Search This Blog

Thursday 24 November 2022

WAPANGAJI WENZANGU - 5

 

     



     

    Chombezo : Wapangaji Wenzangu

    Sehemu Ya Tano (5)

     



    Kuna wakati mwanaume unapofikwa na jambo ni lazima ufanye maamuzi ya kiume,... Kiukweli Swalehe alimpenda sana Zahra lakini kwa nyodo zake akahisi Swalehe sio mtu sahihi kua kama mume wake, Swalehe hakukata tamaa alisota na kusota juu ya Zahra, mpaka ikafikia wakati anapewa ushauri na baadhi ya kaka zake ambao ni mafundi wake, hivyo kuanzia siku hio akaacha kumfuatilia Zahra.....



    Zahra baada ya kufanyiwa uhuni ndipo akajua kuna umuhimu wa kumpenda mwanaume aliekupenda na haijalishi ana kazi gani... Kwasababu mpaka mwanaume kukutaamkia anataka kukuoa, tayari keshajijua anaweza kukuachia pesa ya kula kila siku,...



    Zahra alipigana sana juu ya kumrudia Swalehe mpaka akafanikiwa kumpata, lakini Swalehe hakua na upendo kama ule wa zamani hivyo hata kumkubalia kwake ni kama kishingo upande tu,.... Na ilifikia hatua mpaka akataka kulala nae, sema kuna vikwazo vilijitokeza mpaka akaamua kumuacha, lakini ilibaki kiduchu tu Zahra aliwe na Swalehe,.. Na Swalehe akamuahidi Zahra kuwa akirudi watafanya mapenzi,.. Lakini sasa Swalehe aliporudi kakutana na mtoto wa kitanda aitwaye Farida, hivyo hamu na Zahra ikawa haipo tena....



    Leo usiku walikutana getini, Zahra akiwa anatoka dukani kununua mahitaji madogo madogo, na Swalehe alikua akitoka katika mishe mishe zake... Zahra aliweza kumzuia Swalehe asiingie ndani kwanza, wafanye mazungumzo yao hapo hapo nje



    "swai... Kwanini unanitesa hivyo.. Yaani unalala na mtu mshamba vile, hajui hata kuoga... Kwanini lakini unanitesa?? Niambie kama hunipendi"

    Aliongea Zahra huku akilia sana na hapo anatoka dukani kununua vitu vya kupika...

    "Zahra... Kiukweli labda uniache tu kwa sasa... Yule msichana wa watu ana kosa gani... Msichana wa watu hana pakulala.... Mwache"

    "nimeshajua hunipendi swai... Niambie tu usije ukanichezea"



    Aliongea Zahra mana hamuelewi swai, kwanini alilala na yule mwanamke,

    "lakini zaru, hata wewe mwanzo hukua ukinipenda.... Hata mimi naweza kusema tuwe kaka na dada tu"

    Aliongea Swalehe tena kwa kujikaza sana,.. Na wakati huo Zahra kabaki mdomo wazi....

    "ivi swai una akili wewe... Yaani mimi na wewe leo tuwe kaka na dada"

    "kwani ajabu... Mana mwanzo hata urafiki na mimi ulikua hutaki... Lakini mimi sitaki kulipiza baya kwa baya.. Mimi nataka tuwe kaka na dada tu"

    Aliongea Swalehe, tena kwa kujiamini haswa,... Sasa hatujui Swalehe anajivunia nini kwa hilo mana ana mpango wa kuoa... Na alio mlenga ni Zahra...

    "swai,... Yaani umeuchungulia uchi wangu afu unaniambia mambo ya kaka na dada... Niambie huo ukaka na dada unakujaje baina yetu"

    Aliongea Zahra tena akiwa anatetemeka mno,.. Mana waliingiziana mambo lakini hawakufanikiwa hata kukatika viuno vyao, kukawa na vikwazo, sasa Zahra analia kwakua Swalehe alisha mchumgulia uchi wake afu sasa hivi analeta mambo ya kaka na dada....

    "Zahra, mi nadhani utaelewa tu huko mbele,.. Tafadhali sana, tafuta mwanaume mwingine... Sihitaji kuoa kwa sasa"

    Aliongea Swalehe huku Zahra akimuangalia swai kwa jicho la hasira

    "najua kisa ni huyo malaya wako mchafu kuoga... Sasa tutaona sasa mimi na yeye ama zangu ama zake"

    Aliongea Zahra kisha akaingia ndani kwa hasira, tena huku akitetemeka sana.... Mana hakuamini kama Swalehe angelimjibu hivyo kua kuanzia leo tuwe kaka na dada, yaani ndugu kabisaaa...



    Baada ya Zahra kuingia kwao kwa hasira,.. Swalehe nae akawa anaingia kwake,.. Lakini ile anafika tu mlangoni akakutana na farida kabeba safuria ya ugali tena ikiwa ina moto...



    "we farida... Unakwenda wapi sasa"

    "ndugu yako kanifukuza"

    "ndugu yangu??... Ndugu yangu nani"

    "yupo huko ndani... Sijui ni mama yako mdogo sjui ni shangazi yako..."

    Sasa farida aliposema hivyo, Swalehe akajua huyo ni mama Mwajuma ndio kaanza visa...

    "rudisha hio safuria ndani"



    "wewe, unarudi kufanya nini tena huku"

    Aliongea mama Mwajuma, bila kujua na swai yupo nyuma yake



    "we mtoto hivi wewe ni kiburi sana ee"

    Mama Mwajuma alikwenda tena kuzima jiko... Swalehe akaingia na kuliwasha tena,... Safari hii kawasha Swalehe..



    HAPO NDIPO TULIPO ISHIA JANA



    Sasa Swalehe baada ya kuliwasha jiko hilo, mama Mwajuma akapunguza mikwara.... Mana kazima yeye lakini kawasha Swalehe, na ndio maana pale juu nikasema mwanaume ni lazima muda mwingine uwe na maamuzi ya kiume, Swalehe aliona mbali sana hivyo aliamua kama kuna ubaya wacha uwe ubaya tu....

    "swai, kwani vipi tena baba"

    Aliongea mama Mwajuma tena kwa kitumia pua... Mpaka farida alishangaa sana, kwanini mama mtu mzima anamlegezea mtoto sauti kiasi hicho...

    "aahhh Samahani mama mwaju,.. Kwa sasa atakua akinipikia huyu msichana..."

    Aliongea Swalehe huku akimshika farida begani....

    "kwanini sasa swai... Mimi ndio mwenye haki ya kukupikia.. Kumhuka huyu ulimpa hifadhi tu"

    Aliongea mama Mwajuma kwa sauti ile ile, na hata macho yake hayakua makali juu ya Swalehe....

    "ni kweli, lakini nikiwa kama binadamu... Huyu msichana hana pa kulala mpaka sasa,... Na dada yake anaendelea kumtafutia kazi"

    Aliongea Swalehe,... Sasa mama Mwajuma akajua kuwa kuishi kwa msichana huyu, hapo kwa swai, kutaleta matamanishi ya kimwili, bila kujua farida kaamkia hapo hapo tena kaliwa vizuri sana na Swalehe....

    "sasa swai, mimi nina mdogo wangu wa kike... Naomba nimuombee akaishi nae, ni hapo jirani tuu"

    Aliongea mama Mwajuma, mana aliona kwa uzuri wa farida, yaani haingii hata tone, japo mkubwa dawa lakini sio kitandani jamani.. Mtoto ni mtoto na utamu wa mtu mzima na mtoto, ni tofauti kabisa... Ni kama nanasi na papai... We mwenyewe unajua kitamu ni kipi, lakini vyote vina kazi zake mwilini, ila utamu ni tofauti kabisa...

    "yupo wapi huyo mdogo wako"

    "hapo nyumba ya pili tu"

    "tutajua kesho tunafanyaje, lakini kwa leo wacha apate hifadhi hapa"

    "sawa,.. Kwahio nirudi na chakula changu"

    "Samahani lakini... Huenda nimekupata hasara ya mchele... Kiukweli ungerudi nacho tu"

    Aliongea Swalehe huku mama Mwajuma akibeba mabakuli yake ya vyakula,....

    "mwanangu kesho utapata pa kulala sawa mama"

    "sawa"

    Aliongea mama mwajuma kisha huyoo akaondoka zake.... Swalehe akajitupia kitandani wakati huo kachoka....

    "maji tayari, wacha nikupelekee bafuni"

    Duuuuuu Swalehe haamini kuambiwa maji tayari,... Wakati yeye alikua akiwaza ataanzaje kuoga maji baridi, sasa kayakuta yamesha pashwa.. Wakati huo hata ugali umeshaiva,.. Basi farida alipeleka maji bafuni.. Alipokuja alianza kumvua Swalehe shati... Eeehh mpaka Swalehe anajihisi kua na mke, wakati walaaa.. Farida kweli alikua na mbinu za kijijini, mbali na ushamba wake lakini aliweza kumteka Swalehe.... Sasa Baada ya kumvua shati, Swalehe alishangaa kasukumwa kitandani,.. Mara kavuliwa mkanda na suruali ikatolewa... Akabaki na boxer peke yake...

    "mbona haraka hivi"

    Aliongea Swalehe huku farida akiangusha jicho la mahaba, bila kumjibu kitu....

    Farida aliishika ile boxer na kutaka kuivua, lakini swai alikataa...

    "Unakwendaje na kuoga na boxer?... Hebu vua nitaifua kesho"

    Aliongea farida,.. Sasa ile Swalehe anataka kujibu tu.. Saa mingi sana boxer ipo chini, sasa zakhari imebaki wazi.. Farida akaishika shika kisha akamfunga taulo,...

    "twende bafuni"

    Farida aliongea hayo huku akimvuta waende bafuni... Wakati huo Swalehe kaduaaa, yaani haamini vitu anavyo fanya farida,..

    "kuoga wote au"

    "kwani kuna ubaya"

    "hapana farida ... Mi najiskia aibu kuoga wote"

    "mbona leo alfajiri hujaskia aibu kunipanua mapaja yangu"

    "ahh tuyaache ayo... Hii kuoga niache niende mwenyewe"

    Aliongea Swalehe, na farida ni msikivu...

    "sawa basi... Wacha nikuandalie kachumbari, au hupendi"

    "napenda sana... Kiwe na Pilipili kwa mbali"

    Aliongea Swalehe huku akitoka kwenda bafuni,... Ikiwa ni mida ya saa tatu za usiku...



    Kesho yake asubuhi, Swalehe anakuja kuamka, kakutana na maji ya kuoga.. Aliporudi kakutana na chai ya nguvu,..

    "swai??... Jana usiku ulifanya kazi ngumu sana... Pata supu kwanza kabla ya vyote"

    Aliongea farida akimaanisha kwamba jana usiku Swalehe alikata viuno sana,... Hivyo aanze kugonga supu kwanza... Basi Swalehe alipata chai nzito ya mtoto wa kitanga.. Msambaa mwenzie,..  Baada ya Swalehe kumaliza chai alitoka kwenda kazini,... Kama kawaida kamuachia pesa ya mezani shilingi elfu tatu,



    Baada ya masaa kadhaa farida kampelekea dada yake elfu moja, ili ampikie mtoto, mana shemeji yake hakuacha kitu...

    "farida.... Ahsante sana... Yaani hapa nilikua nawaza nalujaje hapo ndani kwako hata nipate kikombe cha uji"

    Aliongea Semeni huku akilia kabisa, mana mume anamnyanyasa sana, yaani hata pesa ya matumizi haachiwi hata kidogo,..

    "dada, Usijali, kidogo tutakula wote..."

    "haya niambie,... Na leo kakukandamiza"

    "heee, sasa hivi ni kama dozi dada... Naliwa mpaka naskia raha yani"

    "wacha weee.. Mama mwenye nyumba..."

    "mmmhhh dada, bado... Afu kuna yule mama kasema eti niende kuishi kwa mdogo wake"

    "mama gani tena"

    "yule chumba kile..."

    "mama Mwajuma"

    "ndio"

    "kwanini.. Na siku wakati namuomba, kwanini asikusaidie"

    "mimi sijui dada"

    "hakuna kwenda... Akalale mwenyewe.... Wewe tayari umeshapata mume, mdogo wangu tulia.. Wanaume wa sasa ni wababaishaji tu.. Wewe ni mtoto wa kitanga, hata kama hujui sana mpe yele ya kishamba shamba...sema jimwanaume langu ni lilevi tu... Lakini ningempa mapenzi mpaka adate mwenyewe"

    Aliongea Semeni huku farida akicheka

    "sasa kwanini hajadata"

    "mmmmhhh mlevi?? Mlevi na mapenzi wapi na wapi? Bora mnywaji kuliko mlevi"

    Basi walimaliza kuongea mtu na dada yake, sasa kaja ndani kwake kakusanya nguo chafu kisha akawa anazifua

    "enheeeeeee... Nilikua Nakusubiri sana kwa ham we malaya"

    Alikua ni Zahra, tena wakati huo kafunga Kibwebwe kiunoni...

    "heeeeee zaru, haya cha kuniita malaya mimi kwa kosa gani"

    "muone vile.. Eti kwa kosa gani.. Kwani hulijui kosa lako wewe"

    Aliongea zaru tena wakati huo ana hasira mno

    "lakini mimi sijui kosa langu... Na kama ni gesi, sikumwambia kua wewe ndio ulitumia.."

    Aliongea farida akidhani labda Zahra kaja kwa kesi ya gesi kuisha...

    "we msenge nini wewe... Mimi naongelea mambo ya gesi hapa..."

    "Zahra... Tafadhali sana, mimi sihitaji ugomvi na wewe.."

    "ila unahitaji ugomvi na nani"

    "sitaki kabisa"

    "kwanini kupewa hifadhi tu unachukua waume za watu"

    Aliongea Zahra, sasa kule ndani... Leo mama Mwajuma hajaenda kazini, saa ngapi hajasikia kuwa kwanini farida anachukua waume za watu...

    "we zaru? Kuna kitu nimesikia ukikiongea, kama kimenigusa hivi"

    Aliongea mama Mwajuma huku akisogea,.. Kama unavyojua wapambe tena... Baadhi ya wapangaji nao wakaanza kitoka..

    "heheheeeee haaaalooooo...."

    Kuna mpangaji kacheka cheko la kishangingi...

    "mama Mwajuma.... Huyu mdogo wake Semeni ni nyoka... Anauma na kupuliza huyu"

    Aliongea Zahra, huku mama Mwajuma nae akisema

    "we zaru... Kwani kaiba mume wa nani"

    Mama Mwajuma Alimuuliza Zahra kuwa kwani kaiba mume wa nani...

    "kamchukua mume wangu... Sijui kampa nyuma.. Mshenzi huyu natamani kumpiga mimi huyu"

    Aliongea Zahra huku akitishia kumpiga,.. Sasa zaru hajaolewa na wapangaji wanashangaa kuskia zaru kaibiwa mume.. Mume gani huyo asiojulikana....

    "we zaru uliolewa lini wewe... Na huyo mume ni nani... Au wataka kumpakazia mwenzio tu"

    Aliongea mama Mwajuma bila kujua Danga lake ndio huyo huyo mume anae gombewa...

    "we mama wewe.... Ina maana unavyonikuta na Swalehe kule ndani, unaona ni mgomba yule... Yaani na utu uzima huo hujavuta tu picha kua nina mahusiano na Swalehe... Na huyo Swalehe ndio analala na huyu malaya hapa..."

    Aliongea Zahra, sasa mama Mwajuma leo ndio anajua kumbe huyu Zahra ana mahusiano na Swalehe,... Sasa mama Mwajuma kamgeukia Zahra...

    "haya wewe huo uhusiano na yule kijana umeanza lini na umalaya wako.. Hivi zaru utakuwa malaya mpaka lini.. We juzi si ulikua na mwanaume wewe... Sasa kwa taarifa yako wewe ni mtoto sana kwangu... Sasa ama zako ama zangu"

    Mama Mwajuma anachimba mkwara kwa Zahra,... Sasa wapangaji nao wanashangaa kwanini mama Mwajuma kaingilia ugomvi wa watoto

    Sasa farida anashangaa kua huyu mama na Swalehe wakoje,.. Japo jana walibishana pia lakini bado hajajua... Sasa farida akavunja ukimya na kumuuliza mama huyo..

    "Samahani mama angu... Kwani wewe na Swalehe ni mtu na mtoto wake, au ni mtu na shangazi yake"

    Aliuliza farida mana yeye hajuagi kuwa huku mjini mambo ni watoto kwa watu wazima....





    Farida yeye ni mtoto wa kijijini, hakuwahi kusikia kuwa mjini kuna wamama watu wazima ambao wanapenda wavulana wadogo, tena anampenda mvulana ambaye ni mtoto wake hata wa tatu,..



    "we nawe unauliza swali gani hilo... Swalehe ni kama kijana wangu"

    Aliongea mama Mwajuma, huku akiondoka

    "kumbe wewe unampenda swai, heheheeeeeeee haaaaloooo... Nilikua sijui kumbe unamegwa na kitoto kidogo vile"

    Zahra aliongea hayo huku akiweka vidole juu tena kwa kuruka ruka,.. Farida roho ilimuuma sana japo haamini kama kweli mtu mzima kama huyo ana mahusiano na mtoto mdogo kiasi kile,... Yaani kadiriki kumvulia mtoto chupi na kumpanulia mapaja,...

    Sasa mama akarudi mbio kija kupigana na Zahra,.. Mama Mwajuma alikua na mwili wa unene kiasi, hivyo Zahra akamkimbia na pia ni mtu mzima, na kama unavyojua ngumi za kike, kama hawajuvuana nguo ni bahati... Mana zao ni kuvuana nguo ili anapozuia asivuliwe ndipo hapo anapokula kichapo... Sasa Zahra akamuepuka mama mwajuma na kukimbia ndani

    "mbona unakimbia, wewe si msichana mwenye nguvu... Toka sasa nje"

    Aliongea mama Mwajuma wakati huo farida anaendelea kufua nguo za Swalehe pamoja na zake,....

    "halafu na wewe... Utakiona hiki chumba kigumu"

    Aliongea mama Mwajuma huku akimnyooshea farida kidole,...

    "hehehehehehe wewe mama mwaju, haya kumchukia mdogo wangu huko kisa nini"

    Aliongea Semeni ambaye ni dada yake farida,...

    "huyu mdogo wako malaya... Kafuata kazi mjini au kaja kutafuta wanaume"

    Aliongea hivyo mama huyo huku mama abu akiongea kuwa

    "sasa mama mwaju.. Huyo mwanaume alie nae ni wako?"

    "hata kama sio wangu, lakini sio kwa kutembea na wanaume wa humu ndani na kujifanye ni mumewe"

    Aliongea mama mwajuma kisha akaondoka, lakini wapangaji wote wameshajua kuwa mama Mwajuma ana mahusiano na Swalehe,.. Farida alianza kulia pale pale chini,..

    "farida, pole... Ina maana umempenda Swalehe kiasi hicho"

    Dada yake farida alimuuliza mdogo wake, mana kwa mara ya Kwanza kumsikia kuwa anampenda Swalehe kutoka moyoni, alihisi ni janja ya wanawake kama wanavyosema,.. Sasa Semeni leo ndio anashangaa kumbe farida anampenda Swalehe Kiukweli ukweli na sio uongo, yaani hatanii...

    "dada niache,... Ina maana kumbe huyu mama mtu mzima anatembea na mtoto kiasi kile"

    Aliongea farida huku akilia, mara Zahra katoka

    "we malaya, unamlilia nani? Kama ni swai wangu utaishia kuchezewa tu"

    Aliongea Zahra, mara Semeni kaamka nae,... Semeni sio mama mtu mzima ni msichana tu na mtoto wake wa kwanza ana miaka miwili,.. Hivyo bado ni mbichi mbichi, sema shida tu ndio zinamzehesha... Sasa ikawa ni ngumi baina ya mama abu na Zahra,... Kazi iliopo ni ya wapangaji kuwatetea wasiendelee kupigana,.. Na yote hayo sababu ni Swalehe,.. Mtoto wa watu hana kazi ya maana lakini anagombaniwa kama mayai ya mbuni,.. Basi ugomvi uliisha na kila mmoja katulia kwake,.. Kama kawaida farida humpatia dada yake unga ili aweze kupata chakula mana mumewe haachagi pesa ya kula, kwani ni yeye na pombe tu,..



    Jioni Swalehe alirudi nyumbani, lakini alimkuta farida anapika huku akilia,.. Yaani haamini kama mama mtu mzima kama yule anampenda Swalehe mtoto mdogo sana kwake,..

    "alaaa, we una nini... Kuna msiba"

    Aliuliza Swalehe, farida alimkumbatia Swalehe huku akiendelea kulia..

    "swai, nakupenda sana... Nakupenda, lakini nimeumia sana pale nilipojua kuwa mama mwajuma una mahusiano naye.... Ina maana umetembea na yule mwanamke?? Nijibu swai, ni kweli umetembea nae?"

    "ndio"

    "swaaaaaiiiii.... Si kama mama yako yyle jamani, ina maana umerudi ulipotoka swai kwanini lakini"

    "we nani kakupa hizi taarifa"

    "kila mtu anajua"

    "basi pole... Ila nimeachana nae"

    "umeachana nae gani wakati anatishia watu"

    Aliongea farida, na hapo Swalehe ndio anajua ivi kumbe farida anampenda, mana alijua anamtumia tu kwakua hana pa kuishi...

    "ebu pika chakula kwanza tutaongea"

    "mi nataka tuhame hapa... Sitaki kuumia kila siku"

    Farida alitoa wazo la kuhama hapo mana hatoweza kugombana na majirani zake kisa mwanaume,....

    "sasa huyo mama ndio anakutishia au"

    "sio mama Mwajuma tu.. Hata Zahra ananisumbua sana"

    "basi we pika kwanza..."

    Swalehe aliona ni jambo la kawaida na uzuri wa Swalehe ni muwazi, kama jambo ni la kweli anakubali mana hata akificha ni kazi bure... Sasa wakati farida anachota unga,.. Swalehe aliona mbona unga wa juzi tu umepungua kiasi hicho.. "

    "huo unga si wa juzi tu kama sio jana"

    Aliuliza Swalehe, hapo farida akaanza kuogopa... Mana kweli unga hauna hata siku mbili, lakini umefika katikati... Uzuri ni kwamba wote wamekutana wasema kweli,.. Farida alipoulizwa hivyo,.. Pale pale alimuangukia Swalehe na kusema ukweli wote kuhusu yeye na dada yake.... Swalehe alimuelewa kisha akaenda zake kuoga...

    "Unakwenda wapi na panga"

    Aliongea farida baada ya swai kutoka na panga usiku kama saa tatu hivi..

    "nipo hapa nje"

    "na hilo panga"

    "tulia"

    Farida aliogopa sana kwa kitendo cha Swalehe kutoka na panga usiku...



    Saa nne na nusu Swalehe anarudi huko alipo kwenda,... Lakini shati alilovaa lilikua na damu damu.. Farida alizidi kuogopa kabisa, yaani siku hio hakutamani kabisa kulala na Swalehe...

    "swai, umefanya nini lakini"

    "tulia wewe.... Ulizani dawa ya maumivu ni parasetam peke yake"

    Aliongea Swalehe, lakini farida hakiyaelewa maneno hayo,.. Swai alichukua maji ya baridi na kwenda kuoga kwa mara nyingine tena,.. Aliofanikiwa kuona damu kwenye nguo ni farida...



    Wakati huo huo Swalehe akiwa bafuni, ghafla geti kubwa likasukumwa,...

    "mama abu... Mama abu"

    Aliingia mtu na kuita kwa nguvu akimaanisha Semeni ndie alieitwa

    "abeee"

    "mume wako atakufa..."

    Aliongea mtu huyo huku mama abu akianza kuchanganyikiwa kwa kuskia mume wake atakufa,..

    "Uuuuuuuuuwiiiiiiii mume wangu kafanya nini tena"

    Alipiga kelele mama abu huku mjumbe akisema

    "chukua majirani zako twende tukambebe tumuwahishe hospitali"

    Aliongea mjumbe huyo... Baadhi ya majirani wakatoka, lakini swai alikua bafuni anaoga... Alipotoka bafuni akakutana na hizo taarifa toka kwa farida, swai nae hakukaa mana ni jirani yake... Mkuku mkuku mpaka hospitali.... Mr jomo alipigika, kwani pia kakatwa kwenye mikono na miguu kidogo tu, kapigwa mno hata kujitambua hajitambui....

    "kuna nini tena jamani"

    Aliuliza Swalehe baada ya kufika eneo katika wodi ya majeruhi,...

    "shem, sijui ni nini jamani Uuuuuuuuuwiiiiiiii"

    aliongea semen huku akilia sana,..

    "we mama hatutaki kelele"

    Aliongea dokta baada ya mama abu akupiga kelele

    "Samahani dokta, mgonjwa kapatwa na nini labda"

    Swalehe alimuuliza dokta

    "mgonjwa kavamiwa na majambazi.. Na hatuwezi kumtibu mpaka mlete PF3 ndipo atibiwe"

    Aliongea dokta, hapo hapo Swalehe akakimbia kituo cha polisi na kupewa PF3, ili mgonjwa apate matibabu... Pesa za matibabu zilikua ni za Swalehe mana mama abu hana kitu, mume mwenyewe ndio huyo kavamiwa na huenda pesa hana...



    BAADA YA WIKI MOJA KUPITA



    Swalehe akiwa na mgonjwa karibu, mana yeye ndio mwenye dhamana ya kukaa nae,... Lakini kwa wakati huo mgonjwa keshapona imebaki ruksa tu warudi nyumbani

    "vipi hali kaka"

    Swalehe alimjulia hali baba abu au mr jomo,

    "safi tu ndugu yangu..."

    "hali yako unaendelea"

    "aisee safi jirani... Kiukweli nakushukuru sana jirani,.. Umeniokoa kwelikweli"

    "Usijali jirani... Sisi ni binadamu, lazima tusaidiane"

    "sijui nitakulipa nini... Mungu atakulipa tu jirani"

    "Usijali... Haya vipi, kwani ilikuaje usiku ule"

    "weeee jirani.. Kwani hata nakumbuka.. Nilishangaa tu mapanga ya kichwa, mara mtama.. Nilikua nimelewa sana nilikuja kuzinduka nipo hospitalini"

    "walikuwa majambazi wangapi"

    "mmhhhhh wengi sanaaaa... Yaani kila mmoja alikua anapiga upande wake"

    "duuuu pole sana ndugu yangu"

    "ahsante sana, ila pole sana hata wewe.. Mana umenihudumia mpaka sasa nina nafuu"

    Aliongea mr jomo, wakati huo kakaa kitandani...

    "ila jirani... Hio ni laana ya familia yako... Mimi siwezi kuamini kua ulikua huachi matumizi ya familia yako,.. Mtoto wako abu mdogo kiasi kile lakini unashindwaje kumpa huduma"

    Aliongea Swalehe ila ana maana yake mpaka kusema hivyo

    "ni kweli jirani... Nakili kwa hilo,.. Ila siwezi kufanya huu ujinga... Kweli hii ni laana ya familia hii"

    "jirani??.... Acha pombe... Acha kulewa,... Jali familia yako"

    Swalehe Aliongea kisha huyoo akaondoka zake....



    WIKI MOJA BAADAYE



    Swalehe akiwa zake ndani mida ya saa mbili za usiku,...

    "siku hizi naona unga unakaa kaa"

    Aliuliza Swalehe huku farida akijibu

    "ni kweli mume wangu.. Sasa hivi shemeji anaacha hela"

    Alijibu farida tena kwa kumuita mume, ingali bado hawaja oana, kana kwamba tayari Swalehe ana mpango wa kumuoa farida,... Kana kwamba mpaka anakubali kuitwa mume basi ndo ipo....

    "waacha weee, kwahio sasa hivi kama kawaida"

    "ndio.. Toka apigwe na majambazi mpaka leo... Sasa hihi anarudi saa kumi na mbili jioni, tena anakuja na mkate kila siku"

    Aliongea farida lakini Swalehe alikaukia kucheka ile mbaya, Mapaka farida akaanza kushangaa Swalehe anacheka nini

    "we swai jamani sasa unacheka nini"

    "unakumbuka kuna siku nilikwambia sio lazima dawa ya maumivu iwe parasetam,.. Unakumbuka ile siku"

    "ndio nakumbuka ila sikukuelewa kabisa ulikua na maana gani"

    Farida alikaa vizuri ili asikilize maana ya ile sentensi ambayo Swalehe Aliongea siku ile



    Huku kwa Semeni au mama abu,.. Huezi amini baba abu yupo safi anacheza na mtoto na mama anapika,... Mama abu anajiskia raha sana na kujihisi kama mdio kaolewa jana, kumbe kala msoto mpaka basi,.

    Yaani sasa hivi ndoa yake imekua tamu mpaka raha yani..... Kwani kila  akiangalia unga ni mwingi, mchele, yaani kila kitu kama mahitaji ya nyumbani,.. Sasa ilikua ni ndoa na sio ndoano



    Sasa huku kwa Swalehe akiwa na mpenzi wake farida,.... Wakati huo Swalehe anacheka kwa kusikia baba abu sasa hivi anarudi mapema tena na kitoweo kikiwa mkononi....

    "kwani siku ile ulimaanisha nini kusema sjui dawa ya parasetam"

    Aliendelea kuuliza farida kisha Swalehe akakaa vizuri na kusema kuwa

    "sikia farida, kwanza Utanisamehe sana kwa hilo.... Ukweli ni kwamba, mimi ndie nilie mcharanga mapanga baba abu"

    Aliongea Swalehe, huku farida akishtuka na mapigo ya moyo kumwenda bio

    "whaaaaaaaaaaat???"









    Farida hakutegemea kwamba Swalehe ndie aliweza kumpiga mapanga shemeji yake,.. Na sio yeye tu bali ni kila mmoja aliejua tukio hilo hakuweza kuhisi ya kwamba msababishaji ni Swalehe,.. Sasa baada ya wiki kama mbili hivi kupita, Swalehe aliamua kusema ukweli na ni baada ya jomo kupona...



    "whaaaaaaaaaaat???"

    Alishangaa farida huku akishika moyo wake,

    "sasa unashangaa nini"

    "ina maana swai mpenzi wangu kumbe wewe ni jambazi"

    Aliongea farida huku Swalehe akicheka sana, kana kwamba sio kweli kwa yale anayo yafikiri farida..

    "skia nikwambie farida... Lile neno nililokwambia kuhusu parasetam, nilimaanisha kwamba.... Sio lazima mlevi uzungumze nae.. Bali muongeleshe kwa vitendo"

    Aliongea Swalehe lakini farida bado alibaki njia panda...

    "bado sijakuelewa sentensi yako ina maana gani"



    "skia farida... Kwa kawaida, mlevi hua haambiwi akasikia... Kitendo cha wewe kuniambia kua unapeleka unga kwa dada yako ingali mwanaume wake yupo na bado ni kijana mwenye nguvu tena mwenye kazi inayo muingizia pesa.. Kiukweli roho iliniuma, na haikuniuma kwakua umetumia chakula changu, hapana... Bali imeniuma kwanini aitese familia yake??"

    Aliongea Swalehe huku farida akiuliza

    "kwahio, baada ya hapo ukahisi kuongea nae"

    "ndio.. Na siku ile ilikua hivi"



    SIKU ILE SWALEHE KATOKA NA PANGA



    alipotoka na panga alipitia dukani na kununua mayai mawili, na kwakua anaijua kona ya jomo ambayo huitumia wakati wa kurudi nyumbani,.. Alikaa mahali na kumwona jomo akija staili ya ulevi,.. Kana kwamba alilewa sana,... Alichokifanya Swalehe ni kuanza kumziba mdomo kisha akatoa pesa zake zote kama elfu 50 hivi,.. Na kuanza kumshambulia mr jomo,.. Swalehe alikuwa peke yake, sema alikuwa akipiga sehemu tofauti tofauti na kumfanya jomo ajue wako watu zaidi ya mmoja lakini alikua mmoja... Na Swalehe hakutaka kumuacha bila kumkata... Ila Swalehe alikua anachagua sehemu za kukata kwelikweli,.. Ilimradi tu asikate mshipa wowote katika mwili wa baba abu,.. Alimpiga kipigo kikali, kisha akamvua suruali na kumpasulia yale mayai.. Kana kwamba akija kuzinduka anajua kaingiliwa na wenzake... Hicho ni kijuto moja wapo na ni lazima aache ulevi,...  Pesa ya jomo haikuliwa na Swalehe, bali ile pesa ndio iliomtibu jomo kule hospitalini...



    MWISHO WA SIKU ILE USIKU



    "haaaaaaaa... Swaaaaiiiii... Ina maana kumbe kweli ulimkata kata shemeji"

    Aliongea farida baada ya kuambiwa ukweli juu ya kuvamiwa kwa mr jomo

    "ni kweli ni mimi... Ila nilifanya hivyo kwa kusudi moja tu"

    "kusudi gani kama sio kumuua baba wa watu"

    "sikiliza... Mlevi, hua hawekwi kikao.. Wala hasemeshwi...na wala haambiwi acha pombe akaacha.. Ila mtafutie kitu kitakacho mfanya ajute katika maisha yake, na ajue kitu hicho kama sio kulewa asingelifanyiwa.. Hivyo atauchukia ulevi mpaka kufa kwake"



    Swalehe Aliongea mpaka farida akacheka...

    "ina maana kumbe ulikua una maana hio"

    "ndio"

    "sasa angekufa je"

    "najua asingekufa kwasababu hata sehemu nilizokua nakata ni sehemu ambazo sio njia za mishipa... Na kitu ambacho atakuja kujuta ni yale mayai nilio yapasua... Na toka atoke hospitali hajanigusia, kana kwamba kalimezea na kujua kweli aliingiliwa,.. Na siri hii usimwambie dada yako, mana atamwambia na mwisho wa siku tabia itarudi pale pale..."

    Swalehe alimaliza kuongea kisha akapanda zake kitandani

    "Kwahio unasema mlevi haambiwi acha pombe akaacha"

    "ndio... Mjeruhi mahali ambapo anaweza kujutia ulevi wake... Sasa ona sasa mr jomo ni baba mzuri wa familia"

    "Duuuuuuu... Yaani kama sio kinifafanulia,.. Hakiyamungu ningeondoka hapa"

    "mmmhhh ona ulivyo mwongo"

    "kweli vile"

    Basi ilikua ni usiku mzuri sana kwao, na sasa Swalehe na farida wapo katika mbio za kufunga ndoa...



    Kesho yake nyakati za asubuhi, farida akiwa anaosha vyombo,... Swalehe alishatoka kwenda kijiweni mana kazi zake ni za ujenzi hivyo mpaka wapate saiti ya kazi..

    "kaona sasa... Kanajifanya kanajua wanaumeeeeeee"

    Aliongea Zahra, lakini papo hapo dada yake alitoka...

    "we Zahra, kwanini una uchokozi lakini.. Huyo si mchumba wa mtu haya chokochoko ya nini"

    Aliongea fatuma au mama saidi

    "dada, Swalehe ni mpenzi wangu.. Na hata utamu wake naujua... Hili lisambaa sjui lilitoka wapi"

    Aliongea Zahra huku fatuma akishangaa

    "wewe zaru.. Haya huyo swai lini akawa mpenzi wako... Mana mi ninachojua wewe na swai mna ugomvi mpaka mkaanikiana nguo za ndani mlangoni, sasa huo uhusiano ni upi"

    "dada... Swalehe keshanifanya sana hapa ndani kwake"

    Aliongea Zahra, mara mama mwaju nae katoka tena, yaani mama hana hata haya huyu... Wakati huo farida yeye hana stori nao,. Wacha waongee wao ndoa afunge yeye...

    "we Zahra, nimekuskia toka nikiwa ndani... Oohh sjui unajua utamu wake.. Hivi wewe na kishepu chako hicho unaweza kuwa na Swalehe wewe"

    Fatuma alishangaa mbona mama Mwajuma kaingilia hilo balaa... Mana siku ile mama saidi yeye hakuwepo kwahio wapangaji wasiojua kuwa mama mwajuma na Swalehe wana mahusiano ni huyu mama saidi peke yake...

    "mama Mwajuma, mbona sikuelewi"

    "hunielewi nini... Swalehe toka amekuja hapa, anakula juu yangu, kuvaa juu yangu... Kila kitu juu yangu.. Leo mnashoboka tu hapa"

    "lakini mama Mwajuma... Sawa ulikua ukimpa chakula nilikua naona, mana alikua bado ni bachela... Lakini mbona kuna jambo umeingilia hapo, sjui kashepu sjui nini, naona havihusiani na mada hapa"

    Aliongea mama said au dada yake Zahra,

    "sikiliza dada... Huyu mama huyu, umuone tu na utu uzima wake wa bure tu... Huyu ana mahusiano na Swalehe"

    "ati nini?? Yaani yule mtoto ndio katembea na huyu mzee"

    "weeeeee mzee mama ako"

    Zikaamka ngumi,.. Wacha wapigane mama said na mama mwajuma... Farida yeye kimyaa mana anayajua yote hayo hivyo hana hofu nao...



    Ilipofika jioni, farida alizidi kumkazania Swalehe wahame hapo kwenye hilo boma mana anaumia moyo wake pale wanapozidi kumtaja Swalehe kama mpenzi wao, japo kwa sasa haendelei nao... Kweli Swalehe alifanya michakato lakini hakutaka kuondoka hapo mpaka ahakikishe wapangaji wote wamejua kuwa kaoa



    Taarifa zilifika kwa dada mtu... Semeni hakuamini kama mdogo wake ataolewa, mana alikuja mjini kibabe babe tu, na kakutana na bahati ya kuolewa... Kuolewa ni bahati sana na ndio mana kwa sasa ndoa ni adimu sana mitaani... Huezi kuta wapenzi wa miaka 23 kwa 25 wakioana ni kwa bahati sanaaaaa....



    Baada ya dada kujua, taarifa nyumbani,... Kama unavyojua ndoa za kisambaa.. Sjui upeleke hiki mara kile, yaani muoaji anaweza kukata tamaa, lakini swai alijipanga.....



    Tanga Tanzania ndoa ilifungwa tena ya haraka sana, mana katika sheria ya dini inasema MWENYE KUOA /KUOLEWA BASI NA AOE / AOLEWE HARAKA SANA...



    Sasa huku mjini, Zahra anajua fika Swalehe wamekwenda tanga kufunga ndoa na farida...

    "dada, hivi mimi sina bahati ya kuolewa... Nina ubaya gani... Hebu niangalie, yaani napokonywa mwanaume na mtu mshamba mshamba hajui hata kuoga"

    Aliongea Zahra lakini dada yake hakutaka kumsapoti kwa hilo kwani Zahra halujijua kosa lake lilipo...

    "kweli mdogo wangu wewe ni mzuri, una shepu nzuri... Pia unavaa vizuri... Ila kosa lako moja, hujiheshim"

    Aliongea fatuma huku akiondoka...

    "dada... Una maana gani"

    "skia Zahra, wasichana wa siku hizi.. Wengi mtazikosa ndoa.. Kwasababu mna tabia za kimjini... Kitu cha kwanza kabisa.. Mwanaume hua hapendi mwanamke Mjanja, wewe mdogo wangu umekaa kijanja janja sana, mwanaume mwenye malengo hawezi kukuoa kwasababu anahisi ataoa balaa ndani ya nyumba,.."

    Fatuma Aliongea hayo yote baada ya mdogo wake kupokonywa mwanaume,...

    "dada, ina maana na kuvaa kwangu vizuri bado sito olewa"

    "sikiliza Zahra, wanaume hawaangalii mavazi pale wanapotaka kuoa... Wanaangalia tabia... Afadhali mwanzo ulikuwa ukivaa vizuri, lakini ukaja kuiga mavazi ya mjini... Afu sasa kingine, mwanaume hapendi mwanamke muongeaji sana... Kingine mwanaume hapendi mwanamke mjuaji sana"

    "mmhhh dada"

    "ndio hivyo... Sasa hivi unatakiwa ubadirike"



    Baada ya siku mbili Swalehe walirudi kutoka tanga,.. Sasa farida na Swalehe ni mume na mke,... Zahra aliumia moyo lakini haikuwa na jinsi labda haikuwa bahati yake, japo aliikataa mwenyewe kipindi cha mwanzoni.... Huezi amini Zahra alimtafuta ayub yule yule aliowahi kumdanganya na kujifanya tajiri kumbe aliazima vitu vya watu... Namba alishazifutaga lakini kichwani kwake bado zipo japp ni muda mrefu sasa umesha pita

    "hallo ayub mambo"

    "poa.. Nani mwenzangu"

    "ina maana ulifuta namba yangu ayub"

    "sikukumbuki tafadhali, na sasa nipo bize kidogo ofisini... Labda unikumbushe mana nina kikao na wafanya biashara wenzangu"

    Aliongea ayub huku akionekana kweli ni boss

    "ni mimi Zahra"

    "oooohhhh Zahra mpenda pesa.. Habari yako mama"

    "salama tu... Ila tafadhali sana usiniite mpenda pesa"

    "nakuita hivyo... Kwakua nina uhakika bila kujifanya mwenye pesa, nisingelipata penzi lako... Na umenila pesa nyingi sana kisa uzuri wako Zahra"

    Aliongea ayub lakini kama vile alikuwa na dharau fulani hivi...

    "ok tuachane na hayo... Naomba tukutane mjini leo jioni... Nitalipia dina na hata chumba pia ukitaka nitalipia"

    Zahra aliamua kurudiana na ayub

    "hahahahahahahaha, Zahra... Kwa sasa umechelewa.. Tayari nina mke,. Nimeshaoa... Na pia kwa sasa siishi Arusha bali nipo BABATI nimejenga mji wangu huku"

    "Babati??"

    "ndio.. Na pia nina mke na mtoto mmoja"

    Aliongea ayub huku Zahra akianza kulia tena,... Yaani kakosa kote kote

    Zahra alikata simu kwa hasira,...



    Sasa huku kwa ayubu,... Kweli ayub kwa sasa ni tajiri, na ndio yule yule tajiri aliojenga jumba la kifahari kule mjini Babati, na mafundi alikuwepo Swalehe kama mmoja wapo kati ya mafundi 20...

    "kuna malaya mmoja nilitembea nae muda mrefu nikiwa mbeba mzigo"

    Aliongea ayubu kama vile kumhadithia rafiki yake...

    "kwani ulikuaga unabeba mizigo"

    "heeee... Ndio, kabla sijaenda mgodini, nilikua nabeba mizigo kule NMC"

    "alaaaaaa"

    "ndio... Na mungu nae hakunitupa mgodini... Ndio kama hivi hali imekuwa njema"

    "kwahio kakuambiaje huyo mwanamke"

    "naona ana nia ya kurudiana, ila nina mke... Ila kazuri"

    "ahhhh mzuri bila tabia ni mbaya"

    "umeona eee"



    Sasa huku arusha,... Swalehe na farida walikuwa wakihama katika chumba kipyaaa, mana wakiendelea kuishi hapo farida atateseka sana kwa maneno ya mama mwajuma na Zahra,... Hivyo baada ya ndoa yao waliamua kuhama na kuwaachia boma lao,.. Sasa wakatengeneze maisha yao mazuri wakiwa ndani ya ndoa...

    "Nashukuru sana mume wangu kwa kukubali kuhama pale... Nilikuwa nahisi huto nielewa... Ahsante sana... Naapa kukupenda mpaka kufa kwangu, sintosikiliza ya mtu kuhusu wewe... Nakupenda sana mume wangu, utakacho kula nami nitakula.. Utakapo lala, nami nitalala.... Tumuombe mungu nasi tubarikiwe maisha mazuri..."

    Aliongea farida wakati huo kajilaza katika kifua cha Swalehe, tena huku akichezea gaden love za mume wake

    "nami pia nakupenda sana mke wangu.. Ninacho kusihi, tafadhali sana usisikilize ya mtu... Na usidanganywe na mtu... Mana kwa kawaida ndoa huharibiwa na mwanamke,... Na mwanamke huyo sio wewe, bali ni mwanamke ambaye ataanza kukupandikiza umbea, chuki, na dharau juu ya mume wako... Nakupa ujumbe wangu, lakini jieshim, jichunge na ndoa yako.. Na uchunge maneno ya mashoga zako,.. Baya toa, zuri hifadhi... Hapa ni mjini kila mtu hutumia akili yake,... Wengine hutumia akili zao kupotosha ndoa za wenzao kwakua zao zilishaoza... Hivyo kua makini na jiji"

    Aliongea Swalehe kama kumsihi mke wake,....

    "mume wangu.... Masikio yangu, hayasikii neno lolote baya kuhusu ndoa... Mimi ni wako wa milele,..na Kama sikupendi ni kheri nisingelikubali unioe.. Lakini nakupenda nakuheshim na nakujali na ndio maana nimekubali kuolewa nawe... Mume wangu...Kama umetafuta kitoweo Umepata rudi nyumbani tule... Umekosa pia rudi nyumbani tule cha jana... Kama hakuna pia rudi nyumbani tulale"

    Yalikua ni maneno mataam yaliomtoka msichana huyo,.  Swalehe alijikuta akitabasamu kwa mbaaali



    Tukijua huku upande mwingine, Hutaamini macho yako



    Wakati huo huku ndani.... Farida alikua akimpa maneno rafiki yake...

    "Zahra, kwa kawaida huwa kuolewa sio kazi.. Kazi ni kuilinda ndoa yako... Usifuate maneno ya watu,... Kwahio usione ajabu kuolewa, ila jitahidi kuiheshim ndoa yako... Usimjibu mumeo vibaya, mtengee maji pale anaporudi kazini... Mpe vile vitu anavyopenda... Mimi sina cha kukuambia, mana wewe mwenzangu ulikua na kungwi, hivyo najua kakupa somo vizuri... Ila nakuomba sana, mpende mumeo mheshim mumeo... Hapo utaiona raha ya ndoa yako..."

    Aliongea farida huku Zahra akitoa machozi kwa kua.. Kumbe alikua akimkosea sana farida kipindi kile.. Kumbe alikua anamkosea mtu ambae ni nuru katika maisha yake...

    "pia.. Mumeo akipata Shukuru, akikosa muombe mungu kesho apate... Na hata akikosa tena, usikasirike... Zidisha kumuombea mumeo,... Achana na utajiri wa majirani au watu wengine, huo hauwahusu... Mpende mumeo, ipende ndoa yako"



    "PIIIIII... PIIIIIII. PPPPIIIIIIIII"

    Ni sauti ya honi ya gari ikilindima huko nje, mume aliingia ndani fasta na kumchukua mkewe, waliingia ndani ya gari wote ili kumsindikiza mwenzao mpaka kwake.. Ilikuwa ni furaha kubwa kwa Zahra na mumewe....











    Yalikua ni maneno matamu sana yaliomtoka Farida, wakati huo wametulizana katika pango jipya, walilo hama hivi karibuni,.. Tena wamepangisha dabo rumu (rumu mbili zilizo shikana) na maisha yao yalikua na furaha sana



    Tukija huku kwa akina Zahra akiwa katulia pembezoni mwa ukuta, sambamba na chumba chao,.. Alikua ni mwanamke mwenye huzuni sana, na kujiona mwenye nuksi ya wanaume katika dunia hio, alikua akijiangalia sana katika mwili wake... Haikutosha, aliingia ndani na kuvua nguo zake zote katika kioo...

    Dada yake alikua akimuangalia tu mdogo wake kile alichokua akikifanya...

    "we Zahra, haya sababu za kukaa uchi mbele ya kioo ni nini"

    Aliongea dada yake huyo ambaye ni mama Saidi au Fatuma...

    "dada, naumia sana kumkosa Swalehe.. Najiangalia mwili wangu, labda nina kasoro dada"

    Aliongea Zahra huku akilia sana, mpaka dada yake alimwonea huruma mdogo wake...

    "Zahra mdogo wangu,.. Kasoro alio iona Swalehe, haipo kwenye ngozi"

    Aliongea Fatuma huku Zahra akiuliza

    "iko wapi sasa,... Na kama ni kumpenda nimempenda"

    "tatizo sio kumpenda tu... Mwanaume anahitaji vitu vingi vizuri toka kwetu... Busara na hekima ni moja ya vitu wanavyopenda... Unaweza ukavaa chupi tu na ukatembea nayo mtaani.. Ila hekima na husara unayo, ispokua mavazi ndio yatakutafsiri vibaya... Jirekebishe... Ikiwezekana fuata nyayo za Farida, kama kweli unahitaji kuolewa"

    Aliongea dada yake huyo kisha akawa anaondoka, lakini Zahra alimzuia dada yake...

    "dada, hebu shika hili tako langu... Au ni gumu ndio mana sipendwi"

    Aliongea Zahra huku dada akicheka sana

    "Zahra, naona sasa unakwenda kua chizi kisa Swalehe... Alafu nataka kuuliza,.. Hivi mahusiano yako na Swalehe yalianza lini? Mana mimi najua mna ugomvi nyie.. Sasa nashangaa sasa ukisema alikua mchumba wako"

    Aliuliza fatuma huku Zahra akikaa kitandani na kusema...

    "ni kweli dada,.. Mimi na sheby ilikua hivi... Wakati anahamia hapa, sheby alikua akinipenda sana,.. Lakini kipindi kile, nilikua na ayubu, nikajua nimepata mume.. Sasa sheby nikawa simuelewi, saa zingine namtukana.. Saa zingine namletea nyodo na maneno ya kashfa juu yake na wakati huo alikua akinitaamkia kunioa... Ilifikia hatua Swalehe akachoka kunifuatilia, mpaka akaaniacha kabisa,... Sasa nilipo achana na ayubu, ndio nikaanza kumsumbua Swalehe, mpaka nikawa naanika chupi mlangoni kwake kwasababu ndio udhaifu wake... Kiukweli Ilifikia hatua akanisamehe... Sasa tukawa na mahusiano mazuri tu,.. Kuna siku alitaka kunilala (kufanya mapenzi) lakini kila akitaka kuingiza, mara simu imeita... Kila akitaka kuingiza mara mlango umegongwa, Kiukweli siku ile hakufanikiwa kuingiza uume wake kwangu... Na baada ya siku ile.. Kesho yake ndio akapata safari.... Nakumbuka huko alikaa miezi kama sita hivi.. Na ndani ya hio miezi sita ndio akaja farida.... Baada ya Swalehe kurudi,.. Nilishangaa alilala na farida badala yangu... Basi ndio ikawa bifu mimi na farida, mpaka ikafikia wameoana"



    Dada alisikia kila kitu toka kwa mdogo wake....

    "sasa mpaka hapo bado hujaiona kasoro yako"

    Aliongea fatuma au mama saidi...

    "Kiukweli sijaona dada, labda ni kwasababu farida ana shepu kuliko mimi"

    Aliongea Zahra tena kwa kutia huruma sana...

    "Zahra mdogo wangu, mbona wewe ni mzuri,.. Tena mzuri kushinda mimi na una umbo kushinda mimi.. Lakini mbona mimi nina mume.."

    Aliongea fatuma

    "sasa kasoro yangu iko wapi dada"

    "kasoro yako.. Hekima huna... Busara huna... Mavazi mazuri ya heshima uliacha kuvaa.. Wewe na saluni kila kukicha... Angalia Farida, toka amekuja hapa, anasukwa na dada yake msuko wa twende kilioni, haijui saluni... Ulimsema Farida ana chupi zilizo toboka.. Haya wewe mwenye begi zima lenye chupi mpya mbona hujaolewa.... Ulimsema Farida ni mshamba, haya wewe mjanja mbona hujaolewa... Ulimsema Farida hajui kuoga.. Haya wewe unae oga kutwa mara tatu, mbona hujaolewa... Kwahio usidhani kwamba kuvaa kwako vizuri na kunukia labda mwanaume ndivyo anavyo vutaka... Mwanaume anahitaji mwanamke MPOLE, MNYENYEKEVU, ANAEJUA SHIDA NA RAHA... MWENYE KUMHESHIMU MUME... MWENYE KUVAA MAVAZI YA HESHIMA...MWENYE KUIFUATA DINI YAKE... wewe hivyo vyote, ulikua navyo ulipokua kijijini.. Ulipokuja tu mjini ukaviacha.. Ona dada washamba wamekupita... Mtu ana miezi mitatu tu kapata mume.. Wewe una miaka minne sasa.... Na usipobadilika, utachezewa sana"



    Aliongea fatuma au mama saidi kisha huyoo akaondoka zake, Zahra alilia sana, mana maneno ya dada yake yalimchoma na kumuingia haswa,.. Pale pale tabia yake mbaya akaacha, mana ndio nuksi katika maisha yake,.



    Huku nje kwao mama Mwajuma akiwa anamenya viazi kama chakula cha usiku, alikua na watoto wake wakiwa wana andaa chakula cha usiku.



    Ghafla Zahra akatoka nje,.. Huezi amini Zahra kairudia asili yake ya zamani...

    "heeeee, Zahra, ni wewe au macho yangu"

    Aliongea mama mwajuma, lakini Zahra alikaa kimya.. Huku mama mwajuma akisubiri jibu chafu kutoka kwa Zahra, lakini Zahra alikua kimya, kana kwamba, hahitaji ugomvi na mtu...

    "Samahani mama,... Kama nina kosa juu yako, naomba unisamehe. Kwa sasa sina kinyongo na mtu.. Kwan mtu aliekua akitugombanisha, keshaoa sio wakwetu tena. Hivyo sioni haja ya kugombana"

    Aliongea Zahra, hata semeni au mama abuu alitoka nje na kumkumbatia Zahra, mana kaongea point nzuri sana... Hata mama mwajuma aliona kweli haikua na haja ya kuwekeana bifu la hapa na pale...



    BAADA YA WIKI MOJA KUPITA



    Swalehe akiwa kijiweni kwake,.. Na baadhi ya marafiki zake..

    "sasa hivi swai anang'aaa, kuoa raha kweli"

    Aliongea mmoja wa rafiki zake

    "asikwambie mtu bwana, kuoa ni raha"

    Aliongea Swalehe huku rafiki yake mmoja akisema

    "kwaio sasa hivi unaoga maji ya moto"

    "kama kawaida yangu"

    "aaaaaaa Hahahahahahahah"

    Ilikua ni furaha juu yao,... Basi ilifika nyakati za kurudi nyumbani, hivyo swai na rafiki yake mmoja walikua ni wapitaji wa njia moja..

    "unajua bwana swai, kitendo ulicho kifanya, ni kizuri sana, nami natamani sana kuoa.."

    "aliongea bwana Bakari huku Safar ya kurudi nyumbani ikiendelea.

    "ni kweli, na kama uko vizuri, kwanini usioe... Kupata na kukosa ajuaye mungu.. Usiwaze kua, ukiwa na mke afu ukakosa itakuaje"

    Aliongea sheby

    "enheeee.... Sasa kwa wewe ambaye tayari umesha oa... Hebu niambie, siku umekosa, je inakuaje hapo ndani kwenu"

    Aliongea bakari kana kwamba hicho ndicho anacho ogopa sana... Na yote hio ni kwasababu wanawake wengi wanajua raha tu, shida hawazijui, na ndio mana wanaume tunatatazika sana katika swala zima la kuoa..

    "Kiukweli nisikudanganye bwana bakari... Mimi nimeoa juzi juzi tu.. Nina wiki ya pili sasa, na Namshukuru Mwenyezi Mungu, kwani hakunikosesha riziki toka nimeoa.. Ila kabla hamjaoana, ni vyema kuambiana ukweli wa maisha yenu.. Mwambie kabisa bwana kazi yangu ni hii na hii.... Ila sio lazima ajue kipato, labda uamue ajue... Kwahio cha kufanya, hakikisha unampa ukweli wa maisha yako, ajue kazi ya mume wake ina kukosa na kupata, na siku mume kakosa basi walale... Unajua bwana bakari, wanaume wengi tunakosea sehemu moja tu katika kuoa.... "

    Aliongea Swalehe,.. Bakari hapo alikua makini sana kujua kosa lilipo...

    "tunakosea wapi sasa"

    Aliuliza bakari... Wakati huo safari inazidi kwenda

    "unajua, swala la kutafuta mke ni tofauti na kutafuta kahaba... Jinsi tunavyo tafuta kahaba wa kutumia kwa muda, ndivyo jinsi tunavyotafuta mke wa kudumu... Niulize kwanini"

    "haya nakuuliza kwanini"

    "ok safi sana... Wanaume hua tuna tabia ya kujikweza mbele za wanawake,.. Unakuta kwa mfano kazi zetu hizi za ujenzi.. Wapo wanawake ukiwatajia kazi hii hawakuelewi,. Sasa tunajikuta tunataja kazi ambazo sio zakwetu, unajikweza kutaja kazi ambayo inaingiza kipato kikubwa kwa siku,... Hio yote ni ili mwanamke akuelewe na uwe nae... Sasa jua kua anapokukubalia mwanamke huyo,.. Kakubali kwakua unaingiza kipato kikubwa kwa siku, hivyo hakuna siku atashinda au kulala njaa mana mume ana kazi nzuri,.. Sasa umeshaweka mtu ndani, mara kazi zikaanza kuyumba... Mwanamke hatakuelewa hata kidogo, mana anajua kwa kipato unachoingiza kwa siku, hata kazi ikiyumba, bado hakiba ipo kubwa tu... Kwahio ukimwambia sina anakua hakuelewi, na hapo ndipo ugomvi unapoanza mara mmepigana mara mmeachana... Kosa sio lake, kosa ni lako wewe mwanaume, mana ulijikweza mbele yake... Na ikumbukwe kua, siku zote mwanamke hukarili maisha, hivyo mkarilishe maisha yako halisi,.. Mwanamke hua haelewi bali anakarili... Sasa ole wako umkarilishe maisha yasiyo yakwako"



    Aliongea Swalehe huku bakari akibaki kimya na kujikuta ni kweli wanaume wengi tunapenda kujikweza mbele za wanawake, kana kwamba nawewe uonekane umo kwenye waliomo... Usiige maisha ya mtu, fuata yakwako...



    "aaahhhh kweli Swalehe leo umenifungua masikio yangu... Ni kweli na sio mara moja hata mimi nimejikweza sana kwa wanawake... Kumbe nilikua nakosea sana"

    Aliongea bakari huku Swalehe akijibu

    "unakosea sana bakari... Tujikweze kwa wanawake wa muda ila sio mwanamke wa kudumu"



    "nimejifunza kitu.. Na inaonekana hata wewe yalikukuta"

    "ndio... Yaani ile kumtajia tu kazi yangu... Daaahhh niliangaliwa juu mpaka chini.. Kisha akatema mate... Kana kwamba kazi yangu imemtia kichefuchefu"

    "Duuuuuuu, kweli kazi ipo kutafuta mke"

    Aliongea bakari, na hapo walifika eneo la njia ya panda katika kuachana...

    "sasa swai, lini nitamuona shemeji... Tusije kupigana vikumbo mjini huko"

    Aliongea bakari, ili kumjua mke wa sheby

    "aaahhhh, kesho kwakua ni Jumapili.. Utakuja kumuona usijali"

    "nitafrai sana rafiki yangu"

    "basi poa, kama vipi kesho"

    "poa"

    Basi waliagana kisha haooo kila mmoja na njia yake.. Ikiwa ni mida ya saa kumi, mana hakukua na kazi siku mbili hizo...



    Lakini wakati Swalehe anatembea peke yake kwenda kwake, alihisi kuna mtu anamfuatilia kwa nyuma....

    Lakini kila akigeuka haoni mtu, na hapo alipo na kwake hakuna umbali sana ni kama kilomita moja hivi.. Sasa Swalehe akajifanya kasahau kua kuna mtu nyuma, ikafikia mahala, akaguka kwa haraka... Aliona ni mwanamke, na hakua mwingine bali alikua ni Zahra.... Zahra baada ya kuonekana, ilibidi ajitokeze tu... Wakati huo kashikilia fuko la nguo.. Swalehe alipata wasiwasi kua labda Zahra kafukuzwa kwao..

    "ni wewe tena?, ivi Zahra?? Kwanini hutupi uhuru wa ndoa yetu,.. Kwahio unataka tuhame na hapa tulipohamia juzi tu"

    Aliongea swai huku Zahra akiwa kimya, tena kavalia vizuri sana, kana kwamba karudia hali yake ya zamani.... Zahra hakutaka kumjibu, badala yake alishuka chini mwenyewe kwa kupiga magoti.. Swai haamini leo Zahra ndio anapiga goti

    "swai... Najua Mwenyezi Mungu hawezi kunisamehe kama wewe na mkeo hamjanisamehe... Naanza nawewe.. Naomba unisamehe kwa yote niliokufanyia.. Yote ilikua ni mapenzi yangu kwako... Ila kwa sasa nimetua mzigo huo mana tayari wewe ni mume wa mtu... Sasa sitakusumbua tena, na naomba unisamehe kwa kila jambo"



    Aliongea Zahra, swai haamini macho yake, basi swai kwa haraka alimuamsha zaru juu, kisha akamwambia

    "nimeshakusamehe, na pia nakuombea kwa Mwenyezi Mungu, akujaalie mume bora katika maisha yako... Na pia umefanya jambo la maana sana kama umebadilika"

    Aliongea swai huku zaru akijibu

    "ndio, nimeirudia hali yangu ya zamani, kwakua sikuzaliwa na tabia hii, kwahio, nimesha acha... Hata sasa hapa nimeshika nguo zangu ambazo nilizikunja, sasa nimetoka kuzifanya kua ndefu"

    Aliongea Zahra, na hata swai alifurahi sana kuskia hivyo...

    "nimefurahi sana kwa hilo, na nimesha kusamehe... Ila pia nitakuombea msamaha kwa Farida, hilo ondoa shaka"

    Aliongea swai lakini Zahra alikataa

    "hapana, sitaki uniombee msamaha"

    "kwanini? Ina maana unataka ugombane na mke wangu"

    "hapana swai... Sina maana hio,.. Bali nataka nikamwombe msamaha mwenyewe... Naomba unipe nafasi hio"

    Aliongea Zahra, huku swai akiwaza vile jinsi Farida anavyomchukia Zahra,.. Sijui itakuaje...

    "hapana Zahra,.. Sitaki ujue nyumbani kwangu, mana sitaki ugomvi wenu"

    Aliongea swai

    "swai... Nipo chini ya miguu yako... Mkeo namheshimu mno, sitakaa kugombana nae.. Nimesha badirika sana swai"

    Aliongea Zahra huku swai akiamua moja tu...

    "sawa twende"

    Swai alikubali kumpeleka zaru kwa mkewe



    Walifika mahali, nyumba ipo mbele yao... Swai hakutaka kwenda nae,.. Alimpa nafasi yeye kama yeye..

    "mlango ule pale ule... Ndipo alipo Farida, nenda mwenyewe"

    Aliongea swai huku Zahra akitamani kwenda na swai

    "kwanini tusiende wote swai"

    "hapana... Nenda mwenyewe"

    Aliongea swai kisha akawa kama anarudi nyuma hivi, kana kwamba anawapa nafasi waombane msamaha wenyewe na asihusike na lolote kati yao, mana hata kugombana waligombana wenyewe bila ya swai kuwepo, hivyo wakapatane wenyewe pia bila ya swai kuwepo....



    Basi Zahra alifika katika mlango huo, na hapo ndipo wanapo ishi Swalehe na mke wake.. Zahra alikua akisita kugonga mlango,.. Lakini akapiga moyo konde,.. Aligonga

    "ngo.. Ngo.... Ngo.... Ngo... Ngo.. "

    Farida alikua akiandaa mboga za jioni,.. Alifurahi sana kuskia mlango umegongwa, kwani alijua ni mume wake anarudi kazini, na hua kazoea kumchezea kwa kugonga mlango...

    "karibu mume wan....."











    Wakati huo swai yeye kaelekea zake mtaani, mana ni jirani na nyumbani hivyo hana wasiwasi na hilo, na pia hakuwafuatilia akina Zahra na mkewe, kama wanapigana wapigane yeye akiwa hayupo,...



    Zahra alipiga moyo konde kwani alikua akisita kubisha hodi, mana anajua ni kama atamkwaza, kuna wakati alitaka kurudi ili tu asije kukwaza Farida, lakini akaona bado atakua hajasamehewa na watu hao japo mmoja keshamsamehe, bado mmoja ambae ndio mlangwa haswa aliokua akiteseka kwa ajili yake,...

    Zahra aligonga mlango,.. Wakati huo Farida alikua akiandaa mboga zake za jioni,.. Hivyo kusikia mlango unagongwa, alifurahi sana, kwani alijua ni michezo ya mume wake, kugonga mlango....

    "ngo.. Ngo.... Ngo.... Ngo... Ngo.. "



    Farida kwa furaha aliamka na kwenda kufungua mlango...

    "karibu mume wang.... Ni wewe tena?... Umejuaje nyumbani kwangu Zahra??.. Mimi sitaki ugomvi nawewe, nakuomba sana, tumehama pale kwa ajili yenu, leo tena umekuja hapa... Kwahio unataka tuhame na hapa"

    Aliongea Farida tena huku akitamani hata kulia, mana Zahra ndio adui wa ndoa yake, hivyo haoni shida kumchukia... Zahra hakuweza kumjibu, alifanya kama vile alivyofanya kwa Swalehe... Alipiga magoti kumwomba Farida msamaha.... Farida haamini leo Zahra kawa mpole juu yake, wakati ndie aliekua akimdharau kupita kiasi...

    "Farida, kwa sasa sina tabia ulio ijua awali, unavyo niona ndivyo nilivyo kwasasa... Nimejifunza mengi kupitia wewe... Nina hamu ya kuolewa lakini imeshindikana... Farida, naomba unisamehe kwa yote niliokufanyia, ilikua ni akili ya mapenzi ya kitoto tu,.. Najua nilikuumiza sana katika moyo wako.. Naomba unisamehe sana Farida, kuanzia leo mimi ni kama dada yako, nitamheshim mume wako na hata wewe pia.. Nisamehe Farida"

    Aliongea Zahra huku akiwa kapiga magoti bado,... Farida alilia sana,.. Na kulia huko ni kwa furaha, kwani anapenda sana kuona mtu akibadirika na kua mtu mzuri

    Haraka haraka alimnyanyua na kumkaribisha ndani... Zahra haamini kama Farida kamsamehe, mana alijua Farida hatakaa kumsamehe kamwe..

    "wewe nu mwanamke mwenzangu,... Nimefurahi sana kuona umebadirika kiasi hiki... Kama upo hivi basi kuanzia leo, nimekusamehe Zahra"

    Aliongea Farida huku Zahra akifurahi kwa kusamehewa na farida... Kweli alimkosea sana, alimzalilisha sana.. Lakini karudisha moyo nyuma na kumsamehe...

    "kwa hali hii, nakuapia hutakaa utapata mume bora"

    Aliongea farida huku Zahra akishukuru kwa maneno hayo....

    "Ahsante sana wifi yangu.. Nakupenda bure, kumbe ushamba wako ni dili kwa waume zetu.. Nilikua sijui"

    Aliongea Zahra, na hapo sasa ilikua ni stori za kucheka mana tayari wameshakua marafiki, au mawifi..

    "ahahahahaha, Usijali Zahra, tupo pamoja... Haya niambie umepajuaje hapa"

    Aliongea farida huku Zahra akijubu bila kigugumizi...

    "Shem ndio kanionyesha.... Unajua, nilikua natoka kwa fundi, kuongeza nguo zangu zilizokua fupi... Nikaona mtu kama shemeji Swalehe akiwa na rafiki yake.. Nikaona niwafuate nyuma ili nijue kwenu, nije kuwaomba msamaha... Na kweli mpaka rafiki yake akaenda kule na shem akawa anakuja huku.. Ndipo akaniona... Nimemuomba msamaha nae kanielewa, nio akanionyesha kua mnaishi hapa.. Ila baada ya kunionyesha, yeye akaondoka zake... Samahani kama nimekuuzi kukutana na shemeji"

    Aliongea Zahra huku akiwa kavalia vizuri mavazi ya heshima mpaka raha yani daahh...

    "wala Usijali, mimi sina wivu kiasi hicho.. Japo nikiona ntaua mtu atari"

    Aliongea farida kwa utani utani fulani hivi..



    BAADA YA MASAA KADHAA KUPITA



    Swalehe akiwa ndio anafika nyumbani, lakini wakati huo Zahra alisha ondoka zake,..

    "heeee karibu mume wangu,."

    "Ahsante, hali yako vp hapa"

    "safi tu,.. Maji tayari kaoge uje upate chai"

    "eti eeh"

    "ndio"

    Basi ilikua ni ndoa iliojaa furaha sana katika maisha yao....



    Ikiwa ni mida ya saa mbili, tukija huku kwa akina Zahra,.... Zahra akiwa na furaha sana kwani wale watu aliowakwaza wamemsamehe wote...

    "leo mbona kama una furaha hivyo"

    Dada yake alimuuliza, na wakati huo Zahra alikua akisonga ugali...

    "dada we acha tu, nina furaha sana"

    "kwanini? Au ushapata shemeji mpya nini"

    "hapana dada,.. Kwasasa nataka nitulie kwanza kwenye swala la mapenzi"

    Aliongea Zahra kua kwa sasa acha atulie kwanza katika swala la mahusiano

    "sasa furaha hio ni ya nini"

    "nafurahia kwakua nimepajua wanapo ishi Swalehe na mkewe"

    Aliongea Zahra, lakini fatuma alikasirika sana kuskia hivyo...

    "hivi una akili wewe..."

    "kwanini dada"

    "unataka ukavunje ndoa ya watu... Acha ujinga wako"

    Aliongea fatuma au dada yake

    "hapana dada... Nina furaha kwakua nimewaomba msamaha wote wamenisamehe"

    Aliongea Zahra na hapo ndio dada yake akafurahi kuskia hivyo

    "aaaahhh ungesema hivyo sasa"

    "yaani dada,.. Wanaishi kwa furaha sana, mpaka natamani kuolewa... Kwanza dada nikianza kua na mahusiano, staki mwenye pesa.. Mi nataka mwanaume tuanze maisha yetu,... Tuwe matajiri nikiwa nae"

    Aliongea Zahra huku dada yake akiguna

    "mmmhhhh wewe uyo"

    "dada? Ina maana mpaka sasa hujaamini kua nimebadirika"

    "naamini hilo, ila kutopenda pesa, sijui kwakweli"

    "Kiukweli dada hutaamini kwa hilo, ila huo ndio ukweli wangu"



    KESHO YAKE, BAADA YA SIKU HIO KUPITA



    Swalehe akiwa zake barabarani kuelekea kwa rafiki yake bakari, mana siku hio ilikua ni siku ya Jumapili, hivyo ni siku ya kutembeleana... Sasa Swalehe akiwa njiani ghafla aliitwa

    "swaiiiiii..."

    Aligeuka nyuma, kuangalia alikua ni mama Mwajuma... Swai haamini kua kakutana na balaa la mama huyo... Sasa swai alitaka kuendelea na safari kana kwamba hakutaka mazoea naye..

    "we swai we nisubiri"

    Wakati huo mama Mwajuma ana rafiki yake, na kwa muonekano walikua wanakwenda harusini,.. Mana hata mtaa aliohamia swai.. Sio kua ni mbali sana, ni kama mtaa wa tatu kutoka mtaa waliokua wakiishi,.. Katoka mnara wa voda, kaenda kuishi sombetini, hivyo ni kama mtaa wa tatu hivi kutoka walipokuwa wakiishi...

    "skuizi umepata kuma ndogo,.. Langu bakuli unalikimbia... Ila jua mtu mzima dawa swai... Hata kama hutaki bakuli langu, basi nisalimie tu inatosha"

    Aliongea mama Mwajuma tena bila aibu kua ana mwanamke mwenzie...

    "shikamoni mama zangu"

    Alisalimia Swalehe, lakini mama Mwajuma akajibu kuwa...

    "akuuu, labda huyu ndio mama ako"

    Aliongea mama Mwajuma,... Sasa na huyu mama mwingine akajibu kua

    "aaahh we koma,.. Sina mtoto mkubwa kama huyu,.. Tena nakushangaa unalalamika.. Ina maana hujui kukaba mpaka penati wewe"

    Aliongea mama huyo mwingine... Swalehe alichoka... Mana alijua mama huyo atakua na busara kidogo, kumbe ndio walewale...

    "eeeeee mama suzy.. Penati haikabwi jamani na ndio mana nimetulia baada ya yeye kuoa... Mana penati anaachiwa mlengwa peke yake.. Wao wawili tu.."

    "ila kama ni mimi mama mwaju... Huyu mtoto sio wa kumuacha"

    Aliongea mama suzy... Sasa Swalehe akaona bora aondoke zake mana hakukua na la maana...

    "naomba niende jamani"

    Aliongea swai kisha huyoooo

    "we mama mwaju... Kijana mzuri hivi, unamuachaje kwa mfano"

    Aliongea mama suzy.. Kumbe nae mama suzy ni mijimama ya mjini vilevile....

    "hapana, watoto watamu kama hawa hawahitaji haraka... Najua sasa hivi ana hamu na mke wake... Ila nampa miezi mitatu tu... Atamchoka tu"

    Aliongea mama mwaju huku mama suzy akisema

    "au kama huezi niambie...."

    "weeeee,mi Nasubiri yule mtoto wa kike apate mimba... Swai atakuja tu hapa..."

    "ni kabila gani huyu kijana"

    "msambaa huyo"

    Aliongea mama mwaju tena kwa nyodo...

    "kama ni msambaa, basi ni haki yake... Mana hata mimi nilikua nae mmoja.. Weeee, mtoto anato***mba huyo... Yaani tena ndio kanifilisi yule mtoto.."

    "sasa huyo ni cha mtoto.... Huyu ni balaaa"

    "mmmhhhh ila mama mwaju,... Hii tabia tutaiacha lini? Mana umri unakwenda eti"

    "aku mwenzangu... Acha nitomb****we kamwisho mwisho, kama ni dhambi ninazo nyingi tu, hata nikitubu sjui kama zitaisha... Acha watoto wadogo waje kwangu"



    Tukija huku kwa bakari akiwa na Swalehe, kwani alisha fika kwa rafiki yake...

    "Afadhali umekuja, mana najua wewe ndio mshauri wangu"

    Aliongea bakari huku akiweka chai ili wapate kunywa,...

    "mbona chumba chako kimesha kamilika.. Bado mke tu hapa"

    "ni kweli kaka... Ila kumpata huyo mke ni mtihani shekhe"

    "ni kweli kabisa, ila usiwe na haraka na hili"

    "wala sina haraka japo nataka"

    Basi walifurahi huku wakipata chai,.. Masaa yalisonga,.. Kisha waliondoka wote, ili na bakari nae akapajue kwa rafiki yake.... Mana karibuni marafiki zake wote wanajua alipo hamia Swalehe, na hata kaka yake anajua, mana ndio alimsaidia kuhama



    "karibuni hapa ndio nyumbani"

    Aliongea Swalehe, lakini walikuta ugeni humo ndani...

    "aaahh shem karibuni"

    Aliongea Zahra, kumbe Zahra ndio aliokuja, kwani kwa sasa ni marafiki wazuri

    "Ahsante shem"

    Aliongea Swalehe huku wakikaa katika kiti..

    "we mama Rashid, vp chochote huko"

    Aliongea Swalehe huku mama rashid akijibu

    "mbona tayari mume wangu.. Ni nyie tu"

    Aliongea farida, huku akiandaa chakula, na Zahra alikua akiandaa maji, yaani Zahra kawa mwema moja kwa moja, utafikiri wana undugu na farida...



    Sasa bakari bado hajajua mke wa swai ni yupi, mana wote wana hekima kama mapacha....

    "Swalehe, acha nivunje ukimya... Mkeo ni yupi hapa"

    Aliongea bakari lakini wale wanawake hawakusikia swali hilo...

    "mke wangu ni yule mfupi mnene na mweusi,.. Huyu mrefu mweupe, ni ndugu yake"

    "sasa kwanini hunitambulishi mapema"

    Aliongea bakari.... Kisha swai aliwaida wote

    "mama rashid... Huyu ni rafiki yangu, anaitwa bakari, ni fundi mwenzangu"

    "ooohhh karibuni sana shemeji"

    "Ahsante sana shem, nimefurahi kukufahamu"

    "na huyu.. Ni ndugu yake... Anaitwa Zahra"

    Aliongea Swalehe huku Zahra na bakari wakipeana mikono ya kutambuana

    "nashukuru kukufahamu nami naitwa bakari"

    Aliongea bakari lakini papo hapo simu ya swai iliita... Kuangalia jina alikua ni fundi wake...

    Swalehe alitoka nje kwenda kuongea naye...

    "hallo fundi habari yako"

    "salama swai, vipi upo wapi"

    "nipo nyumbani"



    Wakati huo huku ndani, bakari na Zahra, kama vile wanaangaliana kiwizi wizi flani hivi.. Zahra alitoka nje, ghafla na bakari naye alifuata nyuma... Wakati huo Swalehe anaongea na fundi wake



    "Zahra?? Zahra??"

    Bakari aliita baada ya Zahra kutoka nje,.. Sasa farida yeye alikua chumbani, ikumbukwe kua wamepangisha daborumu

    Sasa farida kutoka haoni mtu hata mmoja

    Hakua na wasiwasi sana japo anamuona mume wake anaongea na simu ila wengine hawaonekani....

    "abeee"

    "simama basi bibie"

    Aliongea bakari kisha Zahra akasimama

    "unakwenda wapi"

    Aliuliza bakari,...

    "unajua sijapenda... Umeniangalia sana mpaka najiskia aibu.. Na haileti picha nzuri kwakua ni hapo ni kwa watu"

    "ni kweli, ila sio kwa ubaya... Katika macho yangu, nahisi kuona kitu kizuri kwako"

    "kitu gani hicho shem"

    Aliongea Zahra huku akijifunika funika.. Bakari kumbe tayari keshapenda

    "nilikua natafuta mtu wa kuishi nae katika maisha yangu,.. Sijui kama nimekupata"

    Aliongea bakari lakini Zahra kakaa kimya

    "Zahra?"

    "abeee"

    "unanifaa kua mke"

    Aliongea bakari, Zahra haamini kwa mara nyingine tena anataamkiwa kua mke... Aliwaza sana mambo ya nyuma, na kujisemea katika moyo wake kua



    "Mwenyezi Mungu, ana makusudi yake.. Huenda huyu ndio bahati yangu... Siwezi kumtupa kama nilivyo mtupa Swalehe... Mungu anisamehe, kwani naweza kumringia na nikamkosa..."



    Alijiongelea mwenyewe huku akimjibu bakari...

    "Samahani shem... Labda uende nyumbani kwanza uonane na dada etu mkubwa, akikubali nami nipo tayari"

    Aliongea Zahra, bakari haamini.. Yaani kaona tu kwa muda mchache, kataka mke

    "kuja kwenu sio tatizo... Tatizo lipo kwako, kuridhia maisha yangu... Labda nikwambie ukweli wa kazi yangu.. Na pia maisha yangu kwa ujumla"

    Aliongea bakari lakini Zahra alimkatisha na kumwambia...

    "usijali.. Najua una kazi kama shemeji Swalehe, na sijaipenda kazi yako, bali nitakupenda wewe.. Kama kweli umenipenda, basi twende nyumbani wakakujue"

    Aliongea Zahra kwani hataki tena kuwa na mahusiano yasiojulikana kwa dada yake...

    Na bakari ana haraka ya kuwa na mke.. Alijikuta anakubali.... Sasa swai anashangaa watu wanasonga mbele..

    "we bakari?? Vp mbona sielewi"

    "nakuja bwana kaka nisubiri"

    "skia basi ndugu yangu"

    Aliongea Swalehe lakini ghafla sms iliingia kwenye simu yake... Kuangalia ilikua ni namba ya Zahra, na sms ilisema hivi



    "shemeji Swalehe, naomba usimwambie tabia ulizowahi kuziona kwangu... Amenipenda, nami nimempenda... Na sasa tunakwenda kwa dada akamjue, nataka anione yeye... Tafadhali sana shemeji, nilindie heshima yangu"



    Aliandika hivyo wakati wakiwa wanakwenda,.. Basi Swalehe hakutaka tena kufuatlia... Ila alibaki kucheka tu

    "heeeee wale nao vipi"

    Aliuliza farida baada ya kuona watu wameshikana mikono kuelekea huko

    "washapendana wale"

    "mmhhhh kwani walikua wakijuana kabla ya hapa"

    "hapana, ila bakari anataka mke.. Nadhani hata Zahra vivyohivyo"

    "lakini mbona mapema mno"

    Aliongea farida kisha swai akamjibu

    "kwani mimi nawewe tuna muda gani?? Mbona nimekuoa??... Sheria za dini yetu ya Kiislamu zinasema kuwa... ALIEKUFA NA AZIKWE HARAKA KWAKUA HANA HAKI NA DUNIA TENA.... LAKINI PIA KWENYE NDOA DINI INASISITIZA KUA.. MWENYE KUOLEWA AU KUOA NA AOLEWE AU AOE HARAKA SANA KABLA MMOJA WAO KUBADILI MAWAZO... Hivyo tuyaache yale hayatuhusu sana.. Kama wamependana, acha wakatambulishane..."

    Aliongea Swalehe huku wakiingia ndani na mke wake....



    BAADA YA MASAA KADHAA KUPITA



    Ikiwa ni mida ya jioni hivi... Swalehe akiwa na mkewe, walishangaa ugeni,.. Walikua ni akina bakari wanarudi....

    Zahra alikua na furaha sana, kwani alimrukia farida kwa furaha sana...

    "Zahra una nini wewe"

    "dada katupa baraka zote juu yetu"

    "ina maana umekubaliwa kuoana"

    "yes... Na sasa bakari ni mchumba wangu"

    Aliongea Zahra... Na wakat huo Swalehe na bakari wapo nje....



    "ila bwana kaka una zambi sana wewe"

    Aliongea bakari huku Swalehe akishangaa

    "kwanini sasa, na zambi zangu zinakujaje apo"

    "yaani mi natafuta mke, kumbe shemeji yako yupo huniambii"

    "aaaaaaaaaaaa, sasa mi najuaje kama mtapendana... Tuachane na hayo.. Kesho tuna safari ya kwenda Mwanza, kuna jengo la kwenda kujenga, litachukua miezi miwili"

    Aliongea Swalehe, kwani alipewa taarifa na fundi wake,...

    "aaahhhh.... Sasa mi nitaoa lini aiseee"

    "acha haraka... Fanya kazi Kwanza"





    BAADA YA MIEZI MITATU KUPITA



    Ikiwa leo ni siku ya furaha kwa watu wawili baina ya bakari na Zahra... Lakini mbaya zaidi Zahra alikua akilia sana,.. Wakati huo kafunikwa mtandio maalumu wakati wa kufungishwa ndoa yao... Bakari alipata hofu sana baada ya kuona Zahra analia bila sababu.. Hofu ilimjaa bakari...



    Baada ya ndoa kupita wakiwa wapo nyumbani kwa Swalehe, mana pale kwa Swalehe pana kisehemu kikubwa kubwa kidogo,...

    "farida, hebu kamuulize mwenzio alikua analia nini wakati wa ndoa, mana bakari mpaka sasa ana hofu juu ya hilo"

    Aliongea Swalehe huku farida akitekeleza alicho agizwa na mumewe....

    "unaionaje siku ya leo"

    Aliongea farida kumuuliza Zahra...

    "Kiukweli nina furaha sana... Nalia hivi sio kua sijapenda... Yaani siamini kua nami nimekua mke wa mtu... Siamini kama nimeolewa,.. Nilihisi mume wangu bakari ananidanganya kunioa... Kumbe kweli... Farida??? Nampenda bakari..."

    Aliongea Zahra, na wakati huo bakari yupo na Swalehe nje wakijadili mambo ya kazi,, yaani Swalehe muda wote ni mtu wa kazi, wakati mwenzie anawaza mke waondoke zao....

    "sasa, kwakua tumerudi Mwanza juzi tu... Sasa tusubiri kazi zingine"

    Aliongea Swalehe lakini bakari kama haelewi...

    "aisee mambo ya kazi tutaongea kesho.. Ita tax tuondoke zetu"

    "ahahahahahahahahahahahahahhaha... Aisee una haraka wewe"

    Aliongea Swalehe huku bakari akiingia ndani,.. Alikua anapenda kumuona mkewe kila wakati...

    "mume wangu.. Twende kwetu basi"

    Aliongea Zahra huku akimkumbatia mumewe... Wakati huo tax inaitwa...

    Swalehe alikuja ndani kumchukua bakari,

    "njoo nje... Achana nao wakae ndani hao"



    Wakati huo huku ndani.... Farida alikua akimpa maneno rafiki yake...

    "Zahra, kwa kawaida huwa kuolewa sio kazi.. Kazi ni kuilinda ndoa yako... Usifuate maneno ya watu,... Kwahio usione ajabu kuolewa, ila jitahidi kuiheshim ndoa yako... Usimjibu mumeo vibaya, mtengee maji pale anaporudi kazini... Mpe vile vitu anavyopenda... Mimi sina cha kukuambia, mana wewe mwenzangu ulikua na kungwi, hivyo najua kakupa somo vizuri... Ila nakuomba sana, mpende mumeo mheshim mumeo... Hapo utaiona raha ya ndoa yako..."

    Aliongea farida huku Zahra akitoa machozi kwa kua.. Kumbe alikua akimkosea sana farida kipindi kile.. Kumbe alikua anamkosea mtu ambae ni nuru katika maisha yake...

    "pia.. Mumeo akipata Shukuru, akikosa muombe mungu kesho apate... Na hata akikosa tena, usikasirike... Zidisha kumuombea mumeo,... Achana na utajiri wa majirani au watu wengine, huo hauwahusu... Mpende mumeo, ipende ndoa yako"



    "PIIIIII... PIIIIIII. PPPPIIIIIIIII"

    Ni sauti ya honi ya gari ikilindima huko nje, bakari aliingia ndani fasta na kumchukua mkewe, waliingia ndani ya gari wote ili kumsindikiza mwenzao mpaka kwake.. Ilikuwa ni furaha kubwa kwa Zahra na bakari....





    MWISHO WA STORI HII YA WAPANGAJI WENZANGU....



    MWISHO

0 comments:

Post a Comment

Blog