Search This Blog

Thursday 24 November 2022

NINGEFANYA NINI - 5

 

     



    Chombezo : Ningefanya Nini

    Sehemu Ya Tano (5)

     

    "Mtumeee" nilipiga kelele mikono nikaweka kichwani nilianza kulia kwa sauti, Rajabu alikuja na kuniuliza vipi alijua nimezidiwa



    "Lameck jamanii Lameck, uwiiiii Lameck wangu umepatwa na nini wewe" aisee asikwambie mtu nilikuwa kama chizi niliinuka nikafungua kabati la nguo na kuanza kutoa natupa chini



    "Wewe vipi umechanganyikiwa au?" Rajabu aliniuliza



    Sikumjibu nilikuwa nikitafuta nguo gauni la heshima niweze kuvaa nitoke, nilipolipata nilivaa na kutaka kutoka, Rajabu akaniwahi

    "Embu niambie kuna nin?"



    "Lameck kafa! kafa! kafa jamani ameniacha" nilijikuta naongea tu hapo nikaanza kuona umuhimu wa Lameck nikatamani hata nimuone ili nimwambie yaishe nibaki nae asife,

    "Sasa unataka kwenda wapi? Kwanza una uhakika gani kama kafa?"



    "Nimeona status niache niende kwao" nilifanya fujo, nilihisi kuchanganyikiwa kwa wakati ule





    "Nimeona status niache niende kwao" nilifanya fujo hizo, nikachomoka na kuondoka

    Nilifika hadi alipokuwa akiishi Lameck nilikuta watu wamesharudi kuzika, yaani jamani usiombe yakukute niliishiwa nguvu hata za kutembea, nilipiga magoti na kuanza kulia, nilitamani kila kilichotokea kiwe ndoto niamke tu mwenzenu, kufiwa kunauma kiukweli japo nilimkosea Lameck lakini kilio changu kilitoka moyoni, watu walisogea na kunishika huku na huko, wakaniingiza ndani

    Niliwaona wazazi wake Lameck nao walinitambua kwani tulikuwa tukijuana kupitia picha, nilivyolia ndo nilimfanya mama Lameck nae alie upya, nilimsogelea akanikumbatia

    "Mwanangu ajali imemchukua, alinipigia simu akaniambia mama njoeni Tanzania na baba nataka kuoa kwa haraka msichelewe, kumbe ndo alikuwa anatuita ili tuje kushuhudia kifo chake, ungetulia nyumbani basi mwanangu labda yasingekukuta, Aisha yupo hapa umemuacha mwenyewe mke wako" yule mama aliongea kwa masikitiko huku akilia, hapo nikatambua kuwa Lameck kafa kwa ajali hapo nami nikazidi kulia

    Basi tulibembelezwa tukanyamaza, nilikuwa mpole sina hata raha nikajiinamia, mara nilihisi mtu kanishika mkono niliinua uso na kumuona rafiki yake Lameck, aliniinua tukaenda nje pembeni kabisa

    "Pole kwa msiba lakini hutakiwi kulia tena, Lameck ameshaenda ila tambua haya ni makosa yako Aisha, nilionana na lameck mara ya mwisho baada ya kutoka kwako na kuniambia yote uliyomfanyia, wewe sio wa kumfanyia vile ndugu yangu kiukweli umemuumiza sana, aliniomba nikupigie simu nimsaidie kukubembereza lakini hukupokea, akasema basi muache kama hataki, kisha akaniaga, saa saba usiku napokea simu na kuambiwa Lameck amepata ajali mbaya, ni kwasababu yako"

    Alinilaumu nikaanza kulia na kurudi ndani kiukweli niliumia nikajiona nina hatia, sasa nitafanya nini maji yamesha mwagika

    Siku hiyo nililala hapo hapo matanga yakaisha watu wakaondoka, nami niliwaaga wazazi wa Lameck kuwa nae

    "Sawa ila tuna maongezi na wewe lakini ngoja kwanza tukae kikao cha familia kisha nitakupigia simu uje" alisema baba Lameck basi niliaga walinipa na pesa kidogo ambazo zilikuwa za rambirambi nikaondoka,

    *******

    Nilirudi nyumbani nikiwa sipo sawa kivile, Rajabu alininunia baada ya kukaa kule msibani

    "Ushatoka kumzika bwana ako ukaona ukae wee mpaka mmalize 40 kabisa" alisema hivyo kwa kunikejeli kwani nililala siku mbili tu, hivyo hata 40 haijajulikana itakuwa lini

    Sikumjibu kitu niliingia bafuni nikaoga kisha nikachukua nguo nyingine na kuvaa, mara simu yangu ikaita alikuwa mama Lameck nilipokea haraka na kumsikiliza

    "Mwanangu itabidi kesho uje tuongee, Lameck aliwahi kutuambia kuwa wewe ni mjamzito sasa tushakaa kikao itabidi tuzungumze"

    "Sawa mama kesho nitakuja" nilimkubalia na nikapangiwa muda wa kwenda

    Ilipofika siku ya pili sikwenda kwani sikuona umuhimu ikiwa mimba nilishatoa kwanza niliwaza nitaenda kusema nini, basi nilipigiwa simu sikupokea, nikamwambia Rajab kuwa wazazi wa lameck wanataka waongee na mimi kuhusu mimba akasema hakuna kwenda watumie msg waambie huna mimba, kiukweli sikutuma msg niliogopa

    Zilipita siku mbili nikabadilisha na laini ili kukwepa usumbufu wao, nikiwa nimekaa sebuleni mlango uligongwa nilifungua na kumuona rafiki wa Lameck na wazazi wa Lameck nilishtuka





    Zilipita siku mbili nikabadilisha na laini ili kukwepa usumbufu wao, nikiwa nimekaa sebuleni mlango uligongwa nilifungua na kumuona rafiki wa Lameck na wazazi wa Lameck nilishtuka



    Sikutaka kujua wamepajuaje kwani yule shemeji yangu alipajua vizuri, niliwakaribisha na kuwasalimia



    "Aisha upo sawa wewe?" Baba Lameck aliniuliza



    "Ndio baba"

    "Tumepata wasiwasi kwenye kikao hatujakuona, pia simu yako haipatikani, tukamuomba Denis atulete kwako tulihisi una matatizo" mama Lameck aliongea kwa upole



    "Simu yangu imeharibika pia nilikuwa sipo sawa" nilijibu, wakati huo Rajabu alikuwa chumbani anasikiliza kwani niliweza kuona kitasa cha mlango kikicheza lakini baadae kikatulia, nilijua fika alitaka kutoka lakini katulia



    "Sasa mwanangu kama tulivyokwambia ile majuzi, taarifa kuhusu kuwa na mimba tunazo, kwasasa wewe ndo faraja yetu pamoja na mtoto aliyekuwa tumboni, tumeona tukuchukue ili twende wote London ukaishi huko, uangalie hali yako mpaka utakapo jifungua" waliniambia hivyo, nilishtuka maana sikujua niwaambie nini, nilitamani siku moja kwenda nchi kama hiyo lakini naona ndoto zimefifia



    "Mbona kimya kwani una hofu ya nini mkwe?" Aliuliza baba Lameck,



    Mara Rajabu alitoka na kusalimia



    "Nimesikia kila kitu mlichoongea huyu haendi popote ni mke wangu, alishachana muda na mtoto wenu pia hiyo mimba ilishatoka kwahiyo muacheni" aliongea na kuwafanya washtuke mimi nilihisi ganzi mwili mzima



    "Anachokisema ni kweli?" Mama aliuliza



    "Wee mama kwani huamini au? Haya nenda kampime kama utakuta mimba nendeni, kwanza inukeni muondoke huyu mke wangu sitaki muongee nae" alisema na kunitaka mimi niingie chumbani



    Nilimuomba asiwafokee watu wazima lakini hakuelewa, basi ikabidi wale waondoke na kuomba samahani kwa usumbufu, walisema hawajajua kama mimi nimeolewa, walikuwa ni watu wastaarabu na wapole nilijikuta nikiona aibu na makosa yote niliyabeba mimi, walivyoondoka tu nikamsogelea Rajabu



    "Kwa nini huna adabu wewe, huoni kama umenidhalilisha? Unataka mimi niishi maisha gani, kila mtu unataka anichukie?" Niliongea kwa hasira, basi hiyo siku tuligombana sana,



    Ulipita mwezi mmoja tukiwa watupatani kivile, pale kodi iliisha akakataa kulipa nikatoa akiba zangu na kulipia,



    Siku moja nikiwa napika, mara nilisikia, simu ya Rajabu ikiita nilishangaa kwanini haipokelewi kumbe hakuwepo ila aliweka chaji, nilitoka na kwenda kupokea nikakuta ilishakata, niliangalia na kukuta msg, jina habiba nikalikumbuka lile jina ni mwanamke wake wa muda mrefu alitakaga kumuoa aliandika hivi



    "Hupokei simu kwanini mimi Nina shida na pesa nataka niende hospital"

    Basi nikaingia na shauku ya kusoma na msg za nyuma



    "Mpaka sasa mimba inaingia miezi sita hutaki kuja hata kuniona"



    "Najua pia natamani kukuona lakini huku namalizia nyumba yetu nikuchukue tukae wote usione kama mimi sikujali" Rajabu alijibu hivyo



    Huwezi amini nilianza kutetemeka mikono, sikutaka kuendelea tena kusoma msg nyingine, nilirudisha simu pale pale





    Basi niliacha kusoma ile msg na kukaa kwenye sofa, nilisikia harufu kama mboga inaungua lakini sikuweza kwenda kuishughulikia nilikasirika haswa



    "Wee Aisha usikii kama mboga inaungua au?" Alisema Rajabu baada ya kuingia ndani



    Nilikaa kimya akanifuata na kuniuliza tena, nikampa bonge la Kofi



    "Kwani kama unasikia Mboga inaungua kwanini usiende kuiokoa, au mpaka niende mimi? Wewe huwezi au umezoea kusumbua wenzio?" Nilimwambia kwa hasira huku nikimtolea macho,



    "Yaani kukwambia mboga inaungua ndo unipige kofi?" Alijikuta nae akiniuliza kwa hasira huku akiwa ameshika shavu ujue kofi la kushtukiza linauma jamani



    "Sikia wee Malaya wa kiume, nishajua kama umempa mimba huyo kenge wako, nimeona msg zote unanifanya mimi mjinga eh? Hivi wewe unasahau nimekufanyia mangapi mimi? Mbona huna fadhila wewe? Kukupenda kote nikakupa kila kitu alafu unanifanyia ujinga" nilizidi kupandisha hasira



    "Haya tufanye ushajua ukweli kwahiyo unaamuaje tunaachana au?" Aliniukiza kwa dharau nilikasirika nikataka kumpiga kofi tena akanidaka mkono



    "Nitakupiga usinione mimi fala nitakuvunja nalwambia" alisema na kunisukumiza kwenye kiti



    "Nataka kuonana na huyo kahaba wako anatoa hiyo mimba?" Nilisema kwa hasira akaanza kunicheka



    "Wewe umechanganyikiwa eeh mimi nimtoe mwanamke wangu mimba? Utanitafutia mtoto wewe? Kwanza huna kizazi utanizaliaje?" Aliniambia



    "Na ile mimba uliyonitoa iliingiaje kama sina kizazi labda wewe ndo huna kizazi kwasababu sikuwahi kubeba mimba yako hata siku moja" nilimwambia na mimi kwa kumkashifu ili ajisikie vibaya, akacheka



    "Pole sana yaani wewe kuzaa sahau kabisa ushatoa mimba na kizazi ushatolewa chote kama ulikuwa ujui ndo nakwambia na nilikuwa nakufichia siri ila leo ndo nakupa ukweli maana jeuli" alivyosema hivyo nilishtuka sana nilipiga kelele na kulia, nilianza kumtukana Rajabu akawa ananipiga alinipiga mpaka nilihisi kuchanganyikiwa nilianza kupiga kelele nakufa mara nyingi, nguvu ziliniishia kabisa sikujielewa tena



    Jioni niliamka na kujikuta nipo hospital pembeni yangu kulikuwa na wanawake wawili wamekaa na mwanaume mmoja, nilipowaangalia nikagundua ni majirani zangu pale nilipopanga, waliniambia kuwa walisikia kelele walipokuja ndo wakanikuta tayari nimezimia Rajabu alitoka nje na beg lake la mgongoni akakimbia, mimi wakanipeleka hospital

    ITAENDELEA



    CHOMBEZO- NINGEFANYA NINI?

    SEHEMU YA 31

    Jioni niliamka na kujikuta nipo hospital pembeni yangu kulikuwa na wanawake wawili wamekaa na mwanaume mmoja, nilipowaangalia nikagundua ni majirani zangu pale nilipopanga, waliniambia kuwa walisikia kelele walipokuja ndo wakanikuta tayari nimezimia Rajabu alitoka nje na beg lake la mgongoni akakimbia, mimi wakanipeleka hospital



    "Asante kwa msaada wenu" niliwashukuru



    "Kwani ilikuwaje?" Mmoja aliniuliza hapo nilianza kutoka na machozi



    "Wanaume wabaya sana jamani" niliwahusisha wanaume wote wakati aliyenitenda haswa alikuwa ni Rajabu



    Walinimbembeleza nikatulia, basi kwa kuwa yule jirani yangu alikuwa polisi aliniambia atanisaidia kufungua kesi,



    Tangu siku hiyo sikuwa sawa, nilikuwa nawaza kila siku, kilio ndo ilikuwa sehemu kubwa ya maisha yangu, kuweza kula vizuri nilianza kukonda, homa zilikuwa haziishi, nikaenda hospital na kupima nikagundulika nina virusi vya ukimwi, nilijua kabisa lazima niliambukizwa na Rajabu maana alikuwa hajatulia, nililia sana siku hiyo, dokta akanishauri na kunitia moyo, alinitaka niishi kwa matumaini pia nianze dozi



    Nilitoka pale hospital na kusimama nje, nikimkumbuka Lameck nikaanza kujuta kwa kila jambo nililomfanyia, nilitamani nimuombe msamaha lakini nitamuombea wapi, Lameck ameshafariki tena bila kunisamehe, nilianza kupiga kelele huku nakimbia ovyo kama mtu aliyechanganyikiwa watu walinishangaa nikaanza kuwatukana tu,



    "Mnaniangalia hamnijui? Waone kwanza misura mibaya kama ng'ombe" niliwaambia na kuendelea kukimbia tena,



    Basi nilikuja kupata akili ya kumtafufa Rajabu, niliamua kwenda kule tulipokuwa tunajenga majohe, ilikuwa ni nyumba ya vyumba vitatu, sebule, dining na jiko, choo kilikuwa cha ndani, nilikuta nyumba ilishaisha kila kitu, ilibaki rangi tu nje, lakini ilionyesha tayari kuna watu wamehamia, nilishangaa na kujiuliza nani anaishi pale



    Niligonga akatoka msichana mwenye mtoto mdogo, sikuweza kumjua hata nilipomuangalia



    "Wewe ni nani hapa?" Nilimuuliza



    "Mimi ndo mwenye hii nyumba" alinijibu



    "Umeinunua hii nyumba au? maana sikuelewi hii nyumba ni ya kwangu alafu ilikuwa haijaisha vizuri nashanga nakuja nakuta mtu anaishi" niliongea nikiwa nishaanza kuhamaki



    "Jamani hii nyumba ya mume wangu, yeye alinunua kiwanja na kuanza kujenga, sasa unavyosema yako sikuelewi"



    "Huyo mume wako yupo wapi, nataka kumuuliza nani kamuuzia hapa" nilisema



    "Ngoja nimuite" aliita akiwa pale pale mlangoni, punde mwanaume akatoka, sikuamini macho yangu alikuwa ni Rajabu



    Yaani kama Mungu amenisaidia kunipa ile akili ya kwenda kule majohe



    "Baby huyu mdada kaja hapa alikuwa ana shida na wewe anasema hapa ni kwake" alianza kumuelezea nilivyomwambia



    "Habiba nenda ndani" alisema Rajabu



    Hapo ndo nikagundua kumbe yule ndo habiba mwenyewe niliyewahi kukuta msg zake, yule msichana akatuacha





    "Habiba nenda ndani" alisema Rajabu



    hapo ndo nikagundua kumbe yule ndo habiba mwenyewe niliyewahi kukuta msg zake, yule msichana akatuacha



    "Enhee ulikuwa unasemaje?" Aliniuliza



    "Unaniuliza nilikuwa nasemaje?" Niliuliza na mimi



    "Ndio maana umekuja kwangu sasa sijui shida yako nini?"



    "Hapa ni kwako wewe? Umesahau hiki kiwanja kanunua nani na pesa za kujengea katoa nani? Unajisahaulisha, kwanza kwanini umehamia kwenye nyumba yangu?" Nilimuuliza kwa hasira



    "Wewe usiniletee upuuzi wako hapa, pesa si ulinipa mwenyewe kwani uliniambia nikununulie kiwanja? Ulinipa pesa nami nikaamua kununua kiwanja ili nikijenga niishi na wewe lakini imeshindikana, sasa nini tena unachonitafutia?"



    "Rajabu usinitanie nakwambia, siwezi kukubali uniharibie maisha yangu kiasi hicho, nataka nyumba yangu? Ona umenifanyia mambo mengi machafu, umeniambukiza maradhi, wewe sio binadam" nilimwambia kwa hasira



    "Sasa kama mimi sio binadam kwanini unaniongelesha na hapa unasubiri nini? Ondoka mimi sina shida na wewe tena tushamalizana" aliniambia mara yule mwanamke wake akatoka



    "Kuna nini mbona sielewi nasikia mnagombana tu?" Aliuliza



    "Huyu mwanamke amechanganyikiwa achana nae" Rajabu alimjibu



    "Mimi nimechanganyikiwa? Mwambie ukweli mwanamke wako mimi nani?"



    "Wewe si mbwa tu, ulitaka uwe nani?" Rajabu alisema kwa dharau nikapata hasira



    "Sawa mimi mbwa ila leo ndo utajua kama mbwa koko au kichaa" nami nilijibu kwa kujiamini



    "Jamani embu wee dada ungeenda tu nyumbani kwako" habiba alisema



    "Niende nyumbani kwangu wapi wakati ndo hapa" nilijibu



    "Kwahiyo wewe unatembea na mume wangu na unataka ukae hapa si ndio?"



    "Sina shida na mwanaume wako, labda nikukumbushe tu, tuliwahi kuongea kwenye simu zamani sana siku uliyopiga simu ya rajabu nikaipokea mimi, ukasema wewe ni mchumba wake, sasa tangu wakati ule nilikuwa na Rajabu akanifanyia mabaya mengi huku akikutuchanganya na kama alivyotoka Moro alikwambia anakuja kutafuta maisha basi alikuwa amekudanganya aliishi kwangu na hata hii nyumba ni yangu amejenga kwa pesa yangu, hivyo lazima aondoke na kuniachia kila kitu" nilisema



    "Anhaa kumbe basi mimi siwezi kukutetea wewe uliniibia mwanaume wangu, hivyo kama ukimpa pesa huo ni ujinga wako mwenyewe, acha kutupigia kelele kwanza hii nyumba imeandikishwa jina la mwanangu hivyo siwezi kukubali kutoka hapa, wewe nenda popote" alisema habiba wakawa wameungana



    "Tena ondoka hapa kabla sijakupiga makofi nikuumize" Rajabu alisema



    "Haya nipige, nipige nasema, siwezi kukubali unidhurumu" niliongea kwa hasira



    "Basi nenda unapotaka" alisema habiba nikataka kumzibua kofi Rajabu akawahi wakaanza kunichangia walinipiga mpaka nguo zikachanika, watu wakaja na kutugombelezea, wakanitoa mimi, basi nilistiliwa nguo nyingine na kuondoka



    Nilitafuta sehemu na kukaa pekee yangu na kuanza kulia,



    Yote ni makosa yangu, sikutakiwa kumuamini Rajabu ile siku ya kwanza tu niliyokutana nae, niliona msg akimwambia rafiki yake kuhusu mimi kuwa amenitamani lakini sikufanya lolote, ilitosha kabisa kumuona sio mwanaume sahihi,



    Haikuishia hapo bado Mungu hakuacha kunionyesha ushetani wa huyu mwanaume pale nilipoenda kwao Moro na kunipeleka gest ikiwa ana kwake alafu nikagundua anataka kuoa, kumbe mimi alinichezea nilipaswa kumpotezea pale pale, lakini kwa ujinga wangu nikampa nafasi nyingine wakati tayari nilishakuwa kwenye mahusiano na nilipendwa sana,



    Tamaa zangu za ngono na kutokuridhika kwa Lameck kumenifanya niwe msaliti, hatimae nikaanza kufanya mapenzi kinyume na maumbile bila kufikiria madhara yake, sikutakiwa kurudiana na Rajabu kabisa ikiwa niliachana nae kwa tabia zake chafu, nilimsaliti mtu ambae aliweza kunisaidia nilipokamatwa pia akanitoa kwenye maisha ya mateso na kunipa furaha, pamoja na yote sikumlipa hata jema moja badala yake nikasababisha kifo, kiukweli najutia kila kitu kilichotokea lakini maji yameshamwagika





    Haikuishia hapo bado Mungu hakuacha kunionyesha ushetani wa huyu mwanaume pale nilipoenda kwao Moro na kunipeleka gest ikiwa ana kwake alafu nikagundua anataka kuoa, kumbe mimi alinichezea nilipaswa kumpotezea pale pale, lakini kwa ujinga wangu nikampa nafasi nyingine wakati tayari nilishakuwa kwenye mahusiano na nilipendwa sana, tamaa zangu za ngono na kutokuridhika kumenifanya niwe msaliti,



    Hatimae nikaanza kufanya mapenzi kinyume na maumbile bila kufikiria madhara yake, sikutakiwa kuwa nae kabisa, nilimsaliti mtu ambae aliweza kunisaidia nilipokamatwa pia akanitoa kwenye maisha ya mateso na kunipa furaha, pamoja na yote sikumlipa hata jema moja badala yake nikasababisha kifo,



    Hatimae leo nimeachwa nikiwa sina thamani, sio Aisha yule wa zamani hakuna aliyekuwa akitamani hata kunisalimia, nililia na kuomba Lameck kama ananisikia anisamehe nilianza kuona umuhimu wake sikuacha kumkumbuka, NINGEFANYA NINI?



    Akili yangu ilikuwa ishabadilika, niliwaza kufanya jambo moja kubwa na zito,



    "Lazima wote wafe nitaua tu Mungu atanisamehe, siwezi kukubali maisha yangu yaharibike kisha nikae kimya, nitaua kisha nami nitajiua tu" nilisema na kuanza kutembea nilienda nilipokuwa naishi na kuchukua pesa ilikuwa elfu 30 tu, nilienda kununua petrol, kisha ilipofika usiku kama saa 3 nilitafuta boda boda ikanipeleka majohe hapo nilitafuta sehemu nikakaa mpaka saa Saba usiku nilianza kumwaga ile petrol dirishani mlangoni na iliyobaki nikazungusha kwenye nyumba, kisha nikachukua mjiti nikawasha moto na kuurusha, moto ulianza kupamba nilisikia wakipiga kelele na kutaka msaada nikaanza kuwajibu



    "Kufeni washenzi nyinyi mnajifanya dhuruma eeh sasa mufe tu, tutakutana huko mbinguni" nilisema kiukweli sikutaka kufanya jambo baya kama hilo lakini moyo wangu uliuma yule habiba alikuwa na majibu mabaya kwangu yalinifanya nipanic, unafikiri kwa maumivu na mateso yote aliyonipa Rajabu NINGEFANYA NINI? kuua ndo niliona maamuzi sahihi tu ili kuufanya moyo wangu utulie, wangenipa mali yangu basi tungemalizana ningekubali kuendelea na maisha yangu lakini wote walijitia majeuli,



    Nilianza kusikia sauti ya mtoto nikamuonea huruma sana, kwani hakuwa na hatia, nililia na kaunza kupiga mikelele kama mwehu, watu walijaa na kuanza kuzima ule moto, wengine wakanikamata, nikawa nawapiga na kuwatukana, nikasikia sauti za watu wakisema



    "Hawa wamekufa jamani hawaongei tena"



    Basi nilikuwa nikitukana ovyo na kuwapiga wale watu wasinishike nilianza kuongea ovyo tu



    **********

    Nikiwa nimeamka usingizini nilikuwa nimechoka sana, nilijiangalia na kujiona nimekonda mikono membamba nguo nilizovaa ni chafu mno, nilishangaa imekuwaje, nilipoangalia vizuri palikuwa ni hospital



    Mara akaingia msichana mmoja nilianza kukumbuka alikuwa ni rafiki yangu jesca niliyekuwa nikikaa nae jirani kule Lumo kwa mama zangu, alikuwa ambadilika sana na kuwa mzuri haswa



    "Aisha unanikumbuka mimi?" Aliniuliza

    "Ndio wewe si jesca" nilimwambia

    "Asante Mungu hakika umepona rafiki yangu" alisema



    Nilihisi nimepona ukimwi maana ndo ugonjwa niliokuwa nao



    "Kwahiyo sina virusi tena nimepona kabisa?" Nilimuuliza kwa mshangao



    "Mmhh hata nikikwambia huwezi kuelewa, ila kwa kifupi ulikuwa chizi Aisha" aliniambia hivyo nikashangaa akaanza kunihadithia kila kitu



    Kumbe ile siku niliyomuua Rajabu na familia yake nikapata uchizi kabisa, lakini nilikumbuka kuwa ile siku nilikuwa nikifanya fujo na kutukana watu sikujielewa tena, Kumbe nilichukuliwa na kupelekwa polisi nikikaa miezi sita na baadae sikupewa hukumu yoyote baada ya kuuwa kwani nilipimwa na kuonekana chizi, nilitolewa na kuanza kuhangaika mitaani nikila ovyo na kulala ovyo,



    Akaniambia pia siku moja akiwa anatoka mini aliweza kuniona k koo nikiwa natembea peku na nguo zikiwa chafu tena zimechanika, aliingiwa na huruma na kupanga kunisaidia, baada ya mwezi alifanikiwa kunikamata na kunifunga mikamba akanipeleka hospital,



    Nilishangaa kwani nilihisi ni jana tu ndo nimeua ila jesca aliniambia ndani ya miaka miwili nilikuwa chizi na leo ndo nimeweza kupata akili zangu baada ya kutibiwa kwa muda mrefu na kubadilisha mahospita



    Nilianza kulia upya moyo uliniuma, hakika nilidhalilika sana, tamaa zangu zimeniponza nimekuja kusababisha mtu aliyenipenda kafa, pia nikajikuta nakuwa muuaji bila kutarajia na kuua kiumbe kisichokuwa na hatia yule mtoto mdogo, nilitoa mimba na mwisho nikapoteza uwezo wa kuzaa, nimepata maradhi makubwa kutokana na kuingiliwa kinyume na maumbile sasa navakishwa pempas kama mtoto mdogo, uzuri wangu wote umekwisha, hakuna mwanaume atakayenitaka tena sina thamani,



    Mpaka sasa jesca ndo mtu pekee aliyenipa msaada, nipo kitandani siwezi kufanya chochote kile, niliweza kumuomba jesca aniitie mtunzi anayeitwa Lissa wa mariam ili niweze kumpa historia ya maisha yangu na aweze kuipost watu wajifunze wasiwe na tamaa kama mimi, ningetulia na Lameck pengine leo ningekuwa mama mzuri na wa kuigwa ila nimekuwa mbaya sifai kuigwa na jamnii



    Kwasasa nasubiri siku yangu ya kufa tu ikaribie maana hali yangu ishakuwa mbaya



    *****MWISHO****

     

     

0 comments:

Post a Comment

Blog