Search This Blog

Thursday 24 November 2022

WAPANGAJI WENZANGU - 2

 

     

     



     

    Chombezo : Wapangaji Wenzangu

    Sehemu Ya Pili (2)

     



    Sasa tukija huku nyumbani, tunamwona Zahra analalama mno, na dada yake alikuwa kipau mbele kumsema

    "yaani dada.... ayub ana mwezi sasa hata simu hajanipigia"

    Aliongea Zahra huku dada yake akisema

    "kama umeshampa mwili wako, hio ndio basi tena"

    Aliongea fatuma au mama said,...

    "sijampa bado"

    Zahra alidanganya lakini ukweli ni kwamba tayari keshampa utamu wake, tena alijiachia mno mana alijua ndio mume wake, kumbe nyodo zake ndio zimemponza, na kujikuta analiwa na mbeba mizigo... Na yeye anajua ni tajiri mzuri tu...

    "au labda atakua kasafiri kibiashara"

    Aliongea dada yake huku Zahra akijibu

    "labda itakuwa... Lakini kama kasafiri, ina maana hata simu pia haifanyi kazi"

    "sasa zaru mdogo wangu.. Kama mtu kasafiri nje ya nchi hio namba tapigaje... Kwani wewe ukipiga unaambiwaje"

    "inasema haipatikani"

    "basi atakuwa kasafiri nje ya nchi huyo..... Hebu nenda kalete unga"

    Aliongea dada yake Zahra huku akimtuma Zahra unga,.. Yaani humo ndani unga umeisha hivyo atatakiwa kwenda kiwandani kununua unga... Zahra alichukua pesa, kisha akapanda toyo kwenda kununua unga



    Sasa tukija huku kwa akina abedi na mahmud pamoja na Jeremiah,.. Waliokuwa wakifanya kazi pamoja na kaka yake swalehe,... Ila swalehe yeye hapo kwenye hilo kundi hayupo tena labda wakutane kwenye kazi

    "brooo sasa hivi swai anapiga ndefu"

    Abedi alimwambia hasan ambaye ndio kaka yake swai

    "eehh, naskia sasa hivi yupo Moshi mwezi unaisha huu"

    Aliongea hasan huku wakiendelea kufanya kazi,...

    "ila si anataka kuoa"

    "wacha aoe, si ana kwake bwana"

    Aliongea hasan mana kaishi na ndugu yake miaka mingi sana, hivyo wanajuana vizuri mno...

    "ivi broo,... Tayari umevuta shemeji au.."

    "we shida yako nini kwani"

    "amna... Mana sasa hivi tumeshakua na vyumba vyetu.. Hivyo sio mbaya tuje kumjua shemeji"

    "aaahh badooo... Nilikuwa nataka kila mmoja wenu apate chumba chake... Sioi leo,.. Wacha nile maisha kwanza"

    "ahahahahahaahahahah... Kwahio kumne hukua ukitaka kuoa"

    "ndio.. Nilitaka nanyi muwe na vyumba vyenu sasa"

    Aliongea kaka yake swai,.. Mana aliwatangazia kuwa anataka kuoa hivyo kila kijana ajiweke sawa kuwa na chumba chake,... Kumbe haikuwa kweli



    Sasa tukija huku NMC Zahra akiwa ndio anashuka kwenye bodaboda mana keshafika kiwandani,...

    "shikamoo"

    Zahra alimsalimia mama aliokuwa anauza unga hapo dirishani

    "marahaba... Nikusaidie nini"

    "mama nataka unga wa sembe... Kilo 25"

    "ok...sawa......"

    Mama alitoka ana kumwita kijana mmoja na kumwambia

    "hebu mtume kijana mmoja alete unga wa sembe kilo 25... Haraka sana"

    Aliongea mama huyo kisha akarudi kwa mteja ili apewe pesa, Zahra alilipa pesa ya unga kisha akawa anasubiri.....

    "haraka bwana wewe.... Mpelekee mteja pale"

    Kijana huyo aliokuwa kabeba kiroba cha unga kichwani, alikitua mbele ya mteja ambae ameambiwa ampelekee pale kwenye bodaboda... Lakini sasa Zahra kuna sura aliiona kwa mbaali... Akamuuliza huyo jamaa alioleta unga..

    "Samahani kaka... Eti yule kaka aliobeba gunia la mahindi anaitwa nani"

    "yupi, yule mwenye sweta chafu chafu"

    "enhee yule yule..."

    "yule anaitwa ayub"

    "na ile ndio kazi yake"

    "kwanini unauliza sana dada"

    Sasa Zahra akaona kama vile yuko mbali sana,... Saa ngapi hajaingia ndani pale magari yanapo shusha mizigo...

    "we dada wewe.. Hakuruhusiwi mwanamke kuingia huko"

    "niache... Kama mume wangu yupo huku"

    Zahra hakusikia, alipita hapo getini na kwenda pale wa wabeba magunia, sasa leo ndio anamuona ayub katika uhalisia wake....

    "haaaaaaaaaaaaaaaa Ayubu...."





    Ni ukweli usiopingika kuwa kwa sasa wanawake wamekua ni watu wa kudanganywa kila idara,.. Na yote hio ni sababu yao, mana mwanaume akisema ukweli wa hali yake,.. Mwanamke ni ngumu kumsikiliza na kumpa nafasi katika moyo wake,.. Ni kweli nyinyi wanawake mnavifanya hivyo, hamuezi kutukubali pale tusemapo ukweli wa maisha yetu, hivyo tunalazimika kuwadanganyeni ili tuwapate kimapenzi, na ndio ikawa hivyo mpaka uzao wa kesho, wanawake mtabaki kudanganywa maisha yenu yote, mana mnapenda vitu kuliko mtu... Na sisi wanaume tunalazimika na tutaendelea kulazimika kuwadanganyeni, kwasababu hampatani na ukweli...



    Zahra aliekuwa akijisifu kuwa na mpenzi mwenye maendeleo, na pia aliwahi kumsema dada yake kuwa, pamoja na kuja kwake mjini wa kwanza lakini hakuwahi kupata mwanaume tajiri kama yeye alivyo pata,.. Zahra alijisifu na kujiona mwenye bahati kwa kupata mwanaume mwenye maisha mazuri, tena na zile nyodo zake ndio kabisaa kajiona wa pekee katika dunia..



    Ayubu kazi yake ni kubeba magunia kila kucheapo, ni yeye na magunia... Yeye sio mtu wa kutembea na wasichana wazuri wale wa hiari.. Nikisema wa hiari namaanisha awe demu wake kabisa... Katika pita pita zake ayubu alikutana na Zahra, lakini siku hio hakumsemesha.. Bali moyo wake ulimpenda na hata kutamani kuishi nae kama mke na mume, na uwezo wa kumlisha anao... Lakini katika kufuatilia akagundua kuwa Zahra anapenda wanaume wenye maendeleo, ndipo ayubu Akaanza kujikoki kutoka kwa msimamizi wa kazi anazo fanya... Yaani yule ambaye anawasimamia MAKULI (wabeba mizigo).. Ayub alikuwa tayari kufanya kazi siku nzima kwa bure Ilimradi tu apewe gari la kumtekea Zahra, na ni kweli alipewa na kuanza kumuwinda Zahra,... Mpaka Zahra akaingia kwenye laini akijua amepata mwanaume mwenye hadhi anayo itaka, lakini kumbe sivyo

    Ilifikia mpaka zahanati akajiachia kwa Ayub na kumpa utamu wake,..



    Baada ya Ayub kupata utamu wa Zahra na kujua kuwa sio mwanamke wa kuendelea nae tena mana anapenda makuu,.. Lakini kama angalikuwa hapendi makuu, basi Zahra angeliolewa na Ayub.. Lakini Ayub kaona hapa hakuna mke wa kuoa,.. Sasa kuanzia siku hio aliopewa utamu,.. Kabadilisha line na mazoea nae kaacha, japo kamaliza hata hakiba yake kwa niaba ya Zahra amtafune tu.. Na Zahra akajiachia kwa kujiona kapata na hapo hatoki



    Siku ya leo Zahra anakwenda NMC kununua unga... Lakini kwa mbaali aliweza kuiona sura ya ayub,.. Aliuliza jina na kuambiwa, lakini haikutosha akaona ni bora aingie huko huko kwenye magari yanapo pakia mizigo, na kumuona live bila chenga... Alitahamaki kwa kumuona ni yeye ayubu



    "haaaaaaaaaaaaaa.... Ayubu..."

    Zahra alitahamaki huku machozi yakimtoka... Mana haamini kama kweli huyo ni ayubu

    "nini wewe.... Unaniita unanijua"

    Aliongea ayub huku wabeba mizigo wakijaa hapo, mana ilikuwa ni kiwandani..

    "ayub... Niambie, hii ndio kazi yako au"

    Aliongea hivyo kisha wabeba mizigo wakacheka kweli, na ndio wakajua tayari mtoto wa kike kapigwa changa la macho,..

    "sikiliza we mwanamke... Kwanza nakuona malaya tu... Wanawake wote wanaopenda pesa kwangu ni kama malaya tu mana bila pesa nisingempata, hivyo kwa lugha nyepesi ni kwamba, mnajiuza... Sasa tufanye nilinunua sawa"

    Ayub Aliongea kwa nyodo mno,.. Mara yule msimamizi alikuja tena na ile ile gari,.. Zahra anaona gari aliokuwa anaitumia ayub kila walipoenda...

    "ahsante sana.... Nashukuru"

    "Zahra... Katika maisha ukumbuke kuwa hata tajiri alikuwa masikini,.. Ninacho kushauri mimi kama mteja wako... Kama kweli unataka kuolewa, acha tamaa ya pesa... Hata mimi nilitamani sana kukuoa lakini nimeona sikuwezi kwasababu unapenda vikubwa"

    "sitaki kujua maneno yako mbwa wewe"

    "mimi nikiwa mbwa, basi na wewe utakuwa mbwa... Kwasababu mbwa hawezi kufanya mapenzi na binadamu, lazima afanye na mbwa mwenzie... Hivyo karibu sana kwenye timu ya mambwa"

    Ayub aliongea maneno yaliozidi kumkera Zahra



    "ah ah, ayubu.. Kuna nini hapa mbona kuna malumbano"

    Aliongea huyo jamaa anaye wasimamia akina ayubu...

    "boss... Huyu ndio yule mwehu niliokuwa namtesekea... Yaani huyu ndio aliokuwa anasababisha nafanya kazi bure ili unipe gari nikamteke kimapenzi, na ni kweli kakubali nimekula mzigo hahahahahahahaah"

    "ayubuuu... Basi usimcheke...... Samahani dada, unaweza kwenda, mana hapa ni katika mazingira ya kazi, haturuhu wanawake huku ndani"

    Aliongea jamaa huyo huku Zahra akiwa kanuna karibu kupasuka,... Na hapo hakuwa na ujanja mana yupo kwenye eneo la watu tena wengi wao ni wahuni, na hata ayub ni mhuni vilevile,...

    "waambie na wenzako... Swala la kuolewa sio swala la mchezo... Ni sawa na mwanafunzi wa kidato cha nne kukazana ili aende kidacho tano"

    Aliongea ayub huku jamaa akiingilia

    "ayubuuu.. Hebu fanya kazi bwana.. Alaaaa"

    "amna boss... Awa wanawake wanakera hawa... Sisi tunataka kuoa wanawake wazuri wenye tabia njema tuyaanze maisha nasi tuwe matajiri, lakini wao hawataki kuanza. Wataka kuvikuta tu.. Tajiri nani atakupenda kwa dhati kama hujatafuta nae... Utakula pesa zake lakini ni kwa ajili ya kukutumia tu... Na ndio moja kati ya matumizi ya pesa zake"

    Aliongea ayub huku jamaa akikasirika

    "kwahio unaniambia mimi au"

    "aaahh boss... Nikuambieje wewe bwana..."

    "sasa mtu keshaondoka maneno ya nini sasa"



    Sasa kwa nje huku Zahra alichukua unga wake na kupanda bodaboda kisha huyo akaondoka zake huku akilia sana,... Alipofika nyumbani dada yake alimshangaa sana kwanini anarudi huku akilia,...

    "nini wewe, umeanguka na bodaboda"

    Aliuliza dada yake huku Zahra akiingia mpaka ndani na kujitupa kitandani,.... Dada anazidi kuwa na wasiwasi juu ya kulia kwa Zahra

    "wewe, au kuna simu mbaya umepigiwa toka kijijini"

    Aliuliza fatuma huku Zahra akijibu kwa kutikisa kichwa, kuwa hapana...

    "sasa nini? Hebu amka uniambie vizuri"

    Fatuma alikuwa mkali juu ya mdogo wake, mana alikuwa hasemi na anaona aibu kusema kwa dada yake

    "dada... Samahani sana dada"

    Aliongea Zahra huku akizidi kulia

    "kuna nini lakini"

    "ayubuuu"

    "ayubu kafanya nini"

    Dada anataka kujua huyo ayubu kafanya nini

    "dada... Kumbe ayubu ni mbeba mizigo kwenye viwanda huko"

    Aliongea Zahra... Mara dada yake akaanza kucheka ile mbaya...

    "hehehehehehehehehe halooOOO... Mama wewe, umelivamia jiji mama.. Na mimi nilishawahi kukuambia haya mambo ya wanaume yaache,.. Haya umemuona wapi huyo ayubu wako ambae ni tajiri"

    "tajiri wapi dada Na wakati anafanya kazi za kibega, tena alikuwa anafanya kazi bure ili apewe gari aje anidanganye nalo"

    "heheheheheheheheeh heeeeeee... Mdogo wangu... Ila mimi naamini kila mtu anajifunza kutokana na makosa,.. Nimekwambia mimi mdogo wangu tuliza tako lako hapa.. Anaekupenda atakuona tu.. Haya ona sasa wamejua wewe ni mpenda vya juu... Angalia yaliokukuta"

    Fatuma alikuwa akijiskia raha kwasababu alishawa kumwambia ndugu yake

    "lakini dada..."

    "hakuna cha lakini, hapo tayari umelikosea, lianze upya mama.... Hebju niangalie mimi dada yako, kama ningelikuwa napenda pesa kwa shemeji yako.. Mpaka sasa tusingelikuwa hapa... Mimi nimeanza na shemeji yako akiwa ni mpiga debe pale stendi, na kanificha kazi yake lakini hata nilipokuja kujua... Sikushtuka na wala sikuwaza kumuacha... Kwasababu najua uwezo wa kunilisha anao... Nimekaa naeeee... Mpaka leo ni dereva wa magari makubwa ndio huyo anasafiri kwenda nje za nchi... Sasa hivi tuna kiwanja chetu,.. Akirudi tu, tunakwenda kujenga... Haya niambie, sasa nimtake tajiri wa kazi gani, aje anitese na pesa zake kisa nini.... Mdogo wangu.. Ukipata mwanaume ambae kila siku ana uhakika wa kukuacha hata elfu mbili.. Shikilia mfanye maisha na mtafute zenu... Achana na watu wenye pesa zao.. Sawa tajiri atakupendea tako lako hili.. Lakini kesho atakutana na mwenye sura kuliko wewe,... Atataka kumuoa au hata kumtumia kwa starehe.. Je hujaja kupewa maradhi wewe??... Zahra Mdogo wangu... Matajiri wanapendwa na wengi, usione ni wewe tu unampenda mwenye pesa... Nyie mpo kama mia hivi mnampenda tajiri mmoja... Sasa jiulize kati ya hao mia atamuoa nani... Kua makini Zahra.. Nina imanji utajifunza kwa hili... Karibu tena kwenye ulimwengu wa maisha, mana umesha yakosea, hivyo uanze upya mdogo wangu"



    Fatuma Aliongea kwa kirefu kama kumshauri na kumponda mdogo wake ili jambo hilo lisijirudie tena... Wakati huo Zahra ni wa kulia tu hana cha kumjibu dada yake kwasababu alisha mpa taarifa juu ya wanaume wa mjini...



    Sasa tukijua huku Moshi,... Swai akiwa kazini,... Tena alikuwa akipiga kazi kwa bidii kubwa,

    "aisee... Tupigeni chapu.... Arusha kuna jengo jipya tumeitwa"

    Aliongea fundi huku wakiwa wanamalizia ili kesho warudi mjini

    "acha utani fundi.... Ina maana tunapiga kazi za bandika bandua"

    "kama kawa swai.... Sasa ni mwendo wa kazi tu"

    Aliongea fundi wakati huo swai kashika ndoo ya randi huku akipakalia ukutani,...

    "ebwana eeeehh tushindwe kuendelea wenyewe tu sasa"

    Aliongea Swalehe kana kwamba ana machungu na maisha yake,....

    "na huyo demu wako unaye msemea, kuendelea ni ngumu.... Wanawake wasiojielewa ni chanzo cha kuto endelea ndani ya nyumba"

    "aaahhh usiseme hivyo fundi... Je na wale wanaume walio na starehe, na tuwaweke kundi gani"

    Aliongea Swalehe huku fundi akimjibu

    "usiseme wanaume walio na starehe.. Sema je kaka yangu Hassan tumueke kundi gani.... We unamuona kaka yako alivyo... Kaja mjini lini.. Pale alipo na umri ule hana hata mke.. Tena mimi nikajua nawe utamfuata kaka yako... Ila nimekuona wa maana sana kwakua unazungumzia ishu ya kuoa"

    Aliongea fundi jafe, huku mafundi wote wakichangia mada hio...



    BAADA YA SIKU MBILI KUPITA



    Zahra akiwa nje kibarazani kwao, akiwa anakuna nazi... Mara Swalehe kaingia na ndio anarudi Moshi, wakati huo alikuwa kachoka mno.. Zahra alishtuka kwa kumuona swai, mana ni mwezi toka asafiri moshi kikazi,...

    "swai, Mambozako"

    Heeeee Swalehe alishangaa leo Zahra kamsalimia, wakati yeye anamsalimiaga lakini haitikii.. Leo aliona ni siku njema kwake

    "poa"

    Lakini Swalehe kwa kuchoka aliitikia ti na kuingia ndani, mana anataka kwenda kuoga kisha aandae mambo ya maakuli... Zahra alianza kujipendekeza kwa swai,... Mana ushauri aliopewa na ayub, pamoja na dada yake, aliona swai anafaa.... Swai kachukua maji yake kisha kaingia bafuni.

    "mbona kaitikia mara moja tu.. Au hana mzuka na mimi tena nini"

    Zahra alijiuliza katika moyo wake, mana kaitikiwa mara moja....



    Swai alitoka bafuni ikiwa ni nyakati za jioni saa 12 na nusu za jioni... Hata.. Zahra kamaliza kukuna nazi lakini bado kakaa pale nje akisubiri swai amchangamkie kama mwanzo, lakini swai kapita kama hamuoni vile.. Mara mama Mwajuma huyo

    "haaaaaa swai, umerudi linki babaa"

    mama mwaju alitamani hata kumkumbatia swai lakini akaogopa mana Zahra alikuwepo nje, sasa na yeye ni mke wa mtu, hivyo akionekana watu wataanza kumchulia tofuati

    "Nimerudi leo mama, Shikamoo"

    Alijibu swai huku akimsalimia, na katika vitu mama mwaju havipendi ni kuitwa mama na kusalimiwa shikamoo, lakini hapo kwakua Zahra alikuwepo japo alikuwa upande wa kwao, hivyo mama Mwajuma aliitikia

    "marahaba mwanangu za huko"

    "aahh salama tu"

    "pole na majukumu mwanangu"

    "Ahsante sana mama"

    Mama mwaju anakasirika sana kuskia anaitwa mama.... Zahra aliingia zake ndani lakini mama mwaju akamkimbilia swai na kumwambia,

    "boy... Leo usipike nitakuletea chakula sawa"

    Aliongea mama Mwajuma huku swai akiona Afadhali ata mana alichoka hata kupika asingeweza,.. Mana kachoka mno...

    "sawa mama... Nitashukuru sana"

    "afu hio mama siitaki bwana... Niite jina langu tu... Au kisa nina watoto"

    "we mkubwa wangu lakini mama mwaju"

    "haijalishi"

    Swalehe aliingia zake ndani mana alitamani kwenda kumpumzika



    Ilipofika saa tatu za usiku,... Mara umeme ukakatika,... Zahra alitoka ndani kwao na kwenda kwenye mita ya umeme wakati sio kazi yake kuangalia... Aligundua luku ilikuwa umeishia,.. Sasa alichokifanya Zahra ni kumfuata yule jamaa ambae anachangisha hela ya umeme...

    "hodi"

    "karibu"

    Zahra alikaribishwa na mke wa Januari

    "shkamoo dada"

    "marahaba zaru hujambo"

    "sijambo... Dada nimemkuta shem Januari"

    "ndio yupo.. Karibu ukae"

    "hapana dada... Nilikuwa nataka kuingea nae"

    "sawa kaa hapo nimuamshe"

    Basi Zahra alikaa hapo kwenye sofa akimsubiri Januari

    "haaaa, mbona huwashi taa"

    Januari aliuliza mana alikuwa kalala hivyo hana taarifa za kukatika kwa umeme"

    "umeme umekata, sijui ni luku"

    Aliongea mke wa Januari huku Zahra akidakia

    "shem Januari shkamoo"

    "marahaba... Aahh Zahra, karibu"

    "Ahsante.... Aaahh shem... Nimegundua luku imeisha... Sasa nilikuwa nakuomba nikusaidie kukusanya pesa ya umeme"

    Aliongea Zahra, mana huyu Januari ndie mwenye nafasi ya kukusanya pesa ya umeme kwa wapangaji wote, sasa leo Zahra anataka kumsaidia...

    "ooohhh kumbe luku imekwisha...."

    "ndio"

    "aahhhh sasa wapangaji wenyewe wakorofi, haswa wale wahuni wa vile vyumba viwili vile... Mi naona hutoweza Zahra.. Wacha nikakusanye tu"

    "hapana... Shem... Wewe pumzika tuu.. Na ndio mana sikutaka kukisanya mpaka nikutaarifu... Wacha nikusaidie"

    Wakati mke wa Januari ameanza kuwa na wivu, mana haiwezekani huyu mtoto wa kike aje saa tatu hio na kutaka kumsaidia mume wake kukusanya pesa ya umeme... Wivu ukamjaa mana Zahra ni mtoto mkali kinoma yaani shombe shombe wale

    "mmmhh sawa, jaribu... Ila ukiwashindwa wale wawili, niite... Afu kuna kile chumba cha yule kijana yule mpangaji mgeni... Yule kabla hujaenda angalia pale nje kwake kuna mita ndogo itakuonyesha katumia umeme kiasi gani... Mara ya mwisho palikuwa na yuniti nne... Sasa ukikuta zimezidi, basi mdai zilizo zidi.. Lakini ukikuta ni nne hizo hizo acha"

    Aliongea Januari huku Zahra akiitikia

    "sawa shem"

    Zahra alitoka, lakini sasa cha ajabu chumba cha kwanza kwenda kudai umeme ni chumba cha swai,,.. Sasa kitu cha kwanza akamulika na tochi kwenye ile mita ya swai... Lakini cha ajabu kweli kakuta kuna yuniti nne zile zile,.. Ukumbuke swai alikuwa hayupo, hivyo alilipia hizo nne kisha akaondoka, kwahio ni hizo hizo nne, hazija ongezeka, mana alikuwa hayupo... Zahra alikata tamaaa... Sasa kumbe kuomba kote huko ni ili aingie mpaka ndani kwa swai, akamdai umeme na kumchombeza chombeza huko huko... Lakini sasa kakuta ndio kwanza hazija ongezeka, maana yake hatakiwi kudaiwa umeme.... Zahra alirudi kwanza kwenye chumba chao... Wakati huo ana hasira kweli, mana hako kagiza ndio anataka kukatumia

    "potelea mbali... Hata kama hadaiwi nitakwenda kumdai tu"

    Aliongea Zahra, sasa kama vile anaanza kulazimisha mapenzi kwa swai...

    "alisha sema anataka kuoa... Nimemkubalia lile ombi lake"

    Aliongea Zahra katika moyo  wake na wakati huo anabadilisha nguo na kuvaa kanga moja na chupi tu...

    "wewe, mbona unabadili nguo... Ina maana wataka kulala hivyo"

    Fatuma alimuuliza mdogo wake

    "hapana dada... Nataka kwenda kuoga, naskia joto"

    "mmmhh si umeoga muda ule wewe"

    "joto dada"

    "mmmhh haya bwana"

    Zahra alimaliza kuvaa kisha akatoka sasa nje,... Na chumba cha swai kipo katikati, na sheria ya kudai umeme au maji, lazima uanze mwanzo mpaka mwisho, lakini Zahra anaanzia katikati kwenye chumba cha Swalehe.... Zahra akapumua kwa nguvu kisha akaanza kukinyookea chumba cha Swalehe, na wakati huo kuna giza nene, mana kila mmoja kawasha kibatari chake au sola yake ndani kwake.. Sasa kwa nje kuna giza

    Zahra alijiangalia tako lake, kisha akajitikisa... Akaona kanga inateleza haigandi kwenye tako.. Zahra alikwenda kwenye bomba la maji na kujimwagia maji kwa juma... Ile kanga ikashika mpaka chupi ikaonekana...

    "lazima adate... Tena alivyo mpenzi wa chupi chupi... Mbona atanibaka leo"

    Aliongea Zahra huku akiuelekea malengo wa Swalehe... Sasa ile anafika tu, ghafla na mama mwajuma huyo, wakakutana mlangoni,.. Mama Mwajuma kashika hotpot la chakula... Na Zahra nae kashika elfu tano kama vile keshaanza kukusanya hela ya umeme

    "wewe mtoto wa kike... Haya Usiku huu kwenye chumba cha mvulana na giza lote hili, kulikoni?"

    Mama Mwajuma alimuuliza Zahra,.. Na Zahra nae akamjibu...

    "na wewe kulikoni mke wa mtu, usiku huu kwenye chumba cha mvulana mdogo umefuata nini?"











    Mama Mwajuma akiwa ndani kwake anapakuwa wali,.. Tena kwa makusudi leo kapika wali kuku rost, kaweka chakula kwenye hotpot, kisha akachukua mapaja yote ya kuku na kuyaweka kwenye hotpot lingine,.. Yaani anapelekewa utafikiri ndio baba mwenye nyumba, kumbe ni bwege bwege fulani hivi asiependa makuu.... Baada ya kumaliza kupakuwa alivua nguo zake zote,.. Mpaka chupi... Kisha akavaa chupi nyingine safii mana hapo anatoka kuoga muda sio mrefu,.. Sasa kavaa hio nyingine kisha akachukua kanga nyepesiiiii, akatupia kwa juu... Maashalah, na vile mama Mwajuma ana mtako, mana sio tako, ni mtako haswa... Yaani hata kama mwanaume ni shoga lazima uume usimame kwa jinsi wowowo la mama Mwajuma linavyo tetemeka,..

    "we hadija, laleni haraka sana... Si mumesha kula nyie"

    Asha au mama mwajuma aliwafokea watoto wake wawili, mmoja ana miaka 10, na mwingine ana miaka mitano,... Na watoto hawa wanalala kitanda kimoja kilichopo hapo sebuleni, mana ni vyumba viwili, na watoto wanalala kwenye kitanda aina ya dabodeka, hivyo mama analala mwenyewe kwakua hana mume, ila ni mwanamke mfanya biashara, sema bado hajafanikiwa kujenga... Hao watoto ni HADIJA miaka 10 na SAUNA miaka mitano... Mwajuma mwenye miaka 16 yeye anasoma shule za bweni, hivyo kurudi hapo ni mpaka likizo...

    "sawa mama"

    Hadija aliitikia kisha wakapanda kitandani na kulala,... Hapo mama akaridhika na kubeba mahotpot yake kisha akatoka....



    Wakati huo Swalehe yupo ndani kwake anachati huku anasikiliza mziki, mana umeme umekatika lakini simu yake ina chaji ya kutosha tu, na hapo ndani kwake kuna taa za sola,.. Kana kwamba kuna mwanga kama vile umeme,...



    Sasa huku nje mama Mwajuma na Zahra wamekutana mlangoni..

    "wewe mtoto wa kike... Haya Usiku huu kwenye chumba cha mvulana na giza lote hili, kulikoni?"

    Mama Mwajuma alimuuliza Zahra,.. Na Zahra nae akamjibu...

    "na wewe kulikoni mke wa mtu, usiku huu kwenye chumba cha mvulana mdogo umefuata nini?"



    Aliongea Zahra huku mama Mwajuma akaanza kukasirika na kuona haina haja ya kugombana na huyo mtoto wa kike...

    "mimi huoni nampelekea kijana wangu chakula"

    Mama Mwajuma alijitetea kwa staili hio, na ni kweli kabeba mahotpot ya chakula, hivyo Zahra aliamini ni kweli kabisa...

    "na mimi nakwenda kudai pesa ya umeme, si unaona nimeanza na elfu tano ya kwetu hii"

    Aliongea Zahra huku mama Mwajuma akiamini ni kweli,.. kwahio kila mmoja akaamini kile alicho kisema mwenzie,... Kumbe wote lao ni moja lakini hawajui,.. Sasa mama Mwajuma yeye anajua ishu yake sio ya kitoto itachukua muda, hivyo akamuacha kwanza Zahra aingie...

    "sawa, afu ukitoka basi uje na kwangu uchukue"

    Aliongea mama Mwajuma huku akirudi na chakula chake, na Zahra na haraka zake wala hakumfuatilia mama Mwajuma... Zahra kagonga mlango kisha swai akafungua...

    "nani wewe"

    Alimuuliza kwasababu hakumuona kutokana na giza...

    "ni mimi Zahra"

    "enhee una shida gani saa hizi na giza lote hili"

    Aliuliza swai huku Zahra akijing'ata ng'ata lipsi zake japo swai haoi kwa giza..

    "nimekuja kudai hela ya umeme"

    Aliongea Zahra kisha swai akamuuliza, wakiwa wamesimama hivyohivyo hapo mlangoni, kana kwamba swai yupo kwa ndani na Zahra yupo kwa nje...

    "umeangalia hapo zimetumika ngapi"

    "ndio.. Numeona mbili tu"

    Alijibu Zahra na swai yeye hua hakumbuki kua aliondoka lini na mita yake aliiacha vipi... Sasa swai akaachia mlango na kuelekea mezani kwake ambako kuna pesa zake, lkini alipo achia tu mlango, Zahra kaingia ndani...... Heeeee Zahra haamini kuona vitu vya bei ghali, akiangalia hicho kitanda ndio anachoka kabisa.. Hata yeye mwenyewe hakuwahi kuota kukilalia kitanda kama hicho,... Meza ya kioo, ka TV kake kapo ukutani, chini zulia, jiko anatumia gesi, tena ile kubwa...

    Sasa swai ile kugeuka anashangaa mtu yupo ndani... Hakutaka kuongea

    "haya shika"

    Swai alitoa elfu moja ya umeme ambao katumia

    "mbona ni elfu moja tu"

    "kwani yuniti Za umeme ni shilingi ngapi"

    "sasa ndio unatoa elfu moja jamani swai"

    Zahra Aliongea kwa upole, mara akakaa kitandani,...

    "numetoa pesa ya kiasi changu..."

    Aliongea swai huku kama akimtaka aondoke zake...

    "sasa swai??..."

    "nini"

    "nije tupige pige stori"

    Aliongea Zahra mana mwanamke kumtongoza mwanaume ni ngumu.. Ila anaweza kusababisha atongozwe, sasa ndio anaanza kutafuta njia ya kuja kupiga stori na swai...

    "hapana, nahitaji kulala"

    Aliongea swai huku akiuendea mlango kana kwamba anataka kufunga, maana yake Zahra atoke ili afunge

    "sasa ulale wakati hujala swai jamani"

    "nimesha kula"

    "sasa mama Mwajuma mbona alikuwa analeta chakula"

    "ndio... Na ndio nakisubiri nile"

    "kwaio sasa, lini tutapiga piga stori tukiwa wawili tu"

    "Kiukweli sijui... Afu naomba ukakusanye pesa, mana nataka kufunga mlango mbu zinaingia"

    Aliongea swai huku kweli akitaka kufunga mlango lakini ni mpaka Zahra atoke

    "funga tu"

    "Zahra, nahitaji kupumzika mimi.. Sawa... Toka nje"

    Swalehe kamtolea uvuvi, yaani hataki mazoea,.. Huezi amini Zahra kaduaa tu, mtu aliokuwa akimpenda mpaka kumtaamkia swala la kuoa... Leo anamfukuza kwake... Zahra kwa hasira alitupa ile pesa yake, kisha akaondoka kwa hasira kali... Hata kudai umeme hajaendelea tena..



    "wewe zaru una nini"

    Fatuma au mama Saidi ambae ni dada yake na Zahra, alimuuliza mdogo wake baada ya kumwona anarudi huku akilia...

    "niache nilale dada"

    Aliongea zaru huku dada yake akizidi kumuuliza

    "niambie sasa hivi"

    "dada.. Hivi mimi nina mkosi gani kwenye mapenzi.... Mtu aliokuwa ananipenda kwa dhati, leo ananiona kama mavi"

    Aliongea Zahra huku akilala kwa hasira

    "mbona sikuelewi zaru mdogo wangu"

    "dada... Alikuwa ananipenda sana... Mimi nilijua hilo.. Ila ayub ndio alinichanganya... Alinitaamkia mpaka kutaka kunioa... Leo hataki hata kuniona"

    Aliongea Zahra huku akilia mno tena kwa hasira...

    "nani sasa"

    "niache dada... Niache, mimi nina mkosi.... Ila najua udhaifu wake, nitampata tu kwa njia yeyote ile"

    Aliongea Zahra huku Dada yake akimjibu kuwa....

    "ila Zahra usipotulia mdogo wangu... Utakitembeza hichoooo Mpaka kitaoza.... Kua makini mama huku ni mjini... Ukisikia masikini anataka kukuoa, mama shikilia... Mana hata upate tajiri atakutaamkia tu lakini hakuoi ng'ooo... Kwahio kuwa makini ndugu yangu"

    Aliongea fatuma huku akimfunika mtoto wake aliokuwa kalala,.. Fatuma nae kapangisha dabo rumu,.. Hivyo mtoto wake ana kitanda chake kama cha futi tatu kwa sita,.. Na analala hapo sebuleni ila kamtengea vizuri tu..... Zahra hata kula hakutaka kula... Kalala zake na njaa



    Wakati huo swai kachukua shuka lake na kujifunika kana kwamba anataka kulala,... Na wakati huo alikuwa akijisemea kuwa

    "mama muongo huyu.. Kasema analeta chakula kumbe wapi... Duu, acha nilale njaa kwa leo tu"

    Alijisemea katika moyo wake huku akivuta shuka...



    "ngo, ngo, ngo"

    Mlango wa swai uligongwa.. Na wakati huo ni saa nne usiku, na umeme haujawekwa, mana alietakiwa kudai umeme kasusa na kuacha kudai kwasababu hakuwa na nia ya kudai umeme, bali alitaka tu kuingia ndani kwa Swalehe

    "nani"

    Swalehe aliuliza kwa sauti ya juu... Kisha mama Mwajuma akajibu kwa sauti ya chini ili asisikiwe na wapangaji wengine, mana alikuwa kwa nje.

    "ni mimi mama mwaju"

    Aliongea kwa sauti ya mnong'ono katika tundu la funguo, uzuri ni kwamba swai alisikia na kuamka...



    Mama mwaju haamini kama kuingia kwa mara nyingine tena,...

    "nikajua umejisahau"

    Aliongea Swalehe huku mama mwaju akiweka chakula mezani na kukifunua.... Aaahhh swai haamini, wali wa nyama ya kuku, tena mapaja ya jogoo kaletewa yeye...

    "hapana siwezi kujisahau mpenzi wangu"

    Mama Mwajuma aliongea hayo maneno, Swalehe akashtuka

    "ati nini"

    "swai... Wewe sio mtoto... Hata mimi najielewa kuwa wewe ni mdogo kwangu, lakini ndio nshakupenda mama ako"

    Wamama wasiotaka kujivunga kama wasichana,.. Umeona Zahra kaingia hapo na uzuri wake wote lakini hakusema lolote juu ya kumpenda swai, lakini mama Mwajuma kaja na kasema ukweli wa moyo wake...

    "we mama Mwajuma.. Hivi unaongelea swala gani"

    Aliuliza Swalehe huku mama Mwajuma akimkatisha na kusema

    "hebu kula kwanza.. Acha presha zako"

    Aliongea mama mwaju, huku swai akianza kula... Mara mama mwaju, alinawa mikono kisha akachukua paja la kuku na kutaka kumlisha...

    "mama mwaju unafanya nini"

    "swai, hebu tulia... Wewe si unasema mimi ni mama yako.. Haya acha nimlishe mwanangu"

    Wamama wanaojali vijana, na ndio mana sasa vijana wanakimbilia kwa wamama kama hawa...

    "lakin ma.."

    "hakuna cha lakini buanaaa"

    Mama Mwajuma ana deka mbelw ya swai, sasa katika ile hali ya kumlisha mara ile kanga ikaachia, lakini mama Mwajuma wala hakuhangaika nayo, mpaka ikadondoka chini kabisa... Akabaki na chupi ya bluu, shanga zilizo zunguka kiuno chake...

    "mama mwaju kanga inado..."

    "achana nayo..."

    Sasa swai yeye na nguo za kike ni paka na panya,.. Yaani akiona chuoi za kike basi hisia za mapenzi zinapanda kwa haraka sana....

    "lakini upo uchi mama mwa"

    "acha kelele usiku huu watu wamelala... Hebu kula ulipie chakula changu"









    Swalehe katika maisha yake alikuwa hana tamaa na wanawake, yeye pesa yake alikuwa akijiwekea miaka yote hi na mpaka sasa ni hivyo,. Kwa ujumla maisha ya Swalehe hayajui mwanamke hata kidogo kwani hakuwa akiendekeza wanawake



    Mama Mwajuma ni mama wa watoto watatu wakike wote,... Na mama Mwajuma alisha achana na mume wake miaka kadhaa iliyopita, hivyo dada yake ambaye ni mama mwenye nyumba alimpa mdogo wake sehemu ya kuishi bure, yaani alimpa dabo rumu katika nyumba hio hio ya kupanga kwasababu aliachana na mume wake,... Na kwakua alikuwa na biashara yake ya duka la nguo hivyo liliweza kumlisha yeye na watoto wake na mpaka sasa bado anaendelea na maisha yake ya kipeke yake pake yake..... Kwa muda mrefu aliokaa bila kuwa na mume alijikuta akimpenda mpangaji mpya ambae ni Swalehe,... Kama unavyojua mama zetu nao siku hizi hawapendi wazee wenzao bali wanapenda watoto wao... Mama Mwajuma ana umri wa miaka 38, na ukimuangalia utafikiri ni miaka 25, mana ni mwanamke anaejipenda na pia kajaaliwa maungo katika mwili wake,... Tako analo, sura anayo, hipsi ndio usiseme... Kwa bahati nzuri kajaaliwa kifua kidogo kidogo, na rangi yake ni maji ya kunde hivi...



    Katika maadili ya kawaida, mama mtu mzima kumpenda kijana mdogo, kwa sasa sio jambo la kushangaza, ila mtoto wa kiume pia ni lazima kuonyesha msimamo wake akiwa kama mtoto kwake,... Lakini kwa vile wamama walivyo na ushawishi mkubwa, hua hawaambulii patupu,



    "lakini upo uchi mama mwa"

    "acha kelele usiku huu watu wamelala... Hebu kula ulipie chakula changu"

    Aliongea mama Mwajuma huku Swalehe akishtuka kwa kuskia kula ulipie chakula changu,...

    "nilipie??... Basi kama kuna kulipia"

    Swalehe aliacha kula huku akisogeza lile hotpot la chakula pembeni, wakati huo mama mwaju ana uchupi tu basi, mishanga imezagaa kiunoni na kumfanya Swalehe kupatwa na ham mana keshamzoea kwakua sio mara ya kwanza kukaliwa uchi na mama mwajuma,...

    "sio kulipia kwa hela...."

    Aliongea mama mwaju huku Swalehe akiuliza

    "nalipia nini"

    Aliuliza Swalehe huku mama mwaju akishika zakaria ya Swalehe akimaanisha alipwe zakaria hio...

    "lakini wewe ni mkubwa kwangu mama mwaju.. Siwezi"

    "swai... Mimi sipendi msimamo wako huo ni wakijinga mno"

    "kweli siwezi mama mwaju"

    Aliongea swai huku akitaka kulala,... Mama mwaju alimvuta swai na kumpakata kabisa, japo swai alikuwa hataki, lakini ule mgusano wa matiti ya mama mwaju na kukaa juu ya mapaja yake, alijikuta akilainika kama mwanamke,... Mama mwaju akampelekea swai mdomo,.. Swai akakubali kunyonya denda,... Mama mwaju kuona hivyo akaanza kushusha bukta ya swai...

    "no, no, no,... Sitaki... Sitaki"

    Aliongea swai huku akiamka na kupandisha bukta yake...

    "nini sasa swai mpenzi wangu"

    "nilisha apa... Chumba changu sitaki nikifanyie ngono na mtu asie mke wangu..."

    Aliongea Swalehe huku mama mwaju akichoka na kulegea

    "acha ujinga swai... Sasa maana ya geto ni nini"

    "hili sio geto... Geto linakaa vijana wahuni au hata sio wahuni lakini ni vijana ambao hawaja oa... Na mimi nataraji kuoa, hivyo hapa ni nyumbani ila sio geto... Utanisamehe mama.. Niache nilale"

    Swai aliweka msimamo wa chumba chake, hataki kukifanyia mapenzi hata kidogo...

    "ok... Kuliko nikukose.. Ngoja nikaangalie watoto wangu kama wamelala... Uje,.. Nipe namba yako, nitakubipu uje"

    Aliongea mama mwaju huku akichukua namba ya swai na kuondoka na vyombo vyake,... Mama ana hamu mpaka kwenye koooo



    Wakati huo swai katulia ndani kwake akisubiri simu ambayo atapiga mama mwaju, mana swai nae na hamu hamu zake katamani kwenda kulala na mama mwaju, mana kaja kujichengesha mwenyewe chumbani kwake,... Ghafla simu ya swai inaita, kuangalia, ilikuwa ni namba ngeni kabisa,... Aliipokea kisha akaiweka sikioni

    "njoo,... Ila angalia kama kuna mtu nje wasijue"

    Aliongea mama mwaju, kana kwamba ndiole yeye alie piga simu hio na kumtaka swai aweze kwenda katika chumba cha asha,.... Swai alifunga chumba chake vizuri huku akiangalia pembezoni kama vile mtu anaetaka kuiba kitu,... Aligundua hakuna mtu alie muona, aliingia mpaka ndani kwa asha,.. Wakati huo asha kajitanua kama mtoto mbichi, kumbe ni mama mtu mzima....

    "swai... Tusiongee kwa sauti sana... Watoto wangu wamelala pale"

    Aliongea mama hadija, au mama mwaju, ukipenda muite asha,...

    "sawa"

    Alijibu swai huku asha akitaka kuvua jichupi lake jepesiiii, liliomfanya swai kusisimka kwa haraka...

    "usivue kwanza"

    Aliongea swai.. Huku mama kweli akiacha kuvua.... Mama na mtoto wakabinuana mpaka kitandani ambako ndiko uwanja mkuu wa mapenzi.... Swai alianza kula sahani moja na shanga za asha,... Mpaka alihakikisha ile chupi imeloa kwa chini...



    Kesho yake asubuhi,.. Swai akiwa nyumbani, mana leo hakwenda kwa uchovu wa safari ya jana, sasa akiwa yupo hapo nje anachati chati, ghafla simu yake inaita...

    Kuangalia, alikuwa ni mama yake mzazi aliopo kijijini kwao

    "hallo mama shikamoo mama angu"

    Swai alimsalimia mama yake, aliokwenda kwa jina la WAHIDA

    "marahaba mwanangu hujambo"

    "sijambo mama sijui nyinyi huko"

    "huku hatujambo baba... Ni baba yako anaumwa umwa hivi... Si unajua ugonjwa wake umemrudia tena"

    "aaayaaaa.... Poleni sana mama angu.. Vipi sasa kwa sasa anaendeleaje"

    "hajambo... Ila kuna hela ya hospitali tunadaiwa... Sasa kuliko tuuze mifugo, bora tuwajulishe watoto wetu, kama kipo chochote mtutumie... Tulikuwa na hakiba zetu, nikajua itasaidia lakini imeisha"

    Aliongea mama yake Hassan ambaye ndio mama yake swalehe

    "oke, ni sawa na vipi kuhusu kaka umemtaarifu swala hili"

    "ndio, mwanangu,... Nimempa taarifa ila kasema hayuko vizuri,... Afu kaniamba wewe umehama nyumbani kwake ni kweli"

    Mama yake Swalehe alikuwa hajui kama Swalehe kesha hama kwa kaka yake, na sasa ni mwezi wa pili toka kuhama kwa Swalehe..

    "ndio mama nilisha hama, nina mwezi wa pili sasa"

    "basi ni vizuri, na pia kuacha hili swala la kuumwa kwa baba yako, pia niliposikia kuwa una chumba chako.. Naona sasa nikutafutie mke mwanangu... Uoe sasa"

    Mama Swalehe aliongea hayo huku Swalehe akishtuka kwa kuskia hivyo..

    "mama? ni kweli ni wakati wangu wa kuoa.. Na nataka kweli kuoa hata sasa hivi mama angu... Lakini huu sio wakati wa kuchagulia wake mama... Na kama unavyojua wanawake wa sasa hivi, hakuna mwanamke wa kuoa.. Nikimaanisha wanawake wengi wanataka wanaume wenye maendeleo mama yangu"

    Aliongea Swalehe kwa kumwambia mama yake, sasa kumbe Zahra kasikia hayo maneno, saa ngapi hajaja na kusema

    "swai usimwambie mama mkwe hivyo.... Ina maana mimi sio mwanamke"

    Heeee Swalehe alishangaa kumskia Zahra akiongea maneno hayo,...

    "Zahra, naomba ukae kimya.. Tutagombana sasa hivi"

    Aliongea Swalehe na wakati huo simu bado ipo hewani...

    "lakini swai, ni kosa gani nimekufanyia mimi.... Usimwambie mama kuwa hakuna wanawake,.. Ina maana mimi ni mbuzi"

    Aliongea Zahra huku mama yake Swalehe akisema

    "mwangu, mbona naskia sauti ya kike hapo... Ina maana unaishi na mwanamke"

    Aliuliza mama yake swai huku swai akimjibu

    "hapana mama.. Siwezi kufanya hivyo.. Ni jirani tu"

    "sasa mbona naskia anasema mama mkwe sjui yeye sio mbuzi.. Kuna nini kinaendelea hapo"

    "mama... Hakuna lolote mama angu"

    "ok.. Hebu nitumie basi hio pesa, tukalipe hospitali, mana baba yako bado hajatoka kule"

    "sawa mama... Ni kiasi gani"

    "ni laki mbili mwanangu"

    "duuuu mama laki mbili nyingi sana.. Ila nitajitahidi kituma laki na nusu"

    Aliongea Swalehe lakini mara Zahra kadakia....

    "mama Usijali mimi nitakutumia yote mama mkwe"

    Aliongea Zahra tena kwa kuisogelea simu ya swai...

    "Zahra una nini lakini... Kwenda uko"

    Swalehe alikasirika sana huku akinyanyuka

    "swai mwanangu.... Kumbe una mwanamke hutaki kuniambia, hebu nipe niongee nae... Mtoto mjinga sana wewe, umepata mwanamke hutaki kututambulisha... Mpe haraka niongee nae"

    Heeeee mama yake swai kawa mkali, mana nia ni kumtafutia swai mke, sasa kama keshampata basi, ni bora waowane tu....

    "mama, sio msichana wangu mama, ni jirani tu mama angu"

    "nipe nimuulize kama ni kweli... Tena mtoto wa watu ana jina zuri.. Hebu mpe simu"

    Mama alizidi kutaka kuongea na Zahra,...

    "mama, mimi sikai nae"

    "swaiiiii... Unabishana na mimi"

    Mama yake swai kapagawa kuskia kaitwa mama mkwe, afu mbaya zaidi kasikia atatumiwa hio laki mbili na huyo msichana.... Swai hakuwa na jinsi alimpa simu lakini wakati huo ana hasira kweli yani... Afu kaiweka laudi spika



    "halo mama mkwe, shkamoo"

    Zahra alimsalimia mama yake swai

    "marahaba binti yangu hujambo"

    "sijambo mama.. Za huko"

    "nzuri tu... Eti unaitwa nani"

    "naitwa Zahra"

    "ooohh jina zuri sana... Unampenda mtoto wangu au... Mana nyie wasichana wa siku hizi siwapendi kweli yani"

    "mama.. Nampenda swai, nataka anioe"

    Mara swai akaingilia juu kwa juu

    "we Zahra vipi wewe... Acha ujinga bwana mimi sina mahusiano na wewe"

    Aliongea swai lakini Zahra hasikii

    "waoooo basi mwanangu... Mana nilitaka kumtafutia jiko huku.. Sasa hasemi kuwa kapata.. Mtoto mjinga sana huyu..."

    Aliongea mama yake swai huku Zahra akitabasamu

    "mama, nampenda swai.. Ondoa hofu kuhusu swala hilo... Afu nipatie namba yako nikutumie hio pesa"

    "ooohhh Ahsante sana... Mwambie swai atakupa"

    "hapana... Hatonipa mama"

    "ok.. Ngoja nikutajie"

    Sasa ile nafasi ya kutaka kutajwa namba, swai akawa anawahi kuchukua simu kwa Zahra... Zahra akatoa simu sikioni kisha akaangalia zile namba pale kwenye skrini ya simu, akazishika kwa kichwa... Sasa ile mama anaanza tu kitaja..

    "haya 075"

    Mara simu ikanyakuliwa nankukatwa kabisa...

    "Zahra.. Sitaki mazoea na wewe..."

    Aliongea swai huku akiingia ndani, na wakati huo Zahra katulia tu...



    Aliingia ndani na kuchukua simu yake, kisha akaanza kuingiza namba za mama yake swai katika simu yake, kwahio swai anajua Zahra hajafanikiwa kutajiwa namba, kumbe tayari alisha iangalia kwenye skrini kabla ya kutajiwa...



    Sasa huki kwa Swalehe, akapiga tena simu kwa mama yake...

    "hallo mama"

    "swai hivi una kichaaa wewe"

    "mama saaa unachokifanya huku kunipoteza sasa... Mara kumi utafute mke kuliko huyu uliomsikia.. Mama huyu ni mhuni mama... Mimi siwezi kuishi nae na sijawahi hata kumtongoza jamani... Ni jirani tuuu"

    "sasa kama ni jirani mbona anasema anakupenda na anataka kuolewa na wewe"

    "mama,.. Huyu msichana kajiuza sana, sasa kakosa soko ndio ananiganda mimi"

    Swalehe Aliongea hayo kama kumkandia Zahra, japo sio kweli kuwa anajiuza... Bali Zahra kajifunza kutokana na makosa,.. Aliona mali ni sahihi kwake kumbe kadanganywa..

    "wewe ni muongo... Tena Afadhali upate mke wa huko huko mjini... Mana wa huku kijijini wakija mjini ndio balaaa"

    "hapana... Kama umemtafuta wewe nitaishi nae tu... Mama nakupa ruksa nitafutie mke, ila sio huyu"

    "hebu ngoja kwanza.... Kuna meseji imeingia hapa...."

    Aliongea mama yake Swalehe huku akikata simu na kuangalia msemaji ilio ingia, yaani mama yake swai ni mcharuko mpaka basi...

    "waaaaooooo.... Nimetumiwa laki mbili na nusu"

    Aliongea mama yake Swalehe, mara ghafla,... Simu yake inaita ila namba ilikuwa ni ngeni katika simu yake

    "hallo, Samahani wewe ni nani"

    Mama Swalehe aliuliza huku akiskilizia sauti

    "mama... Naitwa Zahra, ndio mimi niliokutumia hio pesa kalipie hospitalini baba mkwe apone... Ni mimi Zahra mchumba wa mwanao Swalehe"

    Aliongea Zahra huku mama swai akifurahi mpaka basi,.... Karushiwa laki mbili na nusu, wakati swai mwenyewe alikuwa akilia atume laki na nusu badala ya laki mbili... Sasa mtoto wa kike katuma laki mbili na nusu... Shaaaabaashi, chezea kupenda wewe...

    "Ahsante sana mwali wangu.... Lazima uwe mkwe wangu wa halali... Nipate wapi mkwe kama wewe"

    Aliongea mama yake swai huku Zahra akisema

    "sawa mama... Nipiganie mama, nampenda swai... Nipiganie anioe"

    "Usijali, mimi ndio mama yake...  ondoa shaka kwa hilo"

    "Nashukuru sana mama...."

    "ila Zahra... Nyie mna ugomvi na swai, mana hataki kusema kuwa wewe ni mchumba wake"

    Mama aliuliza na Zahra akaanza kuogopa...

    "mama, naomba Nikuambie ukweli kabisa.... Ni kweli, swai alihamia hapa miezi miwili iliopita... Lakini kumbe mwanao alinipenda... Sasa kwa wakati ule nilikuwa na mwanaume ambae alinidanganya kunioa,.. Na nilidhani ana pesa, kumbe hakuwa na lolote... Mama?? Kweli yule mwanaume alinitumia kimwili mara moja tu,... Toka hapo sikumpa tena... Ndipo nikaja kujua kuwa ni muongo na mlaghai wa mapenzi.... Toka siku hio nikarudisha moyo wangu wote kwa mtoto wako.. Lakini kumbe nae kesha kata tamaa ya kuwa nami tena, na hanitaki tena.. Mama? Nampenda sana swai, nipo tayari anioe... Nitaishi na mwanao kwa hali yeyote ile... Mama nihukumu kwa ukweli wangu... Na hio ndio sababu ya swai kunikataa... Mama nisaidie"



    Aliongea Zahra huku akilia, tena Zahra kaongea ukweli wote, na wakati huo mama swai katulia kimyaaa hakutoa neno, wala haongei

    "hallo.... Haloo... Hallo... Hallo mama mkwe... Mamaaa...."

    Zahra akiangalia simu ipo hewani lakini mama swai haongei tena..

    "hallo mama... Hellooo... Hallo?.. Mama mkwe,... Hallo?"

    Zahra alishangaa na kupatwa na wasiwasi juu ya mama yake Swalehe











    Wakati huo Swalehe anaangalia salio kwenye tigo pesa yake, anakutaka hakuna hata salio,.. Ikabidi achukue kadi ya NMB ili aka droo pesa ya kumtumia mama yake kwa maana baba yake kalazwa hospitali na hawezi toka mpaka malipo yafanyike, na wakati huo Swalehe bado hajajua kuwa mama yake keshatumiwa kibunda cha maana.... Na baada ya kutumiwa pesa hio Zahra aliamua kumpigia mama yake swai na wakaanza kuzungumza mpaka Zahra kuongea ukweli mtupu na hakumdanganya mama yake swai... Lakini baada ya Zahra Kumaliza kuzungumza, alishangaa kwa ukimya wa mama yake swai katika simu yake



    "hallo mama... Hellooo... Hallo?.. Mama mkwe,... Hallo?"

    Zahra alishangaa na kupatwa na wasiwasi juu ya mama yake Swalehe



    "Zahra?, Usijali mwanangu.... Unajua nilikuwa nafikiria kwa ukweli ulio utoa hapa... Ni wasichana wachache wanaoweza kusema ukweli, na mimu nimeamini kuwa ni kweli kwasababu umesema mpaka ulikuwa na mwanaume na umeshiriki nae mara moja, yaani nimeshangaakwa ukweli ulio uongea Zahra"



    Mama yake swai aliongea hayo baada ya kukaa kimya mpaka Zahra akakata tamaa juu ya mama swai kumsaidia kuwa na swai kama mke na mume,... Zahra haamini kwa ukarimu wa mama swai, mana hakuamini kama angeliweza kumwamini kiasi hicho...

    "mama... Nashukuru kwa kuniamini... Naomba uongee na swai, nampenda.. Sasa moyo wangu wote umehamia kwake mama"

    Aliongea Zahra huku mama akimjibu

    "Zahra, ondoa shaka, Swalehe ni mwanangu, tena mtoto wangu wa mwisho... Atanielewa tu"

    "nitashukuru sana mama"

    "Usijali mwali wangu mtarajiwa... Nitafanya mpango mpaka swai awe mumeo"

    "mama, sijui nikupe nini mama"

    "Usijali zaru,.. Kuwa huru na pia nashukuru kwa kiasi ulicho nitumia"

    "sawa mama,.. Nikuache uelekee hospitali"

    "sawa zaru... Alafu pia kingine, usiwe na hasira juu yake.. Mana namjua mwanangu ukiwa mkali juu yake.. Ndio utamuuzi kabisaa"

    "mamaa... Yaani mimi nipo chini ya miguu yake... Ni mume wangu, lazima nimpe heshima kubwa"

    "waooooo zaru, natamani kukuona mwali wangu, mana una maneno mzuri"

    "heheheheh... Mama mkwe bwana.. Una simu ya wasap mama"

    "mmmhhh huku kijijini wasap hakuna.. Ngoja kesho mtoto wangu wa kike anakuja, nitampa namba yako afu unitumie picha nikuone mwali wangu"

    "waoooo, natamani Nimuone wifi yangu mama"

    "Usijali zaruu"

    "Ahsante mama"

    "sawa, siku njema mwali wangu"

    "nawe pia mama mkwe wangu"

    "sawa"



    Zaru alikata simu huku akifurahi mno kwa kuongea na mama wa mtu ampendaye, na kuahidi kumsaidia kuolewa naye,....

    "swai, sasa umekuwa wangu... Najua huezi mkatalia mzazi wako... Nitakupenda swai, nikubalie kuwa mkeo"

    Zahra alijisemea katika moyo wake huku akiwaka simu yake chaji mana ilikuwa ikiisha...



    Sasa huku kwa swai, alimpigia simu mama yake na wakati huo yupo njiani kwenda benki kudroo pesa ili aweze kumtumia mama yake....

    "hallo mama?, subiri dakika chache tu nakutumia sasa hivi"

    Aliongea swai huku akiwahi, mana mzee wake kazuiwa kule hospitali

    "ya nini sasa baba...."

    "ya nini kivipi sasa mama angu? Si umetaka pesa muda huu, baba yupo hospitali"

    "Zahra keshantumia laki mbili na nusu,.. Kwani hajakwambia?"

    "ati unasemaje??"

    "ina maana hujasikia au unataka kurudia rudia"

    "mama... Huyo mwanamke mimi simtaki, na kama mmesha aanza mahusiano yenu... Hayo ni yenu mama angu.. Humjui Zahra wewe.. Mtu nimemtajia kazi yangu,.. Kaniangalia juu mpaka chini na kusema ajui hata kucha zake tu siwezi kuzitunza... Leo aje kuwa mke wangu kwa lipi mama"

    Aliongea swai ili kumfanya mama yake asithubutu kuwa na zaru karibu

    "lakini kasema kaachana na huyo mtu wake jamani baba"

    "mama... siiiitaki jaka la moyo, zaru ni jaka la moyo mama simtaki... Kwanza kaka Hasan hana mke... Tumpe kama atawezana nae"

    Aliongea swai mpaka mama yake akakasirika

    "we mshenzi nini wewe... Kwani tunaongea mambo ya Hasan hapa?, na utamuoa tu"

    Aliongea mama swai huku akikata simu,... Swai aliahirisha kwenda NMB, mana pesa ishatolewa

    "huyu mama ana nini lakini"

    Aliongea swai huku akirudi zake nyumbani... Alifika na kutaka kumfuata zaru kule ndani kwao mana dada yake hayupo,.. Sasa anatamani kumfuata ili ampe vidonge vyake,..

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog