Search This Blog

Thursday 24 November 2022

PETE YA KIKE - 4

 

     

     



     

     

    Chombezo : Pete Ya Kike 

    Sehemu Ya Nne (4)





    Tukija huku dukani kwa faima

    "sasa umerudi kazini, chezea tena..."

    Aliongea zamina dada yake na faima akiwa dukani anapouza mdogo wake

    "dada, mimi nakuelewa ila Kiukweli suria hatoki kichwani mwangu,.. Sijui kama huko alipo kama ananisikia"

    Aliongea faima huku zamina akisema

    "wewe acha ujinga, suria, suria kila siku suria... Mtu keshauwawa na dada yake wewe unateseka tu"

    Mara zamina alitulia kwani simu yake iliita...

    "halo shem mambo"

    Alipokea simu hio huku akisema shem, lakini sauti ya huyo shem haikusikika

    "eeeh umefika"

    Aliongea faima kana kwamba huyo shem yupo maeneo hayo...

    "ok njoo kwenye duka moja hivi, ulizia IC (ISLAMIC CLOTH) ndipo nilipo"

    Alimuelekeza mtu huyo

    "umepaona eee?"

    Alijibu mwenyewe kisha akamalizia kusema

    "sawa njoo chap basi"

    Zamina alikata simu kisha akamwambia mdogo wake kuwa

    "acha na wanaume wasio na mbele wala nyuma... Tariki unamkataa bure tu lakini ana hela, acha ufala.. Na ndio huyo anakuja, ongea nae vizuri"

    Aliongea zamina kisha akaamka pale kwenye kiti,.. Alikuja jamaa mmoja sharobaro mno, na pia alionekana kuwa nazo kutokana na nguo kali alizo vaa...

    "ooohhh shem Riki, mambo"

    "poa shem nambie"

    "safi tu... Kumbe we mwenyeji hapa IC?"

    "ndio, mbona ndio mitaa yetu hii"

    "wacha Weeeee"

    "ndio"

    "ok karibu,.. Mwenzio uyo apo.... Sasa faima mi naenda kwa tizo"

    "sawa dada"

    Zamina aliondoka zake hivyo faima akabaki na Tariki, ikiwa wateja wamepungua kidogo....

    "mambo fai?"

    Tariki alimsalimia faima, lakini faima hakuwa na muda nae tena anatamani wateja waje ili asiongee na Riki....

    "nakusalimia tu jamani fai"

    "shida yako nini riki,.. Sitaki kuongea na wewe"

    "lakini fai,... Moyo ndio unanipeleka puta juu yako,.. Mimi ni mtu na pesa zangu, inakuwaje nakosa mtu wa kutumia nae"

    Aliongea Tariki, huku faima ndio kwanza hata habari hana....

    "pesa ni zako na familia yako, hazinihusu hizo"

    "fai ina maana bado unampenda mtu aliokufa.... Umekuwa mkali mpaka nimeamua kumtumia dada yako"

    "tariki tafadhali sana naomba usinichefue"

    Faima alimjibu tariki huku tariki akituma sms kwa zamina mana ndio msaada wake...

    Ghafla simu ya faima inaita.. Kucheki ni dada yake...

    "halloo"

    Aliipokea faima na kuita haloo"

    "acha ujinga wewe, kupenda gani huko mpaka kwa watu waliokufa... Acha ujinga, wanaume siku hizi hakuna sasa potezea hio bahati endelea kupenda mtu aliokufa, na ukumhuke umri wako unazidi kwenda na utahitaji ndoa.. Sasa jifanye unapenda utaolewa na mizimu ya suria"

    Aliongea zamina kisha akakata simu

    Faima alihema kwa nguvu kisha akamuangalia tariki...

    "naomba uondoke na staki uje tena"

    "nini tena faima"

    "nasema tokaaa"

    "ok poa, ila siku ukijiskia... Utanicheki kwenye simu, namba yangu hio hapo"

    Tariki aliacha karatasi yenye namba za simu yake, ili siku faima akifikiria vyema basi amtafute kwa namba hio

    Hivyo tariki aliondoka zake, lakini alipofika mahali alikutana na rafiki yake wa kiume ambaye alikuja naye lakini hakutaka afike nae pale IC, hivyo alimuacha mbali na hata rafiki huyo anajua leongo la tariki...

    "riki vipi"

    Aliuliza rafiki yake huyo, huku riki akijibu

    "mmmhhh ebana mtoto ni mgumu... Nimejigamba nina hela lakini wapi mtoto hajali wala nini"

    Aliongea tariki, kana kwamba hana pesa wala nini sema ilikuwa mikwara ya kutongozea tu....

    "unajua tariki unakosea,.. Na ndio mana mademu hukai nao... Mana unajinadi sana kuwa na pesa wakati hata kazi huna"

    "sasa jumbe kama unavyojua, mademu wa sasa hivi ni wakali kinoma ila kuwapata ni mkwanja, ukumhuke samaki bila chambo humpati ujue"

    "ni sawa, lakini kumbuka yule sio samaki"

    "wacha nijitape tu... Akichomoa poa kwani kwsho si tunakwenda kupata kazi kule kiwandani"

    "na usipo pata je"

    "fresh tuuu"

    "afu sitaki kuamini kuwa hata dada yake anajua una hela"

    "sasa je? Anajua ninazo... We ulizani kwa pamba hizi ataachaje kuamini"

    "duuuuuu, yaani wewe ni zaidi ya Jambazi aiseee"



    Tukiachana na hao tuje huku kwa akina surian na mke wake maimuna waliokuwa ofisini, na msichana mmoja hivi ambae yeye ni jirani yao, baada ya kuskia anatafuta kazi,... Na dada huyo alisomea usekretari, hivyo imekuwa rahisi sana kwake kupata kazi,... Wakiwa hapo ofisini dada alianza kuonyeshwa sehemu yake ya kazi,...

    "sasa wewe ndio sekretari wa kampuni hii, haruhusiwi mtu yeyote kumuona boss bila wewe kuleta taarifa zake kwangu"

    Aliongea surian na hapo alikuwa na mke wake maimuna,

    "sawa boss, nitafanya kazi kadri ya uwezo wangu ni sitakiuka kanuni na taratibu za kampuni hii"

    "ok... Nadhani kwa siku ya kesho utapata changamoto kubwa na kazi kubwa pia kwasababu kwsho ndio siku ya usaili, hivyo wataingia watu watano watano, utamkagua mmoja baada ya mwingine kisha unaniletea barua yake ikiwa na vyeti vyake... Nitakapo ona vyeti ya mhusika, basi mimi ndio nitajua namuweka nafasi gani kitokana na elimu yake"

    "sawa boss,. Naaa... Mfanyakazi anaruhusiwa kuingia ofisini kwako"

    "hapana... Haruhusiwi mtu yeyote kuingia ofisini kwangu, ispokuwa wewe na mke wangu tu... Hivyo ofisi itaingiliwa na watu watatu... MIMI NA MKE WANGU PAMOJA NA WEWE na wewe utaingia kwa kuleta document au taarifa za kitu au mtu fulani, sio kuingia mara kwa mara kwakua unaruhusiwa, na hata awe boss wa kampuni gani, mwambie anisubiri chumba cha meeting (mikutano)... Nadhani umenielewa"



    "nimekuelewa boss... Hivyo kesho, nakagua barua za mtu kisha nakuletea"

    "yes, na uhakikishe barua imekamilika vigezo vyote ndio uilete kwangu kama naipitisha au laa, na kama haijakamilika sitaki usumbufu, mtu huyo arudi akakamilishe vigezo vyote... Sawa Cecilia"

    "sawa boss"

    "ok, nipo ofisini kwa wale watakao tokea leo wapokee tu"

    "sawa boss"



    Ilikuwa ni mipango ya kazi ambayo anatakiwa kufanya sekretari huyo, ikiwa ni kampuni mpya katika mkoa wa tanga, na inahitaji watu takribani 500 (miatano) ikiwa na lengo la kusaidia watu kwa njia ya kuwaajiri, kampuni ya MOON ISLAMIC CLOTH COMPANY, Ipo tayari kwa wafanyakazi kuleta maombi ya kazi



    Kesho yake asubuhi mida ya saa mbili, ndani ya geti la kampuni hio kulifulika watu wengi mithili ya soko, kweli hapo kazi ipo... Watu walikuwa ni wengi mno na uchambuzi huu hautakiwi kufanywa na maimati, mana yeye hutumia nguvu za asili yake, hivyo asije kupitisha watu Ilimradi tu......



    Katikati ya watu zaidi ya miambili alionekana mama yake surian akiwa kashika bahasha yake, naye kaja kuomba kazi kwenye kampuni hio, na watu woote walikuwa na umri usiopungua miaka 18 mpaka 35 lakini mama kajikaza tu kuka mana haoni lika lake kati ya wafanyakazi aliosimama nao... Mama suria au mama asha anachungulia tu kama angalao hata atamuona boss ampe kipaumbele kwakua ni mtu mzima,.. Lakini kwa bahati mbaya au nzuri boss keshaingia ndani na haruhusiwi kutoka wala kuingia mtu...

    "heeee we mama vipi mbona unanisukuma"

    Aliongea dada mmoja huku kama wakimcheka mama yakw suria,.. Yaani laini wangelijua kuwa huyo ndio mama wa bosa wanaye muomba kazi sijui ingelikuwaje, na mama nae hajui kama anakwenda kuomba kazi kwenye kampuni anayomiliki mtoto wake, na hata mtoto hajui kuwa mama yake kaja kuomba kazi,...



    Usaili Ulianza, na vigozo visipo timia unarudishwa ukatimize vigezo, na kama huezi basi usirudi tena... Hivyo kuna wale ambao hawana vigezo basi wanarudi lakini namba zao zimeachwa kwamba watachukuliwa kama masalia tu... Hivyo hata akiondoka namba inaachwa kwa sekretari, siku akihitajika mtu aitwe...



    Wasichana walikuwa wakimcheka mama asha, kwani alikuwa na umri mkubwa sana

    "huyu mama jamani ananikanyaga"

    "we mama ulikuwa wapi ujanani kwako"

    Walikuwa ni wasichana waliokosa heshima ndio walikuwa wakimsema mama huyo, mpaka mama asha akakata tamaa na kukaa pembeni mana alikuwa kwenye nafasi ya kuitwa lakini akajikuta karudi nyuma ili asichekwe na watoto kulingana na umri wake..



    Pamoja na uvumilivu wake wote, zamu yake ilifika akiwa na furaha kwa kupata nafasi, wengine walicheka sana... Na hata sekretari alishtuka kumuona mama mwenye umri mkubwa amekuja kuomba kazi za viwandani...

    "heeeee mama.... Hata wewe"

    Alikuwa sekretari ndio mwenye kuongea

    "ndio mwanangu, nitafanya kazi usinione hivi tuuu"

    Aliongea mama asha au mama surian na mama huyu anasikia tu mtoto wake kafa lakini hana imani hio mana yapata miezi miwili hamjui alipo wala hajawahi kuwasiliana nae

    "mama, umri wako hauruhusu kufanya kazi hapa... Na hata karatasi ya matangazo ilisema ni kuanzia miaka 18 mpaka 35 ndio mwisho... Kwani mama una umri gani"

    Aliuliza sekretari huyo huku mama akiwa mshapu kujibu ili aonekane yupo shapu hata kwa kufanya kazi

    "nina miaka 58"

    "haaaaaaaaaa mama, haiwezekani"

    "jamani nipeni hata kufagia fagia tu"

    "labda ingekuwa hio lakini hata vyeti vya shule huna, hapa naona barua na paspoti saizi tu"

    Aliongea Cecilia huku akisoma barua ya mama huyo

    "nisaidie mwanangu... Ina mana nife njaa na nina uwezo hata wa kudeki vyoo"

    "mama, tatizo ni umri wako ni mkubwa sana... Kwani huna watoto wasomi waje tuwape nafasi"

    Aliongea Cecilia bila kujua boss wake ndio mtoto wa huyo mama lakini hakuna anaejua hilo... Sasa Cecilia aliposema hivyo, mama akakumbuka mtoto suria ambaye ni msomi mpaka basi,....

    "usinikumbushe yaliopita mwanangu, nisaidie kazi"

    "mama, kweli naogopa kufokewa na boss kama nitaipeleka hii barua"

    "jaribu tu, nitasafisha hata vyoo tu"

    "mmhhh mama angu unanipa mtihani"

    Mara ghafla simu ya mezani kwa Cecilia inaita... Alipokea

    "hallo boss"

    "eeehh vipi watu wameisha??"

    "hapana boss bado wapo"

    "sasa mbona huleti document zao"

    "naleta boss.. Ila kuna"

    Cecilia alitaka kusema lakini akasita,.. Sasa alipomwangalia yule mama anatia huruma sana

    "ila nini ceci? Lete document muda unakwenda huu"

    "boss?"

    "nini Cecilia? Lete"

    "boss... Kuna mama mtu mzima hapa, hana vyeti, ana miaka 58..je tunamsaidiaje"

    Aliongea Cecilia, huku akisubiri jibu toka kwa boss surian....

    "hivi we Cecilia una akili kweli,.. Vigezo ni kuanzia miaka 18 mwisho 35, sasa huyo mwenye miaka 58 aliambiwa hapa ni kituo cha watoto yatima kuwa aje kulea watoto??... Lete documents za vijana na nikiona documents kuanzia miaka 36 huna kazi Jinga kabisa wewe"

    Simu ilikata na Cecilia akawa hana jinsi tena zaidi ya kumpa mama karatasi zake...

    "mama, nimejitahidi sana kukusaidia.. Lakini nimetukanwa kama mtoto... Shika bahasha yako mama angu, ila pole sana mama..."

    "boss wako ni mkali kumbe"

    Aliongea mama huyo bila kujua boss huyo huyo ndio mtoto wake wa kumzaa ila anasikia sikia tu kua kafariki dunia...

    Lakini sasa ikumbukwe kuwa maimuna ni jini,.. Sasa kule ndani ofisini maimuna yupo, na hapa kwa sekretari kivuli chake kipo, kwahio kule ni mwili na huku ni kivuli,... Sasa alishangaa kuona Qarina wa surian na Qarina wa huyu mama wanaongea, na yeye kama jini ndio mwenye uwezo wa kuongea na hao Qarina,.. Sasa leo maimuna ndio anajua kumbe huyo mama hapo mapokezi ndio mama yake surian, Yaani ndio mama mkwe wake kabisaa..







    Ama kweli usilo lijua ni usiku wa giza, kwani surian angelijua kuwa anaye mkatalia ni mama yake mzazi kabisa, sijui ingelikuwaje hapo, mana ana uchungu na wazazi wake, anatamani sana kusaidia wazazi wake nao wale raha, lakini mke alio muoa ni jini na kawaida ya majini hua na masharti yao, na moja ya masharti hayo ni kuto isaidia familia yake ispokuwa kwa kufanya kazi, sasa baada ya asha kukataa kuja ku apply (kuomba) kazi, mama aliamua kuja mwenyewe baada ya mtoto wake kukataa,... Sasa boss au kanuni ya kampuni hio haitaki wafanyakazi wenye umri mkubwa, wanahitaji vijana wachapa kazi na sio wazee wasinziaj,....



    Sasa maimuna kutokana na asili yake ya ujini, aliweza kugundua kuwa mama aliopo mapokezi ni mama mkwe wake, na keshaikosa kazi... Maimuna aliumia sana mana hata yeye hakuipenda hali hio, na laiti kama wangeruhusiwa kufanya hivyo, basi angemruhu surian aisaidie familia yake,... Pamoja na maimuna kujua kuwa huyo ni mama yake, lakini hakuna msaada wowote alio ufanya zaidi ya kitulia na hakumgusia surian kuwa huyo mama ni mama yake mzazi kabisa...



    Sasa huku mapokezi, hata kile kivuli cha maimuna kilirudi ndani kwani hakutaka kuyaona machozi ya mama yake surian yakimwagika kwa kukosa kazi, na mbaya zaidi ni umri wake ndio ulimtupa mkono... Basi mama akawa anaondoka huku baadhi ya wasichana wakimcheka kwani aliziba riziki za vijana..



    Lakini Cecilia ambaye ndie sekretari wa kampuni hio naye ni msichana aliojawa na huruma juu ya huyu mama,

    "mama Samahani kaa pale Kwanza"

    Aliongea Cecilia huku mama akikubali mana hajui kwanini kaambiwa akae pembeni Kwanza,



    Muda wa kupokea barua uliisha kwani ilikuwa ni saa 11 za jioni, lakini wameahidiwa waliobaki warudi kesho kwa ajili ya usaili,... Cecilia alimwita mama yule na kuchukua zile karatasi zake,...

    "nipe namba zako za simu, ili siku kazi ikianza nikupigie uje"

    Aliongea Cecilia huku mama akitaka kuuliza lakini akaona wacha aende tu

    "sawa mwanangu, ahsante.. Namba zangu ni hizi hapa"

    Cecilia alichukua namba za mama yake surian lakini sio kuwa Cecilia anajua kuwa huyo ni mama yake surian, hapana hajui... Na Cecilia kaamua kufanya kitu yeye kama yeye ili amsaidie mama huyo..



    Kila mmoja alishaondoka sasa surian ndio anatoka, lakini wakati huo mama yake alisha ondoka baada ya kuachiana namba na sekretari...

    "pole na kazi"

    "ahsante boss, pole na wewe"

    "ahsante... Aahh nadhani ni muda wa kutoka, hakikisha unafunga vizuri... Na ufunguo wa hii ofisi utakaa nao wewe kwasababu mimi nitakuwa wa kwanza kabla yako ila wewe ndio utakuwa wa kwanza kufungua ofisi na kuifanyia usafi na kila kitu,.. Kasoro ofisini kwangu nitabaki na ufunguo wangu pamoja na ufunguo wa mlango mkubwa ili niingie ofisini kwangu"

    Surian aliongea sana kwa kumuachia maagizo Cecilia

    "sawa boss nimekuelewa na ahsante kwa kunipa nafasi hio"

    "ok sawa... Tukutane kesho"

    "sawa boss, niwatakie jioni njema"

    "nawe pia"

    Alijibu maimuna ambaye ndio mke wa surian, mana saa ya kutoka hutoka wote na huingia wote lwani wao hutumia gari moja tu...



    Baada ya nusu saa, Cecilia alipanda daladala mpaka mjini ambapo aliingia katika duka moja la nguo za Kiislamu, na duka hilo ni ICC (Islamic Clothing Centre) ambapo ndipo anapouza faima mchumba wa surian,

    "heeeeee anti, Asalam Aleykh"

    Faima alifurahi na kumsalimia Cecilia kwa furaha kana kwamba wana undugu fulani hawa watu,..

    "waaleykh msalam habari yako fey"

    "ah namshukuru Mungu kwa rekhma zake"

    "mguu huu wako mdogo wangu..."

    Aliongea Cecilia huku faima akiwa makini kumsikiliza anti wake

    "enhee, najua wewe huja na vya maana wewe"

    Aliongea faima kuwa Cecilia hua anakujaga ma mambo ya maana

    "sasa skia, tusipoteze muda.... Kuna kampuni fulani hivi ya nguo za Kiislamu, inaanza kazi jumatatu ijayo, sasa hivi tupo kwenye usaili na mimi nimepata kazi nafasi ya Secretari"

    Aliongea Cecilia huku faima akifurahi mno

    "waaaaooo! Jamani anti hongera, mana ulivyokaa mtaani mpaka basi.. Mungu kakujaalia anti wangu"

    "ahsante sana, ila nina shida na wewe, tena kubwa tu"

    "shida gani hio anti ceci"

    "kama unavyojua, katika kazi hua kuna majaribu sasa kuna mama mmoja kaja kuomba kazi kwenye hio kampuni, na huyo mama ana miaka 58, hana cheti chochote kile... Na pia umri wake umemtupa mkono... Sasa mimi nataka tumsaidie huyo mama"

    Aliongea Cecilia huku faima akishtuka kwa hilo

    "mmhh sasa anti shadya... Mimi nitatoa msaada gani ingali sifanyi kazi huko"

    Aliuliza faima, tena kwa kumuita shadya, kwani Cecilia hua sio jina lake halisi, ni jina alilopewa chuoni na rafiki zake, sasa mwenyewe anapenda kulitumia mana lina muonekano wa kisekretari,...

    "swali lako zuri sana faima... Lakini msaada wako ni vyeti vyako, na paspoti saizi zako... Hivyo tu basi ili yule mama akapate kazi, mana mpaka analia maskini ya mungu... Tumsaidie jamani faima"

    Aliongea shadya au Cecilia, na laiti kama Cecilia angelimuonyesha faima paspoti saizi ya yule mama.. Basi faima angemjua mana ni mama wa mchumba wake,.. Patamu apo...

    "mmmhhh lakini anti, hii si hatari sana, mana huyo mama akiharibu huko kazini kwenu, si nitafuatwa mimi jamani"

    "hapana faima... Nikishakua kopi ya vyeti vyako, nakwenda kubadili majina yote yanakua ya jule mama"

    "mmmmhhhh, sawa.... Lakini huyo mama ane hana watoto, si apumzike tu alishwe na watoto wake"

    "mmmhh mdogo wangu, mimi hata sijui... We tutoe msaada tu"

    "kwahio tunaanzaje, mana vyeti vipo nyumbani"

    "sasa hivi twende tukapige paspoti saizi kabla jua halijazamia"

    Aliongea shadya huku wakiamka na kuingia mlango wa pili ambapo kuna kajistudio ka kupigia picha za paspoti saizi kwa dakika tatu... Walipiga kisha wakatoka, na uzuri ni kwamba ilikuwa ni mida ya kufunga, hivyo faima alifunga duka kisha wakapanda majaji mpaka huko kwao, ambako alikwenda kumpa Cecilia kopi ya vyeti vyake ili kwenda kutoa msaada kwa yule mama... Siku hio Cecilia hakulala, kwani alikwenda kila mahali kuhakikisha anabadili majini ya vile vyeti ili kesho apeleke kwa boss kama mfanyakazi, sasa hapo ile ishu ya vyeti hewa, anaye fanya kazi ni mwingine, na mwenye vyeti ni mwingine,...



    "ZUWENA RASHIDI SURIA... Hahahahahh safi sana"

    Shadya alilisoma jina hilo katika vyeti ambavyo keshavibadilisha majina, na kama unavyoona hayo majina hapo juu, iko hivi



    Ndoa za zamani ilikuwa mwanamke akishaolewa hata jina la ubini wa familia yake hubadilika, yaani atatumia jina la mume wake kama baba yake, lakini wakiachana anatumia jina la baba yake kama kawaida,.. Huu mpangilio upo lakini kwa sasa haufuatiliwi, unakuta mwanamke kaolewa lakini bado anatumia ubini wa baba yake mzazi, ingali inatakiwa ubini unakuwa wa mume wake... Sasa kwenye vyeti hivi ubini ni wa mume wake,.. Babu yake surian anaitwa SURIA... Na baba yake surian anaitwa RASHID, na mama yake anaitwa ZUWENA,... Sasa kwenye vyeti yamewekwa hayo majina yote matatu,....



    Wakati huo huku kwa akina surian, yaani kwa mama yake,.. Mama alikuwa akisali na kumuomba mungu afanikiwe kupata kazi, kwani hali ya maisha yao yamekuwa mabaya mno, kula kwao kumekuwa kwa shida, mtoto waliokuwa wakimtegemea ndio huyo kauza saluni, naye yupo nyumbani kawa mtu wa kulia siku zote, mana kila anapo pita huambiwa kamuua ndugu yake ndio mana anapata pesa nyingi... Mzee Rashidi naye kwenye maombi mana kiuhalisia kule kazi imebuma, sasa shadya au Cecilia kaamua kupita chocho ili kumsaidia mama huyo,..



    "kazi leo imeendaje mume wangu"

    Sauti nzuri ya mwanadada maimuna au maimati kwa jina la uasili wake

    "aah namshukuru Mungu, kazi sio mbaya japo documents ni nyingi lakini zitaisha tu"

    Aliongea surian huku wakiwa kitandani katika hali ya kupapasana,

    "weeee mungu unantia kidole jamani, acha izo baaasi"

    Aliongea muna huku wakichezeana baadhi ya sehemu zao,

    "sasa chupi ya nini saa hizi jamani mke wangu"

    "kwani nimekataa kuivua?, kwanza kuvua chupi ni kazi yako sio yangu"

    "mmmhhh niache nilale mimi"

    "jamani mume wangu, nina hamu ujue"

    "si una vidole wewe"

    "duuuuuu, sasa vidole na hio nanii wapi na wapi"

    "niache nilale nimechoka eti mamuu"

    "basi mume wangu, lala tu... Najua leo umefanya kazi kubwa sana"



    Kesho yake saa 12 kamili asubuhi surian pekee akiwa katika gari, kana kwamba leo kamuacha mkewe nyumbani, sasa kaja kazini peke yake, ikiwa yeye ndio wa kwanza kuingia ofisini, na akiingia yeye moja kwa moja anaingia ofisini kwake, na hayo ni masharti ambayo kapewa na maimuna kuwa hahitajiki kuonekana na wafanyakazi wa kiwandani mpaka siku saba ziishe ndipo aonekane, kwahio Cecilia ndio mfanyakazi wa kwanza kuja ofisini kabla ya wote, kwani yeye ndio mapokezi kwa kila kitu na ndio wa kufanya usafi wa ofisi nzima, hivyo katika wafanyakazi wanaomjua boss, ni Cecilia peke yake,



    Saa moja kamili Cecilia ndio anaingia kazini,.... Alianza kufanya usafi katika ofisi mbalimbali ambazo bado hazijapata wafanyakazi, hususan vitengo vya mameneja na wengine wengi ambao watapata vyeo vya kukaa katika ofisi,... Mana kuna wafanyakazi wa ofisini na wafanyakazi wa viwandani,



    Saa tatu na madakika eneo la kiwanda lilijaa waombaji wa kazi, yaani waliokuja kuomba kazi, walikuwa wengi sana wake kwa waume,... Na hapo utachaguliwa kutokana na sifa za vyeti vyako,... Basi kazi ya kuchukua vyeti na kupeleka kwa boss ilianza,... Cecilia hakutaka kuanza na vyeti feki ambavyo mfanyaji kazi ni mwingine na vyeti ni vya mwingine,... Ilipofikia kundi la kumi, hapo hapo Cecilia akaunganisha na zile documents za ZUWENA RASHID SURIA,.. Sasa hatujui kama surian ataweza kutambua lolote kuhusu documents hizo,..



    Suria baada ya kupewa documents za watu watano, alianza kukagua moja baada ya nyingine,...

    "heeeeee faima kaja kuomba kazi"

    Surian alitoa macho huku akisema faima kaja kuomba kazi,.. Hio ni baada ya kuona picha ya faima na ni kweli ni faima ambaye ni mchumba wake, na wanapendana mno,... Ila wamepoteana baada ya surian kupelekwa ujinini na kukaa zaidi ya miezi mitatu huko chini ya bahari ambako ndiko majini walipo,.. Sasa toka arudi hajawahi kumuona wala kuwasiliana naye kwani yupo ndani ya ndoa, sasa atawezaje kumpigia simu wakati ana ndoa.. Na anampenda faima kupita maelezo,.. Sasa baada ya kutahamaki picha, alikuja kutahamaki kwenye jina...

    "eehh? Kumbe sio faima... Lakini mbona hili jina ni la mama yangu,.. Inakuwaje hapa"

    Aliongea surian kwani jina la ZUWENA sio la mtu mmoja lakini ukiunganisha na ubini wake, lazima likupe mashaka jina hilo

    Alijiuliza mwenyewe bila kupata majibu sahihi.... Aliangalia mara mbili mbili lile jina pamoja na picha,.. Majina ni ya mama yake, na picha ni ya mchumba wake,.. Sasa akaamua kuangalia barua ya mtu huyo,... Sasa alipoangalia kwenye sehemu ya namba za simu, laaaa haulaaaa.... Surian aliamka katika kiti chake na kutaka kutoka nje, wakati ni kosa la jinai kutoka nje, mana ataharibu masharti ya jini maimuna.. Na nia yake ni kwenda kumuona huyo mtu mwenye documents hizi, ni nani??????







    Hakuna binadamu ambaye hampendi mama katika hii dunia, hata wanyama hupenda mama zao,... Hata uwe jambazi kiasi gani, huezi kumkaba mama na kumuua kikubwa tu labda amuibie hela, ila kumuua hawezi, na ukiona binadamu kamuua mama yake, basi jua huyo hakuwa mama yake wa kumzaaa... Kwasababu pindi unapotaka kufanya hivyo unashindwa,. Lakini mama yako kabisa huezi kumuua...



    Surian ni mtoto wa mwisho katika familia yenye watoto wawili, akiwemo asha ambaye ni mtoto wa kwanza katika familia hio, wazazi wa surian waliwekeza pesa nyingi sana kwenye elimu ya mtoto wao ambae ni surian, na ni kweli surian kasoma kwelikweli, yaani mpaka makampuni binafsi yanaogopa kumuajiri kwani kutokana na elimu yake, anatakiwa kulipwa mshahara mkubwa kuliko hata boss mwenyewe anavyo jilipa,.. Unajua mtu unasoma mpaka unaogopwa kuajiriwa,... Surian akienda kuomba kazi huambatanisha vyeti visivyo pungua kumi, ambavyo kasoma katika vyuo mbalimbali hapa nchini,.. Surian ana madigrii mengi, mana kasoma baadhi ya vyuo vikubwa tu... Hivyo hapo kichwani madigrii yamelala....



    Sasa wazazi Waliwekeza Pesa zao katika elimu ya mtoto wao,... Kwa bahati mbaya alikosa kazi nzuri, lakini kwa bahati nzuri kapata mke mwenye asili ya ujini,... Mali zimekuwa nyingi mno, lakini mbaya zaidi anapewa masharti ya msaada juu ya familia yake,.... Hivyo anaruhusiwa kuiajiri familia yake ili ipate pesa ila sio kuwapa,...



    Sasa leo amefanikiwa kuliona jina ambalo mama yake hulitumia, japo koo zipo nyingi lakini kwa mazoea yake alijua fika kuwa huyo aliokuja kuomba kazi ni mama yake,... Lakini pia kama ni mama yake mbona picha ni ya mpenzi wake, sasa inakuwaje hapo... Aliona wacha asome barua ya mtu huyo,... Sasa katika kusoma akaona sehemu ya namba za simu haikujazwa, mana kama ingejazwa angelimpigia simu mtu huyo,... Sasa surian kanyanyuka kwenye kiti kwa hasira ili amwambie Cecilia kuwa kwanini huyo mfanyakazi hakuandika namba za simu,... Sasa ile anataka kutoka nje,.. Akakumbuka kuwa haruhusiwi kuonekana nje mpaka siku saba ziishe ndipo aweze kutembelea wafanyakazi wote, hivyo hapo atawaajiri wafanyakazi kupitia vyeti vyao, na vipicha vyao, lakini sio kuwaona hivi uso kwa uso...



    Surian alirudi katika kiti chake baada ya kukumbuka hilo,.. Alishika simu yake na kumpigia Cecilia

    "hallow Ceci? Njoo ofisini"

    "sawa boss"

    Alimuita Cecilia, na ceci alijua fika kuwa anaitiwa zile documents za ZUWENA,...

    "yes boss"

    "huyu mtu vipi huyu... Kaja mpaka hapo ofisini"

    "ndio boss, kaja ila katoka kasema anakwenda hospitali mtoto wake anaumwa"

    "eeehh ana mtoto huyu mtu"

    "ndio, kwani vipi boss"

    "hapana, nimeona hajaandika namba za simu hapa kwanini hajafanya hivyo"

    Suria Aliuliza hivyo lakini hapo anatamani amuone huyo dada, sasa kuambiwa ana mtoto, akapunguza munkari, mana faima yeye hana mtoto, tena ni bikra kabisaaa....

    "aaahh samahani boss, huyu msichana kasema hana simu"

    "aaahh, sawa.... Ila akipata simu alete namba ofisini kama zilivyo andikwa kwa wenzie... Na huyu nampa nafasi ya kusimamia upande wa wanawake... Atakua supervisor (msimamizi). Jina lake ni zuri sana... Hata sura yake pia, na hii ni sababu ya kumpa hio nafasi sawa"

    "sawa boss"

    "ok kaendelee na kazi"

    Basi surian alilipenda hilo jina na kulipa nafasi nzuri ya kazi kwani lipo kama jina la mama yake,.. Nzuri zaidi sura yenyewe pia ni kama ya mchumba wake, japo ni yeye lakini surian hajui mana hio sura hapo ni ya faima,.. Na jina ni la mama yake kweli



    "duuuuu watu wanafanana, yaani kama faima vile... Ila yote tisa.. Kumi ni hili jina, kama jina la mama yangu vile"

    Surian aliendelea kudiskasi hivyo vyeti na kufanya mfananisho



    Huku kwa Cecilia, sasa kichwa moto, yule mama kapata nafasi kubwa kama ile na istoshe yeye alikuwa amsaidie amuweke mama wa usafi chooni,.. Mana akimuweka huko kiwandani atagundulika mapema kwani boss lazima atembelee maeneo hayo...

    "sina jinsi, wacha nilinde ugali wangu, na niulinde ugali wa mama yule... Atakaa nafasi ya usafi na mshahara wake atachukua ule wa kiwandani"

    Aliongea Cecilia kuwa mama huyo atafanya kazi ya usafi wa vyoo vya kiwanda, mana huko chooni bosa hawezi kwenda... Hivyo pamoja na kuwekwa huko chooni, mshahara wake sio ule wa chooni, atachukua mshahara wa kule alikotakiwa kukaa, halafu sasa yule atakaye kaa kule kama supervisor (msimamizi) atalipwa mshahara wa chooni, hivyo hio ishu ceci kaamua kuicheza yeye kama yeye,... Na uzuri ni kwamba secretari yeye ndio aliopewa dhamana ya kutoa mishahara kwa wafanyakazi,... Yaani analetewa kitita kisha atakaye kuja anakula mshahara wake kama inavyo takikana, kwani pale anapopeleka documents kwa boss,.. Bosa anaziingiza kwenye kompyuta na kuandika kitendo au cheo cha mtu na mshahara wake,.. Hivyo siku mtu anakuja kuchukua mshahara anaangaliwa kwenye kompyuta analipwa kiasi gani kisha anahesabiwa.... Hapo mama surian keshapa kazi tena kwa mshahara mrefu sana,.. Kwani kaandikiwa laki nne,... Na Cecilia kaapa kumpa yote kwani ndio kitengo chake kilivyo ruhusu mshahara huo,....



    Siku ilikwenda vyema na leo walimaliza usaili wa watu wote, japo wapo waliokosa kutokana na vigezo kuto kamilika, lakini waliokamilisha wote walipata kazi,...

    "Cecilia? Hakikisha mpaka wiki ijayo, wafanyakazi wote wawe na NSSF sawa?"

    "sawa boss"

    "ok nakwenda, hakikisha unafunga vizuri, na afu ivi kila mfanyakazi umemwambia kuwa Jumatatu ndio kazi inaanza"

    "ndio boss, wanazo taarifa hizo"

    "ok sawa"

    "sawa boss"

    Surian aliondoka,.. Kafanikiwa kumuajiri mama yake lakini hajui kama kamuajiri mama yake mzazi, na mama pia hajui kama boss wake ndio mtoto wake wa kumzaaa...



    Sasa huku kwa akina aisha, au kwao akina surian, ikiwa ni jioni ya saa 12, mama huyo akiwa anasali nyumbani kwake,... Ghafla simu yake iliita mpaka ikakata kwani alikua katika ibada,... Iliita tena mpaka ikakata...



    Alipomaliza ibada aliiendea simu yake na kukuta kapigiwa zaidi ya mara moja na namba ni moja iliomtafuta,... Masikini ya Mungu salio hana,... Ghafla mumewe anaingia

    "eeh Afadhali baba suri umekuja.. Hebu nipe miatano nikapate vocha,.. Kuna namba ngeni hapa"

    "mke wanguuu... Unaomba maiti damu wewe"

    "oohhh samahani mume wangu,.. Sasa sijui huyu atakuwa nani"

    Mara simu ikaita tena kwa mara ya tatu,...

    "eehhh huyu hapa kapiga tena.... Hallooo"

    "eeh Shikamoo mama"

    "marahaba, ni nani mwenzangu"

    "oohh naitwa Cecilia ni sekretari wa kampuni ya MICCO (Moon Islamic Cloth Company)"

    "Miko ndio kampuni gani"

    "ehehehe, pale ulipoleta barua jana"

    "aaaaaaaaaa, nimekumbuka, kile kiwanda cha nguo za Kiislamu"

    "haswaaaa"

    "enhee mwanangu mpendwa niambie jamani"

    "Jumatatu njoo uanze kazi... Japo sio nafasi nzuri lakini naomba tufanye kazi mama angu"

    "wooooo ahsante sana mwanangu,.. Kiukweli nitafanya kazi yeyote wewe ondoa shaka mpendwa wangu"

    "sawa mama, njoo jumatatu"

    "ahsante sana mwali wangu... Kiukweli natamani uolewe na mwanangu jamani, mana kwa msaada huu"

    "hahahahahahaha... Mama bwana, usijali"

    "ooohhh mwanangu suria uko wapi mwanamke nilio mpenda ndio huyu... Ahsante sana mwanangu"

    "usijali mama"

    "haya jioni njema mwanangu"

    "haya nawe pia"

    Simu ilikata, kumbe wakati huo alikuwa pamoja na faima, kwani faima alimuuliza kiwa vitu alivyo mpa vimesaidia? Ndipo Cecilia akaamua kupiga simu kwa mama huyo

    "weee mama kashukuru huyoo"

    Aliongea ceci huku faima akiwa na shauku ya kujua alichokisema mama huyo, yaani laiti kama faima angejua kuwa huyo mama aliopigiwa ndio mama wa mchumba wake, na vyeti alivyo vitoa, hajui kama katoa kwa ajili ya mama wa mchumba wake..

    "enhee, kasemaje"

    "nakwambia ametamani niolewe na mtoto wake sjui nani kamtaja jina kabisa"

    "Weeeee,... Wamama nao wakifanyiwaga wema tu, utasikia uolewe na mtoto wangu... Duuuu haya kaolewe anti"

    "mmmhhh Mwenzangu wee, mali ina wenyewe hii"

    "mmhhh niambie anti... Siku izi unanene tu"

    "kawaida tuuu"

    "mmmhhh kawaida gani hii unene huo, ona shavu hilo"



    Sasa huku kwa akina asha, mama kapata furaha mpaka analia, kwa kumkumbuka mtoto wake,... Mana kama angelikuwepo naye angelikwenda kuomba kazi kwenye kampuni hio, mana kutokana na elimu yake ana uhakika angechukuliwa,... Mama hajui kiwa surian ndio boss mkubwa katika kampuni hio,...

    "sasa mambo safi kabisa baba asha... Kazi imepatikana"

    "tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema zake..."

    Aliongea mzee huyo ambaye yeye anaumwa, na toka astaafu kazi kazi katika shilika la reli mkoani tanga, mpaka leo hana kazi wala haruhusiwi kufanya kazi yeyote ile kutokana na ugonjwa, kwani kafanya kazi katika shilika la reli kwa muda mrefu hivyo amepata maradhi juu ya kazi yake, anaugua henia kwa muda mrefu hivyo inamsumbua...



    Tukija huku kwa faima akiwa kamsindikiza dada yake mtoto wa mama yake mkubwa Cecilia au shadya, sasa alikuwa akirudi nyumbani baada ya kufunga duka ambalo anauza yeye...

    "fey mambo"

    Alisikia salamu ilio ambatana na jina lake

    "poa"

    Alikuwa ni tariki mwenye kumfuatilia fey kwa ukaribu, na nguvu hio hupewa na zamina,.. Tariki naye ni mmoja kati ya wafanyakazi waliopata kazi kwenye kampuni ya MICCO (MIKO) ila kwa faima anajifanya mtoto wa mashavuni, ili akubaliwe...

    "mbona kama huna raha pindi unionapo, au nakukera Fey"

    "yes, kwa kiasi flani unanikera"

    "samahani kwa hilo... Ila mtoto mzuri kama wewe sidhani kama una roho ya kumchukia mtu.. Mi naona unasingiziwa tu"

    "sema shida yako riki, kwani sihitaji kuongozana na wewe usiku huu"

    Aliongea faima kwani anamfahamu tariki ni mtu anayetaka mahusiano na faima,..

    "Kiukweli sina asili ya usanii, na sihitaji kuwa msanii, ila neno langu kwako litakuwa wimbo kila siku"

    Wakati huo tariki akiongea hivyo safari ilikuwa ikiendelea, japo fey hataki kuongozana, lakini kama vile kakubali flani hivi..

    "enhee, imba niskie"

    Alionge faima kama kwa dharau, kwani anajua moyoni mwake yupo aliojaa....

    "najua neno nakupenda kwako umelisikia mara nyingi, ila yote yana uzito wa tofauti tofauti... Je nakupenda yangu kwako ina uzito kiasi gani Fey?? Nakupenda sana fey.. Niangalie basi, najua yupo umpendae, lakini kama unavyosikia tetesi za hapa na pale kuwa mtu huyo kafariki dunia fey,... Tumuombee huko aliko... Ila isiwe sababu ya kuninyima nafasi,.. Nahitaji kutulia na mwenzi wangu... Nina pesa lakini sitaki kuliongelea hilo kwani wewe sio mfanya Biashara kuwa tuzungumzie mambo ya fedha... Fey,.. Moyo unataka kuangua huu.. Fanya jambo basi jamani... Mana pamoja na fedha zangu lakini haziwezi kuzuia anguko la moyo wangu... Hebu ona... Ona sasa moyo huu hapa unachungulia.. Ona huo huo"

    Tariki alibwabwaja maneno mia kidogo, ila hakuna aliopanda mahindi akavuna mchicha... Kwa mara ya kwanza faima anatabasam kwa maneno mazuri kutoka kwa tariki,...





    Hakika wanaume ni watu wabaya sana, wanaweza kumfanya mwanamke awe atakavyo, iwe kwa mapenzi motomoto au pesa motomoto, mwanamke lazima ukae kwenye namba husika,... Faima aliokuwa mgumu kana kwamba hata kuitika salamu kutoka kwa tariki, kwake ni ngumu, lakini tariki kapiga domo mpaka fey katabasam kwa mara ya kwanza



    "waalakhi leo najipa ushindi japo sijafunga goli"

    Aliongea tariki huku fey akimuuliza riki kuwa

    "wajipa ushindi wa nini"

    "Kiukweli fey, sikuwahi kuliona tabasamu lako, Kiukweli limenipa amani ya moyo na kuona kipo kivuli katika moyo wangu, japo baado hakijasogea"

    Aliongea tarikwa maneno fulani ya uchombezaji,..

    "mmhh una maneno riki,..."

    "sio maneno fey,... Ni moyo wangu hautulii kabisa bila kupata mwenza"

    "bwana, ebu niache niende nyumbani kwanza"

    Aliongea fey kwani mahala walipofika kuna njia ya panda ya kwenda kwao... Hivyo wata achana hapo,.

    "ni sawa fey, nipe imani juu ya makutano mengine"

    "siwezi kukupa imani now coz, siwezi kukuamini moja kwa moja... Nitakujibu swali lako"

    Riki kusikia maneno hayo moyo wake ulimpasuka na kuhisi bahati imemuelemea kuliko wengine

    "sawa madam fey,... Ila jua kwa sasa napata jua na hakuna anayeweza kunipa kivuli, ispokuwa wewe fey... Wacha nikuache ili nikupe nafasi ya moyo wako juu yangu... Bye, ulale salama"

    "nawe pia"

    Kwa sasa fey hakuwa na majibu mabaya kqa riki, kwani keshajua ni mwanaume mwenye maneno mazuri yaliomfanya kutabasamu kipindi kigumu kama hiki ambacho kampoteza mpenzi wake,....





    Baada ya tariki kuachana na fey, alikutana na rafiki yake jumbe,

    "we riki nini sasa"

    "acha weweeeee.... Nani kasema mi nakataliwa... Mtoto keshaanza kuingia laini mpaka kalegea kama papai"

    "muongo riki"

    "aahh... We baki na mineno yako, eti mi muongo"

    Aliongea riki akiwa na rafiki yake mr jumbe,



    BAADA YA SAAA.... SIKU.... KADHAA KUPITA



    Ikiwa leo ndio siku ya Jumatatu, ni siku rasmi ya kufungua kampuni ya MICCO (Moon Islamic Cloth Company) Boss mkuu ambaye ni surian akiwa katika ofisi yake, yaani yeye kuwa wa kwanza katika ofisi yake ndio masharti ambayo kapewa ndani ya siku hizi za karibuni,.. Wafanyakazi walianza kumiminika katika kampuni hio, walimu wa kufundisha wafanyakazi jinsi ya kuzitumia mashine na kutengeneza mavazi maalum ya Kiislamu,.. Shadya au Cecilia ambaye yeye ndio mwenye kujua nani akae wapi na nani akae wapi, kwani yeye ndie alie wapokea na ndio mwenye kujua kila sekta ya mfanyakazi, hivyo walipangwa wote na idara zote zikawa na watu,... Walifelea watu kadhaa tu, lakini haikudhuru kitu chochote,



    Walimu Walianza kazi ya kufundisha wafanyakazi hao, jinsi ya kuanza kufuma uzi mpaka kuja kuwa nguo, ikiwa kiwanda kimeanza na nguo za dini pekee,.... Surian akiwa ofisini kwake anaendelea kugawa vitengo kwa wafanyakazi wa ofisini, yaani mameneja, wapokea oda, wahasibu na wengine wengi ambao wana vigezo vya kukaa ofisini na sio kiwandani,....



    Mama yake surian akiwa kawekwa kwenye nafasi ya chooni, na hio ni kwasababu tu asionekane kwakua umri wake hauruhusu kufanya kazi katika kampuni hio,...

    "samahani sana mama angu, Kiukweli nimefanya juu chini niweze kujenga riziki yako,... Binafsi hata mimi Sitamani ufanye kazi huku,.. Lakini nakuweka huku ili boss asikuone mana huku hawezi kufika"

    Aliongea shadya kama kumwelezea mama huyo ili asijiskie vibaya kwakua umri wake hauruhusu kufanya kazi hapo

    "usijali mwanangu, pia nakushukuru sana kwa kunisaidia... Nitafanya kazi mpaka utajiskia raha mwanangu.."

    Aliongea mama yake surian huku shadya ama Cecilia akisema kuwa

    "usijali mama,.. Pia utakua ukijificha pindi unapohisi boss anakuja, afu pia kwakua namba yako ninayo, basi pale nitakapo ona boss anakuja huku nitakupigia haraka ili asikuone"

    "sawa mwanangu, mimi nikiona tu simu yako, nitajificha mwanangu... Mungu akuzidishie mama"

    "usijali... Na mshahara wako, utalipwa laki nne"

    Aliongea shadya huku mama akibaki mdomo wazi, mana anajua kazi ya kusafisha choo hua haina malipo mazuri sasa anashangaa atalipwa laki nne ingali sio pesa kubwa lakini kwa maisha yao yalivyo magumu kwa sasa, hio pesa kwao ni kubwa sana... Na kama unakumbuka huo mshahara sio wa mfanyakazi wa chooni, bali jina la huyo mama lilipewa kipau mbele cha kusimamia wafanyakazi huko idarani, lakini kwakua umri wake hauruhusu kufanya kazi, hivyo ili boss asimuone ilibidi amueke huku chooni, kisha atafute msichana mingine ampe nafasi ya idarani...

    "mwanangu, ina maana nitalipwa pesa yote hio"

    "hehehehe mama bwana, Usijali hio ni pesa ndogo na pia ukifanya kazi vizuri utaongezewa mshahara"

    Aliongea shadya lakini mama huyo bado haamini kwa malipo ambayo analipwa, ikiwa ndio mshahara wa Kwanza wa kazi yake...

    Mama alitaka hata kupiga magoti kwa kushukuru,....



    Shadya alikwenda idarani na kumweka msichana mwingine kwenye idara aliotakiwa kukaa mama yake surian,

    "kazi yako ni kusimamia wafanyakazi na kuhakikisha wanatoa bidhaa bora na zenye uwingi unao hitajika"

    "sawa dada, nitafanya kazi kadri ya uwezo wangu"

    Aliongea dada huyo huku shadya akimtajia mshahara wake

    "utalipwa laki moja na themanini, ikiwa ndio mwanzo wa mshahara"

    "waoooo, ahsante sana dada... Nashukuru sana kwa kupata mshahara mzuri"

    Dada huyo alifurahi sana,.. Sasa mshahara huo ndio wa mtu wa chooni, na ule wa kitengo chake ndio ule analipwa mama yake suria,... Yaani hapo kuna mgeukano wa kazi na mishahara yao,...



    Basi kazi zilienda vizuri na kila mfanyakazi alishika kitengo chake huku akifundishwa katika mashine yake,.. Kiwanda ni kikubwa sana kana kwamba mpaka sasa kina wafanyakazi mia nne tu, hivyo bado wafanyakazi takribani mia moja ili kufikia idadi ya wafanyakazi mia tano,



    Ofisini wakiwa wamesha kamilika wafanyakazi 21, akiwemo mmoja ambaye ni mfanya usafi katika ofisi na vyoo vya ofisini,... Ila choo cha ofisi ya boss kipo ndani ya ofisi yake na hua mkewe ndio kaamua kumfanyia usafi mume wake, hivyo ofisini kwa surian, atakuja kufanya mkewe peke yake.... Kumbe hata majini wana wivu na wanaume kiasi hicho, kwani hakutaka kutoa nafasi kwa mume wake afanyiwe usafi ofisini kwake,... Hivyo mfanya usafi ataishia nje ya ofisi ya boss na hatakiwi kuingia ndani,.. Hio sio masharti bali ni wivu wa jini maimuna



    Jioni saa kumi na moja mama asha akiwa nyumbani kwake anapiga stori na familia yake, wakiwa watu watatu tu, mana walikuwa wanne pamoja na surian, lakini kwa sasa wapo watatu mana surian katoweka nyumbani hivyo hawajui kama kafariki au yupo hai.. Lakini kwa sisi wasomaji tunajua surian yupo hai na mama huyo anafanya kazi kwa mtoto wake bila kujua,...

    "yaani bana asha, nalipwa mshahara mkubwa jamani, haaaaa... Yaani mpaka natetemeka"

    Aliongea mama huyo huku mzee Rashidi ambaye ndio baba yake surian akiuliza kuwa,

    "kwani kitengo gani wamekupa"

    "baba asha, kwani mimi nimetaka Mashauzi, mimi nafanya usafi wa chooni"

    "haaaaaaaaaa, mama muongo... Ina maana mfanya usafi wa chooni ndio alipwe pesa yote hio"

    Aliuliza asha huku mzee rashid akianza kuogopa kana kwamba labda mkewe kapendelewa kutokana na mwili wake, mana mama surian pamoja na umri mkubwa alio nao lakini anazeheka na umbo lake,...

    "kwahio mama asha, unalipwa laki nne afu unadeki vyoo"

    "ndio baba, asha"

    "uuuuufyuuuuuuuuuu"

    Baba asha alipumua kwa kuchoka na kujua mkewe keshajilipua na vijana mana, mama yake suria kama ni wale wamama wasio jielewa, basi ndio ule wakati wa kuchukua vijana wadogo, japo ana umri mkubwa lakini uzuri na umbo, ni kama bado anavyo,.. Na yote hio ni kwasababu ya matunzo alio tunzwa na mume wake, kwa umri huo kijijini ni mzee wa miaka 70, lakini kwakua yupo mjini basi anakuwa anakwenda na umri wake....

    "baba asha, mbona umepumua kwa nguvu hivyo"

    "aaaaa tutaongea usijali"

    Aliongea mzee huyo huku mama asha akiwa na wasiwasi kuwa mume wake anataka kusema nini,

    "asha mwanangu, naskia nafasi bado zipo, kwanini nawe usiende mwanangu..."

    Aliongea mama huyo kuwa kwanini asha asiende kuomba kazi,

    "aahhh mama, hebu wacha kwanza nitulize akili yangu kwanza mama... Mana sasa hivi hata simu yangu nimeuza na laini nimetupa mana staki mawazo"

    Aliongea asha huku mzes rashid akisema

    "huyu mtoto ana kichaa huyu, yaani kauza na simu afu laini katupa"

    "baba asha, huezi jua... Haya wewe asha kwanini ufanye hivyo"

    "mama.... Yaani kwenye group letu la wasapu nasemwa mimi tu, meseji zinakuja naambiwa mimi muuaji... Sitaki kabisa mimi sitaki"

    "lakini ni bora ungezima simu tu"

    "msijali, nitakwenda kuomba kazi ila sio leo"

    "sasa kama sio leo mwanangu, nafasi si zitajaa"

    "kama sio riziki yangu baba, hata nikienda sasa hivi sitapata"

    "lakini ni vyema kuwahi"

    "basi nitakwenda wiki ijayo"

    Aliongea asha kuwa kakubali kwenda kuomba kazi wiki ijayo,.. Sasa lile agizo la maimuna kumtaka surian aajiri familia yake ndio linakwenda kutimia,...



    "habari za kazi mume wangu"

    Maimuna au maimati alimsalimia mume wake huku akimvua tai, mana suria yeye ndio wa kwanza kuingia kazini na ndio wa mwisho kutoka kazini, hatakiwi kuonwa na mtu yeyote yule ndani ya wiki hizi za karibuni,....basi suria alikwenda kuoga kisha akapata chai ili kusubiri chakula cha jioni, wakiwa wawili tu na mke wake,.... Sasa wakati surian kakaa kwenye sofa akipata chai, na mkewe akiwa jikoni anafanya mambo ya chakula cha jioni,.. Ghafla alianza kushikwa shikwa nyuma ya shingo yake....

    "mke wangu acha utani... Hebu kapike mi nataka kulala"

    Aliongea surian,... Lakini na huku jikoni, maimuna naye kuna kitu kahisi ndani ya nyumba yake,... Huku sebuleni, surian anazidi kushikwa na anaemshika yupo nyuma ya sofa, na kwakua suria anajua ni mke wake hivyo katulia na kusapoti kushika mkono wa huyo mwanamke ambaye anamshika,... Lakini surian kuangalia huo mkono, laaaaaaa haulaaaaaa











    Kabla ya siku hio nyakati za jioni katika himaya ya majini wema ndani ya bahari,.. Sio majini wote wa ndani ya bahari ni wema, wengine ni wabaya, ila kundi hili la akina shaimati na maimati, wao ni kundi la majini wema, ama wazuri, wasio na tabu na mtu,....



    Sasa siku hio shaimati alikuwepo nje akiwa kama malikia wa eneo hilo baada ya murati Sabaha kukiuka masharti yalio wekwa dhidi ya binadamu na majini, sasa malikia wa majini katika himaya hio ni Murati shaimati (shamimu).... Sasa siku ya leo Aliweza kumkumbuka ndugu yake au jini mwenzie ambaye kwa sasa anakula raha ndani ya ndoa yake, na hayupo tena katika himaya hio, japo anaruhusiwa kwenda kusalimia....

    "nimemmisi maimati wangu jamani"

    Ilikuwa ni sauti ya shaimati akiwa chumbani kwake, na nyakati hizo zilikuwa ni za usiku wa saa sita, kulilindima baridi kwa kiasi fulani,...



    "naweza kwenda hata kumuona angalau kwa macho tu"

    Aliongea shaimati akiwa pekee hapo chumbani kwake, kwani hakua na mtu wa Kuzungumza naye,.... Haikupita hata dakika moja shaimati kapotea katika mazingira ya kutatanisha, kana kwamba kaelekea duniani kwa nduguye maimati,...



    Kama kawaida yao au kanuni na masharti yao wao wenyewe kuja duniani kila saa nane za usiku, haijalishi unakwenda kwa ubaya ama kwa uzuri,.... Majini karibu wote wamepewa uwezo mkubwa, ingali wanatofautiana nyenzo kwa wale wazuri na wabaya,.... Shaimati hakuwa na muda wa kufikiri kuwa maimati anaishi wapi, kwani wao wana uwezo wa kunusana popote pale walipo, na mbaya zaidi nyumba ya maimuna au maimati haipo mbali sana na bahari ambayo wao hutokea, hivyo ilikuwa ni rahisi sana kwa shaimati kujua wanapo ishi....



    Ikiwa ni saa nane usiku shaimati akiwa nje ya jengo la ndugu yake ambaye ni maimuna,....



    Na wakati huo huo maimuna alikuwa akipata raha zake toka kwa mume wake,.... Na mbaya zaidi naye kagundua kuwa shaimati yupo nje ya jengo hilo ambalo yeye yupo kwa ndani na wakati huo alikuwa katika hali ya kufanya mapenzi na mume wake ambaye ni surian....



    Sasa maimati kumbe anapenda sana ndugu yake au jini mwenzake aje kuolewa, mana mpaka sasa hajui hata raha ya mapenzi ipoje,... Sasa maimuna akaanza kulia milio ya msisimuo ambayo inaweza kumfanya shaimati kuyatamani maisha ya ndoa, hivyo maimuna akazidisha milio ya kimapenzi kwa makusudi ilo shaimati asikie naye aitamani ndoa ili wote wawe wamesha olewa, mana kule ujinini sio wengi ambao wana asili mbili, na shaimati na maimati ni majini walio shibana...



    Kweli zile sauti taamu ziliweza kupenya kwenye masikio ya shaimati, hivyo akajikuta anaanza kutega sikio ili kusikia ni utamu wa aina gani ambao ndugu yake huupata kila usiku wa saa nane,... Sasa shaimati alikuwa akihisi baridi, lakini ghafla akaanza kuhisi joto, kana kwamba sauti tu inampa joto, je kama angelikuwa shughulini ingelikuwaje,.. Na wakati huo maimuna anazidi kulia milio ile ya hatari hatari, yaani ile ya kumtoa nyoka pangoni... Shaimati alipotea pale nje haikujulikana kaelekea wapi,



    Kesho yake asubuhi sana nyakati za saa 12 na nusu, surian ndio wakati wake wa kutoka nyumbani ikiwa anamaliziwa kufungwa tai na mke wake, na siku hio mke hakuwa tayari kwenda kazini,... Na surian anawahi kazini ili asionwe na wafanyakazi wake kwani kuna masharti kawekewa na mke wake,...



    Ilipofika nyakati za macha shaimati aliingia ndani kwa maimuna, alimkuta anasoma kitabu cha dini, mana hana pakwenda kwa nyakati hizo,

    "heeeeee shamimuuuuu... Karibu"

    Maimuna alimkaribisha mwenzie kwa furaha na kujifanya jana hakumhisi kuja kwake,... Sasa kila mmoja anajua kuwa usiku wa jana hakujulikana, hivyo ndivyo ilivyo kwa majini, huyu kajua kuna jini mwenzie nje, lakini yule wa nje hajui kama kajulikana ndani, na yule wandani kajua kuwa kuna jini nje lakini hajui kama kajulikana kule ndani.... Hivyo ndivyo ilivyo kwa majini,



    "ahsante, heeeeee munaa umenenepa jamani"

    Aliongea shaimati kama kumsifia maimuna kwani ilionekana hali ya mwili wake kuwa mkubwa kiasi fulani,

    "mambo ya ndoa hayo"

    "mmmmhhh kwa unavyo yasifia mhhh"

    "sasa nisi yasifie kwanini? Mana nipo ndani ya ndoa, na nimejua utamu wake na raha zake..."

    "mmmhhh hongera yako mwenzangu"

    "haya niambie, hawajambo huko kwetu"

    Shaimati aliuliza hali ya ujinini kuwa hawajambo

    "aahh nadhani wote wamekumisi sana, ila mimi nimetoka kwa kutoroka ujue"

    "weeeeee, sasa wairati sarika akijua itakuwaje shaimati? Hebu nenda bwana"

    Maimuna alimtaka jini mwenzie aweze kurudi ujinini kwani alitumia njia ya kutoroka usiku ule,

    "nitakwenda,.. Lakini nami nimejikuta nayatamani maisha ya duniani"

    "sawa lakini unatakiwa upewe ruksa ya kuja kuishi duniani"

    Aliongea maimuna huku shamimu akiwa hatamani kurudi ujinini....

    "Kiukweli shamimu nahisi upo huru huku duniani, Kiukweli nayatamani maisha yako ambayo unaishi...."

    Aliongea shamimu huku akiangaza macho huku na kule na kuiona picha ya surian iliopo ukutani

    "waooo shem wangu huyu"

    Aliongea shamimu huku akiisogelea ile picha na kuishika shika, kitu ambacho maimuna hakukipenda, kwasababu alihisi shamimu angemtamani mume wake,...

    "shamimu? Naomba utoke tafadhali"

    Aliongea maimuna huku akiwa kakasirika kwa kitendo cha shamimu kuipapasa picha ya surian kimahaba

    "unanifukuza nyumbani kwako"

    "sina maana hio, ila kuna hisia za ujinga mbele ya uso wako"

    Aliongea maimuna huku shamimu akijibu

    "ni kweli, sikua nikitamani mwanaume kamwe... Lakini sauti za jana, zimenifanya nami nivute hisia kali na kujiuliza ni raha gani ambazo unazipata usiku wa saa nane..."

    Aliongea shamimu ambaye ni jini mwenzie na maimuna, na wote binadamu kwa majini... Yaani wana asili mbili...

    "ni sawa, lakini jaribu kutafuta wako"

    Aliongea maimuna jambo ambalo limemchekesha sana shamimu huku akisema

    "kwani wewe huyu ni wako"

    "una maana gani"

    "mchumba wa mtu huyu... Hapa umempokonya mwanamke mwenzio tunda lake... Sasa limekuwa lako, wakati ulilichuma kwenye mti wa watu"

    Aliongea shamimu huku maimuna akiwa hataki kuyajali maneno yake

    "ok sawa, hata mimi nililijua hilo... We nenda nyumbani kwetu... Na pia nisingetamani kukuona kwa wakati mwingine"

    Maimuna aliamua kama ni mbwai iwe mbwai, lakini sio kwenye swala la mume....

    "sawa, nakwenda, lakini kaa ukijua kua, mti wenye matunda ndio hupigwa mawe"

    Aliongea shamimu kisha akapotea katika mazingira ya kutatanisha, kana kwamba tayari wamesha anza ugomvi kati ya wawili hawa kisa ni mwanaume mmoja tu,.....



    Sasa ilipofika nyakati za jioni, surian akiwa kaketi katika sofa akipata chai safi kabisa.... Na wakati huo katoka kuoga, lakini katika kidole chake hakukua na pete,... Ghafla shamimu alitokea nyuma ya surian na kuanza kumshika shingoni, tena ile kimahaba.. Surian kwa akili yake alijua ni mke wake, mana wanaishi wawili tu na yeye hana nguvu au uwezo wa kujua kuwa kuna jini mwingine kaja... Sasa surian akawa anaushika ule mkono kwa nia ya kusapoti mshiko mshiko wa mkewe,.. Japo alikuwa akimharakisha akapike kwani anataka kulala... Na wakati huo kule jikoni, maimuna naye keshajua kuwa shamimu yupo mdani, sasa hakutaka kutoka mapema ili ajue shamimu kampenda mume wake kweli au alitania... Hivyo akachelewa kutoka na kubaki kuchungulia kwenye upenyo wa mlango,... Aliweza kuona jinsi surian anavyo shikwa shikwa kimahaba na wakati huo suria anajua ni mkewe kwakua yupo nyuma ya mgongo wake



    Lakini surian kuangalia huo mkono, laaaaaaa haulaaaaaa, kumbe hakuwa mkewe... Na aliujua vyema na kukumbuka, siku ile ya Kwanza kupelekwa ujinini alishikwa mkono na huu mkono, hivyo alipo uona tu akastuka na kuamka... Alikuwa ni shamimu,.. Na pale pale maimuna akatokea

    "shaimati, hivi ni tabia gani umeanza... Mbona asili yetu hatupo hivyo ndugu yangu"

    Aliongea maimuna tena kwa upole wa hali ya juu...

    "yaani kitendo cha kumshika mumeo, joto nililo pata... Sijawahi kulipata toka kuzaliwa kwangu.... Ila narudia tena MTI WENYE MATUNDA NDIO WENYE KUPIGWA MAWE... Nakwenda, lakini jua kuwa umedungua tunda la mtu, hivyi sio lako"

    Aliongea shamimu kisha huyoo akapotea,... Maimuna alikasirika sana kwa kitendo ambacho shamimu kakifanya,

    "surian mume wangu, kwanini hujavaa pete yako...."

    Muna alilia na mume wake kwanini hakuvaa pete ambayo kapewa, mana kama surian angelikuwa na pete basi shamimu asingeliweza kumsogelea kamwe,...

    "samahani mke wangu,... Nami nilijua ni wewe ndio upo nyuma yangu na ndio mana nikawa nimetulia... Basi nakwenda kuvaa"

    Aliongea surian kisha akaingia chumbani na kuivaa PETE YA KIKE, ambayo ndio msaada wake juu ya viumbe vibaya na hata vizuri,.. Kwani shamimu ni kiumbe mzuri lakini amekuwa na tamaa ya mapenzi ingali mwanzo hakuwa hivyo.... Ila jambo hilo analijutia sana maimuna kwa kuongeza milio ya mahaba ilio mfanya shamimu kupata hamu



    Kesho yake, kama kawaida surian akiwa kazini ikiwa ni mida ya saa nne za asubuhi,... Kwa ukawaida hatakiwi kutoka ofisini hapo mpaka siku 17 ziishe ndipo anaruhusiwa kuonwa na wafanyakazi wake... Leo mkewe kaja kazini hivyo ndie mwenye kutembelea wafanyakazi kiwandani,.. Wafanyakazi wenyewe wanabaki mdomo wazi kwani maimuna ni mzuri mithili ya malaika, hata wanawake wenzie walikuwa wakimshangaa mwanamke huyo ambaye ndio mke wa boss wao...



    Tukija huku ICC ambako ndipo faima anapo fanyia kazi kwa kufanya mauzo ya nguo za Kiislamu,... Baada ya kufanya biashara na wateja alio kua nao, sasa katulia huku akiwa anafungua simu yake,... Kuna namba ya simu alikuwa akiitafuta na kuipata

    "RIKI, hivi utakuwa mkweli kwangu... Kiukweli naogopa kuumizwa katika mapenzi,.. Sihitaji pesa zako wala uzuri wako.. Nahitaji mapenzi ya kweli ila nahitaji ubadilike"

    Aliongea faima bada ya kuiona namba ya Riki ambaye ni mwanaume aliotokea kumpenda sana hivyo hapo kaitafuta namba ili aweze kumpigia simu amkubalie....



    Lakini kabla hajapiga, alifungua upande wa picha, zake na kuangalia picha ambazo alipiga akiwa na surian,.. Kitendo ambacho kilimtoa machozi kwa mara nyingine tena, hivyo inaonekana anamkubalia tariki ili ampunguzie tu mawazo, ila aliopo moyoni ni surian japo anasikia kafariki dunia....

    "mwaahhh,.. Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi, sitokaa kukusahau surian wangu... Nakupenda kuliko hata ninavyo jipenda... Sijakusaliti, ila nakwenda kumpata mwenzangu atakaye nipotezea mawazo yangu... Nakupenda sana mume wangu, japo nasiki umefariki dunia... Mungu akulaze mahali pema peponi... Amen"



    Aliongea faima baada ya kuangalia picha ambayo walipiga pamoja,... Faima aliweka simu sikioni, alimpigia tariki ili amkubalie ombi lake,... Na simu ilianza kuita.... Ilipokelewa

    "hallow Riki Asalam Aleykh"

    "waaleykh msalam, vipi hali"

    "salama tu"

    "haya niambie bibie, nina furaha sana kuiona simu yako nyakati hizi"

    "ndio... Vipi upo bize sana"

    "hapana, hapana, hapana,... Sipo bize.. Nipo ofisini hapa kuna baadhi ya documents nazi saini"

    "basi nitakwambia baadae Ukimaliza"

    "nooooo niambie sasa hivi.... Usiutese moyo wangu kwa madakika machache yajayo"

    Aliongea tariki na kujifanya mtu wa busara na mwenye pesa....



    Lakini sasa faima kabla hajaongea, alishangaa kusikia sauti ya kike hapo nje ikisema kuwa....

    "surian wako yupo hai"

    Faima alikata simu haraka ili kuangalia hapo nje ni nani kataamka maneno hayo,...

    "waaaaaaoooooo.... Dada shamimu, ulienda wapi"

    Ikumbukwe kuwa shamimu na faima walijengaga urafiki wakati ule walipokuja kutafuta MWANAUME MSAFI, na faima alitoboa siri ya yeye na surian kuwa wao hawajawahi kufanya mapenzi, ndipo shamimu akaanza kumfuatilia mchumba wa faima kwasababu ndio aina ya mwanaume waliokuja kumtafuta, hivyo faima anatakiwa kumlaumu shamimu mana shamimu ndio kasababisha surian kwenda ujinini

    "mbona nipo jamani fey"

    "hapana bwana dada,... Karibu miezi mitatu minne hivi sijakuona"

    "aahh si unajua mambo ya kazi fey"

    "ni kweli,... Haya niambie dada shuu"

    "nipo... Mbona kama ulikuwa unalia"

    "we acha tu dada shuu,... Ni mwezi wa tatu kama sio wa nne, surian wangu sijamuona, naumia sana..."

    Aliongea faima huku akilia na kumuegemea shamimu....

    "mbona surian yupo na hata jana nilimuona"

    Shamimu katumbua jipu lililoiva....

    "unasemaje dada shuu"

    "surian wako jana nilimuona... Na jinsi ya kumpata ni rahisi sana... Ila unatakiwa kuwa mpole, mvumilivu, mnyenyekevu, na mwenye utulivu..."

    "sawa dada shuu... Nipo tayari kutii vigezo vyote,.. Hebu niambie... Nampataje na yupo wapi kwasasa"

    Faima aliuliza kwa umakini huku akiwa katoa macho

    "unaijua kampuni mpya inayotengeneza nguo za dini hapa mkoani Tanga"

    "ndio.... Si hii inayo itwa MICCO"

    "yeeees.... Mmiliki wa kampuni hio ni surian na mke wake"

    Faima kashtuka kwa kusikia neno SURIAN NA MKE WAKE

    "hivi umesema surian peke yake au surian na mke wake"





    Katika maisha haya hakuna kitu kinauma kama kusikia ya kwamba mtu umpendae ameoa au kaolewa, inauma sana,....



    Faima alipatwa na mshangao wa hali ya juu baada ya shaimati kumpa ukweli wa mambo,.. Faima ametokea kumpenda surian toka moyoni mwake, na kajitunza mpaka kesho kwa ajili ya suria, siku zote husikia kuwa suria kafariki dunia tena kwa kuuwawa na dada yake,.. Leo anasikia kuwa suria ndio mmiliki wa kampuni mpya iliofunguliwa hivi karibuni, shaimati pia hakutaka kumficha kuwa suria keshaoa japo kaoa mwanamke ambaye sio asili yake,...



    "hivi umesema surian peke yake au umesema surian na mke wake"

    Faima aliuliza kwa mshangao wa hali ya juu,

    "faima, surian bado ni wako tu.. Ni kweli surian kaoa, lakini bado ni haki yako kwasababu haki za kibinadamu zikiingilia kati, nina uhakika aliokuwa naye atachukuliwa hatua za kisheria, japo hawato muweza"

    Aliongea shaimati na yote hio ni kwasababu ya wivu wa mapenzi, hivyo kaona kuliko maimuna afaidi mwenyewe, bora tunda hilo lirudi kwa aliekua nalo awali,...

    "una maana gani dada shuu, ina maana nu kweli surian kaoa"

    Aliendelea kulia msichana faima huku shaimati akijihisi kua na raha sana kwani tayari keshalitumbua jipu

    "ndio, ila kuoa kwake sio tatizo, mana anamilikiwa na kiumbe kama mimi"

    Faima alishtuka sana kusikia kua suria anamilikiwa na kiumbe kama huyu, kana kwamba rafiki yake huyo sio binadamu bali ni kiumbe,...

    "una maana gani? Ina maana wewe sio binadamu"

    Aliongea faima lakini shuu ama shamimu alimjibu

    "mimi ni nusu ya binadamu, ila ni mapema mno kunifahamu"

    Shuu alijibu kisha akaondoka zake kwa hatua za kawaida tu, wakati huo faima anamwangalia tu mpaka akapotelea uchochoroni,...



    "mbona sielewi, au naota mie?"

    Fey alijiuliza mara kadhaa kua huenda ni ndoto labda ndio imemjia mchana huo... Lakini aliamini haikuwa ndoto bali ni ukweli mtupu



    Huku nyumbani kwa mzee Rashidi akiwa na mtoto wake asha, mana mama kaenda kazini, sasa baba ana wasiwasi na mke wake kwasababu kitengo alicho kipata hakiendani na mshahara ambao analipwa mkewe

    "mwanangu asha, hebu fanya hima ukaombe kazi pale... Mimi nina wasiwasi na mama yako... Ina mana hata wewe inakuingia akilini hio.. Mfagia vyoo alipwe laki nne,.. Hapana.. Hebu kaombe kazi mama"

    "baba, mi najua mama hana lolote ni wasiwasi wako tu baba... Mimi nataka nikaombe wiki ijayo"

    "aahhhh sawa mimi sina wasiwasi sana, ila inawezekanaje Mfagia vyoo alipwe laki nne"

    "huezi jua baba.. Ni bahati ya mtu tu"

    Wakati huo asha akipika chakula cha mchana,.... Ghafla mlango unagongwa, asha akaacha safuria ichemke, akaenda kufungua mlango..

    Hakuamini kumuona shamimu

    "haaaaaaa jani shuu, mambo"

    "poa, mbona umebadilika hivyo, ulikuwa unavaa vizuri, unajisitili sasa mbona umebadilika"

    Aliongea shamimu mana alimuacha akiwa anapiga hela na anajua kwanini alikuwa akipiga pesa....

    "we acha tu shuu, yaani ulipo niacha biashara yangu ilikuwa nzuri, lakini pia ilikuja kuwa mbaya baada ya kusikia kuwa mimi nimemuua mdogo wangu, Kiukweli sikua na raha kabisa"

    "wewe umemuua mdogo wako? Kwani una ndugu wangapi"

    "mmoja tu"

    "sasa umemuua yupi tena"

    "aahh bwana tuyaache hayo... Mambo mengine vipi"

    "safi tu... Vp surian yupo"

    Shamimu aliuliza makusudi japo yeye ndio anajua surian alipo

    "aahh sasa shuu, si ndio nimekwambia hapa surian hayupo, yapata miezi minne sasa na ndio mana nimeambiwa nimemuua ili nipate pesa"

    Aliongea asha huku akitaka hata kulia,

    "sikiliza asha.... Ile pete, ndio ilikuwa sababu ya biashara yako kuwa nzuri, na kama ni surian mbona yupo... Na hata jana nikua naye usiku"

    Aliongea shaimati lakini asha kwa hasira na ghazabu za kujua kua shamimu anaongea uongo, kwani surian hawezi kuwepo mjini bila kuja nyumbani kwao, tena kwa jinsi surian anavyo mpenda mama yake, hawezi kaa hata siku moja bila kuja,..sasa leo anasikia ya kua surian yupo tena hata jana alikuwa naye....

    "asha.... Asha... Njoo basi rafiki"

    Shamimu aliita lakini asha hakutaka kusikia kwani alichokisema shuu ni uongo mtupu, na hatamani kuusikiliza tena,... Basi shaimati aliondoka zake baada ya kujua kuwa asha kagoma kuongea naye... Nia ya shamimu ni kutangaza uwepo wa surian, ili amkomeshe jini mwenzie ambaye anapata raha kupitia mtu huyo,



    Ilipofika mida ya jioni mama asha akiwa nyumbani baada ya kurudi kazini, na kila akirudi kiuno humuuma kwa vile anavyo inama kila wakati kwa kusafisha vyoo, mana vyoo hivyo huchafuka kila wakati,.... Mama asha akiwa nyumbani akifanya maandalizi ya kupika chakula cha mchana, na hapo alikuwa akimpa stori mtoto wake asha

    "wewe ungekuja kuomba kazi mwanangu,... Wasichana wenzio wapo wamejaa tele, yaani wamama hakuna kabisa"

    Aliongea mama huyo huku asha akiwa na msimamo wake kuwa atakwenda lakini ni wiki ijayo

    "nitaenda mama"

    "tena naskia skia huyo boss ni mtotoooo"

    "heeeeee mama,.. Kumbe ndio mana baba ana wasiwasi, haya hivyo umevijuaje"

    "si wafanyakazi walio muona wanasema"

    Mara fsima kaingia huku akiwa na furaha kwa kitendo cha kusikia kuwa surian ndio mmiliki wa kile kiwanda cha nguo za Kiislamu...

    "heeee mwali wangu huyooo karibu mama"

    "ahsante mama, shkamoo"

    "marahaba mwali hujambo"

    "sijambo, shkamo wifi asha"

    "marahaba mambo fey"

    "poa...."

    Lakini kabla faima hajaanza kusema, ghafla mama asha kaanza kusema kuwa

    "hivi faima mwanangu... Mbona hujaenda kuomba kazi kwenye kile kiwanda kipya... Yaani wasichana weeengi wapo humo"

    Aliongea mama huyo huku faima akiuliza

    "kwani wewe umepata kazi"

    "ndio"

    "boss wa kampuni hio unamjua"

    Faima aliuliza makusudi tu mana kaambiwa kuwa boss wa kampuni hio ni surian

    "ndio tena ni kijana mdogo tu"

    "aahhh nitakwenda kuomba tu"

    Sasa faima kajiuliza sasa kama mama mtu anafanya kazi huko na kamjua boss, ina maana shamimu kamdanganya kuwa surian ndio mmiliki wa kiwanda hicho,....

    "nendeni, hata sasa hivi nilikuwa namwambia wifi yako hapa... Aende ili tupate pesa nzuri"

    "sawa mama nitakwenda"

    Faima alianza kupata huzuni tena mana kaja kutoa taarifa kuwa surian yupo pale, sasa anakuja kujua kumbe mama mtu anafanya kazi hapo, sasa kama ni kumuona si angemuona kabla,... Faima akatulia tu wala hakuongelea swala la surian tena mana ataanza kuliza watu,... Ila katika moyo wake alimlaumu sana shamimu kwani kamdanganya vikubwa sana kuhusiana na mchumba wake,....



    Sasa tukija huku nyumbani kwa akina surian akiwa jirani na mkewe wakiwa wamebanana kwenye sofa moja,.. Surian kasahau kama anatakiwa kwenda kuiona familia yake, kasahau kila kitu,...

    "mme wangu,... Nina jambo nahitaji nikwambie"

    Aliongea maimuna huku surian akiwa makini

    "niambie"

    "nina mimba"

    "aaaaaacha utani muna"

    "kweli vile"

    "umepima saa ngapi na wote tulikuwa kazini leo"

    "mimi sina cha kupima... Ina maana umenisahau"

    "aaahh hapana sijakusahau mke wangu, ila sikufahamu kwamba hata mimba mnaweza kuzifahamu bila kupima"

    "uwezo tulio nao ni mkubwa sana,.. Na hata hapa baada ya miezi miwili tuna uwezo wa kujua hata jinsia ya mtoto wetu"

    "ole wako awe wakike, atakuwa sio wangu huyo"

    Aliongea surian huku wakifurahia swala hilo, mana ni muda mchache tu hata mwezi hakuna toka kufunga kwao ndoa, lakini muna anadai kuwa na mimba...



    BAADA YA WIKI MBILI KUPITA



    Ni siku nyingine tena, na ni mwezi toka kampuni ya MICCO kufunguliwa, hivyo wafanyakazi wameshakula mishahara ya kwanza kwanza,... Siku hio mke na mume wakiwa kazini,... Mje alitamani kutoka na mume wake wakatembee mjini, kwa sasa masharti yameisha kwani tayari ule wakati umekwisha,...

    "we nenda tu"

    Aliongea surian kana kwamba hataki kutoka hata nje yaani mazoea ya masharti yamekuwa kweli,

    "jamani baba Rashidi, twende tukale hata chipsi jamani, kila siku uletewe humu, noo bwana twendeee"

    "mama chidi, naomba uende wewe tu"

    "hapana,..."

    "lakini nipo bize, ona oda zinavyo miminika, naondokaje sasa"

    "ok... Shadya?, Shadya"

    "abee boss"

    Aliitwa sekretari Shadya kupewa ile laptop ya boss...

    "fuatilia hizo oda zote hakikisha zinatoka, sawa"

    "sawa boss, nitaifanya kazi hii"

    "haya sasa upo bize tena"

    "lakini mke wangu,... Ile kazi yapaswa nifanye mimi"

    "hapana, wewe ni boss now, unahitaji kutuma tu, hebu twende bwana ukanitembeze kwenye mji wenu"

    Aliongea mwanamke huyo huku surian akikubali kishingo upande,... Gari yao hua wanaipaki pembeni kidogo ya ofisi yao hivyo hata wakitoka hakuna mfanyakazi ambaye atawaona,.. Basi surian aliingia na kupandisha kioo cha gari, kwani tayari tabia ya kuto onekana na watu imeanza kumzoea, yaani hataki kuonwa na watu kabisa... Kasahau kuwa kuna familia yake,...



    MLINZI WA GETI alifanya kazi yake kisha mke na mume wakatoka, lakini ile wanatoka tu na asha nae ndio anaingia, yaani kiduchu kiduchu waonane, na asha hana tetesi zozote kuhusu mdogo wake ndani ya kampuni hio,... Asha akiwa kashikilia vyeti vyake kaja kuomba kazi kama alivyokuwa akilazimishwa na wazazi wake,... Asha anafika ofisini boss hayupo,

    "yaani boss katoka sasa hivi tu"

    Aliongea shadya huku akiwa bize na kazi ambayo kapewa

    "kwahio unanisaidieja dada angu"

    "mmhhhh, hebu ngoja nijaribu kumpigia simu"

    Shadya alichukua simu ya mezani kisha akampigia simu boss wake...



    "umeona sasa, nimetoka sasa hivi tu, na simu napigiwa, ndio mana staki kukaa mbali na ofisini"

    Aliongea surian baada ya kuona simu ya shadya

    "Enhee sema kuna nini tena"

    "aahhh boss... Kuna msichana kaja kuomba kazi"

    "documents zake zimekamilika"

    "mmmhh ndio, ziko sawa"

    "ok mwambie sadiki amsajili na aanze kazi kesho... Afu pia akampange mahali penye upungufu wa wafanyakazi"

    "ok sawa boss ahsante"

    "ok"

    Shadya alikata simu kisha akampeleka asha kwa sadiki,... Sadiki ndio meneja mwajiri wa kampuni hio, hivyo yeye ndio anajua kila kitu kuhusu wafanyakazi, na ni kijana mdogo lika na surian,...

    "boss,... Kuna mgeni hapa"

    "ni nani na katoka wapi"

    "samahani boss,.. Kaleta barua ya maombi ya kazi"

    "aaaoo ok mwambie aingie"



    Huku mjini surian akiwa na mke wake walipaki gari mahali fulani, kisha wakaingia sehemu moja iliokwenda kwa jina la TANGA SPECIAL BITES, waliingia hapo lakini surian alitaka kukaa ndani, japo kwa nje kuna nafasi, yaani surian kwa sasa keshakua mtu wa kujificha ficha kwani keshazoea yale masharti na kayatamani yaendelee vile vile...

    "ndani kuna joto mume wangu, tukae hapa nje"

    Aliongea maimuna huku baadhi ya wanaume wakitoa macho kwani muna ni mwanamke mrembo sana, wakijua ni mwanamke wa kawaida tu

    Surian alikubali kukaa pale nje lakini hajapenda kabisa kukaa hapo nje, kakaa kwa niaba ya mke wake tu,... Basi waliagiza vyuku vipsi na vitu vingi hususan vinywaji safi,... Midomo yao ilianza kuchangamka, lakini ghafla ilisikika sauti ikisema

    "jamani, ona ule sio mzimu wa surian ule?"

    Aliongea dada mmoja ambaye ni mpita njia eneo hilo,.. Lakini muna aliisikia hio sauti peke yake....

    "heeeeee afu mbona ni surian kweli"

    "wewe, sio surian, ule ni mzimu wa surian"

    Walikuwa ni rafiki zake na asha, kama unawakumbuka hawa ndio wale kimbelembele waliomtangazia kuwa kamuua mdogo wake,.... Mara moja walipiga simu kwa asha...

    Wakati huo asha ndio anatoka kiwandani baada ya kuonyeshwa kitengo ambacho kesho atakuja kufundishwa,...

    "heeeeee we mnafiki mzanditi, leo unanipigia simu ya nini"

    Aliongea asha akiwa hata getini hajatoka,

    "asha Punguza jazba.... Wahi hapa Tanga Special Bites ujioneee"

    "nijionee nini, mlivyo nitangazia mimi nimemuua mdogo wangu, mji mzima natengwa kwa ajili yenu..."

    "sasa sikia, surian mdogo wako tunamuona hapa anakula kuku kwa mrija,... Yaani ni tajiri, sasa sijui ni mzimu"

    "ati nini"

    "mdogo wako.. Tunamuona hapa"

    "wapi"

    "hapa Tanga Bites"

    Lakini wakati huo huo wakiongea, muna Aliweza kusikia kila neno kwani yeye anatumia hisia za asili ya pili ambayo ni jini,....

    "ok nisubiri hapo hapo nakuja"

    "chukua toyo jamani asha"

    Wakati huo asha anatamani amtafute mama yake hapo kazini ili ampe habari hizi, lakini mbaya zaidi hajui mama anafanyia kazi upande gani hapo ndani,... Hivyo asha aliamua kuondoka lakini kazini keshasajiliwa tayari,...



    Punde sii punde TANGA SPECIAL BITES asha anafika, kwa haraka haraka akawaona rafiki zake ambao ni fatuma, na amina...

    "we Fatuma, haya yuko wapi surian mdogo wangu"

    Aliongea asha huku akiwa na shauku ya kumuona ndugu yake, ingawaje mwanzoni alikuwa akimchukia kwakua kapendelewa elimu.. Wakati huo surian na mke wake wanakula vyuku kwa kwenda mbele na ila surian hajui kama kaonwa na rafiki zake asha...

    "mdogo wako yule pale"







    Asha anatamani sana amuone mdogo wake ambaye anashutumiwa kumuua kisa ni pesa,... Sasa ili jambo hilo liwe safi katika maisha yake ni lazima surian aonekane,... Amina na Fatuma ni marafiki wa asha ambao walikuwa karibu naye toka kufungua kwa saluni yake,... Lakini walikuja kumwonea wivu baada ya asha kuanza kukusanya pesa nyingi, lakini wakati akikusanya pesa nyingi kutokana na wateja,... Mdogo wake alipotea katika mazingira ya kutatanisha,.. Hii leo rafiki zake wanamwita asha aje kumwona mdogo wake....



    "mdogo wako yule pale"

    Aliongea fatuma huku akinyoosha kidole, lakini ghafla hawakuwa wakiona mtu, hata wao wenyewe walijikuta hawaoni mtu,...

    "yuko wapi"

    Aliuliza asha huku akiangaza macho katika eneo husika

    "walikuwa pale na mwanamke mmoja mzuri sana"

    "sasa wako wapi"

    "walikua pale karibu na meza ile pale"

    Asha aliona rafiki hao walikuwa wakimzingua na kuendelea kumtania au kumchokoza kutokana na kashfa alio nayo,...



    Lakini surian na maimuna, walikuwa pale pale wakiendelea kula kuku maeneo hayo, ila maimuna kamshika surian sikio na ndio sababu hawaonekani, na surian anajua kashikwa kikawaida tu kumbe hapo alipo haonekani,.... Asha aliondoka zake kwa hasira, mana rafiki zake ndio wenye kumchezea akili,... Hata akina Fatuma na Amina waliona ni kama maajabu, kwani sekunde chache waliwaona pale, sasa iweje wasiwaone kwa mara nyingine,... Waliona kweli surian kauwawa kwani ni lazima ule utakuwa ni mzimu wake

    "amina, hii sio bure... Kweli surian sio binadamu"

    Aliongea fatuma huku wakiwa wanarudi majumbani mwao,

    "ni kweli, mana dakika ile ile walikwenda wapi"

    "na kwanini alivyokuja asha tu,.. Wakatoweka, ni kweli asha kamuua ndugu yake"

    Walizidi kuongea mengi sana, lakini hawajui lolote



    Baada ya wiki kadhaa kupita, siku zilizidi kwenda na kiwanda kilizidi kuzalisha bidhaa na kuzisambaza mikoani, na ubora wa bidhaa hizo kutoka MICCO, ilifanya hata wafanyabiashara wa nguo aina hizo wasiagize kutoka dubai au maskati, ama oman,.. Hivyo wamiliki wa maduka ya nguo za Kiislamu walihamia katika kiwanda cha nyumbani,... Kiwanda kulipwa kipaumbele kwani kiliajiri Watanzania 500 na wote wanalipwa kwa mishahara mikubwa kutokana na viwango vya elimu zao,....



    Asha akiwa ndani ya kiwanda na ni wiki kadhaa zimepita toka kuanza kazi hivyo sio mgeni tena katika kiwanda hicho,... Mpaka sasa ni miezi miwili toka Kuanzishwa kwa kiwanda hicho lakini boss mkuu hajulikani sura wala sauti, kwani alipewa masharti ya kuto onekana na wafanyakazi, lakini licha ya siku hizo kuisha surian kawa mzoefu wa kuto onekana na wafanyakazi, na hata hakumbuki umuhimu wa kwenda kuiona familia yake,....



    Wakiwa ndani ya idara yake na rafiki zake ambao aliwakuta kabla yake,...

    "nyie fanyeni kazi boss huyo"

    Aliongea asha huku wakiwa wameshika vitambaa wakiwa tayari kwa kuviweka mapambo kwa niaba ya kutengeneza kanzu,...

    "nani boss?"

    Aliuliza rafiki yake mmoja huku asha akijibu

    "si huyo hapo anakuja"

    "heeeeee nani kakwambia huyo ni boss?.. Huyo ni Meneja anaitwa sadiki"

    Siku zote za asha alizokaa hapo alijua sadiki ndio mkurugenzi mkuu wa kampuni hio, kumbe huyo ni Meneja,....

    "sasa boss wa hii kampuni, ni nani"

    Aliuliza asha huku akitamani sana kumjua boss, mana anakumbuka mama yake alisema boss wao ni mdogo mdogo, sasa asha akadhani labda ni sadiki, kumbe boss ni mtu wa familia yao lakini hawajui na hata boss hajui kama familia yake ipo humu,

    "mmmhhh mwenzetu, hata sisi hatumjui, ni mwezi wa pili huu tunalipwa lakini boss hatumjui"

    Sasa sadiki alifika katika eneo husika ambalo asha yupo,...

    "asha?, nakuhitaji ofisini mara moja"

    Aliongea sadiki huku akiendelea kuzungukia baadhi ya idara kama zinazalisha vyema, au wanapiga stori tu....



    "afu mbona meneja anapenda sana kumuita asha, au ndio wameanza nini mahusiano"

    Aliongea msichana mmoja baada ya kumwona asha anaitwa itwa kila siku na Meneja

    "kwani hukumbuki ndio aliokuja kumfundisha mwenyewe"

    "mmmhhh, haya watu na bahati zao"

    Aliongea dada mmoja, na wakati huo asha anaelekea ofisini,... Kaitwa na Meneja,... Mama akiwa anafanya usafi alimwona mtoto wake akielekea ofisini,.. Mama huyo haruhusiwi kujionyesha kwani kawekwa kwa kificho, ili apate riziki



    "asha,.. Mbona upo kimya toka juzi Nasubiri meseji yako... Nimekununulia simu ili tuwasiliane"

    Aliongea sadiki huku asha akijing'ata vidole, kana kwamba watu hawa wana mpango wa kuwa na mahusiano...

    "lakini boss, mimi nitakujibu... Alafu sasa boss akijua una mahusiano na mfanyakazi, itakuwaje"

    "boss nani tena... Mimi ndio mwenye kauli ya juu, na sitaki kujulikana mimi ndio boss mkuu kwasababu watu sio wazuri hapa mkoani tanga... Najiita meneja ili nionekane wa kawaida tu"

    Aliongea sadiki kama vile kujipa nafasi ya uboss mana anampenda sana asha, lakini sasa asha yeye anatamani uzuri wake autumie kwa boss mkuu, hio ndio nia yake, mana maisha yalisha watupa mkono, na kama tunavyomjua asha mwanzoni alikuwa ni msichana wa kudanga danga sana hivyo hata kuja hapa kwenye hii kampuni shida yake apate mwanaume wa kumchuna,.... Sasa aliposikia kuwa boss wa kampuni hii ni kijana mdogo akajua uzuri alio nao ataweza kumteka awe naye ili maisha yaendelee,.. Sasa alipokutana na sadiki akajua huyo ndio boss mwenyewe, kumbe sadiki ni Meneja na boss ni kaka yake kabisa baba mmoja mama mmoja, ila hajui kama kaka yake ndio mmiliki wa hapa...

    "mbona nilisikia kuna boss mwingine"

    "ndio, ni ili mimi nisijulikane"

    "ok, lakini daki.. Mi naomba vuta subra kidogo nitakujibu tu"

    "asha, mtoto mzuri kama wewe, yanini nikukose... Nataka mke, ona nina maisha mazuri lakini sina mke"

    "ni sawa diki, lakini nipe nafasi ya kufikiri, tatizo ninyi wanaume hamuaminiki"

    "sio wote asha,... Please naomba kesho unipe furaha ya moyo wangu, kama ni mshahara mimi nitaupandisha mara dufu"

    Aliongea sadiki na kujigamba sana kuhusu nafasi yake....

    "kweli diki"

    "ndio, kwani we watakaje... Sema lolote nifanye"

    "usijali, ila kikubwa nataka mama yangu ahamishwe kitengo kutoka kusafisha vyoo kuja kiwandani au hata awe mpishi sio mbaya"

    Aliongea asha akiwa na nia ya kumsaidia mama yake asiende na kazi ya usafi wa vyoo kwa haipendi

    "kumbe yule ni mama yako"

    "ndio"

    "ok ni hilo tu?... Au una Lingine"

    "ni hilo tu, na mshahara wangu sio mbaya kama utapanda kidogo"

    "usijali"

    "mimi shida yangu ni kukumiliki wewe na uwe mke wangu, wala sitaki kukuchezea asha"

    Asha ni msichana mzuri sana sema aliutumia uzuri wake vibaya, na mpaka sasa bado ni kisu, na ndio maana meneja kanasa mwenyewe



    Wakati huo huo suria akiwa ofisini kwake, oda zilikuwa zikiingia nyingi kwa njia ya simu ya secretary, kisha secretary anamtumia boss wake kule ndani na boss anamtumia meneja masoko ili afanye kazi na watu hao, asha anatoka ofisini kwa sadiki, akiwa haamini kama anapendwa na boss, na hapo anapopita ndipo mlango wa boss mkuu ulipo, na ni ndugu yake kabisaaaa, ila hajui



    Ilipofika jioni mida ya saa 12 na nusu, suria akiwa ndio wa mwisho kabisa kutoka,... Na ni ili asionekane na watu, sasa haijulikani ni kwanini mana siku za masharti ya jini maimuna zilisha isha, lakini suria bado haihitaji kuonwa na watu kana kwamba kesha zoea kujificha ficha...



    Sasa huku nyumbani kwa akina asha, akiwa na mama yake jikoni wanapika, kwa sasa maisha yao sio mabaya mana mama keshapokea mshahara wake wa kwanza wa laki nne, sasa hawana ziki za hapa na pale... Wakati huo baba yao akiwa msikitini wao wapo jikoni wanaongea, kama unavyojua mama na mtoto wa kike walivyo...

    "wewe asha,.. Mchana ule niliogopa kukuona na Meneja unakwenda ofisini, nikajua unafukuzwa kazi"

    Aliongea mama yake asha huku asha akitabasamu tu,...

    "mama, ina maana kila nikienda ofisini nakwenda kufukuzwa"

    "ndio, mana juzi tu kuna wasichana wawili walifukuzwa kwa kuvaa nguo fupi, nikajua na wewe pia"

    "hapana mama... Afu mama yule sio meneja ni boss mwenyewe"

    "weeeeeeeeee, usikute kakupenda ndio mana kakudanganya... Yule ni meneja pwiiiii, hata siku nakwenda kuomba kazi, nilimuona kwenye foleni na vyeti vyake"

    "haaaaaaaaa mama unasema kweli"

    "ndio, yule ni Meneja.... Kwani kuna nini"

    "basi mi nikajua ni boss"

    "we asha, hebu niambie ukweli mwanangu, nini kinaendelea wewe na Meneja sadiki"

    "mmmhhh mama bwana tuyaache hayo"

    "najuaaaa,... Najua keshakupenda yule"

    "ni kweli mama, ila mi namtaka boss mwenyewe..."

    "asha mwanangu, umefuta kazi fanya kazi.... Ina mana unataka kurudia ujinga wako wa zamani"

    "mama... Ina maana mimi nikiwa na mahusiano na boss mkuu ni vibaya"

    Aliongea asha huku mama akiangalia chini kama anawaza na kumjibu kuwa

    "sio vibaya mwanangu, lakini kumpata boss mkuu sio mchezo mchezo, ni sawa na kwenda kumuona raisi uso kwa uso"

    "sasa nifanyeje mama.... Ina mana uzuri wangu ipotee bure tuuu"

    "asha... Kama sadiki ana nia nzuri, mlete atujue wazazi wako... Achana na huyo boss mkubwa mwanangu, na pia boss mkubwa naskia ana mke"

    "mke?? We ai umesema ni mdogo"

    "ndio, ila ana mke"

    "ila mama kwani si muislamu, nitakubali niwe hata mke wa pili... Nataka tukiwa kwenye mahusiano, atujengee nyumba"

    Aliongea asha bila kujua boss huyo huyo ni mdogo wake kabisa tumbo moja, lakini kwakua hajawahi kumuona, sio rahisi kujua....

    "ni kweli, lakini hata sadiki anaweza"

    "sitaki bwana..."

    "tatizo lako mwanangu unapenda pesa za haraka jamani... Hebu ngoja nitajaribu kupeleleza ili hata nipate namba ya huyo boss mkubwa"

    Aliongea mama huyo bila kujua boss huyo ni mtoto wake, yaani anataka kumpigania mtoto wake wa kike aolewe na boss ambaye ni mtoto wake wa kiume, ila hawajui wote na hata surian hajui kama familia yake ipo hapo ndani...



    Tukija huku kwa akina surian na mke wake, wakiwa jikoni wote wanapika..

    "mke wangu, nataka nikuletee mfanyakazi wa ndani"

    Aliongea surian huku mke akianza kununa, mana naye ana wivu

    "kwa kazi gani sasa ulete mfanyakazi, kwani ni lini ukakuta nadeki humu ndani... Mana nyumba inajideki wenyewe kila siku... Inajifuta vumbi yenyewe, nguo zinajifua zenyewe, sasa mfanyakazi wa nini"

    Aliongea mke huyo mana ikumbukwe maimuna ni jini, ila ni jini mwenye asili mbili,

    "mimi sipendi uwe unatumia nguvu zako za kijini kufanya usafi, na hii asili siitaki, nataka uwe wa kawaida tu"

    "ni sawa mume wangu, ila mimi ni jini na nitabaki kuwa hivyo.... Kwanza mtoto wako ananipiga mateke"

    Aliongea maimati kana kwamba mtoto alioko tumboni

    "mmmhjh wa juzi tu"

    "hapana... Kwenye asili yetu ya majini hua hatukai miezi tisa kama binadamu wa kawaida... Tunakaa miezi minne na nusu... Na shetani anakaa miezi miwili na nusu"

    "heeeeee... Kwahio keshokutwa tu nina mtoto"

    "sanaaaaa"

    "waooooooo.... Nakupenda jamani mke wangu"

    "nakupenda pia baba watoto wangu"

    Suria alinogewa na penzi la jini huyo na kufumbwa macho asione popote



    Kesho yake ikiwa ni siku nyingine tena, asha akiwa ndani ya kiwanda lakini alionekana kukasirika sana kwasababu mwanaume aliojipendekeza sio yule aliomtaka yeye,... Asha Alishika simu yake ambayo kanunuliwa na sadiki, kwani asha hakuwa na simu baada ya kuiuza,...

    "hallo diki mambo"

    "poa mzima asha jamani"

    "mzima... Nipo kiwandani, nataka tutoke kidogo nikakujibu ombi lako"

    "sawa mama... Toka nikukute nje ya geti hapo kuna hoteli moja nzuri sana nakuja"

    "ok sawa, uwahi mana nataka nirudi kazini"

    "usijali asha wangu"

    Sadiki aliongea hayo kana kwamba kweli kampenda sana asha, lakini asha alikuwa hamtaki sadiki kwani hakuwa boss alio mkusudia,... Asha alitoa laini zake kwenye simu ili akampe simu yake huko nje...



    Huku ofisini sadiki anafurahi kwani anajua anakwenda kupewa utamu wa mwili, ikiwa ni mpenzi mpya kwake, kumbe anakwenda kupewa simu yake.... Sadiki alitoka nje ya kampuni akiwa kama meneja, hivyo hakukua na wa kumuuliza, asha alisha toka nje ya geti kwa kisingizio cha kwenda kununua dawa kwani hajiskii vizuri kiafya.... Walikutana nje kisha sadiki akachukua taxi, kwani angelitoka na gari yake labda angeulizwa anakwenda wapi kwani ilikuwa ni majira ya saa tisa alasiri,



    Sasa huku kwa surian kashika simu yake ya mezani na kumpigia shadya au Cecilia aliopo mapokezi....

    "hallo boss"

    "shadya"

    "abee boss"

    "mwambie sadiki akakague products kabla muda wa kazi haujaisha"

    "aaahh sorry boss, sadiki katoka kidogo nadhani kafuatilia oda"

    "ok basi, nitakwenda mwenyewe"

    Aliongea surian kisha akakata simu,.. Sasa shadya kaka akijiuliza anakwenda mwenyewe yeye au nani, mana toka kampuni kuanza surian hajawahi kwenda kukagua kiwanda wala kuangalia wafanyakazi wake,... Sasa kwa mara ya kwanza surian anatoka kwenye upande wa kiwanda ambako kuna wafanyakazi takribani 500, na wote hao hawamjui boss....



    Shadya alishangaa kweli boss anatoka kwenda kiwandani,... Shadya haamini macho yake, yaani ni kama ndoto, afu mbaya zaidi ile ile idara ambayo asha alikuwepo ndio surian anaingia kuanza ukaguzi wake, kana kwamba kama asha angelikuwepo, basi angemuona ndugu yake, lakini hakuwepo... Wasimamizi walikuwa kipaumbele kumwelekeza boss, kwani shadya alitangulia kuja kutoa taarifa kuwa boss anafika hivi punde,.. Sasa wafanyakazi kila mmoja anasema yakwake...

    "kumbe ni katoto tu... Mi nikajua kuubwa"

    Mmoja kati ya wasichana aliongea hivyo...

    "ila ni hensam jamani,.. Hivi ana mke kweli"

    "heeee mwenzangu mi najuaje kama ana mke au hana"

    "waaoooo kazuri kweli.... Asha yuko wapi si alikuwa anataka kumjua boss mwenyewe"

    "asha atakuwa kaenda uwani"

    Wafanyakazi wa kike walikuwa wakimuwazia sana boss surian... Sasa katika pitapita yake kwenye ukaguzi, akakuta sehemu moja ni chafu...

    "hapa vipi hapa... Mbona idara hii sio safi"

    Aliongea hivyo huku wafanyakazi na wasimamizi wakitetemeka mno

    "hapa palimwagika maji boss"

    "nani kaingia na maji... Na toka wakati wote kwanini msipakaushe"

    "samahani boss..... Nyie, hebu chukueni dekio kausheni hapo"

    huyo ni msimamizi mwenye kutoa sauti hio..

    "sjapenda kabisa... Mabwana usafi wakija hapa ni tatizo kubwa sana... Hivi kama kiwandani ni hivi, je huko chooni kutakuaje..."

    "hapana boss, chooni ni kusafi kila wakati boss"

    "hapana.... Lazima nikakague usafi wa vyoo, mana mtafanya kampuni ipigwe faini au kufungiwa kwasababu ya uchafu"

    Aliongea surian huku akielekea  chooni, na vyoo hivyo vinafanyiwa usafi na mama yake mzazi, na hajui kuwa mama yake naye anafanya kazi kwenye kampuni yake, na hata mama naye hajui kama mwanaye ndio mmiliki wa kampuni hio,...







    Hakuna kitu kinauma kama kumkuta mama yako anafanya kazi za ajabu ingali una uwezo wa kuwapumzisha nyumbani, yaani wawe wanakula matunda yako tu,... Lakini kwa upande wa surian alitamani sana kuwasaidia wazazi wake lakini kutokana na masharti ya jini maimuna, anatakiwa awasaidie kwa njia ya ajira, yaani awaajiri, kitu ambacho surian alikataa kabisa, hawezi kuwatumikisha wazazi wake kisa pesa,... Lakini bila kujua hali za wazazi wake, zilikua mbaya na waliona matangazo na kuja kuomba kazi,... Lakini surian hajui kama mzazi wake mmoja yupo hapa kazini pamoja na dada yake... Na mbaya zaidi mzazi kapangiwa sekta moja mbaya sana, yaani mama wa tajiri akafanye kazi chooni??? Haiwezekani



    Wasimamizi mbalimbali na viongozi wakiwa wanamuongoza kwenda katika vyoo hivyo ili kuhakikisha usafi unakuwa mzuri,.. Sasa shadya alishangaa kumuona boss anaelekea kule chooni,... Na mfanya usafi wa kule chooni amewekwa kwa siri kwasababu umri wake hauruhusu kufanyakazi kwenye kampuni hiyo,. Shadya haraka haraka alimpigia mama yake surian simu....

    "samahani, namba ya mteja unayempigia haipatikani, tafadhali jaribu tena baadaye"

    Ilikuwa ni sauti ya vodacom ikimjulisha shadya kuwa namba ya mteja haipatikani,.. Sasa shadya kichwa kinapata moto kwani yeye ndie alie fanya ujanja mpaka mama huyo akapata kazi, na umri wa mama huyo hauruhusu kabisa.... Shadya alijaribu na kujaribu, lakini wapi simu haipatikani,.... Surian anafika katika eneo la vyoo, wapambe wakaanza kuongea...

    "boss?? Angalia vyoo ni visafi kila wakati"

    Aliongea kiongozi mmoja ambaye ni kama mpambe tu... Na kweli palikuwa pasafi kabisa,... Sasa mama huyo alikuwa anafanya usafi ndani ya choo, hivyo hana taarifa kuwa boss mkuu yupo nje ya vyoo bavyo anavifanyia usafi kila wakati,.. Sasa boss karidhika kuona usafi ambao unafanyika hapo chooni,. Na karidhika nao kwa asilimia zote,... Bila kujua anaye fanya usafi ni mama yake mzazi,.. Aiseee surian anageuka na kuondoka, na mama naye anatoka chooni baada ya kumaliza kufanya usafi,... Mama alishangaa tu kuona kundi la watu wakimalizikia kuondoka, lakini hakujua kama boss wake alikuwepo hapo,... Yaani ilikuwa kiduchu tu aonwe na boss.... Sasa surian hakuwa na haja tena ya kutembelea idarani, alirudi zake ofisini,... Wakati huo shadya anatetemeka kwani anajua tayari kimebumburuka huko chooni,... Alishangaa boss kaingia ofisini kwake bila tabu na mtu.... Shadya alihema kwa nguvu kuashiria labda hakuna kitu,... Lakini hakuamini alitoka kwenda mpaka chooni kuhakikisha...







    ITAENDELEA

0 comments:

Post a Comment

Blog