Search This Blog

Thursday, 19 May 2022

MY DIARY - 4

 







    Chombezo : My Diary

    Sehemu Ya Nne (4)





    Rafiki yako kwa sasa ni marehemu na mwili wake umekutwa kwenye msitu wa tembo. Uchunguzi wa awali wa kipolisi na kitabibu unaonesha kuwa marehemu



    aliuwawa kwa kupigwa risasi na kabla ya hapo inaonesha alibakwa na kuharibiwa vibaya sehemu zake za siri. Kwani inaonesha aliingiliwa kinyume na



    maumbile. Tunaomba uwe mvumilivu kwa taarifa hizi lakini polisi bado wanaendelea na uchunguzi wa swala hilo. Watuhumiwa wantafutwa kwa udi na



    Mwili ulianza kunitetemeka machozi yakinibubujika kama mtu aliyechomwa na mkuki moyoni.Nilishindwa hata kuongea machungu ya nafsi yalinizidi



    nikatamani hata nimpige yule

    polisi aliyekuwa akinipa taarifa. Sikuamini nilichokisikia na niliona ni uwongo tu, Joyce yupo hai huyo wamemfananisha tu.Kufikia hapo machozi yalikuwa



    yakinibubujika sikuamini nilichosikia. Nilihisi labda nipo ndotoni. Nikamuuliza yule polisi je naweza kuuona huo mwili wa marehemu na mimi nithibitishe kwa



    macho yangu kuwa Joyce ni marehemu?



    “ Kwa sasa mwili wa marehemu umepelekwa hospitalini kwa uchunguzi zaidi” alinijibu polisi huyo. Akageuza kumputa yake na kuonesha na kunionesha picha



    za marehemu Joyce kisha akachukua zile nilizokuja nazo akaziscan na kuziingiza kwenye program moja ya kinteleginsia hivyo nikaona jinsi wanavyozifananisha.



    Teknolojia hii ilikuwa ya hali ya juu sana hivyo sikuwa na jinsi zaidi ya kukubaliana na ukweli ambao ulikuwa mbele yangu.



    Polisi alinambia kuwa nitaendelea kusaidia polisi lakini hawataniweka ndani kwa sababu reflection ya maoch inaonesha mtu wa mwisho kuwa naye alikuwa ni



    mzungu. Basi nilimpigia mama yake mdogo lakini alikuwa bado hapatikani. Nilimwandikia meseji kumuelezea kilichokuwa kinaendelea. Basi nilielekea huko



    hospitali ambapo mwili wa rafiki yangu ulikuwa umehifadhiwa. Tuliongozana na afande huyo ambaye alinipa taarifa na pia alikuwa akinifahamu sana kutona na

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    ile kesi yangu ya kipindi kile ambayo iliniweka ndani kwa mda mrefu sana. Cha ajabu na cha kushangaza sikuwa na namba za simu za ndugu wa Joyce hata



    mmoja zaidi ya mama yake mdogo.Nikamkumbuka yule mdogo wake lakini sikujua alikuwa wapi kwa wakati huo.



    Tulipokuwa hospitalini niliwasiliana na yule wakili aliyekuwa akinisaidia kwenye ile kazi yangu. Nilimueleza kinaga ubaga kitu kinachoendelea. Akanambia



    yupo Moshi na tukio hilo limemshtua sana hivyo ataacha shughuli zake zote na kuja hapo hospitalini ili aweze kunisaidia kwa sababu polisi sio wa kuamini sana



    wanaweza kubadilika na kukuweka ndani kwa madai kuwa wewe ni mtu wake wa karibu na lazima ungejua alikuwa na nani dakika chake kabla ya umauti



    kumkuta.



    Nilimwelewa sana wakili lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kuongozana tu na polisi na kwenda nao KCMC.Ndio wangeweza kuniweka ndani ila nilikuwa tayari kwa



    lolote nisingeweza kukimbia kwenye tukio la rafiki yangu Joyce, ukizingatia mimi na yeye tulishaamua kuishi maisha yetu ya



    bila ndugu wala nini. Mimi ndi yeye na yeye ndo mimi, wawili kama dunia yetu wenyewe. Madaktari nao walituambia kuwa mwili wa marehemu pia unahitajika



    kupasuliwa tumboni kwa uchunguzi zaidi. Hapo sasa sikuelewa kwa sababu maelezo ya awali yalisema kuwa aliuawa kwa kupigwa risasi sasa wana mpasua wa



    nini kwanni aliuwawa kwa sumu?

    Haya na maswali mengine magumu ilinibidi nimuulize yule mpelelezi. Na yeye alinijibu kwa kifupi haina shida wacha wafanye kazi yao na ni vizuri kumsubiri



    mkemia atasemaje ili tujirizishe zaidi. Polisi huyo alinambia kuwa kwa kuwa rafiki yake nimepatikana hivyo basi zoezi la upasuaji litafanyika kesho.



    Alinambia niende nikawape taarifa ndugu zake wafanye taratibu za mazishi kwa sababu mwili ukishapasuliwa unatakiwa uzikwe siku hiyo hiyo.Kauli hiyo ilizidi



    kunichanganya sana nisijue mwili wa Joyce utakwenda kuzikwa wapi.



    Sikutaka kupoteza mda nilikwenda moja kwa moja mpaka soko la ndizi mahali ambapo mama yake mdogo na marehemu Joyce alikuwa akifanyia kazi.Nikazidi



    kupagawa ila sikukata tamaa na kuchoka bali nilipanda gari mpaka majengo.Kwa bahati nzuri niimkuta akijiandaa kwenda kwenye sendoff.Hapo kimoyomoyo



    nilisema asante Mungu.Alivyoniona alishtukana sana na swali la kwanza aliniuliza mbona macho mekundu hivyo na tena yamevimba.



    Hapo akawa amenitonesha kidonda na machozi yakaanza kunitoka huku nikishindwa kuvumilia na kupiga ukunga wa kilio.Kilio hicho kiliwashitua mpaka



    majirani waakasogea ili kujua nini kilikuwa kimetokea.Kwa ufupi niliwaeleza kuwa Joyce hatukuwa naye tena duniani.Kauli hiyo ilimfanya mama mdogo na



    yeye ashindwe kuvumilia akaangua kilio. Mama mdogo huyo alilia sana na naweza sema kuwa alichanganyikiwa kwa sababu Joyce pia hakuwa na mahusiano



    mazuri na ndugu yake kwa sababu tangia mama yake mzazi afariki hakuwahi kwenda kwao hivyo hatukujua mwili utawekwa wapi.Ndugu pekee ambaye Joyce



    alikuwa akiwasiliana nae na kuelewana nae ni mdogo wake ambaye yupo mwanza.



    Huyu ni yule ambaye alizalishwa kipindi akiwa shule na mbaya zaidi mwanaume aliyempa mimba aliikataa.Kwa mujibu wa mama mdogo wake huyo na Joyce



    aliamua kurudi chuo mara baada ya mtoto wake kufariki. Sikubahatika kuliua hilo mapema ila niliumia pia kusikia mtoto aliyesasabisha yeye kuchukiwa na



    familia yake alifariki.Sijui familia yao ilikuaje kwa sababu Joyce alitengwa na familia huyo mdogo wake naye alitengwa na familia.Ilibidi nichukue namba za



    huyo mdogo wake na kumpa taarifa za msiba



    Baada ya hapo Nnilimwomba mama mdogo ajikaze na kuwatarifu ndugu wengine habari hizo za msiba.Tulisaidiana hivyo hivyo maana sio siri kila mmoja



    alikuwa na uchungu sana kutokana na mazingira ya kifo hicho. Habari zilizidi kusambaa kwa kasi na majirani walianza kukusanyika hapo kwa mama mdogo.



    Msiba ni msiba tu na ukitaka kujua binadamu wana roho mbaya ni pale tulipowasiliana na baba yake Joyce na kumpa taarifa za msiba.Jibu alilotoa kwa kweli



    lilikuwa ni la kukatisha tamaa kabisa. “ Alituambia tutafute pa kumzika kwa sababu yeye hamtambui kuwa ni mwanaye.



    Lakini baba zake wadogo wao walikuja juu mara baada ya kuelezwa habari za msiba na mazingira yaliyotokea. Wao walisisitiza kuwa wanakuja Moshi na



    watajua nini kifanyike mara baada ya wao kuwasili.Ikumbukwe jambo moja tu ndo lilikuwa linatuumiza kichwa ni kwamba msiba tutaupeleka Arusha au utabaki



    hapo Moshi kwa mama mdogo. Kuna baba mdogo mmoja yeye alitoa wazo kuwa tuwaombe polisi na madakatri kwamba wasimfanyie upasuaji watupe siku



    moja zaidi ili tuweze kujipanga kwa mazishi.



    Wazo hilo mimi binafsi nililinunua moja kwa moja kwa maana lilikuwa na mashiko. Kwa kuwa mda ulikuwa umeenda sana mama mdogo alivua sare ya send off



    na taratibu za mazishi zikawa zimeamishiwa hapo kwa mda.Jina la Joyce mtaani hapo alikuwa geni kwa sababu best yangu huyo alishawahi kukaa sana hapo na



    hiyo ni mara ya mama yake mzazi kufariki na yeye kugombana na baba yake.Historia inaonesha kuwa baba yao na kina Joyce alioa mwanamke mwingine mara



    baada ya mama yao kutoroka na masharti yalipozidi kuwa magumu Joyce na mdogo wake waliamua kuondoka nyumbani na kuja kuishi kwa mama yao mdogo.



    Hapa lazima tujifunze kitu kama wazazi kuna umuhimu wa kuweka misingi mizuri ya kifamilia lasivyo watoto watateseka sana pindi tu wazazi



    wtakapoitilafiana au punde tu mmoja wao atakapoiaga dunia.Ebu fikiria kauli kama hiyo eti baba yake hataki msiba upelekwe nyumbani kwa sababu yeye



    hamtambui kama ni mwanaye.Ukishazaa umezaa haijalishi nini kimetokea au kilishawahi kutokea damu yako ni damu yako tu.Hii iliniuma sana nikajikuta na



    mimi naujiuliza maswali hivi na mimi nikifa leo nitaenda kuzikwa wapi.Au nitazikwa kama mzoga usiokuwa na ndugu dini wala kabila.



    Sikuwa na majibu ya maswali hayo zaidi ya kububujikwa na machozi. Sikujua nini itakua hatima ya maisha yangu maana Joyce ndo alikuwa rafiki ndugu shoga



    na muhimili mkubwa sana katika maisha yangu.Hivyo kuondoka kwake duniani ni pengo kubwa zaidi hata ya kufiwa na wazazi.Siku ilisha hivyo na sikuweza



    hata kula siku hiyo japo nilikuwa sijala tangia asubuhi.Mama mdogo alinisihi sana nile lakini ilishindikana kwa sababu sikuona thamani ya chakula kwa wakati



    huo.



    Asubuhi na mapema baba zake wadogo walishafika na tukaanza kupanga taratibu za mazishi. Walitueleza wazi kuwa wamejaribu kuongea na kaka yao juu ya



    kupeleka msiba Arusha lakini amekataa katu katu hivyo basi ili kuepuka gharama walisema msiba uletwe hapo kwa mama yake mdogo. Mama yake mdogo



    alikubali lakini aliuliza huyo mtu atazikwa kwa imani gani?Hapo palikuwa pagumu kidogo kwa sababu mama yake mdogo Joyce alikuwa ni mlokole na Joyce

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    yeye alikuwa ni mpagani maana hakuna kanisa au msikiti aliokuwa akisali. Baba zake wadogo kwa kurahisisha mambo wakasema swala la imani sio tatizo kwa



    sababu sote ni wamoja na mungu ni huyo huyo yunayemwabudu na kumtumikia.



    Ingawa wao walichukulia kirahisi jambo hilo ila mimi binafsi nilijua kabisa jambo hilo lingeleta utata mkubwa..Mama mdogo saa hiyo hiyo akaondoka na



    kwenda kuongea na mchungaji ili aone kama anaweza kumsaidia kwa jambo hilo.Mchungaji wao naye alitia ngumu kweli kwa madai kuwa hawezi kumzika mtu



    ambaye sio muhumini na mshirika wao.Akasisitiza kuwa atafanya hivyo kama atapata kibali kutoka kwa mchungaji wa kanisa ambalo marehemu alikuwa akisali



    hapo alimaanisha Arusha. Mama mdogo ilibidi aniulize mimi “ hivi wewe na rafiki yako marehemu huko Arusha mlikuwa mkisali kanisa gani’? Nilimjibu kwa



    kifupi kuwa sisi ni zaidi ya wapagani kwani huko Arusha hatukujua mlango wa kanisa ulikuwa ukielekea wapi.



    Mambo yakazidi kuwa magumu sana na tulibaki tunaangaliana tu.Sikuona mantiki ya mchungaji kumfanyia ukatilii mama mdogo kwa sababu mimi niliamini



    kuwa ukimzika mtoto wa muhumiini wako ni sawa tu na kumzika yeye.Hapa na mimi nilijifunza kitu kingine katika maisha.Kuwa hizi dini nazo sio za



    kuzipuuza maana ukifa unaweza kuzikwa kama mzoga tu.Baba yake mdogo akatoa wazo kuwa kuna rafiki yake ambaye ni mchungaji hivyo anaweza kumwomba



    aje hata amsomee sala ya mwisho.Nia ilikuwa aje tu nyumbani amfanyie sala marehemu kisha tumalize swala hilo.Lakini cha ajabu majibu nayo kutoka kwa



    mchungaji rafiki yalikuwa ni hayo hayo ya kukatisha tamaa.Hapo nikajua dini nazo siku hizi ni shida.



    Mda ulizidi kuyoyoma na watu walizidi kukusanyika hapo na hii ni mara baada ya kupewa taarifa kuwa msiba utaletwa hapo.Baadaye yule mchungaji rafiki yake



    yule baba yake mdogo na marehemu alipiga simu na kusema ingawa utaratibu hauruhusu kufanya hivyo yaani kuzika mtu ambaye sio mshirika lakini kwa sababu



    matatizo yametokea na yeye binafsi amebahatika kusoma habari hiyo kwenye gazeti la visa na mikasa hivyo basi ameamua kukata shauri na atakuja kufanya ibada



    ya mwisho ya kumuaga marehemu.



    Taarifa hiyo ilikuwa ni zaidi ya faraja kwa sababu sikupenda au sio jambo zuri kwa mtu kuzikwa kipagani au kienyeji.Sio jambo jema kabisa mtu kuzikwa kama



    mzoga na hata kama alikuwa hasali bado sio kazi yetu kuhukumu hiyo ni kazi ya muumba mbingu na nchi.Hapo pia tulikuwa tukisubiri majibu ya polisi juu ya



    maombi yetu kuwa mwili usifanyiwe upasuaji siku hiyo hili kuruhusu ndugu wa marehemu waliokuwa mbali waweze kuhudhuria mazishi hayo.



    Nilimpigia tena afande na alinihakikishia kuwa ombi langu limekubaliwa ila tujiandae hela ya kulipia mwili wa marehemu kukaa mochwari. Sikuwa na cha



    kumpinga na hapo nikakumbuka kuwapigia wale wafanyakazi wake wa salooni na kuwapa taarifa za msiba.Niliwaambia wafunge saloon na waje Moshi kwenye



    msiba na pia watuletee hizo hela za siku mbili ili zitusaidie hapo msibani. Taarifa hizo ziliwashitu sana hao wadada na walinitupia lawama kwa nini sikuwambia



    tangia jana. Niliwajibu kwa kifupi kwamba hata mimi sikuwa kwenye hali nzuri cha msingi ni kwamba kwa sasa sio mda wa kulaumiana wao waje tu msibani.

    Mdogo wa marehemu kwa jina Marry naye alinipigia simu na kuniambia kuwa tayari alishapanda gari kutoka mwanza na kuja Moshi hivyo atawahi mazishi.



    Hapo pia nikamkumbuka Yule kipopa ambaye alizaa na Joyce ingawa walishaachana lakini niliona ni jambo jema kumpa taarifa kwani huyo ni mzazi



    mwenzie.Naye taarifa hizo zilimshitua sana akanambia atakuja kwenye mazishi na mwanaye ili aje amuage mama yake.Wazo hilo lilinishitua sana kwa sababu



    mtoto wao alikuwa bado ni mdogo sana ndo kwanza alikuwa Nursery school.Ilibidi nimpigie tena na kumwambia naomba hasije na mtoto kwa sababu atakuwa



    anamchanganya kisaikolojia.Na yeye alinijibu kwa kifupi kuwa ni wazo zuri kwa sababu hata yeye alifikiria hivyo kabla



    Basi tuliendelea na taratibu za mazishi na kesho ikafika marehemu akakamilishiwa taratibu zote za uchunguzi na sisi tukakabidhiwa mwili wa marehemu tayari



    kwa kuupumzisha kwenye nyumba ya milele. Basi mchungaji yule aliyejitolea kutufichia aibu alifika akamfanyia ibada ya maziko kisha tukampumzisha rafiki



    yangu Joyce kwenye chumba chenye giza chumba cha sita kwa sita chumba ambacho hakika kila mwanadamu atakipitia.Siku hiyo nililia sana mpaka machozi



    yalikauka na ilikuwa ni siku ya 3 sasa sijala kitu chochote zaidi ya maji na soda.

    Maziko yalifanyika saa saba mchana na tuliamua kuvunja matanga siku hiyo hiyo ili kuruhusu watu watawanyike na kuendelea na shughuli zao. Kwa kweli yule



    mwanaume aliyezaa na Joyce alitusaidia sana na alitoa hela nyingi sana.Watu walikula vizuri na kunywa vizuri kidogo ikanipa faraja kuwa safari ya mwisho ya



    Joyce ilikuwa ni ya matumaini. Lazima nimshukuru kwa sababu alituepusha na aibu ambayo ilikuwa itukute. Ilivyofika saa kumi na moja jioni watu walianza



    kutawanyika na hiyo ni mara baada ya MC kutangaza kuwa msiba ulikuwa umemalizika.

    Baadaye Yule mzazi mwenza na marehemu Joyce aliitisha kikao ambacho kilihudhuriwa na mimi, yeye, na ndugu wa marehemu.Yule baba alikuwa na busara



    sana kwani alianza kwa kusema “nimeona tufanye kikao hichi pamoja kwa sababu nikiwaacha wenyewe nazani mnaweza msielewane.Mimi nimezaa na ndugu



    yenu na siku zote nilikuwa sijui ndugu wa marehemu zaidi ya Leah.

    Lakini leo nimejifunza kitu na kugundua kumbe Leah hakuwa ndugu wa damu wa marehemu bali ni rafiki wa karibu.Aliendelea kuongea baba huyo kwa kusema



    “ Nilikutana na marehemu wiki mbili zilizopita na alinieleza siri kubwa ya maisha yake ambayo hakuna mtu yeyote anayeijua zaidi ya rafiki yake Leah.Hapo



    watu wote walinyanyua masikio juu ili kusikia ni nini mtu huyo anataka kutuambia. “Marehemu nilivyokutana naye wiki hizo mbili alinambia kuwa Leah ndo



    mrithi wa mali zake na ndio atakuwa mama na mlezi wa Lucky mtoto niliyezaa na marehemu.

    Hapo ndugu zote wa marehemu walimtolea mimacho na kumshangaa.Akaendelea kusema siri hii hata mama yake mdogo anaijua. Hapo baba mdogo mmoja wa



    marehemu akamkatiza kwa kumwambia ebu usimsemehe mama yake mdogo kwa sababu yupo hapa hivyo kama ana jambo lolote analijua kuhusu marehemu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    aseme mwenyewe.Mama mdogo akasimama na kusema “marehemu mwanangu wakati wa uhai wake alinieleza kuwa yeye ni muhathirika wa ukimwi na alikuwa



    akiishi kwa matumaini.Hapo kila mtu alifunga mdomo kwa sababu mama mdogo alipasua jipu na kukata mzizi wa fitina.Hivyo marehemu alinikabizi akaunti



    moja ambayo ni fixed deposited account na hiyo alimfungulia mwanaye Lucky.Na alisisitiza kuwa hata baba wa mtoto anatakiwa apewe namba za akaunti ili awe



    anamuwekea mwanaye akiba.

    Pia marehemu alinambia kuwa anamiliki saloon huko Arusha na endapo akifa mda wowote basi salooni hiyo itabaki mikononi mwa Leah ambaye ndio



    msimamizi na mama mlezi wa mwanaye.Mama mdogo hakuishia hapo aliendelea kwa kusema “ marehemu pia alinieleza kuwa ana miliki duka la vitu vya



    urembo wa kike ambalo pia Leah analisimamia ila hilo apewe mdogo wake Marry ambaye yupo hapa.Mama mdogo huyo mara baada ya kuyasema hayo alikaa



    zake chini.Baba mdogo ambaye hakurizika na maelezo hayo alisimama na kusema “ kwa hiyo kama marehemu alijua kuwa atakufa hivi karibuni kwani nini



    hakufuata taratibu za kisheria za kuandika wosia na kurithisha mali. Mimi binafsi sijarizika na maelezo ya mama mdomo labda kama kuna vielelezo vya



    maandishi alifafanua baba huyo ambaye alionekana ni mkorofi sana. Akaendelea kusema “ mali za marehemu zinatakiwa ziuzwe na sisi kama ndugu tunufaike



    nazo, kwanza mnafikiri haya madeni nani atalipa.

    Leah ilinibidi nisimame na kusema jamani maisha ya Joyce mimi nayafahamu hakuna mali yoyote ya maana aliyokuwa nayo zaidi ya hicho kisaloon kidogo na



    kiduka. Hicho kisaluni ni kwamba tupo share mimi na marehemu na hicho kiduka ndo cha kwake na ameshasema apewe mdogo wake.Akaunt ambayo ilikuwa na



    hela ndo hiyo amesema ni kwa ajili ya akiba ya mwanaye. Kwa hiyo mimi sioni kama kuna haja ya kuendelea na kikao maana hakuna cha kujadili tena nilisema



    kwa uchungu na kukaa chini.

    Baba mdogo mmoja alirizika lakini mmoja hakurizika kabisa na akasema sisi ni ndugu wa marehemu na tupo hapa kwa ajili ya kumwakilisha baba yake hivyo



    lazima mtoe maelezo ya kutosha lasivyo hatutakubali jasho la mwanetu lipotee bure.Hapo nilisimama kwa jazba na kutaka kuuliza walikuwa wapi wakati



    marehemu akiwa hai lakini nilibadilsha na kusema “ wewe unatakaje sasa maana maelezo ndo hayo, basi twendeni Arusha mkachukue nguo na vitu vya ndani



    maana ndio havijazungumziwa hapa. Hapo ilibidi mama mdogo asimaame na kujaribu kutuliza hali ya hewa ambayo ilishaanza kuharibika.

    Yaani huyu mzee alinichafua sana sasa sijui alikuwa anazitaka chupi na sidiria za mwanaye au vipi?Nikasema wachukue kila kitu basi maana hasara roho pesa



    makaratasi. Basi kikao kiliisha kwa staili hiyo mimi nilitoa maneno makali kwa sababu huwa sijui kumkopesha mtu.Ndio ebu fikiria watu hawakuwa na



    mchango wowote wakati marehemu akiwa hai sasa leo wanataka mali.Yaani sijui walikula maharage ya wapi hawa.Ilibidi kikao kiishe kwa staili hiyo. Mzazi



    mwenza wa marehemu Joyce aliaga na kuondoka zake.Na hao mababa wadogo pia waliaga na kuondoka zao.

    Nilitamani kuondoka na mimi usiku huo huo lakini niliona naweza kumkwaza mama mdogo.Tuliendelea kukaa hapo na kupeana faraja za hapa na pale huku



    mama mdogo akisisitiza kuwa tuachana na hao watu kwa sababu hawajui A to Z ya Joyce.Kwani kipindi kile anaumwa wewe ukimwangaikia hospitalini zaidi ya



    miezi mitatu wao walikuwa wapi.Aliendelea kuhoji mama na kunifariji kimtindo mtindo. Ila wakumbuke mimi na Joyce tumetoka mbali sana na tulikuwa



    tukiishi zaidi ya ndugu na ndio maana biashara zake zote mimi nilikuwa nazisimamia huku yeye akiendelea na mission town.

    Yule mdogo wake na marehemu ambaye mda wote alikuwa kimya aliamua kusema jambo “ ujue mimi nimekaa kimya mda mrefu kwa sababu bado nakumbuka



    mabaya yote waliotutendea hawa wanaojiita ndugu zetu kipindi kile nilipokuwa mjamzito” Cha msingi wewe dada Leah usiwe na wasiwasi wowote sisi



    tunaelewa milikuwa mkishi vipi wewe na dada Joyce. Aliendelea kueleeza mdogo wa marehemu. “Mimi binafsi sioni haja ya hilo duka la urembo labda uendelee



    kulisimamia na faida yake utakuwa unamtumia mama mdogo ili aongeze hata chumba kimoja hapa.Mimi kwa sasa siwezi kufanya biashara kwa kuwa nimeamua



    kurudi shuleni aliendela kufafanua binti huyo kwa jina Marry.

    Mimi sikuyaamini sana maneno hayo na kwa kuwa hawajui vibiashara vyenyewe mimi niliwambia cha msingi kesho wote yaani mimi , Marry na mama mdogo



    tuende Arusha wakazione hizo biashara na vitu ingine vya marehemu vinavyozungumziwa. “ya nini yote hayo mwanangu cha msingi wewe nenda ukaendelee na



    maisha naamini mimi ni mama yako na tushakuwa ndugu mda mrefu hivyo utakuwa unakuja kunitembelea tu mwanangu.Aliendelea kusisitiza mama huyo.Bado



    sikurizika nikamwambia hata kama yeye hatoendana Arusha lazima tuende na Marry akachuke vitu vya marehemu avilete huku.

    Kwanza naamini kwa mwili wa Marry hauna tofauti sana na mwili wa Joyce hivyo vitu vingi watakuwa wanavaliana.Marry alidakia akasema labda tuende tu



    nikapajue lakini kuhusu nguo za marehemu kamwe siwezi kuvaa na kwa kweli sina ujasiri huo alifafanua marry.Wewe naye bado hujaachaga imani za kizamani



    alimuuliza mama mdogo.Basi tuliendelea na stori za hapa na pale na kwa mara ya kwanza nilisikia njaa maana ilikuwa ni siku ya tatu sijala kitu cha



    maana.Nilimuomba yule dada wa kazi za nyumbani nitengenezee uji mwepesi ili ninyooshe utumbo kabla sijala kitu kizito.



    Nilitengezewa uji nikanywa na baadaye nilikuwa chakula vizuri nikashiba na kupanda kitandani kulala.Nililala kama mfu kutokana na uchovu na usingizi kama



    wa siku tatu hivi.Usiku nikiwa usingizini nilihisi kama tumbo lilikuwa likiniuma.Nilishituka kutoka usingizini na kutoka nje maana nilikuwa naendesha



    sana.Kwa kweli tumbo lilikuwa linauma sana mpaka nikahisi safari ya kumfuata Joyce ilikuwa imefika.Uvumilivu ulinishinda ikabidi niwaamshe wenyeji ii



    wanisaidie.Kadri mda uivyozidi kwenda ndivyo hivyo hali ilizidi kuwa mbaya nikawa najinyonganyonga kama nyoka aliyemwagiwa mafuta ya taa.Kila mtu



    akaingiwa na hofu ikabidi wanikimbize hosptali usiku huo huo.Walinipeleka Mawenzi hospitali na nilipofika nilipokelewa na manesi na wakaanza kuniwekea



    dripu za maji za kutosha.Kila mtu alibaki akishangaa asijue tatizo ni nini maana nilikuwa naugulia kwa kweli.Mimi binafsi nilihisi labda ni kwa sababu nilikuwa



    sijala mda mrefu.

    Usiku uliisha kwa staili hiyo hiyo na asubuhi palipokucha hali ilizidi kuwa mbaya.Daktari akaja na kuniambia nikachukue vipimo ikiwa ni pamoja na ultra



    sound. Hali ilizidi kuwa mbaya nikaanza kutapika damu na hata kabla majibu ya vipimo kutoka waliniandikia rufaa nipelekwe hospitali kubwa zaidi na



    nilipelekwa KCMC.Sikuweza kuelewa kinachoendelea zaidi ya kusikia milio ya ambulance ya gari ya wagonjwa ambalo nilipakiwa.Kila sekeunde moja



    ilivyopita ndivyo hali yangu ilivyozidi kuwa mbaya nikaanza kuona giza mbee yangu na uwezo wa kusikia ukapungua kabisa nikawa nasiki kwa mbali sana.

    Mara nikawa sisikii na kuona kitu tena.Nikajua tu ni giza la mauti lilikuwa limetanda mbele yangu.Hapo nikajua kabisa roho inakacha mwili nikaanza kusali sala

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    zangu za mwisho kimoyomoyo.Mara nikamuona Joyce akinipungia mkono na kuniambia mda wako bado wa kuja huku, utapona ili umlee mwanangu.Hapo



    nguvu zikaanza kunirudia na kuanza kusikia na kuona kila kitu kilichkuwa kinaendelea.Nikajaribu kujipima kwa kuinuka kitu ambacho kiliwashitua manesi



    ambao tayari walishajirizisha kuwa nilikuwa nimekata roho na hapo walikuwa wakiniingiza mochwari.

    Wote walitimua mbio na kusema hajafa hajafa kumbe bado ni mzima.Sikuelewa kwa nini walikuwa wakinipeleka mochwari badala la chumba cha wagonjwa



    mahututi (ICU). Nikahisi labda wamechanganyikiwa au mimi ndo nilikuwa ndotoni.Nikajaribu kujiangalia vizuri nikagunduwa nilikuwa nimezungushiwa shuka



    dizaini ya sanda.Nikainuka kwa nguvu na kuanza kutimua mbio kama vile mwendawazimu.Nilimpamia yule mtunza maiti akadondoka chini na mimi



    nikaendelea kutimua mbio kuelekea lango kuu la kuingia na kutokea hospitalini hapo.

    Nilienda moja kwa moja mpaka kwenye hice ambayo ndo ilikua inaondoka na kuenda mjini.Nilivyoingia tu kwenye gari hilo watu wote waliingiwa na hofu na



    kuanza kuteremka.Hapo nikajiuliza kwa nini wananikimbia na kabla sijapata jibu nilijitazama kwa kupitia kioo cha gari na kugundua nilikuwa natisha sana



    kwani nilikuwa nimewekewa pamba puani na masikioni kama zile wanazowekewaga marehemu.

    Nikazichimoa zile pamba kwa nguvu na kuanza kupikichapikicha pua zangu.Watu wote walikimbia sio dereva sio konda sio abiria nikabaki mimi mwenyewe



    kwenye gari. Kuona hivyo na mimi ilinibidi nishuke lakini wazo likanijia kwa nini nisiondoke na lile gari kwa sababu dereva alikua ameondoka na ameacha



    funguo. Nikashuka ili nizunguke na kuingia kwenye mlango wa dereva. Wakati nashuka watu wote hapo stendi walitimua mbio huku wakisema huyo huyo huyo



    anakuja. Nikawaona Marry, mama mdogo na manesi wote kwa pamoja wanakuja kwa kasi ili wanishike na kunirudisha hospitalini.

    Nikaona hawa watakuwa hawanipendi kabisa yaani walikubali nipelekwe mochwari nikiwa mzima kisa ni vile vimali vya ndugu yao Joyce.Nikasema kwa nguvu



    hapo mmeshachelewa mtajuata kunifahamu na mtajua kama mimi nilikuwaga mtoto wa kishua au wa kabwela.Mimi ni wa kishua bwana nilifundishwa



    kuendesha gari tangua nikiwa shule ya msingi. Sikuwapa nafasi ya kunishika maana niliona wamebeba na kamba kabisa kwa ajili ya kunifunga hivyo niliwasha



    gari na safari ya kwenda mjini ikaanza.



    Niliondoka kwa spidi kali sana zilizowafanya watu wote waliokuwepo hapo stendi ya viasi kushangaa. “Yaaani yule binti ana hatari sana na hasipopata ajali ni



    bahati yake au mikono ya mungu itakua juu yake, hayo yalikuwa ni baadhi wa maneno ya watu walioshuhudia tukio hilo.” Kwa kutumia kioo cha sitemillor



    nilifanikiwa kuwaona wakinifuata kwa kutumia magari na bodaboda. Dereva na konda wake ndo walionekana kuchanganyikiwa sana. Yaani kwa jinsi msafara wa



    magari uliokuwa ukinifuatalia ulivyokuwa mkubwa nilichanganyikiwa kwa kweli na badala ya kufuata njia ya mjini mimi nilifuata njia ya kwenda Kibosho



    Mweka.

    Wakati watu wakiniona kama niyechanganyikiwa vile mimi nilijiona nipo sawa a niliamini kuwa nitafika mjini kwa kutumia njia hiyo.Kwa bahati nzuri au



    mbaya barabara hiyo ilikuwa imejaa matrafiki ambao walikuwa wakisimamia msafara wa Muheshimiwa Raisi ambaye alikuwa akienda Chuo cha wanyamapori



    mweka alipoenda kama moja ya sehemu ya ziara zake mkoani Kilimanjaro. Kutokana na mwendo kasi niliokuwa nao nilijikuta nashindwa kusimama na



    kuwapita matrafiki ambao walikuwa wakizuia magari ili yapishe msafara wa muheshimiwa.

    Niligundua hatari ambayo ingenikuta mara baada ya kukaidi mikono ya matrafiki kuwa nipaki pembeni.Baada ya kuligundua hilo ilinibidi nichepuke pembeni na



    kuingia migombani.Lakini kuchepuka kwangu na kuingia mgombani haikumaanisha kuwa sheria ingeniacha hivi hivi.Ilifika mahali ikabidi nizime gari na kutulia



    tulii kusikilizia nini kitafuata.Tayari nilikuwa nimezungukwa na mapolisi ambao walikuwa wakinifuatilia kwa kutumia pikipiki.Kwa bahati nzuri dereva wa lile



    gari na yeye alishafika hapo na alishawaambia polisi kuwa mimi naugua ukichaa na nilifufuka kutoka mochwari.

    Kwa hiyo watu wote walozunguka gari walikuwa makini wakiogopa kunisogelea maana mtu kufufuka sio jambo la kawaida. Baada ya kugundua kuwa



    wananiogopa ilibidi nishuke mwenyewe na kuendelea kufanya vitu ambavyo nilijua kabisa wataamini kuwa mimi nilichanganyikiwa.Nikakumbuka mateso ya



    selo kipindi kile kwenye kesi ya mauaji ya Msouth hivyo nikaona bila kutumia mbinu lazima watanipeleka polisi.Niliinua mkono wangu mmoja juu na mguu



    mmoja kama vile nafanya mazoezi.

    Bado mbinu hiyo haikusaidia sana kwani kuna mmoja alinifuata a kunikamata akanIfunga pingu na kuniingiza kwenye gari.Nilikuwa mpole na nilishindwa



    kuelewa kama watanipelka tena hospitali au polisi. Lakini kwa vitu nilivyovifanya walikuwa hawana jinsi ilibidi wanipeleke tu hospitalini. Walinirudisha pale



    pale KCMC nilipokuwa mwanzo huku nikiwa chini ya ulinzi mkali utafikiri nimetaka kumuua raisi.Magazeti nayo yakapata kitu cha kuandika kuwa msafara wa



    Raisi waingia doa. Yapo yaliondika kuwa msichana mrembo afufuka na kutia doa msafara wa raisi. Yaani naweza sema nilipata umaarufu kwa mda mfupi sana



    kwani kila mtu alitaka kujua habari zangu mimi ni nani na ilikuaje mpaka nikapelekwa mochwari.



    Basi niliendelea kutibiwa mpaka nikapona na baada ya kupona kabisa nilifunguliwa shitaka la kuendesha gari mwendo kasi na kuvuruga msafara wa



    muheshimiwa raisi. Kesi iliendelea kuunguruma lakini baadaye kwa msaada wa yule wakili aliyenisaidia kipindi kile kesi hiyo ilifutwa kwa madai kuwa siku ya



    tukio nilikuwa nimechanganyikiwa.Madaktari nao waliaamua kunisaidia kwa kuandika taarifa kuwa nilikuwa naugua uchizi. Nilimshukuru Mungu kwa yote



    ambayo yalitokea na kuzidi kufanya kitabu cha kumbukumbu zangu kuwa kikubwa.



    Niliendelea na maisha yangu na nilirudi Arusha. Huko nako nilikuta mambo sio shwari ndugu wa marehemu Joyce walichachamaa kutaka ile salooni na kale



    kaduka wavichukue.Ili kuepusha shari nilikubali kuwaachia vyote na mimi nikaanza upya.Sikuwa na jinsi kwani kuanza upya sio ujinga na kama riziki yangu ipo

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    basi mungu atanijalia nitaipata.Nimepitia majaribu mengi sana hivyo hata hilo niliona kuwa ilikuwa ni muendelezo tu wa historia tata ya maisha yangu. Sikuona



    haja ya kugombania mali za marehemu maana ilikuwa ni kujitia mikosi tu.Ingawa tulikuwa share hiyo Salooni lakini nilimwachia mungu.



    Sikubaki na kitu chochote zaidi ya chumba ambacho tulikuwa tunakaa na Joyce. Niliwaza sana ni kwa vipi nitaweza kuishi Arusha mji wenye gharama kubwa za



    maisha hili hali sina kitu cha kuniingizia kipato.Hapa sasa nilikuwa sina namna zaidi ya kurudia yale maisha yangu ya zamani maisha ya kutegemea wanaume



    kwa kujiuza.Ni kazi ambayo marehemu Joyce alinisihi nisiifanyae kwa sababu mwisho wa siku lazima nitaangukia pua lakini sasa ningefanyaje.Ningepata wapi



    kodi ya kulipia hiyo nyumba.Ningekula nini na je vipi kuhusu mahitaji muhimu ya kike ningeyapata wapi.Ikumbukwe kipindi hicho sikuwa hata na boyfriend wa



    kunihudumia.Maisha niliyokuwa nikiishi pia yalisbabisha nisiwe na marafiki kabisa wa kike.



    Miasha yalibadilka na kuwa magumu na mabaya zaidi.Nikajikuta narudia uelvi na nilikuwa nakunywa pombe kupita kiasi ili kupunguza mawazo.Nilifikiria



    kujiua na siku moja nilichukua sumu ya panya tayari kwa kujimaliza. Usiku wa siku hiyo niliamaua kujimaliza mara baada ya kuona sina thamani yoyote hapa



    duniani.Nilisaga vizuri ile sumu tayari kwa kuilamba.Wakati nasali sala yangu ya mwisho kumuomba mungu baba anisamehe kwa makosa yote niliyotenda



    pamoja na hilo ninalotaka kulitenda la kujitoa uhai nilisikia kama mlango umefunguliwa na mtua akaingia.Ilinibidi nifungue macho na kuangalia ni nani alikuwa



    ameingia.



    Sikuona kitu zaidi ya kusikia sauti yenye mwangwi ya marehmu baba yangu” Leah leahhhhhh leaahhhhhhhhh mwanaaaaanguuuuuuu mwananguuuuuu



    tafadhaliiiiiiii tafadhaliiiiiiiiiiiiiiiii sanaaa saaanaaaaaaaaa usijiueeeeeeeee kumbukaaaaaaaa baabaaaa aaaa yako nilikuachia chiaaaaaaaaa urithiiiiii



    thiiiiiiii.Nilitetemeka sana na nilijaribu kupikicha macho ili nione kama nilikuwa naota au ilikuwa laivu.Haikuwa ndoto ilikuwa ni kweli marehemu baba yangu



    alinitokea na kuniambia nisijiue kwa sababu aliniachia urithi wa madini. Chumba kilikuwa tulivu sana na mawazo ya kujiua yaliniishia.



    Nikawasha redio na kufungulia kwa sauti kubwa saana huku hofu ikiwa imenitawala sana.Nilioka nje na kuangalia huku na kule lakini hakukuwa na



    kitu.Taswira ya utajiri ikanijia na kuanza kujiona ni kama niliyezaliwa upya.Nilipanda kitandani na kulala huku nikimuomba mungu anisaidi kufikia hiyo sehemu



    ambayo madini yalihifadhiwa na marehemu baba yangu.



    Basi maisha ya matumaini yalianza mara baada ya kutokewa na mzuka wa marehemu baba yangu. Siku zikazidi kwenda huku nikiwa napendelea kwenda sehemu



    mbali mbali za starehe nikihamini kuwa huko naweza kupata marafiki wenye feza. Hali hiyo ikanifanya niwe nakutana na mapedeshee na waliojichanganya



    nilikuwa nikitembeaa nao kwa kweli.Nitafanyaje sasa maana ingekuwa labda kweteu ni kijiji ningerudi kwenda kushika jembe na kulima lakini nimezaliwa mjini



    nimekulia mjini na sijui kuhusu kitu kingine chochote zaidi ya kazi ya saloon ambayo na hiyo ndo imeporwa na ndugu wa marehemu yaani baba wadogo wa



    Joyce.



    Sikujibweteka niliendelea kutafuta hela ili nifungue saloon yangu kwa sababu tayari nilishakuwa na uzoefu wa kazi hiyo. Katika harakati hizo ndipo nilipopata



    nafasi ya kushiriki shindano la miss bonge ambalo lilihusisha wanawake wenye maumbile makubwa hasa makalio.Nilijaza form ya kushiriki mara baada ya



    kusikia utaratibu ambao ulikuwa ukirushwa kwenye redio ya hapo hapo Arusha inaitwa Triple A. Nilivutiwa na dau neneo la shilini milioni mbili ambalo



    lilikuwa litolewe kama zawadi kwa mshindi wa kwanza. Nilijiamini kabisa nitashinda shindano hilo kutokana na uzuri wa umbo langu la kibantu. Siku ikafika



    na shindano likanza huku tukiwa tumevalia mavazi ambayo yalikuwa yakituchora na kuonesha jinsi maungo yetu ya mwili yalivyokuwa.Ni uzalishaji tu sema



    utafanyaje sasa na ndo ilikuwa ni mwanya wa kuapta hela kiurahisi.



    Tofauti na wasichana wengine siku hiyo mimi nilishangiliwa sana kwa sababu nilikuwa ni miongoni mwa wasichana wachache ambao walikuwa hawana



    vitambi.Ndio wengi waliojitokeza walikuwa na makalio makubwa lakini pia walikuwa na matumbo makumbwa au naweza kusema ni vitambi.Mimi nilionekana



    mwenye umbo namba nane lenye kuvutia zaidi ya wote walioshiriki shindano lile. Sio majaji sio mashabiki wote waliaamini kuwa mimi nilistahili kushinda



    shindano lile. Shindano hilo lilikuwa na wazamini wengi sana walowezesha kupatikana kwa burudani mbali mbali zilizowafurahisha watu.



    Wakati burudani zikienelea majaji walipiga kura zao zilizowezesha mimi kutangazwa mshindi.Siku hiyo hakukuwa na cha maana sana zaidi ya kujipitisha



    nyukwaani na kuonesha jinsi gani umejaliwa na mungu kwa kuwa na inye na maungo mengine ya mwili makubwa.Sikuamini kama ningeweza kutangazwa



    mshindi wa shindano lile kirahisi vile. Nikapewa cheque ya shilingi milioni mbili na zawadi nyingine kama vile simu ya mtandao ambao ulidhamini shindano



    hilo.



    Shindano hilo likanirudisha kwenye ulimwengu wa umaarufu kwa sababu tangia siku hiyo wanaume wengi wakawa wananisumbua kila mmoja akitaka



    kujiweka. Yaani jamani mwenzenu sijui nilikuwa na nyota gani maana naweza sema ilikuwa ni nyota mbaya ya kupendwa na waume za watu. Maisha yaliendelea



    huku mawazo yangu yote yakiwa kule kwenye zile Tanzanite ambazo marehemu baba yangu aliniachia kama urithi. Tatizo ambalo lilikuwa likinisumbua Leaha



    mimi ni kwamba nilipewa jina la kijiji ambako madini hayo yapo lakini sikujua ni sehemu gani hasa yapo.



    Ikumbukwe nilishajaribu kwenda sehemu hiyo mara kibao bila mafanikio. Kwa hiyo wazo langu la kurudi kuishi Moshi liliongezeka mara baada ya kuzipata zile



    milioni mbili. Kwangu ilikuwa ni lazima niishi Moshi ili nifanikishe ndoto yangu ya kuwa tajiri mkubwa sana. Nilifanikiwa kurudi zangu Moshi nikaanza



    maisha mapya huku nikiwa na wazo la kufungua salooni yangu ya kike.



    Lakini hela hile nilishaitumia katika kulipa kodi na mambo mengine madogo madogo ili kufaniksha kupata makazi mazuri maana sikuona haja ya kuishi maisha



    mabaya hili hali hakuna uhakika wa kuishi miaka mingi.Ilinilazimu kuanza kufanya kazi kwenye salooni za watu lengo ikiwa ni kuonsesha ujuzi wangu, kutafuta



    jina na wateja na pia kutafuta hela ya kuongezea nifungue salooni yangu





    Nilifanya kazi kwa bidii sana jambo ambalo liliniwezesha kupata jina na kuwa maarufu katika fani hiyo ya urembo. Ujue kule Arusha baada ya kutoka rumande



    Joyce alinipelaka kozi ya Hair dressing and beauty. Umaarufu huo uliniongezea wateja na kujikuta nafanya kazi masaa mengi sana.Wakati naendelea kudunduliza

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    dunduliza likatokea tena shindano lingine la mwanamke nyonga au almaarufu kama inyegwedegwede Kwa mnavyojua tena wanawake wa salooni ndo



    tunaongoza kwa kupata habari za mjini hivyo basi wapambe wangu walinishauri nishiriki shindano hilo.

    Tofauti na lile shindano lilofanyika kule Arusha ili lilikuwa ni shindano la kukata mauno.Yaani ingekuwa ni miaka ya 2015 ningeweza kusema lilikuwa shindano



    la kucheza ule wimbo wa chekecha cheketua wa Ali Kiba au ule wa nasema nawe wa diamond. Kama kawida sikulaza damu nilijisajili na kuchukua form za



    shindano hilo na kuzijaza. Na kwa kuwa shindano hilo lilikuwa linahusu kuonesha mauno hivyo nilianza mazoezi ya kucheza musiki hasa ya mwambao kama



    baikoko, taarabu , kigodoro na mingineyo. Kwa kweli naweza kusema kucheza miziki hii kwangu haikuwa kazi ngumu kwa sababu nilishaanza kuicheza tangia



    nikiwa mdogo. Siunakumbuka nilishawahi kushinda kashindano kama hako kule club siku ya kwanza kabisa nilipoenda Club nikiwa na mwalimu John.

    Nilitafuta CD zilizoonesha watu mbali mbali wakicheza nyimbo hizo.Mbali pia na kuwa na hizo CV pia nilikuwa najitaidi kubuni staili zangu mwenyewe



    ambazo niliamini kuwa zinaweza kumpagawisha mtu yeyote.Nilikuwa nachanganya staili za kijamaika na hizi za kwetu, sikuacha pia zile za Nigeria hapo



    nikapata vitu vyangu vya tofauti kabisa.Basi baada ya kujihakikishia kuwa nipofiti kwa mastahili yangu hayo nilisubiri siku ya shindano ifike nikafanye



    yangu.Siku ya shindano ilifika na mimi nilikuwa miongoni mwa washiriki walioingia tatu bora.



    Basi ilivyofika zamu yangu ya kufanya vitu vyangu nilipanda jukwaani huku nikiwa nimevalia kivazi ambacho kilitosha kabisa kunipa ushindi kwani ukumbi



    wote ulizizima kwa makelee ya kunishangilia.Nilivyovyaa kwa kweli ilitosha kuwachengua mashabiki ambao wengi walikuwa ni wanaume tena wenye uchu wa



    mambo hayo ya kukata mauno.Sikutaka kupoteza mda nilianza kazi yangu kwa makeke ili hali nikijua kabisa watu wote waliokuwa wakinitizama walikuwa



    wanaumia roho kutokana na mvuto wa umbo langu niliokuwa nao.

    Nilisikia mijibaba miwili ikiulizana hivi lile wowoo ni la kwake au ni la mchina? Mmoja wao akaropoka “wee kitu original hicho, kwani umemsaahau huyu



    binti tulishakutana nae kule Arusha mpaka tukambatiza jina la soda kubwa tena ya fanta yaani BAMBUCHA.?” Yeah nimekumbuka alidakia mwanaume wa tatu



    waliokuwa nao.



    Akaongeza basi huyu tusimwite tena BAMBUCHA bali tumpe jina la bia kwani inaonesha thamani yake ni kubwa zaidi. Basi wote kwa pamoja wakacheka.



    Wakati nikiendelea kutingisha makalio yangu ambayo kiukweli yalikuwa yakitetemeka kama mawimbi ya bahari, yule aliyetoa hoja akapendekeza jina



    linalofanana na bia eti kutokana na uzuri niliokuwa nao aliniita HAINKEN WOWOWO.

    Ilinibidi nicheke kwa nguvu kitu ambacho kiliwashitua mashabiki wangu waliokuwa wakinifuatilia, hawakujua nilikuwa nikicheka nini wakajua labda



    nilifurahishwa na ule wimbo wa kanga ndembendembe laki si pesa. Wakati nikiendelea kuzungusha nyonga yangu kwa ufundi wa ajabu niliokuwa nao



    niliendelea kufuatilia mazunguzo ya wale watu waliokuwa wamekaa meza ya karibu na jukwaa. Niliendelea kuzungusha nyonga na kwa wale ambao ndo ilikuwa



    ni mara yao ya kwanza kuniona walishangaa sana.



    Lakini kwa wale ambao walishaniona kwenye shindano la miss bonge kule Arusha wasingeshangaa sana kwani kile ndo kipaji nilichojaliwa na mwenyezi



    Mungu.Nilizungusha kisawa sawa huku nikirembua macho yangu kitu ambacho siku zote kilikuwa nikiwaumiza wanaume wenye tamaa. Kwa ufundi wa ajabu



    nilio kuwa nao niliendelea kufuatilia wimbo niliowekewa huku nikilitegeza sikio langu moja kwenye ile meza iliyokuwa karibu yangu. Wale wanaume



    waliendelea kunitumbulia macho huku wakiendelea kubishana juu ya jina gani wangenibatiza kulingana na uzuri wangu.



    Nilibahatika kumsikia mmoja akimwita muhudumu kwa fujo na kumwambia “inaelekea wewe hujui majukumu yako, mbona bia imeisha na umekaa mbali?



    Dada kwa heshima kubwa na kutambua kuwa walikuwa wameanza kulewa alimjibu kwa kumwambia samahani kaka” Sitaki samhani yako niletee bia



    inayofanana na huyo dada kwenye jukwaa. Yule muhudumu alibaki ameduwaa asijue nini cha kufanya. Akauliza jamani kaka mbona sikuelewi nikuletee kinywaji



    gani? Kaka kwa ukali akamwambia kinachofanana na huyo dada.



    Muhudumu akaenda kaunta na alipokuja alikuja na soda kubwa iliyojazia yaani BAMBUCHA. Watu wote kwenye meza yao walishangaa yaani mtu alikuwa



    anakunywa bia na sasa ameletewa Bambucha. Ili bidi wapigwe na butwaa, yule jamaa akamuuliza yule muhudumu kwanini umeleta hii soda? Muhudumu kwa



    kujiamini alisema ‘Ni kwa sababu huyo dada anaitwa BAMBUCHA.Basi watu wote pale mezani waliangua kicheko.



    Basi kwa kuwa kila mtu alipewa nyimbo tatu kuonesha maujuzi ya kuzungusha nyonga na kuchezesha makalio, hivyo mimi niliwekewa wimbo wangu wa



    mwisho. Huku nikibadilisha staili na kucheza ile matata ya kulala chini kisha kuzungusha kama vile upo juu ya mwanaume. Nilimsikia yule mteja akimwambia



    muhudumu niletee HAINKEN WOWOWO na wakati Yule dada akitafakari Heinken wowowo ni ipi, kwa macho yangu ya wizi nilimwona yule kaka akifungua



    pochi yake na kutoa hela na kila kwenye noti ya elfu kumi alikuwa akiandika kitu.



    Sikujua alikuwa akiaandika nini nitakwambia nikishuka jukwaani. Basi nikaamua kuendelea kufanya yangu na nilikuwa namalizia na ile staili ya mdembwedo.



    Hii staili ni mbaya sana kwani unakuwa kama unajizalilisha, hapa wapambe wangu walinimwagia maji kwenye makalio hivyo kuwa ndembendembe. Nilitumia



    vizuri vidole vyangu kuviingiza sehemu ambazo kwa kweli naogopa kusema. Yule kaka akashindwa kuvumilia akanifuata na kunimwagia zile noti za elfu kumi



    kumi.



    Sikujua alinipa shiling ngapi kwa kuwa haikuwa kazi yangu kuokota hela ila kwa utundu wangu niliivuta moja kwa kutumia vidole vya miguu yangu. Nilifanya



    hivyo kwa sababu mara nyingine huwa tunazulumiwa na pia nilitaka kujua yule kaka aliandika nini kwenye zile hela.Mda wa mimi kuendelea kukaa jukwaani



    ulimaliika basi nikashuka chini huku mashabiki wakinipigia mayowe na makelele ya shangwe



    Nilikwenda moja kwa moja kwenye chumba cha kubadilishia nguo na wasiriki wengine waliendelea kufanya mambo yao.Baadaae washiriki wote walimalizika



    na mda wa kutangaza mshindi ulifika. Nakulikuwa hakuna haja ya kupepesa macho mimi nilitangzwa mshindi jambo ambalo lilifanya ukumbi uzizime kwa



    kuraha.Ikabidi mashabiki waniombe nicheze wimbo mmoja ambao ungewafurahisha nakusindikiza ushindi wangu.Kinyume na walivyotarajia mimi sikuwekewa



    tena wimbo wa taarabu bali niliwekewa wimbo wa kinaigeria nakuanza kufanya vitu vyangu.Maneno ya wimbo ule ndo huwa unanipa maksi sana “ baby pull



    over, show me your particular, revese, back, right. Left and front” Hapo sasa mimi kweli nikawa naonesha vitu vyangu vya mbelee, nyuma kushoto na kulia ili

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    mradi kumtukuza mungu kwa kazi nzuri ya uumbaji.Kweli mungu alinipa kipaji maana staili yangu yauchezaji iliwafanya watu kufungua pochi zao na kuja



    kunitunza.Nlipata hela nyingi sana ambazo hata mimi mwenyewe sikuzitarajia. Tamasha likaisha kihivyo na kila mtu akaendlelea na ratiba zake.Leah alipewa



    hela zake zote alizotunzwa pale jukwaani akaendelea na furaha ya yake ya kushangilia ushindi.Kabla sijaondoka nikakumbuka zile noti za kwanza ambazo



    nilipewa na yule kaka ambaye alinibatiza jina la Heinken wowoo badala ya Bambucha. Kweli kuna watu wana akili huku duniani kwa sababu zile noti



    ziliandikwa namba za simu.Niliziangalia zile noti nikatabasanmu na kujisemea kweli wanaume wana mbinu nyingi sana duniani. Basi mara baada ya kuhakikisha



    kuwa zile hela zangu na cheque niliyopata ipo sehemu salama niliamua kumtafuta yule kaka.Nilichukua simu yangu na kumpigia simu yake iliita mpaka ikakata



    bila kupokelewa.Nikaamua kumtumia ujumbe mfupi wa maneno “mshindi wa mwanamke nyonga hapa” Yule jamaa mbona alipiga simu mwenyewe na swali la



    kwanza aliloniuliza ni kuwa nipo wapi.Ilibidi nimjibu kuwa nipo nyumbani.Yule kaka ambaye mimi nilikuwa namjua kabisa kuwa ni star wa bongo movie



    aliniuliza kuwa eti tunaweza onana usiku huo kwa sababu kesho anaondoka alafu alikuwa na jambo la muhimu sana kuhusu maisha yangu.Yaani kusikia jambo



    muhimu kuhusu maisha yangu kwa kweli nilichanganyikiwa. Ilibidi nimjibu kinyonge sasa tuataonana wapi usiku huu. Basi Yule mkaka akanambia kuwa



    wanaelekea club na kama sitojali niungane nao kwa kuwa anaamini kuwa huko tutapata mda wa kuongea zaidi.Kwa kuwa mimi nilitambua ustaa wa kaka yule



    nikaona hakuna haja ya kulaza damu huwezi jua labda anataka kuniingiza kwenye tasnia ya filamu. Nilimuhadi kuwa nitafika maeneo hayo tuliyokubaliana mda



    mfupi baadaye.Kwa kuwa nilikuwa na hela nikaona isiwe tabu ngoja niende zangu home nikaweke hela kisha nivaee nguo za club nikale raha mie mtoto wa



    watu.Nilichukua tax kwa kiburi ya hela zile za kutunzwa.Uzuri safari hii nilikuwa naishi katikati ya mji.Mimi jamani napenda sana mziki kwa sababu ndo



    ilikuwa ni starehe yangu ninayoipenda hivyo msinishangae kabisa mimi kukubali kwenda club kirahisi hivyo. Nilijipara kisha nikaondoka zangu na kwenda eneo



    la tukio na nilivyofika bado sikutaka kutumia hela yangu kulipa kiingilio.Basi nilimwandikia sms na kumuueleza kuwa nilishafika eneo la tukio.Sikuwa mbali



    sana na fikra zangu kwa maana baada ya dakika mbili tu mwanaume huyo alitoka na kuja nje mahali ambako nilikuwa nimesimama.Hakutaka kupoteza mda



    akanilipia kiingilio kisha tukaingia ndani.Tulipitia kaunta na akanambia nichkue kinywaji ninachopenda. Tulikwenda pembeni mafichoni kidogo sehemu ambayo



    tungeweza kuongea bila kuwakera wengine. Tulikaa sehemu ambayo sauti ya mziki ilikuwa sio kubwa ili tuweze kuongea.Naitwa Mark alianza kwa



    kujitambulisha staa huyo wa filamu hapa nchini.Na mimi nikamwambia naitwa Leah japo wengine wananifahamu kwa jina la Bambucha. Hatukuweza kuongea



    sana kwani kampani ya Mark ilisogea karibu yetu hivyo tukawa wengi na stori zikabadilka na kuanza kupiga storiza club na mziki. Na kwa bahati nzuri wanaume



    hao wote walikuwa na mademu zao kwa hiyo aliyefurahishwa na mziki aliamka na kwenda kucheza. Na wengine walicheza palepale pembeni ya meza.Mark nae



    hakujivunga alinipa mkono na kwenda kusasambua. Kama kawida yangu ikija swala la kucheza mziki basi ndo ujue kuwa umenifikisha mahali pake. Sikujivunga



    kwa kweli nilionesha yale maujuzi yangu na hivyo nikawa kivutio cha watu waliofika eneo hilo. Ilifika wakati watu wote waliacha kucheza na kunitazama mimi



    nikifanya vitu vyangu. Mambo yaliendelea na Dj uzalendo ulimshinda ikabidi atoe tu zawadi.Sikushangaa kwa sababu haikuwa mara yangu ya kwanza



    kupewakuponi ya kuingia bure club mara baada ya kutawala stage



    Baadaye mda ulienda sana na nilikuwa nimechoka sana hivyo nilimuaga Mark kuwa nahitaji kuondoka na kwenda kupumzika.Cha ajabu Mark alikata kuwa



    nisondoke na aliniomba tuende kulala nae kwa sababu alikuwa bado hajaniambia kitu ambacho yeye alitaka kuniambia na pia isitoshe yeye kesho anaondoka na



    kwenda Nairobi kwa ajili ya kazi zao hizo za filamu. Aliniweka njia panda kwa kweli kwa sababu ndo ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kukutana na mwanaume



    huyo kivipi nitamwamini na kuenda kulala nae.Nilimueleza ukweli kuwa hiyo ndo siku yetu ya kwanza kukutana sasa ni kwa vipi tunaweza aminiana na kwenda



    kulala wote. Pamoja na vikwazo vyote hivyo bado Mark alisisitiza kuwa kuna jambo la muhimu anataka kuongea na mimi.Hapo nikakumbuka kuwa zile zana



    zangu za kazi nilikuwa nazo ni vile vifaaa vya kupimia ukimwi ambavyo huwa navitumia kabla ya kukutana na mwanaume yeyote nisiyemfahamu.Nikaamua



    kumkubalia huku nikiamini kuwa hiyo ndo kinga yangu pekee iliyobaki kama mwanaume huyo atataka kuzini na mimi usiku huo. Basi tuliondoka na kwenda



    sehemu ambayo mwanaume huyo alikuwa amefikia .Kwa bahati mbaya au nzuri Mark alinipeleka kwenye hile hotel ambayo huwainanikumbusha mambo mengi



    sana hasa mwanume wangu wa kwanza yaani mwalimu John. Yaani sijui kwa nini hoteli hii nilikuwa nikiletwa mara kwa mara na cha ajabu Mark alikuwa



    amekodi chumba namba 10 chumba ambacho pia mwalimu John alikuwa akikipenda sana.Kama kawaida yangu tulipoingia tu chumbani mimi nilikimbilia



    bafuni na mbaya zaidi niliingia na pochi yangu kitu ambacho kilimshangaza Mark. Nilijisafisha vizuri kisha nikava ile kondomu ya kike. Baada ya kuhakisha



    nimevaa kinga vizuri nikachukua kile kipimo cha ukimwi na kukiweka juu kabisaya pochi. Nilitoka huko mawaliwatoni na kumkuta mkaka huyo amewasha



    laptop yake akissoma emaili zake.Basi na yeye akatumia nafasi hiyo kwenda kuoga. Aliniwekea clips za vichekesho na kuniacha nikiendelea kuburudika.Yaani



    japo nilikuwa nimechoka lakini mara baada ya kumuona Erick Omond mchekeshaji maaarufu kutoka nchini Kenya uchovu wote uliisha. Mimi jamani ni



    miongoni mwa Watanzania wachache ambao walikuwa wakimfuatilia sana mchekeshaji huyo hasa kutokana na tabia yake ya kurudia rudia nyimbo za msanii

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    maarufu Tanzania yaani Diamond Platunzmz.Yaani huyu mchekeshaji ni kiboko ule wimbo wa nasema nawe eti yeye kaubadilisha na kuwa nabeba mawe.Basi



    Mark alirudi na kupanda kitandani na tofauti na mimi nilivyofikiria kuwa mwanaume huyo atakuwa na papara sana kutokana na tabia yake ya uchu aliyoionesha



    tulipokuwa kule kwenye shindano la mwanamke nyonga.





    Mark alianza kujitambulisha upya kuwa yeye ni mwandaaji na mcheza filamu. Filamu maarufu ambayo ilimwingiza na kumfanya awe maarufu kwenye tasnia



    hiyo ni ile filamu ya MY WIFE TO BE.Mark alinieleza kinaga ubaga kuwa amevutiwa sana na mimi na anataka kunioa. Hapo mimi ilinibidi nicheke kwa sababu



    sikuwahi kuwaza kuolewa hivi karibuni. Alafu pia mtu tumekuatana leo alafu anatangaza nia ya kunioa jamani si masihara haya. Mimi kwa kweli sikuwahi



    kuwaza kuolewa nilichokuwa nikiwaza ni jinsi gani nitafanya ili kukamilisha ndoto yangu ya kuboresha maisha yangu kupitia yale madini. Niliendelea



    kumsikiliza Mark huku akiongea kwa utulivu sana huku akionesha kama mtu anyemaanisha kitu anacho kiongea. Alinambia kuwa anataka kuniingiza kwenye



    tasnia ya filamu.Ilibidi nimuulize kwani anavyoniona mimi naweza kuwa na kipaji cha kuiigiza?

    Yeah kwa jinsi ninavyokuona una vipaji vingi sana na kama utapewa nafasi ya kupata mafunzo kidogo unaweza kuwa bonge la superstar alisema Mark kwa



    kujiamini. Ilibidi nimshushue kwa kumwambia sikiliza Mark uzuri wa umbo na sura sio kigezo cha kucheza filamu. Mark akacheka na kuniambia mimi sijasema



    uzuri wako ndo utakuingiza kwenye filamu ila nimegundua kuwa unavipaji vingi kama unaweza kucheza na mashabiki jukwaani basi hutoshindwa kucheza na



    kamera wakati wa kushuuuti filamu. Basi nilimuambia hilo la kuingia kwenye filamu sawa ila hilo la kunioa hapana.

    Tatizo nini kwani hujajipanga kuolewa au hautaolewa maishani mwako aliuliza Mark kwa upole. Ujue Mark mimi na historia nyingi sana ambayo kama



    nikukueleza kamwe hutoweza kukaa karibu yangu. Historia yangu ni ndefu sana na bado inaendelea na hata mimi kukutana na wewe sehemu kama zile sio kwa



    sababu nilipenda kushiriki mashindano kama yale basi tu ni hali ya maisha.Pia historia yangu bado haijakamilika labda mpaka hapo nitakapo pata madini



    aliyoniachia marehemu baba yangu kama urithi wangu.Najua historia yangu haitakusitua sana kwa sababu ni mambo yanayotokea duniani lakini historia yangu



    ya uhusiano na mapenzi ni ngumu sana.

    Kwa kifupi kaka yangu kwa sasa hutoniweza kwa sababu nishazoea starehe, yaani mimi sio mwanamke ambaye unaweza niweka ndani nikawa mkeo. Yaani sijui



    kama eti nitaweza kumtunza mwanamme kumfulia kumpikia na mambo mengine muhimu.Ilibidi nimwekee vikwazo ingawa nilijua kama nitapata mwanaume



    atakayenipenda na kunijali ningeweza kubadilka na kuwa kama wanawake wengine.Mark alikuwa akinisikiliza kwa umakini sana huku akitingisha kichwa



    kuonesha huenda mimi sijielewi.

    “Ujue sisi ni watu wazima kwa hiyo sioni kama kuna haja ya kujadili historia zetu kwa sababu ni vitu ambavyo vilishatokea na vilitokea kwa sababu na bila



    hivyo pengine mimi na wewe tusingeweza kukutana alisema Mark.Kwa hiyo nitakuwa ni mwanaume wa ajabu sana kama historia yako ya mapenzi itakuwa



    kikwazo cha mimi kuwa na wewe. Kwa kifupi naweza kusema sihitaji kuijua historia yako ya mapenzi kwa sababu hata mimi ya kwangu sio nzuri aliendelea



    kufafanua Mark.Kauli hiyo sihitaji kujua historia yako kwa kuwa hata ya kwangu sio nzuri ilinifurahisha sana.

    Ikabidi nimuulize kwani historia yake ya uhusiano na mapenzi kwa kifupi ipoje.? Marka akajibu kuwa eti historia yake ni ndefu sana pengine kuliko ya kwangu



    ila kwa kifupi kwa sasa anataka kuanza upya na kuwa na familia.Nikabidi nitumie ladies power nikamwambia niambie basi hata kidogo babee.Bado alisita hapo



    nikaamua kumsogelea zaidi na kumuekea kichwa change kifuani mwake.Basi Mark akaanza kunisimulia “ ujue nilikuwa nikifikiria kuwa ukitaka kuoa



    mwanamke ambaye hatokusumbua basi ni lazima uende kuoa kijijini. Basi mimi nilifanya hivyo kwa kwenda kijijini na kuoa binti ambaye alikuwa ni mshamba



    kabisa.Nikamtoa kijini na kumelta jijini ambapo tulianza maisha.

    Na kwa kuwa alikuwa ameishia form four basi mimi niliamua kumtafutia chuo ili ajiendeleze.Na kwa kuwa alikuwa akipendelea sana mambo ya utalii basi



    nilimpeleka pale chuo cha utalii cha taifa.Basi maisha yakaendelea na kutokana na maji ya chumvi ya Dar basi uzuri wake ukaanza kuonekana.Mtoto akang’aa na



    kuwa kivutio cha wanaume wengi. Siunajua tena rangi nyeupe jinsi zinavyokuwaga hasa zikipata matunzo.Baadaye akalijua jiji na hata mavazi yake yakaanza



    kubadilika. Baadaye akaanza kubadilika na tabia akawa haoni tena thamani yangu kwake. Mbaya zaidi walikuja wazungu hapo shuleni kwao na yeye akawa



    miongoni mwa wanafunzi walifaziliwa kwenda kusoma nje ya nchi.

    Nilitumia nguvu zangu zote kumzuia asiende lakini ilishindikana.Na alianza kunichukia kwa madai kuwa mimi sipendi maendeleo yake.Nikaona isiwe tabu



    mwache tu aende akasome.Na mimi nilikuwa namzuia si kwa nia mbaya eti sipendi asome la hasha bali ni kwa sababu tayari alikuwa na ujauzito wangu



    aliendelea kufafanua Mark.Nilitega masikio vizuri maana nilihisi stori imekuwa tamu huku nijisemea hapa asije akaikatisha na kusema Iitaendela kesho.

    Basi binti huyo akaondoka huku akiwa na kihoro cha kwenda kusoma ulaya aliendelea kusimulia Mark.Basi akiwa ulaya tuliendelea kuwasiliana kwa kutumia



    mitandao ya kijamii hasa ule wa Skype. Siku zilizidi kuyoyoma huku nikiamini kuwa mimba yake iliendelea kukua na itakapofikisha miezi 8 atarudi nchini ili aje



    ajifungulie huku. Mbaya zaidi ilipofika hiyo miezi bado hakurudi na aka niblock kwenye mitandao yote ambayo tulikuwa tunatumia kuwasiliana naye.Akafunga



    akaunt zake za zamani kuanzia WhatsApp, facebook, twiter, instagram, tango, na skype.

    Sikujua nini kimemsibu lakini kila siku iendayo kwa mungu niliendelea kutumia juhudi zangu zote kuhakikisha nampata hewani.Mwaka mzima ulipiata bila



    mawasiliano na mimi nikawa nimekataa tamaa kabisa na haya maisha.Siku moja nikiwa zangu jengo la kitega uchumi nilimuona mtu kama yeye akiingia



    supermarket.Kwa sababu nilikuwa location tukishuti filamu nilishindwa kumfuata ila alikuwa na rafiki yake kipenzi.Hivyo niliamua kumpigia Yule rafiki yake

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    na nilipomuuliza kuwa yupo wapi akanambia yupo jengo la kitega uchumi. Hapo nilikuwa sina haja tena ya kutafuta ushaidi niliendelea na kazi ambayo



    ilinipeleka pale. Niliamua kumpotezea kwa sababu nilijua nikifanya makosa tu nitaharibu kwa sababu hiyo sehemu tulipewa kwa mbinde sana na tulipewa kwa



    mda mfupi sana.

    Hivyo niliona kuwa ni bora niendelee kufanya kazi na baada ya hapo ningemtafuta na kwa kuwa nilikuwa na namba ya huyoo rafiki yake sikuwa na hofu



    sana.Aliendelea kusimulia Mark stori iliyonifanya usingizi wote uniishe na kufuatilia kwa umakini ili niweze kujua nini ulikuwa mwisho wao. “Wewe naye una



    moyo mgumu sana yaani uone kitu chako tena cha ndoa ambacho mlikuwa hamjawasiliana mda mrefu ukiache hivi hivi nilimwambia kuonesha kuwa



    namsikiliza kwa umakini sana.



    Yeah nilikua sina jinsi kwa sababu kazi ndio msingi wa maisha na mimi ndo nilikuwa director pale kwenye ile movie. Kwa hiyo tuliendelea na kazi na



    tulifanikiwa kumaliza salana japo sikuweza kufanya ile kazi kwa ufanisi wangu wa siku zote. “Kwa hiyo nini kilitokea baada ya hapo ilibidi nimuulize swali



    mara baada ya kumuona ametulia tulii kama mtu aliyewaza kitu kingine wakati akisimulia”. Niliona macho yake yalikuwa yametua kwenye mapaja yangu



    ambayo kwa bahati mbaya khanga niliyojifunga ilikuwa imejiachia hivyo kufanya sehemu zile za mautamu kuonekana kidogo.

    Baada ya kuakamilisha ile kazi niliondoka na nilivyofika nyumbani nilimpigia simu yule rafiki yake na nikaomuomba tuonane siku iliyofuata.Kwa kuwa rafiki



    yake alikuwa ni mtu mwelewa sana peace and love alikubali na tukaonana siku iliyofuata.Nilitumia mda mwingi sana kumdadisi kuhusu rafiki yake na baaadye



    alikubali kuniambia ukweli. Biblia inaseam ijue kweli na kweli itakuweka huru hivyo ukweli huo hata mimi uliniweka huru. Nasema ukweli uliniweka huru



    kwa sababu nilijua mambo mengi ambayo nilikuwa siyafahamu na ambayo pengine yalikuwa ni fumbo kubwa sana kwangu aliendelea kusimulia Mark.

    Kwanza niliweza kugundua kuwa Yule mwanamke ile mimba aliitoa hata kabla hajapanda ndege jambo hili lilinifanya niumie sana na kupata uchungu ambao



    kwa kweli hauzungumziki alisema Mark.Hapo ilinibidi nimwambie jamani pole.Pili niliambiwa kuwa alipata bwana mzungu ambaye walifunga naye ndoa na



    sasa ana mimba yake.Tatu niliambiwa kuwa ndugu zake na wazazi wake walihusika kwenye mipango hiyo hivyo walibariki kabisa huyo binti kuniacha mimi



    mumewe wa ndoa na kuamua mtoto wao aolewe upya.Nne ni kwamba huyo mzungu amewaamishia wazazi wake mjini na amewajengea nyumba ya kifahari.

    Kwa hiyo mimi ninavyowapigiana simu na kuwajulia hali kumbe wenzangu huwa wananichora tu. Nakumbuka maneno hayo ya rafiki yake yaliniumiza sana na



    kujikuta nayachukia mapenzi na mbaya zaidi niliwachukia wanawake. Basi kusibitisha ukweli wa huyo rafiki yake niliamua kwenda hadi kwao kumwona. Na



    kwa bahati nzuri au mbaya siku hiyo yeye ndo alinifungulia mlango huku akiwa na tumbo kubwa la ujauzito. Roho iliniuma sana kwa sababu mimba yangu



    aliitoa na kuwa tayari kuibeba ya mtu mwingine. Jamani pole ilibidi nimuhurumie mara baada ya kuona anaangusha chozi.Kweli ukiona mwanaume analia basi



    ujue jambo hilo ni zito.

    Mark hakutoa sauti ya kilio lakini machozi yaliyomdondoka yalitosha kabisa kuelezea machungu aliyoyapata kutokana na tukio hilo la kikatili. Lakini



    namshukuru mungu alinifungua yote haya na kujua ukweli aliendelea kueleza Mark.Basi nguvu ziliniishia na nikadondoka chini na hiyo ni mara baada ya binti



    huyo kuniuliaza nikusaidie nini? Kabla sijamjibu kitu aliniuliza wewe ni nani. Kwa kifupi alinikana kunijua.Niliposhituka nilijikuta hospitali huku nikiwa



    nimezungukwa na baadhi ya marafiki zangu. Tuliweza kusaidiana katika hali ile na baadaye niliweza kuruhusiwa na kurudi nyumbani.

    Sikua na jinsi zaidi ya kukubaliana na ukweli huo japo ulikuwa unauma.Siku zilisonga mbele nikajikuta nimezoea hali ya kuishi upweke na sikuoa haja ya



    kupenda tena. Niliwachukia wanawake wote huku duniani kasorao mama yangu tu.Nikawa nikizini na mwanamke mmoja siwezi kurudiana naye hata kama



    ilinichukua mda sana kumpata.Hali hiyo ilinifanya nitembee na wanawake wengi sana ambao kwa kweli inatisha sana.

    Kuna kipindi niliumwa sana na nilikonda sana nikajua tayari ilikuwa ni ukimwi.Ilinichukua mda sana kabla ya kuamua kupima ugonjwa huo kwa lazima.



    Kilichokuwa kikiniogopesha ni demu ambaye nilizini naye mara ya mwisho kupimwa na kukutwa kuwa alikuwa ni muhathirika. Kwa kweli nilikonda sana kitu



    ambacho mimi mwenyewe kilikuwa kikinishtua sana.Nilijikuta nikikonda na kupungua uzito sana siku hadi siku. Nazani kitu kilichokuwa kikinisumbua ni yale



    mawazo mara baada ya kupata taarifa kuwa yule demu niliyetembea naye alikuwa na ngoma. Baadaye madakatari walinipima kwa nguvu na kwa bahati nzuri



    nilikutwa sina maambukizo ya ukimwi.Nilifanya hivyo tena mara 3 yaani kila mara baada ya miezi 3.

    Kwa hiyo kipindi hicho ndo kile magazeti ya udaku yalikuwa yakikuandika vibaya ilibidi nimuulizea.Maaana kaka huyo kuna kipindi magazeti ya udaku



    yalimuandama sana. Ndo kipindi hicho ambacho nilipitia majaribu sana siunajua tena usupa staa mzigo wa miba alijibu Mark. Basi tangia nipewe majibu kuwa



    nipo salama afya yangu ilizidi kuboreka na kurudi kuwa kama zamani.Tangia siku hiyo nikawa kama malaika nikawaheshimu na kuwaogopa wanawake wote



    huku duniani.

    Sikuwahi kuthubutu kulala na mwanamke na kufanya nae mapenzi zaidi ya kuchombeza tu kama vile nilivyokufanyia wewe ulipokuwa pale jukwaani.Kufikia



    hapo usingizi ulikuwa umenishika sana na sikuwa na uwezo wa kuendelea kumsikiliza tena. Nazani Mark aliligundua hilo mara baada ya kuona siitikii wala



    kuuliza maswali tena. Mark na yeye alivuta shuka na kujifunika.Nilijua kabisa itakuwa ni mtihani mgumu sana kwa Mark kulala na mimi bila kufanya mapenzi.



    Lakini nikasema labda fani yake ya kuigiza inaweza kumfanya avumilie.

    Kwa sababu mda ulikuwa umeenda sana basi wote tulipitiwa na usingizi.Nilikuja kushituka asubuhi pamepambazuka.Nilimtingisha Mark nikagundua bado



    alikuwa kwenye usingizi mzito sana.Nilijaribu kujikagua sehemu zangu za siri ili kujua kama nilipitiwa na mwanume huyo au la.Nikagundua hakufanya kitu



    chochote zaidi ya kulala kama alivyolala.Nilishangaa sana kwa kweli maana mwanaume huyo alionesha kunitamani sana pale nilipokua jukwaaani kwenye



    shindano la mwanamke nyonga. Au ana matatizo ya maumbile huyu, usikute ni hanisi niliwaza na kunyanyuka na kwenda maliwatoni. Niliamua kuoga zangu



    mara baabda ya kugundua kuwa mda ulikuwa umeenda sana na ilishafika saa nne asubuhi.Nilitoka na kumkuta Mark ameshaamka na alikuwa akiongea na simu.

    Niliamua kumfanyia makusudi kwa kubadilisha nguo mbele yake ili nione ni kweli rijali au hanisi.Sikuamini kabisa kama kuna mwanaume anaweza kulala na



    mimi usiku kucha asitamani hata kuomba denda.Nilibadilisha nguo zangu mpaka nikimaliza lakini wala mark hakushituka ndo kwanza alivuta shuka na



    kujifunika vizuri akimaanisha alikuwa bado anahitaji kuendelea kulala. Nilivyomaliza kuvaa nilimueleza kuna mahali nahitajika hivyo tutaonana baadaye.Mark



    akanambia ni sawa lakini bado sijatoa tamko la ombi lake la jana.

    Nilimjibu kuwa anipe mda nitamjibu kwa sababu nahitaji kutafakari maana ndoa sio kitu cha kukurupuka.Mark alinyamza kimya kwa sekunde kadhaa kisha

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    akavuta suruali yake na kutoa wallet na akahesabu noti tano za elfu kumi kumi kisha akanikabidhi.Akanambia kuwa yeye ataondoka na ndege ya mchana ila



    tutawasiliana kama kutakuwa na mabadiliko yoyote yatakayojitokeza. Sikuamini jamani kama nililipwa hela hili hali hakuna kitu chchote alichofanya na mimi



    usiku huo. Nilondoka na kuanza kushuka ngazi taratibu lakini nilivyofika reception nilizuiliwa



    Kwa sababu tuliingia wawili kivipi nitoke mwenyewe. Huwa wanafanya hivi kwa sababu za kiusalama. Ikabidi simu ipigwe kwenye room niliyotoka na Mark



    alipokea na baada ya kusema kuwa yupo salama basi niliruhusiwa na kuendelea na ratiba zangu. Nilitoka mpaka nje ya hotel na nilikutana na hali ya hewa ya



    mvua mvua ikanibidi nipande tax na moja kwa moja nilienda mpaka salooni ambayo nilikuwa nikifanyia kazi. Nilikuwa sina jinsi kwa sababu wikiendi huwa



    napata watejawengi sana ambao huwa wananilipa hela nzuri sana. Mbaya zaidi nilikuwa na appointment na wamama ambao huwa naheshimiaana nao



    sana.Ingawa nilikuwa nimechoka sana lakini bado niliamua kujitutumua na kuheshimu kazi yangu. Yaani nilikuta msururu wa wateja wakinisubiri kwa hamu na



    jamu. Ilibidi niombe radhi kwa kuchelewa kufika lakini kwa kuwa ndo nilikuwa msusi bora nilianza kazi kwa spidi ya hatari. Wanachonipendeaga mimi ni kuwa



    na mkono mwepesi na mtamu usioumiza. Yaani msuko ambo ungesuka kwa msusi nwingine kwa masaa matatu mimi nilikuwa na uwezo wa kusuka kwa masaa



    mawili tu. Nilipambana sana siku hiyo na nilikuwa bize mpaka usiku ukanikutia hapo Mida ya mchana Mark alinipigia simu na kuniambia kuwa ataondoka na



    ndege ya jioni na kama naweza basi nimsindikize mpaka KIA.Nilimwambia tu ukweli kuwa nilikuwa bize sana hivyo isingewezekana. Markilibidi akubaliane na



    matokeo akaondoka zake na kurudi Dar.Basi tuliendelea kuwasiliana kwenye simu na siku zilivyozidi kwenda nikajikuta nazidiwa na mapenzimazito ya kwenye



    simu ya mkaka huyo.Nilitokea tu kumpenda ghafla kwa jinsi alivyokuwa akinijali.Yaani alijua kuhandle maana kwa siku alinipigia simu zaidi ya mara



    tatu.Ingawa huwa nipo bize lakini kwa kweli ikipigwa simu yake ilikuwa ni lazima niipokee.Yaani mwanaume huyu alinirudisha utoto enzi zile ndo nayaanza



    mapenzi.Ukiachilia mbali na mapenzi ya simu mimi naye nilipambana na kufanikiwa kufungua salooni yangu





    *********

    **************

    *****************



    Hapo Mark akanambia “ I just want to wish you happy new born year”( nilikuwa nataka tu kukutakia kheri ya siku ya kuzaliwa).Oooooh my God nilijikuta



    nikiropoka mara baada ya kukumbushwa kuwa siku hiyo ilikuwa ni siku yangu ya kuzaliwa

    Kwa kweli jamani acheni mapenzi yaendeshe dunia kwa sababu huyu mwanaume alinisuprise sana kwa sababu mimi binafsi nilikuwa sikumbuki kabisa kuwa



    siku hiyo ilikuwa ni siku ya kumbukumbu zangu za kuzaliwa.Sikuwahi kusheherekea siku yangu ya kuzaliwa tangia marehemu baba yangu anitoke duniani

    Hivyo nilijikutta machozi yakinidondoka maaa alinikumbusha enzi za uhai wa marehemu baba yangu.Kwa haraka haraka nikajua machozi hayo yanaweza



    mchnagnnya Mark hivyo niliyafuta na kumwambia “asante babe”. Ok usijali alijibu Mark na kuongeza kuwa aliamua kunifanyia surprise na kaniomba aniacche



    ili niendeleaa na shughuli zangu.Alipiga hatua mbili kisha akageuka na kunianglia kimhaba kisha kuniambia “LET ME LOVE TOU” Nilitoa tabasamu zio na



    kumwambia thaks honey. Akaingia kwenye gari na kutoweka eneo hilo.

    Nilipikicha macho yangu kuona kuwa ilikuwa ni ndoto au kweli. Haikuwa ndoto bali ilikuwa ni tukio la ukweli kabisa. Wakati naendelea kuganda pale kama



    mtu aliyepigwa na shoti ya umeme Waridi dada wa salooni alinifuata na kuniambia “happy birthday”. Wewe naye mpaka umsikie shemeji yako anasema ndo



    umuigizie niliamua kumshushua Waridi. Wewe si ulituficha sasa shemeji kakuumbua na uchoyo wako kamwaga mchele kwenye kuku wengi alijibu Waridi.



    Lakini dada unabahati sana ya kupendwa na mwanaume kama huyu handsomeboy na superstar aliendelea kuongea Waridi huku tukiingia saloon. Uzuri wa Waridi



    ni binti mdogo na pia huwa ni mswahili hivyo maneno yake huwa siyatilii maanani.

    “Samahani mteja wangu, mama la mama ilinibidi nimuombe msamaha kwa kumpamba yule mteja ambaye mda wote wa tukio alikuwa akinisubiri. Bila samahani



    fundi wangu maana hayo mambo ya kihindi yaliyokuwa yakiendelea hapo nje ni kiboko alisema mteja huyo. We acha tu shoga leo ni siku yangu ya kuzaliwa na



    mimi nilikuwa sina habari ndo nimekuja kufanyiwa surprise hivyo. “Alafu dada wewe si ulinambia kuwa Mark yupo Dar aliadaakia Waridi”. Si ndo maana ya



    surprise maana hata mimi mwenyewe sijui alifikaje Moshi.

    Ila nimeshangaa sana kumbe hata Tanzania kuna mapenzi ya kihindi alisema yule mteja kauli ambayo mimi niliichukulia kama ni dongo kwangu. Wewe acha tu



    mama yangu kupendwa raha jamani ilibidi na mimi nijdaidai na kujishebedua maana ni wanawake wachache sana wanaopata bahati ya kupendwa na wanaume



    kama hao wanao jua nini maana ya mapenzi. “kweli kabisa dada maana hiyo keki uliyoletewa ni shiidaaaaaaa alidakia Waridi.Uzuri wa Waridi mimi huwa na



    mpenda sana kwa sababu huwa ni muongeaji sana na ukikaa naye kamwe huwezi boreka. Sasa wewe fikiria mimi niliyeletewa zawadi sikujua ni zawadi gani



    lakini yeye tayari alishafungua na kuchungulia na kujua nini kilifungwa huko ndani.

    Basi nikaendelea kumuhudumia yule mama huku na yeye akiniambia kuwa itabidi nikimmaliza hizo zawadi tusifungue hapo hapo na waniimbie wimbo wa



    happybirthday. Tuliendelea na stori mbili tatu huku kila mtu akifanya kazi inayomuhusu hapo salooni.Kulikuwa kuna wanaume wawili waliokuja kufanyiwa



    messaging na nilipowauliza ni halfbody au fullbody massaging waliniambia ni full body.Niliwapa appointment waje saa kumi na mbili maana niliwaambia



    wafanyiwe na Warida wakakataa.

    Huduma hiyo ya kukandwa kandwa, kuchuliwa na kunyooshwanyooshwa viungo ilikuwa ikipendwa sana na wanaume.Pia huduma hiyo ilinipa sana umaarufu na



    kunipa hela nyingi kwa sababu fullbody ilikuwa ni laki moja na half body ilikuwa ni elfu hamsini tu.Na huduma zote zilikuwa hazizidi masaa mawili. Wakati



    wale wateja wakiondoka zao ili waje huo mda niliowambia Warida aliendelea na maswali yake. “Sasa dada kilichokufanya umwage chozi pale ni nini’?Maana



    Mark alipokuambia tu happybirthday machozi yalikumwagika aliendelea kuuliza Waridi.

    Kiukweli mimi huwa sitaki kabisa kukumbuka siku hiyo kwa sababu tangia baba yangu afariki sikuwahi kabisa kusherekea siku hii.Pia huwa sitaki kusherehekea



    siku hiyo kwa sababu huwa linanikumbusha tukio la huzuni sana ambalo lilishawahi kutokea tulipokuwa wadogo.Nakumbuka siku hiyo tulikuwa na familia



    yangu yaani mimi,kaka yangu ,baba na mama yangu.Na nilikuwa na umri kama wa miaka 8 hivi na ilikuwa ni siku ya jumamosi tarehe na mwezi kama huu.

    Nakumbuka pia siku yangu ya kuzaliwa mwaka huo iliangukia kwenye sikukuu ya Iddy al haj.Siku hiyo wazazi wangu walinifanyia bonge la sherehe na baadaye



    walinipeleka sehemu ya kuchezea watoto (childplay ground).Sehemu hiyo ilikuwa na vitu vingi sana kama bembea , treni, magari ya watoto na helkopta na vitu



    vingine vingi unavyovijua wewe.

    Basi tukiwa kwenye furaha hiyo ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwangu na sikuu ya iddy kuna tatizo kubwa ambalo lilitokea.Nakumbuka kuna wazazi ambao



    walikuwa na watoto wao mapacha ambao walikuwa na umri mdogo ambao haukuzidi hata miaka mitano.Watoto hao mapacha wa kike walikuwa wakikimbia



    kimbia huku na kule.Sijui nini kilitokea ila nakumbuka ni uzembe wa wazazi wao na wasimamizi wa sehemu hiyo.Kwa sababu watoto hao walikimbia na



    kwenda kuingia kwenye swimming pool ya wakubwa.Sijui wasimamizi walikuwa wapi maana wale watoto walidumbukia na kupoteza maisha.Tukio hilo



    lilipelekea hata hoteli hiyo ambayo ni maarufu sana kufungiwa leseni yake ya biashara kwa mda.Tukio hili la wale watoto wazuri wadogo kupoteza maisha huwa



    nalikumbuka sana na kunitia huzuni kila ikifikaga siku hii ya kumbukumbu za kuzaliwa kwangu.

    Licha ya hao watoto kufariki lakini siku hii huwa inanikumbusha familia yangu.Huwa nakumbuka sana kaka yangu ambaye naye alidata na maisha haya na



    kuchanganyikiwa kutokana na madawa ya kulevya.Huyu mwanaume kwa kweli alinikumbusha vitu vingi sana.Niliendelea kufanya kazi mpaka nikawamaliza



    wale wanawake wote.Yule mama aliyeshuhudia Mark akileta zawadi alikomaa sana eti anataka kuiona hiyo keki ipoje.Ilinibidi nifungue baadhi ya zile zawadi



    nilizoletewa.Jamani huyu mwanaume ni kiboko wakati Waridi na yule mama wakiangaika na keki mimi nilikuwa nikiangaika na zawadi zingine.Aliniletea nguo



    za ndani tena za kisasa ambazo huwa zinauzwa bei ghali sana.

    Yaani kumbe yale maswali anayoniulizaga tukiwa tunachati kumbe yeye huwa anakariri majibu ninayompa.Maana kila kitu alipatia kuanzia rangi,size na



    muonekano. Kulikuwa na vikorombwezo vingi sana ambavyo vingine sikujua hata vilikuwa ni nini? Lakini vile vitu vidodogo vya urembo kwa mwanamke



    aliviweka.Pia kwa upande wa vitu vya kula kula hakubaki nyuma maana licha ya keki, kulikwa na pipi, ubuyu,chocolate na vingine sijui hata vilikuwa ni

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    vinini.Waridi na yule mama uzalendo uliwashinda ikabidi wakate ile keki ambayo ilikuwa imeendikwa jina langu na kuanza kula utafikiri wao ndo walikuwaa



    wamezaliwa.

    Wakati tukiendelea kula keki mara simu yangu iliita na kuangalia alikuwa ni Mark “helow babe” yes honey nilimjibu kwa kujiamini. “Upo wapi, nimekumiss



    alisema Mark” nikamjibu kuwa mimi bado nipo job je nikitoka nikukute wapi?Mark akacheka kidogo na kuniambia eti amesharudi Dar. ‘stop joking honey, I



    real miss you and I want to spend this night with you”(acha utani honey nimekumiss sana na nataka kuwa na wewe usiku wa leo) ilibidi nimwambie.Kweli tena



    mimi nilikata tiketi ya kuja na kurudi na mda huu ndo nimeingia Dar es salaam alisema Mark kwa kujiamini. -



    Kwa hiyo huku Moshi ulikuwa na ishu gani ilibidi nimuulize kwa hamaki. “Nilikuja tu kukutakia happybirthday na kukuletea zawadi aliendelea kujibu bila hata



    aibu. Yaani nilitamani hata nimg’ate kwenye simu lakini nikasema labda atakuwa ananitania tu kwa sababu anajua kuwa huwa nachelewa kutoka kazini.Basi



    nilimuaga kwa kumwambia tutaonana baadae.Simu ilipokatwa aliingia mwanaume mmoja ambaye alitaka kufanyiwa messaging lakini alikataa kufanyiwa na



    Waridi kwa madai kuwa ananitaka mimi kwa sababu ndo mzoefu na pia huwa namuwezea. Ilinibidi tu niingie kazini maana ndo kazi iliyokuwa ikinipa hela



    nyingi kwa mda mfupi.Akanambia anataka fullbody massaging hivyo akalipia hiyo laki moja. Yaani hii kazi inavishawishi na siku zote nilikuwa sitaki Mark ajue



    maana angenihisi vibaya. Ebu fikiria mwanaume anavua nguo zote alafu sasa unaanza kumkandakanda na kumchua mwili mzima.

    Ujue wanaume wengi wanapenda sana huduma hii kwa sababu huwafanya wajisikie vizuri sana hasa kama atafanyiwa na bint mwenye mvuto kama mimi na



    mwenye uzoefu na kazi hiyo.Ujue ni sisi tu watanzania ndo tupo nyuma lakini wenzetu wazungu huduma hii huwa inapatikana nyumbani na mara nyingi mke



    anamfanyia mumewe kama ishara ya kumjali na kumpenda.Huduma hii huondoa uchovu na kuuweka mwili katika hali nzuri ya furaha. Kwa hiyo wanawake



    jamani jitahidini kuwafanyia waume zenu huko nyumbani la sivyo ndo kama hivi watakuwa wanakuja kwetu na kutuletea hela nyingi wakati nyumbani mmekula



    dagaaa. Pia akikutana na makurubembe na makomba mwiko basi tena ndo umeibiwa mme hivyo.Sasa kama mtu anavua nguo zote na tupo wawili tu chumbani



    unafikiri nini kinaweza kutokea.

    Unajua kwa nini huduma hiii inapendwa sana na wanaume ngoja leo nikupe siri kidogo za kazi hii ili na wewe ujifunze kitu. Unajua kitaalamu katika zile organ



    tano za fahamu touch is most meaningfull( ngozi ndo ima msisimko zaidi). Huduma hii inaleta hisia za ajabu na kuondoa uchovu wote. Basi niliingia kwenye



    chumba kile cha kufanyia message.Chumba hicho kilikuwa kikubwa ambacho kilikuwa na hewa ya kutosha na sehemu ya kuzunguka zunguka. Nikaanza



    kukiandaa kwa kuweka blanketi laini kwenye kitanda pia niliweka na ile mito laini.Pembeni ya kitanda kulikuwa na kiti maalaumu lakini hichi ni kwa ajili ya



    halfbody massage.

    Nikawasha mishumaa na taa zenye mwanga hafifu kisha nikafungulia mziki laini tena ile ya classic.Nikamwambia Yule mteja aingie chumbani hapo huku mimi



    nikipasha mafuta ya kufanyia message.Kulikuwa na mafuta mengi sana kama olive oil, coconut oil,ovacado oil na sweat olmond oil.Yaani hapa leo itabidi



    mnisamehe tu mimi sijui Kiswahili cha haya mafuta. Kwa kuwa mafuta haya huwa yanataka joto lingi niliamua kuyapasha kwa kutumia chombo maalumu



    nilichokiweka juu ya stovu.Nikahakikisha yanapata joto linalohitajika maana yakiwa na moto sana ni tatizo maana anaweza hisi maumivu.

    Basi yule mteja akapanda kitandani na nilimwambia alale na tumbo hili tuanze na mgongo.Na hiyo jamani ni mara baada ya yeye kuvua nguo zote na kubaki uchi



    wa mnyama. Kumbuka nilikwambia hii ni fullbody massage.Nikamwekea mto chini ya kichwa na mto mwingine niliuweka miguuni.Nilimfunika mwili wake



    kwa mataulo mawili makubwa yaliyokuwa yamekauka vizuri. Hapo kwa wale wanaume wanaojiheshimu basi wao huogopa kuvua nguo zote na kubaki na nguo



    ya ndani tu. Ila huyu wa leo hakuwa na aibu yeyote maana mmmmh alivua nguo zote.

    Na mimi sikumuogopa maana nilikuwa kazini.Nilipanda kitandani nikapitisha miguu juu yake huku mmoja ukiwa juu na mwingine chini yaani kama mtu



    anayesubiri kipenga ili aanze mashindano ya riaza.Nikamwekea mikono yangu mgongoni mwake na kuanza kumkandamiza taratiibu.Nikachukua yale mafuta



    nikayapaka mikononi mwangu kisha nikaisugua vizuri kutengeneza joto la ulaini. Nikapitisha mikono yangu laini kwenye mbavu zeke huku nikimtekenya



    tekenya na kucha zangu huku nikimwambia avute pumzi kama mara tatu hivi. Kwa hiyo alikuwa akivuta pumzi na mimi navuta mpaka nikahakikisha anajisikia



    vizuri.

    Hapo nikaanza kumsugua sugua taratibu kuanzia mabegani mpaka mgongoni.Nilianza na spidi ndogo na baadaye niliongeza spidi. Kwa hiyo jinsi alivyoendelea



    kupumua ndivyo na mimi nilijua ni sehemu ipi iliyo na maumivu ya kuchua taratibu na ipi ya kuchua kwa nguvu. Nikawa nashuka taratibu mpaka sehemu zake



    zile za makalio.Nilinilivyofika hapo nikatoa lilie taulo nililokuwa nimetumia kuyafunika makalio hayo. Sasa hapo kuna wanaume ambao huwa wanapenda



    kushikwa makalio na kuna wengine huwa hawapendi.Hivyo nilijaribu kwanza kuyapapsa na nilivyoona ameshituka kwa nguvu nikaogopa nikarudisha mikono



    yangu kwa spidi ndogo juu ya kiuno chake.

    Baadaye niliamia miguuni na kuendelea kutumia utaalamu wangu ambao ndio unawafanya wakatae kufanyiwa na kina Waridi. Unajua wengine wengi huwa



    wanashindwa kutumia dole gumba na kuminyaminya mbavu na sehemu zingine amabazo huwa nauchovu zaidi.Hapa nikaenndelea kutengeneza viduara vidogo



    vidogo mgongoni mwake.Nikaongeza mafuta na kurudia sehemu za hips na miguu.Wakati nipo sehemu za mapajani niligundua pia sehemu zake za makalio



    zilikuwa hazina furaha na zenye uchovu kwani zilikuwa zimekunjamana na kusinyaaa.

    Unajua kitaalamu sehemu hizo japo wanaume wengi huwa hawapendi zishikwe lakini ndo sehemu ambazo huwa zimechoka sana hasa kwa wale watu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    wanaofanya kazi za kukaa mda mrefu kama maboss na wengine.Kwa hiyo ilinibidi niuongeze mafuta na kupachua vizuri kabisa kwa madaa kama vile nesi



    anatafuta mshipa wa kuchoma sindano.Hapo alitulia tulii kama mtu aliyeaamia dunia ingine.Kimoyo moyo nikawa najisemeha kama amehamia dunia ingine na



    kuanza kuwaza ujinga sahuri yake mimi nipo kazini bwana acha nitafute hela. Ndio ni lazima nifanye kazi kwa utaalamu na utundu wa hali ya juu ili waendelee



    kusimuliana huko mjini ili niendelee kupata hela.

    Wewe unafikiri mtu kutoa laki yake sa hivi kwa maisha haya ni jambo dogo.Nikashuka chini mpaka kwenye visigino na viwiko vya miguu.Nilivyofika kwenye



    unyayo akacheka nahisi nilimtekenya na hizi kucha zangu ambapo kipindi hicho zilitengenezwa rasmi kwa ajili ya kazi hiyo. Yaaani nilitamani huduma hiyo ndo



    ningekuwa namfanyia mchumba wangu Mark.Na nauhakika kuwa siku nikimfanyia lazima atanikataza kuwafanyia wanaume wengine, jamani hii kitu ni raha



    mwenye hela zake akajaribu ila usiende zile za vichoroni kwa watu waliovamia fani na wasio na ujuzi wowote.

    Baada ya kumaliza zile sehemu za nyuma nilimwambia ageuke tuhamie sehemu za mbele. Mungu wangu kumbe mwanaume wa watu mawazo yake hayakuwepo



    hapo maana sehemu zake za siri zilikuwa zimesimama.Nikachukua lile taulo na kumfunika asije akasababisha na mimi nikaama kimawazo.Nikajipaka tena



    mafuta kwenye mikono yanu alafu nikachukua mkasi uliokuwepo hapo pembeni na kumgonga kwa nguvu magotini.Nia yangu iikuwa asikie maumivu ili



    mawazo yaamie kwenye maumivi hivyo yule jogoo aliyesimama tayari kwa kuwika arudishe kichwa chake bandani.Nikaanza kupitisha mikono yangu kwenye



    kifua chake na nikapanda juu kidogo na kufanya msisitizo kwenye mabega yake ya mbele na shingoni



    Nikahamia kwenye sehemu za maziwa nikayachuachua na yenyewe ili yawe poa. Niliendelea hivyo huku nikihakikisha kila kiungo cha mwanaume huyo kinapata



    huduma. Badaye nilimwambia ainuke na kukaa kwenye kile kiti maalumu na nilimuuliza anajisikiaje? Yaani badala ya kunijibu swali langu yeye akanikonyeza



    yaani wanaume wengine bhana wewe acha tu. Yaani sijui ndo alishadata na mimi au ni mbwembwe tu baada ya kupewa huduma nzuri. Alafu huyu nahisi ndo



    ilikuwa ni mara yake ya kwanza nahisi alikuwa anasimuliwa tu habari zangu ndo akaja kujaribu. Na ndio maana hata nilivyomwambia afanyiwe na Waridi



    alikataa katu katu. Sikutaka kupoteza mda nilimuacha huko chumbani apumzike kidogo na mimi nikatoka na kwenda kwenye kile chumba kingine cha saloon.



    Nikamkuta Waridi anapiga stori na mteja mwingine wa kike ambaye na yeye alitaka huduma hiyo ya massage. Mda ulikuwa umeenda sana lakini sikuwa na jinsi



    nikamwita Krish muhindi ambaye yeye alikuwa saloon ya kiume ambayo pia ni ya kwangu aje amfanyie huduma dada huyo.Ujue mimi nilikuwa na salooni mbili



    zilizofuatana moja ya kike na ingine ya kiume hivyo niliajiri watu wenye uzoefu na waliosomea mambo hayo.Siunajua tena Mark alinipa mtaji wa kutosha.

    Krish alikuja kwa haraka kwa sababu yeye alishafunga ofisi hivyo ikabidi niingie ndani ili nimtoe yule mwanaume ambaye mimi nilikuwa nikimfanyia



    massage.Cha ajabu nilimkuta bado haja vaa hata nguo.Yaani hizi kazi zetu zilikuwa na changamoto nyingi sana.Ikabidi nimpe makavu live kuwa anipishe maana



    kulikuwa na mteja mwingine. Eti yule mwanaume akaniuliza hawezi kupata huduma ingine? Nilitamani nicheke lakini nilijikaza na kumuuliza sasa wewe si



    ulilipia laki ya full body massage sasa unataka huduma gani ingine.Akaniangalia na kuniambia si ni yale mambo ya kikubwa.

    Nikamjibu kwa kifupi kuwa sisi hatutoi huduma hiyo. Ilimbidi avae nguo zake na kuondoka huku akilipia laki na nusu badala ya laki moja na aliacha namba zake



    za simu eti nimtafute baada ya kumaliza kazi. Yaani huyu baba ana bahati sana yaani angenikuta enzi zangu ningevikomba hivyo viela vyake vinavyomtia jeuri.



    Yaani angemkuta Leah wa kipindi kile ningemchuna mpaka akome. Kwa bahati nzuri au mbaya siku hizi nimekuwa malaika tangia nikutane na



    Mark.Nakajisemea wacha tu nimvundikie Mark wangu ili siku akija akikute kimeiva na kuwa kitu piruuu kabisa. Siunajua tena kisipotumika mda mrefu



    kinajirudi na kujijenga utafikiri ndo kigoli.

    Basi alitoka na kunipa nafasi ya kuandaa kile chumba na kuruhusu yule mteja na Krish waingie kupeana huduma. Walifanya yao na walipomaiza walitoka na



    mimi kufunga ofisi huku nikiamini kuwa Mark bado yupo mjini alikuwa ananitania tu. Nilijua Mark alikuwa ananirusha roho atakuwa hapa hapa mjini yupo



    mahali na marafiki zake wakiponda raha siunajua tena na yeye alivyokuwa akipenda starehe. Tuliondoka zetu na nilimpa nauli Waridi hivyo tukakubaliana



    kuonana kesho . Niliamua kwenda kwanza nyumbani ili nikaoge nile ndo nimtafute Mark.

    Kama kawaida yangu nilipitia kwa muuza chipsi akanifungia chipsi kuku na nikaingia zangu ghetto. Kama kawaida muuza chipsi huyo hakuacha mautani yake



    eti ananipenda lakini anajua kuwa hawezi kunipata kwa sababu yeye nyota yake ni ya chipsi kupendwa na wanafunzi na mimi sio mwanafunzi hivyo hawezi



    kunipata kihurahisi. Unajua wanaume wamekuwa na mbinu nyingi sana unaweza kuona kuwa anafanya utani kumbe ndo mwenzio anamaanisha hivyo.Siunajua



    zile tena shemeji shemeji kulaaa huku anazima taa ukija kushituka unakuta tayari mambo yameshaharibika. Niliingia ndani nikaoga nikala kabisa huku



    nikiendelea kufungua zile zawadi zangu zilizobakia.

    Kumbe alininulia mpaka nguo na viatu na mafuta mazuri na ile perfume ya kiss me ambayo huwa naipenda sana.Nilijikuta bila kutarajia nanyanyua simu na



    kumpigia na neno la kwanza nililomwambia ni LET ME LOVE YOU. Alicheka kwa sababu neno hilo alinambia mchana tukiwa pale saluni mara baada ya



    kukumbatiana kama vile wahindi baada ya kucheza zile nyimbo zao za kuchikuchi.Nikamuuliza yupo wapi lakini bado alijibu vile vile kuwa yeye yupo Dar.



    Hapo nilkasirika maana usiku huo mimi nilikuwa na mizuka ya kuwa naye.

    Nikamuuliza au huku Moshi ana mwanamke mwingine ambaye ndo amefikia?Bado aliendelea kujibu kwa kujiamini kuwa yeye yupo Dar na niache hisia zangu



    mbaya. Kwa hasira nilikata simu kuitupilia mbali, siunajua tena bila kudeka mapenzi hayanogi.Nilivyokata tu yeye akapiga sikupokea na nikaitupilia simu ile



    kitandani na nikaacha kabisa kufungua zile zawadi zake. Sijui kwa nini huyu mwanaume alizinyanyasa hivi hisia zangu. Haya ni mapenzi ganii ya kwenye simu



    wakati mwenzie mimi nilichoka kuvumilia.Ebu fikiria mwaka mzima mtu unamvumilia tu na kumtunzia wakati mimi kila siku napata vishawishi vya



    kutongozwa na wanaume wengi tena wenye hela zao.

    Ujue ile kazi ya saluni hasa ile ya massage ilinisababishia niwe natongozwa sana na kuhongwa lakini bado niliamua kumtunzia Mark. Wakati mwingine



    nilijifariji kwa kale kamsemo kuwa mvumilivu hula mbivu lakini sikusahau kale ka msemo kuwa mvundika mbivu hula mbovu. Mark alipiga simu zaidi ya mara



    tatu lakini sikupokea kwa sababu aliniboa sana maana wewe huwezi toka Dar na kupanda ndege kuja Moshi eti kwa ajili tu ya kuniletea zawadi za happybirthday



    tu hiyo haikuniingia akili kwa kweli. Alivyoona nimegoma kupokea sms yake akatuma meseji iliyosema “LET ME LOVE YOU”(acha mimi nikupende). Eeeeh

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    nilishangaa sana mbona hili neno alikuwa analipenda sana kwani lilikuwa na maana gani. Nikaamua kumjibu kwa kifupi kuwa ameniboa. Hapo hakujibu tena



    sms bali alienda kabisa hewani “am sorry baby” ndo lilikuwa ni neno lake la kwanza.Nikamwambia ajue mimi simuelewi kabisa na haya sijui ni mapenzi gani ya



    kihindi au kifilipino “baby am sorry alirudia tena na ndo neon lake kubwa alilokuwa akipenda kulitumia hasa mara baada ya kunivuruga. Yaani wewe ungekuwa



    una jua maana ya neno am sorry hata usingependa kulitumia kabisa nilimwambia Mark kwa sauti ya ukali.

    Akaniuliza kwani lina maana gani? Am sorry maana yake unathibitisha wewe ni dhaifu na ndio maana unakosea kosea.Alicheka na kuniambia tena am sorry hapo



    ilibidi na mimi nicheke maana alijifanya haelewei kabisa. Alivyoona nimecheka akanambia basi atakuwa alitumii tena neno hilo ila anaomba yaishe.

    Basi tukaanza kuongea mambo mengine siunajua tena biti na mikwara kwenye mapenzi ni muhimu la sivyo utaonekana huna wivu. Lakini ukweli utabaki pale



    pale huwezi kumpangia mwanaume ratiba zake au kumlinda. Kufanya hivyo ni sawa na kulinda bahari wewe unalinda bagamoyo mwenzako wanaogelea



    Zanzibar.Alinambia kuwa mwezi ujao atakuja kwa ajili yangu ili tuende Dar akanivishe pete. Yaani kusikia neno kuvalishwa pete nilinyanyua mkono wangu wa



    kushoto na kuuangalia vizuri kama kweli ulikuwa unastahili kuvalishwa pete.Hapo ikabidi nibadilishe na kuipotezea mada hiyo maana kuolewa sio jambo dogo.





    Nikamuuliza mbona anapenda sana kutumia neno “LET ME LOVE YOU”.Akanambia analipenda tu na hakuna namna ingine acha anipende tu. Akanambia



    ameanza mikakaati ya kuandaa filamu ambayo itaitwa Let Me Love You ambayo pia anataka mimi nishiriki kama muhusika mkuu. Hapo nilifurahi kwa sababu



    moja ya vitu alivyoniahidi ni kuhakikisha kuwa ananiingiza kwenye tasnia hiyo ya filamu. Nikamuuliza kuwa hiyo ameshapata idea akanijibu kuwa hana idea



    yeyote zaidi ya jina hilo. Nikamwambia basi kama ni hivyo aache mimi nitunge stori ambayo itabeba maana ya jina hilo ambalo kwa kweli alipenda sana



    kulitumia.

    Basi alikata simu na tukakubaliana mimi ndo nitunge stori hiyo. Kwani najua basi kutunga stori hata ya page moja. Hapo niliwaza sana lakini sikuapata picha



    hiyo stori iweje. Nilifikiria usiku wote huo lakini sikuwa na idea yeyote baadaaye niliona haina haja ya kujiumiza hizo ni kazi za watu waliopewa kipaji na



    mungu kutunga vitu. Hapo nikakumbuka kuwa kuna mwandishi mmoja ambaye stori zake huwa zinanigusa sana kwani huwa zinaelezea maisha halisi



    yanayotuzunguka stori hizo huwa nazifuatilia kwenye mitandao ya kijamii. Mwandishi huyo pia

    huwa anatoa ushauri wa mapenzi, uhusianao na saikolojia.Mimi huwa nampenda sana kwa sababu kuna kipindi aliwahi kunishauri sana kuhusu maisha ya



    mapenzi na hata ya kawaida pia. Mwandishi huyo alijulikana kwa jina la Eliado. Nilitaka kumpigia simu usiku huo lakini nikagundua kuwa mda ulikuwa



    umeenda sana hivyo nilala zangu na kupanga kuwa nitamtafuta kesho ili niweze kumshirikisha jambo hilo.

    Nililala usingizi mzito sana siku hiyo kwa sababu nakumbuka nilikuwa nimechoka sana na sikuweza kushusha hata neti. Usiku nilishituka usingizini baada ya



    mbu kuning’aata na kunisumbua sana. Niliwachukia sana hao mbu kwa sababu walinikatisha ndoto yangu ambayo nilikuwa nikiota.Ndoto ilikuwa ikielezea jinsi



    harusi yangu na Mark itakavyokuwa. Ndoto ilikuwa tamu sana maana ilinipa taswira ya picha halisi ya maisha yangu ya mbeleni. Nilishusha neti na kurudi kulala



    zangu huku nikitamani ndoto ile ijirudie. Ile ndoto ya harusi yetu mimi na Mark haikujirudia na badala yake niliota ndoto ambayo ilinikosesha raha siku



    iliyofuata.

    Niliota kuwa kwenye lile shamaba la marehemu baba yangu ambapo ndo madini yalihifadhiwa kuna mtu alijenga na aliamua kuliamisha lile kaburi. Ndoto



    iliniweka njia panda kwa sababu haikueleza kuwa yale madini yaliiibiwa au la. Sikujua ile ndoto ilikuwa na maana gani ila kwa kweli ilinishitua sana na kuhisi



    labda yale madini hayapo tena sehemu salama. Siku hiyo ilikuwa mbaya sana kwangu kwa sababu ya mawazo ya madini niliyokuwa nayo.Nikajikuta siku hiyo



    inaisha bila kumtafuta Eliado kwa ajili ya ile stori itakayotengeneza filamu itakayoitwa Let Me Love You.Usiku Mark alinipigia na kuniuliza kama nimeshapata



    hiyo stori ambayo itatengeneza script ya filamu ambayo kwa namna moja au nyingine itaelezea maisha yetu ya kimapenzi.

    Basi nikaona isiwe tabu ngoja nilifanyie kazi wazo la Mark ili mradi yeye si ana taka shorti stori tu kisha mambo mengine atafanya yeye. Kwa kiherehere kabla



    sijamtafuta Eliado nilijaribu kutunga kwa uwezo wangu na niliposhindwa ndo nilinyanyua simu na kumpigia. “Halow, helow vipi habari za siku nyingi” nzuri



    sana sijui ni nani mwenzangu aliuliza mwandishi huyo mara baada ya kupokea simu yangu. Jamani umenisahau niliamua kumlegezea sauti ili tu kumdatisha



    kidogo. “Siunajua mimi na marafiki wengi sana hivyo ni vizuri ungejitambulisha alisema mwandishi huyo kwa kujiamini.” “OK, mimi naitwa Leah kuna kipindi



    nilikutafuta ukanisaidia sana kunishauri kuhusu maisha yangu ya kimapenzi ambayo kwa kipindi hicho yalikuwa yamepoteza dira.

    Basi akanambia karibu na ananisikiliza. Nilianza kwa kumwambi kuwa “sasa leo sitaki ushauri wa mapenzi wala nini bali ninachotaka ni unitungie kastori



    kafupi sana kanachoitwa LET ME LOVE YOU.Alafu sasa stori hiyo ndo nitampelekea mchumba wangu ili tuandae filamu ambayo itaelezea maisha yetu ya



    mapenzi. Kwa hiyo unataka hiyo stori iweje aliniuliza mwandishi huyo.Mimi sina idea yeyote na ndio maana nikakutafute wewe ilinibidi niwe mkweli. Cha



    msingi ni kwamba isiwe ndefu tukashindwa kuigiza kwa mtindo wa filamu. Kuhusu malipo wewe usijali wewe fanya kazi ilinibidi nimuhakikishie ulaji mara



    baada ya kuniuliza swali hilo la malipo.

    Akanambia nimpe lisaa limoja atakuwa amekamilisha swala hilo.Ilinibidi nishangae yaani lisaa limoja tu atakuwa tayari ameshatunga hiyo stori wakati mimi



    Mark alinipa kazi hiyo tangia juzi na sikuweza,Nikaseama kweli muache mungu aitwe mungu kwani ameumba watu wenye vipaji mbali mbali.Nikaendelea na



    shughuli zangu huku na mimi nikijaribu kuvuta taswira ya hiyo Let Me Love You ili nikitumiwa nione kama iatendana na yangu au ndo nitaendelea kuwa kilaza



    kwa upande wa fani za watu. Kweli huyu ni kiboko maana hata kabla ya lisaa alilosema kuisha yaani ndani ya dakika kumi tu alinitumia meseji na kuniambia



    nifungue email yangu tayari ameshafanya yake.Kwa kihoro cha kutaka kujua aliandika nini ndani ya mda mfupi huo nilichukua tablet yangu na kufungua email



    yangu na kuanza kuisoma hiyo stori.Mistari miwili ya mwanzo tu ilinivutia na hako kastori kalisomeka hivi.

    “Licha ya mali na utajiri aliokuwa nao kijana Jimmy bado alipenda kujishusha na kuishi maisha ya kawaida. Kuna wakati alikuwa akiamua kuacha usafiri wake



    wa kifahari na kuamua kutembea kwa miguu. Zoezi la kutembea kwa miguu huwa analifanya karibu kila wiki huku akiamini kuwa ni moja ya sehemu ya



    mazoezi ya mwili.

    Jimmy akiwa katika matembezi yake ya jioni ya siku ya valentine day anamuona binti mmoja akiwa mbele yakee huku akitembea kwa mwendo wa taratibu sana



    lakini alikuwa upande wa pili wa barabara.Tofauti na watu wengi ambao uvalia nguo nyeusi siku hiyi special kwa wapendanao binti huyo alivalia nguo nyeusi.



    Ghafla moyo wa Jimmy unazizima kutokana na uzuri wa binti huyo. Ingawa Jimmy alikuwa akitembea kwa miguu lakini alijiuliza kwa nini binti mrembo kama



    huyo aliamua kutembea kwa miguu.Akajikuta amechanagnyikiwa kwa sababu umbo , suara na muonekano wa binti huyo ndo vilikuwa vigezo vya mwanamke



    ambaye siku moja angependa kuja kumuoa. Mwenyewe alimuita “the girl of my dream” yaani msichana wa ndoto zake.

    Bila kutarajia Jimmy akajikuta amevuka upande wa pili wa barabara na kuanza kutembea nyuma ya msichana huyo.Jimmy alipunguza mwendo huku akiendelea



    kuburudishwa vyema na mjilindimo ya makalio ya binti huyo ambayo yalijazia vizuri na kufanya milindimo ambayo imgempa shida mwanaume yeyote mwenye



    tamaa. Jimmy pamoja na ujanja wake wote lakini bado alishindwa kuelewa ni vipi atamwingilia binti huyo nakuanza kuongea nae.Akajikuta akiendelea

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    kumsindikiza na kuendelea matembezi tofauti kabisa na njia ambayo yeye alitaka kuipita

    Kwa haraka haraka akawaza kuwa huenda binti huyo angefika sehemu aliyokuwa akienda bila hata ya yeye kumsemesha. Jimmy akaamua kujikaza kisabuni na



    kupiga hatua za haraka haraka na kumsogelea mrembo huyo.Bila kutarajia Jimmy akajikuata anaropoka “dada habari”.Yule dada aligeuza shingo yake kama



    twiga mwituni kisha akamuangalia Jimmy kuanzia juu mpaka chini alafu hakujibu salamu hiyo akanyamaza kimya akarudisha shingo yake na kuendeleaa na



    safari yake.Jimmy alijikuta akiishiwa ujanja na kujikuta akirudia tena kutoa salamu kwa kumwambia “dada nakusalimia”.Yule dada akafanya kama mwanzo



    yaani kugeuza shingo kumwangalia chini mpaka juu a kukaa kimya huku akianza kuongeza mwendo.





    Jimmy akawa ameishiwa mbinu akaamua kunyamaza kimya na kuendelea kutembea pembeni ya mrembo huyo.Wakaendelea na matembezii yao kama vile watu



    waliokuwa wakijuana ila waliamua kuwa mabubu tu.Wakafika makutano ya barabara hapo yule binti mrembo akavuka barabara na kwenda ng’ambo ya pili.



    Jimmy akakata tamaa na kuamua kurudi zake alipotoka, akageuka zake huku akimsindikiza yule mrembo kwa macho. Akaanza kupiga hatua kurudi alipotoka



    lakini bado roho yake ilipingana na mwili na akili yake kutokana na maamuzi hayo ya kukubali kushindwa.Akajikuta akijisemea kwa nguvu “No I cant tolerant



    any more, she is a girl of my dream,LET ME LOVE YOU.(Hapana siwezi kuendelea kuvumilia, ni msichana wa ndoto zangu, wacha tu nimpende)

    Jimmy akajikuta anavuka barabara kwa nguvu bila kuangalia kushoto na kulia.Piipiii pipiiiiiii piiiiiii, paaaaaah paaaaaah haaaaaaaaa ni mlio wa honi ya gari



    ndogo aina ya spaciao new model ambao uliambatana na kishindo kuashiria kuwa kuna ajali mbaya ilitokea.Mlio huo na mshindo vilimshitua yule dada ambaye



    Jimmy alikuwa akimfuatilia.Tofauti na Watanzania wengine waliojaliwa roho ya utu, upendo na huruma dereva aliyemgonga Jimmy hakusimama na badala yake



    aligeuza gari yake na kutimua mbio. Binti yule mrembo aliingiwa na huruma na kujikuta akiaamua kumsaidia Jimmy. Binti wa watu alichanganyikiwa mara



    baada ya zoezi lake la kupungia mkono magari kushindikana kwa sababu magari yote yalikuwa yakipita kwa kasi. Binti huyo ikambidi atumie mbinu za kike kwa



    kusimama katikati ya barabara na kuanza kupiga piga miguu kama mtu aliyechanganyikiwa.Hapo alifanikiwa kupata msaada na kumkimbiza Jimmy



    hospitali.Binti huyo hakuweza kumuacha Jimmy mweneyewe pale hospitali hivyo akajikuta anamwangalia mpaka hapo hali yake itakapokuwa nzuri.

    Jimmy alikuja kupata ufahamu na kushituka kutoka usingizni na kujikuta akizungukwa na dripu za damu na maji.Alipoangalia pembeni akakutana na tabasamu



    zito la binti mrembo ambaye alikuwa pembeni yake. Jimmy akauliza kwa sauti hapa nipo wapi? Yule binti akamuangalia kwa huruma kisha akatabasamu na



    kumwambia relax ulipata ajali ndo maana upo hapa hospitalini.Huo ndo ukawa mwanzo wa Jimmy kujuana na binti huyo.Kujuana huko kukapelekea wote



    wawili kuzama kwenye dimdwi zito lenye matope mekundu na yenye umbo la moyo yaani mapenzi.

    Stori hiyo ya Eliado ilishi hapo ikabidi nimpigie na kumuuliza mbona sasa ameikatisha stori na imekuaje ameitunga kwa mda mfupi hivyo yaani dakika kumi



    tu.Hapo Eliado akacheka na kuniambia hiyo stori ilikua kwenye library yake na inaitwa “THE GIRL OF MY DREAM” Hivyo amaikata kipande cha mwanzo wa



    stori hiyo na kunitumia kwa sababu anaamini kuwa kama filamu yetu itaanza kwa mtindo huo itakuwa inavutia sana watazamaji.Ikabidi nikubaliane na yeye ndio



    itavutia sana kwa sababu ndo itakuwa ni mwazno wa mapenzi ya watu wawili sasa nini kitafuata baada ya hapo ilibidi nimuulize swali hilo maana bado aliniacha



    njia panda.

    Akacheka kwanza na kuniambia mbona simple sana kinachofuata hapo ni huyo bint mrembo ambaye ndo kwenye filamu utakuwa wewe kuleza historia yake ya



    mapenzi ambayo ni mbaya sana na ya kukatisha tamaa na inayosababisha wewe kuchukia wanaume na kutowaamini kabisa. alafu Jimmy ataeleza kwa nini



    alivutiwa na kupagawa na wewe mara baada ya kukutana na wewe siku ile ya kwanza. Kwa hiyo ili filamu iwe tamu itakuonesha wew na matukio yako ya nyuma



    na Jimmy na matukio yake ya nyuma na itafafanua kwanini Jimmy anakuona wewe ni msichana wa ndoto zake.Kwa hiyo hilo jina lenu litaingia kwa sababu



    kutokana na maisha ya kuumizwa kimapenzi aliyopitia Jimmy na kujikuta anawachukia wanawake na anajikuta wewe ndo uanweza kuziba pengo hilo hivyo



    kupelekea “LET ME LOVE YOU” na wewe ulikuwa huna mpango wa kumpenda mwanaume lakini kutokana na upendo aliokuonesha mwanaume huyo hauna



    jinsi LET YOU LOVE HIM. Alitoa ufafanuzi mtunzi huyo ufafanuzi ambao ulinifurahisha sana.Ikabidi nimwagie sifa kem kem na ilibidi nimuulize “umesema



    kipande hiki umekitoa kwenye stori yako inayoitwa THE GIRL OF MY DREAM, je haitaleta shida sisi tukiktumia.

    Akanambia haina shida kwa sababu kwenye sehemu ya story writer tuataweka jina lake. Alisistiza kuwa hiyo sio mara yake ya kwanza kuhusishwa kenye filamu



    hivyo itakuwa pia ni mwanzo mzuri wa sisi na yeye kufanya kazi. Basi tukakubaliana kufanya kazi hiyo pamoja na atatusaidia kuendeleza matukio ya stori hiyo.



    Nilikuwa na furaha sana huku nikiamini kuwa ndoto zangu za kuja kuwa mtu maarufu zinaweza kufanikiwa hata kabla ya kuyapata yale madini. Sikutaka



    mbwembwe niliamua kuikopi na kuipesti hiyo stori kama ilivyo na kuifowadi kwa Mark. Baada ya kama lisaa hivi Mark alipiga na kuniuliza kama kweli ilikuwa



    nai mimi nimetunga hiyo stori.Nikamwambia ndo mimi kwani mimi siwezi kutunga stori.

    Akanambia sio kwamba siwezi lakini ile idea ilikuwa nzuri sana na mtu mwenye utaalamu wa uandishi ndo anaweza kubuni vitu kama hivyo.Nikakomaaa na



    msimamo wangu kuwa ni mimi ndo nimetunga nia yangu ni kupata maujiko ya bure.Tuliongea ongea kwenye simu na baadae alikata simu na kuniacha mimi



    niendelea na mambo yangu mengine.

    Maisha yaliendelea huku nikimsubiri wanaume huyo kwa hamu na jamu kwa sababu alinambia atakuja moshi hivi karibuni.Baada ya miezi miwili Mark alikuja



    Moshi na kama kawaida yake alikuja kazini kwangu.Nilimuomba anipe mda kidogo ili niweze kuweka mambo yangu sawa kabla sijawaachia majukumu yote



    hao mabinti wa hapo saloon. Sijui kwa nini huyu mwanaume alikuwa anapenda kuja sana kazini kwangu.Niliweka mambo yangu sawa na baada ya hapo nilienda



    nyumbani kujiandaa tayari kwa kuwa na mwanaume huyo ambAye kwa wakati alikuwa akitawala sana ubongo wangu na hisia zangu.Yaani siku hiyo nilijikuta



    namwaga nguo zote kitandani ili kutafuta nguo ambayo itakuwa ni funiko na kunifanya nionekane binti mdogo mbichi anayechipukia.

    Nikampiga na alinielekeza nimkute kwenye hoteli niliyofikia. Na nilivyofika hapo hata hatukukaa sana alinambia kuwa kuna marafiki zake wanamsubiri



    mahali.Aliwapigia simu na wakamwambia tumkute sehemu inayoitwa Mercury.Tuliingia kwenye gari na kuelekea hiyo sehemu.Sikujua hata hilo gari alilipata



    wapi lakini sikutaka kumuuliza kwa sababu nilijua kwa umaarufu wake lazima alikuwa na marafiki wake wenye uwezo watakuwa wamemwazimisha.Tulifika



    eneo hilo na tulikuta kuna shangwe utafikiri kama vile kulikuwa na sherehe. Yaani huyu mwanaume alikuwa na marafiki wengi sana utafikiri ni kijiji. Lakini



    nikajuiliza mbona paliandaliwa kama vile palikuwa na kitafrija kidogo. Yaani nilipokelewa kama malkia na watu wote walisimama na kuimba wimbo wa karibu

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    shemeji.Ilikuwa ni bonge la surprise kwa kweli sikujua kama ninaweza kupewa heshima kubwa kiasi hicho.

    Niliona pia makameraman ambao walikuwa wakichukua tukio hilo. Kumbe siku hiyo ndo ilikuwa ni siku rasmi ya mimi kutambulishwa kwa marafiki



    zake.Kulikuwa na watu kama 15 tu lakini kulikuwa na shangwe ya kufa mtu.Na tulivyokaa MC alimuomba Mark asimame na kutoa utambulisho.Mark hakuwa



    muongeaji sana aksimama na kusema “Ndugu zangu part yetu sio ya kuongea bali ni ya kula na kunywa hivyo basi nitaomba vitendo vitawale sana kuliko



    maneno.Leo ni siku muhimu sana ambapo nitawadhihirishia marafiki zangu kuwa nimepata mchumba ambaye tutaanza safari ya kuelekea maisha ya ndoa.Kwa



    kifupi leo nitamvalisha pete mpenzi wangu na kumthibitishia kuwa ninampenda na kumuamini.

    Mark baada ya kusema maneno hayo akatoa pete ya gold ambayo ilikuwa inametameta na kunivalisha. Haikuwa pete ya ndoa bali ilikuwa ni pete ya uchumba na



    nilishindwa kuvumilia nilifurahi sana na machozi ya furaha yalinitoka.Pete ile utafikiri ilipimwa vile kwani ilinifiti vizuri sana kwenye kidole changu.Basi



    tuliendelea na party yetu huku vicheko vituko na burudani ikiendelea.Kuna mwanaume mmoja alikuwa akinichekesha sana kwani mda wote yeye alikuwa bize



    akinikonyeza.Sasa sijui pombe zilikuwa zimemkolea au alikuwa akimaanisha.



    *********

    *************

    ********************



    Mark akaendelea kujitapa kuwa yeye huwa habahatishi katika kukamilisha mambo yake kwani binti huyo licha ya kusomea mambo hayo ya urembo pia ni



    mzoefu na ni dada binamu yake.Akanambia kesho dada huyo atapanda ndege kutoka Dar na kuja Moshi kwa ajili ya kazi hiyo.Akanileza pia kuwa amepanga



    kuwa nitakuwa na binti huyo kwa mda wa wiki moja ili kumuelekeza mazingira ya hapo salooni kwangu.Sikutaka kumpinga kwa sababu alionesha kuwa



    alishajipanga sana kuhakikisha hayo yote yanafanikiwa. Pia nisingeweza kutia neno lolote mpaka hapo nitakapo muona huyo Husna ambaye alikuwa



    akizungumziwa.



    Mark akaendelea kujitapa kuwa yeye huwa habahatishi katika kukamilisha mambo yake kwani binti huyo licha ya kusomea mambo hayo ya urembo pia ni



    mzoefu na ni dada binamu yake.Akanambia kesho dada huyo atapanda ndege kutoka Dar na kuja Moshi kwa ajili ya kazi hiyo.Akanileza pia kuwa amepanga



    kuwa nitakuwa na binti huyo kwa mda wa wiki moja ili kumuelekeza mazingira ya hapo salooni kwangu.Sikutaka kumpinga kwa sababu alionesha kuwa



    alishajipanga sana kuhakikisha hayo yote yanafanikiwa. Pia nisingeweza kutia neno lolote mpaka hapo nitakapo muona huyo Husna ambaye alikuwa



    akizungumziwa.

    Hapo pia alitumia hiyo nafasi kuniulizia zaidi ile idea ya stori ya filamu niliyomtumia.Ilibidi nimwambie tu ukweli kuwa ile idea ni ya Eliado mtunzi maarufu



    wa love stories.Basi akanambia haina shida kwa sababu na yeye yupo kwenye sanaa na hiyo idea ni nzuri na ameipenda hivyo basi anaomba siku inayofuata



    tufanye mpango tuonanae naye hili tuone tunachanganya vipi idea ili tuweze kupata kitu kizuri zaidi.Kwa kuwa tulikuwa tumechoka sana tulijikuta tumepitiwa



    na usingizi na kulala fofofoo. Hata yale mawazo yangu kuwa eti usiku nitampandishia mapaja ili adate na kunitimizai haki yangu hayakufanikiwa tena.Maana



    nilikaaj kushituka ilikuwa tayari pameshakucha.Kweli huyu mwanaume ni kiboko maana tulilala mpaka asubuhi bila kufanya lolote.Hii inanikumbusha ile siku



    ya kwanza kabisa ya mimi na yeye kuonana.

    Kwa hiyo siku ndo ikawa imenza hivyo.Nilitamani nisiende kazini lakini sikuwa na jinsi ilinibidi niende tu japo kwa kuchelewa.Nilimuaga na kumuacha Mark



    akiendelea kuupiga usingizi. Cha ajabu tofauti na nilivyotarajia siku hiyo kuwa nitakua boadi kwa sababu Mark alishindwa kutoa maugwadu yangu



    niliyoyarundika kwa mda mrefu siku hiyo nilijihisi mweneye furahaa sana. Kitu kilichokuwa kinanipa sababu za kutabasamu ni yale mawazo mazuri ya Mark



    mawazo yenye tija, chachu na shauku ya maendeleo.

    Niliingia kazini na kabla ya mambo yeyote niliamua kumpigia Eliado ili kumuomba appointment ya kuonana naye ili tupange vizuri kuhusu script ya filamu.Basi



    alinambia kuwa asubuhi yupo bize sana ila tunaweza kuonana kuanzai mida ya saa nane mpaka saa kumi jioni. Na nilimuuliza tutaonana wapi akanambia



    itakuwa vizuri kama tuataenda ofisini kwake. Ikabdi mimi niendeleee na shughuli za hapo saluuni huku nikitafuata njia ya kuwatoroka ili niende nyumbani



    nikapumzike kwa sababu siku hiyo nilikuwa nimechoka sana. Nilizugazuga hapo mpaka saa tano kabla ya kumuaga Waridi na kumuambia kuwa sijisikiii vizuri



    hivyo naenda kupumzika tuataonana jioni. Waridi kama kawaida yake hakuacha kutia neno akanambia kuwa ni haki yangu kwenda kupumzika kwa sababu



    inaelekea kazi ya jana usiku na Mark ilikuwa ni kubwa sana.Ilinibidi nicheke na kusema laiti angejua kilichotokea usiku huu anagenyamaza tu kimya.

    Nilienda ghetto kwangu na kulala na nilikuja kushituka saa saba mara baada Mark kunipigia na kuniuliza tunaenda kula wapi. Nikamwambia popote anapotaka



    yeye ila mimi niko nyumbani anifuate hapo.Basi mda mchache baadaye alifika hapo akiwa na gari ya rafiki yake. Tuliondoka na kwenda sehemu moja inayoitwa



    changbay na hapo tulipata msosi wa nguvu na baada ya hapo tulienda moja kwa moja kwenye ofisi ya Eliado ambayo ilikuwa katikati ya mji.Tulifika na



    tulimkuta akiwa na mteja wake ambaye nazani alikuwa akimpa ushauri.Alituambia anatuomba tumpe kama dakika 15 hivi kisha atamalizana na huyo mteja kisha



    atakuja kuonana na sisi.Kweli baada yam da huo tulionana na kila mtu alikuwa na furaha sana kuonana na mwenzake.

    Tulisalimiana na moja kwa moja tukaanza kujadili kilichotupelaka pale.Mark alimuuelza kuwa amefurahishwa sana na mwanzo mzuri wa ile stori lakini pia



    angependa kujua nini kingefuata mara baada ya Jimmy na Yule binti mrembo kuonana. “Ujue Mark kwa uzoefu wangu filamu ambazo zinaelezea maisha ya watu



    wawili huwa zinavutia sana kama tu kutakuwa na flashback ya kila mmoja wao.Kwa sababu title yenu inasema LET ME LOVE YOU hapo ina maana kuwa



    lazima kuwe na sababu za wahusika kufikia hatua hiyo na sababu ya msingi ninayoiona mimi ni historia ngumu ya mapenzi ambayo kila muhusika atapitia kabla



    ya kuyachukia mapenzi.Lakini pamoja na historia hiyo bado anapata mtu ambaye anampenda na anampa sababu za kusema LET ME LOVE YOU.Aliendela



    kufafanua Mr Eliado ufafanuzi ambao ulimfanya Mark kutingisha kichwa kuonesha anakubaliana na hiyo idea asilimia mia moja.

    Mark akasema haoni haja ya kutafuta zaidi cha msingi yeye ataenda kuiandikia hiyo stori script ya filamu jinsi itakavyokuwa na jinsi wahusika



    watakavyoicheza.Eliado alisema pia kama idea hiyo itakuwa ngumu basi tumpe mda atunge stori ingine ambayo itakuwa rahisi kidogo kucheza.Hapo Mark



    akasema hii ni nzuri sana labda kama utatutungia ya filamu ingine ila hii mimi nimeikubali kwa zaidi ya mia moja. Basi kwa kuwa mwandishi huyo alikuwa na



    kazi nyingi sana tulifanya makubaliano ambayo yalihusisha malipo na Mark kwa jinsi alivyokuwa amemkubali alimuandikia cheque na kumwambia hiyo ni



    advance tu atampa asilimia kumi ya malipo ya filamu mara baada ya kuingia sokoni.Mark nilimpendea hapo kwa sababu siku zote alipenda kugawa riziki kwa

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    watu wengi.Na siku zote mimi na amini kuwa ili ufanikiwe lazima ukubali kushirikiana na watu wengine tena kwa kuwapa hicho kidogo utakachopata.

    Tuliaga na kuondoka zetu na tayari yule dada niliyeambiwa kuwa amepanda ndege kutoka Dar es salaam kuja Moshi kwa ajili ya kusimamia kazi ya saloooni



    alikuwa ameshafika hivyo tukapitia stendi kumpokea. Jamani mwacheni mungu aitwe mungu huyu dada alikuwa ni mrembo sana mapka nikamtamani.Alikuwa



    ni mwembamba mrefu na pia mwenye sura nyembamba kama mdoli.Alijaliwa macho ya kipekee sana na sauti yake ndo ilinifurahisha zaidi yaani utafikiri ya



    mtoto mdogo.Alafu alikuwa na babaface na mambo ya kizungu zungu hivi.Akitembea ndo utapenda hayo madaha yake utafikiri twiga anayetafuta maji au nyasi



    laini.Alikuwa akinyata kwa kweli.Kweli hata mimi nilimkubali tu siku ya kwanza ingawa bado nilikuwa sijajua ufanisi wake wa kazi.

    Nilikaa nae hapo kwangu kwa mda wa siki tatu huku asubuhi tukiamka na kuendelea na kazi.Ndani ya mda huo nikagundua kuwa alikuwa na uzorfu mkubwa



    sana hivyo kazi hiyo alikuwa akiimudu kabisa.Hapo sasa nilimkubali sana Mark na ile kauli yake kuwa yeye huwa hafanyi makosa katika kufanikisha jambo



    alilodhamiria.

    Basi nilitumia mda huo vizuri kuweka mambo yangu sawa ili nikienda Dar niyaache yakiwa shwari kabisa.Niliamua kwenda Arusha kumsalimia yule mtoto wa



    Joyce ambaye alikuwa akisoma shule ya boding.Pia nilimtafuta baba yake nikamsalimia na kwa kuwa niliongozana na Mark basi nilimtambulisha kuwa huyo ni



    mume wangu.Tulimaliza shughuli za huko na tulirudi zetu moshi tayari kwa kuondoka na kuelekea Dar es salaa. Sikusita pia kwenda kumsalimia mama yake



    mdogo na Joyce ambaye kwa sasa ndo nilikuwa namchukulia kama mama yangu na kila mwezi nilikuwa nikimtumia hela ya kula.Na yeye nilimtambulisha kwa



    Mark na kumuelezea nia yetu ya kutaka kuona





    Tupo ndani ya Dar es salaama jiji la maraha na karahaa. Maisha mapya yameanza huku mimi na Mark tukiishia kama mke na mume lakini kamwe alikataa



    kushiriki tendo la ndoa.Kila siku alisisitiza kuwa tutaenda kupima afya lakini ikifika siku hiyo Mark huwa anajifanya yupo bize hivyo tuliendelea na maisha ya



    kila siku ya kutafuta hela.Mark alitumia mda wake mwingi sana kunitambulisha mimi kwa marafiki zake na ndugu zake. Mark alinifanyia tena kipart cha



    kunivalisha pete kama kile alichonifanyia Dar es Salaam na safari hii licha ya marafiki zake pia walikuwepo ndugu zake na wazazi wake.Hii sasa ndo naweza



    kusema kuwa ndo ilikuwa ni Engagement Day kwa sababu hata mama mdogo wa Moshi tulimtumia nauli kuja kushuhudia swala hilo.



    Pia Waridi yule dada wa saloon alikuja na Marry pia yule mdogo wake Joyce hivyo hao ndo walitambulishwa kuwa ni ndugu wangu.Sikuwa na jinsi kwa sababu



    kwa kweli nilikuwa sina ndugu zaidi ya hao hivyo nilikubaliana na matokeo.Baadaye wote hao walirudi Moshi tenalkwandege hivyo kuwatengenezea historia



    maana hakuna hata mmoja aliyewahi kupanda ndege.Hapo sasa nikawa na uhakika kuwa Marka atanioa.



    Tulianza kufanya kilichotupelaka Dar es salaam si unakumbuka pia pamoja na mambo ya kuwajua ndugu jamaa na marafikia lakini pia ilikuwa ni kwa ajili



    kucheza ile movie ya LET ME LOVE YOU.Mark alianza kunifundisha vitu muhimu ninavyotakiwa kuvijua kabla ya kuiingia kwenye tasnia hiyo ya filamu ikiwa



    ni pamoja na kunipeleka kwa mwalimu wa wa chuo cha sanaa cha kaole ambacho kipo bagamoyo. Mwalimu huyo nilikutanishwa naye ili aweze kuniambia vitu



    muhimu vya kuvijua na kuvifanya kabla sijaingia kwenye tasnia hiyo ya filamu.Nakumbuka swali la kwanza aliloniuliza mwalimu huyo ni je nilishawahi kuwa a



    ndoto ya kuigiza fialmu hapo kabla?Nilijibu swali hilo kwa harakaharaka kuwa ndio nilishawahi kuwa na ndoto hiyo na ndoto hiyo imechagizwa na kutiwa



    chachu na Mark.



    Kama kweli una ndoto hiyo kitu cha kwanza na cha muhimu kukijua ni kwamba ndoto hiyo ili ifanikiwe na kuwa kweli ni lazima niwe tayari kujitoa, kujifunza



    na kutenga mda mwingi kwa ajili ya kazi hiyo na pia niwe na shauku ya kujua mambo muhimu yanayohusu tasnia ya filamu. Akanambia kuwa wapo watu wengi



    wanaifanya kazi hiyo lakini hawahifanyi kwa ufanisi kwa sababu hawana mafunzo na hawataki kujifunza. Ujue kipaji ni asilimia chache sana zinazomfanya mtu



    awe muigizaaji bora aliendela kusema mwalimu huyo. Aliongeza kuwa juhudi na bidii ya kujifunza na kujua mazingira yanayokuzunguka ili kuweza kucheza



    filamu ambayo itagusa maisha ya jamii inayokuzunguka ni jambo la muhimu sana.



    Nilitega sikio kwa umakini ili kumsiliza mtaalamu huyo amabye alikuwa pia ni professor wa mambo ya sanaa. Basi akaendelea kunielezea vitu vichache vya



    kuzingatia labla ya kuwa muuigizaji. Hatua muhimu aliyoniambia ni “Learn How to Act”(jifunze jinsi ya kuigiza).Siku zote ni muhimu kujifunza kama unataka



    kufanikiwa kiurahisi.Kwa hiyo alinishauri kama nina mda basi niende kusomea fani hiyo iwe kwa kozi fupi au kwa semina.Kitu cha pili alichokisisitiza ni



    location. Alinambia kwa kimombo kuwa “if you hope to work in film as an actor you need to go where the work is. Hapa alikuwa na maana kwamba kama



    napenda kuwa muigizaji wa filamu ni vizuri nikaenda kuishi sehemu ambapo kazi hizo zinafanyika kwa urahisi.Alinitolea mfano kuwa filamu nyingi za Canada

    CHANZO:  https://deusdeditmahunda.blogspot.com/

    na miji mingine ya Marekani zote zinachezwa Los Angles na New York.Kwa hiyo alisisitiza kwa Tanzania Dar es salaam tayari imepiga hatua katika tasnia hiyo



    na filamu nyingi zinafanyika Dar es salaam.



    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog