Search This Blog

Thursday 24 November 2022

WAPANGAJI WENZANGU - 1

 

     

     



     IMEANDIKWA NA : MOONBOY



    *********************************************************************************

    Chombezo : Wapangaji Wenzangu

    Sehemu Ya Kwanza (1)

     

    FUNDI UJENZI



    Simulizi yetu inaanzia katika jengo moja ambalo lilikuwa likijengwa,.. (SITE) palikuwa na wafanyakazi wengi sana hususan mafundi na wasaidizi pamoja na wakandarasi wenyewe,... Ikiwa ni siku ya Jumamosi nyakati za jioni,.. Ni ile siku ya malipo kwa wajenzi,... Walikuwapo wafanyakazi wengi sana tena wa jinsia tofauti, hata wanawake nao walikuwa wakionekana katika kazi hizo kwani hali ni ngumu hata wanawake wanapiga zege kama wanaume, mana hawapati wanaume wa kuwaletea nyumbani hivyo wameona ni bora kuzifuata huko huko zinako toka...



    Madaftari ya kusaini pesa yako mawili, yaani daftari la mafundi na daftari la wasaidizi,... Mafundi walilipwa elfu ishirini na tano kwa siku, hivyo kwa wiki anatakiwa kusaini shilingi laki moja na hamsini (150,000), kwa wiki.... Lakini pia kuna wasaidizi wao,.. Wao daftari lao husaini shilingi elfu kumi tu kwa siku, hivyo kwa wiki atatakiwa kusaini shilingi elfu sitini (60,000) kwa wiki hivyo sio pesa mbaya sana hata kama una familia maisha yanakwenda







    Baada ya malipo kila mmoja alisambaratika na kwenda makwao, lakini kuna fundi mmoja aliokwenda kwa jina la HASSAN, ana vijana wake wasiopungua wanne,.. SWALEHE, JEREMIAH, ABEDI, MAHMUD, hawa vijana wote wanaishi chumba kimoja pamoja na huyu fundi,... Kwahio chumba kimoja wanalala watu watano,.. Maisha ya mjini ya kutafuta pesa, usione ajabu hata watu kumi kulala chumba kimoja,... Kila mmoja anajipanga kivyake...



    Lakini watu hawa watano wakiwa na fundi wao na pia ni kaka yao ambae amewapokea na kuwahifadhi, japo kila mmoja kaja kivyake au kakutana na Hasan kivyake na kamlalamikia kivyake,.. Hasan mpaka sasa hana mke, na yote hio huenda ni kwasababu anaishi na vijana wengi sana katika chumba kimoja...



    "sasa madogo?, wacheni nikashtue kidogo"

    Aliongea fundi Hasan, huku na wale wakushtua kama yeye wakimuunga mkono,..

    "aisee hata mimi nina hamu na demu, daahh wacha niende bondeni"

    Alionge jelemia huku Abedi na fundi hasan wakielekea baa kutoa loku (kunywa pombe).. Lakini wapo vijana wawili wao hawakuwa watu wa starehe kama walivyo wenzao ambao kila mmoja kataamka starehe yake

    "asee swai, kama kawa basi nenda na zana zetu"

    Aliongea hasan huku wakimkabidhi swalehe na Mahmud zana ambazo wametoka nazo kazini, mana wao hawafiki nyumbani kwa wakati huo, kwakua swalehe na Mahmud wao hawana starehe yeyote ile, walichukua zana za wenzao na kuondoka kurudi nyumbani....

    "aisee tukute vyombo vimeoshwa ee"

    Aliongea abedi huku swalehe akiitikia

    "sawa ndugu"

    "ah ah, nawe unaitikia tu, kwani we ni mke wao"

    Alionge Mahmud au mudi, huku swalehe au swai akijibu

    "sasa tutafanya nini... Tupo kwenye geto la watu, hivyo lazima tuende sawa"

    Aliongea swalehe huku Mudi akimuuliza

    "wewe una muda gani hapa mjini"

    "miaka kumi"

    "sasa miaka yote hio hujajipanga tu"

    Aliongea mudi huku swai akijibu

    "sio miaka yote nilikuwa na kazi... Nina miaka mitatu kwenye kazi hii na bado sijawa fundi"

    Aliongea swai huku wakirudi nyumbani na hapo kila mmoja kabeba begi la mwenzake ambae kaenda baa,

    "lakini hasan si ndugu yako kabisa wewe"

    "ndio,... Baba mmoja mama mbalimbali"

    Alijibu swalehe huku mudi akizidi kumuuliza

    "kwahio miaka yote kumi unaishi nae tu"

    "kama kawaida"

    "duuuuuuu, una moyo... Kuishi miaka kumi geto afu mpaka sasa huna kitu"

    "skia mudi... Mimi nilikuwa sina kazi... Miaka mitatu iliopita ndio broo akaniambia, twende ukawe saidia fundi, na mpaka sasa hata ufundi naweza"

    Aliongea swalehe ambae ni ndugu yake na hasan, kwahio swalehe na hasan ni ndugu, lakini Abedi, mudi, na jelemia wao wamepewa hifadhi tu kama walivyo omba wahifadhiwe mpaka watakapo pata pesa ya kujipangishia vyumba vyao

    "sasa kwanini usiwe fundi"

    "namwambiaga ujue... Lakini yeye ananitishia eti ooohh ufundi sio ishu ya mchezo... Utakuja kutia hasara ujenge nyumba mara ibomoke, sjui nitafungwa... Mambo mengi ndio mana nimetulia tu"

    "ah ayo matisho tu"

    "ni sawa lakini ni mkubwa wangu ujue"

    "kwahio unaogopa ile ASIESIKIA LA MKUU HUVUNJIKA GUU"

    "haswaaaaaaaa"

    "hahahahahahahahahha.... Ila swai tuongee na kurudi nyuma... Muda ulio ishi kwa kaka yako.. Ni mkubwa sana,... Fanya hima uachane nae"

    Aliongea mudi kama kumshauri swalehe

    "wazo lako mudi, ni zuri sana... Lakini umechelewa"

    Aliongea swai huku akicheka kwa kujinadi

    "kwanini nimechelewa"

    "huuu ni mwezi wa ngapi huu"

    "wa kwanza"

    "sasa wa pili mwishoni nahama kwa broo..."

    Aliongea swalehe huku mudi akiwa haamini

    "acha utani wako"

    "aaaaaaaaaa.... Na pia nina maana ya kusema mwezi wa pili... Kwasababu nilikuja Arusha rasmi tarehe 28 mwezi wa pili, sasa nataka niondoke tarehe hio hio mwezi wa pili.. Kwahio mwaka huu mwezi wa pili ndio natimiza miaka kumi kukaa kwa broo... Ila mwezi wa pili sipo"

    "duuuuu umejikomboa wewe... Sisi bado tutabanana na broo wetu"

    Aliongea mudi huku swalehe akimwambia

    "lakini hata wewe una uwezo wa kujipanga ujue"

    "ni kweli, na sio mimi tu.. Hata akina abedi na jelemia wote tuna uwezo ila tumeamua kuvuta nguvu kiasi"

    Aliongea mudu huku akikumbuka starehe yake....

    "ayaaaani, afu nilikuwa napapita eti... Swai una stori za ajabu mpaka napita chakula ya baba"

    Aliongea mudi huku akirudi nyuma, kununua starehe yake,... Kumbe mudi yeye ni mzee wa bangi... Hapa bado swalehe ndio hatujajua starehe yake

    "nishkie begi"

    "nani ashike... Twende uko uko"

    Alionge swai huku akienda nae kwa pusha kununua bangi,... Kama kawaida kwa pusha hua kuna masela wengi sana kwasababu ndio chakula cha baba kilipo

    "aaahhh swai... Mambo vp bwana"

    "poa nambie"

    "guda... Naona chalii yako kaja kuchukua chakula cha baba"

    "eeehh kama kawaida yake mwenyewe"

    Aliongea swai huku akiwa na masela nao wavuta bangi, lakini swalehe yeye havuti chochote kile... Ila anaishi na masela wavuta bangi na wanywa pombe lakini hakuwahi kushawishika kutumia kilevi chochote kile... Na anaishi nao nyumba moja...



    Basi mudi alinunua stiki zake kadhaa, kisha wakawa wanarudi geto,.. Geto hapakuwa mbali sana, walifika wakiwa wamechoka mno,...

    "huu umeme ndio umekata au luku"

    Aliongea swalehe huku akiwasha washa taa,..

    "itakuwa luku hii... Na kama ni luku, hapa ipo kazi ya kukamatana na wapangaji, mana mpaka watoe,... duuu"

    Aliongea mudi huku akitandika kitanda mana asubuhi kila mtu anakurupuka na njia yake, japo kazi yao ni moja laki hakuna anaekumbuka kutandika asubuhi, na hapo ndani kuna vitanda viwiliwili, uzuri chumba wanacho ishi ni kikubwa na kimeenea vitanda viwili vya nne kwa sita...

    "aisee kama umeme umekata wataniua sasa"

    Aliongea swalehe huku mudi akicheka

    "ehehehehehehe najua wataka kuchati.... Na huo ndio ugonjwa wako swai... Yaani ukishika huo mtachi wako hutoki"

    "mbona we ukivuta bangi lako unalegeza macho"

    "basi yaishe... Sasa kabla hujashika hio simu yako... Kwanza tufanye mchakato wa kula... Mi naosha vyombo, we anza kuchambua dagaa"

    Aliongea mudi kama kupeana kazi

    "anza sasa... Mimi nikimaliza nabadika safuria"

    Aliongea swai huku kila mmoja akishika nafasi yake ya kazi mana wao wawili tu ndio wamerudi nyumbani, wengine wameenda kulewa

    "tupikie makamanda"

    "kawaida tu"



    Kesho yake ikiwa ni siku ya Jumapili, mida ya saa mbili asubuhi lakini masela walikuwa bado wamelala mana hakuna pa kwenda siku hio,.. Lakini swai yeye alikuwa bize na simu kana kwamba swalehe starehe yake ni kuchati tu, yaani usiombe simu ikakuingia damuni,.. Yaani kama akili huna hata kwenye kazi utakuwa mvivu, ila swai kwenye kazi anafanya kazi lakini akiwa free, humsumbui kwenda popote,.. Hata ukampe ofa ya nini.. Hataki labda simu iishe chaji na hakuna umeme...

    "oya fanyeni mpango wa chai basi"

    Aliongea hasani huku vijana wakiamka kufanya alicho kisema hasan, mana ndio mkubwa wao na ndio fundi wao na ndio geto kwake, hivyo hawana ubishi juu yake,...



     Baada ya masaa saba wakiwa wanakula chakula cha mchana ili kila mmoja asambaratike na Jumapili yake,... Lakini hasani leo kuna jambo alitaka kuwaeleza vijana wote ambao anaishi nao

    "oya... Mtu wa mwisho kumpokea kwangu ana miaka miwili hapa geto... Ni kweli si kweli"

    Aliongea hasani huku wote wakisema

    "ni kweli broo"

    "sasa ni hivi... Najua baadhi yanu tumefanya starehe sana.. Ila kama hujajipanga utajua mwenyewe... Sasa hivi nataka kuoa... Kwahio nawapa wiki hiii.. Moja tu, kila mtu apangishe chumba chake"

    Aliongea hasani huku baadhi ya vijana wakishika vichwa, mana walikuwa wakila maisha tu..

    "sasa broo, mbona umetushtukiza hivi"

    Aliongea abedi huku hata kula hana hamu

    "nawapa wiki moja tu... Na ndio mana nikasema leo... Mana kama nikisema hio siku mtaniona mbaya mjue"

    Aliongea hasani huku swalehe akitabasamu tu mana wazo analotoa lipo akilini mwake... Vijana wengi walilalamika haswa wale wapenda starehe mana hawaja jiwekea hata pesa ya godoro...

    "broo... Mi naona ungetupa mwezi mmoja, kwasababu wengu wao hapa hawapo vizuri mifukoni mwao"

    Aliongea swalehe, lakini yeye aliongea kama kuwatetea wenzake, na pia yeye mwenyewe ana uwezo wa kuondoka hata siku hio, lakini kajiwekea tarehe ya kuondoka kwa kaka yake,..

    "wewe unasema wao je wewe"

    Hasan alimuuliza mdogo wake

    "broo, mimi hata kesho naweza kuondoka... Lakini nina tarehe maalumu ya kuondoka"

    "kwahio upo vizuri"

    "ndio.. Tena natoka na nguo zangu tu"

    "kitanda chako hiki"

    "atachukua mudi"

    "na wewe"

    Hasan alimshangaa sana mdogo wake mana kitanda kimoja hapo ndani ni cha swalehe, lakini hakihitaji

    "broo, nimekaa sana kwako, hivyo sitaki nipangishe chumba na vitu vya zamani... Nataka vitu vipyaaaa, tena vya maana.."

    Aliongea swalehe huku abedi akisema

    "duuuuu Afadhali wewe swai... Mana mimi hata huo mwezi mmoja haunitoshi"

    Aliongea abedi huku jelemia nae akisapoti

    "aisee ni kweli hata mimi huo mwezi haunitoshi"

    "nyoooooo.... Hapa nawapa huo mwezi tu,.. Kama mtu hawezi atajua mwenyewe, nataka kuoa bwana.. Nimesema hivi nawapata huo mwezi mmoja tu... Ukiisha huu mwezi wa pili sitaki kuona mtu..."

    Aliongea hasani kisha akanawa mikono na kuondoka zake

    "aaaaahh.... Sasa itakuwaje... Aisee swalehe, pangisha basi tuje kuishi"

    Aliongea jelemia huku swalehe akijibu

    "weeeeeee, kwanza hata mimi nikipangisha naoa... Staki kukaa na mtu sawa.. Labda mumwambie mudi"

    SWALEHE alikataa kuishi na mtu mana wao walikuwa wakifurahia maisha bila kujua kuwa kuna maisha baada ya kifukuzwa kwa mtu

    "ah ah swai... Usiwaelekeze kwangu.. Kwani mimi sitaki kuoa... Hata mimi jamani nataka kuoa... Nyie pesa zenu mnapelekea malaya na pombe, haya nendeni mkalalie huko"

    Aliongea mudi ambaye yeye starehe yake ni bangi tu basi..... Swalehe aliondoka zake na wengine kila mmoja aliondoka zake mana siku hio ni siku ya Jumapili



    BAADA YA WIKI MBILI KUPITA



    Swalehe alikutana na dalali mmoja ili ampe kazi ya kumtafutia chumba,..

    "sasa skia mzee,.. Mimi nataka chumba kizuri, kwanza kiwe na maji ndani, kiwe na umeme"

    Aliongea swai huku dalali akiwa na maneno mengi

    "aaahh hapa umefika... Yaani hapa utapata chumba cha aiana yeyote... kwanza kuna chumba kimoja hapo mtaa wa pili ebu twende"

    "wapi apo"

    "hapo mnarani"

    "aaahh mzee mimi siwezi kwenda kuishi ungalimitedi bwana.."

    "ah ah sio ungalimitedi kijana.. We twende, kwanza chumba kizuri"

    Aliongea mzee huyo huku swai akiamka na kumchukua mzee wakakione hicho chumba, wakati huo swai kavalia nguo zake za kazi,..



    "geti hili hapa... Umeona kwanza geti lenyewe kali,... Haya twende ndani"

    Aliongea dalali huyo huku wakiingia ndani,... Kwanza kufika tu wakaona wamama wamekaa vibarazani mwao,

    "umeona, nyumba imechangamka hii, hata mkeo hatokuwa na tabu"

    Aliongea mzee huyo ambaye ni dalali

    "nionyeshe chumba mzee, acha maneno"

    "sasa chaguo ni lako... Unataka dabo rumu au singo rumu"

    Aliongea dalali mana hapo kwenye hilo boma kuna pande mbili, kuna upande wa dabo rumu na upande wa singo rumu... Na inaonekana watu wamehama muda sio mrefu...

    "hawa wamehama kwasababu gani"

    Aliuliza swai huku mzee akijibu

    "mimi sijui.. Ila angalia chumba saafi,.. Maji yale pale... Umeme huoooo"

    "mmmhhh kuna wamama humu duuuuu"

    "ukiona nyumba ina wanawake wengi, ujue ina amani hio"

    "mmmmhhhhh, wana vilanga hao"

    "weeeee ongea taratibu ukisikiwa.."

    Aliongea dalali huku swalehe akiuliza mama mwenye nyumba...

    "mama mwenye nyumba yupo wapi"

    "hapa tutamfuata baba mwenye nyumba ndio kila kitu..."

    "sawa yuko wapi"

    "yeye anaishi nyumba ya pili huku"

    "ok twende"

    "lakini umekipenda chumba hicho"

    "we twende kwa mwenye nyumba"

    Aliongea swalehe mana kakutana na dalali ana maneno mengi sana... Lakini sasa ile wanatoka tu.. Mara dalali kaitwa na wamama waliokuwa wamekaa vibarazani

    "we mzee jumbe njoo hapa"

    Wamama walimuita dalali huyo

    "enhee mnasemaje, kuna mtu anataka kuhama kati yenu?... Vyumba vipo ni nyie tuuuu"

    Aliongea dalali huku wapangaji wakaanza kusema

    "hatuna shida na kuhama sisi... Hivi wewe dalali, unaona hii hadhi ya hii nyumba"

    "ndio"

    "umemuona yule anaepangisha hiki chumba"

    "yule kijana au nani"

    "ndio, yule mwenye kofia kama muuza nyanya"

    "kwani kuna nini jamani"

    Wakati huo swai katulia pembeni na anasikia kwa mbaaali

    "hivi yule na kofia lile, na mandevu yale... Mchafu vile, aje apangishe humu"

    Aliongea Madada mmoja au mama fulani.. Wakati huo swai kasimama nje ya geti akimsubiri dalali aje waende kwa baba mwenye nyumba, lakini ghafla swai anashikwa bega huku akisikia

    "nyie ndio wezi ninao watafuta... Haya niambie unachungulia nini huku ndani... Umeona nini cha kuja kuiba?"

    Alikuwa ni mzee mmoja wa makamo akiwa kamshika swai,..

    "hapana mzee nimekuj"

    "tuliaaaaa... Hapa umeingia kwenye mikono ya jeshi,.. Mimi ndio mzee zubery mwanajeshi mstaafu.... Kaa chini haraka"











    Siku ya balaa ni ya balaa tu, hata iweje lazima itakuwa siku ya balaa mana imesha pangwa kuwa ndio siku yako ya balaa,... Swalehe aliokwenda kutafuta chumba ili apangishe kuondokana na adha ya maisha kwa kaka yake,... Lakini siku hio imeingia balaa...



    Wakati dalali na Swalehe wanatoka kwenda kwa baba mwenye nyumba ili kupata bei ya pango na Swalehe aweze kulipa pango hilo, mana karidhika napo,.. Lakini wakati wanatoka dalali aliitwa na wamama waliokuwa wamekaa vibarazani mwao wakiwa wanapiga umbea, kama unavyojua wamama walivyo na mambo, lakini wamama hao ni wale wale wamama wa mjini, waswahili mpaka wanakera,



    "hivi yule na kofia lile, na mandevu yale... Mchafu vile, aje apangishe humu"

    Aliongea mama huyo huku akiwa kama kashika kiuno hivi...

    "alaaaa Sasa wewe ndio mwenye nyumba au? Wacha tuone kama mwenye nyumba atasema huo ujinga"

    Aliongea dalali huku akiondoka

    "we dalali huku tunaishi watu na hadhi zetu bwana.. Tuletee watu wa maana"

    Aliongea mwanamke huyo huku nje sasa Swalehe kakalishwa chini na mwanajeshi baada ya kukutwa kasimama getini huku akiangalia ndani kama vile mtu aliokuwa akichungulia humo ndani, ndipo mzee mmoja anaesemekana ni mwanajeshi mstaafu akamkuta swai aikiwa katika pozi la kumwangalia dalali anavyo bishana na wamama kule ndani...



    "tuliaaaaa... Hapa umeingia kwenye mikono ya jeshi,.. Mimi ndio mzee zubery mwanajeshi mstaafu.... Kaa chini haraka"

    Aliongea mzee huyo wa makamo huku Swalehe akikaa chini kweli, mana kila akitaka kujitetea kuwa kaja kuangalia chumba, hapewi nafasi ya kuongea,... Lakini mzee alivyotaka tu kupiga simu mara mzee dalali katoke,

    "eh eh, ni nini tena?...... Aahh mzee zuberi habari yako mzee wangu"

    Dalali alimsalimia mzee huyo alietajwa kwa jina la zuberi

    "salama... Umeona hawa ndio wezi hawa... Nimemkuta akichungulia kwenye geti"

    Aliongea zuberi huku dalali akisema

    "ina maana na wewe kijana umeshindwa kuzungumza?"

    Dalali alimuuliza Swalehe kwanini kashindwa kuzungumza

    "hapana dalali, hakunipa nafasi ya kuongea sasa nitasema nini"

    Aliongea Swalehe huku dalali akimwambia huyo mzee zuberi kuwa

    "mzee zuberi, huu mguu ulikuwa wako... Na huyu kijana, anataka chumba hapa kwako... Na ndio tulikuwa tunatoka ili tuje nyumbani sasa nilipofika hapa mlangoni, wanamama wakaniita, hivyo huyu kijana akabakia hapa mlangoni.."

    Aliongea dalali huku mzee zuberi akisema

    "aah sasa kwanini hakusema"

    "sasa mzee wangu, saa ile nilitaka kusema ukanikatisha... Ningefanyeje"

    "haya amka bwana... Samahani sana kijana,.. Sema upole wako umekusaidia sana, mana nina hamu ya kupiga mtu mateke... Lakini kwa bahati nzuri umekuwa mpole... Haya twendeni nyumbani basi... Ila kijana Samahani sana"

    Mzee zuberi Aliongea mengi pamoja na kumwomba Swalehe msamaha

    "hakuna shida mzee wangu,... Basi nina amani kuishi katika nyumba hii mana patakuwa na ulinzi mzuri"

    Aliongea Swalehe huku wakielekea nyumbani kabisa kwa mzee zuberi, mana ni jirani na eneo hilo

    "Usijali, hapa mtaani kuna usalama wa hali ya juu"

    Aliongea mzee zuberi huku wakiingia katika mjengo wa mzee huyo ili kuanza maongezi



    "haya mzee, mimi ni kijana ambaye ninayaanza maisha,... Nimeishi kwa nsugu yangua na sasa nahitaji kupangisha ili nijitegemee"

    Aliongea Swalehe huku mzee dalali akitikisa kichwa,...

    "ni sawa kijana... Vyumba vipo, kama ulivyo ona kuna dabo na kuna singo.. Sasa sijui unataka chumba gani"

    "aaahh mzee mimi nitachukua singo"

    Aliongea Swalehe huku mzee akisema kuwa

    "ok... Sharti la Nyumba hii... Geti linafungwa saa nne usiku, linafunguliwa saa kumi na moja alfajiri.... Nyumba sio genge, sitaki wavuta bangi waingie katika nyumba yangu... Kama wewe ni mlevi, sitaki kukupangia starehe yako.. Lewa huko huko, na ukija pale ingia lala.. Kelele hazitakiwi,.... Kwanza una mke wewe"

    Mzee alitoa mashart yake ya nyumba lakini mwishoni akamalizia kumuuliza Swalehe kama ana mke

    "mzee niuseme ukweli ya kwamba... Sina mke, lakini hivi karibuni jirani kuoa"

    Aliongea Swalehe huku dalali akitikisa kichwa

    "kama huna mke ni hatari sana.. Mana pale kuna wake za watu, kuna wasichana wa kazi, kuna wasichana wengine wa familia za watu... Sasa mvulana kama wewe sijui itakuwaje"

    Aliongea mzee, lakini kabla Swalehe hajajibu, ghafla dalali akadakia

    "ni kweli mzee zuberi.. Lakini mbona pele kuna vijana wawili tena wahuni sana kuliko hata huyu,.. Lakini umewapa chumba"

    "ni kweli mzee mwenzangu... Hata huyu sio kuwa nitamkataa, ila asimalize hata mwaka awe kaoa... Mana ni hatari sana kwa wale wapangaji wenye wake zao, watakuwa na wasiwasi... Wale vijana yenyewe, wakimaliza miezi 6 yao sitaki waongeze.. Waondoke kwasababu watatuletea shida kwenye ndoa za watu"

    Aliongea mzee zuberi huku Swalehe akisema

    "ok mzee wangu... Nimesha kuelewa, sasa nipe bei ya pango"

    Aliongea Swalehe huku mzee zuberi akisema

    "kwani dalali hajakupa bei"

    "hapana mzee"

    "ok.... Kama ulivyo ona ubora wa nyumba nzima, pamoja na vyumba vyake... Singo kwa mwezi mmoja ni shilingi elfu hamsini... Dabo ni shilingi laki moja kwa mwezi, na unatakiwa kulipa miezi sita sita"

    Aliongea baba mwenye nyumba au mzee zuberi, huku Swalehe akisema

    "ni sawa mzee... Mimi nitalipa miezi kumi... Nikimaanisha kwamba nitalipa kuanzia mwezi wa tatu... Mpaka mwezi wa kumi na mbili.... Lakini sasa kwa usumbufu wa umeme katika nyumba za kupanga, nutaweka service miter yangu, ili niwe nalipa umeme nilio utumia mimi"

    Aliongea Swalehe huku dalali akisema

    "safi sana kijana, umejipanga... Na huo ndio ulipaji kodi mzuri, yaani mpaka unasahau"

    "ndio mzee, najua hio miezi kumi ikiisha, basi nina kitu cha kufanya"

    "ok kijana... Kwahio ukiweka hio service miter yako, unataka tufanye nini"

    "unatakiwa ubalansi malipo ya pango, mana hata siku nikihama, siwezi kuitoa.. Hivyo itakuwa yako... Lakini unibalansie kwenye malipo"

    Aliongea Swalehe huku baba mwenye nyumba akiuliza kuwa

    "kwani hio service miter ni shilingi ngapi.."

    "ni laki moja na nusu... Na hapo bado hujamlipa fundi"

    "suuuuu.... Yaani hapo kuna miezi mitatu... Duuuu.... Ila sio mbaya mana atakaekuja kupangisha hicho chumba, atalipa elfu sitini badala ya hamsini... Mana atakuwa na kifaa chake kinacho muonyesha matumizi ya umeme wake... Basi hilo halina shida.. Ila mimi nitakupa miezi miwili kwasababu ya hio service miter... Mana mitatu ni mingi sana kijana"

    "ok sawa.... Wacha kesho nije kufanya malipo, kisha nihamie"

    "sawa, nami wacha nikatengeneze mkataba, ili usumbufu usijitokeze baina yetu"

    "ni sawa"

    Swalehe alitoka pale na kumpa dalali malipo ya kazi yake....



    BAADA YA WIKI MOJA NA SIKU KADHAA



    ikiwa ni tarehe 25 ya mwezi wa pili, jafari alikuwa akikifanyia usafi chumba hicho baada ya fundi wa kuweka ile miter kuchafua... Wapangaji walikuwa wakiangalia hicho kifaa kinacho wekwa pale jirani na mlango wa Swalehe,.. Yaani siku ya kumdai umeme, basi kabla hujaenda kumdai unaangalia hicho kifaa ili ukadai pesa ya YUNITI alizo tumia... Ghafla baba mwenye nyumba huyo katokea...

    "Shikamoo mzee wangu"

    "marahaba kijana... Habari yako"

    "salama tu sjui wewe"

    "aahhh tunamshukuru mungu... Hiki ndio hicho kifaa"

    "ndio, na fundi keshamaliza kazi yake"

    "ohooo.... Sasa wacha niwaite hawa wapangaji wenzako walijue hilo"

    mzee zuberi kama mzee wa nyumba hio, aliwaita wapangaji wake wote, mana nyumba ilikuwa kubwa,.. Jumba lina vyumba 15 huku na 15 huku.. Jumla ni vyumba 30... 15 dabo 15 singo...

    "jamani... Huyu kijana, ni mpangaji mpya katika boma letu... Kijana huyu kaweka service miter yake... Kwa yule anaekusanya pesa za umeme.. Basi kabla hajamfikia mlipa bili... Basi ahakikishe kesha angalia hapa.. Ili ujue unakwenda kumdai kiasi gani cha umeme alio utumia... Tumeelewana"

    Aliongea baba mwenye nyumba na wapangaji hawana la kusema zaidi ya kukubali,...



    Siku iliofuata Swalehe aliingia mjini, kaanza kununua vitu vya ndani hususan fenicha mbalimbali... Kila kitu kisha akavileta usiku, tena umeme ukiwa umekatika, hivyo hata wapangaji hawakuona Swalehe kaingiza nini na fenicha ya bei gani,... Swalehe alinunua kila kitu,... Alianza kupangilia chumba chake,.. Swalehe alinunua meza ya kioo kubwa... Hicho kitanda ndio usiseme, ni vile vitanda vya laki nane mpaka milioni,.. Godoro la laki tatu... TV kubwa kubwa na kistar time chake cha kiushkaji,.. Mbaya zaidi.. Kanunua mpaka kompyuta alivyo na sifa,.. Yaani mziki hapo ndani ni balaaa... Chini zulia kama kawaida ya sifa za wasambaa.... Swalehe alionekana ni kijana aliojipenda zaidi, hakutaka kujiweka vibaya kama alivyokuwa kwa kaka yake... Swalehe alinunua nguo mpaya, yaani maisha mapya na kila kitu chake kipya... Mashuka ni yale ya HOME SHOPPING CENTRE,.. Yaani anataka kuishi kitajiri hataki tabu, alinunua jiko la gesi zile pleti mbili, yaani sehemu mbili za kupikia,alinunua stoku ya chakula, yaani utafikiri ana mke kumbe yupo peke yake,.... Alipomaliza kupangilia chumba chake alikifunga kisha akaondoka zake,... Sasa nia yake yeye atoke kwa kala yake tarehe 28 na siku ya leo ni tarehe 26...basi aliona hawezi kuvuruga tarehe hio, hivyo karudi kubanana na majamaa zake kule geto



    "jamani vijana... Mwezi unaisha huu... Nadhani mnakumbuka nilisema nini"

    Aliongea hasani ambae ndio fundi wao na ni kala yake swalehe,

    "tumekuelewa broo"

    Alijibu swalehe huku wengine kimyaa

    "oya wengine vipi mbona kimya"

    Hassan aliwauliza wale waliokaa kimya kana kwamba hakuna aliofanya kitu chochote mpaka hapo..

    "broo itabidi kesho nisiende saiti ili nikatafute chumba"

    aliongea Mahmud ambae yeye kidogo nae alijipanga hivyo hakuwa na tabu

    "ni wewe tu, ila ujue usipo enda na lako halipo"

    "ni kweli broo lakini... Nitapataje chumba kama nitakwenda saiti"

    "ok ni sawa.... Enhee na nyie wengine"

    "broo tupe mwezi mmoja tena"

    Waliongea akina Abedi na Jeremiah, wao pesa zao huenda baa kulewa na kufanya mambo mengine ya kununua wanawake,

    "ina maana hizi pesa za mwezi huu mmepeleka wapi... Au nilivyosema nawapa mwezi mmoja mkajua utani eee?.... Zimebaki siku mbili tu"

    Aliongea hasani huku akipanda kitandani na kuvuta shuka, kana kwamba wamesha kula muda mrefu



    WIKI MOJA BAADAE



    Baada ya wiki moja kupita,.. Swalehe akiwa ana siku ya tatu toka kuhamia kwa chumba chake.. Sasa ana furaha kwani anajimiliki mwenyewe na maisha yake, mana kama ni kazi anajua, na hata kuishi na mke anaweza labda aamue kutulia kwanza, kwani kijana ukiwa na malengo katika maisha ni lazima ufike mahali ulipo pataka kufika... Usiku swalehe ni kucheza tu gemu kwenye kompyuta mana kitumia sana hajui,...



    Asubuhi na mapema, swalehe kakurupuka kitandani akiwa kabanwa na mkojo ile mbaya, kama unavyo jua mikojo ya asubuhi ilivyo na balaa,.. Katoka fasta fasta na kukimbilia chooni, sasa ukumbuke swai ana lile wenge la usingizi, mana kakurupuka nao... Sasa ile anaingia tu, kapaamiana na mwanamke aliokuwa anatoka kuoga bafuni, japo swalehe yeye alikuwa anaingia chooni, sasa katika ile hali ya kupishana, wakapigana vikumbo, yule dada akadondosha uchupi wake aliokuwa kaushika mkononi baada ya kuufua huko bafuni...

    "pwaaaaaaaaaa"

    Chupi ilidondoka chini, sasa kila mtu kaduaaaa

    "we huoni, unakuja tu kichwa kichwa na kidevu yako iyo..."

    Aliongea msichana huyo mzuri mwenye umbo la kuvutia na hapo alikuwa kavalia kanga yenyewe tuu, mana kama ni chupi ndio hio iliodondoka hapo chini, hivyo hapo ana kanga tuuuuu...

    "Samahani dada angu, ni bahati mbaya tu"

    "kama bati mbaya bomoa, jenga makuti.... Hebu Niokotee nguo yangu haraka"









    Katika maisha usiombe uchukiwe na mwanamke ambaye huna levo nae, yaani utateseka mpaka ukome, na ni Afadhali uwe mbali nae kuliko uwe karibu nae, mana utajiona kinyesi mbele yake,



    Swalehe akiwa na haraka ya kuelekea chooni kujisaidia haja ndogo, lakini ghafla anampamia msichana mmoja mrembo sana na mwenye umbe la pekee,... Alikuwa mweupe wa kupendeza,... Pia alikuwa na heshima kwa baadhi ya watu, kana kwamba anaheshim wathu wenye mionekano ya maisha ila sio mafukara kama Swalehe,...



    "kama bati mbaya bomoa, jenga makuti.... Hebu Niokotee nguo yangu haraka"

    Aliongea msichana huyo, lakini Swalehe alianza kutabasamu kwa mbaali sana, kumbe swai alishampenda msichana huyo siku mbili zilizopita baada ya kumuona...

    "kwa jinsi alivyo Ingia katika moyo wangu... Sioni kazi kumuokotea nguo yake"

    Swalehe aliongea hayo katika moyo wake, na kuinama bila kuogopa, mana aliotakiwa kuogopa ni huyo dada nguo yake isishikwe na mwanaume,... Swalehe aliinama kisha akataka kuishika lakini yule dada akaiwahi na kuiokota yeye mwenyewe huku akisema

    "nyooooo,.. Chupi mno umesimamisha je ungeona ndani ingekuaje??..... Wanaume wengi bwana"

    Aliongea dada huyo kisha akaondoka, sasa Swalehe kuangalia, duuuu kweli nanii ilikuwa imevimba,... Kana kwamba kuona tu ile nguo ya ndani kwake imekuwa tabu...



    Aliingia uwani na kujisaidia kisha akatoka na kwenda ndani kuchukua maji ili akaoge aelekee kazini, yaani kwenda kubebana na zege,... Swalehe alioga kisha akatoka zake,.. Swalehe ni kijana alie jipenda sana katika swala la mavazi, jinsi anavyo vaa huezi amini kuwa anakwenda kufanya kazi za zege,.. Akitoka lazima ujue anakwenda ofisini, lakini kumbe anakwenda kubeba zege huko maana yake ni saidia fundi wa ujenzi,... Swai aliwasha jiko lake la gesi na kutengeneza chai, mana hua hana tabia ya kuharibu pesa kwa kwenda kunywea chai vibandani...



    Baada ya muda fulani Swalehe akawa anafunga mlango wake kana kwamba ndio anatoka kwenda mihangaikoni,... Lakini kwa upande wa pili na yule dada nae alikuwa anatoka,...

    "Zahra"

    Aliitwa dada huyo, sasa swai ndio akamjua jina lake mana toka ahamie hapo hajui jina la huyo dada,..

    "abee dada"

    Kumbe aliitwa na dada yake ambae anaishi nae, na hawa wamepangisha upande wa dabo rumu,... Dada yake Zahra anaitwa FATUMA, mwenye miaka 28, na FATUMA ameolewa na hapo ana mtoto mmoja mdogo sana, mume wa Semeni ni dereva wa magari makubwa, na hua safari zake anaweza kwenda Uganda, Kenya Rwanda, Congo au kila nchi, hivyo anaweza kutumia hata miezi sita mpaka kurudi nyumbani, kutokana na mizunguko ya safari zake,.. Zahra ni msichana mwenye miaka 22, ni binti mrembo alio umbika kila eneo la mwili wake, na Swalehe kampenda kutokana na mavazi yake ya heshima, mana Zahra hatoki nje bila kufunga ushungi, hivyo swai kapendezwa na mavazi hayo na kujikuta akitamani hata kuoa, mana sasa hata akitaka kuoa ni ruksa kwasababu anajimiliki mwenyewe,... Hivyo Swalehe yeye kapendezwa na uvaaji wa Zahra ulivyo wa heshima, licha ya kwamba ana maneno mabaya lakini ni kwa baadhi ya watu,.. Mtoto akifunga ushungi wake anabakiza sura yake ilio nzuri hapo ndipo swai alipokufa na kuoza toka alipo muona

    "wahi kafungue duka mapema, mimi namaliza kumpa saidi chai nimpeleke shule kisha nakuja mjini"

    Aliongea Fatuma ambaye ni dada yake na Zahra, kana kwamba mjini wana kiduka chao cha nguo, kama unavyojua wadada wa mjini wanvyo penda biashara za nguo,...

    "sawa dada, ila ndio nilikuwa naelekea huko, hivyo ondoa shaka"

    "sawa wahi basi midogo wangu... Afu mbona huu ushungi hubadirishi, toka jana mpaka leo"

    Aliongea fatuma au mama said,...

    "ah dada lakini hauja chafuka sana"

    "ok sawa, nenda basi"

    Aliongea fatuma huku Zahra akianza kuondoka, na hapo Swalehe yupo kwa nje ya geti anamsubiri atoke nje angalau waongozane...

    "zaru... Zaru... Zaru jamani si nakuita"

    Swalehe aliita karibia mara tatu hivi kisha Zahra au zaru akageuka...

    "una shida gani na mimi"

    Aliongea zaru huku akiwa kashika kiuno

    "mtoto wa Kiislamu kama wewe hasira za nini... Zaru, kwa jinsi ulivyo dada angu, hupaswi kua na majibu ya aina hio, hata mungu hapendi ujue"

    Aliongea Swalehe huku zaru akamuangalia juu mpaka chini,.. Yaani kampandisha kisha kamshusha kwa macho yake mzuri,

    "hivi wewe unaniita dada?,.. Naweza kuzaliwa na wewe?... Si nakuuliza"

    Aliongea zaru huku Swalehe akikosa cha kuongea, mana sio kwa msuto huo, mtu unampa heshima lakini hataki,...

    "Samahani kama nimekukwaza zaru"

    "tena sio kidogo.... Umenikwaza haswa tu"

    Aliongea Zahra kisha akaondoka kwa nyodo huku Swalehe akijisemea katika moyo wake kuwa

    "wanawake wakali, ndio wazuri katika ndoa... Mana ukali wake ni Sunnah kabla hajaolewa,.. Ila akiolewa hua mpoleeee"

    Swalehe alijiongelea peke yake, huku akijipa moyo kuwa ipo siku Zahra atakuwa mpole baada ya kumuoa, mana ana ndoto nae na anatamani kuwa nae wakati wowote..... Basi Swalehe aliamua kuondoka zake, akiwa na kibegi chake mgongoni ambacho kina zana za kazi na nguo zake za kubadili wakati wa kazi..



    Huku njiani sasa Zahra alionekana kuingia katika gari aina premio, huku akisema

    "ayub mpenzi wangu... Pole kwa kunisubiri, kuna mjinga ananisumhua sana anakera mno"

    Aliongea zaru huku ayub akisema

    "ni nani huyo na anataka nini"

    "mimi hata sijui... Yaani msumbufu kweli"

    "achana nae..."

    Aliongea ayub huku akiendelea kuendesha gari yake taratibu bila matata, wakati huo zaru anafurahi kwelikweli, mana wanawake wanavyopenda wanaume wenye maendeleo mmmhh, kazi kwenu...



    Basi walifika katika duka hilo dogo tu, yaani hata nguo zenyewe zinahesabika, kana kwamba nguo zimeisha zinahitajika zingine kuletwa ili biashara iendelee...

    "sasa, wewe ahuka fungua duka, mimi nataka niwahi kazini... Mana kuna wazungu wananisubiri pale kazini"

    Aliongea ayub huku Zahra akijibu kwa Tabasam zito

    "sawq mpenzi wangu... Kazi njema"

    "sawa bibie... Sasa zaru..."

    Alianza kuongea ayub huku zaru akirudi kwenye gari, mana ilionekana kuna maongezi baina yake na ayub

    "niambie baby"

    "Zahra??.. Ni mwezi sasa toka kuanza kwa mahusiano yetu.. Lakini mbona sijawahi kuonja tunda jamani... Fanya mpango leo hata nami nijisifu kuwa nawe"

    Aliongea ayub kana kwamba toka kuanza kwa mahusiano yao hakuwahi kupewa penzi na Zahra

    "ayub,.. Mimi naogopa utanichezea tu, niambie kuhusu hilo... Mimi staki kuchezewa katika maisha yangu"

    "zaruuuuu... Hebu niangalie.. Mimi ni mwanaume na heshima zangu, why nikuchezee mwanamke mzuri unae nifaa kukua... Hebu kua Siriasi bwana zaru, usitake kunilinganisha na hao vichaa wako"

    Aliongea bwana ayub huku akijifanya kuwa na hasira sana

    "basi mpenzi wangu, nimekutania tu... Basi njoo mchana,.. Dada atakuwepo hapa dukani,.. Tutatoka"

    Aliongea zaru huku ayub akifurahi na kusema

    "kweli"

    "yes... Nakuapia leo tutatoka"

    "siamini zaru"

    "amini hilo"

    Basi ayub aliondoka kwenda zake ofisini kama alivyo mwahidi zaru



    Huku kwenye zege, mwanaume alikuwa akiumia huku mafundi wakipiga stori za wake zao, yaani wanasifia utamu wa ndoa, ulivyo..

    "mi nashangaa vijana na nguvu zao lakini hawataki kuoa... Kama hili, ona lilivyo na nguvu lakini halioi"

    "tatizo vijana wa sasa waoga... Hawataki kujaribu kuoa"

    Basi Swalehe alikuwa akijiskia raha huku akimfikiria Zahra kuwa na ndoto nae katika swala zima la kumuoa, japo anaonekana yupo matawi kuliko Swalehe, lakini vivyo hivyo tu, kama ni riziki yake ni yake tu...



    Sasa tukija huku NMC (National Milling Company) alionekana kijana kama ayub akiwa anapakia mizigo katika gari,.. Yaani ni wale watu wanao beba magunia ya mahindi, kutoa kwenye gari kupeleka kwenye godauni la NMC,... Lakini ni kama vile wamefanana hivi,.. Hivyo ni dhahiri kuwa ayub ana ndugu yake ambae ni mbeba mizigo huku kiwandani...



    Tukiachana na huku, sasa tuje huku kwa Swalehe aliokuwa akimwambia fundi kuwa

    "fundi,.. Mimi nakwenda kuoa muda sio mrefu, tena mtoto mkaliiiiii"

    Aliongea Swalehe huku akiendelea kukoroga zege,..

    "aahhahahahaha, we uliona kuoa ni kuvaa suruali eeehh, usione sisi tuna wake, uliza ilikuwaje"

    Aliongea fundi mmoja aliokuwa akifanya kazi na swai,..

    "sasa mbona unantisha broo"

    "ahahahhaa sio kuwa nakutisha.. Mimi nakuambia ukweli, wanawake wa siku hizi sio kama wa zamani... Wanawake wa siku hizi wanataka uwaachie elfu 30 mezani... Sasa wewe unalipwaje ili uweze kuacha elfu 20 au 30 mezani"

    Aliongea fundi mwingine, mana walikuwa wanawasema vijana wasiotaka kuoa

    "kwahio sasa fundi wewe unanishauri vipi labda"

    Swai alimuuliza fundi huyo na hapo kaka yake swai hayupo, kana kwamba kuna mjengo mwingine kaenda kujenga

    "kikubwa kwanza, mwanamke aelewane na hali yako.. Laa sivyo utaoa leo kesho umeacha"

    Aliongea fundi huku swai akisema

    "duuuu... Hio kazi sasa"

    "oooohooo hahahahahaha... Dogo anakata tamaa ya kuoa huyu"

    Basi ilikuwa ni furaha, kama unavyojua watu wa furaha siku zote ni furaha



    Tukija huku mjini ambako Zahra alikuwa katulia mahali pembezoni mwa duka lao,...

    "wewe mbona umekaa mbali hivyo"

    Dada yake alimuuliza, kwanini kakaa mbali tena kwenye jua

    "amna dada... Namsubiri ayub"

    "mmmhhh mwenzangu na huyo ayb, mmmhh leo nataka nimuone"

    Aliongea dada yake, mana kila siku Zahra anazungumzia maswala ya ayub, kana kwamba kampenda kweli, lakini haijafika hata robo saa, ayub huyo, akiwa na gari yake...

    "waooooooo baby wangu... Nilikuwa Nakusubiri muda wote hapa"

    Aliongea Zahra huku akiingia kwenye gari kisha haoo wakateleza zao mpaka gesti,...



    Kama kawaida waliingia upande wa baa wakaagiza nyama kwanza wakala, kisha ayub akachukua chumba... Wakati huo Zahra anajua leo anakwenda kukanyagwa kizenji,..

    "dada Samahani, vyumba vipo"

    Ayub aliuliza huku Muhudumu akijibu

    "ndio, unataka vingapi"

    "aaahhh dadaaa... Vingapi vipi.. Kimoja tuuu"

    "oohh mi nimesikia vyumba vipo, nikajua wataka zaidi ya kimoja"

    "hapana, nataka kimoja tu"

    "ok.. Sawa"

    Aliongea dada huyo huku akitoa ufunguo na kumkabidhi dada mmoja ili awapeleke katika chumba husika..

    Wakati huo ayub ana shauku ya kwenda kupata utam wa zaru...



    "kwanza tukaoge baby"

    Aliongea Zahra kila mmoja akiwa na nguo za ndani tu,...

    "hapana bwana... Tustareheke kwanza kisha tukaoge"

    Aliongea ayub huku akimpapasa zaru katika kiuno chake ambacho kilipambwa na cheni ya gold,.. Ayub alianza kutetemeka utafikiri hajui mapenzi, maan haamini kama leo anatumia mwanamke mzuri alioumbika vilivyo,....

    "ayubuuuuu.... Una ham sana baby wangu"

    "sanaaaa... Kama nilivyo kwambia, nina mwezi wa saba sasa toka niachane na mpenzi wangu"

    Aliongea ayub wakati huo hata Zahra anaanza kulegea kwa kushikwa shikwa matiti na ayub,..

    "aa... Aa... A... Ayu... Ayubuuuu"

    "nini mamaaa"

    "nipo tayari"

    Aliongea zaru huku ayub akiinyookea chupi ya zaru ili kuweza kuitoa ashughulikie swala zima la huba na yuba zake,.... Zaru kweli aliumbika na akaumbika, hata ayub alikuwa akivua huku akimeza mate, mana haamini kwa uzuri aliokuwa nao zaru leo anafanya mapenzi na mtu kama ayub... Sasa vile ayub alivyokuwa akimvua zaru uchupi wake,.. Zaru alikuwa kaangalia nyuma ya ayub, sasa akawa anampapasa ayub kwa mikono yake laiiiini,.. Lakini alipofika eneo la mgongo wa hapa juu, yaani kutoka shingoni kwa chini... Mgongo wa ayub ulikuwa mgumu mno, tena uliokua na michubuko chubuko flani hivi,.. Sasa zaru akashangaa, mbona ayub yupo hivi....

    "ayub?"

    Aliita zaru huku ayub anamalizia kuvua uchupi wa mtoto wa kike...

    "yes baby"

    "huku mgongoni kwako kukoje... Mbona Pako hivi kama nyoka"







    Aliuliza Zahra huku ayub moyo ukimpasuka kwa swali hilo, ila ayub alinyanyuka huku akitabasamu na kusema

    "unajua baby wewe ni msahaulifu sana, si kuna siku nilikwambia nimepata ajali... Tena Afadhali hivyo, unaona hii sura hiii... Ilikuwa haitamaniki hata kidogo.. Ile ajali iliniburuza mgongo na sura... Namshukuru mungu nimepona... Sasa nashangaa leo unaniuliza, na wakati nilisha kwambia"

    Aliongea ayub huku Zahra akiwa anahuzunika

    "jamani mpenzi wangu, pole sana.. Mimi sikumbuki uliniambia lini"

    Aliongea Zahra huku akihuzunika, na wakati huo kachupi kamesha ruka pembeni na ayub keshamkusanya katika 18 zake.... Zaru leo analiwa mzigo bila kupenda,...



    Wakati huo huku kazini bwana zege anapigika huku akimuwaza zaru,.. Mana kamteka moyo wake ghafla bin vuu, yaani kila akibeba ndoo ya zege, mawazo yake yote ni kwenye kuoa, na mke anayemtarajia kumwoa ni Zahra ambae kwa sasa anachezea fimbo ya ayub,...

    "wewe umesema unaoa... Huyo mwanamke umemuandaa"

    Aliuliza fundi mmoja huku Swalehe akijibu

    "bwana weeee.... Mtoto ni mkali, mtoto ana umbo, mtoto ana macho.. Yaani ndani hakuna haja ya taa.. Mtoto anavaa kiheshima,.. Nita watambulisha siku moja"

    Aliongea swai huku akipiga kazi zake kama kawaida

    "angalia usioe mwanamke vitu"

    Aliongea fundi huyo huku swai akimuuliza

    "mwanamke vitu yupoje"

    "angalia sasa huyu mtoto... Kumbe hata hajui mwanamke vitu yupoje, afu anataka kuoa"

    Aliongea fundi huyo

    "lakini mimi najua nimekaa na kaka zangu hapa... Yaani hapa ndio nataka nijifunze toka kwenu mjue"

    "skia swai, kwanza oa mwanamke anayekubali mazingira yako... Usioe mwanamke ambae anataka muishi maisha ya juu ingali uwezo hamuna"

    "ok huyo ndio mwanamke vitu"

    "haswaaaa... Yaani oa mwanamke asiopenda makuu"

    Aliongea fundi huyo huku swai akielewa wakubwa zake kile anacho kiongea,...



    Baada ya masaa kadhaa na sasa ni jioni, alionekana ayub akiingia NMC na gari yake aina ya premio, aliipaki vizuri kisha akaelekea katika ofisi moja kumpa ufunguo jamaa mmoja

    "Ahsante sana boss.... Nashukuru sana"

    Aliongea ayub huku jamaa nae akimshukuru ayub

    "hakuna shaka... Vipi umemaliza kazi yako"

    "tayari... Tayari... Watoto wazuri kwanini watumiwe na wenye pesa tu.. Je sisi wabeba mizigo tutapata wapi wasichana wazuri"

    Aliongea ayub huku jamaa huyo akisema kuwa

    "ina maana ulikuwa unafukuzia demu"

    "ndio... Mtoto mkali, nina imani na hii kazi yangu asinge nikubali... Na hii ndio dawa yao, mana wanajifanya kupenda vitu vizuri... Kupenda wanaume wenye maendeleo..."

    Aliongea ayub huku jamaa huyo akicheka kwa kitendo alicho kifanya ayub

    "sasa ngoja siku akukute unabeba mizigo, utaachwa"

    "heeeee, sitaki mazoea nae tena... Yaani sasa hivi apite kushoto, labda anikubali na hali yangu ya ubeba mizigo"

    "ebwana eee... Sawa, umesharudi... Ingia kazini... Na tumekubaliana tani kumi utashusha bure, kwasababu nimekuachia gari... Sasa tani kumi zako zile pale... Kateremshe zile gunia 100 kisha zipange godauni"

    Aliongea bwana huyo kana kwamba kumbe ayub kapewa gari kwa makubaliano ya yeye kuja kushusha gari zima la tani kumi ili aachiwe gari

    "hakuna shida broo... Naaza jioni hii mpaka saa nne au tano usiku.. Nitakuwa nishamaliza"

    Aliongea ayubu na wakati huo anakwenda chumba cha kubadilishia nguo na kuvaa nguo za kazi,... Ayub kazi ya ni ya ukibega (kuli) (mbeba mizigo)... Ila wakati huo ana furaha kwakua kafanya mapenzi na mwanamke ambaye hakutarajia kufanya nae mapenzi mana ni matawi ya juu,... Na hivyo ndivyo wanawake wanavyo takiwa kufanyiwa, mana hawataki wanaume wenye maisha ya chini, wao wanataka wanaume wenye levo za juu...



    Sasa huku kwa swai,.. Kesharudi nyumbani kwake sasa alikuwa ana andaa mambo ya kula, mana humo ndani ana kila kiti,... Mchele kilo 50 unga kilo 50 utafikiri ana mke, kumbe yupo peke yake,... Basi Alianza kukaanga mambo yake, mana yupo peke yake happ nyumbani



    Sasa huku kwa akina Zahra na dada yake...

    "mchana kutwa hukuwepo dukani, ulikwenda wapi"

    Fatuma au mama said alimuuliza mdogo wake

    "dada? Nilitoka tu kidogo"

    Alijibu zaru huku dada yake akiwa mkali juu yake

    "zaru mdogo wangu... Hapa ni mjini ujue,.. Acha kudanganywa na wanaume, watakupeleka wapi.. Mi najua ulikuwa kwa ayub, mana niliona mchana kaja pale"

    Aliongea fatuma tena kwa ukali mno

    "dada, lakini ayub ndio mchumba wangu dada"

    "kama ni mchumba wako mbona haji kujitambulisha... Ivi mama akisikia wewe una mwanaume afu mimi simjui itakuwaje... Hebu acha ujinga, wanaume wa sasa ni wachezeaji tu.. Yaani ukiskia mwanaume anataka kukuoa, shikilia akuoe... Laa sivyo utaziogelea sana nanii za wanaume"

    "dada jamani"

    "sio dada jamani... Zaru ulivyokuja ulikuwa mpole sana mdogo wangu, lakini ona sasa... Hata kufunga kichwa ushungi sasa hufungi mpaka uambiwe"

    Aliongea dada yake huyo, wakati huo zaru Kaangalia chini

    "lakini dada,... Ayub ni tajiri, mfanyabiashara maarufu... Nitamleta"

    "enheee hayo ndio maneno sasa... Sio kuzungushana kwenye migari tu huko, mlete nyumbani tumjue"

    Fatuma alipendezwa majibu ya mdogo wake kuwa atamleta ayub ili atambulike na familia yake...



    Ilipofika saa mbili usiku, swai alikuwa kakaa maeneo ya mlangoni kwake akiwa anachat, mana swai starehe yake ni simu tu, yaani akishika simu anataka kuhakikisha mpaka chaji inaisha ndipo aiache,.. Wakati huo kila mpangaji katulia nje ya mlango wake,... Lakini mara ghafla Zahra alitoka kuelekea dukani,.. Swai hakumuacha Zahra atoke mwenyewe, na wakati huo swai keshakula chakula cha usiku, hivyo hapo alikuwa anapunga upepo huku akiperuzi mtandaoni...

    "zaru... Zaru... Zaruuuu jamani si nakuita mamy"

    Aliongea swai huku akiwa kama anamshika zaru mkono

    "ebu niachie mkono wangu"

    Aliongea Zahra huku swai akiuachia mkono wa Zahra

    "Samahani"

    "ivi unataka nini kwangu... Si nilikwambia sitaki mazoea na wewe"

    Aliongea Zahra huku akibinua mdomo

    "zaruuuuu... Sio vyema kuwa mkali mbele ya mwanaume"

    "mwanaume???.... Hivi wakiitwa wanaume nawewe utatoka"

    Aliongea zaru lakini swai hakuwa akikata tamaa, japo maneno yalikuwa makali na ya kukatisha tamaa...

    "basi tuwe hata marafiki tu... Ila sina nia mbaya na wewe"

    Aliongea swai huku zaru akijibu

    "sina shida na rafiki..."

    Aliongea zaru huku swai akisema kwa sauti lakini hakumwambia zaru

    "duuuu kweli kutafuta mke bora yahitaji moyo sio utani"

    Aliongea hayo kwa sauti lakini sio kuwa alikuwa akimwambia Zahra, bali alijisemea mwenyewe kwa sauti, mpaka zaru alisikia...

    "hheheeeee... Kwahio na akili zako zooote, ulikuwa unanifuata fuata ili niwe mkeo au"

    Aliuliza zaru huku swai akisema

    "hapana..., ila ni kweli, nina mpango wa kuoa,.. Lakini wanawake wenyewe ndio nyie wakali kuliko hata wanaume... Kiukweli zaru, nilitamani uwe mke wangu wa ndoa....".

    Aliongea swai huku zaru akiangua kicheko kikubwa kweli

    "heheheeheheheheheheh.... Daaa, ama kweli wagonjwa sio lazima walazwe hospitali,.. Kumbe hata huku mtaani pia mpo.... Hivi wewe... Hivi ulivyo hivi... Kwanza unafanya kazi gani"

    Zaru alimuuliza wakati huo wamesimama mahali tena zaru kasimama kwa dharau mno

    "mimi FUNDI UJENZI,.. Mkandarasi wa majengo"

    Aliongea swai huku akizidi kujigamba akidhani ni kazi inayopendwa na wanawake...

    "kwanza ushantia kichefu chefu klna kazi yako... Yaani hata rangi zangu za kucha huezi kuzilipia... Leo uje uwe mume wangu.. Cheeeeefuuuu... Alafu sikia we bwege... Kuanzia leo.. Mazoea na wewe sitaki... Kwanza mwanaume mwenye una aleji na wanawake, kama nguo tu uliitamani, je mwanamke... Kuanzia leo, mazoea na wewe sitaki"



    Zaru aliongea huku akiondoka kuelekea dukani

    "zaru... Zaru simama basi"

    "wewe.. Unajua nitakuitia Mwizi, kaa mbali na mimi... Hii sio taipu yako, tafuta taipu yako.. Fara wewe"

    Duuuuuu swai alijiskia aibu mana katukanwa mbele za watu,..

    "sawa, lakini sintokata tamaa... Mana niliambiwa mwanamke mkali wakati wa kumuandaa, hua mpole wakati wa kuliwa... Naami ipo siku"

    Aliongea Swai huku zaru akisimama mana kayasikia hayo maneno,.. Swai akaona atatukanwa tena, ikabidi aondoke.... Basi swai katulia zake ndani, lakini ghafla umeme ukakatika

    "aaahh wacha ukate nilale sasa"

    Alijiongelea swai huku akivuta shuka na kutaka kulala, mana simu nayo ilikuwa inaishilia chaji,..



    Lakini akiwa kalala ghafla mlango wake uligongwa,.. Tena kwa upole wa hali ya juu,... Swai anajiuliza ni nani anagonga mlango na wakati huo ni saa tatu usiku,...

    "nani wewe"

    Swai alimuuliza mtu huyo aliokuwa akigonga mlango wake..

    "ni mimi"

    Ilikuwa ni sauti ya kike lakini swai hakuitambua sauti hio, japo ni mgeni katika boma hilo,...

    "Samahani, kama unataka pesa ya umeme, angalia hapo juu Kwanza, ili nitoke na pesa husika ya malipo ya umeme"

    Aliongea swai kama kumtaarifu mtu huyo kuwa kama kaja kuchukua pesa ya umeme, basi aangalie pale juu kuna kifaa kinacho onyesha matumizi yake ya umeme, hivyo aseme kuwa katumia umeme kiasi gani ili atoke na pesa husika...

    "hapana, mimi sio mtu wa umeme"

    Aliongea mwanamke huyo alio nje, lakini swai hakutaka kumuuliza mtu sana, hivyo aliamka na kwenda kufungua mlango....

    "mambo swai??"

    Alisalimia huyo mwanamke kisha swai akajibu

    "salama tu Shikamoo mama"

    Swai alimjua mana anamuona ona na ni mpangaji mwenzie, tena ni mtu mzima kabisa...

    "sasa swai jamani,.. Hio mama inakujaje katika kinywa chako"





    Katika nyumba za kupanga, hua kuna vijimambo vidogo vidogo vya hapa na pale,... MAMA MWAJUMA au ASHA yaani mama huyu anaitwa asha, huyu mwanamke ni mdogo wake mama mwenye nyumba,.. Yaani ZUBEDA ni mke wa baba mwenye nyumba, sasa huyu mama Mwajuma ni mdogo wake na Zubeda, kwahio hapo kapewa chumba bure na shemeji yake ambaye ni mzee zuberi,...



    Swalehe hua anamuonaga tu mama huyo sasa leo alishangaa kumwona nyakati za usiku tena umeme ukiwa umekata... Swalehe alimuuliza kuwa yeye ni nani lakini aliona ni vyema amfungulie mlango ili aweze kumwona... Swale alifungua na kuanza kusalimiana... Lakini mama Mwajuma hakutaka kuitikia salamu ya Swalehe, badala yake akamuuliza

    "sasa swai jamani,.. Hio mama inakujaje katika kinywa chako"

    Aliongea mama Mwajuma baada ya Swalehe kutoa salam ya heshima kwa mama huyo,...

    "lakini wewe ni sawa na mama yangu"

    Aliongea swai huku mama Mwajuma akikataa

    "aaaakuuuuuu.... Mimi sina mtoto mkubwa kama wewe,.. Mtoto wangu wa kwanza ambae ni Mwajuma, ana miaka 16,... Mtoto wa pili ana miaka 10, na mtoto wa tatu ndio huyu ana miaka mitano,.. Haya kisa cha kunizehesha jamani we mkaka"

    Aliongea mama Mwajuma huku swai akiwa anashangaa mama huyo anachokiongea..

    "ok tuyaache hayo... Ulikuwa na shida gani"

    Swai alimuuliza mama huyo huku anaeutaka ujana kwa lazima

    "niingie ndani kwanza,.. Kila mtu asikie jamani we mkaka"

    "lakini mama, kuna giza huku... Na istoshe Sijawasha sola kwasababu nilikuwa nalala"

    Aliongea swai kama kujitetea japo sauti ilikuwa sio kubwa kivile,...

    "hebu niache niingie"

    Mama Mwajuma aliingia kwa nguvu, lakini swai alipo mwangalia mama huyo alimshangaa kumwona kaja na kanga moja tu,...

    "ok umesha ingia... Niambie una shida gani"

    Aliuliza swai huku mama akikaa kitandani na kusema

    "nimekuja kukuomba sabuni ya kuogea... Mana una sabuni nzuri, yaani ukitoka bafuni hua Naipenda ile harufu ya sabuni yako"

    Aliongea mama Mwajuma au asha, huku swai akiwa haamini kwa kitu alichokuja kuombwa,... Swai aliwasha sola yake ili aweze kuiona sabuni ampe aondoke,.. Sasa uzuri swai ana sabuni zake kama tatu hivi, hivyo alichukua mpya na kumpatia mama huyo...

    "sasa mbona umenipa mpya.. Ah ah mimi sitaki mpya, nipe ile ile unayo ogea wewe"

    Aliongea mama huyo huku akifunga kanga vizuri, duuu mpaka swai akafumba macho, mana kafungua kanga mbele ya swai,...

    "acha ujinga wewe, nina chupi ndani... Ulijua sina ee?"

    Mama aliongea wakati huo swai hakutaka kubishana nae, alichukua hio anayo ogea na kumpatia

    "haswaaa, hii ndio niliokuwa nataka mimi.... Nakurudishia sasa hivi"

    "ah hapana, nenda nayo tu"

    "sitaki kubaki nayo bwana"

    Aliongea mama huyo huku akitoka kishangingi falani hivi kwa kutikisa kalio lake,.. Swai alijibwaga kitandani na kusema

    "balaaa gani hili,... Mbona hata sielewi"

    Aliongea swai huku akijifunika shuka lake,...



    Ilipita dakika tano tu, mara mlango uligongwa, swai akajua hio ni sabuni inaletwa...

    Swai akafungua mlango ili amwambie aende nayo tu

    "unaweza kwenda nayo tu mama angu"

    Aliongea swai huku mama akiingia kwa lazima na kuiweka sabuni hio kwenye ndoo ya swai ambayo ndio anaitumia kuogea,...

    "sabuni yako kama pafyumu,.. Nimeipenda sana"

    "ichukue kabisa"

    "hapana.... Nitakua nakuja kukuomba... Siku zote nilikuwa nakuogopa nikajua wewe unavuta bangi kama hao vijana wa vyumba hivyo vingine.. Kumbe wewe huna tabu jamani"

    Aliongea mama Mwajuma na wakati huo kaketi kitandani utafikiri masofa hayaoni,...

    "ok poa... Si tayari, nataka kulala"

    "huna vijimafuta swai"

    "hayo hapo"

    Wakati huo swai kasimama tu anamshangaa mama Mwajuma...



    Lakini sasa mama Mwajuma, pale alipokaa kitandani, pameloana kwasababu alivaa chupi ambayo kaifua bafuni,... Yaani alipomaliza kuoga kafua chupi yake kisha akaivaa, na hapo ana kanga moja, hivyo nguo ile ya ndani imetoa maji na kiloanisha shuka ambalo limetandikwa katika kitanda hicho..

    "ooohhh Samahani swai... Nimeloesha shuka lako... Nipe lingine nikutandikie mara moja"

    Aliongea mama Mwajuma huku swai akimwambia

    "Usijali, nitalitandika tu... Unaweza kwenda"

    Aliongea swai lakini mama Mwajuma hakutaka kuondoka,... Mara akafungua ile kanga yake yote akaiweka pembeni afu akawa anatengenezea chupi yake... Mama Mwajuma alijaa shanga kiunoni, swai alifumba macho wakati huo swai kajizuia tu lakini ilibaki kidogo tu nyeg** zimtoke, mana hajawahi kufanya mapenzi toka kuzaliwa kwake, sasa napoona vitu kwa ukaribu hua anapata msisimko mkali mpaka anatamani kulimwaga hadharani....

    "swai... Acha utoto bwana... Nina chupi, ulijua nimevua zote??... Swai... Fumbua macho basi"

    Aliongea mama Mwajuma, huku akichukua kanga yake na kuivaa,.. Sasa swai alikuwa bado kafunika macho na mikono, kumbe mama Mwajuma alikuwa akiangalia jinsi dudu la swai lilivyo vimba,.. Bila uoga mama Mwajuma alilishika juu ya suruali la swai...

    "nini sasa mama mwaju... Ebu nenda bwana nishakuchoka sasa"

    Aliongea swai baada ya kushikwa uume na mama mwaju... Swai Aliongea kwa sauti mpaka mama mwaju akaogopa sana... Hivyo alitoka zake na kuelekea uwani tena lakini ni jirani na chooni... Sasa kumbe mama mwaju ndio aliozima umeme wa nyumba nzima ili kuwe na giza, aweze kwenda chumbani kwa swai... Mara umeme umerudi,.. Lakini mama mwaju alikuwa kazima.. Swai alilala zake baada ya mama mwaju kuondoka zake...



    Siku, wiki mwezi ulipita, ikiwa ni mjini moshi swai akiwa katika ujenzi wa jengo moja lililopo moshi mjini,.. Na hua analala huko huko saiti mana hawezi kulalia Arusha afu kila siku aende Moshi,.. Hivyo huko huko wanatafutiwa pakulala mafundi wote ambao wamekwenda huko, na hio ndio kazi ya Swalehe, kusafiri kikazi, na anaweza kuchukua mwezi au miezi kadhaa...

    "swai bwana anataka kurudi nyumbani, kakumbuka jimama lake lile"

    Aliongea fundi mmoja, kwani swai aliwapa stori ya mama Mwajuma ambae anamsumbua kila siku,...

    "aaahhh fundiiiii,.. Mi nitembee na mijimama ya nini ndugu yangu"

    Aliongea Swalehe huku akipaka rangi, mana hio ni kontrakti ya ufundi wa rangi,.. Popote pale Swalehe anajiunga, hachagui zege, uselemara, fundi tailizi. Yaani popote anafanya kazini

    "wewe wakati tunakuja si ulisema kuna mama anakusumbua"

    "ndio, lakini sikumtaka mimi... Simtaki.. Mimi namtaka Zahra bwana"

    Aliongea swai huku mafundi wakigeuka

    "Zahra,... Huyo Zahra ndio demu unaetaka kumuoa"

    "ndio"

    "eeehh hongera yako bwana.."

    "ila fundi mtoto ananisumbua huyo, duuu... Na sasa nikirudi narudi na zawadi kwa ajili yake"

    Aliongea swai huku fundi akimuuliza

    "anasumbua nini tena... Kwani si tayari kesha kaa kwenye mkao wa ndoa"

    "hapana.... Mtoto ananiletea nyodo.. Kaniuliza kazi yangu nikamtajia... Duuu kaniambia kuwa kazi yenyewe imemtia kichefuchefu"

    Aliongea Swalehe huku fundi wake wakisikitika mno

    "ebwana jumbe?"

    Fundi alimwita fundi mwenzie

    "sema ndugu"

    "tumpe ushauri huyu fara.... Umemsikia anacho kisema..."

    "nimemsikia..."

    "sikiliza swai?... Juzi juzi tu hapa tulikuambia angalia usioe mwanamke vitu... Sasa hebu angalia sasa, yaani kazi yako tu ni kichefuchefu kwake,.. Je wewe utakuwaje kwake... Swai... Nakushauri kama kaka yako... Huyo sio mwanamke wa kuoa... Angalia njia nyingine.. Bila hivyo utaishia kumaliza pesa zako tu"

    Aliongea fundi huyo huku mwingine akisema

    "kweli swai... Kama umejipanga kuoa, ni vyema sana... Lakini angalia mke ambaye ataendana na maisha yako.. Ila kwa huyo unatuambia sisi... Hafai... Wewe ni fundi sasa... Na Wahenga walisema, NI BORA UKOSEE KUJENGA LAKINI SIO KUKOSEA KUOA.... sasa kuwa makini, wewe ni mdogo wetu"

    Aliongea fundi huyo huku Swalehe akiwaelewa vyema,...

    "kama huyo mwanamke ana nyodo, huyo hafai kuoa swai... Utateseka sana.. Na sisi hatutaki kukuoa mdogo wetu unapata shida juu ya mkeo, tafuta mke bora na sio bora mke"

    Aliongea fundi, huki swai akiingiza kila neno kichwani mwake, mana swai alimpenda sana zaru kwa uzuri wa shepu na mavazi yake, na hakujali kiburi chake, mana Swalehe anaamini ya kwamba, mwanamke mwenye ukali wakati wa kutongozwa basi akiwa ndani hua mpole..

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog