Search This Blog

Thursday 24 November 2022

THE DOM - 2

 

     

     



     

    Chombezo : The Dom

    Sehemu Ya Pili (2)

     



    Wakati huo General nyange akiwa ndio anaweka simu yake katika mfuko, kisha wakaingia ndani wakiwa na makamanda wasiopungua 15,ambao alikuwa nao kwenye sakata lile la kupakia silaha katika gari la kawaida,...

    "sasa, kila mmoja afe na mzigo wake, afu longo longo sipendi"

    Aliongea general nyange, huku makamanda ambao ndio walimu wa wanafunzi wote,...

    "sawa kamanda,.. Lakini mkuu mbona ishu hii tunayo muda mrefu na hakuna aliejua"

    "nalijua hilo, lakini bingo la leo,... Mtafurahi... Kuleni milioni kumi kumi kila mmoja"

    Aliongea general nyange huku akiweka briefcase mezani ili kutoa vitita kadhaa kwa ajili ya kugawanya.. Kweli kila kamanda alipewa kiasi cha milioni kumi, huku akiwataka waelekee katika nyumba zao za hapo hapo kambini,... Kumbe wanafanya biashara ya uuzaji wa silaha za serikali



    JAMANI SIMULIZI HAINA UKWELI JAMANI, MSIJE MKAANZA KUSEMA KUWA NI KWELI.... MANA NYIE DUUU



    Sasa huku ndani kwa sahi, mwaju akiwa ndio kaishika ile simu ya kijana BB,... Lakini ghafla alishangaa kuona picha moja ikiwa katika screen sever, mwaju aliitupa ile simu mezani na kuzidi kujiuliza, huyu kijana ni nani hasa, yaani licha ya kazi yake hii ya upelelezi, bado ufamilia wake una mashaka, mana inawafanya watu kujiuliza mara mbili mbili,...

    "huyu mkaka ni nani haswa.. Na hii picha inamhusu vipi"

    Aliongea mwaju huku akiichukiwa ile simu na kutaka kumpelekea General ambae ndio mkuu wa majeshi,...



    Lakini kabla hajapeleka, kwanza alijiuliza,...

    "au General atakuwa ananichezea akili, mana naweza kumlipoti mtu kumbe ndio najilipoti mimi mwenyewe"

    Aliongea mwaju katika moyo wake

    "ngoja niiweke kwanza... Nikipata kitu kingine, itakuwa bora zaidi..

    Mwaju aliirudisha ile simu kisha akawa anaendelea kutafuta kitu kingine, lakini ukumbuke kuwa sahi hakuja na begi lolote hapa jeshini, kwani hakutarajia kuanza mafunzo siku hio hio, hivyo nafasi ya kwenda nyumbani kwao kuchukuwa baadhi ya vitu, alikosa kabisa na ukizingatia leo ana siku ya pili toka aanze mafunzo yake,.... Mwaju hakutaka kuipeleka ile simu kwanza kabla mpaka apate kitu kingine tofauti na simu... Mwaju aliendelea kutafuta uvunguni, funua makabati ambayo sahi bado hajayawekea kitu chochote kile,...



    Sasa huku msituni pembeni na eneo la jeshi palipokuwa na kazi ya kupakia silaha za jeshi,...

    Sasa Mwarabu akawasha gari ikawaka, lakini kila akiingiza gia na kutaka kuondoka, inakataa alishangaa ni kwanini gari imekuwa na hitilafu kabla ya kuondoka pembezoni mwa jeshi,...

    "hebu kaangalie au kuna jiwe"

    Mwarabu alimtuma mtu wake, na wakati huo kiza totoro, yaani hata tochi hazikuwepo eneo hilo, kutokana na kazi waliokuwa wakifanya watu hawa... Yule kijana alitoka katika gari, na kuanza kumulika mulika kwa siri sana, ili tochi isionekane na watu wengie,.. Sasa kijana akaona propela imefunguliwa,.. Akaona wacha akaifunge,... Kitendo cha kusogea ni kitendo hatari mno kwa kijana huyo,...



    Ukimya ulitawala chini ya gari, hakuwa na mtu akicheza cheza wala kuhema,...

    "mbona harudi huyo,.."

    Mwarabu Alimuuliza jamaa mwingine aliokuwepo eneo la kibini, mana hamuoni akirudi baada ya kuchungulia,...

    "si unamjua jamali alivyo kalegea? Unaweza ukakuta kalala huko ndani"

    Aliongea jamaa mmoja huku akishuka naye kwenda kumwangalia jamali, kweli alipofika chini ya gari alimkuta jamali akiwa kalala, lakini hajajua kuwa ni mtego..... Wakati huo Mwarabu anachukuwa simu yake na kuwapigia wanajeshi waasi ambao waliasi jeshi, ila sio kuwa ni wa kitanzania, bali mwarabu huyu ni raia kutoka kenya, hivyo anawapigia makamanda wao wanasubiri katika njia fulani ya chocho mana hawapitii njia ya moshi ya moja kwa moja, watapita chochote na watapitia boda ya namanga,... Hivyo wanatakiwa kusubiri upande huo huo wa Kenya,..

    "eee halo jabir"

    "yes mkuu"

    "maili tisa tusubirini"

    "sawa mkuu, tupo ready kwa hali yeyote ile"

    "ok"

    Mwarabu anakata tu simu, alishangaa anamulikwa tochi ya macho kisha ikazima,.. Alijua ni watu wake, kumbe sio, ni sahi, jeshi la mtu mmoja.... Mwarabu alitolewa ndani ya gari na wakati huo hakuwa na silaha yoyote ile kutokana na mazingira walio kuwepo, yaani silaha wanazo katika viuno vyao, lakini hazikiwa tayari kwa tukio, mana pembezoni ya jeshi, gaidi gani anaweza kuja.... Sasa kumbe sahi alikuwa akiwavunja shingo mmoja baada ya mwingine,... Hata mwarabu kwake alikuwa mlaini sana kitokana na kustukiza, yaani hakutegemea kukutana na swala kama hilo....

    "General nyange umetusaliti"

    Aliongea mwarabu huku akiwekwa vizuri,

    "hakuna cha General hapa.... Nataka uniambie, silaha mnapeleka wapi"

    "kwani we nani????.............aaaiiiiiii"

    Sahi hatakagi kuulizwa wakati yeye kauliza, Ajibiwe kwanza ndipo aulize,

    "nakuuliza tena, silaha mlizipakia mnapeleka wapi"

    "hapana kamanda, sisi tumeagizwa tu, tuna wakuu wetu nchini Nairobi"

    "kwahio hizi silaha mnapeleka Nairobi?"

    "ndio... Tumeagizwa tu... Lakini wewe si nilikuwa na wewe hapa, mbona umenisaliti"

    Sahi kuona mwarabu anaropoka ujinga, zake ni kuvunja shingo tu, mana mambi ya kutumia silaha kwa sehemu kama hio ni hatari sana,.. Sahi baada ya kummaliza yule gaidi la kiarabu, aliingia katika gari na kuutoa ufunguo, ila aliuweka humo humo kwenye gari ila sio kuupata kirahisi,... Baada ya hapo alizunguka katika gari na kuimulika pleti number ya gari hio, kweli ilikuwa ni gari ya kenya..... Sasa kumbe hio saa ikikumulika sio kuwa ni tochi, bali ni flashi ya kamera, hivyo hapo kapiga picha vizuri sana...



    BB hakuwa na haja ya kuondoka wala kulisumbua gari, alivua gropsi zake baada ya kazi kisha, akazificha mahali kana kwamba hazikufaa kutumika tena, mana kama angewashika bila gropsi, katika upelelezi angejulikana kupitia finger print,... Sahi taarabu anarudi kambini tena kwa umakini wa hali ya juu, wakati huo ni mida ya saa nane za usiku,... Sasa saa ngapi mwaju hajatafuta mpaka kachoka, kila kona ya makabati anakutakana na zana za kijeshi tu, mana kila chumba cha mwanafunzi kinatakiwa kukaa na kila kitu cha kijeshi,.. Sasa mwaju baada ya kutafuta mpaka kuchoka, alijikuta kapitiwa na usingizi,.. Wakati huo sahi ndio anaruka ukuta na kuingia katika anga za jeshi... Yaani ndani ya jeshi, huku akianza kukroo, taratibu... Kwa bahati mwaju anazinduka na kujikuta yupo chumbani kwa sahi,.. Mara moja bila kuchelewa aliamka kwa haraka haraka ili arudi alipotoka







     





    Sasa ile anafika tu nje, ndio anakumbuka kasahau simu ya sahi, ili ampeleke general nyange,.. Lakini alichelewa ilimbidi tu aendelee na safari yake ya kwenda bwenini kwake, wakati huo sahi ndio anaingia chumbani kwake, yaani mwaju angerudi tu, lazima angelikutana nae njiani..... Sahi alipoingia ndani, kwanza alihisi harufu ya mtu aliotoka muda sio mrefu,.. Aliingia kwa umakini zaidi lakini hakukuwa na mtu, kitu cha kwanza kwanza kabisa alikimbilia simu yake, kisha akafungua na ile saa yake ikawa katika mfumo wa simu,... Kumbe sahi alilirekodi lile tukio mwanzo mwisho walipokuwa wakipakia silaha, sahi aliituma ile video iingie kwenye simu yake,.. Pia zile picha za magaidi pia alizikopi katika simu yake ya kwaida, ila kwenye saa bado vipo vyote,



    Asubuhi kama kawaida ni mazoezi kwa kwenda mbele, sahi hakutaka kumwambia mtu kitu chochote kile juu ya tukio la jana, mana hatakiwi kujulikana kama ni yeye ndio kafanya hivyo,... Katika mazoezi kuna makundi mawili, sasa sahi kachagua kundi la kwenda mbali kidogo kwa ajili ya mazoezi, yaani sahi hana wasiwasi mana anajiweza kivyovyote vile,... Sasa hili kundi la pili, katika mazoezi yao likaona kuna gari, ndani ya kundi hilo mwalimu anajua kuhusiana na gari hilo, ila wanafunzi hawajui jambo kama hilo, na nia ya sahi ni kwamba anataka wanafunzi wote wajue kuwa kambi yao inatoa silaha na kuwauzia nchi jirani,..  Kwakuwa mwalimu hawezi kuifanya kuwa siri tena, alijifanya na yeye hajui kisha akapiga simu kwa General nyange,

    "mkuu, kuna gari hapa imetelekezwa"

    "gari??.... Gari gani"

    "gari hii inaonesha ilipakiwa silaha mkuu"

    Sasa kamanda kusogea karibu, ghafla anawaona wale majangili waliouziwa silaha....

    "mkuu... Kuna watu watatu wanaonekana kupoteza maisha"

    Unajua huyu kamanda, anajua kila kitu, lakini hapo ni mbele ya wanafunzi, ambao hawajui lolote, hivyo lazima ajifanye hajui chochote kile kuhusu kupakia kwa silaha hizo..



    Nusu saa mbele, gari limesukumwa mpaka kambini, tena lina silaha zake zote, hakuna hata moja ambayo imesafirishwa,.. Gari lilifikishwa katika kambi ya jeshi, huku maiti waliokutwa katika eneo la tukio wakipelekwa hospitali iliopo hapo hapo jeshini, yaani hospitali ya jeshi

    "kamanda kuti??, haraka sana naomba upelelezi ufanyike"

    Aliongea general nyange huku akiwa na wasiwasi juu ya tukio hilo mana wao ndio waliouza silaha za jeshi na kushindikana kwenda,..

    "sawa mkuu"

    Kamanda kuti alikwenda katika ile hospitali akiongozana na General nyange,

    "dokta, tunaomba uangalie finger print za muuaji katika hizo maiti"

    Wakati huo kikosi cha pili cha akina sahi bado kipo msituni na hakijui lolote kuhusu suala la kukamatwa kwa gari yenye silaha, ila sahi mwenyewe kimyaa, nazidi kujifanya hajui mazoezi...



    Sasa katika hali ya kuwageuza wale maiti,... Kumbe kuna mmoja alikuwa hajafa vizuri, saa ngapi hajatoa macho, na kumwona General nyange uso kwa uso,...

    "vp kijana... Habari yako... Nini kilitokea usiku wa jana??"

    General Nyange aliuliza kwa presha ya hali ya juu mno,...

    "eti, unamjua mtu aliowafanyia tukio hilo"

    Yule gaidi alitikisa kichwa kuashiria ni kweli anamjua mtu aliowafanyia hivyo, kwahio yupo tayari kumwambia General nyange kwakuwa ni mtu wao,... Wakati huo sahi hajui lolote lile kama huku kumbe kuna mmoja hajapatwa na umauti,....

    "dokta, tunaomba ututolee huyu kijana na kubaiskeli cha wagonjwa... Afu kamanda kuti, naomba unikusanyie wanafunzi wote hapa kambini"

    Aliongea general Nyange huku akiwa na hasira juu ya tukio hilo,....

    "lazima tufahamu..... "



    Nusu saa mbele, kundi la pili linawasili kambini kutoka mazoezini, wakati huo kundi la kwanza lipo katika paredi ya utulivu,.. Mbele ya paredi yupo yule gaidi alio tayari kwa kumtaja mtu aliohusika na tukio hilo..

    Sasa sahi hajui hili wala lile,... Alitahamaki kuona sura ya yule gaidi ipo hai,..

    "mungu wangu... Kumbe hili fara halijafa"

    Aliongea sahi huku wasiwasi ukimjia, kwani nia yake ni kugundua mengi zaidi katika kambi hio, sasa endapo atagundulika mapema, itakuwa tabu

    General leo ndio aliokuwa akiwapanga line wenyewe, yaani mpaka wanafunzi wote waka kaa sawa katika line zao,...

    "gidi... Naomba utuonyeshe mhusika wa tukio la jana"

    Sahi pale alipo moyo ulikuwa unakwenda mbio,.. Mana lazima ajulikane ni yeye,... Sasa kumbe huyu gaidi ha......









    Wakati huo gaidi akiletwa hapo paredi, viongozi walikuwa makini sana na gaidi lile, mana ila General nyange anawajua watu hao sema tu anajibalaguza na kuwa na ujasiri ili akamatwe huyo aliewafanyia hivi, na licha ya hivyo, pia General ana wasiwasi sana na kibarua chake kuota nyasi, mana lazima kajulikana uharamia ambao anaufanyaga siku zote, sasa leo kabainika japo mtu aliombaini hajajulikana na ndio wanamsaka kwa udi na uvumba,...



    Yule jamaa aliletwa mbele ya wanafunzi wote, mana hakuna aliefanya wa nje ispokuwa ni hawa hawa wanafunzi au walimu ambao hawaijui hio ishu,...

    Rahim alikuwa kakaa tayari tayari kwa kutajwa mana ana kuna wakati alivyokuwa akiwanyonga alikuwa akiwapiga pocha kupitia saa yake, sasa ule mwanga wa flash huenda akawa kaonekana na mtu huyo, gani aliwekwa katika akiwa hajiwezi mana aliponea chupu chupu kufa,....



    Sasa kumbe huyu gaidi hawezi kuongea kutokana na kile kinyongo alichokipata toka kwa sahi, sauti hana lakini kwa macho tu pia anaweza kumtambua mtu,... Sahi alikuwa na wasiwasi sana juu ya kujulikana,... Lakini sasa ujue sahi ni mpelelezi makini sana, tena ni mtu anaeipenda kazi yake,.. Alimwangalia yule gaidi alivyokuwa anapitishwa karibu lakini cha ajabu alikuwa haangalii sura, yeye alikuwa anaangalia mikono, na hapo ndipo akagundua kuwa mtu huyo alikuwa akiangalia saa za mikononi, mana ndio iliompiga picha, afu mbaya zaidi walikuwa wakikaribia karibu na sahi, afu sahi na ule msaa wake upo mkononi,... Kumbe gaidi hajaona sura ya mtu alio wanyonga, ila kile kitendo cha kuoigwa picha kwa kutumia saa, huyu gaidi ndio kitendo alichokikariri katika macho yake na sio vinginevyo.... Na wakati huo wanafunzi wote mikono mbele, hivyo sahi kuivua hawezi mana mstari umenyooka afu wamesimama kwa utulivu mkubwa, hivyo mtu mmoja akijigusa anajulikana....



    Ghafla alikohoa mwanafunzi mmoja, General kasikia, akauliza

    "nani analeta ujinga"

    Aliuliza sahi mana hajui nani aliokohoa...

    "samahani mkuu, naona ni vumbi vumbi tu"

    Kumbe aliokohoa alikuwa ni sahi, na kudai kiwa amepatwa na vumbi, basi General ndiye aliekuwa anapointi macho ya gaidi pale yatakapotua basi ndio hapo hapo... Huku gaidi akiendeshwa kwa kutumia kibaiskeli cha wagonjwa.... Sasa walipofika karibu na sahi, General wasiwasi wake ni sahi, yaani hata asipo pointiwa yeye lakini ana wasiwasi na huyo kijana, japo ana kopi kopi za mtoto wake aitwaye Sharbiny ambaye nae alikufa katika mazoezi ya kijeshi,.... Sasa walipofika pale walisimamisha kibaiskeli ili tu gaidi apate muda wa kumkagua... Lakini pointi anayoitaka gaidi ni saa, lakini sahi kwa wakati huo hakuwa na saa mkononi,.... Yaani ushapu ni kitu kizuri sana, yaani kitendo cha kukohoa tu na saa imetolewa... Na alifanya hivyo kwasababu akikohoa ni lazima atikisike hivyo upenyo wa kuivua saa ulikuwepo mzuri wakati wa kukohoa... General alipitisha baiskeli mbele, lakini hawakufanikiwa kumjua mhusika,... Sasa hapo General kichwa moto, wakati huo gaidi anarudishwa hospitali, na General anaingia ofisini kwake....



    Wanafunzi wengine hawajui kinachoendelea hapo,... Basi sahi akavaa saa yake na hapo wakaendelea na mazoezi ya hapo hapo kambini mana walishapoteza muda mwingi katika sakata hilo la kumjua mtu aliohusika kuwauwa hawa magaidi na kuzifanya silaha kurudi mikononi mwa kambi ya jeshi



    Mazoezi yakiwa yanaendelea, mwaju alikuwa akimtazama sana sahi,... Mwaju ni mwanafunzi lakini ana muda mrefu hapa shuleni, hakosi miaka miwili au mitatu, na alikuwepo hata kipindi cha mtoto wa General alipokufa huyu mwaju alikuwepo, hivyo hata yeye anamshuku kuwa mtoto wa General, lakini tofauti yao ni sura, yaani sura hawafanani hata chembe, mana Sharbiny alikuwa maji ya kunde afu ana Kidoti kwenye sura upande wa kushoto chini ya jicho lake

    Lakini hayu ni mweusi afu hana kidogo, na oia hawafanani hata kidogo, na huyu anaitwa salehe, na huyo anaitwa Sharbiny, ni watu wawili tofauti kabisa... Lakini mwaju kile alichokiona kqenye simu, kinazidi kumpa mashaka juu ya kijana huyo..



    "mwaju"

    "yes mkuu"

    "nakuitaji ofisini"

    General nyange alimwita mwaju aje ofisini kwake huenda kuna kitu anataka kumuuliza, ila mwaju nae ana ham ya kuongea na General kwa kile alichokiona kwenye simu ya sahi,

    Mwaju pasina uoga wa aina yeyote aliingia ofisini kwa General na anajua kitu anacho itiwa

    "hivi huyu kijana umeshapata fununu zozote"

    Aliuliza mr Nyange au general Nyange

    "yes, jana usiku nilikuwa katika chumba chake"

    "enhee, umemkuta anafanya nini"

    "Kiukweli sikumkuta"

    "what??.... Ulikwenda saa ngapi"

    "ilikuwa ni mida ya saa saba mpaka saa nane za usiku"

    Sasa general Nyange kusikia mida hio ndio alikuwa porini kule wanapakia silaha,...

    "enhee, alirudi saa ngapi"

    "Kiukweli hajarudi, nadhani ni mpaka asubuhi mana nimetoka akiwa bado hajarudi"

    "yes,... Lazima atakuwa ni yeye tu.... Huyu kijana ni wa kumuondoa"

    Aliongea general nyange, maneno yaliomfanya mwaju kushtuka sana

    "General..... Kwanini lakini... Huenda yule ni mtoto wako"

    "ina maana mtoto wangu humjui wewe?... Mtoto wangu anafanana na yule kweli... Yaani hata sura haziendani labda sauti tu"

    "lakini mbona kwenye simu yake nimekutaka picha ya mke wako"

    "ati unasemaje?... Picha ya mke wangu mimi"

    "ndio... Ila ni picha ya mama sheby yule mke mkubwa... Ambae ni mama yake sheby"

    Sasa huyu mwaju, anaijua vizuri familia ya General nyange....

    "huyu kijana ni nani.... Hebu nenda ntakuita kwa wakati mwingine"

    General alijikuta mawazo yakizidi kumpanda katika kichwa chake,...

    "najua sio mtoto wangu, lakini kwanini awe na picha ya mke wangu katika simu yake??.... Huyu kijana kuna kazi imemleta kwa ajili yangu,.. Atakuwa hayupo kijeshi hapa kambini"

    Mzee general alianza kuhisi kuwa sahi atakuwa hajaja kimafunzo japokuwa kaletwa kwa ajili ya mafunzo,...



    Sasa mwaju alikuwa anakumbuka miaka ya nyuma kipindi akiwa na sheby,... Kumbe sheby na mwaju walikuwa ni wapenzi waliopendana sana, wakiwa hapo hapo kambini, lakini sheby alipofariki kwenye mazoezi ndipo kupenda kwake kukaishiaga hapo,... Mpaka leo hajapenda tena mtu wa aina yeyote, sasa anapomuona sahi anamfananisha na sheby mtoto wa General nyange, na wakati mtoto wa General alishakufaga kwa mlipuko wa bomu, katika mabomu ya kufanyia mazoezi kuna moja lilikuwa ni la kweli, hivyo alikufa..







     





    Sasa huku kwa General alimwita mkubwa mwenzake ambae wanalingana vyeo kidogo tu, ila nyange ndio kuu la majeshi....

    "me deo? Unajua huyu kijana mgeni toka aje yaani mimi sipati usingizi kabisa yani"

    Aliongea mr nyange huku akitamani hata kulia, mana wakimpangia njia za kumuua, chuo kitaonekana kina matatizo, mana wanafunzi wanakufa tu, hivyo miaka inayokuja hakutokuwa na wanafunzi, na miaka kadhaa mbele kutakuwa hakuna jeshi, hivyo kumuua hawawezi kwa kubofia nchi kuingia hatarini kwa kukosa jeshi,...

    "kwanza kabla ya yote mi naona ule mzigo tumkabidhi mwenyewe kwanza... Mana huyu kinana akiuona.. Itakuwa tabu"

    "lakini deo, kwanza tumjue huyu kijana ni  nani"

    "wala haina haja sana bwana nyange,.. Huyu kijana ni mdogo sana kwetu, na wala hajatumwa huyu.. Sema sisi ni wasiwasi wetu tu"

    "deo usichukulie jambo hili mzaha mzaha"

    "sikiliza... Huyu mtoto ni wa kuwa nae karibu, kama umegundua ana uwezo basi ni wa kukaa nae karibu"

    "ukae na hatari tena..."

    "kwani una asilimia ngapi za kumhisi"

    "aahhhh nyingi sana, tena na vile kamanda alivyoniambia kiwa ni mtaalamu wa kuruka ruka, ndio nahisi atakuwa mpelelezi huyu"

    "hapana hisia zako tu... Sasa mpelelezi hawezi kuja jeshini... Sasa sikia ngoja tumuite"

    General Deo alitoka nje na kumuita sahi, sahi bila kujua mipango ya mageneral hao alikuja na kuingia, lakini sasa ile anaingia tu ile saa ikawaka taa nyekundu kuashiria hapo ndani kuna kamera, sahi aliizima haraka haraka kabla hajashtukiwa na mageneral, sahi alipiga saluti kubwa kuwapa heshima yao kutokana na vyeo vyao

    "kaa katika kiti"

    Aliongea mr deogratias tena kwa kumbembeleza kwa utaratibu wa hali ya juu, na hawa nao ni mageneral wa zamani wanajua jinsi ya kumteka mtu,

    "jana saa nane ulikuwa wapi"

    Aliuliza mr nyange, huku sahi akiwa na wasiwasi sana, mana anajua jana hajaonekana kumbe kaonekana....

    "nilikwenda msalani"

    "msalani kwa masaa mangapi"

    General anauliza maswali yale yale ya kumkamata, mana kapewa ifo zote kuhusu jambo la jana,.....

    "nilikuwa nasumbuliwa na tumbo la kuendesha"

    Mara mr deo akaingilia kati,...

    "sikiliza kijana.... Jana tumeona ulichokifanya kule porini,... Sasa endepo hutokuwa na sisi, tunakutimua hapa jeshini... Na wala usitake kubisha, hana umeuwa watu wawili, na mmoja ndio huyo yupo hospitali hoi hoi.... Hii ni kesi"

    Sasa sahi yeye alijua tu hapa anapelelezwa kichini chini...

    "nilitokea wapi kwenda huko"

    "tunakujua, na aliekuleta tunamjua wala usitake kutuumiza kichwa... Umeshajua sisi ni wauzaji wa silaha hapa jeshini... Sasa unachokifanya hakitokuseidia lolote.... Ungana nasi.. Yule mgonjwa katuambia kila kitu sema hatujataka kukudhalilisha mbele za watu pale paredi.... Yule mgonjwa kasema, ulikuwa umevaa saa kubwa,.. Afu hio saa inawaka taa... Hapa jeshini waliovaa saa ni walimu tu, sasa je? Wewe ni mwalimu"

    Alipomaliza kuongea mr deo, mara mr nyange akatoa briefcase ya pesa na kuiweka mezani huku akisema

    "kijana... Kabla ya yote... Kuna milioni 100 hii hapa... Yaani ukikubali tu, chukuwa hizo pesa"







    Mr Nyange aliona hakina njia nyingine ya kumteka kijana huyo, ispokuwa pesa tu,... Lakini sasa ubaya wao ni kwamba hawa hawajui kama sahi ni mpelelezi wa serikali, tena mwenye kiwango cha hali ya juu mno,... Kwahio wanachokijua kwa sahi wao wanadhani ni kijana tu ambae anapenda haki hapendi vitu viende tofauti, kumbe sivyo, bali sahi ni mpelelezi tena aliepitia ujeshi nchini korea,.. Lakini hawa hawalijui hilo kuwa sahi ni mpelelezi wa serikali, wanajua ni kijana mpenda haki na ndio mana akazuia silaha kusafirishwa,...



    Sahi alitoa macho kuona lile briefcase la pesa taslimu shilingi milioni 100, na ni zake endapo atakubali kujiunga nao,...

    "sawa,... Ila kila kinachoendelea kwenu nami napaswa kukifahamu"

    Huezi amini sahi alikubali kujiunga nao, na kadhihirisha kuwa yeye ndie alie wauwa wale magaidi kule porini,

    "hilo ondoa shaka kijana, kila kikao lazima tukuhusishe"

    "sawa,...nipo tayari kujiunga nanyi"

    Sahi aliisaliti serikali yake, ila sahi alionekana msaliti kabla, mana kabla hajaja jeshini alionekana na kifaa cha pesa kiitwacho Discate of money (DOM).... Na kifaa hicho kinatafutwa na serikali yake na yeye ndie aliepewa kazi, na yeye ndie anae kimiliki kifaa hicho,... Yaani sahi ni msaliti kabla hivyo hapa kadhihirisha usaliti wake....

    "ok... Ila kijana kuna swali naomba kuuliza. Kuna picha nilishawahi kuiona katika simu yako... Ile picha una uhusiano gani nayo"

    Sahi kabla hajajibu aliitoa simu yake na kuiweka mezani huku akisema..

    "nina rafiki yangu mmoja nilisoma nae, aliitwa Sharbiny... Alikuwa ni rafiki yangu sana, na yeye alikuwa jeshini, mimi nilikuwa sipendi kujiunga na jeshi, lakini rafiki yangu alipofariki dunia, ndipo nikaamua kumuunga mkono... Nakumbuka kabla ya yeye kujiunga tulikuwa tukienda sehemu ya mazoezi ya mapigano,... Na yeye alikuwa akinisihi kujiunga na mafunzo ya jeshi, na aliahidi kunisaidia kwakuwa baba yake alikuwa mkuu wa jeshi,.. Lakini pia sikutaka kujiunga... Nilikuja kujua umuhimu wake pale alipokufa, ndipo nikaamua kujiunga na jeshi... Nilimpenda sana rafiki yangu na ili nimuenzi na kumkumbuka, ndio nimeweka picha ya mama yake katika simu yangu, mana hata mama yake alikuwa ana upendo nami kwakuwa nilikuwa rafiki wa mtoto wake"



    Sahi alimaliza kuongea ukweli wake wa hapo awali,...

    "je huyo baba yake unamfahamu"

    "hapana, sijawahi kumuona"

    "mbona ndio mimi baba wa Sharbiny.. Na ndio mana nikakuuliza kuhusu hio picha"

    "waooooooo.... Kumbe nimefanikiwa kukutana na baba wa rafiki yangu"

    "ndio... Karibu kwenye ulimwengu wa wanajeshi"

    "Ahsante sana mzee wangu"

    Sasa mzee kaamini moja kwa moja kuwa sahi ni rafiki wa mtoto wake, na General Nyange na deo, wanajua kuwa sahi ana wiki ya jeshi na ana wiki ya TSS, basi sahi aliondoka huku akiwa kashika kibegi chake cha pesa akielekea chumbani kwake,



    Wakati huo mageneral wawili wakiwa hapo ofisini kwao, walikuwa wakigongesheana mikono kwa kumjua kijana machachari kama huyu

    "Deo, huyu kijana anafaa tumtumie kwenye kazi zetu,... Tena uzuri ni kwamba kazi yake ina Options mbili.. Anafanya hapa TMA na TSS, sasa urahisi wa kupata ule mzigo uliobakia kule ni mkubwa sana kupitia huyu kijana"

    "Nyange una akili sana, unajua kupata kijana jasiri kama huyu ni ngumu sana"

    "vijana wote tuliowaweka mbele, wamekwisha kufa,.. Hawakuwa na uwezo, sasa kama huyu peke yake kauwa qale wajinga na silaha zikabaki"

    "deoooo.... Hapa tutawini, mana kijana ana kazi za Dar es Salaam, hivyo ni rahisi kufanikiwa kwa urahisi"

    Sasa wakiwa wanazidi kuingea mara ghafla mwaju kaingia,...

    "ooohhh binti karibu"

    Mr deo alimkaribisha mwaju

    "sasa binti, kazi yako tuliokupa imekwisha, sasa huna haja ya kumfuatilia tena, ila ukiona jambo lolote baya kwale, tunaomba utudokezee.... Kwanza shika milioni tano hizi.. Ahsante kwa kazi nzuri, mana bila wewe jana kwenda ndani kwake, imeturahisishia sana kumbana kijana mpaka akakubali"

    "Ahsante sana generally, nitafanya kama ulivyosema, na nitazidi kuwa nae karibu pia"

    Aliongea mwaju huku, akiziweka pesa zake vizuri.. Na pesa hizo ni zile walizouza silaha na hazijakwenda.. Sasa hizo pesa ndio hizi wanazogawa gawa mpaka sasa,...



    Sasa huku nchini Kenya, katika kambi ya waasi waliokuwa wakisubiri silaha toka Tanzania, lakini mpaka sasa ni hewa..

    "mbona hawa watu hawafiki na watakuwa wamepatwa na nini"

    Aliongea mkuu wa kikosi hicho, kila wakipiga simu hazipatikani... Na gari lao huku Tanzania limetelekezwa porini hivyo hakuna hata wakisema wafuatilie watashindwa kujua kilichoendelea, na maiti zimesha zikwa muda mrefu sana... Na yule mgonjwa alishauwawa kwa kauli ya sahi, mana sahi ni mpelelezi na anajua jangili akiwa hai ataleta athari gani... Sasa huku kenya wamechafukwa wanataka silaha na watu wao,...



    Baada ya wiki moja kupita, sahi akiwa anawasili jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mafunzo ya Tss, sasa huku ndipo kazi inapomhusu yeye,. Sahi aliingia katika jumba lake la kifahari, huku akiwa na briefcase ya pesa taslimu shilingi milioni 100,...alizopata kule kambi ya jeshi baada ya kukubali kujiunga na mageneral wauza silaha,... Jumba hilo la serikali ambalo ni maalum kwa maisha ya sahi, lina kamera kila kona lakini kasoro chumba chake cha kulalia ndio hakijawekwa kamera,... Basi alitoa pesa zake na kuzipangilia vizuri katika begi maalum linaloweza kufichika kwa urahisi mzuri... Alitafuta sanduku lake na kuitoa ile DOM (Discate Of Money).. Na kuiangalia kwa kucheka...

    "lazima imjue mwenzake alipo"

    Aliongea sahi akimaanisha kuwa ni lazima ajue codes Number zake zilipo, mana bila codes number haiwezi kuchapa pesa hata kidogo..



    Kesho yake asubuhi akiwa katika gari yake yenye Number za usajili wa usalama wa taifa,.. Kwanza transmission ya sikioni ilikuwa hewa,

    "GU naongea..."

    "ndio mkuu hali yako"

    "salama.. Nakuona umeingia mjini"

    "ndio mkuu na sasa naelekea TSS"

    "ok... Kuwa mpole na kazi yako"

    "sawa mkuu"

    Rais GU ana mawasiliano na sahi kwa kitumia transmission za siri sana, lakini sasa transmission nyingi huonekana katika sikio, sasa mbona ya sahi haionekani, je imeunganishwa vipi mpaka isionekane, mana sikio jeupee, halina kinasa sauti lakini sahi anasikia... Katika geti la TSS, sahi anafunguliwa kama mgeni katika kitengo hicho... Mpaka akaingia katika kile kibanda kilicho kama gereji lakini ukifika hapo hio sehemu inabonyea chini na kukushusha chini, ambako ndio makao makui ya tss,...







     





    Sasa kuna wakuu wa kitengo hicho, kama mageneral, na General mmoja anamjua sahi, ila kuna general mwingine huyo kijana kijana sana, aitwaye JJ huyu ni mtoto wa rais kapewa cheo kutokana na elimu yake, lakini sasa kijana huyo alipo mwona sahi, alishangaa sana zile hatua anazopiga sahi,.. Yaani huyu JJ alikuwa akimshangaa sana BB...

    "mkuu vp mbona unamtazama sana huyu mgeni"

    Aliulizwa na kijana mmoja aliopo katika kitengo cha computer,...

    "huyu mtu ana hatua kama rafiki yangu,.. Yaani anatembea hivyo hivyo"

    Aliongea JJ huku akizidi kumtazama sahi,... Sasa saho nae kajua kuwa anaangaliwa sana na General JJ...

    "habari yako generally JJ"

    Sasa JJ alizidi kutaharuki pale aliposikia sauti ya sahi,... Yaani vinafanana na rafiki yake kasoro sura tu ndio havifanani kabisa...

    "salama tu hali yako"

    "nzuri... Ahh mimi ni mgeni, naitwa salahe Rashidy, nilikuja juzi hapa lakini kwa bahati mbaya sijaweza kuku kuta General wangu"

    "sawa kabisa.... Hakuna shida na hiki ndicho kitengo husika"

    JJ alikuwa akiongea lakini hisia zake zinahisi ni rafiki yake tu, hata iweje, japo rafiki yake alifariki dunia akiwa mazoezini,.. Yaani JJ au Joseph John alikuwa na urafiki mkubwa sana yule mtoto wa General wa jeshini, yaani yule mkuu wa majeshi kule kambini....

    Sahi yeye alipitiliza mpaka katika computer yake, mana siku ile ile, alipatiwa kisehemu chake chenye computer, na sio yeye tu bali ni watu wote wa vitengo hivyi, ni lazima ajue maswala ya computer, na kazi kubwa hufanywa na computer, hivyo lazima uijue computer,....



    Sasa sahi alipofika katika computer yake, aliingiza program ya ile DOM kisha akaanza kuichambua kwa undani wake,.. Ipoje na inafanya kazi vp, na mashine yake ni ipi... Lakini akiwa anaendelea kufanya hivyo mara alibanwa na haja ndogo, hivyo akaacha kile alichokuwa akikifanya kisha akaelekea toilet, mana hapo ni ofisi moja lakini imegawanywa vijichumba vidogo dogo kusudi kila mmoja akae sehemu yake apeleleze kitu chake,.. Sasa sahi yeye kaja kama mwanafunzi lakini kitu alichokiacha katika computer yake, ni kitu kikubwa sana ambacho kilitakiwa kufuatiliwa na mageneral wakubwa ila sio mwanafunukama huyo,... Sasa JJ akawa anakuja katika ofisi ya BB,... Alishangaa sana kwa kile alichokikuta katika skrini ya sahi,...

    "hii si DOM hiii??... Huyu anaitafuta kama nani"

    Aliongea JJ lakini alikuwa kama anajiuliza mwenyewe,.. Joseph hakuridhika na jambo hilo alitoka na kuelekea chooni kule kule alipo sahi ila Joseph hajui kama sahi yupo huko,.. Sasa JJ ndio anapiga simu lakini haijulikani alikuwa akimpigia nani ila ilionekana ni simu ya siri sana... Na huyu ni mtoto wa rais,..

    "halo habari yako mkuu"

    "salama.. Vp mbona kama una wasiwasi hivyo"

    Sasa sahi anasikia ishu nzima ya JJ anavyoongea na huyo mtu... Kama kawaida ya saa yake kurekodi,..

    "kuna kijana ananipa mashaka sana hapa kitengo"

    "ana nini"

    "Naona ana program ya DOM sasa huyu ni nani na ni mwanafunzi"

    "whaaaat?? Unasema ana program ya DOM??.... Kaipata wapi?"

    "siwezi kufahamu, ila mkuu nina wasiwasi na wewe, mana kijana huyu ni mgeni katika kitengo hiki, iweje ajue siri hii.... Kwanza niambie hio DOM ipo"

    "ndio ninayo... Na yule mnunuzi anakuja kuichukuwa mwezi ujao sasa DOM Codes ndio inatakiwa haraka sana"







    Maongezi hayo yalikuwa yakiendelea pasina kujua kuwa palikuwa na mtu akisikia, yaani sahi ana bahati ya kujua vitu kuliko uwezo wake, sasa kitu anachokitafuta na asijue angeanzaje leo anapata njia jinsi ya kukianza... Hapo alipo sahi alikuwa anajiskia furaha sana kwa kujua dom ilipo,... Ila sema hakujua nani aliekuwa akiongea nae

    "kwahio sasa mkuu, huyu kijana tumfanye nini, mana tayari anaifuatilia ishu yetu"

    "huyo hana shida, tayari yupo upande wetu"

    Sasa hapa ndio kama tunapata ufumbuzi juu ya mtu ambe anaongea naye katila simu, ni baada ya kusema kuwa kijana huyo yupo upande wetu

    "sasa mbona hujaniambia kabla"

    "hapo ndipo nilipofanya makosa, lakini.. Kuhusu ishu ya dom hatujamgusia hata kidogo"

    "sasa kwanini anayo programu ya dom"

    "hebu mshirikishe, huenda ana elimu zaidi au anaweza kuipata codes za dom"

    "hebu ngoja nijaribu kuongea nae mana katoka kidogo"

    "sawa... We mshirikishe mwambie mimi na wewe ni kitu kimoja"

    "sawa mkuu, nimekuelewa... Afu unaonaje tukamfanya kipaumbele akailete hio codes, na akifa huko atajua mwenyewe"

    "sawa pia, ila kuwa makini na hilo"

    "usihofu mkuu, tulikuwa tukifikiria chambo tutakitoa wapi sasa ndio hichoo kimejileta"

    "na huyo ataiweza kazi mana ni majasiri mno"

    "basi tuyaache mkuu"

    "sawa"



    Simu ilikata kisha Joseph akarufi katika ofisi ya sahi na kukaa, mana tayari keshajua kuwa wana ushirikiano mzuri na sahi,... Sasa hapa tunagundua kuwa hata huyu mtoto wa rais sio mwema, na ndio anaeiumiza nchi kwa cheo alichopo.. Mana hiki kitendo ni zaidi ya CIA (Criminally International Army).. Na kitengo hiki kinaingia sehemu yeyeote ile ndani ya nchi husika, yaani ni kitengo kisichojulikana lakini kinapoingia mahala hakiwezi kukataliwa kutokana na utambulisho wake...



    Sahi akiwa ndio anafika katika computer yake lakini alishangaa kumkuta Joseph akiwa kaketi katika kiti cha pembeni, sasa sahi akajifanya kama kakosea sana kuiacha ile programu pale kwenye skrini,...

    "Samahani mkuu, ni programu ya kawaida tu"

    Aliongea sahi kujifanya ni muoga kama panya, kumbe hakuna mtu mbaya kama yeye,...

    "wala usijali... Ila nina maswali kadhaa kuhusu hii programu yako hapa"

    "sawa mkuu hakuna shida"

    Hawa watu wawili ni lika moja, lakini Joseph yeye ana cheo kikubwa sana cha ugeneral, ila hata kama awe nani hawezi kuukuta uwezo wa sahi,... Sahi kasomeshwa na mtu binafsi na sio serikali, hivyo hapo anaifanyia serikali na sio mtu binafsi,.. Mana mtu aliomsomesha mpaka sasa yupo madarakani,.

    "hii programu uliipata wapi"

    Aliuliza Joseph huku sahi akijifanya hajui saaana kuhusu hio kitu

    "aaa... Hii programu mbona niliikuta hapa hapa kwenye hii computer"

    "unasemaje??... Ni kweli, na hata mimi nimeshangaa kwanini ipo hapa, na pia nimeshtuka sana kuiona hapa"

    "sio kuwa umekuja nayo"

    "hapana, mimi ni mgeni nitawezaje kuja na kitu kama hiki"

    "unakijua hicho kifaa"

    "yes... Hio ni dom"

    "hii dom ainatafutwa sana,.. Na nitakuwa nawe mstari wa mbele"

    Aliongea Joseph huku akiangalia pembeni kama hakuna mtu anaesikia, kisha akamuinamia sahi na kumwambia

    "sisi sote tupo pamoja... Hio dom sisi tunayo... Ila codes zake ndio hatuna"

    Sahi akajifanya kushtuka sana huku nae akisema

    "aahhh kwani hizi dom zipo ngapi... Mana mimi ninayo yenye codes zake kabisa"

    Joseph alishtuka kuskia hivyo, ilibaki kidogo tu adondoke kwa mshtuko...

    "unasemaje"

    "ndio... Ninayo dom ina codes zake.. Ngoja nikutafutie programu yake"

    "wewe si ulisema hio programu uliikuta hapa wewe"

    "nilikudanganya, hii program ni yangu na hapa nilikuwa nacheki information yake ipoje"

    Sasa sahi akafanya vitu vyake kwenye computer, kachapia chapia hapoo kisha akamwonyesha codes za dom..

    "unaziona hizi... Hizi ndio codes za dom... Alafu dom yenyewe ninayo hapa kwenye begi"

    Sahi aliitoa ile dom kisiri siri, na kumwonyesha Joseph ambae ni mtoto wa rais aliopo madarakani,.. Hivyo mtoto anaihujumu nchi ya baba yake,..

    "we hii kitu umepata wapi"

    "unanitisha tena"

    "hapana, nataka tu kujua umetoa wapi"

    "niliikuta chumbani kwa baba yangu"

    "baba yako anafanya kazi gani serikali"

    "Alikuwa ni mtumishi wa BOT"

    "sasa, tupe hio dom na hizo codes zake... Tutakupatia bilioni moja tasilimu"

    Sahi kusikia neno Bilioni moja, sio pesa ndogo hio, unakula mpaka ucgakae, sasa hapa wamekutana wapelelezi wote, hivyo kikubwa ni kumjua mshindi ni nani na wote ni lika moja, yaa hata umri wa hawa watu ni sawa... Sasa sijui kwanini imekuwa hivyo

    "hio ni pesa kubwa sana mkuu... Lakini, nikikupa hii baba yangu ataniletea shida... Sasa tufanyeje ili nisiletewe shida"

    Aliongea sahi huku akiingiza dom katika begi lake,...

    Joseph alikuwa akiutamani sana mana huenda kule bank alichezewa mchezo siku ile na kuwekewa feki,... Afu mbaya zaidi ile walionayo haina programu,

    "huyo baba yako alistaafu mwaka gani"

    "mwaka jana"

    Sasa kusikia mwaka jana, Joseph akajua lazima huyu baba yake sahi aliondoka na Original kisha akaacha dom feki,.. Na ndio hio wanayoitafutia codes zake, kumbe sio Original...

    "sasa sikia, nitakupatia hio tulio nayo.. Kisha utupatie hio"

    "sawa... Mimi kitu ninachokitaka ni baba yangu asijue kama dom haipo"

    Joseph aliona kapata Zezeta lao la mwaka, yaani bonge la Zezeta... Wasipoangalia watafanywa mazezeta wao...

    Joseph hakuchelewa kuoiga simu kwa General Nyange,..

    "haloo mkuu..."

    "kuna nini tena Joseph"

    "mkuu... Huezi amini kumbe sisi tunamiliki dom feki"

    "ati unasemaje wewe"

    "hio dom ni feki mkuu, yaani tumeingia choo cha kike"

    "kama hii ni feki, hio Original iko wapi"

    "huyu kijana anayo, tena ina codes zake"

    "Whaaaaaat???..... Ati unasema nini"

    "ndio hivyo mkuu"

    "sasa si umwambie akupe, huyo ni mtu wetu"

    "tatizo ni kwamba, anahofia kwa baba yake atajua kuwa dom haipo ndani.. Hivyo angalao tumpe hio feki akamdanganyie"

    "una uhakika hio ni yenyewe"

    "ndio mkuu, na nimeziona codes zake"

    "basi ngoja niitume hii dom nilionayo huku, kisha nawe itume hio... Nampiga simu yule mzungu aje aichukuwe sasa hivi, mana haifai kukaa nayo"







     





    Sasa huku kambini kwa General aliekuwa ofisini kwake pamoja na mr deo General mwenzie

    "deo, hatimae dom original yapatikana"

    "unasemaje nyange"

    "kumbe yule kijana baba yake ni mtumishi wa BOT, na ndie alieondoka na dom original"

    Aliongea mr Nyange huku wakiwa na furaha ya hali ya juu,... Na wao wakiipata wanaiuza kwa mzungu mmoja ambae yeye ndie anamiliki mashine ndogo ya kuchapia pesa, hivyo mzungu huyo akifanikiwa kuwa na dom hio atachapa pesa ya Tanzania ambayo ni laki moja ya noti moja, ni hatari sana mtu binafsi kuachia pesa tofauti na serikali...

    "kwahio, yule yule kijana tuliekuwa nae jana ndio mmiliki wa dom Original?"

    "ndio, na ni dom iliokuwa ndani kwa baba yake"

    "anhaaaa, sasa tutaipataje hio original"

    "lazima tumpatie hii yakwetu ili baba yake akaendeleee kudanganyika"

    "sasa unasubiri nini, ita helikopta hapa uitume haraka"

    Harakati za kutuma dom zilianza huku wakijua kuwa watakapo ipata tu wanaiuza yaani hawataki kukaa na mzigo tena, na hata sababu ya kukaa na mzigo kwa muda mrefu ni kwamba hawaku ukamilisha mzigo huo,....

    "lakini mr nyange, angalia sana uwepo wa huyo kijana.... Mana kuipata dom sio kitu cha mchezo eti"

    "aaahhh hakuna tabu, kama kasema baba yake alikuwa mtumishi wa BOT sasa kuna maswali gani hapo"

    "basi haya, itume"



    Huku TSS sahi alikuwa akiendelea kumwonyesha kazi ya hio dom, unajua wengi wanaitafuta lakini hawajui inafanyaje kazi, japo wanajua ndio kichapisho cha pesa lakini hawajui kinafanyaje kazi,... Sahi akazidi kumpa Joseph jinsi dom inavyofanya kazi katika mashine...

    "sahi, hii mashine upatikanaji wake vipi"

    Aliuliza Joseph baada ya kuoneshwa mashine hio

    "hii mashine, kuipata sio rahisi, unapaswa kuwa tajiri mkubwa sana katika dunia... Na hata serikali binafsi haiwezi kuimiliki mana kuinunua kwake inaweza kufilisi nchi"

    "duuuuuu,... Kwahio yule mzungu ana mashine sio"

    Aliongea Joseph, maneno yaliomshtua sahi mana hajui hio dom inauzwa wapi,..

    "mzungu??...mzungu gani huyo"

    "kuna mzungu anataka kuinunua kwa thamani ya shilingi bilioni 500"

    Sasa sahi ndio anajua kuwa hio dom inauzwa kwa mzungu na gharama ni Bilioni 500,...

    "sasa mnachelewa nini nanyi"

    "wewe si ndio unayo"

    "walete hio feki basi nika mdanganyie mzee kama ipo kumbe ni feki"

    "inakuja usijali"



    Wakati huo helikopta ipo angani kuelekea jijini Dar es Salaam, kuipeleka dom feki,...

    "sahi, tutoke nadhani dom inakaribia Airport"

    "Twende"

    Basi sahi na Joseph walitoka pamoja lakini ni kila mtu na gari yake,...

    Sasa wakiwa wapo njiani, sahi alipokea simu ya Mheshimiwa rais GU,

    "haloo mkuu"

    "habari yako kijana"

    "salama tu Gu"

    "vipi kazi inakwendaje"

    "nakwenda kuchukuwa dom original"

    "sawa... Angalia usije haribu mipango, wasije kukushtukia"

    "usijali mr GU"

    Mazungumzo yao hua sii ya simu ya kawaida, huwa wanatumia transmission iliounganishwa automatically katika sikio la sahi, lakini hio transmission haionekani katika sikio la sahi,...



    Sasa sahi alipokuwa barabarani, kuna gari aliiona, na anaijua hio gari, wakati huo Joseph yupo nyuma ya sahi, na sahi yupo mbele, sasa sahi kaona gari ya mama mmoja hivi anamjua vizuri,... Sasa ile gari ya yule mama ikapaki pembeni,... Sahi alishindwa kuvumilia kumpita huyo mama,.... Sasa hata Joseph pia anaijua hio gari ya huyo mama,... Lakini yeye hakutaka kusimama... Ila hofu ilimjia mr Joseph, kwanini sahi kasimama kwa ajili ya huyo mama... Mama huyo ni mke mkubwa wa General Nyange, yaani mama wa yule marehemu itwae Sharbiny,... Sasa Joseph anashangaa, huyu sahi amemjuaje huyu mama.... Sasa sahi anaharibu kila kitu,.... Lakini sasa huyu mama ndio yule alie onekana kwenye simu ya sahi, ndio huyu hapa

    "shkamoo"

    Sahi alimsalimia mama huyo, mama kwa mshtuko wa sauti ya mtu huyo alijikuta akilia mwenyewe,... Sasa swali linakuja hivi, kwanini sahi anafanana sauti na huyo kijana... Sasa je, hata huyu mama pia hamjui sahi??....

    "huyu sahi, anajuana vipi na huyu mama,... Hapana lazima nimtaarifu General Nyange, je huyu ni nani?"

    Aliongea Joseph huku akichukuwa simu yake na kutafuta jina la mr Nyange,...... Sasa sahi keshaharibu swala la kwenda kuchukuwa dom original....









    Hatimaye Dom original yapatika kirahisi sana, kumbe ile dom tuliokuwa tukiiona kwa sahi ile dom feki,.. Hivyo kwakuwa sahi ni mpelelezi japo kajiunga na watu hao sasa katika hali ya kwenda kuchukuwa dom original, wakiwa barabarani na askari mwenzie aitwaye Joseph John (JJ) sahi kina gari aliiona kitu kilichomfanya nae asimamishe gari baada ya gari hio alio iona kusimama katima sehemu za paking... Sasa kumbe hata Joseph anamjua mama huyo ambae sahi kasimamisha gari kwa ajili yake,



    Joseph aliona hili nalo ni tatizo, hivyo alichukuwa simu na kumpigia mr Nyange wa kule kambini, na mama huyo ni mke wa mr Nyange, ambae ni mkuu wa jeshi

    "haloo mkuu"

    "Enheee vp umeshaipata hio dom"

    "hapana, ndio tunaelekea huko... Lakini tupo hapa njiani tumemwona mama, ila kinachonishangaza ni kwamba mbona huyu kijana anafahamiana na mkeo ambae ni mama yake sheby"

    "ni kweli... Ila huyo pia alikuwa ni rafiki wa sheby, hata mimi huku niliona picha ya mke wangu kwenye simu yake, nikamuuliza ndio akanipa huo ukweli"

    Aliongea mr Nyange na ni kweli hata kule kambini sahi aliulizwa kuhusiana na hio picha katika simu yake, je wana mahusiano gani na mama huyo, na sahi alijibu vizuri tu.. Basi Joseph akawa kaupata ukweli kuwa kumbe nae huyu alikuwa rafiki yake, lakini Joseph bado haamini amini kwasababu yeye ndie rafiki mkubwa wa sahi, na anamjua sahi hakuwa na rafiki mwingine zaifi yake, sasa iweje leo ana rafiki mwingine...

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog