na khana moja mimi siihitaji?”

    “Samahani dada”

    “Hembu nenda kavae nguo zako....unamuonyesha nani hayo makalio yako”

    Amina akaondoka kiaibu aibu na kumfanya mkuu wa shule kumtazama Amina kwa jicho la kui-ba huku akisindikiza kwa muno mzito ulio mfanya madam Zena kuachia kicheko kiliho nifanya na mimi nicheke

    “Mkuu muda wako umesha kwisha”

    “Ahaaa wapi bado ninadai”

    “Na uzee huo ukimpata mtoto kama huyo si atakuua kabla ya siku zako”

    “Wapi binti kama huyo nampiga goli za kizee lazima adate na mimi”

    Madam Zena akaanza kucheka kwa kicheko kikubwa na kwajinsi wanavyo taniana unaweza kusema sio mtu na bosi wake

    “Zena hata wewe ninakuweza tena sana”

    “Hahaaa haa usinichekeshe mkuu mimi utaniwezea wapi wakati hata vijana kama hao kina Eddy wananishindwa”

    “Eti Eddy unamshindwa Zena?”

    “Sijui”

    “Haaa hujui nini sasa?”

    “Haujui maana yake ni jiu tosha kwamba mimi haniwezi”

    “Haaa Eddy unaniaibisha”

    “Nakuaibisha na nini?”

    “Si Zena anasema kuwa humuwezi”

    “Ila mkuu si unaona Zena ni mgonjwa”

    “Mgonjwa wapi kwani wewe unaufanya mguu au nanilio yangu”

    Sote tukajikuta tukicheka kwa furaha huku mimi kicheko changu kikiambatana na swala la mkuu wa shule kushindwa kumpa haki inayo stahili Amina

    “Hayo ndio mambo ninayo yahitaji nataka Eddy na Zena muwe munacheka kama hivyo ila si kuwekeana vinyongo havina msaada wowote kwenye maisha yenu”

    “Mimi mbona Eddy nilisha msamehe”

    “Kweli”

    “Ndio huwa mimi sina moyo wa kumuwekea mtu kisasi”

    “Eddy je umemsamehe ZENA?”

    “Mimi sina tatizo naye nipo powa kabisa”

    “Haya sas nawaomba munyanyuke mupeane mikono”

    Tukasimama na kupeana mikono na madam Zena kisha tukakumbatiana na kila mmoja akarudi kukaa kwenye sofa lake na tukaendelea na mazungumzo ya kawaida na tukamuaga Madam Zena kisha sisi tukarudi shule na sikuwa na haja ya kukaa sana shule nikaga na kuondoka zangu sikuweza kujua kama nitaweza kumkuta mchungaji na watu wake au laa kwani simu yangu tayari imesha zima chaji.Nikakodi bodaboda hadi nyumbani kwangu na sikuona gari la mchungaji likiwa nje kwangu zaidi ya kuusikia mziki ukitoka nyumbani kwangu.Nikashuka kwenye bodaboda na kumlipa pesa yake kufungua geti na kuingia ndani na kukuta gari ya Halda ikiwa imesimama pembeni ya mlango wa kuingilia sebleni

    Nikafungua mlango namtu wa kwanza kuniona ni Rahma na kwaharaka akanikimbilia na kuni-kumbatia kwa furaha na tukaanza kunyonyana midomo yetu na kumfanya Halda kuanza kukunja sura yake kila nilipo mtazama.Tukaachiana na Rahma na akaonekana kunishangaa

    “Baby mbona umekondo tofauti namwanzoni nilipo kuacha?”

    “Wee acha tu kuna vimbanga kwenye hii nyumba hadi ninakonda”

    “Halda alinisimulia nikamuambia kuna maji nitarudi nayo yatakayo weza kuzuia vitu vya ajabu ajabu....Alafu kuna wageni wako hapa walikuja siwaelewi elewi nikawatukana kama nini?”

    “Wakoje?”

    “Wamesema ni watumishi wa bwana mimi nikaona wananizingua nikawajibu mbovu”

    “Ahhha wakasemehe?”

    “Wakasema mkono wa bwana uwe juu yangu na nikakupigia simu ila hukuwa hewani”

    “Simu yangu imekata chaji?”

    “Shem mambo vipi?”

    “Safi mzima”

    “Mimi mzima......Jamani ngoja niondoke kuna mtu ninakwenda kumcheki?”

    “Ok basi baadaye”

    Halda akaondoka na kutuacha mimi na Rahma ambaye nikakuta tayari wameniandalia chakula na taratibu tukaanza kula huku kila mmoja akionekakana kuwa na hamu na mwenzake.Rahma akanyanyuka kwenye kiti alicho kaa na kunikalia kwenye mapaja yangu na tatibu akaanza kunipapasa kila kona ya mwili wagu.Na mimi nikaanza mautundu ya kuzichea chuchu zake huku midomo yangu ikiinyonya shingo yake hadi akaleea.Nikamnyanyua Rahma hadi chumbani kwangu na kuanza kumvua nguo moja baada ya nyingine na yeye akafanya kama nilivyo mfanyia na sote tuajikuta tupo kama tulivyo zaliwa na kazi ikaanza ya kupeana raha kiasi kwamba kila mmoja akawa na kibarua cha kufuruahisha mwenzake

    Rahma akazidi kuongeza kasi ya mashambulizi ila kutokana nimesha mzoe hakunitisha sana zaidi ya mimi kuzibana sehemu zake ambazo siku zote nikimbana huwa niamshinda kwenye mechi zake.Galfa mwili wa Rahma ukaanza kukakamaa huku macho yake yakibadilia na kiini cheusi kikapotea na kukabaikia kweupe tu huku mapuvu yakiaanza kumtoka mdononi kitendo kilicho anza kunichanganya kwani tangu nimjue Rahma sikuwahi kumuaona akiwa katika hali kama hii

    Hali ya Rahma ikazidi kuwa mbaya kitandani na kunifanya nizidi kupagawa hata sikujua nifanye kitu gani kitakachoweza kumrudisha Rahma katika hali yake ya kawaida.Nikasimaa na kuiokota suruali yangu chini na kuivaa kisha nikuitoa simu yangu mfukoni na kukuta haina chaji ikanilazimu kuitafuta simu ya Rahma na ndani ya chumba changu haikuwepo ikanilazimu kwenda sebleni na kuikuta juu ya meza ya chakula nikaichukua na kukuta meseji moja na kwabahati mbaya nikaifungua

    ‘WEWE RAHMA UPO WAPI TUNAKUSUBIRIA NYUMBANI KWENYE KIKAO HUYU MUME WAKO AMESHA KUJA’

    Nikajikuta nikiirudia rudia meseji yake kuisoma kiasi kwamba nikajikuta nikikaa juu ya meza vizuri na kwa haraka namba iliyo tuma meseji ninaifamu ni ya mama yake ambayo alinipa siku moja shuleni.Nikabaki nikiwa nimetulia zaidi ya dakika tano huku nikijikuta rohoni mwangu nikijiwa na wivu mkali ulio andamana na hasira kali,Nikastuka simu yake iikita na kuona ni namba ya baba yake ikiingia na kubaki nikiwa nimeitazama kiasi kwamba nikajikuta nikianza kutetemeka kwa woga,Hadi simu inaka nikajikuta nikiwa kimya nisijue ninafanya niniCHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Wazo la kumpigia Halda likanijia kichwani na nikaanza kuifungua simu ya Rahma sehemu alipo hifadhi majina ya watu mbalimbali na kujikuta zaidi ya dakika kumi nikilitafuta jina la Hilda ila sikulipata kwani sikujua ameliandika vipi ndani ya simu yake.Nikasikia honi ikipiga getini na kwaharaka nikajua atakuwa ni Hilda ambeye ameondoka nyumbani kwetu muda si mrefu na kwa haraka nikanyanyuka na kutoka nje na hatua ya kwanza nikachungulia dirishani kutazama ni nani anaye piga honi na kujikuta nikistuka na kajasho kembemba kakianza kunienda mbio,hii ni baada ya kuliona gari jeusi anina ya Land cruser likiwa limesimama nje kwangu huku likiwasha taa zote mbili

    “Nani huyu?”

    Nilijiuliza mwenyewe kana kwamba kuna mtu pembeni yangu ninaye zungumza naye kumbe nipo peke yangu.Nikamshuhudi Hilda akishuka ndani ya gari hilo na kuanza kupiga hatua za haraka kuja kwenye geti langu kidogo moyo ukanipata matumaini na kujikuta nikulifungua geti na Hilda kwa ishara akamruhusu dereva wa gari kuliingiza ndani na nikabaki nikiwa ni nimeduwaa hadi gari linasimama akashuka jamaa mmoja mweusi kiasi aliye valia vizuri na kujikuta nikirudi katika hali ya kawaida baada ya jamaa kunisalimi

    “AHaaa salama tuu kaka karibuni”

    Nilizungumza huk u nikiliegesha geti langu na endapo kutatoke ishu yoyote niweze kukimbia kuepukana na msala uliopo ndani

    “Eddy huyu anaitwa Rashid ni dereva wao Rahma”

    “Ahaa karibu ndugu”

    “Asante vipi huyo bibie yupo ndani?”

    Swali la dereva nikajifanya kama sijalisikia na kuongoza ndani huku wao wakinifwata kwa nya-ma na mimi moja kwa moja nikaingia ndani na kuukuta Rahma akiwa ametulia huku mapigo yake ya moyo yakienda taratibu kiasi kwamba nikabaki nikimtazama kwa muda.Nikasikia sauti ya Hilda ikimuita Rahma huku akionekana kuja kwenye chumba chetu ikanilazimu kunyanyuka kitandani kwa haraka na kwenye kuufungua mlango na kumkuta akiwa amesimama mlangoni kwetu

    Muambie huyo Rahma kwao wanamsubiria sana na ninampigia simu hapokei”

    “Kwani kwao kuna nini?”

    “Mimi wala sijui ila muambie kuwa kwao wanamsubira tena huyo dereva alitumwa kuja kwangu kumchukua kwa maana nilitoka naye nyumbani kwao”

    Nikabaki nikimtazama Hilda huku nikikosa kitu cha kuzungumza hadi akaanza kuhisi kitu na macho yake yakanitazama kwa muda

    “Eddy mbona una wasi wasi?”

    “Eheee?”

    “Mbona una wasi wasi?”

    “Rahma ana umwa”

    “Nini?”

    “Rahma naumwa na hapa nilipo sijua ni uginjwa gani?”

    “Mungu wangu yupo wapi sasa?”

    “Humo ndani”

    Halda akausukuma mlango na kumkuta Rahma kitandani akiwa amelala na kumshuhudia akianza kumwaga machozi na taratibu sauti yake yakulia ikaanza kuongezeka

    “MIMI NINAWAAMBIA NINI WAZAZI WAKE JAMANI......EDDY UMEMFANYA NINI MTOTO WA WATU”

    “Usilia sasa kwa sauti”

    “Eddy acha nilie bwana umefanya nini mtoto wa watu mbona mimi sielewa?”

    “Sasa wewe ukilia unadhani kutakalika humu ndani”

    Nilizungumza huku nikianza kumvisha nguo Rahma na jasho jingi likazidi kunitiririka mwilini mwangu kiasi kwamba nihata uvishaji wangu nikajikuta mara kwa mara nikikosea kumvisha hadi ninamaliza kumvisha ni zaidi ya dakika kumi.

    “Eddy Rahma ndio huyo amekufa unadhani mimi nitafanyaje na jaki ya MUNGU wazazi wake wakisema ni nani aliye fanya hivi mimi ninakutaja”

    “Sasa hivo utakuwa unaharibu”

    “Sio kuharibu”

    “Kweli vile ni lazima niwambie na nitawaleta hadi hapa kwako”

    Nikatoka sebleni na kumkuta dereva akiwa amesimama akionekana kama kusikilizia mazun-gumzo ambayo tunazungumza mimi na Hilda

    “Kaka vipi kuna kitu gani kimetokea?”

    “Ndugu yangu wewe acha tu kwa maana kuna ishu imetokea......Rahma ametokwa na mapovu na mwili wake umekakamaa sasa Hilda analia lia si unajua tena maswala ya wanawake”

    “Haaa huo ni ugonjwa wake ambao humtokea kila baada miezi sita”

    “Kweli?”

    “Ndio”

    “Ngoja basi nimlete huku”

    “Usimtoe ngoja nimpigie simu mama yake kwa maana ugonjwa wake huu endapo utampata se-hemu alipo hapaswi kutolewa kwenye eneo alilopo na kuna shangazi yake ni mganga wa kihindi na kwa bahati nzuri yupo kwao wamerudi naye huwa ndioyo anamtibu Rahma”

    “Hembu ngoja kwanza unataka umesema kuwa hapaswai kutibiwa sehemu yoyote zaidi ya se-hemu alipo pwatwa na ugonjwa huo?”

    “Ndio na mukimuhamisha tu lazima anafariki?”

    “Mungu wangu.....wewe umejuaje?”

    “Ndugu ni mwaka wa 15 ninafanya kazi kwa kina Rahma na usinione hivi ni kijana ila umri wangu ni mkubwa na Rahma tangu yupo mdogo ninashuhudia matibubu yake yanakuwa hivyo na huo ugonjwa ameridhi kutoka kwa mama yeke”

    Nikajikuta nikijibwaga kwenye kochi huku nikihisi nguvu za mwilini mwangu zikiniishia kiasi kwamba nikabaki nikiwa sina la kuzungumza na nikamshuhudia dereva akipiga simu na kuanza kuzungumza na mama wa Rahma na akaanza kutoa maelekezo ya sehemy alipo kiasi kwamba nikabaki nikitetemeka na akakata simu na kunitazama

    “Wamesemaje?”

    “Wamesema kuwa wanakuja na sasa hivi....Ila si wanakujua wewe?”

    “MIMI.....?”

    “Ndio wewe?”

    “AHhhhhhaaaa”

    “Ohoo basi vyema ukawa makini?”

    “Makini na nini?”

    “Yule mzee hana utani na mtoto wake na huwa hapendi sana watu weusi japo mimi nimepata bahati ya kufanya kazi kwake ila hataki hata kuniona ninazungumza na mwanae”

    “Mmmm sasa..?”

    “Hakuna cha sasa”CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    Akili yangu ikazidi kuchanganyikiwa na kusimama huku mapigo ya moyo yakianza kwenda mbio na sikujua hata ni nini nifanya,Nikaingia ndani kwangu na kumkuta Hilda akiwa amekaa kitandani huku akiwa amemtazama Rahma huku akiendelea kulia na baada ya kuniona akanif-wata na kuanza kunipiga kifuani

    “Eddy wewe ni katili umemuua rafiki yangu kwanini.....?”

    Sikutaka kumjibu Hilda na kitu chochota na kumsukuma pembeni na kufungua kabati langu na kuanza kutafuta nguo ya kuvaa na kwa kiwewe nikajikuta nikichukua vesti na kuvaa na kabla sijatoka nje nikastukia Hilda akinishika vesti niliyo ivaa na kuanza kunivuta

    “Hapa Eddy na kuambia hotoke na nimesha mpigia baba na kaseme anakuja”

    “Wewe nimekuambia niachie nitakubamiza”



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog