Search This Blog

Thursday 24 November 2022

YOUNG PASTOR - 1

 

     

     



     IMEANDIKWA NA : MOONBOY



    *********************************************************************************

    Chombezo : Young Pastor

    Sehemu Ya Kwanza (1)

     Katika kanisa moja kubwa ikiwa ni wakati wa saa nne hivi asubuhi… Kanisa kubwa lenye urefu wa rosheni mbili kwenda juu.. Na rosheni zote zimesheheni waumini wa lika mbalimbali kuanzia watoto wazee na vijana.. Wakati huo wapo mapasta ambao walikuwa wakitoa sifa kwa Bwana Yesu kwa kutumia nyimbo za injili,… Floo ya chini ya kanisa hilo ni sehemu ya kupaki magari, na floo ya katikati ni ukumbi mkubwa yaani kama kuna ndoa basi hapo ndipo mahali pake, ila pia hio floo ya katika imejaa waumini, mana sio siku zote watu wanaoa, na pia ina skrini kubwa karibia ukuta mzima ule wa mbele, hio ni skrini ya kumuonyesha pasta akiwa floo ya juu, yaani ni kama sinema vile,,.. Sasa hio floo ya juu na ya mwisho, ndio kanisa lenyewe,.. Ukiangalia mazabauni yaani imeng’aa kwa maru maru maalum, yaani pale ni sehemu ya pasta pekee. Na wakati huo pasta bado hajaja, hivyo waumi waikuwa wakitoa sifa za bwana Yesu kwa kupitia nyimbo zilizoimbwa na wasanii mahiri nchini,



    Sasa huku chini ilionekana gari moja ya bei mbaya… Ikiwa inapaki, tena ina sehemu yake maalum ya kupaki sio kila mahali,… Ilikuwa ni familia moja iliokuwa ikija kanisani, na ilionekana kuheshimika sana kanisani hapo,… Walikuwa ni wasichana watatu waliotofautiana umri, akiwemo baba yao na mama yao,… Hatua za kuelekea kanisani zilianza taratibu, na kila muumini aliiheshim familia hio,…

    “tumsifu yesu Kristo”

    Ni waumini waliokuwa wakitoa salamu kwa bwana huyo, huku akiwaitikia

    “milele amina”

    Yaani waumini wanapanda kwa ngazi, lakini yeye ana lift yake maalum, yaani yeye na familia yake hutumia wao tu,… Alipofika ndani ya kanisa waumini wote wa floo ya katikati na floo ya mwisho walinyanyuka na kutoa salamu kwa pamoja…

    “tumsifu Yesu Kristo alie hai mbele za mungu”

    Walisema waumini hao huku familia ikiwa ina viti vyao pale mbele, yaani ule ule upande wa waumini, sasa viti vya mbele ni spesho kwa ajili ya familia hio… Lakini pia katika viti hivyo kuna kiti kimoja hakikuwa na mtu, na ni kiti cha mmoja wa familia hio na hakiruhusiwi kukaliwa…. Sasa hatujui huyo aliosalia kukaa pale ni nani,…. Pale pale mr huyo alipanda mazabauni,….



    Kumbe huyo bwana ana kipawa cha UBISHOP yaani ni Bishop Jacob… Ni kiongozi wa makanisa yake yapatayo 50 kwa idadi kamili…. Yaani mzee huyu ana makanisa 50 makubwa kama hili na ni yakwake peke yake… Anayasimamia mwenyewe, licha ya kuwa Bishop, bado pia ni tajiri mkubwa… Mana ana makampuni mengi sana, ana viwanda… Huezi amini ni Bishop anaemiliki ndege binafsi, ana magari ya kutembelea kama utitiri,…..

    “tumsifu Yesu Kristo kwa jina la baba”

    Aliongea Bishop Jacob huku waumini wakipaza sauti zao kwa hali na mali

    “milele aminaaaaaa”

    Raha sana ukiwa na imani ya dini yako….

    Wadada, wamama, wakaka, watoto, wazee…. Yaani malika yote yalijaa hapo, na unambiwa akitoka hapo anakwenda katika makanisa mengine kutoa neno la bwana… Yaani amekuwa mtu wa kutoa neno siku nzima….



    BISHOP ni kipawa au cheo kikubwa ambacho ni ukitoka pasta sasa anaefatia kwenda juu,… Anakuwa ni Bishop, lakini pia Bishop ana mkubwa wake ambaye ni ATBISHOP huyu ATBISHOP huyu sio mtu wa kawaida, huyu anaweza kuwa ATBISHOP wa kidunia au wa kitanzania nzima…. Yaani anasimamia au kuongoza makanisa yote Tanzania. Na sio kuwa ni yake lahasha bali anayasimamia tu, na pia sio kuwa anasimamia yote, lahasha bali kuna matawi mengi sana juu ya haya makanisa… Hivyo atasimamia makanisa ambayo ni tawi fulani pekee, hivyo atakuwepo ATBISHOP mwingine wa kusimamia makanisa ya tawi lake husika… Hivyo ATBISHOP ni mkubwa, tuchukulie mfano wa rais…. Afu huyu Bishop yeye tufanye ni kama mbunge… Hivyo katika mkoa mmoja kunaweza kuwa na ma Bishop hata mia moja.. Kutokana na kila mtu kumiliki jimbo lake yaani makanisa yake…. Nakupa tu kwa ufupi ujue vipawa vilivyo….



    Sasa Bishop Jacob alianza kuhubiri kama ilivyo kawaida yake, ni mchungaji aliojaaliwa kipawa na upako wa hali ya juu katika kutoa neno la Bwana,…. Waumini walikuwa wakilia kutokana uzito mahubiri aliokuwa akihubiri Jacob,… Machozi kila muuni, wengine kama kawaida yao kudondoka chini wakati wa pepo kutoka,… Na yote hayo ni kwasababu ya mchungaji Jacob au Bishop Jacob



    Mahubiri yaliisha na hatimaye ibada ya siku ya Jumapili inakwenda ukingoni,… Lift yake ni ile ile, hachanganyikani na waumini hata siku moja,…. Akiwa na familia yake wanaingia katika gari,…. Lakini wakati wanaingia alitokea mschana mmoja ambae nae ni muumini wa kanisa hilo,..

    “tumsifu yesu Kristo mama”

    Alisalimia mschana huyo huku akimpa mkono mke wa Jacob,….

    “milele amina….. Eva mbona siku hizi huji nyumbani, au kwasababu mwenzio hayupo”

    Aliongea mama huyo aliokwenda kwa jina la Rebecca,.. Sasa hatukujua huyo mwenzie ni nani haswa, lakini eva alipokua akisalimiana na mwanamke huyo, ghawna wale wasichana nao wakaanza kumsalimia eva….

    “heee wifi hali yako”

    Aliongea mtoto mkubwa wa huyo mama aliokwenda kwa jina la Jessica mwenye umri wa miaka 28, ndio mtoto wa kwanza kwenye hio familia, lakini sasa Jessica kamuita eva wifi kitu ambacho hatujui kaolewa na ndugu yake nani, au ndio ile utani tu,… Mara mschana mwingine kasalimia

    “shkamo wifi eva”

    Alisalimia mschana mwingine aliokwenda kwa jina la martha, mwenye umri wa miaka 20…. Kuna mwingine hakutaka kuachwa nyuma kwa salamu

    “wifi eva shkamo”

    Alisalimia mschana mwingine wa mwisho, aliokwenda kwa jina la maria ana miaka 15…

    “amarahaba mawifi zangu hamjambo”

    “hatujambo… Hatukuoni nyumbani”

    “aahhh nitakuja Maria usijali”

    Eva alikuwa ni mschana mzuri sana na mwenye heshima kwa rika zote,

    “mwanangu, kabla mwenzio hajakwenda masomoni, ulikuwa unakuja, lakini sasa hivi huuuji jamani”

    Aliongea Rebecca au mama Jessica, au mama mchungaji,…

    “mama, hata mimi hua nakuwa na ubize sana… Sasa hivi nadili sana maombi, sitaki mwenzangu anikute nipo nyuma, hivyo nami nakua bize na mungu”

    “yesu atakubariki eva,… Na naomba nikutaarifu, mwenzio anarudi wiki ijayo”

    Eva kusikia mwenzie anarudi wiki ijayo, alifurahi na kuruka ruka, alimkumbtia mama mkwe wake karibu kudondoshana, mpaka baadhi ya waumini walishangaa kwa furaha hio alionayo eva…

    “eva utaniangusha jamani”

    “mama, nina furaha kiasi gani juu ya taarifa hio”

    Eva ana mdogo wake wa kike aitwaye HAPPINESS, mwenye miaka 15 alikuja pale baada ya kuona dada yake ana furaha…

    “tumsifu yesu Kristo mama”

    Alisalimia happy huku akiinama chini kuashiria ni heshima ya hali ya juu mno,…

    “milele amina,… Heew happy, umependeza Jumapili ya leo”

    “ahsante mama… Sifa kwa Yesu”

    “amina mwanangu”

    Basi waliongea mengi sana na hatimae kila mmoja kuondoka baada ya ibada kuisha,…



    Kuanzia hapo Eva alikuwa ni mtu wa furaha siku zote, mana sasa usingizi wake karibu kuja… Eva ni mschana aliolelewa katika mazingira ya kidini na anaijua dini haswa, yaani humwambii kitu kuhusu Bibilia,… Eva alipofika nyumbani alimkuta mama yake kesharudi, nyumbani… Ni familia ya kawaida sana…

    “mamaaaa….. Yesu kajibu maombi yangu mama”

    Aliongea eva huku akimkumbatia mama yake,…

    “ni nini eva… Afu leo sijakuona kanisani ulikaa wapi”

    “mama… Leo niliamua kukaa nyuma sana”

    “enheee, yesu kajibu maombi yako kivipi… Mana una furaha kweli yani”

    Aliongea mama huyo huku mama akiwa anaandaa ratiba zake za jumuiya,..

    “mama njoo ndani nikwambie”

    Mama eva aliingia ndani ili kumsikiliza mtoto wake…



    “haya Niambie”

    “mama…. Wiki hii mkwe wako anakuja”

    Mama alishangaa kusikia mkwe wako anakuja….

    “ina maana umeachana na adam unataka uniletee mwanaume mwingine, eva mwanangu ni mawazo gani unayo”

    Mama alikuwa hajamuelewa mtoto wake ana maana gani…

    “mama sio kuwa naleta mwanaume mwingine,…. Namaanisha huyo huyo Adam, anarudi toka masomoni”

    “weeeee…. Unasema kweli”

    “ndio,.. Nilikuwa na mama mkwe pale kanisani ndio kaniambia”

    “jamani eva mwanangu”

    “nini mama…. “

    Familia hio ni familia fukara sana ila wengi wao wanaona wivu kwa mtoto Bishop Jacob, kuoa katika familia hio, na ni kila muumini anajua uhusiano wa Adam na Eva,… Lakini kwakuwa Eva anaishi katika maisha ya kimasikini hivyo kwao ni kama bahati kuolewa na mtoto wa kitajiri, tena mtoto wa Bishop, yaani sio pasta ni Bishop… Kwa wale waikristo nikisema Bishop nadhani mnanielewa..

    “mara paaap adam anashuka kwenye ndege na mke wa kinaigeria… Utafanyeje sasa”

    Mama alimwambia mwanae hivyo mana adam yupo Lagos nchini Nigeria, katika vyuo vya dini ya kikristo, japo adam ana nguvu na miujiza kuliko hata baba yake, lakini akaamua kwenda kujiongeza, sasa akirudi huko ni moto wa kuotea mbali,  Sasa baada ya mama eva kusema hivyo, eva alianza kulia huku akisema kuwa….

    “mamaaaaaa….. Usiseme hivyo”

    “sikuombei umkose mwanangu… Ila wanaume wa siku hizi…. Siwawekei mia kwa mia… Hawakawiii kubadirika”

    “ni kweli mama… Lakini sio kwa mtu mwenye imani kama adam”

    “eva mwanangu, mimi ni mama yako… Nimekuficha mengi sana kuhusu adam…. Na nikisema nikuambie nitakupoteza mwanangu… We mpende tu”

    Eva alitoa jicho kuskia mama yake anasema maneno hayo…..

    “unasemaje mama”

    “una kifua cha kubebea jambo mwanangu, tusije kuanza kupepeana na kanga hapa”

    Aliongea mama yake eva huku wakikaa vizuri kitandani

    “mama… Nipo tayari kumwacha adam kama ana tabia chafu”

    “heeeeee wewe ndio wa kusema hivyo”

    “mamaaaaa Niambie basi nijue”









    Eva alikuwa na wasiwasi mno kuhusu mchumba wake ambaye mama anasema ana siri nzito sana juu ya adam.. Sasa eva kakaa kwa umakini ili kuweza kujua ni siri gani hio ambayo mama anaijua… Eva alitamani hata kutoa chozi, lakini ghafla mama anacheka kweli mpaka machozi yanamtoka kwa kucheka,..

    “kumbe mwanangu unampenda sana adam… Mimi nikajua utakuwa umemsahau kabisa kutokana na muda aliokaa masomoni sana… Kumbe bado unampenda… Kiukweli hakuna lolote mwanangu, nilikuwa nakutisha tuuu”

    Hapo eva akashusha pumzi nzito kisha akachukuwa Biblia na kuanza kusoma kama vile kamkasirikia mama yake…

    “mwanangu usinune basi jamani… Yesu hajafundisha umnunie mama yako eva”

    Eva kweli anajua sheria na mafundisho alio yaacha bwana yesu

    “mama, sijakununia mama angu”

    Aliongea eva huku akimkumbatia mama yake,…

    “najua nimekuuzi mwanangu”

    Mara bite kaja mpaka chumbani,.. Yaani watoto wa huyu mama ni wazuri, mpaka basi sema hali ya maisha kwao ni ngumu mno, na wanaishi hivyo hivyo kwa nguvu za mungu….



    Tukiachana na familia ya akina eva sasa turudi huku kaisani, walikuwepo waumini waliosikia fununu za kuwa mtoto wa bishop jacob yukaribuni kuja Tanzania kutoka masomo, hivyo hizo ndio atori zilizo zagaa katika kanisa hilo… Inaonekana ni jinsi gani adam anapendwa na waumi sasa hatujui adam ana lika gani na ana rangi gani, na yupoje yupoje.. Bali sifa zake ndio huongelewa zaidi….

    “ester, iv umesikia za chini chini kuwa adam yukaribuni kuja”

    Aliongea dada mmoja ambaye ni muumini wa kanisa hilo la mr Jacob

    “adam gani tena…. Au adam yule wa karne ya 5”

    “aaahhh we ester huelewi kwanini”

    “sasa Janet, mi namjuaje huyo adam”

    “si adam wa Bishop Jacob”

    Ester kusikia ni adam wa bishop Jacob nae alitahmaki, walikuwa wasichana wengi na wao pia walitahamaki….

    “we janet muongo… Adam si yupo Nigeria kimasomo wewe”

    “sasa anakuja.. Nimeskia za chini ya kapeti… Wiki hii ndani ya Arusha”

    “eeeeh bwana weee…”

    “alafu sasa…. Umeona kanisa lake”

    Alizidi kuongea janet huku wengi wakiwa hawajui…

    “weeee, ina mana mchungaji Jacob ana kanisa lingine”

    Aliuliza mmoja wa marafiki wa janet

    “sio la mchungaji Jacob ni la adam”

    Aliongea janet tena kwa kujiamini haswa….

    “we janet wewe, unajua bwana yesu hajafundisha uongo”

    “sasa huu ni uongo au ukweli”

    “skia adam, hana mke, adam bado anaishi kwa baba yake… Adam bado ni mdogo, hawezi kabidhiwa kanisa… Kwanza huo upako wa mpaka apewe kanisa kautoa wapi”

    “heeeeeee Cecilia,… Ivi hujui kuwa uchungaji ni wito toka kwa mungu.. Uchungaji aio lazima awe…… “

    Ghafla janet alinyamaza baada ya kumuona mzee wa kanisa akipita maeneo hayo, mana wanacho kiongea ni siri, bado hakikuwekwa wazi kuwa kijulikane, ni nyepesi nyepesi tuuuu…. Baada ya mzee wa kanisa kupita janet aliiacha ile mada mana ni hatari sana kwa midomo yao

    “ester, unajua mimi nawadokezeeni tu.. Sasa tuachane na hii mada”

    “ok, afu… Leo nimemwona eva karuka ruka pale alivokutana na mama mchungaji”

    Aliuliza ester mana jenet kwa fununu hajambo

    “hapo ndio hata mimi nikajua kuwa adam anakuja wiki hii… Mana baada ya pale nikamfuata bite mdogo wake eva ndio nikamuuliza mbona dada yako amekuwa na furaha sana.. Ndio akaniambia kuwa mchumba wake anakuja”

    Aliongea hivyo janet huku akina Esta na wengine wakacheka….

    “ivi janet, eva anajidanganya kabisa kuwa ataolewa na adam…. Aache kutafuta mtoto wa Bishop kama yeye, aje aoe maskini kuliko hata mimi”

    “we ester wewe, chunga mdomo wako huo… Ukisikiwa unaongea huo ujinga, mi simo”

    Aliongea janet huku akishika mkoba wake na kuanza hatua kana kwamba hawahitaji maongezi yanayo muhusu eva…



    Baada ya masaa kadhaa kupita sasa tukiwa huku nyumbani kwa Bishop Jacob, wakiwa mezani wanapata chakula cha usiku…. Na hapo walikuwa wakiomba kabla ya kula,… Kama kawaida wa wakristo lazima waombe maombi marefu tena wengine huchukua hata dakika 10 kwa maombi tu… Familia yenye watu watano, baba na mama na wasichana watatu… Baada ya kuomba walianza kula huku vikisikika vijiko tu vikigongana katika sagani, yaani hawaruhusiwi kuongea wakati wa kula… Ukweli walikuwa ni matajiri sana, yaani haikuwa mboga saba kama tunavyojua… Hata mimi mwandishi, naona kuna vibakuli zaidi ya kumi… Yaani, yaani walizidisha hata sio ile mboga saba… Walimaliza kula hatimae mfanyakazi anapata kazi ya kuwaandalia maji kila mmoja wao, japo wasichana hao wana malezi bora hivyo hawahitaji kuletewa maji.. Wanayafuata wenyewe,…. Baada ya hapo watoto wote waliondoka na kuingia kwenye vyumba vyao, mana kila mschana ana chumba chake… Jumba lenyewe kubwa kama kanisa…

    “haya baba mtoto…. Mwanao ndio huyo anakuja….umemuandalia nini mana sasa akija ni kazi moja hapa mtashindana weeeee”

    “ahahahahahaha…. Mama Jessica,.. Mimi nina tabu gani… Kanisa lake limeshafaa, akija nitawaita wazee wa makanisa yangu yote… Kama anafaaa kuwa mchungaji aendelee”

    “kama anafaa?.. Kivipi.. Kwani huko shule kaenda kufanya nini kama sio kujiongeza… We si unamjua mwanao, yaani kabla hajaenda huko, akishika tu mtu kichwa anadondoka chini na hapo hajaenda Nigeria, je akirudi itakuwaje”

    “na ndio mana nikampeleka kwa rafiki yangu, yaani najua makanisa yote ni ya mwanangu.. Sina pingamizi juu ya hilo”

    “mmmmhhh angalia msije mkaanza ushindani, mana kazi ya mumgu yahitaji uvumilivu toka kwa bwana yesu… Tumuombee mtoto wetu huko aliko”

    “milele amina”

    Walikuwa wakiongea huku wakipata juis kwa mbali,…



    Baada ya siku hio kupita na leo ni siku ya jumatatu, mr Jacob amiwa katika shughuli zake, mana unaambiwa tii wito wa mungu kisha katafute kula… Hivyo siku za juma bishop Jacob yeye huwa bize na kazi zake, na katika makanisa yake kuna wale mapasta wadogo wadogo ambao watakuwepo wiki yote kwa ajili ya maombezi, na Jacob ana ofisi yake inayohusu kanisa… Hivyo ya kanisani ni kanisani na kazini ni kazini… Bishop jacob ni mtu wa kumuomba mungu kila wakati, yeye na Biblia, kwani hata kazini kwake ana Biblia aina zote,.. Wafanyakazi waliopo hapo ni wakristo wote, yaani kila mfanyakazi ana rozali yake mezani, bwana Jacob akiingia ofisini kwake ni yeye na neno la mungu, hataki kupitwa na lolote….

    Akiwa hapo ofisini mara ghafla simu yake inaita, alikuwa ni Bishop james, yaani huyo ni kipawa mwenzie mwenye kipawa cha Bishop,…

    “tumsifu Yesu Kristo james”

    Alisalimia jacob huku akitabasamu kwa mbaali

    “milele amina… Naona kwenye kikao sikuoni huku njiro”

    “aahhh nimetingwa kidogo… Si unajua kijana wangu hayupo sasa hivi nahangaika mwenyewe, mana angalau alikuwa anafuatilia miradi ya baba yake lakini sasa hayupo”

    “aaahhh lakini nadhani ni wito wa mungu juu ya kulitangaza neno la bwana yesu alie hai”

    “ndio, na hana muda atarudi”

    “yesu asifiwe bwana jacob”

    “milele amina… “

    “basi nilikuwa nakujulia hali tu.. Mana sijakuona katika kikao cha leo”

    “hakuna shida mtumishi wa Mungu”

    “haya siku njema na yesu akutangulie”

    “milele amina… nawe pia”

    Simu ilikatika na mzee akaendelea kupata neno la mungu,… Na uzuri wa wakubwa kama hawa hua wana vitabu vya mungu vya pande zote mana hata hapa kwa Bishop jacob, ana kitabu cha Kiislamu, ni kawaida ya viongozi wakubwa hua lazima ujue neno la upande wa pili ili kujua kama kuna utofauti na upande wao,.. Hata papa mwenyewe ana kitabu cha Kiislamu,… Na ndivyo inavyotakiwa kujua upande wa pili wa dini ya mwenzio… Na sio kuwa hawakiwezi kukisoma, wanakiweza haswa… Na sio hao tu hata wale viongozi wa dini ya kiislamu kuna basdhi yao wanaijua Biblia kuliko hata wewe Mkristo ambae ni kitabu chako kotakatifu..



    Tukija huku kanisani alionekana eva akiwa anaomba sana… Na siku hio kulikuwa na maombi ya kawaida tu, na hakui na watu wengi kama ilivyo Jumapili,… Eva ni mschana aliopendelewa kila aina ya mwili wake, yaani kiukweli ana haki ya kuitwa mrembo wa kanisa, japo haitowahi kutokea lakini hio nafasi inamfaa….

    “eti yule, aje kuitwa mama mchungaji.. Inawezekana kweli”

    Aliongea Janet wakiwa katika mlango wa kuingilia, mana eva alikuwa bize na maombi huku akiwa kafumba macho yake….

    “nashangaa hata mimi…. Ww ulizani adam ni wa mchezo mchezo”

    “lakini janet? mbona familia zao zinajuana”

    “hata kama esta, ila sio rahisi adam kumuoa eva”

    “hebu kaone kanajifanya kanajua dini sanaaaaa”

    “weeee janet sio vizuri, huko tunapokwenda sasa ni unafiki jamani janet… Hebu tuyaache hayo”

    Lakini sasa kumbe walipokuwa wakiongea walikuwa wakisikiwa na mzee wa kanisa… Kitu ambacho hajakipenda mzee huyo….  Lakini hakuwaambia kitu chochote…

    “huyu mzee katokea wapi”

    Aliongea janet huku wakimshangaa



    Baada ya siku hio kuisha,… Bwana Jacob akiwa kazini ikiwa ni siku ya Jumanne,.. Alikuwa na rafiki yake aliokuja kumtembelea ofisini kwake,..

    “yusi ni mkuu, madam tumekutana leo basi yesu katenda miujiza”

    “ni kweli bwana Jacob, yesu amefanya makubwa na nadhani anakwenda kufanya makubwa”

    “yesu asifiwe bwana yohana”

    “amina”

    “haya nipe taarifa za jimbo lako”

    Aliuliza kumaanisha ampe taarifa ya makanisa yake yanaendeleaje… Mana hata huyu bwana yohana ni Bishop kama alivyo bwana Jacob.. Hivyo vipawa vyao ni sawa..

    “bwana weee, nataka Yesu afanye miujiza juu ya vijana wetu”

    Aliongea bwana yohana…. Huku bwana Jacob asielewe maana ya maneno ya yohana…

    “ni kweli ila sijakuelewa”

    “aaahhhh, juzi uliniambia kijana wako yupo karibuni kuja… Na ulisema ana kanisa lake lipo tayari, nami najua kabisa kijana wako baado hawezi kukabidhiwa kanisa bila kuoa… Nina binti yangu, kwanini yesu asifanye miujiza juu yao”

    Aliongea bwana yohana huku bwana Jacob akitabasamu…..



    Huku kanisani masikini eva ni mtu wa maombi hataki kushindwa na shetani juu ya watu wanaomuandama kumbe jana mzee wa kanisa alimtonya kuhusu akina janet… Sasa eva wa watu kila kukicha ni yeye na maombi, anamuombea mchumba wake afike salama… Lakini sasa uchumba wao unaingia dosari, bwana yohana nae ana binti yake, nae anataka waowane na mtoto wa Bishop jacob…..



    Sasa huku ofisini katika maongezi ya bwana Jacob na bwana yohana, yanayo husu muunganiko wa watoto hao wawili, na ni kweli sheria za kiwa mchungaji shariti uwe na mke… Japo wengi wanafosi tu.. Sasa leo bwana yohana anakuja kuzima ndoto za eva mwenye tegemezi la kuolewa na adam, mtoto wa mr Jacob……







    Katika dunia hii, hakuna kitu unachoweza kukiwekea mia kwa mia kuwa utakipa, na si katika simulizi kama hizi bali wapo watu waliotamani kupata kitu fulani katika maisha lakini hawakukipata kwa vizuizi tofauti tofauti… Sasa tukija katika upande wa mapenzi, unakuta wewe mwanaume kuna mwanamke unatamani sana kumuona, lakini kuna vigezo au vizuiz vitakavyo sababisha usimuoe.. Au wewe mwanamke una mwanaume unatamani akuoe lakini kuna vizuiz vingi sana ambavyo vitasababisha asikuoe..



    Sasa kwa mwanadada eva, masikini ya mungu, wao hali ya maisha kwao ni ngumu, yaani ni masikini lakini ni mcha mungu.. Kila kukicha yeye na ibada yeye na kanisani, yeye na Biblia, hio yote ni kuiombea familia yake na yeye mwenyewe apate mume bora katika maisha yake, na katika akili yake tayari keshapata mchumba, tena wanapendana sana, na mchumba mwenyewe ni Adam,.. Na Adam huyo huyo ndio anapigiwa debe na Bishop yohana kuwa amuoe mtoto wake….



    Sasa tuje huku ofisini kwa mr Jacob

    “kwanza tumsifu yesu Kristo mr yohana”

    Aliongea mr Jacob huku akitabasamu kwa mbaali kuonesha kiwa ombi la bwana yohana ni zuri sana ila litakuwa na mashaka…

    “milele amina”

    “umeleta jambo zuri sana tena katika wakati muafaka… Lakini katika uwepo wangu pale nyumbani, nasikia sikia kuhusu mchumba wa adam, ila sijafuatilia sana kwa ukaribu mana mimi sikutambulishwa lakini mke wangu analifahamu hilo… Sasa huoni katika hali hii tunaweza kuwavurugia”

    Aliongea mr Jacob, mana kweli anasikiaga habari za Eva kuwa ni mchumba wa adam… Lakini hakutambulishwa…

    “ni kweli bwana Jacob,.. Hata mimi mtoto wangu nilizisikia habari kuwa na mchumba.. Ni mwinjilisti mmoja hivi sasa kwa hadhi ya familia yangu, mtoto wangu hawezi kuolewa na mwinjilisti… Mimi kama baba nilikataa hilo na kakubali… Kwanini usitumie nguzo ya uzazi.. Mana wakijichagulia wenyewe tutaonekana sisi hatuna malezi bora.. Na istoshe mtoto wangu nimemlea katika imani.. Yaani sijui niseme nini… Atukuzwe bwana yesu”

    Aliongea mr yohana huku akimsifu yesu Kristo kwa neema zake

    “amina”

    Aliitikia mr Jacob huku kweli akiingiwa na maneno ya Bishop mwenzie kama yeye…

    “mr Yohana… Kweli mwanangu a DC am ananisikiliza sana, lakini kwenye hili swala… Hahahahaha, sina hakika”

    “basi inaonekana mtoto wako hujamlea vyema”

    “tena hakuna mtoto mwenye heshima kwangu kama adam”

    “najua na ndio mana nimekufata rafiki yangu wa zamani sana”

    “basi wewe niache hilo.. Nitalifanyia kazi”

    “bwana yesu ni mkuu… Hakika hawezi shindwa jambo jema mbele za mungu”

    Saa hio hio maombi yalishuka, yaani hapo hapo kanisani.. Wafanyakazi kusikia maombi nao wakafumba macho na kuanza kuyapokea maombi toka kwa watumishi hao wa mungu….



    Tukija huku kanisani eva akiwa anatoka kanisani baada ya maombi, alikuwa akipita pita katika paking za magari, ikiwa ndio ngazi ya kupandia juu, hivyo akiwa kushika Biblia yake tayari kurudi nyumbani… Akiwa njiani alikutana na akina Janet…

    “shalom”

    Alitoa sifa kama salamu kwa akina janet,

    “shalom eva”

    “yesu asifiwe kwakweli”

    Aliongea eva kutoa sifa ya bwana wake mwokozi alie hai,…

    “unatoka wapi eva”

    Aliongea janet lakini ni kama kumkebehi, mana njia wanayokwenda ndio hio hio anayo toka eva, hivyo hakukuwa na haja ya kumuuliza sana

    “natoka kanisani janet… Esta hali yako”

    “safi tu”

    Aliitikia huku akiangalia pembeni, lakini eva alishaambiwa na mzee wa kanisa kuwa watu hao hawana ahueni nae, hivyo hilo analijua vizuri yu na hana shaka nalo

    “sawa safari njema kwako”

    Aliongea janet huku wakipishana,.. Wakati huo yapata saa 10 za jioni katika misa ya saa 10 ila akina janest wao walichelewa kidogo hivyo eva na waumini wengine walishamaliza ibada ya maombi ya siku hio…



    Sasa ikiwa masaa yamekwenda sana na sasa ni saa mbili za usiku,… Tukiwa katika nyumba ya bwana yohana, nae ana familia kubwa tu kama ya Bwana Jacob,… Ila bwana Yohana yeye ana watoto wanne.. Wakiume wawili na wakike waili.. Ila bwana Jacob yeye ana wakike watatu na wakiume mmoja… Sasa wakiwa wapo mezani wanapata chakula kama vile ilivyo kwa mr Jacob wakati wa kula hakuna kuongea,.. Na watoto walipo maliza kula, kila mmoja alishika kona yake ya kwenda chumbani kwake…. Na hapo baba ana jambo la kuongea na mama na ndio mana watoto wamesambaratika kila mmoja kona zake…

    “Mama Catherine…. Unajua tayari nimeshaongea na mtumishi jacob kuhusu watoto wetu”

    Aliongea bwana Yohana… Lakini mke wake alionekana kutopendezwa na hili mana kama vile atawauzi watoto

    “lakini baba Catherine… Huoni kuwa utamnyima mtoto raha ya maisha… Mana umeuvunja muelekeo wake”

    Aliongea Melissa ambae ndio mama wa familia ya mzee Yohana…

    “mimi ni mzazi ni lazima nifanye maamuzi kama mzazi…. Catherine ni lazima aolewe na mtoto wa mr Jacob”

    “nitafanya nini sasa… Sina cha kufanya juu ya maamuzi yako mtumishi wa mungu”

    “hayo ndio majibu sasa sio kupingana”

    Mama alikubali lakini ni ile kishingo upande… Sasa pendo ambae ndio mtoto wa pili akitoka Catherine mwenye miaka 21 anakuja huyu pendo mwenye miaka 16 hivi au 17..sasa alisikia yale maongezi ya baba na mama… Saa ngapi hajakimbilia chumbani kwa dada yake….



    “dada… Dada… “

    Aliita pendo huku dada akiitikia kwa hasira, mana alikuwa usingizini tayari keshalala…

    “nini we pendo, hujalala tu jamani mdogo wangu”

    “nimesikia kitu kwa baba”

    Aliongea upendo huku Catherine akiamka kwa hofu… Mana baba yake kawa mkali sana kwa sasa…

    “kitu gani tena”

    “baba kamwambia mama… Utaolewa na yule mkaka hensam”

    Sasa upendo kumbe anamjua Adam vizuri sana…

    “mkaka hensam??? Mkaka hensam ndio nani”

    “dadaaa…. Unakumbuka mwaka uliopita, tulikwenda kwenye harusi ya rafiki yako wanjiku… Sasa yule aliokuwa akifungisha ndoa ya wanjiku,… Mtoto wake sasa ndio anatakiwa kukuo wewe”

    “unamaanisha mtoto wa mchungaji jacob”

    “haswaaaa”

    “anaitwa adam”

    “ndio huyo huyo… Japo naskia hayupo”

    “ndio hata mimi najua hayupo… Ila baba ndio kasema”

    Aliuliza kwa umakini mkubwa sana Catherine huku akionekana kama kuipenda taarifa hio…

    “ndio.. Na mama kakubali… Dada yule mkaka ni hensam afu kwao kuna hela”

    “Peleka ujinga huko.. Kwani siai hatuna hela”

    “sawa ila wao wametuzidi ai tuseme ukweli tu”

    “ondoka nenda kalale”

    Upendo aliondoka lakini huku nyuma, Catherine alionekana kushika kifua chake na kuanza kutabasamu… Kumbe nae anampenda adam sema alisikia kuwa adam ana mchumba wake, hivyo akakata tamaa ya kumpenda, sasa ile ndoto yake ni kama imerudi tena kivingine…. Catherine alikuwa ni mzuri.. Mweupe, ana umbo la kipekee, yaani tuseme uzuri wa eva na Catherine ni sawa sema tofauti ni rangi… Catherine ni mweupe, na Eva ni maji ya kunde,.. Ila wote wana maumbo ya kuvutia… Ila Catherine yeye, kidogo anapenda mavazi ya kisasa, hapo ndipo atakapomshinda eva..

    Catherine aliingia Google na kuanza kumtafuta adam katika mitandao ya kijamii,…. Alipomuona roho ilimpasuka na kujikuta anamuita..

    “mume wangu… Mungu kajibu maombi yangu,.. Nilikuwa nikikuota usiku na mchana lakini leo ndoto zinakwenda kuwa kweli”

    Aliongea hivyo kwa sauti huku akiiangalia ile picha….



    Mara mama yake kaingia hapo chumbani, kumbe mama alikuwa akilia jinsi mtoto wake alivyochaguliwa mume… Lakini mama alipoingia hakujulisha kama alikuwa akilia…

    “hujalala tu”

    “ndio mama… Hata usingizi hauji”

    Aliongea Catherine huku akiificha simu yake ili asionekane kama kakubali sana kuolewa na adam..

    “au umesikia wazo la baba ako ndio mana hujalala”

    “wazo gani tena hilo mama”

    Catherine alijifanya hajui chochote kuhusu wazo la baba yake

    “amesema eti uolewe na mtoto wa mchungaji Jacob”

    “mmmhhhh mamaaaa… Sasa na mwinjilisti wangu je”

    “Catherine, ina maana bado hujaachana na huyo mpumbavu”

    “yesu wangu mama… Ina maana keshakuwa mpumbavu tena”

    Kumbe mama aliongea vile kwasababu baba alikuwa akipita huko kwa nje, sasa hakutaka kujulikana kuwa yupo tofauti na mumewe,…

    “mamaaaaaa jamani”

    “ah ah… Sikia sasa… Mimi sipo tayari uolewe na mtoto wa jacob, mana yule ana mchumba wake, afu istoshe yule kijana katembezwa sana na baba yake nchi mbalimbali, anajua starehe za kila aina… Mi sitaki uolewe nae”

    Catherine alinuna ghafla, mana hata huyo mwinjilisti sio kuwa alimpenda sana,…

    “mama mbona mimi nimekubali”

    Mama kusikia hivyo alishtuka na kumwangalia mwanae kwa hasira

    “unasemaje wewe”

    “mama, nilikuwa nikimpenda sana adam, nilikuja kupoteza mawazo juu yake baada ya kusikia ana mchumba”

    “ivi Catherine nikuulize swali”

    Mama alibadirika kabisa na kua na hasira…..

    “swali gani tena mama”

    “ivi usichana wako unao wewe…. Mana ile familia ni ya kitajiri haswa, na haitaki mschana ambae hana bikra…. Sasa kama huyo mwinjilisti wako umeshampa…. Jua adam sio wako mama.. We jishaue tu”









    Katika maisha ya kuoa kuna wanaume hawajali uthamani wa mwanamke, nikimaanisha BIKRA… Na wengi wetu hua tunaoa wanawake wasio na bikra, lakini kuna mahali mwanamke akukosa bikra tu, basi hata kuolewa kwake ni kwa tabu, hususan Zanzibar… Mzanzibari akikosa bikra ataolewa sawa lakini ataishi kwa masimango sana, na hata familia haitompenda sana mana wanahisi kaleta nuksi katika familia yao… Au kama hana bikra pia huenda akaolewa mke wa pili… Kule wanajali sana bikra tofauti tanganyika yetu.. Hua tunaoa tu… Lakini kama na sisi tungelikuwa na mikakati kuwa bila bikra mwanamke haoleki,.. Walahi nakuapia ungekuta kila mschana ana bikra huko mtaani… Lakini sasa hakuna.. Na pia Tanzania wapo ambao bila mwanamke asie na bikra haoi….



    Sasa tukiwa katika simulizi hii ya YOUNG PASTOR, kumbe mr Jacob hataki mtoto wake aoe mwanamke asie na bikra,… Sasa hapa Catherine alikuwa akiulizwa na mama yake kuhusu usichana wake upo au keshampa yule mwinjilisti wake…



    “ivi usichana wako unao wewe…. Mana ile familia ni ya kitajiri haswa, na haitaki mschana ambae hana bikra…. Sasa kama huyo mwinjilisti wako umeshampa…. Jua adam sio wako mama.. We jishaue tu”

    Aliongea mama huyo aitwaye Melissa, ambaye ndio mke wa mr Yohana au Bishop yohana..

    “niambie, mbona wantumbulia macho mimi”

    Mama alikuwa mkali sana juu ya mtoto wake, mana yeye roho ilikuwa ikimuuma kwa kitendo cha mtoto wake huyo kuchaguliwa mchumba ingali ana mchumba wake,….

    “mama, toka nizaliwe… Simjui mwanaume wa aina yeyote ile… Kama huamini nikague uone”

    Aliongea Catherine huku akiamka na kuanza kufunua ahumizi lake ili mama amkague

    “nitolee ujinga wako apa”

    Aliongea mama yake Catherine huku akiondoka na kufunga mlango kwa hasira,… Sasa swali linakuja je? Mbona mama hataki mtoto wake aolewe na adam, kwanini??… Hapo kuna jambo zito hatulijui tu…

    Wakati Catherine bado anaendelea kuangalia picha ya Adam katika mitandao ya kijamii, akiwa anahubiri katika moja ya makanisa yao mwaka uliopita, mana mwaka huu wote hakuwepo Tanzania, hivyo hizo ni picha za awali tena katika tovuti ya kanisa lao, mana adam hata mitandao ya kijamii hajawahi kujiunga… Sasa Catherine alichukuwa picha kadhaa katika tovuti moja inayomiliki makanisa yote, yaani makani yote ya Bishop Jacob, habari zake hupatikana katika tovuti moja… Hivyo Catherine alichukuwa picha kadhaa na kuziposti kwenye ukurasa wake wa Instagram, na kuandika maneno kadhaa katika picha hizo.. Na wakati huo ni usiku yapata kama saa 4 hivi



    Kesho yake ikiwa ni siku nyingine tena,… Catherine aliamka akiwa na furaha sana kwa swala lile, sasa inashangaza kuwa kwanini Catherine alimpenda huyo mwinjilisti ingali alikuwa akimpenda adam… Hapo napo kuna maswali…. Catherine hata kuoga kwake, alikuwa akimuwaza tu adam, yaani sijui ampe nini baba yake kwa kufikiria jambo kama hilo… Hivyo Catherine yupo tayari Eva amkose adam…. Wakati huo mzee yohana nae alikuwa akijiandaa kwenda katika shughuli zake za kawaida, mana ukishatoa wito ulioagizwa na mungu wako juu ya watu wake basi hakuna shida hata ukienda kutafuta kula…



    Wakati huo huku nyumbani kwa akina Eva,… Msichana mpole mtaratibu, akiwa anafanya usafi huku akiimba kwaya za kumsifu bwana yesu…

    “yeeeesuuu alinitendea weema, na kila siku nipo naeeee”

    Sasa akiwa anaimba mara ghafla mama yake katoka…

    “heee eva mwanangu hujaenda kanisani”

    Aliongea mama huyo wakati huo anatoka nae kuelekea kanisani,..

    “mama, bite hayupo kaenda shule… Sasa nani atafanya usafi”

    “sawa.. Hebu hakikisha misa ya pili haikosi sawa mwanangu”

    “sawa mama… Tumsifu Yesu Kristo”

    “milele amina”

    Mama alibeba Biblia yake huku akielekea kanisani…



    Sasa huku kanisani, kuna wale wasichana ambao hawapo kwa ajili ya kumwomba Mungu wao, kazi ni kufuatilia maisha ya watu, hususan ya mwanadada Eva,…

    “heheheheeeee, Yesu kafanya miujiza kwakweli janet”

    Alikuwa ni esta aliomkuta janet akiwa katika bustani ya hapo kanisani anajisomea Biblia,…

    “wewe esta.. Hebu tulia kuna ukurasa unanipa ashki ya kuusoma”

    Aliongea Janet ambae ndio mbea mkubwa lakini cha ajabu umbea aliokuja nao esta Janet haujui…

    “ivi janet, ulijuaje kuwa eva hatoolewa na adam”

    Sasa wakati wanaongea hilo, na mama yake eva ndio anatokea na kusikia hilo neno, japo eva wako wengi, lakini aliposema na adam… Huyu mama ikamjia tu huenda ni eva wake,..

    “una maana gani esta”

    “iv unamjua yule mschana wa mtumiahi yohana”

    “yuleeee… Ndio ana wasichana wawili.. Catherine na Pendo”

    “sasa huyo Catherine… Ona alichoandika juu ya picha ya adam”

    Esta alifungua simu yake na kumwonyesha janet…..





    yalikuwa ni maneno yalioandikwa katika picha alioipost Catherine katika akaunti yake ya Instagram,… Sasa janet alivyo hakaushi kaamka kwa furaha na kupiga kelele

    “nilisema mimi…. Masikini na tajiri wapi na wapi… Mi najua tajiri kwa tajiri masikini na masikini mwenzie”

    Sasa mama eva ndio anasikia hizo habari na kushindwa kuelewa inakuwaje hapa, mana kasikia kila kitu kasolo tu hayo maneno yalio andikwa katika picha ya adam huko Instagram,…

    Mama roho ilianza kumuuma, mana mtoto wake atakuwa katika hali gani endapo atasikia taarifa hizi..

    “Eehh mungu wangu… Pokea maombi ya mwanangu”

    Aliongea mama huyo huku akinyoosha mikono juu katika msalaba uliopo mlango hapo ikiwa na sanamu la Yesu katika msalaba huo…. Mama aliingia ndani lakini akina janet hawakujua kuwa mama eva aliwasikia wakiongea jambo hilo.. Mama alitamani kumwambia mwanae kupitia simu, asije kanisani  lakini sasa alisita mana ni sehemu ya kila mja kumwomba Mungu wake…



    Sasa huku nyumbani kwa akina adam, au Bishop Jacob,.. Akiwa anafungiwa tai na mke wake…

    “sisi leo hatutofika mana tunakwenda kumpokea mtoto…. Na wewe pia usichelewe huko”

    Aliongea mama huyo huku akimkaba mtumishi tai yake…

    “nyie kampokeeni tu…. Ila nitamjulisha mr Yohana kuwa, amtaarifu mtoto wake kuwa adam anakuja”

    Sasa mama adam yeye bado hajagusiwa kuhusiana na habari za adam kumuoa mtoto wa mr yohana..

    “sasa huyo mtoto wa mr yohana na adam wanahusiana vipi”

    “heeeeeeee, mama Jessica, ivi sijakwambia”

    “umeniambia lini mimi jamani baba Jessica”

    “Mr yohana, kasema yupo tayari mtoto wake aolewe na adam… Na sasa adam anatakiwa kuwa mchungaji rasmi, na kama ulivyosema kuwa hawezi kupewa uchungaji bila kuoa… Sasa sio vibaya kumuoa mtoto wa yohana”

    Mama kusikia hayo maneno, kwanza alishika kifua chake kuashiria hio habari kwake sio sahihi kabisa… Mana huyu mama anamjua mtoto wa kike mkubwa wa mzee Yohana, ni mschana mzuri sana na ana tabia nzuri lakini… Mama adam anamjua kiwa Catherine havaagi nguo za heshima japo sio mhuni lakini nguo zake ni za kisasa mno, kitu ambacho mama adam sidhani kama atakubaliana nacho…

    “sasa hapa tunapoteza muelekeo wa mtoto wetu”

    Aliongea mama Jessica huku akiwa hana hata nguvu, mana mume akiamua kitu, basi hata mke kuzuia ni asilimia chache sana….

    “kwanini mama Jessica….. Mtoto wa mr Yohana si unamjua wewe…. Sio mbaya akiwa mwali wako… Nipe koti langu niende kanisani”

    “baba Jessica…. Adam ana mchumba wake lakini”

    “sikutambulishwa, hivyo simjui… Aoe mwanamke ninaemjua mana mr Yohana ana maadili mazuri hivyo najua hata watoto wake watakuwa kama baba yao”

    Mzes Jacob alichukuwa koti lake kisha huyo kaelekea katika gari yake.. Na wakati huo mr Jacob anampigia aimu mr Yohana kuwa amwambie mtoto wake Catherine aelekee Airport mana adam anawasili leo katika uwanja wa ndege wa KIA (Kilimanjaro International Airport)

    Mama alikuwa akisikia taarifa hio ikotolewa kwa njia ya simu.. Lakini mama akiwa na huzuni juu ya mtoto wake kuozeshwa mwanamke ambae ana tabia ya kisasa, japo kwa namna moja ama nyingine ni mschana mstaarabu, lakini mavazi yake tu ndio shida kwa jamii.. Mana hata kanisani kwao yeye hajali anachokivaa…

    “mama, mbona umekuwa mnyonge hivyo, na ulisema leo unapika chakula kizuri kwa ajili ya kaka adam”

    Alikuwa ni Jessica mtoto wa kwanza katika familia hio, ana miaka 28 na adam ana miaka 24,… Kisha anafuatiwa na martha 20  na maria 15, yaani mama kawapangilia vyema watoto wake, wasipishane sana….

    “Jessica, ivi umelisikia wazo la baba yako”

    Aliongea mama huyo kama vile anataka kumpa taarifa hio…

    “taarifa gani tena mama”

    “kasema, Adam atatakiwa kumuoa mtoto wa mr yohana”

    “Whaaaaat???…. Yule mvaa vimini au yupi”

    “huyo huyo”

    “baba kawaza nini lakini”

    “mimi hata sijui”

    “ila mama, yule mschana ni mzuri haswa”

    “mimi sihitaji uzuri wa sura au umbo… Nataka mwanamke mwenye tabia nzuri”

    “sasa mama… Na eva wa watu maskini kama namuona vile”

    “mimi hata sijui nitamwambia nini yule mtoto, mana anavyoniheshim… Mana anajua fika tayari mimi ni mama mkwe wake… Na nimeahamkubali eva kwa asilimia zote”

    “sio wewe tu…. Hata mimi nampenda sana eva… Ila kwa jinsi adam anavyompenda Eva… Heeee patachimbika hapa mjini”

    “kwanza… Mpigie simu eva aje nyumbani… Twende naye Airport”

    “sawa”



    Sasa huku nyumbani kwa akina Catherine, baada ya kupata taarifa kuwa adam anakuja leo na ndege ya saa kumi jioni… Huezi amini Catherine katoka kanisani mpaka nyumbani, hapo kitandani kwake kumejaa nguo na hajui avae ipi ili aende Airport kumpokea mtarajiwa wake… Na taarifa hio kapewa na baba yake live bila chenga, japo alianza kuisikia toka jana… Sasa hapo hajui avae nguo gani,.. Mama vimini…..



    Sasa huku kanisani mzee Jacob akiwa yupo kwenye lifti kuelekea ibadan… Alishika simu yake na kumpigia mtoto wake….

    “halooo, shalom”

    Huyo ni mzee Jacob, lakini sauti ya adam haisikiki hapo

    “habari ya safari mwanangu”

    Ni huyo huyo Jacob ama Bishop Jacob

    “ok sasa…. Katika watu watakao kupokea hapo Airport, mmoja wapo ni mtoto wa mr Yohana”

    Aliongea mzee Jacob huku kama vile adam kamuuliza kitu mzee wake

    “najua hujui baba…. Ila ndio atakuwa mkeo, baba yako nakuchagulia mke mwenye heshima bora.. Anaeijua dini na ana wlimu kama ulivyo mwanangu”

    Aliongea mzee huyo kwa kumsifia Catherine…

    “nimeshasema mimi baba yako.. Na hakuna wa kupinga hilo… Huyo mchumba wako mimi simtambui… Na usipofanya hivyo lile kanisa nitalibinafsisha kwa watu wengine”

    Adam alionekana kukataa swala hilo, lakini mzee akachimba mkwara wa hali ya juu kwa mtoto wake

    “adam, hata wazee wa kanisa hawawezi kukubalia kuwa mchungaji endapo hutakuwa na mke… Mchumba wako yupo hapo Airport anakusubiri.. sawa”

    Aliongea mr Jacob huku akiwa kama anamlazimisha mtoto wake amuoe Catherine…

    “hayo sasa ndio maamuzi mwangu… Hongera kwa kunielewa baba yako”

    Mzee Jacob alionekana kuwa na furaha juu ya adam kukubali wazo la baba yake…



    Baada ya masaa kadhaa kupita, familia ya mr Jacob ikiwa imejaa katika uwanja wa ndege mkoani Kilimanjaro,…. Lakini kati yao mtoto wa mr yohana yupo hapo hapo.. Na pia Eva nae yupo hapo hapo.. Lakini sasa Catherine yeye anajua tu kuwa adam ana mchumba lakini hamjui huyo mchumba mwenyewe, hivyo hapo EVA NA CATHERINE hawajuani kabisa, ila wanajuana tu ile kiumini umini, Eva anamjua Catherine kama mtoto wa Bishop Yohana, lakini hajui kama ni mchumba mwenzie….. Huo ni ubabe alioufanya mama yake adam, na wakati huo masikini eva hajui lolote kuwa kuna taarifa za kitoolewa na Adam…. Eva alikuwa anaruka ruka kwa furaha…. Masikini ya mungu, laiti angelijua kuwa hapo hana chake, basi hata hapo Airport asingetakiwa kuja, sasa mama Jessica au mama adam hakumwambia kitu eva…



    Dege kubwa liliokuwa linatua katika uwanja huo, yaani eva alitamani hata kuifuata ile ndege kabla haijasimama, lakini kapoozeshwa na mama mkwe wake, mana ni mwaka sasa umepita hajamuona mchumba wake,.. Walishuka abiria wote,… Na Adam alikuwa ni abiria wa mwisho kushuka

    Laaaa haulaaaa…..

    SHARBIN RASHIDI KINGAZI ndio mwenye jina la Adam katila simulizi hii, na ndio yeye akiwa kapigilia suti yake saafi… Kweli mwenye mali ni mwenye mali tu… Eva ndio mtu wa kwanza kumuona adam wake,… Yaani hivyo alivyoanza kukimbia, utapenda yani…. Sasa Catherine nae anashangaa huyu anaeanza kukimbia kwa kujiua ua ni nani… Hakuta kujua sana, ila nae alianza kumkimbilia adam… Wakati huo adam kashika kibegi chake.. Mana begi kubwa linabuluzwa na wahudumu wa hapo uwanjani…. Maskini Adam kasimama na asijue amkumbatie yupi kati ya wawili hao

    PATAMU APO……





    Katika maisha ya sasa tunasema mwanaume kama mwanamume lazima uwe na maamuzi ya kiume,.. Adam ni kijana mpole sana na kalelewa katika mazingira ya dini.. Na katika kukua kwake kote hajui undani wa mwanamke hata mmoja, yaani haijui siri ya mwanamke ikoje, mana yake ni kwamba hajawahi kutembea na mwanamke, na mwanamke alioapa kumuoa ni eva pekee ambaye nae ni vivyo hivyo hamjui mwanaume,.. Adam kabla hajaamua maamuzi yake alikumbuka siku anapanga safari ya kwenda Nigeria kimasomo zaidi..



    KABLA YA KWENDA NIGERIA



    “eva… Mimi kesho nasafiri.. Naomba uwe makini na mapepo wachafu juu yako”

    kitendo cha Eva kusikia kuwa Adam anasafiri, moyo ulimpasuka huku akishika kifua chake,…

    “baba mtumishi, unakwenda wapi.. Na unarudi lini… Hivi kuna usalama kweli huko”

    Aliongea eva huku akimshika adam bega lake,..

    “nakwenda kimasomo,… Si unaona kanisa langu linajengwa… Hivyo wacha nikajiongeze angalau”

    “lakini baba mtumishi, upasta siokusoma, upasta ni wito toka kwa mungu… Sasa kwanini lakini”

    “ni kweli,.. Wito numeshaupata na nimeupokea… Na hata sasa naweza kukabidhiwa kipawa hicho, lakini kuna njia ambazo natakiwa kupitia.. Kwa mfano mwanamke anaetaka kuolewa,.. Kabla hajaolewa wanasema lazima awekwe ndani, sasa ule wakati yupo ndani, kuna mambo mengi anafundishwa jinsi ya kuishi ndani ya ndoa yake… Hivyo mimi nakwenda kupewa makatazo yasiofaa nikiwa ndani ya kipawa changu,.. Au yanayo faa, hivyo sina shaka na kipawa changu eva.. Nipo makini sana”

    Adam aliongea adam mtoto wa mr Jacob,…

    “sawa, ila utarudi lini… Siamini kama nitabaki mwenyewe”

    “eva, niruhusu kwa moyo mmoja,.. Itanichukuwa mwaka mmoja”

    “yesu wangu na maria, Uuuuuuuuuwiiiiiiii, baba mtumishi, mbona unakaa sana”

    “ndio wakati unaotakiwa”

    “sawa, sina jinsi juu ya hilo… Naomba uape kwa jina la yesu na mungu wake.. Kuwa utanioa mimi”

    Aliongea Eva kana kwamba haamini kama kweli atamuoa, mana anajua Nigeria kumejaa wasichana warembo na wanaojua dini yao kuliko hata eva, na Adam anapenda msichana anaeijua dini na kuitumikia dini yake vilivyo, sasa huko Nigeria ndio wamejaa wasichana wa aina hio

    “naapa kwa jina la na la yesu na mungu wangu alie hai… Sintokaa kukuwcha eva,… Na endapo umeshindwa kujitunza eva, naomba siku narudi usinisogelee”

    Adam aliapa kisha hapo hapo akamwambia kabisa,… Mana uhusiano wao una miaka lakini hajawahi kumuomba mpaka waoane

    “baba mtumishi wangu… Kama sijajitunza, basi hata kanisani kwenu siji.. Mimi ni mali yako, mshukuru mungu, nakuoenda sana baba mtumishi wangu.. Nitajitunza kama alivyonitunza mama yangu… Nenda urudi baba nakusubiri wewe tu”

    “hata mimi nakuapia, sintokaa kujigusa ispokuwa kwako tu”

    “tumsifu Yesu Kristo alie hai”

    “milele amina”

    “baba mtumishi, unaondoka lini na saa ngapi”

    Eva alimuuliza adam…

    “naondoka kesho, ila itakuwa asubuhi baada ya misa ya kwanza kuisha.. Ila nitapelekwa na baba”

    “lazima nikuone mpaka unavyopanda ndege.. Nikusindikize mpaka mwisho”

    “lakini nitakuwa na baba”

    “nitapanda gari tofauti na yakwenu, lakini nikuone tu”



    Kwaho yake sasa adam na baba yake wakiwa ndio wanafika uwanjani, lakini kumbe eva alishafika kabla yao, shida ya eva amuone baba mtumishi wake anaondoka salama, alitamani kwenda kumuaga lakini iloshindikana, kwasababu mwanamke anaejieshim hatakiwi kujionyesha kwa baba mkwe mpaka utambulishwe, sasa anaejua utambulisho huo ni mama yake adam peke yake, ila baba bado haja tambulishwa,… Adam alimwona eva akampungia mkono kwa mbali… Lakini huezi amini eva aliona liwalo na liwe, hawezi kumpungia kwa mbalimbali kisa hajatambulishwa.. Huezi amini eva alitoka pale alipo na kumkimbilia adam au baba mtumishi wake.. Adam nae hakutaka kujua yupo jirani na baba yake…. Alinyanyua mikono yake kuashiria kumkumbatia eva,… Baba yake rajabu, alishangaa, japo huyo msichana si mgeni katika macho yake, mana pia ni muumini wa kanisa lake… Hakumuwazia sana mtoto wake,… Wakati huo mzee anasonga mbele huku nyuma adama na eva wanaendelea kuagana… Mpaka wanaachana eva anageuka nyuma na adam anaguka mbele kuuelekea mlango wa ndege husika…..



    MWISHO WA KUMBUKUMBU YA ADAM, KABLA YA SAFARI…..



    Sasa adam alipokumbuka hilo,… Lakini pia alikumbuka muda mchache uliopita alipigiwa simu na baba yake kuhusu Catherine,… Adam alitabasam kidogo kisha akaweka brifkesi yake chini na kuamsha mikono kuashiria mapokezi mazuri kwa anaekuja…. Adam alimkumbatia huku akiskia sauti ikisema

    “Ahsante sana mungu baba…. Umenirudishia baba mtumishi wangu”

    Alikuwa ni eva baada ya kukumbatiana na adam wake…. Sasa Catherine anashangaa mbona huyu mschana kakumbatiwa badala yake,.. Catherine hakuwaza mengi sana alijua labda ni muumini wa kanisa lao, hivyo Catherine yeye nguvu zake zote ziliishia kubeba kile kibegi kilichokuwa chini na pia alijiskia vibaya sana, mana kakimbia bure bila mafanikio yeyote… Haikupita muda na familia yote ikamzunguka adam

    “mwanangu, umenenepa wewe, haaa.. Yaani unataka kusema mimi mama yako nilikuwa sikupendi mwanangu”

    Aliongea mama yake adam huku akiwa na furaha ya kumwona mtoto wake tena,.. Dada yake adam nae hakuwa nyuma

    “shalom kaka D”

    “shalom…. Asa d ndio nini, umeanza uhuni dada eti ee”

    “amna bwana,… D nimehisi ni kifupi cha adam”

    “najua dada yangu una maneno mengi kweli wewe”

    Aliongea adam huku wadogo zake wakimsalimia kaka yao, ilikuwa ni furaha kuanzia kwa eva mpaka kwa familia yote, kasoro Catherine pekee,



    Gari ya familia iliandaliwa kisha wakapanda gari lao… Kisha haooo wakaondoka, ndani ya gari furaha iliyokithiri, eva ndio kabisa usiseme, ana furaha ya ajabu kuliko mtu yeyote hapo ndani,…



    Walifika nyumbani, maandalizi ya kupika yalianza,…

    “mama, naomba nimpikie adam”

    Eva aliomba nafasi ya kumpikia adam na wakati huo adam kakaa katika meza, sasa kuna kakitabu chake anapenda kukasoma pale anapokuwa mwenyewe,…

    “martha…. Martha?”

    Adam alimuita mdogo wake ambae ni martha,

    “Abee kaka”

    Aliitika Martha huku akimjia kaka yake

    “ebu niletee kibegi changu kipo katika gari”

    Aliongea adam huku martha akiharakisha agizo la kaka yake, wakati huo eva yupo jikoni, yaani eva keshakubalika na familia yote, swma ubabe wa mr Jacob kutaka mtoto wa rafiki yake aolewe na mtoto wake,.. Mama alikuwa karibu na mtoto wake akimuuliza habari ya masomo mana ni mwaka sasa toka aende Nigeria… Lakini sasa adam alisahau na sio adam tu bali wote walisahau kuwa pale uwanja wa ndege walikuwa wa9 na Catherine,… Hivyo Catherine ndio alibeba kibegi au briefcase ya adam ambayo ina vitabu vya mungu karibia kibegi kizima…

    “kaka sioni mbona”

    “aahhh we nawe akuizi huna macho”

    Wakati huo eva ndio analeta chakula, tayari keshapika, mama alimtabasamia eva kwa chakula alichopika… Na leo ndio mara ya kwanza eva kuingia kwenye hii nyumba, lakini kazoeleka ghafla tu na hapo yeye hajui kama kipo kinachoendelea juu yake..

    “unatafuta nini wifi nikakusaidie”

    “kaka kantuma kibegi chake”

    Sasa eva yeye ndie alipata kumbukumbu ya pale uwanjani…

    “kuna yule dada nilimwona pale uwanjani na ndie aliekibeba, kwani sio ndugu yenu yule”

    Aliongea eva,… Sasa mama ndio anafungukwa na akili,..

    “afu kweli, ivi Catherine alipita njia gani saa ile”

    Aliuliza mama yake adam, kisha adam akamuuliza mama yake kuwa

    “kwani si mlikuja nae”

    “hapana, alikuja kivyake na gari yake”

    “aahhhh… Afu mama, kuna taarifa nimepewa na baba kuhusu yule msichana, mi sielewi mama”

    Mama sasa roho ikamshuka, hayo maneno yalimkuna sana eva, na kutaka kujua kinaga ubaga cha huyo Catherine,..

    “mwanangu, hata mimi sielewi, ni asubuhi tu hapa baba yako ananiambia kuwa eti ndio mwanamke unaetakiwa kumuoa”

    Heeeeee Eva alikuwa nyuma ya mlango, anasikia, yaani ilibaki kidogo tu adondoke,.. Akajikaza kisabuni ila wakati huo alikuwa yupo na Martha, mana hata watoto sio wote wanajua hilo,.. Martha alimshika wifi yake mana anamjua kuwa anampenda sana kaka yake… Martha ni mschana mkubwa ana miaka 20,…

    “lakini mama, ina maana umeshindwa kumwambia baba nina mchumba… Au hajui hilo”

    “nimemwambia lakini akasema mimi sijatambulishwa”

    “sasa ngoja aje… Na eva asiondoke hapa amkute”

    “sasa unaenda wapi mwanangu”

    “nakwenda kuchukuwa kibegi changu”

    Sasa wakati adam anatoka, Martha akamwambia wifi yake kuwa

    “ambatana nae, mana najua huyo Catherine katumia akili kwasababu anajua ni lazima kaka adam atakwenda kule, hivyo nenda nae”

    Aliongea martha, mana anampenda eva kuliko Catherine,..

    “njoo kula kwanza baba”

    Mama Jessica alikuwa akimlazimisha adam ale kwanza, lakini hakutaka kufanya hivyo… Mana hasira zilishamjaa…..

    Wakati huo eva anatetemeka, ivi atamwambia nini mama yake, familia yake yote inajua ataolewa na adam, baadhi ya makanisa yao yanajua uhusiano wa adam na eva,..

    “baba mtumishi, naomba niongozane nawe”

    Aliongea eva huku akihisi kukataliwa na adam

    “yes, ni sawa twende, tena familia yao yote ikakujue”

    Eva hakuamini kumbe adam hakubaliani na swala la baba yake,… Eva aliingia kwenye gari na adam.. Kisha haoo wakaondoka,.. Kweli familia ya mr jacob ni tajiri mno..



    Sasa huku kwa mr yohana, Catherine akiwa kakumbatia begi la adam, yaani kusema kweli hata yeye anampenda sana adam..

    Mama aliingia chumbani kwa mtoto wake, alimkuta kashikilia begi dogo

    “wewe una nini… Mana ulitoka kwa furaha sasa mbona umekiwa hivyo mwanangu”

    Aliongea mama huyo, au mama mchungaji kwa mzee Yohana

    “mama, nimekwenda uwanja wa ndege, nimeambulia kubeba hiki kibegi tu”

    “aaahhhh ina mana adam hajakuona”

    “kaniona sana tu, ila kuna msichana ndio kamkumbatia badala yangu”

    “lakini Catherine mwanangu, nilikuambia adam ana mchumba lakini husikii”

    Aliongea mama huyo na hata yeye huyu mama hataki mtoto wake Catherine aolewe na adam, sasa hatujui ni kwanini

    “mama mimi nampenda hivyo hivyo tu, na nilikuwa sina nguvu kwasababu ni moyo wangu tu, lakini sasa hata baba kaingilia kati hivyo nina nguvu na lazima niolewe na Adam”

    Catherine hakutaka kukata tamaa, na kweli jambo likiingiliwa na wazazi, sidhani kama mtoto atapinga, tena haswa wazazi wa kiume… Hatari sana.. Lakini wakiwa wanazidi kuongea ghafla honi ilisikika nje ya geti lao, mlinzi alifungua geti kisha gari inaingia ndani… Alikuwa ni adam

    “haya si ndio huyo anaingia”

    Aliongea mama yake Catherine huku akifunua pazia…

    “nilijua tu lazima aje…. Mama twende ukanisaidie kuongea nae”

    “ati nini…. We ulifikiri napenda uolewe nae, sipendi hata kidogo.. Umuache mkaka wa watu mpole kiasi kile,.. Mwanangu… Kwani John kakufanya nini lakini”

    “mama tuachane na mambo ya John”

    Catherine aliongea hivyo huku akitoka nje na kile kibegi,…

    Wakati huo adam anashuka katika gari kwa hasira sana,.. Tena kwa dharau anakwenda kumfungulia eva mlango, na wakati huo Catherine anaona live bila chenga…

    “unamuona mchumba wake,… Kwanza ona nguo alizovaa… Pili muangalie juu mpaka chini, kama kuna kitu cha kisasa alichokitia mwilini, hebu jiangalie na wewe mwanangu, kila kitu mwilini mwako ni kitu cha kisasa… Haya Adam huyo hapo, mwambie kuwa unampenda”

    Melissa alimchana mtoto wake live bila chenga,… Kweli Catherine akijiangalia, uzuri anao, shepu anayo. Labda na tabia anayo… Lakini sasa mwili wake umejaa udigitali mwingi mnoo….

    “baba, karibu”

    Alimkaribisha mama kwa shangwe

    “Ahsante mama… Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina mtumishi”

    Adam alimgeukia Catherine kisha…









    Wanasema huezi lazimisha maji kupanda mlima hata siku moja, mzazi wa adam ambae anataka mtoto wake huyo kuoa mtoto wa rafiki yake mr yohana,… Lakini kwa upande wa mtoto wa mr jacob hakuridhika na matakwa ya baba yake,…



    Wakiwa uwanja wa ndege baada ya Catherine kukosa kumbatio toka kwa Adam, alifanikiwa kuondoka na begi dogo la Adam, na aliondoka nalo makusudi ya kwamba ni lazima angelikuja kule nyumbati ili alipate kumbatio kwa uzuri akiwa kwao,.. Kweli akili yake ilizaa matunda kwa kitendo cha adam kufika kwao, ila kupata kumbatio kama alilopata eva pale Airport, hakuweza kulipata…



    “baba, karibu”

    Alimkaribisha mama kwa shangwe

    “Ahsante mama… Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina mtumishi”

    Adam alimgeukia Catherine kisha akamsalimia kwa kumpa mkono

    “shalom dada”

    Aliongea adam huku akimpa mkono Catherine….

    “shalom”

    Catherine aliupokea mkono kiunyonge sana tena ni kwakuwa anamuheshim sana, mana kitendo cha adam kumwita Catherine DADA, alijiskia vibaya sana….

    “Samahani mtumishi… Iv huna taarifa zangu zozote”

    Catherine aliona bora kuongea tu, mana kama mtu mwenyewe hata haonyeshi kuwa na upendo juu yake

    “nimekuja kuchukuwa vitu vyangu, hio ndio taarifa niliokuja nayo”

    Aliongea adam huku akinyoosha mkono wake kuashiria anataka begi lake,….

    “Catherine, unamchelewesha mtumishi”

    Aliongea mama yake Catherine huku Catherine akilitoa begi hilo aliokuwa kalikumbatia,… Mtumishi adam alilipokea begi hilo na kumgeukia mama take

    “mama, asifiwe bwana yesu”

    “milele amina baba”

    “basi mimi naona niwaache”

    “mungu akutangulie mtumishi wangu”

    Aliongea mama yake Catherine huku adam akimpa eva lile begi,… Adam alimfungulia eva mlango, Catherine anaona live bila chenga…. Baada ya kumaliza akaja katika upande wake wa dereva, lakini kabla hajaingia aliita

    “Catherine…. Taarifa zako ninazo, lakini umechelewa… Nina mchumba na nakwenda kumuoa hivi karibu, ndio huyu hapa Eva… Bwana yesu akutangulie Catherine… Ahsante”

    Adam aliingia katika gari kisha huyooo,… Lakini alipokuwa anatoka getini akakutana na baba yake Catherine akiwa katika gari yake, Adam alishusha vioo na kumsalimia

    “Shalom baba mchungaji”

    “shalom mtumishi, habari ya uzima”

    “aahhh Tunamshukuru mungu.. Anatenda miujiza”

    “basi tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina”

    Mzee anajua fika labda adam kamleta Catherine mara baada ya kutoka airport, kumbe kilichofatwa huku ni begi tu… Mzee Yohana anaingia nyumbani kwake, anamkuta Catherine kuvimba haswa…

    “raha gani hii mwanangu, unaolewa na kijana mwenye heshima zake,.. Umeletwa mpaka nyumbani upewe nini mwanangu”

    Aliongea Bishop yohana bila kujua lolote, wakati huo mama yake Catherine yupo ndani anakaukia kucheka tu… Ile kimoyo moyo, mana kweli hapendi mtoto wake aolewe na mtumishi adam

    “baba,… Adam kaja na mchumba wake hapa”

    Aliongea Catherine huku machozi yakimlenga lenga,

    “Unasemaje?”

    “ndio, tena kaniambia kuwa huyo ndio mchumba wake na anatarajia kumuoa wiki hizi… Hivyo hahitaji usumbufu na mtu”

    Aliongea Catherine, wakati huo maongezi yakiendelea, tayari simu ilishawekwa maskioni siku nyingi sana,..

    “hello mr Jacob… Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina”

    “habari ya siku mbili tatu”

    “aaahh bwana yesu ashukuliwe sana”

    “Samahani mr Jacob, kijana wako hujampa taarifa juu ya kinachoendelea”

    Mr Yohana alimuuliza bwana Jacob

    “kwanini Unauliza hivyo ingali anajua kila kitu,.. Namuamini kijana wangu hana shida”

    Aliongea bwana jacob bila kujua kilichoendelea huku

    “numepishana nae getini kwangu hapa sasa hivi tu”

    “si unaona sasa, umbe kaja? Hawa ni watoto wetu bwana”

    “lakini nadhani hayupo tayari kwa hilo mana nimemkuta binti yangu kanuna na istoshe kaja na huyo anaesemekana ni mchumba wake”

    “unasemaje?.. Amekuja na huyo binti mwingine”

    “inavyosemekana”

    “hebu nipe hii siku ya leo… Tutayamaliza, wewe ni rafiki yangu toka utotoni, mpaka sasa tupo pamoja.. Nataka tuwe ndugu sasa, hahahahaha.. Bwana yohana kiwa huru bwana”

    Aliongea mr Jacob huku akiwa na furaha sana juu ya kutaka kumpa mtoto wake mke ambae ni mtoto wa rafiki yake

    “sawa mr jacob, staki binti yangu aolewe na vijana wa ajabu ajabu… Mimi ni mtu na heshima zangu”

    Aliongea mr yohana wakati huo Catherine ndio anazidi kujiskia raha na kupata nguvu zaidi mana swala hilo limeshikiliwa na wazazi,…

    “usijali kabisa ndugu yangu… Bwana yesu atuongoze”

    Aliongea bwana Jacob kisha simu ikakata,



    Huku nyumbani kwa akina adam akiwa ndio anaingia nyumbani kwao, Jessica aliwahi kumpokea mdogo wake, na anamheshimu sana mdogo wake,.. Jessica ndio mtoto wa kwanza katika hii familia,..

    “imekuwaje huko wifi”

    Aliongea Jessica huku akiingiza kibegi ndani,

    “wala hakuna lolote, alimwambia tu kuwa ana mchumba wake”

    Wakati huo wakiulizana hivyo adam hakuwepo hapo, kumbe alishatoka kitambo tu, na Wakati huo ni mida ya saa 11 za jione kwenda saa 12,… Adam alifikia kwenye nyumba moja mpyaaaa, ila imeshaisha ujenzi, kumbe adam ana nyumba kabisa yaani akirudi huko sio mtu wa kukaa tena kwa baba yake,… Ilikuwa ni nyumba kubwa mno na haistahili aishi pekee bali mke.. Katika nyumba hio kila kitu kilisha wekwa, yaani hapo ni kuhamia tu,…



    “ondoa hofu, lazima uilewe na kaka yangu”

    Ni huku kwa akina Adam, Jessica akiwa anamhakikishia eva kuwa ni lazima aolewe na adam,…

    “sawa wifi yangu, ila kama hili jambo wamelishika wazazi, huoni itakuwa ni hatari kwangu”

    “ondoa shaka, mimi namjua vizuri adam… Nimemkuza mwenyewe.. Namjua haoi mtu pale”

    Aliongea Jessica, lakini wakati huo eva anataka kirudi nyumbani,… Haraka haraka Jessica anampigia adam simu..

    “we subiri upelekwe mpaka nyumbani unaogopa nini”

    Aliongea Jessica huku simu ikiwa sikioni

    “sawa”



    “haloo mtumishi… Njoo basi umpeleke mwenzio nyumbani”

    Aliongea Jessica kwa kumuita mtumishi,.. Ni jina ambalo wamelizoea kwa watu wengi na pia kutokana na kipawa chake..

    “sawa nafika hapo sasa hivi”

    Kweli haikuchukuwa muda adam alifika nyumbani kwao na kumchukuwa eva,….



    Sasa huku kazini baba yake Adam anatoka kazini, anawaza cha kumwambia mtoto wake, kwanini kaenda kuleta fujo katika nyumba ya watu,



    Wakati huo mama yake eva alikuwa hana raha mana toka mchana hajamwona mtoto wake,… Bite ambae ndio mdogo wake na eva pia alikuwa ni mtu wa wasiwasi, tena mama ndio kabisa kwasababu asubuhi kuna maneno aliyasikia toka kwa akina janet,.. Mama na mtoto wake bitw wakiwa wamekaa hapo nje kila mmoja kashika tama, na tayari kagiza kameshaanza kutanda,.. Waliona taa za gari zikiwaelekea huku waliko…, taa iliwakera mno mana walikuwa katika dimbwi la mawazo,…. Ghafla gari inasimama karibu yao na adam anashuka na kumsalimia mama mkwe

    “mama, shikamoo mama”

    “marahaba baba, ooooohhh mtumishi? Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina”

    “karibu ndani”

    Wakati huo eva nae ndio anatoka ndani, bite akamkimbilia dada yake baada ya kusalimiana na shemeji yake,… Mama haamini kama leo mwanae kaletwa na gari japo aio mara moja kuletwa na gari, ila kwa sasa kuna changamoto kidogo hivyo lazima kuwepo na mshangao kiasi,…

    “karibu baba mtumishi”

    “Ahsante sana….”

    “biteeee, we bite… Hebu kalete maandazi haraka mtumishi apate chai”

    Aliongea mama kwa kumtuma bite, lakini adam alikataa kupata chai kwa maana ya kuwahi nyumbani,… Kweli kwa akina eva maisha si mazuri, yaani ni watu wanaomtegemea mungu vibiashara vidogovidogo ambavyo mama huyo huweka nje ya kanisa ili apate kuuza angalau hata juisi,… Na ukiwaona huezi jua kama ni watu wa dhiki, mana wahenga walisema kuwa, UMARIDADI HUFICHA UMASIKINI,… Ghafla simu ya adam iliita, kuangalia jina, alikuwa ni baba yake

    “haloo mchungaji”

    Aliita adam huku simu ikiwa sikioni

    “sijakukuta nyumbani upo wapi usiku unaingia huu”

    “aahh nakuja sasa hivi baba”

    “hebu wahi nina maongezi na wewe”

    “sawa”

    Adam hakutaka kuchelewa, alimuaga mama yake eva kisha akatoka zake nje… Aliingia katika gari lakini ghafla eva kaja nae kaingia katika gari,

    “nimeona sms yako, kuwa ukitoka nikufuate”

    Aliongea eva, kumbe hakutaka kumuita mbele ya mama yake…

    “ndio, kwani ni vibaya kumuita mama mchungaji wangu”

    “hahahahaha hapana si vibaya”

    “ok… Shika hiki kiasi, kitawasaidia”

    “lakini baba mtumishi”

    “lakini haitakiwi,… Ashukuliwe baba muumba kwa riziki kupatika…. Kwaheri, tuonane kesho kanisani.. Afu, naomba hio pesa ikiisha unipe taarifa,… Staki mama mkwe akakae juani tena, kuleni vizuri muombeni mungu sana.. Mwezi huu huu naweza kuoa”

    Aliongea adam huku akiwasha gari

    “Catherine au”

    Aliongea eva huku akiwa kashika tama

    “sina uwezo huo, naoa nilichokipenda.. Hata vitabu vya mungu viliandika, Mpende anaekupenda”

    Adam aliongea mengi sana,… Kumbe hata kabla ya adam kuondoka, yeye ndio alikuwa akitegemewa na familia ya eva,.. Mana baba yake eva alikuwa ni mzee wa kanisa moja wapo kati ya makanisa ya mr Jacob, hivyo baada ya kifo cha baba yake eva,… Adam aliamua kubeba jukumu zima la familia hio, mana mzee yule alikuwa akiishi kwa sadaka za waumini, sasa hayupo, nani achukue sadaka.. Hakuna…. Hivyo adam kachukuwa jukumu hilo peke yake…. Na anajua waliteseka sana kipindi yupo masomoni,.. Japo aliwaachia kiasi kikubwa cha fedha,..

    “mtumishi jacob kaniita, hivyo wacha nimuwahi”

    Aliongea adam kumaanisha baba yake kamuita….

    “sawa,… Naomba bwana yesu aingilie kati mahusiano yetu, mana tuna nia njema na huu ulimwengu”

    Aliongea eva,.. Na wakati huo ibada ikadondoshwa hapo hapo kwenye gari,… Mama na mtoto wake bite kusikia ibada inadondoshwa, nao wakaungana nao kwa kupiga magoti kisha kuomba sambamba na wao,..



    Baada ya maombi, adam aliondoka zake…. Sasa eva anakwenda kukagua kapewa kiasi gan,…

    “yesu wangu, kakupa pesa zote hizi”

    Aliongea mama yake eva huku wakizimwaga mezani,…

    “mama, unajua kweli mtumishi adam anaona mbali sana… Hivi kajuaje kuwa humu ndani tunaishi kwa uwezo wa mungu pekee… Kajuaje kuwa hatuna kitu.. Mama?? Ashukuliwe baba Muumba mbingu na ardhi”

    Kiukweli pesa walizopewa zilikuwa ni nyingi, kwa haraka haraka, labda ni kitu kama laki tano hivi, ila inazidi zaidi ya hapo…… Walifurahi sana na kuzidi kumuombea mtumishi adam



    Huku kwa mzee jacob akiwa kaketi Katika sofa la uvivu, yaani lile la kulala,… Ghafla alisikia honi ya gari,.. Alijua tu ni mtoto wake adam ndio anakuja… Kweli alikuwa ni adam, au mtumishi adam







    Wakati huo mzee Jacob baada ya kumsikia mtoto wake adam akiingia, basi aliitisha kikao cha dharura hapo ndani akiwemo mama na dada mkubwa wa adam,... Huku katika paking adam alipaki gari vizuri lakini hakushuka, sasa akawa anawaza ni jinsi gani ataongea na baba yake kuhusu swala la kuoa kwake,.. Lakini akiwa ndani ya mawazo, alikumbuka kitu fulani na kutoa simu yake na kumpigia mtu fulani ambae anajuana nae,..



    Baada ya kuongea na huyo mtu, adam alishuka katika gari, lakini kidogo alikuwa na tabasamu, sasa hatujui aliongea na nani na maneno gani,.. Adam aliingia ndani moja kwa moja mpaka mezani, mana alijua tu kukaa kwa watu hao mezani na hakuna hata mtoto wala mfanyakazi, alijua tu kuna maongezi yanaendelea hapo

    "asifiwe bwana yesu Kristo"

    Alitoa salamu ya kumsifu bwana Yesu Kristo...

    "milele amina"

    Waliitikia wote watu watatu,.. Lakini kabla hajakaa, ghafla simu yake inaingia meseji... Aliifungua na kuisoma kimya kimya kisha akaendelea kukaa...

    "ndio mchungaji, ulisema niwahi nyumbani"

    Aliongea adam huku anamwomba Mungu wake kwa lolote litakalotekea liwe zuri katika maisha yake,....

    "nyumbani kwa mr yohana ulifika saa ngapi"

    Aliuliza mr jacob

    "nilikwenda time za jioni hivi... Kuchukuwa begi langu"

    "begi?? Begi gani tena"

    "aahh wakati nashuka pale Airport,.. Alikuwepo mtoto mchungaji yohana, na yeye ndie aliepokea begi langu"

    "kwanini ulipokwenda huko ulikwenda na mwanamke, ingali nilishakupa taarifa kuhusu mtoto wa mr yohana"

    Aliongea bwana jacob, huku akihitaji jibu la kueleweka toka kwa adam

    "ndio baba... Kwanza samahani kama nitakukosea baba yangu,... Ni kweli ulinipa taarifa juu ya binti yule, lakini baba huoni utakuwa hunitendei haki kwa kunichagulia mke... Hapo utakuwa umenikosea baba... Kweli nataka kuoa lakini sikumtazama Catherine na pia hata kwenye akili yangu haipo kwa Catherine.... Baba, tafadhali sana, sijawahi kukutambulisha, ila nadhani ulishawahi kusikia, sasa mimi nataka kumuoa Eva na sio Catherine"

    Adam aliongea huku mama na Jessica wakitikisa kichwa kumaanisha sawa kabisa kwa kile anacho kiongea bwana adam...

    "yaani eva huyu mtoto wa marehemu paulo"

    "ndio"

    "nipe sababu saba za kumwoa eva"

    "sasa mzee... Nitakuja kuongea sababu hapa, mwisho utaniona nimetusi sasa... Naomba unipe nafasi ya moyo wangu mzee.. Yule msichana mimi simjui, tunakutana tu kwenye kumbi mbalimbali na makanisani, sijui tabia yake sijui ni mzima au naniii.. Eeeeeee babaaa"

    Sasa alipomaliza tu kuongea adam, mara mama nae akaingilia kati na kusema

    "ni kweli.. Kwanza yule mschana anavaa nguo za ajabu sana, yule msichana hata kanisani kwao utamkuta kavaa nguo za ajabu,.. Kwanini tumpe mtoto wetu mwanamke wa ajabu jamani baba Jessica"

    Aliongea mama tena kwa msisitizo mkubwa ili aeleweke,....

    "mimi nimeshasema.... Taka asitake lazima umuoe Catherine... We ulizani utabarikiwaje na mungu usipo oa?? Lazima uoe ili mungu akubariki"

    "sijakataa kuoa baba, tatizo ni mke"

    "nasema hivi napiga simu mwanamke aandaliwe wiki hii uoe na kanisa lako"

    "baba... Samahani sana.... Kama ni kanisa aitaki,... Wacha niwe mwinjilisti wa mitaani nikaitangaze injili kwa waumini waliokosa nafasi ya kufika makanisani... Sitaki kuoa iwe eva ama Catherine... Alafu kesho nahamia nyumbani kwangu"

    Aliongea adam kisha akaondoka,.. Wakati huo simu imeganda skioni kwa mr Jacob,

    "umeona sasa unamvunjia heshima mtoto wetu baba Jessica"

    Aliongea mama huku nae akiamka kumfuata mtoto wake kule alipo elekea, na Jessica nae huko huko... Mara mr yohana anapokea simu

    "haloo bwana jacob"

    "ahahahahah bwana yohana... Habari ya masaa mawili matatu"

    "aahh salama tu bwana jacob vp hali"

    Yohana alikuwa na furaha mana alijua anapewa jibu zuri juu ya adam kukubali kuoa

    "bwana hapa ndio nimemaliza kikao na bwana mdogo... Lakini kiukweli bwana yohana nguvu zangu zimeishia hapo, namuheshim sana kijana wangu... Na kitu ambacho nikiweza mpaka sasa... Sintokubali amuoe mwanamke anaemtaka yeye.. Ila sasa naomba umpe nafasi mtoto wako, awe karibu na kijana wangu, ili angalau wazoeane... Kwasababu hapa kwenye kikao kalalamika sana kuwa, hamtambui Catherine... Kwani wao hukutana katika kumbi mbalimbali na makanisani, sasa hawatambuani, hebu mpe nafasi binti yako awe karibu nae, angalau wajenge hata mazoea.."

    Alimaliza kuongea bwana jacob huku bwana yohana akijibu kuwa

    "aah hilo mbona halina shaka.. Mimi nataka tuwe ndugu kabisa... Sio urafiki tena, na undugu wetu utaunganishwa na watoto wetu"

    "sawa kabisa... Mwambie tu ajitahidi kiasi, mana bwana mdogo ana msimamo huyo, namjua mwenyewe"

    Aliongea bwana jacob wakati huo yupo peke yake hapo sebuleni,..

    "ondoa shaka, hapo watakutana, mana hata Catherine hana mchezo mchezo kabisa"



    Lakini mr Jacob kuna swali alimuuliza bwana Yohana kuhusu binti yake, na wakati huo huo adam ndio anakuja sebuleni kwa ajili ya chakula... Lakini adam aliposikia hilo swali alisita kuja sebuleni kwanza ili asikie vizuri, mana lilikuwa ni swali la siri... Na hata sisi wasomaji hatutakiwi kulijua.... Adam alisikiliza umakini mzee wake akimuuliza bwana yohana kuwa.....



    Hatujui kamuuliza nini lakini adam alisikia peke yake, na hata kuja sebuleni hakuja tena akaishia mlangoni na kurudi chumbani kwake

    Maongezi ya mr jacob na mr yohana yaliisha baada ya kupata vyema, hivyo kwa sasa Catherine ni yeye na juhudi zake za kuwa karibu na adam, kazi ipo hapo...



    Baada ya siku kadhaa kupita na leo ni siku ya Jumapili,.. Familia ya mr Jacob ikiwa katika maandalizi ya kuwahi kanisani katika misa ya kwanza, ikumbukwe kuwa adam toka arudi Nigeria katika chuo cha Biblia, alikwenda kuabudu katika makanisa mengine ya baba yake, mana kuna kanisa kuu na kuna makanisa ya kawaida, na hayo makanisa ya kawaida yana mapasta wengine, mana huyu mr Jacob yeye ni Bishop, hibyo kateua mapasta kwa ajili ya malanisa mengine, sasa kuna kanisa kuu ambalo Bishop mwenyewe hilitumikia kutoa huduma kwa waumini wake,... Sasa kanisa hilo kuu adam hajawahi kufika toka aliporudi masomoni,.. Sasa leo Jumapili ndio anakwenda katika kanisa hilo, wote walikamilika walikuwa kama watu saba hivi skose.. Baba, mama, watoto wanne, na mfanyakazi wa ndani wa kike.. Walipanda katika usafiri tofauti tofauti,... Bishop Jacob alipanda yeye na mtoto wake wa mwisho na mke wake,.. Na adam alipanda yeye na mfanyakazi na dada zake wawili,.. Kanisa wanalo lielekea ni moja..



    Katika kanisa hilo wapo waliokuwa wakiabudu kwa mapambio,.. Na walikuwepo viongozi wenye vipawa kwa ajili ya kutoa huduma kwa waumini wao, na hapo ni katika hatua za kumsubiri mchungaji Jacob ama Bishop jacob kuja kutoa huduma ya neno la mungu,...



    "dada, sjui niwawahishe kwanza, mana nahitaji kwenda kumchukuwa eva ili awahi misa ya kwanza"

    Aliongea adam wakati huo walikuwa njiani...

    "twendeni tu kwani gari si inatosha"

    Aliongea Jessica huku adam akikata kona katika njia ya akina eva, mana eva na mama yake na mdogo wake hua wanachelewa misa ya kwanza, na misa ya kwanza ni bora zaidi kuliko hata misa zinazifuatia... Uzuri aliwakuta wakiwa tayari wamejiandaa, mara moja walipanda gari ili kuwahi misa ya kwanza...



    Huku kanisani, Bishop Jacob akiwa tayari keshafika kanisani na huduma ilianza mara moja, lakini sasa katika waumini wa mbele, alionekana Catherine,... Hii siri ya Catherine kuwepo hapa anaijua mzee peke yake.. Mana aliambiwa kuwa aanze kujenga ukaribu na adam,.. Sasa ndio kaanza kuja kanisani kwao, na hata huyu Catherine wana makanisa mengi kama ilivyo Bishop jacob... Hivyo huku kaja kwa kazi maalumu,.. Bishop Jacob alianza kuhubiri kwa kishindo kama ilivyo kawaida yake,..



    Huku katika lifti ya kupanda juu akiwemo Jessica, Martha, sekwa, Eva, Bitris na mama yao,... Lifti ilifika mahala husika na walitoka ili kwenda katika ukumbi wa maombi, sauti ya Bishop Jacob inasikika ikitoa mahubiri yake mazuri sana.. Lakini ghafla simu ya adam inapata meseji, hivyo kitendo hicho kilimfanya asimame na kuisoma mesji,.. Sasa yeye aliposimama wale aliokuja nao wakatangulia mbele,...

    "mwanangu, namuona Catherine hapa kanisani"

    Adam alishtuka, ilikuwa ni meseji iliotoka kwa mama yake,...

    Lakini hakujali, aliendelea na safari ya kuingia kanisani,...



    Sasa waumini walikuwa wakisikia tu mtoto wa Bishop Jacob karudi, lakini hawakuwahi kumwona kwasababu alikuwa hasalii kanisa hilo,...

    Sasa ile adam anaingia tu,... Hata baba yake alishangaa, waumini walinyanyuka wote na kusema

    "tumsifu yesu Kristo mtumishi adam"

    Hata adam alishangaa, yaani waumini wanampenda kupita maelezo,... Hata Catherine haamini kuwa kanisa zima limenyanyuka kwa ajili ya adam... Mzee jacob haamini, yaani mtoto wake anakubalika kuliko yeye,

    "asifiwe bwana mwokozi wetu"

    Aliongea adam huku akipunga mkono,.. Lakini sasa vile alivyokuwa akipunga mkono, waumini wengi walikuwa wakitetemeka,.. Adam anashangaa mbona baadhi ya wingi wa waumini hutetemeka... Akajaribu kupungia tena... Sasa kumbe adam hajajua kuwa sio waumini peke yao,.. Mana ndio alikuwa akiwapungia mkono,.. Ghafla ilisikika sauti ikisema

    "adam acha, inatosha, hebu chukua kiti na ukae"









    Kawaida ya kanisani au msikitini hapatakiwi kuwa na mapendo, mana pamejaa maombi na dua za kila aina kila siku,…. Hivyo hata pepo au shetani hana nafasi katika nyumba hizi mbili,… Lakini inashangaza ya kwamba katika kanisa kubwa la ROHO MTAKATIFU liliotakaswa kwa damu ya yesu, leo ninaonekana kuwa na mapepo,… Kivipi na wakati linaongozwa na Bishop Jacob, yaani ni wito ulio mkubwa kwa mungu baba



    Adam aliingia na waumini wote kunyanyuka katika viti vyao kisha wakamsalimia adam kwa furaha, mana ni mtu aliojaa upako, aliotakaswa kwa damu ya Yesu na akatakasika, na ni kweli sio uongo, adam hakutaka kukaa kimya kwa salamu ya waumini hao, ilibidi nae kwa furaha kuamsha mkono wake juu na kupungua huku akisema

    “asifiwe bwana mwokozi wetu”

    Lakini sasa cha ajabu na cha kushangaza, aliona watu wakitetema kila anapopunga mkono wake,.. Hio iliashiria kwamba waumini wote hawakuwa sawa,.. Lakini sasa kumbe sio waumini pekee, hata mr Jacob pia ilikuwa ikimtetemesha ile hali ya mkono ukipungwa, huku akitaja jina la mungu… Sasa kwakuwa adam yeye alikuwa haoni nyuma kuwa baba yake nae alikuwa akitetema, ndipo mama yake adam akapaza sauti kwa nguvu na kumfikia adam..



    “adam acha, inatosha, hebu chukua kiti na ukae”

    Aliongea mama yake adam huku akivutwa na mama yake,… Adam alishangaa hili kanisa limevamiwa na nini? Mbona limejaa mapepo kiasi hicho na baba yake akiwa mhudumu mkuu wa kanisa hilo….. Sasa adam alimsikiliza mama yake na kuketi katika kiti, lakini bado kulikuwa na waumini waliokuwa wakipiga kelele, mana wengine walikuwa wakitokwa na mapepo pale adam alipokuwa akipunga mkono,… Na adam mpaka hapo hajui kuwa hata baba yake alikuwa akitetemeka,…. Baada ya muda waumini walitulizwa na huduma ya kutoa neno la bwana ikaanza rasmi, mana palitokea mvurugano kidogo baada ya adam kuingia,…



    “tumsifu yesu Kristo”

    Aliongea mr Jacob lakini mpaka hapo ana wasiwasi sana mana kakutana na mtoto wake ni moto wa kuotea mbali, yaani hafai katika swala la kutoa huduma kwa waumini wake,…. Ibada ilifanyika vizuri na hatmae ilikwisha,.. Vipindi mbalimbali vilifanyika, misa misa zote ziliisha na kuna wale wa maombi ya chain player, waliingia na kuanza maombi yasiokatika…



    Sasa leo ni siku adam anahamia nyumbani kwake,.. Ni nyumba ya kifahari mno,.. Ukizingatia ni kuwa jana mdogo, ndio anaendea miaka 24 sasa,…

    “lakini adam mwanangu,… Wewe bado hujaoa, unahamia huko utaishi vipi,.. Utapikiwa na nani, nani atafua nguo zako, nani atafanya usafi wa nyumba yako mwanangu”

    Alikuwa ni mama yake adam, wakati huo adam alikuwa akipaki nguo zake katika begi, mana kila kitu kule kipo ni yeye kubeba nguo zake na vitu vyake vya thamani,…

    “mama, wacha nihamie kwangu,… Bwana yesu yupo nami,.. Kama mkate mmoja uliwatosha kundi la watu wa bwana Yesu, sembuse mkate mmoja usinitoshe mimi, kwanini”

    Aliongea adam huku akimalizia kupaki nguo zake

    “Kwahio unataka kusema kuwa utakwenda kushindia mkate si ndio”

    Aliongea mama Jessica, mana hataki mtoto wake ahame hapo nyumbani, ingali anatakiwa kuhama..

    Lakini wakiwa bado wanazozana na mama yake mara dada  yake kaingia

    “Jessica,.. Mdogo wako ndio anakwenda hivyo”

    Aliongea mama huku akimuonyeshea Jessica kwa kidole

    “anakwenda wapi? Zimbabwe au”

    Jessica alileta utani mbele ya jambo la usiriasi

    “staki utani wako Jessica… “

    Mama aliongea huku akiwa hataki kweli utani

    “mama, mi naona kweli akae peke yake, mana akizidi kukaa huku, baba atazidi kumbana na kushindwa kufanya mambo yake”

    “kumbuka kuna usafi kule, kumbuka atatakiwa kupika huyu”

    Aliongea mama Jessica

    “mama, mimi nitajitolea kumfanyia usafi kila baada ya siku tatu”

    Jessica alivunja ukimya na kusema kuwa yupo tayari kufanya usafi kila baada ya siku tatu,…

    “iv Jessica kwanini unataka twende tofauti na mimi lakini”

    “mama,… Adam keshakuwa mtu mzima, wacha akae mbali na baba ili kidogo heshima ije”

    Walikuwa wakibishana lakini ilikuwa ni kazi bure,… Adam alimaliza kukusanya nguo zake kisha akazitupia katila gari yake… Mana kama ni mali keshapewa nusu ya mali na baba yake… Hivyo hamtegemei baba yake kwa lolote lile, hata kanisa na hio nyumba pia hakujenga kwa pesa za baba yake, ispokuwa zakwake… Baba alishiriki tu kusimamia ujenzi wa kanisa lakini hana asilimia yeyote katika kanisa hilo



    “labda niwatakie siku njema, mana ndio nakwenda hivi ili niwahi kuandaa vitu vingine”

    Aliongea adam huku akitoka zake

    “adam mwanangu… Usije ukaajiri msichana wa kazi, utakosa sifa za kuchaguliwa na wazee wa kanisa”

    Aliongea mama yake kwa msistizo mkubwa sana

    “mama, najua kila kitu kuhusu hilo.. We ondoa shaka… Baba yangu ananionea sana… Lakini bwana Yesu yupamoja nami”

    “milele amina baba”

    Waliongea ongea kwa kiasi fulani kisha adam huyoo, lakini alisindikizwa na dada zake na mama pia,… Walifika katika nyumba hio mama akamtangulia mtoto wake kuingia katika nyumba hiyo,… Maombi yalianza mara moja ili kama lipo baya basi liweze kutakaswa kwa damu ya Yesu, maombi yalichukuwa muda kiasi fulani, kisha wakaingia ndani,… Basi dada zake na mama wao walianza kufanya usafi, mana si unajua nyumba mpya, lazima kidogo kuwe na usafi japo ilishafanyiwa Usafi muda mrefu, sema hapo ni kama kufuta futa yu… Adam yeye alikuwa akizunguka zunguka huko nyuma ya nyumba kama vile anakagua baadhi ya mambo, wakati huo anaimba nyimbo za kumsifu bwana Yesu Kristo,…. Lakini ghafla simu yake inaita, kuangalia jina alikuwa ni mzee wa kanisa

    “haloo mzee shalom baba”

    “shalom… Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina baba”

    “unahitajika huku kanisa nitajitolea haraka sana”

    Simu ilikata ghafla na kushindwa kuelewa kwanini kaambiwa anahitajika haraka sana,.. Adam hakutaka kujiuliza mara mbili,

    “bwana yesu kuwa nami kila hatua”

    Alinuia baadhi ya maneno kisha akapanda gari

    “baba mtumishi, unakwenda wapi tena”

    Aliuliza mama yake mzazi

    “nimehitajika kanisani mara moja”

    “sawa, uwahi kurudi basi mana hatutochukuwa muda”

    “sawa mama”

    Adam aliondoka kwa usafiri wake, yote hio ni kuwahi alipoitwa na mzee wa kanisa….. Sasa huku ndani sasa mama alimuuliza mtoto wake ambaye ni Jessica kiwa

    “hiv Jessica, umeona kilichotokea asubuhi wakati adam anaingia”

    Aliongea mama huku Jessica nae pia akishangaa

    “mimi pia nilishangaa,.. Kwasababu hata baba nilimwona akitetema kwa maneno machache tu ya adam”

    “sasa lile kanisa linaongozwa na nini, kwasababu sio waumini pekee mpaka mchungaji nae ana hali mbaya”

    “mama, hapa kuna kitu, lakini bwana Yesu Kristo atajafa miujiza na atatakasa kila pembe ya njia yetu”

    “amen”



    Huku kanisani sasa adam akiwa katila lift kuelekea kanisani, na hio ni siku ya Jumapili ambapo asubuhi ndio alifanya kile kituko,… Sasa ile anafika tu ndani ya kanisa, alikutana na viongozi mbalimbali wa makanisa hapa jijini Arusha,.. Lakini alipoangalia vizuri alimwona Catherine na baba yake, ghafla akamwona hata baba yake mr jacob, lakini mr Jacob alikuwa katika moja ya jasira mno,… Adam alijua sasa hapa kumekucha, akiangalia vizuri mpaka wale wanaohusika na mambo ya ndoa wapo, hapo tumbo la adam likaanza kuwaka moto,… Mana hakuutegemea huu wito utakuja kuwa hivyo,

    “asifiwe bwana mwokozi wetu alie hai”

    Alitoa salam huku akivuta kiti akae,

    “milele amina baba mchungaji”

    Adam alikuwa na hofu, mana hapo hakukuwa na muumini mdogo mdogo hata mmoja, yaani wote hapo ni viongozi wakubwa wa makanisa mbalimbali hapa jijini, yaani muumini mdogo mdogo ni Catherine peke yake, sasa haijulikani pana kikao gani









    Adam alikuwa haamini kama leo anafungishwa ndoa ya lazima lazima, mana kama ni kanisa lake tayari limeshakamilika kila kitu, ni yeye kuchaguliwa kuwa mtoa huduma katika kanisa hilo, mana kama ni wito anao na tayari keshapokea wito kuwatumikia kondoo wa bwana,.. Adam alianza kukusanya hasira, na hapo ni mbele ya viongozi mbalimbali wa makanisa yote hapa jijini Arusha… Mabishop wote wamejaa hapo, na haijulikani kuna nini… Lakini wakati adam akiendelea kuwaza kuhusu kikao hicho, ghafla lililetwa joho la rangi nyeusi mchanganyiko na nyeupe,.. Tena joho jipyaaaaa…. Hajakaa vizuri mara yliletwa maji ya baraka,.. Mpaka hapo adam aifurahi sana, na hapo hapo Mabishop wakaanza kufurahi na kupiga makafiri,…

    “haleluyaaaaaaa”

    “ameeeeeeen”

    “nasema haleluya”

    Alisifu Bishop mmoja mkubwa hapo jijini, huku viongozi wengine wakipokea sifa hio,…

    “aaaameeeen”

    “bwana asifiwe sanac

    “ameeen”

    Maji ya baraka yaliletwa kisha akamwagiwa adam,… Yaani hapa sasa ndio anaupokea wito wa kuwa mchungaji rasmi, mana mchungaji wa kanisa ni lazima uchaguliwe na wakuu wa makanisa, sio lazima Mabishop wawepo, hata pasta wa kawaida anaweza kukuchagua kuwa pasta.. Ila sema mr Jacob yeye anajulikana sana na hakupenda mtoto wake apokee wito kwa kusua sua,..

    “mpaka sasa umeshapokea wito, sasa unaweza kuliendesha kanisa lako… Bwana yesu asifiweeeeeeee”

    “aaaaaaaaaaaaaaameeeeeeeen”

    Zilikuwa ni shangwe japo hapakuwa na waumini wengi zaidi ya hao hao viongozi,.. Yaani muumini anatakiwa kusikia tu kuwa tayari mambo yamekuwa mambo,… Mwanamke wa kwanza kumrukia adam alikuwa ni Catherine,… Adam alitamani sana kumkwepa lakini ilishindikana kwasababu kuna baba yake binti, kuna baba yake huyo adam… Afu watu wakubwa walikuepo, na hapo ndio kwa mara y kwanza Catherine analipata kumbatio la adam.. Kumbe Viongozi wote wameshajuzwa kuhusu adam na Catherine, saaa ngapi hawajaanza kusema

    “inapendeza sana… Watoto wa viongozi kuoana, inapendeza sana”

    Aliongea Bishop mmoja ambae nae ni mualikwa, adam hakutaka kuonyesha nidhamu mbaya mbele ya viongozi wakubwa wa makanisa,..



    “kuanzia leo… Sasa una kanisa lako.. Sasa hata ukianza na waumini 10.. Utajua mwenyewe, ni wewe na juhudi zako”

    Ilikuwa ni kauliza ya baba yake adam, ikiongea nae…

    “ni kweli… Hata sisi usione sasa tuna wito wa Bishop, sisi tumeanza na muumini mmoja, mpaka sasa tuna makanisa meeengi sana.. Tena huyu mtoto ana bahati nzuri sana… Sisi enzi zetu tulikuwa na makanisa… Yaani hata halijapauliwa… Lipo wazi kabisa… Lakini wewe unakwenda kuanza uchungaji ukiwa na kanisa la kifahari”

    Yalikuwa ni maneno ya pasta mmoja aliohusika katika swala zima la kumbariki katika kulitoa au kulitangaza neno la Mungu,… Na uzuri adam amekwenda chuo cha Biblia na kuyasoma yote yaliostahiki.. Mana kusoma Biblia kila mmoja anajua,.. Tatizo ni kuifafanua maana zake…

    “bwana Yesu asifiwe”

    Aliongea adam huku akinyoosha mikono,..

    “milele amina”

    “kwanza niwashukuru wote kwa ujioni wenu, naamini yoye hayo ni kwa neema za mungu…. Bwana yesu awatangulie viongozi wangu”

    “ubarikiwe kijana…. Umri wako ni mdogo, ila wito unapoupata huna budi kuufanyia kazi”

    “ni kweli mchungaji… Nashukuru sana kwa kunidhihirishia wito huu… Yesu awabariki saaaana”

    Aliongea adam kwa furaha ya hali ya juu mno, huku akiketi katika kiti,…

    “unajua sisi tunapomchagua mtu kuwa kiongozi wa kanisa fulani,.. Kwanza hata wakati wa kumwita haambiwi, na pia anapokuja hatutakiwi kuonyesha sura za furaha, ispokuwa huzuni mwanzo mwisho”

    Aliongea Bishop mmoja mwenye asili ya kizungu, huku Mabishop wengine wakipokea maneno hayo, kana kwamba ndio torati yao ya kila wanapomteuwa kiongozi mpya wa kanisa fulani,…. Adam alifurahi sana mana alijua kutokana na kukataa kuoa huenda asipate nafasi ya kupata wito wa kuchunga kondoo wa bwana… Lakini pia hakuwa na wasiwasi sana kwasababu siku ile anawekwa kikao na baba, mama na dada, kuna mtu alimpigia simu akiwa yupo nje tena ndani ya gari,… Kama unakumbuka kuna sehemu aliongea na mtu fulani ila sisi hatukujua aliongea na nani… Sasa adam alipokuwa akitoka nje alikutana na mzee wa kanisa lao hilo alipokuepo muda sio mrefu,…

    “ukawachunge vyema kondoo wa bwana…. Hakikisha unakwenda na junsi hali inavyotakiwa. Sawa bwana mchungaji”

    Aliongea mzee wa kanisa na wakati huo Catherine keshapata nafasi ya kumganda adam, yaani siku moja yu kupata nafasi ya kumbatio la adam basi kamganda moja kwa moja…

    “mzee ndio mana juzi nilikupigia simu, kuwa ivi ukikataa kuoa unaweza kweli kukabidhiwa kanisa.. Uliposema ndio… Kiukweli nilifurahi sana mana napenda kuwa mchungaji katika roho, yaani nimejikuta tu napenda, sasa sikutaka ndoto zangu kuishia njiani, au wito wangu kuishia njiani”

    “basi baba mchungaji.. Kilichobaki sasa ni kiteuwa wasaidizi wako katika kanisa lako… Wazee wa kanisa, waalimu, nabiii, na wengine wengi wenye vipawa vyao”

    Aliongea mzee wa kanisa huku Adam akitoa mkono wa Catherine kwenye bega lake,…

    “kama ungelikuwa ni mwanamke mwenye adam, basi huu uzungu wako ulitakiwa uwe mkiwa wawili na mumeo, sio huku kwenye nyumba za ibada”

    Adam alimwambia Catherine, mana Catherine ile nafasi ya kumbatio ndio kapata dezo, kaganda kabisaa… Yaani adam anamchukia sema ni mtumishi wa mungu, hivyo hatakiwi kumchukia mtu kiasi hicho….

    “mtumishi adam… Lakini kwanini unanifanya kuwa mdhaifu kwako.. Eti baba”

    Adam hakutaka kumjibu chochote kile zaidi ya kuagana na mzee wa kanisa…  Kisha akawa analielekea gari lake,… Na Catherine nae yupo nyuma yake

    “huna pakwenda”

    Adam alimuuliza Catherine…

    “baba mtumishi… Hata yesu alikuwa na wafuasi wengi sana mpaka wanawake,.. Lakini hakuambiwa awaoe, sasa siwezi kulazimisha kitu ambacho hakitakiwi,… Mimi ni kondoo wako, nipe nafasi kwenye kanisa lako… Hata ukiniweka kwa waimba kwaya, nitashukuru sana baba mtumishi”

    Catherine aliongea mengi, yaani kama unamuona ungelimuonea huruma, lakini kweli hapo anafunika riziki ya mwenzie ambaye ndio mwenye nafasi ya kuolewa na adam,

    “siwezi kuteuwa mwimbaji wa kwaya anaevaa nguo fupi”

    “nipo tayari kubadirika kwa njia yeyote ile, na pia nitamheshim mama mchungaji mtarajiwa”

    Hapo adam kidogo akapata timaini juu ya maneno ya Catherine

    “apo sasa kidogo umeongea pointi… Nipe muda nitakuchagulia nafasi kanisani kwangu”

    Aliongea adam wakati huo Catherine alitamani hata kupiga magoti kwa kukubaliwa nafasi yeyote ya kanisani kwa pasta adam… Na hivyo ndivyo alivyotaka,.. Sasa mambo yanaiva taratibu, maskini eva wa watu sijui atakaza buti kwa staili gani, mana ndio taratibu anaanza kunyang’anywa mume… Basi adam alipanda gari yake na hata Catherine nae alipanda gari yake kisha kila mtu akapita njia yake… Ukumbuke adam aliwaacha mama yake na dada yake kule nyumbani kwake wakiendelea kufanya usafi mana adam ndio alikuwa anahama siku hio….. Moja kwa moja mpaka nyumbani kwake, lakini kwa bahati mbaya hakuwakuta walikuwa wameshaondoka muda tu, lakini mezani alishaandaliwa kila kitu, sasa maisha ya ubachela ndio anayaanza…. Hapo anawaza kanisa lake litakuwa na vipawa vya aina gani, yaani alikuwa akipanga mengi sana juu ya kanisa lake,…. Lakini ghafla simu yake inaita, kuangalia alikuwa ni mama yake.. Alipo pokea tu akakutana na sauti ya mama yake

    “haleluyaaaaaaaaaa….. Bwana Yesu Kristo atukuzwe kwa kupambana juu yako mwanangu.. Hongera, nimepata taarifa sasa hivi tayari umeshaupokea wito ulioitwa na baba muumba”

    Aliongea mama adam huku akionyesha kuwa na furaha ya hali ya juu, na aliamini mpaka hapo adam hawezi muoa Catherine, mana ilikuwa bila kuoa hapewi wito huo, sasa keshapewa….

    “tumsifu yesu Kristo, baba alie hai”

    “milele amina mwanangu”

    “mama… Kesho nahitaji kwenda kulifungua kanisa na nyimbo za kuabudu,… Siku nzima waumini wajue tayari kanisa limeshafunguliwa.. Mama.. Kanisa langu litakuwa kanisa la kipekee katika huu ulimwengu.. Litakuwa kanisa la uokovu kwa kila muumini”

    “baba nakuunga mkono… Dada yako huyu hapa nae anaruka ruka”

    “mpe simu dada Jessica”

    Adam alitaka kuongea na dada yake, mana alipo waacha, hakusema anakwenda wapi,

    “YOUNG PASTOR in the church… Thanks Jesus, for your power to my brother”

    Alikuwa ni Jessica akiyaongea hayo maneno kwa furaha ya hali ya juu

    “sasa ndio nini hivyo… YOUNG PASTOR ndio maneno gani dada”

    “mtumishi adam… Haijawahi tokea kwa kijana mdogo kumiliki kanisa, tena kwa kishindo… Hata wewe unajua ni kanisa gani linamilikiwa na kijana? Hakuna, yaani wewe ndio wa kwanza”

    “basi sawa lakini hilo jina si sahihi, nitakushtakia kwa mungu”

    “basi baba mtumishi… Ila nina furaha sana juu ya jambo hili, kesho nakuja kushinda kanisani kwa ajili yako kaka yangu”

    Yalikuwa ni maneno ya Jessica, yaani familia nzima ipo nyuma ya adam, yaani inapendeza zaidi kwa hali kama hio…..

    Baada ya masaa kadhaa ikiwa ni usiku, Adam alifanya maombi kabla ya kulala kisha akalala zake ikiwa ndio siku ya kwanza kulala katika jumba hilo kubwa sana…..



    **********************************

    Ghafla alishtuliwa na ngurumo za ajabu, akiangalia saa ni saa nane za usiku, na ngurumo hizo zinatokea humo humo ndani, adam alisali kabla hajafuatilia ngurumo hizo, ilikuwa ni usiku tena tena umeme ulikuwa umekatika,.. Hakuna kitu kibaya kama umeme ukatike afu jumba kubwa tena yupo pekee,…. Alichukuwa simu yake na kuwasha tochi kisha akaanza kuzunguka ndani ya jumba hilo… Alipita vyumba vyote lakini muumgurumo bado ipo kama vile kuna watu wanasali kwa imani ya kishetani,… Lakini kuna chumba kimoja hicho hajawahi kukifungua toka kuzaliwa kwake, yeye hukiona tu.. Hakutaka kukiacha, na kweli katika hicho chumba kulisikika sauti za wati kadhaa wakifanya ibada,.. Wakati huo adam nywele zake zinamchemka.

    Kiukweli ni sauti zilizokuwa zikitisha sana…. Lakini adam ni mtumishi wa Mungu, yupo tayari kufa kwa ajili ya kondoo wake, kama alivyokufa Yesu Kristo kwa niaba ya wakristo wote,.. Adam alikibonyeza kitasa cha mlango na kwa bahati nzuri hawakufunga mlango, hivyo adam akasukuma mlango ule kisha akaingiza kichwa…. Ilisikika tu sauti ikisema

    “haaaaaaaaaaa”









    Ilikuwa ni siku nzuri kwa mchungaji adam kukabidhiwa fimbo zidi ya kondoo atakao wachunga, lakini siku hii hii ya leo, ilikuwa na balaa katika upande wake, kwani siku ambayo anahamia katika nyumba yake hio, na ndio siku anapewa wito dhidi ya kipawa chake,.. Na siku hio hio mishale ya usiku alianza kusikia ngurumo za ajabu katika nyumba hio, sauti hizo zilimfanya ashtuke na kuanza kutoka taratibu ili kubaini ni sauti gani na ni akina nani… Adam alizunguka ndani ya jengo hilo kubwa ambalo kwa wakati huo umeme ulishakatika hivyo alikuwa akitumia simu kama tochi,… Bila uoga aliweza kuzunguka jengo lote,… Sauti zili zilinyamaza wakati akiwa anazunguka.. Lakini sasa katika pita pita, alikipita chumba kimoja, hicho chumba hua anakionaga tu na hajawahi kuingia katika chumba hicho toka kuzaliwa kwake,… Adam alisali pale pale kisha akashika kitasa cha mlango, tayari kwa kufungua… Ndani yake zilisikika sauti za kusali kwa njia ya shetani…. Adam bila kuogopa alifanikiwa kufungua huo mlango na kuingiza kichwa chake,.. Sauti iliyosikika ni ya adam akiwa katahamaki



    ***********************************

    “haaaaaaaaaaaaaa”

    Alikurupuka kitandani huku akifikicha macho yake, kana kwamba alikuwa usingizini, na hio ilikuwa ni ndoto na haikuwa kweli,… Mana umeme ulikuwepo, na pia nyumba alio iota sio hio ya kwake, bali ni nyumba ya familia yao kule alipotoka, yaani alipokuwa akiishi na wazazi wake.. Na ndio mana kuna mahari paliandikwa kuwa, chumba hicho hajawahi kuingia toka kuzaliwa kwake, maana yake ni kule kwa wazazi wake na sip hapo kwake…

    “shindwa kwa jina la Yesu…. Pepo mchafu tooookaaaa”



    Kesho yake adam aliamka asubuhi sana akaingia jikoni kutengeneza chai, mana ikumbukwe kuwa adam ana kampuni ambayo ni mali aliopewa na baba yake ili aendelee maisha yake, na hapo bado hajakabidhiwa mali vizuri, hio aliopewa ni moja ya kampuni za mr Jacob, na mtoto wa kiume ni yeye pekee,.. Adam si mvivu wa kupika, na haruhusiwi kuishi na mwanamke wa aina yeyote yule, hata mchumba haruhusiwi kuishi nae ispokuwa kusalimiwa tu… Au kama anataka kufanyiwa usafi wa nyumba na mmoja kati ya waumini, basi yeye hatakiwi kuwepo pale usafi unapofanyika, anaeruhusiwa kufanya usafi humu au hata kulala, ni dada zake na mama yake tu basi… Ndio wana ruhusa ya kuja kuishi hapa, ila mwanamke yeyote yule haruhusiwi kuishi hapa ispokuwa mkewe tu, hivyo kama pasta hujaona… Basi haruhusiwi kuishi na mwanamke ambaye hujamuoa,… Hata mchumba hairuhusiwi… Wakati akiwa jikoni alikuwa akiikumbuka sana ile ndoto, haijawahi kutokea katika maisha yake



    Sasa huku kanisani kwa adam,… Kumbe taarifa za ufunguzi wa kanisa hilo zilishasambaa kila kona, hivyo palikuwa pakipambwa vizuri kwa ajili ya kuabudu siku nzima kwa furaha,.. Waumini walikuwa wengi sana ingali kanisa ni jipya, hata adam atashangaa sana kuona siku ya kwanza tu ana waumini wengi sana,.. Lakini sasa mwanamke wa mbele sana alikuwa ni Catherine, na inaonekana waumini wengi alikuja nao yeye,… Mapambo ya kila aina yalipambwa katika kanisa hilo lililojengeka kwa vioo vitupu,… Wengine walikuwa wakifanya usafi, wengine walikuwa wakifunga majukwaa, vinywaji mbalimbali kasoro vilevi pekee ndivyo vilivyo kosa nafasi ya kuletwa hapo…



    Huku kwa adam akiwa anakunywa chai baada ya kumaliza kupika, simu yake ilikuwa katika sikio

    “haloo…. Tumsifu yesu Kristo”

    “milele amina baba mtumishi… Hali ya kuamka waionaje”

    Alikuwa ni Eva ndie aliepigiwa simu

    “bwana Yesu ndie kila kitu katika usingizi wangu… Ashukuriwe na bwana muumba mbingu na ardhi”

    “amen, vp baba mtumishi…. Kiukweli sijalala kwa furaha… Nimepata habari kuwa, tayari umeupokea wito toka kwa Bwana wetu”

    “ndivyo ilovyo”

    “Ashukuriwe bwana yesu”

    “amen…. Uko wapi sasa eva”

    “nipo nyumbani najiandaa kwenda kanisani”

    Eva alikua hana taarifa yeyote kuhusu ufunguzi wa kanisa la mchumba wake,

    “mama mchungaji”

    “ndio, baba mchungaji”

    “ina mana huna taarifa juu ya kanisa lako”

    Adam alimuuliza eva, lakini eva kweli hakuwa na taarifa

    “sina taarifa… Na kwanini usingeniambia”

    “Samahani, huenda furaha ilinizidi mpaka kusahau jambo jema kama hili”

    “enhee, nipe taarifa”

    “kuna maombi ya kufungua kanisa, na sasa kila mmoja mbona anajua”

    Aliongea bwana adam huku eva akifurahi sana na kuairisha kwenda kanisani kwa baba yake adam, ili aende kwenye kanisa la mchumba wake,

    “upo wapi sasa baba mchungaji”

    “nipo nyumbani, namalizia kunywa chai”

    “utatoka na familia yako”

    “hapana, nadhani wao wameshatangulia, na hata hivyo mimi sipo kule tena, nimeshahama”

    “weeee baba mtumishi, unasema kweli”

    “ndio, mbona nimehama jana na hapa nakunywa chai”

    “nani kapika hio chai”

    “nimepika mwenyewe, si unajua sheria na taratibu za mchungaji mbae hajaoa”

    “nazifahamu na ndio mana sijatamani nije nikupikie… Ila utateseka sana baba mchungaji,… Nipo tayari kwa hali yeyote baba mchungaji sitaki uteseke”

    “hebu ngoja tutaongea vizuri…  We jiandaa nakupitia hapo nyumbani”

    “sawa baba mchungaji”

    Adam alimaliza kunywa chai haraka iwezekanavyo, kisha akatafuta suti nzuri na kuanza kuinyoosha nyoosha na pasi mara moja… Kisha huyoo kapanda gari yake.. Uzuri wa geti yake inafunguka kwa rimoti, hivyo hakuwa na shida ya mfungua geti,..

     

     

    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog