Search This Blog

Thursday 24 November 2022

NYETO NYETONI - 4

 

     

     



     

    Chombezo : Nyeto Nyetoni

    Sehemu Ya Nne (4)

     

    Vifo vya Snop na mwenzake Sudi vilivuta hisia za watu wengi sana watu walilia mpaka kufikia hatua ya kupoteza fahamu miongoni mwa watu walioumizwa kupita kiasi juu ya vifo hivyo ni Mwanaidi yani kila muda alikuwa ni mtu wa kulia tu! Maana aliwakumbuka kwa mambo mengi hasa wawapo pamoja na Ducha pia alifikiria ni jinsi Gani mdogo wake atakavyochanganyikiwa pindi akifahamu kuwa marafiki zake hawapo tena Duniani huwenda ataathirika kisaikorojia na zimebaki siku chache Sana Shule kufunguliwa.

    ”Mwanaidi mwanangu"

    Akiwa amekaa pale akiwaza na kuwazua akashtuliwa na sauti ya mama yake akimwita akajifuta Machozi na kujiweka sawa

    ”abee Mama"

    ”nafahamu ni jinsi gani unavyojiskia vibaya juu ya vifo vya Wadogo zako nami nikiwa Kama mzazi nimeumia moyo wangu"

    Mama yake Ducha alizungumza hivyo huku naye akijifuta machozi

    “Mamaa"

    “abee Mwanangu"

    ”vipi kuhusu Ducha?"

    “Ducha kafanyaje tena?"

    “sio kafanyaje nilitaka kukuuliza siku nitakayoenda kumfata halafu akafahamu juu ya hili swala itakuwaje?"

    “mmh kiukweli natamani Ducha asiweze kurudi hapa ikiwezekana tumfanyie uwamisho shuleni akasomee huko huko Kibaha"

    “mamaa uwoni Kama tumeshachelewa?"

    “nikweli tumechelewa na hatuna uwezo Tena wa kuzuia hili swala"

    Basi mtu na mama yake walizungumza pale wakapanga siku ya kwenda kumfata Ducha maana vifaa vyote vya Shuleni kanunuliwa vipya kuanzia Madaftari Yunform viatu nakadharika

    Hapa tunamuona bwana mdogo Sudi akiwa amekaa sehemu kwa kujiinamia hakika alionekana kuwa ni mtu mwenye mawazo mengi Sana

    “Huku nilipo ni wapi? Nimefikaje fikaje huku? Snoop wee Snop itikia basi wee matako"

    Sudi alijiuliza hivyo kisha akapaza sauti kumwita Snop

    ”wee Snoop uko wapi jitokeze kudadeki zako"

    Alizidi kuita huku akizunguka huku na kule kumtafute mwishoe akakata tamaa na kuamua kwenda kukaa sehemu ile ya awali akiwa amekaa pale mara kwa mbaali alionekana Snop akimfata kwa mwendo wa taratiibu

    ”unaona sasa, umenipigia mikelele mpaka umesababisha nije kwenye ulimwengu wa roho!"

    Snop alizungumza haliyakuwa akiwa anahema

    “unasemaje wewe?"

    Sudi akauliza

    ”ujaskia au vipi?

    ”ndiyo sijakuskia ila nimeskia tu ukisema ulimwengu wa roho"

    ”kumbe umeskia ehee"

    ”ndiyo nimekuskia ila sijakuelewa unamaanisha kitu gani?"

    ”namaanisha ya kwamba sisi ni Marehemu"

    ”ninii?"

    ”kama nahilo ujaskia jishike tako ujambe"

    Snop alizungumza hivyo akapiga hatua kadhaa kuelekea sehemu Sudi alibaki kumsindikiza kwa macho huku akiwa katika hali ya mshangao

    ”Snop wee Snop embu simama kwanza"

    Sudi aliita huku akimkimbilia ikabidi Snop asimame

    ”unamaanisha kitu gani kusema kuwa sisi ni Marehemu? Na huku ni wapi?"

    Sudi aliuliza maswali mfurulizo ikabidi Snop amsogelee rafiki yake na kumshika mikono

    “Sudi"

    “naamu"

    “tambua ya kwamba sisi tayari tumeshakufa kuanzia Sasa tutaishi kwenye Ulimwengu wa Roho Ulimwengu ambao hatutoweza kushika kitu chochote kile wala hatutoonekana mbele ya macho ya watu wa kawaida

    Tutaishi huku mpaka pale Dunia itakapofikia mwisho. Tafadhari

    Nakuomba usilie acha Mimi niende kusaili jina langu"

    Snop alizungumza kwa hisia na kumfanya Sudi aanze kulia

    “khaa embu angalia kule yule si Ducha"

    Sudi alizungumza huku akinyoosha mkono nikweli aliyeonekana kuja upande ule waliopo wao alikuwa ni Ducha

    Wakati wanaendelea kumtupia macho Ducha wakashangaa kuona kuna kiumbe cha ajabu kikiibuka nyuma ya Ducha muonekano wa kiumbe yule uliwatisha na kuwaogopesha

    ”Ducha kimbia wewe nyuma yako kuna jinii"

    Snop akapaza sauti kumtaka Ducha akimbie Ducha ndiyo kwanza akawa anatabasamu badara ya kukimbia akasimama na kugeuka ili kukiangalia hicho kiumbe

    “wapi unaenda?"

    Yule kiumbe aliuliza huku akijibadirisha kutoka kwenye muonekano wa kutisha na kuwa kiumbe Cha kawaida hakuwa mwingine bali ni bwana mkubwa Chinoge

    “naenda kulee kuwafata marafiki zangu"

    Ducha akajibu

    ”kuwafata wale ni mapema mno twende nyumbani"

    “sio mapema Ducha njoo ujumuike pamoja nasi"

    Kina Snop wakapaza sauti kumwita Ducha

    “lete mkono kijana tuelekee nyumbani kwa maana leo hii ukiamua kuwafata wale nani atawalipia kisasi chao?"

    Chinoge alizungumza hivyo

    Aliuliza hivyo

    Kina Sudi wakaanza kupiga hatua kusogea upande ambao Ducha na Chinoge walikuwa wakizungumza alichokifanya Chinoge ni kumshika mkono Ducha kisha akamvuta kwa nguvu

    “Snoop Sudiii"

    Ducha alipiga kelele kuwaita marafiki zake ghafla alishtuka kutoka usingizini na kujikuta akiwa amelala kitandani akaangaza macho yake huku nakule aliweza kumuona Mwalimu wake akiwa amekaa pembezoni mwa kitanda akahitaji kunyanyuka lakini alishindwa

    Kufanya hivyo baada kuskia maumivu makari mwilini mwake aliuma meno na kubana midomo

    ”pole sana kijana"

    Chinoge alizungumza hivyo

    “uwiiii ihiiiii,, nimefanyaje Tena mbona kama nimeumia?"

    Ducha alipiga kelele huku akiuliza swali

    Muda kidogo wakaingia Madaktari kama wawili wakafanya kumbeba Ducha na kumuweka kwenye kiti chenye magurudumu matatu

    ”mnampeleka wapi?"

    Chinoge akawazuia na kuwauliza swali

    ”kama tulivyoweza kujadiriana kuhusu kijana wako kuwa mguu wake wa kushoto umevunjika kwa hiyo hakuna budi ukatwe ili kuokoa uhai wake"

    Mmoja kati ya wale Madaktari sijui Manesi akajibu

    Ducha alishtuka kuskia vile kuwa anatakiwa kukatwa mguu inamaana atakuwa kilema maishani mwake

    ”si niliwaambia kuwa Mimi sio ndugu yake. Inatakiwa tuwasubilie Wazazi wake kutoka jijini Dar es Salaam ili waweze kukubariana nanyi"

    Chinoge akazungumza hivyo

    ”sikia nikueleze kitu kimoja ndugu yangu jukumu la kuokoa maisha ya kijana wako lipo mikononi mwetu. Kama tukisema tukae tu! kuwasubilia hao wanaotokea mjini likitokea la kutokea huyu Mtoto akapoteza maisha wa kwanza kulaumiwa ni sisi. Kwasasa huna budi kuwa mpole

    Mmoja kati ya Madaktari alizungumza hivyo huku yule mwingine akitoka nnje ya Wodi hiyo haliyakuwa akikikokota kile kiti

    Mwenzake naye akamfata Chinoge akawa kama vile kapigwa na bumbuwazi anakuja kushtuka watu washatoka wodini akafanya haraka kutoka nnje akaangaza macho yake huku na kule aliweza kuwaona kwa mbaali wakielekea upande mwingine

    Akatoka mbio kuwakimbilia alipowafikia tu akafanya kumpiga kipushi yule aliyekuwa anakisukumiza kile kiti Daktari akapepesuka kitendo pasipo kuchelewa Chinoge akamnyanyua Ducha kutoka kwenye kile kiti na kukimbia naye Nnje ya hospitali

    ”wee kakaa embu simama mrudishe mtoto huyo, unaenda naye wapi Sasa"

    Wale Madaktari walipaza sauti kumtaka Chinoge asimame ikiwezekana amrudishe Ducha

    Mwenzao wala hakutaka kuwasikiliza akazidi kukimbia naye kufika sehemu kulikuwa na mzungo yani Kama vile unataka kupandisha ngazi kwenda kushoto

    Chinoge akazunguka kwa kasi na kutoweka Kama vile vumbi

    Mpaka wale Madaktari waliokuwa wanamkimbiza wanafika pale mtu hayupo

    Walimtafuta huku nakule hawakuweza kumuona



    ------------------

    akafanya kumpiga kipushi yule aliyekuwa anakisukumiza kile kiti Daktari akapepesuka kitendo pasipo kuchelewa Chinoge akamnyanyua Ducha kutoka kwenye kile kiti na kukimbia naye Nnje ya hospitali

    ”wee kakaa embu simama mrudishe mtoto huyo, unaenda naye wapi Sasa"

    Wale Madaktari walipaza sauti kumtaka Chinoge asimame ikiwezekana amrudishe Ducha

    Mwenzao wala hakutaka kuwasikiliza akazidi kukimbia naye kufika sehemu kulikuwa na mzungo yani Kama vile unataka kupandisha ngazi kwenda kushoto

    Chinoge akazunguka kwa kasi na kutoweka Kama vile vumbi

    Mpaka wale Madaktari waliokuwa wanamkimbiza wanafika pale mtu hayupo

    Walimtafuta huku nakule hawakuweza kumuona



    Songa nayo

    Sasa



    ”huyu mshenzi sijui atakuwa kaelekea wapi na yule mtoto? Embu zungukia upande ule huwenda atakuwa kajificha sehemu"

    Mmoja kati ya wale Madaktari alitoa maelekezo kwa wenzake kwa wakati huo walishaongezeka wakawa kama watu sita kila mmoja akaelekea upande wake

    “uwiiii,,yalaaa"

    Zilikuwa ni kelele kutoka kwa kaka yake Athumani aliyekuwa kashikiliwa begani huku akikokotwa kuelekea sehemu ya kupumzikia Wagonjwa mguu wake wa kushoto ulikuwa umefungwa hogo

    Bila shaka alikuwa kavunjwa mguu halkadharika pia mkononi kulikuwa na Hogo

    Akakalishwa kwenye benchi na kutakiwa kutulia hapo muda kidogo aliwasili Athumani akiwa kaongozana na Wazazi wake

    “poleni Sana vijana wangu kutokana na maswahibu makubwa yaliyoweza kuwatokea vipi kuhusu Kingo?"

    ”kaka Kingo yeye mpaka Sasa bado ajazinduka yani yuko vilevile"

    Athumani akajibu lile swali kutoka kwa baba yake

    ”aisee kwani ilikuwaje kuwaje mpaka vijana wangu ninao wategemea wakadundwa na mtu mmoja?"

    “baba yule sio mtu ni Jiniasi yani anapiga Kama vile Jet li"

    Athumani akajibu kumbe bwana mkubwa Chinoge aliwatandika wote wawili mpaka kupelekea mmoja wao kupoteza fahamu huku mwingine akimvunja mguu na mkono.

    Chinoge baada kutoweka pale hospitali akiwa kambeba Ducha akaja kuibuka naye sehemu ambayo mara nyingi huwa wanafanyia mazoezi akamshusha chini kwa wakati huo Ducha alikuwa kama vile kapitiwa na usingizi baada ya kumlaza chini akachuma baadhi ya majani akafanya kuyapikicha na kuyatemea mate

    Na kuanza kumkanda kanda Ducha mwilini alipitisha kila sehemu alipokuwa anayapitisha moshi ulifuka huku

    Yale majeraha yakipotea mguu ukajiunga ukawa sawa bin sawia Mwishoe akamnusisha yale majani punde Ducha alipiga chafya mfurulizo akafumbua macho

    ”Asante mwalimu"

    Kauli ya kwanza kuitoa Ducha alimshukuru Mwalimu wake halafu akasimama bila shaka aliweza kufahamu kwakile alichofanyiwa

    ”mwalimu kuna watu ndani ya dunia hii wamenikosea Mimi kwanini wameniulia marafiki zangu? Ndugu zangu vipenzi vyangu nitakuwa na nani mimi?

    Nitahakikisha nawafyekelea mbali wote waliohusika juu ya unyama huu"

    Ducha alizungumza kwa ghadhabu huku akitembea tembea huku nakule

    Akataka kutoweka lakini Chinoge akawahi kumshika mkono

    “tafadhari mwalimu nakuomba niachie"

    “unataka kwenda wapi?"

    ”naenda kunywa damu za watu?"

    ”embu sogea hapa"

    Ducha akasogea na kuinamisha kichwa chake chini Chinoge akaipitisha mikono yake na kumshika Ducha kichwani kuna vitu vilionekana kutoka kichwani mwa Ducha vitu vile viliambaa ambaa angani vikatoweka

    Siku mbili baadae Mwanaidi aliwasili maeneo ya Kibaha bila shaka ni kwaajili ya kumfata Ducha

    ”karibu Sana mjukuu wangu"

    “asante Sana Bibi yangu"

    Mwanaidi aliitikia haliyakuwa akikaa kwenye mkeka akatoa vijizawadi alivyomletea Bibi yake

    “khee inamaana Wazungu wametengeza Sukari nyeupe?"

    “bibi bwana hiyo sio Sukari ni chumvi"

    “khee kumbe kuna chumvi ya Unga?"

    “ndiyo vipi Ducha yuko wapi?"

    “mmh Ducha tokea ulivyomleta sikuile hakai hapa"

    ”khaa anakaa wapi sasa?"

    “anaishi huko Mikongeni kwa Shogaangu yule Binti Kiwambaza si unampata"

    “ndiyo si yule mwenye nywele nyeupe kichwa kizima?"

    “ekhee ndiyo yeye"

    ”kwani bado anaishi eneo lile lile?"

    ”aende wapi sasa? Wakati pale ndiyo kwake"

    “itabidi nikamfate maana leo nimekuja kumchukuwa"

    Mwanaidi akajiandaa na safari ya kuelekea Mikongeni kuna Dereva bodaboda alimsimamisha na kumuomba ampeleke huko baada kuelewana Bei akapanda hao wakaondoka

    Bahati nzuri alimkuta Ducha kashaandaliwa kwaajili ya Safari ya kurejea kwa Bibi yake Bungu

    “Dada"

    “abee mdogo wangu"

    ”mbona unaonekana Kama vile haupo sawa unafikiria kitu gani?"

    Ducha alimuuliza swali Dada yake kwa wakati huo walishapanda Daladala

    “Ducha"

    “nambie Dada yangu"

    “yule jamaa ni nani yako?"

    ”jamaa yupi?"

    “yule uliyekuwa unamwita Mwalimu?"

    ”ni Mwalimu wangu wa Mashowart Artist"

    ”ohoo tukiachana na kumwita mwalimu binafsi nahitaji kumfahamu kiundani?"

    “kwanini unahitaji kumfamu kiundani umetokea kumpenda au?"

    “ndiyo kaka yangu kiukweli nimetokea kumpenda tu!"

    Ducha akatabasamu

    ”hahahahaha"

    ”sasa mbona unacheka"

    ”sicheki Wala nini"

    “kumbe nini?"

    “nafurahia kuona karibuni nitapata shemeji"

    Basi mtu na Dada yake waliendelea kupiga stori za hapa na pale mpaka wanawasili Mbezi mwisho wakapanda Gari ya Temeke wakashuka Riverside hapo wakapanda ya Mbagala lakini muda wote Mwanaidi alionekana kutokuwa sawa na sio Kama anamfikiria Chinoge Kama alivyomueleza mdogo wake la hasha anawafikiria kina Snop itakuwaje Ducha akifika nyumbani kwao halafu asiweze kuwaona marafiki zake.

    Yapata majira ya saa kumi Arasili Ducha na Dada yake wakawasili nyumbani kwao wakapokelewa kwa furaha

    Siku hiyo iliweza kupita kesho yake asubuhi Ducha akaingia kitaani kwenda kununua vitafunwa akapita nyumbani kwa kina Sudi

    Na kumkuta mama yake Sudi akifagia

    Ajabu Ducha alimpita mama yule pasipo kumsalimia kitu ambacho kilimshtua sana mama yake Sudi akadhani labda atakuwa ajamuona akafanya kumwita

    “Duchaa Ducha mwanangu"

    Ducha akasimama na kugeuka alimuangalia yule mama kama vile ni mara yake ya kwanza kumuona

    “vipi ujambo mwanangu?"

    “sijambo shikamoo"

    “marhabaa vipi Bibi ajambo?"

    “ajambo"

    “basi nilikuwa nahitaji kukujulia hali tu mwanangu maana nilivyoona unanipita pale nilishtuka kweli kwa maana sio kawaida yako"

    “sio kawaida yangu kivipi? Kwani wee mmama unanifahamu Mimi?"

    Ducha akauliza swali ambalo lilimshangaza Sana mama yake Sudi

    “mmh wee si Ducha rafiki wa kijana wangu aliyefariki juzi anaitwa Sudi inamaana mara hii umenisahau?"

    “ndiyo mi Ducha Duchani ila sijawahi kuwa na urafiki wowote ule na mwanao wala wewe sikujui"

    Ducha alijibu kwa kujiamini

    “Duchaa"

    Mama yake Sudi aliita Ducha akaputa mkono kama kumpuuza huyo akaendelea na safari yake alinunua vitafunwa wakati wa kurejea kwao akabadirisha njia akapitia kwa kina Snop

    “whaoo hatimae Ducha umerudi jamani kipenzi changu nilikumisije"

    Alikuwa ni bibie Latifa akitamka hivyo basi wakakumbatiana kwa furaha na kupigana mabusu

    ”mi mwenyewe nilikumiss Sana Mchumba"

    “ila pole Sana mpenzi wangu kwa kuondokewa na marafiki zako"

    ”marafiki gani tena hao?"

    ”mmh Ducha jamani kwani huna taarifa kuwa Snop na Sudi wamefariki?"

    ”Snop na Sudi ndiyo kina nani?"

    “khaa Ducha embu acha utani inamaana huwakumbuki marafiki zako vichaa wako kina Snop?"

    “kiukweli kabisa katika maisha yangu sikuwahi kuwa na marafiki kama hao unavyosema nimewasahau mbona wewe sijakusahau?"

    ”ndiyo hapo sasa embu muangalie yule Mama pale"

    Latifa akanyoosha kidole kumuonyeshea mama yake Snop aliyekuwa bize kuanika nguo

    ”nani yule?"

    Ducha akauliza

    ”khaa! Inamaana hadi mama yake Snop umemsahau umkumbuki yule mama si ndiyo mlikuwa mkienda pale anawaandalia chakula mnakula na siku nyingine ulikuwa ukilala kwakina Snop?"

    “Latifa"

    ”abee"

    ”usitake kuniaminisha kitu ambacho hakina ukweli wowote ule ndani yake"

    ”mamaa"

    Latifa akapaza sauti kumwita mama yake Snop aliyeacha kuanika nguo na kuangalia sehemu ambayo sauti ilipotokea kwanza alitabasamu kwa kumuona Ducha kwake aliona Kama vile kamuona mwanaye Snop akafanya haraka kusogea pale na kufikia kumkumbatia Ducha machozi yalianza kumbumbujika

    ”hatimae mwanangu umeweza kurejea nyumbani hiiii hiiii"

    Mama yake Snop alizungumza hivyo haliyakuwa akianza kulia Ducha akafanya kujitoa maungoni mwa yule Mama

    “wee mama una kichaa au vipi? Tokea lini mi nikawa mwanao"

    “Ducha usitamke maneno hayo nikuonapo wewe nisawa na kumuona Snop usinikatae kisa Snop hayupo tafadhari baki na Mimi"

    Mama yake Snop alizungumza haliyakuwa akipiga magoti chini Latifa akawahi kumshika na kumkumbatia

    Ducha akaona kama vile wanamzingua akajiondokea zake

    “Duchaa Duchaaaa,,hiiiihiii,,,haaa"

    Mama yake Snop alipaza sauti kumwita lakini Ducha wala hakugeuka

    Kila sehemu aliyokuwa anakatiza watu walimpa pole

    Akafika nyumbani kwao

    “mama, mamaa"

    Ducha aliingia ndani huku akimwita mama yake kwa wakati huo walikuwa wamekaa sebreni wakimsubilia yeye ili waweze kunywa chai

    “abee mwanangu"

    “uko wapi mama?"

    “nipo huku Sebreni njoo"

    Ducha akaelekea Sebreni na kuikuta familia nzima ikiwa pale Yani wazazi wake wote wawili Mwanaidi na Chande

    “vipi mbona hivyo?"

    Mwanaidi akauliza baada kumuona Ducha akiwa anahema

    ”Sudi na Snop ndiyo kina nani?"

    Ducha akauliza swali ambalo kama sio kuwashangaza basi liliwashtua maana wote walitoa macho pima kumuangalia yeye

    ”nahitaji kuwafahamu nikina nani hao maana wakati naenda kufata maandazi kule kwa Zungu Kuna mmama nilikutana naye pale Muembeni akanisimamisha na kuanza kunichangamkia Mwishoe akajitambulisha kuwa yeye ni mama yake Sudi niliamua kumshiti Sasa wakati narudi nikakutana na Demu wangu Latifa naye akaanza kuniletea porojo za mtu aitwae Snop kama haitoshi akamwita na Mama yake Snop ambaye alinichangamkia pia

    Yule mama alikuja mbiombio na kunikumbatia alianza kuzungumza haliyakuwa akilia heti mwanangu hatimae umerudi sijui nikikuona wewe Ducha ni sawa na kumuona Mwanangu Snop"

    Wakati Ducha anawasimulia hivyo alishangaa kumuona mama yake na Dada yake wakianza kulia

    “sasa mbona mnalia si mniambie hao kina Sudi nikina nani?"

    Ducha akautupa ule mfuko wa maandazi chini akakimbilia chumbani kwake

    Siku ya siku hiyo alishinda chumbani mpaka ilipotimia saa nane mchana alipokuja bibie Fetty

    Akauliza kama Ducha amesharejea kutoka Kibaha akajibiwa tu! Kuwa yupo chumbani kwake akaenda kumgongea Ducha akafungua mlango hakika alifurahi Sana kumuona Fetty akamkumbatia

    “nakuona mdogo wangu siku hizi umekuwa shavu dodo bila shaka korosho za Kibaha zilikupenda"

    Fetty alizungumza haliyakuwa akitabasamu

    “korosho wapi?

    Ni mazoezi tu haya"

    ”khee kwani kuna mazoezi ya kujazia mashavu?"

    ”ndiyo yapo"

    ”unafanyaje fanyaje?"

    ”si unapuliza moto kila siku wiki mbili tu mishavu hiyo"

    ”hahahahaha"

    Fetty akacheka

    ”vipi utaondoka nami?"

    ”ndiyo maana yake"

    ”kwasasa nakuomba umuache nikae naye Kama wiki mbili tatu Kisha utakuja kumchukuwa si unajua ndiyo kwanza karudi jana kutoka kwa Bibi yake nikiwa kama mzazi nahitaji kuona uwepo wake hapa nyumbani"

    Mama yake Ducha alizungumza hivyo maana Fetty alitaka kumchukuwa Ducha

    “sawa mama haina shida basi wiki ijayo nitakuja kumfata"

    Hatimae siku ya kufungua shule iliweza kuwadia Asubuhi na mapema Ducha alielekea shuleni akiwa kaongozana na watoto wengine wa pale mtaani kwao





    ------------------

    ”khee kwani kuna mazoezi ya kujazia mashavu?"

    ”ndiyo yapo"

    ”unafanyaje fanyaje?"

    ”si unapuliza moto kila siku wiki mbili tu mishavu hiyo"

    ”hahahahaha"

    Fetty akacheka

    ”vipi utaondoka nami?"

    ”ndiyo maana yake"

    ”kwasasa nakuomba umuache nikae naye Kama wiki mbili tatu Kisha utakuja kumchukuwa si unajua ndiyo kwanza karudi jana kutoka kwa Bibi yake nikiwa kama mzazi nahitaji kuona uwepo wake hapa nyumbani"

    Mama yake Ducha alizungumza hivyo maana Fetty alitaka kumchukuwa Ducha

    “sawa mama haina shida basi wiki ijayo nitakuja kumfata"

    Hatimae siku ya kufungua shule iliweza kuwadia Asubuhi na mapema Ducha alielekea shuleni akiwa kaongozana na watoto wengine wa pale mtaani kwao



    Songa nayo

    Sasa



    Siku hiyo wanafunzi wengi walionekana kuwa na furaha wakawa wanatambiana kutokana na upya wa vitu vyao

    Kuanzia viatu mabegi na yunfom. Kwa wale waliokuja na vitu vya zamani wakaishia kuchekwa

    “hahahahaha muoneni Musa kavaa nguo za zamani na mbegi wake uliochanika hahahaha"

    Ilikuwa ni kauri ya dhihaka kutoka kwa mwanafunzi mmoja hivi

    ”yule kwao ni masikini wa kutupwa kwanza mama yake ni muokota makopo tu!"

    “hahahaha, kumbe mama yake ni muokota makopo?"

    “ndiyo tena mi nikimuonaga mama yake kabeba kiroba nakimbilia kule bondeni naenda kuyakojolea makopo yote basi akifika pale kuokota anaishikashika mikojo yangu basi mi hua nacheeka mwenyewe"

    “muoneni kwanza kaptura yake imetoboka matakoni hahahaha huyoo chokoraa"

    Musa alitamani hata kulia alichokifanya ni kujiondokea zake pale akaenda kujichanganya na wanafunzi wengine kwa muda huo wanafunzi wote walikuwa kwenye harakati za kufanya usafi

    “hivi wewe wenzako woote tumevaa nguo mpya wewe peke yako umevaa mitambaa ya zamani muone kwanza kichwa kama Nyigu"

    Alipoenda kujichanganya Musa akakutana na kichambo kutoka kwa mtoto wakike aitwae Sophia

    Muda kidogo wanafunzi wote waliitwa mstarini

    Wakatangaziwa hili na lile pamoja na kupatiwa taarifa juu ya vifo vya wanafunzi wenzao Kama kumi hivi akiwemo Snop na Sudi wapo waliofariki kwa ugonjwa wengine kugongwa na gari pikipiki nakadharika

    “toka hapa hatuwezi kukaa na wewe mtu mwenyewe unanuka mikojo"

    Hata walipoingia darasa walianza kumbagua kukaa naye,

    Musa akaangaza macho yake huku na kule akitafuta japo huruma ya Mwanafunzi mmoja ili akakae naye akaliona dawati ambalo lilikuwa tupu akaenda kukaa.

    “Ally njoo ukae hapa"

    “njoo ukae huku"

    Wanafunzi walianza kumpapatikia Ally kukaa naye yani alivyoingia tu darasani

    Ally akaenda kukaa sehemu ambayo aliichagua yeye mwenyewe japokuwa Musa naye aliomba kimoyo moyo Ally akakae pamoja naye

    Dakika si nyingi Ducha naye akatia timu ndani ya Darasa hilo

    “oyoo kichaa wangu mwenyewe huyo Ducha Duchani kwa mara nyingine teena tumekutana"

    Ally alimchangamkia Ducha akaenda mbio mbio kumkumbatia

    “mmh mijitu mingine sijui ikoje kazi kujipendekeza tu!"

    Mwanafunzi mwingine akadakia

    “hata mi ndiyo nashangaa huo Urafiki wa Ally na Ducha umeanzia wapi wakati Vichaa wake Ducha walikuwa kina Sudi"

    “oyaa nyie tulizeni vijambio hivyo"

    Ally akawakata kauli kwa kuwaambia hivyo

    Ducha akabaki kutabasamu akaenda kukaa kwenye Dawati ambaro amekaa Musa

    “Ducha njoo tukae huku"

    Ally alimtaka Ducha atoke pale alipokaa

    Ducha akafanya kupotezea kitendo ambacho kilimfanya Ally naye aende kukaa kwenye Dawati lilelile

    Baadhi ya walimu waliingia kufundisha kila mmoja kwa nafasi yake. Kengere ikalia kuashiria ya kwamba muda wa mapumziko umefika

    Musa yeye

    Alitoka darasani haliyakuwa akiwa mnyonge sana akazunguka nyuma ya Darasa akatafuta sehemu akakaa na kuanza kulia

    Aliinua uso wake kuangalia mawinguni

    “mamaa,,"

    “abee mwanangu"

    ”kwanini unalia?"

    “hapana mi silii mbona"

    ”mamaa unakataa kuwa hulii lakini mi najua nafahamu kuwa unalia maumivu uliyokuwa nayo moyoni mwako ni zaidi ya kaa la moto"

    ”Musa mi silii silii mwanangu"

    “mamaa nakuahidi nitaridhika kwa chochote kidogo unipatiacho sitolia tena mbele yako nikikosa chakula nitajikaza kulala na njaa sitojari kama nitavaa nguo zilizochanika.

    Mamaa sitaki Tena nguo za sikukuu siku hiyo nitajifungia ndani mpaka Sikukuu ipite.

    “Musa usizungumze hivyo mwanangu nitajitahidi kukununulia nguo hata ikiwa ya mtumbani nahitaji kukuona ukiwa na furaha mwanangu"

    “wee vipi mbona unalia?"

    Musa alishtushwa kutoka kwenye dimbwi la mawazo na sauti ya mtoto mwenzake akimuuliza hivyo akafanya haraka kujifuta machozi na kumuangalia huyo aliyekuwa akimuuliza hakuwa mwingine Bali ni Ducha

    “nakuuliza mbona unalia? Umepigwa nani kakupiga?"

    Ducha alimuuliza haliyakuwa akimsogelea

    “huyo ajapigwa wala nini analia kisa kina Amani wanamcheka kwa kuvaa nguo za zamani"

    Swali likajibiwa na Ally

    “na wewe ulimcheka?"

    ”hapana mi sikumcheka"

    “vuwa hilo shati"

    Ally akafanya haraka kuvua

    “na hiyo Bukta, viatu na Soksi"

    “khaa Ducha Sasa navuaje nguo zote mnataka kunibaka ehee?"

    Ally aliuliza

    ”nimesema vuwa"

    “poa haina shida wee si mbabe"

    Ally alizungumza kinyonge akavua nguo zote Ducha naye akavua

    “oyaa wee Dogo nawe vuwa nguo hizo"

    “Ducha Ducha mnataka kunibaka nyie"

    Ally alizidi kujihami Musa naye akavua

    “sasa sikieni niwaambie kitu kimoja wewe Dogo utavaa Nguo zangu Mimi nitavaa za Ally halafu Ally atavaa za kwako"

    Ducha alitoa maelekezo huku akichukuwa nguo za Ally

    “yani Mimi nivae nguo mbovu si ndiyo?"

    Ally aliuliza kengere ya kurudi Darasani ilishalia wakafanya haraka kuvaa

    “unaitwa nani ndugu yangu?"

    “Musa"

    “ohoo mi naitwa Ducha

    Kituko walivyoingia Darasani wanafunzi wote walitoa macho pima kumshangaa Ally

    “wee Ally vipi mbona umevaa nguo za yule masikini?"

    “kausha kiande wewe kwani nikivaa nguo zake naye akivaa zangu wewe kinakuuma kitu gani hasa mamaye zako

    Ntakuja kukubaka nikutie mimba mngese mkubwa wewe"

    Ally alianza kutukana mitusi mikubwa mikubwa sio kama kachukia kauli ya yule Mwanafunzi la hasha kule kuvalishwa Yunfom mbovu ndiyo kulimuuma zaidi sema hakuwa na la kufanya licha ya kumuogopa Ducha pia alikuwa anamuheshimu kwa maana nikama mtetezi wake tokea wakiwa Darasa la kwanza alikuwa akitetewa sana na Ducha pindi kina Snop wanapotaka kumzingua

    Yule Mwanafunzi akaamua kukaa kimya

    “nimsikie mjinga yoyote anachekacheka mamae nitamtia kidole cha Matako kisha apate mimba azae nyie wote Mbwa tu Tena Mimbwa koko"

    Akapiga ngumi kwenye Dawati kishindo kilichotokea kiliwafanya wanafunzi wote washtuke

    “Ally wee Ally inatosha mwamba embu njoo ukae basi"

    Ducha akajaribu kumtuliza kishingo upande Ally akaenda kukaa

    Muda wa kutoka Darasani ulipotimia kuna baadhi ya Watoto wakapeleka Umbeya kwa kaka yake Ally aliyekuwa akisoma Sekondari iliyopo mkabara na Shule hiyo ya Msingi

    “wee Ally embu kuja hapa"

    Ally akapiga hatua za unyonge kumsogelea kaka yake

    “hizi ndiyo nguo zako mpya ulizonunuliwa au?"

    “sio hizi bwana"

    ”za kwako ziko wapi sasa?"

    “kavaa Musa"

    “yuko wapi huyo Musa?"

    “yule kulee anaondoka"

    Kaka mtu akafanya haraka kumkimbilia alipomfikia akamshika mkono

    “hivi wee pimbi unajiona mbaabe mwenyewe Yani unakuja Shuleni na nguo za zamani kisha unawavua wenzio mpya huku ukiwapa za kwako si ndiyo ehee?"

    Kaka yake Ally aliuliza kwa Ghadhabu na kumfanya Musa aogope sana alianza kutetemeka

    “kaka aliyefanya hivyo sio huyu"

    “kumbe nani sasa?"

    “Duchaa huyo"

    “Duch,,,,aa"

    Kaka ake Ally alijikuta akilitamka jina la Ducha kwa kitetemeshi alimkumbuka vyema kuna kipindi alizibuliwa ngumi za uso mpaka akavimba macho na mdomo

    “vipi kuna nini hapa?"

    Lilikuwa swali kutoka Ducha naye alishajongea pale

    “huyu alinitaka nimvulie hizi nguo"

    “ahaa sio Mimi aliyekutaka uvue ni kaka huyo"

    Ally alikataa kuwa sio yeye

    “Musa kuanzia sasa wewe ndiyo mimi na Mimi ndiyo wewe yoyote atakae kuzingua ni sawa na kunizingua mimi

    Hutakiwi kumuogopa kenge yoyote yule

    Sasa unaweza kwenda nyumbani"

    Ducha alitamka kauli hiyo kiukakamavu zaidi hali iliyomfanya Musa atabasamu

    Kaka yake Ally alishajiondokea zake zamani

    Kuanzia siku hiyo Musa Ducha na Ally walikuwa ni marafiki wakushibana kizuri zaidi Ducha alianzisha Dojo la kuwafundisha ngumi marafiki zake kila siku jioni walikutania Chemba aliwafundisha vitu vingi ikiwemo Staili ya Fighting fish Wing Chun na nyinginezo

    Musa alianza kutembea kifua mbele hakuwa tena Musa yule muoga muoga watu waliokuwa wakimzingua mama yake waliipata fresh maana aliwatandika ile kisawa sawa kwa upande wa Ally naye alikuwa na kibesi mpaka nyumbani kwao kipindi cha nyuma alikuwa anamuogopa kaka yake ila tokea aanze kujifunza Mashowart alianza kumvimbia siku ambayo kaka yake alijichanganya alimtandika Kama mtoto kuanzia siku hiyo heshima nyumbani kwao ikawepo

    Siku zilizidi kuyoyoma hatimae miezi minne iliweza kukatika pasipo Ducha kuonyesha dariri yoyote ile ya kuwakumbuka kina Snop

    Kitu ambacho kiliwaumiza vichwa ndugu jamaa na watu wake wa karibu. Swala la Ducha kuwasahau kina Snop halikuwa ni jambo la kawaida inakuwaje watu wote awakumbuke kasoro Marehemu tu! Au ndiyo asiekuwepo na lake halipo yani hata kwenye picha akionyeshwa hakumbuki chochote

    “Ducha unamkumbuka huyu?"

    ”nani?"

    “huyu aliyeshika manati?"

    ”kwani nani huyu mbona kapiga picha pamoja na mimi?"

    ”Ducha mdogo wangu jamani humjui huyu si Snop na huyu

    Hapa aliyepiga msamba ni Sudi"

    Ducha akakaza macho kuiangalia ile Picha kwa umakini mwishoe akatikisa kichwa akaichukua ile Picha na kutaka kuichana Mwanaidi akawahi kumnyang'anya

    “dadaa ichane hiyo picha Tena kaichome moto"

    “kwanini?"

    “nimesema kaitie moto"

    ”siwezi kufanya hivyo wewe kama umewasahau tuachie sisi tunao wakumbuka"

    Wakati mtu na Dada yake wakizozana kuhusu swala la picha

    Upande mwingine mama yao akiwa na mama yake Sudi na Snop walionekana wakiwa Kiringeni kwa mganga sijui wameenda kufanya nini





    ------------------

    Hapa aliyepiga msamba ni Sudi"

    Ducha akakaza macho kuiangalia ile Picha kwa umakini mwishoe akatikisa kichwa akaichukua ile Picha na kutaka kuichana Mwanaidi akawahi kumnyang'anya

    “dadaa ichane hiyo picha Tena kaichome moto"

    “kwanini?"

    “nimesema kaitie moto"

    ”siwezi kufanya hivyo wewe kama umewasahau tuachie sisi tunao wakumbuka"

    Wakati mtu na Dada yake wakizozana kuhusu swala la picha

    Upande mwingine mama yao akiwa na mama yake Sudi na Snop walionekana wakiwa Kiringeni kwa mganga sijui wameenda kufanya nini?



    Songa nayo

    Sasa



    ”karibuni chana chana chanaa,"

    Mganga aliwakaribisha kwa mbwembwe zote kila mmoja akaonyeshwa sehemu ya kukaa

    “iyaaaaa,,chandaweee, nyiku,,nyikoo iiiichaaa hakika mnaonekana mna matatizo makubwa chana chachaa ahaa

    Itabidi wewe na huyu muwende nnze anaetakiwa kuyafahamu hayo matatizo ni huyu

    Ichaaaa,,"

    Mganga alizungumza kwa kiswahili kibovu huku akipiga chafya na kukoroma

    Mama yake Sudi na Snop wakatoka nnje kama walivyoambiwa ndani akabaki Mganga na mama yake Ducha

    ”ahaa najua wewe unafahamu kila kitu kuhuchu kijana wako Duchani na ichtoche haya mambo uliyoniletea utanichababichia matatinjo makubwa chana

    Chiyawezi kabichaa ahaa"

    “sasa kama huyawezi kwanini umewataka wenzangu watoke nnje?"

    ”bachi waite waambie wainginje"

    “Mama Snop"

    “abee"

    “rudini ndani mara moja"

    Basi wakaingia ndani na kukaa kwenye kimkeka chakavu Mganga aliwaangalia kwa zamu

    “nyie kina mama naomba mnichikilize kwa umakini chana tena Chana

    Kitendo mnachotaka kukifanya chi kizuri kabicha tambueni Ducha chi mtoto wa kawaida kama mfikiriavyo. Imekuwa vyema chana kwa yeye kuondolewa zile kumbukumbu kwa maana,,,,

    Mara ghafla sauti nzito ya kishindo iliweza kusikika nnje kila mmoja alishtuka na kushikwa na hali ya uwoga.

    “kwa chacha mnaweza kwenda"

    Mganga aliwaambia hivyo

    “tunaendaje Sasa wakati bado haujatuweka wazi kwa kile ambacho ulikuwa unatuelezea?"

    Mama yake Ducha akahoji

    “Tabibu kiukweli kabisa tunapenda kufahamu huhusu Ducha umesema kuwa si mtoto wa kawaida kama sio wa kawaida kumbe yeye ni nani? Na kwanini aondolewe kumbukumbu za wenzake?"

    “nani kachema Ducha chio mtoto wa kawaida nimechema ondokeni"

    Mganga alivimba na kuwataka waondoke maana alishahisi hali ya hatari iko mbeleni mwake

    Nao hawakuwa na jinsi zaidi ya kunyanyuka wakatoka nnje huku wakiulizana hili na lile

    “imekuaje tena mtu ambaye tulimtumainia kwaajili ya kututatulia tatizo letu katutolea nnje?"

    ”mi mwenyewe hata nashangaa Tabibu kabadirika ghafla baada ya kile kishindo kusikika bila shaka hapa kuna kitu si bure au wee unaonaje Shogaangu?"

    “au Kama vipi twendeni kwa Mgosi maeneo ya Tuangoma kule"

    ”mmh Mgosi tena?"

    “ndiyo Mgosi"

    “naskia huyo Mgosi hana cha uganga wala nini ni tapeli wa kutupwa"

    “hee! Umeskia kwa nani Tena mbona mi niliwahi kuambiwa kuwa kuna siku alimuibua mtoto aliyekuwa kawekwa Msukule miaka mitano?"

    “huo ni uwongo Sasa hakuna cha kumuibua wala nini alichokifanya Mgosi ni janja ya nyani yeye na Washirika wake ndiyo waliokuwa wamemteka yule mtoto wakaenda kumficha huko wanapopajua wao"

    “khee!"

    “usishangae Shogaangu mjini hapa kila mmoja wetu anaishi kwa mipango"

    “sasa tukiachana na Mgosi nani mwingine wakuweza kutusaidia?"

    “ishu ni kukomaa na huyu huyu kesho nitamuagiza Mwanaidi aje kumtega si mnajua huyu naye anavyopenda Chini bila shaka atanasa tu!"

    Basi walikubaliana pale sijui wao wameshindwa nini kumtega maana Kama chini wanazo

    Tukija kitaani kwa Muarabu siku hiyo washkaji walikuwa na kikao cha kuchangishana pesa kwaajili ya kukodi Gari ambayo itawapeleka Coco Beach siku ya Krismas kila mtu alitakiwa atoe elfu mbili

    “yoyote asietoa hela kwenye hii safari aendi"

    “ndiyo maana yake hatuhitaji wapenda vitonga sisi"

    “kwani Nahiya kashatoa?"

    “wee wa wapi wewe wakati wenzako tumesema Mademu wanaenda bure"

    “kwanini waende bure?"

    “skia nikwambie kitu Julias unapolipia wewe hiyo Elfu mbili ni sawa na kumlipia demu wako ndiyo maana tukaonelea wao hawana aja ya kutoa"

    ”sasa kwa mimi nisiekuwa na demu itakuwaje?"

    “hata ukienda na sabuni sio mbaya"

    “khaa yani niende Beach na sabuni?"

    “si ndiyo demu wako huyo mzee wa Nyeto Nyetoni"

    Wakati wanaendelea kujadiriana pale mara akapita Ducha akiwa kaongozana na Ally ikabidi Julias apaze sauti kumwita Ducha

    “oyoo Ducha Duchani mnyama mnyamani"

    Basi nao wakajongea pale maskani wakapeana tano

    ”vipi masela naona mmejikusanya wenyewe kuna ajenda gani hapa? Kama kuna ubwabwa tuambiane mapema"

    Ducha aliuliza huku akitafuta sehemu ya kukaa

    “hakuna Cha ubwabwa wala nini hapa tulikuwa tukichangishana chapaa kwaajili ya kwenda Coco Beach"

    “ohoo kumbe huo ndiyo mtonyo kiasi gani kinatakiwa kwakila mmoja wetu?"

    ”elfu mbili tu kaka"

    Ducha akaingiza mkono mfukoni akatoa noti ya shiling elfu kumi na kumkabidhi yule jamaa

    “hiyo ya mtu tatu"

    “yani wewe huyu na yule mwingine nani vilee?"

    “Musa"

    Basi majina yakaandikwa Ducha na Ally wakanyanyuka na kuondoka zao

    “oyaa Ducha chenji yako hii"

    “hiyo bakini nayo kama kuna washkaji wawili wasiotoa waandike tu!"

    Ducha aliwaambia hivyo Julias akataka arejeshewe hela yake ili akatwe kwenye ile hela aliyoiacha Ducha

    ”unaumwa kimavi wewe hii hela Ducha kasema tuwaandike wasiotoa ambao hawana kitu kabisa na safari wanaitaka ajabu wewe unataka tukurejeshee"

    ”sasa bila Mimi kumwita hapa hiyo hela ungeipatia wapi?"

    “kumwita sio ishu kwani Ducha hajagi hapa maskani oyoo Brother Chande shikamoo"

    Wakiwa wanazozana Chande naye akawasili pale wakamchangamkia na kumuamkia

    Kitu usichokijua ni kwamba Chande ni mkubwa wa majambazi naweza kusema yeye ni Jambazi sugu na vijana wake wote anaofanya nao matukio ya kiuharifu ni vijana ambao wanaishi mbali na mji yani katika mkoa wa pwani yeye peke yake ndiyo anaishi Dar,

    Ukimuona huwezi kudhania kuwa huyu mtu ni katiri wa makatiri yote sababu ya Ucheshi roho ya huruma na upendo aliokuwa nao kwa watu wote wenye kumzunguka hapo mtaani kwao ndiyo maana hakusita kumuua kijana ambaye alisababisha umauti kwa Sudi

    “vipi vijana mbona mkusanyiko mkuubwa kunani hapa?"

    Chande aliuliza

    “sio hivyo kaka embu angalia daftari hili"

    Chande akalipokea na kulitupia macho

    ”aisee inamaana kwenye hii safari Ducha naye yupo?"

    “ndiyo kaka"

    “basi nami nitakuwepo"

    “oyooo piga kelelee"

    Vijana walishangilia baada kumsikia Mwamba wa Miamba kuwa naye atakuwepo hakika waliona kuwa wamepata ulinzi tosha siku hiyo Beach hakuna wa kuwazingua

    “mpaka Sasa kimepatikana kiasi gani?"

    Chande aliuliza basi yule kijana akazitoa pesa zote na kuanza kuzihesabu

    ”ni elfu stini na saba"

    ”embu zilete hapa"

    Chande akakabidhiwa kile kiasi cha pesa akazisunda mfukoni akatoa Wallet yake akachomoa kibunda cha pesa na kumkabidhi yule kijana

    ”bila shaka hizo zitatosha kwa kutupeleka na kuturudisha"

    ”ndiyo kaka oyoo piga kelelee"

    “Chande Chande, Chande,"

    Hakika ilikuwa nderemo na vifijo wakimshangilia Chande kwa kuwapatia kiasi cha pesa laki tatu na nusu ukiachana nakile kiasi ambacho walichangishana wao.

    Siku iliyokuwa ikisubiliwa kwa hamu ikaweza kuwadia Asubuhi ya Krismas walioenda Makanisani walienda majira ya saa saba mchana walishapanda kwenye Daladala kubwa mbili

    Safari ya kuwapeleka Coco Beach ikaanza

    Madereva walishindana kwa mbwembwe

    Nyimbo ziliimbwa vijana walikunywa pombe pamoja na kuwachezea Mademu zao

    Waliokuwa wakishindana kulicheza sebeni lililokuwa likilindima ndani ya Gari hizo

    Ducha na Machizi wake walikuwa wamekaa siti ya nyuma kabisa wametulia tuli kama vile sio wao

    “ebwanaa ehee kumbe wakubwa wanafaidi ehee mi sijui ntakuwa lini mamae cheki mitako ilee natamani nikayashike"

    Ally alizungumza huku akijaramba ramba midomo laiti Majambaika wawili wangekuwepo sijui ingekuwaje yani Sudi na Snop

    “si ukayashike"

    “wee mi naogopa"

    “unaogopa kitu gani sasa?"

    “atanipiga"

    “kweli wee fala yani wewe wakupigwa na Mwanamke Kama yule kweli subiri kwanza nikuitie"

    “ahaa usimwite Ducha kausha basi"

    “Nahiya wee Nahiya"

    Ducha akapaza sauti kumwita yule binti

    “Nahiya unaitwa kulee"

    Kuna mwenzake akamshtua

    “na nani?"

    ”Ducha anakwita kule nyuma"

    Nahiya akaangalia siti ya nyuma na kumuona Ducha basi akatasamu na kwenda kumsikiliza

    “nambie kipenzi changu"

    “naomba umkatikie Dogo huyo anataka kuuchezea Msambwanda huo"

    Nahiya pasipo kujiuliza akamgeuzia matako Ally na kuanza kumkatikia

    Ally alianza kubabaika

    “yashike Sasa unaogopa nini?"

    Ducha alimuhimiza Ally ayashike

    Nahiya naye kwa kutaka sifa ndiyo kwanza akamkalia.

    “tumefika,,tumefikaa,,eheee,,Mtoto mdogo ukimshika tako serikali inasema umembakaa,,eheee"

    Zote zilikuwa ni kelele kutoka kwa vijana na watoto walishawasili maeneo ya Coco Beach kwanza walikusanywa pamoja

    “tembeeni mtembeavyo kila mmoja wenu ahakikishe saa kumi nambili kamili anakuwa hapa"

    Chande alizungumza hivyo basi wakaitikia Tawile baba ndipo wakatawanyika

    “ebwana ehee angalia zinga la toto lile"

    Mmoja kati ya vijana wa kihuni alizungumza hivyo kuwaambia wenzake wote wakageuza macho yao kumuangalia huyo binti

    “duuh mtoto ana kishundu hatari"

    Mwingine akatamka hivyo wakanyanyuka kwa pamoja na kuanza kupiga hatua kumfatiria Nahiya ndiyo binti ambaye walikuwa wakimsifia

    “oyaa tufanyeni juu chini kuhakikisha ya kwamba huu mzigo leo tunaula"

    ”mambo bibie"

    Mmoja wao akajitosa kwenda kumtongoza bibie

    ”safi tu!"

    Nahiya aliitikia huku akimuhimiza Shogaake aliyeongozana naye waondoke mara wakashtukia wakizungukwa na kikundi cha vijana wale

    “kaka Chandee"

    Nahiya alipiga kelele kumwita Chande ambaye hakuwa mbali ile sauti ikamfikia akaangalia wapi ilipotokea si akawaona wale vijana wakiwa wamewazunguka kina Nahiya akatoka mbio kuwafata

    “oyaa nyie Mbwa waachieni hao watoto wakike"

    Chande alizungumza hivyo

    ”unatuamrisha hivyo ukiwa kama nani?"

    Kijana mmoja aliuliza huku akichomoa kisu kidogo kutoka kiunoni akamfata Chande kwa kasi alipomfikia akanyoosha mkono ili amchome kisu

    Chande akaudaka mkono wa yule kijana

    Mara kohoo mkono ulivunjwa

    “mamaa wee nakufaaa, "

    Kijana alipiga kelele wenzake nao wakachomoa visu vyao kumbe kila mmoja alikuwa na kisu

    Chande akawa na mtihani wa kukwepa vile visu huku akirusha ngumi za maana

    Mwingine akavunjwa mguu waliobaki wakaona ehee wacha wakimbie maana huyu mtu ni balaa

    “oyaa brother inatosha muachie basi"

    Kuna kijana mwingine aliyekuwa amevalia nadhifu alisogea eneo lile na kumtaka Chande amuachie yule kijana ambaye alikuwa kavunjwa mkono maana Chande alikuwa kamkunja kwa kumkaba hakujari cha mkono kuning'inia wala nini

    “wee mtoto wa malaya ulikuwa unataka kuwafanya kitu gani Dada zangu?"

    Chande aliuliza

    “oyaa si nimekwambia muachie inatosha uskii au?"

    Yule kijana akaja kumtikisa Chande kwa kumgusa begani alichokifanya Chande ni kumuachie aliyemkunja na kumtandika zinga la kofi yule kijana alipepesuka

    “khaa yani unanipiga Mimi? Unijui ehee? Sasa subiri nitakuonyesha"

    Yule kijana alizungumza hivyo akatoka mbiombio hapa tunaziona njemba tatu zikiwa zimevalia Kombati za kijeshi wakiwa bize kupanga hili na lile

    “kakaa,, kakaa,, nimepigwa"

    Yule kijana alikuja mpaka pale na kutamka hivyo haliyakuwa akilia kumbe miongoni mwa wale Wajeda mmoja wao ni kaka yake

    “ongoza njia"

    Akatakiwa kuongoza njia

    Wote watatu walienda

    “nani aliyekupiga?"

    “yule pale"

    Ajabu Chande wala hakuwaogopa ndiyo kwanza akajiweka sawa kwaajili ya kukabiliana nao

    Wanajeshi walimvamia kwa mateke na ngumi mfurulizo Chande akawa anapanchi na kukwepa japokuwa nyingine zilimpata naye akawa anajibu mapigo

    Vijana wenye kumfahamu Chande ukiachana na wale aliokuja nao walimshangilia na kumtaka akaze kwani Mwanajeshi ni vazi tu! Si vinginevyo Hakuna cha kuogopa hapo

    Chande akavimba mbichwa na kuzidi kupambana ndani ya dakika kumi wanajeshi walikuwa hoi

    Ndipo inasikika sauti ya Mtu akipiga makofi ya pongezi wote wakageuka kuangalia

    Hakuwa mwingine bari ni bwana mkubwa Madebe ndani ya Kombati iliyosheheni vyeo

    Chande akajiweka tena sawa ili kukabiliana na huyu aliyekuja

    Madebe akatikisa kichwa kama kumsikitikia





    ------------------

    Vijana wenye kumfahamu Chande ukiachana na wale aliokuja nao walimshangilia na kumtaka akaze kwani Mwanajeshi ni vazi tu! Si vinginevyo Hakuna cha kuogopa hapo

    Chande akavimba mbichwa na kuzidi kupambana ndani ya dakika kumi wanajeshi walikuwa hoi

    Ndipo inasikika sauti ya Mtu akipiga makofi ya pongezi wote wakageuka kuangalia

    Hakuwa mwingine bari ni bwana mkubwa Madebe ndani ya Kombati iliyosheheni vyeo

    Chande akajiweka tena sawa ili kukabiliana na huyu aliyekuja

    Madebe akatikisa kichwa kama kumsikitikia



    Songa nayo

    Sasa



    Madebe akawa anapiga hatua za taratibu kumsogelea Chande ambaye alijiweka vyema kwa kukunja ngumi hakuweza kufahamu kama huyu aliyekuja mbele yake ni mtu hatari Sana

    Alipokaribiwa tu alirusha ngumi mbili tatu ambazo zote zilikwepwa akarusha teke mguu ukakutana na kiwiko huku akiongezewa kwa kupigwa ngumi ya kifua iliyomfanya Chande arudi nyuma kwa kupepesuka

    Akajiweka tena sawa na kumfata Madebe kwa kasi safari hii

    Alijaribu kubadirisha mapigo lakini wapi! Kila akipiga mwenzake anazitoa kwa kupanchi na kukwepa tena kwa dharau

    Madebe akawa anajipangusa kila akiguswa anajipangusa

    Ndani ya Dakika tano waliokuwa wakimshangilia Chande wakanyamaza kimya baada kushuhudia mtu wao akipigwa kama mtoto

    Chande alishadebweda sema alijitahidi kupambana kiume ikawa kila akirusha ngumi

    Anapigwa yeye

    Mwishoe Chande alipiga magoti chini ikiwa na maana nguvu ya kusimama hakuwa nayo

    ”embu vijana mkamateni huyu pimbi?"

    Madebe alizungumza hivyo nao bila kuchelewa wakamshika na kuanza kumburuza kumpeleka barabarani walimburuza huku wakimshushia kipigo cha maana Kama ujuavyo wanajeshi upigaji wao ni hatari kina Nahiya walilia kumlilia Chande wakafanya kukusanyika sehemu moja

    ”hivi nyie watoto mna wazimu ehee?"

    Lilikuwa swali kutoka kwa Binti mrembo wa haja akiwauliza kina Ducha

    ”nikweli tuna kichaa na kichaa chetu kimetokana na wewe hapo"

    Ducha akajibu kwa niaba ya wenzie

    “mmh kivipi kitokane na mimi?"

    Yule Binti akauliza

    ”wee mwenyewe ujioni kwajinsi ulivyo fungashia mtoto bambataa"

    Ducha akajibu na kutaka kumshika yule binti

    “hata kama nimefungashia au kuchomekea nyie inawahusu kitu gani? Watoto wadogo mnataka kupalamia vitu vya kikubwa embu kwendeni zenu huko"

    Yule binti alizungumza kwa kubetua midomo

    “nani mtoto sasa?"

    Ducha akauliza

    “khee kwani hamjioni Kama nyie ni watoto hapo mlipo mnanuka shombo ya maziwa ya mama zenu"

    ”wewee embu acha dharau zako mbona wewe unanuka Shombo ya mboo hatusemi"

    “uwiiiii wee mtoto umesemaje?"

    ”kwani wee ulisemaje?"

    “Mudi,,wee Mudii"

    Yule Binti akapaza sauti kuita Mudi muda kidogo kuna jamaa mbavu nene alionekana akija mbiombio uwelekeo ule

    “vipi tena my dear mbona wapiga kelele"

    Yule jamaa baada kufika pale aliuliza huku akiweka suruwali yake vyema maana kule kukimbia kwake ikawa Kama inamvuka na kumfanya aonekane kavalia kata kei

    ”si hawa hapa watoto wamenifatiria kutokea kule Coco mpaka huku Namanga njia nzima walikuwa wananitukana heti mi ni Malaya najiuza,,

    Wakati yule binti anazungumza Mudi akaokota moja kati ya miti na kuwaonyeshea kina Ducha waliokuwa wamesimama pasipo kuwa na wasiwasi wowote

    “nyie mafala kum* za mama zenu yani mnadiriki vipi kumtusi mke wangu mtarajiwa Sasa kwa usalama wenu kila mmoja alale chini nimtandike bakora"

    “hahahaha,, teh,,teh,,teh

    Oyaa mmemsikia huyu matako mkund* kunuka anachokizungumza kudadeki zake"

    Kina Ducha kwanza walicheka huku Musa akizungumza hivyo

    Ile kauli ndiyo ilizidi kumchukiza Mudi akafanya kuwafata na kuinua mkono wake juu kwaajili ya kumpiga mmoja wao alichokifanya Musa ni kudunda kwenda juu akakita mgongoni mwa Ducha aliyefanya kuinama kifuti kikatua usoni Mudi alipiga yowe la uchungu Ally akaserereka na kupiga ngumi kwenye pumbu

    Wakati Ducha akifutuka na teke moja zito lilitua shingoni Mudi akaenda msobemsobe akadondoka chini chali

    Kina Ducha wakakimbia kurejea zao Coco Beach walishamzimisha mtu

    Sauti tu za kilio kutoka kwa yule binti ndizo zilizosikika masikioni mwao akimlilia mpenzi wake

    Walipowasili maeneo ya Beach walishangazwa kidogo baada kuwaona wenzao wakiwa wamekusanyika sehemu moja huku wengine wakionekana kulia kwa kwikwi

    “nyie vipi tena mbona mnaonekana kulia? Kuna tatizo lolote limetokea?"

    Ducha aliuliza

    Hakuna aliyekuwa na jibu zaidi ya kutikisa vichwa

    “au kuna mmoja wetu kazama baharini?"

    Musa naye akauliza

    “sio hivyo Musa"

    ”kumbe nini sasa?"

    “kaka Chande kapigwa na kukamatwa na Wanajeshi"

    “khaa! Wamempeleka wapi sasa?"

    Ducha akauliza

    “wapo naye kule kwenye Clabu"

    Ducha akawataka kina Ally wamfate lakini wenzake walikataa

    “hapana Ducha hatutakiwi kwenda kule hata tukienda hatutoweza kumsaidia Chande kwa maana Wanajeshi sio watu wa mchezo mchezo tutapigwa sisi"

    Musa alizungumza hivyo Ducha aliwaangalia marafiki zake kwa zamu kisha akatoka mbio kuelekea sehemu ambayo aliambiwa Chande kashikiliwa

    ”Duchaa usiende huko Duchaa

    Wenzake walipaza sauti kumwita

    Sehemu yenyewe haikuwa mbali na pale

    Ducha aliweza kumuona Chande akiwa kakalishwa chini huku damu zikionekana kumchuruzika puani na mdononi hakika alikuwa na majeraha mengi usoni mwake.

    Ducha alijipa ujasiri wa aina yake alifanya kusogea mpaka pale alipokuwa kashikiliwa Chande

    “nyie Mbwa embu muachilieni kaka yangu"

    Ducha alipaza sauti kuwaambia hivyo heti aliwaita Wanajeshi ni Mbwa ni kauri ambayo kama sio kuwachefua basi iliwauzi kupita kiasi

    “wee mtoto unasemaje?"

    Mmoja kati ya wale wanajeshi aliuliza huku akipiga hatua kumsogelea Ducha aliyeanza kurudi kinyume nyume

    Alipomkaribia akanyoosha mkono kwa niya ya kumkamata Ducha akainama na kurusha ngumi iliyotua ubavuni yule Mwanajeshi kwanza alibonyea kwa maana ile ngumi ilimuingia ile kisawa sawa

    “oghooo,,ighiiii"

    Alitoa mghuno wa maumivu

    Wenzake kuona vile wakaja mbio na kumuweka Ducha kati muda huo Madebe alikuwa kakaa pembeni akiwaangalia tu!

    Basi wakafanikiwa kumtia mikononi

    Ducha alikukuruka kujitoa mikononi mwa wale Wanajeshi lakini wapi wakamlaza chini kuna mti ukakatwa akatandikwa fimbo mbili za nguvu

    Ducha alilia kwa maumivu

    “mwaliiimu"

    Ducha alipiga kelele kumwita mwalimu wake ni kelele ambazo zilifatiwa na upepo mkali kuvuma

    Watu walijiziba nyuso zao maana ule upepo haukuwa wa kawaida michanga ilitimka mithiri ya vumbi

    Ghafla bin vuu bwana mkubwa Chinoge akaibuka na kufikia kutembeza kichapo tafrani iliyowatokea Wanajeshi wale ilikuwa ni balaa

    Wakati Chinoge akipambana vyema na Wanajeshi wale watatu Ducha akabiduka Tiktaka na kujibimbilisha alipokuja kukaa sawa akaachia zinga la teke lililotua usoni mwa Madebe mzee mzima alipepesuka akajishika usoni na kujiangalia Kama atakuwa katolewa damu au vipi

    “usirudie makosa"

    Alishtuliwa na sauti ya Chinoge

    Binafsi alibabaika kidogo akabaki kumuangalia tu usoni

    Chinoge alizungumza kauli moja tu kisha akapotea

    Ducha alishamchukuwa Chande na kuondoka naye

    Sauti pekee iliyokuwa ikisikika ndani ya gari ni sauti ya mziki uliokuwa ukirindima

    Wakati vijana kwa watoto wote walikuwa kimya bila shaka kila mmoja alikuwa akitafakari kile ambacho kimetokea Coco Beach

    Ukiachana na ujasiri wa Ducha je yule kiumbe aliyejitokeza pale na kumsaidia Ducha ni nani?

    Hakuna aliyekuwa na jibu kamili juu ya yule kiumbe

    Chande alishushwa Mbagala Zakhiem na kuwahishwa hospitali wakati wengine wakiendelea na safari ya kurejea majumbani mwao

    “yule mtoto ni nani? Imekuwaje Chinoge akajitokeza kuja kumsaidia kuna uhusiano gani baina yao ni Mwanae au vipi?"

    Ni maswali mfurulizo aliyokuwa akijiuliza bwana mkubwa Madebe akiwa amekaa kwenye kiti akaitoa simu yake mfukoni iliyokuwa ikiita akaipokea na kuiweka mfukoni

    “nambie kijana"

    ”kila kitu nishafanikisha mkuu"

    ”ehee ndiyo nakusikiliza"

    ”yule dogo anaishi Mbagala kwa Muarabu kama unataka kwenda Kilungule anasoma shule ya msingi Nzasa darasa la tatu"

    “ohoo vizuri sana kijana na vipi kuhusu nyumba namba ngapi?"

    Kiukweli nyumba yao haina namba ila niliipiga picha nitakutumia kwa njia ya whatsapp"

    “kazi nzuri kijana na vipi kuhusu jina lake?"

    “anaitwa Ducha Duchani Yani anafahamika Mbagala nzima"

    ”ok nikutakie siku njema kijana"

    Simu ikakatwa Madebe akaiweka simu mezani akawa anafikiria kitu akasimama na kuvuta droo ya meza akaichomoa Bastola kwanza akaiangalia kuna risasi ngapi baada ya kujiridhisha akaifutika kiunoni akachukuwa simu yake na kutoka nnje

    Kumbe alikuwa ndani ya ofisi ya kijeshi alipotoka nnje kulikuwa na Wanajeshi kibao wakiendelea na pilikapilika za hapa na pale

    Madebe aliangalia saa yake ya mkononi akapanda pikipiki safari ya kuelekea Mbagala ikaanza akiwa mitaa ya Boma mataa almanusura amgonge kijana mmoja aliyevuka Barabara akiwa mbiombio huku mkononi akiwa kashikilia mkoba wa kike

    “jamani mwizii, mwizii, mkoba wangu,,jamanii,,hiii,,mkoba, wangu"

    Ni kelele zilizoweza kusikika kutoka kwa binti mmoja akililia mkoba wake kumbe yule kijana ni mwizi alichokifanya Madebe ni kuizungusha Pikipiki yake akapita kwenye tuta na kuanza kumfatiria yule mwizi

    Kwani aliona kama ataamua kumkimbiza kwa miguu hatoweza kumfikia kwa haraka

    Yule kijana naye alizidi kukimbia Ghafla akashtukia akipigwa zinga la kibao cha kichogoni akapepesuka na kudondoka chini

    Akanyanyuliwa kwa kukunjwa akapigwa kibao cha shavuni

    Kilichomfanya awe na mawenge fulani watu walishajazana pale kutaka kufahamu kunani

    Kuna Maafande nao wakajongea na kutaka kumkamata Madebe kwa kosa la kumpiga yule kijana hadharani

    Madebe akatoa kitambulisho chake na kuwaonesha Maafande walitetemeka si kidogo wakaishia kupiga Saruti bwana mkubwa akauchukuwa ule mkoba na kuondoka nao alimkuta yule Binti ambaye sisi tunamfahamu kuwa anaitwa Mwanaidi Dada yake Ducha akiwa kaegemea kibanda cha machinga huku akijifuta machozi

    “pole sana Dada yangu shika mzigo wako huu"

    Alizungumza hivyo Madebe huku akinyoosha mkono kumpatia mkoba wake kwanza Mwanaidi hakuweza kuamini macho yake akaupokea ule mkoba na kuufungua akaangalia ndani yake

    ”vipi kila kitu chako kipo sawa?"

    “ndiyo kaka yangu Asante sana sijui hata nikushkuru vipi"

    “usijari Binti siku zote katika maisha kuna kusaidiana leo kwako kesho huwenda ikawa kwangu"

    Alizungumza hivyo Madebe huku akipiga hatua kuifata Pikipiki yake Mwanaidi alibaki kumsindikiza kwa macho mpaka pale alipotoweka mbele ya upeo wa macho yake naye akafanya utaratibu wa kupanda Daladala inayotokea Kawe kuelekea Mbagala laiti Kama Madebe angelifahamu kuwa Mtoto anaemfatiria kuwa ni ndugu na Binti yule bila shaka angempakia kwenye Pikipiki

    Yapata majira ya saa tano Asubuhi

    Muda huo wanafunzi wengi walikuwa kwenye pilikapilika za kununua vitu vya kula na kunywa baada kutoka mapumziko

    Nikweli Ducha alikuwa yupo Darasa la tatu

    “oyaa Ducha unaitwa kulee"

    Kuna Mwanafunzi alikuja mbio mbio mpaka pale walipokaa kina Ducha na kumwambia hivyo Ducha akaangalia Nani anaemwita lakini hakuweza kumuona vizuri akasimama na kwenda kusikiliza wito

    “habari yako kijana vipi hujambo?"

    Madebe akajifanya kumchangamkia Ducha na kumpatia mkono

    Ducha pasipo kunyoosha mkono wake wala kuitikia ile salamu alimuangalia Madebe kwa kumshusha na kumpandisha

    “hivi wewe ni Mwanajeshi wa aina gani? Wenzako wanalinda Raia na mali zao ajabu wewe unawapiga raia wako"

    Ducha alianza kuzungumza kwa kupaniki.

    ”ohoo mkuu tuachane na hayo kwanza pia kumbuka sikufanya vile kwa kukusudia nilikuwa nawatetea Vijana wangu wa kazi naomba unisamehe mkuu"

    Madebe alizungumza kwa sauti ya upole

    ”sawa nimekusamehe je umefata kitu gani huku?"

    “nimekufata wewe mkuu"

    “umenifatia nini? Au unataka kunirudishia nilivyokupiga?"

    “hapana sio hivyo Ducha"

    “khaa inamaana hadi jina langu unalijua aisee umelijuaje?"

    “si mtu maarufu wewe"

    “nani maarufu?"

    “si wewe hapo! Yani Mbagala nzima unafahamika"

    “ahaa wapi"

    “ndiyo hivyo kijana umeanza kuwa mtu maarufu angali ukiwa mdogo"

    “bwana ehee embu acha kunichora kwanza nambie ulichoniitia"

    Basi Madebe akamtaka Ducha wakakae sehemu kwaajili ya mazungumzo

    ”khaa si unaskia kengere inalia hiyo wacha mi nirudi zangu Darasani"

    Ducha alizungumza hivyo

    ”vipi una simu?"

    Madebe akauliza swali la kijinga Sana mtoto mdogo kama Ducha simu anaitolea wapi

    “nilijua tu kuwa wee jamaa akili zako hazina akili"

    “hahahaha sawa"

    “sema nini nitakupatia namba za Dada yangu kwa sharti moja tu! Usije ukamtongoza"

    “sawa haina shida nipatie tu!"

    Basi Ducha akataja namba za simu ya Mwanaidi kisha akaelekea zake Darasani

    “Duchaa,, wee Ducha"

    Mwanaidi alipaza sauti kumwita mdogo wake huku akigonga mlango

    “nini tena Dada unasemaje?"

    “embu fungua mlango kuna simu yako huku"

    “hee simu yangu nani kaninunulia?"

    Ducha aliuliza huku akifungua mlango

    ”embu shika simu hii uwongee na mtu wako"

    “nani kwani?"

    ”mi simjui yee kasema tu namtaka Ducha halafu tabiya ya kuwapa namba yangu wahuni wenzako ukome nyau"

    Mwanaidi alizungumza hivyo na kumpatia simu Ducha

    “ahaa kumbe simu yenyewe ya masimango Kama vipi mwambie huyo mshkaji kuwa Ducha hayupo"

    “sasa namwambiaje haupo wakati anakusikia hapa"

    “wee si umesema nisiwape namba masela wangu?"

    “sio hivyo bwana Ducha embu pokea basi uzungumze naye huyu jamaa kasema anaitwa Madebe sijui Manyanga"

    ”ohoo kumbe Madebe"

    Ducha akaichukuwa simu na kuiweka sikioni

    “vipi ushamaliza kubishana na Dada yako?"

    Sauti ya Madebe ikasikika upande wa pili ikiuliza hivyo

    ”ahaa achana naye anazingua huyu"

    Basi waliweza kuzungumza mambo kadhaa majira ya usiku Ducha akiwa amelala akaota ndoto kuwa yupo sehemu moja hivi amekaa

    “oyoo Ducha mambo vipi?"

    “safi tu!"

    “hivi Ducha kipindi chote hicho ulichokuwa huko Duniani bado umetusahau tu!"

    “kuwasahau kivipi na nyie nikina nani?"

    “khaa yani utatuuliza sisi nikina nani wee una kichaa au?"

    “halafu sikia wee fala usiniambie kuwa nina kichaa hunijui sikujui ntakuzingua Sasa hivi?"

    “umzingue nani wee fala tu"

    Ducha akasimama na kumkunja Sudi ambaye naye akafanya kumkunja Ducha wakawa wamekunjana Snop akaingilia kati kuwaachanisha

    “Ducha acha"

    Sauti ya ukari ilisikika kutoka kwa Chinoge akimtaka Ducha asipigane

    Wote wakaachiana

    “wee si unajifanya umetusahau sisi ehee? Basi haina noma ila kaa utambue kuwa Sudi na Snop ni wamoja tu si umetutenga sababu tumefariki"

    Sudi alizungumza huku akianza kulia

    “vijana mnaweza kwenda"

    Bwana mkubwa Chinoge alishawasili pale na kuwataka kina Snop waondoke

    “mwalimu nikina nani wale?"

    Ducha aliuliza huku akiwasindikiza kina Snop kwa macho alichokifanya Chinoge ni kumshika Ducha kichwani

    “Sudiiiiiii"

    Ducha alipiga kelelee kumwita Sudi kelele ambazo zilimfanya ashtuke kutoka usingizini akiwa anahema

    Mlango wa chumbani kwake ukafunguliwa mama yake akaingia mbio mbio akiwa kaongozana na Mumewe pamoja na Mwanaidi

    ”yuko wapi Sudi? Yuko Snop?"

    Pindi walipoingia tu wakakutana na maswali hayo kutoka kwa Ducha





    ------------------

    “wee si unajifanya umetusahau sisi ehee? Basi haina noma ila kaa utambue kuwa Sudi na Snop ni wamoja tu si umetutenga sababu tumefariki"

    Sudi alizungumza huku akianza kulia

    “vijana mnaweza kwenda"

    Bwana mkubwa Chinoge alishawasili pale na kuwataka kina Snop waondoke

    “mwalimu nikina nani wale?"

    Ducha aliuliza huku akiwasindikiza kina Snop kwa macho alichokifanya Chinoge ni kumshika Ducha kichwani

    “Sudiiiiiii"

    Ducha alipiga kelelee kumwita Sudi kelele ambazo zilimfanya ashtuke kutoka usingizini akiwa anahema

    Mlango wa chumbani kwake ukafunguliwa mama yake akaingia mbio mbio akiwa kaongozana na Mumewe pamoja na Mwanaidi

    ”yuko wapi Sudi? Yuko Snop?"

    Pindi walipoingia tu wakakutana na maswali hayo kutoka kwa Ducha



    Songa nayo

    Sasa



    Lilikuwa ni swali ambalo Kama sio kuwashtua Basi liliwaogopesha

    “mbona hatuwafahamu hao watu nikina nani kwani?"

    Mwanaidi akajifanya kupotezea lile swali badara yake akauliza yeye

    Ducha alimuangalia Dada yake kwa umakini Sana

    “naomba ukaniletee maji ya kunywa"

    Ducha akaomba maji ya kunywa Mwanaidi akafanya haraka kwenda kumletea

    ”maji haya hapa kaka yangu kipenzi"

    Mwanaidi alizungumza hivyo huku akimpatia kikombe cha maji Ducha aliyapokea na kuyanywa yote

    ”haya fanyeni kutoka chumbani kwangu nahitaji kulala"

    Ducha baada kunywa maji aliwaomba watoke chumbani kwake nao wakafanya hivyo haliyakuwa wakiwa na wasiwasi mioyoni mwao

    Ducha akajilaza huku macho yake akiangalia juu ya dari

    “kwani nani kamkumbusha?"

    ”mmh Mama kabra ya kuuliza hilo swali inabidi ujiulize kwani nani aliyemsahaurisha?"

    ”mmh hakika napata ukakasi mkubwa sana juu ya jambo hili"

    “kwani mama Ducha ni nani?"

    “unauliza Ducha ni nani? Inamaana nawe ushaanza kuwa na mawenge ehee?"

    “sio hivyo mama"

    Yote yalikuwa ni majadiriano baina ya Mwanaidi na mama yake kwa upande wao usingizi ulishakata walikaa Sebreni wakizungumza hili na lile

    Mpaka kunakucha asubuhi na mapema Ducha aliamka akajiandaa kwenda shule, siku hiyo Ducha alichukuwa kisu kabatini na kukificha kwenye Begi lake la shule

    “mama mi naenda"

    “haya mwanangu nikutakie masomo mema"

    Ducha alimuaga mama yake akatoka nnje kwa mwendo wa taratiibu alitembea kufika kwenye kichochoro kimoja wapo

    Aliangalia kushoto na kulia kisha akapotea kimiujiza.

    Ndani ya nyumba moja wapo maeneo ya Mbagala Kizuiani ziliweza kusikika kelele za Mwanadada akilia kwa sauti

    “hiii nisamehe mume wangu sirudii tena uwiii nakufa Mimi yalaa,, nimekoma sirudii"

    Sauti ya kilio chake ziliambatana na vishindo bila shaka alikuwa akipigwa

    ”mmh mi ndiyo maana sitakagi kuwa na Mwanaume Mwanajeshi angalia Sasa Amina kila siku amekuwa ni mtu wa kupigwa pasipo sababu"

    ”wee naye wawapi nani aliyekwambia ukiolewa na Mwanajeshi utakuwa wa kupigwa? Tambua kupiga ni hurka ya mtu awe Kondakta dereva wa Daladala sijui migari mikubwa au mbeba zege muuza Duka nakadharika Kama kazoea kupiga wanawake utapigwa tu!

    Wangapi wana wanaume wanajeshi hawajawahi hata kukalipiwa"

    “lakini huyu

    Samweli kazidi kumgeuza mwenzake ngoma jamani"

    “mi niliwahi kumwambia Amina kuwa Samweli sio mtu mzuri akaniona mi mbeya sijui namuonea wivu kuwa na Mwanajeshi angalia Sasa anavyotolewa ngeu"

    Yote yalikuwa ni mazungumzo kutoka kwa majirani waliokuwa wamejazana nnje

    Wengine wakawa wanachungulia dirishani

    Ndani ya chumba nikweli bibie Amina alikuwa akipigwa na mkanda wa suruwali mpigaji hakuchagua sehemu ya kupiga alimlarua popote pale iwe usoni kichwani

    Amina alilia kwa maumivu huku damu zikimchuruzika juu ya nyusi nyingine puani na mdomoni alijaribu kukinga mikono kuomba msamaha lakini Samweli hakutaka kusikia

    “ulikuwa wapi mpaka Maharage yakaungua mshenzi wewe?"

    Samweli aliuliza huku akiachia zinga la kofi likatua shavuni mwa Amina hata nafasi ya kujibu hakuwa nayo akaongezewa teke la tumbo

    “wee Samweli wewe kumbuka Amina ni mjamzito huyo unampigaje namna hiyo utakuja kumuua jamani"

    Kuna Mwanamama aliyekuwa akichungulia dirishani Uvumilivu ulimshinda na kuamua kuzungumza hivyo

    Alichokifanya Samweli ni kushika kitasa cha mlango akatoka nnje huku akimuacha Amina akigalagala pale Sakafuni kwa kujishika Tumboni Damu zilianza kumtoka sehemu ya mbele

    “fala gani huyo anaejaribu kunikeme,,,oh,,"

    Samweli alitoka nnje na kuuliza swali ambalo alishindwa kumalizia kuzungumza akajishika Shingoni damu zilimchuruzika Kama vile kuku kishingo aliyechinjwa akadondoka chini puuh alipapatika kwa muda na kutulia kumbe kuna kisu kilikuja kwa kasi na kukita Shingoni mwake

    Majirani walishikwa na taharuki wasikimbie mchezo

    Wakati majirani wakikimbia hovyo ghafla Ducha akaibuka akausogelea mwili wa Samweli akakichomoa kile kisu akakipangusa Damu na kutoweka

    Taarifa za kuwawa kwa Samweli ziliweza kufika kwa Wanajeshi wenzake wakafanya haraka kuwasili eneo la tukio Kuna baadhi ya watu walikamatwa

    Amina aliwahishwa hospitali

    “Ducha,wee,Ducha"

    ”nini bwana?"

    ”kengere ishalia twenzetu kwa mama Vitumbua"

    ”nyie nendeni"

    ”tunaendaje Sasa wakati mshiko unao wewe"

    ”si mchukuwe hela ipo kwenye Begi"

    Musa akalichukuwa Begi la Ducha na kufungua zipu

    “khaa Ducha umekuja na kisu shule?"

    Musa aliuliza na kumfanya Ally atake kuchungulia ndani ya Begi.

    Ducha akawahi kulichukuwa Begi lake akakaza macho kumuangalia Musa kama vile ni mara yake ya kwanza kumuona

    ”wewe shida yako ni hela au kutaka kufahamu kilichomo humu?"

    Ducha akauliza

    ”shida yangu ni hela"

    Ducha akapapasa na kutoa noti ya elfu mbili na kuwapatia Ally na Musa wakatoka zao

    Ducha aliangaza macho yake kuangalia nnje kwa kupitia dirishani mara kwa mbaali aliweza kumuona Askari polisi akiwa kasimama na kijana mmoja hivi wakizungumza kitu alimuangalia kwa umakini yule Askari mpaka alipoagana na yule kijana Ducha akatoweka

    Yule Askari akiwa amesimama sehemu akijiandaa kuvuka Barabara ghafla akajishika Shingoni lilikuwa ni tukio la kustusha na kuogopesha kuona Afande yule akitenganishwa kiwiliwili na kichwa

    Likawa tukio la pili kutokea kwa siku moja Tena kwa mda mfupi tu kule Mwanajeshi huku Askari polisi wote wakiuwawa kwa kuchinjwa

    “ujuwe mwenzako hapa najiuliza kwanini Ducha kaja nakisu shuleni?"

    ”kwani wewe inakuhusu nini? Kama vipi na wewe kesho njoo nacho"

    ”sasa nije nacho cha kazi gani?"

    ”ndiyo ukaushe sasa sio kuropoka ropoka tu! Kama vile umetekenywa tako"

    “ohoo Ally hayo matusi sasa"

    ”sio matusi nakwambia ukweli wee ujaona jinsi Ducha alivyokuangalia kwa jicho baya ehee?"

    ”nilimuona"

    ”basi ujuwe alikumaindi kishenzi"

    “oyaa nyie vibwengo"

    Wakashtuliwa na Sauti ya Ducha akiwaita hivyo walipomuangalia wote mwa pamoja walishtuka baada kumuona Ducha akiwa kashika kisu

    “Ducha kwani hicho kisu cha nini?"

    Ally aliuliza

    “cha kuchinjia paka"

    Ducha alijibu kiutani akakifutika kile kisu kiunoni

    Hakuna aliyehitaji kuhoji mpaka muda wa kutoka shuleni ulipotimia wanafunzi wakatawanyika kwenda majumbani

    Hapa tunamuona Chande akiwa bize kufanya mazoezi ya kunyanyua chuma alinyanyua kama roundi sita mara akashtuka baada kuona kile chuma kimeongezeka uzito kutoka kilogram hamsini mpaka mia moja alijikakamua kukinyanyua lakini wapi chuma kilikuwa kimembana kifuani kila akijitahidi kukitoa alishindwa alijaribu kupiga kelele kuita watu ili waje kumsaidia sauti nayo wala haikutoka

    Alibanwa ile kisawasawa

    Nguvu zilianza kumuishia mwishoe akapoteza maisha.

    Kifo cha Chande kiliwashtua watu wengi Sana naye alikutwa akiwa amekatwa koromeo wakati tuliona kuwa alibanwa na chuma ndugu jamaa na marafiki walilia

    “uwiiii,, jamani Chandee,,hiii"

    Sauti ya kilio kutoka kwa Mwanaidi ilisikika masikioni mwa Ducha aliyekuwa bize kucheza na Mbwa wake aitwae Max

    “Chande,,jamani Chandee,,hiiiiiii,,haaaa,,"

    Mama yake Ducha naye akawa analia majirani wakafanya kazi ya ziada kuwatuliza kwa upande wa Ducha wala hakuonekana kuguswa na chochote juu ya kifo cha Chande akaingia zake Chumbani kwake

    “Dunia ina watu wanafki sana yani Ukiwaangalia machoni ni kama watu kumbe moyoni hawana utu mliniulia rafiki zangu ndugu zangu Snop na Sudi nanyi hamna budi kwenda kuzimu nitauwa kila jambazi kila Askari na Mwanajeshi na yoyote yule atakaejaribu kufatiria hili jambo. Kama mlishindwa kufatiria vifo vya ndugu zangu kipindi chote hicho mkakaa kimya. Basi ni vyema na hili mkae kimya"

    Ducha alizungumza kwa kuuma meno kisha akatoweka kama vile upepo.

    Vijana wazee kwa watoto walifurika nyumbani kwa kina Chande wakina mama walilia kumlilia Chande wenzake aliokuwa akishirikiana nao kwenye swala zima la ujambazi walionekana wamekaa pembeni wakiteta jambo

    “bila shaka mzigo wa jana alikuwa nao Marehemu na leo ndiyo tulipanga tukutane kwaajili ya Mgao wetu sasa itabidi tufanye juu chini ili mmoja kati yetu aweze kuingia Chumbani kwa jamaa akaulete ule mzigo"

    Basi mmoja kati yao akapiga hatua kuingia ukumbini kulikuwa na Wanawake kibao wamekaa pale akasalimia na kutokezea mabanda ya Uwani

    “vipi tena Baba unataka kwenda kufanya nini Chumbani kwa Marehemu?"

    Kuna Mwanamama akamuuliza yule jamaa baada kumuona akishika kitasa cha mlango

    “kuna kitu nimeagizwa na Sheikhe"

    Jamaa akajibu hivyo akafungua mlango na kuingia ndani taratiibu akausindika ule mlango ile anageuka tu akakutana na kisu shingoni akatoa ulimi nnje akajishika Shingoni

    Ducha akaibuka Chumbani mule akakishika kisu na kutoweka nacho huku Nnje wenzake walikuwa wakimsubilia yeye muda ulizidi kuyoyoma pasipo yeye kurejea hawakuweza kufahamu kama mwenzao tayari ameshauwawa majira ya saa kumi Alasir mwili wa Marehemu Chande ulishaandaliwa ukaswaliwa ukabebwa safari ya kuelekea makaburini ikaanza

    “embu nenda kamuangalie"

    Akaagizwa mmoja wao wakati Wengine wakiongozana na wazikaji kuelekea makaburini

    “Ducha mbona wee hulii?"

    Lilikuwa swali kutoka kwa mmoja kati ya watoto wa pale mtaani kwao

    “tokea lini Ducha akalia?"

    Mtoto mwingine akamuuliza yule aliyeuliza swali

    kama ujuavyo Wanawake wa Kiislamu hawaruhusiwi kwenda kuzika basi

    Mwanaidi alikuwa amekaa kwenye mkeka kule kulia alishanyamaza alionekana kuchezea simu yake kubwa aina ya Infinix hot8 mara ikawa inaita akaiacha iite kwa mda kidogo ndipo akaipokea

    “habari yako Dada yangu?"

    “safi tu! Nambie"

    “kwasasa hapa kwa Muarabu wee uko wapi?"

    “nipo huku karibu na Shule ya Chekechea Nzasa"

    “ohoo kama hautojari unaweza ukanifata hapa bondeni kuna vijana wanaosha Pikipiki"

    ”sawa nisubiri nakuja Sasa hivi umevaaje wewe?"

    “nipo na kombati za Jeshi"

    “mmh kumbe mtu mwenyewe ni Mwanajeshi?"

    “ndiyo Dada yangu"

    Wakati Mwanaidi anazungumza na simu alishasimama na kuanza kuelekea huko bondeni kufika sehemu akasimama na kupunga mkono

    Kumbe alikuwa ni bwana mkubwa Madebe

    “khaa kumbe ni wewe?"

    Mwanaidi alishangazwa Sana kumuona mtu yule maana alishamkumbuka kuwa siku kadhaa nyuma aliwahi kumsaidia kule Ilala Boma

    “ooh inamaana wewe ndiyo Dada yake Ducha?"

    “ndiyo Mimi"

    “hakika Mungu ni waajabu sana na bila shaka alikuwa na makusudio yake kutukutanisha sikuile"

    Madebe alizungumza hivyo Mwanaidi akabaki kutabasamu tu

    “jamanii muwaji hukuu,,jamaniiii,,"

    Kelele zilisikika kutoka kwa wamama na kuwafanya Madebe na Mwanaidi waende kule mbiombio

    Yule Jambazi aliyeagizwa kwenda kumuangalia mwenzake si aliufungua ule mlango kuchungulia hivi ndani akashtuka baada kumuona mwenzake akiwa kalala chini

    Akaingia chumbani moja kwa moja Damu zikawa zinachuruzika kupitia mlangoni ndipo wamama wakaanza kupiga kelele jamaa kuskia vile akatoka nnje na kuanza kukimbia lakini hakuweza kufika mbali alishtukia akichotwa zinga la mtama akadondoka chini kuja kumuangalia aliyemtendea kitendo hiko ni Mwanajeshi

    Akafanya kubimbilika na kuachia zinga la teke lililotua kifuani mwa Madebe akarudi nyuma na kujipangusa

    Akaiweka mikono yake nyuma yani kama vile kafungwa kamba au pingu

    Jambazi akawa anashambulia kwa ngumi na mateke Madebe alikwepa alipokuja kuiachia mikono yake ngumi nzito ilitua shavuni mwa yule Jambazi na kumfanya apepesuke ilikuwa ni Super punch kumbe Bwana mkubwa bado anaitumia

    Mara Madebe akainama kukikwepa kitu kilichokuwa kinakuja kwa kasi na kukita Shingoni mwa yule Jambazi

    Akadondoka chini na kuwa kimya

    Madebe aliangaza macho huku na kule kuangalia wapi kilipotokea hicho kisu lakini hakuweza kung'amua kitu chochote kile.





    ------------------

    kitendo hiko ni Mwanajeshi

    Akafanya kubimbilika na kuachia zinga la teke lililotua kifuani mwa Madebe akarudi nyuma na kujipangusa

    Akaiweka mikono yake nyuma yani kama vile kafungwa kamba au pingu

    Jambazi akawa anashambulia kwa ngumi na mateke Madebe alikwepa alipokuja kuiachia mikono yake ngumi nzito ilitua shavuni mwa yule Jambazi na kumfanya apepesuke ilikuwa ni Super punch kumbe Bwana mkubwa bado anaitumia

    Mara Madebe akainama kukikwepa kitu kilichokuwa kinakuja kwa kasi na kukita Shingoni mwa yule Jambazi

    Akadondoka chini na kuwa kimya

    Madebe aliangaza macho huku na kule kuangalia wapi kilipotokea hicho kisu lakini hakuweza kung'amua kitu chochote kile.



    Songa nayo

    Sasa



    Yule jambazi alikuwa amelala chini huku mpini wa kisu ukionekana kuning'inia shingoni mwake damu zilimchuruzika kama vile chemchem roho ilishaacha mwili. Madebe aliusogelea ule mwili kwa Tahadhari akaushika mpini wa kisu na kukichomoa ikawa kama vile kafungulia bomba la vua alichokifanya ni kutoa kitambaa na kuufunga ule mwili shingoni mwa Jambazi kidogo ilisaidia damu kutokutoka kwa wingi baada ya hapo akaitoa simu yake na kupiga sijui wapi ila alisikika akizungumza

    “ndiyo ni kwa Muarabu hapa kama unataka kwenda Kilungule, ehee ndiyo Afande"

    Wakati Madebe anazungumza na simu watu walishajazana pale na kumzunguka kwa upande wa Mwanaidi alikaza macho yake kukiangalie kile kisu kilichokuwa kimetapakaa damu akawa anajiuliza kuhusu kile kisu mbona kama nikisu chao kimefania au vipi akafanya kukisogelea na kuinama ili akiokote

    Madebe akawahi kumzuia kwa kumkalipia

    ”wee binti achaa usikishike hicho kisu"

    Mwanaidi akarudi nyuma kwa hofu waliokuwa wameenda kuzika nayo walisharejea na kukuta msibani kuna majanga

    “inamaana Sharo naye kauwawa aisee sikubari lazima niuwe mtu hapa"

    Mmoja kati ya majambazi alizungumza kwa uchungu huku akiingiza mkono kiunoni ili kuichomoa Bastola yake mwenzake akamzuia na kumtaka atulie vinginevyo wanaweza wakauwawa wote ving'ora vya magari ya Polisi viliweza kusikika punde tu wakawasili pale Wananchi wote waliombwa wakae mbali na eneo lile Uchunguzi ulianza kufanyika huku baadhi ya watu wakiulizwa maswali ya hapa na pale

    “silaha yenyewe iliyotumika kumuulia huyu mtu iko wapi?"

    Mmoja kati ya maafande aliyoonekana kuwa ni kiongozi wa msafara aliuliza akaonyeshwa kile kisu kabra ya kukishika alivaa Gropsi akakishika kile kisu na kukitia kwenye kimfuko miili yote miwili ikabebwa na kupakizwa kwenye Gari

    “Mamaa"

    ”Abee"

    “kisu kwani kiko wapi?"

    “sikipo hapo kabatini kwa juu"

    Ukimya kidogo ukatanda Mwanaidi akawa anapapasa kukitafuta kisu

    “mama mbona sikioni?"

    “basi kaangalie kwenye beseni la vyombo"

    Mwanaidi akafanya hivyo kwa bahati nzuri aliweza kukiona kikiwa kimeoshwa kiko safi kabisa kwanza

    Alivuta pumzi kwa ndani na kuzishusha alikiangalia kile kisu mara mbili mbili picha ya kile kisu ikamjia kikiwa kimetapakaa damu akajikuta akipiga kilele kisu kikamponyoka na kudondoka chini

    “Mamaa,, weee,,nakufaa,,"

    Kelele zake ziliwafanya kina Ducha na mama yake waje mbiombio ndani na kumkuta Mwanaidi akiwa kajikunyata kwa hofu

    “nini tena binti yangu?"

    “dadaa, kuna nini?"

    Yalikuwa ni maswali aliyoulizwa na mama yake pamoja na Ducha

    Wakafanya kumkumbatia

    Musa akainama kukiokota kile kisu

    “wee,, usikishike hicho kisu ni hatarii,,

    Mwanaidi alipiga kelele kama vile mwehu Musa aliruka pembeni kisu alishakishika akafanya kukiachia kama vile kapigwa shoti ya umeme

    “wee Mwanaidi una nini kwani hiki kisu kimefanyaje?"

    Mama yake alimuuliza huku akikiokota kile kisu

    ”mamaa,, usikishike hicho kisu utakufaa"

    “Ducha embu nenda kamwambie Mwinyi aje na Bajaji ili tumpeleke Dada yako hospitali huwenda maralia imempanda kichwani"

    Ducha akafanya haraka kufata Bajaji

    Lakini Mwanaidi alikataa katakata kwenda hospitali na kudai kuwa yeye haumwi ni mzima wa hafya

    ”sasa kama ni mzima wa hafya hiki kisu unakiogopea kitu gani wakati kila siku unakishikaga unakatia nyama unamenyea viazi kukata nyanya vitunguu ajabu leo hii unakiogopa kama si kushikwa na uchizi kitu gani?

    Mama yake Ducha alizungumza hivyo

    “sio hivyo mama"

    ”kama sio hivyo kumbe nini?"

    “hiki kisu ndiyo kilichotumika kumuulia yule mkaka"

    ”khaa hivi wee mtoto unaakili kweli yani kuona kisu kimefania na cha kwetu ukadhania ni hiki sio mbona hivi visu vimejaa kibao masokoni na mitaani"

    Mwanaidi akabaki kimya akifikiria kitu

    Ndani ya makao makuu ya jeshi la polisi kulikuwa na kikao cha dharula.

    Ndani ya kikao hicho kulikuwa na mipango maarumu ikipangwa kikubwa ni kuhusu mauwaji yaliyoweza kuibuka hivi karibuni kwa watumishi wa Serikali kuwawa kila siku si chini ya Askari watatu wanauwawa Tena vifo vyao vya kutatanisha

    Ndipo kesi inaangukia kwa Makomando watatu wenye kutumainiwa mmoja anaitwa Cooper Making, huyu ni mmoja kati ya Makomando wenye kutumainiwa aliyeweza kushiriki mission nyingi za hatari akiwa na kikosi kazi cha Ma FBI kabra ya yote aliwahi kuwa jasusi mwenye kuogopeka zaidi ya Corona nikisema Jasusi ni mtu ambaye alikuwa akifanya kazi kwa niaba ya nchi yake au nchi nyingine kwenye maswala ya Kinyuklia na mengineyo

    Cooper tukiachana na nyanja alizoweza kupitia mpaka kuamua kuwa Komando wa Siri Cooper makazi yake ni Tandale kwa Tumbo

    Alipopanga chumba kimoja

    Mwingine anaitwa Gulam mwenye Asili ya Kisomari huyu naweza kusema yupo kwenye kitengo nyeti Sana cha usalama wa taifa mwingine ni mwanadada aitwae Cynthia sifa za huyu Mwanadada tukiachana na uwezo wake mkubwa wa Mashowart pia anauwezo wa kupambana na viumbe visivyoonekana kwa macho ya kawaida

    Siku mbili baadae tokea kikao kile cha Siri kifanyike bwana mkubwa Cooper alianza kuifanya kazi yake kwa usiri kama ujuavyo

    Usalama wa Taifa au CIA sio watu wa kujionesha onesha mbele za watu unaweza ukamuona mtu mtaani kwenu kuwa ni mzoa takataka au Muuza maji kwenye Madumu kumbe ni Askari mpelelezi wa hatari

    Cooper aliwasili mitaa ya kwa Muarabu akiwa kama muuza koni alipiga vinyanga huku akipaza sauti kuita koni koni

    “wee muuza koni"

    Kuna mdada wa kikubwa hivi alipaza sauti kuita koni kwa maana mtoto wake alikuwa akililia koni Basi Cooper akaweka kindoo chake chini

    “mama,,wee kipochi jamani mwizii

    Kuna kijana hata alipotokea alifika pale na kukikwapua kipochi cha yule mdada aliyekuwa akijiandaa kutoa hela ya koni

    Kijana aliyekwapua kile kipochi alikimbia mbio

    Cooper alimuangalia yule kibaka Kisha akamtaka yule Mwanadada amuangalizie vitu vyake akaanza kumkimbiza

    Ulikuwa ni mkimbizano wa aina yake walikatiza kichochoro hiki na kile Cooper alionekana kuifahamu vyema Mbagala kuliko yule Mwizi maana kuna muda alikuwa anakatizia njia nyingine na kumtokezea kwa mbele

    Kibaka alikimbia wee akaja kutokezea sehemu ambayo kulikuwa kama Dojo ndani yake kulikuwa na washkaji kibao

    Kina Ducha nao walikuwepo wakifanya mazoezi ya Boxing kuingia kwa kijana yule kuliwashtua si kidogo

    “oyaa vipi mbona tunashtuana?"

    Swali hata halikujibiwa Cooper naye akaingia

    “khaa yani umeingia humu ukiwa mkuku mkuku kumbe ulikuwa unakimbizwa na huyu mrugaruga sio?"

    Mmoja kati ya vijana alimuuliza yule mwenzake

    “huyu fala ni mnoko tu asietaka sisi tule"

    Yule kibaka akazungumza hivyo huku akimsogelea Cooper kwa kujiamini si yupo na wenzake

    “sijakukimbiza kwa shari mkuu nilichokuwa nakihitaji kutoka kwako ni kile kipochi ulichompora yule Binti"

    Cooper alizungumza kwa kujihami hakutaka kujionesha mbele ya vijana wale kuwa yeye ni nani

    “Idiiii"

    Ducha alipaza sauti kumwita yule jamaa kwajina la Iddy akageuka kumuangalia Ducha

    “fanya kumpatia hiko kipochi"

    Ducha alizungumza hivyo

    “halafu wee dogo acha uchoko"

    Iddy alitamka hivyo

    Ducha alimfata Iddy kwa kasi na kumnyang'anya kile kipochi akampatia Cooper naye pasipo kuzubaa akaondoka zake

    “wee Iddy achana na Ducha atakuumiza ohoo"

    Wenzake walipaza sauti kumtaka Iddy asijaribu kupigana na Ducha lakini Iddy alishapaniki kwanini kipochi chake arudishiwe yule mtu haiwezekani akachukuwa kipande cha bomba na kutaka kumchapa nalo Ducha aliyeanza kujihami kwa kulikwepa

    Iddy akawa anapiga hovyo hovyo pasipo kumpata mrengwa Ducha akadunda ukutani alijipinda kama vile chewa akaachia zinga la teke lililomfanya Iddy ajibamize Ukutani

    Ngumi dabo dabo zilimuangukia kama sio wenzake kuja kumshika Ducha angetolewa meno yote ya mbele

    “sepa zako tokaa kuanzia leo hatukutaki ndani ya Camp letu jikatae huko"

    Iddy akiwa anavuja Damu alijikuta akifukuzwa kisa tu kujaribu kupigana na Ducha

    Kumbe Cooper hakuwa ameondoka alibana sehemu kuwaangalia alishangazwa Sana na ujasiri wa mtoto yule kupigana na mtu mkubwa aliyemzidi umri hadi kimo.

    Akiwa kabana pale ghafla kuna sauti ya kama upepo sijui mvumo aliweza kuisikia akafanya kugeuka ikawa kufumba na kufumbua kisu kuonekana kikija kwa kasi

    Cooper asikimbie mchezo kila akikimbia kisu nacho kipo nyuma yake akadunda kwenye mstimu alipokuja kukaa sawa akajitupa kwenye mapira ya Gari akatulia hapo kimyaa huku akipumua kwa kasi

    Akaitoa simu yake na kumpigia sijui Gulam au Cynthia

    “ni Ghost"

    Cooper alizungumza hivyo na kukata simu hakuweza kufahamu kile kisu kilitokea wapi na kimepotelea wapi?

    “ehee ulimpatia wapi?"

    “kulee karibu na Matitu"

    “khee umefika naye hadi kule?"

    “ndiyo Dada yangu"

    ”ohoo pole sana"

    Yule Binti alifurahi Sana kurudishiwa kipochi chake kuonyesha Shukrani akampatia Cooper elfu ishilini lakini Cooper aliikataa

    “shika bwana"

    “hapana Dada yangu mi nilikufanyia kwa wema tu wala huna haja ya kunilipa

    “pokea bwana au ni ndogo nikuongeze nini?"

    Alizungumza hivyo yule Binti huku akiongeza elfu Ishilini nyingine ajabu Cooper akazipokea na kuzitia mfukoni mwa yule mtoto Kisha yeye huyo akaondoka zake Binti akabaki kutabasamu tu!

    Hapa tunamuona Komando mwingine aitwae Gulam akiwa amekaa kwenye sofa mkoni alikuwa kashika simu yake kubwa sijui alikuwa akiperuzi kwenye Mitandao ya kijamii au alikuwa akiwasiliana na mtu kwa kuchati

    “Ghost"

    Gulam alitamka kauli hiyo akaiweka simu mezani na kufikiria kitu akasimama na kuingia Chumbani muda akatoka akiwa kashika kidude cha kuwekea Moto pindi unapotaka kuchoma Ubani akafungua mlango wa Sebreni na kutokezea ukumbini hapo ukumbini Sasa kulikuwa na Wadada kibao wa kikubwa wakiwa bize na mambo yao bila shaka ni wapangaji wenzake

    “Salome"

    Gulam aliita hivyo

    “abee mume wangu"

    ”mmh nimekuwa mumeo tena?"

    ”kwani vibaya mi kukuita mume jamani Gulam mi nataka unioe hivi utaishi peke yako mpaka lini?"

    Salome alizungumza hivyo

    ”mda wa mimi kuoa bado embu naomba uniwekee Moto kwenye kichanja"

    Gulam alizungumza hivyo

    Salome akakipokea na kumuwekea Moto Gulam akarudi ndani kwake na kukiweka kile kichanja mezani akafungua kabati na kutoa kikopo chenye Udi ndani yake

    Akachota udi na kuutia kwenye moto huku akiita

    “Husnat,,,yaa Husnat,,Husnat,,"

    Aliita hivyo Kama mara tatu ghafla taa na tv vilivyokuwa vinawaka hadi simu vyote vilizima kukawa Giza totoro ni Moto pekee ndiyo ulionekana kuwakawaka

    Muda kidogo kuna mwanga mkari ulioneka kutokea ukutani alionekana Binti mrembo wa haja akijongea pale kwa mtindo kama vile anapaa

    “Gulammmmmm kwanini unapenda kurudia makosaa?"

    Husnat aliuliza hivyo sauti yake ilikuwa ina mwangwi wa hatari







    ------------------

    Salome akakipokea na kumuwekea Moto Gulam akarudi ndani kwake na kukiweka kile kichanja mezani akafungua kabati na kutoa kikopo chenye Udi ndani yake

    Akachota udi na kuutia kwenye moto huku akiita

    “Husnat,,,yaa Husnat,,Husnat,,"

    Aliita hivyo Kama mara tatu ghafla taa na tv vilivyokuwa vinawaka hadi simu vyote vilizima kukawa Giza totoro ni Moto pekee ndiyo ulionekana kuwakawaka

    Muda kidogo kuna mwanga mkari ulioneka kutokea ukutani alionekana Binti mrembo wa haja akijongea pale kwa mtindo kama vile anapaa

    “Gulammmmmm kwanini unapenda kurudia makosaa?"

    Husnat aliuliza hivyo sauti yake ilikuwa ina mwangwi wa hatari



    Songa nayo

    Sasa



    Husnat alionekana kuchukizwa kupita kiasi hata ongea yake haikuwa ya taratibu

    “kila mda umekuwa ni mtu wa kurudia makosa yale yale, hivi wee Mwanaume unanitafuta kwa kitu gani?"

    ”nisamehe"

    “mara ngapi nimekusamehe ajabu hutaki kuskia"

    “nipe nafasi ya mwisho sitoweza kufanya Tena makosa"

    ”okhoo,,akhaakhaa kila siku unasema hivyo hivyo haya nambie umeniitia kitu gani?"

    Husnat alizungumza kwa ghadhabu akajipweteka kwenye sofa na kumkazia macho Gulam aliyeonekana kuwa mpole kama vile kamwagiwa maji ya baridi

    “Gulam yani kwa faida yako wewe unataka kuniingiza mimi kwenye matatizo makubwa aisee juu ya hili swala siko tayari kukusaidia"

    Husnat alibwatuka na kusimama yani kule kumuangalia Gulam machoni alishaweza kubaini kila kitu akajiandaa kuondoka

    ”Husnat kipenzi kwanini umenibadirikia

    Leo hii umefikia hatua ya kunikalipia kama vile mi mwanao? Umesahau kabisa kiapo tulichokula baina yangu mi na wewe?

    Mambo mangapi tumefanya tukiwa pamoja

    Husnat embu ikumbuke Kashmir nakule Baghdad"

    Gulam alizungumza kwa upole huku akipiga hatua kumsogelea Husnat alipomkaribia akanyoosha mikono yake na kukishika kiuno kiteke cha binti huyo wa Kijini

    Mwenye ngozi nyororo yenye kumeremeta Utasema nyota ya jahaa.

    Kule kushikwa kiuno kulimsisimua sana Husnat

    “sio hivyo Gulam wee mwenyewe unafahamu ni jinsi gani nakupenda ila sihitaji uniumize nilishakwambia ukinihitaji hakikisha unazima kila kitu chenye mwanga kwa maana vinaniumiza"

    Safari hii Husnat alizungumza kwa upole

    “basi nisamehe kipenzi sitofanya hivyo tena"

    “mmh unasemaga tu!"

    ”kweli tena safari hii sitokuumiza"

    “na ukiniumiza je nikufanyaje?"

    “ninyonye damu yote"

    ”na ntakunyonya kweli wee nitanie tu! Tena ntakunyonya Kama hivi"

    Husnat alizungumza kiutani akaupeleka mdomo wake uliodakwa na mdomo wa Gulam

    Kukuru kakara kwenye Sofa waliangukia ambapo Husnat binti jini tayari mvua ilishanyesha kwenye kitumbua chake wadudu walimnyevua hasa, lakini Gulam alijifanya kama haelewi alianza kumsaura nguo moja badara ya nyingine kisha alimweka kwenye Sofa kama vile anataka kumvalisha mtoto pampasi

    Yeye akiwa amepiga magoti sakafuni, alimpanua miguu Husnat aliyekuwa amepagawa kwa nyege, kwa makusudi aliupeleka ulimi wake uliokuwa na mate kidogo mpaka kwenye kitumbua kitamu na kuanza kukichezea kiarage na ulimi wake

    “aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiii ooooouhhhhh Guuuulaaam,,maaaaaaaaaaaaa,,"

    Husnat wa watu alilalamika na kumwaga bao lake lililoruka juu kama nyuklia hakika Nyege zilimpanda hasa,alikuwa hajielewi kabisa

    Basi Gulam aliufungulia vyema mtutu wake wa nguvu anaouaminia kwenye shughuli za mashambulizi kama hayo ulikuwa umedinda hasa mpaka mishipa ilijitokeza,hakuwa haba maumbile yake,alijaaliwa mtutu Mboo kubwa na nene kwa hafya ya Mwanamke

    "Gulaaam,,,ingiiiizaaaaaaaaaa,,,,,aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,"

    Husnat alikuwa moto alichokifanya Gulam hakuchelewa, alimweka sawa na kulishika dudu lake,kile kichwa alikilengesha vyema kweny kitumbua na kuanza kukandamiza taratibu ili dudu lizame

    “aaaaaaaaaaaaaaaah,,,sssssssssssssssssssss,,,aaaaaaaaaaaaaaaaah,,,,oooooshiiiiiiiiiiiiiiiiiii,,"

    Alilalamika Husnat huku dudu likizama taratibu kwenye kitumbua chake,tena liliteleza vyema hasa,hapo ndipo alizidi kuchanganyikiwa Dudu lilibana vyema kwenye kitumbua chake

    Taratibu nje ndani, mchezo juu ya Sofa ulimi ulikuwa kifuani mwa Husnat ukimnyonya Chuchu zake, ya kulia na ya kushoto kwa zamu.Hapo ndio alimchanganya hasa,utamu ulizidi mpaka akawa anamkumbatia kwa nguvu kiasi ambacho Gulam alikuwa akipampu kwa shida

    “aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaashiiiiiiiiiiiiii,,,,amamamaaaaaaaaaaaa,,,,ooooussssssssssssssssssssssss,,,aaaaaaaaaaaaaaaah"

    Aliendelea kukolezwa na utamu ambapo Gulam aliongeza kasi kidogo.

    Husnat alikuwa akipaza sauti pale ambapo alikaribia kumwaga,mpaka muda huo tayari alishamwaga bao mbili mfurulizo, ni kama Gulam alikuwa anamwotea, Binti huyo aliunyanyua mguu wake na kuushikilia kwa juu ambapo aliendelea kumsugua kwa kasi mpaka akakojoa tena

    “nakupendaaaaaaaaaaaaa,,,Gulaaaaaaam,,,,,

    ,mamaaaaaaaaaaaaaayangu,,,,,mzaziiiiiiiiiiiiiiiii uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiaaaaaaaaaaaaaaaaaah"

    Husnat alilalamika hivyo wakati akimwaga bao lake la tatu ulalamikaji wake Kama vile Mwanamke wa kibinadamu na hii ni kawaida Majini hupenda kufanya kila kitu Kama Wanadamu

    Gulam sasa ndio akaanza kujikongoja akilitafuta lake,kwani alikuwa akimsugua huku mawazo yako sehemu nyingine, alicholinda ni uimara wa dudu lake tu,hakutaka kumwaga haraka,ila alipoona mtoto mwenyewe ameshakojoa mara nyingi,naye aliona ni muda muafaka,ndani ya dakika kumi na tano

    “aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaah,,,oooooooo

    ooooghrrrrrrrrrrrrrr,,,,aaaaaaaaaaaaaaaaah"

    Alilalamika hivyo na kumwaga bao lake,hakuchomoa dudu lake, walibaki wakiangaliana huku kila mmoja kijasho kikimtoka

    nakupenda Mume wangu kuanzia Sasa nipo tayari kukusaidia"

    ”asante Sana mke wangu twende kwanza tukajisafishe halafu tuje tupange yetu"

    ”haya Mume nibebe"

    Husnat alideka kwa wakati huo sehemu yote iling'aa kutokana na Mng'aro wake basi Gulam akafanya kumnyakua na kuelekea naye Chumbani moja kwa moja wakaingia bafuni

    Wakati wanaogeshana ghafla bin vuu taa ziliwaka na kumfanya Husnat aanze kutatarika

    Gulam akafanya kumshika na kumkumbatia hakuweza kufahamu ni Nani aliyewasha hizo taa kwa maana mlango wa Chumbani kwake alikuwa kaufunga

    “Gulam pale mwanzo nilipokutamkia kuwa sitoweza kukusaidia nilimaanisha kitu! Wala huna haja ya kujiuliza kuhusu hizi taa kuwa kawasha nani"

    Husnat alizungumza hivyo haliyakuwa akijitoa maungoni mwa Gulam

    “unamaanisha kitu gani kuzungumza hivyo?"

    ”shika hili tauro ujifunge kiunoni Kisha utoke mpaka room kuna mgeni wako"

    Husnat hakujibu lile swali zaidi ya kumpatia Tauro Gulam akalipokea kabra ajatoka Husnat alimdaka mkono

    “tafadhari Gulam nenda kwa upole kuwa mnyenyekevu juu ya huyo mtu, usijifanye ni mjuaji haya nenda"

    Husnat alizungumza kwa upole

    Mpaka Gulam akawa anajiuliza mara mbili mbili huyo Mgeni wake aliyekuja ni nani?

    Akaanza kupiga hatua za taratibu kuelekea Sitting room

    Alipotokezea pale kwanza alishangazwa Sana kumuona bwana mkubwa Chinoge akiwa amekaa kwa kukunja nne huku akiwa amekodoa macho yake kuangalia tv kubwa iliyotundikwa ukutani

    Mezani kulikuwa na Box la juisi na Glass ambayo ndani yake kulikuwa na kinywaji hicho

    Akaangalia mlango wa kutokea nnje akaweza kubaini kuwa upo wazi inamaana huyu pimbi katumia funguo malaya kuingilia chumbani kwangu Gulam akasahau kabisa kile ambacho alitahadharishwa na Husnat akaenda kusimama mbele ya Tv na kujishika kiuno

    “wewe ni nani? Umeingiaje ingiaje ndani ya chumba changu?"

    Gulam akahoji

    “hayo maswali ungeenda kumuuliza malaya wako lakini sio mtu kama Mimi"

    ”fuck you"

    Gulam akaachia tusi huku akifutuka na kuachia teke moja zito Chinoge akawahi kuinama teke likatua kwenye Glass ikadondoka chini na kuvunjika

    Gulam akadunda kwenye sofa na kuachia mateke ya Dabo dabo Chinoge akawa anapanchi na kukwepa

    Gulam akajikuta akirudishwa nyuma kwa kurushwa akaenda kujibamiza kwenye Tv

    Hata ajakaa sawa alishtukia akipigwa ngumi za maana

    Hapo ndipo alipokumbuka kauli ya Husnat kuwa awe mpole juu ya Ukomando wake mbele ya huyu kiumbe yeye nikama mtoto

    “Chinoo acha,, tafadhari nakuomba msamehe"

    Husnat alitoka chumbani mbio mbio na kumkuta Chinoge akijiandaa kumnyongelea mbali maana alishakishika kichwa cha Gulam kilichobaki ni kukizungusha tu!

    Gulam alikuwa katepeta si kidogo

    “Husnat"

    “abee baba"

    “je huyu mtu unampenda?"

    “ndiyo baba"

    “kama kweli unampenda Basi utakutana naye kuzimu"

    Chinoge alizungumza hivyo Kisha akakizungusha kichwa

    “hapanaa,, usimuuwe"

    Husnat alipiga kelele kumtaka baba yake Mdogo asimuulie mpenzi wake

    (KWA WALE WANAOFATIRIA SIMULIZI ZANGU KUANZIA MTAA WA TATU MPAKA HII YA NYETO NYETONI BILA SHAKA MTAKUWA NA KUMBUKUMBU NINJA ICE ALIKUWA NA WATOTO MMOJA ALIZAA NA VIVIAN MWINGINE NA MARIAM MABINTI AMBAO WALICHEZA KAMA MA FBI KWENYE MTAA WA TATU KWENYE SIMULIZI YA LATIFA NA MWAJUMA NINJA ICE ALIPATA MTOTO MWINGINE AMBAYE NDIYO HUYU HUSNAT KUNA IKRAM YUSRATH NA BINTI AITWAE SHADIA WATOTO HAWA WAKO KWENYE TAWALA TOFAUTI ZA KUZIMU WANAMUHESHIMU CHINOGE KAMA BABA YAO MDOGO KWA MAANA ANA UWEZO MKUBWA KAMA BABA YAO MZAZI ALIYEPOTEZA MAISHA MIAKA KADHAA NYUMA)

    Basi Husnat alilia Sana kumlilia mpenzi wake

    “baba, huyu hawezi kuletwa kuzimu anapelekwa kwenye ulimwengu wa Roho"

    “muache aende

    Husnat wewe ni mshenzi unaewasaidia washenzi kama hawa

    Una bahati sana ni damu ya kaka yangu"

    “nisamehe baba yangu ni Shetani tu!

    Alinipitia"

    “hahahahaha"

    Chinoge alicheka kwanza yani Husnat yee mwenyewe kawa jamii ya Mashetani Sasa iweje Shetani ampitie

    ”inamaana na wewe ulipitiwa na shetani"

    “ahaa,, ahaa hapana Binadamu tu alinipitia"

    “sawa nimekusamehe waweza ukaenda nyumbani"

    Chinoge alitamka hivyo alianza yeye kutoweka halafu akafatia Husnat

    Walipotoweka tu kile kisu kiliibuka na kuzama Shingoni mwa Marehemu damu zilititirika kwa wingi na kusambaa Sakafuni

    *******

    Hapa tunamuona Ducha akiwa amekaa na Madebe wakizungumza hili na lile

    ”ujuwe sipendi kukuona ukiwa umevaa haya mavazi yako"

    Ducha alizungumza kumwambia Madebe kuwa anachukia kumuona akiwa kavaa Gwanda za kijeshi

    ”kwanini?"

    “usiulize kwanini ila kuanzia leo ukihitaji kuonana nami usije ukiwa umevaa hizi nguo"

    ”sawa nitafanya hivyo iwapo utaweza kunisaidia kuonana na Chinoge"

    ”khaa inamaana unataka kumkamata Mwalimu wangu kisa aliwapiga wenzako?"

    ”hapana sina niya hiyo"

    ”kumbe unamtakia kitu gani?"

    ”namuhitaji tu! Wee nielekeze nitampatia wapi?"

    ”subiri basi nikuitie

    Mwaliiiimu"

    Ikawa kufumba na kufumbua Chinoge kuibuka safari hii hakuja kwa staili ya upepo wala kimbunga Chinoge alimuangalia Madebe haliyakuwa akitabasamu

    Madebe akanyoosha mkono kumpatia kiganja Chinoge naye akafanya hivyo basi wakasalimiana kwa kushikana Ducha akaondoka zake Basi mtu na shemeji yake walizungumza mambo mengi tukumbuke Madebe amemuoa Dada yake Chinoge aitwae Mariamu Sijui Khadija yule,

    Wakati wanaendelea kuzungumza kile kisu kilionekana kuja kwa kasi usawa ule ambao Madebe alikuwa kasimama naye hakuwa na hili wala lile mpaka pale aliposhtukia akisukumizwa pembeni na shemeji yake kisu kikakita kifuani mwa Chinoge mpaka akacheuwa Damu nyeusi.

    Chinoge alipepesuka na kudondoka Chini

    Madebe alipiga kelele kuita msaada ambapo kina Mwanaidi na Majirani walikuja mbiombio

    Pembezoni mwa mitaa hiyo tunamuona Ducha akiwa kakaa chini akilia

    “nisamehe Mwalimu,,hiiii,,hiii,,"

    Wakati Ducha analia Chinoge alishabebwa na kupakizwa kwenye Gari safari ya kumkimbiza hospitali ilishaanza alifikishwa hospital ya Zakhiem kwanza Wauguzi waligoma kumpokea wakidai ripoti kutoka kituo cha Polisi walipomuona Madebe akishuka ndani ya gari wakafanya haraka kumpokea na kumkimbiza Wodini

    Kukawa na pilikapilika za hapa na pale

    “wee Janet"

    “abee"

    ”yule mgonjwa tuliyempokea sasa hivi yuko wapi?"

    “mgonjwa gani tena?"

    ”si yule mkaka aliyekuwa kachomwa kisu kifuani"

    ”mmh unamsemea yule aliyeletwa na Mjeshi?"

    ”ndiyo huyo Sasa usiongee kwa sauti"

    “si yupo wodi namba mbili kule"

    ”hayupo"

    ”hayupo kivipi wakati Mimi nimetoka Sasa hivi embu twende"

    Basi wakaelekea huko hawakuweza kumuona walimtafuta kila sehemu mgonjwa hayupo

    “au atakuwa kapoteza maisha"

    Wakati wanaulizana wakashtukia Madebe kawasimamia pembeni yao walianza kubabaika

    ”vipi hali ya mgonjwa wangu?"

    ”mmh mmm,, kidogo ajambo"

    ”wee naye badara umwambie hayupo unamwambia ajambo"

    ”khaa hayupo kivipi?"

    ”kwakweli hatujui kaelekea wapi? Maana alikuwa kalala kitandani mi nikawa navuta dawa kwenye bomba la sindano ili nimchome ile nageuka hivi sioni mtu kitanda cheupe"

    Yule Muuguzi akazungumza hivyo

    Madebe alitikisa kichwa Kisha akatabasamu akatoa kiasi cha pesa na kumpatia Janet halafu huyo akaondoka zake hakika aliwaacha njiapanda

    ***********

    “Husnat mjukuu wangu kwanini unalia?"

    Ibnuwas alimuuliza mjukuu wake kwa wakati huo alisharejea kuzimu haliyakuwa akilia

    ”nijibu Sasa kitu gani kimekufanya mpaka udondoshe chozi la Damu

    Husnat wala hakuwa na jibu zaidi ya kuendelea kulia punde upepo mkali ulianza kuvuma

    Bwana mkubwa Chinoge aliibuka haliyakuwa kajishika kifuani hata

    Akadondoka chini puuh nakuwa kimya

    “babaaaa"

    “mjukuu wangu jamanii

    Husnat na Bibi yake walipiga kelele huku wakimkimbilia Chinoge





    ------------------

    “Husnat mjukuu wangu kwanini unalia?"

    Ibnuwas alimuuliza mjukuu wake kwa wakati huo alisharejea kuzimu haliyakuwa akilia

    ”nijibu Sasa kitu gani kimekufanya mpaka udondoshe chozi la Damu

    Husnat wala hakuwa na jibu zaidi ya kuendelea kulia punde upepo mkali ulianza kuvuma

    Bwana mkubwa Chinoge aliibuka haliyakuwa kajishika kifuani hata

    Akadondoka chini puuh nakuwa kimya

    “babaaaa"

    “mjukuu wangu jamanii

    Husnat na Bibi yake walipiga kelele huku wakimkimbilia Chinoge



    Songa nayo

    Sasa



    Hali haikuwa nzuri kwa bwana mkubwa Chinoge alikuwa amelala chini huku akionekana kupumua kwa tabu, akabebwa na kwenda kulazwa juu ya kitanda

    Ibnuwas aliomba kila mmoja asogee pembeni ili aweze kumfanyia matibabu

    “Mamaa"

    “abee Mwanangu"

    ”hii ni sumu kutoka tawala ya Duchani"

    ”khaa inamaana wanataka kumuangamiza na huyu kisa kuwa karibu na kile kitoto?"

    “sio hivyo mama"

    ”sio hivyo kumbe nini sasa?"

    “Ducha ndiyo aliyemchoma hiki kisu chenye sumu"

    Ibnuwas alizungumza hivyo huku akinyoosha kidole sehemu

    Mara alionekana Chinoge akizungumza na Madebe

    “huyu kijana si ndiyo kaka yake yule Binti aitwae Milfat?"

    Bibi yake Ninja Ice aliuliza

    ”ndiyo yeye"

    Ibnuwas akajibu ndipo wakaweza kuliona lile tukio la kisu kilichorushwa nakuja kumchoma Chinoge

    ”mbona kama aliyekusudiwa kuchomwa ni mwingine?"

    ”ndiyo aliyekusudiwa ni yule pale Mwanajeshi, sema alichokifanya mjukuu wako ni kumuokoa"

    “na kwanini Ducha alitaka kumuua huyu Kijana?"

    “kwa sasa Ducha ana kisasi juu ya marafiki zake embu oneni pale"

    Ibnuwas alizungumza hivyo kisha akaileta Video yenye kuonyesha Historia ya Ducha na marafiki zake

    Mpaka siku ambayo Sudi na Snop waliuwawa

    ”Mungu wangu wee inamaana Maadui zake ni watu wa aina tatu? Majambazi, Polisi, na Wanajeshi? Ni haki yake kufanya hivyo lakini naona Kama anakosea ilitakiwa awauwe wale wote waliokuwepo siku ya tukio sio

    Kila mtu!"

    “subiri kwanza nimpatie Matibabu Kijana wetu halafu hayo mengine tutazungumza baadae"

    Basi matibabu ya kuitoa sumu mwilini mwa Chinoge ilianza dakika si nyingi alizinduka na kukaa kitako

    “pole Sana mjukuu wangu"

    Bibi mtu alitoa pole kwa mjukuu wake Chinoge alikaza macho yake kumuangalia Husnat mpaka akawa anaogopa

    ”vipi tena mbona unamuangalia Sana binti yako?"

    Bibi mtu akauliza Chinoge wala hakujibu lile swali akasimama

    “kwa mara nyingine Tena naomba niondolewe hiki Kipawa!"

    Ilikuwa ni kauli yake ya kwanza kuitamka kauli ambayo iliwashangaza Majini wote ndiyo miaka kadhaa nyuma Chinoge alijivua Uwezo wote wa kijini

    Akaurudisha ili aweze kumsaidia Ducha ajabu leo hii anaomba kuondolewa

    ”kwanini unataka iwe hivyo?"

    ”sihitaji maswali"

    “Hafidhi mjukuu wangu,,

    “nyamazaa mi sio mjukuu wako

    Ibnuwas utanitoa hiki Kipawa cha kijini au hunitoi?"

    “bora uniuwe lakini sipo tayari kufanya hivyo"

    Ibnuwas akajibu hawakuwa tayari kuipoteza ngao yao binafsi Chinoge ndiyo silaha yao iliyobaki baada ile ya awali kutoweka ulimwenguni iweje leo hii na yeye aombe kuondolewa

    Chinoge akawa anatembea tembea huku nakule Majini wote walikuwa kimya

    Muda kidogo kuna mwanga mkali ulionekana juu angani wote wakainua nyuso zao kuangalia hakuna aliyeweza kuamini macho yake baada kuonekana Ninja Ice akiambaa ambaa

    Kule juu

    Wakafanya kumpungia mikono naye akafanya hivyo kisha akatoweka alipotoweka tu na Chinoge naye akatoweka haliyakuwa akiacha tabasamu zito limetanda kwa majini wote

    Kumbe ujio wa taswira ile ulikuja kuzituliza hasira za Chinoge maana alishaanza kupaniki

    “jamanii, njoeni muone kuna damu hukuu"

    Ni kelele zilizoweza kusikika kutoka kwa mmoja kati ya wapangaji waliopanga nyumba moja na Gulam kelele zake ziliwafanya wapangaji wote wakurupuke kutoka usingizini wakatoka mbiombio mpaka ukumbini

    ”khaa nini hiki?"

    Yule Binti ambaye usiku wajana alimpatia Gulam moto aliuliza kwa hamaki huku akijaribu kuusukuma mlango

    Damu zilionekana kutiririka kutokea chumbani nyingine zilishagandiana

    ”Gulam, wee Gulam fungua mlango jamani"

    ”ohoo subirini kwanza nipige simu

    Polisi"

    Mmoja kati ya wapangaji akawataka wenzie watulie wasijichukulie maamuzi ya kutaka kuuvunja mlango simu ikapigwa polisi dakika si nyingi maafande takribani wanne waliweza kuwasili nao wakajaribu kugonga mlango lakini wapi uamuzi uliofikiwa ni kuvunja mlango risasi moja tu ilipigwa kwenye kitasa mlango wenyewe ukafunguka maafande wakavamia ndani

    Walipoingia tu kila mmoja akabaki kutumbua mimacho Kama vile mjusi aliyebanwa na mlango kiwiliwili cha Gulam kilikuwa kimelala chini haliyakuwa kichwa chake kikiwa kimewekwa Mezani hakika yalikuwa ni mauwaji ya kutisha simu ikapigwa kwa bibie Cynthia na mwenzake Cooper ni bibie Cynthia pekee ndiye aliyeweza kuwasili eneo la tukio

    Kiwiliwili kikabebwa na kichwa chake gumzo likabaki mtaani huku vyombo vya habari vikitangaza juu ya mauwaji hayo.

    Kutangazwa kwake ikawa kama vile kuwafumbua macho na masikio wale wote waliokuwa wakimfahamu Marehemu kuwa ni Muuza genge pale mtaani kwao Mabinti wengi walimpenda kutokana na ucheshi wake hasa waendapo kununua bidhaa gengeni kwake hupenda kuwaongeza Nyanya vitunguu bamia nakadharika muda mwingine hata huwakopesha pasipo kuwadai chochote

    Kumbe nyuma ya panzia Marehemu alikuwa kitengo cha usalama wa taifa kule kuuza genge sijui kutembeza mitumba mtaani ni kuzuga tu

    “mmh ndiyo maana enzi za uhai wake hakuhitaji kujihusisha kimapenzi na Mwanamke yoyote yule akihofia kujurikana kuwa yeye ni nani?"

    “ndiyo hivyo mwenzangu kuna watu wenye kujielewa kama Marehemu halafu kuna wale wa misifa kitu kidogo tu anakutishia maisha kisa yupo Serikalini"

    ”kiukweli kabisa kutokea moyoni mwangu nilitokea kumpenda Gulam kupita kiasi, ajabu mwenzangu hakuonyesha hisia zozote zile za kunihitaji, zaidi ya kuniheshimu Kama Dada yake"

    “unajua nini Salome kuna baadhi ya wanaume wanahasiwa ili wasije wakaharibu kazi si unajua sie Wanawake hatuna koromeo la kutunza Siri"

    ”mmh huko kwenye kuhasiwa si kwa Gulam"

    ”kwanini isiwe kwake?"

    ”nakwambia hivyo kwasababu kuna siku niliingia chumbani kwake pasipo kubisha hodi nikamkuta akipiga Punyeto"

    “wee usinambie inamaana Gulam alikuwa anapiga Nyeto?"

    “ndiyo hivyo shost tena hiyo siku niliweza kufanikiwa walau kuinyonya Mboo yake"

    “khaa inamaana ulilala naye?"

    ”wee naye embu jaribu kutofautisha kuinyonya na kulala naye"

    “sa sindiyo ulifanya naye mapenzi?"

    “sio hivyo bana"

    “kama sio hivyo kumbe nini?"

    “sikia nikwambie kitu Win hiyo siku niliingia chumbani kwake ahaa sio chumbani ni Sitting room nilipoingia tu ndiyo nikamkuta kalishikilia dudu lake kubwa akilichezea

    Kwanza alishtuka akafanya haraka kujifunika na shuka nilimuangalia kwa jicho la matamanio Basi nilimsogelea nikapiga magoti nikanyoosha mkono wangu nikaitoa ile shuka na kuitupia pembeni nikalishika Dudu lake taratiibu nilianza kulinyonya kwa madaha huku nikikichezea kitumbua changu,,,

    Muda wote huo Gulam alikuwa ananiangalia tu!

    Basi mtoto wakike nilifanya manjonjo mpaka akanikojolea mdomoni licha ya kunikojolea lakini kitu bado kilikuwa kigumu nikavua chupi na kutaka kuikalia ajabu alinizuia na kunitaka nitoke nnje"

    Basi mtu na Shogaake waliendelea kuzungumza pale

    Tukija upande wa Ducha Duchani muda wote yeye alikuwa ni mtu wa kukaa na kulia tu!

    Hata kula hakuhitaji

    “sijui kitu gani kimeweza kumkumba kijana wangu? Mbona kipindi cha nyuma hakuwa hivi jamani?"

    Mama yake Ducha alizungumza kwa kuuliza

    Ducha alianza kuwa mzembe hata shuleni alikuwa anakoromewa na kupigwa makonzi na mitama kutoka kwa watoto wasiomfahamu Ally na Musa wakawa na kazi ya ziada kumtetea rafiki yao hawakuweza kufahamu kitu gani kilichomsibu mpaka amekuwa hivyo. Darasani kwenyewe alikuwa analala tu! Hata muda wa kuandika hakuwa nao akirudi nyumbani anajifungia chumbani kutwa kucha hafya yake ilianza kudhoofu

    Kuna siku Mwanaidi alimpigia simu Madebe na kumuomba afike nyumbani kwao,

    Siku hiyo Madebe hakuwa na nafasi akaahidi kufika kesho yake.

    Nikweli kesho yake majira ya Asubuhi aliweza kuwasili pale

    “bora ulivyokuja kaka yangu kwa maana hapa tulipo tunamatatizo makubwa juu ya mdogo wangu Ducha"

    Mwanaidi alizungumza hivyo kumwambia Madebe

    “matatizo gani Tena Sister?"

    Ikabidi Mwanaidi amsimulie

    “aisee inamaana hata kula chakula hataki?"

    ”ndiyo yani hataki kabsaa"

    “kwasasa yuko wapi?"

    “usiku wa jana alipelekwa hospitali na kutundikiwa dripu tatu za maji"

    “daah"

    “ndiyo hivyo kaka yangu hapa kwenyewe nimeagizwa nimuandalie mtori haijurikani kama atakubari kula au vipi!

    ”fanya kumuandalia naimani juu ya ujio wangu leo atakula"

    “nilishaandaa mbona hapa nilikuwa nakungojea wewe tu ili tuelekee hospital"

    “sawa twende"

    Basi wakatoka safari ya kuelekea Hospitali ikaanza wakiwa njiani walizungumza mambo mengi.

    Walipofika hospitali

    Walimkuta mama yake Ducha akiwa kakaa kitandani akimnywesha Ducha juisi

    “ohoo karibu Sana baba yangu"

    Mama yake Ducha alimkaribisha Madebe kwa furaha na kumtaka akae pale ili amnyweshe juisi Ducha

    “asante sana mama yangu vipi mgonjwa wetu anaendeleaje?"

    “hali ya mgonjwa nikama unavyo muona leo kidogo ajambo"

    ”lete chakula hiko"

    Kupitia Madebe mgonjwa siku hiyo alikubari kula Madebe akaomba kumchukuwa Ducha ili akakae naye kwake ni ombi ambalo lilikubaliwa

    Siku mbili baadae Ducha aliwaaga marafiki zake kwa kukumbatiana Musa alikuwa analia

    “msijari masela wangu ipo siku nitarudi hata hivyo kimwili hamtakuwa nami ila kinafsi tupo pamoja acha niende huko kutuliza Akili yangu juu ya kumuwaza Mwalimu wangu"

    Ducha alizungumza hivyo akapanda ndani ya gari hao wakaondoka

    Sauti ya honi ikilia kwa fujo ndiyo iliyomshtua Ducha kutoka usingizini akajipangusa macho yake na kuangalia mbele ya kioo cha Gari kulikuwa na Bajaji iliyopaki kwa mtindo wa kuzuia barabara

    Mara mwenye ile Bajaji alionekana kuja mbiombio na kupanda akaiwasha na kuiweka pembeni kisha akashuka na kupiga magoti

    “nisamehe Sana bwana mkubwa kuna mtu alinichukulia Simu yangu so nikajikuta naiacha bajaji na kumkimbiza kwa miguu"

    Jamaa alianza kujitetea

    Madebe alimuangalia yule jamaa kisha akakunja kona kuelekea mitaa ya Mbezi Beach

    Kwa mbele kidogo lilionekana jumba kubwa la kifahari lililozungushiwa ukuta kwa nnje zilionekana njema mbili zilizovalia kombati za kijeshi wakiranda randa huku na kule Madebe akapiga honi Geti likafunguliwa huku zile njemba zikikakamaa kwa kupiga saruti Madebe akaingiza Gari ndani kuna mlinzi mwingine akaja kumfungulia mlango wa Gari Madebe alipotaka kwenda kumfungulia Ducha aling'aka kwa hasira

    “hapana usinifungulie"

    Ikabidi yule mlinzi akae pembeni Ducha akafungua mlango Mwenyewe akateremka kutoka ndani ya Gari

    Wakaongozana kuingia ndani

    “baba,,babaaa"

    Zilikuwa ni kelele za shangwe kutoka kwa watoto wa Madebe wapatao wawili wakija mbiombio kumlaki baba yao akafanya kutanua mikono maana walipomfikia wakamrukia naye akawabeba alicheza cheza nao pale

    “baba huyu nani?"

    ”anaitwa Ducha"

    “ohoo Duta"

    ”sio Duta ni Ducha"

    ”ahaa kumbe Bucha"

    ”embu tokeni zenu huko"

    Ikabidi Madebe awafukuze wanaye maana wanaleta utani na jina la mwenzao

    “ohoo my husband umerudi"

    Sauti nyororo ya bibie Mariam ilisikika kutokea juu gorofani alionekana akiteremka ngazi na kuja kumkumbatia mumewe kipenzi wakapigana mabusu

    Ducha aliwaangalia tu

    Mpaka ulipofika muda wa yeye kutambulishwa

    “mke wangu huyu ndiyo yule mtoto niliyewahi kukusimulia kuwa ana talent kubwa Sana katika swala zima la mapambano"

    “ohoo bila shaka ni Ducha Duchani?"

    “ndiyo mwenyewe"

    Mariam akanyoosha mkono ili kumsalimia Ducha waliposhikana Ducha alivyo mshenzi akamtekenya kwa kidole cha kati mpaka Mariam mwenyewe akashtuka

    “kwa hiyo brother huyu ndiyo Shemeji"

    Ducha aliuliza kwa uchangamfu

    ”ndiyo mama watoto wangu kipendacho roho"

    “ohoo nashkuru Sana kwa kumfahamu"

    Baada ya utambulisho Ducha akaenda kuonyeshwa chumba chake

    *******

    “bibi"

    ”abee mjukuu wangu"

    “kesho mi naondoka yani narejea zangu mjini"

    ”mmh Hafidhi mjukuu wangu mbona waondoka mapema hivyo? Kwanini usisubilie mpaka tutakapo vuna mpunga ili nikupatie kiasi cha pesa kidogo"

    “hapana Bibi mi sihitaji hata sentano kutoka kwako kama pesa ninazo"

    ”sawa mjukuu wangu mi Sina kipingamizi wacha Basi nikuandalie zawadi zakwenda kuwapelekea huko Mjini"

    Siku hiyo Bibi mtu alimuandalia mjukuu wake zawadi kibao majira ya Saa tatu Asubuhi bwana mkubwa Chinoge alikuwa ndani ya Gari akirejea Mjini

    ilishapita wiki mbili tokea tukio la kuwawa kwa Gulam chumba chake kilifungwa kwa muda siku ya siku kikafunguliwa mama mwenye nyumba akaambiwa yupo huru kukipangisha ikawa Kama bahati Chinoge kuwasili maeneo yale akiwa kaongozana na Dalali wa vyumba nyumba na mashamba bila kusahau viwanja na flemu za kufanyia biashara







    ___________

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog