Search This Blog

Thursday 24 November 2022

RATIFA & MWAJUMA - 5

 

     

     

     

    Chombezo : Ratifa Na Mwajuma Season 1

    Sehemu Ya Tano (5)

     



    “hivi wee mtoto unakichaa nini?"

    Baba mkwe aliniuliza huku akiziokota zile risasi na kuzitia mfukoni akainuka kunifata, aliweza kuipata jeuli hiyo baada kuwaona sijui vijana wake au

    Mademu zake wakiwa wamefika hapo hospital.

    Sikuogopa wala nini ndio kwanza nikamsogelea, aliponifikia akataka kunipiga kibao nikawai kuudaka mkono wake na kumsukumiza

    Akadondoka chini kama mzigo. Hakika nilikuwa na akili za usiku hivi kama kweli namuhitaji Mwajuma mbona napambana na wakwe zangu.

    Kikundi cha wale vijana wakaja mbio kutaka kunipiga nikageuka kuwatizama kina

    Meja niliwaona nao wakiinuka nikawapa ishara watulie niwaonyeshe Show ambayo

    Mara nyingi tunaonaga kwenye video ikifanywa na

    Wachina, Wazungu ama Wajapani

    ikiwa kama niekti tu. Vijana wale waliponifikia mmoja akajianda kunipiga ngumi nilikwepa na kuzunguka kisha nikakimbia

    sio kama niliwaogopa sikutaka kupigana kwenye eneo la Jeshi maana hizi ni kesi zingine. Nilikimbia mpaka soko jipya lililopo Kawe huku nyuma majamaa yakinifata kwa kasi.

    Nikatokezea viwanja vya Tanganyika

    Pekasi nikaruka ukuta na kuingia ndani. Nao wakafanya hivyo, nikasimama na kujisemea

    sasa hapa nafinya kuku mmoja mmoja.

    Nikakunja ngumi

    “hahahaha hivi wee Dogo wa kutukunjia ngumi sisi

    bila shaka ufahamu sisi ni nani

    tena imekuwa vizuri umejileta huku sehemu ambayo tushachimba kaburi lako. Umeliona lile pale!"

    Aliongea mmoja wao na kunifanya nigeuze kichwa kuangalia hilo kaburi kumbe ilikuwa ni janja yake tu.

    Nikashtuka nikipigwa ngumi za haraka haraka zilizonipata usoni na kifuani nikayumba na kudondoka chini

    Kabla sijainuka nikainuliwa na kupigwa vifuti vya mbavuni huku nikisindikizwa na viwiko vya mgongo.

    Ndani ya dakika tano mwanaume nikadebweda na kulala chini damu zikinitoka mdomoni na puani.

    Sijui nimechanika mdomo au vipi maana nilijisikia maumivu makari sana.

    “Inuka sasa ukunje tena ngumi shoga mkubwa wee!"

    Aliongea yule Jamaa na kunikanyaga kichwani na Buti lake sijui la Mgambo au vipi akanisinya kwa kunikandamiza chini ya mchanga,

    Nilitamani kina Kaunda wangekuwepo wanisaidia lakini si niliwaambia watulie tu.

    “Hafidhi acha upumbavu mjukuu wangu unawaache Mbwa kama hawa wakutawale inuka upambane sisi tunasubiria damu zao!"

    Sauti ya Bibi ikanifanya niinuke kwa kasi niliachia ngumi kwa yule jamaa aliyekuwa kanikanyaga nilimrusha mita kadhaa akajibamiza kwenye ukuta na kutulia kimyaa. Wenzake wakashangaa na kunivamia nilikuwa nakwepa makombora yao sijui mateke ngumi mwingine akavua mkanda wa Suruwali anikabe nao, vumbi lilitimka ndani ya Viwanja hivyo na kuwafanya wapita njia na wafanya

    Biashara ndogo ndogo katika maeneo hayo wajazane kuangalia show ya bure.

    Ndani ya dakika kumi niliwazimisha wote

    hakuna aliyeweza kunyanyuka nikarudi zangu hospitali

    Nikiwa mzima sina hata Arama ya kuguswa nilimkuta

    Othman peke yake ndio amekaa kwenye benchi.

    “Vipi kaka?"

    “powa tu ndugu mbona upo peke yako kina Kaunda wako wapi?"

    “Dahaa wamekufatilia wewe ndugu kwani hujakutana nao?"

    “Sasa ningekutana nao kulikuwa na haja gani ya kuwaulizia?"

    “sawa tuachane na hayo ila Mama yako alikuwa anakwita,"

    “Othman unasema?"

    “Mama yako alikuwa anakwita Daktari alitoka na kuniambia hivyo"

    Niliingia Wodini mbiombio sikuweza kuamini aisee baada kumkuta Mama yangu akiwa amekaa kitako pale kitandani huku

    Nasra akimlisha chakula. Hata

    Madaktari walibaki na mshangao inawezekana vipi mtu aliyepigwa risasi ya kifuo apone

    Siku hiyohiyo yote ni miujiza yake Mola

    “Mama!"

    “Abee mwanangu afadhali umekuja"

    “Mama umzima kabisa? Umepona?"

    Nilimuuliza maswali na kumshika begani

    “Hafidhi mwanangu vipi ushaenda

    Kibaha kuchukuwa dawa?"

    “mmh! Mama"

    “mama nini nijibu ushaenda au laa?"

    “sasa Mama ningeenda muda gani wakati yametokea majanga kama haya!"

    “basi nenda sasa hivi kwani hali

    ya ndugu zake Baba yako si nzuri,"

    Sikutaka mjadara nikatoka wodini na kumkuta Othmani akiwa anachezea simu yake nikampita bila kumsemesha

    “samahani kijana bila shaka wewe ndio Hafidhi j Ikram?"

    Lilikuwa ni swali kutoka kwa Daktari nikaitikia ndio Mimi akaniambia basi kuna binti anahitaji kukuona humu wodini. Nikaingia na kumkuta

    Mwajuma amekaa kitako

    huku akinyweshwa sijui uji au

    maziwa na Mama yake pia alikuwepo

    Baba yake

    “whaoo baby huyoo afadhali umekuja maana nilikuwa na kimuhemuhe cha kutaka kukuona.

    Embu uninyweshe uji my love!"

    Mwajuma aliongea na kuchukuwa bakuri la uji yani niliwaona wakwe zangu wamekunja sura kwa hasira

    Wakaangalia pembeni

    Mwanaume nikaenda kukaa kalibu na

    Mwajuma na kulipokea Bakuri kwa mbwembwe zote maana niligwida funda mbili

    “ohoo wee mtoto basi utamaliza uji wa mgonjwa huo!"

    Mama mkwe aliongea huku kainua shingo utasema

    Kuku kishingo Mumewe akatabasamu

    Basi nilifanya vituko Mara nijambe

    nijifanye Daktari

    Mwajuma alicheka mbavu hana

    Wakwe nao wasicheke mchezo mi zinga la

    Comedian nikakumbuka kauli ya

    Mama nikatoka baada kumuaga

    Mwajuma nilianza safari ya kuelekea Ubungo ilipo

    stendi ya Magari ya Kibaha.

    Nikiwa ndani ya Daladala ya Ubungo nimekaa kwenye siti ya peke

    Kumbe konda alikuwa akinidai nauli sasa kutokana na msongo wa mawazo niliokuwa nao sikumuona wala kusikia vile Visenti vyake akivitingisha kama muuza Karanga kwenye kikapu akaniangalia anavyojua yeye na kumwambia

    Dereva wake kuwa kuna mijitu inajifanya vipofu ili wasidaiwe nauli wapande bure sasa

    Wapenda vitonga kama hawa wavunjiwe mayai viza kwenye makalio,

    Dereva akauliza bwege gani asietaka kulipa nauli usawa wenyewe huu wa Magu, nikaonyeshwa Mimi

    Nilikuja kushtuka nikikunjwa na kunyanyuliwa juu juu na pandikizi la Baba sijui hata alipandia wapi na kwanini anikunje vile

    “Si mnamuona huyu Kenge kumbe anaona ehee?"

    Aliongea Konda na kunifanya nishangae kwani nani alimwambia mimi kipofu

    “oyaa Brother tafadhali nishushe kwanza kisa nini mpaka unikunje"

    Niliongea kwa jaziba huku nikining'ia

    Wakati kichwa changu kikiwa nnje maana kwa ndani ya Gari asingeweza kuninyanyua mi mrefu kidogo

    Nikajikuta nasachiwa na Binti mmoja hivi

    “kumbe pesa anazo si hizi hapa kupenda Vitonga tu Mwanaume

    Mzima,"

    Nikaona uboya huu nilipeleka miguu yangu ikagusa kwenye

    Mlango wa Gari nikajishtua kwa kudunda ndipo yule

    Mbaba akaniachia nilidunda tena na kuachia mateke

    Ya uso huku nikimtembezea ngumi za chembe

    Nikaruka na kumdaka yule Binti nilimuwasha makofi yasiokuwa na idadi akaenda chini

    Chali

    Nikamgeukia Konda na Dereva wake wasikimbie na kuliacha gari mchezo

    Nikazunguka upande wa Dereva nikapanda na kutia gia nilichochea moto mpaka Ubungo hiyo Mawasiliano nikaipaki na kushuka

    Kuna baadhi ya abilia wakabaki kujiuliza Mimi ni mtu wa aina gani mbona nimefanya jambo la kishujaa kama lile.

    Basi niliweza kwenda Kibaha nikapata dawa na kuipeleka

    Nyumbani kwa Baba mdogo, huku

    Mama na Mwajuma wakiruhusiwa kutoka hospitali,

    Zilipita siku kama tatu tokea tukio lile litokee huku kijana ambaye

    alimgonga yule Afande kisha kwenda kuiboa nyumba ya

    Mfanyabiashara maarufu hapa nchini

    Mpaka sasa jeshi la polisi wapo katika kufanya uchunguzi ili waweze kumnasa huyo

    Mtuhumiwa. Nilipoisikia taarifa hiyo

    Nilicheka kwa dharau maana ni sawa na kukitafuta kivuli chako wakati unakiona sema unashindwa kukikamata

    Sharifa akazidi kumsumbua mama akitaka

    kuongea nami kila wakati mpaka siku

    Ambayo nikamuelekeza nyumbani

    akasema atakuja kesho yake

    niandae chumba tu kwani atakaa kwangu wiki nzima

    “hapana huwezi kulala nyumbani kwa dizaini hiyo wakati unafahamu fika naishi kwenye nyumba ya wazazi wangu!"

    Nilimjibu Sharifa na kumtaka afute wazo lake

    la kutaka kuja kukaa nyumbani kama anakuja kusalimia sawa sio kulala

    “sawa isiwe kesi basi tafuta Guest yeyote nzuri

    tukajichimbie huko wiki nzima tukiponda raha malipo yote juu yangu,"

    Kwanza nilikaa kimya nikifikilia kwenda kukaa Guest wiki nzima si mchezo

    “Hafidhi mbona upo kimya niambie basi"

    “Sharifa naomba unisikilize kama unahitaji penzi nitakupa lakini sio mpaka tulale usiku

    kucha kwahilo siko tayari"

    “Kweli umenichoka kama hutaki basi ila tambua kitu kimoja Mimi sio Mwanamke wa kunichezea kisha uniache hivi hivi!"

    Sharifa aliongea kwa hasira na kukata simu nilijuta kumuelekeza nyumbani

    kitu kingine nilimtamani tu haja zote nilizimaliza kulekule Kilwa kiwawa kwenye Vichaka

    ndio maana alipokuja mjini na kuanza kunitafuta

    Sikuhitaji kuonana nae

    Sasa nishampa ramani ya nyumbani

    Kisha kanitisha itakuwaje





    Kitendo cha Sharifa kuniambia yeye sio Mwanamke wa kumchezea kisha nimuache kilinifanya niwe na mawazo kwa kiasi kikubwa, niliwaza na kuwazua

    Mwishoe usingizi ukanipitia nikiwa nimekaa kwenye sofa pale sebuleni. Nilikuja kushtuka sijui

    saa ngapi baada kuamshwa na Mama

    “Hafidhi mwanangu,

    “naamu"

    Niliitikia kiuvivu huku nikifumbua macho na kuyafumba.

    “kuna msiba Baba yako Mdogo amefariki jioni hii"

    “Mungu wangu mama unasema?"

    Niligutuka na kukaa kitako pale kwenye sofa na kumuuliza mama haliyakuwa nimemkazia

    macho.

    “Ndio hivyo Muhammed hatupo nae tena"

    Mama alinijibu na kuanza kulia basi tukawa na kazi ya kubembelezana tu, kiukweli Baba Mdogo alikuwa ni mtu mbaya kwetu alishawai kumwagia

    Maji ya chooni pamoja na kumpiga Mama yangu.

    kipindi hicho Mimi nilikuwa bado mdogo

    ukazuka ugomvi mkubwa baina yake na Baba kwani baba alitaka kumuua Mdogo wake baada kupewa hizo taarifa. Kama isingekuwa ndugu kuingilia kati leo hii tungeongea mengine lakini ndio hivyo

    Mdogo mtu kamfata kaka yake huko alipokwenda,

    hatukuwa na jinsi tena ya kulala nyumbani kwa usiku ule tukajiandaa kwenda msibani kulala

    Matanga.

    Tulipofika msibani mke wa marehemu aliponiona Mimi ndio akazidisha kilio nikaenda kumkumbatia huku nami mchozi ukinitoka

    Nilikumbuka vyema jinsi mwanamke huyu alivyokuwa na roho nzuri juu yangu aliweza kuninunulia baadhi ya mahitaji muhimu kipindi nasoma shule ya msingi.

    Nikawa nikifika nyumbani kwake iwe asubuhi mchana au usiku lazima aniandalie chakula nikipendacho. Hakika alitokea kunipenda mpaka ikafikia hatua alikuwa akiniita mpenzi

    tukawa tukitoka kwenda sehemu mbalimbali

    Mikadi beach

    Coco beach Lidars na kwingineko hakika alinipenda kupita kiasi mpaka Baba Mdogo akaanza kuchukia nahisi ndio kisa cha kuanzisha bifu na Mama,

    kuna siku Ba Mdogo alirudi nyumbani kwake akiwa amelewa sana na kutukuta Mimi na mkewe tukiwa tunalishana chakula,

    Akatuangalia bila kuitikia salamu zetu japokuwa mimi nilimuamkia kama Mara mbili hivi na mkewe akamuuliza za huko mume wangu.

    Akabaki kimya na kuelekea chumbani

    “sasa mpenzi wacha kwanza nikamuandalie maji ya kuoga Baba yako wewe endelea kula tu,"

    Mama Mdogo akaingia chumbani dakika si nyingi nilianza kusikia sauti ya mtu akipigwa huku ikiambatana na sauti ya Ma Mdogo akilia

    Nilinyata mpaka mlangoni na kusikiliza

    Niliweza kumsikia Ba Mdogo akitoa onyo

    “sasa chagua moja nikupe talaka

    Uwende kijijini kwenu ukalime mikonge au huyu Mjusi kenge asikanyage tena nyumbani kwangu

    haiwezekani Mimi uniwekee vinyama viwili wakati natafuta kwa jasho langu. Alafu yule bwege unamjazia tu minofu kila siku

    Anang'ang'ania tu nyumbani kwangu

    sasa kwa taarifa yako siku nyingine nikimkuta nitawachinja wote mafala nyie eti Ma Mdogo sijui mwanangu kumbe mtu na bwanaake

    hivi wewe Emmy wakutembea na mtoto wa kaka yangu Mimi tambua yule ni damu yangu

    Baba yake kaniachia ziwa Mimi leo hii aisee kudadeki!"

    Baba Mdogo aliongea kwa hasira na kuendelea kumpiga Ma Mdogo Emmy ndipo niliweza kufahamu kitendo cha kuitana sijui wapenzi mara anilishe chakula kilimuuma sana

    Ba Mdogo niliondoka kimya kimya tokea siku hiyo sikuweza kukanyaga kwa Ba Mdogo hata nilipokuwa nikikutana na Ma Mdogo popote pale nilikatisha njia nyingine ili kumkwepa bifu

    letu baina yangu na Ba Mdogo likaendelea tukikutana tunatupiana maneno tu, mara ya mwisho

    Alikuja na Shangazi kwa nia ya kumuua Mama kama isingekuwa uwezo niliopewa na Bibi mama nae tungemzika.

    Nilikumbuka kila kitu nikiwa nimekumbatiana na Ma Mdogo Emmy basi ndugu wengine walikuja kutubembeleza nikaenda kukaa kwenye mkeka

    “pole sana kijana"

    “Asante"

    Niliitikia pole hiyo pasipo kumuangalia huyo anaenipa pole ni nani, kwani nilipoisikia sauti yake nilishamtambua

    “unajuwa kifo bwana ni kitu cha ajabu sana, kifo ni siri nzito iliyofichikana hakuna aijuae hiyo siri

    zaidi ya Allah pekee kupitia kifo

    Binadamu tumeweza kufahamu uwepo wake Muumba wa mbingu na aridhi. Lait kama kungekuwa hakuna kifo leo hii binadamu tusingeweza kuishi kwa hofu ya kumuogopa Muumba wetu, japokuwa wapo Wanadamu wasiokuwa na hofu hata chembe

    ila kifo ni Mawaiza tosha kwa yule mwenye kuhitaji kukumbuka,"

    Nilimsikiliza vizuri Shekhe Ally kwa jinsi alivyokuwa akinihutubia maana niliacha Madrasa aliyokuwa akisomesha yeye kipindi tukimwita Hostadhi Ally leo hii amekuwa Shekhe mkuu na Imamu wa msikiti wa

    Mitaa ya kwetu

    “Shukrani Shekhe wangu kwa darasa lako"

    Nilitoa shukrani na kunyanyuka nilipiga hatua kuelekea ndani ambako kulikuwa na vilio na vicheko kama ujuavyo kwenye msiba sio watu

    wote watalia wengie watahuzunika kwa muda tu

    Kisha watacheka kama kawaida. Nilipoingia

    ndani nikaitwa na Shangazi

    Mdogo yani huyu ndio kitinda mimba.

    Kiumri tupo sawa sema kanizidi miezi mitano tu

    “Assalam alaykum yaa qhairat,"

    “embu niamkie bwana Mimi hizo salamu za kiarabu sizifahamu nini maana yake!"

    “Shangazi bwana embu nikufafanulie kuhusu umuhimu wa hii salamu.

    Miongoni mwa Fadhila ambazo Mwenyezi Mungu katufadhilisha sisi Waislamu umati huu wa bwana Mtume

    Ni mamkizi yetu tunayo amkiana sisi kwa sisi.

    Kwanza katika faida Kubwa ya mamkizi yetu ni Dua hua twaombeana sisi kwa sisi,

    Kisha ni amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake katusisitiza Umuhimu wake ,

    lakini sisi tunaipuuza na ni hasara kwetu wenyewe kwa kupuuza haya maamkizi.

    “tokea lini Hafidhi nikamuamkia mtu wee itikia tu kama hufahamu ndio basi tena,"

    Nilimwambia Shangazi huku nikitabasamu na kutaka kuondoka akanishika mkono na kunivuta

    “sasa mbona unataka kuondoka kabla sijakwambia nilichokuitia?"

    “niambie basi mi nataka kwenda kulala"

    “wee nawe unataka kulala kwani ushakula?"

    “hapana sijala sema sijisikii kula"

    “Hafidhi mwanangu kuna siri nzito sana nahitaji kukufichulia leo hii ni siri ambayo nimekaa nayo

    tokea udogoni"

    Shangazi aliongea kwa sauti ya chini.

    “lakini kabla sijakueleza chochote niahidi mwanangu kuwa siri hii utoweza kuitoa kwa yeyote mpaka siku ya kufa kwako!"

    Nilikaa kimya pasipo kujibu chochote

    “nijibu basi wala usiogope!"

    “ndio nakuahidi ewe Shangazi yangu"

    “nilikuwa nataka nikwambie kuhusu kifo cha Baba yako kuna watu wamehusika na hilo

    Swala ukihitaji uzibitisho shika hii

    Flashback utaona kila kitu please nakuomba usiitoe siri hii usalama wa maisha yangu upo mikononi mwako,"

    Shangazi aliongea huku akianza kutetemeka nilichukuwa ile Flashback na kuiweka mfukoni

    Nikamshika Shangazi na kumkumbatia alianza kulia

    kilio ambacho kilinizibua masikio kuwa

    kumbe kifo cha Baba yangu kilipangwa na watu kitu gani aliwakosea watu hao mpaka kufikia hatua ya

    kumuua.

    Sasa kila aliyehusika atajuta Wallahi tena nilijisemea moyoni mwangu. Tukaenda kuchukuwa chakula na kuanza kula

    “si ulisema usiku huu hujisikii kula imekuwaje unakula tena?"

    “sio nakula tena ndio kwanza Sahani ya kwanza, unajuwa nini

    Shangazi kuna msemo unasema hivi ukila cha mwenzako au usile lakini tambua cha

    Kwako kitakuja kuliwa pia,"

    “Unamaanisha nini kutoa msemo huo?"

    “kama unakumbuka siku ya msiba wa Baba huyu Ba Mdogo alikula sahani tatu za Ubwabwa leo hii tunakula cha kwake,"

    “ha!ha!ha!ha! Hapo nimekupata yani ukizika nawe utazikwa si ndio ehee?"

    “ndio maana yake"

    Niliweza kuongea na Shangazi sijui mpaka saa ngapi nikaenda chooni kujisaidia wakati natoka

    Nikakutana na Gogisu

    “hee wee vipi mbona umekuja bila taarifa?"

    “samahani mkuu ila nimekuja hapa niweze kukuaga,"

    “Uniage kwani unaenda wapi?"

    “Naenda mbali sana"

    “mbali wapi au hakuna jina?"

    “Ndio mkuu hakuna jina ila ni mbali sana nasikitika kukaa mbali na mkuu wangu sema sina jinsi niende huko,"

    “Gogisu!"

    “Rabeka mkuu"

    “si ulisema Mimi ndio mkuu wako?"

    “ndio mkuu"

    “sasa mbona unataka kuondoka bila ruhusa yangu? Nahiyo sehemu unaenda kufanya nini?"

    “Nimeitwa na Bibi yako kwenda kumsaidia kazi moja nzito sana,"

    Basi sikuwa na jinsi kumtakia safari njema

    Akanitolea heshima zote na kupotea nilitafuta sehemu ambayo naweza nikalala

    “Nasra naomba shuka!"

    “wee vipi kwani umeambiwa Mimi nagawa mashuka hapa!"

    “Ugawe usigawe naomba shuka nikalale!"

    “kama sina je?"

    “Hauna kivipi wakati hiyo hapo umeikalia"

    “Sasa hii si nimefanya kama tandiko hii nyingine ndio najifunika,"

    “Si ulale kwenye mkeka embu nipe hiyo shuka!"

    Nililazimisha utasema shuka yangu.

    “haya shika hii lione bichwa kama

    Madenge"

    Nilicheka kwa kauli ya Dada nikaenda kulala sema sikuweza kupata usingizi mapema

    Mawazo yalianza kunisonga niliwaza mambo mengi sana hasa kuhusu hii

    Flashback aliyonipatia Shangazi na kusema kuna siri nzito yenye kuhusu kifo cha Baba

    Nilitamani nirudi nyumbani niweze kuitazama.

    Pia niliwaza kuondoka kwa Gogisu kumbe ukimya wa Bibi umetokana na kwenda hiyo sehemu

    Ya mbali sana usingizi ukanipitia.

    Kesho yake Asubuhi nilishtushwa na kelele za watu wakilia safari hii vilio vilizidi

    “Kaka Hafidhi embu inuka ukaone huku!"

    Nasra alikuja mbio akilia na kunishika mkono

    Na kunitaka niinuke niliutoa mkono wangu

    Huku nikipiga kelele

    “niachie bwana kwani nimekwambia siwezi kunyanyuka!"

    “Wamemuua Shangazi Sabrina hiiiiiiii.

    Weee Mungu eheeee mbona unatupunguza sisi tu

    Baba Mdogo hatujamzika leo hii umemchukuwa

    Shangazi!"

    Nilimshika Nasra na kumtikisa

    “Nasraa unasemajee unaongea nini? Mbona sikuelewi ewe ndugu yangu?"

    Nikamuachia na kutoka mbio kuelekea sehemu ambayo kuna watu walikuwa wamejazana.

    Nikafunga break ya ghafla miguu ikawa

    mizito kunyanyua hata hatua moja mbele ama kurudi nyuma. Nilibaki kutoa macho pima

    Kuuangalia mwili wa Shangazi Sabrina ukining'inia kwenye kitanzi.

    Nilianza kulia kama mtoto Mdogo hakika lilikuwa pigo juu ya pigo huku Ba Mdogo kule Shangazi. Nilishindwa hata kunyanyuka nilianza kutambaa kusogea sehemu ambayo

    Mwili wa Sabrina ulikuwa umelazwa baada kushushwa kutoka juu ya Kitanzi

    “Hihihihihihaakhaaa, Shangazi embu fumbua macho niambie nani kakutendea hivi nijibu aisee, Shangazi fumbua macho!!!

    Nilipiga kelele huku nikimtikisa nikaja kushikwa na kina Kaunda maana waliambiwa wafanye hivyo kwani polisi washafika.

    “Ok niacheni kwanza"

    Niliongea kwa sauti ya upole wakaniachia nikajiweka sawa na kujisachi mfukoni

    Mungu wangu Flashback sikuwa nayo nilijisachi kila mfuko sikuweza kuiona nikaenda mbio sehemu ambayo nilikuwa nimelala nilitafuta hakuna kitu

    Nikarudi eneo ambalo nilianza kutambaa tafuta tafuta na wewe flashback haipo. Nilipiga kelele kwa hasira

    “Mamaaaaweeeeee!!!

    Watu waliniona kama vile nishakuwa chizi kweli nina haki ya kuwa hivyo,

    Hatimae tulienda kuzika mtu na Dada yake walizikwa siku moja tena kalibu na kaburi la kaka yao

    “Inna lillah wainna ilahi rajiun"





    “Takbir hahahahaha takbir tehe!tehe!tehe!"

    Walikuwa ni baadhi ya marafiki zake marehemu Ba Mdogo wakiwa wamelewa vibaya mno wakawa wakipiga Takbira huku wakicheka ni kitendo ambacho kiliniuzi mno niliwaangalia kwa hasira sema wakati huo Shekhe Ally alikuwa akitoa

    Khutuba kidogo baada miili kufukiwa.

    “Ndugu zangu Waislamu naomba tufahamu kitu kimoja kifo ni kitu ambacho hakuna kiumbe

    Ambacho ataweza kukimbia awe tajili au masikini.

    Leo hii tumeweza kuwapumzisha wenzetu

    kuna maswali wataulizwa leo hii

    Labda niwaambie kuhusu maswali hayo pamoja na majibu yake,"

    “Oyaa acha kuzingua hakuna cha maswali wala majibu kwanza wewe umejuaje uliwahi kuingia nini?

    Alafu nyie Mashekhe ubwabwa mna mbwembwe

    utasema wazee wa kanisa wenye kununua

    Papal kwa bei ya shilling mia tano kesho yake anawadanganya waumini

    Eti hili papai nimebarikiwa na Bwana ukilipata hili papai basi bwana atakubariki katika maisha yako yote. Waumini wakisikia hivyo wataanza kuligombea matokeo yake Papai la mia tano linauzwa

    Laki mbili, kwanza sisi njaa zinatuuma

    Oyiii masela twenzetuni!"

    Aliongea mmoja kati ya wale marafiki wa Ba Mdogo kisha wakaondoka pasipo kusuburia Dua

    “Shekhe unaweza kuendelea"

    Nilimwambia Shekhe Ally aliyekuwa amekaa kimya akiangalia jinsi kikundi cha watu wakiondoka.

    Tukabaki watu wachache tu.

    “Maswali watakayo ulizwa ndugu zetu waliotangulia mbele ya haki. Hata mimi na wewe tutaulizwa

    Utaulizwa: Man Rabbuka?

    Mola wako ni nani?

    Utajibu: Allahu Rabbi. Mwenyezi Mungu ni Mola wangu.

    Utaulizwa: Man Nabiyyuka?

    Ni nani Nabii wako?

    Jibu: Muhammadun Nabiyyi. Muhammad ni mtume wangu

    Utaulizwa: Ma Dinuka? Dini yako ni ipi ?

    Jibu: Al-Islamu Dini. dini yangu ni Uislamu

    Utaulizwa: Man Imamuka? Ni nani Imamu wako?

    Jibu: Al Qur'an Imami. Imamu wangu ni Al -Qur'an

    Utaulizwa: Aina Qiblatuka? Iko wapi Qibla chako?

    Jibu: Al-Ka'batu Qiblati. Qibla changu ni Ka'aba

    Utaulizwa: Man Ikhwanuka? ndugu zako wakina nani?

    Jibu: Al-muslimun Wal Muslimat Ikhwani. Muislamu mwanaume na Muislamu mwaanamke wote ni ndugu zangu

    Majibu ni rahisi sana?

    Lakini, sisi je tuna uwezo wa kujibu kwa urahisi?

    Wakati mwili wetu umelazwa chini ya tumbo la ardhi.

    Wakati kuna giza kinene, utakuwa na hofu.

    mwili unatetemeka.

    Ambapo hakuna mtu anayeweza kusaidia.

    Ndiyo, Hakuna mtu ambaye anaweza kutusaidia.

    Ni matendo yako mema uliyoyafanya katika maisha ya duniani ndio yatakusaidia.

    Astaghfirullahal 'Adzim. Utusamehe Ya Allah Sisi ni watumishi wako daima tunafanya dhambi na uovu tusamehe

    Ya Allah.Turuhusu sisi, daima milele kutafuta Maghfirah yako na baraka zako ..

    Tuonyeshe njia kuelekea mwanga wa nuru. Utuongoe kwenye njia iliyo nyooka. Hivyo Usitufanye sisi kama wale waliopotea.

    Aamiin yaa Rabbal 'Aalamiin

    ya Allah Tafadhali ya Allah tusaidia wote na utukinge na adhabu yako ya moto wa Jahannam na utupe pepo yako ya Jannatul Firdaus. Aamiin Yaa Rabbal 'Aalamiin

    Shekhe alimaliza kila kitu tukaitikia

    “Aamin"

    Na kufuta nyuso zetu kwa viganja vya mikono tukarudi nyumbani, njia nzima Mwanaume nikipanga ni jinsi gani nitawafundisha adabu hawa Mbwa walioleta Dharau kule makaburini ndani ya usiku huu nitawaonyesha kuwa Mungu yupo.

    Sikupitia msibani nilienda moja kwa moja

    Nyumbani na nilipofika nikaingia ndani na kukaa kwenye sofa

    “Shangazi kwanini ulikubari kuhatarisha maisha yako juu ya swala hili? Shangazi ni bora ungekaa kimya usingeniambia chochote kuhusu jambo hilo.

    Shangazi je flashback ulinipatia kweli au uliichukuwa?

    Shangazi hao watu ni kina nani na wanataka nini katika familia yetu? Angalia sasa umeondoka na kuniacha njia panda sijui wapi pa kuanzia!"

    Niliongea huku machozi yakinitoka nikiwa naendelea kuongea huku nikilia nikasikia

    Mlango wa uwani ukigongwa nikainuka

    pasipo kuitikia ile hodi nikajifuta machozi na kwenda kufungua mlango

    “Whaoo Bibi huyoo, khaa bibi umekuja,"

    Mgeni mwenyewe alikuwa ni bibi mzaa Mama kutoka Kilwa kiwawa nilifurahi sana tena sana nikihisi sasa matatizo yangu yote yata kwisha.

    nikaingia nae chumbani kwangu kwakuwa kulikuwa na joto nikamuashia feni

    “Assalamu alaykum yaa Jaddat..."

    “Mmh ndio nini?"

    “si nakusalimia ewe bibi yangu"

    “Sitaki salamu hizo embu nisalimie kilugha chetu"

    “Bibi bwana mi sijui"

    “Ha!ha!ha!ha na lazima usahau maana hujaja Kilwa takribani miaka sita sasa kwanini usisahau. Haya vipi huyu Mwanangu kaelekea wapi?"

    Nilishangazwa sana na kauli ya Bibi kusema kuwa sijaenda Kilwa Takribani miaka sita

    Wakati ndani ya mwaka huuhuu nilienda au sababu nilikaa siku mbili tu ndio maana anasema hivyo.

    “Ahaa Mama yupo msibani"

    “msiba wa nani tena?"

    “Baba Mdogo Muhammed na Shangazi Sabrina wamefariki"

    Nilimjibu bibi akaonekana kama kufikilia kitu hivi kisha akaniuliza

    “Unataka kusema Sabirina yule aliyekuja kipindi kile?"

    Kiukweli bibi kuita Sabrina hawezi Mara nyingi alikuwa akiita Sabirina ndivyo alivyo uliza.

    “ehee ndio huyo!"

    “Mungu wangu wee alikuwa akisumbuliwa na nini?

    “Maralia"

    Nilimjibu kimkato sikutaka kumwambia kuwa amenyongwa nikifahamu hata yeye anafahamu kuhusu kifo cha Ba Mdogo ni kutokana na kuadhibiwa kwa Bakora za Gogisu kumbe niwazavyo Mimi sivyo. Nilenda msibani kumwita mama hakika Mama na Nasra walifurahi sana kusikia Bibi amekuja tukaongozana mpaka nyumbani mtu na

    Mwanae walikumbatiana kwa furaha.

    “haya mizigo ya mkeo iko wapi?"

    “Ipo chumbani kwangu hapa nasubiria muda nikalale na mke wangu!"

    “hahahaha"

    Basi tulicheka si kidogo.

    “Aka sitaki mume gani umenisusa miaka sita sasa hujaja kuniona mpaka Mimi nifunge safari ndio ujidae Mke wangu. Kwa taarifa yako unitafuni ng'oo!"

    Bibi alianza kukataa eti ataki kulala na Mimi

    Si unajua matani ya Bibi kwa mjukuu wake wa Kiume

    “Lakini Mama mumeo si alikuja miezi mitatu iliyopita"

    “Aje wapi?"

    “si Kilwa au vipi?"

    “hajaja bwana mbona Mimi sijamuona,"

    Bibi akakataa kuwa sijaenda Kilwa ni kitu kilicho tushangaza sana hasa Mama akaniangalia kwa sekunde kadhaa akaichukuwa simu yake iliyokuwa ikiita. Na kusema

    “whaoo mkwe wangu huyo anapiga simu!"

    “Mkweo yupi?"

    Niliuliza kwa taharuki huku nikimsogelea Mama

    Akaipokea na kuongea

    “Halloo mwanangu kipenzi hujambo?"

    “sijambo shikamoo Mama"

    “Marhabaa mwanangu vipi kwema huko?"

    “kwema tu vipi mume wangu upo nae hapo?"

    “hapana sipo nae,"

    “Mamaaa"

    Alikuwa ni Ratifa ndiye aliyepiga simu na kuniulizia ajabu mama kamjibu eti sipo nikaita hivyo

    “Mama nini embu tulia niongee na mwanangu mie"

    “Ha!ha!ha!ha! Mama bwana mbona nimeisikia sauti ya mume wangu hapo?"

    Ratifa alicheka na kuuliza

    “Ahaa kumbe huyu bichwa maji ndio mumeo basi yupo hapa, haya shika simu uongee na mtoto mzuri!"

    Mama alimjibu kwa kuniita bichwa maji kisha akanipatia simu

    “mbona mnanipa pulesha tena?"

    “Bibi bwana sio pulesha sema Plesha"

    Nasra akamkosoa bibi

    “Embu toka zako kwanza ushapata mume?"

    “Apate mume wapi mtu mwenyewe Nunga Yembe"

    Nilidakia kujibu na kumfanya Ratifa acheke na kuniambia niache ugomvi

    “Mama umemsikia mwanao ananiita Mimi nunga yembe ehee"

    “Hivi hii mitoto yako haijaacha kugombana tu?"

    “Wamuachie nani kila kukicha ugomvi yani ikipita siku mbili bila kusikia wakitupiana maneno mbona nitanenepa

    Jana tu walikuwa wakigombea shuka kule msibani"

    Mama akamjibu Bibi nikaenda Chumbani kwangu niweze kuongea na Ratifa maana pale

    Sebuleni kuna kelele balaa"

    Niliongea kama nusu saa hivi na kuniambia niende nyumbani kwao nikajitambulishe pamoja na kupeleka barua ya posa. Nikamwambia asijali ndani ya mwezi ujao kama sio Mwanzoni basi mwishoni nitafanya hivyo. Nikakata simu na kuirudisha kwa Mama ile Namkabidhi tu

    Mesegi ikaingia ya Tigo pesa

    “Asante mkwe kwa kunijali"

    Ratifa alikuwa katuma kiasi cha pesa tsh..laki moja na Tisini elfu

    “Mama hiyo pesa yakwangu nilimwambia anitumie!"

    “Embu kwenda zako soma Mesegi hii!"

    Nikaishika simu na kuisoma hiyo Mesegi

    “Nafahamu ni kiasi kidogo sana nilichokutumia ewe Mama yangu sema naomba ukipokee kitakusaidia kwa siku mbili tatu ni Mimi mkweo Ratifa.

    Nilimaliza kuisoma ile Mesegi na kusonya.

    Nikaenda chumbani kwangu kulala sio kama nilichukia kitendo cha Ratifa kumtumia pesa Mama hapana bali kudeka kwangu tu.

    Nikiwa kitandani nikakumbuka kukana kwa Bibi kuwa Mimi sijaenda Kilwa miezi mitatu iliyopita. Tena amekataa mbele ya Mama inakuwaje hii mwishoe nikatabasamu baada kukumbuka ndani ya usiku huu atakuja kunifata tu hapo ndipo nitakapo

    Muuliza sababu ya kukataa kwake.

    Yapata majira ya saa saba usiku Mwanaume nilikuwa bado sijapitiwa na usingizi nikainuka na kuongea Kilugha cha Kijjini kisha nikapotea na kuibukia Tabata Makuburi nilitembea kwa mwendo wa haraka njiani niliweza kushuhudia Mambo mengi sana hasa vitimbi vya Wachawi na Wanga wakiwachezea watu vile watakavyo wao yani walikuwa wakicheka mbavu hawana nikajisemea

    Naenda hivi ole wenu saa ya kurudi niwakute mtaisoma number

    Mabwege nyie.

    Safari yangu nilikuwa nikimfata mmoja kati ya watu walioleta mambo ya Mzaha kule Makaburini

    Je nini kitaendelea?"





    Hatimae niliweza kufika sehemu husika. Nyumba ilikuwa imezungushiwa uzio, nikajiuliza nipitie getini au niruke ukuta? Nilipiga mahesabu mwishoe nikachupa na kurukia ndani

    Nilitua taratiibu bila kishindo niliangaza macho huku na kule nikaanza kutembea kwa kuambaa na ukuta. Huku nikijificha kwenye Mauwa

    Nilishtushwa na sauti za mbwa wakibweka kwa ukali siku zote mbwa ana uwezo wa kuona viumbe ambavyo haviwezi kuonekana kwa macho ya kawaida. Kwa binadamu, kumbe wakati naingia tu walishaniona wakaanza kubweka ikiwa kama njia moja wapo ya kunitisha na kunitaka niondoke.

    Nilisimama na kuwaangalia mbwa wale

    Kuna kitu nilikifanya mbwa wakanyamaza na kutulia kimya kwa kukaa chini.

    Hakika nilikuwa Nina kila aina ya mbinu za kijasusi kitendo cha kuwatuliza mbwa ni moja kati ya mbinu tosha kwa maadui zako.

    Nilisogea hadi kwenye mlango mkubwa wa kuingilia ndani nikaingia pasipo kugusa chochote na kuwaacha mbwa wamepigwa na butwaa. Nilipoingia ndani ya nyumba hiyo nikapiga mahesabu wapi kilipo chumba cha huyu bwege

    Nikapandisha ngazi na kutokezea kwenye korido. Niliangaza macho na kuhisi chumba ambacho kilikuwa upande wa kushoto nikaingia chumbani

    Kwanza nilisimama baada kuona kitu ambacho si ruhusa kwa watoto kuangalia

    kikifanyika pale kitandani alikuwa ni. Mlengwa wangu akimsurubu binti fulani hivi ambaye sikuwai kumuona kabla mzee wangu akaanza kugonga hodi kwenye Zipu ya suruwali utasema anaona?

    Nilisimama kwa muda nikiangalia jinsi binti alivyokuwa akijituma kwa kukatika viuno baada kuukalia mtalimbo wa Mzee yule

    “Ohooooo,,,,,asssssssmmmmmaaaa

    aaaahapooo,,,,haaaaaaaa"

    “Stumai"

    “Abee Babaaassssssuwiiiiii"

    “usiniite baba sema mpenzi,"

    “ahaaaa,,,,mpenziiiiusiiiiiii",

    Binti alikuwa akiongea kwa sauti ya kukatakata yote kutokana na kuzidiwa kwa utamu. Nilikaa pembeni nikisubiria wamalize nianze kazi yangu japo kuwa nilikuwa naumia mtalimbo wangu ulituna mpaka nikahisi misuri inataka kukatika. Nilifumba macho kwa muda lakini haikusaidia kitu

    Binti alikuwa akitoa vilio vya ajabu usimpimie

    “Nitakuongeza mshahara Mara tatu iwapo utakubari ombi langu,"

    “whao nitafurahi sana niombe tu mpenzi"

    “nataka unipe nyuma nasikia kutamu sana embu nipe nionje!"

    “hapana mpenzi kwahilo sipo tayari kwanza kufanya huku ni dhambi pili utanifanya nipate shida wakati wa kujifungua. Tatu

    utaniumiza na kunifanya nijambe hovyo,"

    “wewe nani amekwambia uwongo huo hakuna kitu kama hicho embu badirisha line hiyo!"

    Nilibaki kujiuliza kwanini Wanaume wengi wanapenda kuwaingilia kinyume na maumbile

    Wake zao aidha wapenzi wao

    nini shida nini tatizo je starehe ya muda mfupi ndio ikufanye uteseke

    Chembechembe za mavi zikiingia kwenye kitobo cha mkojo njia ikaziba nini kitatokea juu yako

    Unatamani vipi kupita njia ambayo Mungu ameikataza amuna hofu nyinyi?

    Nilijiuliza huku Binti yule baada kupewa maneno matamu na ahadi za kununuliwa sijui nyumba na

    Gari akikubari akakaa vizuri

    Kwa kujipanua makalio yake ilibidi nitoke kwanza nnje.

    Nisione ushetani huo.

    “mamaaaaa,,uuuuh,,aaaah,,mungu wangu,,aaaagh,,weweeee,,mmaaaa

    maaaa!!!

    Zilikuwa sio kelele za mautamu bali ni kutokana na maumivu makali aliyohisi Binti huyo baada kukubari kutoa tigo.

    “Okhgoo,,,,pole sana baby shika hii kama kianzio"

    Nilimsikia yule mzee akiongea sekunde si nyingi Mlango ukafunguliwa akatoka

    Mlengwa wangu niliyekuwa nikimsubiria kwa hamu kabla ya kutoka akaangalia kushoto na kulia kisha akaanza kunyata kuelekea chumbani kwake

    Kumbe kile chumbe kilikuwa cha house girl.

    Nami nikawa namnyatia kwa nyuma alipoingia tu chumbani kwake nikamtokezea kufumba na kufumbua nilimpiga ngumi ya uso akayumba na kupiga kelele nikamshika na kupotea nae.

    Nilimpeleka Baharini nilimpa mateso ya ajabu huku nikimsisitizia kuwa Mungu yupo

    “Nisamehe nipe walau dakika moja nitubu madhambi yangu tafathali usiniuwe,,"

    Alilia kama mtoto Mdogo

    “sawa nimeweza kusikia kilio chako

    unapewa huo muda ole wako uwende kinyume utajuta!"

    Niliongea kwa sauti ya ukali nikashika mshipa wa fahamu . Nikamzimisha na kumtupa.

    Nikamuacha kulekule ufukweni mi nikasepa.

    Kesho yake Asubuhi na mapema kama kawaida yangu nilienda beach kufanya mazoezi

    Nikarudi nyumbani

    “Hafidhi mwanangu yani umenidanganya mpaka Mimi mama yako,"

    “nimekudanganya kitu gani?"

    “uliniaga unaenda Kilwa kwa bibi yako nikajitolea kukupa nauli nikakupa na Vitenge sijui Kanga

    nikifahamu unaenda kweli Kilwa kumbe mwenzako una yako,"

    “Mama bwana hivi unamsikiliza bibi wakati akili yake haina akili. Mimi nilienda Kilwa tena wale kuku alinipa yeye mwenyewe Bibi sasa iweje aseme hivyo!"

    Niliongea nikiwa nishaanza kukasirika maana huyu bibi anataka kunizingua.

    “Hafidhi naomba utambuwe kitu kimoja uwongo ni dhambi niambie ukweli tu ulienda wapi?

    Kama kweli ungeenda Kilwa Kiwawa usingerudi kwa haraka vile. Yani siku mbili tu

    Ukarudi kweli!"

    Mama alianza kuja juu kwa kuongea kwa sauti nikatoka nnje na kumkuta bibi akimsaidia

    Nasra kukaanga Bagia sikutaka hata salamu nikaanza kumuuliza

    “Hivi bibi uko serious?"

    Akaniangalia pasipo kuongea neno lolote kisha akauliza

    “Siko Sirozo kwani vipi?"

    Nilitabasamu baada bibi kusema sirozo akimaanisha Serious japokuwa nilikuwa na hasira.

    “Bibi eti umesema Mimi sijaja Kilwa wakati nilikuja wakati nikiwa njiani nilikimbizwa na Simba

    nilifika nyumbani kwako mbiombio mpaka

    Babu na Wajomba zangu wakamfatilia huyo Simba hukumbuki tu?"

    Niliongea haraka haraka nikiwa nahema

    “Mmh kiukweli hukuja Kilwa labda ulikuwa ndotoni kama Mimi muongo mbona Mama yako kaongea na babu yako kamuuliza nae akajibu hujaja,"

    “Bibi acha kunichanganya sasa subiri nikwambie kitu kimoja wewe ni Mchawi!"

    “Mtumee wee Hafidhi mjukuu wangu Mimi ni nani?"

    “ehee wewe ni Mchawi haiwezekani Mimi nije Kilwa useme sikuja hivi sio wewe uliokuwa ukinitokea kila siku Usiku na kuniomba nije Kilwa

    kuchukuwa kitambaa kwenye mbuyu? Nijibu kama sio wewe kumbe ni nani? Unajifanya humjui

    Gogisu si ndio ehee?"

    Niliamua kumwaga mchele kwenye Kuku wengi ilibidi mama anishike na kuniingiza ndani

    Maana majirani walishaanza kujazana wakitaka kufahamu nagombana na nani mbona naongea kwa sauti. Bibi nae akaingia ndani na kuomba mizigo yake

    “Rehema mwanangu nisamehe Mimi mama yako wala huna haja ya kumuadhibu mwanao.

    Muache tu cha umuhimu nipatie mizigo yangu nirudi nyumbani kwangu"

    Bibi aliongea hivyo wakati huo mama alikuwa akinichapa Bakora za matako,

    “hapana Mama usiseme hivyo usiondoke,"

    Mama alilia na kumpigia magoti mama yake.

    Hakika ya shetani ni mbaya sana Asubuhi hiyo kaingia ndani ya nyumba yetu na kufanya ndugu tugombane

    Tukiwa ndani Nasra akaomba afunguliwe mlango

    basi akafunguliwa hakuingia peke yake

    Alikuwa kaongozana na Shekhe Ally sijui alienda kumwita au alimpigia simu.

    “Assalam aleykum Warahamatulah wabarakatu.

    Kasema Allah mtukufu katika Suratil Shuura aya ya kumi na tano basi kwa haya waite nawe simama sawa sawa kama ulivyo amrishwa ,wala usiyafuate matamanio yao. Na sema naamini aliyo teremsha Allah mtukufu katika vitabu .na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu .Allah Mtukufu ni Mola wetu

    Mlezi.

    Hafidhi kijana wangu nini shida?"

    Shekhe Ally alisalimia na kutoa khutuba kidogo.

    Nilimuangalia kwanza mama nikamtazama bibi Mara Dada mwishoe nikamaliza kwa Shekhe Ally yani niliwatizama kwa zamu,

    “Hafidhi mwanangu tafadhali tuambie kila kitu wala usiogope Mama yako nipo hapa!"

    Sikuwa na jinsi kuanza kusimulia nilisimulia mwanzo mwisho sema kuna baadhi ya mambo nilificha. Kwanza sikutaka kujitaja Mimi nimekuwa nani zaidi ya kumalizia kwa kusema

    Hiyo ndio sababu iliyonifanya nimwite bibi

    Mchawi.

    “Mungu wangu wee inamaana Hafidhi unaniona Mimi ndio nakutokea na kukuchukuwa?"

    “ndiyo!"

    “hapana si kweli bila shaka kutakuwa na kitu hapo Wallah Mimi sio mchawi nawala sijawahi kuwa na tabia hiyo tafadhali Shekhe niaguwe

    niondolee hivyo vitu mwilini mwangu!"

    Bibi aliongea huku akilia na kwenda kupiga magoti mbele ya Shekhe

    Basi Shekhe Ally alianza kusoma kwa sauti ya chini

    ?????? ???????? ????????????? ??????????

    ???? ? ?????? ?????? ?????????? ? ????????? ??????? ???????? ??? ???????? ???????? ??????????? ???????? ???????? ??? ???????????? ? } kila dakika akazidisha sauti mwishoe akanyamaza na kusema





    Baada Shekhe kumaliza kusoma akasema

    “ndugu zanguni hakika ya hili jambo ni zito kwa kiasi kikubwa maana, linahitaji kutazamwa kiumakini sana. Sasa wacha Mimi niende

    Kesho Allah akijaalia naweza kuja na majibu yote. Tuseme Insha Allah!"

    “Insha Allah"

    Wote tukatamka hivyo Shekhe akaaga na kuondoka nami nikatoka na kuelekea maskani kiukweli sikuwa sawa kabisa nilikuwa nikitembea kwa kujivuta utasema mfungwa aliyefungwa minyororo asiweze kukimbia. Nilikaa chini na kushika kichwa

    Nilianza kuwaza hatua moja mpaka nyingine mwishoe niliinuka na kugeuza nirudi nyumbani. Sikuweza kufika maskani siku hiyo nilijifungia chumbani kwangu kimyaa

    “Hafidhi embu fungua mlango chakula tayari"

    Nilimsikia mama akiniambia hivyo

    Sema sikutaka kula chochote kwa siku hiyo kwani tokea Asubuhi sikutia chochote kitu tumboni mwangu kwanza hiyo hamu ya kula itoke wapi

    katika majanga kama haya. Mama akazidi kugonga mlango nikamsikia na bibi nae akiniita yani sauti yake ni ileile aliyokuwa akiniitia usiku pindi anaponitokea.

    “nimeshiba nyie nendeni mkale tu!"

    “umeshiba kitu gani wakati hujala chochote basi fungua mlango,"

    “mimi ndio mwenye tumbo nishasema nimeshiba

    Sitaki kula mbona mnanilazimisha nyie watu vipi!"

    Niling'aka kwa hasira ndipo wakaondoka. Mara nikamsikia Nasra akiniita na kusema

    “kaka simu yako hii wifi Ratifa anapiga,"

    Nilifungua mlango kumbe ilikuwa danganya toto nilikutana na mama akiwa kashika sahani ya ubwabwa

    “haya shika kwanza chakula ule kisha utaongea na huyo Ratifa"

    “mama bwana si nilikwambia mimi nimeshiba,"

    Niliongea huku nikiipokea sahani kiukweli nilikuwa na njaa mpaka nikahisi utumbo unauma kwa kunyongorota.

    “kumbe sitaki nataka ehee wee jifanye kususa utakuja kufa

    Shauri yako, kwanza nilikuwa nakivizia hiko chakula nimpelekee Sheby,"

    Nasra aliniambia huku akining'ong'a nilimuangalia kwa jicho kali mpaka mwenyewe akajistukia na kuondoka nikarudi chumbani.

    Ilipotimia saa sita usiku mwanaume nilihitaji

    kutoka ili nianze upelelezi wangu nilitaka kufahamu kila kitu na kwakuanzia niliingia chumbani kwa Nasra ambapo bibi ndio analala.

    Nilimkuta kauchapa usingizi mwenyewe anakoroma. Nikasimama pembeni ya kitanda na kuanza kumwita

    “Bibi,bibi hamka bibi hakika mkuu wako nimekuja kukuamsha hamka twende kazini!"

    Niliongea kwa sauti ya chini sana. Lakini bibi hakuamka nikapata wazo la ghafla kama itawezekana ndani ya Usiku huu nifunge safari

    Mpaka Kilwa kiwawa, sikutaka kutafakari sana niliongea Yale maneno na kuweka nia kufumba na kufumbua nilijikuta nikisafiri kwa kasi ya upepo

    Nilikata mawimbi na miamba huku nikipita katikati ya Jangwa. Kila nilipopita nilitimua vumbi hakika ilikuwa ni safari ndefu kidogo mpaka nikaingiwa na hofu kuwa nitashindwa kurudi kwa usiku ule.

    Nikaingia Kilwa na kukuta kila aina ya vibwanga asikwambie mtu vijijini kuna mambo usione watu wanabanana mijini ukadhani wanapenda kuishi Mjini na kulalamika maisha magumu kumbe wamekimbia Vijijini hakufai kuna kila aina ya Uchawi, niliangaza macho kuangalia Wazee wa vijiji wakioneshana mambo, huyu ajigeuze Simba

    yule ajigeuze Yanga Mara Azam yani ilikuwa vurugu mechi wakati wanakijiji wamelala. Kwakuwa sio rengo nililojia nikapiga hatua za haraka kuelekea sehemu ambayo kuna Mbuyu kwa mara ya kwanza nilipokuja nilikuta kitambaa chekundu nikaambiwa nikichukuwe.

    “Nani wewee,"

    Sauti nzito ilisikika nyuma yangu ikiniuliza. Niligeuka kwa kujiamini na kumuangalia huyo anaeniuliza hivyo ni nani. Kumbe walikuwa ni wale wazee.

    “mimi ni mkuu wenu"

    “Ha!ha!ha!ha! Mkuu wetu kivipi na umetokea wapi?"

    Walianza kucheka kutokana na jibu langu kisha nikaulizwa swali. Nikajitambulisha ajabu wakasema Mimi sio mkuu wao dakika si nyingi akafika huyo mkuu wao. Kila mmoja akapiga magoti kumsujudia Astaqhafirullah yani binadamu anasujudiwa hatari hii.

    Nilipigwa na bumbuwazi baada yule mkuu wao kugeuka na kuniangalia Mimi sikuweza kuamini Aisee ni bibi

    “kijana unaitwa nani? na umetokea wapi?"

    Nilitamani hata kucheka yani bibi ananiuliza mi nani ujinga huu sema cha ajabu sauti yake ilikuwa ya kiume.

    “kijana nijibu haraka kwani sijaja hapa kupoteza muda!"

    “Sina haja ya kujitambulisha Mimi ni nani wakati ushanifahamu kitu kingine sihitaji kuchezewa michezo ya kitoto kwanza Gogisu yuko wapi?"

    Niliongea huku nikimfata na kumuulizia Gogisu

    “Vijana embu mkamateni huyo mjinga anataka kutupanda kichwani tambua hii ni himaya ya Mzee Mkalipa tutakunywa damu yako leo!"

    Alitoa vitisho pamoja na kuamrisha nikamatwe bila kutambua wanafanya makosa makubwa sana kutaka kunishika Mimi Ghafla kuna kiumbe kilikuwa kikija kwa kasi

    Kutokea juu huku akitema moto. Uliowapata baadhi ya wazee wakaaza kupiga kelele kwa maumivu na kukimbia hata bibi nae alipotea eneo zima nilibaki peke yangu

    Huku kile kiumbe kikitua chini kwa kishindo alikuwa ni Gogisu nilishangaa sana kumuona wakati aliniaga anaenda mbali sana sehemu ambayo ameitwa na bibi.

    “Gogisu ni wewe mbona umerudi ghafla?"

    “Hapana mkuu Mimi sio Gogisu"

    Alinijibu yule kiumbe huku akipiga magoti mbele yangu"

    “Khaa! Mara hii umesahau jina lako ehee haya niambie unajiita nani?"

    “Kiukweli mkuu Mimi naitwa Figisu yani

    Gogisu ni kaka yangu yeye ametumwa katika sayari ya Mars

    Atakaa huko kwa kipindi kirefu kidogo,"

    Nilimuangalia huyu kiumbe ndipo nikapata picha sio Gogisu

    Nilimuangalia kwa muda huyu kiumbe

    Kisha nikamuuliza

    “Sawa Gogis,,,,ahaa Figisu na imekuwa ni vizuri sana umeweza kuja je naweza kukuuliza chochote utanijibu?"

    “ndio mkuu lakini kabla hujauliza naomba nikujibu maswali yako yote!"

    “khaa! Sasa utanijibu vipi wakati sijakuuliza chochote?"

    “Nafahamu kile ambacho unataka kuniuliza ndio maana nikaona haina haja ya wewe kuusumbua mdomo wako kuuliza hayo maswali,"

    Hakika Figisu alinifanya nistaajabu sana kutokana na yale maneno yake inawezekana vipi

    Kujibu maswali kabla ya kuuliza. Sema sikuwa na jinsi kumpa ruhusa afanye hivyo tukatafuta sehemu tulivu na kukaa

    “haya nijibu hatua kwa hatua"

    “usijali mkuu kwanza kabisa yule umuonae kama Bibi yako kiukweli kabisa sio mwenyewe

    Labda nikupe historia kwa ufupi maana nikikusimulia kwa urefu tunaweza kukaa hapa kwa mwezi mzima stori itakuwa bado kuisha.

    Katika karne ya Kumi na sita tokea Mungu alipoumba ulimwengu na viumbe vyote

    vilivyopo katika ulimwengu huu. Kila kiumbe kilihishi kwa raha mustarehe kulikuwa hakuna shida ya aina yeyote ile, mpaka siku ambayo alikuja kuumbwa kiumbe mwingine ambaye ni jamii ya

    Binadamu. Tokea kuumbwa kwake na kukosea baadhi ya mambo na kupishana kauli na

    Mkuu wetu tukajiwekea kisasi ndani ya mioyo yetu

    Tulianza kupambana usiku na mchana

    Lakini binadamu yule alikuwa na nguvu za ajabu kila tukikutana kwenye vita anatushinda

    Ndipo siku moja mkuu wetu aliota ndoto kuwa katika mwaka elfu moja na tisini na moja

    Atazaliwa mtoto mwenye spanachi ya ajabu kupitia mtoto huyo ndiyo mtaweza kupambana na

    Jeshi la Wanadamu yani ikabidi tukae tukiomba zaidi ya karne Elfu moja iweze kufika kijana huyo

    Azaliwe ajabu alipozaliwa tukamkosa japokuwa tuliweza kupandikiza mbigu zetu kwa huyo

    Mtoto tukasubiri miaka mingine

    Ndipo ukazaliwa wewe tukakusubiria ukuwe tukukabidhi jeshi

    Ndipo tukatumia kivuli cha bibi yako baada kutambua hauna nguvu yeyote ya kupambana pia kuna mabinti unawapenda, siku uliyokuja kuchukuwa kitambaa hukufikia kwa bibi yako

    Ulifikia katika familia ya Majinni

    Hata yule binti uliyekutana nae na ukafanya nae mapenzi nae ni Jinni,"

    “Mungu wangu na Mtume!"

    Nilishtuka si kidogo na kutamka hivyo

    Figisu akatabasamu na kuniambia usiogope mkuu.

    “Unataka kusema Sharifa ni Jinni sio?

    Je na yule Somowe?

    Na kwanini mnichaguwe Mimi wakati mimi ni kutokea jamii ya maadui zenu?"

    Niliuliza maswali mfurulizo nikitegemea kupata majibu kwa wakati mmoja

    “Ndio mkuu wale wote ni Majinni

    Kuhusu kukuchaguwa wewe nishakueleza una

    Spanachi yetu ipo kifuani kwako

    Baada yule Hafidhi j Ikram wa kwanza kumkosa ikahamia kwako!"

    “sasa itakuwaje inamaana mnataka niuwe binadamu wenzangu sio?"

    “Hapana sio hivyo tunataka kuwaangamiza wale wote wenye kufanya makosa au kwenda kinyume na Muumba wetu, kwani hata sisi miongoni mwetu kuna maadui wenye kuwatumia

    Binadamu ndivyo sivyo. Mkuu mi naenda ukiwa na shida yeyote niite nipo hapa kukaimu nafasi ya

    Gogisu"

    Alipoongea hivyo akapotea.

    Je nini kitaendelea?"







    Nipo hapa kukaimu nafasi ya Gogisu"

    Baada yule kiumbe kuongea hivyo akapotea sikutaka kujiaminisha sana maneno yake

    Nilinyanyuka na kuelekea kule Mbuyuni niliweza kufika nikasogea na kuutaza ule

    Mbuyu kiumakini sana ndani ya usiku mnene mwanaume nipo katikati ya msitu. Tena mbali na nyumbani. Ni sauti za wanyama wakilia ndizo zilizoweza kusikika,

    Nikauzunguka ule mbuyu na kuelekea nyumbani kwa bibi ajabu nilipofika nilikuta pori tu.

    Hakuna cha nyumba wala mashamba sijui nimepotea njia au vipi? Nilijiuliza kichwani mwangu sema sikutaka kukata tamaa nilizidi kuitafuta nyumba ya bibi. Hatimae nilifanikiwa kuiona ipo

    Kule kijijini na wala sio kule Mashambani, hapo ndipo nilipoamini kila kitu kweli bibi ana haki ya kusema vile. Kwakuwa muda ulikuwa umeyoyoma sana

    Nikaanza safari ya kurudi nyumbani

    Nilifika nyumbani yapata saa kumi na moja alfajir

    Nikapanda kitandani na kulala.

    Nilikuja kuamka sijui saa ngapi maana hata mazoezini sikuweza kwenda

    nilitoka nnje nikamsalimia

    Bibi pamoja na Mama sema Nasra nilimkaushia

    “wee bichwa Mimi unajifanya hunioni ehee?"

    Sikumjibu kitu nikaingia kwanza chooni baada hapo nilijiswafi Mama akaniagiza niende

    Kisevule kuchukuwa mzigo wake kwa Mama

    Komwe ambaye alikuwa ni jirani yetu sema kahama kitambo kidogo kwakuwa siku aliyohama nami nilikuwa mmoja kati ya vijana tuliomsaidia kupakiza Vitu kwenye Gari kisha nikaenda mpaka

    Huko Kisevule kushusha vitu.

    Basi nilijiandaa kwa safari hiyo nilitaka niende kwa upepo nikasita yani Asubuhi yote hii kunaelekea mchana sasa nikataka kwenda kuchukuwa

    Bajaji yangu ambayo nimemuachia Kaunda yani sikumbuki hata mapato yake anakabidhiwa nani.

    Nikaona wacha nipande Daladala tu.

    Niliweza kufika mpaka Kisevule nilipokelewa kwa furaha sana na Mama yake Komwe

    “ohoo karibu sana mwanangu naona siku hizi umekuwa bonge la baba!"

    Nilitabasamu kwa maneno yale. Basi nilikaa kwenye kiti nikaandaliwa chakula cha mchana niweze kula

    “Hivi Komwe yuko wapi?"

    “yupo kazini"

    “ahaa kumbe siku hizi kakubari kufanya kazi maana kipindi kile alikuwa hataki kufanya kazi yeyote ile,"

    “ndiyo hivyo mwenzako kapata mtoto wa Kisukuma basi hapumui kutwa kucha anahangaika kutafuta pesa tu!"

    “Basi ongera yake,"

    Niliongea nae mambo mengi sana mama yake Komwe hatimae Niliaga na kuondoka nikiwa njiani naelekea Stendi nikamuona Binti mrembo wa haja mapigo yangu ya moyo yakaanza kwenda kasi

    Nilijikuta namtamani ghafla tu. Sijui nikoje mimi

    Basi nilipiga hatua za haraka kumfata nilipomfikia nikamtolea salamu

    “dada mambo vipi?"

    “ahaa safi tu"

    Nae akaitikia huku tukipeana viganja vya mikono nilimuuliza jina lake na anaishi wapi. Hakuwa mwepesi kunijibu zaidi ya kuondoka

    na kutembea harakaraka kama vile mtu

    Aliyeona kitu cha hatari. Kwakuwa nilikuwa namuhitaji kwa udi na uvumba sikuwa na budi kumfatilia nyumanyuma

    Tulitembea umbali mrefu kidogo tukikata mitaa na kuingia kichochoro hiki tukitokea kile

    Tulifika sehemu moja hivi kulikuwa na mafundi

    Seremala yule Binti akasimama na kumsogelea jamaa mmoja sijui aliongea nae nini

    Ghafla nilishuhudia yule binti akipigwa kibao cha shavuni vua ya makonde ikamuangukia yule

    Binti alilia kwa maumivu akadondoka chini lakini jamaa hakuacha kumpiga

    Nilibaki kujiuliza binti mrembo kama yule

    kafanya kosa gani mpaka anapigwa namna ile.

    Kuna kijana alijitokeza kutaka kumsaidia yule

    Binti cha ajabu mafundi wote

    Wakaanza kumshamburia yule kijana, walimpiga

    vibaya mno nikasogea katikati ya umati wa watu uliokuwa umejazana. Niliweza kumsikia Mama mmoja akisema

    Siku zote hawa Black Mamba wanajifanya hii Kisevule wao ndio wababe

    ipo siku yao Mungu atasikia kilio chetu

    Juzi wamenipigia Binti yangu kisha wakambaka

    leo hii yupo hospitali hajiwezi kwa lolote!"

    Aliongea mama yule na kuangua kilio

    Nikaingiza mkono mfukoni na kutoa kitambaa

    Nikajifunga usoni.

    Sijui hata nilipenya vipi kwenye umati ule nilijikuta naseleleka tu na kwenda kumchota mtama jamaa mmoja nilimrusha juu kimo cha

    Mbuzi huku nikimshika mwingine nikamvuta na kumbamiza kwenye Mstimu

    nilidunda na kutua juu ya meza ambayo wanakatia

    Mbao nikaruka juu kukwepa Msumeno ambao ulikuwa unataka kukita miguuni mwangu

    Nilimuachia teke la uso jamaa ambaye alitaka kunikata Miguu

    Nakwambia nilianzisha mpambano nikifahamu wapo wachache tu kumbe wapo wengi

    Wengine walikuwa wamekaa nyuma ya ukuta wakivuta Bange vile vishindo viliwashtua na kuja mbio,

    Sema nilipambana kiume huku nikitumia zaidi

    Style ya Wushu nilikoswakoswa na nyundo ya kichwa yani jamaa alijivuta kwa nguvu zote

    Kunipiga ya kichwa nikainama ile nyundo ikapita na kwenda kutua kichwani kwa mwenzake.

    Niligeuka nyani maana nilikuwa situlii sehemu moja

    Nilikimbilia nyuma ya ukuta. Huko sasa nikamwita

    Figisu sijui alikuja kwa njia gani!

    Kwani upepo ulianza kuvuma vijana walitupwa huku na kule kwa kubamizwa kwenye ukuta

    Ndani ya dakika moja tu

    Figisu akasikika akisema

    “Nishamaliza kazi mkuu, vipi kuna nyingine?"

    “Asante ndugu kwa kazi nzuri unaweza kwenda"

    Nilimsogelea yule jamaa ambaye alikuwa akimpiga yule Mrembo nikamuinamia pale chini

    Alikuwa hajitambui kabisa nikachukuwa Msumeno na kuushika mkono ambao ulitumika kumpiga yule binti nikataka kuukata

    “huu ndiyo mkono uliotumika kumpigia mtoto wakike sio?"

    Nilimuulize huku nikiuvuta nikaushika Msumeno vizuri

    “jamani Sudy anakatwa mkono huku, tafadhali kaka yangu usifanye hivyo msamehe,"

    Alikuwa yule binti akipiga kelele na kuniomba nisifanye hivyo nikamtazama kwa sekunde kadhaa kisha nikafungua kitambaa na kumuonyesha

    Sura yangu. Sauti ya ving'ora vya magari ya polisi ndio ikanishtua

    Nikafunika kitambaa chapu nikadunda na kurukia upande mwingine wa Ukuta kisha nikapotea.

    Nikaibuka kitaa cha nyumbani. Nilipofika nyumbani nilikutana na

    Ugeni bibiye Ratifa amekuja. Aliponiona akanikimbilia na kunikumbatia

    I miss you baby"

    Ratifa aliongea huku akihitaji kugusanisha ndimi zetu sio siri Mtoto amezidi kuwa mrembo yani anang'aa utasema Dhahabu zilizowekwa kwenye chumba chenye kuangaziwa na Jua la asubuhi

    “Baby mama anatuangalia ujuwe!"

    Nilimwambia hivyo

    Ujio wa Ratifa ilikuwa ni furaha kwangu lakini nilipokea taarifa za kushtusha pia kuwa Shekhe Ally amefariki nilishangaa sana.

    “Ndio hivyo mwanangu sisi wenyewe tulikuwa hapa tukimngojea atuletee suruhisho la jana

    ndipo tukasikia vilio vikitokea nyumbani kwake kwenda kuuliza ndio tukapata taarifa hizo, amefariki ghafla alikuwa haumwi wala nini na Swala ya saa

    Saba ameswalisha yeye.

    Aliporudi nyumbani kwake akaingia chumbani kujipumzisha. Kumbe ndio ilikuwa baibai

    Mkewe akaenda kumuamsha ajiandae na swala ya saa kumi ndio akamkuta Mumewe ameshatoa

    Shahada!"

    Mama alisimulia huku machozi yakimtoka hakika lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa familia yake

    Wake zake wamebaki wajane







    Nilibaki kujiuliza kuhusu kifo cha Shekhe Ally kuwa cha ghafla vile. Sema siku zote alipangaro Mwenyezi Mungu halina makosa. Nilienda msibani usiku ule watu walikuwa kwenye matanga, niliangaza macho huku na kule sikuweza kung'amua kitu juu ya kifo cha Shekhe Ally nikarudi nyumbani na kumkuta

    Mama akiwa amekaa kwenye mkeka akiwasimulia Hadithi kina Ratifa nikapitiliza mpaka chumbani kwangu nikajilaza kitandani chali nikiwaza na kuwazua juu ya mustakabari mzima wa maisha yangu. Nilikuja kushtuliwa na sauti ya mlango wangu ukifunguliwa ilionyesha mfunguaji alikuwa akinyata. Nami nikafumba macho na kutulia huku nikifumbuwa kwa kuibia kumbe alikuwa ni Ratifa mtoto akiwa kavaa kanga moja tu kwa kujifunga rubega.

    Nikisema Rubega bila shaka mabinti wengi wananipata

    Alipiga hatua kadhaa misiri ya mtu anaetaka kupaa. Nilizidi kujikausha na kujifanya nakoroma

    Aliponifikia akakaa juu yangu akafanya kama kunikatikia hivi mwili mzima ukasisimka huku Mzee wa kujificha kwenye suruwali au boxer Akianza kutuna kwa kasi.

    Bibiye akaniinamia na kufafanya chuchu zake mchongoko zinichomechome kifuani kwangu

    Akaitoa ile kanga na kubaki mtupu kabisa hapo nilijikuta nafumbua macho utasema umeme wa tanesko umerudi ghafla.

    Nikamvamia na kuanza kuzinyonya chuchu zake

    “Assssssssssohooooooooommmmm,,

    ,,ahaaaaaaa,,,,,opsiiiiiiii,,,aaaaaaaaa Ratifa alianza kugugumia huku mtalimbo wangu ukiwa tayari ushaanza kuingia kwenye kitumbua chake kilichotuna kutokana. Akawa akiinuka kwa juu kuonyesha nisiingize yote nami nikawa namfata juujuu

    Nikimpa zile za utalijua jiji bishoo. Alianza kunikatika mwishoe kitu kikawa laini akaikalia yote ikazama pwahaaaaa

    Nisisimulie sana usije ukatumia sabuni ni hatari kwa hafya yako.

    Kutokana na shukhuri nzito niliyofanya kwa bibiye nikapitiwa na usingizi. Nikaja kushtuka yapata majira ya saa Tisa usiku nikaenda kwanza kuoga kwani katika mambo yangu nilikatazwa kuwa na Janaba Mara ya mwisho kufanya hivyo ni kule Sinza baada kumpata binti anaekwenda kwa jina la Janeth.

    Kuanzia siku hiyo nikapewa onyo nisiingie kazini nikiwa na janaba.

    Baada kuoga nilivaa na kupotea safari yangu ilinipeleka mpaka nyumbani kwa kina Mwajuma huko

    Kunduchi sehemu anbayo waliamia baada nyumba yao ya Mbezi kubomolewa.

    Nilipofika maeneo hayo nikaingia ndani na kuanza kukisaka chumba cha

    Mwajuma

    Niliweza kufahamu Mwajuma atakuwa chumba gani. Ajabu wakati naingia ndani ya chumba hiko niliweza kuona kama watu hivi wakiwa wanatoka kupitia

    Pembeni ya chumba. Sikutaka kujiuliza nami nikapitia njia ileile na kuwaona wakiwa wapo mbele yangu,

    “hivi ulimchikia akijamba wakati nilipomkalia?"

    Mmoja kati ya wale watu akauliza swali kwa kiswahili cha kimakonde eti ulimchikia wenzake badara ya kujibu wakaanguwa vicheko tu.

    “Hahahahaha

    Tehe!tehe!tehe ndio kamwene nilimchikia akijamba puhuu"

    “nyie kina nani na mmekuja kufanya nini kwa mchumbaangu?"

    Sikutaka kuwakawiza pale pale nikapaza sauti kuwauliza

    Wakaanza kubabaika pasipo kujibu kitu

    “Figisu kuja hapa nataka unifyekee hao kunguni wote"

    Nilimwita Figisu na kumpa Amri awauwe wale Wachawi kufumbu na kufumbua akawabeba wote na kuondoka nao

    Nikarudi chumbani kwa Mwajuma nilianza kutumia uwezo wangu kuondoa nguvu za Giza ambazo alikuwa amewekewa mule Chumbani. Kisha nilikaa kitandani na kumbusu kwenye paji lake la Uso nikapotea.

    Kesho yake asubuhi na mapema tuliweza kusikia taarifa ya habari ikitangaza kuwa Watu wanne wanaosadikika ni wachawi wamekutwa wamekufa baada kunasa juu ya Mbuyu,

    Miili ya watu hao ambao haijafahamika wametokea wapi imehifadhiwa katika hospitali ya Tegeta kibaoni

    Yeyote anaombwa kufika sehemu hiyo kuweza kuitambua miili hiyo.

    Nilienda msibani kwa Shekhe Ally kwani alikuwa anazikwa baada swalat Dhuhuri ya Swala ya saa saba

    Nikiwa msibani nilianza kuhisi kama vile kuna mambo sio

    Nikaongea Luga yangu na kujionea

    Viumbe wa ajabu wakiwa wametanda kila sehemu huku sauti ya Shekhe ikisikika kutokea ndani alikuwa akilia kwa maumivu

    Nikainuka na kutaka kuingia ndani.

    Nilipofika mlangoni nikazuiwa

    Na mmoja kati ya ndugu wa marehemu akinitaka nirudi nilipotoka kwani ndani kuna kisomo. Maarumu kinasomwa, wakati Mimi namsikia Shekhe akilia huku akiomba msamaha

    Nikafanya kitendo ambacho kiliwafanya wafiwa washangae kwa kumpushi yule

    Baba akayumba na kudondoka chini. Nikaingia na kusimama nikatoa macho pima

    Baada kuona vile viumbe wakiwa wanamchapa Bakora Shekhe huku wakimtaka aingie kwenye Jeneza. Hakika ilikuwa ni taswira ya kutisha sana nilikaza

    Sura na kupiga kelele

    “Muacheni!!!

    Sauti yangu ilikuwa kali mpaka watu wote walijiziba masikio. Na kufanya wengine wakimbie kwa uwoga, nikapiga hatua kuusogelea

    Mwili wa Shekhe nikaushika kichwani na kuanza kuongea maneno ya ajabu ajabu mwili ulianza kutingishika huku nikikitaka kile Kivuli ambacho kilikuwa kikichwa kije kulala juu ya Mwili wenyewe.

    Hakika duniani kuna mambo na vijimambo

    Watu wote walitoka nnje na kuchungulia ndani kwa Uwoga hakuna cha

    Hostadhi wala nani wote nnje. Unachezea kufa wewe.

    Basi kile kivuli kikaja kulala kama nilivyo kiamrisha Shekhe akapiga chafya na kuinuka akakaa kitako

    Na kuanza kujishangaa kutokana na vazi ambaro alikuwa kavishwa ni

    Sanda

    “nipo wapi hapa? Mbona nimevaa hivi?"

    “Ewe Shekhe wangu tulia kwanza"

    Nilimtaka atulie basi akatii amri nilitoka nnje na kuita baadhi ya watu lakini walikuwa waoga kunisogelea

    “Inakuwaje Mashekhe wazima kama nyie mnaoifahamu Quraan vyema mushikwe na uwoga kwa kiasi hicho embu njooni Shekhe

    Kazinduka huku!"

    Nikarudi ndani na kumtaka Shekhe anyanyuke na Avae nguo zake nilizomletea.

    Akavaa na kutoka nnje wake zake waliokuwa wakilia tokea jana hawakuweza kuamini walimkimbilia mume wao na kumkumbatia. Nilirudi nyumbani nikiwa nimechoka huku taarifa yakwamba nimeifufua Maiti zikisambaa kama umeme, kesho yake Asubuhi niliitwa msikitini kulikuwa na kisomo kizito sana juu yangu. Kisomo ambacho kiliongozwa na Shekhe Ally alisema kuwa kisa cha yeye kufanywa vile na

    Viumbe wale ni kitendo cha yeye kuwaita na kuwataka waniachie huru. Ndipo yakatokea mabishano kati yao na kufikia hatua ya kumtupia makombora. Kwakuwa alikuwa hajajiandaa kupambana nao ndio wakamdhuru

    Sasa kwakuwa wamechokoza nyuki

    Wacha wanywe Asari.

    Kijana weka ubani!"

    nikanyoosha mkono nichote ubani

    Nikasikia sauti ya bibi akilia na kunitaka nisifanye hivyo

    “Hafidhi mjukuu wangu tafadhali usifanye hivyo embu achana na huo mpango toka ndani ya hiyo nyumba!"

    Mara nikamsikia Sharifa akinisihi Nisiweke ubani Mara Gogisu akiniambia mkuu tutetee usikubari kutuangamiza nikarudisha mkono wangu nyuma nilishindwa kuchota ubani.

    “Hafidhi usiwasikilize hao wanataka kukupotosha kumbuka Allah aliposema hakika ya Shetani ni adui kwa Mwanadamu iweje wewe ukubari kuwakumbatia?"

    Nilichota ubani kwa speed ya ajabu na kutia kwenye Kigae cha moto kisomo kikaanza kila waliokuwa wakisoma ndipo kichwa changu kilianza kuniuma

    Nilijishika kichwani niliona kama msikiti ukizunguka macho yakaanza kufumba mwishoe nikapoteza fahamu.

    “Hafidhi mjukuu wangu njoo!"

    “Hapana usiende njoo kwa Shekhe wako hapa"

    Kulikuwa na mvutano baina ya bibi na Shekhe Ally kila mmoja akiniita niende upande wake huku wakitupiana Makombora mazito mazito

    Shekhe alikuwa kasimama huku kashikilia kitabu kisichokuwa na shaka yeyote ndani yake

    Akisoma kwa haraka na kufanya Bibi wa kishetani azidi kutatalika mwishoe nilikimbilia kwa Shekhe

    “Hafidhi!!!

    Niligeuka baada kuisikia sauti hiyo alikuwa ni Ratifa & Mwajuma wakiniita kwa pamoja sema nilikuwa nishafika kwa Shekhe nikawapungia mkono wa kwaheli.

    Nilikuja kuzinduka na kukuta watu

    Wamenizunguka kwa mbali nilimsikia Shekhe akisoma

    “Shekhe kijana amezinduka"

    Basi alikuja karibu yangu na kuwaambia vijana waniinue

    Nilikaa kitako tukabaki kutazamana

    “Hakika ya Allah (S.w.t) Amekutoa kwenye himaya ya viumbe wabaya

    Ja nini kitaendelea





    Baada ya kisomo

    Hafidhi alizinduka je nini kiliendelea?

    Tuwemo..........

    Shekhe Ally alinieleza mambo mengi tu huku akinitaka nijiepushe na mambo machafu. Kama vile Zinaa unywaji wa Pombe, na mengineyo mengi tu mfano wa hayo. Kwani kufanya hivyo itakuwa sababu ya Majinni wale kurudi tena kwangu. Na wakirudi hawatokuwa na Huruma watahitaji kuniangamiza tu. Nilimsikiliza Shekhe Ally mwishoe nikarudi nyumbani. Njia nzima nilibaki kujiuliza maswali chungu nzima

    Kumbe nilikuwa nikihishi kwenye himaya ya Majinni, nilifika nyumbani mama akaniuliza vipi za huko, nikampa maelezo yote

    Basi alipiga magoti chini na kumshukuru Mwenyezi Mungu,

    “Ratifa mpenzi,"

    “abee"

    “kesho au kesho kutwa nahitaji kwenda nyumbani kwenu kujitamburisha nataka nikuoe"

    “Ohoo asante Mungu wangu unasema kweli baby?"

    “Ndio maana yake kuanzia sasa navunja vitendo vyote vya Kishetani Shetani tokaa"

    “Ameen,"

    Ratifa aliitikia Ameeni ghafla akadondoka chini na kuanza kutapatapa nilishituka nikapaza sauti kumwita Mama

    “Mamaa"

    Basi alikuja chumbani kwangu mbiombio na kunikuta nimemshika Ratifa aliyekuwa akitokwa na damu masikioni puani

    Mdomoni nilizidi kumwita Ratifaaa!"

    Lakini hakuitikia zaidi ya kutupa mikono yake huku na kule mfano wa mgonjwa mwenye kifafa.

    “umemfanyia nini tena mtoto wa watu?"

    “sijamfanya kitu kadondoka mwenyewe,"

    Nilimjibu mama nikiwa natweta si kidogo hakika ilikuwa ni balaa

    “Nasraa embu kamwite Shekhe harakaa"

    Mama aliongea huku akilia nilitoka mbio kuwahi nyumbani kwa Shekhe maana niliona Nasra atachelewa nilimkuta Shekhe akila chakula cha mchana

    “Hafidhi vipi mbona hivyo unahema kijasho kinakutoka?"

    “Twende nyumbani kuna matatizo"

    Niliongea harakaharaka na kumshika mkono alikuwa hata bado hajanawa

    “tulia basi kijana ninawe kwanza kisha nichukuwe kitabu,"

    Nikaingia ndani kwake na kubeba kitabu. Yani hata sikuambiwa sema akili yangu ilikuwa ishaharibika. Kuna msemu kuwa Siku ya kufa nyani miti yote hutereza sijui wanamaanisha nini kusema hivyo.

    Tuliweza kufika nyumbani lakini tulikuta vilio nilishtuka sana dahaa

    Ratifa alikuwa kashapoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha sana. Nililia kilio ambacho nilimkufuru muumba wangu, nilitamani hata Mimi nife,

    Kulikuwa hakuna ndugu hata mmoja anaepafahamu nyumbani kwao kina Ratifa lakini kupitia simu yake tuliona number zilizoseviwa Mama, Baba na wengineo

    Tukapiga number ya baba yake ikapokelewa ilikuwa ngumu kidogo kumueleza juu ya kifo cha Binti yake.

    “Haloo Baba shikamoo"

    “Marhabaa kijana bila shaka wewe ni Hafidhi?"

    Kwa mara ya kwanza niliamkia kisha nikashangaa huyu mzee kanifahamu vipi!

    “ndio Mimi"

    “Ahaa nashukuru sana kijana kwa kuisikia sauti yako vipi huyo mwenzio hajambo?"

    Nilishindwa nimjibu nini nikaanza kulia simu nikaidondosha chini.

    Meja akaikota na kuiweka sikioni maana nilikuwa nimeweka Loudspeaker ili kuanzia Mama sijui Mjumbe wa nyumba kumi na Mwenyekiti wa Serikali za mitaa waweze kusikia maana ilikuwa ni kesi mtu kufia nyumbani kwenu ghafla vile

    Serikali haiwezi kukuelewa kiurahisi

    “Haloo mzee"

    “Ndio kijana mwambie mwenzako asilie kwa kiasi hiko hakika Ratifa ni mbishi

    Tulimwambia asiende jijini Dar es Salaam tena kwani mizimu ya kwetu imekasirika. Yeye akabisha Masikini ya Mungu binti yanguu naomba mniletee mwili wake Stendi ya Bukoba

    Nitalipa gharama zote, hiiiiiiii"

    Kauli ya Baba yake Ratifa ilimshangaza kila mtu eti kachukuliwa na mizimu ya kwao. Nilitamani kuwa na uwezo wangu ili nikapambane nao. Lakini sikuwa nao kama yale Maneno sikukumbuka hata moja. Kwakuwa kila mtu alikuwa kasikia kauli ya baba mzazi. Siku hiyo tulilala matanga Usiku nikiwa nimelala nikasikia sauti ya binti akilia kwa uchungu nikafumbua macho kuangalia alikuwa ni Mwajuma nae kaja msibani sijui nani kampa taarifa.

    Nilinyanyuka na kumfata aliponiona nae akaja mbio kunikumbatia tuliangua vilio utasema watoto wadogo. Tukawa na kazi ya kubembelezana mpaka tukatulia Mwili wa marehemu Ulichukuliwa tokea mchana kwenda kufanyiwa uchunguzi nini kilichomuua majibu yakaja eti kilichosababisha kifo cha ni Mshituko, inawezekana ikawa hivyo kuwa aliona kitu kibaya au Alishtushwa na kauli yangu ya kumwambia kuwa nataka kumuoa. Sema yote kwa yote tumuachie Mwenyezi Mungu ndio mpangaji wa yote. Pia kauli ya Baba yake izingatiwe. Ndani ya usiku huo

    Zilifanyika taratibu zote kama kuchangishana pesa juu ya kupata usafiri ambao utabeba Mwili wa marehemu na baadhi ya Majirani,

    Mwajuma akasema haina haja ya kuchangishana kama usafiri wa kwenda na kurudi upo tujiandae tu kwa safari. Saa kumi na moja Alfajir tulikuwa tupo Kibaha kwa Mfipa tukijaza mafuta Gari tatu Daladala aina ya Coaster, hakika safari ilikuwa ndefu asikwambie mtu.

    “Jamani niwaambie kitu hii safari inaweza kutuchukuwa hata siku mbili au Tatu kuweza kufika Bukoba

    Maana ni mbali"

    Aliongea dereva. Na kunifanya nishtuka nikataka kupinga kwa kusema mbona Mimi nilikuja usiku na nikaondoka usiku huo huo iweje Gari ishindwe kufika haraka sema nilinyamaza baada kugundua Yale mambo yangu ni

    Yenye nguvu kubwa,

    “Sasa kama hivyo mwili wa marehemu si utaharibika!"

    Nilijikuta nikiongea hivyo

    “Lakini Athumani si ungesema tokea kule msibani ili tuchukuwe ndege ya kukodi"

    Mwajuma aliongea na kufanya watu tukenue meno baada kusikia

    Ndege usafiri ambao

    Kuna watu tokea anazaliwa Utoto wake ujana wake, utu uzima

    Uzeeni mpaka anakufa hajawahi kupanda, sasa sisi

    Kusikia ndege mbona Bahati hii lakini ndiyo tulikuwa mbali na jiji la Dar Es Salaam, baada safari ndefu tuliweza kuwasili

    Bukoba majira ya saa

    Tatu usiku tuliwakuta ndugu na jamaa wakitusubiria kwa bamu mwili uliposhushwa tu

    Ukaswaliwa na kwenda kuzikwa usiku uleule

    “hivi mzee unamaanisha nini kusema vile"

    Baada mazishi kesho yake nilimfata Baba yake Ratifa na kumuuliza.

    Akaniangalia kwa dakika kadhaa na kunijibu neno moja tu kuwa ni Mira

    Zao

    “nini maana ya Mira niweke wazi mzee?"

    Kijana punguza hasira nafahamu fika kuwa una machungu makubwa sana moyoni mwako. Kuliko hata sisi wazazi wake. Lakini hatuna jinsi ya kukubaliana na kile kilichotokea. Kwani sisi wote tutarejea kwenye Udongo, Kila nafsi itaonja umauti,"

    Nilitamani nimtie ngumi ya Uso huyu mzee sema nikaminya nikakumbuka kauli ya

    Shekhe Ally kuwa kama nikinywa pombe au kuzini, basi

    Majinni yatanirudia nikaona njia pekee ni kumuingilia Mwajuma nilimfata na kumuomba tutafute sehemu tuweze kuzungumza.

    Kupitia Vijana wa maeneo hayo niliweza kupata chumba kwenye Guest bubu

    “Baby unataka kufanya nini bwana"

    “Embu acha utoto tufanye kimoko tu mwenzako Nina ugwadu"

    “si usubiri tukirudi Dar mwenzako sijisikii vizuri ukicheki tumekuja kwenye msiba itakuwa sio tabia nzuri ahaa,"

    Mwajuma akalalamika nikaona anazingua tu nilitaka kumbaka sema nikaona sio freshi.

    Nikainuka na kuelekea mlangoni nikiwa nimekasirika

    “Sasa unaenda wapi?"

    “Naenda kutafuta Malaya wa kukata kiu yangu wee si unajiona keki kisa umebaki peke yako,"

    Nilimjibu na kufungua mlango.

    “Baby sio hivyo haya basi njoo ufanyee"

    Niligeuka mbio na kuruka kitandani

    Nilivua nguo harakaraka yani sikufanya hata maandalizi nikamvua Chupi na kumchomeka

    “Babiiiiiiii,,,,taratiiiibu,unaniumizaaaa,,,,

    asssssss,,,

    Kiukweli nilikuwa nafosi tu mautundu yangu yote niliweka pembeni

    Nikazidi kumpampu huku nikilinyonya ziwa lake la kulia utamu raha

    Ghafla Ratifa akaibuka chumbani mule na kutufanya wote tushituke.





    Hakika tulishtuka sana tukabaki kukodoa macho kumuangalia Ratifa aliyekuwa kasimama mlangoni. Sema kwa upande wangu sikuwa na hofu kiviile. Yote sababu ya kuwa nimezoea sana kuona viumbe vya ajabu wenye kutisha. Mfano wa Gogisu, sembuse huyu Ratifa katujia katika vazi lake la Sanda,

    Mwajuma ndiyo akazidi kutetemeka, akajishika kichwa sijui kilikuwa kikimuuma au vipi? Mwishoe akawa kimyaa. niliuchomoa mtalimbo wangu uliokuwa umesinyaa ghafla. Na kuanza kumtikisa Mwajuma huku nikimwita

    “Mwajumaa, tafadhali fumbua macho,"

    “Kwasasa hawezi kufumbua macho mpaka nitake Mimi. Hafidhi usitake kujifanya hunioni, naona hujali lolote juu ya ujio wangu. Wakati umeniita mwenyewe sasa basi

    Niambie ulichoniitia!"

    Ratifa aliongea huku maneno yake yakijirudia ndani ya chumba kile.

    “mimi sijakwita"

    “sawa hujaniita wacha mi niende"

    Baada kusema vile Ratifa akapotea huku Mwajuma akifumbua macho na kuniita

    “baby"

    “naamu"

    “kichwa kinaniuma please nipeleke nyumbani"

    Mwajuma aliongea kwa sauti ya upole utasema yupo usingizini. Basi tukatoka na kurudi msibani.

    Kesho yake Alfajir na mapema tukaingia kwenye Magari na kuiyanza safari ya kurudi jijini Dar es Salaam na kuiacha Bukoba, safari ilikuwa ndefu kama tulivyoenda ndivyo ilivyokuwa saa ya kurudi. Sema tulitumia siku moja na nusu kuwasili jijini Dar es Salaam tukapokelewa na ndugu jamaa na marafiki ambao hawakutaka kwenda nasi.

    “Hafidhi mwanangu vipi za huko?"

    “nzuri tu maana tuliweza kufika salama na tukazika bila tatizo lolote"

    “ohoo basi ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu na kumuombea mwenzako apumzike salama huko alipokwenda!"

    “sawa Mama nina hakika sitoacha kumuombea Dua kila siku iyendayo kwa Mungu"

    Ziliweza kupita siku saba tokea turudi kutoka Bukoba kila mtu alianza kusahau juu ya kifo cha Ratifa. Lakini mimi sikuweza kusahau kwa muda huo. Na sitoweza kusahau kamwe katika maisha yangu haya yaliyo bakia mpaka siku naingia kaburini. Nilimkumbuka Ratifa kwa mambo mengi sana nikaliandika jina lake kwenye Bajaji yangu, ambayo niliichukuwa na kuingia nayo Barabarani Mimi mwenyewe. Huku Mwajuma akiniaga kuwa anaelekea masomoni baada kupata ufahuru na sasa anaelekea Canada kwa kuendelea na muhura mwingine. Siku aliyoondoka alinisihi sana nisimsaliti nimngojee

    Amalize masomo yake ili tuje kuwa mke na mume. Nami nikamuahidi sitoweza kumsaliti ila nae aniahidi kwa kunituzia boma langu.

    ***********

    Ulishatimia mwaka mmoja tokea Ratifa afariki na Mwajuma kuelekea masomoni. Sikuweza kutokewa tena na Majinni wala Vibwengo nikawa nikiendelea na kazi yangu ya Dereva bajaji huku nikiwasiliana na Mwajuma kupitia mitandao ya kijamii kama vile

    Facebook Instagram hasa

    Whatsapp mpaka ikafikia hatua tukawa tukilizishana kimwili kupitia Sex Charting.

    kila mmoja akafurahia tendo hilo kwani ilikuwa kama vile tupo kitandani. Kuhusu Janeth nilisikia tu alikuwa akidaiwa pesa nyingi sana na

    Baadhi ya Saccos sijui vikoba kwani alikopa

    pesa kwaajili ya kuisimamia harusi ya

    Kaka yake, alikopa kama Milioni mbili, kweli harusi ilikuwa ya kifahari watu walikula na kunywa

    Mpaka kusaza kijana aliyeowa hata wiki mbili bado akampa talaka mkewe huku

    Janeth akishindwa kurudisha mkopo huo

    Akajalibu kuniomba nimsaidie eti niuze bajaji.

    Nikamjibu tu bajaji sio yangu ni ya Mama

    “Baby kama ya mama si tuiuze tu ili tulipe deni la watu. Siku tukipata pesa tutamnunulia nyingine"

    Ndivyo alivyoniambia

    “tulipe deni la nani? Wakati unakopa hizo pesa Mimi nilikuwepo tena ukome kuniambia ujinga kama huo

    yani niuze bajaji ya mama kisa upuuzi wako ulioufanya nenda kamwambie huyo

    Bwege mwenzio msaidiane kutafuta pesa ya watu!"

    Niling'aka kama kuonekana mwanaume

    Suruwali au vikaptura sawa tu lakini siwezi kuchunwa kibwege hivyo.

    Ndio ukawa mwisho wa Mimi na Janeth sikuweza kuonana nae tena mpaka ukatimia muda wa

    Mwajuma kumaliza masomo yake. Kabla hajarudi nikaenda kwa Shekhe Ally na kumueleza

    Azma yangu ya kutaka kuoa hakika alifurahi

    Sana na kunitakia baraka njema wakati nakumbuka nilizini na Mwajuma lakini

    si Gogisu si Bibi wala Jinni Sharifa aliyeweza kunitokea, basi barua ya posa ikaandaliwa

    Shekhe Ally akafunga safari mpaka

    Kunduchi nyumbani kwao kina Mwajuma na kuikabidhi posa ile

    Nasikia Mama yake Mwajuma alicheka mpaka machozi yalimtoka

    hakika hakuweza kuamini kutoka na matendo mabaya aliyokuwa akitufanyia leo nitathubutu

    Kutaka kumuowa Mwajuma,

    Siku ya siku bibiye akarudi nchini Tanzania bila kunipa taarifa eti kaja kimyakimya akitaka kunifumania

    “Wee kaka"

    “Naam"

    “nataka bajaji"

    “Bajaji yangu mbovu nenda tu kachukuwe nyingine"

    “sitaki nyingine naitaka yako"

    “sasa sister si nishakwambia hii mbovu ndio naiweka sawa,.Akidaa!

    “niambie Mwamba"

    “Embu msikilize huyo Sister anataka bajaji"

    “msikilize mwenyewe kwanza anataka bure"

    Nilikuwa naonge huku nikiwa bize kufunga

    Vizuri sip ring chini ya Bajaji so nilikuwa sifahamu nazungumza na nani.

    Sasa ile kusikia Akida akisema mteja mwenyewe anataka bure nilijikuta nakunja ndita kwa hasira na kutoka kule chini ili nimtukane

    huyu Sister duuu

    Mungu wangu alikuwa ni Mwajuma nilihisi kama vile naota nikabaki kumtazama

    kumbe wakati anaongea na Mimi hakuwa peke yake alikuwa na binti mwingine ndiyo aliyekuwa akiongea.

    Akanirukia na kuanza kunipiga mabusu

    huku kina Akida sijui Kaunda

    Wakipiga honi kwa fujo jamani jamani

    ---------------

    Basi tulikumbatiana kwa furaha huku tukinyonyana denda kwa pupa.

    Ni kitendo kilichochukuwa takribani dakika tatu, ndipo tukaachiana hakika Mwajuma alikuwa kanona si mchezo kuonyesha huko Canada anakula vinono

    “whaoo hatimae baby umerudi"

    “ndio maana yake nimekuja kimyakimya niweze kufumania"

    “sasa hiyo kifumania ndiyo uje kazini hapa kazi tu hakuna michepuko"

    Niliongea huku nikimtupia jicho la kiwiziwizi yule Binti mwingine. Nae mtoto alikuwa kaumbika si mchezo rangi ya ngozi yake si nyeusi wala maji ya kunde mtoto. Alikuwa na rangi ya weupe uliofifia ilimfanya vyema sana.Umbo lake number nane, yaani hakuwa mnene wala mwembamba. Saizi ya kati ila alijaaliwa makalio makubwa wastani. Tena makalio yake bila shaka ni malaini. Yote ni mawazo yangu juu ya mrembo huyu

    Nikimsaminisha japo hayo makalio sijayashika. Hapo kati sasa maeneo ya hipsi na kiuno,,,,,,,,,

    “Baby kutana na rafiki yangu kipenzi anaitwa

    Regina Gilbert"

    Nilishtushwa na sauti ya Mwajuma akitowa utambulisho kwangu.

    “Regina kutana na shemeji yako anaitwa Hafidhi j Ikram ndiyo mume wangu mtarajiwa baba wa watoto wangu"

    “whaoo nashukuru sana kumfahamu"

    Basi tukapeana mikono kwa ishara ya salamu nilikiandaa kidole changu cha kati kwa kutaka kumtekenya bibiye Regina kwenye kiganja chake cha mkono sema nikasita kufanya hivyo.

    “sasa baby unaonaje tukaenda sehemu tuweze kupata chakula cha mchana"

    “ni wewe tu, maana mi mwenyewe hapa nilikuwa na ubao ndiyo nilikuwa narekebisha

    Bajaji niende nyumbani,"

    “basi sio mbaya twenzetu pale Mwenge nasikia kuna

    Mgahawa mzuri tu"

    “embu nisubirini basi"

    Nikatoka mbio kumfata Akida na kumuomba anipe Bajaji yake.

    “Baby bwana bajaji ya nini wakati usafiri ule pale!"

    “Shemu embu mwambie sijui anafikilia nyie mmekuja kwa miguu"

    Niliangalia kwanza huo usafiri Mungu wangu ilikuwa ni gari aina ya Benzi macho ya paka yenye rangi nyekundu.

    Basi tukaenda kupanda

    “Baby si utaendeesha?"

    “mi siwezi kuendeesha gari zangu bajaji pikipiki"

    Nilimjibu Mwajuma na kuingia ndani ya gari nikakaa siti ya nyuma funguo akapewa Regina

    “sasa Mimi nitaendeesha vipi wakati hiyo sehemu

    Sihifahamu?"

    Hakika mtoto alikuwa na sauti tamu utasema

    ndege aina ya Chiriku

    “shika bwana si nitakupatia maelekezo"

    Mwajuma akamjibu huku na yeye akija kukaa siti ya nyuma safari ikaanza

    Huku nyuma tulianza kuchezeana michezo ya kutekenyana mara tunyonyane midomo yetu

    Kupitia kioo kile cha juu ya gari

    Nilimuona Regina akicheka cheka na kutabasamu.

    Tuliweza kufika mgahawani na kupata chakula siku hiyo tuliweza kuongea mambo mengi sana hasa kuhusu ndoa yetu

    Mwajuma aliniambia kuwa Baba yake katununulia nyumba maeneo ya Tabata Bima baada kula fungate tutaenda kuanza maisha mapya kwenye nyumba yetu.

    Hakika nilifurahi sana tena sana

    Nikapata muda wa kuongea na Regina nilijaribu kurusha ndoano yangu kwa binti mrembo lakini nikaambulia patupu. Alinitolea nnje kwa kusema

    Binafsi yeye na Mwajuma ni marafiki wakubwa

    Na urafiki wao ni zaidi ya ndugu kwahiyo hayuko

    tayari kugombana na Mwajuma kisa

    mapenzi na istoshe yeye ana mtu wake.

    Akaniaomba nitulie na wangu. Mwanaume sikutaka kukata tamaa nilizidi kumsumbua bibiye

    siku baada ya siku mpaka akatishia kumueleza Mwajuma kila kitu. Hapo kidogo nikawa mpole kwani sikuwa tayari kumpoteza Mwajuma.

    Siku ya siku ikafika niliweza kufunga ndoa

    na Mwajuma ni harusi ambayo ilifaana sana yani ilikuwa babu kubwa watu walikula na kusaza

    huku wanandoa tukipewa Zawadi yakwenda kula fungate katika jiji la Paris Nchini Ufaransa

    Siku ambayo naondoka mama alilia yeye na Dada Nasra kwani hawakupenda nikae nao mbali

    Niliwakumbatia na kuwatoa hofu kuwa safari sio

    kifo nitarejea tu.

    Tulikaa katika Paris kwa wiki mbili tukarejea tulienda wawili tukarudi watatu mwingine alikuwa tumboni mwa Mwajuma furaha ilizidi kifani

    Maisha yalizidi kusonga nilikaa karibu na

    Mke wangu na kumpatia huduma za hapa na pale akiwa kama mwanamke mjamzito

    Huku lile pepo la kumtaka Regina likiwa halipo tena

    Mwajuma akaomba Nasra aje kuishi nasi achilia mbali kuwa mawifi wao walikuwa ni marafiki wakubwa tu.

    Miezi Tisa ikatimia Mke wangu wangu alishikwa na uchungu na kuwahishwa hospitali.

    Mimi mwenyewe sikuwepo nilikuwa nipo Arusha baada kuagizwa kufatilia mzigo na Baba mkwe kwani Mimi ndio nilikuwa kila kitu juu ya biashara zake zote. Nilipigiwa simu na kuambiwa hongera mke wako kajifungua mtoto wa kike

    Nilirukaruka kwa furaha na kusema hatimae Ratifa kazaliwa. Niliporudi na kumtia machoni

    Mwanangu alikuwa ni mtoto mzuri hatari kila mtu alimsifia nikampa jina la Ratifa wala si Latifa

    usikosee sema Ratifa usiweke L

    Siku moja ilikuwa yapata majira ya saa tatu usiku tulikuwa tupo sebuleni tukila chakula cha usiku yani Mimi Mama mkwe Dada Nasra

    Mwajuma na Mama huku Ratifa akiwa ananyonya

    Ndipo simu yangu ikawa inaita nikaichukuwa kuangalia mpigaji ni Regina nikaipokea

    “Haloo shemeji"

    Ajabu alianza kulia na kunifanya ninyanyuke kwenye kiti nikaelekea chumbani

    “haloo unalia nini si useme nini shida nini tatizo niambie"

    “Hiiiiiiii, shameji njoo unisaidie nakufaaa hukuu!"

    Nikakata simu nikavaa viatu na kuchukuwa funguo ya pikipiki ndio usafiri wa haraka kwangu Mimi

    “Baba Ratifa unaenda wapi tena usiku wote huu

    Mama aliniuliza sikumjibu kitu nikatoka hadi

    Nnje na kumuomba mlinzi afunguwe Geti.

    Nikakwea pikipiki na kutoka kwa speed

    Zote nikafika kwa Regina nikaingia kwa tahadhari

    ile nagusa kitasa cha mlango tu na kuingia ndani

    Nikashikwa mkono na kuvutwa

    Vupuu mpaka ukutani nilimshika yule mtu kwa kumzungusha

    Na kutaka kumbwaga masikini kumbe alikuwa ni Regina mtoto akiwa yupo uchi wa mnyama

    Nilimdaka kabla hajadondoka chini na kumtuliza kifuani kwangu tukabaki kuhema

    kila mmoja akimuangalia mwenzake.

    “Shemejii,,,,, sikutaka amalizie kuongea chochote niliuvamia mdomo wake na kuanza kumnyonya denda kwa pupa.

    Kumbe nae alipanga kila kitu ndiyo maana nikamkuta vile. Sikumbuki hata nguo zangu nilivuwa mwenyewe. Au nilivuliwa, hakika Regina ana stahili sifa ya pekee baada kuona

    Mtalimbo wangu umesimama utasema msumari. Basi

    alijipanua mapaja yake, pale katikati palibaki wazi ambapo aliushika mtalimbo kisha akauchomeka,,,kwenye kitumbua chake kinono

    “aaaaaaaaaaaaas

    hiiiiiiiiiiiiiiiiiiii,," Alianza kulalamika baada ya mtalimbo kuzama ndani ya kitumbua ambapo ni kama filimbi ilipigwa ili viuno vianze.

    “mpenzi wangu naomba unisugue taratibu mpenzi,,aaaaa

    ashiiiiiiiiiii,,,taratibu babaaaa,,,yote,

    ,eeee,,,yakwakoooo,,,ooooshiii

    iiiiiii,,usiwe na pupa kula bila papara nimekupanuliaaaa kitumbua chako,,,,

    unisugueeeee,,,,,,,, jamaniiiiiiiiii,,"

    Mtoto aliongea huku ulimi wake ukiwa sikioni mwangu na kuzidi kunipagawisha

    Nilimpapu zile za kichinachina

    Nikakojoa nilipomwaga tu umeme ukakatika huku mvua kubwa ikianza kunyesha radi zilipiga.

    “Yalaa nakufaa nisaidie

    Hukuu uwiiiii!"

    Zilikuwa ni kelele za Regina kwani aliingia chumbani kwenda kuchukuwa taa ya chaji nikakurupuka mbio na kwenda chumbani sikuweza kuamini

    Iseee baada kumkuta Regina akinyonywa damu na Gogisu

    Nikiwa bado nashangaa sijui nifanye nini

    simu yangu ikaanza kuita nikarudi kwanza sebuleni na kuichukuwa Suruwali yangu nikaisachi na kuitoa simu mpigaji ni Nasra

    “haloo kaka mtoto kapotea huku"

    “what?"

    “Ratifa kapotea,"

    Nikamsikia na mama akisema hivyo"

    Ndipo niliweza kufahamu kuwa ile kauli ya Shekhe Ally ni ya kweli nilikuwa natetemeka sijui hasira au hofu nikavaa nguo zangu na kwenda chumbani

    Nilipofika hakuna cha Gogisu wala

    Regina nikapiga kelele na kutamka ile Lugha

    Khaa si nikajikuta nipo nyumbani.



    ****MWISHO WA MSIMU WA KWANZA*****

    FUATILIA MSIMU WA PILI



    ******MWISHO******

     

     

0 comments:

Post a Comment

Blog